Title Devis

Biblia inaposema upanga wa mmoja ukawa kinyume na mwenzake inamaana gani? (Ezekieli 38:21)

SWALI: Je ni kitu gani hasaa kilikuwa kinatokea mpaka wafikie hatua kama ile, je! Ni utahira ulikuwa unawapata au ni nini hasaa?


JIBU: Silaha mojawapo ambayo tuona Mungu alikuwa akiitumia kuwashindania watu wake mara myingi wawapo vitani, Ni hii ya “machafuko” yaani Ni kuwavuraga maadui washindwe kuelewana na hatimaye kuanza kushambuliana wao kwa wao.

Kwamfano wa matukio kama hayo tunaweza kuyathibitisha katika habari hizi;

Wana wa Israeli Walipoizunguka Yeriko.

Waamuzi 7:22

[22]Wakazipiga zile tarumbeta mia tatu, naye BWANA akaufanya upanga wa kila mtu uwe juu ya mwenziwe, na juu ya jeshi lote, jeshi likakimbia mpaka Bethshita, kuendelea Serera, hata mpaka wa Abel-Mehola, karibu na Tabathi.

Sasa tuone ni njia zipi alikuwa anazitumia Mungu mpaka wauane wao kwa wao, watu ambao walikuwa wamekubaliana kabisa kwenda vitani?

1). Bumbuazi

Hii ni hali ya kutoweza fikiri vema, kuwa kama mtu fulani nusu aliyerukwa na akili.

Kumbukumbu la Torati 28:28

[28]BWANA atakupiga kwa wazimu, na kwa upofu, na kwa bumbuazi la moyoni;

Hii ni hali yakutokuwa sawa katika ufahamu, unamwona mwenzako kuwa ndiye adui, na hatimaye vita vinaanza kabla hata ya maadui wenyewe kufika..hili ndio yamkini Bwana alilowapiga watu wa Yeriko.

Kama tu vile Mungu alivyowapiga upofu watu wa Sodoma na Gomora wasione mlango wa Lutu, vivyo hivyo hawa wanapigwa katika eneo la fikra wasifiri vema wauane, wao kwa wao.

2) Kutofautiana kauli.

Hii ni namna ambayo mnapisha usemi. Kiasi kwamba hakuna mtu wa kumsikiliza mwenzake, huyu anataka hili, Yule hili, kila mmoja haafikiani na mwenzake hatimaye chuki inatokea, matengano na mwisho kuanza kupigana wao kwa wao.

Watu wa Babeli walipigwa ‘usemi’ isipokuwa tu wao hawakufikia hatua ya kuuana, lakini ni namna tu hii hii .(Mwanzo 10)

3) Shuku na visasi

Hii ni hali ya kuwashuku wenzako kuwa ni wasaliti, hivyo ghafla kupoteza imani nao, na kuanzisha vita ili kujilinda…mfano wa hili tunaliona kwenye ile vita ya Yuda na majeshi ya wamoabu, waamoni na wameuni walipokutanika kupigana na taifa la Mungu..ghafla moabu Na amoni wakaipiga Seiri, halafu baadaye wakarudiana Wao kwa wao.

2 Mambo ya Nyakati 20:22-23

[22]Nao walipoanza kuimba na kusifu, BWANA akaweka waviziao juu ya wana wa Amoni, na Moabu, na wa mlima Seiri, waliokuja juu ya Yuda; nao wakapigwa.

[23]Kwani wana wa Amoni na wa Moabu waliwaondokea wenyeji wa mlima Seiri kuwaulia mbali na kuwaharibu; nao walipokwisha kuwakomesha hao wakaao Seiri, wakajitia kuharibu kila mtu mwenziwe.

Hii ya visasi inatokeaje?

Labda mmoja alikuwa na chuki na mwenzake, hivyo unamlipizia kisasi, na huyu naye kaona ndugu yake kauliwa anaamka kumtetea, mara kabila hili na hili hatimaye taifa zima linaiingia katika kujiharibu.

Hivyo Mungu anapotaka kutupigania, silaha hii huwa anaitumia hata katika agano jipya hususani hapo kwenye kugonganisha ndimi.

Kwamfano mtume Paulo alipokamatwa awekwe barazani ili ahukumiwe…kwa hekima ya Roho alipewa kujua kuwa katikati ya baraza wapo mafarisayo na masadukayo. Hivyo alilolifanya ni kuwachonganisha ndimi, badala ya kumshambulia yeye..wakaanza kushambuliana wao kwa wao…hiyo ni silaha ya Bwana ambayo kwa hekima ya Roho aliitamka..

Matendo ya Mitume 23:6-7

[6]Paulo alipotambua ya kuwa sehemu moja ni Masadukayo, na sehemu ya pili ni Mafarisayo, akapaza sauti yake katika ile baraza, Ndugu zangu, mimi ni Farisayo mwana wa Farisayo; mimi ninahukumiwa kwa ajili ya tumaini la ufufuo wa wafu.

[7]Alipokwisha kunena hayo palikuwa na mashindano baina ya Mafarisayo na Masadukayo, mkutano ukafarakana.

Ni vema kufahamu aina hii ya silaha ni mbaya kuliko ile ya kushindana na adui yako.

Lakini ni vema kufahamu kuwa hata shetani hutumia silaha hii, pale tunapotoka nje ya mpango wa Mungu.

Israeli iliingia kwenye vita vya wao kwa wao, na kupelekea mauaji mengi sana…

Ni nini kilitokea?

Baadhi ya wana wa Benyamini waliendekeza dhambi ya uasherati mpaka ikafikia hatua inayokaribia ile ya sodoma Na Gomora na Israeli yote ilipopata taarifa, wakataka wawatoe hao watu wauliwe, lakini wabenyamini wakawaficha kwasababu ni watu wa kabila lao. Machafuko yakaanzia hapo, hatimaye wakauana Sana. (Waamuzi 19-21)

Hata sasa silaha hii shetani hupenda kuirusha kwenye kanisa la Mungu, watu wapoteze upendo na utakatifu ili waanze kulana na kung’atana..kwasababu ya wivu, visasi na vinyongo.

Wagalatia 5:14-15

[14]Maana torati yote imetimilika katika neno moja, nalo ni hili, Umpende jirani yako kama nafsi yako.

[15]Lakini mkiumana na kulana, angalieni msije mkaangamizana.

Lazima tuijue hila hii ya shetani na kukataa kuipa nafasi.. Na Bwana atatuhifadhi, na matokeo itakuwa ni yeye kuleta machafuko kwa maadui zetu wanaposimama Kinyume na sisi.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, tunashindanaje vita vya kiroho?

VITA VYA IMANI NI VITA ENDELEVU.

Nini maana ya huu mstari ” Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;”?(2Timotheo 4:7)

Print this post

Ipi tofauti ya Kukemea na kukaripia? (2Timotheo 4:2)

Jibu: Tuanzie ule mstari wa kwanza..

2Timotheo 4:1 “Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu walio hai na waliokufa; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake;

2 lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, KARIPIA, KEMEA, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”.

“Kukaripia” ni kulaani au kukosoa kosa lilolofanyika… Kwamfano mama anaweza kumkaripia mwanae kwa tabia ya Uvivu, kwamba aiache hiyo tabia, kwani ni mbaya na itamletea madhara huko mbeleni..na kukaripia mara nyingi kunaambatana na kutoa elimu,ushauri au darasa juu ya hilo kosa..

Lakini “Kukemea” inaenda mbali zaidi, kwani kunahusisha kulaani kitendo kibaya na  kutoa amri ya zuio ya jambo hilo lisiendelee kutokea… Kwamfano Mama anaweza kumkemea mwanae kwa kosa la Wizi, Kwamba tendo hilo ni kosa na lisirudiwe tena! (hiyo inakuwa ni amri, sio ombi tena wala ushauri).

Serikali inaweza kukemea vitendo vya mauaji, ubakaji  au rushwa.. kwamba vitendo hivyo ni vibaya na havipaswi kutendeka kwani ni uvunjifu wa sheria, hivyo kutofanya hayo ni amri na sio ombi wala ushauri..

Na katika Biblia, Neno la Mungu linatuagiza “Kukaripia” na “Kukemea”

2Timotheo 4:2 “lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, KARIPIA, KEMEA, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”.

Zipo tabia au mienendo iliyopo kati ya watu ambayo kiuhalisia inahitaji “kukaripiwa” na mingine “kukemewa”  na Neno la Mungu linatufundisha kufanya hivyo bila kuogopa pale inapobidi. (hususani ndani ya kanisa)

Kwamfano vitendo vya wivu, uvivu, uzembe, utegeaji ndani ya kanisa, (hivyo katika hali ya uchanga vinaweza kukaripiwa tu na vikaisha), lakini vinapozidi mipaka vinapaswa vikemewe!.

Lakini vitendo vingine kama vya Ulevi, Uchawi, uzinzi, uasherati, wizi, utukanaji, fitina na vingine vinavyofanana na hivyo, havihitaji kukaripiwa bali KUKEMEWA, kwamba visiendelee kufanyanyika na hiyo inakuwa ni “Amri” na sio “Ombi wala ushauri”, maana yake mtu akiendelea kufanya hayo makusudi baada ya kuonywa mara nyingi, ni haki yake kutengwa kwa muda mpaka atakapojirekebisha ili asilichafue kanisa la Kristo.

1Wakorintho 5:11 “Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.

12 Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani?

13 Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu. Ninyi mwondoeni yule mbaya miongoni mwenu”.

Hapo anaposema “ndugu” anamaanisha Ndugu katika Imani (mkristo), hususani Yule ambaye tayari analijua Neno la Mungu, lakini hataki kubadilika yuko vile vile ndani ya kanisa ni mlevi, au mzinzi,  au mwizi, huyo kama amekemewa na hakubali kubadilika, Biblia imetoa ruhusa ya kumtenga kwa muda, ili asilichafue kanisa..

Lengo la kumtenga ni ili atafakari na asione kanisani ni mahali pa kufanyia mchezo, au pango la wanyang’anyi.. Akifanyiwa hivyo itampa muda wa kutafakari na kama ni mtu wa kujali basi atatambua makosa yake na kujirekebisha na hivyo atarudishwa kanisani… Lakini kwa wale wengine walioingia kwenye wokovu hivi karibuni (ambao bado ni wachanga) hao hawawezi kutengwa wanapofanya makosa yale yale waliotokea nayo duniani kwani bado ni wachanga wanahitaji kufundishwa zaidi..Lakini kwa wale wengine waliokaa miaka na hawabadiliki, Neno limeruhusu kuwatenga kwa muda.

Hivyo kwa hitimisho ni lazima kukaripia mabaya, lakini pia kukeme na kuonya pia..Kwani hata Bwana Yesu Kristo huwa anatukemea pale tunapoondoka kwenye njia (Ufunuo 3:19)

Neno hilo “Kukemea” linaweza kutumika pia katika kutoa pepo, kwasababu pepo anapokuwa ndani ya mtu, huwa anamtesa Yule mtu, na si haki yake kumtesa.. hivyo tunapoamuru pepo atoke ndani ya mtu maana yake tunatoa “AMRI” sio “Ombi”.. kwamba hizo shughuli zake anazozifanya ndani ya mtu, zisimame na amtoke Yule mtu, Pepo hatulikaripii bali tunalikemea (Luka 9:42)

Bwana atubariki na kutusaidia sote.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAMBO MANNE(4) YAFANYAYO NENO LA MUNGU.

Vita vya kiroho, na mwamini Mpya.

Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote (Yohana 16:23)

NAYE ALIKUWA HANA BUDI KUPITA KATIKATI YA SAMARIA.

Kumwambia mtu mwenye dhambi kuwa atakwenda kuzimu asipotubu Je! ni kuhukumu?

Print this post

FUNGUA KINYWA CHA ROHO MTAKATIFU KIHUDUMU.

Ahadi mojawapo ya Roho Mtakatifu Kwa wote waliompokea ni kupewa uwezo wa kuzungumza “ufahamu wa Mungu”, kwa vinywa vyao.

Ufahamu huu unaweza kujifunua katika maumbile mbalimbali aidha kwa kueleza habari zilizopita, au habari zijazo, au zinazoendelea sasa hivi, au kutoa maelekezo, au faraja, au neno la hekima, au maarifa, au uponyaji au baraka..Namna zote hizi kwa lugha rahisi kuitwa utabiri/ unabii.

Ukiwa kama mwamini ni vema kufahamu sehemu kubwa sana ambayo Roho Mtakatifu anaitumia kuhudumu ni katika vinywa vyetu. Ndio maana siku ile ya kwanza ya pentekoste aliposhuka, alikaa juu ya wale watu kama “ndimi za moto”. Maana yake ni kuwa huduma yake hasaa hujidhihirisha katika ndimi…ndio maana akaweka moto wake juu ya ndimi zao, lugha zao zikabadilishwa wakaanza kunena kwa lugha mpya.

Kwahiyo kinywa cha mtu aliyeokoka, ni kinywa cha Mungu duniani. Usipojifunza kukifungua kinywa chako kiufasaha, ujue hiyo ni namna mojawapo ya kumzimisha Roho Mtakatifu ndani yako.

Watu wengi hawajui kuwa kila mmoja amepewa uwezo wa kutabiri/ kuhutubu na sio suala la huduma fulani ya kinabii tu, hapana utauliza hilo lipo wapi kwenye maandiko? Soma..

Matendo 2:17 wana wenu na binti zenu watatabiri..

Lakini pia 1 Wakorintho 14:31. Inasema..

[31]Kwa maana ninyi nyote mwaweza kuhutubu mmoja mmoja, ili wote wapate kujifunza, na wote wafarijiwe.

Kuhutubu kama ilivyotumika hapo, ni kutabiri/ kusema ufahamu wa Mungu. Jambo ambalo ni la wote sio baadhi.

Sasa unafunguaje kinywa cha Roho Mtakatifu na unafanya hivyo katika mazingira gani?

Usisubiri mpaka karama fulani ije juu yako, yaani kuonyeshwa/kufunuliwa.. hapana…kwasababu tayari una Roho Mtakatifu ndani yako anza kusema maneno yanayolanda na ahadi za Neno la Mungu, bila kufikiri- fikiri

Kwamfano…

Umepelekwa kwenye mashtaka fulani kwa ajili ya Neno. Au unatakiwa uwasilishe hoja, au ufundishe Neno, au uhubiri, au umekwenda mtaaani kushuhudia.. usianze kusema mimi nitawezaje kuhubiri, au kujieleza, sijui sheria, sijui vizuri biblia, sijui kupangilia maneno…hupaswi kufikiri hivyo. bali ukumbuke ulishapewa kinywa cha moto, tangu siku ulipoamini, wewe nenda kisha anza kuzungumza huko huko katikati ya maneno yako Roho Mtakatifu ataunganika na wewe.

Mathayo 10:18-20

[18]nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa.

[19]Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.

[20]Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu.

Mwingine atakuambia mimi siwezi kuomba masafa marefu ninaishiwa na maneno…ndugu hupaswi kukatisha maneno na kuacha Kuomba, ukaenda kulala.. endelea kutafakari huku ukizunguza na Mungu wako Habari mbalimbali za kwenye maandiko, na ghafla tu baada ya muda kidogo utaona unaingia kwenye mkondo fulani wa kimaombi, linatoka neno hili kwenye ufahamu linakuja neno hili la kuombea…ulikuwa umepanga uombe Saa 1, unajikuta unaomba matatu.hapo ni Roho Mtakatifu amekupa Kinywa cha kuomba..na ndani ya maombi hayo ni utabiri tosha, kwasababu sio ufahamu wako, bali ni wa Mungu ndani yako.

Vilevile jifunze kutoa sauti katika uombaji wako wa mara kwa mara..ndio tunafahamu Maombi sio sauti, hata kimoyo- moyo Mungu anasikia, lakini usimzimishe Roho..

Watu wengi wanatamani kunena kwa lugha lakini, wanazuia vinywa vyao kutoa sauti.. wanategemea vipi wanene kwa lugha mpya..unapojiachia Kwenye maombi huku unatoa sauti ni rahisi sana kujazwa Roho Na kuomba kwa lugha.

Eneo lingine labda mtu ni mgonjwa..anahitaji maombi…Fungua kinywa chako kwa ujasiri mtamkie uponyaji…unaweza kudhani ni maneno yako, hujui kumbe Ni Roho Mtakatifu Ameyaingilia na kulifanya tayari kuwa Neno la kinabii la uponyaji, na hatimaye anapokea uponyaji wake saa hiyo hiyo.

Uwapo na Watoto wako, Acha kuzungumza nao, habari za kidunia dunia tu..wawekee mikono wabariki kwa Imani kama vile Isaka alivyowabariki Yakobo na Esau na maneno yale yakawa kweli. Vivyo hivyo na wewe tabiri juu ya watoto wako unataka wawe nani wawapo watu wazima.

Uwapo kazini na marafiki zako, penda kuzungumza maneno ya ki-Mungu wakati mwingi kwasababu huko huko unabii unaweza kupita bila wewe kujijua… mwangalie kayafa

Yohana 11:49-52

[49]Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote;

[50]wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima.

[51]Na neno hilo yeye hakulisema kwa nafsi yake; bali kwa kuwa alikuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, alitabiri ya kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa hilo.

[52]Wala si kwa ajili ya taifa hilo tu; lakini pamoja na hayo awakusanye watoto wa Mungu waliotawanyika, ili wawe wamoja.

Hivyo kinywa cha ni kinywa cha Roho Mtakatifu usikifunge Bali kijaze Maneno ya Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VIASHIRIA VINGINE VYA ROHO MTAKATIFU KUWEPO NDANI YAKO.

TULITAFUTE KWA BIDII TUNDA LA ROHO.

KWA KUWA ROHO BORA ILIKUWA NDANI YAKE.

Print this post

Ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo.

SWALI: Tukisoma Kitabu cha Waebrania tunaona mwandishi akitaja vitu viwili vya Mungu visivyoweza Kubadilika ambavyo tumepewa viwe kama nanga ya Roho, je ni vipi hivyo? Au Maana yake ni nini?

Waebrania 6:17-19

[17]Katika neno hilo Mungu, akitaka kuwaonyesha zaidi sana warithio ile ahadi, jinsi mashauri yake yasivyoweza kubadilika, alitia kiapo katikati;

[18]ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo, tupate faraja iliyo imara, sisi tuliokimbilia kuyashika matumaini yale yawekwayo mbele yetu;

[19]tuliyo nayo kama nanga ya roho, yenye salama, yenye nguvu, yaingiayo hata mle mlimo ndani ya pazia,


JIBU: Ukisoma hiyo habari vifungu vya juu na vile vinavyoendelea mbele yake. Habari inayozungumziwa pale ni ya Ibrahimu na jinsi Mungu alivyompa ahadi ya mbaraka pamoja na uzao wake. Na jinsi alivyokuja kuitimiza

Lakini tunaonyeshwa ahadi ile pekee aliyopewa, haikutosha kumfanya Ibrahimu, aamini bali Mungu Ili kumthibitishia kuwa atavipokea kweli kweli basi aliongezea Na kiapo.

Mwanzo 22:15-17

[15]Malaika wa BWANA akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni

[16]akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema BWANA, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,

[17]katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;

Kwasababu kiapo ni kifungo cha mwisho ambacho Mtu humaliza shuku zote, mashaka yote mijadala yote..

Ilimbidi Mungu aweke kiapo ijapokuwa angetimiza Ahadi zake bila kiapo. Lakini ilimbidi afanye vile ili kumpa uthabiti Ibrahimu juu ya maadhimio yake.

Hivyo mambo hayo mawili yasiyoweza Kubadilika ya Mungu ni;

1)Neno lake(ambalo lilikuja kama ahadi),

2) lakini pia Kiapo, ambacho hukata maneno yote.

Na kweli tunakuja kuona yote Mungu aliyomuahidi Ibrahimu yalitokea kama yalivyo..

Lakini Ahadi hiyo haikuishia kwa Ibrahimu, bali ilitimilizwa yote na Bwana wetu Yesu Kristo.

Ambao sisi tuliomwamini, tunaingizwa Katika ahadi hizo..alizozithibitisha Kwa kiapo kupitia Bwana wetu Yesu Kristo. Ambaye Mungu alimthibitisha kama kuhani mkuu wa milele mfano wa Melkizedeki kuhani Wa Ibrahimu (rohoni)..

Waebrania 7:21-25

[21](maana wale walifanywa makuhani pasipo kiapo; bali yeye, pamoja na kiapo, kwa yeye aliyemwambia, Bwana ameapa wala hataghairi, Wewe u kuhani milele;)

[22]basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.

[23]Tena wale walifanywa makuhani wengi, kwa sababu wazuiliwa na mauti wasikae;

[24]bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.

[25]Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.

Hivyo sisi tuna Neno la ahadi..kwamba tunaomwamini tunapokea uzima wa milele kama yeye.. Lakini pia jambo Hilo amelikolezea Kwa kiapo kuwa hatalibatilisha..Ni hakikisho kubwa sana..Haleluya!

Hivyo ni wajibu wetu kuendelea mbele kwaujasiri na bidiii katika imani na kumtumikia yeye kwasababu yupo pamoja nasi, wala kamwe hawezi kutuacha hata Iweje.

Kwasababu Neno lake ni hakika, alilotuahikikishia Na kiapo juu.

Je umempokea Bwana Yesu kwenye Maisha yako?. Fahamu kuwa hakuna tumaini lolote nje ya Kristo. Okoka leo.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Je mkristo anaruhusiwa kuoa mke wa ndugu yake aliyefariki?

Katika agano la lake, iliruhusiwa Kufanya hivyo, ikiwa mtu amefiwa na ndugu yake na hana mtoto, aliruhusiwa kwenda kumwoa mke wa ndugu yake ili amwinulie uzao, lakini halikuwa kwa lengo la kimahisiano ya kindoa kana kwamba ni wapenzi. Bali kwa kusudi tu la kumwinulia uzao.

Kumbukumbu la Torati 25:5-10

[5]Watakapoketi pamoja mtu na nduguye, mmojawapo akafa, wala hana mwana wa kiume, mke wa yule aliyekufa asiolewe nje na mgeni; nduguye yule mumewe amwingilie amweke kwake awe mkewe, kumfanyia yampasayo nduguye mumewe. 

[6]Na iwe, yule mzaliwa wa kwanza atakayemzaa, amfuate nduguye aliyekufa kwa jina lake, lisije likafutwa jina lake katika Israeli. 

[7]Na yule mtu kwamba hapendi kumtwaa mke wa nduguye, aende huyo mke wa nduguye langoni kwa wazee, akawaambie, Nduguye mume wangu yuakataa kumsimamishia nduguye jina katika Israeli, hataki kunitimizia yampasayo nduguye mume wangu. 

[8]Ndipo wamwite wazee wa mji wake waseme naye; naye akisimama na kusema, Sitaki mimi kumtwaa mwanamke huyu, 

[9]ndipo mke wa nduguye amkaribie mbele ya hao wazee, amvue kiatu chake mguuni mwake, na kumtemea mate ya uso; kisha atajibu yule mwanamke, aseme, Mume akataaye kumjengea nduguye nyumba yake na afanywe hivi. 

[10]Na jina lake katika Israeli liitwe, Nyumba ya mvuliwa kiatu. 

Halikadhalika tunapokuja kwenye agano jipya hatuoni pia agizo lolote la moja kwa moja linalokatazama ndugu kuoa mke wa ndugu yake aliyekufa…

Zaidi inasema mwanamke Yeyote anapokuwa mjane yupo huru kuolewa na ‘Yeyote’ amtakaye katika Bwana.. 

1 Wakorintho 7:39

[39]Mwanamke hufungwa maadamu mumewe yu hai, lakini ikiwa mumewe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye yote amtakaye; katika Bwana tu. 

Warumi 7:3

[3]Basi wakati awapo hai mumewe, kama akiwa na mume mwingine huitwa mzinzi. Ila mumewe akifa, amekuwa huru, hafungwi na sheria hiyo, hata yeye si mzinzi, ajapoolewa na mume mwingine. 

Hiyo ikimaanisha kuwa anaweza akawa huru kuolewa hata na ndugu wa kaka yake (aliyefariki)…

Lakini lazima tufahamu kuwa si kila jambo linalohalalishwa kibiblia linaweza likafaa katika mazingira yote au majira yote, yapo mambo mengine ya kuzingatia, mfano utamaduni wa mahali fulani..

Kwasababu Biblia bado inatuambia…

1 Wakorintho 10:23

[23]Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo. 

Kwa mfano kwa wayahudi ilikuwa ni tamaduni Watu kusalimiana kwa ‘busu’ la upendo. Lakini katika mazingira ya jamii zetu jambo kama hilo huleta ukakasi, au kutoa tafsiri nyingine hata kama nia sio mbaya..ndio maana tunaishia kipeana mikono, na ikizidi sana kukumbatiana kwa jinsia tu zinazofanana.

 

Vivyo hivyo katika jambo hili, kuoa mke wa ndugu yako aliyefariki, kijamii halina munyu ndani yake.

 

Hivyo twaweza sema kijamii halikubaliki, lakini kibiblia halijakatazwa..ukiniomba mimi ushauri nitakuambia usifanye hivyo..kaoe pengine..lakini ukimwoa mke wa ndugu yako aliyekufa pia hujafanya dhambi ikiwa tu, pana makubaliano kamili katika pande zote mbili, lakini pia wewe mwenye uwe haupo katika ndoa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> 

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NDOA NA IHESHIMIWE NA WATU WOTE.

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

https://wingulamashahidi.org/2019/08/31/bwana-yesu-alikuwa-anamaanisha-nini-kusema-marko-219%e2%80%b3walioalikwa-harusini-wawezaje-kufunga-maada

Print this post

Umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu

SWALI: Yule tajiri alimaanisha nini kumwambia Lazaro, achovye ncha ya kidole chake majini uuburudishe ulimi wake?

Luka 16:24

[24]Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.

JIBU:

Habari hiyo la Tajiri na Lazaro, Bwana Yesu aliieleza kufunua uhalisia wa jehanamu jinsi ulivyo… Na mambo ambayo mtu aliyeukataa wokovu atakutana nayo baada ya kifo.

Anaeleza jinsi yule tajiri alivyokufa katika hali ya dhambi..na hatimaye akajikuta mahali pale pa mateso, ambapo hakutana hata ndugu zake wafike, tunaona hata alipoomba mtu atokaye kwa wafu aende kuwahubiria ndugu zake akaambiwa hawatashawishwa…Ni kuonyesha kuwa mahali pale palikuwa pa mateso Sana, kiasi cha kutaka mwingine yeyote kufika.

Lakini tukio lingine tunaonyeshwa akimwomba Ibrahimu Amruhusu Lazaro achovye ncha ya kidole Chake majini amburudishe ulimi wake, nalo pia akaambiwa haiwezekaia kwasababu kuna kizuizi kikubwa Sana katikati yao.

Sasa swali linakuja tukio lile linamaana gani Je kiu kile ni halisi au ni ufunuo?.

Bwana Yesu alipokuja duniani.. aliona Dunia nzima ina Kiu kikubwa sana.. na hivyo inahitaji maji ya kuweza iponya.

Sasa maji inayohitaji sio haya ya mtoni..bali maji ya rohoni ambayo ni ya uzima, na mtu pekee awezayo kutoa hayo ni yeye mwenyewe..hakuwahi kutokea mtu aliyeweza kuyatoa.

Kama tunavyojua mwili ukikosa maji, mwishowe utakufa..Ndivyo ilivyokuwa sisi sote, hapo mwanzo kabla ya Kristo, Wote tulikuwa wafu kiroho..

Utauliza vipi kwa watakatifu wa kale kama akina Musa na Eliya?…Wale walikuwa wanaishi kwa ahadi ya Kristo, Hivyo walitii madhihirisho yake aliyokuwa akijifunua kwao kwa namna mbalimbali huku wakiiongejea ahadi kamili ya ukombozi ambayo alikuja kuikamilisha yeye mwenyewe (Yesu Kristo) alipofufuka Katika wafu..(waebrania 11)

Yeye mwenyewe Alisema..

Yohana 7:37-39

[37]Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.

[38]Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.

[39]Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.

Sasa kiu hii ni ya nini?

Ya maisha….

Tangu zamani mwanadamu amekuwa akitafuta ‘maisha’ ambayo hata sasa hajayapata…ndio maana wengi wanakimbilia kutafuta elimu, fedha na utajiri wakidhani kuwa ndio wamepata maisha, lakini hivyo vipo mbali sana na maisha …vitakufanya ule vizuri tu, unywe vizuri, ulale vizuri kama maandalizi ya heri ya kifo chako baadaye..kwasababu Haviwezi kukudumishia maisha.. vinapooza tu kiu..lakini haviondoi kiu.

Yesu amekuja kuondoa kiu.

Sasa watu Ambao watapuuzia kuyapokea maji hayo ambayo Yesu anatupa…wakifa Katika hali hiyo hiyo huko waendapo ni majuto makubwa.

Kwasababu watataka hata tone dogo la maji hawatapata…yaani kiwango kidogo tu cha neema ya uzima hawatapata…

Leo Yesu hatupi maji tu, kwa kipimo fulani bali anapanda kabisa chemchemi za maji ndani yetu Ambazo zinabubujika uzima wa milele.

Yohana 4:14

[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.

Madhara ya kukosa maji ya uzima si tu baada ya kufa…hata hapa Hapa duniani.. mtu ambaye hana Kristo rohoni anajulikana kama nchi kamena matokeo yake ni kuwa makao ya mapepo yanakuwa Ndani yake hata kama hujui..

Angalia Yesu alichokisema juu ya hilo.

Mathayo 12:43-45

[43]Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate.

[44]Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa.

[45]Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya.

Yanakwenda mahali pasipo na maji…yaani moyo ambao hauna Kristo ndani yake.

Ndugu…umeona hatari waliyonao wenye dhambi, hapa duniani na baada ya kifo?

Shetani asikupumbaze, tubu leo kwa kumpokea Bwana Yesu katika maisha yako ili upate ondoleo la dhambi zako haraka sana.

Hizi ni siku za mwisho, dunia hii inakwisha…vilevile hujui ni siku Gani utakufa…Acha kuchezea maisha yako, ukafanana na yule tajiri aliyekosa maji ya uzima angali akiwa hai.

Okoka leo..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Jehanamu ni nini?

MILANGO YA KUZIMU.

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Print this post

WALIKUWA WAKINUNUA NA KUUZA, WAKIOA NA KUOLEWA KAMA ISHARA YA KANISA !

Bwana Yesu alitutahadharisha kuwa karibia na kurudi kwake, tabia za watu zitabadilika na kukaribia kufanana na zile za watu wa Nuhu na Lutu.

Luka 17:26 “Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.

27 Walikuwa WAKILA NA KUNYWA, walikuwa WAKIOA NA KUOLEWA, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote.

28 Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa WAKILA NA KUNYWA, walikuwa WAKINUNUA NA KUUZA, wakipanda na kujenga;

29 lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote.

30 Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu”.

Sasa ishara hii ya watu kununua na kuuza,  kuoa  na kuolewa na kula na kunywa ilikuwa inalenga makundi mawili, kundi la kwanza ni WATU WASIOMJUA MUNGU, na kundi la pili ni WATU WANAOMJUA MUNGU, hetu tuanze tathmini ya kundi moja baada ya lingine.

       1. WATU WASIOMJUA MUNGU.

Kipindi cha Nuhu na Sodoma na Gomora walikuwa wakila kwa anasa, na kunywa kwa kulewa, na wakamsahau Mungu, lakini pia walikuwa wakioa na kuolewa kwa ndoa haramu (maana yake za watu waliocha waume zao au wake zao, au wa jinsia moja) vile vile walikuwa wakinunua vitu haramu na kuuza vitu haramu kwa njia zisizo halali, ikiwemo dhuluma na rushwa, na utapeli na wakamsahau Mungu, hivyo gharika ikawachukua wote.

Ndicho kinachoendelea sasa kwa watu wengi walio nje ya wokovu, rushwa ni kitu cha kawaida kwao, kuoana kiholela ni kitu cha kawaida, (yaani mtu kuoa/kuolewa leo na kesho kuachana na kwenda kuoa/kuolewa na mwingine ni jambo la kawaida), hali kadhalika kuhudhuria kwenye karamu za ulafi na kula bila kiasi pamoja na kulewa ni mambo ya kawaida kila mahali, ndio maana utaona Bar ni nyingi kila kona.

Lakini hiyo ni ishara kwa watu wasiomjua Mungu, ambayo kiuhalisia pia inatangaza kwamba tunaishi katika siku za mwisho, lakini hebu tuangalie kwa upande mwingine kwa watu wa Mungu (kanisa.)

     2. WATU WANAOMJUA MUNGU (Kanisa)

Utauliza je! Watu wanaomjua Mungu pia wanaangukia katika hili kundi la kula na kunywa, kuoa na kuolewa, kununua na kuuza?.. Jibu ni ndio!.. sasa labda utauliza ni kwa namna gani?.. hebu tusome maandiko yafuatayo..

Luka 14:16 “Akamwambia, Mtu mmoja alifanya karamu kubwa akaalika watu wengi,

17 akamtuma mtumwa wake saa ya chakula awaambie wale walioalikwa, Njoni, kwa kuwa vitu vyote vimekwisha kuwekwa tayari.

18 Wakaanza wote kutoa udhuru kwa nia moja. Wa kwanza alimwambia, NIMENUNUA SHAMBA, SHARTI NIENDE NIKALITAZAME; tafadhali unisamehe.

19 Mwingine akasema, Nimenunua ng’ombe jozi tano, ninakwenda kuwajaribu; tafadhali unisamehe.

20 Mwingine akasema, NIMEOA MKE, na kwa sababu hiyo siwezi kuja”

Nataka tuone huo udhuru hao watu walioutoa!.. Kumbuka hao ni waalikwa, maana yake watu wenye mahusiano na mwenye harusi, na huo ni mfano ambao Bwana aliutoa kuhusu karamu ya mwanakondoo itakayofanyika mbinguni baada ya unyakuo,

 Kwamba sasa anawaaalika watu, lakini waalikwa (yaani watu wanaomjua Mungu) wanatoa udhuru!, kwamba Nimeoa Mke, wengine nimenunua shamba sharti nikalitazame!.. Je huoni haya ndio yale yale Bwana aliyoyasema kwamba siku za mwisho watu watakuwa wakioa na kuolewa, na kununua na kuuza?

Kumbe ishara hii pia inatimia kwa watu wa Mungu!.. watu wasiomjua Mungu wao wataoana ndoa haramu, watanunua vitu haramu na kuuza kwa njia haramu.. lakini watu wa Mungu wataoa kihalali, na kununua na kuuza kihalali lakini watavifanya hivyo kuwa udhuru utakaowazuia kumsogelea MUNGU zaidi.

Hii ni hali halisi kabisa ya kanisa la leo!.. Asilimia kubwa ya tunaojiita wakristo, shughuli zimetusonga kiasi cha kuupunja muda wa Mungu, hatuombi tena kwasababu ya wingi wa kazi, hatuifanyi tena kazi ya Mungu kwasababu ya majukumu ya kifamilia na ndoa!, hatukusanyiki tena pamoja na wengine kwasababu ya mialiko mingi tuliyonayo ya kula na kunywa!..

Je unajua matokeo yake ni nini?.. Hebu tuendelee na mistari ile..

“20 Mwingine akasema, NIMEOA MKE, na kwa sababu hiyo siwezi kuja,

21 Yule mtumwa akaenda, akampa bwana wake habari ya mambo hayo. Basi, yule mwenye nyumba akakasirika, akamwambia mtumwa wake, Toka upesi, uende katika njia kuu na vichochoro vya mji, ukawalete hapa maskini, na vilema, na vipofu, na viwete.

22 Mtumwa akasema, Bwana, hayo uliyoagiza yamekwisha tendeka, na hata sasa ingaliko nafasi.

23 Bwana akamwambia mtumwa, Toka nje uende barabarani na mipakani, ukawashurutishe kuingia ndani, nyumba yangu ipate kujaa.

24 Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu”.

Matokeo yake ni kwamba Neema tuliyoipewa watapewa watu wengine , wote wenye kuwa na udhuru mwingi kwa Bwana wapo katika hatari ya kukosa kuingia mbinguni, wapo katika hatari ya kukumbana na gharika ya mwisho ya moto kulingana na Biblia.

Je wewe upo kundi gani?..  Unakula na kunywa kwa anasa au kihalali?, na kama kihalali je hiyo kwako ni udhuru wa kumtafuta Mungu?.. je wewe unanunua na kuuza kiharamu au kihalali?.. na kama ni kihalali je hiyo kwako ndio udhuru wa kutojitoa kwa Mungu?.. majibu yapo kwako na kwangu.

Bwana atusaidie tusiwe watu wa udhuru, bali tumtumikie Bwana kwa moyo wote, kwani hiyo ni amri tuliyopewa.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ISHARA YA KANISA LA LAODIKIA

Je mtu anaweza kubatizwa mara mbili?

Je tumepewa kujua nyakati na majira ya kurudi kwa Bwana au la?.

KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.

MGAWANYIKO WA ISHARA ZA UJIO WA BWANA YESU KRISTO.

Print this post

Yesu alimaanisha nini kusema ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’?

SWALI: Bwana Yesu alikuwa na maana gani kusema ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’.

Luka 13:33

[33]Pamoja na hayo imenipasa kushika njia yangu leo na kesho na kesho kutwa; kwa kuwa haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu.


JIBU: Bwana Yesu alikuwa anaeleza asili ya mji wa Yerusalemu nyakati zote ulivyokuwa wa mauaji, mji ambao ungepaswa uwe wa kupokea manabii wa Mungu, lakini kinyume chake uligeuka mji wa kuwaua Manabii…

Sasa kusema maneno yale ni kutokana na taarifa aliyoletewa na wale mafarisayo kuwa Herode anataka kumwangamiza, hivyo aondoke pale aende mji mwingine…ndipo Bwana Yesu akawaambia ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’ yaani haipaswi nabii afe nje ya Yerusalemu…

Akimaanisha nini?

Manabii wengi wa Mungu, waliuliwa pale pale Yerusalemu hivyo hata na yeye kuangamia hapo si jambo geni, …

Na ndivyo ilivyokuwa

Mfano wa hao katika maandiko alikuwa;

Zekaria mwana wa Yehoyada (2Nyakati 24:20-21). Ambaye aliuliwa hekaluni

Mwingine ni Uria nabii (Yeremia 26:20 – 24)

Na manabii wengine wengi ambao hawajatajwa, moja kwa moja katika maandiko waliuawa Yerusalemu…ndio sababu ya Yesu kusema maneno Haya;

Mathayo 23:37-39

[37]Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!

[38]Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa. 

[39]Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana. 

Jambo hili hujirudi sasa rohoni..

Watu wote ambao wanaipinga injili mioyoni mwao leo, hata kama hawajashiriki moja kwa moja kuwarushia mawe watu wa Mungu, ni shirika moja tu na wale waliokuwa wanawaua manabii wa Bwana zamani.

Ndivyo walivyodhani mafarisayo kwamba wenyewe hawahusiki na mauaji ya manabii wa Bwana, angali wanampinga yeye waziwazi, kwa unafiki wao aliwaambia maneno haya..

Mathayo 23:29-36

[29]Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki,

[30]na kusema, Kama sisi tungalikuwako zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao katika damu ya manabii.

[31]Hivi mwajishuhudia wenyewe, ya kwamba ninyi ni wana wao waliowaua manabii.

[32]Kijazeni basi kipimo cha baba zenu.

[33]Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum?

[34]Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji;

[35]hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu.

[36]Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.

Hii ni hatari kubwa sana kwa walio nje ya Kristo.

Mwamini Yesu leo uoshwe dhambi zako. Upokee uzima wa milele. Kwingineko si salama.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote (Yohana 16:23)

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

Kwanini MUNGU aangamize watoto kwenye gharika ya Nuhu?

Print this post

Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote (Yohana 16:23)

SWALI: Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote ’

Kwanini ajiangue kwa namna hiyo angali yeye ndiye mwokozi wa kutegemewa kila kitu?

Yohana 16:23

[23]Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.

JIBU:

Kama tunavyojua hakukuwahi kutokea kiongozi aliyekuwa na matokeo makubwa duniani kama Yesu Kristo.

Namna ya uongozi wake, Kwa jinsi ulivyokuwa thabiti na bora Matokeo yake ndio tunayoana mpaka sasa duniani kwenye imani.

Hivyo maisha yake na huduma yake sio tu vinatufundisha njia ya wokovu lakini pia vinatufundisha namna kiongozi bora anavyopaswa Awe.

Matokeo Ya mitume wake kuwa nguzo kwa makanisa ya vizazi vyote ni matokeo ya namna ambavyo alivyowakuza anawakuza.

Bwana Yesu hakutengeneza Wafuasi, bali alitengeneza watu kama Yeye…Na hivyo katika kuwafundisha wanafunzi wake aliwakuza Ki vitendo zaidi kuliko maneno ya vitabu vingi vya kidini na mapokeo.

Kwamfano utaona kuna mahali anawatuma wawili waenda kuhubiri injili mahali ambapo angepaswa kwenda yeye mwenyewe, lakini aliwaacha waende.

Luka 10:1

Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.

Mahali pengine aliwaacha watoe pepo na waliposhindwa hakusema ‘wanangu nyie ni wachanga, basi nitakuwa nawasaidia tu’…hapana Kinyume chake aliwakemea Kwa upungufu wa imani zao.

Vivyo hivyo katika tukio hili, wanafunzi wake walitarajia kila siku watakaa naye wamuulize maswali yeye, kisha awajibie kutoka kwa Baba.. Ni sawa na mtoto mchanga ambaye kila siku anasubiria atafuniwe tu chakula apewe…unadhani hilo litaendelea sana?

Vivyo hivyo hilo halikuwa lengo la Bwana Yesu, bali alitaka kuwafundisha kanuni za wao wenyewe kumuuliza Mungu na kujibiwa moja kwa moja kama yeye alivyokuwa anajibiwa…

Na njia moja wapo ilikuwa ni yeye kuondoka, kisha kwa kile kitendo cha wao kumkosa Bwana wa kumuuliza, wajifunze kuomba kisha Roho ajae ndani yao, ndipo waanze sasa kupokea mafunuo ya kweli na ujasiri kutoka kwa Mungu..

Lakini pia waombe jambo lolote kwa jina la Yesu, wapokee mahitaji yao. Na Kweli mambo hayo yalianza Kutokea baadaya ya Pentekoste.. wote walikuwa ni kama ‘Yesu-dunia’ hakuna hata mmoja alifikiri au kuwaza kwamba kuna umuhimu tena wa Yesu kutembea nao, kimwili bali waliweza kuyafanya yote.

Hiyo ni tabia ya kiongozi bora…huwafanya wanafunzi wake kuwa kama yeye, na wakati mwingine kutenda hata zaidi ya yeye…Yesu aliwainua zaidi kwa kusema.

Yohana 14:12

[12]Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.

Hiyo ndio sababu kwanini aliwaambia hayo maneno.

Yohana 16:23-24

[23]Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.

Hata sasa Bwana anataka kuona ukomavu kama huu ndani ya maisha ya wakristo wengi.. Ikiwa kila siku utakuwa unategemea Mchungaji wako akuombee, ni lini utaweza wewe mwenyewe kuomba na kuwaombea wengine? Sababu ya watu wengi kutojibiwa maombi yao na Mungu ni hiyo.. Ameshakomaa kiroho, Mungu anaona anaouwezo wa kupambana na tatizo yeye mwenyewe, atataka kiongozi wake amsaidie..

Hicho kitendo kinapunguza utendaji Kazi wa nguvu za Mungu, kwasababu yeye hataki tumgeuze mwanadamu Mungu..Ukiokoka, fahamu kuwa Roho Mtakatifu yupo ndani yako, na kuanzia huo wakati na kuendelea unawajibu wa kuufanyia mazoezi wokovu wako, jifunze kuomba mwenyewe, jifunze kuombea watu, soma biblia mwenyewe Mungu akufundishe..

Hizo ndio hatua bora za ukuaji kiroho.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUNA WAKATI YESU ATAPITA NA WATU HAWATAJUA.

TOFAUTISHA KATI YA MAFUNDISHO YA YESU, NA YA WAANDISHI.

ALITOKA HUKO, AKAENDA MAHALI KARIBU NA JANGWA.

Print this post

FAIDA NYINGINE YA MAOMBI YA KUSHUKURU.

Jambo jingine Kuu la kujifunza kama mkristo ni Kumshukuru Mungu kila wakati na kwa kila jambo, kwamaana maandiko ndivyo yanavyotufundisha..

1Wathesalonike 5:18 “shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu”.

Kuna mambo yanafunguka tu yenyewe baada ya kumshukuru Mungu!..haihitaji nguvu nyingi.. Maombi ya shukrani ni maombi yanayougusa moyo wa Mungu zaidi hata ya kupeleka mahitaji!, kwani ni yanauelezea uthamani wa Mungu katika maisha ya mtu, ni maombi ya kushuka sana na ya kuithaminisha kazi ya Mungu katika maisha yako au ya wengine, na hivyo ni maombi yenye nguvu sana na kuugusa moyo wa Mungu kuliko tunavyofikiri.

Na kiuhalisia maombi ya kushukuru ndiyo yanayopaswa kuwa maombi ya kwanza kabisa kabla haya yale ya toba na mahitaji..kwasababu, uzima tu ulionao ni sababu ya kwanza kumshukuru Mungu, kwasababu usingekuwa nao huo hata maombi mengine usingeweza kuomba..

Leo tuangalie faida moja ya kumshukuru Mungu, kwa kujifunza kupitia Bwana wetu YESU KRISTO.

Kama wewe ni msomaji wa Biblia utagundua kuwa kila wakati ambapo Bwana YESU alitaka kufanya MUUJIZA usio wa kawaida, alianza kwanza kwa kushukuru..

Kwamfano kipindi anaigawa ile mikate kwa watu elfu nne alianza kwanza kwa kushukuru..

Mathayo 15:33 “Wanafunzi wake wakamwambia, Tupate wapi mikate mingi hapa nyikani, hata kushibisha mkutano mkuu namna hii?

34 Yesu akawaambia, Mnayo mikate mingapi? Wakasema, Saba, na visamaki vichache.

35 Akawaagiza mkutano waketi chini;

36 akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, AKASHUKURU AKAVIMEGA, akawapa wanafunzi wake, nao wanafunzi wakawapa makutano.

37 Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate makanda saba, yamejaa”.

Pengine unaweza usione uzito wa shukrani katika huo muujiza wa mikate… hebu tusome mahali pengine palipoonesha kuwa ni SHUKRANI ya Bwana ndio iliyovuta ule muujiza mkuu wa mikate.

Yohana 6:23 “(Walakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia mpaka karibu na mahali pale walipokula mikate, WAKATI BWANA ALIPOSHUKURU)”..

Hapo anasema.. “wakati Bwana aliposhukuru”… Kumbe! Ile shukrani ilikuwa na maana kwa  sana kwa muujiza ule kutendeka.. Na wala pale hapaonyeshi kwamba Bwana YESU alimwomba Baba augawe ule mkate!.. la! Bali alishukuru tu kisha akaumega!, muujiza ukatendeka.

Kuna mambo mengine unahitaji kushukuru tu na kuendelea mbele!, na mambo yatajiweka sawa yenyewe, kuna nyakati hutahitaji kuomba sana.. bali kushukuru tu, na kumwachia Bwana..na maajabu yatatendeka..

Pia utaona kipindi kile kabla ya Bwana kumfufua Lazaro alianza kwanza kwa KUMSHUKURU MUNGU..

Yohana 11:39 “Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne.

40 Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?

41 Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, BABA, NAKUSHUKURU KWA KUWA UMENISIKIA.

42 Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma.

43 Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje.

44 Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake”.

Umeona? Ni shukrani tu, ndio iliyomtoa Lazaro kaburini..

Je na wewe unayo desturi ya kumshukuru Mungu?..  Maombi ya shukrani yanapaswa yale maombi marefu sana,  kwani tunazo sababu nyingi sana za kumshukuru Mungu, kama umeokoka, huo wokovu ulio nao ni sababu ya kumshukuru Mungu hata masaa sita mfululizo, kwasababu kama ungekufa kabla ya kuokoka leo ungekuwa wapi?.

Kama unapumua hiyo ni sababu ya kumshukuru Mungu, kwasababu wapo walioondoka na wengine ni wema kuliko hata mimi na wewe.

Na zaidi ya yote si tu kushukuru kwa mambo mema au mazuri Mungu anayokutendea, bali hata kwa yale ambayo yameenda kinyume na matarajio yako, ni lazima kushukuru, kwasababu hujui kwanini hiyo jambo limekuja kwa wakati huo, endapo Ayubu asingemshukuru Mungu kwa majaribu aliyokuwa anayapita zile Baraka zake mwishoni asingeziona.

Ni hivo hivyo mimi na wewe, hatuna budi kumshukuru Mungu kwa vyote, viwe vizuri au vibaya.. kwasababu tunajua mwisho wake utakuwa mzuri.

Yeremia 29:11 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UNAZO KILA SABABU ZA KUMSHUKURU MUNGU

Kwanini BWANA awaagize wakoma wakajionyeshe kwa Makuhani?(Luka 17:14

KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU. 

Maombi kama sehemu ya maisha ya mwamini mpya.

Nini maana ya Selahamalekothi?

Print this post