Swali: Biblia inasema tumeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, maana yake nini?
Jibu: Tusome.
Mwanzo 1:26 “Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. 27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.
Mwanzo 1:26 “Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.
Mfano wa Mungu, ni UTU WA NDANI, yaani vitu vyote vinavyopatikana ndani ya roho na nafsi ya mwanadamu, kama vile Furaha,upendo, amani, hasira, wivu, ghadhabu, huruma n.k. Huo ndio mfano wa Mungu, ndio maana utaona kama Mungu alivyo na hasira, mwanadamu naye ana hasira, kama Mungu alivyo na wivu, mwanadamu naye ana wivu, kama Mungu anavyotawala, mwanadamu naye anatawala n.k.. Hiyo yote ni kwasababu kaumbwa kwa mfano wa Mungu. Ndio maana biblia pia inawataja wateule wa Mungu kama miungu.
Yohana 10:34 “Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu?. Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka)”.
Lakini sura ya Mungu ni utu wa nje… yaani mwonekano wa nje kama macho, pua, mdomo, mikono, miguu, masikio n.k. Kwaufupi umbile la miili yetu ni nakala ya umbile la Mungu. Hii miili haikubuniwa tu, na tukapewa sisi, hapana!. Bali Mungu aliinakili kutoka katika umbo lake mwenyewe na mwonekano wake.
Na hilo umbo akalitengeneza kwa malighafi ya nyama, ndio likawa sisi… Lakini la kwake limetengenezwa kwa malighafi gani? Hakuna anayejua, lakini linafanana kimwonekano na miili yetu.
Ni sawa na ile midoli ya plastiki, inayoning’inizwa masokoni, ile imetengenezwa kwa sura ya mwanadamu…mwili wa mdoli ule ni malighafi yake ni plastiki na wa mwanadamu ni wa nyama, lakini kimwonekano inafanana, ingawa mwanadamu si mdoli.. Kadhalika na sisi tunafanana na Mungu kimwonekano, lakini malighafi iliyounda umbo lake hilo la kiroho, hakuna anayejua.
Kwahiyo sisi tumeumbwa kwa mfano kamili wa Mungu, Ndio maana sehemu nyingi Mungu anahubiri tufanane na yeye katika utu wetu wa ndani…kwasababu inawezekana kabisa sisi kufanana na yeye kwamaana katuumba kwa mfano wake. Kama yeye ni mwenye upendo, na sisi anataka tuwe na upendo wakati wote kama yeye, kwasababu, katuumba kwa mfano wake. Hawezi kututwika mzigo mzito ambao anajua hatutaweza kuubeba.. Kwahiyo alivyotuambia kwamba tuwe na upendo, na wakamilifu, anajua kabisa jambo hilo linawezekana kwetu, kwasababu sisi ni kama yeye..
Mathayo 5:48 “Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”
Wanyama hawajaumbwa kwa mfano wa Mungu ndio maana hawajaamriwa tuliyoamriwa sisi, kwasababu pengine yangekuwa ni juu ya uwezo wao,. Lakini sisi, mema yote yapo chini ya uwezo wetu endapo tukiamua… “Kuwa wakamilifu duniani na kufanana na Mungu inawezekana kwa asilimia zote”.(Zaburi 16:3).
Na hatuamui kwa midomo tu bali kwa vitendo, pale tunapotubu na kumpokea Roho Mtakatifu, hapo unashuka uwezo juu yetu wa kutugeuza kuwa kama Mungu,.. Ulikuwa unamchukia ndugu yako, sasa hiyo chuki inahama, badala ya kumchukia ndugu yako unakuwa unachukia dhambi, hivyo unakuwa kama Mungu. N.k
Bwana azidi kutubariki sote.
Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali. Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Muhtasari wa maelezo haya kwa njia ya video unaweza kuyapata hapa chini.
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya ‘Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu’ ?
Nguo za magunia katika biblia ni zipi?
Kikuku/vikuku ni nini katika biblia?
Nini maana ya “yasiyokuwapo hayahesabiki”(Mh 1:15)
THAWABU ZA SIRI, ZA WATAKATIFU MBINGUNI.
Rudi nyumbani
Print this post
SWALI: Watu ambao hawajasikia kabisa injili, halafu wakafa katika kutokujua chochote kuhusu Yesu, je wao huhesabika kuwa hawana dhambi? Kufuatana na andiko hili?
Yohana 15:22 “Kama nisingalikuja na kusema nao, wasingalikuwa na dhambi; lakini sasa hawana udhuru kwa dhambi yao”.
JIBU: Yesu hakumaanisha kuwa mtu yoyote ambaye hakusikia habari zake, kuwa hatahukumiwa kabisa hapana, bali alimaanisha kuwa watu wa namna hiyo hawatahukumiwa kwa maneno yake, bali watahukumiwa kwa kitu kingine..
Na ndio maana biblia inasema..
Warumi 2:11 “kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu. 12 Kwa kuwa wote waliokosa pasipo sheria watapotea pasipo sheria, na wote waliokosa, wenye sheria, watahukumiwa kwa sheria”.
Warumi 2:11 “kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu.
12 Kwa kuwa wote waliokosa pasipo sheria watapotea pasipo sheria, na wote waliokosa, wenye sheria, watahukumiwa kwa sheria”.
Unaona hapo anasema,..”waliokosa” pasipo sheria “watapotea” pasipo sheria, hasemi wataokolewa pasipo sheria, hapana bali watapotea..kwasababu walikosa katika mambo mengine, na ndio katika hayo hayo Mungu atawahukumia, lakini hatatumia ile sheria ya torati kuwahukumu, kwasababu hiyo hawakuijua hapo kwanza.
Ni vizuri tukafahamu kuwa kuna mambo ya asili ambayo Mungu kayaweka mioyoni mwa wanadamu wote, kiasi kwamba hata kama hajawahi kusikia sheria imekataza kuua, wao wenyewe hawataua, kwasababu wanajua ni makosa..Ukienda kwenye jamii za watu ambao wanaishi maporini hawajui utandawazi ni nini, hawajafikiwa na chochote, bado utawakuta na ustaarabu wao wa maisha na utakuta wamejiwekea mipaka ambayo wanajua kabisa yoyote atakayeivuka ni makosa.
Wanajua kabisa mwanaume kulala na mwanaume mwenzake ni makosa, wanajua, kuiba mali ya mwingine sio sawa, wanajua, kuwapiga wazazi wao ni vibaya, n.k.…hayo mambo hawahitaji kufundishwa na Mungu au mtu yeyote, ni sheria ambayo tayari ipo ndani ya mioyo yao.
Ukisoma tena sehemu nyingine utaona Bwana YESU anasema..
Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. 48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo”.
Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.
48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo”.
Unaona tena, anasema yeye asiyejua, lakini amefanya yastahiliyo mapigo atapigwa kidogo.. Kwahiyo, hakuna mwanadamu yoyote ambaye hataingia hukumuni, wote wataingia.
Lakini mbaya Zaidi itakuwa kwetu sisi ambao tumeshasikia habari za Kristo, lakini hatuzitendei kazi, tumeshasikia habari za wokovu wa msalaba lakini tunazipuuzia, sasa sisi tutahukumiwa kwa injili yake. Na adhabu yetu itakuwa ni kubwa sana, kuliko za watu ambao hawajawahi kabisa kusikia habari za Yesu.
Hivyo tuikwepe hukumu ya Mungu. Inatisha.
Shalom.
Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika? Ina maana gani?
Nini maana ya “Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati”
Maashera na Maashtorethi ni nini?
TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 6
Baadhi ya watu na misemo ambayo haipo katika biblia.
WhatsApp
Shetani anaweza kuwekwa mbali nasi au akaondoka mbele yetu kwa namna kuu tatu.
1) Kumfukuza ni kwa kumkemea:
Wakati mwingine shetani anatukaribia sana ili kutujaribu tuanguke katika dhambi. Na tusipokuwa makini atafanikiwa hivyo pindi tunapojikuta katika mazingira kama hayo hatua inayofuata ni kumfukuza kwa kumkemea kwa vinywa vyetu.
Bwana Yesu alimfukuza shetani mara nyingi, utaona kule jangwani, alimfukuza, akamwambia “Nenda zako shetani” Neno hilo linamaanisha ondoka hapa, ni sawa na kufukuzwa.. ndipo akamwacha baada ya kukemewa mfano asingemfukuza angefululiza kumjaribu tu pale..
Mathayo 4:8 “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, 9 akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia. 10 Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake 11 Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia.”.
Mathayo 4:8 “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake,
9 akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.
10 Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake
11 Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia.”.
Wakati mwingine alikuwa na Petro, shetani naye akamvaa ili alipindishe kusudi la Mungu juu yake.. Lakini utaona Bwana Yesu wakati ule ule alimkemea na kumwambia nenda nyuma yangu shetani kwani huyawazi yaliyo ya Mungu bali ya wanadamu.
Mathayo 16:22 “Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata. 23 Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu”.
Mathayo 16:22 “Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata.
23 Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu”.
Hata sisi, shetani anaweza kutusogelea kwa njia mbalimbali, hivyo hatuna budi kutumia vinywa vyetu kumkemea, pale pale. Wewe ni dada unaona mwanaume anakutongoza, anaanza kuzungumza na wewe mazungumzo ya kizinzi, hapo hapo unapaswa umkemee, lakini ukimwamwacha ataendelea hivyo hivyo na mwisho wa siku atakuvaa moja kwa moja kama alivyomvaa Yuda wakati ule. Na kitakachokuwa kimebakia kwako ni kujiua kiroho, kama sio kimwili kabisa.
Hivyo lazima tutumie vinywa vyetu kumfukuza shetani, tunapomwona anatusogelea sogelea, Kama vile tunavyotoa pepo, Kama alivyofanya Bwana.
2) Pili, ni kwa kumseta chini ya miguu yetu.
Njia hii ni tofauti kidogo na ile ya kwanza hapa, hutumii mdomo tena, bali unatumia matendo Zaidi.. Biblia inasema..
Warumi 16:19 “Maana utii wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya. 20 Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. [Amina.]
Warumi 16:19 “Maana utii wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya.
20 Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. [Amina.]
Unaona, unapokuwa mjinga katika kutenda mambo maovu, na mwenye hekima katika kutenda mambo mema, kidogo kidogo, unazipunguza nguvu za ibilisi kwa kiwango kikubwa sana juu yako, na baadaye Mungu anamseta chini ya miguu yako mara moja, kama tunavyojua kitu kikisha kaa chini ya miguu yako, hakina nguvu tena, hakina ujanja wowote, kimeshindwa…Unaweza kukifanya vyovyote vile unavyotaka
Vivyo hivyo na sisi tukiwa watu wa namna hiyo, kamwe shetani hatokaa atuweze, Kwa urefu wa somo hilo tutumie ujumbe inbox, tukutumie. Wakati mwingine shetani anakuwa mgumu kwetu kumshinda, kwasababu ya mienendo yetu isiyompendeza Mungu. Tunakuwa wepesi kukimbilia mambo maovu, na mambo ya Mungu tunakuwa wazito. Tukisikia kuna thamthilia Fulani imetoka, au series, tunakuwa wakwanza kuzifuatilia, lakini tu kufuatilia mafundisho ya biblia hilo hatuna muda nalo.. Kwa namna hiyo shetani atatusumbua sana.
Jaribu kuyaelekeza maisha yako kwa Mungu muda mrefu, utaona jinsi gani shetani anavyokuwa mwepesi kumshinda na hila zake, ni kwasababu tayari Mungu anakuwa ameshamseta chini ya miguu yako, hana nguvu yoyote ya kukushinda.
3) Na njia ya tatu ni ya kumfanya yeye mwenyewe kukimbia:
Hii ni ndo njia kuu, ukishaona mpaka adui yako anakukimbia kila akikuona anakula kona, basi ujue huo ni Zaidi ya ushindi, na kila utakapokwenda, yeye ndo anahama hapo kabla hujafika na sio wewe.. Sasa hapa ndipo tunapopaswa tupafikie watu wote.
Yakobo 4:6 “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu. 7 BASI MTIINI MUNGU. MPINGENI SHETANI, NAYE ATAWAKIMBIA”.
Yakobo 4:6 “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.
7 BASI MTIINI MUNGU. MPINGENI SHETANI, NAYE ATAWAKIMBIA”.
Unaona, ukimtii Mungu, ukinyenyekea chini ya Mungu, ukayashika maagizo yake, ukawa unazikataa kazi za shetani, Hapo hakuna kingine cha ziada Zaidi ya shetani mwenyewe kutafuta mahali pengine..
Anakukimbia kabisa, kama Wafilisti walivyomkimbia Daudi wakati ule anapigana na Goliathi. Sote tunapaswa tufikie hatua hii. Hakuna kumpa upenyo wowote, mpaka afikie hatua akituona akimbie mwenyewe.
Lakini hiyo itawezekana tukiwa watiifu kwa Mungu, na kuyapinga mawazo yake mara kwa mara.
Bwana akubariki.
Kumbuka hizi ni siku za mwisho. Na hilo shetani analijua, hivyo kajidhatiti kweli kweli, tena akiwa na ghadhabu nyingi biblia inatuambia hivyo (Ufunuo 12:12), ili akutafute mtu kama wewe ambaye hujaokoka, au hujasimama vema katika Imani. Swali ni je! Umeokoka? Je! Umebatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamwishwa katika maji mengi, na kwa jina la YESU KRISTO..
Kama hayo hayapo ndani yako, ndugu yangu, hutaweza kumfukuza shetani akujiapo, hutaweza kumseta chini ya miguu yako, apiginapo na wewe, na wala hataweza kukukimbia. Bali atakuvaa kama alivyofanya kwa Yuda, na mwishowe atakupeleka kukua kiroho kama sio kimwili kabisa.
Hivyo kama hujamkaribisha Yesu katika maisha yako, muda ndio huu, tubu, dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, kisha tafuta ubatizo sahihi wa kimaandiko, Na Bwana atakumiminia kipawa cha Roho Mtakatifu, ikiwa utahitaji ubatizo huo, basi wasiliana na sisi kwa namba hizo hapo chini.
Na Mungu akubariki.
ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.
JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.
MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.
INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.
MZUNGUKO WAKO NI UPI?
SWALI: Mtumishi wa Bwana napenda kufahamu Neno hili kwenye Isaya 41:14 kwanini Yakobo amefananishwa na mdudu?
JIBU: Tuanzie kusoma juu kidogo mstari wa 8 na kuendelea ili tupate picha nzuri Zaidi..
Isaya 41:8 “Nawe, Israeli, mtumishi wangu; Yakobo, niliyekuchagua; mzao wa Ibrahimu, rafiki yangu; 9 wewe niliyekushika toka miisho ya dunia, na kukuita toka pembe zake, nikikuambia, Wewe u mtumishi wangu; nimekuchagua wala sikukutupa; 10 usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu. 11 Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia. 12 Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako. 13 Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia. 14 USIOGOPE, YAKOBO ULIYE MDUDU, NANYI WATU WA ISRAELI; mimi nitakusaidia, asema Bwana, na mkombozi wako ni Mtakatifu wa Israeli. 15 Tazama, nitakufanya kuwa chombo kikali kipya cha kupuria, chenye meno; utaifikicha milima, na kuisaga; nawe utafanya vilima kuwa kama makapi. 16 Utawapepeta, na upepo utawapeperusha; upepo wa kisulisuli utawatawanya; nawe utamfurahia Bwana, utajitukuza katika Mtakatifu wa Israeli”.
Isaya 41:8 “Nawe, Israeli, mtumishi wangu; Yakobo, niliyekuchagua; mzao wa Ibrahimu, rafiki yangu;
9 wewe niliyekushika toka miisho ya dunia, na kukuita toka pembe zake, nikikuambia, Wewe u mtumishi wangu; nimekuchagua wala sikukutupa;
10 usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
11 Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia.
12 Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako.
13 Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia.
14 USIOGOPE, YAKOBO ULIYE MDUDU, NANYI WATU WA ISRAELI; mimi nitakusaidia, asema Bwana, na mkombozi wako ni Mtakatifu wa Israeli.
15 Tazama, nitakufanya kuwa chombo kikali kipya cha kupuria, chenye meno; utaifikicha milima, na kuisaga; nawe utafanya vilima kuwa kama makapi.
16 Utawapepeta, na upepo utawapeperusha; upepo wa kisulisuli utawatawanya; nawe utamfurahia Bwana, utajitukuza katika Mtakatifu wa Israeli”.
Kama tunavyoweza kuona hapo Mungu anawafananisha Israeli watu wake na wadudu, viumbe wanyonge wasio na uwezo wala nguvu yoyote ya kushindana, au kujitetea, tena mdudu anayezungumziwa hapo ni yule mnyoo, ambaye hawezi kutembea umbali mrefu, ni rahisi kukanyagwa, na kupotea,..
Hiyo ni kuonyesha kuwa watu waliochaguliwa na Mungu ni kama wadudu tu, masalia ya dunia, mabaki, watu wasiokuwa na kitu chochote cha kujivunia, , wasioweza kufanya lolote,
Kumbuka wakati Mungu anayazungumza hayo maneno taifa la Israeli wakati huo halikuwa taifa hodari sana kama mataifa mengine duniani, ulinganisha na Babeli au Misri, au Ashuru, au Tiro, au Sidoni, bali lilikuwa ni taifa la kawaida tu linyonge.
Lakini kwasababu lilimfanya Mungu kuwa tegemeo lao, ndio maana likaonekana kuwa ni tishio ulimwenguni kote,.Na mataifa yakawa yanaliogopa taifa hilo kwa jambo hilo tu moja la Mungu wao Yehova.
Sasa kulingana na vifungu hivyo tunaona Mungu akilifariji dhidi ya maadui zao ambao watakuja kukusanyika kupigana nao, na ndio hapo utaona akiwaambia japo wao ni kama wadudu tu, lakini atawafanya kuwa kama chombo kikali cha kupuria, chenye meno, ya kuisambaratisha milima mikubwa na kuisagasaga..(Mstari wa 15-16). Na sote tunajua jinsi Mungu alivyokuwa akilipigania taifa hili katika vita vigumu vilivyoshindakana
Na sisi pia, tukimfanya Mungu kuwa tegemeo letu, haijalishi tutakuwa ni dhaifu kiasi gani mbele za watu, tutakuwa ni wadudu wadogo kiasi gani, lakini tutaiangusha milima mikubwa, na mambo mengine yote ambayo hayawezekaniki. Lakini hiyo yote. Ni mpaka tumfanye Mungu kuwa kila kitu kwetu. Kama ilivyokuwa kwa Israeli.
Isaya 41:8 “Nawe, Israeli, mtumishi wangu; Yakobo, niliyekuchagua; mzao wa Ibrahimu, rafiki yangu;”
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Ni kwanini mifugo ya Yakobo iliongezeka kwa wingi kiasi kile?
Mataifa ni nini katika Biblia?
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 7 (Yeremia na Maombolezo)
Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?
SIKU YA TAABU YA YAKOBO.
Jibu: Katika agano la kale zilitolewa sadaka mbali mbali, na sadaka zote zilizotolewa zilikuwa ni lazima zifike madhabahuni pa Mungu, ili sadaka iitwe sadaka ni lazima ihusishe madhabahu. Isipohusisha madhabahu hiyo haiitwi tena sadaka bali mchango, au zawadi, au msaada. Lakini chochote kinachotolewa na kupelekwa kwenye madhabahu ya Mungu, hicho kinaitwa sadaka.
Sasa katika agano la kale, wana wa Israeli Bwana aliwaagiza wamtolee sadaka, kila mtu kwa hiari yake, na si kwa kulazimishwa..
Kutoka 35: 4 “Kisha Musa akanena na mkutano wote wa wana wa Israeli, akawaambia, Neno hili ndilo aliloliamuru Bwana, akisema, 5 Katwaeni kati yenu matoleo kwa Bwana; MTU AWAYE YOTE ALIYE NA MOYO WA KUPENDA, ayalete matoleo; dhahabu na fedha na shaba”
Kutoka 35: 4 “Kisha Musa akanena na mkutano wote wa wana wa Israeli, akawaambia, Neno hili ndilo aliloliamuru Bwana, akisema,
5 Katwaeni kati yenu matoleo kwa Bwana; MTU AWAYE YOTE ALIYE NA MOYO WA KUPENDA, ayalete matoleo; dhahabu na fedha na shaba”
Hapo Bwana anasema..“kila mwenye moyo wa kupenda” na sio kulazimishwa.. Maana yake kama mtu hajisikii kumtolea Mungu, basi halazimishwi, lakini atajipunguzia Baraka zake kutoka kwa Mungu.
Sasa katika agano la kale yalikuwepo makundi kadhaa ya sadaka, (yaani aina za sadaka watu walizokuwa wanamtolea Mungu). Zilikuwepo sadaka za Wanyama, kama vile Ng’ombe, Mbuzi, kondoo, na Njiwa, Hawa walikuwa wanaletwa Nyumbani kwa Mungu, na kuchinjwa, na kisha damu yao kutumika kufanya upatanisho, na baadhi ya viungo vya miili yao kuteketezwa juu ya madhabahu, na sehemu ya nyama iliyobakia isiyoteketezwa juu ya madhabahu, walikuwa wanapewa makuhani, pamoja na watoto wao..
Pamoja na hayo pia zilikuwepo sadaka za vyakula.. Ambapo watu walikuwa wanaleta nafaka zao kama sadaka kwa Mungu, Ndio hapo zinazaliwa sadaka za Unga na sadaka za vinywaji. Na katika makundi yote hayo ya sadaka, yote yalitolewa fungu la kumi, na malimbuko.
Sasa sadaka za unga, zilikuwa zikihusisha unga (wa ngano au shayiri) uliosagwa vizuri, na kisha kupelekwa kwenye madhabahu, huo unaweza kuwa kilo kadhaa, au pungufu kidogo, na mtu akishaupeleka, Kuhani anachukua kiwango kidogo cha huo unga, na kuuchanganya na ubani, na kisha kuuchoma huo unga pamoja na ubani ule..Na kiwango kingine cha unga kilichobakia kisichochomwa (ambacho kinakuwa ni kingi) wanapewa makuhani, kama riziki yao.
Walawi 2:1 “Na mtu atakapomtolea Bwana matoleo ya sadaka ya unga, matoleo yake yatakuwa ya unga mwembamba; naye ataumiminia mafuta, na kutia na ubani juu yake; 2 kisha atauleta kwa wana wa Haruni, hao makuhani; naye atatwaa konzi moja katika huo unga mwembamba, na katika mafuta yake, na huo ubani wote; kisha kuhani atauteketeza kuwa ndio ukumbusho wake juu ya madhabahu, ni kafara ya kusongezwa kwa njia ya moto, ya harufu ya kupendeza kwa Bwana; 3 na huo uliosalia wa ile sadaka ya unga utakuwa ni wa Haruni na wanawe; ni kitu kitakatifu sana katika sadaka zilizosongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto”.
Walawi 2:1 “Na mtu atakapomtolea Bwana matoleo ya sadaka ya unga, matoleo yake yatakuwa ya unga mwembamba; naye ataumiminia mafuta, na kutia na ubani juu yake;
2 kisha atauleta kwa wana wa Haruni, hao makuhani; naye atatwaa konzi moja katika huo unga mwembamba, na katika mafuta yake, na huo ubani wote; kisha kuhani atauteketeza kuwa ndio ukumbusho wake juu ya madhabahu, ni kafara ya kusongezwa kwa njia ya moto, ya harufu ya kupendeza kwa Bwana;
3 na huo uliosalia wa ile sadaka ya unga utakuwa ni wa Haruni na wanawe; ni kitu kitakatifu sana katika sadaka zilizosongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto”.
Na kama mtu atapenda asilete unga, bali alete unga uliokandwa tayari na kuokwa (Yaani mkate kamili), basi yalikuwepo maagizo ya jinsi ya kuuandaa huo unga (mkate), na kuuleta madhabahuni.. kwamba huo unga uliokandwa na kuokwa haupaswi kuwekwa hamira wala asali. (Walawi 2:4-11).
Mistari mingine inayozungumzia sadaka hiyo ya unga ni pamoja na Kutoka 29:40-41, Kutoka 30:9, Kutoka 40:29, Walawi 5:13, Walawi 6:15, Walawi 9:17, Walawi 14:10.
Na pamoja na kuwepo sadaka hiyo ya unga, ilikuwepo pia sadaka ya kinywaji ambayo ilikuwa inaambatana na hii ya unga, Isipokuwa katika sadaka ya kinywaji kilichokuwa kinatolewa ni Divai, (Kwasababu ndio kinywaji kilichokuwa cha gharama na heshima, kwa enzi hizo, na kwa tamaduni za kiyahudi), Na Divai haikutumika kwa matumizi ya ulevi, wala anasa,bali kwa matumizi matakatifu. (Kutoka 29:41)
Sasa sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji (Divai) zinafananishwa na mwili na damu ya Yesu. Kristo aliutoa mwili wake na damu yake kama sadaka, kwa ajili yetu..Na Mungu aliruhusu watu wamtolee sadaka hiyo ya unga na ya kinywaji katika agano la kale, kufunua mwili wa Yesu na damu yake katika agano jipya. Na pia aliruhusu makuhani wa agano la kale washiriki sehemu ya sadaka hiyo, kufunua “ushirika wa meza ya Bwana” kwa makuhani wa agano jipya.
Mathayo 26:26 “Nao walipokuwa wakila Yesu alitwaa mkate, akabariki, akaumega, akawapa wanafunzi wake, akasema, Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu 27 Akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, Nyweni nyote katika hiki; 28 kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi”.
Mathayo 26:26 “Nao walipokuwa wakila Yesu alitwaa mkate, akabariki, akaumega, akawapa wanafunzi wake, akasema, Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu
27 Akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, Nyweni nyote katika hiki;
28 kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi”.
Kwahiyo kama vile makuhani walivyoshiriki sehemu ya unga(mkate) na sehemu ya divai iliyokuwa inaletwa madhabahuni, vivyo hivyo na sisi pia tunashiriki mwili na damu ya Yesu, ili tuwe na sehemu katika madhabahu ya Bwana. Kwasababu wote tuliompokea Yesu, tunafananishwa na makuhani wa Bwana.
Ufunuo 1:5 “tena zitokazo kwa Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake, 6 NA KUTUFANYA KUWA UFALME, NA MAKUHANI KWA MUNGU, naye ni Baba yake; utukufu na ukuu una Yeye hata milele na milele. Amina”.
Ufunuo 1:5 “tena zitokazo kwa Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake,
6 NA KUTUFANYA KUWA UFALME, NA MAKUHANI KWA MUNGU, naye ni Baba yake; utukufu na ukuu una Yeye hata milele na milele. Amina”.
Hivyo kuna umuhimu mkubwa sana wa kuishiriki meza ya Bwana, kwa kila aliyemwamini Yesu, na kuishi katika Neno lake.
Yohana 6:53 “Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. 54 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. 55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli”.
Yohana 6:53 “Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.
54 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.
55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli”.
Kama hujajua namna ya kushiriki meza ya Bwana, na ungetamani kujua basi unaweza kutujuza kwenye box la maoni, chini kabisa mwa somo hili, ili tukutumie somo juu ya hilo kwa urefu.
Bwana atubariki.
Mafundisho mengine
MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.
Je tunapaswa tushiriki Meza ya Bwana mara ngapi?
NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?
JE! KUNA UMUHIMU WOWOTE WA KULIPA ZAKA?
ALIYOKUTANA NAYO YESU, YERIKO.
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima, karibu tujifunze maneno ya uzima, Leo tutaangalia juu ya wito, na jinsi unavyoweza kutofautiana kati ya mtu na mtu.
Tusome vifungu hivi,.
Mathayo 11:18 “Maana Yohana alikuja, hali wala hanywi, wakasema, Yuna pepo. 19 Mwana wa Adamu alikuja, akila na kunywa, wakasema, Mlafi huyu, na mlevi, rafiki yao watoza ushuru na wenye dhambi! Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa kazi zake”.
Mathayo 11:18 “Maana Yohana alikuja, hali wala hanywi, wakasema, Yuna pepo.
19 Mwana wa Adamu alikuja, akila na kunywa, wakasema, Mlafi huyu, na mlevi, rafiki yao watoza ushuru na wenye dhambi! Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa kazi zake”.
Kama tunavyojua Yohana mbatizaji, aliitwa kwa namna ya kitofauti sana, aliishi maisha ya kuwa mbali na watu kwa muda mrefu jangwani, na kama tunavyojua huko jangwani hakuna vyakula vizuri, au mavazi mazuri, biblia inasema chakula chake kilikuwa ni nzige, na asali basi!, hakujua juisi ya zabibu, wala supu ya makongoro, wala kuku, wala mayai, wala yogati, wala pizza, wala pilau, bali aliishi maisha ya kawaida kabisa, ya kula vyakula vya jangwani siku zote za maisha yake, na alikuwa na Amani katika maisha yale, wala hakuwa anaona kuna ugumu wowote au uzito wowote kuishi vile.
Vivyo hivyo na mavazi yake yalikuwa ya ngozi, magumu yasiyo na mvuto ..ndio maana Bwana aliwauliza wale watu..
Luka 7:24 “… Mlitoka kwenda nyikani kutazama nini? Unyasi ukitikiswa na upepo? 25 Lakini mlitoka kwenda kuona nini? Mtu aliyevikwa mavazi mororo? Jueni, watu wenye mavazi ya utukufu, wanaokula raha, wamo katika majumba ya kifalme”.
Luka 7:24 “… Mlitoka kwenda nyikani kutazama nini? Unyasi ukitikiswa na upepo?
25 Lakini mlitoka kwenda kuona nini? Mtu aliyevikwa mavazi mororo? Jueni, watu wenye mavazi ya utukufu, wanaokula raha, wamo katika majumba ya kifalme”.
Unaona? Lakini maisha hayo ya kuishi majangwani na ya kula mapanzi hayakuwa kanuni kwamba kila mtu ayaishi, na sio kwamba ukiyaishi wewe ndio yatakufanya uwe wa rohoni zaidi ya wengine hapana.. Tunamwona Bwana Yesu yeye alipokuja, biblia inasema alikuwa anakula na kunywa..
Yeye hakuishi jangwani kama Yohana mbatizaji, bali aliishi katikati ya watu, na alikuwa anahudhuria karamu nyingi , na sherehe mbalimbali alizoalikwa na watu wa kawaida pamoja na watu wakubwa kama vile mafarisayo na waandishi, na watoza ushuru. Kwa ufupi hakujizuia kula chochote kizuri alichokaribishwa..mpaka ikafikia hatua watu wengine wakamwona huyu mbona kama ni mlafi, na mlevi? Unaona..
Lakini alikuwa anaufahamu wito wake, na kusudi lake aliloitiwa hapa duniani, Na sote tunajua hakuna mwanadamu aliyewahi kuishi maisha makamilifu yasiyokuwa na dhambi kama Bwana Yesu.
Hata na sisi pia, wito wa Mungu unatofautiana kati ya mtu na mtu.. Lipo jambo Mungu anaweza akawa ameliweka ndani yako, na unaona kabisa ukilifanya katika hali hiyo, ndio litakupa Amani kuliko kufanya katika mazingira kama ya mtu mwingine, ukishaona hivyo wewe fanya bila kuwaangalia watu.
Kuna watu wameitwa katika hali ya uhuru, na kuna watu vilevile wameitwa katika hali ya utumwa biblia inasema hivyo..Ikiwa uliitwa kutumika ukiwa chini ya mamlaka fulani usione vibaya kuwa hivyo, mtumikie Mungu kwenye nafasi yako, kwa uaminifu, na ukalitimiza kusudi la Mungu vema tu, kama alivyofanya Nehemia, yeye alikuwa ni mnyweshaji wa mfalme, lakini kwasababu alijua nafasi yake na cheo chake alichopewa, alikuwa chachu kubwa ya kuikarabati upya Yerusalemu.
Lakini pia kama uliitwa katika hali ya uhuru, (sio chini ya mamlaka Fulani,) na unaona vema kutumika katika hali hiyo, basi mtumikie Mungu kwa bidii katika nafasi hiyo.
1Wakorintho 7:20 “Kila mtu na akae katika hali ile ile ambayo alikuwa nayo alipoitwa. 21 Je! Uliitwa u mtumwa? USIONE NI VIBAYA lakini kama ukiweza kuwa na uhuru, afadhali kuutumia. 22 Kwa maana yeye aliyeitwa katika Bwana hali ya utumwa, ni huru wa Bwana. Vivyo hivyo yeye naye aliyeitwa hali ya uhuru, ni mtumwa wa Kristo”.
1Wakorintho 7:20 “Kila mtu na akae katika hali ile ile ambayo alikuwa nayo alipoitwa.
21 Je! Uliitwa u mtumwa? USIONE NI VIBAYA lakini kama ukiweza kuwa na uhuru, afadhali kuutumia.
22 Kwa maana yeye aliyeitwa katika Bwana hali ya utumwa, ni huru wa Bwana. Vivyo hivyo yeye naye aliyeitwa hali ya uhuru, ni mtumwa wa Kristo”.
Vivyo hivyo kuna walioitwa kuoa/kuolewa, na wengine kutokuoa, au kutokuolewa.. Ikiwa wewe huoni shida yoyote kuishi maisha ya kuwa na mke au mume, endelea na wito wako huo huo, mtumikie Mungu, sio lazima uishi kama yule au wale.. Lakini pia ikiwa umeitwa katika kuoa, au kuoelewa, vilevile umtumikie Mungu kwa uaminifu katika nafasi hiyo.. usione ni vibaya.
1Wakorintho 7:27 “Je! Umefungwa kwa mke? Usitake kufunguliwa. Umefunguliwa? Usitafute mke. 28 Lakini, kama ukioa, huna hatia; wala mwanamwali akiolewa, hana hatia; lakini watu kama hao watakuwa na dhiki katika mwili nami nataka kuwazuilia hayo.
1Wakorintho 7:27 “Je! Umefungwa kwa mke? Usitake kufunguliwa. Umefunguliwa? Usitafute mke.
28 Lakini, kama ukioa, huna hatia; wala mwanamwali akiolewa, hana hatia; lakini watu kama hao watakuwa na dhiki katika mwili nami nataka kuwazuilia hayo.
Mathayo 19:11 “Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa. 12 Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumboni mwa mama zao; tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi; tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee”.
Mathayo 19:11 “Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa.
12 Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumboni mwa mama zao; tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi; tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee”.
Hivyo wito unatofautiana kati yetu sisi kwa sisi, usijilaumu sana kwanini haupo kama yule, au kama Fulani, au kwanini haufanani na Yohana mbatizaji, Zaidi tumia muda wako kutafuta mapenzi ya Mungu Katika nafasi uliyopo kama alivyofanya Nehemia, kisha uujenge ufalme wa Mungu. Kuna wengine wamebarikiwa ujuzi, kuna wengine mali, kuna wengine ulezi, kuna wengine karama n.k. Hakuna kiungo cha Kristo kinachoweza kukosa kabisa nafasi yake katika kanisa, ikiwa kitamaanisha kweli kumtumikia Mungu.
Hivyo tuanze sasa kujua nafasi za wito wetu, na tuzitumie, kuujenga ufalme wa mbinguni.
KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.
KUNA UMUHIMU WA KUWA MTU WA KURIDHIKA.
JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?
KWANINI MIMI?
UNYAKUO.
Bwana Yesu alisema..
Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako; 44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi, 45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki….. 48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.
Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki…..
48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.
Kumuombea anayekuudhi sio kitu kirahisi hata kidogo, huo ndio ukweli..afadhali ungeambiwa achana naye tu yapite, lakini unaagizwa umuombee, si jambo jepesi, Lakini hivyo ndivyo vipimo vya ukamilifu wa mtu kwa Mungu. Hakuna njia ya mkato.
Pale unapoona jirani yako anakuzungumzia vibaya, mpaka anakuharibia pengine siku yako, badala umchukie na kumwekea vinyongo, au umzungumze na wewe vibaya , unaambiwa na Yesu umuombee.. Ukishindwa kufanya hivyo, basi wewe bado hujawa na tabia kama za Mungu ndani yako, bado hujawa mkamilifu kulingana na maandiko.
Bwana Yesu alitoa, mfano hai akasema, hata Mungu mwenyewe, huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua yake waovu na wema..Kiasi kwamba mchawi anatoka kuwaloga watu usiku, na kuwasababishia matatizo, lakini asubuhi anaamka na mvua kwenye shamba lake, na linastawi vizuri sana , mpaka anavuna, na kuuza, na kupata chakula kwa ajili yake na watoto wake na cha akiba.
Jambazi, anatoka kuiba usiku na kuharibu, na akiamka asubuhi anakutana na jua kama wewe unavyoliona, sio kwamba Mungu anapendezwa na tabia zake, la, lakini anaonyesha rehema zake kwao pengine siku moja watatubu, na kuacha njia zao.
Na sisi pia kuna wakati tulishawahi kuwa waovu mbele za Mungu, kiasi kwamba ilikuwa ni haki ya Mungu atulipizie kisasi tuondoke chini ya jua, lakini mara nyingi tumeona hakufanya chochote, mpaka sasa tumetubu tumeokolewa, na tunamtumikia. Laiti kama asingekuwa mvumilivu kwetu, leo hii tungekuwa kwenye moto wa jehanumu.
Huo ndio ukamilifu wa Mungu, na yeye pia akatupa agizo hilo hilo kwamba tuwaombee wale wanaotuudhi, wale ambao tunawaona ni maadui zetu haswa haswa, tuwaombee, tusijifanye sisi ni washupavu sana, tunajua kupambana, tunajua kusimamia haki zetu, tukadhani kuwa mawazo ya Mungu ni kama ya kwetu, badala ya kuwaombea mema, tukaanza kuwaombea vifo, kuwaombea njaa, kuwaombea wasifanikiwe..n.k.
Mungu atahuzunishwa na sisi, na kutuona kama ni wachanga wa njia zake.
Kumbuka hatujaitwa kuwaiga wanadamu, bali tumeitwa kumuiga Mungu. Kama vile Yesu alivyosema,…
Yohana 5:19 “Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo ayatendayo Mwana vile vile”.
Haijalishi wanadamu wote watasema, wapige maadui zako. Lakini maneno ya Yesu ni tuwaombee. Hata kama yataonekana ni maombi magumu kwetu, lakini kwa Mungu ni manukato. Tujizoeshe kuwa watu na namna hiyo kila siku. Ndipo tutakapoona Mungu akituzidishia na sisi rehema zake kila siku.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).
SWALI: Kwanini Yoshua aliambiwa yeye ni kinga kilichotolewa motoni? Hichi kinga kilichotolewa motoni kina maana gani kibiblia?
JIBU: Kinga ni kama kijiti, hivyo inaposema kinga cha moto inamaanisha kijiti cha moto. Neno hilo utaliona sehemu kadha wa kadha katika biblia, na hususani wakati ule, Yoshua kuhani mkuu alipokuwa amesimama mbele za Mungu, na shetani naye amesimama pembeni yake kumshitaki, Lakini yule malaika aliyekuwa amesimama pembeni yake, aliyazungumza maneno haya;
Zekaria 3:1 “Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye.2 Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; JE! HIKI SI KINGA KILICHOTOLEWA MOTONI?3 Basi, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu sana, naye alikuwa akisimama mbele ya malaika.4 Naye huyo akajibu, akawaambia wale waliosimama mbele yake, akisema, Mvueni nguo hizi zenye uchafu. Kisha akamwambia yeye, Tazama, nimekuondolea uovu wako, nami nitakuvika mavazi ya thamani nyingi”.
Sasa ukisoma kwa ukaribu maneno hayo, utaona sio Yoshua anaambiwa yeye ni kinga kilichotolewa motoni, bali ni Yerusalemu ndio inayofananishwa na kinga kilichotolewa motoni.
Kama tunavyojua kipande chochote cha mbao kikiingia kwenye moto, huwa hakina namna ni lazima kiteketee tu, tofauti na vitu vingine kama chuma. Sasa kama kimetolewa motoni, inamaanisha kimenyakuliwa kutoka katika uharibifu uliokuwa unakila.
Hivyo Malaika wa Mungu alikuwa anamwambia shetani, kuwa Yerusalemu, ambayo Mungu alikuwa ameiteketeza ili ipotee kabisa milele, sasa ameihurumia na kuiokoa tena imsimamishie nyumba, na Yoshua huyu aliyesimama hapa ndiye atakuwa kuhani mkuu katika nyumba itakayojengwa Yerusalemu.
Israeli tangu ilipoasi Mungu aliiweka katika moto wa mfalme wa Babeli Nebukadreza, ili aingamize kabisa, Na ndio maana ukisoma Yeremia 29: 22 Utaona Mungu anatoa unabii kwa wale manabii wa uongo waliokuwa wanaitabiria Israeli habari za amani wakati hakuna amani, na kuwaambia kwamba huyu mfalme wa Babeli ndio atakuwa wa kwanza kuwaoka, hawa manabii katika moto.
Yeremia 29:22 “Tena katika habari zao laana itatumiwa na wafungwa wote wa Yuda, walioko Babeli, kusema, Bwana akufanye uwe kama Sedekia, na kama Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwaoka motoni”
Neno hilo utaliona tena, sehemu nyingine kwenye biblia ambapo Mungu aliiadhibu Israeli kwa mapigo ya kila namna, mfano wa Sodoma na Gomora, aliitia katika moto wa uharibifu, lakini baadhi yao aliowapa neema ya kuokoka hawakutambua kuwa wamenyakuliwa katika moto, kama vinga vilivyokuwa vinateketea, bali waliendelea kutenda maovu..
Amosi 4:7 “Tena nimeizuia mvua msiipate, ilipobaki miezi mitatu kabla ya mavuno; nami nimenyesha mvua juu ya mji mmoja, nikaizuia mvua isinyeshe juu ya mji mwingine; sehemu moja ilipata mvua, na sehemu isiyopata mvua ilikatika.8 Basi kutoka miji miwili mitatu walitanga-tanga kuendea mji mwingine wapate kunywa maji, wasipate ya kuwatosha; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.9 Nami nimewapiga kwa ukavu na koga; wingi wa bustani zenu na mashamba yenu ya mizabibu, na mitini yenu na mizeituni yenu imeliwa na tunutu; Lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.10 Nimewapelekea tauni, kama tauni ya Misri; vijana wenu nimewaua kwa upanga, na farasi wenu nimewachukulia mbali; nami nimeupandisha uvundo wa matuo yenu na kuuingiza katika mianzi ya pua zenu; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana. 11 Baadhi yenu nimewaangamiza, kama hapo MUNGU ALIPOIANGAMIZA SODOMA NA GOMORA, NANYI MKAWA KAMA KINGA KILICHONYAKULIWA MOTONI; LAKINI HAMKUNIRUDIA MIMI, ASEMA BWANA.
Amosi 4:7 “Tena nimeizuia mvua msiipate, ilipobaki miezi mitatu kabla ya mavuno; nami nimenyesha mvua juu ya mji mmoja, nikaizuia mvua isinyeshe juu ya mji mwingine; sehemu moja ilipata mvua, na sehemu isiyopata mvua ilikatika.8 Basi kutoka miji miwili mitatu walitanga-tanga kuendea mji mwingine wapate kunywa maji, wasipate ya kuwatosha; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.9 Nami nimewapiga kwa ukavu na koga; wingi wa bustani zenu na mashamba yenu ya mizabibu, na mitini yenu na mizeituni yenu imeliwa na tunutu; Lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.10 Nimewapelekea tauni, kama tauni ya Misri; vijana wenu nimewaua kwa upanga, na farasi wenu nimewachukulia mbali; nami nimeupandisha uvundo wa matuo yenu na kuuingiza katika mianzi ya pua zenu; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
11 Baadhi yenu nimewaangamiza, kama hapo MUNGU ALIPOIANGAMIZA SODOMA NA GOMORA, NANYI MKAWA KAMA KINGA KILICHONYAKULIWA MOTONI; LAKINI HAMKUNIRUDIA MIMI, ASEMA BWANA.
Soma pia Isaya 7:4
Hata sasa, dunia inapopitia katika majanga mengi ya maafa, lakini tukijiangalia sisi bado tupo hai, tujue kuwa ni Mungu anatutaka sisi tutubu, kama sio kwenda kumtumikia kama iliyokuwa kwa Yoshua.
Tunapoepushwa na matetemeko ya ardhi, vimbunga, magonjwa makali ya kuua kama hili la CORONA, tujue kuwa ni vinga vilivyo nyakuliwa motoni, tunapaswa tujue huu ni wakati wa kutubu na kumrudia Mungu wetu kwasababu ulimwengu upo motoni.
Lakini tukipuuzia tukajiona kama sisi ni wa kipekee sana, tujue kuwa tutakutana na adhabu kali Zaidi ya hizi tulizonazo sasa hivi. Mungu ni moto ulao.
Tuyatambue makosa yetu tumrudie Mungu.
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2
Nini maana ya uvuvio?.
Kuwatema farasi, maana yake ni nini?
UFUNUO: Mlango wa 15
Jibu: Tusome..
Waefeso 2: 20 “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni”.
Katika mstari huo yapo mambo makuu mawili ya kuzingatia kwa makini.
1) Msingi na 2) Mitume na manabii
Tukianza na Msingi.
Hapo anasema mmejengwa juu ya “Msingi” na si “misingi”. Maana yake ni msingi mmoja tu, na si mingi.. Na anaendelea kwa kusema..”mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”..na sio “mmejengwa juu ya mitume na manabii”.. Maana yake ni kwamba msingi waliokuwa nao mitume na manabii ndio sisi pia tunajengwa juu ya huo.. Mtu akisema “natembea juu ya misingi na kanuni za Baba yangu au babu yangu, hajamaanisha anatembea juu ya baba yake”..Bali juu ya kanuni na taratibu alizorithishwa na Baba yake, ambazo hata baba yake alikuwa anazifuata na kuziishi….Kadhalika na hapo, Neno la Mungu linasema, mmejengwa juu ya msingi wa Mitume na manabii, maana ya kuna msingi ambao Mitume na manabii walikuwa wanaiishi na kuifuata, na hatimaye wakairithisha kwa kizazi kinachofuata. Kwa misingi hiyo ndio sisi tunajengwa.
Sasa kabla ya kujua vizuri huo msingi ni nini, hebu tujue kwanza hawa Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapo ni wakina nani?..
Tofauti na inavyodhaniwa kwamba Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapo, ni kundi la manabii na Mitume wanaozuka leo… unakuta inatokea mtu fulani mahali fulani anayejiita Mtume au Nabii, anaanza kujigamba kwamba karama yake ndio karama kuu yakulijenga kanisa. Na kwamba yeye ndio msingi na kanisa, limejengwa juu yake. Jambo ambalo ni uongo, tena kwa asilimia zote.
Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapo ni Manabii wote wa agano la kale, na Mitume wa kanisa la kwanza wa agano jipya. Hao Msingi waliouweka na kuufuata ndio msingi sisi tunaojengwa juu ya huo na huo si mwingine zaidi ya biblia takatifu, ambapo ndio tunanukuu maneno kutoka huko. Ndio maana leo hii, msingi ni biblia takatifu, Maneno yaliyoandikwa na Mitume kama Paulo, Petro, Yohana, Yakobo n.k hayo ndio msingi wetu leo hii, ndio maana leo hatunukuu Neno la Nabii yeyote aliyepo leo, wala Mtume yeyote aliyepo leo na kulihubiri hilo, kana kama ni Neno la Mungu, badala yake tunanukuu maneno yaliyoandikwa na Mtume Paulo, au Nabii Isaya, au Nabii Yoeli n.k..Hao ndio mitume na manabii ambao tumejengwa juu ya msingi wao.
Kwahiyo mtu yeyote anayejiita mtume au nabii au mwalimu au muinjilisti, na anasema na kujivuna kwamba kanisa limejengwa juu yake, na kujivuna kwamba yeye ndio nguzo kuu, au karama yake ndio karama kuu…kwa kufuatia huo mstari, mtu huyo anadanganya aidha kwa kujua au kwa kutokujua.
Msingi wetu sisi ni biblia takatifu, ambayo imeandikwa na mitume wa Yesu na manabii wa agano la kale, hao ndio Mababa. Na kiini cha biblia takatifu ni YESU KRISTO. Vitabu vyote katika biblia vimebeba habari au unabii wa Yesu Kristo, hakuna kitabu hata kimoja kisichobeba ufunuo wa Yesu Kristo ndani ya biblia. Kwasababu yeye ndio Mungu mwenyewe katika Mwili. (1Timotheo 3:16).
1Wakoritho 3:11 “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo”.
Je umemwamini Yesu?, umepokea Roho Mtakatifu?..Kama bado mwamini leo na kumkabidhi maisha yako, naye atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu (Matendo 2:38)
Maran atha!
Je! Imani ya mitume ipo katika maandiko?
Mtume Paulo alikuwa na maana gani kusema katika 1Wakorintho 15:31″…NIKAKUFA KILA SIKU?
TUSIWE WATU WA KUPUNGUKIWA AKILI.
JINSI PAULO ALIVYOPAMBANA NA UJINGA WA ROHONI.
POPOBAWA NI KWELI YUPO?
Ukichunguza utaona Mungu kaweka vitu vingi vya asili katika mzunguko wake. Na kulikuwa na sababu maalumu wa yeye kufanya hivyo..
Mhubiri 1:6 “Upepo huvuma kusi, hugeuka kuwa kaskazi; hugeuka daima katika mwendo wake, na upepo huyarudia mazunguko yake. 7 Mito yote huingia baharini, walakini bahari haijai; HUKO IENDAKO MITO, NDIKO IRUDIKO TENA”.
Mhubiri 1:6 “Upepo huvuma kusi, hugeuka kuwa kaskazi; hugeuka daima katika mwendo wake, na upepo huyarudia mazunguko yake.
7 Mito yote huingia baharini, walakini bahari haijai; HUKO IENDAKO MITO, NDIKO IRUDIKO TENA”.
Hakushindwa kuufanya upepo upotelee tu huko hewani, au maji yapotelee tu ardhini, lakini ameamua kuyaweka katika mzunguko, kiasi kwamba hayo maji unayoyamwaga sasa hivi kwenye sinki, kuna wakati Fulani yatakurudia wewe na utayatumia tena.
Hiyo ni kufunua kuwa kuna mambo mengi ya rohoni yapo kwenye mzunguko wake, na tusipoitambua mizunguko hiyo, yatatupita mengi kama sio kupata hasara nyingi sana.
Lolote unalolifanya sasa hivi, liwe ni jema au baya, moja kwa moja linaingizwa katika mzunguko huu wa rohoni usioonekana. Kama ni baya litaondoka lakini siku moja litakurudia tu.. haijalishi litachukua umbile gani.
Kama ni jema vilevile litakurudia tu, haijalishi litachukua umbile gani baadaye.. Hivyo ni vizuri ukajua wewe upo katika mzunguko upi, Na ndio maana Bwana Yesu alisisitiza sana maneno haya.
Mathayo 7:12 “Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; …”.
Luka 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.
Ufunuo 13: 10 “Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga…”
Hizi ndio kanuni za asili ambazo mtu yeyote akizitumia hata kama sio mkristo, zitamletea majibu tu. Na ndio maana watu wengi wanashangaa kwanini mataifa yaliyoendelea yanazidi kutajirika, japokuwa hayamchi Mungu.
Ukiangalia utagundua kuwa yanatoa misaada mingi kila mwaka kwa mataifa maskini, na ndio maana yanazidishiwa.
Vilevile ukimpa Mungu, Ni kama vile umeingizwa kwenye mfumo wa mzunguko wa Baraka zake rohoni, pengine utaona kama umepoteza, lakini siku isiyokuwa na jina kitakurudia tu, kikiwa kimeshindiliwa na kusukwa sukwa, na kumwagika, kinaweza kisirudi kwa namna ile ile, lakini kitarudi kwa thamani ile ile tena mara dufu.
Mithali 11:25 “Nafsi ya mtu mkarimu itawandishwa; Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe”.
Lakini ukiwa mwovu, unaiba, unawarusha watu, unadhulumu haki za wengine, mchoyo, mbinafsi, unawachonganisha wengine, unaua, moja kwa moja unaingia katika mzunguko huo wa laana za waovu, na mwisho wa siku malipo yake yatakurudia kichwani pako ukiwa hapa hapa duniani, tena kwa kusukwa-sukwa na kuzidishiwa na kumwagika.
Mithali 11:31 “Tazama, mwenye haki atalipwa duniani; Basi mwovu na mkosaji si mara nyingi Zaidi”?
Kwa maneno hayo machache Mungu atufumbue macho yetu tuelewe tupo katika mzunguko upi. Ili tuishi maisha ya mafanikio hapa duniani.
Maran Atha.
HALI ZETU JINSI ZINAVYOWEZA KUATHIRI UTOAJI WETU.
KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1
Neno Bildi linamaanisha nini kwenye biblia(Matendo 27:28) ?
BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?
JE UPENDO WAKO UMEPOA?