Title February 2020

JE SALA YA ROZARI TAKATIFU NI YA KIMAANDIKO?

Historia fupi ya Rozari kama inavyosomwa na kanisa katoliki.(kulingana na wakatoliki inajulikana kama Rozari takatifu)

Rozari asili yake ni neno la kiingereza “rosary” lenye maana ya “bustani ya maua ya waridi”…Maua ya Rose kwa kiingereza ndio yanaitwa “waridi”..Kwahiyo bustani yake ndio inayoitwa rosary.

Katika sehemu za Ulaya kuna utaratibu wa kupelekeana maua hayo ya waridi ni kama ishara ya kuonyeshana upendo (Ingawa upendo halisi hauwakilishwi kwa maua)…

Hivyo yapo maua hayo ya waridi yaliyo ya rangi ya nyekundu na Nyeupe. Hivyo wakatoliki wanaamini kuwa Maria ni mama mtakatifu kwao, hivyo anastahili kupelekewa mfano wa ua hilo la waridi..na Hivyo sala ya rozari ndio kama ishara ya kumpelekea mama huyo ua hilo jeupe la Waridi kama ishara ya upendo wao kwake.

Sasa Historia ya hiyo sala ya rozari takatifu kwa wakatoliki ilianzia wapi?

Ilianzia karne ya 3 ambapo kulikuwa na watu wanaojulikana kama wahermiti kulingana na Wakatoliki. Watu hawa waliamua kuwa wanasoma kitabu cha Zaburi kila siku SURA ZOTE 150. Lakini baadaye wakazipunguza na kukusudia kusoma sura zote 150 kwa muda wa wiki moja.

Kwa kuwa walikuwa ni watu wasio na elimu, walitumia mbegu ndogo za mimea kuwakilisha kila zaburi moja wanayoisoma..Hivyo wakawa na mbegu 150, kwa idadi ya zaburi zote 150, hivyo kila walipokuwa wanamaliza kusoma zaburi moja waliweka mbegu moja katika kapu ili iweze kuwasaidia kujua wapo zaburi ya ngapi..n.k

Baadaye kulingana na kanisa katoliki, wanasema watu hao majirani zao walivutiwa na sala hiyo ya zaburi, na wao pia wakaanza sala kama hiyo lakini wakawa wanasali sala ya “Baba yetu uliye mbinguni” mara 150, badala hiyo ya Zaburi.

Baadaye tena wakabadilika na kuanza kutumia shanga 150 zilizopitishwa kwenye kamba badala ya vimbegu vidogo  vya mimea walivyokuwa wanavitumia hapo kabla.

Ilipofika karne ya 11 kadinali wa kikatoliki Mt. Peter Damiani, aliibadilisha sala hiyo kutoka katika kusali “Baba yetu uliye mbinguni” mara 150…Na kuwa “salamu Maria” mara 150.

Baadaye tena akatokea kiongozi mwingine wa kikatoliki akazigawanya hizo sala katika makundi 15..na kila baada ya salamu Maria 10 aliiweka Baba yetu uliye mbinguni…ikiwa vile vile kamba yenye vishanga 150.

Baada ya kipindi fulani tena wakavipunguza vile vishanga na kubakia vishanga 50 tu. Hivyo ndio mpaka leo wanasali rozari yenye vishanga hivyo 50.

Lakini Je jambo hilo ni  la kimaandiko?

Jibu ni la! Si la kimaandiko kwasababu hakuna sehemu yoyote katika maandiko tumeagizwa tusali sala ya “Salamu Maria”. Kwasababu Maria si mtu anayetuombea..yeye alishakufa, wafu wote hawana habari na mambo ya maisha yetu haya…..Anayetuombea ni mmoja tu biblia imemtaja ambaye ni ROHO MTAKATIFU.

Warumi 8:26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa”.

Umeona? ni Roho Mtakatifu na si Bikira Maria. Na Roho Mtakatifu hatumuombi atuombee na kusema “Salamu Roho Mtakatifu tunaomba utuombee”..hapana Roho Mtakatifu anatuombea pale na sisi tunapoomba..aidha kwa kunena kwa lugha au kwa maneno dhahiri..Yeye ni kama Mkalimani wetu mbele za Mungu. Mkalimani hawezi kuzungumza kama wewe huzungumzi.n.k

Hivyo sala yoyote inayohusisha kumwomba Mtakatifu fulani aliyekufa atuombee ni sala ya upotofu..inayowafumba watu macho na kuwafanya wawe wavivu wa kuomba wenyewe na kutamani  kila wakati kuombewa tu! Na mtu anayesali sala hiyo anamwabudu shetani bila yeye kujijua.

Hali kadhalika sala halisi inatoka ndani ya Moyo, na si desturi au utaratibu fulani au fomula fulani ya kufuata. Unapotumia mfumo fulani wa kuhesabu shanga na kutimiza idadi fulani ya maneno..hapo utakuwa husali chochote zaidi ya kutimiza wajibu tu..Na hatuendi kumwomba Mungu ili kutimiza wajibu..Mungu anataka ibada halisi inayotoka ndani ya moyo wa mtu hata kama itamchukua mtu maneno machache lakini maadamu imetoka katika moyo uliomiminika mbele zake..hiyo inathamani kubwa sana mbele za Mungu kuliko maneno elfu yasiyo na maana.

Ukitumia mfumo fulani bila kuomba kwa Roho ni sawa na umemwekea Mungu baba, nyimbo zilizorekodiwa katika kaseti azisikilize afurahi..Umeona? ukifanya hivyo ni kumdharau Mungu..anachotaka kutoka kwetu ni nyimbo zinazotoka ndani ya vinywa vyetu zinazotoka moyoni..na sio nyimbo zilizorekodiwa…Kadhalika na sala anataka zinazotoka mioyoni mwetu na si zinazojirudia rudia kama kaseti.

Hivyo kwa hitimisho..sala ya Rozari  si sala ya kimaandiko..Imebuniwa na Shetani, na lengo lake ni kuwaharibu watu kiroho. Hivyo kama upo huko ndugu..toka haraka sana!..Anza kumwabudu Mungu leo katika Roho na Kweli..Tupa hiyo rozari usiisali tena…umeshaujua ukweli, na pia washirikishe wengine wasiojua ukweli huu..

Hizi ni nyakati za mwisho shetani anatumia kila namna  kuwazuia watu wasiijue kweli. Na anawatumia watumishi wake ambao kwa nje wanaonekana ni watakatifu, wanaonekana ni watumishi wa Mungu kumbe ndani ni Mmbwa mwitu wakali.

Bwana akubariki sana.

Ikiwa bado hujaokoka na unatamani kuokoka basi hujachelewa..kumbuka kuokoka sio dini mpya..bali ni kitendo cha kumpokea Yesu maishani mwako na kufanyika kiumbe kipya..kumkiri kwamba yeye pekee ndiye njia ya kweli na mpatanishiwa wa Mungu na wanadamu. Ukimkiri namna hiyo na kudhamiria kuacha dhambi kwa vitendo na kujikana nafsi yako na kumfuata yeye…ataingia moyoni mwako na kukubadilisha na kukufanya kuwa kiumbe kipya. Hivyo tubu na baada ya kutubu nenda katafute ubatizo sahihi wa kimaandiko wa kuzamishwa katika maji tele (Yohana 3:23) na kwa Jina la Yesu Kristo.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!

UPAKO NI NINI?

SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?

LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?

Je! Bikira Maria ni MALKIA WA MBINGUNI?

JE BIKIRA MARIAMU ALIZAA WATOTO WENGINE?

Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mariamu Magdalene ni nani. Na hilo jina amelitolea wapi?

SWALI: Ndugu zangu Huyu Mariamu MAGDALENE ni nani?”..Je! Magdene ni jina la baba yake au ni Jina la ukoo wake?.


JIBU: 

Mariamu Magdalene( wengine wanamwita Magdalena) ni yule mwanamke ambaye tunamwona kwenye biblia akitolewa pepo saba na Bwana Yesu.. 

Luka 8:2 “na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,

3 na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao. “

Ni mwanamke aliyefuata na Bwana Yesu tangu huo wakati hadi mwisho wa huduma yake ambaye yeye pamoja na wenzake, ndio waliokuwa wanamuhudumia Bwana kwa mali zao. 

Mariam Magdalene tunamwona tena siku za mwisho mwisho kabisa kabla za  Bwana Yesu kupaa yeye ndiye aliyeagizwa  kwenda kuwaeleza wanafunzi wake juu ya kufufuka kwake.

Yohana 20:11 “Lakini Mariamu alikuwa akisimama karibu na kaburi, nje yake, analia. Basi akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi. 2

12 Akaona malaika wawili, wenye mavazi meupe, wameketi, mmoja kichwani na mmoja miguuni, hapo ulipolazwa mwili wake Yesu.

13 Nao wakamwambia, Mama, unalilia nini? Akawaambia, Kwa sababu wamemwondoa Bwana wangu, wala mimi sijui walikomweka.

14 Naye akiisha kusema hayo, akageuka nyuma, akamwona Yesu amesimama, asijue ya kuwa ni Yesu.

15 Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa.

16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu).

17 Yesu akamwambia. Usinishike; kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini enenda kwa ndugu zangu ukawaambie, Ninapaa kwenda kwa Baba yangu naye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu naye ni Mungu wenu.

18 Mariamu Magdalene akaenda, akawapasha wanafunzi habari ya kwamba, Nimemwona Bwana, na ya kwamba amemwambia hayo”.

Na kuhusu Hilo jina la Magdalene sio jina la baba yake, au la ukoo wake, Hapana aliitwa Mariamu Magdalene kuonyesha asili yake tu, ili kumtofautisha na Mariamu wengine kwenye biblia…Kumbuka hili jina Mariamu limetumika mara nyingi kwenye biblia..Hivyo ili kuwatofautisha hawa Mariam wote, huyu aliitwa mariamu Magdalene kuonyesha na Mariam aliyetokea huko mji wa MAGDALENE uliokuwa kando kando magharibi mwa bahari ya Galilaya huko Israeli. Lakini hilo sio jina la Baba yake au ukoo wake..Hapana ni jina la mji aliotokea.

Ni kama tu yule mwanamke Msamaria, hilo jina Msamaria sio jina la baba yake, hapana bali ni jina la mji anaotokea unaoitwa SAMARIA uliopo katikati ya Israeli.

Bwana akubariki.

Pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

RABONI!

JE BIKIRA MARIAMU ALIZAA WATOTO WENGINE?

Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

Je! ni vema kwa mkristo kwenda hospitali au kutumia miti shamba anapougua?

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

Tuwaonapo nzige wa jangwani ni nini tunajifunza?


Shalom.. Karibu tuongeze jambo lingine kuhusu ufalme wa mbinguni..

Bwana Yesu alipotuambia utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake…Alimaanisha kweli ufalme huo ili kuupata inahitaji kuutafuta…Lakini jambo ambalo hatujui pia ni kuwa ufalme huo haujafichwa katika mambo magumu sana, kiasi kwamba itatuhitaji tuwe na shahada kubwa za elimu, au maarifa makubwa kuzijua, badala yake siri hizo zimefichwa katika mambo madogo sana, na hayo ndiyo yanayofanya ufalme huo usionekane kirahisi..Mambo mepesi sana ambayo huwezi kutazamia kama kweli hapo ndipo siri za Mungu zilipo.

Kwa mfano embu tafakari Bwana Yesu alivyosema..Watafakarini Kunguru (Luka 12:24),..hawapandi, wala hawavuni, wala hawana maghala lakini baba yenu wa mbinguni anawalisha hao wote, je ninyi si Zaidi kuliko hao wote?. Ikiwa wewe unaishi Dar es alaam au sehemu za pwani utakuwa umeshakutana na kunguru wengi sana, lakini kama Bwana Yesu asingelizunguza hili neno, ungekuwa unaona kama ni viumbe vyenye kero Fulani, vinaishi mjini tu kuuchafua mji, lakini kumbe siri moja ya ufalme wa mbinguni ipo hapo, kiasi kwamba mtoto wa Mungu akiitumia basi, atafanikiwa sana,

Kama hujui ni mmoja wa ndege wachache sana wanaoishi miaka mingi, kunguru anaishi mpaka miaka 80, anaishi mjini mahali wanaposema Maisha magumu(vyuma vimekaza), na kila siku anakula, anakunywa! Sasa ni rahisi kusema kunguru ndivyo walivyoumbwa staili hiyo ya maisha..Lakini Bwana Yesu anasema..Je! wale wanachokipi cha kuwapita nyie mpaka waishi Maisha ya kutokujisumbukia kama yale?..

Ndugu kama wewe umekosa Imani ya maneno kama hayo ya Kristo, nataka nikuambie wapo wenzako wanaishi kwa Neno hilo na Bwana anawahudumia kwa kila kitu Zaidi hata ya kunguru, mmojawapo ni mimi, hakuna siku inayopita bila kuwa na ushuhuda mpya maishani mwangu…mpaka nimeshazizolea naziona ni kawaida tu..Lakini zamani nalipoanza tu kuliamini hili Neno, nilijaribu kumweleza mchungaji mmoja kulitokea utata mkubwa.. Haijalishi Tutajaribu kuleta tafsiri nyingine tuzijuazo lakini Maneno ya Yesu ni imara, yatathibitika milele na milele..Hayo ndio mambo marahisi ambayo Mungu anajifunua ndani yake, lakini yanadharauliwa na wengi.

Leo hii tunasikia tena kuna jambo limezuka la wadudu wanaojulikana kama NZIGE WA JANGWANI, sana sana katika ukanda wa Afrika Mashariki. Tupaswa pia tujiulize maswali Je! Tupowatazama hawa wadudu tunaona tu maafa na majanga au tunaona pia kitu kingine ndani yake?..

Lakini biblia inawataja nzige kama moja ya kiumbe vinne vyenye AKILI nyingi sana..

Soma..

Mithali 30:24 “Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo; Lakini vina akili nyingi sana.

25 Chungu ni watu wasio na nguvu; Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari.

26 Wibari ni watu dhaifu; Lakini hujifanyia nyumba katika miamba.

27 NZIGE HAWANA MFALME; LAKINI HUENDA WOTE PAMOJA VIKOSI VIKOSI.

28 Mjusi hushika kwa mikono yake; Lakini yumo majumbani mwa wafalme”.

Kama hujawahi kufuatilia tabia ya nzige hawa, basi fahamu kuwa hawana tofuati sana na nzige hawa wa kawaida tunaowaona ambao kila mmoja anajitegemea kivyake, tofauti ipo tu pale ambapo wameshakuwa wengi huwa wote wanabadilika tabia, wanajikusanya pamoja..kisha wakishajikusanya wanaanza kuruka katika wingi wao, kama kimbunga, ukitazama kwa mbali unaweza ukaona kama ni vumbi tu linakuja jinsi walivyo wengi, unaambiwa katika kilometa moja ya mraba, wapo nzige Zaidi ya milioni 150, na katika kimbunga hicho wapo Zaidi ya nzige bilioni 100, na wote hawa wanaruka pamoja.

kwa siku wanaweza kusafiri zaidi ya kilimeta 150, sasa licha ya wao kuwa wengi hivyo unaambiwa katika kuruka kwao na kupishana kwao wakiwa bado hivyo mabilioni kwa mabilioni huko juu, hawagongani wakiwa angani, wala hawagusani, japokuwa wanaruka karibu karibu sana..Hawana kiongozi wa kuwaweza katika mstari, na kuwasimamia na kuwaambia wewe pita hapa, au wewe pita kule, lakini wanayo akili ya hali ya juu, ya kuwafanya waruke kwa ustaarabu, wakiwa na anza moja, ya kuelekea upande mmoja..

Na ndio hiyo inayowafanya wafanikiwe kufika mbali wote wakiwa pamoja, wahame kutoka taifa moja hadi lingine wakiwa na idadi hiyo hiyo ya majeshi..Na kusababisha maafa makubwa sana ya mazao isiyoelezeka..

Embu fikiria kikundi kimoja kinachojaza eneo la kilometa moja ya mraba, kwa siku moja kinauwezo wa kutafuna mazao, yanayoweza kuliwa na watu elfu thelathini na tano (35,000) ..Na wenyewe wakivamia basi wanamaliza mamilioni ya Hektari za mraba.. Na ndio maana wanakuwa tishio sana kwa mataifa..Hawa ndio mfano wa wale walitumwa kuitafuna nchi yote ya Misri.

Sasa, kwanini Biblia inatuambia wanaakili nyingi..Ni kwasababu Mungu anataka ni sisi tupate hekima ndani yake ili tufanikiwe katika kumshinda adui..

Si mpango wa Mungu tangu zamani tuwe na viongozi juu yetu sisi wa kutuongoza..Wana wa Israeli walimwomba Mungu awape mfalme juu yao..Mungu alikasirishwa sana na mawazo yao, kwasababu Mungu alitamani wamtumikie yeye wakiwa na nia moja kila mmoja bila kushurutishwa na mtu Fulani wa pembeni..(Soma 1Samweli 8:1-22)

Leo hii na sisi, tukitaka ulimwengu huu, tumshinde Shetani, hatuhitaji mpaka tuambiwe na watu Fulani majukumu ya kufanya..Bali sote kwa pamoja kila mmoja kwa nafasi yake, na kwa karama Mungu aliyopewa anyanyuke kwa nguvu zake aishambulie kambi ya Adui shetani kwa kuihubiri injili, tusisibirie mpaka Mchungaji wetu atuambie hivi au vile, tusisubiri mpaka viongozi watushurutishe tutoke tukaifanye kazi ya Mungu…Kwa jinsi shetani anavyoaharibu hakuna mtu asiyejua kuwa huu ni wakati wa mapambano..

Sisi ikiwa kila mmoja atasimama kwa nafasi yake, kama vile HAWA NZIGE WA JANGWANI.. Tukatoka tukiwa na lengo moja la kumuharibu ibilisi na kazi zake zote..Basi tujie kuwa kuzimu itabakia kuwa gofu..shetani atapata hasara isiyokuwa ya kawaida..Watu watamkimbilia Kristo kwa namna isiyoelezeka…Na tukitoka wote kama Jeshi kiongozi wetu akiwa ni Roho Mtakatifu na si mtu, kamwe hatutapishana kauli, kamwe hatutagongana katika njia zetu kama jinsi hawa nzige kwa wingi wao wasivyogongana wakiwa angani..

Lakini hiyo yote ni mpaka mimi na wewe, kutokuongejea mpaka tupangiwe majukumu ya kufanya na mtu Fulani, au mhubiri Fulani, au mpaka kanisa litupangie majukumu..

Naamini katika wakati huu wa kumalizia, tutalitafakari na hilo, katika kazi ya ujenzi wa ufalme wa mbinguni..Bwana azidi kutupa neema yake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

UHURU WA ROHO.

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

SAA YA KUHARIBIWA IIJIAYO ULIMWENGU WOTE.

SIKU ILE NA SAA ILE.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU NA ZA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USHAURI KWA MWANAMKE WA KIKRISTO.

Mwanamke wa Kikristo unapaswa ujue nini?


Karibu tujifunze Biblia, ambayo ndiyo mwanga wa njia zetu na Taa iongozayo miguu yetu.

Ujumbe huu unakuhusu wewe binti wa Mungu ambaye pengine una bidii ya kumtafuta Mungu, karibu leo tujifunze baadhi ya mambo ambayo yatakusaidia katika safari yako ya imani, na yatakayokuongezea maarifa ya kutosha ya namna ya kutembea na Mungu kwa jinsi anavyotaka wewe utembee naye.

Jambo la kwanza la kuzingatia binti wa Mungu usomapo biblia…usikimbilie kusoma habari za wanaume kama wakina Musa, Daudi, Ezekieli, Yohana au Paulo…Ni vizuri kusoma hayo yote!..lakini nataka nikuambie kwamba ukikimbilia kusoma habari za hao bila kusoma kwanza habari za wanawake wenzako kama wewe katika maandiko hakika nakuambia utakuwa umeukwepa msingi mkubwa sana na wa muhimu katika maisha yako.

Kabla ya kutaka kujifunza habari za Daudi na Ushujaa wake…Hebu ingia ndani kwanza kajifunze habari za bibi yake Daudi aliyeitwa RUTHU, ni jinsi gani alimpendeza Mungu..kayasome maisha yake na kajifunze habari zake kwa mapana na marefu jinsi alivyoishi na wakwe zake na jinsi alivyompendeza mumewe Boazi..Ikiwezekana kamata kalamu na karatasi zinakili zile points zote, zishike hizo na kuziishi ndizo zitakazokusaidia sana kuwa mwanamke unayeishi kwa kumpendeza Mungu kuliko kujifunza habari za ushujaa wa Daudi. Ushujaa wa Daudi kwako wewe mwanamke hauna manufaa sana kwako zaidi ya ushujaa wa Ruthu bibi yake Daudi, au ushujaa wa Abigaeli mkewe Daudi.

Kabla ya kujifunza kwa kina habari za Daudi jinsi alivyomwangusha Goliathi..hebu kajifunze kwanza habari za Abigaili mke wa Daudi jinsi alivyomzuia Daudi kwenda kumwaga damu, kajifunze kwanza jinsi Abigaili alivyomnyenyekea Daudi…ziige hizo tabia kwanza za mke wa Daudi, kabla ya kwenda kuziiga za Daudi.(1Samweli 25:2)

Hali kadhalika kabla ya kwenda kujifunza juu ya Imani ya Ibrahimu..Hebu kwanza jikite kumsoma kwa undani SARA!..Zitafute siri za mafanikio za Sara kabla ya kutamani kuzitafuta za Ibrahimu..za Ibrahimu hazitakusaidia sana wewe mwanamke zaidi ya za Sara..Ibrahimu aliambiwa akatahiriwe na asingefanya hivyo alikuwa anakwenda kinyume na maagizo ya Mungu sasa wewe Tohara inakusaidia nini, hayo maagizo yanakufundisha nini wewe?…Lakini ukijiingia ndani kujifunza Jinsi gani Sara alimpendeza Mungu..ukazijua siri zote za maisha ya Sara hakika hutabaki kama ulivyo, na shetani hatakaa akuweze kamwe kama alivyowashindwa wakina Sara.

Sara alifikia hatua ya kumweshimu mumewe mpaka akafikia hatua ya kumuita mumewe “Bwana” (kasome 1Petro 3:6)..Hebu na wewe iga kwanza hayo mazuri ya Sara kabla ya kukimbilia kutamani mazuri ya Ibrahimu.

Vivyo hivyo kabla ya kukimbilia kujifunza juu ya Petro, Yohana au Mathayo wanafunzi wa Bwana Yesu..hebu tenga muda kwanza kujifunza juu la kundi lingine la waliomfuata Yesu kwa bidii mfano wakina (Mariamu Magdalene, Susana, wakina Martha na Miriamu)…Ingia ndani kujifunza maisha ya hawa wanawake watakatifu ni jinsi gani walivyompendeza Mungu…usikimbilie kujifunza juu ya Mitume jinsi walivyokuwa hodari wa kwenda vijiji na vijiji kuhubiri…hayo hayatakusaidia sana zaidi ya kujifunza juu ya wanawake wakina Susana walivyomhudumia Bwana kwa mali zao..Hawakuwa miongoni mwa waliotumwa na Bwana kuzunguka huko na huko…. lakini sehemu kubwa ya Huduma ya Bwana michango ilitoka kwa hawa wanawake watakatifu.. Hilo ndio Jeshi kubwa linalomtumika Bwana!!

Luka 8:1 “Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu; na wale Thenashara walikuwa pamoja naye,

2 na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,

3 na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, NA WENGINE WENGI, WALIOKUWA WAKIMHUDUMIA KWA MALI ZAO”.

Kabla ya kujifunza mazuri ya Tajiri Zakayo jinsi alivyomkaribisha Bwana nyumbani kwake na kutoa zaidi ya Nusu ya mali zake na kuwapa masikini(Luka 19:1-8)…Hebu kajifunze kwanza juu ya Martha jinsi alivyomkaribisha Bwana nyumbani kwake na akatoa Marhamu ya Nardo safi yenye thamani nyingi akampaka Yesu miguuni..na wala hakwenda kuiuza na kuwapa maskini kama ambavyo angefanya Zakayo…Na hiyo ikamsababisha kumpendeza Yesu zaidi ya alivyofanya Zakayo.(Yohana 12:1-7). Kajifunze ni kwanini alifanya vile Martha na wewe ukafanye vilevile…

Usitangulie kujifunza juu ya mazingira Bwana Yesu aliyowatokea Mitume wake 12..shughulika sana kujifunza juu ya mazingira aliyowatokea wale wanawake walio mashujaa wa Imani..Hata hivyo Pamoja na Utume waliokuwa nao wakina Petro lakini hawakuwa wa kwanza kujua kwamba Bwana amefufuka..badala yake ni wale wanawake watakatifu ndio walioifunua siri hiyo wa kwanza ya kufufuka kwa Bwana.. Mariamu ni mwanamke wa kikristo aliyekaa katika nafasi yake na ndiye aliyekuwa wa kwanza kujua kwamba mwokozi anazaliwa ulimwenguni na Zaidi ya yote yeye ndiye aliyempokea..ni wanawake hao hao ndio waliokuwa wa kwanza kujua Mwokozi hayupo kaburini yu hai!….Huoni kama kuna siri kubwa sana hapo?…hata kuja kwa pili kwa Kristo si ajabu baadhi ya wanawake watakatifu ndio watakaokuwa wakwaza kujua…sasa kwanini leo unaikimbia nafasi yako wewe mwanamke wa kikristo??…Unataka kuwa PETRO?

Na wanawake wengine wote katika biblia ambao walikuwa ni mashujaa wa Imani.. kajifunze kwao kabla ya kwenda kujifunza juu ya mashujaa wa Imani wa kiume..kajifunze jinsi walivyovaa, kajifunze jinsi walivyojisitiri…kajifunze juu ya akina Debora jinsi alivyokuwa mnyenyekevu kwa Baraka na Israeli yote, kajifunze juu ya akina Hana, Rahabu, Dorkasi, Esta na wengineo wengi.

Nenda pia kasome, Waraka ule wa pili wa Yohana ambao uliandikwa kwa mama yule mteule jinsi alivyowalea Watoto wake na kuwatunza, mpaka wakakaa katika hiyo kweli, na sifa zake zikavuma katikati ya mitume wa Kristo, na kuaswa kuwa asiyaache matendo yake, bali aipokee thawabu tilimlifu..

Halidhalika, kasome maandiko yanayowazungumzia wanawake wengi, tabia zao mbaya ujiepushe nazo..Na moja ya tabia ambayo imendikwa ni ile ya Udadisi (Au kwa lugha ya kisasa umbea/usengenyaji) soma 1Timotheo 5:13. Itakufaa Zaidi kuliko mambo mengi unayoyasoma katika biblia..

Vivyo hivyo katika makosa usikimbilie kujifunza makosa ya wanaume wa kwenye biblia…kwamfano kosa la Daudi kulala na mke wa Uria sehemu yako ipo wewe kama mwanamke?..au linakufundisha nini?…zaidi somo lile linawafaa wanaume…Wewe kajifunze jinsi wanawake kama YEZEBELI walivyomchukiza Mungu..kajifunze ni tabia gani alizokuwa nazo mwanamke Yezebeli zilizomfanya Mungu amchukue…Yezebeli alikuwa ni mchawi, muuaji na mwanamke anayejipamba uso….Ni mwanamke pekee aliyekuwa anapaka uwanja machoni ndani ya Biblia nzima hakuna aliyekuwa kama yeye..(kasome 2Wafalme 9:30), vivyo hivyo kajifunze kwa wanawake waliofanya makosa kama Mke wa Luthu, makosa yale na wewe usiyafanye, Mke wa Ayubu…kajifunze wanawake wengine waliofanya makosa kama Yule mke wa Ahasuero aliyeitwa Vashti, ambaye alikuwa na kiburi hamweshimu mume wake, kisa tu yeye ni mzuri mpaka kusababisha nafasi yake kuchukuliwa na mwanamke mwenye adabu kama Esta. Jifunze juu ya viburi vya hao vilipowafikisha kabla ya kujifunza juu ya kiburi cha mwanamume Kora aliyemdharau Musa mtumishi wa Mungu.

Bwana akubariki sana…Naamini kwa hayo machache pamoja na mengine mengi Bwana atakayokufunulia utapiga hatua moja katika kuyatenda mapenzi ya Mungu, Ewe mwanamke wa kikristo.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

EWE MKE! HESHIMA YAKO IPO KWA WAKWE ZAKO.

RABONI!

MARIAMU AKUTANA NA ELISABETI.

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

Je! Mungu anaupendeleo kwa wanaume zaidi ya wanawake?

CHAPA YA MNYAMA

Rudi Nyumbani:

Print this post

EWE MKE! HESHIMA YAKO IPO KWA WAKWE ZAKO.

Heshima na Baraka za mwanamke uliyeolewa zipo kwa wakwe zako (hususani mama mkwe wako).

Vitabu viwili vikuu vilivyoitwa kwa majina ya wanawake ni Esta, na Ruthu. Vimeitwa hivyo sio kwasababu tu Mungu anataka kupitisha ujumbe wake wa wokovu kwa kanisa, lakini pia upo ujumbe mahususi unaowahusu wanawake.

Leo tutamtazama Ruthu kwa maneno machache sana. Wanawake wengi wanapitia mikwaruzo katika ndoa zao, na kikubwa ni saikolojia wanayojijengea kabla na baada ya kuolewa kwao, kuhusu wakwe zao, hususani mama-mkwe..Na hapo ndipo panapokuwa chanzo cha matatizo yote…Wanawake wengi wanaoniuliza juu ya matatizo ya ndoa zao, nimegundua kuwa asilimia kubwa hawana mahusiano mazuri na wakwe zao.

Nataka nikuambie ulipokuwa hujaolewa Baraka zako zilikuwa kwa wazazi wako waliokuzaa, lakini unapoolewa ujue kuwa Baraka za ndoa na za uzao wako zinahamia kwa wakwe zako haijalishi ni wabaya kiasi gani..

Kama tunavyofahamu habari ya Ruthu, na Orpa, wote hawa wawili waliolewa na watoto wa Naomi mkwe wao, lakini kwa bahati mbaya, Naomi akafiwa na mume wake na watoto wake wote wawili akabakia kuwa mjane, hivyo akawa hana mume wala mtoto wala mjukuu,..Lakini Naomi kwa ukarimu wake akawatangazia uhuru wakwe zake, warudi makwao kila mmoja akaolewe tena kwasababu bado walikuwa ni vijana na pia bado hawajazaa..Orpa akakubali kuondoa kurudi kwao, lakini Ruthu hakukubali kwasababu alijua Baraka zake zipo wapi…

Hivyo akaamua kurudi na mkwe wake nchi ya Israeli, akajitoa tu kama wakfu kuwa kama mjakazi wake, walipofika wakaishi pamoja,Na Ruthu akawa anamtumika mkwe wake kama mtoto wake kwa amani tu..Ruthu aliipoteza nafsi yake, ili tu amrudhishe mama mkwe wake, lakini alijua ndani yake haitakuwa bure kuwa vile.

Lakini kama tunavyojua, ni nini kilifuata baadaye..Licha tu ya Ruthu kuolewa na Yule tajiri Boazi ndugu yake Naomi, lakini watu wote walimwona kuwa anastahili kuliko watoto 7 wa Naomi..

Ruthu 4: 13 “Basi Boazi akamtwaa Ruthu, naye akawa mke wake; naye akaingia kwake, na Bwana akamjalia kuchukua mimba, naye akazaa mtoto wa kiume.

14 Nao wale wanawake wakamwambia Naomi, Na ahimidiwe Bwana, asiyekuacha leo hali huna wa jamaa aliye karibu; jina lake huyu na liwe kuu katika Israeli.

15 Naye atakurejezea uhai wako, na kukuangalia katika uzee wako; kwa maana mkweo, ambaye akupenda, NAYE ANAKUFAA KULIKO WATOTO SABA, ndiye aliyemzaa.

16 Basi Naomi akamtwaa yule mtoto, akamweka kifuani pake, akawa mlezi wake”.

Embu jiulize wewe mwanamke uliyeolewa, Je, mkwe wako alishawahi kukuona unastahili kuliko watoto wake wote alionao?.. Alishawahi kujivunia kwako kwa namna hiyo? Kama hakuna chochote alichowahi kujivunia kwako, lipo tatizo.

Na kama hiyo haitoshi, Ruthu ambaye alikuwa ni mwanamke wa kimataifa, akahesabiwa katika uzao wa Kiyahudi kama vile Rahabu alivyohesabiwa kwa tendo lake tu hilo , na huko huko baadaye ndipo alipokuja kutokea Mfalme Daudi.. Uzao wa kifalme na uzao wa Bwana wetu Yesu Kristo.

Jaribu kufikiria tena jinsi uzao wake ulivyobarikiwa zaidi hata ya wanawake wengi wa kiebrania waliozaliwa na Ibrahimu…Na hiyo yote siri ilikuwa kwa MAMA MKWE WAKE na si penginepo. Ni yeye tu na Esta ndio waliopata nafasi ya vitabu vyao kuandikwa majina yao.

Hata wewe mwanamke uliyeolewa au unayekwenda kuolewa.. Timiza jukumu lako la kuwapenda wakwe zako kwasababu huko ndipo uzao wako utakapobarikiwa na ndipo ndoa yako itakapokuwa na amani..

Wewe kama siku zote huna habari na wakwe zako, unawasengenya, huwahudumii, huwaheshimu, unagombana nao, unawapenda kinafki tu, unafanya ili kutimiza wajibu tu, lakini hujitoi kwao, unaifikiria familia yako tu na ndugu zako…usitazamie kuwa Utabarikiwa uzao wako.

Biblia inakupa fundisho, litii ulifuate , watu wengi wenye matatizo ya ndoa huwa chimbuko ni hapo, pasipo hata wao kujua. Ikiwa humpendi mama wa mume wako, na usimpende na mume wako pia, lakini kama unampenda mume wako basi mpende na mama yake na ndugu zake ndipo utakapoishi kwa rah ana amani katika familia yako. Unaweza ukasema mimi ninaishi kwa raha, hao wakwe wananihusu nini..ni kweli utaishi leo kwa raha, lakini uzao wako unaweza usiishi kwa raha huko mbeleni..Na vile vile Maisha yako pia yanaweza yasiwe ya baraka.

Hiyo ni sheria ya Mungu ambayo ipo katika maandiko, ikiwa utataka kuwazaa akina YESE na Mfalme Daudi basi ambata na wakwe zako bega kwa bega, na kanuni hiyo itakulipa..Epuka mafundisho na injili za kwenda kupiga maadui zako, na kuwalenga wakwe zako..hapo utakuwa unazipiga baraka zako mwenyewe, utakuwa unajimaliza mwenyewe, ukidhani unajihami kumbe unajimaliza…Ukiona kuna kasoro Fulani ipeleke kwenye sala ukimwomba Mungu azidi kukupatanisha na wakwe zako sana, maana milango ya baraka zako ndio ipo huko.. siku zote zingatia hilo

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIKIMBILIE TARSHISHI.

Usikimbilie tarshishi hakuna uzima

Jina la Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe daima. Karibu tujifunze Neno la Mungu ambalo ndio mwanga wa njia yetu na Taa iongozayo miguu yetu.

Kama ni msomaji wa biblia utakumbuka habari za Nabii Yona jinsi alivyoukimbia uso wa Bwana na kuelekea Tarshishi. Lakini umewahi kujiuliza TARSHISHI ulikuwa ni mji wa namna gani?…Ninawi tunaujua ndio uliokuwa mji mkuu wa Ashuru..lakini Tarshishi je!

Hebu kwa ufupi tujifunze juu ya huu mji na kisha tutapata jambo jipya ambalo linaweza kutusaidia katika nyakati hizi za hatari tunazoishi.

Mji wa Tarshishi ni mji ambao ulikuwa mahali panapoitwa Tiro..ambapo kwa sasa ni nchi ya Lebanoni…Nchi ya Lebanoni ni nchi iliyopo kaskazini mwa Israeli, kama vile Kenya ilivyo kaskazini mwa Tanzania (Na mpaka leo hiyo nchi inaitwa hivyo hivyo Lebanoni haijabadilika, inakaliwa na Waarabu sasahivi, lakini haina tena utajiri/ushupavu uliokuwa nao wakati ule)..

Sasa wakati wa vipindi vya wafalme wa Israeli nchi hii ya Tiro (Lebanoni) ambao mji wake mkuu ni Tarshishi ndio ulikuwa ni mji wa kibiashara mkubwa kuliko miji mingine yote. Ulikuwa unasifika kwa kuwa na MERIKEBU NYINGI ZA KIBIASHARA kuliko miji mingine yote. Na ulikuwa ni mji wenye uzoefu wa ki-biashara

Biblia inasema katika kitabu cha Ezekieli…

Ezekieli 27:12 “Tarshishi alikuwa mfanya biashara kwako, kwa sababu ya wingi wa utajiri wa kila aina; kwa fedha, na chuma, na bati, na risasi, walifanya biashara, wapate vitu vyako vilivyouzwa”

Yeremia 10: 9 “Iko fedha iliyofuliwa ikawa mabamba, iliyoletwa kutoka Tarshishi, na dhahabu kutoka Ufazi,….”.

Unaona? Vilevile Miti ya Mierezi ambayo ilitumika katika ujenzi wa hekalu la kwanza la Sulemani, ilitoka huko Lebanoni, kulikuwa hakuna mahali pengine ambapo miti hiyo ilikuwa inapatikana, na njia ya usafirishaji iliyokuwa inatumika kusafirishia miti hiyo ni bahari (Njia ya Maji). Kwa ufupi sehemu kubwa ya malighafi za ujenzi wa hekalu la kwanza la Sulemani zilitoka huko Tiro, ambao mji wake mkuu ni Tarshishi. Hata Dhahabu Sulemani alizozitumia kutengenezea vyombo vyake zilitoka huko Lebanoni..Sulemani alinunua dhahabu nyingi kutoka huko Lebanoni mpaka kufikia kiwango cha kuwa tajiri sana hata kuona kutumia madini ya fedha(silver) kutengenezea vito vyake ni kama kujishushia heshima..

1Wafalme 10: 21 “Na vyombo vyote vya kunywea vya mfalme Sulemani vilikuwa vya dhahabu, na vyombo vyote vya nyumba ya mwitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu iliyosafika; hakuna vya fedha, fedha haikuhesabiwa kuwa kitu siku za Sulemani.

22 Kwa kuwa mfalme alikuwa na merikebu za Tarshishi baharini pamoja na merikebu za Hiramu; mara moja katika miaka mitatu huja merikebu za Tarshishi, zikileta dhahabu, na fedha, na pembe, na nyani, na tausi.

23 Basi mfalme Sulemani akawapita wafalme wote wa duniani kwa mali, na kwa hekima.”

Huko Tarshishi walikuwepo pia manahodha waliobobea sana, na pia kulikuwa na watu wenye elimu ya ujenzi kubwa sana..baadhi ya wajenzi wa hekalu lile la mfalme Sulemani aliwatolea huko huko Lebanoni.

Hivyo ipo mistari mingi sana katika biblia inayoelezea ushupavu wa Tarshishi…ipo mingi sana unaweza kuipitia kwa muda wako upatapo nafasi…Kasome (Ezekieli 27: 25-27, Ezekieli 38:13, 1Wafalme 22: 48, ).

Sasa kwa kuielewa sifa ya Huu mji wa wa Tarshishi tunaweza kujua ni kwanini Yona alikimbilia huko…Na kwanini alipanda merikebu…Kumbuka kutoka Israeli mpaka Tarshishi(huko Lebanoni) kulikuwepo na njia ya nchi kavu nzuri tu..lakini yeye alikwenda kupanda merikebu. Ni sawa leo mtu atake kwenda Tanga..aache kupanda basi achague kutumia ferry/meli pale bandarini Dar es salaam aende Tanga. Ni lazima anayo sababu ya kufanya hivyo..

Na ni wazi kuwa sababu yenyewe si nyingine Zaidi ya biashara…Yona pengine alikuwa na mizigo yake anakwenda kufanya biashara.. Tarshishi haukuwa mji wa kitalii..ulikuwa ni mji wa kibiashara..hivyo alipoisikia sauti ya Mungu ikimwambia aende Ninawi kuhubiri yeye akaona njia pekee ya kuipotezea hiyo sauti ni kuzama kwenye biashara zake…wala hakuchagua kukimbilia miji mingine kama Misri, au Moabu ambayo angepata pumziko..yeye alikuwa na sababu ya kwenda Tarshishi.. Angalau apate riziki kidogo.

Lakini kama tunavyojua ni nini kilimtokea njiani. Biashara iliishia pale pale, wakapata hasara merikebuni kwa kutupa bidhaa zao majini kupunguza uzito.. na mtaji wote ukaishia palepale.

Sasa kitu cha muhimu cha kujifunza hapo ni nini?..Usiikimbie sauti ya Mungu leo inayokuambia fanya jambo fulani au tii jambo fulani, usiidharau sauti hiyo na kukimbilia kufanya biashara zako. Ni kama bahati tu Yona alipata neema mipango yake ilikatishwa katikati haikukamilika…..angeweza kuachwa aende huko anakokwenda na Mungu akamtafuta mtu mwingine wa kwenda Ninawi kuhubiri na watu wa Ninawi wakaokoka lakini Yona huko alikokimbilia akafanikiwa na utajiri wake lakini akafa na huku hajalitimiza kusudi la Mungu aliloletewa duniani, na mwisho wa siku kupotea katika ziwa la moto milele.

Hivyo leo isikie sauti ya Mungu lipo kusudi la wewe kuwepo hapa duniani la kufanya mapenzi ya Mungu.. usilikimbie kusudi hilo kwa kisingizio cha kufanya biashara, Hizo biashara ni za muhimu sawa..lakini kulitimiza kusudi la Mungu ni muhimu Zaidi..Una safari 5-6 za kwenda China kila mwezi lakini huna siku ya kukaa kufunga na kusali na kulitafakari Neno. Mwaka unapita hujawahi kufunga useme angalau nautafuta uso wa Mungu. Hujawahi kusema angalau mwezi huu wote sitasafiri nitajikita katika kutafuta kujua mapenzi ya Mungu kwangu…Unatengeneza pesa lakini hutengenezi hazina yako mbinguni..Nchi zinakujua, Benki zinakujua, lakini mbinguni hujulikani.

Watu wengi wananiambia, mtumishi ninatamani kujifunza Neno, wengine wanasema ninatamani kwenda kanisani lakini kazi zinanisonga, shughuli zinanifanya kuwa buzy,..Nataka nikuambie unayo hatari kubwa sana ya kuiokosa mbingu.

Unakimbilia Tarshishi unaiacha Ninawi?..Unakimbilia kufanya uwekezaji unasahau kutangaza habari za ufalme wa mbinguni..Kumbuka Neema aliyoipata Yona sio atakayoipata kila mtu. Simama katika nafasi yako muda ni mchache, usiruhusu mbegu yako kusongwa na kitu chochote.

Bwana atusaidie.

Ikiwa hujampa Kristo Maisha yako..na unakazana kuifuata njia ya Ninawi!..nakushauri geuka leo..Bwana Yesu alisema “Baba yetu wa mbinguni anajua kuwa tuna haja na hayo yote, bali tuutafute kwanza ufalme wake na haki yake, na hayo mengine yote tutazidishiwa”..Hivyo tubu leo kwa kukusudia kuacha dhambi, na kupunguza masumbufu ya Maisha haya ambayo yanakuvuta na kukusonga ukae mbali na Mungu wako.

Luka 21:34 “ Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, NA MASUMBUFU YA MAISHA HAYA; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;

35 kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima.

36 Basi, kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu”.

Chukua hatua leo, na Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

UVUMILIVU WA MUNGU ULIPOKUWA UKINGOJA.

Biblia ni nini?

ANGALIA USIJE UKANG’OA NGANO KATIKATI YA MAGUGU.

UTHABITI WA AGANO LA MUNGU KWA MKRISTO.

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?

Rudi Nyumbani:

Print this post

SAA YA KUHARIBIWA IIJIAYO ULIMWENGU WOTE.

Saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote Inakuja..

Ufunuo 3:10 “Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi”.

Kuna saa ya kuharibiwa inakuja huko mbeleni, ni wakati ambapo kila mtu kwa macho yake atakuwa anaona jinsi dunia inavyokwenda kuisha ndani ya kipindi kifupi sana, kutokana na dhiki, na mapigo, pamoja na mambo ya kutisha yatakayokuwa yanaendelea duniani wakati huo.. Kipindi hicho kitakuwa ni kifupi sana, kisichozidi miaka 7 tu. Na kitaanza muda mfupi tu baada ya unyakuo kupita.

Unyakuo ndio utakaokuwa kalenda ya kututambulisha kuwa dunia imebakisha umri wa miaka 7 tu. Na ndio maana itamgharimu Mungu awaondoe kwanza wale wateule wake watakatifu ambao walikuwa wanalishika Neno la Subira yake.. Watu ambao maisha yao yote, mawazo yao yote yalikuwa yanaelekea mbinguni tu, waliojikana nafsi, waliotengwa na ulimwengu, hao tu ndio Mungu atakaowanyakua ..Ili kupisha uharibifu huo kuchukua nafasi yake.

Kama tu vile alivyomwondoa Henoko, kwa kumnyakua asikutwe na gharika, …ndivyo itakavyokuwa kwa watu hao wachache sana, watanyakuliwa wasionekane duniani, kama vile alivyomtenga Ibrahamu akawa mbali na Sodoma na Gomora ndivyo itakavyokuwa kwa wale ambao wanaishi Maisha ya uaminifu sasa, wataondoshwa katika ulimwengu huu kabla ya siku ile ya uharibifu, na watakwenda kumlaki Bwana Yesu mawinguni na moja kwa moja safari ya kwenda kumwona Baba itaanzia hapo.

Lakini wale wengine ambao ni wakristo-vuguvugu, hawatakwenda popote, watakuwa mfano wa Nuhu wataishuhudia dhiki, wataingia katika misukosuko ya dhiki kuu na mateso makali ambayo biblia inasema haijawahi kuwepo tangu kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu, kama vile Nuhu alivyokuwa katika dhiki ndani ya Safina..Kama vile Lutu alivyokuwa anapitia dhiki ile ya misukosuko sodoma ya Gomora ilivyokuwa inachomwa, siku zake zote alikuwa ni mbioni tu,..ndivyo itakavyokuwa kundi hilo kubwa la wakristo wanaosema wameokoka lakini Maisha yao hayana ushuhuda wowote hawaishi kama watu wanaomngojea Bwana wao. Dhiki hiyo itakuwa ni sehemu ya Maisha yao. Mpinga-kristo atawawinda huku na huko kama kuku..

Ndugu biblia inavyosema DHIKI basi ujue ni dhiki kweli kweli ,licha tu ile ya mpinga-kristo yatakuwepo pia mapigo mengine ya Mungu kwa wale watakaoipokea chapa, kasome Ufunuo 16, hadi mwisho kabisa , wanadamu wataadimika kama Dhahabu biblia inasema hivyo katika (Isaya 13),kama leo hii usivyoweza kuikota dhahabu kama mawe barabarani ndivyo itakavyokuwa kwa watu wakati huo, Kama alivyotoka tu Nuhu na wenzake 7 katika ya mabilioni ya watu ndivyo itakavyokuwa siku hiyo, kama walivyotoka watatu tu yaani Lutu na Watoto wake wawili ndivyo itakavyokuwa kwa mabilioni ya watu waliopo leo hii duniani.. kikundi kidogo sana, na tena watakuwa ni wale watakaowahifadhi wayahudi katika ule wakati wa dhiki za mpinga-kristo, Lakini wewe uliyepo leo hii unaipinga injili sasa , siku hiyo utakuwa ni jivu limelala hapo chini au mzoga, na ndege watakuwa wanakula nyama yako.

Tukiachilia mbali ile vita ya Harmagedoni, siku yenyewe ambayo Bwana atashuka na mawingu ambapo kila jicho litamwona, na watu watamwombolezea, misingi ya dunia hii unayoiona itatikisika, na kutakuwepo na tetemeko kubwa la ardhi ambalo halijawahi kuwepo, kumbuka wakati huo hayo yanaendelea tayari dunia imeshakuwa giza, hakuna jua wala mwezi, wala nyota yoyote angani, tetemeko hilo litaitikisa milima, mpaka hivi visiwa vyote unavyoviona leo hii vitahama, wewe wakati huo utakuwepo wapi Siku ya kuharibiwa? Wafalme, watakuwa wakilia wakiomba milima iwaungukie wafe, lakini wasikumbane na hiyo hasira ya mwana-kondoo.

Ufunuo 6:12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,

13 na nyota zikaanguka juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi.

14 Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake.

15 Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,

16 wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo.

17 Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama”?

Unaona?

Mambo haya utayashuhudia wewe ambaye bado upo nje ya Kristo, na wewe ambaye unaishi Maisha ya uvuguvugu sasahivi. Dalili zote zinathibitisha kuwa sisi watu wa kizazi hichi, haya mambo yatatupata, na dalili kubwa ni kuwa huu ni wakati ambao watu wanamejisahau, na pale watu walipojisahau na wanaona kuna Amani biblia inasema Hapo ndipo uharibifu unapokuja kwa ghafla (1Thesalonike 5:2)….Swali ni Je! Tumejiwekaje tayari..

Je! Bado unaishi Maisha ya kubahatisha? Utasema tena ni kwanini mnahubiri hivyo kana kwamba mnao uhakika kuwa Yesu atarudi wakati wetu..Ndio tunahubiri hivyo kwa nguvu zote kwasababu anayejua siku na saa ya kiama, ametuambia tuhubiri hivyo kwa nguvu sana…

Luka 14:33 “ Angalieni, kesheni, [ombeni], kwa kuwa hamjui wakati ule utakapokuwapo.

34 Mfano wake ni kama mtu mwenye kusafiri, ameiacha nyumba yake, amewapa watumwa wake amri, na kila mtu kazi yake, naye amemwamuru bawabu akeshe.

35 Kesheni basi, kwa maana hamjui ajapo bwana wa nyumba, kwamba ni jioni, au kwamba ni usiku wa manane, au awikapo jimbi, au asubuhi;

36 asije akawasili ghafula akawakuta mmelala.

37 Na hilo niwaambialo ninyi, nawaambia wote, Kesheni.

Sasa ikiwa wewe, unasikiliza injili ya mapepo inayokuhubiria kuwa dunia haitaangamizwa, ujue kuwa upo hatarini sana,. Kama hujamaanisha kumfuata Bwana Yesu, basi ni heri ukafanya hivyo sasa kabla mlango wa neema haujafungwa..Chaguo ni lako, uamuzi ni wako..Lakini fahamu tu wale wanaolishika Neno la Subira yake leo hii, hao ndio watakaoepushwa na saa ile ya kuharibiwa..

Bwana, Mkuu wa uzima wetu akubariki.

Maran Atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Ikiwa sisi tuliumbwa na Mungu,Je! Mungu aliumbwa na nani?

Nini maana ya huu mstari ” Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;”?(2Timotheo 4:7)

SALA YA ASUBUHI

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ni kura ya aina gani waliipiga wale watu waliosafiri na Yona?

Ni kura ya aina gani waliipiga wale watu waliosafiri na Yona..hata ikamwangukia Yona? Na je! Mungu anatumia kura kuchagua watu?


JIBU: Biblia haijasema ni kura gani ilipigwa pale, kama ni ya kurusha kete au kwamba kila mmoja aliandika maoni yake binafsi na walipoyaleta yote yakaonekana yanamlenga Yona…Hakuna ajuye, na wala biblia haijaandika..Lakini yote katika yote ni kwamba kura ilipigwa pale na ikamwangukia Yona.

Kikubwa tunachoweza kujifunza ni kwamba..Mungu anaweza kutumia njia yoyote kukamilisha kusudi lake..anaweza kutumia njia iliyo rasmi au isiyo rasmi…Kwamfano kama wewe ni mwanafunzi mzuri wa Biblia utagundua kuwa Mungu alimpa Daudi ufalme wote wa Israeli kwa njia ya fitina..Mungu Alimwahidia atakuwa Mfalme juu ya Israeli yote na akampaka mafuta kwa mikono ya Nabii Samweli…lakini siku ilipofika ya unabii huo wa kuwa Mfalme wa Israeli kutimia..hakupata ufalme kwa njia ya uchaguzi bali kwa njia ya fitina. Yaani mfalme aliyekuwa madarakani (mtoto wa Sauli )alifanyiwa fitina ndipo Daudi akaingia madarakani….

Kwani siku hiyo walitokea tu watu Fulani waliokuwa wanaishi kwenye nyumba ya Mfalme na hao watu wakamvizia mfalme aliyekuwa madarakani wakampiga na kumuua na kumkata kichwa,..na kumpelekea kile kichwa Daudi na kumwambia leo Mungu amewalipiza kisasi maadui zako. Ingawa Daudi hakukubaliana na uovu wao…lakini kukawa hakuna namna ni lazima kiti cha ufalme kikaliwe na mtu mwingine na huyo hakuwa mwingine zaidi ya Daudi (kasome 2Samweli 4:5-12).

Kwani Israeli walipoona mfalme wao kauawa kukawa hakuna namna zaidi ya kumweka Daudi Madarakani awe mfalme.. Na unabii wa yeye kuwa Mfalme juu ya Israeli yote ukatimia pale.

Hali kadhalika Mungu anaweza kumchagua mtu kwa njia yoyote ile iwe rasmi au isiyo rasmi..Na anaweza kumtumia mtu yoyote Yule kukamilisha kusudi lake, anaweza kumtumia mwovu au mwenye haki…kwa jinsi apendavyo yeye. Akitaka kumweka mtu mahali anaweza kutumia kura au asitumie kura. Mathiya alichaguliwa kwa kura kuwa miongoni mwa Mitume 12 wa Bwana Yesu kuchukua nafasi ya Yuda. Lakini Petro na Mitume wengine hawakuchaguliwa kwa kura…Na hiyo haikumfanya Mathiya asiwe miongoni mwa wale mitume 12.

Kadhalika Yona alichaguliwa kwa kura ili kuadhibiwa na Mungu. Mungu angeweza kuwaonyesha maono wale watu kuwa Yona ndio chanzo cha matatizo, lakini pale hakuitumia hiyo njia…angeweza kumtuma malaika akawatokea na kuwaambia Yona ndie chanzo cha lile tatizo lakini haikumpendeza..

Hata katika chaguzi za viongozi wa shule, kijiji, mtaa, au nchi…wote wanaochaguliwa na kushika nafasi hizo ni Mungu ndio kawaweka pale…Iwe wamewekwa kwa njia iliyo halali au isiyo halali kama ya uwizi wa kura au la!,..hiyo haijalishi..Ni Mungu ndio kawaweka pale..(Siku ya mwisho ndio watakwenda kujibu kwanini waliiba kura au kwanini hawakuwa waaminifu katika nafasi hizo)..Lakini maadamu tayari wapo katika hizo nafasi ni Mungu ndiye kawaweka…

Maraisi wote waliopo madarakani ni Mungu ndiye kawaweka katika nafasi hizo haijalishi waliiba kura au hawakuiba..haijalishi ni madiktekta au sio madiktekta, haijalishi wanamjua Mungu au hawamjui..Ni Mungu ndiye kawaweka kwa kusudi lake maalumu…wengine kwa kusudi kama la Farao, wengine kama la Yeroboamu, wengine kama la Nebukadneza, wengine kama la Mfalme wa Ashuru, wengine kama Manase, wengine kama Hezekia… Kila mmoja kawekwa pale na Mungu kwa kusudi maalumu…

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?

JE! MUNGU NI NANI?

Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

KUOTA UMETUMBUKIA SHIMONI.

SI KILA KIPENDEZACHO KINATOKA KWA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

SALA YA ASUBUHI

Sala ya Asubuhi inapaswa iweje?..Na je kuna sala ya jioni pia?

Hakuna sala rasmi ya Asubuhi iliyotungwa kwamba watu wafuate mfumo wake lakini ni wajibu wa kila mtu anayeitwa mkristo kusali..Katika kusali au kuomba kuna vitu vikuu vitatu vya kuzingatia katika sala yoyote ile.. Cha kwanza ni Shukrani, cha pili ni kupeleka mahitaji na cha tatu ni kutangaza

Katika sala ya Asubuni pia ni muhimu kuzingatia hivyo vipengele vitatu. Mwishoni somo hili kuna somo lingine lenye kichwa kinachosema “FAIDA ZA MAOMBI”. Nakushauri ulisome ili uweze kuelewa uchambuzi wa vipengele hivyo vitatu vya maombi.

Lakini kama ndio kwanza umempa Kristo maisha, basi sala hii hapa chini kwa Asubuhi inaweza kukufaa. 

Unapoamka kabla ya kufanya kitu chochote kile, hata kabla ya kwenda kupiga mswaki.. Sali sala hii kwa kumaanisha na kwa muda mrefu kwa jinsi uwezavyo ukitaja hata  mambo ambao hayajaandikwa katika sala hii.

Sema…

Ee Baba yangu, Mungu muumba wa mbingu na nchi, nakushukuru kwa kuniamsha nikiwa mzima wa afya,(hata kama umeamka na udhaifu fulani mdogo huna buni kumshukuru Mungu pia)

Nasema ahsante sana ni kwa Neema zako tu, wapo ambao hawajaweza kuamka leo lakini mimi nimeamka.

Nakuomba unipe Neema yako katika siku ya leo inayoanza nikatembee katika mapenzi yako, nisikutende dhambi wala nisikuhuzunishe kwa jambo lolote, naomba ukaniepushe na majaribu yote, na mipango yote mibaya ya yule Adui aliyoipanga juu yangu na juu ya watu wangu na vitu vyangu na afya yangu na shughuli zangu katika hii siku ya leo.

Nijalie pia siku hii ya leo angalau niongeze kitu kimoja katika ufalme wako, hata itakapofika tena jioni nikapate kushuhudia matendo yako makuu na kukushukuru. Naomba haya machache katika Jina la Yesu Kristo.

Amen’.

Kumbuka pia tuna wajibu wa kusali muda wote na mahali popote sio tu asubuhi, au jioni…hapana bali hata tukiwa tunatembea, tunafanya kazi..tuna wajibu wa kuomba…sala ya jioni pia ni ya muhimu sana kama tu ilivyo sala ya Asubuhi.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI.

FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

HERI NINYI MLIAO SASA, KWA SABABU MTACHEKA.

JE NI KWELI MTU ANAWEZA KUTOKA NJE YA MWILI WAKE?.

MTAIFAHAMU KWELI NAYO HIYO KWELI ITAWAWEKA HURU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao.

SWALI: Biblia inamaana gani kusema   “Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao, maana, wakizidiwa na tamaa kinyume cha Kristo, wataka kuolewa;nao wana hukumu kwa kuwa wameiacha imani yao ya kwanza”.(1Timotheo 5:11-12).

Ni kwanini wahukumiwe kwa kuolewa kwao tena, wakati biblia inaruhusu wajane kuolewa?


JIBU: Kama ukisoma kuanzia mistari ya juu utaona zamani za mitume kulikuwa na utaratibu wa kuwakumbuka wajane katika posho la kanisa..Na kulikuwa na masharti yake ili uweze kuandikwa,

  • Sharti la kwanza ni lazima awe ameshuhudiwa kuwa huko nyuma aliishi na mume mmoja tu,

1Timotheo 5:1 “Mjane asiandikwe isipokuwa umri wake amepata miaka sitini; naye amekuwa mke wa mume mmoja”;

  • Pili ni lazima awe ameshudiwa kuwa na matendo mema, na awe ameshawahi kutoa  mchango wowote( wa huduma) katika kanisa la Mungu..

1Timotheo 5.10  “naye ameshuhudiwa kwa matendo mema; ikiwa amelea watoto, ikiwa amekaribisha wageni, ikiwa amewaosha watakatifu miguu, ikiwa amewasaidia wateswao, ikiwa amefuata kwa bidii kila tendo jema”.

  • Na tatu, awe hana amefikisha umri wa miaka 60 na Zaidi. Kama tulivyoona hapo kwenye mstari 1
  • Nne, Awe hana ndugu, wala wana, wala jamii ya kumsaidia.

5.4 Lakini mjane akiwa ana watoto au wajukuu, na wajifunze kwanza kuyatenda yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe, na kuwalipa wazazi wao. Kwa kuwa hili lakubalika mbele za Mungu.

  • Tano, awe ameweka tumaini lake lote kwa Bwana. Yaani ameamua  kudumu  katika kumtumikia Bwana na katika kufanya dua mchana na usiku.

5.5  Basi yeye aliye mjane kweli kweli, ameachwa peke yake, huyo amemwekea Mungu tumaini lake, naye hudumu katika maombi na sala mchana na usiku.

Hivyo mjane yeyote ambaye alikuwa amekidhi hivyo vigezo basi alikuwa anaruhusiwa kuandikwa katika kanisa, na kanisa lilikuwa linawatambua watu kama hao, na walikuwa wanatengewa fungu lao maalumu.

Lakini sasa kama tayari alishajitoa kikamilifu kwa Bwana namna hiyo, ameshaingia katika nadhiri kama hizo kwamba tumaini lao lote sasa ni kwa Bwana tu, mpaka anafikia hatua ya kuchukua uamuzi wa kwenda kuandikwa katika kitabu cha kanisa kwamba ni yeye ni mjane kweli kweli aliyemwekea Mungu tumaini lake lote, halafu inatokea ghafla tu anageuka na kutaka  kuja kuolewa tena….Sasa katika mazingira kama hayo watu wa namna hiyo maandiko haya ndio yanayowahusu.

5.12 wana hukumu kwa kuwa wameiacha imani yao ya kwanza..

Na ndio maana mtume Paulo akatoa angalizo kabisa, wajane wazee ni heri wasiandikwe waolewe, kwa namna nyingine ni kwamba  kama wanajijua siku moja  watakuja kuolewa basi wasijiingize katikati  ya wajane kweli kweli waliodhamiria kumuishia Mungu maisha yao yote vinginevyo watakuwa wanajitafutia hukumu ya bure..wakizidiwa na tamaa.

Ubarikiwe.

Mada Nyinginezo:

Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?

Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?

NDOA NA TALAKA:

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

JE! UNAYATUNZA MAVAZI YAKO?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post