Jinsi sodoma na gomora ilivyokuwa inavutia sana.
Mwanzo 13:10 “Lutu akainua macho yake, akaliona Bonde lote la Yordani, ya kwamba lote pia lina maji, kabla Bwana hajaharibu Sodoma na Gomora, lilikuwa kama bustani ya Bwana, kama nchi ya Misri hapo unapokwenda Soari.
11 Basi Lutu akajichagulia Bonde lote la Yordani; Lutu akasafiri kwenda upande wa mashariki; wakatengana wao kwa wao”.
Ndugu kama ulikuwa hujui, basi leo ujue, kuwa dhambi ni kitu kinachovutia sana! Kama dhambi ingekuwa haivutii hakuna mtu leo hii angenaswa na mtego wowote wa dhambi..Wengi wetu tunajua habari ya Lutu na mjomba wake Ibrahimu jinsi walivyopishana kauli kutokana na wingi wa mali walizokuwa nazo, mpaka ikafikia hatua sasa wajitenge kila mmoja achague upande wake wa kukaa.
Lutu akapewa kipaumbele cha kwanza cha kuchagua, akafanya utafiti wake wa mji bora wa kukaa, ndipo akaitazama miji yote iliyokuwa kando kando na pale walipokuwepo yeye na Ibrahimu, mwishowe akafanikiwa kuona miji mizuri sana, ambayo hakukuwa na mfano wake katika kaanani yote na miji yenyewe ni Sodoma na Gomora. Biblia inasema miji hiyo ilikuwa mfano wa BUSTANI YA MUNGU (Edeni). Ilikuwa nzuri karibia ifanane na Edeni..Hivyo sio kila mahali panapoonekana pazuri Mungu yupo…Uzuri wa sodoma na Gomora ulifananishwa na Edeni, lakini ilikuwa ni bustani ya shetani…Shetani naye anayo Edeni yake ambayo kwa uzuri inakaribi Ilikuwa ni miji yenye kijani kibichi, yenye chemchemi za maji, na mwonekano wa kuvutia.
Vivyo hivyo ilikuwa ni miji yenye ustaarabu uliomakini, yenye uchumi mkubwa, yenye fursa nyingi za biashara, isiyo na njaa wala kiu, miji ambayo mtu ukiishi unajua nini maana ya maisha,.mbali sana na hiyo Kaanani ambayo alikuwa anaishi yeye na Ibrahimu, ambayo ni jangwa tupu, hakuna hata chakula cha kutosha maji yenyewe ni ya shida, kama nusu-kijiji tu..
Na hiyo ndiyo sababu mojawapo iliyowafanya watu wa miji ile wasimwongope Mungu, wamuone kuwa si kitu cha maana sana kwao, wakaanza kujiamulia kuishi tu kama wapendavyo kama wanyama, wanazini wao kwa wao jinsia moja, wanazini na wanyama. N.k.
Sasa Lutu yeye hakuangalia nyuma ya pazia kuna nini..Yeye maadamu anaona fursa, na maisha mazuri akaamua kuingia moja kwa moja, kumbe kama sio neema ya Mungu ndio ulikuwa mwisho wake..
Biblia inatuambia wazi kabisa kama ilivyokuwa katika siku za Lutu ndivyo itakavyokuja kuwa katika siku za kuja kwake mwana wa Adamu.. Wote tunajua jinsi dunia ya leo ilivyo tofauti sana ile ya zamani, ustaarabu uliopo leo hii ni mkubwa sana, utajiri uliopo duniani leo hauwezi kulinganishwa na ule uliokuwepo wakati ule, teknolojia, elimu, uchumi, miundombinu ni ya ajabu sana, kiasi kwamba ukimleta mtu wa karne ya 18 ukamuonyesha miji ya kisasa iliyopo duniani pamoja na teknolojia tulizonazo anaweza kusema huu sio ulimwengu wa wanadamu, bali ni kitu kingine…
Lakini mambo hayo mawili yanakwenda sambamba, “mafanikio pamoja na uovu vinashadiiana”.. Leo hii huoni jinsi ndoa za jinsia moja zinavyohalalishwa kila mahali mambo ambayo huko zamani hayakuwepo?, ndoa za wanyama na wanadamu, uzinzi sasahivi kila mahali mtu akiwa na simu ya mkononi tu, tayari anaufahamu uzinzi wote wa ulimwenguni..jambo ambalo hata sodoma halikuwepo, Mungu leo hii anatukanwa hadharani, ukipeleka habari za Mungu tu unaonekana kama mpinga-uhuru wa haki za kibinadamu, unaonekana kama mtu wa kale mwenye itikadi za kizamani.
Na wana wa Mungu wanapoona, mbona Mungu hachukui hatua yoyote dhidi yao, nao pia wanakwenda kujichanganya na maovu yao, ..Hawajui kuwa wanajiangamiza wao wenyewe bila kujua.
Kule Sodoma..Siku ya maangamizo ilipofika haikumaliza hata siku moja, mji ile ilikuwa imeshakuwa jivu yote..Vivyo hivyo na siku ya maangamizi ya huu ulimwengu ambayo ipo mbioni kutokea ambayo biblia ilishasema itakuja kwa ghafla sana, tena na cha kuogopesha zaidi itakuja katika kipindi cha amani,..soma.
1Wathesalonike 5:2 “Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.
3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.
Sasa kama na wewe upo katikati ya sodoma, usidhani itakuwa ni rahisi, kupona wakati huo ..
Mungu alishatuasa watoto wake tutoke huko, tujitenge nao mambo ya ulimwengu.. (Ufunuo 18:4)..Tusiyakaribia hata kidogo…Tutoke Sodoma wala tusiikaribie hata kidogo…Tukae nayo mbali sana maelfu ya Maili…Kumbuka sio tu Sodoma na Gomora pekee yake ndio ziliteketezwa wakati wa Nuhu..Biblia inasema hata ile miji iliyokuwa kando kando ya Sodoma na Gomora iliteketezwa pia (kasome Yuda 1:7)..Haikuwa na maasi kama Sodoma na Gomora..lakini kitendo tu cha kuwa karibu na miji hiyo tayari ilikuwa imeshanajisika nayo pia..Kadhalika leo..tunaaswa tukae mbali na uchafu wa dunia hii, wala tusifungwe nira na wasio amini kwa jinsi isivyo sawasawa. (2Wakorintho 6:14) ili nasi tusije tukachanganywa huko huko katika hasira ya Mungu.
1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.
16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.
17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”.
Unaona? Ikiwa umeokoka halafu bado unapenda kwenda disko basi ujue upo Sodoma, umeokoka na bado unasikiliza miziki ya kidunia, unavaa nguo za kikahaba, vimini na masuruali, ujue unaishi sodoma bado..Na siku ile ya Unyakuo hutakwenda popote.. utabaki hapa chini ukingojea hukumu ya Mungu kulingana na Biblia.
Ni maombi yangu, hutachukuliwa na tamaa kama za Lutu, kwa kupenda mambo haya ya kitambo ya ulimwenguni, bali sote tutajitahidi tumtazame Kristo na mambo ya ufalme wa mbinguni, hadi siku ile ya ukombozi wetu utakapofika.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Ufisadi una maanisha nini katika biblia? (Ufisadi ni nini? Ni uwizi wa fedha nyingi au?)
JIBU: Neno ufisadi tofauti na linavyotafsiriwa siku hizi kwamba ni mtu anahujumu uchumi wa Taifa Fulani au shirika Fulani. Lakini katika biblia tafsiri yake ni tofauti.
Katika biblia neno fisadi limetumika kumtambulisha mtu mwenye tabia ya uzinzi na uasherati uliopindukia ambao hata haujali jinsia, umri wala maadili (unahusisha chochote kile ilimradi tu ni zinaa inafanyika)..Kwa lugha nyingine (ni ukahaba/umalaya mchafu). Hivyo popote pale katika biblia linapoonekana neno hili fahamu kuwa linamaanisha “ukahaba/ umalaya wa namna hiyo”.. Kwamfano tunaweza kusoma baadhi ya mistari michache inayozungumzia tendo hilo…
Waefeso 4:19 “ambao wakiisha kufa ganzi wanajitia katika mambo ya ufisadi wapate kufanyiza kila namna ya uchafu kwa kutamani”…..
Waefeso 5:18 “Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;”…
Maana yake ni kuwa ulevi na ukahaba/Umalaya ni pacha, vinakwenda sambamba…
Mstari mwingine ni kama huu..
Tito 1:6“ ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni WAFISADI wala wasiotii.
7 Maana imempasa askofu awe mtu asiyeshitakiwa neno ,kwa kuwa ni wakili wa MUNGU;asiwe mtu wa kujipendeza nafsi yake,asiwe mwepesi wa hasira,asiwe mlevi wala mgomvi,asiwe mpenda mapato ya aibu”.
Maana yake ni kwamba Watoto wa Maaskofu pia hawapaswi kuwa Malaya wala makahaba wala kujihusisha na vitendo vyovyote vya zinaa. Wanapaswa wawe watakatifu katika mwenendo wao ili wawe kielelezo kwa kanisa la Mungu. Mtu yoyote anayetaka kazi ya uaskofu kama Watoto wake ni wachafu kwa viwango hivyo biblia inasema hastahili kuwa Askofu..anapaswa awageuze kwanza Watoto wake ndipo aweze kulichunga kundi la Mungu.
Pia Wagalatia 5:19 inasema… “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, UFISADI.”.. Na 2Wakorintho 12:21 pia inasema…“Nami nitakapokuja tena, Mungu wangu asije akanidhili kwenu, nami nikawasikitikia wengi waliokosa tangu hapo, wasiutubie uchafu, na uasherati, na ufisadi walioufanya”…
1Petro 4:3 “ Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;
4 mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika UFISADI ule ule usio na kiasi, wakiwatukana”
Mistari mingine pia ni katika kitabu cha Petro…
2 Petro 2:6 “ tena akaihukumu miji ya Sodoma na Gomora, akiipindua na kuifanya majivu, akaifanya iwe ishara kwa watu watakaokuwa hawamchi Mungu baada ya haya;
7 akamwokoa Lutu, yule mwenye haki aliyehuzunishwa sana na mwenendo wa UFISADI WA HAO wahalifu”. Kama tunavyojua miji ya Sodoma na Gomora kiwango cha uasherati walichofikia..hata kuwatamani Malaika.
Na mistari mingine mingi inazungumzia tendo hilo…Unaweza kupitia binafsi mistari ifuatayo..(Marko 7:22, Warumi 13:13, 2Petro 2:18, na Yuda 1:4).
Je! Swali linakuja….Mafisadi watakwenda mbinguni?..Jibu ni la! Kama biblia ilivyosema hapo juu…
Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, UFISADI,
20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, KATIKA HAYO NAWAAMBIA MAPEMA, KAMA NILIVYOKWISHA KUWAAMBIA, YA KWAMBA WATU WATENDAO MAMBO YA JINSI HIYO HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU”.
Unaona biblia imetuonya mapema kabisa kwamba watu wafanyayo hayo hawataurithi uzima wa milele?..Je ulevi ni suluhisho la kupunguza uzinzi na uasherati?..Jibu ni la! Kinyume chake Ndio kichochoe kikubwa cha ukahaba na umalaya huo(Ufisadi). Lakini Roho Mtakatifu ndiye jawabu la kuondoa tamaa ya uasherati na uzinzi.. kama Waefeso 5:18 inavyosema.. “Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;”…
Je umempokea Roho Mtakatifu?..ambaye ndiye msaada wetu wa kushinda dhambi? Kama bado unangoja nini?
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, NANYI MTAPOKEA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFU.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.
40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi.
41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu”.
Njia ya kumpokea huyo Roho Mtakatifu ndiyo hiyo hapo juu..Kutubu kwa kudhamiria kuacha dhambi na kwenda kubatizwa….Na wewe Tubu leo, ukabatizwe katika Jina la YESU na utapokea kipawa hicho cha Roho Mtakatifu, kwasababu Mungu sio mwongo, Naye atakupwa uwezo huo wa kuzishinda hizo tamaa mbaya.
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Kifo ni nini?, Je ni kweli kila nafsi itaonja mauti?.
Kifo sio mtu, wala si kitu bali ni “hali”…Kitu kinapopitia hali ya kukosa “UHAI”. Tayari kitu hicho kinakuwa kimekufa.
Kwamfano tuchukue kifaa kinachoitwa SIMU. Simu ikikosa chaji simu ile inazima hivyo tunaweza kusema “imekufa chaji”..Sasa kitendo cha umeme kukosekana kwenye ile simu…Ni sawa na simu ile imekufa..kwasababu haiwezi kuwaka, spika zake haziwezi kufanya kazi, kadhalika haiwezi kutoa mlio wowote wala kufanya chochote mpaka ichajiwe tena.
Vivyo hivyo Uhai wa Mungu ni kama “UMEME” ndani mwetu…Huo unapokosekana au unapotoka ndani ya mwili wa mtu…Mtu yule anakuwa amekufa. Hawezi kunyanyuka, hawezi kuona kupitia macho..hawezi kuhisi, hawezi kujibu, hawezi kufanya chochote kile..Mwili wake unakuwa umekufa.(Hivyo kifo ni nini?..Ni hali ya uhai wa Mungu kutoka ndani ya kiumbe hai)
Lakini kitu cha kipekee na cha muhimu kufahamu ni kwamba..Mtu kaumbwa na sehemu mbili kuu, nazo ni UTU WA NDANI, na UTU WA NJE. Utu wa nje ndio mwili ambao ndio huu wenye vidole, macho ni mikono…Huu uhai wa kiMungu unapoondoka unazima!.
Kadhalika kuna utu wa ndani..Huu wa nje unapozima wa ndani bado upo..unakuwa bado una uhai wa Mungu. Hivyo unaendelea kuishi..Unaendelea kuona, kusikia, kufahamu ingawa hautumii macho ya damu na nyama wala viungo vya damu na nyama…Unatumia viungo vya rohoni kuona, kusikia, kuelewa n.k
Kama mtu alikufa akiwa ndani ya Imani ya Mwana wa Mungu Yesu Kristo, analo tumaini la kufufuliwa na kuvalishwa mwili mpya wa utukufu na kwenda mbinguni kwa Bwana…ambao huo haufi wala hauzeeki. Lakini kama mtu alikufa katika ndambi anakuwa hana tumaini hilo zaidi ya kungojea kwenda kutupwa katika Ziwa la Moto.
Je ni kweli kila nafsi itaonja mauti?
Jibu ni hapana! sio kila nafsi itaonja mauti…kwani mpaka sasa kuna ambao hawajaonja mauti na wameshavuka kutoka mautini kuingia uzimani…Mfano wa watu hao ni HENOKO na ELIYA. Hawa walinyakuliwa juu bila kuonja mauti..Hivyo ni uongo kusema kwamba kila nafsi itaonja mauti.
Vivyo hivyo biblia inasema siku ya Unyakuo wa kanisa itakapofika, wapo watakatifu ambao siku hiyo itawakuta wakiwa hai. Hao Biblia imesema watanyakuliwa wakiwa hai ambapo kufumba na kufumbua miili yao itabadilishwa na kuwa kama ya Malaika, na wataungana na watakatifu waliofufuliwa na kwa pamoja watakwenda kumlaki Bwana mawinguni.
1Wakorintho 15:51 “Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,
52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika”.
Na pia jambo hilo biblia imeliweka vizuri katika mstari ufuatao..
1Wathesalonike 4:13 “Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.
14 Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.
15 Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.
16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele”.
Hivyo wapo ambao hawataonja mauti kabisa…Na dalili zote zinaonyesha kwamba unyakuo unaweza kutokea katika kizazi chetu hichi kwasababu kila dalili zimeshaonekana na hata zimezidi na kuonekana vitu vingine ambavyo ni zaidi ya zile dalili…maana yake ni kwamba kuna uwezekano wa kulishuhudia tukio la unyakuo kwa macho yetu..
Je umejiandaa?..Utakuwa miongoni mwa watakaonyakuliwa?..kumbuka biblia inasema waasherati, wazinzi, waabudu sanamu, walevi, na wanaoupenda ulimwengu kuliko kumpenda Mungu hawataurithi uzima wa milele.
Bwana atusaidie sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Ogopa wadanganyifu, ambao wanakuambia suluhisho la ndoto Fulani uliyoota labda tuseme kuota umetumbukia shimoni, au umekimbizwa na nyoka,au umezama kwenye maji au unafanya uasherati na mtu usiyemjua kwamba ukanunue dawa yao Fulani itakusaidia kutatua hilo tatizo.. Wengi wanaokuambia hivyo kama si washirikina basi uwe na uhakika ni matapeli.. Ndoto, au maono, ni mambo yanayotoka ndani ya mtu, yaani katika utu wake wa ndani, Hivyo hayawezi kutibiwa kwa tiba za nje, kama vile dawa na vidonge, Ni sawa na mtu aliyefiwa, huwezi kumwambia nenda kameze PAIN KILLER, tatizo lako la huzuni litakwishwa, badala yake utatumia njia ya kumfariji, ndipo hapo atakapogangika kwasababu ugonjwa wake ni wa moyoni na si nje..
Hivyo ni vizuri kufahamu, ndoto asili yake ni rohoni, Kwahiyo tiba yake ni lazima iwe ya rohoni na si ya nje.
Zipo ndoto za aina tatu.
Sasa kama kuota umetumbukia shimoni: Mara nyingi wengine wanaota wapo ukingoni mwa shimo wanakaribia kuanguka, wengine wapo tayari chini kabisa kwenye shimo refu lenye giza, wengine wananing’inia ikingoni mwa shimo na kila wanapojaribu kujivuta juu watoke wanajiona ni wazito sana, wanahitaji msaada..n.k. zote hizo ujumbe wake ni mmoja. Kuwa maisha yako yapo hatarini kama hutachukua uamuzi ulisohihi Mungu anaokuagiza uufanye.
Ikiwa wewe umeokoka (yaani maisha yako yamefichwa ndani ya YESU KRISTO): Na ndoto kama hii kuota umetumbukia shimoni imekujia kwa uzito sana, au imejirudia rudia mara nyingi, basi ongeza umakini wako kwa MUNGU,kwasababu mahali unaweza kwenda kukwamba usisonge mbele katika imani yako, pili omba sana, hususani katika mazingira uliyopo, na mambo unayoyafanya yote hakikisha unamtanguliza Mungu kwanza..Na Bwana atakuvukisha au kukukwepesha kabisa na majaribu hayo.
Soma (Yeremia 38:6, Maombolezo 3:52-57).
Lakini kama wewe hujaokoka na unafanya mojawapo ya hivi vitu:
Mithali 22:14 Kinywa cha malaya ni shimo refu; Anayechukiwa na Bwana atatumbukia ndani yake.
Mithali 23: 27 Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.
Ukiendelea kuwa na tabia hiyo, mwisho wako utakuwa ni mbaya..Utaingia mahali ambapo utashindwa kutoka milele.
Mithali 26: Achimbaye shimo atatumbukia mwenyewe; Naye abingirishaye jiwe litamrudia.
Zaburi 7: 14 Tazama, huyu ana utungu wa uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.
15 Amechimba shimo, amelichimba chini sana, Akatumbukia katika handaki aliyoifanya!
16 Madhara yake yatamrejea kichwani pake, Na dhuluma yake itamshukia utosini.
Hayo yote yanajumuisha watu wote waovu..Kuwa hatma ya maisha yao ni shimo refu la mauti kama hawatatubu.
Hivyo yatengeneza mambo yako kwa Mungu haraka iwezekanavyo..Kumbuka Yesu ndio njia, na kweli na Uzima (Yohana 14:6), anakuonyesha hivyo kwasababu anakupenda ili utubu umgeukie yeye, uache dhambi ayasafishe maisha yako. Ni nani ajuaye kuwa leo kukukutanisha na ujumbe huu ni kwa makusudi yake maalumu UOKOKE LEO?..Hivyo usipuuzie wito huo, mruhusu leo ayaokoe maisha yako akutoe katika shimo hilo refu la mauti ambalo upo sasa, au kama haupo basi siku si nyingi utakuwepo,ukiendelea na tabia yako.
Lakini Ikiwa unatii na upo tayari kufanya hivyo sasa.
Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Fanya Hivyo na Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
CHAGUA NI JIWE LIPI LITAKALO KUFAA KWA UJENZI.
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
MAONO YA NABII AMOSI.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!
Najisi ni kitu gani?
“Najisi” ni kitu chochote kinachokwamisha na kuundoa usafi wako wote, heshima yako yote au hadhi yako yote uliyokuwa nayo ..Kwamfano unaweza ukawa na nguo yako nyeupe, lakini kawino kadogo tu cheusi kakapita kwenye mfuko wa shati hilo, kakakufanya usilavae tena shati hilo kwa doa lile ..Sasa kale kadoa cha wino ndio najisi hivyo kameitia unajisi nguo nzima isifae tena..
Vivyo hivyo kwa watakatifu, yapo mambo mengi unaweza kweli ukayadhibiti na ukawa safi lakini mambo madogo madogo yakakuharibia ukaonekana sio safi tena mbele za Mungu haijalishi umejitahidi kuyazuia hayo mengine kiasi gani..
Ukisoma katika agano la Kale Mungu aliwaorodheshea wana wa Israeli mambo ambayo yatawafanya kuwa najisi..Na mojawapo ni kuigusa maiti, ya mtu aliyekufa au mnyama..Hata kama wewe ni kuhani ilikuwa ukigusa tu maiti basi hutaruhusiwa kufanya chochote hadi siku ya tatu ambapo utajiosha na kujitakasa kwa maji safi..Ukishamaliza kujisafisha hiyo peke yake haitoshi kuundoa unajisi kabisa, itakupasa usubiri hadi siku ya saba bila kwenda popote ndipo utakaporuhusiwa kuingia katika kusanyiko la Mungu.(Soma Hesabu 19:12).
Kadhalika na baadhi ya wanyama kama vile nguruwe, na wengine wasioweza kucheua walikuwa ni najisi, ukiwala tu tayari umeshajitia unajisi.
Halikadhalika ilikuwa ukitokwa na uchafu sehemu zako za siri iwe ni mwanaume au mwanamke tayari umeshajitia unajisi, hivyo kama wewe ni mwanaume ulikuwa unaoga kwa maji safi, kisha unausubiri mpaka jioni hufanyi chochote ndipo ikishafika jioni utaruhusiwa kuingia kwenye kusanyiko la Mungu (Walawi 15:16), Lakini kama wewe ni mwanamke labda upo katika siku zako basi utasubiri siku 7, ndipo uruhusiwe kuingia katika kusanyiko(Walawi 12:4).
Vilevile kwa mwanamke aliyezaa, tayari ametiwa unajisi kwa tendo lile, hivyo kama amezaa mtoto mwanaume basi atasubiri siku 33 pamoja na siku 14 za uchafu wa siku zake, lakini kama amezaa mtoto wa kike atasubiria siku 66 pamoja na siku nyingine 14 pia..
Hivyo siku zote hizo za unajisi mtu haruhusiwi kuingia katika kusanyiko lolote la Mungu wala kutoa kafara yoyote kwa Mungu, japokuwa tayari ulishajisafisha na unaonekana upo safi lakini inakugharimu usibirie, kinyume chake ukifanya hivyo adhabu yake ilikuwa ni kifo..
Sasa tukirudi katika agano jipya..Unajisi wetu sio wa mwilini tena bali wa rohoni, yote hayo yalikuwa yanafunua unajisi wa Rohoni ambao ndio mkuu, Bwana Yesu alisema..
Mathayo 15:18 ‘Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.
19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano;
20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula kabla hajanawa mikono hakumtii mtu unajisi’.
Kama vile tulivyoona unajisi wa mwilini, unaweza ukawa kweli umeshaoga na kusafishika lakini ulikuwa bado huruhusiwi kuingia uweponi mwa Bwana kwa kitambo Fulani, aidha kwa siku moja, au kwa wiki, au kwa mwezi, au kwa miezi miwili inategemea na aina ya unajisi uliokuwa nao..Vivyo hivyo na unajisi wa rohoni, mtu unaweza kweli ukasemehewa kwa alilolifanya lakini hilo bado lisimfanye arudi uweponi mwa Bwana muda huo huo..bali kinaweza kupita kitambo kirefu sana..
Kama Bwana Yesu alivyosema, mawazo mabaya ni moja ya mambo yanayomtia mtu unajisi, unaweza ukawa wewe sio mzinzi lakini ndani yako muda wote unawaza uzinzi, sasa hapo tayari jambo hilo limeshautia doa utakatifu wako, umejitia unajisi.. Utakwenda kutubu kweli na pengine Mungu atakusamehe, lakini kurudi kule uweponi mwa Bwana, ambapo ulikuwa nako mwanzoni kunaweza kukuchukua muda sana..ndio maana tunapaswa tuwe makini sana..
Mawazo kama haya yanapokujia ndani yako hupaswi kuyapa nafasi hata kidogo, unayakataa na kuyakemea, na hapo hapo kupeleka mawazo yako katika Neno la Mungu na ahadi zake. Hiyo ndiyo njia pekee ya kutokujitia unajisi na mawazo ya namna hiyo..Vilevile unaacha kutazama au kuangalia vitu ambavyo vinachochea unajisi huo..Kama utakuwa mtazamaji wa movie za kidunia muda wote ambazo hizo ndani yake huwezi kosa maudhui ya uasherati unategemea mawazo hayo yasikutawale? Yatakutawala tu, unasikiliza miziki ya kidunia yatakutawala tu, unachati kwenye magroup yao, unasikiliza mazungumzo yao, unasoma visa vya hadithi za kiasherati, unafuatilia magazeti ya kiasherati…mawazo kama hayo yatakuteka, na itakuwa nguvu kujitawala..matokeo yake unajitia unajisi, na kuifanya bidii yako kuwa sio kitu mbele za Mungu..
Kama wewe ni mtukanaji au unazungumza maneno yasiyofaa, au msengenyaji…tayari unajitia mwenyewe unajisi, haijalishi unafunga, saumu yako ni bure tu..kwasababu doa tayari limeshaingia,..unapaswa ujifunze kukizuia kinywa chako.
Na ndio maana ukitoka tu kuwaza mambo kama hayo maovu, au ukitoka tu kuzungumza maneno hayo, unaona ndani yako ukame mkubwa, ile nguvu labda ya kusali imepungua ghafla, au ule uwepo wa Mungu ghafla umepotea ndani yako..Sasa ukishaona hivyo basi ujue tayari ulishajitia unajisi..Unapaswa ukatubu na uache kivitendo..na hiyo inaweza kuchukua muda kidogo mpaka kuurudisha tena uwepo wa Mungu karibu na wewe…Hayo ndiyo madhara ya kujitia unajisi…inasababisha uwepo wa Mungu kukaa mbali na wewe kwa muda.
Hivyo biblia ilishatuonya tuilinde mioyo yetu, kuliko kitu kingine chochote,(Mithali 4:23) kwasababu humo ndimo zitokazo chemchemi za maji ya uzima. Hivyo Bwana atusaidie sote tukae mbali na unajisi wa aina yoyote, ili safari yetu isiwe na vikwanzo visivyokuwa na lazima.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Akawaambia Enendeni ulimwenguni mwote,MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE.(Marko16:15.) Yesu Anamaanisha nini kusema MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE?
Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?
Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?
ZIKUMBUKE FADHILI ZA MUNGU
UNYAKUO.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
MJUMBE WA AGANO.
Je wakristo tunaruhusiwa kusheherekea valentine’s day(siku ya valentine)? siku ya wapendanao?
Valentine kulingana na Historia alikuwa ni kuhani wa kikatoliki aliyekuwa anaishi Rumi katika karne ya 3..Aliishi Wakati wa Utawala wa Mfalme wa Rumi, aliyeitwa Claudius wa pili…Huyu Claudia alikuwa mpagani na akatengeneza sheria za kuwazuia wakristo kufanya baadhi ya mambo…Historia inasema huyu Claudia ilifika wakati akatamka kuwa Wanajeshi wote wa Rumi wanapaswa wawe wamejitoa kikamilifu kwa nchi yao..hivyo hawapaswi kuoa..Kwahiyo akapitisha sheria kwamba hakuna mwanajeshi yoyote anayepaswa kuoa. Akiamini kuwa jeshi bora linajengwa na watu ambao hawajaoa.
Lakini huyu Valentine (au valentino)..hakukubaliana na hilo shauri…Hivyo akawa anawafungisha ndoa kwa siri baadhi ya wanajeshi hao..Lakini alikuja kujulikana na taarifa zikamfikia mfalme..na akahukumiwa kifo.
Wakati akiwa huko gerezani historia inasema alimpenda binti wa mkuu wa gereza aliyekuwa kipofu, na alimhudumia mpaka akapata kuona tena…Na siku yake ya kuuawa ilipofika alimtumia mwanamke aliyempenda kadi yenye sahihi hii…“kutoka kwa Valentino wako”. Na akenda kuuawa..siku hiyo ya February 14, mwaka 270.
Miaka mingi ilipopita ndio baadhi ya watu wakaichagua iwe ni siku ya kupelekeana kadi zenye ujumbe wa mapenzi kama Valentino alivyofanya kwa yule mwanamke kabla ya kuawa kwake.
Sasa hadithi hiyo inahusiana nini na ukristo?..Valentino kumtumia kadi mwanamke huyo sisi inatuhusu nini?..Je! nini kiliendelea baada ya pale?…hakuna anayejua wala historia haijaeleza…Hivyo ni hadithi tu ambazo hazina faida yoyote kwetu sisi kuzienzi wala kuzishika…zaidi zinatutoa kwenye mstari wa imani yetu..
Ni hadithi tu ambazo maudhui yake ni kuongeza maasi na maovu duniani..na karamu za ulafi ambazo biblia imetuonya katika..1Petro 4:3…na kuchochea uzinzi..
Siku ya wapendanao ni ipi?..Bila shaka ni kila siku, hakuna siku moja maalumu ambayo upendo unazidi Zaidi au unaenziwa!…Upendo upo kila siku… kama ni upendo halisi!..lakini kama sio upendo halisi..labda unaweza kuwa na siku yake moja maalumu ya kuongezwa nguvu inayoitwa valentine’s day..Lakini kwa wakristo wa kweli upendo ni kila siku, unabubujika kila siku, kila saa..
Kwahiyo “Valentine’s day” ni sikukuu za kipagani, ambayo lengo lake ni kuwafanya watu wazame katika ulimwengu zaidi..na kuwafanya waupenda ulimwengu Zaidi ya kumpenda Kristo. Siku hii ndio siku disko zinajaa watu, siku hii ndio siku ambayo idadi kubwa ya watu wanafanya uasherati, siku hii ndio siku ambayo idadi kubwa ya watu ndio wanakwenda kulewa pombe…Wala hata sio siku ya watu kwenda kanisani, sio siku ya watu kwenda ibadani kumwabudu Mungu au kusali…Ni siku maalumu shetani aliyoiandaa ya watu kuzama ulimwenguni kusambazo upendo bandia ambao hata watu ambao hawajaona wanapelekea kadi hizo..Sasa itakuwaje sikukuu ya kiMungu hiyo?. Ni ushujaa gani kauonyesha kwa ajili ya kanisa la Kristo mpaka siku yake ihadhimishwe?
Upendo tunaopaswa tuusambaze ni upendo wa Kristo, Na sio upendo wa Valentino.
Bwana atusaidie kwa hilo.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Je! mtu anapofunga kwa muda wa SAA 24,anapaswa kunywa maji au kitu chochote?
SWALI: Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yefhta, ya kumtoa binti yake kafara? Je Mungu anakubali sadaka za kuteketeza watu?
JIBU: Kabla ya kwenda kwa Yeftha turudi kwanza kwa Ibrahimu…swali ni je! Kwanini Mungu amwambie Ibrahimu akamtoe mwanawe kama sadaka ya kuteketezwa?..Je Mungu anaziridhia sadaka za kuchinja watu na kutoa kafara?..Kwanini asingemwambia akamtoe mbuzi tu na si mwanae? Ni muhimu kufahamu nyakati na majira Mungu aliyokuwa anatembea na watu wake…Zamani sana kabla Taifa la Israeli halijazaliwa…Kulikuwa hakuna mfumo maalumu wa kumwabudu Mungu…wengi walikuwa hawajui mapenzi kamili ya Mungu..Sheria ilivyokuja ndipo angalau watu wakaanza kumwelewa Mungu anataka nini.. Hivyo kabla ya Torati watu walikuwa hawaelewi kwa mapana Mungu anataka nini na hataki nini, au anapendezwa na nini na hapendezwi na nini…
Hivyo watu pia walikuwa wanatoa sadaka za kuteketeza watu (Au kuwapitisha watu kwenye moto) wakidhani wanampendeza Mungu…hali kadhalika watu walikuwa wanajitoa hata wao wenyewe wachomwe moto kama sadaka ya kuteketezwa wakijua wanampendeza Mungu… Hivyo hata wakati wa Ibrahimu, sadaka za watu kujitoa kuteketezwa zilikuwa zinaendelea…Na hivyo hata Ibrahimu alikuwa anajua ni sawa chochote kile Mtu anaweza kukitoa kama sadaka ya kuteketezwa kwa Mungu wake…
Kwasababu sheria bado ilikuwa haijaja!..Kwasababu sheria/Torati ndio ilikuwa kuwafumbua watu macho kuelewa mambo gani Mungu hayapendi na yapi anayapenda.
Warumi 7:7 “Tusemeje, basi? Torati ni dhambi? Hasha! Walakini singalitambua dhambi ila kwa sheria; kwa kuwa singalijua kutamani, kama torati isingalisema, Usitamani”.
Na Mungu aliutumia huo huo mfumo wao wa kuteketeza watu kumjaribu Ibrahimu…Ili kupitia huo amwonyeshe kuwa yeye haridhii sadaka za kuteketezwa watu..Ndio maana unaona alimwambia Ibrahimu akamtoe mwanawe kama sadaka ya kuteketezwa…na alipokuwa anaenda hata kabla ya kumchinja mwanawe Mungu alimzuia akamwonyesha mwanakondoo pembeni…akimfundisha kuwa Sadaka za kuwachinja wanadamu kama wanyama na kuwateketeza kwenye moto hazikubali na wala hazimfurahishi….bali sadaka za wanyama ndizo anazozikubali..ndio maana hakumruhusu amchinje mwanawe badala yake alimtumia mwanakondoo ambaye alitokea pale pale alipokuwepo…
Angekuwa anapendezwa na sadaka za watu asingemzuia Ibrahimu kumchinja mwanawe. Hivyo hiyo ikawa somo kwa Ibrahimu na wanawe kutojaribu kutoa sadaka za kuteketezwa watu..kwani Mungu hazikubali hizo hata kidogo. Na ilipofika wakati wa Sheria Mungu alitoa amri kwamba watu wasiwatoe wana wao kama sadaka ni machukizo na ni dhambi..Kasome Walawi 20:1-5,
Yeremia 7:30 “Maana wana wa Yuda wametenda yaliyo maovu machoni pangu, asema Bwana; wameweka machukizo yao ndani ya nyumba hiyo, iitwayo kwa jina langu, hata kuitia unajisi.
31 Nao wamepajenga mahali palipoinuka pa Tofethi, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ILI KUWATEKETEZA WANA WAO NA BINTI ZAO MOTONI; jambo ambalo mimi sikuliagiza, wala halikuingia moyoni mwangu”.
Soma tena..
Yeremia 19:4 “Kwa sababu wameniacha mimi, nao wamepafanya mahali hapa kuwa mahali pageni, nao hapa wamewafukizia uvumba miungu mingine wasiowajua, wala wao, wala baba zao, wala wafalme wa Yuda; nao wamepajaza mahali hapa damu ya wasio na hatia;
5 nao wamemjengea Baali mahali pake palipo juu, ili kuwachoma moto wana wao, wawe sadaka za kuteketezwa kwa Baali; tendo nisiloliamuru mimi, wala kulinena, wala halikuingia moyoni mwangu;”
Na mwisho..
Yeremia 32:33 “Tena wamenigeuzia visogo vyao, wala si nyuso zao; ingawa naliwafundisha, niliondoka mapema na kuwafundisha, lakini hawakusikiliza ili wapate mafundisho.
34 Bali waliweka machukizo yao ndani ya nyumba iliyoitwa kwa jina langu, ili kuinajisi.
35 Tena walijenga mahali palipoinuka kwa Baali, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ILI KUWAPITISHA WANA WAO NA BINTI ZAO KATIKA MOTO KWA AJILI YA MOLEKI, JAMBO NISILOWAAGIZA; WALA HALIKUINGIA MOYONI MWANGU KWAMBA WALITENDE CHUKIZO HILO; wapate kumkosesha Yuda”.
Mistari yote hiyo Bwana anasema tendo la kuteketeza watu kwenye moto hata halikumwingia moyoni mwake kabisa..Ni machukizo kufanya vile….Ndio maana hata Mungu alimzuia Ibrahimu. Sasa pamoja na kuwepo kwa sheria hizo..Bado wana wa Israeli walikuwa wanaendelea kufanya hizo sadaka..kama Bwana anavyosema hapo juu…Sasa tukirudi kwenye Biblia ndio tunamkuta Mtu ambaye anaitwa Yeftha ambaye alizaliwa baada ya sheria hiyo kuwekwa..
Huyu Yeftha alikuwa ni Mwamuzi wa Israeli ambaye alichaguliwa na Mungu kabisa…habari zake unaweza ukazisoma kwenye kitabu cha Waamuzi, historia ya maisha yake…Lakini kuna kipindi alitaka kwenda vitani kupigana na maadui zake ambao walikuwa ni maadui pia wa Taifa zima la Israeli..mtu huyu akamwekea Mungu nadhiri…pasipo kufikiri, akamwahidi Mungu endapo akipata ushindi chochote kitakachokuja mbele yake kumlaki atakitoa kuwa sadaka ya kuteketezwa..Bila kufikiri kuwa anaweza kuja hata ndugu yake au mwanawe…na aliposhinda akaja binti yake aliyemzaa kumlaki. Na kwasababu ameshaweka nadhiri ni lazima aitimize…hivyo akampitisha mwanawe kwenye moto…
Waamuzi 11:30 “Naye Yeftha akamwekea Bwana nadhiri, akasema, Kwamba wewe utawatia wana wa Amoni mkononi mwangu kweli,
31 ndipo itakuwa ya kwamba, kile kitakachotoka katika milango ya nyumba yangu kunilaki, hapo nitakaporudi na amani kutoka kwa hao wana wa Amoni, kitu hicho kitakuwa ni cha Bwana, nami nitakisongeza kiwe sadaka ya kuteketezwa”.
Sasa utauliza Yeftha alifanya dhambi kumpitisha mwanawe motoni?..Jibu ni ndio kwasababu alikwenda kinyume na Torati ya Mungu…iliyosema “msiwatoe wana wenu kuwapitisha motoni”…
Na utauliza pia je! Asingemtoa mwanawe pia angekuwa amefanya dhambi?..Jibu ni ndio angekuwa amefanya dhambi kwasababu amemwekea Mungu nadhiri ya upumbavu ambayo ameshindwa kuitoa…
Hivyo aidha angeitoa au asingeitoa bado Yeftha alikuwa hatiani?……Ingawa Yeftha alikuwa anamambo mengi ya kujifunza kutoka kwake lakini kwa hilo lilimtia doa kama lile la mke Uria lilivyomtia doa Daudi. Na ndio maana Yeftha hakutawala muda mrefu Israeli..alitawala miaka 6 tu wakati wengine walikuwa waamuzi wa Israeli hata kwa miaka 40..yeye alikaa miaka sita tu akafa..na ndiye mwamuzi aliyetawala muda mfupi kuliko wote.. Lakini yote hayo Mungu aliyaruhusu ili sisi tujifunze kwamba tusiweke nadhiri za upumbavu..Tujihadhari na nadhiri tunazoziweka…Nadhiri tuiwekeayo tuahakikishe inakubalika na Neno la Mungu na tumeifikira kwanza kabla ya kuiweka ili tusije tukajikuta tumejiweka katika mtego…(hali kadhalika tukio lile la Yeftha pia limebeba siri nyingine juu ya Yesu Kristo). Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Jehanamu ni nini?
MUNGU KUSEMA NA WEWE PEKEE, HAITOSHI KUKUPA USHINDI.
SADAKA YA MALIMBUKO.
JE UNAMTHAMINI BWANA?
JE KUCHOMA MAITI NI DHAMBI?
KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).
SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?
Hili ni swali ambalo lilikuwa sana katika kichwa changu kabla sijamfahamu Yesu Kristo, vilevile lipo katika vichwa vya watu wengi leo hii duniani, na nimeshaulizwa pia mara nyingi na baadhi ya watu?.. Hili swali linaibuka kutokana na jinsi watu tulivyojikuta tu ghafla tumetokea duniani bila hata ya kikao Fulani cha makubaliano, na jinsi tunavyoondoka ghafla bila hata ya taarifa zozote,.. Hapo ndipo tunajiuliza sasa maana ya Maisha ni nini? Na ni nani aliye nyuma yake?..Hivyo inatufanya kila mmoja kwa njia yake mwenyewe aanze kuchunguza na kutafiti na kujaribu kila njia na kila mbinu, ili mwisho wa siku apate jibu lake moja ambalo litampa sababu ya yeye kuwepo hapa duniani..
Hata kama ni wewe leo hii unajiuliza swali hilo, hujakosea hata kidogo kufiria hivyo, unawaza vyema kabisa.. Lakini nataka nikupe ushauri mmoja, kabla hujaanza kuchunguza kwa njia zako wewe mwenyewe embu jaribu kwanza kutafuta waliowahi kujiuliza swali kama hilo na hatua walizochukua na mwisho wao ukawaje?..Ili usije ukajikuta unarudia njia zilezile za kwao, na mwisho wa siku ukafikia pale pale walipo ukawa umepoteza muda mwingi wa utafiti ambao sio wa lazima.
Lakini leo hii nitakupa majibu ya kibiblia.. Na kitabu pekee ambacho kimetoa majibu ya maswali hayo ni kitabu cha Muhubiri..Hivyo kama unahitaji kupata jibu la swali hilo nakushauri ukisome kitabu chote kile kwa utaratibu na kwa umakini kisha utapata jibu lake mwishoni.
Aliyeandika kitabu kile ni Sulemani mwana wa Daudi, ambaye biblia inarekodi sio tu alikuwa ni mfalme mkuu sana bali pia alikuwa ni mtu mwenye Hekima kuliko watu wote waliokuwa wanaishi duniani wakati ule, na alikuwa pia ni mtu Tajiri ambaye hakukuwa na mfano wako, kabla yake na hata baada yake..
Sasa ilifikia kipindi akatamani kujua sana nini maana ya Maisha, na atafanya nini ili apate raha duniani, au apate jibu moja la uhakika kuhusu Maisha ya wanadamu,..Akasema nitajaribu kila kitu, na kila njia kwanza naanzana na Elimu, akaitafuta elimu kwa bidii, akaipata akawa na elimu kubwa ya kufahamu kila kila mnyama, na mmea, na viumbe vyote duniani (1Wafalme 4:33-34) na hekima iliyopo ndani yao, akaweza kutatua mafumbo magumu sana, akatunga mithali nyingi sana. Na akaandika vitabu vingi sana, hiyo yote ilikuwa ni kwa lengo la kupata labda jibu Fulani la Maisha pengine angegundua jambo Fulani ambalo lingemsaidia kupata kanuni rahisi ya watu kuishi duniani, au Maisha ya raha, na ya uhuru au ya furaha..lakini alipojaribu kufanya hivyo, ndivyo alivyozidi kuongezea huzuni na masikitiko anasema hivyo (Mhubiri 1:18) ..
Akasema nitajaribu wanawake..Akaenda kuoa wake 700 wazuri wanaotoka katika majumba ya kifalme tu, na Masuria 300, aangalie labda akiwa na hao atayafanya Maisha kuwa bora duniani, au ya furaha ..hilo nalo halikumletea majibu aliyokuwa anayatafuta..
Akajajiengea makasri makubwa, na kujiwekea posho ya chakula cha mwaka mzima, kila siku kwake ilikuwa ni sherehe..lakini bado hakukipata alichokuwa anakitafuta..
Akajaribu pombe, akawa anakunywa divai, lakini bado hakuna lolote aliloliona ndani yake lingeweza kufichua fumbo kubwa la maisha..akajaribu “upumbavu na wazimu” biblia inasema hivyo katika (Mhubiri 1:17), yaani mambo yote ambayo unaweza kuona ni ya kipumbavu, au wendawazimu kama vile kujitukuza, pengine kucheza dansi, n.k. lakini hakuna hata mmoja liliweza kumpa maana ya mambo yote, ..
Akajaribu kuwa na malengo makubwa akawa mfanya biashara mkubwa duniani, aione labda akishafanikiwa hapo atakipata kitu alichokuwa anakitafuta..lakini bado anasema hakukipata..
Ndipo katika dakika za mwisho, sasa katika uzee wake..Anagundua siri hii kuwa mambo yote ni ubatili, mito inapotoka ndipo huko huko inaporudi, jua linapochomozea ndipo huko huko litakuja kuchomozea tena, upepo unapovuma ndio kulekule utakaporudi kila kitu kipo katika mzunguko wake, Yule Mungu niliyeanzana naye, nitakapojitaabisha kwenda mbali naye, nitakaposema simtaki tena nataka nitafute mwenyewe akili zangu niijue ukweli wa Maisha, ndiye yule yule mwisho wa siku nitamrudia…
Unaweza Ukaona kumjua yeye kunakunyima uhuru wa kuishi..Utakwenda kutafuta unachokitaka katika moyo wako, lakini mwisho wa siku utamrudia yeye..Na hapo utakuwa umeshachelewa sana..
Ndio maana Mhubiri anamalizia kwa kusema…Jumla ya mambo yote ni UMCHE MUNGU…
Mhubiri 12:13 “Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.
14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya”.
Unaona,..Mhubiri ni mmojawapo wa waliotusaidia sisi kufanya utafiti, ili na sisi tusianze tena kupoteza muda mwingi kukimbizana na mambo ya Maisha tuanze kutafiti kwa akili zetu..tukidhani kuwa tutafika mahali Fulani paki pekee ambako wengine hawajafika kuhusu maisha,…kumbe tupo kwenye mzunguko ule ule wa zamani..
Leo hii tutamwacha Mungu tukatafute fedha, lakini tukishaiapata bado tutaona mbona hatujalipata lile kusudi lenyewe ndani yetu?..Tutamdharau Mungu tutasema tukatafute hekima yetu wenyewe…ni kweli tutafahamu vyote lakini mwisho wa siku swali litaendelea kubakia pale pale maana ya Maisha ni nini?
Jibu pekee la maana ya Maisha lipo kwa yeye aliyetuumba?
Mche yeye basi!… Na kumcha yeye ni kuingia katika kanuni yake.. Ambayo aliiweka tangu zamani kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwenguni.. Na kanuni yenyewe ndio hii..
Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”.
Ukimpata Yesu Kristo, hapo pekee ndipo utakapojua maana ya Maisha ni nini.. Kwasababu yeye anakupa uzima wa milele..Ukiwa na uzima wa milele wasiwasi wako utakuwa ni nini tena?….hutakuwa na hofu yoyote, na Maisha yako yatakuwa ya amani na furaha hapa duniani sikuzote..yaliyo mbali na utumwa wa hofu za Maisha..Hofu za kuogopa kesho itakuwaje..kwasababu Sulemani ndivyo alivyosema katika ..
Mhubiri 8:6 “Kwa maana kwa kila shauri kuna wakati na hukumu; kwa sababu mashaka ya mwanadamu yaliyo juu yake ni makubwa;
7 kwa kuwa hajui yatakayokuwako; kwa maana ni nani awezaye kumweleza jinsi yatakavyokuwa?
Hivyo kama na wewe bado unatafuta maaana ya Maisha, basi leo hii fahamu kuwa jibu ndio hilo hapo juu..acha kutanga tanga, mfuate YESU, akuponye nafsi yako, akupe tumaini la uzima wa milele..Uishi kwa amani siku zako zote ulizopo hapa duniani..Kwasababu kwingine kote hutapata..na kama ukijaribu kutafuta peke yako, ukweli ni kwamba utarudi hapo hapo kwa Mungu..Na wakati huo utakuwa umeshachelewa tayari.
Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo..Na kwamba unataka Kristo aingie ndani ya Maisha yako, akupe tumaini hilo na amani hiyo ya wokovu..
Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Ukizingatia hayo Bwana atakuangazia Nuru zake za wokovu daima hadi siku ile ya mwisho.
Ubarikiwe sana
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.
Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?
KARAMA YA MUNGU NI UZIMA WA MILELE.
Ikiwa sisi tuliumbwa na Mungu,Je! Mungu aliumbwa na nani?
NITAPOKEAJE NGUVU YA KUSHINDA DHAMBI?
JE UNAMTHAMINI BWANA?
CHACHU YA MAFARISAYO NA CHACHU YA HERODE.
Kusudi la Mungu ni lipi?
Jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze maneno ya uzima,
Baadhi yetu tunadhani mpaka Mungu atakapotuambia tufanye hivi au tufanye vile ndipo hapo tutakuwa na uhakika kuwa tunalolifanya ni kusudi la Mungu,… Lakini Jambo lingine ambalo pengine hatufahamu ni kuwa kila wazo au kusudi tunalolifanya liwe ni jema au ni baya..ndani yake limebeba kusudi la Mungu..Hata shetani alipoingiwa na wazo la tamaa la kuwa kama Mungu, mpaka akaleta migogoro kule mbinguni, na baadaye akatupwa huku chini duniani na kuendelea na uharibifu wake, alikuwa analitimiza kusudi la Mungu.. na ndio maana Mungu hakumuua tangu ule wakati hadi sasa..Ni kwasababu anayohuduma yake hapo, Siku atakapomaliza kusudi lote la Mungu ndipo atakapoharibiwa katika lile ziwa la Moto.
Yuda alipoingiwa na wazo la kumsaliti Bwana Yesu, Ni kweli lilikuwa ni wazo bovu lakini ndani yake, kulikuwa na kusudi la Mungu timilifu kabisa, ilikuwa ni lazima iwe vile ili Kristo asulibiwe tupate wokovu..Ipo mifano mingi ya namna hiyo katika biblia mfano Farao kuwa na moyo mgumu, Samsoni kwenda kuwapenda wanawake wa kifilisti, n.k.
Leo tutatazama tena katika maandiko, Taifa lingine ambalo Mungu alilichagua kufanya mapenzi yake ya kuyapiga mataifa, japo lilikuwa halijui kuwa linaifanya kazi ya Mungu…Na kupitia hilo ndio tutajifunza somo letu la leo.
Isaya 10:5 “Ole wake Ashuru! Fimbo ya hasira yangu, ambaye gongo lililo mkononi mwake ni ghadhabu yangu!
6 Nitamtuma juu ya taifa lenye kukufuru, nitampa maagizo juu ya watu wa ghadhabu yangu, ateke nyara, na kuchukua mateka, na kuwakanyaga kama matope ya njiani.
7 Lakini hivyo sivyo akusudiavyo mwenyewe, wala sivyo moyo wake uwazavyo; maana katika moyo wake akusudia kuharibu, na kukatilia mbali mataifa, wala si mataifa machache.
8 Maana asema, Je! Wakuu wangu si wote wafalme?”.
Kwa ufupi taifa hili la Ashuru enzi za wafalme lilikuwa ni moja katika ya mataifa matatu yenye nguvu duniani..mengineyo yakiwemo Misri, na Babeli..Ni sawa na leo Marekani, Urusi na China jinsi yalivyo na nguvu za kijenzi duniani.. Ndivyo ilivyokuwa wakati huo..
Sasa kama wewe ni msomaji wa biblia utagundua kuwa Hili taifa la Ashuru lilikuwa ni kubwa, na lenye nguvu sana kijeshi, hili ndio Mungu alilolitumia kulichukua taifa la Israeli utamwani(yale makabila yote 10), na lile moja lililosalia ndio lilikuja kuchukuliwa utumwani na babeli baadaye..
Na sio tu Israeli peke yake, hapana, bali ukisoma biblia utaona liliyapiga na mataifa mengine mengi sana..kama biblia inavyotuambia hapo sio machache. Na ni Mungu mwenyewe alilinyanyua liwe na nguvu kiasi hicho ili alitumie hilo kuyapiga hayo mataifa yote ambayo yalikuwa yanaabudu sanamu.
Lakini sasa..ukisoma kwa makini mstari wa 7 unasema.. Lakini hivyo sivyo akusudiavyo mwenyewe, wala sivyo moyo wake uwazavyo; maana katika moyo wake akusudia kuharibu…
Unaona?..moyoni mwake alikuwa hafikirii kuwa ndiye Mungu anayemtumia kulipiza kisasi, bali yeye alikuwa anafiriki kuwa anayakomesha yale mataifa yaliyokuwa hayamtii, au alikuwa anawaza kujiongezea tu himaya yake,..apate mali nyingi na mateka mengi..Hivyo akawa anafanya kwa bidii sana na kwa jinsi alivyokuwa anafanya bidii Zaidi kutaka awe ngome thabiti kwa kuyapiga mataifa ndivyo alivyokuwa analitimiza kusudi la Mungu kirahisi Zaidi pasipo yeye kujijua…
Na ndio maana Bwana Yesu alimwambia Yuda…uyatendayo uyatende upesi..(Yohana 13:27)..Yaani yale maazimio mabovu yaliyokuwa ndani yake ya kutaka apate pesa kwa kumsaliti Bwana ayafanikishe upesi kwasababu kwa kupitia hayo ataharikisha pia kusudi la Mungu lifanyike haraka..
Lakini hawa wote tunaona mwisho wao ulivyokuja kuwa mbaya..Mataifa hayo yalikuja kuangamziwa vibaya..vilevile na Yuda..
Sasa nachotaka uone ni kuwa kanuni hiyo hiyo, wakati mwingine ndiyo Mungu huwa anayoitumia hata kutimiza mapenzi yake makamilifu ndani ya watu wake.
Mungu akitaka kufanya jambo lolote jema, labda tuseme la kumwokoa mtu fulani mlevi aliyeshindakana.. kwanza ataanza atamnyanyua mtu fulani..Na mtu huyo hajui kuwa ametumwa kwa mlevi, yeye akilini mwake anaweza kufikiri labda ni mtu tu fulani pale stendi……Lakini kumbe ndani yake anakwenda kulitimiza kusudi la Mungu alilolipanga juu ya mlevi Fulani aliyeko mahali pale.
Kwamfano anaweza ukasema ngoja nitoke nikasambaze kipeperushi vya injili stendi ya mabasi..Akatoka na vitano, akawapa watu 5 kisha akaondoka zake, mmoja wa wale 5 akawa sio mkristo, akakichukua akakisoma kisha akakiacha pale pale stendi kwenye daladala..Na baada ya muda mfupi akaja mtu mwingine akakiona kwenye siti kikamvutia akakichukua akaenda nacho nyumbani..akakiweka kwenye kabati ikapitia hata miaka 2,siku moja mume wake ambaye ni mlevi ametoka bar, akiwa katika kuyatafakari Maisha yake ya dhambi, akajisema moyoni Eee Mungu, Kama wewe unanipenda mimi basi naomba unionyeshe ni nini cha kufanya..Na saa hiyo hiyo wakati anayafikiria hayo anafungua kabati lake atafute biblia anakutana na kile kipeperushi ulichokisambaza wewe miaka 2 iliyopita, na ndani yake anakutana na ujumbe ambao ulikuwa unaendana na jambo lile lile alilokuwa anamwomba Mungu…Na mlevi huyo usiku huo huo anampa Bwana Maisha yake.. Na mbingu inaandika wewe umelitimiza kikamilifu kusudi la Mungu alilokupa la kwenda kumuokoa mlevi..ingawa wewe hujui chochote kinachoendelea.
Lakini ilikuwa ni sharti kwanza wazo fulani jema liingie ndani yako, kisha kwa kupitia hilo ulitimize kusudi la Mungu ambalo ulikuwa hujui ni lipi..Huo ni mfano tu..
Kwahiyo hivyo ndivyo Mungu anavyotimiza mapenzi yake kwa kupitia watu..Hatuwezi kuijua kazi yote ya Mungu..na ndio maana biblia inatuambia..
Mhubiri 11:4 “Mwenye kuuangalia upepo hatapanda; Naye ayatazamaye mawingu hatavuna.
5 Kama vile wewe usipojua njia ya upepo ni ipi, wala jinsi mifupa ikuavyo tumboni mwake mja mzito; kadhalika HUIJUI KAZI YA MUNGU, AFANYAYE MAMBO YOTE.
6 Asubuhi panda mbegu zako, Wala jioni usiuzuie mkono wako. Kwa maana wewe hujui ni zipi zitakazofanikiwa,kama ni hii au hii,au kama zote zitafaa sawasawa”.
Hivyo sisi tukijitoa kufanya kila kitu chema kinachohusiana na kazi yake, basi huko huko ndipo atakapotimiza kusudi lake alilolipanga kwa watu wake..
Na tena tukifanya kwa bidii Zaidi ndivyo Mungu atakavyotutumia Zaidi kutimiza makusudi yake..Kwahiyo kama wewe unahubiri basi ongeza bidii Zaidi katika kuhubiri kwako, usiangalie ni matunda mangapi leo hii nimeyapata kwa Kristo au la, maadamu unachokifanya kinaleta manufaa katika ufalme wa mbinguni, endelea usianze kujiuliza uliza, je ni kweli ninafanya mapenzi ya Mungu au la..Wewe fanya tena kwa bidii sana..na huko huko Mungu atakafanya kazi zake mwenyewe..Hivyo anza sasa kutumika..kwa kile Mungu alichokukirimia.
Lakini kama wewe ni mwovu kama lilivyokuwa taifa la Babeli, na Misri na Ashuru, ambayo baadaye baada ya kumaliza kusudi la Mungu la kuyapiga mataifa mengine, nayo pia yaliharibiwa..pamoja na Yuda na ibilisi mwenyewe siku ya mwisho, ndivyo itakavyokuwa na kwako, wewe ambaye unawapiga wengine, unawadhulumu wengine, unawaibia, unawasambazia ukimwi kwa makusudi mwisho wako utafika, pengine Mungu anaweza kukutumia kuwaadhibu hao lakini na wewe hutasalimika.. Mungu atakupiga na utakwenda Jehanaumu, na kule kitengo chako kitakuwa ni kikubwa Zaidi…Ni heri ukatubu dhambi zako sasa, Ili uokolewe.
Anza kuwaza vema kuyatenda yale yampendezayo Mungu.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Karibu tujifunze Biblia.
Hizi tabu tunazoziona na kuzipitia sasa upo wakati umewekwa zitakwisha…
Ufunuo 21:3 “Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.
5 Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.
6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.
7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu”
Magonjwa ni mambo ya kwanza..Yatapita yote!…HIV haitakuwepo kule ng’ambo, Kansa haitakuwepo, upofu hautakuwepo, kutokusikia hakutakuwepo, ulemavu wa Ngozi, akili, wala viungo hautakuwepo, vita havitakuwepo, chuki wala kuchukiwa hakutakuwepo, maadui hawatakuwepo, visasi havitakuwepo, kuteswa hakutakuwepo, kupapambana kutafuta Maisha hakutakuwepo, vifungo havitakuwepo, magereza na mahabusu hayatakuwepo kule, maumivu, huzuni, unyonge na uchungu havitakuwepo, kupanda na mwingine kuharibu hakutakuwepo,…
Ni paradiso ya furaha isiyo ya kifani…Kule hakuna vidonda tena…wala kulia, wala kupokea taarifa mbaya za misiba…wala hofu haitakuwepo tena…wala mashindano wala mateso….Hayo ni mambo ya kwanza…Furaha tutakayoipata tutakapoingia huko itaimeza uchungu wote tuliokuwa tunaupitia duniani…
Hutakuwa na muda wa kukumbuka kwamba ulishawahi kupitia tabu…Utahisi uliumbiwa tu raha tangu zamani…Furaha utakayoipata huko hutakumbuka kwamba kuna siku ulishawahi kuteseka sana ukiwa duniani kiasi cha kufa…Hutakumbuka hata kidogo..utasahau kabisa!…Utajiri utakaoupata huko hutakumbuka kwamba ulishawahi kuwa maskini duniani…Utaona kama hukuwahi kuishigi sehemu nyingine Zaidi ya hiyo hapo kabla….Ni furaha isiyoelezeka…
Tujitahidi sana tufike huko kwasababu siku za kwenda huko zimekaribia sana kulinga na unabii wa kibiblia…Siku yoyote isiyotegemewa na wengi..parapanda italia, wafu watafufuliwa kwanza wale waliokufa katika Imani na utakatifu..na sisi tuliomwamini Yesu na kuishi Maisha ya usafi tutawaona na kwa pamoja wakitoka makaburini mwao, kisha tutaungana nao..na kufumba na kufumbua miili yetu itabadilishwa na kung’aa kama ya malaika wa mbinguni..na tutanyakuliwa juu mawinguni kukutana na Bwana wetu Kristo akitungoja mawinguni ili kutupelekwa mbali sana kule juu zaidi ya nyota zote na sayari zote kwenye Mbingu za Baba yetu Mungu mwenyezi..huko tutakwenda kula mema yote Mungu aliyotuandalia…
Ni mbali sana, juu sana, yaani “mbingu, na mbingu-za-mbingu-za-mbingu” Mungu aketipo kama biblia inavyomzungumzia katika 2Nyakati 6:18 .. Huko ndiko kutakuwa makao yako wewe ambaye leo hii umedhamiria kung’ang’ana na Yesu, uliyedhamiria kusema iwe isiwe siuachi wokovu..
Lakini tusipojiandaa leo, kinyume chake tukaendelea kudumu katika mambo ya dunia hii,..tukaendelea kudumu katika uasherati, wizi, ulevi, utukanaji, ibada za sanamu, tukaendelea kuidharau Injili ya msalaba wa Yesu, halafu Unyakuo ukipita leo hatutakwenda popote na hata tukifa kabla ya unyakuo kutokea hatutafufuliwa kwenda mbinguni.
Sasa itatufaidia nini kupata majumba tele leo, kupata viwanja vyote leo, kupata wake/ waume wengi leo, kupata umaarufu wote na kisha kupata hasara ya nafsi zetu?..si ni heri niendelee tu kuwa maskini lakini nisiikose mbingu…Kwasababu kama umaskini wangu utanifanya nimsogelee Mungu Zaidi, kama utanifanya muda wangu mwingi niutumie kwa Bwana, kama utanifanya nisiwe mtu wa kula rushwa au kupokea rushwa ni heri niendelee kuwa maskini lakini niwepo miongoni mwa wale watakaokwenda na Bwana siku ile..Kwa maana najua utajiri nitakaokuwa nao kule hautalinganishwi ni utajiri wa kupita wa hapa duniani.
Kwa kumalizia mstari huo mstari hapo juu unasema..
Ufunuo 21:5 “Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.
6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.
7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
8 Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.”
Maji ya UZIMA YANAPATIKANA BURE…kama hujaokoka, mlango wa wokovu upo wazi sasahivi..kwasababu bado huijui baadaye yako pengine umebakisha masaa tu ya kuishi, hivyo okoka leo..pale ulipo jitenge dakika chache omba toba kwa Mungu wako kwa yote na Maisha yote ya dhambi uliyokuwa unayaishi huko nyuma..Tubu kwa kumaanisha kabisa na kwa vitendo..dhamiria kuacha kuanzia leo pombe, rushwa, sigara, zinaa, wizi, uvaaji vimini, na suruali na uwekaji wa makeup kwenye uso wako..dhamiria kuacha yote hayo na kisha katafute ubatizo sahihi ukabatizwe..kumbuka ubatizo sahihi sio wa kunyunyiziwa..kama ulinyunyiziwa basi ulifanyiwa hivyo kimakosa..hivyo unapaswa ukabatizwe tena katika ubatizo sahihi wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa Jina la Yesu Kristo kwaajili ya ondoleo la dhambi zako (Marko 16:16, Matendo 2:38, Matendo 8:16, Matendo 19:5, na Matendo 10:48). Na Bwana mwenyewe kupitia Roho Mtakatifu atakayeingia ndani yako atakuongoza kufanya yaliyosalia yaliyo mapenzi yake.
Wote tufike mbinguni..AMEN.
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Petro aliambiwa na Bwana Yesu UKIONGOKA WAIMARISHE NA NDUGU ZAKO. Je! kuongoka maana yake nini?