Historia ya wimbo wa tenzi – Ndio dhamana Yesu wangu. (Blessed assuarance)
Wimbo huu ulindikwa na mwanamke mmoja aliyeitwa Fanny Crosby, Mwanamke huyu japo aliishi kwa miaka 95 akiwa kipofu,lakini hakuacha kuitumia neema Mungu aliyompa kutangaza injili kwa njia ya Nyimbo zenye muundo wa Tenzi za rohoni na nyinginezo, katika maisha yake alifanikiwa kuandika nyimbo zaidi ya 8000, Na hii nyimbo “Ndio dhamana Yesu wangu” Ikiwa mojawapo, Nyingine inayojulikana sana mpaka leo ni “Usinipite mwokozi” yeye pia ndio aliyeiandika nyimbo hii alipokuwa amewatembelea wafungwa gerezani(angalia historia yake chini).
Phoebe Knapp
Sasa Siku moja alipokuwa amemtembelea rafiki yake nyumbani kwake aliyeitwa Phoebe Knapp, ambaye alikuwa ni mtunzi wa sauti za nyimbo, wakiwa nyumbani kwake Phoebe alianza kupiga mdundo wake aliokuwa ameutunga, kisha baada ya muda alimuuliza Fanny, Je unaweza kuniambia mdundo huu ni wa nyimbo gani?
Ndipo Fanny akamwambia “Ndio dhamana Yesu wangu”. Basi hapo ndio pakawa mwanzo wa mdundo na utunzi wa wimbo huo (1873).
Ndio dhamana Yesu wangu.
Ndiyo dhamana, Yesu wangu; |
Hunipa furaha za mbingu; |
Mrithi wa wokovu wake, |
Nimezawa kwa Roho wake. |
Habari njema, raha yangu, |
Yesu ndiye Mwokozi wangu, |
Habari njema, raha yangu, |
Yesu ndiye Mwokozi wangu. |
Kumsalimu moyo wangu, |
Mara namwona raha yangu; |
Aniletea malaika, |
Wananilinda, tutaokoka. |
Habari njema, raha yangu, |
Yesu ndiye Mwokozi wangu, |
Habari njema, raha yangu, |
Yesu ndiye Mwokozi wangu. |
Sina kinyume; nashukuru, |
Mchana kutwa huja kwangu; |
Usiku kucha kuna nuru; |
Mwokozi wangu; ndimi nuru. |
Habari njema, raha yangu, |
Yesu ndiye Mwokozi wangu, |
Habari njema, raha yangu, |
Yesu ndiye Mwokozi wangu. |
Hali na mali; anitwaa! |
Mara namwona anifaa, |
Nami nangonja kwa subira; |
Akiniita, nije mara. |
Habari njema, raha yangu, |
Yesu ndiye Mwokozi wangu, |
Habari njema, raha yangu, |
Yesu ndiye Mwokozi wangu. |
*****
Uimbapo wimbo huu kumbuka ni kipofu ndiye aliyeuandika, nawe pia unaposema “Ndio dhamana Yesu wangu” Basi awe kweli wokovu wako. Mpende yeye bila unafki na kumtumikia kwasababu ndiye aliyekufa kwa ajili yako.
Je! Umeokoka? Unajua kuwa Unyakuo upo karibu sana, kwasababu tunaishi katika kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia? Na kwamba hatutakuwa na kanisa lingine zaidi ya hili? Siku hizi zimekwisha, Hivyo kama upo tayari kumpa Yesu maisha yako leo ili wimbo huu uwe na maana kweli kwako. Basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>>KUONGOZWA SALA YA TOBA
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
USINIPITE MWOKOZI Lyrics
YOTE NAMTOLEA YESU_Tenzi za Rohoni.
BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics
CHA KUTUMAINI SINA lyrics
KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
MPINGA-KRISTO
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
UFUNUO: Mlango wa 1
Yote namtolea Yesu_tenzi za rohoni|Swahili hymn.
Wimbo huu uliandikwa na ndugu mmoja wa kimarekani aliyeitwa Judson W. Van DeVenter, Ndugu huyu alilelewa katika mazingira ya kikristo, aliokoka akiwa na miaka 17, kuanzia huo wakati wito wa kujitoa kikamilifu ulianza kuita ndani yake,lakini bado hakufanya uamuzi huo. DeVenter alifanikiwa kusoma mpaka chuo kikuu na kutunikiwa shahaba ya Sanaa, aliajiriwa kama mwalimu na mwongozaji katika shule za sanaa, hiyo ilimfanya aweze kusafiri sehemu nyingi mbalimbali katika bara la Ulaya kutokana na kazi yake ya sanaa.
Zaidi ya hilo alisomea pia na kufundisha elimu ya muziki, ilimchukua miaka 5 mpaka “Kumtolea yote Yesu”, Na hiyo ilikuwa ni baada ya marafiki zake kumshawishi sana, aingie katika kazi ya kumtumikia Mungu.
Mwaka 1896 Siku moja alipokuwa anafanya huduma ya muziki katika kanisani, hii ndio siku aliyoamua kuyasalimisha maisha yake ya ki-utumishi moja kwa moja kwa Kristo akiwa na miaka 41, aliamua kujitoa moja kwa moja kwa ajili ya kuifanya kazi ya unjilisti, na ndipo hapo huu wimbo “Yote namtolea Yesu” ulipozaliwa ndani ya moyo wake.
YOTE WA YESU.
Yote Namtolea Yesu. |
Nampa moyo wote, |
Nitampenda siku zote, |
Namwandama kila saa. |
Yote kwa Yesu, |
Yote kwa Yesu, |
Yote kwako, Ee Mwokozi, |
Natoa sasa. |
Yote namtolea Yesu, |
Nainamia pake; |
Nimeacha na anasa, |
Kwako Yesu nipokee |
Yote kwa Yesu, |
Yote kwa Yesu, |
Yote kwako, Ee Mwokozi, |
Natoa sasa. |
Yote namtolea Yesu, |
Nifanye niwe wako; |
Nipe Roho yako, Bwana, |
Anilinde daima, |
Yote kwa Yesu, |
Yote kwa Yesu, |
Yote kwako, Ee Mwokozi, |
Natoa sasa. |
Yote namtolea Yesu, |
Nami naona sasa; |
Furaha ya ukombozi; |
Nasifu jina lake. |
Yote kwa Yesu, |
Yote kwa Yesu, |
Yote kwako, Ee Mwokozi, |
Natoa sasa. |
*****
Je! Na sisi tunapouimba wimbo huu tunaweza kumtolea Yote Yesu?. Je! mali zetu tunaweza kumpa yeye, nguvu zetu tunaweza kuzielekeza kwake?, akili zetu tunaweza kuzitumia ziitende kazi ya Mungu? Kama sivyo basi wimbo huu tutauimba kinafki.
Bwana atutupe kutambua hayo.
Shalom.
Je! Umeokoka? Ikiwa bado hujaokoka na unahitaji kuokoka leo, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo mbalimbali ya Neno la Mungu, kwa njia ya whatsapp yako, basi tutumie ujumbe kwa namba hii :+255 789001312
Mada Nyinginezo:
YESU KWETU NI RAFIKI
NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics
BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics
KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
MAONO YA NABII AMOSI.
Neno Kristo, na Masihi ni kitu kimoja, isipokuwa kwa lugha ya Kiebrania linatamkwa kama Masihi, lakini kwa lugha ya kigiriki linatamkwa kama Kristo.
Yohana 1:41 “Huyo akamwona kwanza Simoni, ndugu yake mwenyewe, akamwambia, Tumemwona Masihi (maana yake, Kristo)”.
Hivyo Neno hili Kristo/Masihi linamaanisha mtiwa mafuta.
Mtiwa mafuta ni mtu yeyote aliyechaguliwa au aliyetengwa na Mungu kuwa wakfu kwa ajili ya kutimiza kusudi lake Fulani..Aidha na kuokoa, au kutawala, au kuchunga.
> Hivyo manabii wote unaowasoma katika biblia walikuwa ni masihi au Kristo kwa Mungu, kwa lengo la kuitabiria Israeli, na kuwaelekeza maagizo yatokayo kwa Mungu.
1Nyakati 16:22 “Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu”.
> Makuhani wote tunaowasoma katika biblia walikuwa ni masihi au maKristo wa Bwana wakifanya kazi ya upatanisho wa dhambi za watu na makosa yao.
> Waamuzi wote unaowasoma katika biblia walikuwa ni masihi wa Bwana waliotiwa mafuta kwa lengo la kuwakomboa wanadamu.Wakina Gideoni, Samsoni, Yeftha wote hao walikuwa ni masihi wa Bwana.
> Vilevile wafalme wote iwe ni wa wale waliotoka Israeli, au hawajatoka Israeli tunaowasoma katika biblia walikuwa ni masihi wa Bwana kwa ajili ya kuwaongoza watu wake.
1Samweli 24:5 “Lakini halafu, moyo wake Daudi ukamchoma, kwa sababu amekata upindo wa vazi lake Sauli.
6 Akawaambia watu wake, Hasha! Nisimtendee bwana wangu, masihi wa BWANA,neno hili,kuunyosha mkono wangu juu yake,kwa maana yeye ni masihi wa BWANA”.
Isaya 45:1 “Haya ndiyo Bwana amwambiayo Koreshi, masihi wake,ambaye nimemshika mkono wake wa kuume,ili kutiisha mataifa mbele yake,name nitalegeza viuno vya wafalme;ili kufungua milango mbele yake,hata malango hayatafungwa.
2 Nitakwenda mbele yako, na kupasawazisha mahali palipoparuza; nitavunja vipande vipande milango ya shaba, na kukata-kata mapingo ya chuma”;
Lakini hao wote walikuwa ni kivuli cha MASIHI/KRISTO MKUU NA HALISI atakayekuja, ambaye alitiwa mafuta mengi sana yasiyoelezeka kuliko wote, biblia inasema hivyo, na huyo si mwingine zaidi ya YESU.
Waebrania 1:8 “Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,Mungu,ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.
9 Umependa haki, umechukia maasi; KWA HIYO MUNGU, MUNGU WAKO, AMEKUTIA MAFUTA, MAFUTA YA SHANGWE KUPITA WENZIO”.
Na ndio maana haitwi tu Yesu peke yake, bali anaitwa YESU KRISTO.
Yesu Kristo ametiwa mafuta ya mengi sana ya kuwakomboa wanadamu. Yeye anayo mafuta yote ya kikuhani ndani yake, anayo mafuta ya kifalme ndani yake, anayo mafuta ya kinabii ndani yake, anayo mafuta ya kichungaji ndani yake.. Yaani kwa ufupi mafuta yote ya karama za Mungu yapo ndani yake.
Hivyo mtu akimwamini Yesu, basi amepata kila kitu, ikiwemo ukombozi wa roho yake.
Lakini tahadhari ni kuwa biblia imetabiri kuwa siku za mwisho kutatokea makristo wengi wa uongo ili kuwadanganya watu wengi.
Mathayo 24:24 “Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule.
25 Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele”.
Kumbuka anasema watatokea makristo, hasemi ma-yesu, ikiwa na maana kuwa watakuwa ni watiwa mafuta lakini ni watiwa mafuta ya uongo, watakuwa wanaweza kweli wakawaombea watu kwa jina la Yesu na wakapona lakini injili yao ni injili potofu isiyoweza kumwokoa yeye, wala hao anaowaongoza.
Na ndio maana Bwana Yesu alisema..
Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.
Hivyo je! Swali na wewe umechukuliwa na hili wimbi la makristo wa uongo?
Tunaishi katika wakati mgumu na wa hatari kuliko yote katika historia, hivyo kama maisha yako yapo mbali na Kristo basi ujue upo hatarini sana kupotezwa.
Kwanini usimpe Kristo leo maisha yako ayabadilishe, kisha yeye mwenyewe akupe Roho wake Mtakatifu atakayekusaidia kuijua kweli yote ya kimaandiko, ambaye atakaa ndani yako kukulinda mitego yote ya ibilisi?. Kama leo upo tayari kufanya hivyo, na unasema sitaki tena maisha ya dhambi nataka Yesu aniokoe awe peke yake masihi ndani yangu. Basi fungua link hii kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
UPAKO NI NINI?
KUWA MWAMINIFU KWA MANENO YAKO MWENYEWE,
AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.
Yakobo alikuwa na watoto wangapi?
REKEBISHA YAFUATAYO ILI MAMBO YAENDE SAWA.
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU UPENDO.
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
Kuwa mwaminifu kwa maneno yako mwenyewe, ni muhimu sana!.
Jina la Bwana wetu Yesu libarikiwe. Karibu tujifunze biblia.
Mwinjilisti mmoja alichukuliwa katika maono mbinguni akakutana na Bwana Yesu, alionyeshwa mambo mengi yatakayotokea baada ya Maisha haya, kwa wema na waovu, lakini Pamoja na hayo kuna mambo mengine aliambiwa ambayo naamini leo tukiyatafakari yatatusaidia.
Na jambo mojawapo aliloambiwa lilikuwa ni kuhusu “uaminifu”…kulingana na maelezo yake, anasema Bwana Yesu alimwambia haya maneno;
“Neno langu ni nguvu inayoshikilia vitu vyote. Kwa kiwango ambacho unavyoamini Neno langu ni kweli, ndivyo unavyoweza kufanya vitu vyote. Wale ambao wanaamini kwamba maneno Yangu ni kweli, basi watakuwa pia wakweli kwa maneno yao wenyewe, Ni asili yangu kuwa kweli, na uumbaji huliamini Neno Langu kwa sababu mimi ni mwaminifu na kwake.
Wale ambao ni kama mimi, pia huwa ni wakweli kwa maneno yao wenyewe. Neno lao ni hakika, na ahadi zao ni za kuaminika. ‘ndio’ yao inamaanisha ‘NDIO!’ na ‘hapana’ yao inamaanisha ‘HAPANA!’. Ikiwa maneno yako mwenyewe sio kweli, ni lazima pia utaanza kutilia shaka maneno Yangu, kwa sababu udanganyifu uko moyoni mwako. Ikiwa wewe sio mwaminifu kwa maneno yako mwenyewe, ni kwa sababu bado hujanijua kabisa mimi ni nani, mimi ni mwaminifu kwa maneno yangu. Ili kuwa na imani, lazima uwe mwaminifu kwa maneno yako. Nimekuita utembee kwa imani kwa sababu mimi ni mwaminifu. Hiyo ni asili yangu”.
**mwisho**
Ndugu moja ya tatizo kubwa linalowakabili wakristo wengi wa sasa, ni kukosa UAMINIFU. Na uaminifu unaanza kwa mtu kukosa uaminifu kwa mambo yake mwenyewe kwanza. Kwamfano mtu baada ya kumpa Yesu Maisha yake, akaahidi kwamba hatasengenya tena, hatatukana, hataiba, hatafanya hichi au kile anaahidi pia atamtumikia Mungu, au atakuwa mtu wa kumtolea Mungu sana n.k..lakini baada ya muda kupita anaanza kwenda kinyume na kile alichokisema au alichokipanga. Ndugu hiyo ni hatari sana.
Maneno hayo ya mwinjilisti huyo aliyoambiwa na Bwana, nayaamini asilimia mia kuwa ni kweli. Hata katika hali ya kawaida kama huwezi kuwa mwaminifu kwa mali yako mwenyewe ni Dhahiri kuwa haiwezekani kuwa mwaminifu kwa mali ya mwingine. Kama kiatu chako mwenyewe hukitunzi wala hukijali utakijali vipi kiatu cha mwingine aliyekuazima ukivae kwa muda tu!. Uaminifu wa mtu unaanza kwa kile alichonacho yeye mwenyewe, ndipo aweze kuwa mwaminifu kwa kitu cha mwingine.
Kadhalika huwezi kuwa mwaminifu kwa Maneno ya Mungu, kama sio mwaminifu kwa maneno yako mwenyewe.
Katika Luka 16:10 Bwana Yesu alisema maneno haya..
“Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia”.
Hivyo tujifunze kuyashika maneno yetu wenyewe..Ndipo tutakapoona Neno la Mungu likiwa na nguvu juu ya maisha yetu… Ukisema sitaki hichi au kile!, au nataka hichi!..basi kishikilie hicho kweli kweli usiwe na mawazo mawili mawili… Hiyo nguvu ya Maamuzi ndio chanzo cha nguvu zako za kiroho. Hata likitokea jambo mbele yako, na ukanukuu mstari Fulani kwenye biblia kwa Imani, basi jambo lile ulilolitamka kufuatia mstari huo uliounukuu, litatimia kama ulivyolisema kwasababu wewe pia huwa ni mkweli katika maneno yako…Hivyo Mungu atahakikisha na yeye analifanya neno lake kuwa kweli juu yako. Lakini tusipokuwa wakweli kwenye maneno yetu, basi kuna uwezekano pia neno la Mungu lisiwe kweli juu yetu. Tunaweza tukalinukuu sana na tusiona matokeo yoyote.. kwasababu sisi wenyewe sio waaminifu.
Bwana atusaidie, na atubariki.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Je! Ni ipi tarehe sahihi Evil-merodaki alimtoa Yekonia gerezani?
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
ZABURI 91, NI ZABURI YENYE NGUVU NYINGI.
SABATO TATU NI NINI?
Je! Mtume Paulo alikuwa ni Mrumi, Myahudi au raia wa Tarso?
JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?
NA UPEPO WA KUSI ULIPOANZA KUVUMA KIDOGO,
Hakuna mtu anenaye katika Roho,kusema Yesu amelaaniwa
Kwanini Amelaaniwa aangikwaye msalabani?
Kutundikwa msalaba au kwa jina lingine kutundikwa mtini, ilikuwa ni adhabu iliyotekelezwa kwa watu wenye makosa ya hali ya juu sana.
Adhabu hii ilikuwa sio tu ilikuwa inatekelezwa na watu wa mataifa mengine kama wengi wanavyodhani ni Warumi tu, hapana bali pia ilikuwa inatekelezwa na Israeli pia.
Ni adhabu yenye mateso mengi sana, na vilevile ni adhabu ya aibu. Waliokuwa wanatundikwa msabani walikuwa sana sana ni wauaji. Makosa ambayo yalikuwa yanathibitisha kuwa wamelaaniwa na Mungu.
Kumbukumbu 21:22 “Akiwa mtu ametenda dhambi ipasayo kufa, akauawa, nawe ukamtundika juu ya mti;
23 mzoga wake usikae usiku kucha juu ya mti; lazima utamzika siku iyo hiyo; kwani aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu; usije ukatia unajisi katika nchi yako akupayo Bwana, Mungu wako, iwe urithi wako”.
Utasoma sehemu nyingi, katika biblia mifano ya watu waliangikwa msalabani. (Mwanzo 40:18-19, Esta 2:22-23, Esta 7:10)
Jambo hilo hilo tunaliona mpaka katika kipindi cha karibu na agano jipya, katika ule ufalme wa Rumi, wafungwa wote waliokuwa na kesi kubwa za mauaji au wizi, n.k. Adhabu yao ilikuwa ni kuangikwa/kutundikwa msalabani ukiwa hai.
Lakini cha ajabu ni kwamba, adhabu zilizokuwa zinawahusu watu waliolaaniwa, zilimkuta mtu ambaye hakuwahi kutenda dhambi hata moja..Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO
Wagalatia 3:13 “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, AMELAANIWA KILA MTU AANGIKWAYE JUU YA MTI;
14 ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani”.
Lakini ni kwanini yamkute hayo yote?
Je ni ilikuwa ni bahati mbaya tu? Au Mungu alishindwa kumzuia? Jibu ni la, ilitokea vile kwa makusudi kabisa, ili ile hati ya mashitaka ya waliolaaniwa ifutwe juu yetu, aliibeba yeye ile hati ya laana, na ndio maana pale ambapo Baraba muuaji alipopaswa auawe, Yesu aliuawa badala yake, pale ambapo wewe mzinzi ungepaswa uhukumiwe milele kwa makosa yako, Yesu aliichukua laana hiyo siku ile msalabani, pale ambapo wewe uliye na dhambi ambazo nyingine ni aibu kuzitaja, Yesu alizichukua, hatia zote kwako.
Lakini hizo haziwezi kufutika juu yako, hivi hivi tu, bali ni mpaka uende kuzisalimisha msalabani.
Na ndio maana unahitaji kumpokea Yesu maishani mwako, vinginevyo hati ya mashitaka ya dhambi zako zitaendelea kubakia juu yako hadi siku ya mwisho, na utahukumiwa kama mkosaji.
Lakini ikiwa leo upo tayari kumpokea Yesu maishani mwako, basi leo leo atazifuta dhambi zako bure kabisa, haijalishi wewe ni mwenye dhambi kiasi gani.
Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.
5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
Hivyo kama upo tayari leo kumpa Yesu maisha yako, basi uamuzi huo ni wa busara, hivyo fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Tafadhali Share na wengine, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au katika namba hii hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?
Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?
MASOMO MBALIMBALI YA NENO LA MUNGU.
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
UTASIMAMA PEKE YAKO SIKU ILE.
USINIPITE MWOKOZI Lyrics
Je! Watoto wa Ibrahimu/Wana wa Ibrahimu walikuwa ni wangapi?
Jumla ya wana wa Ibrahimu walikuwa ni nane (8). Kulingana na Biblia.
Mwana wa kwanza alikuwa ni Ishmaeli, ambaye alizaliwa na kijazi wa mke wake Sara aliyeitwa Hajiri (Mwanzo 16:1-4).
Mwana wa Pili, alikuwa ni Isaka,(Ndiye mwana wa Ahadi) ambaye alizaliwa miaka 14 baada ya Ishmaeli kuzaliwa.
Mwanzo 21:1 “Bwana akamjia Sara kama alivyonena, na Bwana akamfanyia kama alivyosema.
2 Sara akapata mimba akamzalia Ibrahimu mwana wa kiume katika uzee wake, kwa muhula alioambiwa na Mungu. 3 Ibrahimu akamwita jina lake Isaka, yule mwana aliyezaliwa, ambaye Sara alimzalia”.
Sara alipofariki, Ibrahimu akaoa mke mwingine, aliyeitwa Ketura. (Mwanzo 25:1-2)
Huyu Ketura ndiye aliyemzaliwa Ibrahimu wana wengine 6. Kufanya jumla ya watoto wote wa Ibrahimu kuwa 8, Biblia haielezi kuwa alikuwa na wana wengine wa kike.
Lakini katika wana hao wote, ni mmoja tu, aliyekuwa mrithi wa Ibrahimu, naye ni Isaka. Na siri moja ni kuwa wale wana wengine Ibrahimu aliwapa zawadi nyingi, lakini Isaka alipewa vyote, zawadi pamoja na urithi, kwasababu yeye ndiye aliyekuwa mwana wa Ahadi kutoka kwa Mungu.
Mwanzo 25:5 “Ibrahimu akampa Isaka yote aliyokuwa nayo.
6 Lakini wana wa masuria aliokuwa nao Ibrahimu, Ibrahimu akawapa zawadi, naye akawaondoa katika mahali alipokaa Isaka mwanawe, wakati wa uhai wake, waende pande za mashariki, mpaka nchi ya Kedemu”.
Vivyo hivyo na sisi, tunaweza sote tukawa ni watu wa Mungu, tulioumbwa na Mungu, lakini si sote tukawa wana wa ahadi wa Mungu mfano wa Isaka. Wana wa ahadi ni wale waliozaliwa mara ya pili (yaani waliokoka). Na hao ndio Mungu kawaandalia vyote, thawabu pamoja na urithi wa ufalme wa mbinguni.
Ambapo Yesu alikwenda kuwaandalia waliompokea, Na siku atakaporudi, atawagawia urithi huo ambao alikuwa akiwaandalia kwa miaka 2000. Mambo ambayo jicho halijawahi kuoa wala sikio kusikia.
Swali la kujiuliza Ni je! na wewe ni mmojawapo wa wana wa Ahadi? Kama hujaokoka na kusimama, bado hujawa mwana wa ahadi, Lakini habari njema ni kuwa nafasi bado ipo lakini haitakuwepo siku zote ya wewe kufanyika hivyo.. Kama upo tayari leo hii kufanyika mtoto wa Mungu, na kuachana na dunia, na kutaka Yesu akuokoe, basi uaumuzi huo ni wa busara kwako, unachopaswa kufanya ni kufungua hapa ili upate maelekezo ya sala ya toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Tazama chini kwa masomo mengine ya rohoni.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp yako mara kwa mara tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
WATOTO WA YESE KATIKA BIBLIA.
Wafilisti ni watu gani.
Israeli ipo bara gani?
KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?
MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.
NENO NI LILE LILE, LAKINI UJUMBE NI TOFAUTI.
KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.
Watoto wa Yese katika biblia walikuwa ni wangapi?
Kitabu cha Samweli kinaonyesha Yese alikuwa na wana nane(8), Daudi akiwa ndio mwana wa mwisho kabisa, Lakini kitabu cha Mambo ya Nyakati wa kwanza kinaonyesha Yese alikuwa na Wana saba (7). Sasa swali linakuja Je! takwimu zipi ni sahihi? Je! biblia inajichanganya yenyewe?
Jibu ni hapana..
Tusome..
1Samweli 16:10 “Yese akawapitisha WANAWE SABA mbele ya Samweli. Samweli akamwambia Yese, Bwana hakuwachagua hawa.
11 Kisha Samweli akamwambia Yese, Watoto wako wote wapo hapa? Naye akasema, AMESALIA MDOGO WAO, na tazama, anawachunga kondoo. Basi Samweli akamwambia Yese, Tuma watu, wamlete; kwa sababu hatutaketi hata atakapokuja huku”.
Soma tena.
1Nyakati 2:13 “na Yese akamzaa Eliabu, mzaliwa wake wa kwanza, na wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama;
14 na wa nne Nethaneli, na wa tano Radai;
15 na wa sita Ozemu, na wa saba Daudi;
16 na maumbu yao ni Seruya, na Abigaili. Na wana wa Seruya walikuwa, Abishai, na Yoabu, na Asaheli; hao watatu.”
Sasa ukiangalia hapo utaota kitabu cha Mambo ya Nyakati hakijatoa idadi Fulani kwamba wana wa Yese kuwa walikuwa ni saba tu, hapana badala yake kimeorodhesha majina, Sasa kama wewe ni msomaji mzuri wa biblia utagundua kuwa kitabu cha mambo ya Nyakati kiliandikwa miaka ya mbeleni sana ukilinganisha na kitabu cha Samweli. Na kitabu hicho cha Mambo ya Nyakati wa kwanza kilikuwa kimejikita zaidi katika kuelezea uzao wa makabila ya Israeli(Vizazi vya wana wa Israeli).
Hivyo ilikuwa ni kawaida mtu asiyekuwa na uzao hakuweza kuorodheshwa katika orodha hiyo. Kwahiyo ni sahihi kusema Yese alikuwa na wana 9, lakini mmojawapo alifariki, pengine akiwa bado hajapata uzao, na hivyo mwandishi wa kitabu cha Mambo ya Nyakati akaona hakukuwa na haja ya kumworodhesha pale. Ni kama tu Samweli alivyoacha kuwaorodhesha dada zao wawili. Kama isingekuwa kitabu cha Mambo ya Nyakati kuwaorodhesha ni rahisi kudhani walizaliwa wana wa kiume tu kwao, lakini kulikuwa hakuna haja ya kuwaorodhesha pale, kutokana na muktadha ya maudhui ya pale, kwamba waliokuwa wanahitajika na wana wa kiume, tu.
Ndivyo ilivyokuwa hata kwa mwandishi wa kitabu cha Mambo ya Nyakati, walioorodheshwa na wale wenye uzao tu.
Kwahiyo kwa kuhitimisha ni kuwa Yese alizaa watoto nane (8) wakiume, na wawili (2) wa kike, Lakini mmoja baadaye alikuja kufa, wakabakia wana wa kiume 7 ndio wale walioorodheshwa katika 1Nyakati.
Shalom.
Tafadhali, angalia masomo mengine chini, ujifunze zaidi;
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo mballimbali kwa njia yaWhatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Adamu alikuwa na watoto wangapi?
Nuhu alikuwa na watoto wangapi?
JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 8 (Kitabu cha Ezekieli)
JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?
YAKINI NA BOAZI.
MANENO ALIYOWEZA KUTAMKA YESU TU PEKE YAKE.
NAMWANDAMA BWANA Lyrics~ Swahili?| Trust and Obey
Nyimbo hii iliandwa mwaka 1887, na Mchungaji mmoja aliyeitwa John H Sammis, (Mmarekani), ambaye alifanikiwa pia kuandika nyimbo nyingine Zaidi ya 100 zenye maudhi ya tenzi.
Historia ya wimbo huu ilianza siku moja, katika mkutano wa injili uliofanyika huko Massachusetts Marekani mwaka 1886, katika mkutano huo alisimama kijana mmoja ambaye alitoa ushuhuda wa wokovu wake, Kijana huyu alikuwa hajui mambo mengi kuhusu Mungu, ni mchanga katika wokovu, Lakini katika maneno yake machache alisema..
“Sina uhakika sana, lakini nitakwenda kuamini na kutii”
Maneno hayo yalimgusa sana mwendesha mziki aliyekuwa katika mkutano huo aliyeitwa Danieli Towner, mpaka akaamua kuyaandika maneno yale kwenye kikaratasi, na kisha baadaye akamtumia Rafiki yake ambaye alikuwa mchungaji aliyeitwa John H Sammis, huyo ndiye akauandika wimbo huo, “Namwandama Bwana”. Ambao ndani yake una vina vya maneno ya huyo kijana, nitaamini nitii.
Alipokuwa anauandika, alizingatia vipengele tofauti tofauti ya Maisha yetu tunayopaswa kutii.
NAMWANDAMA BWANA lyrics.
*****
Namwandama Bwana kwa alilonena, | ||||||||||||||||||||||||||||||||
Njia yangu huning’azia; | ||||||||||||||||||||||||||||||||
Nikimridhisha atanidumisha | ||||||||||||||||||||||||||||||||
Taamini nitii pia. | ||||||||||||||||||||||||||||||||
Amini utii, njia pweke ni hii | ||||||||||||||||||||||||||||||||
Ya furaha kwa Yesu: amini ukatii | ||||||||||||||||||||||||||||||||
Giza sina kwangu wala hata wingu, | ||||||||||||||||||||||||||||||||
Yeye mara huviondoa,
|
******
Ni nini tunaweza kujifunza katika historia ya wimbo huu Namwandama Bwana ?
Ushuhuda wako, hata kama utakuwa ni mdogo vipi, unaweza ukawa chanzo cha baraka cha watu wengine wengi duniani na kuwaokoa. Kama kijana huyu angeudharau ushuhuda wake, leo hii tusingekuwa na tenzi yenye faraja ya kipekee kama hii maishani mwetu.
Hivyo nawe pia usigope kushuhudia mambo makuu ya Mungu maishani mwako.
Shalom.
Mada Nyinginezo:
TENZI ZA ROHONI
USINIPITE MWOKOZI Lyrics
BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics
NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics
KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili.
UNYAKUO.
UFUNUO: Mlango wa 1
NI KITU GANI PETRO NA YOHANA WALIKIGUNDUA KABURINI?
Jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, Natumai u mzima, karibu tujifunze Maneno ya Uzima kama ilivyo wajibu wetu, maadamu siku ile inakaribia.
Leo tutatazama kwa ufupi juu ya aliyoyatenda mwanamke mmoja aliyeitwa Rispa, mwanamke huyu alikuwa ni suria wa mfalme Sauli. Sasa ilitokea siku moja Israeli ilipitia katika njaa ya mfulilizo wa miaka mitatu, hakuna mvua yoyote juu, mpaka wakajiuliza ni nini hiki? Maandishi ya zamani tofauti na biblia yanasema Daudi akajiuliza pengine kuna watu wanaabudu miungu kwa siri, wakaangalia wakaona mbona sio, wakaangalia kwa kila namna, na wakachunguza kila kitu lakini bado hakuna kilichowapa jibu,
Ndipo Daudi akaona aende moja kwa moja kumuuliza Mungu, pengine labda ni yeye kamkosea, Lakini Mungu akamjibu na kumwambia kuwa kosa lipo katika nyumba ya mfalme Sauli, kwa kuwa yeye alikwenda kuwaua watu ambao walishaingia nao maagano tangu zamani kwamba hawatawaua kwa kinywa cha akina Yoshua (Yoshua 9:15)
Lakini mfalme Sauli hilo hakulijali, akawaua hao watu (wagibeoni), ndipo Mungu akaliona hilo na kuifanya nchi ya Israeli ikae katika njaa kwa miaka mitatu mfufulizo..
Sasa Daudi alichokifanya ni kuwaendea wale wagibeoni, na kuwauliza wawafanyie nini, ili hiyo laana indoke juu yao, ndipo Wagibeoni hawakutaka kitu kingine chochote, bali walitaka tu kumlipizia kisasi Sauli kwa uzao wake, hivyo wakamwomba wapewe wazao wa Sauli waliobaki wawaue kwa kuwatundika kwenye miti milimani. Ndipo Daudi akawajalia haja yao, akawapa wana 7 wa Sauli.
Sasa wawili kati ya hao wana 7 walikuwa wa huyu suria mmoja wa Sauli aliyeitwa Rispa. Tusome.
2Samweli 21:9 “akawatia mikononi mwa Wagibeoni, nao wakawatundika mlimani mbele za Bwana, nao wakaangamia wote saba pamoja; wakauawa siku za mavuno, za kwanza, mwanzo wa mavuno ya shayiri.
10 Naye Rispa, binti Aya, akatwaa nguo ya magunia akajitandikia mwambani, tangu mwanzo wa mavuno hata waliponyeshewa mvua toka mbinguni; wala hakuacha ndege wa angani kukaa juu yao mchana, wala wanyama wa mwitu usiku”.
Unaweza kutengeneza picha mama anayeona watoto wake wakiuliwa kikatili mbele ya macho yake, kwa makosa ya watu wengine, halafu hawazikwi, wameachwa pale msalabani ni uchungu kiasi gani, anausikia..
Lakini kama tunavyosoma hapo huyu Rispa, hakuondoka pale mlimani, bali tangu siku hiyo watoto wake walipotundikwa, alikaa pale pale, kuhakikisha kuwa maiti za wanawe zinaheshimiwa, hakuruhusu ndege aje kula mizoga yao, wala usiku fisi waje kula mifupa.. Na zamani zile ilikuwa mizoga haiondolewi kwenye miti, mpaka hapo Mungu atakapojibu maombi, hivyo kama majibu yakija baada ya wiki moja, ndipo inashushwa pale mtini, yakija baada ya mwezi mmoja ndipo itakaposhushwa, vivyo hivyo hata yakija baada ya mwaka mzigo hiyo itaendelea kubakia pale mtini kwa mwaka mzima.
Na maandiko yanatuambia, mama yule hakuondoka pale mchana wala usiku tangu mwanzo wa mavuno ya shayiri mpaka mvua iliponyesha.. Mwanzo wa mavuno ya yashiri ni mwenzi wa 3-4, na mvua kunyesha ni mwezi 10..Hivyo mwanamke huyu alikaa pale mlimani kwa kipindi kisichopungua miezi 6..
Tengeneza picha, usiku na mchana, unafanya kazi ya kulinda, kuhakikisha maiti za wanao hazivunjiwi heshima kama mizoga ya wanyama, kwa kuliwa na ndege au fisi..alikaa pale mpaka ikawa ni mifupa tu imening’inia lakini hakuruhusu fisi achukue hata kidole cha wanawe.
Lakini tukirudi huku upande wa pili, Daudi akashangaa japokuwa tumewatimizia Wagibeoni haja zao, lakini mbona kama mvua inachelewa tena kwa miezi kadhaa?
Ndipo akasikia kuwa kumbe mama wa wale watoto wawili, tangu kipindi kile cha mauaji, hakuondoka pale mlimani akilinda maiti za wanawe.
Hilo likamfikirisha sana Daudi,, akawaza, kama mama huyu anazithamini maiti na mifupa ya wanawe waliotundikwa mitini na wao sio kitu kikubwa sana, Si zaidi mimi kuthamini mifupa ya Mfalme Sauli aliyeuliwa vivyo hivyo kama wao, (1Samweli 31:10-13) isitoshe ni mtiwa mafuta wa Mungu, mfalme wa Israeli na mimi sijui hata mifupa yake ilipo, Ndipo Daudi akatuma watu kwenda kuichukua mifupa ya Sauli iliyokuwa mbali sana, ng’ambo ya mto Yordani, akaileta Israeli, wakaifanyia maombolezo ya kitaifa, akaichanganya akaichukua ni mifupa ya wale watoto 7 waliouliwa, wakaenda kuzikiwa pamoja.
2Samweli 21:11 “Kisha akaambiwa Daudi hayo aliyoyafanya huyo Rispa binti Aya, suria wa Sauli.
12 Akaenda Daudi, akaitwaa mifupa ya Sauli na mifupa ya Yonathani mwanawe mikononi mwa watu wa Yabesh-gileadi; waliyoiiba katika njia ya Bethshani, hapo Wafilisti walipowatungika, katika siku hiyo waliyomwua Sauli huko Gilboa;
13 naye akaileta toka huko hiyo mifupa ya Sauli, na mifupa ya Yonathani mwanawe; nao wakaizoa mifupa yao waliotundikwa.
14 Kisha wakaizika mifupa ya Sauli na ya Yonathani mwanawe katika nchi ya Benyamini, huko Zela, kaburini mwa Kishi babaye; wakafanya yote aliyoyaamuru mfalme. Na baadaye Mungu aliiridhia hiyo nchi”
Na kwa tukio hilo likapelekea Mungu kuileta mvua juu ya nchi.
Ni nini tunajifunza?
Bidii ya mwingine, na kujali kwa mwingine, kunaweza kukawa sababu ya wewe Mungu kukuzuilia baraka zako. Unasema wewe ni mkristo, umeokoka, Lakini Mungu akimtazama mtu mwingine ambaye hamwabudu Mungu mkuu unayemwabudu wewe lakini ana bidii usiku na mchana ya kumtafuta mungu wake, ujue kuwa mbingu itazuliwa juu yako.. Haijilishi utasema umeokoka kiasi gani.
Ikiwa watu wa dini nyingine wanamfanyia mungu wao dua mara 5 mpaka 10 kwa siku, lakini wewe unaambiwa uombe lisaa limoja kwa siku, huwezi unategemea vipi mbingu isifungwe juu yako?, Hata kama utakuwa umetimiza vigezo vingine vyote, yule mwingine atabakia kuwa hukumu tu kwako.
Yatupasa tujirekebishe, ikiwa wao wanafunga siku 30 kila mwaka, sisi tunapaswa tuende zaidi ya hapo, lakini kama inapita mwaka mzima hujawahi kufunga hata wiki moja, mbingu zitafunga tu juu yako.
Ikiwa wanazingatia kushika aya za vitabu vyao vya dini kwa bidii, lakini wewe mkristo hujui hata biblia inavitabu vingapi, hujawahi hata kusoma kitabu kimoja cha biblia ukakimaliza chote, unasubiria tu kuhubiriwa, mbingu zitafungwa juu yako. Mpaka siku utakapojua tatizo ni nini.
Hivyo sote tujitathmini, Na Bwana atusaidie.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tuyatafakari maandiko pamoja.
Katika maisha, hakikisha unarekebisha vitu vinne. 1) Kazi unayoifanya 2) Kabila unalotoka 3) Nchi unayotoka 4) Mahali unapotoka.
Haya ni mambo makuu manne ambayo ni nguzo katika kuyajenga au kuyaharibu maisha. Na kimojawapo kisipokaa sawa mbele za Mungu, basi kitakuletea tufani kubwa katika maisha.
Hebu tuisome kidogo habari ifuatayo..
Yona 1:7 “Wakasemezana kila mtu na mwenzake, Haya, na mpige kura, mpate kujua mabaya haya yametupata kwa sababu ya nani. Basi wakapiga kura, nayo kura ikamwangukia Yona.
8 Ndipo wakamwambia, Tafadhali utuambie, wewe ambaye mabaya haya yametupata kwa sababu yako; kazi yako ni kazi gani? Nawe umetoka wapi? Nchi yako ni nchi ipi? Nawe u mtu wa kabila gani?
9 Akawaambia, Mimi ni Mwebrania; nami namcha Bwana, Mungu wa mbingu, aliyeziumba bahari na nchi kavu.
10 Ndipo watu wale wakaogopa mno, wakamwambia, Ni jambo gani hili ulilolitenda! Kwa maana watu wale walijua ya kuwa amekimbia, ajiepushe na uso wa Bwana, kwa sababu alikuwa amewajulisha.
11 Basi wakamwambia, Tukutende nini, ili bahari itulie? Kwa maana bahari ilikuwa inazidi kuchafuka“
Walipoanza kwenye nchi, aliwaambia yeye ni Mwebrania..hivyo wakajua moja kwa moja ni mtu wa Taifa la Israeli,ametokea katika mojawapo ya miji ya kule, alipoendelea mbele kidogo, kwenye shughuli anayoifanya akasema yeye anamcha Mungu (yaani maana yake ni mtumishi wa Mungu), anayehudumu katika shamba la Mungu, na kwamba ameikimbia kazi ya Mungu, ndipo walipoelewa tatizo lipo hapo, wakaogopa na kutafuta suluhisho kabla mambo hayajazidi kuharibika.
Sasa endapo Yona ingekuwa hajaikimbia kazi ya Mungu na baharini imewachafukia vile, basi tatizo ni lazima lingekuwa aidha kwenye kabila analotokea, na kama sio kwenye kabila basi kungekuwa na tatizo kwenye nchi anayotokea..au mahali anapotokea.
Hivyo Nataka uone leo kwamba kazi yako unayoifanya inaweza kuwa chanzo cha Tufani na misukosuko, hakikisha kazi unayoifanya yoyote ile aidha ya mikono, iwe inampendeza Mungu kwa viwango vyote, uwe mwaminifu katika kazi yako na pia jiepushe na hila na wizi. Vilevile kama unafanya kazi ya Mungu hakikisha hukwepi majukumu yako kama mtumishi, wala huifanyi kwa ulegevu vinginevyo utakumbana na tufani kama iliyokuta Yona.. Na mkristo yoyote ni lazima awe na jukumu katika kazi ya Mungu. Hivyo jihakiki sana.
Yeremia 48:10 “Na alaaniwe mtu afanyaye kazi ya Bwana kwa ulegevu”
Vile vile kabila unalotoka linaweza kuwa chanzo cha matatizo. Makabila mengi yana mila na desturi zilizo kinyume na Neno la Mungu, makabila mengi yana matambiko na ushirikina, jiepushe na hayo yote baada ya kuokoka. Zipo mila nyingine ambazo ni aibu hata kuzisema hapa..Hizo zote ni rahisi kukusababisha tufani katika maisha yako, na hasira ya Mungu kuwaka juu yako. Jiepushe na hizo mila…Sisemi kwamba ujiepushe na ndugu zako au wazazi wako wanaofanya hizo mila!, na uwachukie na kuwasema Hapana!..endelea kubaki na ndugu zako, waheshimu,wapende, watunze, waombee, na ishi nao kwa furaha zote na kushirikiana nao kwa mambo mengine yote mazuri wanayoyafanya lakini usishiriki mila hizo zilizo kinyume na neno la Mungu.
Pia nchi unayotokea au mahali ulipo panaweza kuwa chanzo cha tufani katika maisha yako..Hivyo ni wajibu wa kushiriki mambo mazuri yanayoendelea katika nchi yako, na kuyakataa yale mabaya yote, Nchi inaweza kuhalalisha ndoa za jinsia moja kisheria kabisa!, nchi inaweza kuhalalisha uvutaji wa bangi, nchi inaweza kuhalalisha utoaji mimba, nchi inaweza kuhalalisha ndoa za wanadamu na wanyama n.k.
Nchi ya namna hiyo tayari ipo chini ya laana na hasira ya Mungu na watu wake ni hivyo hivyo..Hivyo ni wajibu wa wewe uliyeokoka unayeishi ndani ya nchi kama hiyo, kujitenga kwa kutofanya hayo mambo au kukubaliana nayo, ili usiwe miongoni mwa wanaomwudhi Bwana Mungu. Na kujitenga sio kutoongea nao, au kutofanya nao kazi kwenye kampuni moja!..hapana..bali kujiepusha na njia zao, mfano wa Danieli, Meshaki, Shedraka na Abednego jinsi walivyoishi katikati ya taifa la Babeli lakini hawakushiriki matendo ya watu wa Babeli, na walifanikiwa sana katikati ya Taifa lile ovu.
Bwana atusaidie na Bwana atubariki
Na mwisho kabisa kama umejaliwa kupata watoto, au unampango wa kuwa na watoto..kumbuka kuwalea katika njia inayowapasa, angali wakiwa wadogo, kwasababu wakiwa wakubwa hawataiacha biblia inasema hivyo, Na pia wewe mwenyewe kama hujaokoka!. Mlango wa Neema upo wazi, usiidharau injili hata kidogo inayohubiriwa kwako bure! Bila kutozwa chochote… Hata vitu vingi vinavyoishiaga kutolewa bure mara nyingi huwa ni vya gharama sana na vya muhimu sana, kwasababu kama vingeuzwa basi hakuna mtu angeweza kununua..
Hata madawa yanayotolewa bure! Mengi ni ya gharama ya juu sana, yananunuliwa ghali sana aidha na serikali au mashirika binafsi lakini yanakuja kutolewa bure tu kwa watu ili kuokoa maisha!. Na wokovu ni wa gharama sana na wa muhimu kwa kila mtu, ndio maana tunapewa bure!, hivyo usiudharau, Laiti tungetozwa fedha ili kuupata, basi hakuna ambaye angeweza kuununua, hata dunia nzima tungekusanya nguvu zetu zote, tusingeweza kununua wokovu wa mtu mmoja tu! Licha ya watu wa dunia nzima. Mpokee Yesu leo kama hujampokea, na ukabatizwe na kupokea Roho Mtakatifu. Kwa usalama wa maisha yako.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
YONA: Mlango 1
YONA: Mlango wa 2
JINA LA MUNGU NI LIPI?
USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.
KUMCHA MUNGU NI NINI? NA MTU ANAMCHAJE MUNGU?
JE NI LAZIMA MKRISTO AOE/AOLEWE?
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..
KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU NA ZA LUTU.