Kasirani ni nini? (Kutoka 23:21)

Kasirani ni nini? (Kutoka 23:21)

Swali: kumtia mtu au malaika kasirani ndio kufanya nini? (Kutoka 23:21).

Jibu: Turejee..

Kutoka 23:20 “Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea.

21 Jitunzeni mbele yake, mwisikize sauti yake; WALA MSIMTIE KASIRANI; maana, hatawasamehe makosa yenu; kwa kuwa jina langu limo ndani yake.

22 Lakini ukiisikiza sauti yake kweli, na kuyatenda yote ninenayo mimi; ndipo mimi nitakuwa ni adui wa adui zako, na mtesi wa hao wakutesao”.

Kumtia mtu “Kasirani” ni kumfanya mtu “Akasirike”. Hivyo hapo biblia iliposema msitie Kasirani yule malaika maana yake “wasimkasirishe” kwasababu hatawasamehe.

Na ni vitu gani ambavyo vingemtia yule malaika kasirani?.. si vingine Zaidi ya “kumwacha Mungu na kuabudu miungu mingine, pamoja na kutolishika Neno lake”.. Utaona wana wa Israeli mara kadhaa walimtia kasirani yule malaika walipokuwa jangwani na hata walipoingia ile nchi ya ahadi.

Tukio moja la wazi lililoonesha dhahiri, malaika wa Bwana kutiwa kasirani na wana wa Israeli ni kipindi ambacho walikawia kuyaondoa yale mataifa waliyoyakuta katika nchi ya ahadi na walipoingia agano na miungu yao.. jambo ambalo lilikuwa ni chukizo kubwa mbele za  Mungu na kwa malaika wake ambaye aliyempeleka awaingize katika ile nchi ya ahadi.

Waamuzi 2:1 “KISHA MALAIKA WA BWANA ALIKWEA JUU KUTOKA GILGALI KWENDA BOKIMU. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi;

2 nanyi msifanye agano lo lote na hawa wenyeji wa nchi hii; zipomosheni nchi madhabahu zao; lakini hamkuisikia sauti yangu; je! Mmefanya haya kwa sababu gani?

3 Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu.

4 Ikawa, hapo huyo malaika wa Bwana alipoyanena maneno haya, kuwaambia wana wa Israeli wote, ndipo hao watu wakainua sauti zao na kulia

5 Nao wakaliita jina la mahali pale Bokimu; nao wakamchinjia Bwana sadaka huko”.

Hata leo watu wanawatia kasirani Malaika wa Mungu.. Kwani maandiko yanasema kila mtu aliyeokoka anaye malaika wake asimamaye mbele za Mungu kupeleka habari zake njema na kumhudumia mtu huyo soma (Mathayo 18:10 na Waebrania 1:13-14).

Hivyo inapotokea mtu anafanya mambo yaliyo kinyume na Neno la Mungu, basi Malaika asimamaye naye anachukizwa na kuhuzunishwa pia.

Lakini pia si Malaika tu wanatiwa kasirani, bali pia hata Mungu wetu tunamtia Kasirani kwa maovu yetu.. Wana wa Israeli walimtia BWANA MUNGU kasirani walipokuwa jangwani na hata sasa sisi wa wakati huu tunamtia KASIRANI kwa maovu yetu.

Kumbukumbu 9:7 “Kumbuka, usisahau ulivyomtia Bwana, Mungu wako, KASIRANI JANGWANI; tangu siku uliyotoka nchi ya Misri hata mlipofika mahali hapa, mmekuwa na uasi juu ya Bwana

8 Tena mlimkasirisha Bwana katika Horebu, Bwana akakasirika nanyi hata akataka kuwaangamiza.

9 Na hapo nilipokwea mlimani kwenda kuzipokea mbao za mawe, nazo ni mbao za agano Bwana alilofanya nanyi, ndipo nikakaa mle mlimani siku arobaini usiku na mchana; sikula chakula wala kunywa maji”.

Soma pia Kumbukumbu 31:29.

Bwana atusaidie tusivuke mpaka wa Neno lake na kumkasirisha.

Amen.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! MUNGU NI NANI?

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

MUNGU MWENYE HAKI.

Malaika wa maji ni yupi na Je kuna aina ngapi za malaika?

KAA MAJANGWANI.

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments