Karibu tujikumbushe mambo machache, ambayo yanaonekana ni madogo lakini ni ya umuhimu sana, katika mapambano ya Imani.
Kuna tofauti ya sadaka na msaada. Unapomsaidia maskini huo ni msaada, na una thawabu zake mbele za Mungu..lakini sadaka ina matokeo makubwa zaidi kuliko msaada.
Sadaka ni nini?
Sadaka ni matoleo yoyote yanayohusisha madhababu!.. Katika agano la kale, sadaka iliyokuwa inakubalika kwa Mungu ni ile iliyokuwa inapelekwa mbele ya madhabahu ya Mungu katika nyumba ya Mungu…iwe ni kafara ya kondoo, au sadaka ya mazao au chochote kile. Vigezo ni lazima ipelekwe katika hema ya kukutania au katika nyumba ya Mungu.
Usipeleke sadaka yako kwa maskini, ukifanya hivyo utakuwa hujatoa sadaka bali umetoa msaada, utabarikiwa kwa ulichotoa lakini si kama ungeitoa kama sadaka. Sadaka ni lazima ihusishe madhabahu ya ki-Mungu.
Hata watu wanaokwenda kwa waganga huwa wanapewa masharti ya kupeleka sadaka..Na ile sadaka wanapewa maagizo ya kuiacha pale kwenye madhabahu zao, ili ilete matokeo wanayoyataka, kama ni kuku ataambiwa ampeleke hapo wamchinjia hapo hapo na kumwacha pale pale…Huwezi kusikia wanapewa maagizo na waganga na kuambiwa wakachinje jogoo mweusi nyumbani halafu wakawape maskini, au wakaipeleke kwa mganga mwingine,! Huwezi kusikia hicho kitu!.watakuambia leta hapa (kwenye hii madhabahu) hiki au kile kama sadaka yako, kwasababu ili kitu kiwe sadaka ni lazima kihusishwe na madhabahu.
Kwahiyo hakuna sadaka pasipo madhabahu.
Bwana Yesu alisema maneno haya katika
Mathayo 23:18 “Tena, Mtu atakayeapa kwa madhabahu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa sadaka iliyo juu yake, amejifunga”.
Maneno hayo yanaelezea uhusiano uliopo kati ya sadaka na madhababu.
Kwahiyo kama wewe ni mkristo, sadaka yako peleka kanisani na mahali unapokuzwa kiroho (kwamfano kwenye mikutano ya injili, semina n.k), ndipo utakapobarikiwa Zaidi… Bila kusahau kusaidia maskini na wenye uhitaji ambako pia kuna thawabu kubwa kutoka kwa Mungu. Lakini sadaka ina nguvu mara nyingi Zaidi ya hiyo, endapo utaelewa ufunuo wake!.. Ongeza bidii sana katika kutoa sadaka kuliko kupeleka michango yako sehemu nyingine.
Kuna fikra mbaya sana ambayo shetani kaisambaza kwenye akili za watu wengi, ambayo imewasababishia watu wengi kukosa baraka zao. Na hicho ni saikolojia ya kwamba ukiipeleka sadaka kanisani basi ni kuwatajirisha wale wachungaji na watumishi!, na hivyo ni afadhali kuipeleka kwa maskini, Hiyo ni saikolojia ya Adui, usikubali ikutawale.
Bwana Yesu alisema pia maneno haya..
Mathayo 5:23 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako”.
Mathayo 5:23 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,
24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako”.
Mambo haya yanaonekana ni madogo machoni pa wengi, lakini yana umuhimu mkubwa sana. Hivyo ni muhimu sana kuyafahamu na kuyazingatia. Zaka yako ipeleke nyumbani kwa Bwana, Sadaka zako za shukrani vilevile ipeleke nyumbani kwa Bwana.
Mungu akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 693036618/ 0789001312
Mada Nyinginezo:
TUMTOLEE MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Ubatizo wa moto ni upi?
MASOMO MBALIMBALI YA NENO LA MUNGU.
UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.
JE KUVAA PETE NI DHAMBI?
JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?
Rudi Nyumbani:
Print this post
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima, Nakukaribisha tena tuyatafakari maneno ya uzima.
Leo tutatazama kwa ufupi Habari ya watu wawili. Wakwanza ni mtu mmoja anayeitwa Yairo mkuu wa sinagogi, na wa pili ni mwanamke mmoja aliyekuwa anatokwa na damu kwa muda mrefu lakini baadaye alikuja kuponywa na Bwana Yesu kwa kulishika tu pindo la vazi lake.
Sasa lipo jambo moja la kusisimua nataka ulione kwa hawa watu wawili ambalo kila mmoja lilikuwa kichwani mwake. Embu tusome kidogo;
Luka 8:40 “Basi Yesu aliporudi mkutano ulimkaribisha kwa furaha, maana walikuwa wakimngojea wote. 41 Na tazama, mtu mmoja akaja, jina lake Yairo, naye ni mtu mkuu wa sinagogi, akaanguka miguuni pa Yesu, akamsihi aingie nyumbani kwake; 42 kwa kuwa binti yake yu katika kufa, ambaye ni mwana pekee, umri wake amepata miaka kumi na miwili. Na alipokuwa akienda makutano walimsonga. 43 Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu ye yote, 44 alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi lake; na mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma”.
Luka 8:40 “Basi Yesu aliporudi mkutano ulimkaribisha kwa furaha, maana walikuwa wakimngojea wote.
41 Na tazama, mtu mmoja akaja, jina lake Yairo, naye ni mtu mkuu wa sinagogi, akaanguka miguuni pa Yesu, akamsihi aingie nyumbani kwake;
42 kwa kuwa binti yake yu katika kufa, ambaye ni mwana pekee, umri wake amepata miaka kumi na miwili. Na alipokuwa akienda makutano walimsonga.
43 Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu ye yote,
44 alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi lake; na mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma”.
Sasa ukiangalia hapo, utaona huyu Yairo, alikuwa na binti yake aliyepatwa na matatizo katika umri wake wa miaka kumi na miwili (12), Na wakati huo huo alikuwepo yule mwanamke alitokwa na damu kwa muda wa miaka kumi na miwili (12). Ipo sababu kwanini biblia imeutaja umri wa mtoto na muda wa mwanamke kutokwa damu.
Kwamfano biblia inatuambia huyu Yairo hakuwa na mwana mwingine isipokuwa yule binti tu, pengine alimlea kwa taabu na shida, akiwa na matumaini kuwa huyu ndiye atakayekuja kuwa heshima yake ukubwani, pengine aliona mwelekeo mzuri wa binti yake, kama vile Yokebedi(mama yake Musa) alivyoona uzuri wa Musa tangu akiwa mdogo, akaamua kumficha ambapo kweli baadaye tunaona akaja kuwa nyota ya Israeli mwokozi wa Israeli,
Vivyo hivyo pengine huyu Yairo naye alimwona binti yake kuwa ni mzuri atakuja kuwa mcha Mungu kama Hana, au Sara, na kumletea fahari kwake, hivyo pengine akajitahidi kumlea katika maadili tangu anapozaliwa, mpaka anafikisha umri wa miaka 11, lakini alipofikisha umri wa miaka 12, ghafla akaanza kuona mabadiliko katika afya ya mtoto wake, miezi ya kwanza kwanza, hali inaanza kuwa mbaya mpaka inakaribia miezi ya katikati mtoto ndio yupo mauti uti kabisa,..katika hali kama hiyo anawaza afanyaje mtoto wake anakwenda kufa?
Je! Aruhusu maono yake yafe katika umri wa miaka 12,akizingatia kuwa ndio mwana pekee aliye naye? au afanye nini?. Lakini kama tunavyosoma habari, hakuruhusu jambo hilo litokee, hakuruhusu ndoto zake alizozihangaikia tangu zamani zizimwe na shetani katika mwaka wake wa 12 wa Maisha ya mwanawe, hapo ndipo akaanza safari ya kumtafuta Yesu.
Lakini huku nako upande wa pili, kulikuwa na mwanamke aliyetokwa na damu naye kwa muda mrefu, ambaye pia harakati zake za kutafuta uponyaji, zilianza tangu kipindi yule binti anazaliwa, tangu mwaka wa kwanza, akaendelea hivyo hivyo mpaka mwaka wa 2,..3…4, bila mafanikio mpaka mwaka wa 11, (Biblia inasema alikuwa ameshapoteza pesa zake nyingi kwa madaktari bila mafanikio) na ulipofika mwaka wa 12 bado hajapata alichokuwa anakitafuta, lakini naye siku moja akasikia Yesu yupo mjini..akasema sitakubali uponyaji wangu niliokuwa ninautafuta kwa miaka yote hii 12, leo hii ukatishwe na kukata tamaa, nitakwenda kukutana na Yesu.
Hivyo wote hawa wawili kila mmoja akaanza safari yake kivyake, na kama tunavyoisoma Habari Kristo aliwaponya wote, na wakapata walichokuwa wanakihangaikia, na kukiongojea.
Hata leo, tunapaswa tujifunze kuwa upo wakati wa kuyashindania yale maono ya kumtumikia Mungu ambayo tulikuwa tumeshaanza kuyafanya tangu zamani,haijalishi leo hii ni kipingamizi kikubwa kiasi gani kimesimama mbele yako, tunapaswa tuyashindanie…
Kwa kumkabidhisha Yesu hayo matatizo bila kuruhusu yaangamie kabisa..
Wapo watumishi ambao walishaanza kumtumikia Mungu,na walishapiga hatua fulani lakini pengine wakapitia vitisho Fulani vya ibilisi wakaacha kuhubiri, au kutumika. Ndugu usiruhusu taabu yako uliyoisumbukia iwe bure.
Kumbuka wapo wengine wamekuwa wakimwomba Mungu wapate kama tu hicho ulichonacho kwa muda mrefu, pengine tangu ulipoanza wewe kutumika, lakini bado hawajakipata, na hawakati tamaa kumwomba Yesu, na atawapa, kwanini wewe uruhusu kukata tamaa?
Mwaka wa 12 wa mtoto ya Yairo, Sio sawa na miaka 12 yule mwanamke aliyokuwa anangojea uponyaji wake..Hivyo na wewe, tatizo lako mpito lisikwamishe katika kazi yako ya utumishi Mungu aliyoiweka ndani yako.
Ili tushinde, ni lazima tushindane, Hivyo songa mbele.
Na sio tu kwenye kuifanya kazi ya Mungu, bali pia katika vitu vingine vyote unavyovitafuta vilivyo mapenzi ya Mungu, hupaswi kukata tamaa kabisa.
Bwana akubariki sana.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.
NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE
KUOTA UMEFUNGA NDOA.
NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.
FUKUZA TAI WOTE JUU YA SADAKA YAKO.
WhatsApp
Kuota upo gerezani kunamaanisha nini?
Ndoto ya namna hii inaanguka katika makundi makuu matatu (3) ya watu.
Sasa ni vizuri ukajitathmini kwanza wewe mwenyewe na ukajijua upo katika kundi lipi kati ya hayo, ili upate tafsiri sahihi ya ndoto yako. Sasa tukianzana na kundi la kwanza.
Ikiwa wewe unajijua kabisa umeokoka, na umesimama katika Imani na hakuna chochote kinachokuyumbisha, Lakini cha kushangaza umejikuta katika ndoto upo gerezani, au kifungoni na hujui utatokaje. Nataka nikumbie hupaswi kuwa na hofu,.Shetani anaona Imani yako, na bidii yako kwa Mungu, na hivyo atafanya kila njia kukuzuia, au pengine ameshaanza kufanya hivyo katika Imani yako, wewe kusonga mbele, atajaribu kukusonga usifike mahali Fulani, lakini hawezi kufanikiwa.
Ipo mifano kadha wa kadha katika biblia, utaona magwiji wote wa Imani walipokuwa wanafanikiwa katika kumcha Mungu shetani hakutulia tu hivi hivi, badala yake alinyanyua vikwazo vya vifungo. Kwamfano utamwona Yusufu, wakati alipokataa kulala na mke wa Boss wake (Potifa), alisingiziwa na kutupwa gerezani na akakaa kule kwa muda wa karibu miaka 2..Lakini Yusufu hakuacha kumcha Mungu, kwasasababu, vifungo haviwezi kumshika mteule wa Mungu daima, Na sote tunajua ni nini kilikuja kumpata Yusufu baada ya lile jaribu, ilikuwa ni kufanyika kuwa waziri mkuu wa Misri,
Vilevile utamwona Yeremia naye, alifungwa gerezani kwasababu alikuwa anawatabiria Israeli Habari za kweli za Mungu,(Soma vitabu vya Wafalme na Yeremia chote)
Utamwona tena Yohana Mbatizaji, yeye naye walimshika na kumtupa gerezani kisa tu, alimweleza mfalme Herode kosa lake la kuzini na mke wa ndugu yake, (Marko 6:17)
Halikadhalika utawaona mitume wa Kristo, akina Petro na Yohana vifungo viliwakuta, Paulo alipokuwa kuwa anasafiri katika ziara zake za kuhubiri injili Roho Mtakatifu alimshuhudia kabisa na kumwambia;
Matendo 20:23 “ isipokuwa Roho Mtakatifu mji kwa mji hunishuhudia akisema, ya kwamba vifungo na dhiki vyaningoja.24 Lakini siyahesabu maisha yangu kuwa kitu cha thamani kwangu kama kuumaliza mwendo”.
Wakati mwingine alipokuwa na Sila, walimkamata na kumtupa gerezani, lakini wakiwa kule gerezani, hawakufadhaika, bali walimwimbia Mungu na kumsifu,
Matendo 16:25 “Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza”.
Vivyo hivyo na wewe, ikiwa ni mkristo ambaye unajijua umesimama kikamilifu katika Imani, unaweza ukawa unapitia sasahivi vipingamizi vya kiimani, au vitakuja mbele yako kipindi sio kirefu, utakutana na shetani kutaka kukuzuia usisonge mbele na hicho unachomfanyia Mungu, basi usiogope, wewe fanya kama Paulo na Sila, zidi kumwimbia Mungu na kumsifu, na kuomba kwa bidii, kwasababu ipo hatua nzuri Zaidi Mungu anataka kukuvukisha.
Na ndio maana umeoteshwa ndoto kama hiyo upo gerezani, kifungoni. Usiogope, zidisha matendo yako kwa Mungu, wewe ni shujaa..
Lakini kama wewe ni mkristo ambaye ni vuguvugu au ulishaanza kupoa, hapo mwanzo ulikuwa umesimama lakini sasahivi ni kama vile umerudi nyuma, na umeota ndoto kama hii upo gerezani, Hiyo ni tahadhari kubwa sana kwako.
Kumbuka shetani anakuwinda usiku na mchana,..Kwenye biblia alikuwepo mtu mmoja aliyeitwa Samsoni, yeye ni mfano wa wakristo vuguvugu wa leo, alilaghaiwa na uongo wa shetani mpaka akatoa siri ya nguvu zake. Na wote tunajua kilichomkuta baada ya pale ni nini?.
Alitobolewa macho, akatupwa gerezani na kufanyishwa kazi hata Zaidi ya punda..
Waamuzi 16:21 “Wafilisti wakamkamata, wakamng’oa macho; wakatelemka naye mpaka Gaza, wakamfunga kwa vifungo vya shaba; naye alikuwa akisaga ngano katika gereza”
Ndivyo ilivyo hata na wewe, Mungu amekuotesha upo gerezani, ni kwamba upo karibuni kutekwa na ibilisi au pengine tayari ameshakuteka kabisa..Biblia inasema kurudi kwake nyuma mpumbavu kutamwangamiza.
Hivyo unachopaswa kufanya ni kutubu na kumgeukia Mungu haraka sana, kama unafanya mambo ambayo hayampendezi heri uache mara moja, Kwasababu Mungu hataki uangamie. Na ndio maana kakupa tahadhari hiyo.
Lakini sasa kama wewe, upo dhambini tangu zamani, hujawahi kuwa na Habari na Mungu, kisha umeota upo gerezani,..Ni Mungu anazungumza na wewe, na kukuonyesha hali yako ilivyo rohoni. Kwamba upo vifungoni, shetani amekunasa, shetani anaitesa roho yako.
Lakini habari njema ni kuwa lengo kuu mojawapo la Yesu kutumwa duniani ilikuwa ni kuwafungua na kuwaacha huru waliofungwa na ibilisi..
Hivyo ikiwa wewe ni mkristo jina tu, au mwislamu, au muhindu, au mpagani,.. Sikiliza unabii Mungu aliompa Yesu zamani..alisema.
Isaya 42:6 “Mimi, Bwana, nimekuita katika haki, nami nitakushika mkono, na kukulinda, na kukutoa uwe agano la watu, na nuru ya mataifa; 7 kuyafunua macho ya vipofu, KUWATOA GEREZANI WALIOFUNGWA, kuwatoa wale walioketi gizani katika nyumba ya kufungwa. 8 Mimi ni Bwana; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu”
Isaya 42:6 “Mimi, Bwana, nimekuita katika haki, nami nitakushika mkono, na kukulinda, na kukutoa uwe agano la watu, na nuru ya mataifa;
7 kuyafunua macho ya vipofu, KUWATOA GEREZANI WALIOFUNGWA, kuwatoa wale walioketi gizani katika nyumba ya kufungwa.
8 Mimi ni Bwana; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu”
Na ndio maana Yesu alisema..
Zaburi 61:1 “Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, KUWATANGAZIA MATEKA UHURU WAO, NA HAO WALIOFUNGWA HABARI ZA KUFUNGULIWA KWAO”.
Hivyo leo umejiona upo vifungoni, pengine unateseka kutafuta njia ya kutoka huwezi, Yesu anakuita leo akuokoe,.
Zaburi 69:33 “Kwa kuwa Bwana huwasikia wahitaji, Wala hawadharau wafungwa wake”.
Ukimpokea Yesu, atafanya mabadiliko makubwa katika Maisha yako, atakufungua katika laana nyingi ambazo hata wewe mwenyewe hukuwahi kuzijua, laana za ukoo, na laana za mapepo na majini, ikiwa utakuwa tu tayari leo kusema Bwana Yesu njoo niokoe yote hayo yatafanyika kwako.
Kwahiyo Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Na ukimaliza kufanya hivyo basi Kristo anaanza sasa kuyafanya mabadiliko hayo moyoni mwako, na utaona jinsi anavyokufungua kifungo kimoja mpaka kingine. Kama alitufanyia sisi hivyo, atakufanyia na wewe, Hivyo amini tu na fungua moyo wako!
Bwana akubariki.
Pia tazama mafundisho mengine chini tayakusaidia kiroho sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au kwa namba hii +255 789001312
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
RABI, UNAKAA WAPI?
TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!
TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.
MTETEZI WAKO NI NANI?
KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?
KIAMA KINATISHA.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Jina la Bwana libarikiwe.
Kuna kitu kimoja cha kipekee ambacho Mungu katuumbia sisi wanadamu “nacho ni uponyaji wa asili”
Huu uponyaji wa asili upo katika miili yetu na vile vile upo katika roho zetu. Na huo Uponyaji tumepewa bure wanadamu wote kama zawadi na Mungu wetu, na huo hauhitaji uwe mkristo au utumie jina la Yesu kuupata. Upo tu Mungu kauweka ndani ya kila mtu.
Kwamfano unapojikata na kisu mkononi kwa bahati mbaya, inaweza kukuchukua wiki kadhaa tu kupona na nyama yako ikarudi vile vile, au unapoanguka na kuchubuka sehemu ya mwili wako, baada ya wiki kadhaa au mwezi Ngozi yako itakuwa imesharudia katika hali yake kama ilivyokuwa mwanzo, litabaki kovu tu lakini si jeraha!..
Kwahiyo ni kitendo cha muda tu..lakini mwisho wa siku utapona majeraha yako yote. Vinginevyo Mungu wetu asingeuweka huo uponyaji wa asili basi dunia ingekuwa ni jehanamu..pangekuwa si mahali pa kuishi.
Na katika roho ni hivyo hivyo, yapo majeraha ya rohoni ambayo mtu unaweza kuumizwa au kujiumiza mwenyewe. Majeraha hayo yanaweza kutokana na mambo Fulani Fulani ya kimaisha, na hayo pia Mungu kayawekea uponyaji wake wa asili…
Ndio maana unaweza ukakasirika sana sasahivi, ukapita muda kadhaa ile hasira inaanza kutulia na mwishowe inaisha kabisa… hapo ni uponyaji unafanya kazi yake.
Hivyo kama vile tunavyotumia njia za kuponya majeraha ya nje tutumie njia hiyo hiyo kuyatibu yale ya ndani.
Tukiumia kwa majeraha ya nje kama vidonda, huwa tunavisafisha vizuri, tunavipaka dawa na kisha tunavifunga..na kikubwa Zaidi tunahakikisha hatuvitoneshi, baada ya siku moja au mbili tunarudia tena hilo zoezi, mpaka mwishoni tunapona kabisa. Sasa zoezi hilo la kukisafisha na kukifunga na kuzuia kukitonesha ndilo litasaidia kidonda kile kipone haraka, lakini kisipofanyiwa matunzo hayo..basi hakitapona haraka, na matokeo yake kinaweza kuzidi kuwa kikubwa Zaidi na kutengeneza tatizo lingine likubwa zaidi.
Na majeraha ya ndani tunayaponya kwa njia hiyo hiyo. Pale tunapoumizwa na watu au mazingira Fulani kama wakristo, njia ni hiyo hiyo;
Yohana 8:32 “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.
Fanya hivyo siku ya kwanza, rudia tena siku zinazofuata, kila siku soma maandiko, funga, omba na usijikumbushe kumbushe…Kwa kufanya hivyo nakuambia ukweli..Haitapita kipindi kirefu utaona mabadiliko makubwa sana. Utapona majeraha yako ya muda mfupi sana. Kwasababu umeiwekea mazingira yanayofaa, ile nguvu ya uponyaji wa asili kufanya kazi ndani yako.
Lakini usipofanya hivyo..Utakuwa na majeraha ambayo hayaponyeki kila kukicha…Utaishi Maisha ya kuumia kila siku, na ya chuki, na ya vinyongo. Kila mtu utamwona ni adui yako, na kila Neno litakuwa linakuumiza. Utakuwa na majeraha ya miaka 20 iliyopita ambayo hayajapona bado! Utakuwa mtu wa kutokusamehe…Nakuambia ukweli sio mpango wa Mungu kuwa na majeraha ya rohoni kwa miaka 10..Ukiona una kinyongo, au bado unaumia kwa jambo lililotokea miaka 10 au 20 iliyopita..jaribu kutafuta suluhisho mapema..kwasababu kuna uwezekano nguvu ya msamaha haipo ndani yako, na jeraha unapozidi kuliacha huwa ndio linazidi kuwa kubwa kila siku na kuweza kuzaa tatizo kubwa Zaidi ya hilo.
Zaburi 38:5 “Jeraha zangu zinanuka, zimeoza, Kwa sababu ya upumbavu wangu”
Na sababu ya kutopona majeraha ndio hizo hapo juu kutofunga jeraha na kutoweka dawa!.. Unaweza kuwa unatatizo la kutopata mtoto, na ukasikia watu wanakusema vibaya..na hilo likawa ni jeraha kwako!..lakini kama Neno la Mungu halipo ndani yako; kama hujui Habari za akina Sara na wengineo ambao Mungu aliwafungua matumbo katika uzee wao, kama hujui Habari za Hana na Raheli ambao walisemwa kupita maelezo, basi hutaweza kupona haraka jeraha ulilonalo. Kwahiyo Neno la Mungu ndio dawa, inayoharakisha uponyaji wa ki-Mungu.
Zaburi 147:3 “Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuziganga jeraha zao”
Ndicho kinachowakuta watu wasiolijua Neno la Mungu (watu wa kidunia), wanahangaika na majeraha ya muda mrefu yasiyopona kwasababu hawana dawa, wala hawaijui dawa..Hivyo jeraha lolote lililo ndani yako, lisiwe kikwazo cha wewe kuikosa mbingu anza sasa kuusafisha moyo wako.
Mwisho kama hujaokoka, wakati umeenda sana, wakati wowote Kristo anarudi, biblia inasema..itatufaidia nini tuupate ulimwengu mzima halafu tupate hasara za nafsi zetu?. Mambo ya ulimwengu yanapita lakini Neno la Mungu lipo pale pale. Mgueukie leo Kristo, utubu dhambi zako, uoshwe kwa damu yake, ukabatizwe na kisha upokee Roho Mtakatifu, ambaye atakuongoza katika kuijua kweli yote ya maandiko.
Maran atha
SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.
ALIJARIBIWA SAWASAWA NA SISI KATIKA MAMBO YOTE.
MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.
NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;
UTASIMAMA PEKE YAKO SIKU ILE.
JIRANI YANGU NI NANI?
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.
Shalom, karibu tena tujifunze maneno ya uzima ya Mungu wetu YEHOVA.
Kuna wakati Mungu anaweza kukaa kimya na kuruhusu mambo Fulani yatokee, ili aone watu wake watamzungumziaje kuhusu jambo hilo, Na hapo ndipo tunapopaswa tuwe makini, kwasababu mtu akikosa kujua makusudi ya Mungu ni nini, halafu akamzungumzia tu kutokana na mawazo yake au uonavyo yeye, anaweza kujisababishia hasira yake iwake juu yako.
Kuna jambo moja la namna hiyo ambalo lipo hasaa kwetu sisi watu wa kanisa la Laodikia, ambalo tunamzunguzia Mungu isivyopasa. Kosa hilo lilifanywa na watu wa kale na sisi bado tunataka kulirudia Na leo hii tutaliona katika biblia.
Kosa lenyewe lilifanywa na wale marafiki watatu Ayubu (yaani Elfazi, Sofari na Bildadi). Mawazo yao yalianzia pale, walipoona Mungu kamletea Ayubu majanga makubwa kama tunavyoyasoma katika biblia.. Walipoona ghafla mali za Ayubu zimepukutika, baadaye tena familia yake ikaondoka, na zaidi ya yote, magonjwa ya mauti yakawa yanamwandama…
Hivyo hawa marafiki zake watatu ambao walikuwa ni wenye hekima kweli kama yeye, na wakati mwingine wenye upendo, kiasi kwamba kufunga safari toka mbali kuja kumfariji Rafiki yao, na kulia naye, ni jambo la upendo mwingi..Lakini walikosa kujua kitu kimoja..Wao walidhani kigezo pekee cha mtu kukubaliwa na Mungu ni kuwa na mali, na utajiri, na mafanikio na Maisha mazuri basi…
Hivyo watu wote waliokuwa wanawaona barabarani kama matajiri, na wenye mali, walihitimisha kuwa ni marafiki wa Mungu wakubwa, Halikadhalika wale wanaopatwa na matatizo na shida, wanatumika chini ya laana kubwa ya Mungu..Hilo tu ndilo lilikuwa kikwazo kwao, lakini mengine yote hawakuwa na hatia..
Sasa ulipofika wakati wa Rafiki yao kipenzi Ayubu kukutwa na majanga kama yale, ndipo wakahitimisha kuwa Ayubu sasa kuna mahali alimkosea Mungu, tena mahali pakuwa sana, na hivyo ni lazima akiri, na atubu makosa yake, wakawa wanamshurutisha kwa nguvu, wakijaribu kushuhudia mabaya yake kwa kila namna..kwa kumwambia maneno kama haya:
Ayubu 4:7 “Kumbuka, tafadhali, ni nani aliyeangamia akiwa hana hatia? Au hao waelekevu, walikatiliwa mbali wapi? 8 Kama mimi nilivyoona, hao walimao maovu, Na kupanda madhara, huvuna yayo hayo. 9 Kwa pumzi za Mungu huangamia. Na kwa kuvuma kwa hasira zake humalizika”.
Ayubu 4:7 “Kumbuka, tafadhali, ni nani aliyeangamia akiwa hana hatia? Au hao waelekevu, walikatiliwa mbali wapi?
8 Kama mimi nilivyoona, hao walimao maovu, Na kupanda madhara, huvuna yayo hayo.
9 Kwa pumzi za Mungu huangamia. Na kwa kuvuma kwa hasira zake humalizika”.
Ayubu 8:3 “Je! Mungu hupotosha hukumu? Au, huyo Mwenyezi hupotosha yaliyo ya haki? 4 Kwamba watoto wako wamemfanyia dhambi, Naye amewatia mkononi mwa kosa lao; 5 Wewe ukimtafuta Mungu kwa bidii, Na kumsihi huyo Mwenyezi; 6 Ukiwa wewe u safi na mwelekevu; Hakika yeye sasa angeamka kwa ajili yako, Na kuyafanya makazi ya haki yako kufanikiwa. 7 Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, Lakini mwisho wako ungeongezeka sana.
Ayubu 8:3 “Je! Mungu hupotosha hukumu? Au, huyo Mwenyezi hupotosha yaliyo ya haki?
4 Kwamba watoto wako wamemfanyia dhambi, Naye amewatia mkononi mwa kosa lao;
5 Wewe ukimtafuta Mungu kwa bidii, Na kumsihi huyo Mwenyezi;
6 Ukiwa wewe u safi na mwelekevu; Hakika yeye sasa angeamka kwa ajili yako, Na kuyafanya makazi ya haki yako kufanikiwa.
7 Tena ujapokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, Lakini mwisho wako ungeongezeka sana.
Ayubu 15:34 “Kwa kuwa jamii ya hao wasiomcha Mungu watakuwa tasa, Na moto utateketeza mahema yenye rushwa”.
N.k n.k, hatuwezi kuorodhesha mistari yote hapa, lakini soma kitabu cha Ayubu kuanzia sura ya 4-25, utaona, msimamo wao hao watu jinsi ulivyokuwa mkali na ule ule, Kwamba Ayubu kupatwa na misiba ile ni matokeo ya uovu wake aliomtendea Mungu, Pamoja na familia yake..
Lakini kwasababu Ayubu alikuwa anamjua Mungu vizuri, hakuhitimisha kuwa kupitia shida, au mtu kuwa maskini au kupungukiwa ni kwamba Mungu amekukataa, badala yake alianza kuwaeleza siri ambayo walikuwa hawaijui akawaambia, wapo watu ambao wamemkataa Mungu, ambao hawaamini hata uweza wa Mungu, lakini Mungu huyo huyo anawapa, afya, amebariki kazi za mikono yao, amewafanikisha kwa kila kitu watakacho, na zaidi ya yote wamepewa Maisha marefu, lakini mwisho wa siku watakufa na watashuka kuzimu kwa ghafla…Hivyo kigezo cha kufanikiwa sio kigezo kuwa Mungu amekukubali..
Ayubu 21:7 “Mbona waovu wanaishi, Na kuwa wazee, naam, na kuongezeka kuwa na nguvu? 8 Kizazi chao kinathibitika nao machoni pao, Na wazao wao mbele ya macho yao. 9 Nyumba zao zi salama pasina hofu, Wala fimbo ya Mungu haiwapigi. 10 Fahali wao huvyaza wala hapungukiwi na nguvu; Ng’ombe wao mke huzaa, asiharibu mimba. 11 Huwatoa kama kundi watoto wao. Na watoto wao hucheza. 12 Huimba kwa matari na kwa kinubi, Na kuifurahia sauti ya filimbi. 13 Siku zao hutumia katika kufanikiwa, Kisha hushuka kuzimuni ghafula. 14 Walakini walimwambia Mungu. Tuondokee; Kwani hatutaki kuzijua njia zako. 15 Huyo Mwenyezi ni nani, hata tumtumikie? Nasi tutafaidiwa nini tukimwomba? 16 Tazama, kufanikiwa kwao hakumo mkononi mwao; Mashauri ya waovu na yawe mbali nami. 17 Je! Ni mara ngapi taa yao waovu huzimishwa? Na msiba wao kuwajilia? Na Mungu kuwagawanyia uchungu kwa hasira yake? 18 Ili wawe kama mabua makavu mbele ya upepo, Kama makapi yaliyochukuliwa na dhoruba”?
Ayubu 21:7 “Mbona waovu wanaishi, Na kuwa wazee, naam, na kuongezeka kuwa na nguvu?
8 Kizazi chao kinathibitika nao machoni pao, Na wazao wao mbele ya macho yao.
9 Nyumba zao zi salama pasina hofu, Wala fimbo ya Mungu haiwapigi.
10 Fahali wao huvyaza wala hapungukiwi na nguvu; Ng’ombe wao mke huzaa, asiharibu mimba.
11 Huwatoa kama kundi watoto wao. Na watoto wao hucheza.
12 Huimba kwa matari na kwa kinubi, Na kuifurahia sauti ya filimbi.
13 Siku zao hutumia katika kufanikiwa, Kisha hushuka kuzimuni ghafula.
14 Walakini walimwambia Mungu. Tuondokee; Kwani hatutaki kuzijua njia zako.
15 Huyo Mwenyezi ni nani, hata tumtumikie? Nasi tutafaidiwa nini tukimwomba?
16 Tazama, kufanikiwa kwao hakumo mkononi mwao; Mashauri ya waovu na yawe mbali nami.
17 Je! Ni mara ngapi taa yao waovu huzimishwa? Na msiba wao kuwajilia? Na Mungu kuwagawanyia uchungu kwa hasira yake?
18 Ili wawe kama mabua makavu mbele ya upepo, Kama makapi yaliyochukuliwa na dhoruba”?
Unaona? Hata baada ya kuelezwa maneno hayo, hilo halikuwafanya marafiki wa Ayubu wabadilishe mitazamo yao, msimamao wao bado ulikuwa ni ule ule, kwamba Ayubu kakosea mahali!, ndio maana yale yote yamempata…Mungu kamwe hawezi kuruhusu mabaya kama yale yamkute mja wake..hilo haliwezekani,
Lakini mwisho kabisa mwa kitabu cha Ayubu tunaona Mungu anasimama na kuanza kuzungumza sasa, akamwambia Ayubu maneno yafuatayo..
Ayubu 42:7 “Basi ikawa, baada ya Bwana kumwambia Ayubu maneno hayo, Bwana akamwambia huyo Elifazi Mtemani, HASIRA ZANGU ZINAWAKA JUU YAKO, na juu ya hao rafiki zako wawili; kwa kuwa ninyi HAMKUNENA YALIYO SAWA KATIKA HABARI ZANGU, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu. 8 Basi sasa, jitwalieni ng’ombe waume saba, na kondoo waume saba, mkamwendee mtumishi wangu Ayubu, mjisongezee sadaka ya kuteketezwa; na huyo mtumishi wangu Ayubu atawaombea ninyi; kwa kuwa nitamridhia yeye, nisiwatende sawasawa na upumbavu wenu; kwani ninyi HAMKUNENA MANENO YALIYONYOKA KATIKA HABARI ZANGU, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu”
Ayubu 42:7 “Basi ikawa, baada ya Bwana kumwambia Ayubu maneno hayo, Bwana akamwambia huyo Elifazi Mtemani, HASIRA ZANGU ZINAWAKA JUU YAKO, na juu ya hao rafiki zako wawili; kwa kuwa ninyi HAMKUNENA YALIYO SAWA KATIKA HABARI ZANGU, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu.
8 Basi sasa, jitwalieni ng’ombe waume saba, na kondoo waume saba, mkamwendee mtumishi wangu Ayubu, mjisongezee sadaka ya kuteketezwa; na huyo mtumishi wangu Ayubu atawaombea ninyi; kwa kuwa nitamridhia yeye, nisiwatende sawasawa na upumbavu wenu; kwani ninyi HAMKUNENA MANENO YALIYONYOKA KATIKA HABARI ZANGU, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu”
Ni lipi tunafundishwa?
Kwa bahati mbaya, hata sasa mawazo kama haya mabovu yapo vichwani mwa baadhi yetu (Hususani wahubiri wa leo). Tunamwazia Mungu katika utajiri tu na mafanikio? Na mahubiri yetu kila siku ni hayo, na tunatumia mistari baadhi baadhi ya kusimami, kama walivyofanya wakina Bildadi, Sofari na Elfazi.
Ndugu unayosoma ujumbe huu, ikiwa na wewe unamnenea Mungu maneno kama hayo, ikiwa na wewe unamuhubiri Mungu kwa njia hiyo tu, ikiwa biblia unayoisoma unaona mistari tu kufanikiwa kimwili, na unawafundisha wengine hivyo..angalia sana..Hasira ya Mungu isije ikawa juu yako.
Kumbuka: (Sio kwamba tusihubiri mafanikio, la! Kwa Mungu yapo mafanikio, makubwa sana! lakini usihubiri kwamba wote ambao hawajafanikiwa na maskini wamepungukiwa na kitu kwa Mungu wao, hapo utakuwa hujamzungumzia Mungu vizuri). Hata ufanyaje huwezi elewa njia zote za Mungu, hivyo epuka kulazimisha kila jambo, na kutaka liwe kama wewe unavyotaka liwe. Sio kila mtu mwenye ulemavu ana laana!, sio wote wenye magonjwa ya muda mrefu yasiyopona kafungwa na nguvu za giza!..sio vipofu wote unaowaona au viziwi ni laana inawafuata… Wengine Mungu karuhusu wawe hivyo kwa makusudi yake yeye (kasome Yohana 9:1-3)
Yakobo 2:4 “ Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao?”
1Wakoritho 10:11 “Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani. 12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.
1Wakoritho 10:11 “Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.
12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.
Maran atha!
Je Mungu anawapenda watu wote au ana chuki?
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.
Jehanamu ni nini?
JAWABU LA MAISHA YA MTU.
KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili.
Historia ya nyimbo KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili~ Tis So Sweet to Trust in Jesus.
Wimbo huu uliandikwa na mwanamke mkristo wa kiingereza aliyeitwa, Louisa M. Stead, Mnamo mwaka 1882, Ni wimbo unaoeleza furaha mtu anayoweza kuipata katika kumtegemea Kristo, Lakini nyuma ya uandishi wa wimbo huu, imelala historia nzito ya Maisha aliyopitia Louisa M stead,
Ilikiwa ni siku moja Louisa na mumewe Pamoja na mtoto wao wa kike aliyeitwa Lily, walipanga safari ya kwenda matembezi, wakiwa ufukweni mwa kisiwa kimoja ghafla walisikia sauti kama ya mtu inapiga kilele za kuzama, kwenda kukimbia kuangalia wakamwona kijana mmoja, hilo lilimfanya mume wa Louisa, ajaribu kwenda kumwokoa, lakini katika jitihada zake za kufanya hivyo kwa bahati mbaya wote wawili wakazama, wakafa (kijana Pamoja na mume wake), mbele ya macho ya Louisa na binti yake.
Maisha yao baada ya hapo yalianza kuporomoka, Maisha yakawa magumu, Lakini wakagundua kuwa Mungu hakuwaacha katika hali zao, aliwatimizia mahitaji yao, hapo ndipo Louisa na binti yake walijifunza kumtegemea Mungu, na ndipo akauandika wimbo huu;
*****
Baadaye Louisa na binti yake wakasafiri kwenda Afrika kusini kwa kazi ya umishionari.
Lakini ni nini tunajifunza katika wimbo huu na uandishi wake?
Mimi na wewe tunaweza tukawa hatujapitia katika hali ngumu kama aliyopitia yeye, lakini yeye aliyeyapitia amemwona Mungu akimpigania, mpaka anaimba na kusema, “Nimemwona thabiti”..Hiyo ni kuonyesha kuwa hata wewe ukimwamini Yesu na kumtegemea, ..Utamwona thabiti/hakika akiwa na wewe katika maisha yako haijalishi leo unapitia mahali pagumu kiasi gani.
Imba wimbo huu ukikumbuka matendo yote makuu aliyokutendea nyuma. Na hakika utausikia uwepo wake nafsi mwako.
Tazama chini historia za nyimbo nyingine za Tenzi.
Tafadhali share na wengine.
NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics
MWAMBA WENYE IMARA
USINIPITE MWOKOZI Lyrics
BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics
CHA KUTUMAINI SINA lyrics
UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.
NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?
Utauwa umewahi kusikia maneno haya mawili yakitamkwa miongoni mwa wakristo. (Shalomu na Maranatha) Lakini pengine huelewi maana yake!.
Nini maana ya Shalomu?
Shalomu au Shalom ni neno la kiebrania lenye maana ya “AMANI” Kwa kiingereza “PEACE”. Hivyo wayahudi pamoja na wakristo wa kanisa la kwanza walipokutana walisalimiana na kwa salamu ya neno hilo “Shalomu”.
Pia Mungu wetu jina lake ni YEHOVA-SHALOMU, maana yake “Mungu wa amani”
Waamuzi 6:22 “Gideoni akaona ya kuwa ni malaika wa Bwana; Gideoni akasema, Ole wangu, Ee Bwana MUNGU! Kwa kuwa nimemwona Bwana uso kwa uso. 23 Bwana akamwambia Amani iwe pamoja nawe; usiogope; hutakufa. 24 Ndipo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu hapo, akaiita jina lake, Yehova-Shalomu; hata hivi leo iko huko katika Ofra ya Waabiezeri”.
Waamuzi 6:22 “Gideoni akaona ya kuwa ni malaika wa Bwana; Gideoni akasema, Ole wangu, Ee Bwana MUNGU! Kwa kuwa nimemwona Bwana uso kwa uso.
23 Bwana akamwambia Amani iwe pamoja nawe; usiogope; hutakufa.
24 Ndipo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu hapo, akaiita jina lake, Yehova-Shalomu; hata hivi leo iko huko katika Ofra ya Waabiezeri”.
Kasome pia Warumi 15:33, Warumi 16:20, Wafilipi 4:9, 1Wathesalonike 5:23, Waebrania 13:20
Na Bwana wetu Yesu anajulikana kama Mfalme wa Amani (kasome Isaya 9:6, Waebrania 7:2).
Hivyo kama Mungu wetu ni Mungu wa Amani na mwana wake wa pekee Yesu Kristo ni Bwana wa Amani, Basi na sisi pia tunapaswa tuwe watu wa Amani na watu wote ili tufanane na yeye, na sio Amani ya midomo tu! bali ya vitendo. Neno Shalom litokapo vinywani vyetu liwe ni udhihirisho wa kitu kinachoendelea katika maisha yetu kwamba tunayo Amani na watu wote. Na lisiwe linatoka tu vinywani na huku mioyoni mwetu kuna unafiki, shari na chuki. Ukitamka tu! na huku moyoni mwako kuna vinyongo na hasira, na shari basi utakuwa hujaelewa nini maana ya shalomu.
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”
1Petro 3:10 “Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila. 11 Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana“.
1Petro 3:10 “Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.
11 Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana“.
Maana ya Maran atha
Ni neno la kiebrania hivyo hivyo lenye maana ya “Bwana wetu anakuja” ni neno la Faraja kwa wakristo wote wanaomgonja Bwana....1Wakorintho 16:23
Bwana atubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?
NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?
MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.
SWALI: Nini maana ya hili Neno “watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa” (Hosea 4:6).
JIBU: Maarifa yanayozungumziwa hapo sio maarifa ya darasani.. ingawa hata hayo ya shuleni pia ni maarifa na yana nafasi yake katika maisha, lakini yaliyozungumziwa hapo sio hayo..
Maarifa yanayozungumziwa hapo ni maarifa ya kumjua Mungu.
Mithali 1:7 “Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu”
Hali kadhalika biblia inaposema “Mkamate sana Elimu, usimwache aende zake, maana yeye ndio uzima wako (Mithali 4:13)”.. Tafsiri ya kwanza ya mstari huo sio Elimu ya kidunia, bali ni elimu ya Ufalme wa Mbinguni.
Mathayo 13:51 “Yesu aliwauliza, Mmeyafahamu hayo yote? Wakamwambia, Naam. 52 Akawaambia, Kwa sababu hiyo, kila mwandishi mwenye ELIMU YA UFALME WA MBINGUNI amefanana na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale”
Mathayo 13:51 “Yesu aliwauliza, Mmeyafahamu hayo yote? Wakamwambia, Naam.
52 Akawaambia, Kwa sababu hiyo, kila mwandishi mwenye ELIMU YA UFALME WA MBINGUNI amefanana na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale”
Kasome pia (Yohana 7:15-17, Marko 1:27,1Timotheo 6:3-5, Matendo 17:18-34), Na pia kuna somo tuliloliandikwa lenye kichwa “Fahamu majira tuliyopo na nini unapaswa uwe nacho”, upatapo nafasi lipitie utapata kuelewa Zaidi.
Kwahiyo mbele za Mungu mtu asiye na Elimu ni yule asiyezijua siri za ufalme wa Mbinguni ikiwemo uweza wa Mungu, na mtu asiye na maarifa ni yule asiyeyajua maarifa ya kimbinguni (maana yake hajui chochote kuhusu Mungu), haijalishi atakuwa na Elimu ya kidunia kubwa kiasi gani; awe profesa, awe dokta awe waziri au awe mtu yeyote yule mwenye elimu kubwa..kama hana Elimu na Maarifa ya ufalme wa mbinguni, basi mbingu inamwona ni hana Elimu wala maarifa yoyote…Na hivyo Ataangamizwa.
Sasa tukirudi kwenye huo mstari wa Hosea kuna kitu cha kujifunza Zaidi..Hebu tuusome tena kwa makini..
Hosea 4:6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe, usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeisahau sheria ya Mungu wako, mimi nami nitawasahau watoto wako”
Ukisoma kwa makini hapo inasema “watu wangu wanaangamizwa!” na sio “wanaangamia”..Maana yake ni kwamba mtu akikosa maarifa ya kimbinguni kuna kitu cha nje kitamwangamiza. Hataangamia tu peke yake..La! bali kuna kitu kitakuja kumwangamiza.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba maarifa ni kama “ULINZI”. Unapokuwa na maarifa mengi ya kumjua Mungu basi ni ngumu kushambuliwa na Adui yetu shetani na majeshi yake.
Mithali 1:26 “Mimi nami nitacheka siku ya msiba wenu, Nitadhihaki hofu yenu ifikapo; 27 Hofu yenu ifikapo kama tufani, Na msiba wenu ufikapo kama kisulisuli, Dhiki na taabu zitakapowafikia. 28 Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika; Watanitafuta kwa bidii, wasinione. 29 KWA KUWA WALICHUKIA MAARIFA, WALA HAWAKUCHAGUA KUMCHA BWANA. 30 Hawakukubali mashauri yangu, Wakayadharau maonyo yangu yote. 31 Kwa hiyo watakula matunda ya njia yao, Watashiba mashauri yao wenyewe. 32 Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza. 33 Bali kila anisikilizaye atakaa salama, Naye atatulia bila kuogopa mabaya”.
Mithali 1:26 “Mimi nami nitacheka siku ya msiba wenu, Nitadhihaki hofu yenu ifikapo;
27 Hofu yenu ifikapo kama tufani, Na msiba wenu ufikapo kama kisulisuli, Dhiki na taabu zitakapowafikia.
28 Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika; Watanitafuta kwa bidii, wasinione.
29 KWA KUWA WALICHUKIA MAARIFA, WALA HAWAKUCHAGUA KUMCHA BWANA.
30 Hawakukubali mashauri yangu, Wakayadharau maonyo yangu yote.
31 Kwa hiyo watakula matunda ya njia yao, Watashiba mashauri yao wenyewe.
32 Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.
33 Bali kila anisikilizaye atakaa salama, Naye atatulia bila kuogopa mabaya”.
Kwahiyo ni jukumu letu kila mmoja kuyatafuta Maarifa ya Mungu kwa bidii ili tusiangamizwe!..Ukikosa maarifa ya ki-Mungu, utawaogopa wachawi, ukikosa maarifa ya ki-Mungu hutajua tunaishi siku gani hizi, na hivyo utapotea katika hiki kizazi, na mwisho kwenda kuangamizwa katika moto wa milele.
HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?
MSHIKE SANA ELIMU.
CHEMBE YA NGANO ISIPOANGUKA KATIKA NCHI, IKAFA,
Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?
USITOKE NJE YA HIFADHI YA MUNGU.
KUMCHA MUNGU NI NINI? NA MTU ANAMCHAJE MUNGU?
DAKIKA MOJA TU, INAKUFANYA UMWAMINI SHETANI?
Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate ‘Neno la siku’ kila asubuhi. Na mistari mingine mingi ya faraja ..kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/GRri9BATojl2FNGbOJpjC6
Mistari ya biblia ya uponyaji.
Inawezekana wewe ni mgonjwa na pengine unapitia katika hali ya kukata tamaa kabisa ya kupona, au unao ugonjwa usioponyeka mfano Ukimwi au Kansa, lakini nataka nikuambie jambo moja, kwa mwanadamu ni kweli haiwezekani lakini kwa Mungu hakuna linaloshindikana,
Hapo kabla nilikuwa ninasikia tu shuhuda za watu wengine kuponywa, nikadhani pengine mimi sistahili, lakini nilipokuwa katika dhambi siku moja Yesu Kristo aliniponya ugonjwa wangu wa sikio uliokuwa unanisumbua kwa muda mrefu, Na hapo ndipo ulipokuwa mwanzo wa kumtazama Kristo kwa sura nyingine, na kuendelea hapo aliniponya mara kadhaa tena katika vipindi tofauti tofauti nilipougua..Kama alinifanyia mimi niliyekuwa na dhambi, atakufanyia na wewe pia.
Kwa maana Yesu mwenye upendo yeye mwenyewe alituambia hivi..
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”.
Hivyo nawe pia unapoitafakari mistari hii, nakuombea kwa Mungu ikafanyike Uponyaji mkubwa ndani ya mwili wako na maisha yako kwa ujumla, katika jina la YESU KRISTO.
Zaburi 23:1 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. 2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza. 3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. 4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”.
Zaburi 23:1 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.
2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”.
Zaburi 30:2 “Ee Bwana, Mungu wangu, Nalikulilia ukaniponya”.
Ufunuo 21:4 “Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita”.
2Wafalme 20:5 “Rudi, ukamwambie Hezekia, mkuu wa watu wangu, Bwana, Mungu wa Daudi baba yako asema hivi, Nimeyasikia maombi yako, na kuyaona machozi yako; tazama, nitakuponya; siku ya tatu utapanda nyumbani kwa Bwana”.
Zaburi 146:8 “Bwana huwafumbua macho waliopofuka; Bwana huwainua walioinama; Bwana huwapenda wenye haki”;
3Yohana 1:2 “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”.
Yeremia 17:14 “Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka; uniokoe, nami nitaokoka; kwa maana wewe ndiwe uliye sifa zangu”.
Zaburi 118:17 “Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana”.
Zaburi 119:50 “Hii ndiyo faraja yangu katika taabu yangu, Ya kwamba ahadi yako imenihuisha”.
Mathayo 8:17 “ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu”.
Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
Mathayo 14:14 “Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao”.
Yeremia 30:17 “Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana, kwa sababu wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni Sayuni, ambao hapana mtu autakaye”.
Isaya 57:18 “Nimeziona njia zake; nami nitamponya; nitamwongoza pia, nitamrudishia faraja zake, yeye na hao wanaomlilia. 19 Mimi nayaumba matunda ya midomo; Amani, amani, kwake yeye aliye mbali, na kwake yeye aliye karibu; asema Bwana; nami nitamponya”.
1Petro 2:24 “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa”.
Mathayo 9:35 “Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina”.
Yakobo 5:14 “Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana”.
Zaburi 6:2 “Bwana, unifadhili, maana ninanyauka; Bwana, uniponye, mifupa yangu imefadhaika”.
Mathayo 8:1 “Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata. 2 Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa. 3 Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika”.
Mathayo 8:1 “Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata.
2 Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.
3 Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika”.
2Wakorintho 12:9 “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwafuraha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu”.
Zaburi 107:19 “Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.20 Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao, 21 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.”.
Zaburi 107:19 “Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.20 Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao,
21 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.”.
Zaburi 103:2 “Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, Wala usizisahau fadhili zake zote. 3 Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote”
Zaburi 103:2 “Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, Wala usizisahau fadhili zake zote.
3 Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote”
Kumbukumbu 7:15 “Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote; wala hatatia juu yako maradhi yo yote mabaya uyajuayo ya Misri, lakini atayaweka juu ya wote wakuchukiao”.
Hosea 14:4 “Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha”.
Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. 2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa; 3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa;
3 Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga;
Amini!, Endelea kuamini, uponyaji wako hakika umekufukia.
Tafadhali Share, na kwa wengine ujumbe huu wa faraja,.
Pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya biblia kwa njia ya email au kwa Whatsapp tutumie ujumbe kwa namba hii: +255693036618 / +255789001312
YESU MPONYAJI.
Aponywa Ukimwi.
Ameponywa kansa iliyokuwa katika hatua ya Nne.
MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.
Kumcha Mungu ni kukoje?
Kumcha Mungu ni Neno la jumla, linalomaanisha kujishughulisha na mambo yote yanayompendeza Mungu ikiwemo; kumpenda, kumtii, kumwogopa, kuchukia uovu, kumtumikia yeye, kufanya mapenzi yake, kumwabudu, kumfanyia ibada n.k. hiyo ndio maana ya kumcha Mungu..Ni tendo la jumla linalomaanisha kufanya mambo yote anayotaka wewe uyafanye.
Na ni jukumu la kila mwanadamu chini ya jua kumcha Mungu. Na biblia imetoa faida nyingi za kufanya hivyo.
Tutaziorodhesha faida chache hapa, naamini kwa kuzijua hizo itakusaidia na wewe ambaye bado hujajua faida za kumtii Mungu, kukupa hamasa na wewe uanze kufanya.
Mithali 14:27 “Kumcha Bwana ni chemchemi ya uzima, Ili kuepukana na tanzi za mauti”.
Unaona unapokusudia kusema leo, naanza kumtafuta Mungu, basi hapo hapo tayari unafungua mlango wa chemchemi za uzima wa milele kububujika ndani yako.
Mithali 1:7 “Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu”.
Leo hii ukachagua kumtafuta Mungu katika maisha yako, ukajinyima kufuatana na njia za ulimwengu, basi Mungu anakupa zawadi nzuri sana ijulikanayo kama maarifa..Maarifa hayo mtu mwingine yoyote hawezi kupewa, Ukiwa unaendelea tu kuishi maisha ya kumpendezesha Mungu, kuna kipindi kitafika utaanza kuona mabadiliko fulani ndani yako ambayo yatakutofautisha ki-uelewa wewe na Mtu mwingine.
Mfano tunamwona Danieli na Wenzake watatu (Shedraki, Meshaki, na Abednego), wao walipoitwa na mfalme walichagua fungu la kumcha Mungu kuliko kujifurahisha na vyakula najisi vya kifalme..Na hiyo ikawapelekea baadaye mwishoni walipokuja ku-dahiliwa na mfalme, wakaonekana wao ni bora mara 10 zaidi ya wale wenzao waliokuwa wanajifurahisha katika vyakula vya kifalme.
Danieli 1:17 “Basi, kwa habari za hao vijana wanne, Mungu aliwapa maarifa na ujuzi katika elimu na hekima; Danieli naye alikuwa na ufahamu katika maono yote, na ndoto. 18 Hata mwisho wa siku zile alizoziagiza mfalme za kuwaingiza, mkuu wa matowashi akawaingiza mbele ya mfalme Nebukadreza. 19 Naye mfalme akazungumza nao; na miongoni mwao wote hawakuonekana waliokuwa kama Danieli, na Hanania, na Mishaeli, na Azaria; kwa hiyo wakasimama mbele ya mfalme. 20 Na katika kila jambo la hekima na ufahamu alilowauliza mfalme, akawaona kuwa walifaa mara kumi zaidi ya waganga na wachawi waliokuwa katika ufalme wake”.
Danieli 1:17 “Basi, kwa habari za hao vijana wanne, Mungu aliwapa maarifa na ujuzi katika elimu na hekima; Danieli naye alikuwa na ufahamu katika maono yote, na ndoto.
18 Hata mwisho wa siku zile alizoziagiza mfalme za kuwaingiza, mkuu wa matowashi akawaingiza mbele ya mfalme Nebukadreza.
19 Naye mfalme akazungumza nao; na miongoni mwao wote hawakuonekana waliokuwa kama Danieli, na Hanania, na Mishaeli, na Azaria; kwa hiyo wakasimama mbele ya mfalme.
20 Na katika kila jambo la hekima na ufahamu alilowauliza mfalme, akawaona kuwa walifaa mara kumi zaidi ya waganga na wachawi waliokuwa katika ufalme wake”.
Hivyo na wewe ukiamua leo kumcha Mungu, yaani kutafuta kuyatenda mapenzi yake yapo maarifa mengine yatokayo mbinguni yataingia ndani yako kukutofautisha na ulimwengu wote.
Zaburi 111:10 “Kumcha Bwana ndio mwanzo wa hekima, Wote wafanyao hayo wana akili njema, Sifa zake zakaa milele”.
Sulemani alichagua kwanza kumcha Mungu, ndipo akapata hekima ambayo iliwazidi watu wote ulimwengu..Hekima inakusaidia kupambanua mambo, inakusaidia kuelewa hata maandiko..Leo hii unaweza kusoma biblia usiielewe, lakini ukiwa ni mtu wa kutafuta kumjua Mungu na kuzidi kutaka kujifunza kutenda mapenzi yake, hekima hiyo Mungu anaileta ndani yako, na kujikuta unapata ufahamu wa kuyaelewa maandiko, na kupambanua mambo.
Mithali 10:27 “Kumcha Bwana kwaongeza siku za mtu; Bali miaka yao wasio haki itapunguzwa”.
Kama ulidhani ni kuwaheshimu tu wazazi ndio kunaongeza siku za kuishi..Basi leo ujue kuwa ukiishi kwa kumpendeza Mungu nako pia kunazidisha siku zako za kuishi duniani. Mwangalie Ibrahimu, mwangalie Ayubu, mwangalie Yakobo n.k. hawa wote walikuwa ni wacha Mungu, na Mungu akawapa maisha marefu.
Mithali 14:26 “Kumcha Bwana ni tumaini imara; Watoto wake watakuwa na kimbilio”.
Ukijibidiisha wewe kumtumikia Mungu, faida zake haziishi tu kwako, bali mpaka wa watoto wako,utakapokuwa haupo duniani, ndivyo ilivyokuwa kwa watoto wa Ibrahimu, na watoto wa Yakobo na watoto wa Yusufu,
Mithali 22:4 “Thawabu ya unyenyekevu ambao ni kumcha Bwana Ni utajiri, na heshima, nayo ni uzima”.
Kama ukijibidiisha kuifanya kazi yake, Mungu anakupa na utajiri pia juu yake, wakati wake ukifika..
Bwana Yesu alisema..
Marko 10:29 “Yesu akasema, Amin, nawaambieni, Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili, 30 ila atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, na ndugu wake, na mama, na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele”.
Marko 10:29 “Yesu akasema, Amin, nawaambieni, Hakuna mtu aliyeacha nyumba, au ndugu waume, au ndugu wake, au mama, au baba, au watoto, au mashamba, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili,
30 ila atapewa mara mia sasa wakati huu, nyumba, na ndugu waume, na ndugu wake, na mama, na watoto, na mashamba, pamoja na udhia; na katika ulimwengu ujao uzima wa milele”.
Hizo zote ni faida zitokanazo na mtu Yule anayejishughulisha na mambo ya Mungu.
Ikiwa wewe umeokoka tayari, ni biblia pekee ndio itakayokuwa msaada wako wakati wote.Ukiwa msomaji wa Biblia itakayokusaidia kulifanya lile joto la kumcha Bwana liendelee kudumu ndani yako.. Lakini ukiwa sio msomaji wa biblia, yaani ni mivivu, ni rahisi kulipunguza kama sio kuacha kabisa kuyafanya mapenzi ya Mungu, biblia ni mwanga hiyo pekee ndio inatoa faraja, inatoa tumaini, inatia nguvu, inaonya, inakumbusha, inaongoza, inashauri..Hivyo ikiwa wewe ni msomaji mzuri wa biblia ni rahisi kwako kuishi maisha ya kumcha Mungu sikuzote..
Na ndio maana Mungu aliwapa wana wa Israeli, mpaka na wafalme maagizo haya kujifunza torati daima;
Kumbukumbu 17:18 “.. ajiandikie nakala ya torati hii katika chuo, kufuata hicho kilicho mbele ya makuhani Walawi; 19 na awe nayo, asome humo siku zote atakazoishi; ili apate kujifunza kumcha Bwana, Mungu wake, ayashike maneno yote ya torati hii na amri hizi, kwa kuyafanya; Hivyo nawe pia jifunze biblia kwa muda mwingi uwezavyo. Na pia jitenge na mambo maovu Mithali 8:13 “Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia’.
Kumbukumbu 17:18 “.. ajiandikie nakala ya torati hii katika chuo, kufuata hicho kilicho mbele ya makuhani Walawi;
19 na awe nayo, asome humo siku zote atakazoishi; ili apate kujifunza kumcha Bwana, Mungu wake, ayashike maneno yote ya torati hii na amri hizi, kwa kuyafanya;
Hivyo nawe pia jifunze biblia kwa muda mwingi uwezavyo. Na pia jitenge na mambo maovu
Mithali 8:13 “Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia’.
Kwa kufanya hivyo faida zote tulizo zihorodhesha hapo juu zitakuja juu ya maisha yako.
Lakini kama hujaokoka, na unataka leo uanze safari yako na Mungu, basi uamuzi, huo ni mzuri, hapo ulipo Bwana anaweza kukusamehe na kukuokoa kabisa..Ikiwa tu utakuwa tayari kutubu kwa kumaanisha..Hivyo kama upo tayari kufanya hivyo basi bofya hapa, kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe: +255 789001312
WEWE NI BWANA UNIPONYAYE.
Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?
TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.
YATAMBUE MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO.
NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.
MANENO ALIYOWEZA KUTAMKA YESU TU PEKE YAKE.