Category Archive Home

“Akaiona imefagiwa na kupambwa” Maana yake nini (Luka 11:26).

Swali: Bwana YESU alisema pepo anapomtoka mtu na baadaye akirudi na kukuta nyumba yake imefagiliwa na kupambwa huenda kuchukua pepo wengine saba,.. maaa yake nini kusafishwa na kupambwa?.. je mapepo wanapenda sehemu safi?


Jibu: Awali ya yote tuisome mistari hiyo.

Luka 11:24 “Pepo mchafu amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika; asipoona, husema,

25 Nitairudia nyumba yangu niliyotoka.

26 Hata afikapo, akaiona imefagiwa na kupambwa, ndipo huenda akachukua pepo wengine saba, walio waovu kuliko yeye mwenyewe, wakaingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza”.

Sasa kabla ya kujua nini maana ya “kufagia na kupambwa” hebu tuelewe kwanza maana ya nyumba kiroho..

Maandiko yanasema Miili yetu ni Hekalu la Roho Mtakatifu..

1 Wakorintho 6.19 “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;

20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu”.

Soma pia 1Wakorintho 3:16 utaona jambo hilo hilo..

Sasa kama miili yetu imekusudiwa iwe Hekalu/nyumba ya Roho Mtakatifu, maana yake ni kwamba isipokaliwa na Roho Mtakatifu basi itakaliwa na roho chafu za mapepo, maana yake badala ya mwili kuwa Nyumba ya Roho Mtakatifu, sasa inakuwa ni nyumba ya mapepo.

Hivyo mpaka hapo tumeshaelewa kuwa Nyumba inayozungumziwa hapo katika Luka 11:25-26, si nyingine zaidi ya miili yetu.

Sasa swali la pili: Nini maana ya kupambwa na kufagiliwa.

Hebu tena tutumie maandiko tujue mapambo ya nyumba ya Mungu (yaani miili yetu) ni yapi, na mapambo ya mapepo ni yapi.

1Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, KUSIWE KUJIPAMBA KWA NJE, YAANI KUSUKA NYWELE; NA KUJITIA DHAHABU NA KUVALIA MAVAZI;

4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao”.

Angalia mstari wa tatu (3) anasema.. Kujipamba kwenu KUSIWE!, Zingatia hilo neno KUSIWE!!.. Maana yake ni kwamba mapambo yake ni kwamba mapambo yafuatayo si ya ki Mungu bali ni ya Ibilisi, ndio maana anasema hapo KUSIWE!.. Sasa hebu tuendelee tuangalie hayo mapambo..

…”Kujipamba kwenu, KUSIWE KUJIPAMBA KWA NJE, YAANI KUSUKA NYWELE; NA KUJITIA DHAHABU NA KUVALIA MAVAZI..”

Oo kumbe! kuweka wigi, kuvalia mavazi (ya kikahaba), na kuvaa dhahabu masikioni na shingoni na vikuku miguuni na mikononi ni mapambo ya mapepo, na tena tumeshaona kuwa “nyumba” tafsiri yake kiroho ni “miili yetu”, hivyo tunapoweka hereni masikioni, wigi kichwani, cheni shingoni na vikuku miguuni, tafsiri yake ni kwamba nyumba zetu (yaani miili yetu) tumeipamba kwa mapambo ya kipepo, ambayo yale mapepo yakiona yanafurahi na kwenda kutafuta pepo wengine saba, na kurudi kumwingia mtu.. Hii ni ajabu sana!.

Na ndio maana wengi (wanaume na wanawake) wanaopamba miili yao na kuvaa kikahaba wanakuwa wanasumbuliwa na mapepo na ndoto mbaya!, kwanini?..kwasababu miili yao ni nyumba iliyofagiliwa na kupambwa..

Sasa utauliza kufagiliwa ni kufanya nini?…Kufagiliwa ni maandalizi ya mapambo!..Maandalizi yote ya kiroho na kimwili kabla ya mtu kujitia mapambo ya nje ni “kufagia”..

Lakini hebu tuangalie mapambo ya ki MUNGU ni yapi!.. Tuendelee na mistari ile..

“Kujipamba kwenu, KUSIWE KUJIPAMBA KWA NJE, YAANI KUSUKA NYWELE; NA KUJITIA DHAHABU NA KUVALIA MAVAZI;

4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu”.

Bali anasema mapambo yetu yawe Utu wa moyoni, yaani Roho ya Upole, na utulivu (kwa ufupi utakatifu).
Je! mama, dada, au kaka ni mapambo gani unayo?..ya nje au ya ndani??.. ni kweli utaonekana wa kisasa, unayekwenda na wakati, lakini fahamu kuwa mapambo hayo ndio mapepo wanayoyaangalia.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10 atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Print this post

VUNJA MADHABAHU, ANGUSHA NGUZO, KATA ASHERA NA CHOMA SANAMU.

Haya ni mambo manne yanayopalilia matatizo kuanzia ngazi ya kifamilia mpaka ya kitaifa!. (Madhabahu, Nguzo, Ashera na Sanamu).


Kumbukumbu 7:5-6 “Lakini watendeni hivi; zivunjeni madhabahu zao zibomosheni nguzo zao, yakateni maashera yao, ziteketezeni kwa moto sanamu zao za kuchonga.

6 Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa BWANA, Mungu wako; BWANA Mungu wako, amekuchagua kuwa watu wake hasa, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa nchi”

Labda utauliza mambo haya ni mambo gani kwa undani wake na yanaathiri vipi maisha.

   1. Madhabahu:

Madhabahu ni mahali popote panapotolewa dhabihu (sadaka).

Sadaka ina nguvu, ndio maana hakuna mganga anayetoa huduma bila sadaka,

Sasa si kwamba sadaka anahitaji tu  kwaajili ya mahitaji yake..La! bali anajua uchawi wake hautafanya kazi ipasavyo pasipo sadaka, kwahiyo madhabahu ni mahali mahususi kwa sadaka..

Katika biblia BWANA MUNGU aliwaagiza wana wa Israeli wazivunje madhabahu za wakaanani..

Na zilikuwa ni nyingi na za aina tofauti tofauti…na pasipo kuchagua waliambiwa wazivunje zotewasibakishe hata moja, kwani zitakuwa ni chanzo cha matatizo..

Ikimaanisha kuwa madhabu za mashetani ni za kuvunja si za kuziacha, kwani zinapeleka harufu mbaya mbele za MUNGU, na hivyo kuleta matatizo mengi…

Ikiwa kuna mahali ipo madhabahu wanapotolea sadaka karibu nawe, na hiyo madhabahu inakuhusu kwa namna moja au nyingine (kimila), ivunje bila kuogopa!..kama alivyofanya Gideoni, usiiache kwani yaweza kukuletea matatizo.

     2. NGUZO

Nguzo ni miimo ya Mahekalu ya ibada, yaweza kuwa Hekalu la MUNGU (soma 1Wafalme 7:21 na Mwanzo 28:22),  au yaweza kuwa hekalu la mashetani (Soma 2Wafalme 10:26-27).

Maana yake mahali popote penye msingi wa hekalu la miungu ni lazima pabomoshwe.

   3. ASHERA.

Ashera ni miti na maua yaliyokuwa yanazunguka mahekalu ya miungu, ambapo mimea hiyo iliaminika na kuabudiwa kama sehemu ya miungu.

Bwana aliwaambia wana wa Israeli wakate-kate maashera yote lisibaki hata moja (Kutoka 32:12-14).

Hali kadhalika yapo maashera hata sasa, utakuta upo mti fulani unaaminika kama ni wa kiungu na watu wanaenda kufanya matambiko hapo (hiyo ni ashera), ni ya kukata, wengine si miti bali maua tu…

Ondoa maashera katika nyumba yako, ondoa katika nyua yako na uzio wako kwani yaweza kuwa chanzo cha matatizo mengi.

   4. SANAMU.

Sanamu ni kitu chenye umbile la mtu kinachowekwa katika mahekalu na kuabudiwa.

Hizi nazo Bwana aliagiza zichomwe moto,

Sasa swali linakuja, vipi kama Madhabahu hizi, na ashera, na nguzo na sanamu zipo mbali?.

Kama zipo mbali na upeo wa kuzifikia, tunazo silaha zinazosafiri masafa marefu zaidi ya silaha zote zilizowahi kutengenezwa na mwanadamu au zitakazokuja kutengenezwa.

Silaha hiyo ni Maombi.

Maana yake katika maombi Unazivunja madhabahu kwa Imani, unaangusha Nguzo kwa imani, unakata maashera kwa imani, na unazichoma moto hizo sanamu kwa imani kupitia jina la YESU.

Na kwa jinsi utakavyotamka, zitateketea kule zilipo kwa namna hiyo hiyo, lakini usiingie kwenye maombi ya vita kama wewe si askari mwenye silaha hizi za Waefeso 6:10-15.(utajitafutia matatizo zaidi).

Pia usiache kuzibomoa kwa mikono yako kama zipo mbele ya upeo wa macho yako. (Upo unaziona sio tu kuombea, bali kuzimoa kwa mikono kabisa).

Ukifanya hivyo utakuwa umeusafisha uwanda, hakuna laana juu ya mahali ulipo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI.


Sehemu ya kwanza.

Zaburi 66:20 “Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu, Wala kuniondolea fadhili zake”.

Maombi ni zaidi ya silaha yoyote ile yenye ubora inayofahamika, leo nataka tujifunze kupitia mfano mdogo sana wa simu ya mkononi.

Kawaida ili uweze kuongeza uwezo wa simu yako, huna budi kujiunganisha na internet..

Internet ni mtandao usioonekana kwa macho, unaoratibu mawasiliano ya haraka na taarifa za haraka.

Sasa simu yako inapoungwa na internet ndipo unapoweza kupakua (kudownload) vichocheo vya simu vinavyoitwa application.

Applications zile zinasaidia kuongeza uwezo wa simu yako..

Kama unataka simu yako iweze kusoma baadhi ya makala unahitaji kichocheo husika cha kusomea makala hizo.

Vile vile kama unahitaji simu yako iwe na uwezo wa kucheza nyimbo kwa mpangilio, itakugharimu kupakua (download) vichocheo hivyo n.k

Simu zenye vichocheo (applications) nyingi mbalimbali ndizo zenye uwezo mkubwa..na zile zisizo na vichocheo kabisa huwa zina uwezo mdogo na changamoto nyingi.

Sasa na mwili wa Mtu ni hivyo hivyo, kuna mambo hatuwezi kufanya wala kuwa nayo pasipo hivi vichocheo vinavyoongeza uwezo.

Kwamfano huwezi kusoma biblia na kuielewa kama hujaongezewa nguvu.. Utakuwa ukishika tu unalala!.

Huwezi kuhubiri kama hujaongezewa nguvu, utakuwa unaona aibu tu!.

Huwezi kuishi maisha masafi kama hujaongezewa nguvu utajaribu lakini utashindwa…n.k.

Sasa kazi ya Roho Mtakatifu ni kutuunganisha sisi na mtandao wa kimbinguni, kama vile simu inavyoungwa na internet.

Na tunapoungwa na mtandao wa kimbinguni basi tunaweza kupakua (download) vichocheo vya kimbinguni..

Na tunavipakua vichocheo hivyo kwa njia moja tu ya MAOMBI!.

Unapoomba maana yake unapakua (download) visaidizi vya kimbinguni, ambavyo vinakuongezea nguvu katika utu wa ndani.

KUMBUKA: Maombi hayakupi kitu! Bali YANAKUONGEZEA NGUVU YA KUFANYA NA KUPATA KITU.

Ndio maana baada ya maombi utaona ile nguvu ya kusoma Neno inaongezeka, ile nguvu ya kuhubiri inaongezeka, ile nguvu ya kushinda dhambi inaongezeka, ile nguvu ya kuendelea na wokovu inaongezeka..

Utaona ile nguvu ya kuendeleza maono yako inaongezeka,..ukiona hivyo jua ni vichochezi vya kimbinguni vimeingia ndani yako vinafanya kazi..HIYO NDIO NGUVU YA MAOMBI!!.

Na kawaida hata vichochezi vya simu (application) vinakuwa updated mara kwa mara, vivyo hivyo na mwombaji huwa haombi mara moja na kuacha, bali anakuwa na desturi ya kuomba mara kwa mara ili kuimarisha vichochezi vyake.

Lakini usipokuwa mwombaji, utabaki, hutaona mabadiliko yoyote katika eneo lolote la kiroho na kimwili…kila kitu kitakuwa kigumu hakiendi..

Na kama ulikuwa mwombaji na ukapunguza kuomba, na vile vichocheo pia vinapungua nguvu.

Anza kuwa mwombaji, kuna mambo hayawezekaniki pasipo maombi hususani yale ya mfungo.

Mathayo 17:21 “Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

NI KWA NAMNA GANI KRISTO ALIZIBEBA DHAMBI ZETU?

Ili kuelewa Msamaha wa dhambi jinsi unavyofanya kazi, kwamba ni kwa namna gani Bwana YESU alibeba dhambi zetu, twaweza kuelewa kwa kutafakari mfano huu mrahisi.

Katika sheria za Mahakama inapotokea mfungwa aliyehukumiwa  kifungo, akafariki katikati ya kifungo hiko, na ikathibitishwa na jeshi la magereza pamoja na ripoti za madaktari, na akazikwa basi kile kifungo chake kinakuwa kimefika mwisho, na kesi yake inakuwa haiendelei tena (inafutwa)..

Sasa ikitokea yule mtu akafufuka baada ya siku kadhaa anakuwa hana kesi tena (yupo huru) kwani  kesi yake ilishafutwa, kutokana na ripoti za mahakama na madaktari..

Na zaidi sana mahakama haziamini ufufuo, hivyo itaendelea kuamini kuwa yule mtu alishakufa na taarifa zilithibtishwa na jeshi la magereza pamoja na madaktari.

Sasa ni hivyo hivyo kwa Bwana YESU, yeye alikubali kubeba hatia zetu na makosa yetu yaliyo mengi na akakubali kuhukumiwa kama yeye ndiye aliyeyatenda yale makosa..

Lakini alipokuwa anaanza kukitumikia kile kifungo kwa mateso makali (ambayo kiuhalisia yamgekuwa ya daima)..alikufa katikati..

Na sheria ya hukumu ni kwamba kifo kinahitimisha kifungo cha Mtu, hivyo Kristo alipokufa kifungo chake cha adhabu na mateso kikafikia mwisho, akawa hana hatia tena wala ule mzigo wa dhambi (yupo huru na dhambi sawasawa na maandiko).

Warumi 6:7 “kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi”

Lakini muujiza ni kwamba baada ya siku tatu akaonekana yu hai, na kwasababu hukumu yake ilishafutwa kwa kifo chake, akawa huru na kifungo hiko baada ya kufufuka, ndio maana hatuoni akilia kwa uchungu wa maumivu baadaa kufufuka, bali tunaona ana utukufu mwingi.

Kwahiyo laiti Kristo asingekufa angeendelea kuhesabika laana na mwenye hatia kwaajili ya dhambi zetu nyingi alizozobeba, ingempasa aendelee kukaa katika hali ya adhabu daima, na aendelee kutengwa na MUNGU daima.

Wagalatia 3:13 “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti”

Lakini kifo chake kimehitimisha hukumu yake, ambayo sisi ndio tungepaswa tuitumikie.

Sasa tunapomwamini ndipo tunaingia katika huo mkondo wa kuondolewa dhambi..

Lakini tunapomkataa basi dhambi zetu zinabaki palepale..ni rahisi tu hivyo!.

Je umemwamini Bwana YESU?..Je umebatizwa kwa ubatizo sahihi wa Maji mengi na wa Roho Mtakatifu?.

Kama bado unasubiri nini?…je bado huoni tu gharama kubwa Bwana YESU aliyoingia kwaajili yetu ili tupate ondoleo la dhambi?.

Mpokee YESU leo wala usingoje kesho.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Fahamu Maana ya Mithali 15:24 Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;

SWALI: Nini Maana ya Mithali 15:24?

Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini.

JIBU: Hapo yapo mambo matatu,

  1. Mtu mwenye akili.
  2. Njia ya uhai,
  3. Na uelekeo wa njia hiyo.

Mtu mwenye akili ni mtu mwenye uwezo wa kufikiri/kupambanua vema na kufanya maamuzi sahihi katika maeneo mbalimbali ya maisha yake. Hivyo hapo anasema mtu mwenye akili anajua vema kuichagua njia yake ya uhai.

Anasema njia yake hutoka chini kuelekea juu. Kwa lugha ya picha ni barabara iliyopinduliwa na kusimamishwa wima kama ngazi,  na sio mfano wa barabara hizi tulizonazo zilizolala chini, ambazo uelekeo wake ni aidha kaskazini na kusini, au mashariki na magharibi.

Sasa hapa anasema njia yake ya uhai huenda juu, ili atoke kuzimu chini. Akiwa na maana husafiri kutoka kuzimuni kuelekea uzimani juu kwa Mungu.

Hufunua nini?

Safari ya mtu mwenye akili, hufikiri kumtafuta Mungu juu alipo,

Wakolosai 3:1 Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu. 2 Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi.

Hufikiri ukuaji wa kiroho, atokea hatua moja ya utakatifu kwenda nyingi, kiwango kimoja cha Imani kuelekea kingine kama Kristo (2Petro 1:5-10, Waefeso 4:13). Ni mtu ambaye kila siku anakwenda mbali na njia ya mauti. Mawazo yake yapo juu sikuzote kumjua Kristo na mapenzi yake yote.

Lakini kinyume chake ni ukweli, mtu asiye na akili barabara yake haijasimama wima, bali imelala. Atawaza atoke hatua moja kwenda nyingine lakini hakuna ukuaji wowote au kuongezeka kokote. Huwenda anachowaza tu sikuzote ni kutoka katika umaskini kwenda katika utajiri, kutoka katika kiwango kimoja cha elimu kwenda kingine, kutoka katika cheo kimoja kwenda katika kingine..Hatua zake ni za kidunia tu, akidhani ndio uzima wake upo hapo. Kumbe kapotea njia.

Si kwamba vinapingwa vya dunia hapana, ni vizuri na vinafaa, lakini havina uzima wa milele ndani yake. Ili uwe na akili hakikisha unampokea Kristo, kisha unaanza kukua kiroho, kila siku unafikiri njia ya kuyakimbia machafu ya kidunia. Hapo barabara yako itakuwa umesimama kama ngazi na hivyo utaiponya nafsi yako.

Je! Umeokoka?. Kama ni la! Basi wakati ndio sasa fungua moyo wako mkaribishe Yesu akuokoe hizi ni nyakati za hatari, tubu leo upokee wokovu. Ikiwa upo tayari kumkaribisha Kristo moyoni mwako, basi waweza kubofya hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba. Bwana akubariki. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Maana ya Mithali 29:9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha. 

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Biblia inasema nini kuhusu mtu ‘Mwenye kujipendekeza (Mithali 29:5)

Print this post

Kuonja ni kufanya nini? (Kutoka 15:25).

Swali: Kuonja kunakozungumziwa katika kitabu cha Kutoka 15:25 kunamaanisha nini?.

Jibu: Turejee mistari hiyo..

Kutoka 15:24 “Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema,Tunywe nini? 

25 Naye akamlilia BWANA; BWANA akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, AKAWAONJA HUKO

Kuonja kunakozungumziwa hapo ni kuonja kiroho na si kimwili, siku zote mtu anayeonja kitu, lengo lake ni kukipima ubora wake, kilingana na vigezo anavyovitaka.

Na kiroho MUNGU anatuonja sisi mara kwa mara kwa kuangalia matendo yetu kama tupo sawa mbele zake…

Kwamfano utaona Bwana YESU anatumia lugha hiyo ya kiroho katika kitabu cha Ufunuo kuyapima matendo yetu..

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. 

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu”

Umeona hapa?…matendo yetu yanapimwa kwa kinywa cha Bwana..kama tu Moto mbele zake basi tuna heri, lakini kama tu baridi au vuguvugu ni Ole!.

Kwahiyo hata kipindi wana wa Israeli wakiwa wanatoka Misri kuelekea nchi ya ahadi.. Mungu alikuwa anawaonja matendo yao…

Na kuna kipindi aliwatapika walipomjaribu na kumnun’unikia.

Lakini si tu Bwana akiyekuwa anawaonja, bali pia aliwaambia kuwa hiyo nchi wanayoiendea itawaonja matendo yao, na kama yakiwa mabaya itawatapika, kwa kuwa pia iliwatapika wenyeji waliokuwa wanaiishi kutokana na mateendo yao maovu.

Walawi 18:25 “na hiyo nchi imekuwa najisi; kwa ajili ya hayo naipatiliza uovu wake juu yake, na hiyo nchi YATAPIKA wenyeji wake na kuwatoa. 

26 Kwa hiyo mtazishika amri zangu na hukumu zangu, wala msifanye machukizo hayo mojawapo; yeye aliye mzalia, wala mgeni aketiye kati yenu; 

27 (kwa kuwa hao watu wa nchi wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi imekuwa najisi;) 

28 ili kwamba hiyo nchi ISIWATAPIKE NA NINYI PIA, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa iliyotangulia mbele yenu”.

Je umempokea YESU?.

Je wewe ni moto?, au baridi au una uvuguvugu?…Uvuguvugu maana yake ni kuwa upo mguu mmoja nje!…mguu mmoja ndani!, leo unaenda kanisani kesho unaenda Bar, leo unatoa sadaka kesho unabeti, leo unavaa nguo ya sitara kesho nguo ya aibu..hapo Bwana amesema atatapika mtu wa namna hiyo.

Bwana atusaidie tumtii ili tusiwe miongoni mwa watakaotapikwa.

Maran atha!.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

ELOI ELOI LAMA SABAKTHANI?

Zaburi 22:1 Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, Na maneno ya kuugua kwangu? 2 Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu Na wakati wa usiku lakini sipati.

Maneno haya ukiyatafakari, utagundua ni ya mtu aliyefikia hatua mbaya sana ya kukaribia kukata tamaa kwasababu ya aidha magumu, au huzuni, au mateso yasiyoelekeza anayoyapitia, akiangalia kulia, haoni  tumaini lolote, akiangalia kushoto haoni mkono wowote wa Mungu ukimsaidia licha ya kuomba na kulia sana, kwa muda mrefu.

Sehemu nyingine anasema, amekataliwa kila kona, amekuwa kama msikwao kwa ndugu zake.

Zaburi 69:10 Nilipolia na kuiadhibu roho yangu kwa kufunga, Ikawa laumu juu yangu.

11 Nilipofanya gunia kuwa nguo zangu, Nikawa mithali kwao. 12 Waketio langoni hunisema, Na nyimbo za walevi hunidhihaki. 13 Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana, Wakati ukupendezao; Ee Mungu, Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, Katika kweli ya wokovu wako.

14 Uniponye kwa kunitoa matopeni, Wala usiniache nikazama. Na niponywe nao wanaonichukia, Na katika vilindi vya maji. 15 Mkondo usinigharikishe, wala vilindi visinimeze, Wala shimo lisifumbe kinywa chake juu yangu.

16 Ee Bwana, unijibu, maana fadhili zako ni njema, Kwa kadiri ya rehema zako unielekee. 17 Wala usinifiche uso wako, mimi mtumishi wako, Maana mimi nimo taabuni, unijibu upesi.

Mwandishi huyu alikuwa ni  Daudi, alipitia kipindi kirefu sana cha kujiona kama vile Mungu kamtupa, hadi kuna wakati akaona heri aende kuomba hifadhi kwa maadui zake wafilisti ambao hapo mwanzo aliwafukuza na kuwaita makafiri (wasio tahiriwa), lakini safari hii kwa unyenyekevu wote, anaenda kuwa mmoja wa askari wao, ili tu apate hifadhi, asiangamie kabisa. Huyo ni mtu ambaye maji ya shingo yalimfikia kwelikweli.

Sio kwamba alikuwa haombi, au hamlili Mungu?. Au kwamba ana dhambi kuliko wengine, mpaka awe mtu wa bahati mbaya hivyo Hapana, nyakati zote alikuwa mwombaji, lakini akafika mahali katika uhalisia wa kibinadamu aliona kama Mungu amemwacha kabisa.

Lakini kwasababu huruma za Mungu zilikuwa nyingi juu yake alimpa moyo mkuu, wa kuendelea kumngoja Bwana. Ndio maana  sehemu nyingi katika Zaburi anasisitiza sana Neno hili ‘mngojeeni Bwana’ (Zaburi 37:7, 25:3, 31:24,38:15, 40:1).

Sasa moja ya  maneno machache ya Daudi yaliyonikuliwa na Bwana Yesu lilikuwa ni hili.

Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha?

Mathayo 27: 45 Basi tangu saa sita palikuwa na giza juu ya nchi yote hata saa tisa.

46 Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?

Je! Unadhani kauli hiyo Yesu aliyoitoa alimaanisha kweli ameachwa?

Hapana, tangu mwanzo alikuwa anajua Mungu yupo pamoja naye, na kwamba saa yake imekaribia, muda si mrefu anakwenda kuinuliwa na kutukuzwa, tena sehemu nyingine anasema alishangalia pale msalabani (Wakolosai 2:15). Lakini kuinukuu kauli ile ni kuonyesha ubinadamu wetu, unavyoweza kutuhubiria tuwapo katikati ya shida, kwamba Mungu ametuacha hususani pale tunapopitia shida, na mateso.

Yesu alinukuu ubinadamu wetu kukumbuka mfano wa yale aliyoyapitia Daudi..

Lakini tunaona dakika chache baada ya pale, pindi tu alipokata roho, makaburi yakapasuka, wafu wakatoka makaburini, pazia la hekalu likapasuka, na baada ya siku tatu akafufuka, ukombozi wetu mkuu ukapatikana, ‘Lakini ni kwa maneno ya kudhaniwa kuwa Mungu amemwacha’.

Mathayo 27:50 Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.

51 Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka;

miamba ikapasuka; 52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala; 53 nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi.

Ndugu, upitiapo hatua hizo ambazo mawazo yako yanakufundisha kuwa Mungu hayupo na wewe tena, amekuacha, kwasababu ya shida unazozipitia muda mrefu, magonjwa yasiyokoma, umeomba mpaka umechoka, umelia hadi ukomo,wewe ona ni kawaida,…. Piga moyo konde Mngojee Bwana. Daudi alistahimili hatimaye akathibitishwa kwenye ufalme ambao ulidumu pamoja na vizazi vyake vingi tofauti na wafalme wengine wa Israeli. Mngojee Bwana, kimaombi, kwasababu baada ya joto huja mvua.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI YESU ALIMUITA BABA YAKE “ABA”?

kiaramu ni lugha gani? je ilizungumzwa na Yesu?

Nzi wa Misri, na Nyuki wa Ashuru vilimaanisha nini? (Isaya 7:18-20).

Print this post

Biblia inaposema sisi ni ukuhani wa kifalme, maana  yake nini?

1Petro 2:9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;


JIBU: Katika vifungu hivyo biblia inaeleza kwa ukubwa sifa zetu sisi tuliomwamini Yesu Kristo, jinsi zilivyo kuu, anasema sisi ni mzao mteule, na pia watu wa milki ya Mungu. Lakini sifa nyingine ndio hiyo ya ukuhani wa kifalme.

Angeweza kusema sisi ni  ukuhani wa kisomi, au ukuhani wa kiroho, au ukuhani ki-mbingu, au ukuhani wa kitajiri. Lakini anatumia Neno ukuhani wa kifalme. Ikiwa na maana kuwa tunao ukuhani lakini si ukuhani tu bali wenye asili ya kifalme.

Sifa kuu ya kuhani, ni kuweza kumkaribia Mungu kusema naye, na kufanya upatanisho kwa ajili ya watu wengi. Mfano wa Haruni na uzao wake. Tunaona hawa tu ndio waliopewa neema ya kuweza kumkaribia Mungu katika kiti chake che rehema, kuzungumza naye na kuomba rehemu kwa taifa zima. Wengine wote walikaa nje ya hema.

Lakini pia sifa ya mfalme ni uweza, mamlaka, nguvu, na utajiri.  Mfalme anatawala, mfalme ana nguvu ya kijeshi, mfalme ni lazima awe tajiri na mwenye utiisho.

Sasa tukirudi kibiblia, Haruni na walawi wote ambao waliopewa sifa ya kikuhani, hawakuwa na ukuhani wa kifalme ndani yao. Waliishia tu kukaa hemani, na sio ni makuhani na wakati huo huo ni wafalme, lakini pia wafalme wengi (Mfano wa Daudi, Sulemani n.k.)hawakuwa na ukuhani pia ndani yao.. Hivyo waliishia tu kutawala lakini sio kuingia hekaluni kuvukiza uvumba. Alitokea mfalme mmoja kujaribu kufanya kazi hizo mbili kwa wakati mmoja, aliishia kupata ukoma kwasababu hakukuwahi kutokea mtu mwenye uwezo huo wa kutembea katika vyeo vyote viwili kwa wakati mmoja (2Nyakati 26:16-21).

Lakini yupo aliyetabiriwa na manabii kuwa atakuwa kuhani mkuu lakini pia mfalme. Na huyo si mwingine zaidi ya Bwana wetu Yesu Kristo. (Waebrania 7:11-17), Yeye alikuwa kuhani lakini pia alitokea katika kabila la kifalme la Yuda, kwa jinsi ya mwili.

Na mpaka sasa anatawala kama kuhani mkuu wetu, lakini pia mfalme wetu. Amewazidi makuhani wote, amewazidi wafalme wote.

Hivyo na sisi tuliozaliwa na yeye, tunarithi vyote alivyonavyo, maandiko yanasema hivyo (1Petro 1:3-4), Tunafanyika sio tu makuhani, ambao tunamkaribia Mungu kusema naye ana kwa ana, na kuwapatanisha wengine na yeye, lakini pia  tunafanyika wafalme wenye mamlaka yote, na nguvu, na utajiri.

Sisi tumepewa mamlaka ya kukanyaga nge na nyoka, na nguvu zote za Yule mwovu, mamlaka ya kupooza kila aina ya magonjwa na madhaifu, mamlaka ya kufungua na kufunga jambo lolote. Vilevile tumepewa na utajiri wote wa hekima na maarifa ndani ya Yesu Kristo (Waefeso 1:3).

Na zaidi mamlaka ya ufalme tuliyonayo itakuja kudhihirika vema mbeleni kwenye utawala wa miaka 1000 wa amani wa Yesu Kristo duniani. Jinsi tutakavyo milika na kutawala na yeye kama wafalme, na yeye akiwa kama mfalme wa wafalme. (Ufunuo 19:16)

Ufunuo 5:10 ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.

Je!, umeipokea neema hii?

Ni nini unachosubiri usimpe Kristo maisha yako? Tafakari ahadi kubwa namna hii unapewa bure, ni nani anayeweza kufanya hivyo? Saa ya wokovu ni sasa, na wakati uliokubaliwa na Mungu ndio huu, okoka leo, usamehewe dhambi zako, jina lako liandikwe katika kitabu cha uzima.

ikiwa upo tayari kumpokea Yesu, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya “Uweza wa kifalme utakuwa begani mwake” (Isaya 9:6)?.

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Ulimwengu wa Roho ni nini? Na mtu anawezaje kuwa wa rohoni?

Print this post

Je mkristo anaweza akawa na mapepo?

JIBU: Swali la kwanza la kujiuliza, je! mkristo ni mtu gani?..Mkristo ni mtu aliyemwamini,Yesu Kristo, kisha akapokea msamaha wa dhambi,kwa toba ya kweli, ubatizo na kutiwa muhuri na Roho Mtakatifu.

Mtu wa namna hiyo anakuwa na Kristo ndani yake. Na mtu mwenye Kristo Hawezi kuwa na mapepo, kwasababu Yesu hana pepo.

Vifungu hivi vinatuthibitishia kuwa hilo jambo haliwezekani;

1 Yohana 4:4

[4]Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia.

2 Wakorintho 6:14

[14]Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?

Kuonyesha kuwa giza na nuru haviwezi kuwepo sehemu moja, wakati mmoja.

Lakini swali linakuja inakuwaje kuna baadhi ya watu waliokoka wanaonekana kuwa na mapepo ndani yao?

Kama tulivyoona mkristo hawezi kuwa na mapepo, lakini ni vema kufahamu kuwa kuna tofauti kati ya kukaliwa na mapepo, na kushambuliwa na kipepo. 

Mtu aliyeokoka hawezi kukaliwa na mapepo, lakini anaweza akashambuliwa au kusumbuliwa na  uwepo wa mapepo, hicho ndicho kinachoweza kumtokea, lakini sio kwamba ana mapepo ndani yake.

Sababu zinazoweza mpelekea asumbuliwe nayo, ni hizi kuu tatu;

  1. Kutoijua kweli vema
  2. Uchanga wa kiroho
  3. kutenda dhambi.

Tukianza na sababu ya kwanza.

  1. Kutoijua kweli.

Kukosa kujua nafasi na mamlaka uliyo nayo ndani ya Kristo, shetani anaweza kukusumbua kwelikweli. Na wakati mwingine kukutesa. mapepo yanaweza kuwasumbua watu kifikra na kwa kuwawekea mawazo machafu akilini mwao, kuwashitaki, kwa kuwatupia ndoto mbaya, au kuwakaba usiku, au kuwaletea majaribu mbalimbali, lakini huyu mtu akijua kuwa ameshakabidhiwa mamlaka yote ya kukanyaga nge na nyoka na nguvu zote za yule mwovu,(Luka 9:1), akaitumia vema, shetani atamwogopa kumsogelea kwasababu anajua nguvu ya kimamlaka iliyo ndani yake ni thabiti haitoki mdomoni bali inasukumwa na ufalme wa Mungu ulio nyuma yake.. Ni sawa na mtu anayetoa amri kwa kinywa chake mwenyewe na yule anayetoa kwa agizo la raisi watu watamwogopa yule anayetoa kwa mamlaka aliyopewa na raisi. Hivyo ni muhimu sana kuitafakari na kuiamini mamlaka uliyopewa na Kristo ndani yako ili hayo maroho  unapoona dalili ya kutaka kukusumbua unatamka jina la Yesu mara moja tu yanatetemeka na kukimbia. Mamlaka hiyo amepewa mkristo yoyote aliyeokoka, haijaishi ni mchanga au mkomavu.

2) Sababu ya pili ni uchanga wa kiroho.

Ukiokolewa, kwasababu ya kutoondoka mara moja kwa baadhi ya tabia, au msingi au mienendo ya kale, hivyo tabia hizo mara nyingine zinakuwa ni upenyo wa uwepo wa kipepo kuzunguka zunguka karibu yako. Vitu vichanga sikuzote hushambulika kirahisi, unyasi ukiwa mdogo hutikiswa sana na upepo, Ndio maana ni lazima uanze kuukulia wokovu, kwa kujifunza Neno, kujizoesha utakatifu, maombi, ibada, mambo ambayo adui hapendi kwasababu ni kama moto kwao.  Mtu asipokuwa mkristo wa vitendo, sikuzote atasumbuliwa na roho za kidunia, na hatimaye atajiona kama ni ana mapepo kabisa, na akiendelea kuishi hivyo, mpaka kurudi nyuma atakufa kiroho, na Roho Mtakatifu kuondoka ndani yake, na mapepo ndio yatapata nafasi ya kumtawala kabisa.  (2Petro 1:5-10)

3) Kutenda dhambi

Mtu aliyeokoka, akaanza kutenda dhambi za makusudi, anarudia yale yale kila siku, jambo hilo ni upenyo mwingine wa mapepo kumsumbua, kwasababu anakuwa ameyapa nafasi, na maandiko yanasema tumsimpe ibilisi nafasi. (Waefeso 4:27).

Kwamfano umeacha ulevi, baada ya kuokoka, na umekuwa hivyo kwa muda mrefu sasa, halafu ghafla unaanza tena kuwa mlevi, Mungu anakuonya uache hutaki, unaendelea kunywa pombe..kitendo hicho kinaweza kukupelekea kusumbuliwa sana na mapepo. Mfano tu wa Yule ambaye anatawaliwa nayo.

Mathayo 12:43 Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika,asipate.

44 Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na

kupambwa.

45 Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye

mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya.

Hivyo kwa hitimisho, ni kuwa mtu aliyeokoka, hawezi kukaliwa na mapepo, yaani kutawaliwa au  kupagawishwa, au kuendeshwa nayo.. Isipokuwa anaweza kushambuliwa, kusababishiwa madhara, lakini kuvamiwa na uwepo wao. Ndio maana tumeambiwa tuvae silaha zote za haki, ili tuweze kumpinga shetani (Waefeso 6:10). Kwa kulijua Neno, utakatifu, maombi, na ibada.

Bwana akubariki.                                                               

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.

Je mtu anaweza akawa hajaokoka akaombea mtu na Pepo likamtoka,

 

Print this post

Ni mji gani mtakatifu shetani aliomchukua Bwana YESU? (Mathayo 4:5)

Je huu mji mtakatifu shetani aliomchukua Bwana katika Mathayo 4:5 ni mji gani?.. maana tunajua shetani hawezi kumiliki vitu vitakatifu?


Jibu: Turejee..

Mathayo 4:5 “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu.
6 akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako”.

Mji Mtakatifu unaozungumziwa hapo ambao shetani alimpeleka Bwana YESU ni YERUSALEMU (Ya duniani) iliyopo pale Israeli..

Kumbuka ipo YERUSALEMU YA MBINGUNI, ambayo itakuja kushuka baada ya hukumu ya mwisho, na Yerusalemu hiyo Mpya shetani hawezi kufika wala watu ambao hawajamwamini Bwana hawataingia (kulingana na maandiko).

Ufunuo 21:1 “Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.

2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.

3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao”.

Ruka mpaka mstari wa 23-27..

“23 Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-Kondoo.

24 Na mataifa watatembea katika nuru yake. Na wafalme wa nchi huleta utukufu wao ndani yake.

25 Na milango yake haitafungwa kamwe mchana; kwa maana humo hamna usiku.

26 Nao wataleta utukufu na heshima ya mataifa ndani yake.

27 Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo”.

Lakini Mji shetani aliompeleka Bwana ulikuwa ni Yerusalemu ya duniani, (ule mji ule wa Daudi), mahali pale ambapo Hekalu la Sulemani lilijengwa..Yerusalemu hii ya duniani shetani anaweza kufika wakati wowote na mtu mwingine yoyote anaweza kufika, (awe mtakatifu au asiwe mtakatifu), anaweza kufika, na hata leo watu wanafika pale..

Na shetani alimpomfikisha Bwana YESU katika Hekalu, alimpandisha mpaka kwenye kinara chake, na kumwambia ajirushe chini, kwa maana imeandikwa atawaagiza malaika nao watamwokoa na ajali ile (sawasawa na Zaburi 91:11-12).

Lakini Kwakuwa Bwana YESU alikuwa amejaa Roho Mtakatifu, alizijuza hila na mbinu zote za ibilisi, na aliweza kumjibu kwa Neno, kuwa imeandikwa tusimjaribu Bwana MUNGU wetu.

Ni jambo gani tunaweza kujifunza hapo?

shetani anapotaka kumjaribu mtu anayemcha MUNGU hampeleki kwa waganga wa kienyeji, wala hampeleki kwenye mazingira ya dhambi ili atende dhambi, bali anampeleka sehemu takatifu, kama kanisani, au katikati ya watu wanaomtafuta MUNGU,
Ndio maana utaona leo mtu amesimama lakini anaanguka/anaangushwa katika dhambi na mtu/watu wa kanisani.

Utaona Askofu, au mchungaji, au mwinjilisti, au Nabii, au Mtume au mwimbaji wa kwaya anaanguka katika uzinzi na watu wa kanisani, ni mara chache sana na watu wa nje, kwanini?.
Kwasababu shetani anajua sehemu pekee ya kumjaribu mtu aliyeokoka na kusimama ni kanisani, akimletea wanaojiuza huko barabarani ni ngumu kuanguka..

Ndicho alichotaka kujaribu kufanya kwa Bwana YESU kumpeleka Hekaluni, kwanini asingempekeka kwenye vinara vingine vya mahali pengine, badala yake akachagua Hekalu?.. ni kwasababu alijua hapo ni rahisi kumwangusha Bwana.

Hivyo na sisi tuliookoka ni muhimu kuwa makini katika nyumba ya MUNGU kwani huko huko shetani anaweza kupata nafasi.

Bwana atusaidie.
Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 3)

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

Je! Yesu aliwezaje kuchukuliwa na shetani juu ya kinara cha hekalu kujaribiwa?

Print this post