Category Archive Home

UTIMILIFU WA TORATI.

Tukisoma Agano la Kale, biblia inaelezea maisha ya watumishi wake, jinsi walivyokuwa na jinsi walivyoishi. Tunajua kabisa wengi maisha yao hayakukamilika, kwasababu torati waliyopewa isingeweza kuwakamilisha na kuwa wakamilifu, Kwasababu torati yenyewe haikutimilika..

Ndio maana utamwona Mtu kama Daudi aliyependwa sana na Mungu, alioa wake wengi, na mwanawe Sulemani alikuwa na wake wengi vile vile. Utamwona Daudi mtu aliyeupendeza Moyo wa Mungu alikuwa anaua, na aliua watu wengi na bado BWANA hakumuhesabia makosa.

Utamwona Daudi hakubatizwa lakini bado alikuwa ni mtu anayeupendeza moyo wa Mungu. Alikuwa anashindana na kuwatakia shari maadui zake, na kuwachukia lakini bado alikuwa ni mteule wa Bwana.

Sasa kwa jicho la haraka haraka unaweza ukasema, kama Daudi alikuwa ana wake wengi, alikuwa anawashambulia na kushindana na maadui zake, alikuwa anaua na bado ni mtumishi wa Mungu, na mimi sio vibaya nikifanya hayo hayo na bado kwani Mungu atakuwa na mimi. Ni rahisi kusema hivyo.

Lakini ningependa ufahamu kitu kimoja, agano la kale(au agano la kwanza) lilikuwa sio utimilifu wa mambo yote…lilikuwa ni muhtasari tu wa Agano halisi la Mungu. Na ndio maana Bwana Yesu alisema katika..

Mathayo 5:17 “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza.”

Unaona hapo? Bwana alikuja KUITIMILIZA, yaani kuifanya ieleweke vizuri…yaani ikiwa na maana kuwa, Torati iliposema USIUE, Haikumaanisha tu kumkamata mtu na kuutoa uhai wake bali iliimanisha kwanza USIMCHUKIE KABISA NDUGU YAKO, Vivyo hivyo Torati iliposema USIZINI, Haikumaanisha tu kwenda kufanya zinaa ya nje, hapana bali ilimaanisha pia MTU HATAKIWI KUTAMANI KABISA NDANI YA MOYO WAKO. Kwahiyo unaweza ukaona hapo kutoka “kuzini” mpaka “kutokutamani” huko ni kukitimiliza kile kipengele kilichosalia..kwasababu Torati asili yake ni Rohoni.

Hivyo Daudi na watakatifu wa agano la kale walipokuwa wanaua hawakuwa wanafanya jambo lililosahihi, ingawa kwa wakati ule Bwana aliruhusu wafanye vile kwasababu wakati wa Utimilifu wa Torati, ulikuwa bado haujafika.

Kadhalika Daudi, na Sulemani mwanae, na watakatifu wote wa Agano la kale walipooa wake wengi, walikuwa hawafanyi jambo lililo sahihi machoni pa Bwana, ilikuwa sio mpango kamili wa Mungu wawe na wake na wengi, Lakini Bwana aliliruhusu waendelee kuoa wake wengi na kutoa talaka,hivyo hivyo mpaka UTIMILIFU utakapofika.

Watakatifu wa agano la kale, walikuwa wanaapa, lakini hayakuwa ni mapenzi ya Mungu mwanadamu yeyote aape, lakini Bwana aliwaruhusu waendelee kufanya hivyo mpaka wakati wa Utimilifu utakapofika. Na mara nyingine aliruhusu ifanyike hivyo kwasababu tu ya ugumu wa mioyo yao.

Ndipo wakati wa UTIMILIFU ulipofika, Mungu alimtuma mwanawe mpendwa Yesu Kristo ili kuhubiri UTIMILIFU wote WA TORATI.

Na ndio hapo Bwana Yesu alisema..

Mathayo 5:21 “Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue, na mtu akiua, itampasa hukumu.

22 Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto”.

Mathayo 5:27“Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; 28 lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake”.

Mathayo 5.33 “Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako;

34 lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu;

35 wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa Yerusalemu, kwa maana ndio mji wa Mfalme mkuu.

36 Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi.

37 Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu”

Mathayo 5:38“Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino;

39 Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili.”

Kaka/dada unayesoma haya, UMESIKIA kwamba imenenwa unaweza ukaokolewa tu, maadamu unatenda mema, na kuzishika amri 10 za Mungu, lakini Kristo anasema.. Mtu hawezi kuuona ufalme wa mbingu, asipozaliwa mara ya pili.

Na tena umesikia mahali wanasema ubatizo sio wa lazima, mbona hata Daudi hakubatizwa lakini Mungu alimkubali, Ndugu usiamini huo uongo leo KRISTO ANAKUAMBIA… “AAMINIYE NA KUBATIZWA ATAOKOKA ASIYEAMINI ATAHUKUMIWA” (Marko 16:15-16).

Umeona hapo? Anasema asiyeamini atahukumiwa, Ndugu yangu usipoamini na kubatizwa utahukumiwa, hayo ni maneno ya Mkuu wa Uzima mwenyewe YESU KRISTO, Na yeye hawezi kusema uongo.

Inawezekana mahali Fulani umesikia mtu Fulani akikuambia kwamba unatakiwa umfuate Yesu tu, kwa wepesi usijiweke rehani saana..Lakini yeye anakwambia leo

Luka 9:23-25 “..Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha. Kwa kuwa yamfaa nini mtu kuupata ulimwengu wote, kama akijiangamiza, au kujipoteza mwenyewe?.”

tena umesikia mahali pengine wakisema kuwa ni ruksa kuwa na wake wengi au waume wengi..lakini kristo mtimilifu wa torati anakuagiza leo maneno haya

Luka 19: 9 “nami nawaambia ninyi, kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini…..

7 wakamwambia, jinsi gani basi musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?

8 akawaambia, musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi”.

Tena umesikia dhehebu Fulani likisema, mtu akifa leo hupitia kwanza TOHARANI kutakaswa dhambi zake kisha atakwenda mbinguni, na wengine wanasema mtu akifa amekufa wala hakuna kiyama ya wafu. Lakini Bwana Yesu anasema “27 Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu;(Waebrania 9:27)”. Unaona? Usidanganyike ndugu kufanya ibada za wafu, au kuwaombea wafu, wala usidanganyike kuwa ukifa leo ni unapotea tu kama wale masadukayo walivyokuwa wanaamini. Fahamu kuwa ukishakufa wewe utakuwa ni wakusubiria hukumu aidha peponi au jehanum, Hivyo usikubali kusikiliza hadithi za kutungwa, zitakazokufanya ustarehe katika dhambi zako ukidhani kuwa kuna nafasi ya pili uko uendako, au kuna kupotea tu hakuna hukumu.

Ndugu, mtii YESU KRISTO leo, usiseme kwasababu Daudi alikuwa na wake wengi, basi na wewe ndio uwe na wake wengi, usiseme kwasababu Daudi hakubatizwa na wewe usiutafute ubatizo leo, usiseme kwasababu Daudi alikuwa anashindana na maadui zake na kuwaua na wewe leo ukatafute kuwaangamiza wale wanaokuchukia.. usifanye hivyo mtimilifu wetu yesu kristo ndiye anayetuagiza tusifanye hivyo. tusishindane na watu waovu, wala tusijilipize kisasi. sio kila njia ya watakatifu wa agano la kale ilikuwa ni kamilifu, mtazame YESU Kristo yeye ndiye njia na kweli na uzima. na ndiye aliyepakwa mafuta kutufundisha maneno ya uzima. huyu yesu kristo ndiye aliyefanyika bora kuliko wanadamu wote na malaika wote..na ndio maana ile sauti ilitoka mbinguni na kusema… “huyu ndiye mwanangu mpendwa wangu msikieni yeye”.

Waebrania 2: 1 “Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi,

2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika mwana [yesu kristo], aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.

3 yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa ukuu huko juu;

4 amefanyika bora kupita malaika, kwa kadiri jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao.”

Mwamini YESU uokolewe hizi ni saa za majeruhi.

ubarikiwe

tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine na mungu atakubariki.


Mada Nyinginezo:

UBATIZO SAHIHI

MVUTO WA TATU!

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.


Rudi Nyumbani

Print this post

NJAA IPO?, USIACHE KULA ASALI.

NJAA inaficha uchungu wa kitu, mtu mwenye njaa hata akipewa mboga iliyochungu kiasi gani, bado ataiona ni tamu tu, kwasababu NJAA ipo ndani yake, lakini kwake yeye aliyeshiba, hata chakula kiungwe kwa viungo vingi kiasi gani bado ataona tu kuna kasoro nyingi ndani yake..Ni kwasababu njaa haipo ndani yake.

Unaweza ukajiuliza ni kwanini Neno la Mungu linafananishwa na ASALI? Sababu ni hizi kwanza Asali ni kitu kitamu kuliko vyakula vyote na matunda yote, pili asali ni chakula kisichoharibika kinadumu milele, ni kitu kisichoisha ubora wake kwa mamilioni na mamilioni ya miaka ipo vile vile tofauti na kitu chochote kile kinachoweza kulika, Bwana anasema:

“Mwanangu, ule asali, kwa maana ni njema, Na sega la asali lililo tamu ulionjapo. 14 Basi utaijua hekima kuwa tamu kwa nafsi yako; Ikiwa umekwisha kuiona; Ndipo itakapofuata thawabu; Wala tumaini lako halitabatilika.” (Mithali 24: 13)”.

Lakini japo asali ni tamu kuliko vitu vyote kamwe hatuwezi kuuona utamu wake pale nafsi zetu zikiwa zimejikinai, tukijiona kuwa tunajua, tumefika, hakuna mtu anayeweza kutuongezea kitu cha ziada katika ukristo wetu ni dini zetu tu, tukijiona kuwa sisi ni bora kuliko wengine,

tunawadharau wengine wote, hatutaki kuwasikiliza wala kuwahudumia?, tunasema wale sio wa dhehebu letu, hivyo hatuwasikilizi hawana chochote cha kutuongezea, n.k. ..

Hapo hata kama tutalifahamu Neno la Mungu kwa wingi kiasi gani, hata kama tutakuwa na mafunuo mengi kiasi gani, hata kama tutahubiri mikutano mingi kiasi gani, hata kama tutawaombea wagonjwa wakapona kiasi gani..ULE UTAMU WA NENO LA MUNGU HATUTAUHISI KAMWE NDANI YETU.

Na ndio hapo mtu wa namna hiyo anaishia kuwa wa kidini tu, kama wale mafarisayo na masadukayo, walivyokuwa kipindi kile cha Yesu. Walimwona Bwana kama mtu asiyekuwa na dini, wala elimu, walimwona Bwana kama mtu mwenye pepo, walimwona Bwana kama mwana wa Seremala maskini tu asiyejua kitu, , hivyo pale alipokuja na Neno la Uzima kutoka kwa Mungu, walimdharau japo waliufahamu kuwa anachosema ni ukweli lakini kwa kuwa waliridhika tu na dini zao na mapokeo yao, walikuwa wameshiba nafsini mwao, wakaupinga wokovu…..kwani hekima inasema:

“Nafsi iliyoshiba hukinai sega la asali; Bali nafsi yenye njaa huona kila kitu kichungu kuwa kitamu.” (Mithali27:7).

Embu leo hii, turuhusu nafsi zetu ziwe na NJAA kwa ajili HAKI na KWELI ya Neno la Mungu Ili endapo maagizo yanayoonekana kuwa ni magumu yatokayo katika Neno la Mungu yatakapokuja mbele yetu tuyaone kuwa ni matamu hata kama yataonekana kuwa ni machungu kwa watu wengine, walioshiba. Pale biblia inapotuagiza mara baada ya kuamini kwetu tukabatizwe kwa kuzamishwa katika maji tele,na katika jina la YESU basi sisi tuwe wepesi wa kutii,maadamu nafsi zetu zina njaa ya haki, hata kama tutaona kisima, au mto au bahari vipo mbali nasi basi tufanye hivyo tu kwasababu Roho zetu zina njaa..Tufanye kama yule Mkushi aliyehitaji kubatizwa akiwa njiani, katika safari yake.

Matendo 8: 35 “Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.

36 Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?

37 Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]

38 Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza”.

Tusifanane na hao walioshiba, wameshakinai sega la asali ambao pamoja na elimu zao kubwa za dini wakilijua hilo wamelipuuzia kama jambo lisilo na umuhimu sana.

(Luka 6:21 Heri ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashiba.)

Pale biblia inapotuonya tuvae mavazi ya kujisitiri, na tusivae mavazi yaipasayo jinsia tofauti (kumb 22:5). Basi tuone kuwa hicho ni chakula kitamu kwa kutii haraka sana, kwa kwenda kutupa vimini, na suruali, na kaptura ambazo ni za jinsia tofauti na za kwetu [wanawake]. Sisi tusifanane na hao walioshiba wanaosema Mungu haangalii mavazi bali roho, tukiwaacha wale waliojikinai wanaosema tunaishi chini ya neema na wala sio sheria..Sisi tuziache tu nafsi zetu ziwe na njaa..ndipo tutakapoliona Neno la Mungu ni tamu kwetu.

Tuwe kama Daudi, anasema “MAUSIA YAKO NI MATAMU SANA KWANGU, KUPITA ASALI KINYWANI MWANGU Zaburi 119:103.”

Pale biblia inapotuonya tusiabudu sanamu wala mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni wala chini duniani, basi moja kwa moja tusijione kuwa dini zetu ni bora kuliko Neno la Mungu, tusione kuwa viongozi wetu wa dini ni bora kuliko Neno la Mungu, tusione kuwa dhehebu letu ni zaidi ya Neno la Mungu na kupuuzia, na kuzidi kuabudu sanamu za wafu na kuzifanyia ibada na kusali rozari za kipagani vitu ambavyo Neno limekataza. Sisi tutii tu hata kama dini zetu zinatukemea. Kwasababu tunataka kwenda mbinguni.

Mathayo 5:6 “Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa.”

Tule asali sana maadamu tuna njaa, lakini ole wetu endapo tumeshiba, kwani ni jambo gani litakalotuburudisha lenye utamu zaidi ya asali?.

Dumu katika Neno la Mungu.

Ubarikiwe DAIMA wewe umtafutaye BWANA.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

UBATILI.

WANA WA MAJOKA.

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI

MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA


Rudi Nyumbani

Print this post

UNAMFAHAMU MUNGU WA KWELI?

Mwanzo Bwana alipowatoa wana wa Israeli katika nchi ya Misri, hakuwakuta ni wakamilifu kwa asilimia zote kama anavyotaka yeye, kwasababu kule Misri walipokuwepo hakukuwa na utaratibu wowote wa kumwabudu Mungu wa kweli, na wala wana wa Israeli walikuwa hawamjui kwa kina Mungu wa Ibrahimu, walikuwa wanayo kama historia vichwani mwao kuwa kipindi Fulani nyuma Mungu alimtokea Baba yao Ibrahimu na kumpa maneno mengi ya Ahadi, walisikia tu kipindi Fulani Mungu, aliipiga dunia kwa njaa lakini alimfunulia Yusufu aliyekuwa mwisraeli kama wao juu ya majanga hayo  yatakayokuja..hawakumjua sana kwa undani, Mungu wao ni Mungu wa namna gani…Walimjua tu ni Mungu hodari na atakayekuja kuwaokoa katika matatizo yao basi.

Na kwa jinsi walivyokuwa wanaendelea kukaa katika nchi ya Misri, pasipo kumsikia kwa vizazi vingi,  kidogo kidogo walianza kumdhania Mungu wa Yakobo ni  kama miungu ya kimisri,  walidhani kwamba Mungu wa Yakobo baba yao anaweza akatengenezewa mfano wa kinyago Fulani kama wa-Misri wanavyoifanyia miungu yao. Waliona kwasababu wa-Misri wanatolea dhabihu sanamu zao huku wanaendelea na roho zao mbaya, na bado wanapata mvua nakufanikiwa wakajua na Mungu wa Yakobo yuko hivyo hivyo, wanaweza wakamtolea dhabihu, na sadaka lakini maisha yao yakaendelea kuwa vile vile, wakaendelea kuwa na kiburi chao, matusi yao, malalamiko yao, uuaji wao, n.k.

Hivyo kwasababu waliishi na Wa-Misri kwa muda mrefu, kwa zaidi ya miaka 400, ule utamaduni au ule mfumo wa kuabudu walioutumia wa-Misri, uliwaingia na wao pia kudhani kuwa Mungu wa Israeli naye anaabudiwa kama inavyoabudiwa miungu ya kimisri..

Hata katika maisha ni kawaida kuona mazingira Fulani yakiwaathiri watu Fulani na kudhani watu wote wako kama wao. Utakuta  kwamfano familia Fulani ina utaratifu wa kukaa pamoja, na kula pamoja mezani..lakini mmoja wa familia hiyo anatoka na kwenda kutembelea familia nyingine na kutazamia kuikuta familia ile ipo kama ya kwao, badala yake anakuta kila mtu yupo kivyake, baba na mama hawaongei, kila mtu na ratiba zake..lazima itamshangaza kidogo kwasababu amekuta kitu asichokitegemea..

Ndivyo ilivyokuwa kwa Wana wa Israeli, Bwana Mungu wakati anakuja kuwatoa ilikuwa ni shida sana wao kumwelewa na ndio maana tunaona Bwana Mungu aliwapitisha kwanza jangwani kabla ya kuwaingiza nchi ya Ahadi ili awafundishe yeye ni nani, na anataka nini kutoka kwao.

Utaona baada tu ya kutolewa nchi ya Misri, pamoja na kufanyiwa miujiza yote ile, wakaanza kunung’unika na kulalamika, ni kwasababu gani walikuwa wanafanya vile? Ni kwasababu walikuwa hawamjui bado Mungu wa Israeli kuwa hapendi watu wanaonungu’unika, wao walidhani Mungu wa Israeli ni kama miungu ya kimisri ambayo ukiinung’unikia tu haiwezi kufanya lolote, walidhani ni kama ile miungu ya kimisri ambayo ukiilalamikia na kuitukana haikufanyi chochote.

Na ukiendelea mbele zaidi utaona wana wa Israeli wanaanza kufikiria kutengeneza ndama ya kusubu ili iwarudishe Misri, ni kwanini walifanya vile? ni kwasababu walidhani Mungu wa Israeli ni kama miungu ya kimisri, kwamba inafika mahali inashindwa kufanya jambo Fulani, na hivyo kuitafutia njia mbadala.

Na mambo mengine mengi, waliyoyafanya wana wa Israeli yaliyomkasirisha Mungu yalitokana na kutomjua Mungu wa YAKOBO ni nani? Yalitokana na kumdhania Mungu wa Baba yao Ibrahimu ni mfano wa mmojawapo wa miungu ya Misri, isipokuwa yeye ana nguvu kidogo kipita yao.

Kwasababu hiyo basi iliwachukua muda mrefu sana kumjua Mungu wa Israeli ni nani..Mpaka Bwana alipoanza kuwapa sheria ndio kidogo kidogo ndipo Alipoanza kuwaambia yeye ni MUNGU  MMOJA, na hakuna mwingine zaidi yake wala wa kufananishwa na yeye, hivyo wasiwe na miungu mingine ya kando ila yeye peke yake. ALIPOANZA KUWAAMBIA YEYE NI MUNGU MTAKATIFU NA HIVYO ANAWATAKA NA WAO WAWE WATAKATIFU KAMA YEYE ALIVYO..

Walawi 11: 45 “Kwa kuwa mimi ni Bwana niliyewaleta kutoka nchi ya Misri, ili kwamba niwe Mungu wenu; BASI MTAKUWA WATAKATIFU, KWA KUWA MIMI NI MTAKATIFU”. 

Ndipo walipoanza kumwelewa Mungu kuwa sio kama miungu ya Misri waliyoizoea kwamba unaweza ukaitumikia na bado ukaendelea kuwa mwizi, unaweza ukaitolea dhabihu na bado ukaendelea kuwa mnung’unikaji, unaweza ukaitumikia na bado ukaendelea kuwa muuaji au mwizi unaweza ukaiabudu na  kuiimbia na bado ukaendelea kuilalamikia, unaweza ukaifuata na bado ukaendelea kuwa mzinzi, au mlaji rushwa, au mtu mwenye chuki, kwamba unaweza ukawa na miungu mingine midogo midogo mingi ya pembeni ya kukusaidia pale Mungu mkubwa anapokwama,   n.k ndipo walipojua kuwa Mungu wa Israeli sio kama walivyokuwa wanamdhania kama miungu ya Misri waliyoizoea Ndipo walipomwelewa vizuri Mungu wa Israeli ni Mungu mtakatifu sana  na hana msaidizi na yupo mmoja,Iliwachukua miaka zaidi ya 40 kumwelewa vizuri Mungu wa Israeli..

Na baada akili zao kubadilishwa kumjua Mungu wa kweli ni Mungu wa namna gani, ndipo wakaweza kutembea na Mungu.

Kaka/Dada unayesoma haya..swali ni lile lile   “Je! Unamjua Mungu wa kweli??” Kumbuka unaposema umetoka kwenye dhambi ni sawa na Bwana kakutoa nchi ya Misri ambayo ulikuwa ni mtumwa wa dhambi? Lakini je! Baada ya kutoka huko umemfahamu Mungu unayemtumikia?? Au unamchukulia Mungu, kama ile miungu uliyokuwa unaiabudu kabla ya kumpokea yeye??…

Biblia inasema katika agano jipya pia..

1 PERTO 1: 13 “kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake yesu kristo.

14 kama watoto wa kutii msijifananishe NA TAMAA ZENU ZA KWANZA ZA UJINGA WENU;

15 bali kama yeye ALIYEWAITA ALIVYO MTAKATIFU, NINYI NANYI IWENI WATAKATIFU KATIKA MWENENDO WENU WOTE;

16 kwa maana imeandikwa, MTAKUWA WATAKATIFU KWA KUWA MIMI NI MTAKATIFU.

17 na ikiwa mnamwita baba, yeye ahukumuye kila mtu pasipo upendeleo, kwa kadiri ya kazi yake, enendeni kwa hofu katika wakati wenu wa kukaa hapa kama wageni”.

Huwezi ukasema umetolewa katika utumwa wa dhambi na bado unasujudia sanamu, huwezi ukasema umetolewa katika utumwa wa dhambi na bado ukawa mwasherati, au mlevi, au mtukanaji…Huwezi ukasema umeokolewa kutoka katika utumwa wa dhambi na bado unavaa nguo zinazoonyesha maungo yako, unavaa nguzo zinazo kubana, unavalia vimini, suruali na kupaka wanja..Hizo zote ni tamaduni za miungu ya ki-Misri na huwezi kumtumikia Mungu wa kweli kwa tamaduni za ki-Misri.

Ndugu yangu kama unataka kwenda na Bwana, mtii anayokuambia leo, Geuka upate ufahamu, usidanganyike kwamba Mungu anaangalia roho haangalii mwili, usidanganyike kwamba wanaopaka lipstick,na wanja na wanaovaa hereni, na wigi wataingia mbinguni..Usidanganyike kuwa wanaofanya masturbation, na wanaotazama pornography, na wanaoishi na wanawake/wanaume ambao hawajaoana kuwa wataingia mbinguni, usidanganyike kuwa ukiwa vuguvugu, nusu Mungu nusu ulimwengu, utaingia mbinguni.. Bwana anasema mwenyewe kuwa ATAKUTAPIKA!!  Kwasababu yeye ni mtakatifu na hivyo tutakuwa watakatifu kama yeye alivyo..

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, AMBAO HAPANA MTU ATAKAYEMWONA BWANA ASIPOKUWA NAO;”

Ni maombi yangu kuwa utamjua Mungu wa kweli ni nani, kama hujamjua na utachukua uamuzi thabiti wa kumfuata yeye kwa viwango anavyotaka yeye vya UTAKATIFU. Na kama hujabatizwa nakushauri ufanye hivyo mapema, kwasababu ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi, na kwa Jina la Yesu  ni wa muhimu sana, katika kuikamilisha safari yako ya wokovu.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali “Share” ujumbe huu kwa wengine na Bwana atakubariki.


Mada Nyinginezo:

TAWI LIZAALO HULISAFISHA ILI LIZIDI KUZAA.

NGUVU YA MUNGU YA UUMBAJI

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.

MNGOJEE BWANA


Rudi Nyumbani

Print this post

MAMBO YATAKAYOTOKEA ISRAELI SIKU ZA HIVI KARIBUNI.

Ishara kubwa Bwana Yesu aliyowapa wanafunzi wake ambayo kwa hiyo waliambiwa watakapoiona basi wajue kuwa “muda wa mavuno umekaribia” ni ishara ya MTINI. tukisoma

Mathayo 24:32 inasema “Basi KWA MTINI JIFUNZENI mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu;

33 nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni.

Na tunajua kuwa “mtini” alioumaanisha hapo si mwingine zaidi zaidi ya TAIFA LA ISRAELI (Yeremia 24), Ikiwa na maana kuwa tutakapoona taifa la Israeli linaanza kuchipua na kuchanua tena, basi majira ya mwisho wa dunia yamekaribia sana. Kumbuka Mungu katika mpango wake wa wokovu alianza na Israeli na katika kutimiliza atatimiliza na taifa hilo hilo, kwasababu makao ya MFALME YESU atakapokuja kwa mara ya pili kuutawala huu ulimwengu mzima katika nchi ya wenye haki, hayatakuwa katika mojawapo ya nchi hizi za mataifa tulizopo sisi na zitakazokuwepo huko hapana, bali makao yake yake makuu yatakuwa pale Israeli nchi takatifu. Alishuka hapo mara ya kwanza, atashuka hapo hapo mara ya pili. Hivyo ni lazima kwanza pale patakaswe kisha mataifa mengine yafuate kabla ya yeye kuteremka ulimwenguni.

Hivyo Mungu akishamaliza kupatakasa Israeli, ndipo atakapoitumia Israeli kuitakasa dunia nzima kwa fimbo yake. Na ndio maana Mungu alisema hivi juu ya Israeli. 

Yeremia 51:20 “ WEWE U RUNGU LANGU NA SILAHA ZANGU ZA VITA; kwa wewe nitawavunja-vunja mataifa; na kwa wewe nitaharibu falme;

21 na kwa wewe nitamvunja-vunja farasi, na yeye ampandaye; na kwa wewe nitalivunja-vunja gari la vita, na yeye achukuliwaye ndani yake;

22 na kwa wewe nitawavunja-vunja mwanamume na mwanamke; na kwa wewe nitawavunja-vunja mzee na mtoto; na kwa wewe nitawavunja-vunja kijana mwanamume na kijana mwanamke;

23 na kwa wewe nitamvunja-vunja mchungaji na kundi lake; na kwa wewe nitamvunja-vunja mkulima na jozi yake ya ng’ombe; na kwa wewe nitawavunja-vunja maliwali na maakida.”

Unaona?. Sasa kulingana na unabii wa kibiblia katika hatua tuliyopo sasa tunatazamia kushuhudia VITA KUU MBILI KUBWA zitakazopiganwa pale Israeli kabla ya mambo yote kuisha. Vita ya kwanza ni ile inayozungumziwa katika Ezekieli 38-39, ambayo ndio itakayofuata muda mfupi ujao Na vita ya pili ni ile ya HAR-MAGEDONI (Ufunuo 16:16), hiyo itakayokuja kuhitimisha utawala mbovu wa huu ulimwengu, inajulikana kama vita ya Mungu mwenyezi.

VITA YA ULIYOZUNGUMZIWA KATIKA EZEKIELI 38-39.

Siku zote Mungu kabla hajafanya jambo kubwa litakaloleta madhara huwa anatanguliza kwanza madogo madogo ili kuwakumbusha watu wachukue tahadhara kwani makubwa zaidi ya hayo yanakuja mbeleni. Na ndio maana Bwana Yesu alisema, kutakuwa na vita, na tetesi za vita, kutakuwa na njaa na matetemeko ya ardhi, hayo yote ni MWANZO WA UTUNGU, Unaona Hapo utungu wenyewe bado haujafika. Ukifika inamaanisha maafa yatakuwa makubwa zaidi kuliko haya tuyaonayo. Na ukitazama kwa ukaribu haya matetemeko ya ardhi tunayoyaona ulimwenguni na kusema ni makubwa, yanayoangamiza maelfu haya yote si kitu, Yapo matetemeko hasa yatakayokuja siku ile ya mwisho hii dunia itakapoikiswa pale visiwa na milima vitakapohama kwa nguvu ya tetemeko la ardhi ambalo Mungu atalileta mwenyewe duniani kote, na mvua ya mawe makubwa sana ambayo haijawahi kunyesha tangu ulimwengu kuumbwa, hapo ndipo wanadamu wote waliosalia wakati huo watalia na kuomba milima iwaangukie wajisitiri mbali na hasira ya Mungu. Ni mambo ya kutisha sana.

Ufunuo 6.12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,

13 na nyota zikaanguka juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi.

14 Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake.

15 Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,

16 wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo.

17 Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama?”

Vivyo hivyo na kwenye suala la magonjwa na vita. Magonjwa yaliyopo leo yanatabika na homa zake ni za wastani, kadhalika na yanapatikana maeneo Fulani Fulani tu sio kila mahali haya yote ni mwanzo wa utungu,lakini yale yatakayoletwa na Mungu katika siku ile ya ghadhabu ya hasira yake, biblia inasema kutakuwa na jipu baya na bovu juu ya watu wote ulimwenguni walioipokea ile chapa ya mnyama. Jaribu kufikiri ukimwi na kansa,au ebola ni magonjwa yanayoogopeka, Lakini biblia hayajayaona hayo, mpaka kulizungumzia hili jipu bovu tu lenyewe…ni baya kiasi gani mpaka wanadamu watamtukana Mungu kwa maumivu ya ugonjwa huo. Sio kutamani kuwepo huko ndugu.

Sasa tukirudi kwenye suala la vita. Leo Tunaweza kushuhudia vita ya kwanza na vya pili vya dunia vilivyoua watu zaidi ya watu milioni 80, huo ni mwanzo tu wa utungu, na lakini ipo vita itakayopiganwa siku za mwisho ambayo ndio ile ya mwisho inayojulikana kama HAR-MAGEDONI. Watu watakaouawa ni idadi kubwa mito ya damu itabubujika Israeli kwa wingi wa watu watakaouawa.

Sasa tuitazame Israeli kama jinsi ilivyofananishwa na mtini kuchipuka kwake, ambako kulikuwa ni mwaka 1948.

Tunaona kuwa tangu huo wakati Israeli ilipokuwa Taifa huru tena, mvutano mkubwa ulianza kujitokeza mashariki ya kati na duniani kote kwa ujumla. Nchi za kiharabu zikiigombani Israeli na mataifa mengine yakizisapoti.Mpaka kupeleka Israeli kuwa na maadui wengi pande zake zote. Watu wasifahamu kuwa jambo hilo linatoka kwa Bwana mwenyewe ili kuonyesha kuwa moja ya hizi siku mataifa yote yatahukumiwa na rungu la Bwana Israeli.

Hiyo Iliendelea hivyo hivyo mpaka kupelekea mwaka 1967 mataifa yote ya urabuni yakiongozwa na Syria kujikusanya kwa ajili ya kuipoteza Israeli katika ramani ya dunia. Lakini jambo hilo kama tunavyosoma katika historia, Israeli ilizipiga silaha zao za vita na vita kuisha ndani ya siku 6 tu. Kupeleka mpaka Israeli kuteka sehemu ya kubwa ya taifa lake ambalo hapo kabla lilikuwa haliyamiliki pamoja na nchi za kando kando.

Sasa hayo nayo ni mwanzo wa utungu ili kutupa sisi picha ya mambo yatakayokuja kutoka siku za hivi karibuni. Hii ilikuwa ni mataifa ya uarabuni lakini siku zinakuja mataifa yote ulimwenguni yataungana kwenda kupigana na Israeli hiyo ndiyo vita ya Har-magedoni.

Hivyo tukisoma kitabu cha Ezekieli 28-39, tunaona vita nyingine hapa ukiwa na muda wako mwenyewe unaweza kusoma sura zote mbili upate kuiona habari nzima ni vita ambayo itapiganwa tena kipindi hichi karibu na unyakuo kutokea. Embu Tusome mistari michache tu ya mwanzo.

Ezekieli 38

EZEKIELI: MLANGO 38

1 Neno la Bwana likanijia, kusema,

2 Mwanadamu, kaza uso wako, umwelekee Gogu, wa nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki, na Tubali, ukatabiri juu yake,

3 useme, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ewe Gogu, mkuu wa Roshi, na Mesheki, na Tubali;

4 nami nitakugeuza na kutia kulabu katika mataya yako, nami nitakutoa, pamoja na jeshi lako lote, farasi na hao wapandao farasi, wote wamevaa silaha za namna zote, jeshi kubwa sana, wenye ngao na kigao, wote wakishika upanga;

5 Uajemi, na Kushi, na Putu, pamoja nao; wote wana ngao na chapeo;

6 Gomeri, na vikosi vyake vyote; nyumba ya Togarma, pande za mwisho za kaskazini, na vikosi vyake vyote; naam, watu wengi pamoja nawe.

7 Ujiweke tayari, naam, jiweke tayari, wewe na majeshi yako yote waliokukusanyikia, nawe uwe jemadari wao.

8 NA BAADA YA SIKU NYINGI UTAJILIWA; KATIKA MIAKA YA MWISHO, UTAINGIA NCHI ILIYORUDISHIWA HALI YAKE YA KWANZA, BAADA YA KUPIGWA KWA UPANGA, ILIYOKUSANYWA TOKA KABILA NYINGI ZA WATU, juu ya milima ya Israeli, iliyokuwa ukiwa wa daima; lakini imetolewa katika kabila za watu, nao watakaa salama salimini wote pia.

9 Nawe utapaa juu, utakuja kama tufani, utakuwa kama wingu kuifunika nchi, wewe, na vikosi vyako vyote, na kabila nyingi za watu pamoja nawe.

10 BWANA MUNGU ASEMA HIVI; ITAKUWA KATIKA SIKU HIYO, MAWAZO YATAINGIA MOYONI MWAKO, NAWE UTAKUSUDIA KUSUDI BAYA;

11 nawe utasema, Nitapanda juu niiendee nchi yenye vijiji visivyo na maboma; nitawaendea watu wanaostarehe, wanaokaa salama, wote wakikaa pasipo kuta, ambao hawana makomeo wala malango;

12 ili kuteka mateka, na kuwinda mawindo; uugeuze mkono wako juu ya mahali palipoharibika, ambapo sasa panakaliwa na watu, na juu ya watu waliokusanyika toka mataifa, waliopata ng’ombe na mali, wakaao katikati ya dunia.

13 Sheba, na Dedani, na wafanya biashara wa Tarshishi, pamoja na wana-simba wake wote, watakuambia, Je! Umekuja kuteka mateka? Umekusanya jeshi lako, ili kuwinda mawindo? Kuchukua fedha na dhahabu, kuchukua ng’ombe na mali, kuteka mateka mengi sana?

14 Basi, mwanadamu, tabiri, umwambie Gogu, Bwana MUNGU asema hivi; Katika siku ile watu wangu, Israeli, watakapokaa salama, hutapata habari?

15 Nawe utakuja kutoka mahali pako, kutoka pande za mwisho za kaskazini, wewe, na watu wa kabila nyingi pamoja nawe, wote wamepanda farasi, kusanyiko kubwa, na jeshi kuu;

16 NAWE UTAPANDA JUU UWAJILIE WATU WANGU, ISRAELI, KAMA WINGU KUIFUNIKA NCHI; ITAKUWA KATIKA SIKU ZA MWISHO, NITAKULETA UPIGANE NA NCHI YANGU, ILI MATAIFA WANIJUE, nitakapotakaswa kwako, Ewe Gogu, mbele ya macho yao.

17 Bwana MUNGU asema hivi; Je! Wewe ndiwe niliyemnena zamani za kale, kwa vinywa vya watumishi wangu, manabii wa Israeli, waliotabiri siku zile kwa muda wa miaka mingi, ya kwamba nitakuleta upigane nao?

18 Itakuwa katika siku hiyo, Gogu atakapokuja kupigana na nchi ya Israeli, asema Bwana MUNGU, ghadhabu yangu itapanda katika mianzi ya pua yangu.

19 Kwa maana katika wivu wangu, na katika moto wa ghadhabu yangu, nimenena, Hakika katika siku ile kutakuwako tetemeko kubwa katika nchi ya Israeli;

20 hata samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama wa kondeni, na vitu vyote vitambaavyo juu ya nchi, na wanadamu wote walio juu ya uso wa nchi, watatetemeka mbele ya uso wangu; nayo milima itatupwa chini, na magenge yataanguka, na kila ukuta utaanguka chini.

21 Nami nitaita upanga, uje juu yake katika milima yangu yote, asema Bwana MUNGU; nao upanga wa kila mtu utakuwa juu ya ndugu yake.

22 Nami nitamhukumu kwa tauni, na kwa damu; nami nitanyesha mvua ifurikayo, na mvua ya mawe makubwa sana, na moto na kiberiti juu yake, na vikosi vyake, na watu wa kabila nyingi walio pamoja naye.

23 Nami nitajitukuza, na kujitakasa, na kujidhihirisha, mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana”.

Sasa Nchi ya Magogu, biblia inayoitaja hapo ni eneo linalojulikana kama URUSI kwasasa. Hivyo nchi hii leo tunaoina ni nchi yenye nguvu sana kiasi kwamba inalitishia hata taifa la Marekani kwa nguvu zake na ukuu wake. Lakini biblia inasema siku moja mawazo yataliingia hili taifa ili kwenda kuishambulia Israeli. Na kibaya zaidi halitashuka peke yake, hapana bali litashuka na majeshi ya mataifa mengine mengi kama tunavyoyasoma hapo juu. Na mengi ya hayo yatakuwa na haya mataifa ya kiharabu, ambayo hayo kimsingi ni maadui wa Israeli tangu zamani, pamoja na nchi nyingi zilizokando kando ya Urusi.

Wote watapanga vita kuiendea ile nchi ndogo sana Israeli. Kama tunavyoona hata sasa Taifa linaloongoza kuwa na maadui wengi duniani ni taifa la Israeli, hivyo Urusi kwa kujipendekeza na kujionyesha kuwa yeye anayo nguvu na kwamba anaweza kuwasaidia watu waliwashindwa ISRAELI. Yeye naye siku hiyo atapanga vita na mabomu yake ya Atomiki ili kwenda kulisambaratisha taifa lile. Hawajui kuwa hapo ndipo Mungu alipokusudia uwe mwisho wa mataifa hayo yote chini ya jua. Siku hiyo Urusi itapotezwa kwenye ramani ya dunia, kwasababu Bwana atakuwa upande wa Israeli. Na wa-Rusi siku hiyo watasoma maandiko haya ya Ezekieli na kutambua kuwa unabii huo ulikuwa unawahusu wao.

Kumbuka vita hiyo japo itauwa watu wengi sana kiasi kwamba biblia inasema mizoga yao itakuwa inazikwa kwa muda wa miezi 7 ikikusanywa tu, na silaha zao zitakuwa zikitumika kama kuni kwa muda wa miaka 7, lakini huo utakuwa ni mwanzo tu wa utungu. Vita yenyewe kuu bado. Vita ya Har-magedoni ambayo itahusisha mataifa yote ulimwenguni.

Tutakuja kuizungumzia vizuri vita hii [Har-Magedoni] katika makala nyingine. Lakini tufahamu kuwa vita inayozungumziwa katika Ezekieli 38-39 ipo mbioni kutokea, kama tunavyoona sasahivi mvutano ulivyo mkubwa mashariki ya kati na ishara kuwa vita vinajiandaa kupiganwa muda wowote. Hivyo ndivyo Mungu anavyozidi kuitasa Israeli kidogo kidogo, Na ndivyo pia wanavyojiandaa kumpokea Masiya wao.

Swali tujiulize wakati sasahivi neema inarudi Israeli, mimi na wewe mpaka mambo hayo yatakapotokea tutakuwa wapi? Kumbuka ndugu tuliambiwa tukiyaona hayo yanaanza kutokea basi tunyanyue vichwa vyetu, kwa kuwa ukombozi wetu umekaribia. Ikiwa na maana UNYAKUO wetu upo karibu.

Kristo yupo mlangoni ndugu. Unasubiri nini usiufanye leo wito wako na uteule wako imara?. Walioishi kipindi chote cha nyuma kuanzia miaka ya 1900 kurudi nyuma mpaka kipindi cha kanisa la kwanza hawakukishuhudia kitu hichi sisi tunachokishuhudia leo yaani taifa huru la Israeli. Na biblia ilishasema kizazi hiki hakitapita, sasa unasubiri nini usiushindanie wokovu katika muda huu mfupi uliobaki?.

Ungependa mambo hayo yakukute kwa ghafla, Bwana amesema dunia hii itaangamizwa kwasababu ya maovu yake. Na wenye haki watapata kwa Mungu waepushwe nayo.. je! Na wewe ungependa uwe miongoni mwa watakaoharibiwa katika ile siku ya Bwana? Kama sivyo mgeukie Kristo, ambaye yeye ndio safina pekee iliyothibitishwa na Mbingu kwa wokovu wa mwanadamu.

Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Print this post

MAMBO YATAKAYOTOKEA ISRAELI SIKU ZA HIVI KARIBUNI.

Ishara kubwa Bwana Yesu aliyowapa wanafunzi wake ambayo kwa hiyo waliambiwa watakapoiona basi wajue kuwa “muda wa mavuno umekaribia” ni ishara ya MTINI. tukisoma Mathayo 24:32 inasema “Basi KWA MTINI JIFUNZENI mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu;

24.33 nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni.

Na tunajua kuwa “mtini” alioumaanisha hapo si mwingine zaidi, zaidi ya TAIFA LA ISRAELI (Yeremia 24), Ikiwa na maana kuwa tutakapoona taifa la Israeli linaanza kuchipua na kuchanua tena, basi majira ya mwisho wa dunia yamekaribia sana. Kumbuka Mungu katika mpango wake wa wokovu alianza na Israeli na katika kutimiliza atatimiliza na taifa hilo hilo, kwasababu makao ya MFALME YESU atakapokuja kwa mara ya pili kuutawala huu ulimwengu mzima katika nchi ya wenye haki, hayatakuwa katika mojawapo ya nchi hizi za mataifa tulizopo sisi na zitakazokuwepo huko hapana, bali makao yake yake makuu yatakuwa pale Israeli nchi takatifu. Alishuka hapo mara ya kwanza, atashuka hapo hapo mara ya pili. Hivyo ni lazima kwanza pale patakaswe kisha mataifa mengine yafuate kabla ya yeye kuteremka ulimwenguni.

Hivyo Mungu akishamaliza kupatakasa Israeli, ndipo atakapoitumia Israeli kuitakasa dunia nzima kwa fimbo yake. Na ndio maana Mungu alisema hivi juu ya Israeli. 

Yeremia 51:20 “ WEWE U RUNGU LANGU NA SILAHA ZANGU ZA VITA; kwa wewe nitawavunja-vunja mataifa; na kwa wewe nitaharibu falme;

21 na kwa wewe nitamvunja-vunja farasi, na yeye ampandaye; na kwa wewe nitalivunja-vunja gari la vita, na yeye achukuliwaye ndani yake;

22 na kwa wewe nitawavunja-vunja mwanamume na mwanamke; na kwa wewe nitawavunja-vunja mzee na mtoto; na kwa wewe nitawavunja-vunja kijana mwanamume na kijana mwanamke;

23 na kwa wewe nitamvunja-vunja mchungaji na kundi lake; na kwa wewe nitamvunja-vunja mkulima na jozi yake ya ng’ombe; na kwa wewe nitawavunja-vunja maliwali na maakida.”

Unaona?. Sasa kulingana na unabii wa kibiblia katika hatua tuliyopo sasa tunatazamia kushuhudia VITA KUU MBILI KUBWA zitakazopiganwa pale Israeli kabla ya mambo yote kuisha. Vita ya kwanza ni ile inayozungumziwa katika Ezekieli 38-39, ambayo ndio itakayofuata muda mfupi ujao Na vita ya pili ni ile ya HAR-MAGEDONI (Ufunuo 16:16), hiyo itakayokuja kuhitimisha utawala mbovu wa huu ulimwengu, unajulikana kama vita ya Mungu mwenyezi.

VITA YA ULIYOZUNGUMZIWA KATIKA EZEKIELI 38-39.

Siku zote Mungu kabla hajafanya jambo kubwa litakaloleta madhara huwa anatanguliza kwanza madogo madogo ili kuwakumbusha watu wachukue tahadhara kwani makubwa zaidi ya hayo yanakuja mbeleni. Na ndio maana Bwana Yesu alisema, kutakuwa na vita, na tetesi za vita, kutakuwa na njaa na matetemeko ya ardhi, hayo yote ni MWANZO WA UTUNGU, Unaona Hapo utungu wenyewe bado haujafika. Ukifika inamaanisha maafa yatakuwa makubwa zaidi kuliko haya tuyaonayo. Na ukitazama kwa ukaribu haya matetemeko ya ardhi tunayoyaona ulimwenguni na kusema ni makubwa, yanayoangamiza maelfu haya yote si kitu, Yapo matetemeko hasa yatakayokuja siku ile ya mwisho hii dunia itakapotikiswa pale visiwa na milima vitakapohama kwa nguvu ya tetemeko la ardhi ambalo Mungu atalileta mwenyewe duniani kote, na mvua ya mawe makubwa sana ambayo haijawahi kunyesha tangu ulimwengu kuumbwa, hapo ndipo wanadamu wote waliosalia wakati huo watalia na kuomba milima iwaangukie wajisitiri mbali na hasira ya Mungu. Ni mambo ya kutisha sana.

Ufunuo 6.12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,

13 na nyota zikaanguka juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi.

14 Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake.

15 Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,

16 wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo.

17 Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama?”

Vivyo hivyo na kwenye suala la magonjwa na vita. Magonjwa yaliyopo leo yanatabika na homa zake ni za wastani, kadhalika na yanapatikana maeneo Fulani Fulani tu sio kila mahali haya yote ni mwanzo wa utungu,lakini yale yatakayoletwa na Mungu katika siku ile ya ghadhabu ya hasira yake, biblia inasema kutakuwa na jipu baya na bovu juu ya watu wote ulimwenguni walioipokea ile chapa ya mnyama. Jaribu kufikiri ukimwi na kansa, au ebola ni magonjwa yanayoogopeka, Lakini biblia haijayaona hayo, mpaka kulizungumzia hili jipu bovu tu lenyewe…ni baya kiasi gani mpaka wanadamu watamtukana Mungu kwa maumivu ya ugonjwa huo. Sio kutamani kuwepo huko ndugu.

Sasa tukirudi kwenye suala la vita. Leo Tunaweza kushuhudia vita ya kwanza na vya pili vya dunia vilivyoua watu zaidi ya watu milioni 80, huo ni mwanzo tu wa utungu, na lakini ipo vita itakayopiganwa siku za mwisho ambayo ndio ile ya mwisho inayojulikana kama HAR-MAGEDONI. Watu watakaouawa ni idadi kubwa mito ya damu itabubujika Israeli kwa wingi wa watu watakaouawa.

Sasa tuitazame Israeli kama jinsi ilivyofananishwa na mtini kuchipuka kwake, ambako kulikuwa ni mwaka 1948.

Tunaona kuwa tangu huo wakati Israeli ilipokuwa Taifa huru tena, mvutano mkubwa ulianza kujitokeza mashariki ya kati na duniani kote kwa ujumla. Nchi za kiharabu zikiigombania Israeli na mataifa mengine yakizisapoti.Mpaka kupeleka Israeli kuwa na maadui wengi pande zake zote. Watu wasifahamu kuwa jambo hilo linatoka kwa Bwana mwenyewe ili kuonyesha kuwa moja ya hizi siku mataifa yote yatahukumiwa na rungu la Bwana Israeli.

Hiyo Iliendelea hivyo hivyo mpaka kupelekea mwaka 1967 mataifa yote ya urabuni yakiongozwa na Syria kujikusanya kwa ajili ya kuipoteza Israeli katika ramani ya dunia. Lakini jambo hilo kama tunavyosoma katika historia, Israeli ilizipiga silaha zao za vita na vita kuisha ndani ya siku 6 tu. Kupeleka mpaka Israeli kuteka sehemu ya kubwa ya taifa lake ambalo hapo kabla lilikuwa haliyamiliki pamoja na nchi za kando kando.

Sasa hayo nayo ni mwanzo wa utungu ili kutupa sisi picha ya mambo yatakayokuja kutoka siku za hivi karibuni. Hii ilikuwa ni mataifa ya uarabuni lakini siku zinakuja mataifa yote ulimwenguni yataungana kwenda kupigana na Israeli hiyo ndiyo vita ya Har-magedoni.

Hivyo tukisoma kitabu cha Ezekieli 28-39, tunaona vita nyingine hapa ukiwa na muda wako mwenyewe unaweza kusoma sura zote mbili upate kuiona habari nzima ni vita ambayo itapiganwa tena kipindi hichi karibu na unyakuo kutokea. Embu Tusome mistari michache tu ya mwanzo.

EZEKIELI: MLANGO 38

1 Neno la Bwana likanijia, kusema,

2 Mwanadamu, kaza uso wako, umwelekee Gogu, wa nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki, na Tubali, ukatabiri juu yake,

3 useme, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ewe Gogu, mkuu wa Roshi, na Mesheki, na Tubali;

4 nami nitakugeuza na kutia kulabu katika mataya yako, nami nitakutoa, pamoja na jeshi lako lote, farasi na hao wapandao farasi, wote wamevaa silaha za namna zote, jeshi kubwa sana, wenye ngao na kigao, wote wakishika upanga;

5 Uajemi, na Kushi, na Putu, pamoja nao; wote wana ngao na chapeo;

6 Gomeri, na vikosi vyake vyote; nyumba ya Togarma, pande za mwisho za kaskazini, na vikosi vyake vyote; naam, watu wengi pamoja nawe.

7 Ujiweke tayari, naam, jiweke tayari, wewe na majeshi yako yote waliokukusanyikia, nawe uwe jemadari wao.

8 NA BAADA YA SIKU NYINGI UTAJILIWA; KATIKA MIAKA YA MWISHO, UTAINGIA NCHI ILIYORUDISHIWA HALI YAKE YA KWANZA, BAADA YA KUPIGWA KWA UPANGA, ILIYOKUSANYWA TOKA KABILA NYINGI ZA WATU, juu ya milima ya Israeli, iliyokuwa ukiwa wa daima; lakini imetolewa katika kabila za watu, nao watakaa salama salimini wote pia.

9 Nawe utapaa juu, utakuja kama tufani, utakuwa kama wingu kuifunika nchi, wewe, na vikosi vyako vyote, na kabila nyingi za watu pamoja nawe.

10 BWANA MUNGU ASEMA HIVI; ITAKUWA KATIKA SIKU HIYO, MAWAZO YATAINGIA MOYONI MWAKO, NAWE UTAKUSUDIA KUSUDI BAYA;

11 nawe utasema, Nitapanda juu niiendee nchi yenye vijiji visivyo na maboma; nitawaendea watu wanaostarehe, wanaokaa salama, wote wakikaa pasipo kuta, ambao hawana makomeo wala malango;

12 ili kuteka mateka, na kuwinda mawindo; uugeuze mkono wako juu ya mahali palipoharibika, ambapo sasa panakaliwa na watu, na juu ya watu waliokusanyika toka mataifa, waliopata ng’ombe na mali, wakaao katikati ya dunia.

13 Sheba, na Dedani, na wafanya biashara wa Tarshishi, pamoja na wana-simba wake wote, watakuambia, Je! Umekuja kuteka mateka? Umekusanya jeshi lako, ili kuwinda mawindo? Kuchukua fedha na dhahabu, kuchukua ng’ombe na mali, kuteka mateka mengi sana?

14 Basi, mwanadamu, tabiri, umwambie Gogu, Bwana MUNGU asema hivi; Katika siku ile watu wangu, Israeli, watakapokaa salama, hutapata habari?

15 Nawe utakuja kutoka mahali pako, kutoka pande za mwisho za kaskazini, wewe, na watu wa kabila nyingi pamoja nawe, wote wamepanda farasi, kusanyiko kubwa, na jeshi kuu;

16 NAWE UTAPANDA JUU UWAJILIE WATU WANGU, ISRAELI, KAMA WINGU KUIFUNIKA NCHI; ITAKUWA KATIKA SIKU ZA MWISHO, NITAKULETA UPIGANE NA NCHI YANGU, ILI MATAIFA WANIJUE, nitakapotakaswa kwako, Ewe Gogu, mbele ya macho yao.

17 Bwana MUNGU asema hivi; Je! Wewe ndiwe niliyemnena zamani za kale, kwa vinywa vya watumishi wangu, manabii wa Israeli, waliotabiri siku zile kwa muda wa miaka mingi, ya kwamba nitakuleta upigane nao?

18 Itakuwa katika siku hiyo, Gogu atakapokuja kupigana na nchi ya Israeli, asema Bwana MUNGU, ghadhabu yangu itapanda katika mianzi ya pua yangu.

19 Kwa maana katika wivu wangu, na katika moto wa ghadhabu yangu, nimenena, Hakika katika siku ile kutakuwako tetemeko kubwa katika nchi ya Israeli;

20 hata samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama wa kondeni, na vitu vyote vitambaavyo juu ya nchi, na wanadamu wote walio juu ya uso wa nchi, watatetemeka mbele ya uso wangu; nayo milima itatupwa chini, na magenge yataanguka, na kila ukuta utaanguka chini.

21 Nami nitaita upanga, uje juu yake katika milima yangu yote, asema Bwana MUNGU; nao upanga wa kila mtu utakuwa juu ya ndugu yake.

22 Nami nitamhukumu kwa tauni, na kwa damu; nami nitanyesha mvua ifurikayo, na mvua ya mawe makubwa sana, na moto na kiberiti juu yake, na vikosi vyake, na watu wa kabila nyingi walio pamoja naye.

23 Nami nitajitukuza, na kujitakasa, na kujidhihirisha, mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana”.

Sasa Nchi ya Magogu, biblia inayoitaja hapo ni eneo linalojulikana kama URUSI kwasasa. Hivyo nchi hii leo tunaoina ni nchi yenye nguvu sana kiasi kwamba inalitishia hata taifa la Marekani kwa nguvu zake na ukuu wake. Lakini biblia inasema siku moja mawazo yataliingia hili taifa ili kwenda kuishambulia Israeli. Na kibaya zaidi halitashuka peke yake, hapana bali litashuka na majeshi ya mataifa mengine mengi kama tunavyoyasoma hapo juu. Na mengi ya hayo yatakuwa na haya mataifa ya kiharabu, ambayo hayo kimsingi ni maadui wa Israeli tangu zamani, pamoja na nchi nyingi zilizokando kando ya Urusi.

Wote watapanga vita kuiendea ile nchi ndogo sana Israeli. Kama tunavyoona hata sasa Taifa linaloongoza kuwa na maadui wengi duniani ni taifa la Israeli, hivyo Urusi kwa kujipendekeza na kujionyesha kuwa yeye anayo nguvu na kwamba anaweza kuwasaidia watu waliowashindwa ISRAELI. Yeye naye siku hiyo atapanga vita na mabomu yake ya Atomiki ili kwenda kulisambaratisha taifa lile. Hawajui kuwa hapo ndipo Mungu alipokusudia uwe mwisho wa mataifa hayo yote chini ya jua. Siku hiyo Urusi itapotezwa kwenye ramani ya dunia, kwasababu Bwana atakuwa upande wa Israeli. Na wa-Rusi siku hiyo watasoma maandiko haya ya Ezekieli na kutambua kuwa unabii huo ulikuwa unawahusu wao.

Kumbuka vita hiyo japo itauwa watu wengi sana kiasi kwamba biblia inasema mizoga yao itakuwa inazikwa kwa muda wa miezi 7 ikikusanywa tu, na silaha zao zitakuwa zikitumika kama kuni kwa muda wa miaka 7, lakini huo utakuwa ni mwanzo tu wa utungu. Vita yenyewe kuu bado. Vita ya Har-magedoni ambayo itahusisha mataifa yote ulimwenguni.

Tutakuja kuizungumzia vizuri vita hii [Har-Magedoni] katika makala nyingine. Lakini tufahamu kuwa vita inayozungumziwa katika Ezekieli 38-39 ipo mbioni kutokea, kama tunavyoona sasahivi mvutano ulivyo mkubwa mashariki ya kati na ishara kuwa vita vinajiandaa kupiganwa muda wowote. Hivyo ndivyo Mungu anavyozidi kuitasa Israeli kidogo kidogo, Na ndivyo pia wanavyojiandaa kumpokea Masiya wao.

Swali tujiulize wakati sasahivi neema inarudi Israeli, mimi na wewe mpaka mambo hayo yatakapotokea tutakuwa wapi? Kumbuka ndugu tuliambiwa tukiyaona hayo yanaanza kutokea basi tunyanyue vichwa vyetu, kwa kuwa ukombozi wetu umekaribia. Ikiwa na maana UNYAKUO wetu upo karibu.

Kristo yupo mlangoni ndugu. Unasubiri nini usiufanye leo wito wako na uteule wako imara?. Walioishi kipindi chote cha nyuma kuanzia miaka ya 1900 kurudi nyuma mpaka kipindi cha kanisa la kwanza hawakukishuhudia kitu hichi sisi tunachokishuhudia leo yaani taifa huru la Israeli. Na biblia ilishasema kizazi hiki hakitapita, sasa unasubiri nini usiushindanie wokovu katika muda huu mfupi uliobaki?.

Ungependa mambo hayo yakukute kwa ghafla, Bwana amesema dunia hii itaangamizwa kwasababu ya maovu yake. Na wenye haki watapata kwa Mungu waepushwe nayo.. je! Na wewe ungependa uwe miongoni mwa watakaoharibiwa katika ile siku ya Bwana? Kama sivyo mgeukie Kristo, ambaye yeye ndio safina pekee iliyothibitishwa na Mbingu kwa wokovu wa mwanadamu.

Bwana akubariki.

Tafadhali “share” kwa wengine ujumbe huu.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 HOME

Print this post

MAFUNUO YA ROHO.

Neno Ufunuo maana yake “NI KITU KILICHOFUNULIWA”..Ikiwa na maana kuwa, hapo kwanza kilikuwa kimefungwa na sasa kimefunuliwa. Hapo kwanza kilikuwa hakionekani sasa kinaonekana, hapo kwanza kilikuwa hakieleweki sasa kinaeleweka.

Zipo funuo za aina nyingi. Mwana sayansi alipochunguza vitu vya asili ndipo akapata ufunuo wa kutengeneza ndege, alipochunguza kwanini Tai anapaa ndipo alipogundua kitu kinachoitwa ndege, Baada ya uchunguzi wa tabia za mawimbi ya sauti na mwangwi akapata ufunuo wa kutengeneza kifaa kinachoitwa simu..ambapo hapo kwanza mambo hayo yalikuwa hayajulikani. Hivyo hivyo mpaka Akapata ufunuo wa kutengeneza magari na mambo mengine mengi.

Hivyo Roho ya mwanadamu Mungu aliyoiweka ndani yake ndiyo inayovumbua mambo ambayo kwa akili za kawaida yanaonekana kama hayawezekani. Lakini roho ya mwanadamu haiwezi kuvumbua chochote endapo mtu hatakaa katika hali ya utulivu na katika hali ya uchunguzi wa hali ya juu. Ndio maana wanasayansi na wagunduzi wengi, wanapoteza masaa mengi ya utafiti kwa kutulia na kutafakari na kujifunza pasipo kujichanganya na mambo mengi..lengo lao sio wajiumize hapana! Lengo ni ili waweze kuipa akili nafasi ya kutafakari mambo kwa undani kwa utulivu na utaratibu pasipo kuingiliwa na mambo mengine. Na hivyo wanapata matokeo makubwa wanapata Ufunuo/ uvumbuzi wa jambo Fulani..Yale mafumbo magumu waliyokuwa hawawezi kuyapatia ufumbuzi Roho zao zinawapatia ufumbuzi.

Kadhalika na Roho Mtakatifu naye..yeye ndiye ayachunguzaye mafumbo ya Mungu, na kuyapatia ufumbuzi..Na ndio maana ukisoma kitabu cha Ayubu 28, Utaona Bwana akiitafuta tafuta hekima kwa kuichunguza, hata kuipata na kumwambia mwanadamu..Hivyo utaona Roho ya Mungu, inapeleleza na kutafuta tafuta duniani kote mambo yamuhusuyo Mungu na Mwanadamu.

Zekaria 4: 7 “..naam, hizi saba ndizo macho ya Bwana; yapiga mbio huko na huko duniani mwote”.

Kwahiyo ili mtu awe na ufahamu juu ya mambo ya Mungu, ni lazima awe na Roho Mtakatifu kwasababu yeye pekee ndiye ayajuaye na kuyachunguza na kuyavumbua mambo ya Mungu..Kama vile  mwanadamu yeyote ili avumbue jambo Fulani ni lazima awe mwanadamu vivyo hivyo na kwa Mungu, ili kuyafahamu mambo yake ni lazima tuwe na Roho yake ndani yetu.

1Wakorintho 2: 10 “LAKINI MUNGU AMETUFUNULIA SISI KWA ROHO. MAANA ROHO HUCHUNGUZA YOTE, HATA MAFUMBO YA MUNGU.

11 Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu.

12 Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu”

SASA NI KWA NAMNA GANI TUNAWEZA KUPOKEA MAFUNUO KUTOKA KWA ROHO MTAKATIFU ALIYE NDANI YETU?

Ni kwa njia moja tu tunayoweza kupokea Mafunuo ya Roho Mtakatifu..Na hiyo si nyingine zaidi ya kama ile ile wana-sayansi wanayoitumia…Wao wanajifungia ndani na kutafakari, na kusoma vitabu vingi, na kujizuia na mambo mengi…ILI Roho zao ziinuke zipate umakini wa hali ya juu ili kupata ufunuo.

Kadhalika na Ufunuo wa Roho, hauji tu kwa kuusubiria, hapana, bali unakuja KWA KUJIZUIA NA MAMBO MENGI YA ULIMWENGU HUU, NA KUFUNGA, na KUSOMA VITABU VINGI, VYA HISTORIA NA VYA WAHUBIRI MBALI MBALI AMBAO BWANA KAWATIA MAFUTA KWELI, na KWA KUCHUNGUZA VITU VYA ASILI KWA UNDANI sana. Kwa kujiweka katika hayo mazingira unampa ROHO MTAKATIFU NAFASI KUBWA SANA YA YEYE KUKUFUNULIA JAMBO AMBALO HAPO KWANZA ULIKUWA HULIJUI. Kwa kukufunulia Siri iliyopo ndani ya Yesu Kristo kwa undani.

Tunaweza tukaona mifano kadha wa kadha kwenye Biblia..Danieli baada ya kuchunguza chunguza kwa wahubiri waliomtangulia kabla yake mambo waliyokuwa wanayahubiri…alikutana na nyaraka za nabii Yeremia ambazo zilikuwa zimeandikwa miaka kamili ya wana wa Israeli kukaa utumwani..Na baada ya kupata ufunuo huo, akaendelea kumwomba Mungu aelewe vizuri maana ya hayo mambo..Na ndipo akaamua kufunga na Bwana akamfunulia zaidi ya pale, Malaika Gabrieli alikuja na akamfunulia MAJUMA SABINI YATAKAYOANZA BAADA YA WAO KUTOKA UTUMWANI.

Danieli 9: 1 “Katika mwaka wa kwanza wa Dario, mwana wa Ahasuero, wa uzao wa Wamedi, aliyetawazwa kuwa mfalme juu ya milki ya Wakaldayo;

2 katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.

3 Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu”.

Mfano mwingine tonamwona Yule Mkushi aliyekuwa ametoka Yerusalemu kuhiji enzi za Mitume wa Kristo aliyekuwa anatafuta kuchunguza kwa bidii maandiko, Na katika kusoma kwake alikutana na maandiko magumu sana hakuyaelewa yaliyoandikwa na nabii Isaya…lakini kwasababu alikuwa na kiu ya kutaka kujua Bwana alimtimizia haja ya moyo wake na kumtumia ufunuo kupitia Mtumishi wake Filipo..Jambo hilo tunaweza kulisoma katika kitabu cha…

Matendo 8: 26 “Malaika wa Bwana akasema na Filipo, akamwambia, Ondoka ukaende upande wa kusini hata njia ile itelemkayo kutoka Yerusalemu kwenda Gaza; nayo ni jangwa.

27 Naye akaondoka, akaenda; mara akamwona mtu wa Kushi, towashi, mwenye mamlaka chini ya Kandake malkia wa Kushi, aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu,

28 akawa akirejea, ameketi garini mwake akisoma chuo cha nabii Isaya.

29 Roho akamwambia Filipo, Sogea karibu na gari hili, ukashikamane nalo.

30 Basi Filipo akaenda mbio, akamsikia anasoma chuo cha nabii Isaya; akanena, Je! Yamekuelea haya unayosoma?

31 Akasema, Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza? Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye.

32 Na fungu la Maandiko alilokuwa akilisoma ni hili, Aliongozwa kwenda machinjoni kama kondoo, Na kama vile mwana-kondoo alivyo kimya mbele yake amkataye manyoya, Vivyo hivyo yeye naye hafunui kinywa chake.

33 Katika kujidhili kwake hukumu yake iliondolewa. Ni nani atakayeeleza kizazi chake? Kwa maana uzima wake umeondolewa katika nchi.

34 Yule towashi akamjibu Filipo, akasema, Nakuomba, nabii huyu; asema maneno haya kwa habari ya nani; ni habari zake mwenyewe au za mtu mwingine?

35 Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.

36 Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?

37 Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]

38 Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.

39 Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.

40 Lakini Filipo akaonekana katika Azoto, na alipokuwa akipita akahubiri Injili katika miji yote, hata akafika Kaisaria”.

Unaona! Ukichunguza wote hawa, Roho Mtakatifu aliwafunulia kwasababu walikuwa na kiu, na walikuwa wanajitahidi kusoma maandiko na kuchunguza. Roho Mtakatifu hawezi kukufunulia jambo lolote kama hutaki kujizuia na mambo Fulani, na kuchukua gharama Fulani, Kama hutaki kutaka kujua mambo yanayokuja ya kwenda mbinguni basi hutajua chochote mpaka kanisa litakaponyakuliwa na hivyo kubaki katika dhiki kuu ya Mpinga-Kristo, na kutupwa katika lile ziwa la moto baadaye. Utaendelea kufikiri tu bado mamilioni ya Miaka mpaka Kristo arudi.

Mfalme Nebukadneza wa Babeli ambaye hakuwa hata mkristo, wakati Fulani usiku alipokuwa amejiegeza kitandani mwake akitafakari ni mambo gani yatakayotokea siku za Mwisho…pasipo kujua chochote usingizi ukampitia akiwa bado katika hayo mawazo na alipokuwa katika usingizi ule akaota ndoto sanamu kubwa ipo mbele yake ina kichwa cha dhahabu, na kifua cha shaba na mikono ya fedha na miguu ya chuma..Aliposhtuka aliisahau ile ndoto, lakini alijua kabisa ni ndoto yenye mahusiano na siku za mwisho, kwasababu ndio mawazo aliyokuwa anayawaza kabla hajalala..(Danieli 2:27-29)..na kwa kupitia Nabii Danieli Roho aliweza kumfunulia Nebukadneza mambo yatakayokuja kutokea siku za Mwisho.

Unaona hapo? Roho anawafunulia hata watu wasiokuwa wake, mambo yatakayokuja kutokea siku za mwisho, Na wewe je! Alishawahi kukufunulia kwamba tunaishi katika nyakati gani?, na ni mambo gani yatakayokuja kutokea siku za mwisho? Ulishawahi kukaa chini na kutafakari mambo yatakayokuja kutokea nyakati za Mwisho? Ulishawahi kukaa chini ukatafakari yale maneno Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake katika Mathayo 24??…aliposema mmoja atatwaliwa mmoja ataachwa ulishawahi kuketi chini na kutafakari mambo hayo?.

Muhubiri mmoja, Mjumbe wa Mungu anayeitwa WILLIAM BRANHAM, siku moja asubuhi wakati ametoka kulala tu! Akiwa amejiegemeza kichwa chake juu ya mto, akitafakari itakuwaje siku ile atakayoenda kumwona Bwana mawinguni, akiwa anatafakari akidhani kuwa mwendo ndio amekaribia kuumaliza, ghafla alisikia sauti ndogo ikimwambia “akaze mwendo ndio kwanza safari inaanza” wakati anaitafakari hiyo sauti alijikuta ametokea mahali palipo pazuri sana pa utulivu, penye nyasi nzuri ambazo anasema hajawahi kuziona hapo kabla, akawaona wadada na wakaka wengi wa makamu ya miaka kama 20-30 hapo, wamevaa vizuri sana, wanamjia wakiwa na nyuso za furaha, wote wakawa wanamkumbatia kila mmoja akimwambia “oo ndugu yetu wa thamani…oo ndugu yetu wa thamani” wote walionyesha nyuso za furaha na raha isiyokuwa ya kawaida..William akasikia ile sauti ikimwambia “hawa wote unaowaona ni wale watu uliowaleta kwa Kristo kupitia injili yako, waliotangulia kulala, sasa wako hapa wanakushukuru” Akashangaa sana kuona jinsi walivyo wengi..

Wakamwuliza akisema..lakini mbona wengine niliwaleta kwa Kristo wakiwa wazee, inakuwaje hapa nawaona wote ni vijana, akaambiwa huku hakuna wazee wote ni vijana..Akasikia ile sauti ikimwambia “siku ile ya mwisho” akaze mwendo ndio kwanza tu anaanza safari. Lile ono likampotea na alivyorudi katika hali yake ya kawaida, hiyo ilimtia nguvu kukaza mwendo zaidi ili siku ile afike sehemu ile ya Raha.

Unaona! Huyu ndugu BRANHAM ni moja ya watu, waliokuwa wakitafakari tu vitandani mwao, kama Mfalme Nebukadneza alivyofanya na ROHO MTAKATIFU akawafunulia baadhi ya mambo yajayo.

Ni maombi yangu kuwa BWANA ATAKUKIRIMIA NA WEWE KUYAFAHAMU MAFUMBO YAKE. Ni maombi yangu kuwa Bwana atakupa ukurasa mpya kuanzia leo, kutaka Kupata ufunuo kutoka kwake, Ni maombi yangu kuanzia leo Bwana atakujalia kutafuta kujifunza kwa bidii kama Danieli, mpaka Kupata kufunuliwa mambo yajayo. Ni maombi yangu kuwa Bwana atakupa kutafakari na kudadisi mambo yajayo mpaka atakapokupa ufunuo kama aliompa Nebukadneza, au aliompa mhubiri William Branham, Ni maombi yangu kuwa Bwana atakupa kuyadadisi maandiko sana, mpaka Roho atakapomtuma Mtumishi wake atakayekuelewesha vema mafumbo yake..kama alivyofanya kwa Yule Mkushi alipotumiwa Filipo.

Bwana Yesu akubariki.

Usiache “kus-share” ujumbe huu kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

TUSIPOUTHAMINI WOKOVU TUTAPATAJE KUPONA?

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.

MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI


Rudi Nyumbani

Print this post

ITAFAKARI VEMA KAZI YA MUNGU

Tukijua kuwa Mungu ni zaidi ya sisi tunavyofikiri, Na kwamba hukumu zake hazichunguzi (kama inavyosema Warumi 11:33), Siku hiyo tukifahamu mambo hayo kwa undani tutaishi maisha ya kumwogopa na ya kujichunga kila siku, Siku tukijua kuwa mambo yote mtu atendayo aidha yawe maovu au mema hayaji kwa nguvu zake mwenyewe bali ni kutoka kwa Mungu, ndipo tutakapomwopoga sana Mungu na kujua kuwa yeye si mwanadamu na kwamba mawazo yake si mawazo yetu.

Biblia inasema:

Mhubiri 7:13 “Tafakari vema kazi yake Mungu; kwa sababu ni nani awezaye kukinyosha kitu kile alichokipotosha yeye?”.

Watu wengi hawapendi kusikia maneno hayo kwamba Mungu anao uwezo wa kumletea mtu nguvu ya upotevu ili apotee,. Ni kweli Mungu hawezi kumletea mtu nguvu ya upotevu kwa yeye ambaye hajaijua neema bado lakini kwake yeye aliyeisikia na kuipuuzia na kuikataa, nguvu hiyo ya upotevu inaachiliwa juu yake, na nguvu hiyo haitoki kwa shetani bali inatoka kwa Mungu mwenyewe.

Soma >>

1Wathesalonike 2:10 “na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.

11 KWA HIYO MUNGU AWALETEA NGUVU YA UPOTEVU, WAUAMINI UONGO;

12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu.”

Kama tu vile mtu anayempokea Kristo kwa mara ya kwanza Mungu huwa anamshushia uwezo /nguvu ya kushinda dhambi na kufanyika kuwa mtoto wa Mungu (Yohana 1:12), kadhalika na wale ambao wanaikataa neema ya msalaba au wanaoipuuzia sasa, utafika wakati hii nguvu ya upotevu itokayo kwa Mungu inaachiliwa wao nao juu yao. Hivyo watu wa namna hiyo inafika wakati hata wahubiriweje injili, hata wauone ukweli kiasi gani, hawawezi tena kuamini. Hali yao ya rohoni inazidi kuwa mbaya kuliko hata waliyokuwa nayo mwanzoni, kule kuchomwa rohoni pale mtu anapotenda jambo baya kunakufa, dhamira yake inakuwa imekufa, mtu kama huyo dhambi inakuwa ni kitu cha kawaida sana kwake, hata akibaka mnyama, hata akiua, hata akifanya ushoga, hata akikufuru mbele za Mungu kwake ni kama jambo la kawaida tu,.

Ni kwasababu gani?, Ni kwasababu ile nguvu ya upotevu itokayo kwa Mungu imeachiliwa juu yake ili auamini uongo siku ile akahukumiwe ili ashuke moja kwa moja katika ziwa la moto, kwasababu hakuipenda kweli apate kuokolewa bali alijifurahisha katika udhalimu.. Na Watu wa namna hiyo kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda ndio mwisho wa siku wanaishia kuipinga biblia, wanaishia kusema hakuna Mungu, biblia ni kitabu kilichotungwa na watu, wanakuwa wanaishi tu kama wanyama duniani wasioweza kujizuia. Watu wa namna hiyo wanawaona hata wale wengine wanaotafuta wokovu kama ni watu wasioelimika, watu waliokata tamaa ya maisha, watu wajinga wasio na mwelekeo.

Biblia imetumia lugha hii kuwazungumzia jinsi walivyo watu wa namna hiyo..

Yuda 1:11-16 “ni mawingu yasiyo na maji, yachukuliwayo na upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung’olewa kabisa;

13 ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; ni nyota zipoteazo, ambao weusi wa giza ndio akiba yao waliowekewa milele.

14 Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu,

15 ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizozitenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake.

16 Watu hawa ni wenye kunung’unika, wenye kulalamika, waendao kwa tamaa zao, na vinywa vyao vyanena maneno makuu mno ya kiburi, wakipendelea watu wenye cheo kwa ajili ya faida.”

Sasa watu wa dizaini hii hata uwahubirieje injili hawawezi kubadilika wala hawatakaa wabadilike kwasababu ni Mungu wenyewe ndiye aliyewakusudia mabaya, na ndio maana biblia inasema:

Mhubiri 7:13 “Tafakari vema kazi yake Mungu; kwa sababu ni nani awezaye kukinyosha kitu kile alichokipotosha yeye?”.

Ndugu, Njia za Mungu huwa ZINATISHA, na ndio maana tumeambiwa TUZITAFAKARI VEMA KAZI ZAKE, sio tu kuzichukulia juu juu, Tukidhani kuwa hukumu za Mungu zinachunguzika kwamba nitaokoka tu siku moja! Au Tunasema Mungu ataokoa tu!, Mungu tu ataokoa tu! Na huku tunadumu katika dhambi tukidhani kuwa neema ni kitu cha kukifanyia mzaha. Kumbuka hilo neno lenyewe NEEMA ni kitu kinachoonyesha kuwa ni jambo AMBALO HUKUSTAHILI KULIPATA NI KWA HURUMA TU UMEPEWA, lakini unaendelea kulifanyia mzaha kana kwamba ulistahili kuipata ni haki yako?.

Unadhani NGUVU HIYO YA UPOTEVU itakapokujia juu yako ikiwa hautubu leo, na kusimama imara katika Kristo siku ile ya hukumu utasema Mungu ni MDHALIMU alikuletea mabaya kwa makusudi?. Ndugu Itafakari vema kazi ya Mungu ili ujue leo hii unasimamia wapi?.

Mungu alishamaliza mambo yote kabla hata ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, majina ya watakaookolewa Mungu alishayaandika katika kitabu cha uzima kabla ya misingi ya ulimwengu kuwekwa biblia inasema hivyo

Ufunuo 17.8 “Yule mnyama uliyemwona alikuwako, naye hayuko, naye yu tayari kupanda kutoka kuzimu na kwenda kwenye uharibifu. NA HAO WAKAAO JUU YA NCHI, WASIOANDIKWA MAJINA YAO KATIKA KITABU CHA UZIMA TANGU KUWEKWA MISINGI YA ULIMWENGU, watastaajabu wamwonapo yule mnyama, ya kwamba alikuwako, naye hayuko, naye atakuwako”.

Embu tafakari kwa makini habari hii utajifunza jambo.

Warumi 9:11 “(kwa maana kabla hawajazaliwa wale watoto, wala hawajatenda neno jema wala baya, ili lisimame kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya matendo, bali kwa sababu ya nia yake aitaye),

12 aliambiwa hivi, Mkubwa atamtumikia mdogo.

13 Kama ilivyoandikwa, Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia.

14 Tuseme nini basi? Kuna udhalimu kwa Mungu? Hasha!

15 Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye.

16 Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu.

17 Kwa maana maandiko yasema juu ya Farao, ya kwamba, Nilikusimamisha kwa kusudi hili, ili nionyeshe nguvu zangu kwako, jina langu likatangazwe katika nchi yote.

18 Basi, kama ni hivyo, atakaye kumrehemu humrehemu, na atakaye kumfanya mgumu humfanya mgumu.

19 Basi, utaniambia, Mbona angali akilaumu? Kwa maana ni nani ashindanaye na kusudi lake?

20 La! Sivyo, Ee binadamu; wewe u nani umjibuye Mungu? Je! Kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwani kuniumba hivi?

21 Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?

22 Ni nini basi, ikiwa Mungu kwa kutaka kuonyesha ghadhabu yake, na kuudhihirisha uweza wake, kwa uvumilivu mwingi, alichukuliana na vile vyombo vya ghadhabu vilivyofanywa tayari kwa uharibifu;

23 tena, ili audhihirishe wingi wa utukufu wake katika vile vyombo vya rehema, alivyovitengeneza tangu zamani vipate utukufu;”

Je! Wewe ni chombo cha ghadhabu kilichowekwa tayari kwa uharibifu, au ni kile chombo cha rehema?. Jua tu ikiwa unaukwepa msalaba, ikiwa unaukwepa wokovu, ikiwa unaikwepa toba, ile nguvu ya upotevu mfano wa ile iliyokuwa juu farao ambayo HATA AONE MIUJIZA MIKUBWA KIASI GANI HAWEZI KUTUBU, NDIYO ITAKAYOKUJA JUU YAKO KAMA UTAENDELEA KUUPINGA WOKOVU NDANI YA MOYO WAKO.

TAFAKARI VEMA KAZI YAKE MUNGU. Ili ujiokoe nafsi yako, Epuka Injili ya maneno ya faraja kila siku unaambiwa kwamba Mungu ni Mungu wa rehema. Lakini upande wa pili wa Mungu hagusiwi ambao unasema BWANA NI MWINGI WA HASIRA, ni nani awezaye kusimama mbele ya hasira yake, ni nani awezaye kukaa katika ukali wa hasira yake? (Nahumu 1 )

Kwa kulijua hilo, utafahamu kuwa Mungu hadhihakiwi na hapo ulipo hupaswi kuendelea kudumu katika dhambi. Na ndio maana biblia inasema “(Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)”

Kwa nini usiwe mmojawapo wa kondoo wa Kristo?. Ikiwa upo tayari sasa kuwa mmojawapo unachopaswa kufanya ni kukusudia wewe mwenyewe kutoka moyoni mwako Kutubu na kuacha dhambi kabisa..Kumbuka kutubu ni KUGEUKA( au KUACHA) na sio sala ya toba tu.

Hivyo ukiwa umedhamiria kufanya hivyo wewe moyoni mwako kwa dhati kabisa na kutaka kumwishia Kristo kuanzia sasa na kuendelea. Unachopaswa kufanya ni kwenda kutafuta mahali ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kimaandiko, yaani ubatizo wa kuzamishwa, katika maji mengi na jina linalotumika liwe ni JINA LA YESU KRISTO na si linginelo. Ili upate ondoleo la dhambi zako, Kulingana na matendo 2:38,na Bwana mwenyewe atakupa Roho wake Mtakatifu kuanzia huo wakati na kuendelea kukusaidia kuukulia wokovu na kuishinda dhambi.

Mungu akubariki sana.

“Share” Ujumbe huu kwa ndugu zako, Na Mungu atakubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

UNAFANYA NINI HAPO?

UMETEKWA NA UPENDO WA KRISTO?

WAKATI WA JIONI KUTAKUWAKO NA NURU.

TUZO UTAPEWA KULINGANA NA NAFASI YAKO.

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.


Rudi Nyumbani

Print this post

SADAKA ILIYOKUBALIKA.

 

SADAKA ni moja ya maagizo muhimu sana, na yanayobeba Baraka nyingi sana kwa Mtu, kama ikitolewa kulingana na Neno na kwa Hiari ya mtu pasipo kulazimishwa au kusukumwa na mazingira Fulani. Lakini sadaka hiyo hiyo isipotolewa jinsi inavyopaswa inaweza ikaleta LAANA kubwa sana, badala ya Baraka. Kwasababu biblia inasema katika..Mithali 15:8 “Sadaka ya mtu mbaya ni CHUKIZO KWA BWANA; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake”.

Biblia inaposema mtu mbaya ina maana gani?

Mtu yeyote Yule ambaye haishi kulingana na Neno la Mungu, mtu huyo ni mbaya mbele za Mungu. Mtu yeyote anayejua kuwa kufanya jambo Fulani ni dhambi na bado analifanya mtu huyo ni mbaya mbele za Mungu. Mtu yoyote anayejua uasherati ni dhambi na bado anaufanya, mtu yeyote anayejua rushwa ni dhambi na bado anatoa au anapokea, mtu yeyote anayejua usengenyaji ni dhambi na bado anasengenya, mtu yoyote anayejua kuwa matusi ni dhambi na bado anatukana mtu huyo mbele za Mungu ni mtu Mbaya,

Mtu yoyote anayejua ulevi, anasa, wizi ni mbaya na bado anafanya mambo hayo mtu huyo ni mbaya mbele za Mungu, Na hivyo sadaka zake ni MACHUKIZO MAKUBWA MBELE ZA MUNGU. Apatapo chochote kwa njia hizo na kuzipeleka Madhabahuni kwa Bwana sadaka yake mtu huyo ni MACHUKIZO, na hivyo atakuwa ameenda kujitafutia laana badala ya Baraka. Kwahiyo kwake linakuwa ni chukizo litakalomletea Uharibifu wake mwenyewe. Biblia inasema katika..

Kumbukumbu 23: 17 “PASIWE NA KAHABA KATIKA BINTI ZA ISRAELI, wala pasiwe na HANITHI katika wana wa Israeli wanaume.

18 USILETE UJIRA WA KAHABA, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; KWANI HAYA NI MACHUKIZO KWA BWANA, MUNGU WAKO, YOTE MAWILI”.

Unaona hapo! Bwana alikataza sadaka zozote, zitokanazo na njia zilizo nje ya Neno lake, zisifike kabisa nyumbani mwake.

Watu wanapokosa shabaha ni kufikiri kuwa Ukristo ni kwenda kanisani na kutoa sadaka, basi au kusaidia wajane na mayatima…Hawajui kuwa Ukristo ni zaidi ya hapo. Kumpendeza Mungu sio kumpa yeye sehemu ya mali yako na kuishi maisha unayotaka..Hapana Mungu sio mfanya biashara kwamba anakutafuta wewe ili apate kitu kwako, wala sio mwana-Hisa kwamba anawekeza kwetu ili baadaye apate kitu kutoka kwetu. Yeye mwenyewe anasema Dunia yote ni yake, sasa ana haja na kitu gani? Bwana Yesu alisema maneno haya..

Mathayo 9: 13 “Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA;”

Na pia anasema katika Waebrania 10:6

“Sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi hukupendezwa nazo;

7 Ndipo niliposema, Tazama, nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa) NIYAFANYE MAPENZI YAKO, MUNGU.”

Unaona hapo? Bwana anachotaka kutoka kwetu ni REHEMA, yaani anataka mtu atubu, asafishike na kuwa msafi kweli kweli anayekubaliwa na Mungu, atende mapenzi ya Mungu…Hiyo ndio sadaka inayompenda Mungu.

Wakati Fulani Mfalme Sauli alipewa maagizo kutoka kwa Bwana akawaangamize jamii ya watu Fulani, aangamize na mifugo yao yote na kila kitu, ili kutimiza kisasi cha Bwana juu ya hao watu, lakini Sauli hakufanya vile, hakuitii sauti ya Mungu kwa kuangamiza kila kitu, na badala yake akamuacha mfalme wao hai, na akachukua wale ng’ombe walionona ili akamtolee Mungu wa Israeli sadaka zile mambo ambayo Mungu alimkataza asiyafanye.. Kwa mawazo yake alijua Mungu atamheshimu na kumpenda kwasababu amemletea sehemu zilizonona za nyara za Maadui zao. Lakini mambo yalimbadilikia mbeleni alipokutana na Samweli nabii wa BWANA…

1 Samweli 15: 20 “Sauli akamwambia Samweli, Hakika mimi nimeitii sauti ya Bwana, nami nimemleta Agagi, mfalme wa Waamaleki, tena nimewaangamiza Waamaleki kabisa.

21 Ila watu waliteka nyara, kondoo na ng’ombe walio wazuri, katika vitu vilivyowekwa wakfu, KUSUDI WAVITOE DHABIHU KWA BWANA, MUNGU WAKO, huko Gilgali.

22 Naye Samweli akasema, JE! BWANA HUZIPENDA SADAKA ZA KUTEKETEZWA NA DHABIHU SAWASAWA NA KUITII SAUTI YA BWANA? Angalia, KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU, NA KUSIKIA KULIKO MAFUTA YA BEBERU.

23 Kwani KUASI NI KAMA DHAMBI YA UCHAWI, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme”.

Kwa kosa hilo moja tu! Sauli alipoteza ufalme wake, na Mungu alimwacha tangu siku ile. Kwasababu hakuwa mtii mbele za Mungu na badala yake akadhani kuwa uhusiano wake yeye na Mungu haujalishi sana, bali kinachojalisha ni kiasi gani cha sadaka anachomtolea.

Mahali pengine Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake..

Mathayo 5: 23 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, NA HUKU UKIKUMBUKA YA KUWA NDUGU YAKO ANA NENO JUU YAKO,

24 Iache Sadaka Yako Mbele Ya Madhabahu, Uende Zako, Upatane Kwanza Na Ndugu Yako, Kisha Urudi Uitoe Sadaka Yako”.

Unaona! Unaweza ukawa tayari umeshajiandaa kutoa sadaka yako kwenye madhabahu ya Mungu, lakini ndani ya moyo wako kuna mtu mmegombana, au kuna mtu umemkosea, au kuna mtu umemsengenya au kitu kilicho kibaya umekifanya, Bwana Yesu anatuonya Nenda kwanza kapatane na ndugu yako kisha ndipo uje utoe ile sadaka,.. Lakini tusipofanya hivyo na kuitoa ile sadaka.. yatakukuta kama yaliyomkuta Mfalme Sauli. Badala ya kupokea Baraka unapokea Laana. Badala ya kuinuliwa unashushwa.

Hivyo maisha yetu matakatifu ndio sadaka ya kwanza Mungu anayoitaka katika maisha yetu, ukiwa mwasherati tubia kwanza uasherati wako kwa kumaanisha kuuacha kwasababu maana ya kutubu sio kuomba msamaha tu! Bali ni KUGEUKA ndipo ukamtolee Mungu sadaka yako, ukiwa mlevi tubia kwanza ulevi wako kwa kumaanisha kuuacha kabisa ndipo ukamtolee Bwana sadaka zako, na vivyo hivyo mambo mengine yote yaliyo nje na Neno lake unayoyafanya. Yaache kwanza ndipo ufikirie suala la Sadaka..

Isaya 1: 11 “Huu wingi wa sadaka zenu mnazonitolea UNA FAIDA GANI? Asema Bwana. Nimejaa mafuta ya kafara za kondoo waume, na mafuta ya wanyama walionona; nami siifurahii damu ya ng’ombe wala ya wana-kondoo wala ya mbuzi waume.

12 Mjapo ili kuonekana mbele zangu, ni nani aliyetaka neno hili mikononi mwenu, kuzikanyaga nyua zangu?

13 MSILETE TENA MATOLEO YA UBATILI; uvumba ni chukizo kwangu; mwezi mpya na sabato, kuita makutano; SIYAWEZI MAOVU HAYO NA MAKUTANO YA IBADA.

14 Sikukuu zenu za mwezi mpya na karamu zenu zilizoamriwa, NAFSI YANGU YAZICHUKIA; MAMBO HAYO YANILEMEA; NIMECHOKA KUYACHUKUA.

15 Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.

16 JIOSHENI, JITAKASENI; ONDOENI UOVU WA MATENDO YENU USIWE MBELE ZA MACHO YANGU; ACHENI KUTENDA MABAYA;

17 JIFUNZENI KUTENDA MEMA; TAKENI HUKUMU NA HAKI; WASAIDIENI WALIOONEWA; MPATIENI YATIMA HAKI YAKE; MTETEENI MJANE.”

Neema ya Bwana Yesu Kristo izidi kuwa nawe.

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Rudi Nyumbani

Print this post

NI WAKATI UPI UTAUONA USO WA KRISTO?

Habari ya huyu kipofu unaweza ukawa umeshaisoma mara nyingi sana, lakini lipo jambo limejificha ambalo kila mtu anapaswa alijue, tafadhali soma tena kwa utaratibu na kwa utulivu kisha tutatazama ni wapi tunapaswa tuzingatie sana sana pale tunapodhani kuwa Mungu kutufanikisha au kutuwezesha katika mambo yetu ni uthibitisho kuwa tumemwona yeye.

Embu tusome tena pamoja kwa utulivu:

Yohana 9:1-41 
“1 Hata alipokuwa akipita alimwona mtu, kipofu tangu kuzaliwa. 

2 Wanafunzi wake wakamwuliza wakisema, Rabi, ni yupi aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi wake, hata azaliwe kipofu? 

3 Yesu akajibu, Huyu hakutenda dhambi, wala wazazi wake; bali kazi za Mungu zidhihirishwe ndani yake. 

4 Imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenipeleka maadamu ni mchana, usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi. 

5 Muda nilipo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu. 

6 Alipokwisha kusema hayo, alitema mate chini, akafanya tope kwa yale mate. Akampaka kipofu tope za macho, 

7 akamwambia, Nenda kanawe katika birika ya Siloamu, (maana yake, Aliyetumwa). Basi akaenda na kunawa; akarudi anaona. 

8 Basi jirani zake, na wale waliomwona zamani kuwa ni mwombaji, wakasema, Je! Huyu siye yule aliyekuwa akiketi na kuomba? 

9 Wengine wakasema, Ndiye. Wengine wakasema, La, lakini amefanana naye. Yeye mwenyewe alisema, Mimi ndiye. 

10 Basi wakamwambia, Macho yako yalifumbuliwaje? 

11 Yeye akajibu, Mtu yule aitwaye Yesu alifanya tope, akanipaka macho akaniambia, Nenda Siloamu ukanawe; basi nikaenda na kunawa, nikapata kuona. 

12 Wakamwambia, Yuko wapi huyo? Akasema, Mimi sijui. 

13 Basi wakampeleka kwa Mafarisayo yule aliyekuwa kipofu zamani. 

14 Nayo ilikuwa sabato, hapo Yesu alipofanya zile tope na kumfumbua macho. 

15 Basi Mafarisayo nao wakamwuliza tena jinsi gani alivyopata kuona. Akawaambia, Alinitia tope juu ya macho, nami nikanawa, na sasa naona. 

16 Basi baadhi ya Mafarisayo wakasema, Mtu huyo hakutoka kwa Mungu, kwa sababu haishiki sabato. Wengine wakasema, Awezaje mtu mwenye dhambi kufanya ishara kama hizo? Kukawa matengano kati yao. 

17 Basi wakamwambia yule kipofu mara ya pili, Wewe wasemaje katika habari zake kwa vile alivyokufumbua macho? Akasema, Ni nabii. 

18 Basi Wayahudi hawakusadiki habari zake, ya kuwa alikuwa kipofu, kisha akapata kuona; hata walipowaita wazazi wake yule aliyepata kuona. 

19 Wakawauliza wakisema, Huyu ndiye mwana wenu, ambaye mnasema kwamba alizaliwa kipofu? Amepataje, basi, kuona sasa? 

20 Wazazi wake wakawajibu, wakasema, Tunajua ya kuwa huyu ndiye mwana wetu, tena ya kuwa alizaliwa kipofu; 

21 lakini jinsi aonavyo sasa hatujui; wala hatujui ni nani aliyemfumbua macho. Mwulizeni yeye mwenyewe; yeye ni mtu mzima; atajisemea mwenyewe. 

22 Wazazi wake waliyasema hayo kwa sababu waliwaogopa Wayahudi; kwa maana Wayahudi walikuwa wamekwisha kuafikiana kwamba mtu akimkiri kuwa ni Kristo, atatengwa na sinagogi. 

23 Ndiyo sababu wale wazazi wake walisema, Ni mtu mzima, mwulizeni yeye. 

24 Basi mara ya pili wakamwita yule mtu aliyekuwa kipofu, wakamwambia, Mpe Mungu utukufu. Sisi tunajua ya kuwa mtu huyo ni mwenye dhambi. 

25 Basi yule mtu akajibu, Kwamba yeye ni mwenye dhambi sijui. Najua neno moja, kuwa mimi nalikuwa kipofu na sasa naona. 

26 Basi wakamwambia, Alikutendea nini? Alikufumbua macho jinsi gani? 

27 Akawajibu, Nimekwisha kuwaambia, wala hamkusikia; mbona mnataka kusikia tena? Ninyi nanyi mnataka kuwa wanafunzi wake? 

28 Basi wakamshutumu, wakasema, Wewe u mwanafunzi wake yule; sisi tu wanafunzi wa Musa. 

29 Sisi tunajua ya kuwa Mungu alisema na Musa; bali yule hatujui atokako. 

30 Yule mtu akajibu, akawaambia, Hii ni ajabu! Kwamba ninyi hamjui atokako, naye alinifumbua macho! 

31 Twajua ya kuwa Mungu hawasikii wenye dhambi; bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake, humsikia huyo. 

32 Tokea hapo haijasikiwa ya kuwa mtu ameyafumbua macho ya kipofu, ambaye alizaliwa hali hiyo. 
33 Kama huyo asingalitoka kwa Mungu, asingeweza kutenda neno lo lote. 

34 Wakajibu, wakamwambia, Ama! Wewe ulizaliwa katika dhambi tupu, nawe unatufundisha sisi? Wakamtoa nje. 

35 Yesu akasikia kwamba wamemtoa nje; naye alipomwona alisema, Wewe wamwamini Mwana wa Mungu? 

36 Naye akajibu akasema, Ni nani, Bwana, nipate kumwamini? 

37 Yesu akamwambia, Umemwona, naye anayesema nawe ndiye. 

38 Akasema, Naamini, Bwana. Akamsujudia. 

39 Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu. 

40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwapo pamoja naye wakasikia hayo, wakamwambia, Je! Sisi nasi tu vipofu? 

41 Yesu akawaambia, Kama mngekuwa vipofu, msingekuwa na dhambi; lakini sasa mwasema, Twaona; basi dhambi yenu inakaa.”

Amen!

Katika habari hiyo kuna maswali kadhaa ya kujiuliza,

La kwanza ni kwa nini Bwana hakumponya huyu kipofu wakati ule ule alipokutana naye hadi kumwambia kwanza aende kunawa katika birika la ALIYETUMWA ( yaani SILOAMU?) ndipo atakapofunguliwa macho yake.?Unadhani alishindwa kumfungua macho muda ule ule?.

Pili Kulingana na habari baada ya kufunguliwa macho yake ni kweli alipata kuona kwa namna ile Kristo aliyokuwa anaitarajia?.

Ukichunguza kwa makini utaona kuwa Yule mtu hakumjua YESU ni nani, wala alipotokea wala alipoenda wala hakumwona uso wake hata baada ya kufunguliwa macho yake. Haikujalisha alifunguliwa macho kiasi gani yeye alichoweza kufanya ni kwenda tu kuendelea kufanya shughuli zake za nyumbani kwao za kila siku mpaka ilipofikia wakati majirani zake walipoanza kumuuliza habari za kufunguliwa macho yake..Ndipo akaanza tena kunena habari za YESU.

Kama tunavyosoma alianza kupitia mitikisiko pindi tu alipoanza kumkiri Kristo maishani mwake. Hapo ndipo vita kutoka kwa watu mbali mbali, kutoka kwa wakuu wa dini vikaanza, kukanwa na wazazi, kupuuziwa na majirani kulipoanza. Kwasababu kumbuka kwa wakati ule wayahudi wote walikuwa wameshakwisha kupatana kuwa akitokea mtu yeyote atakayemkiri Kristo kuwa ni mwokozi adhabu yake itakuwa ni kutengwa na sinagogi daima, kwa leo tunaweza kusema kutengwa na kanisa. Na kumbuka kutengwa na sinagogi kwa wakati ule ni zaidi ya hapo, kulikuwa ni sawa na kutengwa na jamii nzima ya wayahudi kwasababu Taifa zima lilikuwa na DINI moja na Utamaduni mmoja..Tofauti na sasahivi ambapo mtu akitengwa na jamii yake anaweza akakubaliwa na jamii nyingine kwasababu tamaduni zipo nyingi na kuna haki nyingi za kibinadamu mtu kuishi anavyotaka…Hivyo mtu aliyekuwa anadhubutu kufanya vile alikuwa hachukui uamuzi mwepesi, bali ni uamuzi wa kujikana kweli kweli, ulikuwa ni uamuzi mzito mno.. Na ndio maana ukisoma wapo wengi waliomwamini YESU lakini pale ilipofikia hatua ya kumkiri walishindwa

Yohana 11: 42 “WALAKINI HATA KATIKA WAKUU WALIKUWAMO WENGI WALIOMWAMINI; LAKINI KWA SABABU YA MAFARISAYO HAWAKUMKIRI, WASIJE WAKATENGWA NA SINAGOGI.

43 Kwa maana walipenda utukufu wa wanadamu kuliko utukufu wa Mungu.

44 Naye Yesu akapaza sauti, akasema, Yeye aniaminiye mimi, haniamini mimi”

Na kama tunavyosoma baada ya Yule kipofu kujadiliana na wale mafarisayo kwa muda mrefu ndipo waakamua kumchukua kwa nguvu na kumtupa nje ya Sinagogi…Maskini mtu Yule akitazama wazazi wake hawakutaka kusimama upande wake japo walijua ukweli kuwa ni Yesu ndiye aliyemponya, wale majirani zake hakuweza kumtetea kwa wakati ule wakiogopa kutengwa na jamii nzima, wala mtu yeyote aliyefahamu ukweli hakudhubutu kusimama upande wake, wote walikaa kando wakiogopa kumkiri BWANA, Hivyo Yule mtu akafukuzwa asionekane tena katikati ya mikusanyiko ya waaminio iliyokuwa katika miji ile, ilikuwa bado nusu tu apigwe kwa mawe kama angeendelea kudumu eneo lile na kushindana na wale viongozi wa dini,..

Lakini tunasoma alipokuwa mwenyewe pale nje ndipo Kristo AKAMJIA. Haleluya, na kwa kuwa yeye hakuwahi kumwona uso wake hata siku moja japo alifunguliwa macho na yeye, alipokuja Bwana hakuweza hakumtambua, mpaka Bwana alipomuuliza “WEWE WAMWAMINI MWANA WA MUNGU? Ndipo Yule mtu akajibu: Ni nani, Bwana, nipate kumwamini?..Bwana akamwambia “UMEMWONA, NAYE ANAYESEMA NAWE NDIYE.” Akasema, Naamini, Bwana. Akamsujudia.

Na mwishoni Bwana akamalizia na kumwambia maneno haya..

“39 MIMI NIMEKUJA ULIMWENGUNI HUMU KWA HUKUMU, ILI WAO WASIOONA WAONE, NAO WANAOONA WAWE VIPOFU.

40 Baadhi ya Mafarisayo waliokuwapo pamoja naye wakasikia hayo, wakamwambia, Je! Sisi nasi tu vipofu?

41 Yesu akawaambia, Kama mngekuwa vipofu, msingekuwa na dhambi; lakini sasa mwasema, Twaona; basi dhambi yenu inakaa.” 

Kaka/dada inawezekana Bwana alishakufungua katika vifungo vyako kule “KWA ALIYETUMWA (SILOAMU)”..Siloamu wako anaweza akawa mchungaji Fulani, mtumishi Fulani, huduma Fulani vyovyote vile. Inawezekana ulipokwenda ulipokea majibu ya maombi yako uliyokuwa umemwomba Mungu siku nyingi, ulipokwenda uliponywa, ulipokwenda ulifunguliwa, ulipokwenda upata kile ulichokuwa unakihitaji kwa muda mrefu..Lakini je! Ni KWELI ULIKUTANA NA KRISTO?. ULIUONA USO WAKE?

Yule kipofu japo alifanyiwa muujiza mkubwa kama ule lakini hakuwahi kumjua Kristo, wala kumwona sura yake..Lakini baada ya kuanza kumkiri tu na kuichagua ile njia ILIYOOGOPWA NA WENGI, iliyokuwa ya hatari ya kujikana maisha kwa ajili ya jina lake. Ndipo alipokwenda kukutana na YESU uso kwa uso kule nje! Na kumfahamu vizuri yeye ni nani. Unadhani alishindwa kumkana kusema tu vile ili kuwaridhisha mafarisayo. Hakushindwa lakini alitaka kutafuta kitu kilicho bora zaidi ya aliyotendewa, Alipotengwa kando ndipo Yesu akamjia.

Ni wengi leo hii, wanadai wamemwona Mungu katika maisha yao kisa tu wamefanikishwa katika mambo yao na shughuli zao. Lakini ukiyatazama maisha yao je ni kweli wameiendea njia ya msalaba, ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba wako kwa ajili ya Kristo, na kuamua kuishi maisha matakatifu, utagundua hawajafanya hivyo na bado wanadai wamemwona Mungu.

Wanaogopa wakijaribu kufanya hivyo watatengwa na wazazi wao, wanaogopa kudharauliwa na marafiki zao, wanaogopa kuonekana ni watu wa ajabu washamba, wakiogopwa kuchukiwa na watu wa ulimwengu huu… Hawajui kuwa kule kufanikiwa kwao ilikuwa ni kwa ajili ya kulikiri jina la Kristo kwa maisha yao na si kwa midomo tu. Na pia ni kwa ajili ya wao kujitengenezea njia nzuri ya kwenda kukutana na Kristo lakini wao wanaikwepa. Dada/Kaka Kristo anapatikana katika njia iliyokataliwa, hapatikani kwa  wakuu wa dini,wala wa madhehebu anapatikana nje kule mahali palipokataliwa..Yule kipofu hakukutana na Kristo alipokuwa na wale mafarisayo, na wakuu wa dini, hapana badala yake alikutana na Yesu mahali ambapo hata yeye mwenyewe hakutarajia, mahali walipokuwa wamemtenga.

Kumbuka Kristo leo hii ametupwa nje na ulimwengu, Na ndio maana anasema Ufunuo 20: 20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.

Ili uwe na mahusiano binafsi na YESU katika maisha yako ni lazima uchukue uamuzi wa kujitwika msalaba wako na kumfuata.

Ni wale tu watakaokubali kutupwa na wao nje ndio watakaokutana na Kristo huko vinginevyo utabakia kumsikia tu, haijalishi ni kwa namna gani utakuponya magonjwa yako, haijalishi ni kwa namna gani atakufanikisha katika biashara zako, haijalishi ni kwa namna gani atakukirimia mahitaji yako. Kama hutakubali kutupwa nje na ulimwengu kwa ajili ya jina lake, hutakaa UMWONE YESU KAMWE!

Ndio maana sehemu nyingine Bwana Yesu anajulikana kama JIWE KUU LA PEMBENI ambalo limekataliwa na waashi wengi. Kristo hapatikani kwa Padre, kwa Mchungaji, kwa Papa, kwa Watumishi, au kwa mtu yoyote anayejiita Mtu wa Mungu.. Kristo anapatikana mahali palipokataliwa na Ulimwengu..Mahali penye njia nyembamba.. 

Luka 13: 22 “Naye alikuwa akipita katika miji na vijiji, akifundisha, katika safari yake kwenda Yerusalemu. 

23 Mtu mmoja akamwuliza, Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache? Akawaambia, 

24 JITAHIDINI KUINGIA KATIKA MLANGO ULIO MWEMBAMBA, KWA MAANA NAWAAMBIA YA KWAMBA WENGI WATATAKA KUINGIA, WASIWEZE”.

Njia ni nyembamba ndugu iendayo uzimani..Tujitahidi uipite hiyo sasa, kabla Mlango wa Neema haujafungwa, kwa kumwamini Yesu Kristo, Mkuu wa Uzima, na MSHIKAJI WA MAMLAKA YOTE, Kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na Kwa Jina lake, na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Bwana akubariki sana.Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA.

NJIA YA MSALABA

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.


Rudi Nyumbani

Print this post

JE! UNAMPENDA BWANA?

Bwana Yesu alisema “MTU AKINIPENDA  ATAZISHIKA AMRI ZANGU (Yohana 14:15)” lakini tunaona hiyo pekee haitoshi kwasababu kama  ingekuwa inatosha Bwana asingemwambia tena Mtume Petro mahali pengine  maneno haya…

Yohana 21:15 “ Basi walipokwisha kula, Yesu akamwambia Simoni Petro, Je! Simoni wa Yohana, wewe wanipenda kuliko hawa? Akamwambia , Naam ,Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Lisha wana-kondoo wangu.
16 Akamwambia tena mara ya pili, Simoni wa Yohana, wanipenda? Akamwambia, Ndiyo, Bwana, wewe wajua kuwa nakupenda. Akamwambia, Chunga kondoo zangu.
17 Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu.

Kwahiyo tunaona licha ya kuzishika amri zake, kuna mambo mengine matatu ya yatakayokamilisha upendo wetu kwa Kristo.  Nayo ni (1) KULISHA WANA-KONDOO WAKE, (2) KUCHUNGA KONDOO ZAKE (3) KULISHA KONDOO ZAKE.

KUZISHIKA AMRI:

Kuzishika Amri za Mungu ni kuzielewa, kuzipenda na kuziishi, na sio kuzikariri  na yeyote aziishie amri za Mungu  amri hizo zinapaswa zisiwe nzito kwake, Maagizo ya Mungu yanapaswa yawe ni mepesi kwake kuyashika kwasababu Roho wa Mungu anakaa ndani yake, hivyo Nira ya Kristo kwake inakuwa ni laini, na mzigo unakuwa mwepesi,hajisikii uzito wala hajilazimishi kuzitimiza sheria za Kristo ndani yake..

Hatatumia nguvu nyingi kujizuia kutenda dhambi, hivyo anakuwa anazitimiza pasipo kujiweka katika utumwa, hawi chini ya utumwa wa sheria, kwasababu Nia ya Mungu sio sheria zake ziwe mzigo mzito kwetu, nia yake sio tuzishike amri zake kwa uchungu na mateso na utumwa ..hapana na ndio maana alisema katika..

Kumbukumbu 30: 10 “ukiwa utaifuata sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa kuyashika maagizo yake, na AMRI ZAKE zilizoandikwa katika chuo hiki cha torati; ukimwelekea Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote.

11 Kwa maana maagizo haya nikuagizayo leo, SI MAZITO MNO KWAKO, WALA SI MBALI.

12 Si mbinguni, hata useme, Ni nani atakayetupandia mbinguni akatuletee, aje atuambie tusikie, tupate kuyafanya?

13 Wala si ng’ambo ya pili ya bahari, hata useme, Ni nani atakayetuvukia bahari, akatuletee, aje atuambie, tusikie, tupate kuyafanya?

Unaona ili kuzishika Amri za Mungu,  ni lazima Kuwepo na wepesi ndani yako ambao Mungu ameuweka, ili Sheria zake zisiwe nzito mno kwako. Hivyo kwa kuishi maisha kama hayo ya kutimiza sheria za Mungu pasipo utumwa. Huko ndiko kuzishika Amri za Mungu. Na huko ndiko kumpenda Bwana. Lakini kufanya hivyo pekee hakutoshi kuonyesha upendo wetu kwa Bwana. Lipo jambo lingine la ziada la kufanya ili kutimiza upendo wetu kwake.

Na jambo hilo si lingine zaidi ya kulitazama kundi la Mungu kwa kulilisha na kulichunga.Ndio maana Bwana alimwuliza Petro mara tatu swali lile lile? Je! wanipenda?

 NINI MAANA YA KULISHA KONDOO WAKE:

Kama neno lenyewe lilivyo “kondoo wake”  ikiwa na maana kuwa sio kondoo wa mtu Fulani, bali ni kondoo wa Kristo. Hivyo mtu hawezi kujiamulia tu, njia au namna ya kuwalisha,  kwa lugha nyingine Petro aliambiwa yeye ni  mchungaji aliyeajiriwa kuwachunga na kuwalisha kondoo, hivyo kondoo hata mmoja asipolishwa inavyopaswa ataulizwa na aliyemwajiri, kwasababu kondoo sio wake, bali ni wa mtu mwingine.

Kondoo wanawakilisha watu wa Kristo waliomwamini yeye, na wachache wanaohitaji kumwamini.. hao ndio kondoo wa Kristo, biblia inasema tuwalishe hao, na chakula chao sio nyasi bali ni NENO LA MUNGU lisilochanganywa na chochote..  Kazi kubwa ya mchungaji ni kwenda huku na huko kutafuta mahali penye nyasi zinazowafaa kondoo.. Kadhalika Sisi kama wakristo tuliookolewa tunalo jukumu la kuwaongoza wenzetu, au kuongozana sisi kwa sisi mahali panapopatikana Neno la Uzima.

Ukimwona ndugu yako anahangaika huku na kule, ni wajibu wako kama mkristo kumwelekeza kwa upendo mahali ambapo anaweza kuishibisha nafsi penye Neno la Uzima. Huko ndiko kumpenda Kristo. Maadamu ndani yetu kuna nuru kidogo ambayo haimo ndani yao.

KUCHUNGA KONDOO WAKE.

Kama neno lilivyo “kondoo wake” ikiwa na maana kuwa “sio kondoo wa  mtu fulani” bali ni kondoo wa Yesu Kristo, hivyo hatuwezi kujichagulia njia ya kuwachunga..Tunapokea maagizo kutoka kwake namna ya kuwachunga.

Sasa Bwana Yesu alisema “Tujihadhari na mbwa mwitu wakali” na pia alisema “tujihadhari na mbwa mwitu wanaokuja na mavazi ya kondoo”…Sasa dhumuni la mbwa mwitu kuvaa mavazi ya kondoo ni ili na yeye aonekane kama kondoo ili asitumie nguvu nyingi kuwakamata kondoo. Sasa hao Bwana ndio aliosema tujichunge nao sana, na tukiisha kujihadhari nao, tuwachunge na ndugu zetu dhidi yao.. HUKO NDIKO KUCHUNGA KONDOO WAKE.

Sasa hawa mbwa-mwitu ndani ya mavazi ya kondoo ni wakina nani?

Mathayo 7: 15 “Jihadharini na manabii wa uongo, WATU WANAOWAJIA WAMEVAA MAVAZI YA KONDOO, WALAKINI KWA NDANI NI MBWA-MWITU WAKALI. Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?”

Unaona, Manabii wa uongo ndio mbwa-mwitu ndani ya mavazi ya kondoo.  Na manabii wa uongo sio tu manabii, hapana bali hata waalimu wa uongo, wachungaji wa uongo, watumishi wa uongo, wainjilisti wa uongo, maaskofu wa uongo, mashemasi wa uongo, wapendwa wa uongo, waimbaji wa uongo n.k hawa wote kwa pamoja wanaunda kundi linalojulikana kama manabii wa uongo.

Yaani watu wote ambao kwa nje wanajulikana kama ni wakristo lakini ndani katika maisha yao ya siri sio wakristo hata kidogo, ni watu wa ulimwengu huu, walevi, watukanaji, vuguvugu, waasherati, walaji rushwa n.k…Na bado wanahubiri na kushuhudia na kuimba. Wengine wanajiita PAPA wakiwapoteza watu waabudu sanamu Mungu alizozikataa.Hiyo ndio roho  ya mpinga-kristo.

Hao ndio Bwana, aliotuonya tulichunge kundi lake dhidi yao, ikiwa tumeona mtu ajiitaye mkristo halafu ni mwasherati au mlevi au mwabudu sanamu,tunapaswa tujihadhari naye Hatupaswi kuwashauri watoto wa kiroho(kondoo wa Kristo) kuambatana nao, ni lazima tutawachunga kondoo wa Mungu dhidi yao..Na zaidi ya yote tutawafundisha hila za hao manabii wa uongo, na Roho ya Mpinga Kristo inavyotenda kazi, Biblia inasema

1Wakoritho 5: 9 “Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi.

10 Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang’anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia.

11 Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba MSICHANGAMANE NA MTU AITWAYE NDUGU, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.

12 Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani?

13 Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu. NINYI MWONDOENI YULE MBAYA MIONGONI MWENU.”

Hivyo tunapoona ndugu yetu, anapotea na uongo wa adui ni jukumu letu sisi,  kumwokoa, hatuwezi tukasema tunampenda Kristo na tukaacha kulipenda na kundi lake, Popote pale tulipo katika hatua yoyote ile ya kiroho, ni wajibu wetu kuwasaidia walio chini yetu..

Hata katika familia jukumu la kulea watoto sio la wazazi peke yake, lakini utakuja kukuta kwamba hata watoto wana jukumu la kuleana wao kwa wao..kaka au dada anawalea wadogo zake na hao wadogo wanawalea walio wadogo zaidi. Na katika familia ya Mungu ni hivyo hivyo, ndio jukumu tulilopewa kulishana na kuchungana.

Kuchunga kondoo wa Kristo sio jukumu la mchungaji kanisani tu au muhubiri bali ni jukumu la Kila Mkristo.

Bwana atusaidie sote tuweze kumpenda yeye kweli kweli, KWA KUZISHIKA AMRI ZAKE na KULICHUNGA KUNDI dhidi ya mbwa mwitu wakali lake na KULILISHA chakula cha Neno la Uzima.

Mungu akubariki.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine…

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MAFUNUO YA ROHO.

ITAFAKARI VEMA KAZI YA MUNGU

SADAKA ILIYOKUBALIKA.

JE! MUNGU ATAIANGAMIZA DUNIA TENA BAADA YA GHARIKA YA NUHU?

MANENO HAYA YANA MAANA GANI? “..KWA SABABU HAMTOI ROHO KWA KIPIMO. (YOHANA3:34)”

NI KWA JINSI GANI MUNGU ANAPATILIZA MAOVU YA BABA ZETU SAWASAWA NA KUTOKA 20:5-6?

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.


Rudi Nyumbani

Print this post