Swali: Kati ya Simoni Petro na Mariamu Magdalene ni yupi aliyekuwa wa kwanza kutokewa na Bwana YESU baada ya kufufuka kwake?, kwa maana katika Luka 24:34 tunasoma kuwa ni Simoni ndiye wa kwanza kutokewa na Bwana, lakini tukirudi katika Marko 16:9 tunaona ni Mariamu Magdalene je hii imekaaje?.
Jibu: Turee mistari hiyo..
Luka 24:33 “Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao,
34 wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, NAYE AMEMTOKEA SIMONI”.
Hapa tunaona anatajwa Simoni, lakini turejee Marko 16:9..
Marko 16:9 “Naye alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, ALIMTOKEA KWANZA MARIAMU MAGDALENE, ambaye kwamba alimtoa pepo saba.
10 Huyo akashika njia akawapasha habari wale waliokuwa pamoja naye, nao wakali wanaomboleza na kulia”.
Hapa tunasoma ni Mariamu Magdalena ndiye aliyetokewa kwanza, sasa swali ni yupi aliye sahihi au biblia inajichanganya?..
Jibu ni La! Biblia haijichanganyi na wala haina kasoro yoyote… Sasa kama ni hivyo ni nani aliyetokewa wa kwanza?
Jibu, aliyetokewa wa kwanza na Bwana YESU alikuwa ni MARIAMU MAGDALENE, kama maandiko yanavyoonyesha hapo juu (Marko 16:9).. huyu ndiye aliyekuwa wa kwanza kumwona Bwana kwani baada tu ya kukuta jiwe limeviringishwa mbali na kaburi aliondoka na kwenda kuwafuata akina Petro kuwapasha yaliyojiri, na Petro pamoja na Yohana walipokwenda kaburini kuhakiki hizo taarifa za Magdalene, walikuta tu vitambaa vya sanda, na walipoondoka ndipo Bwana YESU akamtokea Mariamu Magdalene kama mtu wa kwanza (na saa hiyo akina Petro wameshaondoka).
Yohana 20:1 “Hata siku ya kwanza ya juma Mariamu Magdalene alikwenda kaburini alfajiri, kungali giza bado; akaliona lile jiwe limeondolewa kaburini.
2 Basi akaenda mbio, akafika kwa Simoni Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, Wamemwondoa Bwana kaburini, wala hatujui walikomweka.
3 Basi Petro akatoka, na yule mwanafunzi mwingine, wakashika njia kwenda kaburini.
4 Wakaenda mbio wote wawili; na yule mwanafunzi mwingine akaenda mbio upesi kuliko Petro, akawa wa kwanza kufika kaburini.
5 Akainama na kuchungulia, akaona vitambaa vya sanda vimelala; lakini hakuingia.
6 Basi akaja na Simoni Petro, akaingia ndani ya kaburi; akavitazama vitambaa vilivyolala,
7 na ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezongwa-zongwa mbali mahali pa peke yake.
8 Basi ndipo alipoingia naye yule mwanafunzi mwingine aliyekuwa wa kwanza wa kufika kaburini, akaona na kuamini.
9 Kwa maana hawajalifahamu bado andiko, ya kwamba imempasa kufufuka.
10 Basi wale wanafunzi wakaenda zao tena nyumbani kwao.
11 Lakini Mariamu alikuwa akisimama karibu na kaburi, nje yake, analia. Basi akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi.
12 Akaona malaika wawili, wenye mavazi meupe, wameketi, mmoja kichwani na mmoja miguuni, hapo ulipolazwa mwili wake Yesu.
13 Nao wakamwambia, Mama, unalilia nini? Akawaambia, Kwa sababu wamemwondoa Bwana wangu, wala mimi sijui walikomweka.
14 Naye akiisha kusema hayo, akageuka nyuma, akamwona Yesu amesimama, asijue ya kuwa ni Yesu.
15 Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa.
16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu)”.
Hivyo baada ya kumtokea Mariamu Magdalena ndipo akamtokea Simoni Petro, katika tukio ambalo halijarekodiwa katika Biblia.
Kwahiyo Simoni Petro alikuwa ni Mtume wa kwanza kutokewa na Bwana YESU lakini si mtu wa kwanza, aliyekuwa wa kwanza ni Mariamu Magdalena na Simoni Petro anasimama kuwa wa kwanza kati ya Mitume wa Bwana.
Mtume Paulo analiweka hilo vizuri zaidi..
1Wakorintho 15:4 “na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko;
5 na ya kuwa ALIMTOKEA KEFA; tena na wale Thenashara;
6 baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi hata sasa, ila baadhi yao wamelala;
7 baadaye akamtokea Yakobo; tena na mitume wote;
8 na mwisho wa watu wote, alinitokea mimi, kama ni mtu aliyezaliwa si kwa wakati wake”.
Je umempokea YESU?.. Unao uhakika wa kwenda naye mawinguni atakaporudi?… fahamu kuwa tunaishi majira ya siku za mwisho, siku yoyote parapanda ya mwisho inalia na wafu waliokufa katika Kristo watafufuliwa kuungana na walio hai katika Kristo na kunyakuliwa juu, je utakuwa wapi siku hiyo?, ikiwa leo habari ya msalaba kwako ni upuuzi mtupu!.
Neema ya Bwana YESU itusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mariamu Magdalene ni nani. Na hilo jina amelitolea wapi?
MAMBO YA KUJIFUNZA KWA KLOPA NA MKE WAKE!
Nyongeza ya majina ya watu katika biblia
Jina la Mwokozi YESU libarikiwe.
Wakati Fulani Bwana YESU aliuona “Mtini” (yaani mti unaozaa matuna aina ya Tini) usio na matunda na matokeo yake aliulaani.
Mathayo 21:18 “Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa.
19 Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; AKAUAMBIA, YASIPATIKANE MATUNDA KWAKO TANGU LEO HATA MILELE. MTINI UKANYAUKA MARA.
20 Wanafunzi walipoona, walistaajabu, wakisema, Jinsi gani mtini umenyauka mara?”
Sasa ukifuatilia vizuri hii habari utaweza kufikiri kwamba Bwana YESU alikuwa anaweza kuwa amekosea kuulani.., kwani ule mtini haukuwa msimu wake wa kuzaa matunda…
Hata wewe ukienda kutafuta machungwa kwenye mchungwa nje na msimu wake ni wazi kuwa hutashangazwa pale utakapokuta ule mchungwa hauna tunda lolote.Zaidi sana utashangazwa kama endapo umefika msimu halafu hukukuta machungwa.. Lakini sasa tunasoma Bwana YESU ilikuwa kinyume chake alijua kabisa si msimu wake Mtini kuzaa lakini aliulaani hivyo hivyo.
Sasa kwanini aulaani??
Sababu zipo nyingi, lakini hii yaweza kuwa kuu kuliko zote… ULE MTINI ULIONYESHA SIFA ZOTE ZA NJE KUWA NA MATUNDA lakini haukuwa na matunda! (Maana yake ulikuwa unahubiri udanganyifu).
Unaonaje umewekewa bahasha tatu mbele yako, halafu kati ya hizo bahasha tatu mbili zinaonekana kabisa kwa macho kuwa ndani hazina kitu, lakini moja inaonekana imetuna (kana kwamba ina fedha), halafu unaichagua hiyo iliyotuna kisha ndani unakuta hamna kitu, bila shaka utakwazika na unaweza ukaichana ile bahasha, ili isiendelee kudanganya wengine.
Vivyo hivyo Kristo alijua kabisa ule si wakati wa Tini kwani mitini mingine yote ilikuwa na sifa zinazofanana kwa wakati huo, lakini ajabu ni kwamba huu Mtini mmoja ulikuwa na mwonekano wa tofauti kana kwamba unao matunda, pengine wakati mitini mingine ilikuwa imekauka inapukutisha huu ulikuwa na majani mabichi, ulikuwa unahubiri udanganyifu kwamba unao matunda na kumbe hauna, na ili kuondoa udanganyifu huo suluhisho ni kukatwa/kulaaniwa.
Naam na maisha ya wakristo wengi yamejaa UDANGANYIFU, ni kama wanasifa zote za kuitwa wakristo lakini ukichunguza kwa undani hawana matunda!. Kwa nje wana majina ya kikristo, ni wahubiri, wana biblia nzuri na kubwa, wana nafasi katika kanisa, lakini ndani si wakristo, hawana matunda!, ni watu vuguvugu wale Bwana aliosema atawatapika katika Ufunuo..
Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.
16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi”.
Toka katika uvuguvugu, ili kuepuka laana ya KRISTO, kama umekusudia kuwa Moto, kuwa Moto mpendwa, kama umeamua kuchagua baridi maandiko yanasema ni heri uwe baridi kabisa kuliko kuwa hapo katikati, vuguvugu..
Bwana YESU atusaidie sana.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tafsiri ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;
Je Bwana YESU alipanda mlimani na wanafunzi wake baada ya siku sita au nane?
MWISHO WA MAVUNO, NI MWISHO WA DUNIA.
Biblia unapozungumzia kuhusu kupewa jina jipya inamaanisha nini?
Jina kuu la BWANA WETU YESU KRISTO Libarikiwe, karibu tuyatafakari maandiko.
Endapo akitokea mtu faulani mkuu sana na kujigeuza na kujifanya mtumwa, na kuvaa nguo za chini ya hadhi yake, mtu huyo ni rahisi kupitia dharau kama watu wengine wa hadhi za chini, na kejeli, na hata kupitia mateso na kukataliwa….lakini laiti watu wanaomdharau wangemjua kwa undani ni mtu wa namna gani, hakuna hata mmoja angeonyesha kejeli au dharau!.. wote wangemheshimu na kumwogopa!.
Ni hivyo hivyo kwa Bwana YESU, walimsulibisha lakini hawakujua yeye ni nani, walidhani ni mwalifu tu, au mfano tu wa manabii wengine waliopita, kumbe! Hawakujua kuwa ni ALFA na OMEGA mwenyewe!. Naam hata mimi pengine ningekuwepo kipindi hiko, ningefanya hapo hayo! Kwasababu wanadamu sisi ni wale wale hatuna jipya!.
1Wakorintho 2:7 “bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;
8 ambayo wenye kuitawala dunia hii hawaijui hata mmoja; maana kama wangaliijua, wasingalimsulibisha Bwana wa utukufu”.
Baada ya kuyatafakari hayo..hebu shika biblia yako ufuatilia maandiko yafuatayo maana leo utajua ya kwamba YESU KRISTO ni MUNGU mwenyewe katika MWILI wa kibinadamu!!?..na si mtu wa kawaida!.
Sasa si kwamba ukiishia kuamini tu ni Mwana wa MUNGU utakuwa umepotea!..la ni sahihi na ndio msingi!, lakini zaidi ya hapo, YESU ni zaidi ya tunavyomfikiria, ni jambo gumu kulielewa lakini unapolielewa linakuwa ni tamu na zuri..
Hebu tuyapeleleze maandiko kidogo kumhusu yeye katika kitabu cha Ufunuo..
Ufunuo 1:8 “Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi”.
Hapa MUNGU aliyeumba Mbingu na Nchi anajitambulisha kama Alfa na Omega!.. hapana shaka juu ya hilo, lakini hebu tuendelee mbele kidogo kumsoma huyu Alfa na Omega anaendelea kusemaje…
Ufunuo 21:5 “Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.
6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. MIMI NI ALFA NA OMEGA, MWANZO NA MWISHO. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.
7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu”.
Hapa tena huyu MUNGU wa mbingu na nchi ambaye ndiye ALFA na OMEGA, (yaani mwanzo na mwisho) anasema atayafanya yote kuwa mapya na atampa kila mwenye kiu ya maji ya uzima bure!.. Bila shaka hiyo ni karama ya MUNGU na njema sana… Lakini hebu tusogee tena mbele tumwone huyu ALFA na OMEGA anasema nini tena na anajizungumziaje..hapa ndipo tutashangaa!!.
Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
13 MIMI NI ALFA NA OMEGA, MWANZO NA MWISHO, WA KWANZA NA WA MWISHO.
14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.
15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.
16 MIMI YESU NIMEMTUMA MALAIKA WANGU kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi”.
Mstari wa 12 unaosema “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami,” na ule wa 16 unaosema “MIMI YESU NIMEMTUMA MALAIKA WANGU kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa.”… Mistari hii inatupa uzito kuendelea kumfikri YESU kama mtu wa kawaida, lakini inatulazimisha kumfikiri kama ALFA na OMEGA, kwamaana ndivyo alivyojitambulisha hapo.
Oo kumbe! YESU ni Alfa na Omega, na ndiye Mungu mwenyezi katika umbile la kibinadamu, sasa tunaelewa kwanini Mtume Paulo alisema siri ya UTAUWA (yaani Uungu) ni KUU, kwamba MUNGU alidhihirishwa katika mwili..
1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.
Hayo maneno kwamba “Mungu alidhihirishwa katika mwili, na akachukuliwa juu katika utukufu” yanatufanya tufikiri mara mbili mbili kuwa YESU ni nani?.. Naam hata Bwana YESU mwenyewe kuna wakati aliwalazimisha watu kumfikiri yeye mara mbili mbili kuwa ni nani… Labda utauliza ni wapi hapo katika maandiko, twenda pamoja..
Mathayo 22:42 “Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi.
43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema,
44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako?
45 Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe?
46 Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu ye yote tangu siku ile kumwuliza neno tena”
Hawa walikuwa wanamjua Masihi (YESU) kama mwana wa Daudi, na ni kweli maandiko yamesema hivyo, lakini sasa inakuwaje Daudi amwite Masihi kama Bwana wake na wakati huo huo awe mtoto wake??.. hata mimi ningeulizwa hilo swali, ningekwama!..
Maana yake kuna siri nyingine katika YESU tusizozijua, ambazo ukisoma maandiko kwa makini na kwa msaada wa Roho Mtakatifu utaziona!..
Sasa si dhambi kujua kama YESU ni mwana wa Daudi peke yake, wala si kosa kutambua kuwa ni Mwana wa MUNGU peke yake, na hiyo haiwezi kumtolea mtu tiketi ya kuingia mbinguni, lakini maandiko yanathibitisha kuwa YESU KRISTO ni zaidi ya tunavyomjua au kumfikiri, kama YEYE ni MUNGU MWENYEWE KATIKA MWILI..NUKTA KUBWA!!!.
Huenda Lugha zetu za duniani na udhaifu wetu wa kufikiri unakuwa ni mgumu kupokea hilo!, lakini huo ndio ukweli na ni lazima tuupokee, kama tu ilivyo ngumu kufikiri na kupokea kwamba inakuwaje MUNGU hana mwanzo!.. hapo ukifikiri sana unakwama!, lakini unaamini hivyo hivyo kwasababu yeye ni MUNGU, vile vile kuhusu UUNGU wa YESU usiumize kichwa kutafuta kulifanya lieleweke kichwani mwako sasa, labda tutaelewa vizuri baada ya maisha haya, lakini hatuna budi kuamini hilo!.
Na kumwelewa YESU namna hii inatufanya tusiuchezee Wokovu wetu, maana hatujakombolewa na damu ya mtu, wala myahudi bali ya MUNGU mwenyewe!.
Kwa maarifa ya ziada Kuhusu Uungu wa YESU zaidi pitia Tito 2:13, na Isaya 9:6
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?
Isaya 6:1
[1]Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu.
Je unayajua makao hasaa ya Mungu?
Ni kweli tunafahamu Mungu anaketi katika kiti chake cha enzi, lakini ni kiti kilicho wapi hasaa?
Je! handakini? Mabondeni? Mapangoni? Kichakani? hasha!
Maandiko yanatueleza “Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana”
Kwahiyo na sisi lazima tuyajue makao hayo, ili tumfikie, vinginevyo tutajikuta tunaabudu Mungu mahali Ambapo kiti chake hakipo.
Katika biblia sehemu yoyote unapokutana na hili Neno “mahali pa juu”, Moja kwa moja utaona palihusishwa Na ibada..Yaani madhahabu zilijengwa pale ili kumtolea Mungu dhabihu. (1Samweli 9:12-13, 1Wafalme 3:2)
Yalikuwa ni maeneo yote yaliyoinuka mfano milimani. Kwasababu huko ndiko Mungu alikuchagua kujidhihirisha, na sio mabondeni, au mapangoni.
Ni kwanini?
Kwasababu Mungu anakaa sehemu Bora kuliko zote, sehemu iliyozidi vyote, sehemu ya juu ya juu kuliko zote. Hakai penginepo, Mungu hawekwi chini, haabudiwi mabondeni..kamwe hiyo sio sifa yake.
Hivyo ni vema ukafahamu sifa yake hii, ili tujue namna sahihi ya kumwendea.
1). Makazi:
(Mbinguni)
Kimakazi Mungu anaketi mbinguni.. Kwasababu Mbingu ni bora kuliko dunia hii.
Isaya 66:1
[1]BWANA asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?
Ndio maana tuna ujasiri na Mungu, akatie sehemu Bora zaidi ya hii, ambayo alisema atatukaribisha katika makao hayo baadaye.
Bwana Yesu alituambia tukisali tuseme Baba yetu uliye mbinguni.. (Mathayo 6:9). Hata alipoomba aliinua macho yake juu(Yoh 17:1), na sisi tumtakaripo Mungu, tuiweke picha hiyo akilini mwetu. Kwamba Baba yetu yupo mbinguni.
Na kutoka huko ndio tunatarajia mema yetu yaje, Na wenyeji wetu kushuka.(Yerusalemu mpya).
2) Viumbe.
(Mwanadamu).
Mwanadamu ametukuka kuliko viumbe vyote, amemvika uwezo na mamlaka (Zab 8:4-6). ndio maana amechagua kuketi ndani ya moyo wa mwanadamu na sio kiumbe kingine chochote. Mungu hakai ndani ya swala, au sungura, au simba.. amechagua makao yake kuwa ndani ya mwanadamu tu.
Na aliyetufungulia lango hilo ni Yesu Kristo mwokozi wetu, kama mwanadamu wa kwanza ambaye Mungu alikaa ndani yake kikamilifu. Pasipo yeye kamwe Mungu asingekaa ndani ya moyo wa mwanadamu.
Ukimkosa Kristo umemkosa Mungu ndani yako.
Hivyo wewe uliyeokoka, fahamu kuwa Mungu anakaa ndani yako, hivyo wajibu wa kujichunga sana na kumpa Mungu ibada ya kweli( Warumi 12:1)
Ndio maana anapouheshimu mwili wako umemuheshimu Mungu. Kama mwanadamu ogopa sana kujiharibu kwasababu wewe ni mahali pa juu sana palipoinuka pa Mungu.
1 Wakorintho 3:16-17
[16]Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
[17]Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.
3) Tabia
(Utakatifu)
Mungu ni mtakatifu, hivyo amechagua usafi zaidi ya uchafu, yeye ni Nuru si giza, ni mkamilifu si mwenye kasoro.
Hivyo tufahamu kuwa, tukimwendea yeye? kwa kupenda usafi? Lazima tutamwona.Lakini tukisema tunamtafuta na huku ni wachafu, hapo bado hatujamfikia Mahali pake pa juu anapoketi.
Isaya 57:15
[15]Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.
Sehemu nyingine anasema..
Zaburi 24:3-4
[3]Ni nani atakayepanda katika mlima wa BWANA? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake?
[4]Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, Wala hakuapa kwa hila.
Soma pia, Zab 15
4) Uweza:
(Imani)
Mungu si dhaifu, hivyo jambo lolote linaloonekana lina Nguvu, lililotukuka, lipitalo uwezo au ufahamu wa kibinadamu ni lake.
Ndio maana mtu anayemwendea Mungu kuomba yasiyowezekana kibinadamu, amemfikia Mungu.
Anaitwa Mungu wa miungu, Ibrahimu alimwamini Mungu kwa yasiyowezekana akawa rafiki wa Mungu, watu wote walio wa Imani ndio wanaomwona Mungu, Akiwatendea miujiza. Fahamu kuwa Mungu anavutiwa zaidi na yale yasiyowezekana Kibinadamu kuliko yale yanayowezekana..Jifunze kuishi kwa Imani, maana hapo ni mahali pake pa juu.. ondoa mashaka Ndani yako. Utamfikia Bwana hakika.
5) Ibada:
(Heshima)
Katika eneo la ibada, Mungu hafanyiwi Ibada ilimradi ibada. akiabudiwa ni lazima iwe katika Roho na kweli. Tunamtolea ibada ya juu sana..ikiwa ni sadaka Hatumpelekei kilema, bali ile ya juu zaidi, ikiwa ni sifa tunamsifu kwa nguvu zetu zote, kama Daudi,bila kujali kitu, kama ni kumtukuza Basi tunamtukuza sana na kumwadhimisha kwa viwango vyote.
Kwasababu yeye ndiye Mungu wetu astahiliye sifa zote.
Hivyo yatupasa maeneo yote hayo, tuyatambue, kisha tumwabudu kiufasaha Mahali pake pa Juu palipoinuka.
Zaburi 113:5-6
[5]Ni nani aliye mfano wa BWANA, Mungu wetu aketiye juu; [6]Anyenyekeaye kutazama, Mbinguni na duniani?
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Jina la Mwokozi wa pekee YESU KRISTO libarikiwe.
Je unajua tupo katika kipindi cha UFUFUO?.. Utauliza ufufuo gani?.. Turejee maandiko yafuatayo..
Yohana 5:25 “Amin, amin, nawaambia, SAA INAKUJA, NA SASA IPO, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai.
26 Maana kama vile Baba alivyo na uzima nafsini mwake, vivyo hivyo alimpa na Mwana kuwa na uzima nafsini mwake”.
Hapo Bwana YESU (Mkuu wa uzima) anasema “SAA INAKUJA” na “SASA IPO” Je unaielewa vizuri hii kauli?
Anaposema “Saa inakuja” maana yake kipindi Fulani cha mbeleni kinachokuja…. Na anaposema “sasa ipo” maana yake ni kipindi alichopo yeye.
Sasa swali alikuwa ana maana gani kusema vile?
SAA INAKUJA: Hiki ni kipindi cha mwisho wa dunia, (wakati wa unyakuo wa kanisa) ambapo wafu waliokufa katika Kristo watatoka makaburini na kuvikwa miili ya utukufu na kisha kumlaki Bwana mawinguni.
1Wathesalonike 4:13 “Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.
14 Maana, ikiwa twaamini ya kwamba YESU ALIKUFA AKAFUFUKA, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, MUNGU ATAWALETA PAMOJA NAYE.
15 Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.
16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; NAO WALIOKUFA KATIKA KRISTO WATAFUFULIWA KWANZA.
17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele”.
Hiko ni kipindi cha Ufufuo wa siku za mwisho ambacho yoyote aliyekufa hapaswi kukikosa..kwani si wote watakaofufuliwa na kwenda kwenye unyakuo.
NA SASA IPO: Hiki ni kipindi ambacho Bwana YESU alikuwepo duniani, ambapo watu walikuwa wanafufuliwa roho zao zilizokufa katika dhambi..
Kitendo cha kumwamini YESU na kutubu na kubatizwa ni sawa na kufufuka kutoka katika WAFU, utauliza kwa namna gani?..
Turejee kidogo ile habari ya mwana mpotevu ambaye alitapanya mali kwa maisha ya uasherati na alipozingatia kurudi kwa baba yake kutubu, baba yake alimtafsiri kama aliyekuwa amekufa na sasa amefufuka.
Luka 15:29 “Akamjibu baba yake, akasema, Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu
30 lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona.
31 Akamwambia, Mwanangu, wewe u pamoja nami sikuzote, na vyote nilivyo navyo ni vyako.
32 Tena, kufanya furaha na shangwe ilipasa, kwa kuwa huyu ndugu yako ALIKUWA AMEKUFA, NAYE AMEFUFUKA; alikuwa amepotea, naye ameonekana”.
Umeona? Si kwamba huyu kijana alikuwa amekufa kimwili, La! Bali kiroho, na alipotubu na kugeuka akahesabika kama aliyefufuka..
Je bado na wewe ni MFU na ilihali tunaishi katika SAA YA UFUFUO?.. Kumbuka usipofufuliwa sasa utu wa ndani kama huyu kijana mpotevu, hutaweza kuupata ufufuo wa siku ile ya Mwisho Bwana YESU atakaporudi, na siku hiyo imekaribia sana..
Maisha unayoishi ya dhambi ni uthibitisho wa MAUTI iliyopo ndani yako, na hiyo itaathiri hata mambo yako mengine uyafanyayo.
Fufuka leo kwa kumwamini BWANA YESU KRISTO, ili akuoshe dhambi zako kama maandiko yasemavyo..
Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza.
15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;
16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.
17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana”.
Saa ya UFUFUO Ni SASA… Saa ya Ufufuo ni Sasa, Saa ya UFUFUO NI SASA!
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nini maana ya “SAA INAKUJA” na “SASA IPO” (Yohana 4:23).
YEYE AJAYE ATAKUJA WALA HATAKAWIA.
Jina la Mwokozi YESU libarikiwe karibu tujifunze biblia.
Tabia ya kujifanya hujui na ilihali unajua ni mbaya na hatari, kwani ni sawa na kumjaribu MUNGU.. Kipo kisa kimoja kwenye biblia cha watu waliojifanya hawajui mbele ya Bwana YESU na matokeo yake hayakuwa mazuri.
Marko 11:27 “Wakafika Yerusalemu tena; hata alipokuwa akitembea hekaluni, walimwendea wakuu wa MAKUHANI, NA WAANDISHI, NA WAZEE,
28 wakamwambia, Ni kwa mamlaka gani unatenda mambo haya? Naye ni nani aliyekupa mamlaka hii uyatende haya?
29 Yesu akawaambia, Nitawauliza neno moja, nanyi mnijibu, kisha nitawaambia ni kwa mamlaka gani nayatenda haya.
30 UBATIZO WA YOHANA ULITOKA MBINGUNI, AU KWA WANADAMU? NIJIBUNI.
31 Wakasemezana wao kwa wao, wakisema, Kama tukisema, Ulitoka mbinguni, atasema, Mbona, basi, hamkumwamini?
32 Ila tukisema, Ulitoka kwa wanadamu, waliogopa watu; maana watu wote walimwona Yohana kuwa nabii halisi.
33 WAKAMJIBU YESU, WAKASEMA, HATUJUI. YESU AKAWAAMBIA, WALA MIMI SIWAAMBII NINYI NI KWA MAMLAKA GANI NAYATENDA HAYA”.
Watu hawa walikuwa wanajua kabisa ubatizo wa Yohana ulikuwa umetoka kwa MUNGU, lakini wakawa wanajifanya hawajui, na walipomwuliza Bwana YESU wakitegemea kuwa atawapa jibu la moja kwa moja, kinyume chake Bwana aliwajibu “WALA MIMI SIWAAMBII NINYI NI KWA MAMLAKA GANI NAYATENDA HAYA”.
Kwahiyo kumbe kuna maombi, au haja au dua au maulizo ambayo tunaweza kumpelekea Bwana YESU na tusipewe majibu yake!.
Ndio! kama maandiko yamesema wazi kuwa wizi ni dhambi, na tunalijua hilo hatuwezi tena kwenda tena na kumwuliza MUNGU kama kuiba ni dhambi au la! Kwani tayari tumesoma na tunajua… ukienda kumwuliza ni kumjaribu na hakuna majibu yoyote yatakayotoka..
Kama maandiko yamesema wazi kuwa uzinzi na uasherati ni dhambi, na tunajua hilo, hatuwezi tena kwenda kurudia kumuuliza MUNGU atufunulie kwenye ndoto au tuisikie sauti yake ikisema kuwa ni dhambi…hapo itakuwa ni kumjaribu.
Kama dhamiri yako inakushuhudia kabisa kuwa hilo unalolitenda, au hiko unakokivaa au unakokishikilia ni dhambi, na maandiko yamekudhihirishia wazi, huwezi tena kwenda kumwuliza MUNGU akuhakikishie, unaweza usipate majibu yoyote, na ukaishia kusema MUNGU hasikii maombi.
Sio kwamba MUNGU hasikii maombi, ni kwamba MUNGU anataka usikie kwanza Neno lake na kulitii, lililoadikwa katika kitabu chake kitakatifu BIBLIA.
Biblia ni sauti ya MUNGU isiyo na marekebisho, na iliyo ya wazi kabisa.. ukitaka kuisikia sauti ya MUNGU ya wazi kabisa, soma Biblia, wala usiende kwa mchungaji, wala askofu, wala usisubiri uote ndoto, wewe soma Biblia tu!, utapata utamsikia MUNGU.
Mwisho acha kujifanya hujui kama kuna Jehanamu, acha kujifanya hujui kuwa kuvaa kidunia ni makosa, acha kujifanya hujui kwamba ibada za sanamu ni makosa, acha kujifanya hujui kuwa matambiko na makosa, acha kujifanya hujui kuwa kuishi na mke/mume wa mtu ni dhambi!.
Usimwulize Bwana MUNGU kama pombe unazouza ni mapenzi yake au la!, na ili hali unajua kabisa pombe ni makosa, hutapata majibu yoyote, zaidi unaweza ukaisikia sauti ya shetani kinyume chake.
Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kama Kristo alizichukua dhambi zetu na kutusamehe kwanini kila siku tunatubu?.
KILA SILAHA ITAKAYOFANYIKA JUU YAKO HAITAFANIKIWA.
MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MFUNGO.
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wathesalonike wa kwanza.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI (Sehemu ya pili)
Wabadili fedha ni watu gani kwenye biblia? (Mathayo 21:21)
MGAWANYIKO WA ISHARA ZA UJIO WA BWANA YESU KRISTO.
Kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi, maana yake nini? (Zab.18:26)
Katika kanisa, Mungu aliweka huduma mbalimbali, karama mbalimbali, na utendaji kazi tofauti tofauti, ili kulikamilisha kanisa lake na kuupanda ufalme wake duniani kama alivyokusudia.
Sasa katika upande wa huduma, Mungu aliziweka huduma kuu tano, ambazo zenyewe zinasimama kama kuliongoza kanisa, kulikuza, kulichunga, ni kama nguzo za kanisa ambazo husimama wakati wote, Nao ni;
Mitume, manabii, wainjilisti, wachungaji na waalimu. (Waefeso 4:10-12)
Kwa urefu wa maelezo ya huduma hizo jinsi zinavyotenda kazi basi bofya hapa upitie >>> TOFAUTI YA MITUME, MANABII, WAINJILISTI, WACHUNGAJI NA WAALIMU NI IPI?
Lakini sambamba na hizo aliweka wengine katika kanisa, wanaoshirikiana na hawa watano (5).
Ambao ni WAZEE WA KANISA, MAASKOFU na MASHEMASI
Tuangalie kazi ya kila mmoja;
Tamaduni za kiyahudi tangu zamani walikuwa na desturi ya kuteuwa wazee (watu waliokomaa kiumri), wenye hekima na busara na uzoefu wa Kidini kufanya maamuzi na Kutoa hukumu mbalimbali katikati ya jamii ya wayahudi Soma (Kutoka 3:16, Kumbukumbu 1:9-18)
Hata baadaye kanisa lilipokuja kuanza, nyakati za mitume, tunaona bado walirithi utaratibu huo katika nafasi za kiuongozi ndani ya kanisa. Isipokuwa haikuhitaji awe ni lazima mzee Kiumri, lakini ni lazima Awe amekomaa Kiroho.
Nafasi hii hasaa iliwahusu wanaume, Kwasababu katika nyaraka za mitume hatuoni mahali popote kama kuna mfano wa mwanamke aliyeteuliwa kuwa mzee wa kanisa.
Ukisoma Tito 1:6, inaeleza sifa zao, anasema wazee wawe waume wa mke mmoja..
Tito 1:5-6
[5]Kwa sababu hii nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru;
[6]ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii.
(Matendo 14:23)
Zingatia: Hii haiwafanyi wanawake wasiwe na kazi yoyote katika kanisa hapana, wanaweza kusimama kama huduma-kivuli ambazo zaweza Kuonekana kama za wazee wa kanisa, waalimu, mashemasi, kama wasaidizi wenye huduma hizo, lakini sio rasmi kwao. Mfano wa hawa kwenye biblia walikuwa ni akina Fibi, prisila,
KAZI ZA WAZEE WA KANISA:
1). Kulichunga kundi,
Matendo 20:28
Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.
(Soma pia 1Petro 5:1-4)
ii) Kufundisha vema watu.
1 Timotheo 5:17
[17]Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha.
Tito 1:9
[9]akilishika lile neno la imani vile vile kama alivyofundishwa, apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga.
iii) Kutatua migogoro ya kiimani ndani ya kanisa.
Utakumbuka wakati ule makanisa ya mataifa yalikuwa yakitaabishwa, na wayahudi juu ya kushika torati, hivyo kukatokea mkanganyiko mkubwa, na kuwalazimu wawafuate wazee kule Yerusalemu ili walitatue tatizo hilo, na kama tunavyosoma baada ya hoja nyingi, walifikia hitimisho sahihi la Roho Mtakatifu.
Matendo 15:6 Mitume na wazee wakakusanyika wapate kulifikiri neno hilo.
7 Na baada ya hoja nyingi Petro akasimama, akawaambia, Ndugu zangu, ninyi mnajua ya kuwa tangu siku za kwanza Mungu alichagua miongoni mwenu ya kwamba Mataifa walisikie neno la Injili kwa kinywa changu, na kuliamini
iv) Kuwaombea wagonjwa.
Yakobo 5:14-15
[14]Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.
[15]Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.
2) MAASKOFU.
Maana ya Askofu ni mwangalizi.
Kazi yake kubwa ni kuliangalia kanisa,/ kulisimamia, mfano kusimamia malengo ya kikanisa, kulinda fundisho, na kusimamia uchungaji ulio bora.
Japokuwa mahali pengine maaskofu wanatajwa kama wazee wa kanisa. (Tito 1:5-9).
Lakini tofauti yao hasaa ni kwamba wazee wanayasimamia makanisa madogo madogo, lakini maaskofu ni waangalizi wa makanisa (yote/baadhi), Wazee wanaweza kuwa wengi, lakini maaskofu ni cheo, cha uangalizi hivyo aweza kuwa mmoja au wachache, wazee wanaweza kuwa na wajibu wa kufundisha, na kuchunga, lakini maaskofu hasaa katika kuongoza. Vilevile kwenye maandiko hatuoni mahali popote nafasi hii ikihusisha wanawake.
Sifa za maaskofu na wazee, wa kanisa zinafanana.
Sifa za mtu kuwa mzee wa kanisa. (Tito 1:5-9, 1Timotheo 3:1-7)
3) MASHEMASI.
Mashemasi ni mtumishi wa kanisa. Huduma hii ilitokea katika kanisa kwa mara ya kwanza, mitume walipokuwa wanahudumu na kuona kuwa baadhi ya mapungufu kwamba wajane wanasahaulika katika huduma ya kila siku, ndipo ikalazimika wateue watu saba, ndani ya kanisa watakaoweza kusimamia mambo yote ya kimahitaji ya kundi. (Matendo 6:1-7), mmojawapo alikuwa ni Stefano.
Kazi za mashemasi:
i) Kulihudumia kundi katika masuala ya mahitaji ya mwilini ya kundi:
Hususani kwa maskini, wajane, wenye mahitaji, mayatima.
ii) Kuongoza kwa mifano:
Lazima wawe kipaumbele kitabia, uaminifu, na nidhamu Na kuonyesha roho ya kiutumishi
iii) Kusimamia shughuli za kikanisa:
Ujenzi, taratibu za kiibada na mikutano, kusimamia hazina na mali za kanisa.
Sifa za mtu kuwa shemasi:
Zinatajwa kwenye 1Timotheo 3:8
1Timotheo 3:8 Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana,si watu wanaotamani fedha ya aibu.
9 wakiishika siri ya imani katika dhamiri safi. 10 Hawa pia na wajaribiwe kwanza; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia.
11 Vivyo hivyo wake zao na wawe wastahivu; si wasingiziaji; watu wa kiasi, waaminifu katika mambo yote.
12 Mashemasi na wawe waume wa mke mmoja, wakiwasimamia watoto wao vizuri, na nyumba zao.
13 Kwa maana watendao vema kazi ya shemasi hujipatia daraja nzuri, na ujasiri mwingi katika imani iliyo katika Kristo Yesu
Hivyo wazee, maaskofu na mashemasi, ni nguzo muhimu za kulifanya kanisa kusimama, katika nidhamu ya kitabia na kimapokeo, pamoja na kihuduma.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?
Maombi ya shabaha kwaajili ya Kazi/kibarua/shughuli/biashara/elimu.
UTANGULIZI: Ni muhimu kujua hili: lengo kuu au kiini cha Wokovu ulioletwa na BWANA YESU KRISTO sio sisi tuwe matajiri au tupate mafanikio ya huu ulimwengu!.
Mafanikio ya dunia hii ni moja ya faida za mwisho mwisho kabisa za kusudi la msalaba wa Bwana YESU kwasababuwalikuwepomatajiri kabla ya Bwana YESU kuja duniani, hivyo KRISTO asingeweza kuja kutegua mtego aukutatua tatizo ambalo lilishatatuliwa huko nyuma.
Ingekuwa lengo lake ni ili tufanikiwe tuwe matajiri, angetuambia tu tusikilize hekima za Sulemani na tungefanikiwa, hakukuwa na haja ya kuja kumwaga damu yake.
Lakini suala la ondoleo la dhambi hilo halikuwahi kufanyika huko nyuma, hakuna aliyewahi kuondolewa dhambi, kwani dhambi zilikuwa zinafunikwa tu! (Soma Waebrani 10:3-4)..
Sasa hiko ambacho kilishindikana kutendeka huko nyuma (katika Agano la kale) ndicho kilichokuwa cha kwanza na cha msingi kilichomleta BWANA YESU duniani, na kitu hiko si kingine zaidi ya ONDOLEO LA DHAMBI.…kiasi kwamba mtu akikosa ondoleo la dhambi hata awe na vitu vyote ulimwenguni bado anayo hasara kubwa soma (Mathayo 16:26).
Kwahiyo ni muhimu kujua msingi huu, ili tunapokwenda kujifunza juu ya MAOMBI JUU YA KAZI au BIASHARA, Usiweke moyo wako wote huko!.. Yatumie tu maarifa haya kama sehemu ya maisha, lakini jali zaidi hatima ya roho yako, kupitia damu ya YESU na UTAKATIFU.
Sasa tukirudi katika kiini cha somo!.. Ikiwa unafanya kazi za mikono, labda tuseme biashara, tumia kanuni hii ya Maombi kupata FAIDA YA KILE UNACHOKIFANYA!!.
Badala ya kuombea bidhaa zako, kama sabuni unazouza, au dawa unazouza, au kingine chochote kwamba kiwe na mvuto, kuanzia leo punguza kuomba maombi ya namna hiyo, badala yake omba maombi yafuatayo.
– Kila mteja anayekuja kwako mwombe neema ya Wokovu, ikiwa bado hajampokea YESU, maombi ya namna hiyo yanamtoa yule mtu kutoka katika vifungo vya ibilisi na hatimaye kumfungua kabisa, na anapofunguliwa aweza kuwa mteja wako wa ajabu sana, au akawaleta na wengine wengi mahali ulipo.
– Ikiwa tayari ameshampokea YESU mwombee azidi kusimama katika imani, na mwombee akawe Nuru kwa wengine wengi, ombea na familia yake kama unaijua, hiyo ndio njia bora ya kuombea kazi yako au biashara yako..
– Unafanya biashara ya chakula, na wateja wako ni watu wa kidunia, badala ya kuombea madishi na chakula unachokipika kwamba wakipende, hebu waombee wampende YESU, halafu uone kama hiko chakula chako hawatakipenda, zaidi ya vyakula vya wengine wote.
– Pale ofisini acha kuombea uso wako kwamba upate kibali, sawa waweza kuomba hivyo, lakini isizidi sana kiasi kwamba hujui kitu kingine cha kuomba zaidi ya hicho, badala yake anza kuomba watu wa ofisini kwako wamjue MUNGU, wakimjua MUNGU wewe utapata kibali tu!, wala hutatumia nguvu nyingi.
– Pale shuleni acha kuombea walimu wakupende, hebu waombee wamjue YESU na kumpenda, halafu uone kama hawatakupenda na wewe.
– Unauza bidhaa, waombee wateja wako wamjue YESU na kumpenda zaidi ya bidhaa zako, halafu uone matokeo.
Ukitaka kufunga kwaajili ya biashara yako!, Funga kwa maombi ya kuwaombea wateja wako wokovu na Neema zaidi, kama unayo list, anza mmoja baada ya mwingine, wapatanishe na KRISTO hivyo uone kama KRISTO pia hatakupatanisha nao, utaona kazi zako zinaenda, shule yako inaenda, biashara yako inaenda, kazi yako inaenda.
Lakini ukijikita tu kuziombea bidhaa kama vile waganga wanavyotoa dawa za kwaajili ya biashara, matokeo yake yatakuwa ni madogo sana.
Hivyo OMBA lakini omba kwa shabaha/target.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mistari ya biblia kuhusu maombi.
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine: