Wahuni ni watu gani katika biblia?

Wahuni ni watu gani katika biblia?

Jibu: Kibiblia “Mhuni” ni mtu anayefanya mambo yaliyo kinyume na maadili. Kwamfano mtu anayetanga kuzaa nje na ndoa, huyo kibiblia ni mhuni.

Katika biblia neno Mhuni/wahuni limeonekana mara moja tu! Katika kitabu cha Ayubu 30:8.

Ayubu 30:8 “Wao ni wana wa wapumbavu, naam, WATOTO WA WAHUNI; Walifukuzwa kwa mijeledi watoke katika nchi”

Na mambo mengine yote ambayo mtu anaweza kuyafanya kinyume na maadili, mfano uvaaji mbaya, uongeaji mbaya, utafutaji mbaya n.k mambo hayo ni mambo ya  kihuni, na hivyo anayeyafanya ni mhuni.

Na Wahuni wote hawatairithi Nchi, watafukuzwa watoke katika nchi..kulingana na hilo andiko.

Mathayo 5:5 “Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi”.

Jihadhari na uhuni, kama wewe ni binti uvaaji wa nguo fupi ni uhuni!, uvaaji wa vimini ni uhuni,  uvaaji wa suruali ni uhuni (biblia inasema mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanaume na mwanaume asivae mavazi yampasayo mwanamke), kuvaa nguo unayoonyesha mapaja, au mgongo ni uhuni, kunyoa kijogoo kwa mwanaume ni uhuni, kuvaa nguo za mlegezo ni uhuni, kuvaa nguo za kubana ni uhuni n.k

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mshahara wa Mbwa ni upi? Kama tunavyousoma katika Kumbukumbu 23:18

Kutazama Nyakati mbaya ni kufanyaje?.

MUNGU ATAKUUA UKIWA MBAYA MACHONI PAKE.

Nini maana ya “wanawake saba watamshika mtu mume mmoja”

MAPENZI YA MUNGU NI YAPI?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments