Title 2025

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza 

Kitabu hichi ni moja ya nyaraka   zilizondikwa na  mtume Paulo katika agano jipya, 

Waraka huu amegusia mambo mengi, hasahasa katika eneo la marekebisho na maonyo. Unagusia nidhani na taratibu za kikristo zinazopaswa zifuatwe ndani ya  kanisa, unazungumzia pia eneo la uhalisia wa ufufuo wa wafu katika siku ya mwisho pamoja eneo la upendo.

Na huu ndio uchambuzi wake katika maeneo mama; 

1) Matabaka ndani ya kanisa. (1:10-17, 3:1-4:21)

Paulo anatoa onyo juu ya migawanyo ambayo ilianza kutokea ndani ya kanisa iliyozaa  wivu na fitina, ambayo ilisababishwa kwa baadhi ya watu kujiwekea matabaka kwa kujivunia viongozi kwa kusema mimi ni wa Paulo, mimi ni wa Apolo, mimi ni wa Kefa. Akiwatahadharisha na kuwasihi  kwa kuwaeleza kwamba wao ni wahudumu tu katika nafasi mbalimbali, bali mkuzaji ni Kristo. Na hivyo hawapaswi kujivunia wao, bali Kristo

2) Usahihi juu ya hekima ya Mungu

Kristo ni hekima ya Mungu na nguvu ya Mungu.(1:18- 2:16)

Eneo la pili Paulo anatoa ufahamu hasaa juu ya hekima anayoitambua Mungu, akionyesha kuwa hekima ya ulimwengu huu, kwa Mungu ni upuzi, bali hekima ya Mungu ameificha ndani ya Kristo Yesu, na hivyo amewachagua watu wadhaifu na wanyonge kuwadhihirishia hiyo. Akionyesha kuwa mtu asitegemee sana kumwona Mungu katika mambo yanayodhaniwa kuwa ni makuu, bali katika Kristo Yesu.

1 Wakorintho 1:24

[24]bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu. 

3) Nidhamu ya kimwili ndani ya kanisa la Kristo, (1Wakorintho 5-6)

 Katika eneo hili Paulo anastaajabishwa kwa kuzuka kwa zinaa mbaya ambayo haionekani hata  kwa mataifa yaani mtu na mzazi wake kuzini,. Akiwaagiza kutoa hukumu juu ya watu kama hao, hata kwa kuwakabidhi shetani (lengo ni waponyeke)

Kwasababu wakiachwa mwisho wao huwa ni kulichafua kanisa, (kulitia unajisi), 

Vilevile tunaona Paulo akitoa agizo kuwa kanisa halipaswi kuchangamana na wazinzi.

Akisisitiza kuwa mtakatifu sio tu awe amehesabiwa haki bali pia awe ameoshwa  na kutakaswa na udhalimu wote.

Anawaagiza pia watakatifu hawapaswi kupeleka mashtaka yao kwa watu wa kimataifa, bali kanisa ni zaidi ya mahakama ambayo watakatifu wanapaswa watatulie migogoro yao hapo. 

4) Ndoa na useja. (1Wakorintho 7)

Paulo anaeleza kwa upana, taratibu ya kindoa, katika eneo la haki zao za ndani na kuachana, na wito wa utowashi(useja). Katika eneo la haki, anasisitiza kuwa kila mwanandoa anapaswa atambue kuwa hana haki juu ya mwili wake mwenyewe, bali mwenzake, lakini pia katika kuachana, anaeleza ikiwa mwanandoa mmoja haamini, Yule aliyeamini hapaswi kumwachwa mwenzake, ikiwa bado anataka  kuendelea kuishi naye. Lakini pia anatoa pendekezo lake Mtu akitaka kumtumikia Mungu kwa wepesi zaidi bila kuvutwa na mambo ya mwilini na dhiki za kiulimwengu. Basi akikaa bila kuoa/kuolewa afanya vema zaidi.

5) Uhuru wa mkristo.(1Wakorintho 8-10)

Anaeleza jinsi gani mkristo anapaswa kukabiliana na dhamiri yake na ile ya wengine,katika maamuzi ayafanyayo kwa ujuzi wake,  akigusia eneo la vyakula (hususani vile vilivyotolewa sadaka kwa sanamu), kwamba hivyo havituhudhurishi mbele za Mungu, lakini tukila pia tuangalie wengine wanaathirikaje. Tusije tukawakwaza kwa ujuzi wetu. Paulo anaeleza ili tuweze kufikia hapo yatupaswa kuyafanya yote katika upendo.

1 Wakorintho 8:11-13

[11]Na yule aliye dhaifu aangamizwa kwa ujuzi wako, naye ni ndugu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake. 

[12]Hivyo, mkiwatenda dhambi ndugu zenu na kuitia jeraha dhamiri iliyo dhaifu, mnamtenda dhambi Kristo. 

[13]Kwa hiyo, chakula kikimkwaza ndugu yangu, hakika sitakula nyama hata milele, nisije nikamkwaza ndugu yangu. 

Lakini pia anaeleza haki waliyonayo mitume, kwamba wanaouwezo wa kula katika fungu la kanisa, lakini hawakutumia ujuzi wao wote, ili waweze kuifikisha injili kiwepesi kwa watu bila kuwazuilia na wengine.

6) Adabu na nidhani katika kukusanyika ndani ya  kanisa la Mungu( 1Wakorintho 11)

Paulo anatoa utaratibu wa ki-Mungu wa namna ya kuhudumu, kufuatana na hali ya kijinsia. Kwamba kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha mwanamume ni Kristo na kichwa cha Kristo ni Mungu. Hivyo mwanawake anapaswa wafunikwe vichwa awapo ibadani, ili kuonyesha kichwa chake(mumewe) kinamilikiwa na Kristo. Na kwamba wanawake wanapaswa watii uongozi (1Wakorintho 14:34-40)

Paulo anaeleza pia nidhani katika kushiriki meza ya Bwana, kwamba inapaswa ifanywe katika ufahamu na utaratibu sahihi wa rohoni, vinginevyo itapelekea hukumu badala ya baraka

7) Karama za Roho (1Wakorintho 12-14)

Paulo anazungumzia kwa undani karama mbalimbali ambazo Mungu ameziweka katika kanisa na kwamba zinapaswa ziwe kwa lengo la kufaidiana na kujengana. Lakini anaeleza kipawa kilicho bora zaidi ya karama zote, nacho ni upendo, ambacho anakieleza kwa urefu katika sura inayofuata ya 13, kwamba hichi kimezidi vyote.

1 Wakorintho 13:1-8

[1]Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. 

[2]Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. 

[3]Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu. 

[4]Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 

[5]haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; 

[6]haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; 

[7]huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. 

[8]Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika. 

8) Kufufuliwa kwa wafu. (1Wakorintho 15)

Katika eneo hili Paulo anahimiza  fundisho la kufufuliwa kwa wafu, akionyesha jinsi lilivyo umuhimu katika imani ya kikristo, na hiyo ni kutokana na baadhi ya watu waliozuka ndani ya kanisa kufundisha fundisho la kisadukayo kwamba hakuna ufufuo wa wafu. 

Akieleza jinsi Bwana atakavyokuja kwamba siku ya kurudi kwake parapanda italia na wote kwa pamoja (tulio hai na waliokufa) tutaipokea miili mipya ya utukufu itokayo mbinguni.

9) Michango kwa watakatifu. (1Wakorintho 16)

Katika sehemu hii ya mwisho Paulo anawaagiza juu ya utaratibu wa changizo kwa ajili ya watakatifu, kwamba vifanyike kila siku ya kwanza ya juma wakutanikapo, anawaagiza pia wakeshe, wawe hodari, na mambo yao yote yatendeke katika upendo.

Kwa hitimisho ni kuwa waraka huu unalenga hasa marekebisho, juu ya mambo mengi yaliyokuwa yanatendeka kwasababu ya ujinga, upumbavu, na dhambi ndani ya kanisa la Kristo. Na Ukweli ni kwamba mambo kama haya haya ni rahisi kuonekana hata katika kanisa la leo. Waraka huu tuusomapo yatupasa tuutazame kwa jicho la kikakanisa je! makosa kama ya wakorintho yapo katikati yetu, kama ni ndio basi tujirekebishe haraka sana.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Warumi.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini BWANA awaagize wakoma wakajionyeshe kwa Makuhani?(Luka 17:14

Jibu: Turejee kuanzia ule mstari wa 12..

Luka 17:12 “Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,

13 wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!

14 Alipowaona aliwaambia, Enendeni, MKAJIONYESHE KWA MAKUHANI. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika”.

Sababu kuu ya Bwana YESU kuwaagiza hawa wakome wakajinyeshe kwa Makuhani ni kwasababu Makuhani ndio watu wa mwisho kutangaza kama mtu ni Mkoma au si Mkoma, baada ya uchunguzi.

Kwani zamani mtu akihisiwa au akijihisi mwenyewe kama ni mkoma basi sheria ilikuwa ni kwamba anaenda kwa Kuhani, na kisha kuhani anauchunguza mwili wake na baada ya uchunguzi akibainika kwamba anao Ukoma, basi huyo mtu anakuwa najisi na anatengwa,

Sheria hiyo tunaisoma katika kitabu cha Mambo ya Walawi Mlango wa 13.

Walawi 13:9 “Pigo la ukoma litakapokuwa katika mtu, ndipo ataletwa kwa kuhani;

10 na kuhani ataangalia, na tazama, ikiwa pana kivimbe cheupe katika ngozi yake, na malaika yamegeuzwa kuwa meupe, tena ikiwa pana nyama mbichi iliyomea katika kile kivimbe,

11 ni ukoma wa zamani ulio katika ngozi ya mwili wake, na kuhani atasema kuwa yu najisi; hatamweka mahali, kwa kuwa yeye yuna unajisi”

Kwahiyo endapo wale watu kumi wenye ukoma wangefika kwa Kuhani na baada ya kukaguliwa wakakutwa na madhaifu hayo yaliyotajwa hapo juu, basi wangekuwa NAJISI..maana yake ni wenye ukoma ambao haujatakasika/kupona.

Na kama tayari walishachunguzwa zamani na kubainika wanao ukoma, na sasa wanarudia tena vipimo kwa kuhani ili kubaini kama ukoma wao umepona basi endapo wangekutwa. bado wanao basi wangeendelea kuwa najisi na kutengwa….

Lakini tunaona watu hao kumi (10) wakiwa njiani kuwafuata Makuhani ili waangaliwe, wakiwa njiani walijikuta wametakasika ule ukoma, walijikuta ngozi zao zimerudia hali zao za zamani, kama Naamani alivyoponywa ukoma wake. (2Wafalme 5:14).

Luka 17:14 “Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.

15 Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;

16 akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.

17 Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?

18 Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu”

Mambo makuu mawili ya kujifunza kufuatia habari hiyo

   1.Uponyaji wa YESU unahitaji imani yenye Matendo.

Laiti kama  hawa wenye ukoma wangeyadharau maneno ya Bwana YESU  aliyowaambia kuwa wakajionyeshe kwa Makuhani, na wangeenda njia nyingine, hakika wasingepona, wangebaki vile vile.

Lakini walipochukua hatua ya kwenda kwa Makuhani, kumbe maili kadhaa mbele muujiza wao ulikuwa unawangoja, kama tu ilivyokuwa kwa Naamani alipoambiwa akajichovye mara saba Yordani.

Hali kadhalika na wewe, shida au ugonjwa wowote ulio nao, kazi uliyobakiwanayo ni moja tu, kuyaamini maneno ya Bwana YESU na kuendelea mbele katika Neno lake, Muujiza wako utakutana nao mbele, usianze kuutafuta dakika hiyo hiyo.

  2. Kurudi kumpa MUNGU utukufu na kushuhudia.

Hili ni jambo la pili la kujifunza. MUNGU wetu anapendezwa na watu wa Shukrani.

Angalia mtu huyu alirudi kumshukuru MUNGU na kutoa ushuhuda na Bwana YESU akatafsiri tukio hilo ni kama kumpa MUNGU utukufu..

Huwenda MUNGU alishakutendea jambo fulani kubwa je uliwahi kurudi na kumtukuza mbele ya wengi?..Au je una mpango wowote wa kumtukuza katika hilo unalomwomba sasa akutendee?..Jibu unalo wewe.

Je tayari umempokea YESU?..Unao uhakika Bwana akirudi leo unaenda naye?.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Kufifiliza ni kufanya nini? (Kumbukumbu 32:25).

Jibu: Turejee…

Kumbukumbu 32:25 “Nje upanga UTAWAFILILIZA Na ndani ya vyumba, utisho; Utaangamiza mvulana na msichana,  Anyonyaye pamoja na mwenye mvi”.

Kufifiliza ni “kuangamiza” hivyo neno hilo katika maandiko hayo limesimama badala ya “kuangamiza mtu”..ambapo matokeo yake ni msiba wa mtu muhimu katika nyumba.

Hivyo andiko hilo laweza kueleweka hivi..

Kumbukumbu 32:25 “Nje upanga UTAWAANGAMIZA Na ndani ya vyumba, utisho; Utaangamiza mvulana na msichana,  Anyonyaye pamoja na mwenye mvi”.

Je unaye YESU moyoni?.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Kuwanda ni kufanya nini?

Jibu: Turejee..

Waamuzi 3:17 “Kisha akamsongezea Egloni, mfalme wa Moabu, hiyo tunu; basi Egloni alikuwa ni mtu AYELIWANDA sana”.

Kuwanda ni kiswahili kingine cha “kunenepa sana”.. Hivyo mtu aliyewanda maana yake ni “mtu aliyenenepa sana”.

Hivyo mstari huo wa Waamuzi 3:17 unaweza kueleweka hivi…

Waamuzi 3:17 “Kisha akamsongezea Egloni, mfalme wa Moabu, hiyo tunu; basi Egloni alikuwa ni mtu ALIYENENEPA sana”.

Neno hilo pia tunaweza kulisoma katika Yeremia 50:11 na katika habari za Yeshuruni katika Kumbukumbu 32:15. 

Kwa habari ndefu kuhusiana na Yeshuruni basi fungua hapa 》》》Yeshuruni ni nani katika biblia?

Je wewe kiroho umewanda/nenepa katika nini?..katika maovu au katika haki?…

Ni hatari kubwa KUWANDA katika mabaya…

Yeremia 5:28 “WAMEWANDA sana, wang’aa; naam, wamepita kiasi KWA MATENDO MAOVU; hawatetei madai ya yatima, ili wapate kufanikiwa; wala hawaamui haki ya mhitaji.

29 Je! Nisiwapatilize kwa mambo hayo? Asema BWANA; na nafsi yangu, je! Nisijilipize kisasi juu ya taifa la namna hii?”

Je unaye Roho Mtakatifu?. Kumbuka Roho Mtakatifu ndiye muhuri wa MUNGU (Waefeso 4:30).

Bwana YESU anarudi (Maran atha).

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Je Bwana YESU alipanda mlimani na wanafunzi wake baada ya siku sita au nane?

Swali: Je Bwana YESU alipanda mlimani na wanafunzi wake baada ya siku ngapi?..ni Sita au Nane?, Kwa maana katika Mathayo 17:1 na Marko 9:2 panaonyesha ni baada ya siku sita (6) lakini tukisoma Luka 9:28 panaonyesha ni siku ni nane (8) Je ukweli ni upi?.


Jibu: Turejee mistari hiyo..

Mathayo 17:1 “Na baada ya SIKU SITA Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani”

Hapa ni kweli tunasoma “Siku sita” na Marko 9:2 tunasoma vile vile ni siku sita (6).

Tusome tena Luka 9:28..

Luka 9:28  “Baada ya maneno hayo yapata SIKU NANE, aliwatwaa Petro na Yohana na Yakobo, akapanda mlimani ili kuomba”.

Hapa tunasoma ni siku nane (8) na si sita tena, swali ni je! Biblia inajichanganya?, au mwandishi mmoja amekosea?

Jibu ni La! Biblia haijichanganyi na wala hakuna mwandishi aliyekosea, wote wapo sawa na maneno yote ni hakika, kwasababu biblia ni kitabu kilichohakikiwa na Roho Mtakatifu mwenyewe na hakina makossa (Mithali 30:5).

Sasa kama ni hivyo kwanini  panaonekana  kuna tofauti ya siku?..

Mwandishi wa kitabu cha Luka alionyesha jumla ya siku walizokaa mlimani, na Mwandishi wa kitabu cha Mathayo na Marko wakaonyesha siku walizoondoka katika makazi yao na kuelekea mlimani.

Sasa ni kwamba baada ya Bwana kuwaambia wanafunzi wake kuwa wapo ambao hawataonja mauti hata watakapoona ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu, zilipita siku sita akawachukua wanafunzi wake baadhi (ambao ni Petro, Yohana na Yakobo) akapanda nao mlimani.

Na biblia haijaeleza katika hizo siku sita kabla ya kupanda mlimani walikuwa wanafanya nini au walikuwa wapi, pengine waliachana kidogo, au walikuwa katika huduma zilizowatenga kwa muda siku sita, mpaka ilipofika siku hiyo ya kupanda mlimani….hiyo yote haijaeleza lakini inasema tu baada ya siku sita alipanda nao mlimani, na ndicho Mwandishi Mathayo na Marko walichokieleza.

Lakini sasa Luka yeye hakulenga kuelezea siku waliyopanda mlimani, kwamba ni baada ya siku sita za yale maneno, bali yeye alisema “YAPATA SIKU NANE”… Hilo Neno “Yapata” ni neno la ujumla, likielezea Muda wa safari Nzima, kuwa ni SIKU NANE (8), Maana yake baada ya siku sita walipanda mlimani sawasawa na Mwandishi Mathayo na Marko na kule mlimani walikaa siku mbili (2), na kufanya jumla ya siku kuwa nane, ndicho mwandishi alichokilenga. (kwahiyo muda waliokaa mlimani ni siku mbili, lakini walipanda baada ya siku sita).

Kwahiyo biblia haijajichanganya hapo, bali ni uelewa wetu ndio unaojichanganya.

Je umempokea BWANA YESU?.. Na je unajua kuwa dalili zote zinaonyesha kuwa kizazi tulichopo ni cha mwisho?..Je umejiandaaje? Taa yako inawaka?

Luka 12:35  “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;

36  nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na

Je bado unaendelea na maisha ya dhambi?, bado unakunywa pombe?, bado unazini, bado unajichua, bado unavaa kidunia?

Muda umeisha, msikilize Roho Mtakatifu, na usizisikilize roho zidanganyazo.

1Timotheo 4:1“Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani”

Maran tha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TABIA SITA (6) ZA WANAFUNZI WA YESU.

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

Je maombi ya mlimani yana ulazima wowote kwa mkristo?

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini Mungu azungumze na Ayubu kupitia upepo wa kisulisuli (Ayubu 38:1)

Ayubu 38:1

[1]Ndipo BWANA akamjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli, na kusema,


JIBU: Tukumbuke kuwa Mungu ana njia nyingi za kuzungumza na watu. Na kila njia huwa na maana fulani nyuma yake.

Utakumbuka Alipokutana na Musa alizungumza naye katika kijiti kinachoungua lakini hakiteketei..Kuwafundisha wana wa Israeli kuwa atakuwa pamoja nao hata katika moto wa majaribu lakini hawatateketea kabisa.. 

Kwamfano akina Shedraki, Meshaki na Abednego, walipojaribiwa kwa kutupwa tanuruni, hawakuungua au Danieli kwenye tundu la simba, hakupatwa na dhara lolote kwasababu walimtumaini Mungu. 

Kutufundisha kuwa hata  sasa, na sisi tuliomwamini Kristo, hakuna jaribu la aina yoyote linaloweza kutufanya sisi tuangamie na kupotea mbali na uso wa Mungu. Kwasababu yeye yupo nasi sikuzote.

Halikadhalika tunaona na hapa pia anamtokea Ayubu katika upepo wa kisulisuli..

Kisulisuli hutafsirika kama aina nyingine ya janga, mfano tu wa gharika au tetemeko. Kazi ya kisulisuli huwa ni kuzomba vitu  dhaifu labda makapi, au vitu ambavyo havina msingi imara…

Isaya 40:24

[24]Naam, hawakupandwa; hawakutiwa katika ardhi kama mbegu; naam, shina lao halikutia mizizi katika ardhi; tena awapuzia tu, wakanyauka, upepo wa kisulisuli wawaondoa kama mabua makavu. 

Hivyo Mungu kutumia njia hii, ni kumwonyesha Ayubu kwamba hata katika zomba-zomba za kiroho yeye yupo huko na watu wake.

Vitu vyote vya Ayubu vilizombwa, Kuanzia mali, watoto,.mifugo, hadi mke wake kwasababu ya udhaifu wa imani akazombwa na hila za shetani. Wao wakidhani kuwa Mungu amewaacha kumbe alikuwa nao daima. Tufahamu kuwa dhoruba, tufani, giza, au mwanga..vyote kwake ni sawasawa.

Lakini pia kuna wakati Mungu anazungumza katika utulivu. Utakumbuka tena habari ya Eliya wakati ule anamfuata Mungu kule mlima Horebu, akitarajia Mungu aseme naye katika fujo. Lakini hakumwona Mungu, katika matetemeko wala moto, bali katika sauti ndogo ya utulivu.

Kuonyesha kuwa Mungu husema nasi pia katika utulivu.

1 Wafalme 19:11-12

[11]Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za BWANA. Na tazama, BWANA akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunja-vunja miamba mbele za BWANA; lakini BWANA hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini BWANA hakuwamo katika lile tetemeko la nchi; 

[12]na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini BWANA hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu. 

Hivyo ikiwa umeokoka na umesimama imara na Bwana ni vizuri kufahamu kuwa nyakati zote, Mungu yupo nasi. Ni kawaida watu wakishapitia changamoto fulani hufikiri kuwa Mungu hayupo nao, kumbe sivyo nyakati zote nm ziwe za majaribu, za visulisuli, za mafuriko n.k. Tunapaswa tumwone yeye,.kwasababu yupo pamoja na sisi.

Kwasababu ndiye msaada wetu.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JINSI YA KUSHINDA VISULISULI(Mithali 10:25)

UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

Rudi Nyumbani

Print this post

Masheki ni akina nani? (Ayubu 29:10).

Swali: Masheki ni watu gani kama tusomavyo katika Ayubu 29:10?

Jibu: Turejee..

Ayubu 29:10 “Sauti yao masheki ilinyamaa, Na ndimi zao zilishikamana na makaakaa yao”.

Masheki ni jina lingine la “Wana wa wafalme”

Hivyo hapo aliposema.. “Sauti yao masheki ilinyamaa..”  ni sawa na kusema “sauti zao wana wa wafalme zilinyamaa”.

Neno hili pia tunalisoma katika..Zaburi 68:31, Zaburi 83:11 na Zaburi 105:22, na zote zina maana ile ile moja (wana wa wafalme ambao ni wakuu wa nchi).

Zaburi 68:31 “]Masheki watakuja kutoka Misri, Kushi itamnyoshea Mungu mikono yake mara”.

Je umempokea YESU Mwokozi?. na kukamilisha haki yote kwa ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU? (sawasawa na Matendo 2:38)?

Kama bado basi tengeneza mambo yako hayo kabla ule mwisho haujafika.

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wathesalonike wa pili.

Kichwa cha waraka huu kinasema. “ Waraka wa pili wa Paulo mtume kwa Wathesalonike”

Kutuonyesha kuwa Paulo ndiye mwandishi wa waraka huu, kwa kanisa hili la Thesalonike.

Lakini pamoja na hilo tunaona Waraka huu wa pili kama ulivyo ule wa kwanza anawataja pia Timotheo na silwano(Sila), kama waandishi wenza.

Aliundika akiwa Korintho, sawasawa na taarifa tunazozipata katika kitabu cha Matendo 18,.

Maudhui makuu ya waraka huu yalikuwa ni matatu(3), nayo ni; 

  1. Kuwatia moyo watakatifu katika dhiki zao.
  2. Kurekebisha opotofu uliojitokeza kuhusu ujio wa pili wa Bwana Yesu.
  3. Lakini pia kutoa maelezo juu ya  wajibu wa mkristo katika maisha yake ya kila siku.

Kwa maelezo mafupi tuyaangazie maeneo hayo matatu.

1) Eneo la kwanza: kuwatia moyo watakatifu

> Paulo anawatia moyo watakatifu kwa uthabiti wa imani yao ambayo imesimama sikuzote hata ilipopitia kwenye dhiki nyingi na adha.

2 Wathesalonike 1:4

[4]Hata na sisi wenyewe twaona fahari juu yenu katika makanisa ya Mungu kwa ajili ya saburi yenu, na imani mliyo nayo katika adha zenu zote na dhiki mnazostahimili. 

> Lakini pia anawaeleza hatma ya watu wanaowaletea adha, kwamba Mungu ni wa haki, na atawalipiza kisasi hao wanaowatesa. Kwa kuwaadhibu kwa maangamizi ya milele.(1:8-9)

2 Wathesalonike 1:6

[6]Kwa kuwa ni haki mbele za Mungu kuwalipa mateso wale wawatesao ninyi; 

> Lakini anaeleza ahadi ya raha ambayo Mungu amewawekea waamini huko mbeleni watesekao kwa ajili yake.

2 Wathesalonike 1:7

[7]na kuwalipa ninyi mteswao raha pamoja na sisi; wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake 

2) Eneo la pili: Upotofu juu ya siku ya Bwana

Anarekebisha upotofu uliozuka  juu ya siku ya Bwana,kama kweli tayari imeshakuwapo au la, hivyo katika sura hii ya pili,  anawaonya kwa kuwaambia siku hiyo haiji kabla ya ule ukengeufu  kwanza kuja, na yule mwana wa kuasi, mwana wa uharibifu (mpinga-kristo) kufunuliwa.

2 Wathesalonike 2:1-3

[1]Basi, ndugu, tunakusihini, kwa habari ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, na kukusanyika kwetu mbele zake, 

[2]kwamba msifadhaishwe upesi hata kuiacha nia yenu, wala msisitushwe, kwa roho, wala kwa neno, wala kwa waraka unaodhaniwa kuwa ni wetu, kana kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwapo. 

[3]Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu; 

Akiwa na maana kuwa kabla ya Kristo kurudi mara ya pili, ukengeufu wa kiroho mkubwa sana utatokea, na yule mpiga-kristo kujidhihirisha na kujulikana kwa kazi zake.

Ambazo zitakuwa ni kama ifuatavyo;

> Kujiinua juu ya kila kitu kiitwacho Mungu, akijifanya yeye ndio kama Mungu.

2 Wathesalonike 2:4

[4]yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu. 

> Atakuwa na utendaji kazi wa shetani ndani yake, kwa kufanya maajabu ya uongo ili kuwadanganya wote waliomkataa Mungu katika fahamu zao.(2:9-12)

> Lakini mwisho wake utakuwa ni kuangamizwa na Yesu.(2:8)

Paulo anaendelea kusema kwasasa hawezi kutenda kazi kwasababu yupo azuiaye, mpaka atakapoondolewa.

2 Wathesalonike 2:6-7

[6]Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake. 

[7]Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa. 

Na huyo si mwingine zaidi ya Roho Mtakatifu. Lakini kumbuka Sio kwamba  ataondolewa lakini mifumo yake inayozuia utendaji kazi wa mpinga-Kristo itafikia mwisho..Kwamfano kanisa kunyakuliwa, na mifumo ya kiutawala iliyoruhusiwa na Mungu maalumu kudhibiti kazi zake, kuachwa kutumiwa na Mungu, na malaika wanaohuduma duniani kwa ajili ya usalama wa watakatifu, kuondolewa.. 

Vitu kama hivi vitakapoondolewa basi mpinga-Kristo atapata uhuru wote kutendakazi kwa jinsi apendavyo.

3) Na sehemu ya tatu  anayoeleza juu ya  wajibu wa mkristo katika maisha yake ya kila siku. 

Paulo anawasisitiza watakatifu juu ya kuiombea huduma, ili injili ya Kristo itukuzwe, lakini pia aweze kuepushwa na watu wabaya.

Pamoja na hilo anatoa tahadhari kuhusu uvivu, akiwasisitiza wafanye kazi kwa mikono yao, pengine kwasababu ya ufahamu usio sahihi waliokuwa nao hapo mwanzo, kwamba mwisho tayari umekwisha fika.

Pia anawatia moyo watakatifu wasikate tamaa katika kutenda mema. Huku akiwahiza wadumu katika mapokeo yao tu waliyowaachia, na si mengineyo.

mwisho anamaliza na salamu pamoja na baraka kwa kanisa.

Kwa ufupi tuusomapo waraka huu Bwana anataka tuendelee kuthibiti katika imani,.haijalishi ni dhiki za namna gani tutazipitia.

Lakini pia tuwe na ufahamu sahihi juu ya siku za mwisho. Kwasababu tatizo hili lipo hata sasa, baadhi ya watu wakiamini kuwa siku ya Bwana imeshakuja. Lakini kama tulivyojuzwa hapo, haiwezi fika kabla, mpinga-Kristo kudhihirishwa na hilo litakuwa wazi kabisa duniani kote.

Na mwisho ni wajibu wetu kuombea huduma, na wanaojitaabisha kuhubiri injili ili walindwe na watu wabaya. Je unamwombea mchungaji wako?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wathesalonike wa kwanza.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?

Rudi Nyumbani

Print this post

ANZA MWAKA NA KUSAMEHE

Maandiko yanasema Makwazo hayana budi kuja (Luka 17:1)

Unapofanyiwa jambo baya na Mtu wako wa karibu au wa Mbali, huwa ni ngumu kusahau…

Kama umeshaokoka na ni mtu uliye mwepesi kusamehe na kusahau, basi Bwana amekutengeneza kwelikweli na umetengenezekeka, Lakini kama ndani yako kuna UGUMU wa kusamehe, fahamu kuwa hilo ni tatizo ambalo unapaswa ulitafutie ufumbuzi haraka sana, mwanzoni mwa mwaka.

Umeumizwa na Ndugu, umeumizwa na Mpendwa mwenzako, umeumizwa na Rafiki, umeumizwa na Mke, Umeumizwa na Mume, umeumizwa na watoto, mchungaji, mshirika wako, mkufunzuki wako au mtu mwingine yeyote, leo itoe hiyo sumu..

Fanya jambo  hili  moja ili ushinde hali hiyo ya kutokusamehe na hatimaye uachilie msamaha.

UTAFAKARI MSAMAHA WA YESU.

Tafakari ni mambo mangapi mabaya uliyoyafanya au unayoyafanya kwa MUNGU, unaweza ukawa hujawahi kumfanyia mtu ubaya, lakini vipi MUNGU?.. Je hujawahi kumfanyia ubaya kabisa?..huna dhambi kabisa??, huna kasoro kabisa??.. Hilo ni jambo lisilowezekana. (2Nyakati 6:36)

Tafakari tu mawazo yako kwa siku yanavyo vuka na kuwa machafu, na MUNGU anakutazama tu!, tafakari ni vipindi vingapi umewaka hasira moyoni na Mungu anakutazama tu, tafakari ni mangapi amekusamehe, na ni mangapi unayohitaji ukusamehe.

Hayo yote uliyoyafanya na unayoyafanya Mungu anayatazama tu, na yupo tayari kukusamehe, au huenda ameshakusamehe, sasa kama wewe umesamehewa mengi hivyo bure kabisa, vipi na wewe kwanini usimsamehe yule aliyekokosea mwaka jana, au mwezi jana, au siku ya jana??.

Wakati mwingine si lazima yeye akuombe msamaha,  Wewe samehe tu hata kama hajaja kukuomba msamaha, maana hata BWANA aliwasamehe wale wasiomwomba msamaha..

Luka 23:34 “Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.

35  Watu wakasimama wakitazama. Wale wakuu nao walikuwa wakimfanyia mzaha, wakisema, Aliokoa wengine; na ajiokoe mwenyewe, kama ndiye Kristo wa Mungu, mteule wake.”

Wengine watakukosea na daima wataendelea kujiona wapo sawa, na wengine wataendelea kukukosea  tu!.. Lakini kanuni ni ile ile KUSAMEHE..

Hivyo kwa kuutafakari mambo ya maisha yako, na kasoro zako mbele za MUNGU, Huwezi kukosa sababu za wewe kutosamehe.

Kwa kumalizia hebu tafakari kwa undani maandiko yafuatayo…

Mathayo 18:21  “Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?

22  Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.

23  Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.

24  Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.

25  Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.

26  Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

27  Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.

28  Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho.

29  Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

30  Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.

31  Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka”.

Kumbe tusipokuwa na TAFAKARI ya kutosha kwa msamaha BWANA aliotupa, yaweza kuwa sababu ya sisi pia kutosamehewa!. Lakini kama tukifakari kwamba na sisi tumeshafanya mengi mabaya, ambayo hayakustahili msamaha basi na sisi pia tutasamehe.

Mhubiri 7:20 “Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ambaye afanya mema, asifanye dhambi.

21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.

22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine”.

Mwombe Bwana katika mwanzo wa mwaka huu akuumbie  “Moyo wa kusamehe”.. Ni yeye ndiye anayetoa huo moyo, ikiwa tutamwomba, kwa kumaanisha kabisa, Hivyo jifungie chumbani kwako, au tafuta sehemu yoyote yenye utulivu na mwambie Bwana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TAFAKARI SANA KABLA YA KUAMUA HATIMA YAKO.

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

Maana ya Mithali 19:11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake.

Je! Kiongozi wa dini anaouwezo wa kusamehe dhambi?

BWANA ANASAMEHE.

Rudi Nyumbani

Print this post

Shetani alitoka wapi?

Swali: Je shetani yule audanganyaye ulimwengu alitoka wapi?


Jibu: shetani kwa asili aliumbwa na Mungu, na kabla ya kuwa shetani alikuwa akiitwa “Kerubi afunikaye”

Ezekieli 28:14 ” Wewe ulikuwa KERUBI MWENYE KUTIWA MAFUTA AFUNIKAYE; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto”.

Na MUNGU alimwumba akiwa mkamilifu (asiye na dosari) kama tu MAKERUBI wengine, lakini baadaye moyo wake uliinuka akajidanganya mwenyewe kuwa anaweza kuwa kama MUNGU (aabudiwe kama MUNGU) Na ndipo Uovu huo ukaonekana ndani yake, na hakutaka kubadilika.

Ezekieli 28:15 “Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako”

Na baadaye alipoasi ndipo akawa shetani, na maana ya shetani ni Mshitaki/Mchongezi, maana yake anawashitaki wanadamu mbele za MUNGU mchana na usiku.

Ufunuo 12:9 “Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.

10  Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana AMETUPWA CHINI MSHITAKI WA NDUGU ZETU, YEYE AWASHITAKIYE MBELE ZA MUNGU WETU, MCHANA NA USIKU”.

Kwahiyo shetani aliumbwa na MUNGU, na akaasi na  ataharibiwa na MUNGU katika ziwa la MOTO baada ya hukumu ya kile kiti cheupe.

Ufunuo 20:10 “Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele”.

Bwana atuepushe na ibilisi.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

NYOTA YA ASUBUHI.

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

Rudi Nyumbani

Print this post