Shalom,
Bwana Yesu alituambia tusalipo tuseme hivi..
Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, UFALME WAKO UJE,..
Ni kweli, tunajua kuwa siku moja ufalme wake utakuja duniani..Lakini upande wa pili wa shilingi yaani sisi tunaousubiria ufalme huo unadhani tungepaswa tuwe katika hali gani?..Nadhani ulishawahi kujikuta katika hali ya kumsubiria mtu au kitu mahali Fulani halafu kwa bahati mbaya kikachelewa/akachelewa kidogo, ile hali unatakayokuwa nayo wakati ule bila shaka si ya kawaida, dakika tano tu utaziona kama ni lisaa limoja limepita, na ndio maana kila sekunde utampigia simu kumuuliza umefika wapi? Mbona sikuoni? Fanya haraka bwana!, Kimbia au chukua pikipiki,, nimesimama hapa muda mrefu nakungoja tu sikuoni? Ni nini kimekukumba? Umekwama wapi? ..n.k.. Unaona Hiyo yote ni kumuharakisha ili tu afike, kwasababu kusubiri kunaumiza.
Lakini haiwezekani ukasema unamsubiria mtu, halafu masaa matatu yanapita, na bado huna hata wasiwasi, humpigii simu kumuuliza hata amefika wapi, au huna hata mpango wa kuulizia atafika saa ngapi, wewe umesimama tu unasema unamngoja, ni wazi kuwa hilo jambo haliwezekani vingenevyo utakuwa na shughuli zako nyingine za kando.
Na ndicho hicho Mungu anachotaka kuona kutoka kwetu, sisi tunaosema tunamngojea Bwana, ni lazima tuwe tunamkumbusha juu ya siku ile ya kuja aihimize ifike haraka, UFALME WAKE UJE HARAKA! (upesi)..Ndugu hichi ni kipengele muhimu sana ambacho Mungu anatazamia kila mkristo wa kweli aliyezaliwa mara ya pili awe anamwomba yeye daima, na ndio maana Bwana Yesu alikiweka katika sala hiyo ya msingi.
Kipimo kizuri cha kujitambua kama kweli umejiweka tayari kwa ajili ya kwenda mbinguni au La, basi ni kwenye kipengele hichi, Jipime je! Ndani yako ipo ile shauku ya kutamani siku ile ya mwisho ifike au La?. Kama haipo basi ujue hata unyakuo ukipita leo hii huendi popote, utabaki tu hapa duniani.
Ni kama tu Mwanafunzi shuleni, yule aliyejiandaa vizuri na mtihani wa mwisho, pale anapokumbuka tu mtihani wa taifa unakuja, huwa anatamani siku hizo zifike haraka amalize zake akapumzike, lakini yule ambaye hajajiandaa, utaona yeye ni kinyume chake, atatamani hata muda uzidi kuongezwa tu wa kuendelea kubaki shule…kwasababu hakujua kilichompeleka shuleni.
Na sisi kama wakristo wapitaji hapa duniani Bwana anatazamia, kila siku tunapoamka tunapolala tunapaswa tumwombe, tutamani na tumkumbushe jambo hilo, kuwa siku ile ya kwenda zetu kwa Baba mbinguni ifike haraka. Aharikishe neema ya wokovu ya kuwaokoa watu wake, mambo yaishe haraka tukapumzike kwake milele. Siku ya unyakuo, siku ile ambayo tutamwona Bwana wetu Yesu uso kwa uso mawinguni ifike!, Tukaile ile karama ya mwanakondoo na malaika mbinguni tuliyoandaliwa tangu zamani.
Siku ambayo tutaiona mbingu mpya na nchi mpya, kwa mara ya kwanza ikishuka ambayo haitakuwa na machozi tena, wala misiba, wala magonjwa, wala vita, wala matetemeko, wala chuki, wala mashindano, wala mahangaiko ya dunia hii, wala umaskini, wala ubaguzi.. siku hiyo tunaiomba na tunaitamani ifike.
Hili ni jambo ambalo kila siku tunatakiwa tumwombe Mungu, Unaweza ukaliona halina thamani machoni pako, lakini mbele za Mungu lina maana sana.. Lakini sisi tukiwa kila mara tunapomwendea Mungu ni kuomba tu magari, nyumba, biashara, wake, kila siku mambo ya kiduniani tu ndiyo tunayompelekea yeye….Hatuna muda wa kutafakari kuwa hii dunia inafika mwisho, na dunia inapita (1Yohana 2:17) Tujue kuwa Mungu anatuona kama hatujastahili kuurithi ufalme wake. Tupo tu.
Anza leo kujijengea desturi hii, ya kumhimiza Mungu, juu ya ufalme wake, aliotuahidia tangu zamani uje haraka ulimwenguni, Na hiyo ni ndio inayothibitisha kuwa kweli tunatamani unyakuo ufike haraka, kweli tunatamani kufutwa machozi, Hizo ndizo hoja zenye nguvu kwa Mungu wetu.
Kama tu viumbe vyenyewe (swala, twiga, mbwa, tausi, punda, ng’ombe n.k.) wanatazamia kwa shauku siku hiyo ya sisi kutukuzwa, inakupasaje wewe na mimi? Ambao ndio warithi wenyewe..Tunapaswa macho yetu yaelekee kule Zaidi.
Warumi 8:18 “Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama utukufu ule utakaofunuliwa kwetu. 19 Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu. 20 Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili; si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye atiyevitiisha katika tumaini”.
Warumi 8:18 “Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama utukufu ule utakaofunuliwa kwetu.
19 Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.
20 Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili; si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye atiyevitiisha katika tumaini”.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
JIFUNZE KUELEWA MAANA YA KUOA/KUOLEWA KABLA YA KUINGIA HUKO.
JINSI DHAMBI INAVYOMGHARIMU MTU SANA.
JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?
JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.
Rudi Nyumbani:
Print this post
JIBU: Mungu anaweza kuzungumza na mtu moja kwa moja, au akatumia malaika wake kumpa mtu ujumbe au akamtumia mwanadamu…na mara chache sana anaweza kutumia hata wanyama (Hesabu 22:30). Au vitu vya asili (Ayubu 12:7-9).
Sasa wanadamu na wanyama ni viumbe wa mwilini, Mungu hawezi kuzitumia roho zao kuzungumza na sisi…kwamfano Mungu hawezi kutumia roho yangu au ya mtu fulani kuzungumza na roho ya mtu mwingine…akitaka kuzungumza na mtu, atampa ujumbe katika roho, mtumishi wake, kisha huyo mtumishi atautoa huo ujumbe kwa mhusika. Ni Roho Mtakatifu pekee na Malaika watakatifu ndio wenye huo uwezo wa kuzungumza na sisi kwa njia hiyo ya rohoni kwasababu wao ni wa rohoni..
Malaika anaweza kuonekana kama mtu na kumpa mtu ujumbe na vile vile anaweza kuzungumza na mtu moja kwa moja kwenye roho yake bila kutumtokea wala kuonekana.
Jambo la muhimu la kufahamu ni kwamba…Malaika wa Mungu hawazungumzi kitu kama watakavyo wao…kila wanachokisema au kila ujumbe wanaotupa ni ujumbe kutoka kwa Roho Mtakatifu kama ulivyo (haujaongezwa wala kupunguzwa). Kwahiyo sauti zao ni sauti za Roho Mtakatifu mwenyewe…Ikiwa na maana kuwa Malaika anapozungumza na wewe rohoni, ujue kuwa ni Roho Mtakatifu anazungumza na wewe, kwasababu Malaika anazungumza kitu alichoambiwa na Roho Mtakatifu akiseme vile vile.
Kwamfano hebu tusome mistari michache ifuatayo..
Mwanzo 22:10 “Ibrahimu akanyosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe. 11 Ndipo MALAIKA WA BWANA AKAMWITA KUTOKA MBINGUNI, AKASEMA, IBRAHIMU! IBRAHIMU! NAYE AKASEMA, MIMI HAPA. 12 Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee. 13 Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe. 14 Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire,kama watu wasemavyo hata leo,Katika mlima wa BWANA itapatikana. 15 MALAIKA WA BWANA AKAMWITA IBRAHIMU MARA YA PILI KUTOKA MBINGUNI 16 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee, 17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao”
Mwanzo 22:10 “Ibrahimu akanyosha mkono wake, akakitwaa kisu ili amchinje mwanawe.
11 Ndipo MALAIKA WA BWANA AKAMWITA KUTOKA MBINGUNI, AKASEMA, IBRAHIMU! IBRAHIMU! NAYE AKASEMA, MIMI HAPA.
12 Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.
13 Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.
14 Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-yire,kama watu wasemavyo hata leo,Katika mlima wa BWANA itapatikana.
15 MALAIKA WA BWANA AKAMWITA IBRAHIMU MARA YA PILI KUTOKA MBINGUNI
16 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,
17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao”
Umeona katika tukio hilo…hapo ni Malaika wa Bwana anazungumza na Ibrahimu kama Mungu mwenyewe…kiasi kwamba ni ngumu kujua kama huyo ni Malaika au Mungu anayezungumza hapo..
Tusome tena..
Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu. 2 MALAIKA WA BWANA AKAMTOKEA, KATIKA MWALI WA MOTO uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea. 3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei 4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa. 5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu. 6 TENA AKASEMA, MIMI NI MUNGU WA BABA YAKO, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu”.
Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.
2 MALAIKA WA BWANA AKAMTOKEA, KATIKA MWALI WA MOTO uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea. 3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei
4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.
5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.
6 TENA AKASEMA, MIMI NI MUNGU WA BABA YAKO, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu”.
Wengi wetu tunaijua hii habari ya Musa kuona kijiti kilichokuwa kinaungua lakini hakiteketei, na wengi wetu tunajua kwamba ni Mungu ndiye aliyemtokea Musa…lakini kiuhalisia sio Mungu aliyemtokea Musa…Bali ni Malaika wa Mungu ambaye alibeba maneno ya Mungu kama yalivyo, ndiye aliyemtokea Musa katika kile kijiti kilichokuwa kinawaka lakini hakiteketeiSiku zote Malaika anapotoa ujumbe ni kama tu msemaji wa Raisi anayesoma waraka wa Raisi mbele ya watu..atasoma mpaka sahihi ya mwisho iliyoandikwa (mimi Raisi nimesema haya yote yaafanyike)!…
Waamuzi 2:1 “Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi”.
Umeona na hapo? Malaika anasema “Mimi nimewatoa Misri na kuwaleta katika nchi niliyowaapia baba zenu,…milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi”. Ukitafakari hakuna mahali popote Malaika alishaingia agano na wana wa Israeli, ni Mungu ndiye aliyeingia agano na wana wa Israeli..Kwahiyo hapa ni Malaika anazungumza ujumbe wa Mungu, ni kama vile anarudia kuzungumza kile kitu Mungu alichomwambia azungumze..(Ni kama vile anasoma waraka).
Malaika mara nyingi hawana hichi kitu cha “Mungu kasema”…wenyewe wanarudia kuzungumza kile Mungu alichokisema…Hivyo hiyo inafanya kuwa ngumu sana kuitofautisha sauti ya Roho Mtakatifu na ya malaika…Kwani Malaika atakapozungumza nawe katika roho yako hatasema…Mungu kasema fanya hivi au vile….utasikia tu sauti inasema “Mimi Bwana nimesema”..na wewe unaweza kudhani ni Bwana kazungumza nawe kumbe ni Malaika wake.
Sasa kilicho cha muhimu sio kutafuta kujua kuzitofautisha hizi sauti kwasababu haisaidii chochote…kilicho cha muhimu ni kujifunza kutii kile unachoambiwa…iwe ni Roho Matakatifu kazungumza kupitia kinywa cha malaika au kazungumza yeye mwenyewe moja kwa moja…kilicho cha muhimu na maana kwetu ni kukitii kile tulichokisikia maadamu tumehikiki ni Ujumbe kutoka kwa Mungu…
Bwana atubariki.
Je! kuchora tattoo ni dhambi?
KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.
WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.
USIPUNGUZE MAOMBI.
SHETANI ANAITHAMINI HATA MAITI YAKO.
IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!
KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?
SWALI: Je! Siku ipi ambayo Mfalme wa Babeli alimtoa vifungoni mfalme wa Israeli(Yekonia/Yehoyakini). Je! Ni ile tarehe 25 ambayo tunaisoma kwenye Yeremia, au ile ya tarehe 27 tunayoisoma kwenye kitabu cha 2Wafalme..Na Je! biblia imekosea uandishi?
JIBU: Tusome..
2Wafalme 25:27 “Ikawa katika mwaka wa thelathini na saba wa kuhamishwa kwake Yekonia mfalme wa Yuda ,katika mwezi wa kumi na mbili ,SIKU YA ISHIRINI NA SABA YA MWEZI ,Evil-merodaki,mfalme wa Babeli ,katika mwaka wa kwanza wa kutawala kwake,akamwinua kichwa Yekonia,mfalme wa Yuda,akamtoa gerezani”.
Lakini Yeremia inasema..
Yeremia 52:31 “Hata ikawa, katika mwaka wa thelathini na saba wa kuhamishwa kwake Yehoyakini, mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kumi na mbili, SIKU YA ISHIRINI NA TANO YA MWEZI, Evil-merodaki, mfalme wa Babeli, katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, akamwinua kichwa chake Yehoyakini, mfalme wa Yuda, akamtoa gerezani. 32 Akasema naye maneno mazuri, akaweka kiti chake juu ya viti vya wafalme waliokuwa pamoja naye huko Babeli”.
Yeremia 52:31 “Hata ikawa, katika mwaka wa thelathini na saba wa kuhamishwa kwake Yehoyakini, mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kumi na mbili, SIKU YA ISHIRINI NA TANO YA MWEZI, Evil-merodaki, mfalme wa Babeli, katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, akamwinua kichwa chake Yehoyakini, mfalme wa Yuda, akamtoa gerezani.
32 Akasema naye maneno mazuri, akaweka kiti chake juu ya viti vya wafalme waliokuwa pamoja naye huko Babeli”.
Kwa ufupi kama tunavyoifahamu habari tunajua kuwa wana wa Israeli walimuasi Mungu sana mpaka ikafikia hatua ya wao kupelekwa tena utumwani Babeli kama walivyopelekwa zamani enzi za Misri.
Hivyo waliochukuliwa mateka, yaligawanywa katika makundi makuu matatu:
Kundi la kwanza ndio lile lililokuwa chini ya Mfalme, Yehoyakimu, ambalo Danieli alikuwa miongoni mwao.
Kundi la Pili, lilikuwa chini ya huyu Mfalme Yekonia/Yehoyakini, ambapo Nabii Ezekieli naye alikuwa ndani ya kundi hili.
Na kundi la tatu lilikuwa ni la mfalme Sedekia, ambaye huyu alionyesha kiburi kwa Nebukadneza ikamfanya mpaka atobolewe macho, na kusababibishia kundi kubwa sana la wa-Yuda kuchukuliwa utumwani.
Sasa Tukirudi kwa huyu Yekonia ambaye yeye alichuliwa katika awamu ya pili alipokuja kuchukuliwa yeye hakuleta ubishi kwa Mfalme wa Babeli badala yake alijisalimisha kwa amani yeye na familia yake, hivyo Evil-Mordekai hakumuua, na badala yake alimchukua na kumwekwa vifungoni Babeli,..Alikaa huko hadi ulipofika wakati wa mfalme wa Babeli kumuhurumia na kumtoa..
Jibu ni kwamba biblia haijajichanganya hapo, ikumbukwe kuwa hata leo hii mfano Raisi wa nchi akitoa tamko la wafungwa kadhaa kupokea msamaha, na hivyo wawe huru, haimaanishi kuwa ni siku hiyo hiyo wanatoka gerezani..Bila shaka kutakuwa na shughuli za makaratasi ambazo zitafuata baada ya hapo kwa kwa muda, aidha, kwa siku kadhaa, au wiki kadhaa, na ndipo baadaye wawe huru.
Vivyo hivyo ilivyokuwa kwa Yekonia, tarehe 25 yake ilikuwa ni kama tamko la yeye kuwa huru, na siku ya tarehe 27 ndio ikawa siku yake ya kuwa huru. Hivyo waandishi kutofautiana haimaanishi kuwa kuna hitilafu, kinyume chake ni kuwa wote wapo sawa. Mmoja aliichukua siku ya tamko, na mwingine akaichukua siku ya kuwekwa huru.
Ubarikiwe.
NINAJUA MAWAZO NIKUWAZIAYO:
MNARA WA BABELI
TUPO KATIKA ZAMU YA NNE YA MWISHO.
USITUMAINISHWE NA MANENO YA UONGO.
DANIELI: Mlango wa 9
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Shalom, karibu tujifunze maandiko.
Katika maisha kumbuka kumtolea Mungu, kamwe usilisahau jambo hilo, uwe ni mchungaji, mwalimu, nabii, au muumini wa kawaida au yeyote Yule…maadamu tayari umeshamkabidhi Yesu maisha yako, kamwe usisahau kumtolea Mungu…Wengi wanakidharau hichi kipengele…ni kweli kabisa hatuwezi kumpa Mungu chochote kile kwasababu vyote vinatoka kwake…lakini utoaji wetu una nafasi kubwa sana katika moyo wa Mungu. Kutoa ni ishara ya kuonyesha unajali, unapenda na unathamini.. haijalishi hicho unachokitoa ni kidogo kiasi gani lakini kina nafasi kubwa sana katika moyo wa Yule unayemtolea.
Hebu tafakari mwanao anatoka shule anakuletea zawadi ndogo tu ya kalamu anakwambia mama/baba nimepita pale nimeona kalamu nzuri nimeinunua itakufaa kwa kazi zako…ukizingatia hiyo hela aliyonunulia ni wewe ndio uliyempa…Bila shaka kitendo hicho kitakugusa sana moyo…badala ya kuichukua ile kalamu kwa furaha kwamba umepata kitu kutoka kwa mwanao, badala yake utaichukua kwa moyo mwingine…itakutafakarisha sana, zaidi itakupa nafasi ya kumjua mwanao vyema, na kumpenda na kumwamini…na zaidi ya yote kutafuta kumlipa hata mara kumi ya kile alichokufanyia wewe.
Na ndio hivyo hivyo tunapokuwa na moyo wa kumtolea Mungu…fedha ile, au sadaka ile au chochote kile unachompa…kwake haendi kukitafsiri kama fedha, bali anakitafsiri kama moyo wa upendo, wa kumjali na wa kumheshimu..Utajisikiaje Mungu ajihisi unampenda??..bila shaka ni jambo zuri. Na lina thawabu sana.
Na pia kumtolea Mungu sio jambo la kukumbushwa…na wala hatulazimishwi na Mungu kumtolea yeye… “Kutoa ni kitu ambacho kinatoka ndani ya mtu baada ya kujua umuhimu wa kufanya hivyo”..
Na sehemu sahihi ya kumtolea Mungu ni mahali linapofundishwa Neno lake (ndio tafsiri ya sadaka)..Na Mungu wetu hazikusanyi sadaka hizo na kuzihifadhi mbinguni,…sadaka hizo zinatumika kwa kuiendeleza kazi yake kwa kutumia watumishi wake..Hivyo unapotoa kiwango Fulani cha fedha kama sadaka yako, fedha hiyo inakwenda kwa watumishi wa Mungu na hao ndio wanaoipangia bajeti kwa hekima ya Roho…Lakini kumbuka pia Mungu ananjia nyingi za kuifanya kazi yake iendelee kuwepo…hivyo wewe au mimi sio jiwe kuu la pembeni kwamba tusipomtolea basi atakwama!…ana njia zaidi ya milioni moja kulisimamisha kusudi lake pasipo hata mtu yeyote kutoa chochote.
Esta 4:10 “Ndipo Esta akasema na Hathaki, akamtuma tena kwa Mordekai, kusema, 11 Watumwa wote wa mfalme wanajua sana, hata na watu wa majimbo ya mfalme, ya kwamba mtu ye yote, akiwa mwanamume au mwanamke, atakayemjia mfalme katika ua wa ndani, wala hakuitwa, kuna sheria moja kwake, ni kwamba auawe; isipokuwa yeye ambaye mfalme atamnyoshea fimbo ya dhahabu, ili aishi; wala mimi sikuitwa niingie kwa mfalme yapata siku thelathini. 12 Basi wakamwambia Mordekai maneno ya Esta. 13 Naye Mordekai akawaagiza wampelekee Esta jibu la kusema, Wewe usijidhanie kuwa wewe utaokoka nyumbani mwa mfalme, zaidi ya Wayahudi wote. 14 Kwa maana wewe ukinyamaza kabisa wakati huu, ndipo kutakapowatokea Wayahudi msaada na wokovu kwa njia nyingine; ila wewe utaangamia pamoja na mlango wote wa baba yako; WALAKINI NI NANI AJUAYE KAMA WEWE HUKUUJIA UFALME KWA AJILI YA WAKATI KAMA HUO? ”
Esta 4:10 “Ndipo Esta akasema na Hathaki, akamtuma tena kwa Mordekai, kusema,
11 Watumwa wote wa mfalme wanajua sana, hata na watu wa majimbo ya mfalme, ya kwamba mtu ye yote, akiwa mwanamume au mwanamke, atakayemjia mfalme katika ua wa ndani, wala hakuitwa, kuna sheria moja kwake, ni kwamba auawe; isipokuwa yeye ambaye mfalme atamnyoshea fimbo ya dhahabu, ili aishi; wala mimi sikuitwa niingie kwa mfalme yapata siku thelathini.
12 Basi wakamwambia Mordekai maneno ya Esta.
13 Naye Mordekai akawaagiza wampelekee Esta jibu la kusema, Wewe usijidhanie kuwa wewe utaokoka nyumbani mwa mfalme, zaidi ya Wayahudi wote.
14 Kwa maana wewe ukinyamaza kabisa wakati huu, ndipo kutakapowatokea Wayahudi msaada na wokovu kwa njia nyingine; ila wewe utaangamia pamoja na mlango wote wa baba yako; WALAKINI NI NANI AJUAYE KAMA WEWE HUKUUJIA UFALME KWA AJILI YA WAKATI KAMA HUO? ”
Unaona hapo? Malkia Esta alidhani yeye asipoongea chochote ndio wayahudi watakufa..lakini Mordekai anamjibu na kumwambia asijidhanie kuwa asipozungumza chochote ndio wayahudi watakufa kinyume chake Mungu anaweza kufungua njia nyingine ya wokovu na wayahudi wote wakapona na yeye akafa katika huo umalkia wake…Lakini alipojinyenyekeza ndipo Mungu akamtumia yeye (Esta) kuwa wokovu kwa Israeli..Lakini angekaa kimya, Mungu angefungua wokovu kwa njia nyingine.
Ndivyo hivyo hivyo na sisi tunapojinyenyekeza na kumtolea Mungu,..basi sisi tunafanyika kuwa sehemu ya yeye kulikamilisha kusudi lake, tunafanyika sehemu ya yeye kuifanya kazi yake iendelee….Badala ya kumtumia mtu Fulani anakutumia wewe…Kama Mordekai alivyomwambia Esta “WALAKINI NI NANI AJUAYE KAMA WEWE HUKUUJIA UFALME KWA AJILI YA WAKATI KAMA HUO? ”..Lakini kama hatutaki, wala hatulazimishi, kazi zake zitaendelea kama kawaida kwasababu atawatumia wengine na si sisi…na kuwabariki hao na si sisi.
Bwana atusaidie kuyajua hayo, na kuyafanyia kazi kwa vitendo na si kwa midomo tu.
Maran atha!
CHUKIZO LA UHARIBIFU
DAKIKA MOJA TU, INAKUFANYA UMWAMINI SHETANI?
NA UPEPO WA KUSI ULIPOANZA KUVUMA KIDOGO,
USIHUSISHE HISIA KATIKA KUMTOLEA MUNGU.
ESTA: Mlango wa 4
EPUKA MUHURI WA SHETANI
RAFIKI WA KWELI NI YUPI?
Shalom, Ni siku nyingine tena Bwana ametukirimia kuiona kwa neema zake nyingi, Hivyo nakukaribisha tuyatafakari kwa pamoja maneno makuu ya Mungu wetu maadamu siku ile inakaribia.
Leo tutakitazama tena kitabu cha mwanzo, hususani juu ya uchaguzi waliouingia watu wawili, ambao tutaona hatma zao mbeleni zilikuja kuwa nini katika kizazi cha saba..
Mtu wa kwanza tutakayemwangalia atakuwa ni Kaini na pili Ni Sethi.
Kama tunavyojua Kaini alikuwa ni mtu wa kwanza kuikaribisha laana ya Mungu katika Maisha yake, aliambiwa atakuwa mtoro na mtu asiyekuwa na kikao duniani.. Sasa wengi wetu leo hii tunapomfikiria Kaini kwa laana alizopewa na Mungu tunamwona kama ni mtu aliyekuja kufanana na kichaa tu kama wale waokota makopo na maskini..Lakini ninao uhakika kama wengi tungekuwepo wakati ule anaishi duniani basi wengi wangejipendekeza sana kwa Kaini, hususani wale wanaoangalia mafanikio ya mtu kama ndio kipimo cha kubarikiwa na Mungu, Kwasababu biblia inatuonyesha, sio tu Kaini alikuwa ni mtu mwenye maendeleo makubwa bali uzao wake wote pia baada yake, (yaani Watoto wake),walikuwa ni watu wenye akili nyingi, wenye elimu, na ujuzi wa kuvumbua mambo mbali mbali, (Soma 4:16-24).
Hivyo kama kubarikiwa kimwili na kiakili, basi Kaini alibarikiwa mara nyingi sana Zaidi hata ya Sethi,
Lakini tukirudi kwa Sethi sasa, ambaye alizaliwa kulijaza pengo la Habili, mambo yalikuwa tofuati kidogo, yeye muda mfupi tu baada ya kumzaa, mwanaye Enoshi,Akatafakari akaona mbona hali sio kama inavyopaswa iwe? Mbona bado kama haya Maisha yanaonekana ni bure bila Mungu hata kama tunajihangaisha vipi, Mbona kama mwenye hii dunia amekaa kimya na hatusemeshi, kwanini na sisi tuendelee kubakia tu hivyo hivyo tunajiamulia tu mambo yetu wenyewe bila yeye..Hapana hii sio sawa, ni lazima kuanza kumtafuta Mungu.
Sethi na Watoto wake wakaanza kuweka mipango Madhubuti na namna ya kumtafuta Mungu, pengine wakaanza kujifunza kusali, wakaanza kujifunza kufunga, wakaanza kujifunza kuishi Maisha ya haki, ili tu walau wampate Mungu waliyempoteza, walianza kujifunza kumtolea Mungu sadaka mbalimbali, Wakaliita jina la Bwana kwa nguvu zote na kwa bidii..
Biblia inatuambia..
Mwanzo 4:26 “Sethi naye akazaa mwana; akamwita jina lake Enoshi. HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.”
Tofauti na Kaini Pamoja na uzao wake, wao uvumbuzi ulikuwa ni bora kuliko kitu kingine, uchumi, ulikuwa ni wa maana Zaidi katika Maisha kuliko kitu kingine chochote, elimu na ustaarabu ndio vilikuwa ni kiini cha ustaarabu wao..na Mungu hakuwa kitu kwao.
Lakini nataka uone matokeo ya kila mmoja alipofika katika kizazi kile cha saba..
Ukitazama pale, utaona Ule uzao wa Sethi, waliendelea hivyo hivyo kumwita Bwana bila kuchoka, ndipo akazaliwa mtu mmoja aliyeitwa Henoko, mtu huyu alikuwa mzao wa saba alitembea na Mungu hadi kufikia hatua ya kumpendeza na kunyakuliwa..akaenda moja kwa moja kifuani mwa Mungu..
Unaweza kuona hiyo ilikuwa ni bidii ya wao kuliita jina la Mungu, hadi mtu wao wa saba kunyakuliwa.
Lakini upande wa pili wa Kaini, mambo yalikuwa tofauti, mtu wa saba aliitwa Lameki, yeye ndio aliyekuwa mbaya mara kumi Zaidi hata ya Kaini baba yake..Licha ya kwamba yeye ndiye alikuwa mwanzilishi wa ndoa za mitara duniani, lakini alikuwa ni muuaji wa watu wasiokuwa na hatia wengi.. Lakini cha ajabu ni kuwa uzao wake uliendelea kuwa na mafanikio makubwa duniani, tusome..
Mwanzo 4:19 “Lameki akajitwalia wake wawili, jina la wa kwanza ni Ada, na jina la wa pili ni Sila. 20 Ada akamzaa Yabali; huyo ndiye baba yao wakaao katika hema na kufuga wanyama. 21 Na jina la nduguye aliitwa Yubali; huyo ndiye baba yao wapigao kinubi na filimbi. 22 Sila naye akamzaa Tubal-kaini, mfua kila chombo cha kukatia, cha shaba na cha chuma; na umbu lake Tubal-kaini alikuwa Naama. 23 Lameki akawaambia wake zake, Sikieni sauti yangu, Ada na Sila; Enyi wake za Lameki, sikilizeni usemi wangu; Maana nimemwua mtu kwa kunitia jeraha; Kijana kwa kunichubua; 24 Kama Kaini akilipiwa kisasi mara saba, Hakika Lameki atalipiwa mara sabini na saba”.
Mwanzo 4:19 “Lameki akajitwalia wake wawili, jina la wa kwanza ni Ada, na jina la wa pili ni Sila.
20 Ada akamzaa Yabali; huyo ndiye baba yao wakaao katika hema na kufuga wanyama.
21 Na jina la nduguye aliitwa Yubali; huyo ndiye baba yao wapigao kinubi na filimbi.
22 Sila naye akamzaa Tubal-kaini, mfua kila chombo cha kukatia, cha shaba na cha chuma; na umbu lake Tubal-kaini alikuwa Naama.
23 Lameki akawaambia wake zake, Sikieni sauti yangu, Ada na Sila; Enyi wake za Lameki, sikilizeni usemi wangu; Maana nimemwua mtu kwa kunitia jeraha; Kijana kwa kunichubua;
24 Kama Kaini akilipiwa kisasi mara saba, Hakika Lameki atalipiwa mara sabini na saba”.
Ndugu, hata leo zao hizi mbili zipo duniani..Na zao hizi kwa agano jipya hazijaanza leo wala jana, bali tangu wakati wa Kristo Yesu kuwepo duniani..Uzao wa kwanza ndio ule wa kanisa la kwanza la mitume lililojulikana kama Efeso…Tangu ile siku ya pentekoste watu walianza kuliita jina la Bwana, na Kristo akawahidia kuwa atawanyakua..Lakini Unyakuo Mungu alikwisha upanga kwa mtu wa saba, ambalo ndio kanisa la Saba na la mwisho, ndio hili tunaloishi mimi na wewe, lijulikanalo kama Laodikia (Ufunuo 3)..
Hivyo moja ya hizi siku watakatifu wa kanisa hili watondolewa duniani ghafla kwa tukio maarufu lijulikanalo kama Unyakuo. Watakatifu wataondolewa! Kuipisha dhiki kuu duniani.
Lakini sasa ule upande wa pili uzao wa Ibilisi, huo tangu zamani hauna Habari na Mungu, wenyewe unatazama tu mambo ya duniani, elimu, pesa, uchumi, mafanikio, ukiueleza Habari za Mungu unakucheka, unakudhihaki, unakuona,, ukiuambia hizi ni siku za mwisho utakuambia wacha hadithi za kizee..
Ndugu tunaishi ukingoni mwa wakati, kama wewe ni mkristo, basi usiache kuliiita jina la Bwana kwa bidii maadamu una muda, kwasababu wakati si mrefu aidha uwe hai au uwe umekufa, parapanda italia na utaenda kwenye unyakuo mfano wa Henoko. Na hapo ndipo utakuwa mwisho wa mateso yako.
Lakini wewe kama Habari hizi za wokovu ni kelele tu kwako, nakushauri ubadilike sasa. Mgeukie Kristo na yeye atakupokea kigeuza nia yako.
Bwana akubariki.
Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?
Mtu astahiliye hofu ni yupi?
Je! ni vema kwa mkristo kwenda hospitali au kutumia miti shamba anapougua?
Tamaa yako itakuwa kwa mumeo.Ni tamaa ipi ya Hawa?
TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!
WhatsApp
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze maandiko…Si vibaya tukajikumbusha yale ambayo tumeshawahi kujifunza mahali tofauti tofauti…
biblia inasema katika..
1Wathesalonke 4:4 “kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima 5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu”.
1Wathesalonke 4:4 “kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima
5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu”.
Biblia imetufundisha kujizuia, maana yake ni yale ambayo unaweza kuyafanya, unajinyima kuyafanya…Kadhalika imetufundisha pia kuiweza miili yetu…Kuiweza miili yetu hakuna tofauti sana na kujizuia…Kuuweza ni hali ya wewe kuuendesha mwili na si mwili kukuendesha wewe.
Na moja ya vitu vinavyowaendesha watu wasiomjua Mungu ni tamaa ya uasherati..ndio inayozungumziwa hapo katika mstari wa 5.
Na hiyo ili iondoke ni lazima kujifunza kuulazimisha mwili kukutii wewe, na huko kwanza kunakuja kwa kumkaribisha Yesu katika maisha, na baada ya hapo kumpokea Roho Mtakatifu ambaye atakusaidia kukupa nguvu za kuweza kuutiiisha mwili wako…sio kwamba Roho Mtakatifu atakuzuia usitende dhambi hapana!..Yeye atakupa uwezo wa wewe kuishinda dhambi inayofanya kazi katika viungo vyako (yaani mwili wako)
Yakobo 4:1 “Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu?”
Na baada ya kumwamini na kumpokea Yesu, hatua inayofuata ni kujitenga mbali na vichocheo vyote vya tamaa….shetani anatamani utubu tu lakini usiache ile dhambi….anataka utubie uzinzi/ uasherati lakini hataki ufanye uamuzi wa kuacha kutazama picha chafu za ngono, anataka utubie anasa na matusi lakini hataki uache kuisikiliza ile miziki ya kidunia ambayo hiyo ndio kichocheo cha kwanza cha mambo hayo..n.k
Vitu vyote vinavyokusababishia kulipuka tamaa unajiweka mbali navyo…kama ni vipindi kwenye tv na movie, unajitenga navyo, kama ni aina Fulani ya marafiki, ni hivyo ivyo kama ni magroup Fulani kwenye mitandao, unayaacha…Ni wewe kufanya uamuzi kwanza..kwa kufanya hivyo utafanikiwa kuuweza mwili wako..
Hivyo tunaonywa tujifunze kuiweza miili hii…Inawezekana kabisa kuishinda na ni rahisi sana, ndio maana biblia imesema tujifunze kuiweza! ingekuwa haiwezekani kabisa kuiweza, basi Mungu si dhalimu asingetupa jukumu zito kiasi hicho.
Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?
JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?
BIBLIA INATUASA TUFANYE NINI KATIKA ZAMA HIZI ZA UOVU?
KUTAHIRIWA KIBIBLIA
USIFE NA DHAMBI ZAKO!
JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?
Zipo siri nyingi za ufalme wa mbinguni ambazo Mungu amezificha katika agano la kale, na ndio maana biblia inatuambia torati ni kivuli cha mambo yanayoendelea katika agano jipya (Waebrania 10:1)..
Kwa mfano embu tuiangazie ile Habari ya Musa baada ya kutoroka Misri na kukimbilia katika jangwa la Midiani, kwa ufupi biblia inatuambia alipofika kule alikutana na binti mmoja wa kikushi (ki-Afrika) aliyeitwa Sipora, Ambaye alifanikiwa kumwoa na akaishi naye kama mke wake kwa kipindi kirefu sana, pengine Zaidi ya miaka 30 Na…
Lakini siku moja Musa alipokuwa anachunga mifugo ya mkwewe kule jangwani baada ya miaka 40 kupita tangu atoke Misri, ghafla alitokewa na Mungu na kupewa maagizo ya kuwarudia tena ndugu zake kule Misri kwa lengo la kuwaokoa. Ndipo Musa akatii mara moja kushuka Misri, lakini kuna jambo nataka ulione pale, kwamba Musa hakuondoka Midiani na kwenda na Mke wake ili ashuhudie lile kusudi la Mungu la kuwaokoa wana wa Israeli..Bali alimwacha kwao, salama akaondoka yeye peke yake Pamoja na Haruni.
Na baadaye Bwana alipomaliza kuwakomboa wana wa Israeli kule Misri kwa mkono wa Musa, na kuwavukisha bahari ya shamu, shughuli yote ile nzito ilipokwisha ndipo tunamwona sasa, Sipora akiletwa na Yethro baba yake kwa Musa kule jangwani..
Unaweza kujiuliza ni kwanini Sipora hakwenda Misri na Musa..
Musa anamfunua Kristo, na Sipora anamfunua bibi-arusi wake..
Sasa kama vile Musa alipowakimbia ndugu zake kule mwanzoni, walipotaka kumshitaki kwa farao, lakini alitoroka na kukimbilia jangwani na huko akakutana na Sipora ndivyo ilivyo kwa Yesu Bwana wetu, ndugu zake wayahudi (yaani Waisraeli)
walipomkataa, akawaacha ukiwa kama maandiko yanavyosema (katika Mathayo 23:27-39), akaenda zake mbali nao, mahali wasipopajua wao (Yohana 7:33-36), ndipo huko huko akakutana na sisi watu wa mataifa, tukapewa neema tusiyostahili ya kufanyika bibi-arusi wa Kristo..
Sisi(watu wa mataifa) tunafananishwa na Sipora kwa Kristo..
Na kama vile Musa alivyotumia muda mwingi wa kuishi na Sipora kabla ya kuwarudia tena ndugu zake, vivyo hivyo na Kristo naye ameishi na kanisa lake takatifu la mataifa sasa kwa takribani miaka 2000. (Ndio maana neema ipo kwetu sasa, sisi watu wa mataifa ndio tunaomtumainia Yesu kuliko waisraeli,..Wayahudi sasa hawamwamini Kristo hata kidogo.)
Lakini siku moja isiyo na jina, ghafla, Musa aliona kijiti kinateketea moto na muda huo huo Mungu akamwambia aondokea arudi kuwaokoa wana wa Israeli ambao walikuwa wanamlilia tangu zamani awaokoe dhidi ya maadui wao.. Ndivyo itakavyokuwa siku ile ambayo Mungu atapowarudishia tena hii neema ya wokovu wana wa Israeli ili waokolewe na maadui zao..Itakuwa ni ghafla tu ya siku moja..
Ipo siku Wayahudi watarudiwa na Mungu tena, na ufalme utarudishwa kwao Soma..
Matendo 1:6 “Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme? 7 Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe”.
Matendo 1:6 “Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme?
7 Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe”.
Umeona hapo!..maana yake yapo majira yanayokuja ya Mungu kuwarudishia Israeli ufalme!
Siku hiyo Mungu atamtuma Kristo tena ulimwenguni kuja kuwaokoa, lakini hatakuja mikono mitupu kama ilivyokuwa hapo mwanzo, bali atakuja na fimbo mkononi mwake, kuyaadhibu mataifa, na kipindi hicho kitakuwa ni kipindi cha dhiki kuu ya ajabu ambayo haijawahi kutokea duniani..
Mapigo Kristo atakayoyaleta duniani yale ya Musa ni mfano mdogo sana, soma Ufunuo 8,9,16, utaona pale..
Lakini cha ajabu ni kuwa katikati ya mapigo hayo Mke (Bibi-arusi )wa Yesu Kristo hatakuwepo..(kama vile Sipora jinsi alivyokosekana wakati Musa anashuka Misri)
Sasa atakuwa wapi?
Jibu lipo wazi, atakuwa ameshakwenda kwenye unyakuo siku nyingi!!.. Hivyo dhiki zote na mapigo yote hayatamuhusu hata kidogo kama ilivyokuwa kwa Sipora..
Na jambo lingine ambalo ni vizuri ukajua ni kuwa, Bibi-arusi(mke) huwa anathamani kubwa, kuliko ndugu machoni pa mhusuka..Na ndio maana utaona hata pale Haruni na Miriamu ndugu zake Musa walipojaribu kumzungumzia vibaya tu Sipora, Mungu aliwaadhibu saa hiyo hiyo (Hesabu 12).
Hiyo ni kuonyesha kuwa thamani ya kuwa bibi-arusi wa Kristo ni kubwa kuliko kitu kingine chochote.. Unaona ni jinsi gani mimi na wewe tulivyo na nafasi kubwa machoni pa Kristo Zaidi hata ya wale wayahudi unaowaona kule Israeli wanaoishika torati?, Lakini hiyo ni mpaka tutakapokubali kuutii wokovu.
Na kumbuka sio kila anayesema nimeokoka ni bibi-arusi, hapana, kigezo cha kuwa bibi-arusi wa Kristo ni sharti uwe bikra rohoni, yaani umejitenga na mambo maovu, kwa Maisha matakatifu unayoishi na vilevile unao uhusiano wa karibu na Kristo aliyekuokoa.. Lakini sio kwa kutamka tu..
Hizi ni siku za mwisho, Kama bado hujampa Kristo Maisha yako, au haujaitengeneza taa yako vizuri fahamu kuwa Unyakuo upo mlangoni sana, Siku moja inapopita ujue kuwa ndivyo unavyoikaribie ile siku, pengine ni leo usiku, pengine ni kesho tu, pengine mwezi huu hauishi Kristo atakuwa amesharudi..Jiulize akirudi na kukuta katika hali hiyo uliopo, utajibu nini na injili zote unahubiriwa?
Kumbuka aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi.
Wayahudi macho yao yalifumbwa wasimwamini Kristo, lakini siku za mwisho watakwenda kumwamini Kristo atakaporudi kwao (upatapo muda kapitie vipengele hivi Warumi 11 na Zekaria 12)
USISUBIRI MPAKA MUNGU AKUAMBIE, NDIO UFANYE!
KUPATA MAONO YA MBINGUNI SIO KUFIKA MBINGUNI.
NEEMA YA MZALIWA WA PILI.
NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.
Je! Ni dhambi kwa kijana aliyeokoka kuvaa suruali za kubana (model), kunyoa mitindo (mfano kiduku), ?
Umewahi kujiuliza Zamu ya nne ni nini? Kama tunavyoisoma katika Mathayo 14:25?
Tusome,
Mathayo 14:25 “Hata wakati wa ZAMU YA NNE ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari. 26 Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu”.
Mathayo 14:25 “Hata wakati wa ZAMU YA NNE ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.
26 Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu”.
Miji ya zamani ilivyojengwa ni tofauti na miji za nyakati hizi zetu…Miji ya zamani ilijengwa huku imezungukwa na ukuta pande zote…na Mara nyingi ukuta huo ulikuwa ni mrefu sana na mageti yake makubwa kiasi kwamba hata gari la farasi liliweza kupita juu ya ule ukuta bila shida yoyote, mfano utaona ule ukuta wa Yeriko, ndivyo ilivyokuwa na miji yote mikubwa ni lazima izungushiwe ukuta, hata Babeli Pamoja na Yerusalemu ilijengwa kwa mifumo hiyo, na lengo la kuizungushia kuta ndefu ni kujilinda dhidi ya maadui…Mji ambao ulikuwa hauna ukuta ulikuwa unajulikana kama mji dhaifu..Na mageti ya mji usiku yalikuwa ni lazima yafungwe.
Na hilo tu peke yake lilikuwa halitoshi, katikati pia ya zile kuta Pamoja na pembezoni walikuwa wanatengeneza minara mirefu (iliyojulikana kama minara ya walinzi)..Minara hiyo walikuwa wanawekwa walinzi, ambao watakesha kwa zamu usiku kutazama pande zote kwa usalama wa mji.
Sasa walinzi hao walikuwa wanalinda kwa zamu (yaani kwa kupokezana)..masaa matatu matatu kwa vipindi vinne…zamu ya kwanza walikuwa wanaanza kulinda kuanzia saa moja jioni mpaka saa tatu usiku…kisha wanapokea wengine kulinda zamu ya pili kuanzia hiyo saa tatu usiku hadi saa sita usiku…kisha wanaingia wengine kulinda zamu ya tatu inayoanza saa sita usiku mpaka saa 9 usiku na mwisho inaingia zamu nyingine ya mwisho ya walinzi wengine kumalizia zamu ya mwisho ya 4, inayoanza saa 9 hadi saa 12 asubuhi.
Kwahiyo ilikuwa ni desturi tukio likitokea usiku, muda ule lilolotukia ulitambulika kwa ZAMU na si kwa masaa kama sasa nyakati zetu hizi tunavyofanya..
Hali kadhalika na sisi wakristo ni walinzi katika roho..tunamngojea Bwana arudi katikati ya hili giza nene la maasi na maovu ya dunia, na hatujui atarudi muda gani…hajaja katika zamu ya akina Petro ambao walikuwa macho wanakesha, mpaka wanaondoka duniani, halikadhalika hakuja katika zamu ya watu wa kanisa la pili na la tatu na la nne…na sasa tupo kanisa la mwisho la saba (lijulikanalo kama Laodikia kulingana na Ufu. 3:14)…ambapo ndio tupo ile zamu ya mwisho YA NNE, ni lazima Bwana aje katika hichi kipindi, hatujui siku, tarehe wala mwaka…lakini majira tunayajua…tupo wakati wa kurudi kwa Bwana mara ya pili.
Luka 12:36 “nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara. 37 Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia. 38 NA AKIJA ZAMU YA PILI, AU AKIJA ZAMU YA TATU, na kuwakuta hivi, heri watumwa hao. 39 Lakini fahamuni neno hili, Kwamba mwenye nyumba angalijua saa atakayokuja mwivi, angalikesha, wala asingaliacha nyumba yake kuvunjwa. 40 Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu”.
Luka 12:36 “nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.
37 Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia.
38 NA AKIJA ZAMU YA PILI, AU AKIJA ZAMU YA TATU, na kuwakuta hivi, heri watumwa hao.
39 Lakini fahamuni neno hili, Kwamba mwenye nyumba angalijua saa atakayokuja mwivi, angalikesha, wala asingaliacha nyumba yake kuvunjwa.
40 Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu”.
Tupo katika dakika za hatari sana, kama katika watu ambao wangepaswa wawe macho juu ya suala la Unyakuo wa kanisa basi ni sisi, lakini cha ajabu ni kuwa wengi wetu tunachukulia kimzaha mzaha tu, tunaishi kama tunavyotaka,tukidhani na mbinguni pia tutaingia tu kama tunavyotaka..Tupo buzy ni shughuli za ulimwengu huu, hatuna habari na Mungu..Bwana atusaidie katika hili ili sote tujue zamu tuliyopo, kuwa ndio ile zamu ya nne ya mwisho, na kwamba zamu hii haitapita kabla Kristo hajarudi…Wakati umeenda sana ndugu.
Je! umesimama imara na wokovu.
Bwana atupe macho ya kuliona hilo.
USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.
SI KWA FAIDA YA MWENYEZI, BALI KWA FAIDA YETU.
Kwanini wakristo wengi ni maskini?.
Ni kwa namna gani Yesu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka?
Ni uthibitisho upi unaoonyesha kuwa kuna MBINGUNI na KUZIMU?
SWALI: Katika Wakolosai 3:11 tunaona neno “Mshenzi” likitajwa.Kwanini Neno hili liwekwe pale?
Wakolosai 3:11 “Hapo hapana Myunani wala Myahudi, kutahiriwa wala kutokutahiriwa, mgeni wala MSHENZI, mtumwa wala mwungwana, bali Kristo ni yote, na katika yote”.
Mshenzi kulingana na kamusi ni mtu asiyejali mambo ya Ki-Mungu, asiyekuwa na staha, au adabu ni rahisi kujiamulia tu mambo yake mwenyewe, hata kuua yeye hajali, na mara nyingi anakuwa ni mkatili na mnyama.
Sasa enzi hizo za kanisa la kwanza kulikuwa na kundi maalumu lililojulikana kama washenzi, jamii ya watu hao walikuwa wanaishi kando kando mwa bahari ya Nyeusi(Black sea) ambao kwasasa ni maeneo ya Urusi, Ni watu ambao walikuwa hawana elimu na walikuwa ni wafugaji wanaohama hama, pia walikuwa ni wakatili na wanyama sana, walikuwa mara nyingi wanafananishwa na wanyama wa mwituni kwa ukatili wao.
Hivyo watu wa namna hiyo, waliitwa washenzi.. Lakini cha ajabu ni kwamba na wao pia walihesabiwa kustahili neema ya Yesu Kristo.
Hata sasa zipo jamii nyingi za watu ulimwenguni wa namna hizi au zaidi hata huku Afrika, ambazo zinaweza kuonekana kama hazistahili kupokea neema ya injili kwa staili yao ya maisha, kwa kuwa nyuma kimaendeleo, watu wake kuwa ni wajinga, ma-bushmen, wanaotembea uchi, wanakula nyama za watu, hawana imani na kitu chochote kile n.k.(Ambao kwa namna nyingine wangeitwa washenzi ) Lakini kumbe hao nao Mungu anawatazama na neema yake ya wokovu inapaswa iwafikie kama wengine..
Hiyo ni kutufundisha kuwa hatupaswi kuchagua mtu bali ni sharti injili ihubiriwe kwa kila kiumbe.(Mungu hana ubaguzi kwa mtu yoyote yule, katika suala la wokovu hatatazami rangi, wala ukabila wala utaifa, wote ni watu wake wanaostahili wokovu sawa kupitia mwanawe mpendwa Yesu Kristo, ambaye ni Bwana wetu)
TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.
KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 2
TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?
Je ni sahihi kumtenga mtu anapofanya dhambi kanisani?
SWALI: Andiko hili lina maana gani?..1Timotheo 5: 22 “Usimwekee mtu mikono kwa haraka, wala usizishiriki dhambi za watu wengine. Ujilinde nafsi yako uwe safi”
JIBU: Maana ya awali ya mstari huo sio ile inayodhaniwa na wengi ya “Mtumishi wa Mungu, kumwekea mikono mtu mwenye tatizo fulani au ugonjwa fulani” na kumwombea…Hiyo sio maana ya msingi ya mstari huo…inaweza kuwa maana ya pili ya mstari huo …lakini maana ya msingi kabisa ya mstari huo ni “kuwekewa mikono kwa ajili ya utumishi”.
Huu ni waraka ambao Mtume Paulo alimwandikia Timotheo ambaye alikuwa ni mtumishi wa Mungu…Paulo alimfundisha madaraka ya kuitumishi kwa uongozo wa Roho Mtakatifu, ambayo unaweza kuyasoma yote katika wakara huo (yaani kuanzia sura ya kwanza hadi ya mwisho). Na mojawapo ya madaraka aliyompa ni madaraka ya kuwawekea mikono watumishi wapya, wale ambao tayari karama zao zimeshaanza kuonekana katika kanisa hivyo wapo tayari kuifanya kazi ya ki-utumishi katika mwili wa Kristo..kama jinsi yeye alivyowekewa..
1Timotheo 4:14 “Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa KUWEKEWA MIKONO YA WAZEE”
Kwahiyo hapa Timotheo naye anaagizwa wakati wa kuwawekea mikono watumishi wapya (mfano..maaskofu wapya, wachungaji wapya wa makanisa, waalimu, au manabii) asiwe na haraka!…bali achukue muda kumsoma mtu yule, tabia yake, mwenendo wake, je kama ni kweli kaitwa, ama ni kweli ana nia ya Kristo, kama ni kweli amekidhi vigezo vyote vya kimaandiko..Ndipo amtie mikono na kumbariki.
Kwasababu wale waliotiwa mikono ni kama wamehalalishwa kuwa wamestahili kulitumikia kundi la Mungu, na hivyo watu wengi ni rahisi kuwaamini, kwahivyo endapo akiwekewa mikono mtu ambaye si sahihi, ambaye hana nia ya Kristo, ni mtu wa kidunia tu, anawaza fedha au ukubwa tu…na kundi lote likimwamini, basi ni rahisi kuleta uharibifu mkubwa sana katika kanisa…Ndio maana hapo juu Mtume Paulo anamwagiza Timotheo na kumwambia “asiwe mwepesi kumwekea mtu mikono kwa haraka”, maana yake achukue muda kumchunguza..
Na hata sasa makanisani inapaswa iwe hivyo hivyo..Kabla ya mtu kuwekewa mikono kuwa mchungaji, au askofu, au shemasi, au nabii, au mwalimu ni lazima awe ameshajaribiwa na kuhakikiwa vya kutosha ili asije akaliharibu kundi, vigezo vya uaskofu vinapatikana katika hiyo hiyo 1Timotheo
1Timotheo 3:1 “Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema. 2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha; 3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha; 4 mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu; 5 (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?) 6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi 7 Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.”.
1Timotheo 3:1 “Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.
2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;
3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;
4 mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu;
5 (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)
6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi
7 Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.”.
Hiyo ndio maana ya awali ya KUMWEKEA MTU MIKONO, iliyomaanishwa katika mstari huo…Maana ya pili ndio ile inayojulikana na wengi, ambayo ni ya kumfahamu mtu kwanza kabla ya kumwekea mikono kumwombea..
Wengi hususani watumishi mtu anapokuja ana tatizo fulani, au ugonjwa fulani ni wepesi kumwekea tu mikono pasipo kumjua mtu huyo kwa undani..ili tu mtu aonekane ni mtumishi wa Mungu…pasipo kujua ni hatari kufanya hivyo…Kwasababu unaweza kujikuta unalaani kilichobarikiwa au una bariki kilicholaaniwa.
Kwamfano mtu unaweza kukuta anafanya kazi ya madawa ya kulevya, au ujambazi, au ya ukahaba au uzaji pombe..na yeye anakuja kwako kuomba kazi zake ziende vizuri (mtu kama huyo alishawahi kunifuata mimi)..na wewe pasipo kufikiri, kwasababu kaja tu kutafuta msaada kutoka kwako, unamwekea mikono na kumbariki katika jina la Bwana…(hapo umebariki kilicholaaniwa.).
Badala yake ungepaswa umhoji kwanza shughuli anayoifanya, na kama akikiri ni ya madawa ya kulevya basi, unamhubiria kwanza atubu na kumpa Kristo Maisha yake, na kutafuta kazi nyingine ndipo umeombee baraka kwa Mungu wako na ndipo huyo mtu abarikiwe..
Wengine ni makahaba na hawajui kama katika ukahaba wao wanamkosea Mungu (nimewahi kukutana na kahaba ambaye katika ukahaba wake aliniambia anamwamini Mungu, na huwa Mungu anamleteaga wateja, na huwa anaiombeaga biashara yake mara kwa mara ili iende vizuri)..baada ya kumhubiria sana ndipo alipoelewa kwamba alikuwa anafanya makosa pasipo kujijua…Sasa mwanamke kama huyu, anapokwenda kanisani au kwa mtumishi ambapo hataulizwa maisha yake ni rahisi watu kuibariki kazi iliyo laaniwa na Mungu..Hivyo ni kuwa makini sana.
Na pia tumeonywa hapo! Tusizishiriki dhambi za watu wengine, unapomwekea mtu mikono kwa pupa ni rahisi kuzishiriki dhambi za yule mtu, kadhalika unaposhirikiana na watu waovu katika kanisa ambao wanajua kabisa mambo wanayoyafanya ni kinyume na maandiko lakini bado wanaendelea kuyafanya huko ni sawa na kuzishiriki dhambi zao..
Bwana atusaidie tuwe wakamilifu mbele zake daima.
VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.
Uasherati wa Kiroho maana yake nini?
HAKI HAIMWACHI KUISHI.
NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME
JIEPUSHE NA MASHINDANO YA DINI.
KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?
YA KALE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA