Category Archive Home

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze maandiko…Si vibaya tukajikumbusha yale ambayo tumeshawahi kujifunza mahali tofauti tofauti…

biblia inasema katika..

1Wathesalonke 4:4 “kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima

5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu”.

Biblia imetufundisha kujizuia, maana yake ni yale ambayo unaweza kuyafanya, unajinyima kuyafanya…Kadhalika imetufundisha pia kuiweza miili yetu…Kuiweza miili yetu hakuna tofauti sana na kujizuia…Kuuweza ni hali ya wewe kuuendesha mwili na si mwili kukuendesha wewe.

Na moja ya vitu vinavyowaendesha watu wasiomjua Mungu ni tamaa ya uasherati..ndio inayozungumziwa hapo katika mstari wa 5.

Na hiyo ili iondoke ni lazima kujifunza kuulazimisha mwili kukutii wewe, na huko kwanza kunakuja kwa kumkaribisha Yesu katika maisha, na baada ya hapo kumpokea Roho Mtakatifu ambaye atakusaidia kukupa nguvu za kuweza kuutiiisha mwili wako…sio kwamba Roho Mtakatifu atakuzuia usitende dhambi hapana!..Yeye atakupa uwezo wa wewe kuishinda dhambi inayofanya kazi katika viungo vyako (yaani mwili wako)

Yakobo 4:1 “Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu?”

Na baada ya kumwamini na kumpokea Yesu, hatua inayofuata ni kujitenga mbali na vichocheo vyote vya tamaa….shetani anatamani utubu tu lakini usiache ile dhambi….anataka utubie uzinzi/ uasherati lakini hataki ufanye uamuzi wa kuacha kutazama picha chafu za ngono, anataka utubie anasa na matusi lakini hataki uache kuisikiliza ile miziki ya kidunia ambayo hiyo ndio kichocheo cha kwanza cha mambo hayo..n.k

Vitu vyote vinavyokusababishia kulipuka tamaa unajiweka mbali navyo…kama ni vipindi kwenye tv na movie, unajitenga navyo, kama ni aina Fulani ya marafiki, ni hivyo ivyo kama ni magroup Fulani kwenye mitandao, unayaacha…Ni wewe kufanya uamuzi kwanza..kwa kufanya hivyo utafanikiwa kuuweza mwili wako..

Hivyo tunaonywa tujifunze kuiweza miili hii…Inawezekana kabisa kuishinda na ni rahisi sana, ndio maana biblia imesema tujifunze kuiweza! ingekuwa haiwezekani kabisa kuiweza, basi Mungu si dhalimu asingetupa jukumu zito kiasi hicho.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?

BIBLIA INATUASA TUFANYE NINI KATIKA ZAMA HIZI ZA UOVU?

KUTAHIRIWA KIBIBLIA

USIFE NA DHAMBI ZAKO!

JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

Zipo siri nyingi za ufalme wa mbinguni ambazo Mungu amezificha katika agano la kale, na ndio maana biblia inatuambia torati ni kivuli cha mambo yanayoendelea katika agano jipya (Waebrania 10:1)..

Kwa mfano embu tuiangazie ile Habari ya Musa baada ya kutoroka Misri na kukimbilia katika jangwa la Midiani, kwa ufupi biblia inatuambia alipofika kule alikutana na binti mmoja wa kikushi (ki-Afrika) aliyeitwa Sipora, Ambaye alifanikiwa kumwoa na akaishi naye kama mke wake kwa kipindi kirefu sana, pengine Zaidi ya miaka 30 Na…

Lakini siku moja Musa alipokuwa anachunga mifugo ya mkwewe kule jangwani baada ya miaka 40 kupita tangu atoke Misri, ghafla alitokewa na Mungu na kupewa maagizo ya kuwarudia tena ndugu zake kule Misri kwa lengo la kuwaokoa. Ndipo Musa akatii mara moja kushuka Misri, lakini kuna jambo nataka ulione pale, kwamba Musa hakuondoka Midiani na kwenda na Mke wake ili ashuhudie lile kusudi la Mungu la kuwaokoa wana wa Israeli..Bali alimwacha kwao, salama akaondoka yeye peke yake Pamoja na Haruni.

Na baadaye Bwana alipomaliza kuwakomboa wana wa Israeli kule Misri kwa mkono wa Musa, na kuwavukisha bahari ya shamu, shughuli yote ile nzito ilipokwisha ndipo tunamwona sasa, Sipora akiletwa na Yethro baba yake kwa Musa kule jangwani..

Unaweza kujiuliza ni kwanini Sipora hakwenda Misri na Musa..

Musa anamfunua Kristo, na Sipora anamfunua bibi-arusi wake..

Sasa kama vile Musa alipowakimbia ndugu zake kule mwanzoni, walipotaka kumshitaki kwa farao, lakini alitoroka na kukimbilia jangwani na huko akakutana na Sipora ndivyo ilivyo kwa Yesu Bwana wetu, ndugu zake wayahudi (yaani Waisraeli)

walipomkataa, akawaacha ukiwa kama maandiko yanavyosema (katika Mathayo 23:27-39), akaenda zake mbali nao, mahali wasipopajua wao (Yohana 7:33-36), ndipo huko huko akakutana na sisi watu wa mataifa, tukapewa neema tusiyostahili ya kufanyika bibi-arusi wa Kristo..

Sisi(watu wa mataifa) tunafananishwa na Sipora kwa Kristo..

Na kama vile Musa alivyotumia muda mwingi wa kuishi na Sipora kabla ya kuwarudia tena ndugu zake, vivyo hivyo na Kristo naye ameishi na kanisa lake takatifu la mataifa sasa kwa takribani miaka 2000. (Ndio maana neema ipo kwetu sasa, sisi watu wa mataifa ndio tunaomtumainia Yesu kuliko waisraeli,..Wayahudi sasa hawamwamini Kristo hata kidogo.)

Lakini siku moja isiyo na jina, ghafla, Musa aliona kijiti kinateketea moto na muda huo huo Mungu akamwambia aondokea arudi kuwaokoa wana wa Israeli ambao walikuwa wanamlilia tangu zamani awaokoe dhidi ya maadui wao.. Ndivyo itakavyokuwa siku ile ambayo Mungu atapowarudishia tena hii neema ya wokovu wana wa Israeli ili waokolewe na maadui zao..Itakuwa ni ghafla tu ya siku moja..

Ipo siku Wayahudi watarudiwa na Mungu tena, na ufalme utarudishwa kwao Soma..

Matendo 1:6 “Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme?

7 Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe”.

Umeona hapo!..maana yake yapo majira yanayokuja ya Mungu kuwarudishia Israeli ufalme!

Siku hiyo Mungu atamtuma Kristo tena ulimwenguni kuja kuwaokoa, lakini hatakuja mikono mitupu kama ilivyokuwa hapo mwanzo, bali atakuja na fimbo mkononi mwake, kuyaadhibu mataifa, na kipindi hicho kitakuwa ni kipindi cha dhiki kuu ya ajabu ambayo haijawahi kutokea duniani..

Mapigo Kristo atakayoyaleta duniani yale ya Musa ni mfano mdogo sana, soma Ufunuo 8,9,16, utaona pale..

Lakini cha ajabu ni kuwa katikati ya mapigo hayo Mke (Bibi-arusi )wa Yesu Kristo hatakuwepo..(kama vile Sipora jinsi alivyokosekana wakati Musa anashuka Misri)

Sasa atakuwa wapi?

Jibu lipo wazi, atakuwa ameshakwenda kwenye unyakuo siku nyingi!!.. Hivyo dhiki zote na mapigo yote hayatamuhusu hata kidogo kama ilivyokuwa kwa Sipora..

Na jambo lingine ambalo ni vizuri ukajua ni kuwa, Bibi-arusi(mke) huwa anathamani kubwa, kuliko ndugu machoni pa mhusuka..Na ndio maana utaona hata pale Haruni na Miriamu ndugu zake Musa walipojaribu kumzungumzia vibaya tu Sipora, Mungu aliwaadhibu saa hiyo hiyo (Hesabu 12).

Hiyo ni kuonyesha kuwa thamani ya kuwa bibi-arusi wa Kristo ni kubwa kuliko kitu kingine chochote.. Unaona ni jinsi gani mimi na wewe tulivyo na nafasi kubwa machoni pa Kristo Zaidi hata ya wale wayahudi unaowaona kule Israeli wanaoishika torati?, Lakini hiyo ni mpaka tutakapokubali kuutii wokovu.

Na kumbuka sio kila anayesema nimeokoka ni bibi-arusi, hapana, kigezo cha kuwa bibi-arusi wa Kristo ni sharti uwe bikra rohoni, yaani umejitenga na mambo maovu, kwa Maisha matakatifu unayoishi na vilevile unao uhusiano wa karibu na Kristo aliyekuokoa.. Lakini sio kwa kutamka tu..

Hizi ni siku za mwisho, Kama bado hujampa Kristo Maisha yako, au haujaitengeneza taa yako vizuri fahamu kuwa Unyakuo upo mlangoni sana, Siku moja inapopita ujue kuwa ndivyo unavyoikaribie ile siku, pengine ni leo usiku, pengine ni kesho tu, pengine mwezi huu hauishi Kristo atakuwa amesharudi..Jiulize akirudi na kukuta katika hali hiyo uliopo, utajibu nini na injili zote unahubiriwa?

Kumbuka aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi.

Wayahudi macho yao yalifumbwa wasimwamini Kristo, lakini siku za mwisho watakwenda kumwamini Kristo atakaporudi kwao (upatapo muda kapitie vipengele hivi Warumi 11 na Zekaria 12)

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

USISUBIRI MPAKA MUNGU AKUAMBIE, NDIO UFANYE!

KUPATA MAONO YA MBINGUNI SIO KUFIKA MBINGUNI.

NEEMA YA MZALIWA WA PILI.

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Je! Ni dhambi kwa kijana aliyeokoka kuvaa suruali za kubana (model), kunyoa mitindo (mfano kiduku), ?

Rudi Nyumbani:

Print this post

TUPO KATIKA ZAMU YA NNE YA MWISHO.

Umewahi kujiuliza Zamu ya nne ni nini? Kama tunavyoisoma katika Mathayo 14:25?

Tusome,

Mathayo 14:25 “Hata wakati wa ZAMU YA NNE ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.

26 Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu”.

Miji ya zamani ilivyojengwa ni tofauti na miji za nyakati hizi zetu…Miji ya zamani ilijengwa huku imezungukwa na ukuta pande zote…na Mara nyingi ukuta huo ulikuwa ni mrefu sana na mageti yake makubwa kiasi kwamba hata gari la farasi liliweza kupita juu ya ule ukuta bila shida yoyote, mfano utaona ule ukuta wa Yeriko, ndivyo ilivyokuwa na miji yote mikubwa ni lazima izungushiwe ukuta, hata Babeli Pamoja na Yerusalemu ilijengwa kwa mifumo hiyo, na lengo la kuizungushia kuta ndefu ni kujilinda dhidi ya maadui…Mji ambao ulikuwa hauna ukuta ulikuwa unajulikana kama mji dhaifu..Na mageti ya mji usiku yalikuwa ni lazima yafungwe.

Na hilo tu peke yake lilikuwa halitoshi, katikati pia ya zile kuta Pamoja na pembezoni walikuwa wanatengeneza minara mirefu (iliyojulikana kama minara ya walinzi)..Minara hiyo walikuwa wanawekwa walinzi, ambao watakesha kwa zamu usiku kutazama pande zote kwa usalama wa mji.

Sasa walinzi hao walikuwa wanalinda kwa zamu (yaani kwa kupokezana)..masaa matatu matatu kwa vipindi vinne…zamu ya kwanza walikuwa wanaanza kulinda kuanzia saa moja jioni mpaka saa tatu usiku…kisha wanapokea wengine kulinda zamu ya pili kuanzia hiyo saa tatu usiku hadi saa sita usiku…kisha wanaingia wengine kulinda zamu ya tatu inayoanza saa sita usiku mpaka saa 9 usiku na mwisho inaingia zamu nyingine ya mwisho ya walinzi wengine kumalizia zamu ya mwisho ya 4, inayoanza saa 9 hadi saa 12 asubuhi.

Kwahiyo ilikuwa ni desturi tukio likitokea usiku, muda ule lilolotukia ulitambulika kwa ZAMU na si kwa masaa kama sasa nyakati zetu hizi tunavyofanya..

Hali kadhalika na sisi wakristo ni walinzi katika roho..tunamngojea Bwana arudi katikati ya hili giza nene la maasi na maovu ya dunia, na hatujui atarudi muda gani…hajaja katika zamu ya akina Petro ambao walikuwa macho wanakesha, mpaka wanaondoka duniani, halikadhalika hakuja katika zamu ya watu wa kanisa la pili na la tatu na la nne…na sasa tupo kanisa la mwisho la saba (lijulikanalo kama Laodikia kulingana na Ufu. 3:14)…ambapo ndio tupo ile zamu ya mwisho YA NNE, ni lazima Bwana aje katika hichi kipindi, hatujui siku, tarehe wala mwaka…lakini majira tunayajua…tupo wakati wa kurudi kwa Bwana mara ya pili.

Luka 12:36 “nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.

37 Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia.

38 NA AKIJA ZAMU YA PILI, AU AKIJA ZAMU YA TATU, na kuwakuta hivi, heri watumwa hao.

39 Lakini fahamuni neno hili, Kwamba mwenye nyumba angalijua saa atakayokuja mwivi, angalikesha, wala asingaliacha nyumba yake kuvunjwa.

40 Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu”.

Tupo katika dakika za hatari sana, kama katika watu ambao wangepaswa wawe macho juu ya suala la Unyakuo wa kanisa basi ni sisi, lakini cha ajabu ni kuwa wengi wetu tunachukulia kimzaha mzaha tu, tunaishi kama tunavyotaka,tukidhani na mbinguni pia tutaingia tu kama tunavyotaka..Tupo buzy ni shughuli za ulimwengu huu, hatuna habari na Mungu..Bwana atusaidie katika hili ili sote tujue zamu tuliyopo, kuwa ndio ile zamu ya nne ya mwisho, na kwamba zamu hii haitapita kabla Kristo hajarudi…Wakati umeenda sana ndugu.

Je! umesimama imara na wokovu.

Bwana atupe macho ya kuliona hilo.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.

SI KWA FAIDA YA MWENYEZI, BALI KWA FAIDA YETU.

Kwanini wakristo wengi ni maskini?.

Ni kwa namna gani Yesu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka?

Ni uthibitisho upi unaoonyesha kuwa kuna MBINGUNI na KUZIMU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Katika biblia Neno “Mshenzi” linatajwa.Kwanini liwekwe?

SWALI: Katika Wakolosai 3:11 tunaona neno “Mshenzi” likitajwa.Kwanini Neno hili liwekwe pale?


JIBU: Tusome..

Wakolosai 3:11 “Hapo hapana Myunani wala Myahudi, kutahiriwa wala kutokutahiriwa, mgeni wala MSHENZI, mtumwa wala mwungwana, bali Kristo ni yote, na katika yote”.

Mshenzi kulingana na kamusi ni mtu asiyejali mambo ya Ki-Mungu, asiyekuwa na staha, au adabu ni rahisi kujiamulia tu mambo yake mwenyewe, hata kuua yeye hajali, na mara nyingi anakuwa ni mkatili na mnyama.

Sasa enzi hizo za kanisa la kwanza kulikuwa na kundi maalumu lililojulikana kama washenzi, jamii ya watu hao walikuwa wanaishi kando kando mwa bahari ya Nyeusi(Black sea) ambao kwasasa ni maeneo ya Urusi, Ni watu ambao walikuwa hawana elimu na walikuwa ni wafugaji wanaohama hama, pia walikuwa ni wakatili na wanyama sana, walikuwa mara nyingi wanafananishwa na wanyama wa mwituni kwa ukatili wao.

Hivyo watu wa namna hiyo, waliitwa washenzi.. Lakini cha ajabu ni kwamba na wao pia walihesabiwa kustahili neema ya Yesu Kristo.

Hata sasa zipo jamii nyingi za watu ulimwenguni wa namna hizi au zaidi hata huku Afrika, ambazo zinaweza kuonekana kama hazistahili kupokea neema ya injili kwa staili yao ya maisha, kwa kuwa nyuma kimaendeleo, watu wake kuwa ni wajinga, ma-bushmen, wanaotembea uchi, wanakula nyama za watu, hawana imani na kitu chochote kile n.k.(Ambao kwa namna nyingine wangeitwa washenzi ) Lakini kumbe hao nao Mungu anawatazama na neema yake ya wokovu inapaswa iwafikie kama wengine..

Hiyo ni kutufundisha kuwa hatupaswi kuchagua mtu bali ni sharti injili ihubiriwe kwa kila kiumbe.(Mungu hana ubaguzi kwa mtu yoyote yule, katika suala la wokovu hatatazami rangi, wala ukabila wala utaifa, wote ni watu wake wanaostahili wokovu sawa kupitia mwanawe mpendwa Yesu Kristo, ambaye ni Bwana wetu)

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 2

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

 

Je ni sahihi kumtenga mtu anapofanya dhambi kanisani?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya ‘Usimwekee mtu mikono kwa haraka’?

SWALI: Andiko hili lina maana gani?..1Timotheo 5: 22 “Usimwekee mtu mikono kwa haraka, wala usizishiriki dhambi za watu wengine. Ujilinde nafsi yako uwe safi”


JIBU: Maana ya awali ya mstari huo sio ile inayodhaniwa na wengi ya “Mtumishi wa Mungu, kumwekea mikono mtu mwenye tatizo fulani au ugonjwa fulani” na kumwombea…Hiyo sio maana ya msingi ya mstari huo…inaweza kuwa maana ya pili ya mstari huo …lakini maana ya msingi kabisa ya mstari huo ni “kuwekewa mikono kwa ajili ya utumishi”.

Huu ni waraka ambao Mtume Paulo alimwandikia Timotheo ambaye alikuwa ni mtumishi wa Mungu…Paulo alimfundisha madaraka ya kuitumishi kwa uongozo wa Roho Mtakatifu, ambayo unaweza kuyasoma yote katika wakara huo (yaani kuanzia sura ya kwanza hadi ya mwisho). Na mojawapo ya madaraka aliyompa ni madaraka ya kuwawekea mikono watumishi wapya, wale ambao tayari karama zao zimeshaanza kuonekana katika kanisa hivyo wapo tayari kuifanya kazi ya ki-utumishi katika mwili wa Kristo..kama jinsi yeye alivyowekewa..

1Timotheo 4:14 “Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa KUWEKEWA MIKONO YA WAZEE”

Kwahiyo hapa Timotheo naye anaagizwa wakati wa kuwawekea mikono watumishi wapya (mfano..maaskofu wapya, wachungaji wapya wa makanisa, waalimu, au manabii) asiwe na haraka!…bali achukue muda kumsoma mtu yule, tabia yake, mwenendo wake, je kama ni kweli kaitwa, ama ni kweli ana nia ya Kristo, kama ni kweli amekidhi vigezo vyote vya kimaandiko..Ndipo amtie mikono na kumbariki.

Kwasababu wale waliotiwa mikono ni kama wamehalalishwa kuwa wamestahili kulitumikia kundi la Mungu, na hivyo watu wengi ni rahisi kuwaamini, kwahivyo endapo akiwekewa mikono mtu ambaye si sahihi, ambaye hana nia ya Kristo, ni mtu wa kidunia tu, anawaza fedha au ukubwa tu…na kundi lote likimwamini, basi ni rahisi kuleta uharibifu mkubwa sana katika kanisa…Ndio maana hapo juu Mtume Paulo anamwagiza Timotheo na kumwambia “asiwe mwepesi kumwekea mtu mikono kwa haraka”, maana yake achukue muda kumchunguza..

Na hata sasa makanisani inapaswa iwe hivyo hivyo..Kabla ya mtu kuwekewa mikono kuwa mchungaji, au askofu, au shemasi, au nabii, au mwalimu ni lazima awe ameshajaribiwa na kuhakikiwa vya kutosha ili asije akaliharibu kundi, vigezo vya uaskofu vinapatikana katika hiyo hiyo 1Timotheo

1Timotheo 3:1 “Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.

2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;

3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;

4 mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu;

5 (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)

6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi

7 Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.”.

Hiyo ndio maana ya awali ya KUMWEKEA MTU MIKONO, iliyomaanishwa katika mstari huo…Maana ya pili ndio ile inayojulikana na wengi, ambayo ni ya kumfahamu mtu kwanza kabla ya kumwekea mikono kumwombea..

Wengi hususani watumishi mtu anapokuja ana tatizo fulani, au ugonjwa fulani ni wepesi kumwekea tu mikono pasipo kumjua mtu huyo kwa undani..ili tu mtu aonekane ni mtumishi wa Mungu…pasipo kujua ni hatari kufanya hivyo…Kwasababu unaweza kujikuta unalaani kilichobarikiwa au una bariki kilicholaaniwa.

Kwamfano mtu unaweza kukuta anafanya kazi ya madawa ya kulevya, au ujambazi, au ya ukahaba au uzaji pombe..na yeye anakuja kwako kuomba kazi zake ziende vizuri (mtu kama huyo alishawahi kunifuata mimi)..na wewe pasipo kufikiri, kwasababu kaja tu kutafuta msaada kutoka kwako, unamwekea mikono na kumbariki katika jina la Bwana…(hapo umebariki kilicholaaniwa.).

Badala yake ungepaswa umhoji kwanza shughuli anayoifanya, na kama akikiri ni ya madawa ya kulevya basi, unamhubiria kwanza atubu na kumpa Kristo Maisha yake, na kutafuta kazi nyingine ndipo umeombee baraka kwa Mungu wako na ndipo huyo mtu abarikiwe..

Wengine ni makahaba na hawajui kama katika ukahaba wao wanamkosea Mungu (nimewahi kukutana na kahaba ambaye katika ukahaba wake aliniambia anamwamini Mungu, na huwa Mungu anamleteaga wateja, na huwa anaiombeaga biashara yake mara kwa mara ili iende vizuri)..baada ya kumhubiria sana ndipo alipoelewa kwamba alikuwa anafanya makosa pasipo kujijua…Sasa mwanamke kama huyu, anapokwenda kanisani au kwa mtumishi ambapo hataulizwa maisha yake ni rahisi watu kuibariki kazi iliyo laaniwa na Mungu..Hivyo ni kuwa makini sana.

Na pia tumeonywa hapo! Tusizishiriki dhambi za watu wengine, unapomwekea mtu mikono kwa pupa ni rahisi kuzishiriki dhambi za yule mtu, kadhalika unaposhirikiana na watu waovu katika kanisa ambao wanajua kabisa mambo wanayoyafanya ni kinyume na maandiko lakini bado wanaendelea kuyafanya huko ni sawa na kuzishiriki dhambi zao..

Bwana atusaidie tuwe wakamilifu mbele zake daima.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

HAKI HAIMWACHI KUISHI.

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

JIEPUSHE NA MASHINDANO YA DINI.

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

YA KALE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA

Rudi Nyumbani:

Print this post

PALE UNAPOKUWA NA SABABU ZA KUMLAUMU MTU, UFANYE NINI?

Ni mara chache sana inatokea mtu anakosana na mwingine bila sababu yoyote, (Hiyo mara nyingi huwa inatokea kutokana na wivu), Lakini kutokuelewana kwingi au kuchukiana na watu, au kutokusameheana, au kukosana na watu mara nyingi huwa kunatokana na sababu Fulani..Kwamfano utakuta mtu amemdhulumu mwenzake, tukio hilo linamfanya yule aliyedhulumiwa amchukie yule mdhulumuji, au mtu amemuua ndugu yake, hilo linamfanya ndugu ya mfiwa amchukie yule muuaji..Au pengine amemtukana, au amemdhalilisha kwa namna moja au nyingine, au amemsengenya, au amempiga n.k…Hizo zote ni “sababu” zinazoweza kumfanya mtu asimpende yule mwingine..

Zinaweza zikawa ni sababu za msingi kabisa ambazo hata ukifa mbele za Mungu, unaoujasiri wa kumwambia Mungu ni kwanini ninamlaumu mtu yule, ni kwasababu alikuwa ni muuaji, ni fisadi, ni mchawi n.k.

Lakini Je biblia inatufundisha nini tunapojikuta katika mazingira kama hayo?

Inasema..

Wakolosai 3:12 “Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu,

13 mkichukuliana, na kusameheana, MTU AKIWA NA SABABU YA KUMLAUMU MWENZAKE; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.

14 Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.

15 Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani”.

Soma tena huo mstari wa 13 Unasema.. “Mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake”.. unaweza ukawa na sababu zote za msingi za kumlaumu mzazi wako kwanini hakukupeleka shule wakati ulikuwa na uwezo, unazo sababu za msingi za kuwalaumu viongozi wako, au waalimu wako kwanini hawakuwajibika kutimiza wajibu wao.. Lakini biblia inasema…Kama Bwana alivyotusamehe sisi, vivyo hivyo na sisi tuwasamehe wao.

Mtu mwingine anaweza kusema mtu Fulani nilimsaidia hiki na kile, lakini baadaye alipokuwa hana shida, alianza kunizungumzia maneno mabaya kwa watu wengine akiniita mimi mchawi.. Hivyo maisha yangu kamwe sitakaa nimpende yule mtu, Ni kweli unazosababu zote za kufanya hivyo, kwa hali ya kibinadamu sababu zote zipo za kumwekea kinyongo..Lakini Mungu anatuambia Pamoja na sababu zetu, tunapaswa tuwasamehe kama vile Bwana alivyotusamehe sisi.

Tukijua kuwa Mungu naye anazosababu za kutosha za kutuhukumu na sisi, kwa mambo yote maovu tunayomtendea kila siku, lakini anatusamehe tu bure, Matusi tuliyokuwa tunatukana yalimtosha kutuhukumu na kututupa kuzimu, dhambi tulizozifanya zinatosha kumpa Mungu sababu za kutushusha Jehanum.

Na ndio maana anatuambia tena mahali pengine..

Luka 6:37 “…. msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa”.

Unaona? Zipo faida nyingi za kusamehe(kuachilia), na faida mojawapo ambayo ni kubwa, ni kwamba utasikia mzigo mzito umedondoka moyoni mwako, na utaona amani ya ajabu imemwagika ndani yako.Lakini ukibakia na vinyongo, ujue kuwa Mungu naye atakuwekea kinyongo.

Hatuna budi kujifunza hili kila wakati, kwasababu maisha ya humu ulimwenguni yamejaa makwazo ya kila namna, kama hutakutana nalo leo, basi utakutana nalo kesho.. Hivyo na sisi tukiruhu makwazo yatawale mioyo yetu, kwa kutokuwasamehe wale ambao wanatuudhi, au kutukera kwa makusudi, tujue kuwa tuna dalili kubwa ya kutoiona mbingu.

Hivyo tujifunze kusamehe, na kuachilia hata kama tunazo sababu zote za kufanya hivyo.

Mwisho kabisa soma kisa hiki na Bwana akubariki.

Mathayo 18:23 “Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.

24 Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.

25 Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.

26 Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

27 Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.

28 Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho.

29 Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

30 Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.

31 Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka.

32 Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi;

33 nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe?

34 Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.

35 Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake”.

Bwana akabariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

NGUVU YA MSAMAHA

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

 

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 4

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIPUNGUZE MAOMBI.

Katika Maisha usijaribu kufanya kosa la kupunguza maombi…Ni heri ukapunguza muda wa kufanya mambo mengine ambayo unaona ni ya muhimu lakini usipunguze kuomba hata kidogo!..Kama tayari ulishaanza kuwa muombaji, halafu ukaanza kupunguza unamtengenezea adui nafasi ya kufanya uharibifu mkubwa sana katika maisha yako.

Kuna siri moja Bwana aliwaambia wanafunzi wake kuhusu maombi.. alisema “KESHENI, MWOMBE, MSIJE MKAINGIA MAJARIBUNI; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu (Mathayo 26:41)”

Hilo Neno “msije mkaingia majaribuni” ni neno kubwa sana…Hivi unajua ni kwanini Bwana alisema “hata nywele zetu zote za kichwani zimehesabiwa (Mathayo 10:30 )?”….Ni kwasababu kuna kiumbe kingine ambacho kinatutafuta sana hata kwa vitu vidogo…na hicho si kingine zaidi ya ibilisi….wengi hawajui kuwa shetani hata baada ya kufa maiti yako bado ina thamani kwake..sasa si zaidi nywele zako?, si Zaidi mate yako?, si Zaidi vidole vyako, si Zaidi mikono yako?..naam vyote hivyo anavihitaji sana…Ndio maana biblia inasema hapo, hata nywele zetu zote zimehesabiwa (maana yake zinalindwa zisipotee hata moja wala zisitumike na adui).

Shetani akikukosa kukuua na ajali siku hiyo, atatafuta hata ujikate na kisu tu wakati unaosha vyombo, akikosa kukutoboa jicho siku hiyo atatafuta hata uchubuke tu!..akikukosa kukupatia ugonjwa fulani wa mauti kama HIV, atafanya juu chini siku hiyo angalau upate tu mafua yatakayokusumbua, na akikukosa kwenye mafua pia hataridhika atatafuta njia hata uchomwe na mwiba barabarani! Ili uumie tu!,…hivyo vile vitu vidogo unavyovidharau ambavyo unahisi shetani hawezi kujishuhulisha navyo, yeye kwake bado anavyo nafasi navyo.

Lakini mtu ukiwa mwombaji kila siku…kabla ya kulala au wakati wa asubuhi, au mchana upatapo nafasi nzuri ya utulivu…unampa shetani wakati mgumu wa kupata  nafasi katika Maisha yako. Lakini usipokuwa mwombaji matukio ya ajabu ajabu yatajifululiza katika Maisha yako ambayo hutajua hata chanzo chake ni nini?…kama ni mfanyakazi unaweza kujikuta unagombana kazini tu au unagombezwa!, au unafika huko jambo lile ambalo ulikuwa umelipanga liende vizuri halijaenda vizuri, umeamka mzima jioni unarudi ni mgonjwa wa kupindukia..na mambo kama hayo (hayo ni majaribu ya kimaisha)…sasa majaribu ya kiimani ndio hayo unajikuta umeingia katika mazingira ya kuikana Imani au kuisaliti…

Unakumbuka dakika chache baada ya Bwana Yesu kumwambia Petro na wenzake waamke wasali ili wasije wakaingia majaribuni, walipopuuzia ni nini kilifuata?…masaa kama matatu baadaye kabla hata jogoo hajawika na hata kabla ya usingizi wao kuisha waliamshwa na kikosi cha watu wenye marungu na mapanga…na moja kwa moja baadhi ya wanafunzi wakakimbia mpaka mwingine alikimbia uchi wakamwacha Bwana peke yake (hiyo tayari ni kuikana imani)..Na sio hilo tu!…Petro naye kwa kujifanya shujaa kwamba anaweza kushinda majaribu bila nguvu ya maombi, alipomfuata Bwana kule alipopelekwa yeye naye akaikana Imani, (alimkana Bwana mara tatu kwamba hamjui).

Na sisi ni hivyo hivyo, usipokuwa mwombaji…asubuhi utaamka na ujumbe wa watu wanaokutaka uwape rushwa ili jambo lako Fulani lifanikiwe….Lakini kama ukiwa mwombaji, mambo hayo Mungu anakuepusha nayo!..utaona yule ambaye angepaswa akuombe rushwa, unashangaa hata hakuombi na bado anakupa haki yako ile ile…

Ukiona umepunguza kuomba jua tayari umeanza kurudi nyuma kiimani…hiyo ni dalili ya kwanza, dalili ya pili ni kupunguza kusoma neno.

Maombi yanafananishwa na lile tukio la Nabii Musa, aliponyoosha mikono yake juu wakati wa vita…alipoionyoosha juu wana wa Israeli kule vitani walikuwa wanapata nguvu ya kuwapiga maadui zao na kuwashinda…lakini alipoishusha nguvu ziliwaondokea wana wa Israeli na kuhamia kwa adui zao na kuwashinda wana wa Israeli..Na sisi ni hivyo hivyo nguvu za Mungu zinashinda juu ya Maisha yetu dhidi ya nguvu za Adui endapo tu na sisi kila siku/kila wakati tutakuwa tumeinyanyua mikono na mioyo yetu juu kuomba…Hizo ni faida chache tu za maombi zipo nyingi hatuwezi kuwa na muda wa kuzichambua zote hapa.

Hivyo usiache kuomba kabisa!..na kumbuka ndugu kuomba sio sala ile ya kuombea chakula!..au sio ile sala la “Baba yetu”…Hiyo haitoshi…kiwango cha chini kabisa biblia imetuambia angalau lisaa limoja kwa siku, ukienda masaa 3 au 4 ni vizuri Zaidi…na pia maombi sio kwenda kuombewa na mtumishi Fulani wa Mungu au ndugu yako!!..Maombi ni wewe kama wewe kusimama mwenyewe kuomba kwa bidii!.

Kumbuka tena, shetani anashida na nywele zako, ana shida na Maisha yako na anashida na viungo vyote katika mwili wako, na sio hata kwa njia ya uchawi au kwa kuwatumia wachawi…anayo idadi kubwa ya mapepo kuliko wachawi..hivyo kazi zake nyingi anatumia mapepo yake kuzifanya hata zaidi  ya wachawi….asilimia kubwa sana ya watu wanasumbuliwa na mapepo wakidhani ni wachawi!

Hivyo ng’oa nanga leo anza safari ya maombi ya kina kila siku!..kama umerudi nyuma rudia desturi yako kabla mambo hayajazidi kuwa mabaya.

Kama hujampa Bwana Maisha yako!..hizi ni siku za mwisho, Kristo anakaribia kurudi…hivyo geuka leo mkabidhi Maisha yako naye atakusamehe.

Bwana akubariki na Bwana atubariki sote.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP



Mada Nyinginezo:

HISTORIA YA ISRAELI.

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

SHETANI ANAITHAMINI HATA MAITI YAKO.

UCHAWI WA BALAAMU.

WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UHARIBIFU HAUNA KIFUNIKO.

Ayubu 26:6 “Kaburi li wazi mbele yake, Uharibifu nao hauna kifuniko”.

Kama tunavyojua mashimo mengi yanayochimbwa huwa yanawekwa mifuniko juu, ili kusudi kwamba ikitokea mtu mgeni akapita kwa njia ile iwe ni mchana au usiku kwa bahati mbaya asitumbukie,

Lakini biblia inatumbia kaburi la mauti lipo wazi sikuzote, na uharibifu hauna kifuniko..

Uharibifu kwa jina lingine ni kuzimu.. Akimaanisha kuwa kuzimu haina mfuniko wowote, mfano ikitokea umepita katika njia hiyo kwa namna yoyote, basi kutelezea humo na kuzama ni mara moja..haijui huyu ni mgeni, au ni mwenyeji au ni mtoto. Ukizama umezama!.

Na ndio maana leo hii mtu akifa katika dhambi, moja kwa moja atajikuta ghafla tu yupo kuzimu, (Ayubu 21:13). atajiuliza amefikaje fikaje huko. Lakini ndio hivyo tayari ameshafika huko mahali ambapo hatatoka tena milele,.atakachokuwa anasema huko ni Laiti ningejua, laiti ningefahamu, nisingefanya hiki au kile..

Biblia inatuambia..

Isaya 5:14 “Kwa hiyo kuzimu kumeongeza tamaa yake, kumefunua kinywa chake bila kiasi; na utukufu wao, na wingi wao, na ghasia yao, naye pia afurahiye miongoni mwao, hushuka na kuingia humo”.

Unaona? Unashuka kwa ghafla sana, tusitamani tufike huko. Kila inapoitwa leo, tumwombe Mungu vilevile tujitahidi kukaa mbali na dhambi kwa kadiri tuwezavyo.

Watu wote wanaochukuliwa katika maono na kupelekwa kule, na kuonyeshwa sehemu tu ya mambo yanayoendelea humo, huwa hawatamani kuhadithia, kwasababu wote wanaowaona humo, ni vilio vya majuto tu, wanatamani wapewe dakika hata moja warudi watengeneze mambo yao lakini haiwezekani tena..

Ayubu 7:9 “Kama vile wingu likomavyo na kutoweka, NI VIVYO HUYO ASHUKAYE KUZIMUNI HATAZUKA TENA KABISA.

10 Hatarudi tena nyumbani kwake, Wala mahali pake hapatamjua tena”.

Utatamani urudi duniani siku hiyo itashindikana…Mfano tu wa Lazaro na yule Tajiri…Yule tajiri aliomba akawahubiriwe ndugu zake ili wasifike mahali pale alipo pa mateso lakini ilishindikana..Na Watu wanaoshuka huko ni wengi sana wasiohesabikia. Hivyo mimi na wewe tulio hai, tuikwepe dhambi…

Tusipende kufuata mikumbo ya watu, kisa wanakwenda Disko na sisi tuende, kisa wanavaa nguo za kikahaba na sisi tuvae, kisa wanafanya uasherati na sisi tufanye..kisa wanatumia pombe na sisi tutumie ..Kamwe usiwaige hao..Kwasababu wanaoshuka huko ni wengi sana, na kuzimu haijai watu..(Mithali 27:20, Mithali 30:16)

Kumbuka hizi ni zile siku zilizotabiriwa za maasi kuongezeka. Kwahiyo usishangae kuona wimbi kubwa la watu wanaofanya dhambi hadharani bila hofu.

Zaidi macho yetu yaelekee mbinguni, kwani unyakuo upo karibu, Au hata kama hautakukuta wakati wako, basi tufahamu kuwa kifo nacho hakipo mbali, Hivyo ni wajibu wetu kujiimarisha na kujithibitisha kwamba tupo katika mstari wa Imani.

Luka 12:35 “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;

36 nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

IELEWE SAUTI YA MUNGU.

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 2

MADHARA YA KUTOA MIMBA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?

2Timotheo 3:6 Inazungumzia watu wanaowachukua wanawake wajinga mateka, Je! Mstari huu una maana gani?


JIBU: Ukianzia kusoma tokea mstari wa kwanza utaona pale Paulo anamwonya Timotheo juu ya baadhi ya tabia za ajabu ambazo zitaanza kujitokeza katika siku za mwisho, alimwambia..

2Timotheo 3:1 “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari…”

Ukiendelea kusoma utaona akizihorodhesha tabia zenyewe zitakazozuka..anasema watatokea watu wanaopenda fedha, watu wenye kiburi,wasio safi, wanaopenda anasa kuliko kumpenda Mungu..n.k. Lakini ukushuka mpaka mstari wa tano anasema tabia nyingine kuwa, nyakati hizo kutaibuka pia wimbi la watu wenye mfano wa utauwa, lakini wakizikana nguvu zake, na hapa ndipo pa hatari zaidi..Tusome..

2Timotheo 3:5 “wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.

6 Kwa maana katika hao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu, na kuchukua mateka wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi, waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi;

7 wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli”.

Unaona hapo?

Na wanawake pia wanahusishwa na watu hawa wanatajwa kuwa wao ndio waathirika wakubwa wa wimbi hilo la hao watu wanaojifanya kuwa ni watu wa Mungu(wenye mfano wa utauwa) lakini nyuma yake hawana Habari na Mungu hata kidogo (ni vyombo vya ibilisi dhahiri).

Hapa ndipo wewe kama mwanamke unapaswa ujichunge sana, tupo katika nyakati za hatari, kwasababu shetani tangu Edeni alikuwa anaufahamu mlango mwepesi wa kuuingilia ni mwanamke na si mwanaume (1Timotheo 2:14).. Leo hii utaona watu wa aina hii, hifadhi yao imekuwa wanawake wengi.., tena biblia inatumia neno

“Wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi na waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi ”.

Ikiwa na maana kuwa wanawake hawa suala la wokovu kwao halina maana sana,(ni wajinga katika roho) wanachotafuta ni mambo ya mwilini tu, wabarikiwe kazi zao, wapewe waume, wapate fedha, wapigiwe maadui zao, na huku waendelee na mavazi yao ya nusu uchi barabarani, waendelee kuwasengenya majirani zao, waendelee kuzini, waendelee kuishi kidunia..

Hawataki kujishughulisha na mambo ya rohoni,(hawaupendi utakatifu hata kidogo!) wakiona tu nabii yule ni mtanashati, anachekesha, ana magari, ana majumba, ana wafuasi wengi bila kujiuliza mara mbili kwasababu tu kashajiita ni mtu wa Mungu wanaingiwa na tamaa wanakwenda kujiunganisha naye.

Hayo yote, ni mambo yaliyotabiriwa kuwa yatatokea katika siku za mwisho, na tunayaona sasa.. Na kibaya Zaidi wanawakaribisha kwenye majumba yao, wewe angalia utaliona hilo, ni mara chache sana utawaona kwenye nyumba zenye mchanganyiko wa wanaume, muda wote utawaona wanazunguka kwenye nyumba za wanawake tu, na wakigundua mwanamke huyo kaolewa hawataenda kwake au kama wakienda wataenda wakati mumewe hayupo!…(Na wanawachukua mateka kimwili na kiroho)

hiyo yote ni ili maandiko yatimie, kwamba siku za mwisho watatokea watu wa namna hiyo.

Na ndio maana mtume Yohana alipomwandika wakara yule MAMA Mteule, mtakatifu kuwa alimwonya asiwakaribishe watu kama hawa ambao wanakuja kwake lakini hawaleti mafundisho ya Kristo..

2Yohana 1:10 “Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo [ya Kristo/utakatifu], msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu.

11 Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu”.

Hivyo wewe kama mwanamke, iga mfano wa huyo “Mama mteule” Ipende kweli. Na sisi wote kwa Pamoja vivyo hivyo tu tutafute utakatifu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KWANINI UNAPASWA UJIWEKE TAYARI SASA, KABLA YA ULE WAKATI KUFIKA?.

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

YONA: Mlango wa 4

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU NA ZA LUTU.

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?

Dalili ya kwanza ya uchanga mkubwa wa kiroho ni hofu ya wachawi…Ukijiona unaogopa wachawi, au “uchawi” huo ni uthibitisho wa kwanza kabisa kwamba wewe ni mchanga kiroho, na Neno la Mungu bado halijakaa ndani yako, haijalishi upo madhabahuni unahubiri kwa miaka mingapi! Bado ni mchanga.. Mtu anayeogopa wachawi au anayewatukuza mno wachawi hana tofauti ni kima anayeogopa kinyago cha mtu shambani, kinachomtishia asile mazao…

Uchawi ni sehemu ndogo sana ya vita vya mkristo!..Idara kubwa ya shetani sio “vitunguli na vibuyu”..Hiyo ni idara ndogo sana ya shetani, ambayo hata pasipo kujijua Mungu tayari anakulinda nayo pasipo hata wewe kujijua. Sasa kama wewe ni msomaji wa biblia hebu nionyeshe mahali popote ambapo Bwana Yesu alizungumzia habari za wachawi/uchawi..au mahali popote alipokuwa anawafundisha wanafunzi wake aliwaonya wajihadhari na wachawi???…

Idara kubwa na kuu ya shetani ni roho ya mpinga-Kristo ambayo hiyo inakwenda kinyume na Kristo…Na hiyo inatenda kazi ndani ya kanisa, na inatumia watumishi wa uongo wanaojigeuza na kuwa kama watumishi wa Mungu! Na inakaribiana sana na roho ya kweli. Ndio hiyo hata Bwana alikuwa anapambana nayo,(ndio ile iliyokuwa inafanya kazi ndani ya mafarisayo na masadukayo) na ndio Bwana aliwaonya sana mitume wajihadhari na hao…

Mathayo 7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali”.

Idara hiyo iliwasumbua sana mitume walipokuwa wanahubiri injili, mpaka wengine kuuawa, ilihusika kuwaua wakristo Zaidi ya milioni 80 duniani kote kikatili tangu kipindi cha kanisa la kwanza, inaua rohoni inaua pia mwilini, ndio hiyo hiyo inazungumziwa sehemu kubwa kwenye kitabu cha Ufunuo. Na ndio hiyo itakayokuja kufanya kazi katika kipindi cha dhiki kuu.

Sasa tukirudi kwenye mada..je! Mnyama paka kulia usiku juu ya bati ni uchawi?..

Jibu ni La!..sio uchawi…ukisikia paka analia usiku nje sio uchawi!!!….Paka wanaolia usiku ni kutokana na sababu za mazaliano..(sauti zile wanazitoa ili kuvutia mazaliano)..Paka wa aina yeyote Yule wakati wa mazaliano ni lazima atoe hizo sauti, awe ni paka wa kahaba, awe wa kanisa, au wa mtumishi wa Mungu…ni lazima ikifika kipindi cha mazaliano atoe hizo sauti, na anaweza kutoa wakati wa mchana au wakati wa usiku…na sauti hizo ni lazima zifanane na sauti za watoto wachanga!!…kama hatatoa sauti zinazofanana na za watoto wachanga basi kuna kasoro katika huyo paka!..paka asiye na kasoro yoyote ni lazima atoe hiyo sauti.

Sasa kwanini wanatoa hizo sauti zinazofanana na watoto wachanga???…Ndivyo Mungu alivyowaumba!..kama tu sauti wanazotoa kanga, au mbuzi au kuku wanapofikia wakati wa mazaliano au wakati wa kutaga!!. Na paka macho yake usiku ni lazima yang’ae yanapopigwa na mwanga…Na paka wana tabia zinazofanana na chui..ni wepesi kupenya mahali hata kama ni padogo sana..na wanapotembea si rahisi kusikika, na ni wepesi wa kutoroka mahali kwa haraka, kufumba na kufumbua unaweza usiwaone mahali walipopotelea…ndivyo walivyoumbwa!..(ili sisi tumtukuze Mungu, kwa uumbaji wake), na paka wote tabia zao ni kama za chui kupenda kutembea usiku na sehemu zilizoinuka!..

Kwahiyo ni kawaida kutembea juu ya mabati na ukuta wakati wa usiku, na hata kukimbizana!..na wanatabia pia za kuingia ndani kwa mtu hata kama hawajakaribishwa, hivyo kama hujafunga mlango anaweza kuingia mpaka ndani na hata kuzalia huko…na wanatabia ya kuwa ving’ang’anizi (utamfukuza atarudi tena, na utarudia hivyo mara kwa mara), ndivyo walivyoumbwa!!

Na sio dhambi kufuga paka! wa rangi yeyote Yule (awe mweusi, mweupe, kahawia au yeyote yule), kama ndani una panya wengi!..wanafaa kwa shughuli hizo za kuwadhibiti…au kwa fahari/(kwa kupenda tu) sio dhambi kuwafuga…tena ni vizuri zaidi kama una mapenzi nao!

Na bundi na popo ni hivyo hivyo…wameumbwa kipekee na Mungu (hawatembei mchana bali usiku na vyakula vyao vinapatikana huko huko gizani). Hawa si wanyama wa kufuga ndio maana unawaona wapo kivyao vyao..

Sasa wengi wasiokuwa na maarifa wanakuwa na hofu wanapowaona wanyama hawa wanaonyesha tabia zao hizo za kipekee walizopewa na Mungu, ambazo hazionekani kwa wanyama wengine!…na kuishia kusema ni wachawi wamewatembelea…wanaposikia paka usiku wanalia batini kama watoto wachanga, wanakosa usingizi na kuamini wachawi wamewatembelea!..wanapoona popo wametoka mitini jioni na kutanda angani, wanakosa amani..wanapoona bundi kasimama anamacho kama ya mtu, nguvu zinawaishia kabisa!!…wanajua sasa ni wachawi wanafanya kazi zao!!….kumbe ni kukosa tu maarifa!. Mwisho wa siku wanaishia kuwaua hao viumbe wakidhani ndio wamemshinda shetani!..

Na hiyo inamfanya mkristo kupoteza muda mwingi, hata wiki nzima,au mwezi mzima, au miaka na miaka kupambana katika sala dhidi ya wanyama hao(akiamini kuna uchawi ndani yao)…paka kaonekana kaingia ndani hapo hapo, maombi ya kufunga mwezi mzima yanaanza!..maji ya upako yatakwenda kutafutwa mitaa yote!, kila mtumishi ataitwa!..mwisho wa siku ni hofu hofu kila mahali…kila mtu unayekutana naye unahisi ni mchawi!, nimewahi kusikia watu wanasema na kuamini mende na mijusi, wanatumika kiuchawi!..hivyo ukiona mende ndani kwako ni wachawi kuna nguvu za giza hapo!

Usikose maarifa ndugu, wala usipoteze muda wako kwa vitu visivyokuwa na maana…Ukisikia paka wanalia batini usiku, kama wanakukera toka nje wafukuze! Wataondoka, na muda huo ombea mambo mengine ya muhimu kama, familia yako, kanisa na huduma yako kama unayo, ombea na wengine..usianze kushindana kukemea wanyama hao ambao wapo katika ulimwengu wao..Ukiona kelele za kuku usizozielewa hebu nenda kaulize kwanza uzijue tabia za viumbe hao kabla ya kuchukua maamuzi yasiyokuwa na maarifa!, kama sauti za fisi a zinakukera usiku basi hama nenda maeneo ya mjini hutazisikia kamwe..

Ni hofu tu ambazo shetani anawajengea watu waaamini kwamba yeye ni mkuu kuliko Mungu…ili wamwogope yeye zaidi ya Mungu. Wewe kama ni mkristo, unapaswa uwe na ujasiri na Imani yako useme “wachawi hawana kitu kwangu” Kama vile Bwana alivyosema “shetani hana kitu kwangu”..Kisha endelea kuishi Maisha yako ya kawaida.

Bwana akubariki!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

 Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako,katika kufanya maombezi?

MASHAHIDI 40 WALIOUAWA MJINI SEBASTE, NI UJUMBE KWETU.

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

JE! TUNAPASWA KUUAMINI UNABII WA SYLVIA BROWNE?

Rudi Nyumbani:

Print this post