Category Archive Home

Silaha za Nuru ni zipi? (Warumi 13:12)

SWALI: Silaha za Nuru ni zipi?

Warumi 13:12 Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru


JIBU: Ni lazima tufahamu ulimwengu wa roho upo katika pande mbili,

  1. Upande wa nuru
  2. na upande wa giza..

Upande wa Nuru ni wa Kristo (Yohana 1:4-5), na upande wa giza ni wa ibilisi.

Na pande hizi hazijawahi kupatana hata kidogo, na kama hazijawahi kupatana maana yake zipo vitani na kama zipo vitani basi zote zina silaha zake, kuhakikisha zinajilinda, lakini pia kushambulia, ili kuua utawala mwingine. Ndio hapo kwanini tunaambiwa tuzivae silaha za nuru. Maana yake mtu anaweza akawa ni wa nuru lakini akawa hana/hajui kuzitumia silaha za Nuru.

Vifungu vifuatavyo ni kututhibitishia kuwa Nuru na giza vipo katika mapambano;

2Wakorintho 6:14 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?

 

Wakolosai 1:12 mkimshukuru Baba, aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu katika nuru.
13 Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake

 

Sasa silaha za Nuru ambazo mtu akiwa nazo ataweza kujilinda na mashambulizi ya giza, lakini pia ataweza kuushinda ufalme wa giza ni hizi;

  1. Neno la Mungu.
  2. Haki (Ya Mungu katika Kristo Yesu)
  3. Kweli (Usahihi wa kimaandiko)
  4. Utakatifu
  5. Imani
  6. Injili
  7. Maombi

Silaha hizi, ndio zile zinazotajwa pia kwenye Waefeso 6:10-18, kama silaha za haki.

  • Kweli Kiunoni
  • Dirii ya Haki kifuani
  • Ngao ya Imani
  • Upanga wa Roho
  • Utayari wa injili ya Amani
  • Sala na Maombi
  • Chapeo ya wokovu

Kwa maelezo marefu juu ya silaha hizi, fungua hapa usome >>>  Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?

Mtu akiwa na mambo haya, ataweza kulishinda Giza, kotekote.. Ambalo, silaha zake ni kama zifuatazo;

  1. Uongo: Ambao huzaa Mafundisho ya uongo,
  2. Uasherati: Uzinzi, tamaa ya macho,
  3. Majivuno :  Ambayo hupelekea uasi,
  4. Chuki : Huzaa Kutokusamehe, unafki, migawanyo
  5. Hofu : mashaka, kupoteza imani na Mungu
  6. Uchawi na uganga: Huzaa ibada za sanamu, miungu, na uvamizi wa mapepo

Swali ni Je! Umejivika silaha Nuru ?

Ikiwa upo nje ya Kristo, huwezi kusimama, unahitaji wokovu kwanza, ikiwa upo tayari kufanya hivyo wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi

Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, tunashindanaje vita vya kiroho?

NGUVU YA “KUKATAA” UNAPOPAMBANA VITA VYA KIROHO

Print this post

HEKIMA ILIYO SAHIHI, KATIKA HIMIZO LA UTOAJI SADAKA.

Mfalme mmoja wa Israeli aliyeitwa Yoashiliingiwa na wazo la kutaka kuikarabati nyumba ya Mungu (Hekalu), na kuamsha tena shughuli za kiibada zilizokuwa zimeharibiwa Na watawala wabovu waliotangulia..

Hivyo kwa kuwa alijua ukarabati unahitaji fedha, alichukua hatua ya kuwatoza watu kodi ya nyumba ya Mungu..Ambayo iliagizwa katika torati na Musa..(2Nyakati 24:9)

Hivyo akawateuwa  Walawi, walisimamie jambo hilo tangu mwanzo hadi mwisho, lakini likawa kama linacheleweshwa…

Mpaka baadaye akawauliza tena, kwanini kazi inacheleweshwa, kwa kuona hakuna chochote kilichofanyika..

Lakini mfalme akaja na mkakati mwingine, ili shughuli hiyo ifanyike kwa haraka na wakati, akaona kuliko Kuwalazimisha watu kulipa kodi ngoja aweke sanduku kubwa katika lango la hekalu na kupiga panda kwa watu wote wa Yuda waje kumtolea Mungu wao kwa hiari, bila shuruti..

Na wazo lile likapendwa na watu wengi, na hatma yake makusanyo yakawa mengi, kila siku mpaka wakapata fedha za kuwaajiri wajenzi ili kulikarabati hekalu, na kutengeneza vyombo vya nyumba ya Mungu.

2 Mambo ya Nyakati 24:6-14

[6]Mfalme akamwita Yehoyada mkuu wao, akamwambia, Mbona hukuwataka Walawi waitoze Yuda na Yerusalemu kodi ya Musa mtumishi wa BWANA, na ya kusanyiko la Israeli, kwa ajili ya hema ya ushuhuda?

[7]Kwa kuwa wana wa Athalia, yule mwanamke mwovu, walikuwa wameibomoa nyumba ya Mungu; na vitakatifu vyote vya nyumba ya BWANA wamewapatia mabaali.

[8]Basi mfalme akaamuru, nao wakafanyiza kasha, wakaliweka nje langoni pa nyumba ya BWANA.

[9]Wakapiga mbiu katika Yuda na Yerusalemu, kumletea BWANA kodi aliyoiweka Musa mtumishi wa Mungu, juu ya Israeli jangwani.

[10]Wakafurahi maakida wote na watu wote, wakaleta na kutia ndani ya kasha, hata wakaisha.

[11]Ikawa wakati walipoletewa kasha wasimamizi wa mfalme kwa mkono wa Walawi, nao wakaona ya kwamba kuna fedha nyingi, huja karani wa mfalme, na msimamizi wake kuhani mkuu, wakatoa yaliyomo kashani, kisha hulichukua kasha, na kulirudisha mahali pake. Ndivyo walivyofanya siku kwa siku, wakakusanya fedha tele.

[12]Na mfalme na Yehoyada waliwapa hao waliofanya kazi ya utumishi wa nyumba ya BWANA; nao wakawaajiri waashi na maseremala ili kuitengeza nyumba ya BWANA, na hao pia wafuao chuma na shaba ili kuitengeza nyumba ya BWANA.

[13]Hivyo mafundi wakafanya kazi yao, nao wakaimaliza, wakaisimamisha nyumba ya Mungu kama ilivyopasa, wakaifanya imara.

[14]Nao walipokwisha, wakaleta mbele ya mfalme na Yehoyada fedha iliyobaki, vikafanyizwa kwayo vyombo vya nyumba ya BWANA, vyombo vya utumishi, navyo vya kutolea, na miiko, na vyombo vya dhahabu na fedha. Wakatoa sadaka za kuteketezwa katika nyumba ya BWANA, daima, siku zote za Yehoyada.

Ni nini tunafundishwa Na Roho Mtakatifu..

Utoaji wenye baraka na anaouhitaji Mungu ni ule wa hiyari na sio wa kulazimishwa…kama kanisa la Kristo Lazima tufikie hatua hii, kwamba viongozi hawawashurutishi watu kutoa mchango,mfano Zaka, Kama vile himizo la kodi, kwamba usipotoa unachukuliwa sheria ya kinidhamu …lakini pia watu nao wanawajibika wenyewe kumtolea Mungu kwa uaminifu na moyo..kanisa lifikiapo hatua hii ya kiroho, Mungu huliongezea baraka sana.

Usikubali kukumbushwa-kumbushwa, au kuhimizwa-himizwa kumtolea Mungu, Bali mtolee Mungu zaka zako, sadaka zako, kwa moyo wa furaha, Bwana atakubariki.

2 Wakorintho 9:6-8

[6]Lakini nasema neno hili, Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu.

[7]Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.

[8]Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;

Bwana awabariki..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Nini maana ya kumwabudu Bwana katika uzuri wa utakatifu?

SWALI: Katika sehemu nyingi kwenye maandiko tunaona, Mungu akiwaagiza watu wake Wamsifu au wamwabudu katika uzuri wa utakatifu, nini maana ya uzuri wa utakatifu?

1 Mambo ya Nyakati 16:29

[29]Mpeni BWANA utukufu wa jina lake;  Leteni sadaka, mje mbele zake; Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utakatifu; 

Zaburi 29:2

[2]Mpeni BWANA utukufu wa jina lake;  Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utautakatifu.

Soma pia..

Zaburi 96:9, 2Nyakati 20:21


JIBU: Kuna mambo mawili hapo.

Jambo la kwanza ni “Uzuri” na jambo la pili ni “utakatifu”

Hasemi tumwabudu Bwana katika utakatifu…hapana bali anasema tumwabudu Bwana katika uzuri wa utakatifu..

Kwa namna nyingine anamaanisha hivi; tuuone uzuri ulio katika utakatifu ndio tumwabudu yeye Katika huo.

 

Tunaweza tukaujua utakatifu…ambao mfano wake ni kama vile maisha ya upendo, haki, usafi, adabu, amani, utu wema. n.k. Lakini tusione uzuri wa mambo kama hayo mioyoni mwetu au maishani mwetu…wengine wanaona kama utakatifu wa Mungu ni kitu cha kutisha, lakini kumbe Sio..

 

Siku tukiona uzuri wake ndio hatutakuwa na unafki pale tunapoambiwa tufanye jambo lolote katika utakatifu.. 

 

Kwasababu tusipoona hilo, hatma yake huwa ni kutimiza ibada kama tu agizo fulani au utaratibu wa kidini au nidhamu fulani lakini sio katika furaha na faida tuipatayo katika huo utakatifu.

 

Kwamfano Ibada tu yenyewe ni tendo takatifu lakini je tunaifurahia ibada na kujiona tunanufaika sana mioyoni mwetu katika hizo au tunamtimizia Mungu tu haki yake ya kuabudiwa, lakini hakuna chochote kitufurahishacho ndani yake?

Ibada ifanywayo katika uzuri wa utakatifu ni lazima itaambatana na sifa hizi; 

 

Itakuwa Katika Roho na kweli (Yohana 4:24)

 

Itafanywa Katika Moyo mweupe( Zaburi 24:3-4). Mfano kusamehe, na amani moyoni.

Itajaa shukrani na kumfurahia Mungu: 

Zaburi 139:14

[14]Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa 

Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha.  Matendo yako ni ya ajabu, 

 

Itamwadhimisha Mungu na kumfurahia sana, kwa maajabu yake na matendo yake makuu, kwa viwango visivyo vya kawaida

Itaambatana na maisha ya utakatifu:

Warumi 12:1

[1]Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. 

Maisha yetu ni ibada tosha, mwonekano wako, uvaaji wako, usemi wako, tabia yako, vitaakisi utakatifu wa Kristo.

Je umeuona uzuri wa Mungu, uzuri wa ibada, uzuri wa kukusanyika, uzuri wa uumbaji wake, ambavyo ndio uzuri wa utakatifu? Kama ni ndio basi utamsifu na kumwabudu pia katika tabia zake.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?

Ibada ni nini,Na je ili ikamilike inapaswa iwe na nini na nini?

DHABIHU ZA ROHO NI ZIPI? (1Petro 2:5)

Print this post

Nini maana ya ‘kupelekea mkono’ (Esta 2:21)

SWALI: Nini maana ya “kupelekea mkono” kama ilivyotumika kwenye maandiko. Esta 2:21

Esta 2:21

[21]Ikawa siku zile, Mordekai alipokuwa akiketi mlangoni pa mfalme, wawili katika wasimamizi wake mfalme, Bigthana na Tereshi, wangoje mlango, walighadhibika, wakataka kumpelekea mikono mfalme Ahasuero.

JIBU:

Kupeleka Mkono, ni neno linalomaanisha “kutaka kudhuru”. Kwamfano katika hiyo habari tunaona Mordekai kama msimamizi wa malangoni pa mfalme aligundua njama za watumishi wenzake wengine ambao walitaka kwenda kumuua mfalme..hatujua aidha kwa kumwekea sumu, au kumchoma upanga, au hatua nyingine yoyote ilitayo madhara.

Kitendo hicho kibiblia, huitwa “kupeleka mkono”

Tunaweza kuona jambo lingine kama hilo, wakati fulani Daudi alimkaribia sana mfalme kwa kiwango ambacho angeweza kumuangamiza kama angetaka..lakini akasema nisinyoshe mkono wangu kwa masihi wa Bwana. Maana yake nisimuue.

1 Samweli 24:4-7

[4]Nao watu wa Daudi wakamwambia, Tazama, hii ndiyo siku ile aliyokuambia BWANA, Angalia, nitamtia adui yako mikononi mwako, nawe utamtenda yo yote utakayoona kuwa mema. Basi Daudi akainuka, akaukata upindo wa vazi lake Sauli kwa siri.

[5]Lakini halafu, moyo wake Daudi ukamchoma, kwa sababu amekata upindo wa vazi lake Sauli.

[6]Akawaambia watu wake, Hasha! Nisimtendee bwana wangu, masihi wa BWANA, neno hili, kuunyosha mkono wangu juu yake, kwa maana yeye ni masihi wa BWANA. 

[7]Basi Daudi akawazuia watu wake kwa maneno hayo, asiwaache kumwondokea Sauli. Kisha Sauli akatoka pangoni, akaenda zake.

Bwana akubariki..

Je umempokea Kristo kama Bwana na mwokozi wa maisha yako?

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo.. basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii.. Pia kufahamu tafsiri ya maneno mengine ya kibiblia tazama chini.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ESTA: Mlango wa 1 & 2

Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Paulo kwa Timotheo (1Timotheo)

Kutia mkono chini ya paja kama ishara ya kiapo, kulimaanisha nini?

Print this post

Mapokeo ni nini?

Mapokeo ni mafundisho, mifumo au taratibu zisizokuwepo ndani ya Biblia zilizotengenezwa na watu na kurithishwa kutoka kizazi hata kizazi.

Yapo mapokeo yaliyo mema na yaliyo hatari kwa Imani.. Mfano ya mapokeo mazuri yasiyo na madhara katika imani kama endapo yakifanyika kwa ufunuo ni pokeo ya kuadhimisha siku ya kufufuka kwa Bwana Yesu.. katika Biblia hakuna agizo la kuadhimisha siku ya kufufuka kwa Bwana, hivyo mtu asiyeadhimisha hafanyi makosa, lakini pia anayeadhimisha kwa ufunuo wa kutafakari ufufuko wake, pia hakosei, hivyo huu ni mfano wa pokeo lisilo la hatari.

Na mfano wa mapokeo ambayo ni hatari na yapo kinyume kabisa na Biblia, ni yale yanayofanyika ndani ya  ukatoliki, kama kuadhimisha Ekaristi pamoja na ibada za watakatifu (Hizo hazipo kabisa ndani  ya Biblia), na ni hatari kiroho, kwani kuabudu sanamu au kuitumikia Biblia imekataza jambo hilo katika Kutoka 20:4-5.

Pia mfano wa pokeo lingine lililo baya na hatari kiroho ni ubatizo wa watoto.. Pokeo hili ni maarufu sana lakini ni hatari sana, Kwasababu kwenye Biblia hamna mahali popote watoto wadogo walibatizwa, bali tunaona tu waliwekewa mikono na Bwana Yesu.

Sumu ya mapokeo mabaya  ni ile Bwana Yesu aliyoionyesha katika Marko 7:7-13, kuhusu “Heshima kwa mzazi”

Marko 7:7 “Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu,

8 Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika MAPOKEO YA WANADAMU.

9 Akawaambia, Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu.

10 Maana Musa alisema, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Amtukanaye babaye au mamaye kufa na afe.

11 Bali ninyi husema, Mtu akimwambia babaye au mamaye, Ni Korbani, yaani, wakfu, kitu changu cho chote kikupasacho kufaidiwa nacho, huwa basi;

12 wala hammruhusu baada ya hayo kumtendea neno babaye au mamaye;

13 huku mkilitangua neno la Mungu kwa MAPOKEO YENU mliyopokeana; tena mwafanya mambo mengi yaliyo sawasawa na hayo”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba tunaweza kuishi bila mapokeo na bado tukamwona Mungu na ni vizuri zaidi kuishi bila mapokeo kwani mapokeo mengi yanawafanya watu kuwa mateka wa elimu za uongo, ndivyo Biblia inavyosema..

Wakolosai 2:8 “Angalieni mtu asiwafanye mateka kwa elimu yake ya bure na madanganyo matupu, kwa jinsi ya mapokeo ya wanadamu, kwa jinsi ya mafundisho ya awali ya ulimwengu, wala si kwa jinsi ya Kristo.

9 Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! taratibu za kufunga ndoa yaani harusi] ni agizo la Mungu au ni mapokeo tu ya kibinadamu?

TOFAUTI KATI MAASKOFU, MASHEMASI, WAZEE WA KANISA NI IPI?

KAMA MKRISTO NI LAZIMA UWE NA DESTURI HII.

Je ni Wokovu gani Simeoni aliouona? (Luka 2:30)

Matasa ni nini? (1Nyakati 28:17)

Print this post

‘laana ya torati’ maana yake ni nini?

SWALI: Nini maana ya ‘laana ya torati’, ambayo Kristo alikuja kutukomboa kutoka katika hiyo?

Wagalatia 3:13

[13]Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;


JIBU:

Mungu alimpa Musa Torati ambayo ndani yake haikuwa na baraka tu pale Mtu alipoitii, bali pia ilikuwa na laana nyuma yake pale mtu alipoiasi..

Sasa hizo laana ndio ziliitwa “laana ya torati”, yaani adhabu, hukumu na kutengwa na uso wa Mungu.

Ukisoma Kumbukumbu la torati sura ya 27 – 28 inaeleza kwa undani juu ya baraka na laana mtu azipatapo pale anapoitii Au kunapoikataa torati..

Kwamfano

Kumbukumbu la Torati 27:26 inasema;

[26]Na alaaniwe asiyeyaweka imara maneno ya torati hii kwa kuyafanya. Na watu wote waseme, Amina.

Hivyo wanadamu, wote hawakufanikiwa kuzishika amri zile, na sheria Mungu alizowapa, na matokeo yake ikiwa ni laana juu ya kila mtu.

Warumi 3:10-12,23

[10]kama ilivyoandikwa, ya kwamba,  Hakuna mwenye haki hata mmoja. [11]Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu. 

[12]Wote wamepotoka, wameoza wote pia; Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja…

[23]kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;

Sasa Kristo alipokuja, alifanywa laana kwa ajili yetu..sawasawa na hiyo Wagalatia 3:13, maana yake aliichukua hukumu yetu ya makosa kwa kupigwa na kufa kwake pale msalabani ili sisi tuponywe..

Warumi 8:1

[1]Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.

Ndio maana mtu yeyote ambaye hajamwamini Kristo bado yupo Chini ya hukumu na adhabu, kwasababu atataka kumpendeza Mungu kwa kutegemea tu nguvu zake mwenye, na hatimaye mwisho wa siku atashindwa..kwasababu hakuna mwanadamu aliyewahi kuishika torati yote…

Atasema haibi, hasemi uongolakini wakati huo huo ana mawazo mabaya, yote hayo ni makosa na dhambi…na mshahara wa dhambi sikuzote ni mauti..(Warumi 6:23)

Umeona umuhimu wa Yesu maishani mwetu?

Unasubiri nini usimwamini, akutoe katika laana hiyo, ili uhesabiwe bure kwa neema yake?

Mpokee sasa akuokoe…bofya hapa kwa mwongozo wa sala hiyo…

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NJIA/BARABARA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Neema ni nini?

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 21:3 Kutenda haki na hukumu  Humpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka.

SWALI: Nini maana ya Mithali 21:3

[3]Kutenda haki na hukumu  Humpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka.

JIBU:

Mstari huo unatufundisha mambo ambayo Mungu huvutiwa nayo zaidi…

Mungu hupendezwa zaidi na sisi tunapoishi maisha ya haki, tunatenda mema, tunawajali wengine, tunaishi sawasawa ni viwango vyake vya kiroho hapa duniani..kwake hiyo ni bora zaidi ya sadaka zetu tumtoleazo.

Sadaka huwakilisha mambo yote Ya kidini tunayoweza kumfanyia Mungu, mfano ibada, fedha, mifungo, maombi, kuhubiri, kuimba n.k

Bwana huvutiwa zaidi na mioyo na tabia zetu, na sio zile Ibada za nje tu..

Haimaanishi kuwa hapendezwi na hivyo vitu hapana…bali hivyo vifanywe baada ya kutii kwanza..

Tunaona jambo kama hilo amelisisitiza sehemu nyingi kwenye maandiko; Tukianzia kwa Sauli alimwambia, hivyo;

1 Samweli 15:22

[22]Naye Samweli akasema,  je! BWANA huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu  Sawasawa na kuitii sauti ya BWANA? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu,  Na kusikia kuliko mafuta ya beberu.

Mika 6:6-8 inasema;

[6]Nimkaribie BWANA na kitu gani, na kuinama mbele za Mungu aliye juu? Je! Nimkaribie na sadaka za kuteketezwa, na ndama za umri wa mwaka mmoja?

[7]Je! BWANA atapendezwa na elfu za kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je! Nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa kosa langu, mzao wa mwili wangu kwa dhambi ya roho yangu?

[8]Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na BWANA anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!

Soma pia..

Isaya 1:11-17 – Inasema…Bwana huchukizwa na sadaka za watu wanaishi katika dhambi

Hivyo ni lazima tujiulize Je! tunatenda haki kwa wengine?

Je! Tunatembea kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wetu?

Je! tunamtii Mungu, kuliko vitu vingine vyovyote?

Je tunawahurumia wengine…?

Mambo kama haya ndio yenye uzito zaidi kwa Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE NI KUTII AU KUPATA KWANZA MAARIFA?

Maana ya 2Wakorintho 9:11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote

MCHE MWORORO.

Print this post

Je kuna Yohana wangapi katika biblia?

katika agano jipya wapo watu wanne ambao wametajwa kwa jina la Yohana.. Wawili kati ya hao ndio hujulikana sana…ambao ni Yohana mbatizaji na Yohana mtume wa Yesu ..hawa wametajwa Sehemu nyingi katika agano jipya..

1) Yohana Mbatizaji

Mfano vifungu ambavyo utamsoma Yohana mbatizaji ni kama vifuatavyo:

  • (Luka 1) – Kama mwana wa Zekaria na Elisabeti
  • (Mathayo 3:13-17), Kama aliyembatiza Yesu
  • (Marko 6; 14-29)- Kama aliyekatwa Kichwa na Herode.

2) Yohana mtume.

Hivi ni vifungu vinavyomtaja Yohana Mtume;

  • (Mathayo 10:2) – Kama mmoja wa mitume 12 wa Yesu
  • (Marko 1:19) Kama ndugu wa Yakobo, na mwana wa Zebedayo

Na ndiye mwandishi wa injili ya Yohana, pia na nyaraka zote tatu (1,2, 3 Yohana, ) pamoja na kitabu cha Ufunuo.

3) Marko (Msaidizi wa huduma ya Paulo na Barnaba)

Yohana mwingine ni Marko, ndiye mwandishi wa kitabu cha Marko,..anatajwa katika kitabu cha Matendo 12:12, 13:5, Wakolosai 4:10

Na ndiye aliyekuwa Msaidizi wa Paulo na Barnaba katika ziara zao za kupeleka injili kwa mataifa.

4) Yohana babaye Petro

Yohana mwingine ni Baba wa Simoni Petro anatajwa katika;

Yohana 1:42

[42]Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe).

Soma pia Yohana 21:15-27

Hivyo jumla Yao ni wanne…

Je ungependa kufahamu Zaidi watu wengine Katika biblia? Kama ni ndio basi jiunge tazama chini kwa makala nyingine..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Filipo ni nani na je! Kuna Filipo wangapi katika biblia?

Maherodi walikuwa ni akina nani, Na kazi yao ilikuwa ni ipi?

Kwanini nguo za waliomwua Stefano ziwekwe miguuni mwa Sauli?.

Print this post

Kijana ni nani kibiblia?

Biblia haitoi umri fulani maalumu kwamba mtu akiufikia huo basi ndio huitwa kijana.. Japokuwa ni mtu ambaye yupo umri wa hapo katikati yaani utoto na utu uzima, lakini hutambulika kwa kuangalia vitu kama hatua za ukuaji wake, uwajibikaji wake na uzoefu wake wa kimaisha.

Kwamfano katika biblia watu hawa walitajwa kama vijana.

  • Ishmaeli (mwanzo 21:14-20)
  • Isaka (Mwanzo 22:5)
  • Yusufu mwanzo 42:22. (Akiwa na miaka 17)
  • Mfalme Sauli (1Samweli 9:2)
  • Timotheo (1Timotheo 4:12)

Na wengine kadha wa kadha..

Yafuatayo ni Mambo ambayo kijana yeyote anatarajiwa awe nayo kibiblia.

1) Awe anamtafuta Mungu Na kulitii Neno la Mungu.

Mhubiri 12:1

[1]Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo. 

Zaburi 119:9

[9]Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako. 

2) Awe na hekima na tabia ya uongozi, (yaani wakati wote ajifunze kuwa kielelezo.)

1 Timotheo 4:12

[12]Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.

3) Awe na nguvu za rohoni, za kumshinda shetani.

Mithali 20:29

[29]Fahari ya vijana ni nguvu zao,..

1 Yohana 2:14

[14]Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.

Lakini pia kijana anakabiliwa na tamaa za ujanani kama vile uzinzi, anasa,starehe..hivyo Anatarajiwa azikimbie wakati wote.

2 Timotheo 2:22

[22]Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.

Kutokana na vigezo hivyo tunaweza Kuona ujana pengine huanzia umri wa kubalehe, mpaka wakati mtu anapungua Nguvu zake mwilini.. labda Miaka 12-45…japo yaweza kupungua au kuzidi..

Zingatia:

Ikiwa wewe ni kijana, hakikisha maonyo hayo unayatendea kazi mapema…

Lakini ikiwa wewe ni mzazi na una mtoto, fahamu kuwa siku moja atakuwa kijana,hivyo kabla adui hajamtumia, anza kumjengea misingi mizuri ya kutembea katika Imani ya wokovu, naye hataicha njia hiyo mpaka atakapokuwa mtu mzima

Mithali 22:6

[6]Mlee mtoto katika njia impasayo,

Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VIJANA NA MAHUSIANO.

Je Bwana YESU alikuwa na amri ya kumwingiza mtu katika ufalme wa MUNGU au hakuwa nayo?

Fahamu maana ya Mithali 10:5 Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima; 

Print this post

Kuseta ni nini?

Kuseta kama ilivyotumika kwenye maandiko maana yake ni kukiharibu kitu, aidha kwa kukiponda, kukikanyaga, au Kukivunja vipande vipande.

Kwamfano kwenye maandiko kama haya tunaweza kuona neno hilo..

Warumi 16:19-20

[19]Maana utii wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya.

[20]Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi.

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. [Amina.]

Hapa Mungu anaonyesha kwamba pale tunapokuwa mbali na mambo mabaya ndivyo anavyomponda shetani chini ya miguu yetu..

Kuonyesha kuwa njia kuu ya kumshinda shetani sio kumkemea bali ni kujitenga na mambo maovu.

Vifungu vingine ni kama hivi..

Zaburi 110:5

[5]Bwana yu mkono wako wa kuume;  Ataseta wafalme,  Siku ya ghadhabu yake.

Hapa Mungu anaonyesha ukali wa ghadhabu yake juu ya watu waovu..hata wale wanaoonekana ni wakuu, hawataikwepa hasira yake atawaharibu kwa kuwaponda- ponda.

kwa hitimisho ni kuwa kuseta ni kuharibu kabisa Kabisa ..Na Mungu amekusudia kufanya hivyo sio kwetu bali kwa shetani… Ni sisi tu kuishi maisha yanayomlingana yeye ikiwa tayari tumeshaokoka…Lakini ikiwa ni kinyume na hapo tutaingia katika mkondo huo huo wa shetani, wa kuharibiwa endapo hatutamwamini Yesu Kristo leo.

Je upo tayari kumpokea Yesu leo? Kama ni ndio basi bofya hapa >> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MWEKE SHETANI MBALI NA WEWE.

SI SHETANI BALI NI WEWE. (CHAGUA MEMA)

DANIELI: Mlango wa 2

Print this post