Category Archive Home

MUNGU WETU HUONDOA CHANZO PAMOJA NA MKONDO WAKE.

Jina la Mwokozi YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze Biblia Neno la MUNGU wetu, lilio taa na mwanga wa njia yetu.

Unapofika wakati MUNGU wetu wa UPENDO, anapotaka kututoa sehemu moja kwenda sehemu nyingine kwa kuondoa matatizo makuu yanayotishia maisha yetu, basi huo haondoi tu chanzo cha tatizo bali pia na mkondo wake wote anauondoa.

Ili tuende pamoja, hebu turejee wakati Bwana YESU anazaliwa, maandiko yanasema Herode alitafuta kumwua mtoto YESU, lakini Yusufu na Mariamu kupitia onyo la Malaika wa Bwana waliambiwa wakimbilie Misri ili Herode asimwue mtoto.

Lakini jambo la ajabu ni kwamba baada ya Herode kufa, biblia inatuambia hakufa peke yake bali na wengine waliokuwa na nia kama ya kwake ya kumwangamiza mtoto, ambao biblia haijawataja majina yao.

Mathayo 2:19 “Hata alipofariki Herode, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto huko Misri,

20 akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mamaye, ushike njia kwenda nchi ya Israeli; kwa maana WAMEKUFA WALIOITAFUTA ROHO YA MTOTO”.

Hapo anasema “WAMEKUFA”..na si “AMEKUFA”  Maana yake hakuwa mmoja bali wengi, maana yake si Herode peke yake, walikuwepo na wengine waliokuwa na nia kama ya Herode…huenda wakuu wa majimbo waliofanya kazi na Herode, au makuhani au raia wa kawaida.

Kwahiyo waliokuwa wanaitafuta roho ya mtoto, hawakuwa wachache, bali wengi (ulikuwa ni mkondo) na wote walikufa..Herode alikuwa tu ni kichwa cha pweza, lakini mikia ilikuwa mingi!.

Endapo Yusufu na mtoto wangeendelea kubaki Bethlehemu walikuwepo wapelelezi wengi hivyo taarifa kuhusu mtoto zingemfikia Herode haraka, hata baada ya yale maangamizi kupita bado hatari ilikuwepo, kwahiyo suluhisho ni wote wafe kwanza ndipo usalama uwepo wa Bwana YESU kurudi Israeli.

Sio hilo tu, utakumbuka pia ile habari ya Malkia Esta, wakati Hamani, adui wa wayahudi alipoandika waraka wa wayahudi wote kuuawa, katika siku moja!.. kama ni mwanafunzi wa Biblia utagundua kuwa si Hamani peke yake aliyekuwa adui wa waisraeli kwa wakati ule!, bali walikuwepo wengine wengi katika kila jimbo la mfalme Ahasuero,  Hamani yeye alikuwa ni kichwa tu cha pweza kama alivyokuwa Herode!.

Ndio maana mambo yalivyoharibika kwa Hamani, hakufa peke yake bali na maadui wote wa wayahudi katika ufalme wote.

Esta 9:1 “Hata ulipofika mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari, siku yake ya kumi na tatu, amri ya mfalme na mbiu yake ilipowadia kutekelezwa; ambayo siku ile ADUI ZA WAYAHUDI walitumaini kuwatawala, bali kumebadilika kinyume, hata Wayahudi waliwatawala wale waliowachukia;

2 siku ile ile Wayahudi wakakusanyika mijini mwao katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero ili kuwatia mikono wale watu waliowatakia hasara; wala asiweze mtu kuwazuia, kwa kuwa hofu yao imewaangukia watu wote. …….

5 Basi Wayahudi wakawapiga adui zao wote mapigo ya upanga, na machinjo, na maangamizo, wakawatenda kama wapendavyo wale waliowachukia.

6 Hata huko Shushani ngomeni Wayahudi wakawaua watu mia tano, na kuwaangamiza…………

16 Nao Wayahudi wengine waliokaa katika majimbo ya mfalme walikusanyika, wakazishindania maisha zao, wakajipatia raha mbele ya adui zao, wakawaua waliowachukia, WATU SABINI NA TANO ELFU; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono”.

Watu zaidi ya Elfu 75 walikufa pamoja na HAMANI, ingawa kwa haraka tunaweza kuona kama aliyekuwa adui wa wayahudi alikuwa ni Hamani peke yake, kumbe hakuwa peke yake bali ulikuwa ni mkondo mkubwa ibilisi alioutengeneza kwa muda mrefu!.

Hivyo ukiona mtu mmoja mashuhuri anafanya vita na wewe katika vitu vilivyo sahihi unavyovifanya basi fahamu kuwa hayupo peke yake bali upo mkondo wa ibilisi nyuma yake!, na wakati wa MUNGU ukifika huwa anakiondoa chanzo na mkondo wake, ili amani irejee..

Na MUNGU anapokiondoa chanzo na mkondo wake si lazima awaue maadui zako kama inavyodhaniwa  na wengi, La! Kifo chaweza kuwa njia ya mwisho kwa MUNGU wetu dhidi ya tunaowaona kama maadui zetu,

Lakini badala yake MUNGU anaweza kuwahamisha na kuwapeleka mbali au kukuhamisha wewe ukae mbali nao sehemu salama, au  anaweza kuwabadilisha na kuwafanya watu wazuri (wakamrudia MUNGU)..na lile tatizo likawa limeondoka, na hambadilishi yule chanzo tu peke yake, bali na mkondo mzima, Ndio hapo unashangaa watu waliokuwa wanakuchukia na kukupiga vita sasa wanakupenda, waliokuwa maadui zako sasa mnaishi kwa amani n.k

Swali: Niombe maombi gani ili Mungu aondoe chanzo cha matatizo na mkondo wake?

Badala ya kufikiri namna ya kuomba, fikiri kuzitengeneza njia zako mbele za MUNGU, njia zako zinaponyooka mbele za MUNGU (kwa kuishi maisha ya kumpendeza MUNGU), basi MUNGU anashughulika na vyanzo vyote na mikondo yake, kwa kukurejeshea amani..

Mithali 16:7 “Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye”.

Lakini usiponyoosha njia zako kwa MUNGU, na ukategemea maombi tu peke yake, bado safari itakuwa ndefu, Maisha yetu yanajalisha sana katika kuelezea vyanzo vya matatizo tuliyonayo, yakizidi kuwa safi mbele za MUNGU ndivyo matatizo yatakavyozidi kuwekwa mbali.

Je umempokea YESU?.

Unao uhakika Bwana YESU akirudi leo unakwenda naye?

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni kwa namna gani Bwana YESU alikula Siagi na Maziwa? (Isaya 7:15)

Kuonja ni kufanya nini? (Kutoka 15:25).

NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

NIONYESHE MARAFIKI ZAKO, NIKUAMBIE TABIA ZAKO.

Print this post

PEPETO LA BWANA LINAPITA.

Shalom,

Je unajua Pepeto ni nini na kazi yake ni ipi?

Turejee Mathayo 3:11-12.

Mathayo 3:11 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.

12 Ambaye PEPETO LAKE li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya NGANO yake ghalani, bali MAKAPI atayateketeza kwa moto usiozimika”.

Pepeto ni kifaa maalumu chenye umbile kama la “UMA” ambacho wakulima wa nafaka kama ngano, wanakitumia kupuria/kupepetea ngano.. sasa jamii zetu zinatumia NYUNGO kupepetea nafaka kama mchele na ngano, ambapo ungo ule unazurusha juu nafaka kisha upepo unatenga ile nafaka na makapi.

Lakini zamani wakulima wa ngano hawakutumia nyungo, kwani kulikuwa na matita mengi ya ngano, hivyo UNGO usingetosha kuimaliza kazi yote, hivyo walitumia kifaa hiko kinachoitwa Pepeto, ambacho kinafanana sana na UMA. (Tazama picha chini).

pepeto ni nini

Sasa kiroho Ngano ni “NENO LA MUNGU”, na makapi ni “NDOTO NA MAONO YA UONGO” katika siku za mwisho Bwana atatenga Neno lake na maono ya uongo, na watu wanaolifuata Neno lake na wanaofuata manabii wa uongo.

Yeremia 23:25 “Nimesikia waliyoyasema manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema, Nimeota ndoto; nimeota ndoto.

26 Je! Mambo hayo yatakuwa katika mioyo ya manabii wanaotabiri uongo hata lini, manabii hao wenye udanganyifu katika mioyo yao wenyewe?

27 Wanaodhania ya kuwa watawasahaulisha watu wangu jina langu kwa ndoto zao, wanazomhadithia kila mtu jirani yake, kama vile baba zao walivyolisahau jina langu, kwa ajili ya Baali.

28 Nabii aliye na ndoto, na aseme ndoto yake; na yeye ALIYE NA NENO LANGU, na aseme neno langu kwa uaminifu. MAKAPI NI KITU GANI KULIKO NGANO? Asema Bwana”.

Mstari wa mwisho hapo anasema, “Makapi ni kitu gani kuliko Ngano” ikimaanisha kuwa makapi ni unabii/ndoto za uongo zinazotolewa na manabii wa uongo si kitu mbele ya Neno la MUNGU linalofananishwa na Ngano.

Kwahiyo katika siku za mwisho, YESU KRISTO ambaye ndiye pepeto lenyewe, atatenga makapi na ngano, na wanaotumainia makapi na wale wanalotumainia Neno lake.

Hizi si siku za kupelekwa huku na kule na manabii wa uongo, wanaoshinda kutwa kuchwa kutabiri maono ya uongo, wakiwaaminisha na kuwatumainisha watu katika vitu vya ulimwengu huu, kwamba kuwa na hivyo ndio kielelezo cha kwanza cha kukubaliwa na MUNGU.

Bwana YESU alisema, itamfaidia nini mtu apate ulimwengu mzima na kisha apate hasara ya nafsi yake (Marko 8:36)?..maana yake utabiriwe na nabii au mchungaji au mtume kwamba utapata hiki na kile cha ulimwengu huu, na wakati huo huo haioni dhambi maishani mwako, je hayo aliyokutabiria yatakufaidia nini ikiwa utapoteza uzima wa milele?

Hizi ni siku za mwisho na pepeto hili limeshaanza kupita, na Roho Mtakatifu anawatenga walio wa kwake, hatua hizo zikimalizika kinachofuata ni unyakuo wa kanisa, ambapo walioishi na kulifuata Neno la MUNGU watakusanywa ghalani (mbinguni).. lakini waliofuata makapi watatupwa katika lile ziwa la moto, ndivyo maandiko yanavyosema..

Mathayo 13:29 “Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.

30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu…

40 Basi, kama vile magugu yakusanywavyo na kuchomwa motoni; ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia.

41 Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi,

42 na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAMBO SITA, AMBAYO MUNGU HUTUMIA KUONDOA UOVU NDANI YA MTU.

Ipi tofauti kati ya Uhai na Uzima kibiblia?

KIMBIA MACHAFU YA DUNIA. (2Petro 2:20)

Je kibiblia ni sahihi kuadhimisha jumapili ya mitende?

“Amdhaminiye mgeni hakosi ataumia;Achukiaye mambo ya dhamana yu salama

Print this post

JINSI MATENDO YA IMANI YANAVYOWEZA KULETA UTAMBULISHO MPYA KWA MTU.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe daima.

Je unajua matendo ya Imani, yanaweza kuleta utambulisho mwingine kwako tofauti na ule wa kwanza, na kibali kipya.

Turejee Biblia, kisa cha Daudi kumwua Goliati, biblia inaonyesha kuwa kabla ya Daudi kumwua Goliati, alikuwa anaishi nyumbani kwa Mfalme Sauli katika jumba la kifalme, na kazi yake pale ilikuwa ni kupiga kinubi, wakati roho mbaya ilipomjia Sauli.

1Samweli 16:21 “Basi Daudi akamwendea Sauli, akasimama mbele yake, naye akampenda sana; naye akapata kuwa mtu wa kumchukulia silaha zake.

22 Kisha Sauli akapeleka watu kwa Yese, akasema, Tafadhali, MWACHE DAUDI ASIMAME MBELE YANGU; MAANA AMEONA KIBALI MACHONI PANGU.

23 Ikawa, ile roho mbaya kutoka kwa Mungu ilipomjilia Sauli, ndipo Daudi akakishika kinubi, akakipiga kwa mkono wake, naye Sauli akaburudishwa, na ile roho mbaya ikamwacha”.

Hapa tunaona tayari Mfalme Sauli amemjua Daudi na tena amemfanya kuwa mchukua silaha wake, sasa ni ngumu kumfanya mtu kuwa mchukua silaha, kama bado hujamjua wala kumkubali.

Lakini tukiendelea kusoma habari hii mbele kidogo baada ya Daudi kumwua Goliati tunaona jambo lingine la kushangaza.. kwamba Sauli anamwuliza tena Daudi yeye ni mwana wa nani, kana kwamba alikuwa hamjui hapo kwanza..

1Samweli 17:54 “Naye Daudi akakitwaa kichwa chake yule Mfilisti na kukileta Yerusalemu; lakini silaha zake akaziweka hemani mwake.

55 Basi Sauli, hapo alipomwona Daudi akitoka ili kumwendea yule Mfilisti, alimwambia Abneri, jemadari wa jeshi, Je! Abneri, kijana huyu ni mwana wa nani? Abneri akamjibu, Ee mfalme, kama iishivyo roho yako, mimi siwezi kusema.

56 Basi mfalme akasema, Uliza wewe, KIJANA HUYU NI MWANA WA NANI.

57 Hata na Daudi alipokuwa yuarudi kutoka katika kumwua yule Mfilisti, Abneri alimtwaa, akamleta mbele ya Sauli, naye anacho kichwa chake yule Mfilisti mkononi mwake

58 Basi Sauli akamwuliza, Wewe, kijana, u mwana wa nani? Naye Daudi akamjibu, Mimi ni mwana wa mtumishi wako, Yese, mtu wa Bethlehemu.”

Kama Daudi asingefanya tendo lile la imani na kishujaa, la kumwua Goliati, Mfalme asingemjua Daudi, ingawa tayari alishajitambulisha kwake na hata kuishi naye… Baada ya tukio hilo tunazidi kuona kibali cha Daudi kuongezeka kwa kiwango kingine.

1Samweli 18:1 “Ikawa Daudi alipokwisha kusema na Sauli, roho ya Yonathani, ikaambatana na roho ya Daudi, Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe”.

Hapo kabla Yonathani huwenda alikuwa anamwona Daudi kama mwimba ngojera tu! kwenye nyumba ya mfalme.

Kama Goliati akiendelea kusimama katika maisha yako usipomwangusha kwa imani unaweza kuendelea kubaki pale pale, lakini kama ukichukua mawe matano kama Daudi na kumwangusha chini, basi hapo umefungua kibali kipya!..  Jina lako linakuwa sio lile lile tena, nafasi yako sio ile ile tena, kujulikana kwako kunakuwa sio kule kule tena.

Goliati ni roho yoyote inayojiinua ya vitisho, na Goliati wa kwanza katika maisha yetu ni Dhambi!.. Huyu ndiye anayesumbua!, ndiye anayeficha kibali chetu, ndiye anayeficha nafasi zetu na kutuzuilia kusonga mbele, tukiweza kumwangusha huyu na jeshi lote la wafilisti (magonjwa, shida, na mambo mengine yatesayo) yanakimbia, na tunabaki washindi na wenye kibali kingine.

Je umetubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha?..kama bado ni nini unasubiri?.. kumbuka kuomba msamaha sio kutubu, bali toba halisi inakamilishwa kwa kuacha matendo yote mabaya ya giza, maana yake baada ya kuomba msamaha wa dhambi kutoka kwa MUNGU, kinachofuata ni kuacha zile njia mbaya, ikiwemo kujitenga na makundi ya watu yanayopalilia dhambi iliyokuwa inakusumbua.

Vile vile kuacha kufanya vitu, au kuangalia vitu vilivyokuwa vinakukosesha, na pia kuacha kuvaa mavazi yaliyokuwa yanakaribisha dhambi maishani mwako. Kwa kufanya hivyo utakuwa umemwangusha Goliati na kubali chako kitaongezeka kama ilivyokuwa kwa Daudi.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini MUNGU alimzuia Daudi asimjengee HEKALU? (1Nyakati 17:12)

Daudi alikuwa na wake wangapi, na je ni halali kuwa na wake wengi?

Waanaki ni watu gani katika biblia?

JE! UNAWEZA KUWA NA GEUKO KAMA LA DAUDI?

Je! aliyemwua Goliathi ni Daudi au Elhanani.

Print this post

Je! Petro na wenzie walitambuaje kuwa wale walikuwa ni Musa na Eliya?

Swali: Katika kitabu cha Mathayo 17:4 Mtume Petro na wenzie waliwezaje kufahamu kuwa wale ni Musa na Eliya?


Jibu: Turejee habari hiyo kuanzia ule mstari wa kwanza..

Mathayo 17:1 “Na baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani;

2 akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang’aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru.

3 Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.

4 Petro akajibu akamwambia Yesu, Bwana, ni vizuri sisi kuwapo hapa; ukitaka, nitafanya hapa vibanda vitatu, kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya”.

Biblia haijaeleza kama Musa na Eliya walijitambulisha katika maono yale, ikiwa na maana kuwa kuna njia nyingine iliyowafanya Petro na wenzie kujua kuwa wale ni manabii Musa na Eliya na si wengine.

Sasa njia Pekee iliyomfanya Petro na wenzie kufahamu kuwa wale walikuwa ni Musa na Eliya na si wengine, ni UFUNUO WA ROHO MTAKATIFU.

Kama vile ufunuo wa Roho Mtakatifu ulivyomjia Petro kumhusu YESU.

Mathayo 16.15 “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?

16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.

17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”.

Umeona hapo?, aliyemwambia Petro kuwa YESU ni KRISTO tena ni MWANA WA MUNGU aliye juu sio YESU mwenyewe!, bali ni ufunuo wa alioupokea kutoka kwa Baba.

Na hiyo sio ajabu kwani walikuwa wameenda mlimani kuomba.. ni kawaida kwa watumishi wa MUNGU kupokea mafunuo ya mambo yaliyopo, au yajayo wanapokuwa katika maombi, hususani kama hayo ya mlimani.

Kwahiyo Mtume Petro na wenzie walipata ufunuo wa ujio au uwepo wa manabii hao wawili wakiwa katika maombi, utaona jambo kama hilo lilishatokea tena kwa Petro wakati yupo kwa Yule Simoni mtengenezaji wa ngozi wa kule Yafa, wakati ambapo Roho Mtakatifu alimfunulia alipokuwa katika maombi kuwa kuna watu watatu wanamwulizia, hivyo aende nao asiogope!, na kweli ikawa hivyo..

Matendo 10:17 “Hata Petro alipokuwa akiona shaka ndani ya nafsi yake, maana yake ni nini maono hayo aliyoyaona, wale watu waliotumwa na Kornelio, wakiisha kuiulizia nyumba ya Simoni, wakasimama mbele ya mlango,

18 wakaita; wakauliza kwamba Simoni aitwaye Petro anakaa humo.

19 Na Petro alikuwa akiyafikiri yale maono. Roho akamwambia, Wako watu watatu wanakutafuta.

20 Basi ondoka ushuke ufuatane nao, usione tashwishi, kwa maana ni mimi niliyewatuma.

21 Petro akawashukia wale watu, akanena, Mimi ndiye mnayemtafuta. Mmekuja kwa sababu gani?”

Kwa namna hiyo hiyo, huenda Petro na wenzake walipokea ufunuo kuwa wale ni Musa na Eliya, labda walipokea ufunuo huo muda mchache kabla hawajawatokea, au wakati ule ule walipotokea.

Kikubwa tunachoweza kujifunza ni kuwa tuwapo katika uwepo wa MUNGU kama katika maombi, ni rahisi kupokea ufunuo wa Roho Mtakatifu kwani tunakuwa tupo katika roho, na mtu anapokuwa katika roho anayatambua mambo yote ya rohoni pasipo kuambiwa!

Hivyo ni muhimu sana kuwa waombaji, na wasomaji wa Neno la MUNGU, endapo akina Petro wangekuwa si watu wa kusoma maandiko, ni dhahiri kuwa wasingemjua Musa wala Eliya na hiyo ingezuia Roho kuwafunulia watu hao, kwani Roho Mtakatifu anamfunulia mtu kitu ambacho kinahusiana na Neno la MUNGU.

Je na wewe ni mtu wa kudumu uweponi mwa MUNGU? Je KRISTO YESU?..Je unao uhakika kwamba akirudi unaenda naye?

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini Eliya afunge Mbingu miaka mitatu na nusu? (1Wafalme 17:1)

TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?

Je! Tutatambuana tukifika mbinguni?

Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?

Kwanini Mungu alimchagua Musa, na si mtu mwingine?

Print this post

UFAHAMU UFUNGUO WA KUMPENDA BWANA ZAIDI

Je unaujua ufunguo wa wewe kumpenda Bwana zaidi?.. kuna jambo ukilifanya basi upendo wako kwa MUNGU utaongezeka kwa kiwango kikubwa sana.. Utajikuta unampenda MUNGU zaidi, unamheshimu zaidi na unamtumikia zaidi.

Na ufunguo huo si mwingine zaidi ya kuutafakari MSAMAHA WAKE KWAKO KWA MAPANA!.. Unaweza kuona jambo la msahama kwako ni dogo tu!.. Lakini nataka nikuambie Msamaha wa MUNGU kwako una uhusiano mkubwa sana na UPENDO WAKO KWAKE!.

Maandiko yanasema “aliyesamehewa sana hupenda sana, na aliyesamehewa kidogo hupenda kidogo”

Luka 7:47 “Kwa ajili ya hayo nakuambia, Amesamehewa dhambi zake ambazo ni nyingi kwa kuwa amependa sana; lakini asamehewaye kidogo, huyo hupenda kidogo”.

Hebu tafakari huu mfano: Mtu mmoja alikuwa anadaiwa shilingi 500 na mwenzake na akasamehewa na mwingine aliukwa anadaiwa shilingi laki 5 na mtu huyo huyo mmoja, naye pia akasamehewa kiasi chote cha pesa (shilingi laki 5)..

Je yupi kati ya hao wadaiwa wawili waliosamehewa, atampenda zaidi Yule aliyewasamehe?.. Bila shaka Yule aliyesamehewa deni kubwa ndiye atakayempenda zaidi aliyemsamehe, na hata kumheshimu sana..

Lakini Yule aliyesamehewa deni dogo, anaweza kuwa mtu wa shukrani lakini si katika kiwango kikubwa, na wala hawezi kutoa heshima ya kiwango kikubwa kwa yule aliyemsamehe.

Ni hivyo hivyo katika upande wa Imani, watu waliojiona ni wenye dhambi nyingi na kubwa kubwa!, na kujiona kama hawajastahili msahama kwa makosa yao, wanapoungama na kupokea msamaha, huwa wanampenda sana Bwana YESU na kumheshimu.

Lakini watu wanaojiona ni wasafi au watakatifu sana, kwamba hawamkosei sana MUNGU huwa hata upendo na MUNGU hawana, au upo kwa kiwango kidogo.

Sasa kiuhalisia wote tumemkosea MUNGU pakubwa sana!.. ukijiona huna dhambi nyingi, basi fahamu kuwa kuna shida kwako ya kutafakari, ambayo hiyo sasa ndio unapaswa ushughulike nayo.

Unapaswa ushughulike na hiyo hali mpaka ifikie hatua ujijue kuwa hukustahili, na wewe ulikuwa ni mbaya mno, na mbovu, na makosa yako yalikuwa makubwa sana!.. ukiweza kufikia hiyo tafakari, basi jua matunda yako ni wewe kumpenda BWANA na kumheshimu sana.

Unawezekana wewe sio mwizi, au muuaji au mzinzi lakini hebu tafakari vipindi ulivyomsema ndugu yako, na MUNGU alikufumbia macho, ingawa ulistahili adhabu ya mauti papo kwa hapo.

Hebu tafakari vipindi ulivyotamani vitu visivyofaa moyoni mwako, na MUNGU alikufumbia macho ingawa ulistahili kufa papo kwa hapo.

Hebu tafakari vipindi ulivyokasirika bila sababu, tafakari vipindi uliyokuwa unawaza mawazo mabaya, tafakari vipindi ulivyodanganya na kusema uongo, tafakari vipindi miguu yako ilipokuwa inaelekea kufanya maovu, tufakari vipindi ulivyotukana mdomoni na moyoni mwako, tafakari mambo ya upumbavu uliyoyafanya mitandaoni,  hayo yote si kwamba MUNGU alikuwa haoni, au hata sasa hayaoni, anayaona yote!.

Inawezekana hujawahi kuua, lakini tafakari vipindi ulivyokuwa mbinafsi, tafakari visasi na vinyongo ulivyokuwa navyo, na huenda unavyo hata sasa, tafakari udunia wote ulioufanya, rudi nyuma kumbuka tukio moja baada ya lingine katika maisha yako, yatakafari sana halafu fikiri YESU AMEJITWIKA makosa yako yote hayo, ambayo kama si rehema zake huenda ungekuwa umeshakufa na upo KUZIMU sasa!.

Lakini alikizuia kifo kisikupate!, umempa nini?, au una umaalumu gani hata akusamehe hayo yote?, kwani waliokufa bila kupata huu msamaha wana kasoro gani zaidi yako?.

Je huoni kama aliyekupa huu msahama ni wa thamani kubwa? Huoni kama amekusamehe makubwa sana.. bado humpendi tu!.. ungepaswa uwe kuzimu muda huu, lakini bado unaishi! Bado kwako unamwona vile vile?

Ndugu tenga muda sana utafakari msamaha wa YESU, kwani ndio uliobeba funguo za kumpenda YESU zaidi, Ukiutafakari msamaha wa YESU utaishia kumpenda, lakini pia kumwogopa (kutokutenda dhambi tena)

Zaburi 130:4 “Bwana, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama?

4 Lakini kwako kuna msamaha, Ili Wewe uogopwe”.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NGUVU YA MSAMAHA

UMUHIMU WA KUOMBA MSAMAHA.

NI KWA NAMNA GANI KRISTO ALIZIBEBA DHAMBI ZETU?

JE UMEUPOKEA UWEZA WOTE WA UUNGU NDANI YAKO?

Hadhari ni nini kibiblia? (Mithali 1:4)

Print this post

Yesu aitwaye Yusto alikuwa ni nani? (Wakolosai 4:11).

Swali: Je huyu Yesu anayetwaja katika Wakolosia 4:11 alikuwa ni nani, na je ni kwanini aitwe hilo jina tukufu?


Jibu: Turejee..

Wakolosai 4:11 “Na YESU AITWAYE YUSTO; hao ni watu wa tohara. Tena hao peke yao ni watendaji wa kazi pamoja nami kwa ajili ya ufalme wa Mungu; nao walikuwa faraja kwangu”.

Katika Biblia Kristo mwokozi wetu hakuwa wa kwanza kuitwa jina YESU, bali walikuwepo watu wengine kadhaa kabla yake walioitwa kwa hilo jina, kwani lilikuwa ni jina linalojulikana Israeli yote,

Na tafsiri ya jina YESU ni  (YEHOVA-MWOKOZI), kama vile ilivyokuwepo YEHOVA-YIRE ambayo tafsiri yake ni YEHOVA mpaji n.k

Kwahiyo YESU ni jina lililokuwepo hapo kabla, kama tu Simeoni aliyeitwa Petro, hakuwa wa kwanza kuitwa Simeoni, au Yuda aliyemsaliti Bwana YESU hakuwa wa kwanza kuitwa Yuda, kwani hata mtoto wa Yakobo,  aliitwa Yuda, na ndio ukoo Bwana YESU aliotokea.

Sasa ni kitu gani kilichomtofuatisha YESU mwokozi wetu na maYesu wengine?.. si kitu kingine bali ni kiunganishi cha mwisho cha jina hilo,.. Aliyetufia anajulikana kama YESU KRISTO,  maana yake YESU MTIWA MAFUTA na MUNGU…

Wengine wanaitwa “Yesu wa Yusto”, wengine “Bar-YESU” (soma Matendo 13:6) lakini ni mmoja tu anaitwa “YESU KRISTO”.. Huyu kwa jina lake hili ndio tunapata ondoleo la dhambi na wokovu (Matendo 4:12).

Na kwa jina la YESU KRISTO, Tunafunguliwa na kuponywa magonjwa yetu, na ziadi sana ndio kwa jina hili tunapaswa tuhubiri na kuhubiriwa ili tupate ukombozi.

Lakini katika hizi siku za mwisho shetani amewanyanyua maYesu wengi wa uongo, ambao na si Yule wa uzima.

2Wakorintho 11:3 “Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.

4 MAANA YEYE AJAYE AKIHUBIRI YESU MWINGINE AMBAYE SISI HATUKUMHUBIRI, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye!”

Yesu mwingine, (asiye KRISTO) anahubiriwa sasa na manabii na watumishi wa uongo, ambaye yeye hahitaji utakatifu.. ukiona unahubiriwa kwa jina la YESU lakini injili hiyo haikupeleki kuwa msafi mwilini na rohoni, badala yake unazidi kuwa wa kidunia, fikiri mara mbili ni Yesu gani uliyempokea, kwahiyo hatuna budi kujipima.

Lakini tukirudi kwenye swali!, Je huyu Yesu aitwaye Yusto alikuwa ni nani?..

Huyu Yesu aitwaye Yusto, alikuwa ni mmoja wa wafuasi wa Bwana wetu YESU KRISTO, ambaye alishirikiana na akina Paulo (watumishi wa MUNGU) kuhubiri injili, na alikuwa ni Myahudi (ndio maana Biblia inasema hapo alikuwa ni mtu wa tohara, maana yake aliyetahiriwa).

Maana ya jina Yusto ni “mwenye haki”.. na aliitwa “Yesu aitwaye Yusto”, kumtofautisha na YESU KRISTO. Huyu hakusimama kutaka aabudiwe, bali kinyume chake alikuwa anamhubiri YESU KRISTO.

Je umempokea Bwana YESU KRISTO?. Kama bado unasubiri nini?

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE BWANA YESU ALIMTOKEA YUDA BAADA YA KUFUFUKA KWAKE?.

MANENO SABA YA YESU MSALABANI.

YESU MNAZARETI,  ANWANI YA MSALABA.

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Print this post

Je YESU KRISTO alikuwa na wadogo zake?

Swali: Je YESU alikuwa na dada na kaka (ndugu wa kike na kiume), kama watu wengine?


Jibu: Ndio! Bwana wetu YESU KRISTO alikuwa na ndugu wengine wa kike na kiume, waliozaliwa na Mariamu mamaye!, maandiko yanathibitisha hilo katika Mathayo 13:55-56 na Marko 6:3.

Mathayo 13:54 “Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii?

55 Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? NA NDUGUZE SI YAKOBO, NA YUSUFU, NA SIMONI, NA YUDA?

56 NA MAUMBU YAKE WOTE HAWAPO HAPA PETU? Basi huyu amepata wapi haya yote?”

Kulikuwa na sababu ya kuanza na “Mwana wa seremala (Yusufu) na  kisha Mariamu mamaye na kumaliza na akina Yakobo, Yusufu, Simeoni na Yuda na maumbu (yaani wadada)”.. Ikimaanisha kuwa iliyokuwa inatajwa hapo ni familia, na si ukoo.

Ikimaanisha kuwa Marimu baada ya kumzaa Bwana YESU hakuendelea kuwa Bikira, bali alizaa watoto wengine pamoja na Yusufu mumewe, na watoto hao walikuwa wakike na kiume kama walivyotajwa hapo juu.

Ipo imani kuwa Mariamu hakuendelea kuzaa watoto wengine baada ya kumzaa Bwana YESU na kwamba watoto hao waliotajwa hawakuwa watoto waliozaliwa na Mariamu bali walikuwa ni ndugu wengine kama watoto wa mjomba, au baba mdogo ambao walikuwa karibu sana na Mariamu na Yusufu..

Hoja hii ni dhaifu na haina ukweli, kwani kusingekuwa na sababu ya MUNGU kuruhusu Mariamu achumbiwe na YUSUFU kama hawakuwa na mpango wowote wa kukutana na kuzaa watoto huko mbeleni,.. Malaika angeweza kumtokea Mariamu hata kabla hajachumbiwa, na hilo lingeweza labda kutufanya tuamini kuwa Mariamu aliendelea kuwa bikira mpaka anakufa!.

Lakini kitendo cha mpango wa MUNGU kuingilia kati wakati ambao tayari Mariamu kashachumbiwa, na kuonyesha kuwa hao tayari wamekusudiwa kuwa mume na mke na kuzaa watoto, na hata hivyo kipindi ambacho Yusufu amekusudia kumwacha Mariamu kwasababu ya ujauzito wake, bado kulikuwa na nafasi ya Malaika kumruhusu Yusufu amwache Mariamu, na kumruhusu akaoe mwanamke mwingine, ili Marimu abaki bikira maisha yake yote.

Lakini tunaona Yule Malaika hakumruhusu Yusufu amwache mkewe, ikifunua kuwa Yule ataendelea kuwa mke na ataendelea kutumika kama mwanamke mara baada ya kumzaa Bwana YESU.

Kwahiyo Bwana YESU alikuwa na ndugu wengine na Mariamu hakupaa, wala hakufa bikira, bali alikuwa na watoto wengine, na kati ya hao (yaani Yuda na Yakobo) ndio walioandika vitabu vya Yuda na Yakobo vya agano jipya katika Biblia.

Lakini pamoja na kuwa Bwana YESU alikuwa na ndugu wengine katika mwili, bado alisema kuwa ndugu zake hasa ni wale wayafanyayo mapenzi ya Baba yake.

Luka 8:19 “Wakamwendea mama yake na ndugu zake, wasiweze kumkaribia kwa sababu ya mkutano.

20 Akaletewa habari akiambiwa, Mama yako na ndugu zako wamesimama nje wakitaka kuonana nawe. 21 Akawajibu akasema, Mama yangu na ndugu zangu ndio hao walisikiao neno la Mungu na kulifanya”.

Je umempokea YESU?, Je Umefanyika kuwa ndugu yake Bwana kwa kulishika Neno lake na kulifanya?

YESU ANARUDI.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni halali kubatiza watoto wadogo?

HUYU SI YULE SEREMALA, MWANA WA MARIAMU?

Je! Tutatambuana tukifika mbinguni?

JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?

Ipi tofauti kati ya Sheria na kanuni kibiblia.

Print this post

Je hakukuwa na njia nyingine ya ukombozi zaidi ya kifo cha BWANA YESU?

Kwanini Mungu alichagua njia ya kifo cha msalaba kuwa njia ya ukombozi na si njia nyingine?, kwamba hakukuwa na njia nyingine ya ushindi? Amen.

Jibu: Ni kweli, MUNGU hakushindwa kutumia njia nyingine ya ukombozi wetu tofauti na hiyo ya kifo cha mwanawe wa pekee, kwani yeye ni MUNGU anayeweza mambo yote.

Lakini siri ya kwanini KIFO kitumike kama NJIA ya ukombozi wa dhambi ya mwanadamu ni matokeo ya dhambi za mwanadamu.

Bwana MUNGU alimwambia Adamu kabla ya kuasi kuwa pindi tu atakapokula matunda ya mti ule wa ujuzi wa mema na mabaya basi atakufa! (Mwanzo 2:17).. Hilo neno ATAKUFA!… Ndilo linalojibu swali letu, kwanini KRISTO afe ili kutukomboa sisi!.

Maandiko yanasema mshahara wa dhambi ni MAUTI! (Warumi 6:23).. Maana yake ili dhambi iweze kulipwa ni lazima MAUTI ihusike.. Kwahiyo KRISTO alipokuja ili aiondoe dhambi ya mwanadamu ilikuwa ni lazima alipe hilo deni!.

Hata mtu aliyepewa mkataba wa kazi, akiukatisha ule mkataba ni sharti alipe gharama za mkataba ule, na vivyo hivyo Kristo ili akatishe mkataba tuliongia sisi na dhambi, ni sharti alipe gharama za dhambi ambayo ni MAUTI.

Kwahiyo alikikubali kifo ili dhambi iondoke kwetu, na hakukuwa na njia nyingine ya mbadala ya kuondoa dhambi!.

Je umempokea YESU kama BWANA na MWOKOZI wa maisha yako?

Kama bado hufajanya hivyo, ni heri ukafanya hivyo sasa, kwa maana hizi ni siku na ule mlango wa rehema unakaribia kufungwa.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Fahamu maana ya 2 Wakorintho 8:9 alikuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.

MANENO SABA YA YESU MSALABANI.

YESU MNAZARETI,  ANWANI YA MSALABA.

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

JE UTAKATIFU NI MATENDO YA SHERIA?

Print this post

Nini maana ya Selahamalekothi?

Ilikuwa ni desturi ya wayahudi kuyapa majina, maeneo yote ambayo walikutana na Mungu kipekee.

Kwamfano Yakobo alipokutana na Mungu mahali fulani palipoitwa Luzu, kwa kuona maono yale ya ngazi kushuka kutoka mbinguni, na malaika wanashuka na kukwea, hakuondoka hivi hivi bali alipaita mahali pale Betheli yaani ‘ nyumba ya Mungu’ (Mwanzo 28:10-22).

Sehemu nyingine Mungu alipowasaidia Israeli kuwapiga wafilisti kwa kishindo kikubwa, Samweli alilisimamisha jiwe na kuliita Eneb-ezeri akimaanisha ‘hata sasa Bwana ametusaidia’ na 1Samweli 7:12.

Hivyo pia tukisoma kisa cha Mfalme Sauli na Daudi, tunaona mara nyingi Daudi alipowindwa ili auawe alifanikiwa kumtoroka Sauli, lakini upo wakati ambao alihusuriwa pande zote, Daudi akawa hana namna isipokuwa kungojea tu kuuliwa palepale pangoni, sasa wakati ambapo Sauli amemkaribia sana Daudi. Taarifa za ghafla zilimfikia na kuambiwa kwamba wafilisti wamevamia Israeli, hivyo ikambidi aache kumfuatilia Daudi arudi Israeli kupambana na adui zake.

Sasa tendo hilo la wokovu halikumwacha Daudi awe vilevile kinyume chake, alipaita mahali pale Selahamalekothi

1 Samweli 23:26-28

[26]Sauli akaenda upande huu wa mlima, na Daudi na watu wake wakaenda upande huu wa mlima; naye Daudi akafanya haraka sana kwenda zake kwa hofu ya Sauli; kwa sababu Sauli na watu wake wakamzunguka Daudi na watu wake ili kuwakamata.

[27]Lakini akaja mjumbe kwa Sauli, kusema, Njoo upesi, kwa kuwa Wafilisti wameishambulia nchi.

[28]Basi Sauli akarudi kutoka kumwinda Daudi, akaenda kinyume cha Wafilisti; kwa hiyo wakapaita mahali pale, Selahamalekothi.

Selahamalekothi ni neno la kiebrania lenye maana ya MWAMBA WA KUTOROKEA.

Daudi na watu wake walipaita mahali pale hivyo kufuatana ba jinsi Mungu alivyowaepusha na mkono wa Sauli, kwa njia isiyodhaniwa/ kutegemewa hata kidogo.

Ni kwanini wayaite majina maeneo hayo?

Ni Ili kuendelea kukumbuka matendo makuu Mungu aliyowatendea wasizisahau wafidhili zake kabisa.

Je na sisi ni alama gani tunaacha mahali ambapo tunamwona Mungu ametutendea makuu. PENDA kuandika shuhuda zako, ili wakati ujao zikusaidie kukumbuka fadhili za Mungu umshukuru.

Kikawaida Mungu huwa anatufanyia maajabu mengi Sana kila siku, lakini tunakuwa wepesi kuyasahu, ni vema tujifunze kwa namna yoyote kutunza kumbukumbu, hata kama si kwa kuandika lakini kwa njia zozote zile, mfano wa mababa zetu hawa.

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Pango la Makpela ni lipi, je lina umuhimu wowote kwetu?

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

SIKU YA HOFU YANGU NITAKUTUMAINI WEWE.

Print this post

“Hakuna aniulizaye unakwenda wapi”, maana yake nini? (Yohana 16:5).

Swali: Bwana YESU aliposema kuwa “wala hakuna mmoja wenu aniulizaye unakwenda wapi” alimaanisha nini? (Yohana 16:5)?


Jibu: Turejee..

Yohana 16:5 “Lakini sasa mimi naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka, WALA HAKUNA MMOJA WENU ANIULIZAYE, UNAKWENDAPI?

6 Ila kwa sababu nimewaambia hayo HUZUNI IMEJAA MIOYONI MWENU”.

Maneno haya Bwana YESU aliwaambia wanafunzi wake usiku ule mmoja kabla ya kusulibiwa kwake kwamba umefika wakati wa yeye kuondoka na kuwaacha….Na kwasababu ni maneno ya kuhuzunisha, wanafunzi wake waliingiwa na hisia kiasi cha kushindwa hata kumwuliza anakokwenda.

Si kwamba walikuwa hawataki kujua Bwana anakokwenda, La! Walikuwa wanatamani sana…lakini ile hali tu ya kufikiri kumwuliza hivyo haikuwa katika vichwa vyao kwa wakati ule, kwani walikuwa wanatafakari zaidi ni nini kitaendelea kwao baada ya Bwana kuondoka!.. Hivyo hiyo ikazuia hata kufikiri kumwuliza anakokwenda!.

Naam hata taarifa  za mtu kufariki zinapowafikia wafiwa, ni wafiwa wachache sana wanaweza kufikiri Yule mtu ameenda wapi, wengi wanaishia kuhuzunika na kufikiri maisha ya upweke watakayokumbana nayo baada ya hapo kwa kumkosa Yule mtu katika kipindi chote cha maisha yao!.

Ndivyo ilivyokuwa kwa wanafunzi wa YESU, hisia zilifunika tafakari ndani yao, na Kristo aliliona hilo, ndipo akawaambia yale maneno kwamba yafaa yeye aondoke ili msaidizi aje (yaani Roho Mtakatifu), nao watapokea nguvu mpya.

Yohana 16:6 “Ila kwa sababu nimewaambia hayo huzuni imejaa mioyoni mwenu.

7 Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu”.

Na wakati ulipofika wa Roho Mtakatifu kushuka juu yao, wote walipokea nguvu kana kwamba BWANA YESU mwenyewe katika mwili anatembea nao, huzuni na unyonge wote ulipotea na badala yake ujasiri na nguvu viliingia ndani yao.

Je na wewe umempokea Roho Mtakatifu?.. kama bado basi mwamini Bwana YESU, na tubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha kisha tafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38, na Bwana atakupa kipawa hiko.

Matendo 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VIASHIRIA VINGINE VYA ROHO MTAKATIFU KUWEPO NDANI YAKO.

KUWA NA  MAFUTA YOTE YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO.

ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?

Print this post