Biblia inamaana gani inaposema “Mungu wa neema yote”
1 Petro 5:10
[10]Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu.
Tafsiri ya Neema ni kukubaliwa kusikostahili.. au upendeleo usio na sababu. Kwamfano pale mtu anapomwajiri mtu asiye na ujuzi kisha akampa nafasi au mshahara mkubwa wa kiwango cha sawasawa na yule mwenye elimu nyingi na uzoefu..hiyo tunaiita neema.
Hivyo katika ukristo msingi mkuu wa wokovu wetu unategemea neema ambayo ililetwa na Bwana wetu Yesu Kristo(Yohana 1:17).
Yaani Tunakubaliwa na Mungu kuwa sisi tumestahili kuingia katika ufalme wa Mungu na kuwa watoto wake, kwa kumwamini tu Yesu Kristo bila kutegemea matendo yetu wenyewe kama kigezo cha sisi kufikia kiwango hicho.
Neema hiyo hujulikana kama neema ya wokovu. Ambayo ndio neema kuu, iliyomfanya Kristo aje duniani kufa kwa ajili yetu kama fidia ya dhambi ili sisi tuitwe waliostahili. (Waefeso 2:8-9)
Lakini pamoja na hayo Mungu hana mipaka kwamba anatoa neema ya aina moja tu yaani ya wokovu peke yake…hapana anazo Neema nyingi, ambazo zinaingia katika nyanja mbalimbali za maisha ya mwanadamu.
Sehemu nyingine katika biblia huitwa. Neema juu ya neema..
Yohana 1:16
[16]Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema.
Neema hii unamwezesha mtu, kuwa na matokeo katika Huduma na ustahimilivu wote. Ndiyo ambayo Paulo na Barnaba walipewa, iliyowafanya waweze kukichukua kijiti cha injili na kufanikiwa kukipeleka kwa mataifa.
Matendo ya Mitume 13:2
[2]Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.
Mbeleni utaona maandiko yanasema..
Matendo ya Mitume 14:26
[26]Na kutoka huko wakaabiri kwenda Antiokia. Huko ndiko walikoombewa neema ya Mungu kwa ile kazi waliyokwisha kuitimiza.
Hivyo wewe kama mtakatifu ukitaka mafanikio katika huduma au karama yako. Kujifunza kuomba neema ya Mungu katika huduma ni liwe ni sehemu ya maisha yako. Kwasababu hiyo Ipo kukusaidia…Na utapata matokeo ambayo hayategemei zaidi nguvu zako. Ndicho walichokuwa wanakiomba sana mitume.
Matendo ya Mitume 15:40
[40]Lakini Paulo akamchagua Sila, akaondoka, akiombewa na wale ndugu apewe neema ya Bwana. Neema ya kupokea vitu.
2 Wakorintho 9:8
[8]Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;
Kumbukumbu la Torati 8:18
[18]Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.
Hata kupata vitu kiwepesi, hasaa hutegemea neema ya Mungu, kama mkristo ni lazima ujifunze kumwomba Mungu neema ya kufanikishwa, katika mambo yako yote ya kimaisha, isizitegemee tu nguvu zako au akili zako, hata kama jambo ni jepesi vipi, ikiwa ni kazi Omba Mungu akupe neema ya mafanikio, ikiwa ni biashara omba Akupe neema ya kupata Faida Zaidi, ikiwa ni elimu omba Mungu akuongezee akili zaidi.
Zaburi 68:9
[9]Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema; Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu.
Ni sifa ya Mungu kauchilia neema yake kwa watu wake pale wanapochoka huwatia nguvu mpya, wao wenyewe wanashangaa wanainuka tena na kuendelea mbele.. Ndio maana tunasema Mtu anayedumu katika wokovu maisha yake yote, hata anapopitia katika tufani, Pepo na mawimbi, bado hatetereki.. Ni neema ya Kristo inakuwa imehusika hapo kumvusha, si nguvu Zake.
Jifunze kuiomba hii namna ya neema.
Matendo ya Mitume 6:8
[8]Na Stefano, akijaa neema na uwezo, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa katika watu.
Karama za Roho, mfano miujiza, uponyaji, lugha, unabii, utume, uchungaji, n.k, ni vipawa ambavyo hutolewa bure na Roho Mtakatifu, Hakuna jitihada Yoyote ambayo mtu atafanya aweze kukunua nguvu za kumfufua mfu, au kuona mambo ya mbeleni Ayatolee unabii, au kuundoa Ukimwi kwenye damu Ya mtu, isipokuwa kwa neema za Mungu, kutembea na yeye.
Ni neema ambayo tunapaswa tuiombe, ambayo inamfanya Mungu aachilie mafuta mengi ndani yako ya kutembea katika vipawa hivyo, ili kulijenga kanisa.
1 Petro 4:10
[10]kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu.
2 Wakorintho 1:12
[12]Kwa maana kujisifu kwetu ni huku, ushuhuda wa dhamiri yetu, ya kwamba kwa utakatifu na weupe wa moyo utokao kwa Mungu; si kwa hekima ya mwili, bali kwa neema ya Mungu; tulienenda katika dunia, na hasa kwenu ninyi.
Inategemea nguvu ya Mungu (neema), kutembea katika hali ya kutimiza mapenzi yote ya Mungu katika utakatifu… maana yake ni kuwa mwanadamu Akijifunza kumpa Nafasi Roho Mtakatifu ndani yake. Atajaliwa kuishi Maisha yote yampendezayo Mungu, sawasawa na Wagalatia 5:16
2 Wakorintho 8:1-3
[1]Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia;
[2]maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na umaskini wao uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao.
[3]Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao;
Hii ni uwezo wa kutoa vitu/ maisha/ chochote kwa wengine bila kujali nafsi yako mwenyewe.
Jifunze kumwomba Mungu neema ya utoaji. inafaida kubwa sana kwa wengine, kwa binafsi lakini pia katika kukua kwa ufalme wa Mungu.
2 Wakorintho 8:9
[9]Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.
1 Petro 1:13
[13]Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.
Yapo mambo Mengi mema tusiyoyajua, ambayo tutapewa tukifika kule ng’ambo Kristo atakaporudi.. ni mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia, biblia imehitimisha kwa kuyaita “neema”
Je Umepokea neema zote? Lakini zaidi ya yote neema ya wokovu?. Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari leo Yesu akusamehe dhambi zako, basi tawasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya chapisho hili upate msaada huo.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NI MAJIRA YAPI YA NEEMA WEWE UPO?
TAHADHARI YA NEEMA YA MUNGU.
UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?
Waefeso 6:16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu
Waefeso sura ya 6, inaeleza mapambano ambayo yapo rohoni kati ya sisi na ufalme wa giza, na namna ambavyo tunapaswa tusimame kushinda vita hivyo, kwa kuvaa zile silaha zote za haki zinazotajwa pale. Kama vile chapeo ya wokovu, dirii ya haki, kweli kiunoni, upanga wa Roho, na ngao ya Imani,.
Lakini pia katika vifungu hivyo tunaelezwa mojawapo ya silaha ya adui, nayo ni “mishale ya moto”. Swali Je hii mishale ya moto ni ipi?
Mishale ni silaha zilizotumika zamani, za kumshambulia adui kwa mbali, na hivyo ili kuziboresha waliweka moto kwa mbele ili zitakapomfikia adui basi zilete madhara zaidi ya yale tu ya kutoboa, bali kuunguza kama sio kumuharibu kabisa adui.
Tofauti na silaha kama rungu, au upanga ambavyo vinahitaji uso kwa uso kutumika. Kwa mbali havina matokeo.
Tukirudi katika ulimwengu wa sasa mishale ya vita ni makombora, Kwanini hapo shetani anaonekana akirusha mishale kutokea mbali? Ni kwasababu kwa karibu hamwezi mwamini, kwani nguvu zilizo ndani yake ni nyingi kuliko alizonazo.
Shetani hutumia sana ulimi kuleta, aidha udanganyifu, mafarakano, vita n.k. Ndio maana maandiko yanasema;
Yakobo 3:5 Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.
6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum.
7 Maana kila aina ya wanyama, na ya ndege, na ya vitambaavyo, na ya vitu vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha kufugwa na wanadamu.
8 Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.
9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu.
10 Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo.
Hawa alidanganywa na Nyoka kwa ulimi, Mafundisho ya uongo, huanzia katika maneno. Hivyo sisi kama watoto wa Mungu ni lazima tuijue silaha hii na kuidhibiti kwanza sisi wenyewe ndani yetu, kuhakikisha hatutumiki kama warusha mishale, kwa kusema yasiyopasa, lakini pia kusimama kwa imani kuhakikisha, tunakuwa thabiti kiimani, kwa kupuuzia, au kutokuweka moyoni kila Neno linalosemwa kinyume chetu, sambamba na kuwa makini kwa kupima kila neno tunaloambiwa kama kweli ni la Mungu au la!.
Mkristo usipojua silaha hii ya adui, utajikuta kila kukicha unaishi kwa machungu ya maneno ya watu, huna raha, una mashindano, au utajikuta unaanguka katika mikono ya manabii wa uongo, na hatimaye shetani anakuwa amekupata.
1Petro 4:12 Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.
13 Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.
14 Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia
Majaribu yote hutoka kwa Yule mwovu, lengo lake ni kumwangusha mwamini ili amwasi Mungu, hata wakati ule Bwana Yesu anakaribia kusulubiwa, alimwombea Petro ili imani yake isitindike, kwasababu alijua wataingia kwenye majaribu makubwa, kwa upungufu wa maombi yao. Vivyo na sisi yatupaswa tuwe waombaji ili tuizime mishale ya majaribu mbalimbali ya adui tusiyojua pembe ipi yanatokea. Na pia tunapojikuta ndani ya hayo majaribu, yatupasa kuishikilia imani yetu hasaa, kwa kuamini kuwa Bwana yupo pamoja nasi kutengeneza njia ya kutokea.
Shetani akijua kuwa hana nguvu ya kumshinda mwamini moja kwa moja, hivyo hupenda kuinua ujasiri wake kama silaha, na akiwa mbali anajua akirusha mishale yake kisha Yule mtu akiiogopa basi anamwangusha. Ndio hapo huleta vitisho, mfano wa kipindi kile cha wana wa Israeli walipopewa agizo la kwenda kumjengea Mungu nyumba Yerusalemu, tunasoma baada ya kipindi kifupi maadui zao wakainuka, na kuwasemelea kwa mfalme, hatimaye marufuku ikatoka, wasiendeleze ujenzi, hivyo mahali pa Mungu pakabaki gofu tu la msingi kwa muda mrefu, kisa hofu ya utalawa mpya. Lakini baada ya muda mwingi sana, tunaona Mungu akawaamsha mioyo Hagai pamoja na Zekaria, na kuwaambia Israeli kwanini wameacha kuijenga nyumba ya Bwana. (Hagai 1:1-9), walipogundua makosa yao, kwa kuruhusu hofu, Ndipo walipoamka kwa ujasiri tena na kuijenga, Mungu akawafanikisha sana.
Vivyo hivyo na sisi, tumepewa agizo la kuhubiri injili, ikiwa itapingwa, au tutatishiwa kuuawa au kufungwa, ikiwa tutapitishwa kwenye miiba au miamba hatupaswi kuogopa mishale hiyo, bali tusimame kwa imani kama akina Shedraki na Danieli, wakiwa katika matanuru ya moto, na matundu ya simba hawakutetereka. Bali walimtumaini Mungu anayewaokoa, na hatimaye kweli ikawa vile.
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba ipo kweli mishale mingi ya moto, ya adui lakini hiyo mitatu ndio mikuu. Na tukiweza kusimama kwa imani basi shetani pande zote anakuwa ameshindwa kabisa kabisa, (Akiwa karibu na vilevile akiwa mbali) linda kinywa chako /puuzia/ pima maneno unayoyasikia, vilevile kuwa mwombaji ili usiingie majaribuni/ uyashinde majaribu, Lakini zaidi sana kamwe usiogope vitisho vya adui, kwasababu hawezi kufanya lolote kwa ihari yake mwenyewe.
Mungu akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi
Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?
Kamwe usifundishe kitu ambacho wewe mwenyewe hukitendi.. Usiwafundishe wengine kumcha MUNGU ilihali wewe mwenyewe uko mbali na MUNGU!.. Usiwafundishe wengine umuhimu wa kuomba ilihali wewe mwenyewe hufanyi hivyo..
Kuna madhara makubwa ya kuwafundisha watu kitu ambacho wewe mwenyewe hukifanyi au hukiwezi.. Katika Biblia walikuwepo Mafarisayo ambao walikuwa wanawatwika watu mizigo ambao wao wenyewe hawakuiweza..
Mathayo 23:2 “Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa;
3 basi, yo yote watakayowaambia, myashike na kuyatenda; lakini kwa mfano wa matendo yao, msitende; maana wao hunena lakini hawatendi.
4 Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao”.
Na tena kitabu cha Warumi kinazidi kuliweka hilo vizuri zaidi…
Warumi 2:21 “basi wewe umfundishaye mwingine, je! Hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, waiba mwenyewe?
22 Wewe usemaye kwamba mtu asizini, wazini mwenyewe? Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?
23 Wewe ujisifuye katika torati, wamvunjia Mungu heshima kwa kuiasi torati?
24 Kwa maana jina la Mungu latukanwa katika Mataifa kwa ajili yenu, kama ilivyoandikwa”.
Mitume wa Agano jipya pamoja na Manabii wa agano la kale, hawakuwahubiria watu vitu wasivyoviishi wao, bali waliwafundisha watu yale wanayoyaishi ili wawe vielelezo..
Ezra 7:10 “Kwa maana huyo Ezra alikuwa ameuelekeza moyo wake KUITAFUTA sheria ya Bwana, na KUITENDA, na KUFUNDISHA maagizo na hukumu katika Israeli”.
Hapa Ezra kwanza alianza kwa KUITAFUTA sheria ya Bwana, na AKAITENDA na ndipo AKAWAFUNDISHA wengine.. Ni lazima na sisi tupitie hizi hatua tatu; KUTAFUTA, KUTENDA na KUFUNDISHA.
Tukiiruka ile ya kwanza na ya pili na kuifanya hiyo ya Tatu ya kufundisha, hatutakuwa mashahidi wazuri, na wala ushuhuda wetu hautakuwa na nguvu, tutakuwa ni mashabiki wa injili na si wahubiri wa Injili.. Injili inahubiriwa kwanza katika matendo ndipo mafundisho, hatuwezi kufundisha tusichokitenda!, hapo tutakuwa waongo, au watu wa kutafuta faida zetu.
Bwana YESU atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MWOMBENI BWANA WA MAVUNO APELEKE WATENDA KAZI.
TENDA AGIZO LA YESU, HILO NDIO LITAKALOKULINDA.
MATENDO YETU YANAPIMWA KATIKA MIZANI.
Mtande ni nini? Ni funzo gani lipo nyuma yake?
Utakuwa Kichwa na si Mkia maana yake nini? (Kumbukumbu 28:13).
Jibu: Turejee Matendo
Matendo 16:6 “Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, WAKIKATAZWA NA ROHO MTAKATIFU, WASILIHUBIRI LILE NENO KATIKA ASIA.
7 Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa,
8 wakapita Misia wakatelemkia Troa”.
Biblia haijataja sababu za moja kwa moja kwanini Roho Mtakatifu awazuie wasiingie Asia kuhubiri injili lakini zifuatazo zinaweza kuwa sababu za Roho Mtakatifu kuwazuia Paulo na wenzake wasiingie hiyo miji kuhubiri injili.
1. WAKATI WA INJILI KWA HIYO MIJI ULIKUWA HAUJAFIKA.
Kila mahali pana wakati wake wa kuhubiri injili kulingana na mapenzi ya Mungu, kwamfano kuna wakati ambao injili ilikuwa haijaruhusiwa kuhubiriwa kwa watu wa mataifa isipokuwa wayahudi tu peke yao, na kipindi hiko ni kile ambacho Bwana YESU alikuwa yupo bado duniani.
Mathayo 10:5 “Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akawaagiza, akisema, Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie.
6 Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
7 Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia”.
Maneno hayo ya Bwana Yesu yanaonyesha kuwa wakati wa injili kwa watu wa mataifa ulikuwa haujafika, lakini haikumaanisha kuwa Mataifa hawakuwa katika mpango wa Mungu wa kupokea Injili, walikuwepo lakini muda wao ulikuwa bado haujafika.
Na hapa katika Asia ni hivyo hivyo, huwenda muda wao wa kufikishiwa injili ulikuwa bado.
2. WATUMISHI WENGINE WALIKUWEPO WAKIHUBIRI INJILI.
Kama muda wao wa kupokea Injili ulikuwa umefika na bado Roho Mtakatifu akawazuia akina Paulo kufika miji hiyo, sababu nyingine ni kwamba labda walikuwepo watumishi wengine wakihubiri katika hiyo miji, hivyo hakukuwa na haja ya akina Paulo kwenda huko tena wasije wakajenga juu ya msingi wa wengine kama Neno la Mungu linavyosema katika Warumi 15:20.
Warumi 15:20 “kadhalika nikijitahidi kuihubiri Injili, nisihubiri hapo ambapo jina la Kristo limekwisha kutajwa, nisije nikajenga juu ya msingi wa mtu mwingine”
3. WATUMISHI WENGINE WAMEKUSUDIWA KWENDA KUHUBIRI KATIKA HIYO MIJI.
Na kama hakukuwa na watumishi wengine waliokuwa wanahubiri katika miji hiyo, basi sababu nyingine ya Roho Mtakatifu kumzuia Paulo na wenzake kufika huko Asia huwenda ni kwasababu Roho Mtakatifu alikuwa amepanga/kusudia watumishi wengine ndio wakahubiri kwenye hiyo miji mbali na Paulo na wenzake.
Kikawaida Roho Mtakatifu ndiye anayepanga watu na mahali watakapokwenda..Paulo asingeweza kwenda miji yote peke yake, ni wazi kuwa ipo miji mingine ilikusudiwa kupelekewa injili na watumishi wengine/mitume.
4. WALIIKATAA INJILI.
Hii yaweza kuwa sababu ya mwisho ya Roho Mtakatifu kuzuia injili isiingie Asia kupitia Paulo na wenzake… Inawezekana Roho Mtakatifu alishatanguliza watu huko waliohubiri Neno la Mungu lakini wakaikataa ile injili.. na matokeo yake ni kufungiwa dhambi sawasawa na Yohana 20:22-23..
Yohana 20:22 “Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.
23 Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa”.
Kufungiwa dhambi kunakuja pale ambapo Neno la Mungu linahubiriwa kwa watu na wale watu wanalikataa kwa makusudi na hata kuwaua au kuwafukuza watumishi wa MUNGU, inapotokea wale watumishi wanakung’uta mavumbi kwenye miguu yao na kuondoka hapo wanakuwa wameufungia dhambi ule mji au mtaa, matokeo yake ni kwamba Roho Mtakatifu hawezi tena kupeleka wahubiri hapo mahali, wale watu watabaki vile vile kwasababu walishamkataa Roho Mtakatifu.
Mathayo 10:14 “Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, KUNG’UTENI MAVUMBI YA MIGUUNI MWENU.
15 Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule”.
Tunachoweza kujifunza ni kuwa Injili sio kitu kinachoweza kupatikana kila wakati, upo wakati ambapo Neema ikishaondoka mahali hairudi, au hata ikirudi yaweza kuchukua muda sana, hivyo hatuna budi kuiheshimu sana Neema ya Mungu.
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je Paulo, alihimiza kusikiliza nyimbo za kidunia kulingana na Matendo 17:28
Paulo aliwapaje watu karama ya rohoni?
Je ni sawa kuukubali udhaifu kama mtume Paulo alivyojisifia kwa huo? (2Wakorintho 12:9-10)
Kwanini Paulo, alihukumu wakati hukumu hairuhusiwi?
Paulo alikuwa anamaanisha nini kusema “Mnatenda vema kuvumiliana naye” (2Wakorintho 11:4).
SWALI: Biblia inasema maziwa ni kwa watoto wachanga, lakini chakula kigumu ni cha watu wazima. Mfano wa chakula hichi kigumu ni kipi?
Waebrania 5:12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu. 13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga. 14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya
JIBU:
Kabla ya kufahamu hicho chakula kigumu, ni vema kujua kwanza maziwa ni yapi.
Hivyo ukiendelea kusoma vifungu vinavyofuata anasema..
Waebrania 6:1 Kwa sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu, 2 na wa mafundisho ya mabatizo, na kuwekea mikono, na kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele. 3 Na hayo tutafanya Mungu akitujalia.
Sasa hayo mafundisho ya kwanza ya Kristo ndio maziwa. Yaani Mafundisho ya toba, imani kwa Mungu, ubatizo, kuwekewa mikono, kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele ni mafundisho ya watoto wachanga..kiroho hujulikana kama maziwa..
Kimsingi mtoto akiendelea kunywa maziwa tu peke yake daima, kitakachotokea baadaye ni kudumaa kama sio kufa kabisa, hivyo itafika wakati tu atahitaji chakula kingine ili aendelee kuishi. Vivyo hivyo na sisi, vipo vyakula ambavyo tunapaswa tule, kwa jinsi tunavyoendelea kukua kiroho.
Vifuavyo ndio vyakula vigumu vya kiroho vya watu wazima:
Mathayo 5:44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
Kwanini ni chakula kigumu?. Kwasababu jambo hilo linaenda kinyume na asili ya mwanadamu, linafunua asili ya ndani kabisa ya Kristo, ambayo si rahisi mtu aliyemchanga kiroho, kuielewa, au kulipokea nyakati za mwanzoni, yaani kumwombea na kumpenda Yule ambaye anaiwinda roho yake au aliyemjeruhi, ..
Wafilipi 1:29 Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;
Kwanini ni chakula kigumu?. Kwasababu mwamini mchanga, mara nyingi atapenda kuambiwa maneno ya faraja, baraka, na mafanikio, awapo kwa Kristo, lakini mkristo aliyekomaa, anayaona mapenzi ya Mungu pia hata katika majaribu na kuyashangalia.
1Wathesalonike 3:3 mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo
Soma pia 1Petro 1:6-8, 4:13, Wakolosai 1:24, Luka 6:22-23
Waebrania 5:14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya
Mkristo aliyekomaa kiroho, anafundishwa na Mungu kutambua na kugawanya vema mambo yote, kujua vilivyo najisi na visivyo najisi, mafundisho ya kweli na yale ya uongo, anafundishwa, busara, ujuzi na hekima hata katika kuhubiri injili kwa makundi yote, bila kuanguka na kunajisika, kwasababu amepewa roho ya upambanuzi ambayo huja kwa kuzoeshwa na Mungu kwa kipindi Fulani cha muda kupitia Neno lake.
1Wakorintho 9:20 Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria.
21 Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria. 22 Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.
Soma pia, 1Wakorintho 8:6-13, Yohana 2:1-12, Mathayo 11:19.
Kwanini ni chakula kigumu? Kwasababu mtu ambaye ni mchanga kiroho, akijihusisha katika viwango hivyo, hupotea na kunajisika kama sio kupotea kabisa. Ndicho kilichowatokea Adamu na Hawa kuuvamia mtu wa ujuzi wa mema na mabaya nje ya ratiba ya Mungu, matokeo yake wakayavuna mabaya, wala sio mema.
Katika wokovu ipo fimbo ya Mungu; Mzazi yoyote huwa hatoi zawadi tu, sikuzote, hacheki na mwanawe siku zote, lakini pia kuna wakati fimbo hutumika, Vivyo hivyo Mungu ni Baba yetu, huadhibu, pale tunapokosea..
Waebrania 12:11 Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.
Kwanini ni kigumu? Kukubali marekebisho kwa kuadhibiwa kama sehemu ya kutengenezwa na Mungu, si jambo rahisi mtu kulikubali mkristo ambaye hajakomaa. Yeye atakachojua tu, kuwa Mungu ni upendo.
Luka 9:23 Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.
Kwanini ni chakula kigumu? Aliye mchanga kiroho kukubali kukataa mapenzi , kuingia gharama kuacha vyote na kuyakubali ya Mungu tu, si jambo rahisi kwa mwanafunzi wa ngazi ya chini.
Wafilipi 2:3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.
4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;
8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba
Kwanini ni chakula kigumu?.
Mkristo mchanga kiroho, si rahisi kuangalia mambo ya wengine, mfano wa Kristo, si rahisi kujinyenyekeza na kukubali kutembea kama mtumwa ili kuwatumikia wengine.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Maisha Mapya ya wokovu yanasukumwa na maombi. Kama Neno ni chakula, basi maombi ni maji. Vilevile huwezi tenganisha maisha ya wokovu na uombaji.
Ni tendo la kuongea na Mungu, lakini pia kumsikia. Maombi sio maneno matupu tu, au utaratibu wa kidini, bali ni mahusiano halisi kati ya sisi na Mungu.
Yeremia 33:3
[3]Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.
Maandiko hayatoi ukomo wa maombi. Zaidi sana yanasisitiza tuombe kila wakati na bila kukoma.
1Wathesalonike 5:17 ombeni bila kukoma;
Waefeso 6:18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;
Hivyo Maombi ni tendo endelevu la wakati wote.
Mathayo 26:41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.
Luka 3:21 Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu
zilifunuka
Mathayo 17:20 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.
21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]
Wafilipi 4:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Zipo aina mbalimbali za maombi, ili kufahamu kwa kina bofya hapa >> KUNA AINA NGAPI ZA MAOMBI?
Ramani kuu ya maombi tulishafundishwa na Bwana Yesu Kristo. Ambayo ndio ile Sala, ijulikanayo kama “Sala ya Bwana”. Hivyo kufahamu namna ya kuiomba fungua hapa >>>> Namna bora ya kuiomba sala ya Bwana
Miongozo mingine itakayokusaidia kutanua upeo wako wa uombaji kwa lengo la ukuaji wa kiroho Bofya hapa >>> MWONGOZO WA MAOMBI YA KUJIKUZA KIROHO.
Haya ni mafundisho, mengine yatakayokusaidia kujua kwa undani kuhusu maombi;
Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?
MWONGOZO WA MAOMBI YA ASUBUHI.
JINSI YA KUVURUGA MIPANGO YA MUNGU.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Ahadi ya Roho Mtakatifu ni ya kila mwamini. (Matendo 2:39). Ni msaidizi ambaye Mungu alitupa ili kutuwezesha kuishi maisha ya wokovu kwa viwango vya ki-Mungu hapa duniani.
Hivyo siku ile ulipomkubali Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yako. Tayari ulipokea Roho Mtakatifu siku hiyo hiyo.
Isipokuwa Huwezi ukahisi chochote ndani, bali kwa jinsi unavyoendelea kutii kwa kumfuata Bwana utaziona tu kazi zake ndani yako.
Na hizi ndio kazi zake kuu azifanyazo Roho Mtakatifu anapokaa ndani ya mtu;
Yohana 16:13
[13]Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.
Yohana 14:26
[26]Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
Warumi 8:26 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
Wagalatia 5:16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana
hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
Hivyo humfanya aendelee kuishi maisha ya utakatifu (Yohana 16:8)
Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu
1Wakorintho 12:7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.
8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo
Roho yeye yule;
9 mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule
mmoja;
10 na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho;
mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha;
11 lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake
kama apendavyo yeye
Matendo 1:8
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi
wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
Hivyo faida zote hizi hudhihirika ndani ya mtu kwa wingi , hutegemea jinsi mtu huyo anavyompa Roho Mtakatifu nafasi ndani yake. Ndio maana ni vema wewe kama mwamini mpya ujue mambo haya ili usije ukajikuta unamzimisha Roho Mtakatifu ndani yako. Ukawa unaisha maisha ya kama mtu ambaye hajaokoka.
Moja ya agizo la Bwana Yesu kwetu sisi, ni kwamba “tujikane nafsi”. Kujikana maana yake ni kuyatakataa matakwa yetu wenyewe ya mwilini na kukubali yale ya Mungu tu. Ulikuwa mlevi unakuwa tayari kukaa mbali na ulevi, ulikuwa ni kahaba unauaga ukahaba wako. n.k.
Kuwekewa mikono kunanyanyua mafuta Ya Roho Mtakatifu ndani ya mtu kwa namna nyingine. Na matokeo yake ni kuwa unaambukizwa pia neema.. Katika maandiko tunaona wapo watu kadha wa kadha waliojazwa Roho kwa namna hii. (Matendo 8:17, Matendo 19:6 , 2 Timotheo 1:6 )
Kiwango cha chini ambacho Bwana alituagiza ni SAA moja. Zaidi Pia katika maombi yako mwambie Bwana nijalie kuomba kwa Roho ( kwa kunena kwa lugha) ikiwa bado kipawa hichi hakijakushukia, Ni muhimu pia.
Zingatia: Katika uombaji wako,jifunze kutoa sauti, pia jiachie mbele zake. Huwezi kunena kwa lugha moyoni.. ni lazima kinywa kihusike hivyo Jifunze kuomba huku kinywa chako kikitoa maneno kabisa. Hiyo ni nidhamu nzuri katika hatua za ujazwaji Roho.
Tunajazwa Roho Kwa kuitambua sauti yake inatuagiza nini. Na sauti yake ni biblia. mahali Pekee penye uwepo wote wa Mungu ni kwenye Neno lake.
Hivyo zingatia sana hilo. Mkristo ambaye hasomi NENO, kamwe hatakaa aweze kumsikia wala kumwelewa Roho Mtakatifu.
Ukizingatia hayo basi, utaona uzuri wa Roho Mtakatifu ndani yako.
Mafundisho ya ziada kuhusu Roho Mtakatifu
YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO.
NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?
JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.
Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni ipi?
NAMNA YA KUNENA KWA LUGHA MPYA
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Nehemia 8:10 “Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU”.
Hapa anaposema “Furaha ya Bwana ni Nguvu zetu” hamaanishi “kufurahi kwa Bwana ndio Nguvu zetu”, hapana bali anamaanisha “Furaha yetu sisi katika Bwana ndiyo Nguvu yetu”.. Maana yake tunapofurahi tukiwa ndani ya MUNGU hiyo ni Nguvu kwetu..
Neno la Mungu linasema katika 1Wathesalonike 5:16 na Wafilipi 4:4 kuwa tufurahi siku zote katika Bwana..
Wafilipi 4:4 “Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini”
Furaha ya Bwana inapokuwa ndani yetu, ndivyo tunazidi kupata NGUVU za mambo yote.. Sasa tunaivutaje Furaha ya MUNGU ndani yetu?..Kwa mambo haya sita (06), furaha ya Mungu itaingia ndani yetu.
1. KUOKOKA
Mwimbaji mmoja wa Tenzi no. 22, (wimbo; Kale nilitembea) alisema hivi katika ubeti mmoja …
“ Hicho ndicho chanzo cha kufurahi kwangu, hapo ndipo mzigo uliponitulia…
usifiwe msalaba, lisifiwe kaburi linalozidi yote, asifiwe Mwokozi”.
Akimaanisha Msalaba ndio chanzo cha kwanza cha Furaha yake, na hiyo ni kweli kabisa.. Mtu aliyemkimbilia YESU huyo kafungua mlango wa kwanza wa mkondo wa Furaha katika maisha.. kwasababu yeye mwenyewe alisema tukienda kwake atatupumzisha na mizigo tuliyotwikwa na shetani na tutapata raha.
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu”
2. MAOMBI.
Huu ni ufunguo wa pili wa Furaha ya kiMungu.. Bwana YESU alisema tuombe ili furaha yetu iwe timilifu..
Yohana 16:23 “Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.
24 Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu”.
Unapokuwa mwombaji wa mara kwa mara, ukiwa binafsi au katika kikundi cha maombi, kamwe huwezi kupungukiwa Furaha, kwani maombi yanaumba Furaha ya kiMungu yenyewe ndani ya mtu.
3. KULIISHI NENO LA MUNGU.
Huu ni ufunguo wa tatu wa Furaha ya Mungu: Tunapolitenda Neno la Mungu/amri za Mungu moja kwa moja Furaha ya Bwana inaumbika ndani yetu, ambayo ndio chanzo cha nguvu yetu.
Yohana 5:10 “Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.
11 Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na FURAHA YENU ITIMIZWE”.
4. KUIFANYA KAZI YA MUNGU.
Huu ni ufunguo wa Nne wa Furaha ya kiMungu ndani.. Unapojishughulisha na kazi yoyote ya Mungu, iwe kuhubiri mitaani, au kufanya huduma kanisani, au kumtolea Mungu sadaka, au shughuli nyingine yoyote ile ya kikanisa au nje ya kanisa inayohusu ufalme wa Mbinguni, hiko ni chanzo kikubwa sana cha Furaha ya kiungu, ambacho ndicho chanzo cha Nguvu za MUNGU.
Watu wenye kumtumikia Mungu kwa nguvu zao au mali zao wamejaa furaha siku zote.. hata kama watapitia vipindi vya huzuni, lakini kwa kipindi kifupi sana Furaha yao inarejea na wanakuwa na nguvu nyingi za rohoni, wanapotazama matunda ya kazi yao katika Mungu furaha yao inaongezeka.
2Wathesalonike 2:19 “Maana tumaini letu, au furaha yetu, au taji ya kujionea fahari, ni nini? Je! Si ninyi, mbele za Bwana wetu Yesu, wakati wa kuja kwake?
20 Maana ninyi ndinyi utukufu wetu, NA FURAHA YETU”.
5. KUMSIFU MUNGU.
Huu ni ufunguo wa tano wa Furaha ya kiMungu, tunapomsifu Mungu katika Roho na Kweli, Furaha ya kiMungu inaumbika ndani yetu.. na matokeo ya Furaha hiyo ni Nguvu ya Mungu..
Zaburi 43:4 “Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu; Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu”.
Msifu Mungu kwa vitu unavyoviona, msifu Mungu kwa uumbaji wake, msifu kwa upendo wake, msifu kwa miujiza yake n.k
6. KUSOMA NENO LA MUNGU.
Hiki ni chanzo sita cha Furaha Mungu, Mtu anayesoma Neno la Mungu maisha yake yatatawaliwa na Furaha tu siku zote..
Yeremia 15:16 “Maneno yako yalionekana, nami nikayala; na MANENO YAKO yalikuwa ni FURAHA KWANGU, na shangwe ya moyo wangu; maana nimeitwa kwa jina lako, Ee Bwana, Mungu wa majeshi”.
Ukiwa na Furaha ya Mungu utakuwa na Nguvu ya Kuendelea mbele katika mambo yote, utakuwa na nguvu ya kuomba, utakuwa na nguvu za kusubiri, utakuwa na nguvu ya kuinua wengine nk n.k.
Anza leo kuitafuta Furaha ya Mungu kwani hiyo ndio Nguvu yako, na kama tayari ipo ndani yako basi zidi kuipalilia kwa kufanya mambo hayo sita na mengine yanayofanana na hayo.
Mungu akubariki.
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.
MUNGU HAJARIBIWI NA MAOVU BALI MEMA.
Ubatizo ni agizo la Bwana katika hatua za awali za wokovu. Wapo watu wanaosema Ubatizo hauna maana, ndugu usijaribu kufanya hivyo, unaweza usiwe na maana kwako, lakini unaomaana kwa yule aliyekupa hayo maagizo.
Mathayo 28:19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
Ikiwa yeye hakuwa na dhambi wala kasoro yoyote alibatizwa, kwanini sisi tusibatizwe?
Mathayo 3:13 Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe.
Ubatizo ni ishara ya nje ya kile ulichokiamini, kuwa umekufa kwa habari ya dhambi, kisha ukafufuka katika upya na Kristo.
Warumi 6:3-4
[3]Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?
[4]Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.
Ni yule aliyeamini, yaani kuupokea ujumbe wa injili kwa geuko(toba).
Matendo 2:41
Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa;…
Haraka sana, tangu siku ile alipoamini. Ubatizo sio mpaka umekomaa kiroho au kimafundisho, hapana, bali ulipopokea tu wokovu, wakati huo huo unastahili ubatizo.
Matendo ya Mitume 2:38
[38]Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
Ni ule wa kuzamishwa katika maji tele (Yohana 3:23, Matendo 8:36-38 ),
Na kwa jina la Yesu Kristo.(Ambalo ndio Jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu) [Mathayo 28:19, matendo 8:16, 10:48, 19:5]
Ndio, ili kufuata mkondo sahihi wa kimaandiko, huna budi kubatizwa tena.
Kwakuwa umeokoka, na bado hujapata huduma hiyo basi waweza tafuta Kanisa la kiroho, ambalo linaamini katika ubatizo wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo ili utimize agizo hilo.
Lakini ikiwa utapenda kusaidiwa na sisi. Basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi kwa msaada huo:
+255693036618 / +255789001312
Bwana akubariki.
Mistari ya kusimamia kila ukumbukapo tendo la ubatizo.
Wakolosai 2:12 Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu.
Wagalatia 3:27 Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo.
Bwana akubariki.
Kwa mafundisho zaidi kuhusu ubatizo
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Dini ni mfumo au utaratibu wa kumwabudu Mungu. Kwamfano ukienda mahali ukaona watu wamekusanyika na kukubaliana kuabudu kitu Fulani, ni lazima utaona tu utaratibu, au mwongozo au miiko wamejiwekea ya kuifuata na kuishika, ili ibada yao iwe na matokeo. Sasa huo utaratibu ndio unaitwa dini.
Hata imani yetu ndani ya Kristo, inasukumwa na dini. Hatumwabudu tu Mungu kama tunavyotaka bali Mungu aliweka utaratibu na njia ya kuifuata.
Lakini Dhehebu, ni “aina ya dini”. Ambayo huzalika ndani ya imani ile ile moja. Kwamfano utaona wakristo imani yao ni moja kwa Kristo Yesu, na msingi wa kuegemea ni biblia ile ile moja takatifu. Lakini ndani yao kuna michipuko mingi tofauti tofauti ya kitaratibu na ufanyaji ibada, kulingana na walivyoielewa biblia. Ndio hapo utaona wengine wanajiita wapentekesto, wengine wakatoliki, wengine wasabato, n.k. Sasa hii yote ni michupuko, ambayo mengine inakaribiana sana na uhalisia, na mengine inakwenda mbali na kweli ya Mungu.
Lakini cha kumshukuru Mungu ni kuwa biblia imeshaeleza asili ya dini ya kweli inapaswa iweje….
Yakobo 1:26 Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai. 27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.
Kwamba ni lazima itakuwa ya kimatendo zaidi. Yaani utafunzwa utakatifu, na kujitoa.
Hapana, kwasababu Yesu hakuja kuleta dhehebu jipya duniani. Kwani alipokuja alikuta tayari yapo madhehebu mengi yamesha-zaliwa kama tu ilivyo sasa, mfano Mafarisayo, na masadukayo. Lakini hakuwahi kutetea lolote kati yao. Bali alisisitiza watu kumwamini yeye, kama ndio njia ya kweli na uzima mtu asipofanya hivyo hawezi kumwona Baba (Yohana 14:6).
Ikiwa na maana haijalishi una dhehebu zuri kiasi gani. Ukikosa shabaha ya Ukristo, bado mbinguni huendi. Waamini wengi wanashikilia zaidi dini, jambo ambalo ni jema, lakini dini ni kisaidizi cha imani. Sio imani yenyewe, ni sawa na shule na elimu, tunaweza kusema shule ni kisaidizi cha elimu, lakini sio elimu yenyewe.
Hivyo ni busara kuchukua tahadhari ya dhehebu unalotaka kumwabudia Mungu, kwasababu ukweli ni kwamba madhehebu mengine hayana ubora wa kumfanya mtu awe mkristo kamili.
Kwamfano dhehebu lisilo, patana na imani katika Kristo Yesu tu, au lisilofundisha utakatifu, au lisilo amini juu ya vipawa vya Roho Mtakatifu, au linalochanganya ibada ya Mungu na sanamu, bali linasisitiza mambo ya mwilini tu, hilo halikujengi, bali linakupoteza.
Lifananishe kwanza na biblia yako, huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie, kisha ndio ufanye maamuzi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?