Theofania ni neno la kiyunani lenye muunganiko wa maneno ya mawili “theos (Mungu)” na “faino (kuonekana)”. Hivyo ukiunganisha linazalika neno “kuonekana kwa Mungu”
Theofania sio kuonekana kwa Mungu katika ule utimilifu wake wote, hapana, kwasababu maandiko yanasema hakuna mtu awezayo kumwona Mungu akaishi (Kutoka 33:20). Hivyo Theofania ni njia mbadala (isiyo ya moja kwa moja) ambayo Mungu aliitumia kujitokeza na kuongea na watu, kuthibitisha agano lake, au kuwapa maagizo.
Mfano wa njia hizo,
> Ni kijiti cha moto, alichotumia kuzungumza na Musa kule jangwani. (Kutoka 3)
> Mtu Yule aliyeshindana na Yakobo mweleka (Mwanzo 32:24-30)
> Melkizedeki (Mwanzo 14: 18-20)
> Yule mtu wanne aliyewatokea Shedraka, Meshaki na Abednego ndani ya moto (Danieli 3)
> Nguzo ya moto na wingu jangwani (Kutoka 13:21-22)
> Mungu kumtokea Samweli (1Samweli 3:10)
> Maono ya Ezekieli (Ezekieli 1)
Yesu Kristo alipozaliwa katika mwili, sio tena theofania, Bali ni utimilifu wote wa Mungu katika mwili.
Wakolosai 2:9 Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili.
Hapo mwanzo watu hawakumwona Mungu katika utimilifu huo, kwasababu kama wangemwona Mungu wangekufa kwasababu ya dhambi. Lakini Kristo alipokuja kuondoa dhambi kwa damu yake, wanadamu wote tunamwona Mungu katika utilimilifu wote, kwa Roho Mtakatifu aliyemweka ndani yetu.
Tunakikaribia kiti cha rehema, na neema kwa ujasiri bila kufa kama kule mwanzo, kwasababu damu ya Yesu inanguvu ya kuzificha dhambi zetu zote. Ukimwona Kristo(moyoni) umemwona Mungu (Yohana 14:6-11)
Ndio maana ni kwanini leo hii mtu huwezi kumfikia Mungu bila Yesu Kristo.
Okoka leo upokee neema hii, ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya toba. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Wanethini ni kundi la watu ambao walitumika katika hekalu, ambao sio asili ya wayahudi. Wanatajwa sana kwenye kitabu cha Nehemia na Ezra. Maana ya neno ‘Nethini’ kwa kiyahudi linamaanisha “waliotolewa”. Wakimaanisha watu waliotelewa kuwasaidia walawi katika shughuli za hekaluni.
Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyowataja;
Ezra 8:20 na katika Wanethini, ambao Daudi, na wakuu, walikuwa wamewaweka kwa ajili ya utumishi wa Walawi, Wanethini mia mbili na ishirini; wote wametajwa kwa majina yao.
Nehemia 7:73 Hivyo makuhani, na Walawi, na mabawabu, na waimbaji, na baadhi ya watu, na Wanethini, na Israeli wote, wakakaa mijini mwao. Hata ulipowadia mwezi wa saba, wana wa Israeli walikuwa wakikaa katika miji yao.
Soma pia, (Ezra 2:43, 2:58, 7:24)
Biblia haituonyeshi moja kwa moja asili yao ni wapi, lakini wanazuoni wengi huamini walitokea katika chimbuko la wale wagibeoni waliowadanganya Israeli wakati ule mpaka wakafanya nao maagano, Ambao Yoshua aliwapa kazi ya kupasua kuni, na kuteka maji.
Yoshua 9:27 Siku iyo hiyo Yoshua akawafanya kuwa ni wenye kupasua kuni, na wenye kuteka maji, kwa ajili ya mkutano, na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana, hata siku hii ya leo, katika mahali hapo atakapopachagua
Mbali na hawa wagibeoni wengine wanaweza wakawa ni wageni au mateka., ambao baadaye wakaja kuwekwa kwenye utumishi wa hekaluni.
Wanethini hawakufanya kazi zozote za kikuhani, ikumbukwe kuwa ilikuwa ni kosa, mtu ambaye sio myahudi tena wa kabila la Lawi kufanya shughuli zozote za kihekalu, Hawa walikuwa wanafanya kazi za usaidizi ule wa nje, kama vile kutweka maji, kukusanya kuni, usafi, na kazi nyingine zilizohitaji msaada wa pembeni.,Ili kuwaruhusu walawi wasilemewe wajikite zaidi katika kazi za hekaluni.
Maandiko yanaonyesha walikuwa na makao yao maalumu palipoitwa Ofeli kule Yerusalemu karibu na hekalu (Nehemia 3:26)
Hata Baadaya ya uhamisho wa Babeli, tunaona mabaki yaliyorudi Israeli kufanya shughuli za kihekalu, hawa wanethini pia walirejea
Kwa ufupi wanethini walikuwa ni la watu (wasio-wayahudi) waliowekwa kwa ajili ya kusaidia shughuli za hekaluni.
Licha ya kwamba Mungu ameliita kanisa lake na amelitenga, limtumikie lenyewe katika shughuli zote za kimadhabahu. Lakini Bado Bwana anaweza kunyanyua watu wengine nje ya kanisa, kusaidia kanisa kusonga mbele. Mfano wa hawa ni Yule akida wa kirumi ambaye alilipenda taifa la Israeli na kulijengea sinagogi (Luka 7:1-5). Hakuwa myahudi lakini aliwasaidia wayahudi.
Hata sasa wanethini wapo wengi, hawapaswi kuzuiliwa, endapo wanasaidia kanisa au kazi ya Mungu, kwasababu ni Bwana ndiye aliyewavuta.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SWALI: Kwanini Yesu akubali ombi la mapepo, na si kuyaamulia adhabu yake mwenyewe, au kuyafukuza kabla hata hayajaongea?
Luka 8:31 Wakamsihi asiwaamuru watoke kwenda shimoni. 32 Basi, hapo palikuwa na kundi la nguruwe wengi wakilisha mlimani; wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale. Akawapa ruhusa.
JIBU: Maneno hayo aliyasema baada ya kukutana na mtu yule aliyekuwa amevamiwa na jeshi la mapepo, yaliyomfanya akae makaburini muda mrefu, bila nguo. Hivyo kama tunavyosoma yale mapepo yalipomwona tu Yesu, kabla ya tamko lolote yenyewe yakamfuata na kuwasilisha ombi lao kwa kusihi sana. Kwamba yawaingie wale nguruwe waliokuwa jirani wakichungwa. Yesu akasiliza ombi lao, akayapa ruhusa. Yakamtoka Yule mtu, na kuwaelekea wale nguruwe, na saa ile ile Yule mtu akawa mzima.
Zipo sababu mbili.
Ni wazi kuwa Bwana alilitafakari wazo lao, na kuona kama lingeweza kuleta madhara yoyote au uharibifu wowote wa mpango wa Mungu. Na akaona kinyume chake ni kuwa kusudi la Mungu litaendelea kuthibitika hata katika ombi lao, kwasababu kutoka kwao na kuwaingia wale nguruwe kisha kwenda kujitupa ziwani. Ilikuwa ni udhihirisho wa wazi kwa watu kuwa mapepo ni halisi, lakini pia yanatabia ya uuaji. Kwamfano kama angemponya tu, bila ishara yoyote, pengine wengine wangesema “aah huyu akili zilimruka tu!” alikuwa na stress zake, au maisha yalimtinga sana, akachizika, hivyo amekutana na mwanasaikolojia mzuri amemweka sawa… Lakini kuona mapepo yale yameruhuisiwa kwenda kuingia viumbe vingine, halafu yakawaendesha ziwani kuwaua, ilikuwa ni ishara bora zaidi ya kazi za Mungu.
Utakumbuka mapepo yenyewe yalimwambia Yesu ‘tuna nini nawe, je umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?’
Mathayo 8:29 Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?
Maana yake ni kuwa mapepo yalijua kuwa walishawekewa wakati wao wa mateso baadaye kule shimboni na atakayekuja kuwapeleka huko ni Kristo. Hivyo hapa yanamkumbusha Bwana asibatilishe mpango huo, na kuwaadhibu mapema.
Pengine hiyo ndio sababu nyingine ya Bwana kutotoa adhabu kali kwao, ni kuwa mpango wa hukumu ungebatilika.
Kitendo cha mapepo kujisalimisha yenyewe kuomba kupunguziwa adhabu, ni kuonyesha mamlaka kuu iliyo ndani ya Kristo. Ambayo hata sasa ipo ndani yetu. Hatufundishwi kuongea na mapepo, bali kuyakemea kwa mamlaka yote. Ambayo yaweza tokea mengine hata kabla ya kukemewa yakaomba yenyewe nafasi ya kupunguziwa adhabu. Hilo linawezekana!
Tumia mamlaka uliyopewa ndani yako. Fukuza pepo wote.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Gengeni ni wapi, wale nguruwe walipoteremkia? (Marko 5:13)
DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.
Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?
Marko 4:35-36
[35]Siku ile kulipokuwa jioni, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo.
[36]Wakauacha mkutano, wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja naye.
Vifungu hivi vinazidi kutueleza tabia ya Bwana wetu Yesu Kristo na huduma yake jinsi ilivyokuwa ya kitofauti sana hapa dunia.
Kujitoa kwake kulikuwa ni kwa gharama sana tofauti na sisi tunavyoweza kufikiri, embu fikiria kisa kile cha pale kisimani alipokutana na yule mwanamke msamaria, na kuanza kumshuhudia habari zake mpaka kupelekea wimbi kubwa la watu Samaria kumfuata.
Kwa jicho la kawaida unaweza kudhani ilikuwa ni huduma ya kawaida lakini kiuhalisia haikuwa ni jambo lililomruhusu sana kimwili. Kwani maandiko yanatuambia alichoka sana kwasababu alikuwa katika safari ndefu kutoka uyahudi Kwenye Galilaya.
Tunasoma akiwa na njaa na kuchoka ‘alijibwaga’ hivyo hivyo pale kisimani, akawaruhusu wanafunzi wake kwenda mjini kutafuta chakula..
Lakini Mwanamke yule alipokuja kisimani hakusema ngoja nipumzike kwanza, nivute pumzi, kinyume chake alianza muda ule ule kusema naye..hata baadaye alipoletewa chakula ale hamu yake ya kula ilikatwa na ile kazi ya Mungu Aliyokuwa anaifanya.
Yohana 4:6-8,30-33
[6]Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.
[7]Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.
[8]Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula…..
[30]Basi wakatoka mjini, wakamwendea.
[31]Huko nyuma wanafunzi wakamsihi wakisema, Rabi, ule.
[32]Akawaambia, Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.
[33]Basi wanafunzi wake wakasemezana, Je! Mtu amemletea chakula?
Vivyo Hivyo tena wakati mwingine alikuwa anawahubiria Makutano mchana kutwa, mpaka ilipofika jioni ambapo alipaswa aende kupumzika kidogo, ili kesho aendelee na huduma. Maandiko yanatuambia akawaambia wanafunzi wake “Tuvuke Ng’ambo”.
Kibinadamu jambo kama hilo la safari Nyingine mpya lingetemea kwanza maandalizi fulani labda ya chakula, au mavazi, au kushughulikia mahitaji mengine…lakini kwakua kusudi la Mungu lilimsukuma kwa nguvu wakamchukua Vilevile alivyo katika chombo Mpaka ng’ambo..hakuna kuoga, wala kupumzika, wala kuwatembelea marafiki na ndugu, ni kuunganisha ziara nyingine, sio kwamba alikuwa hachoki hapana alichoka sana, kuthibitisha hilo utaona akiwa katikati Ya safari ile alipitiwa na usingizi kwa sababu ya uchovu (4:38)
Hii inatuonyesha wazi utayari wa Kristo ambao uliathiri mpaka hali zake za kimwili.
Kwasababu yeye ni yule yule jana na leo na hata Milele, utayari ule ule aliokuwa nao zamani anao hata leo.
Kristo haitaji maandalizi wala hali ya kimazingira, katika kutumika Na sisi. Ni rahisi Kudhani mpaka Bwana atende miujiza tunahitaji kwanza maandalizi ya Maombi na mifungo na mikesha, au mpaka Bwana amwokoe mtu tunahitaji tuwe na elimu nyingi ya biblia, au uzoefu kumbe si lazima..
Ni kweli mambo hayo ni muhimu katika baadhi ya mazingira lakini si yote. Anataka tuwe wepesi wa kumchukua yeye vilevile kama alivyo katika mazingira yoyote?
Yupo tayari kwenda na sisi popote, maadamu tu sisi tunakuwa tayari kumchukua katika safari zetu kwa imani. Hatupaswi kujali tutatolea Wapi fedha za huduma kumuhubiri Kristo.
Ikiwa umeokoka, ni nini unasubiri Usimtumikie Mungu wako?. Unataka uwe kama Martha ambaye alijisumbua na maandalizi mengi wakati lililohitajika ni moja tu, kumsikiliza Kristo? Kumchukua vilevile kama alivyo.
Yesu alipowaacha mitume hakuwapa mitaji ya maspika, au vyuo vya kusoma au majengo ya kuabudia…aliwaambia enendeni nami nitakuwa pamoja nanyi mpaka ukamilifu wa dahari. Msibebe fimbo wala mkoba, wala pesa kibindoni, wala kanzu mbili.(Mathayo 10:5-10)
Kwa tafsiri nyingine anasema nichukueni hivi hivi nilivyo, msijali hali yangu, nanyi mtaona Maajabu mbeleni.
Bwana atujalie kujua matamanio yake, ili tusizuiliwe kuhudumu naye popote, kwenye mazingira yoyote.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Masomo mengine:
RABI, UNAKAA WAPI?
Yesu alipopanda kuomba kwanini atokewe na Musa na Eliya na sio manabii wengine?
SAUTI NYUMA YA ISHARA.
Swali: Neno la MUNGU linamaanisha nini linaposema “mtu atachukua dhambi yake au uovu wake”?
Jibu: Turejee andiko hilo..
Walawi 5:17 “Na kama mtu akifanya dhambi, na kutenda mambo hayo mojawapo ambayo Bwana alizuilia yasifanywe, ajapokuwa hakuyajua, ni mwenye hatia vivyo, NAYE ATACHUKUA UOVU WAKE”
Tusome tena..
Walawi 24:5 “Nawe nena na wana wa Israeli na kuwaambia, Mtu awaye yote atakayemlaani Mungu wake ATACHUKUA DHAMBI YAKE”.
Utalisoma tena neno kama hilo katika Walawi 7:18, Hesabu 9:13, Ezekieli 44:10-12..
Katika Agano la kale Bwana MUNGU aliruhusu mtu kulipizwa kisasi endapo amefanya jambo la kusudi lililo baya.. kwamba UHAI kwa UHAI.. jino kwa jino..jicho kwa jicho..
Maana yake kama mtu amemkata mwenzake mkono naye pia ni lazima akatwe mkono, kama mtu amemwua mwenzake sharti naye pia auawe..
Walawi 24:17 “Na mtu ampigaye mtu hata akafa, lazima atauawa;
18 na atakayempiga mnyama hata akafa atalipa; uhai kwa uhai.
19 Na mtu akimtia mwenziwe kilema; vile vile kama alivyofanya, naye atafanyiwa vivyo;
20 jeraha kwa jeraha, jicho kwa jicho, jino kwa jino; vile vile kama alivyomtia mtu kilema, naye atalipwa vivyo”.
Lakini yapo matukio ambayo yalikuwa yakifanyika yanakuwa HAYANA KISASI!, kwamfano mtu aliyesikika kamtukana MUNGU au kulilaani jina la MUNGU, mtu huyo sheria ilikuwa ni kuuawa kwa kupigwa mawe, sasa wale watu waliomwua kwa kumpiga mawe baada ya kuthibitika uasi wa Yule mtu, hao hawawezi kulipwa kisasi kwamba nao wauawe kwasababu sheria imesema uhai kwa uhai.
La! Bali wataachwa hai,.. sasa hiko kitendo cha hawa wauaji kuachwa Hai na kutokulipwa kisasi ndio tafsiri yake kwamba “Yule aliyekufa kauchukua uovu/dhambi yake mwenyewe”.. maana yake hajaacha dhambi kwa waliomwua!.
Lakini laiti kama atauawa pasipo hatia na ikathibitika hivyo, basi wauaji wale watabeba dhambi ya mauaji hivyo nao pia watauawa, kama sheria isemavyo kwamba uhai kwa uhai na jino kwa jino. Sasa kitendo hiko cha kuuawa kwa kosa la mauaji yasiyo na hatia, ndicho kinachoitwa kubeba dhambi ya aliyekufa.
(kumbuka si kwamba watabeba makosa ya Yule mtu, la!, Yule mtu atabaki na dhambi zake alizozifanya.. bali hawa wauaji watabeba lile kosa moja tu la mauaji ya mtu asiye na hatia), hivyo watahukumiwa tu kama wauaji waliomwua mtu asiye na hatia.
Na lugha nyingine ya kubeba dhambi ya mtu ni kubeba damu ya mtu. Hivyo mahali popote katika biblia Bwana MUNGU anaposema kuwa “nitaitaka damu mikononi mwa mtu” maana yake ni hiyohiyo kwamba “kwamba atamhukumu muuaji kwa kosa la kumwua asiye na hatia”.. na anaposema damu yake itakuwa juu yake mwenyewe aliyefanya kosa, maana yake ni kwamba aliyeuawa hatalipiwa kisasi kwa waliomwua.
Zifuatazo ni baadhi ya dhambi ambazo mtu akizitenda basi alibeba dhambi zake mwenyewe, wala waliomwua hawakuwa na hatia ya kulipwa kisasi wala kushtakiwa.
Je hata sasa (Agano jipya) sheria hizi zipo?.
Katika Agano jipya hatuna sheria yoyote ya kisasi, Bwana YESU alitufundisha hilo katika Mathayo 5:38-41, ikiwa na maana kuwa hatujapewa ruhusa ya kumwua mtu au kulipiza kisasi bali kisasi ni juu ya Bwana (soma Warumi 12:19).
Kwahiyo kama hatujapewa ruhusa ya kulipa kisasi, au kutoa hukumu ya aina yoyote kama katika kipindi cha agano la kwanza, basi maana yake ni kwamba mtu yoyote Yule alipaye kisasi atakuwa na hatia pasipo kujalisha makosa aliyoyafanya ndugu yake!..
Muuaji wa aina yoyote ile, atabeba kosa la mauaji, (Bwana ataitaka damu ya aliyemwua mikononi mwake).. hata kama amemwua mtu aliyemlaani MUNGU, bado ni kosa!..katika agano la kale haikuwa makosa lakini agano jipya ni kosa!.
Kwahiyo hatujapewa ruhusa ya kuua kwa kosa lolote lile, tukifanya hivyo tutakuwa na hatia na Bwana ataitaka damu ya aliyekufa mikononi mwetu.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Orodha ya majina ya Miji ya Biblia (Agano la kale) na Sasa
Agano la Chumvi ni nini? (2Nyakati 13:5)
Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?
Ndio Maandiko yanatuonyesha kuwa tutatambuana tukifika mbinguni. Ifahamike kuwa fahamu zetu au kumbukumbu zetu za hapa ulimwenguni hazitaondolewa kabisa, tufikapo mbinguni, kila pito tulipitialo, na kila jambo lililowekwa na Mungu sasa hapa duniani, lina sehemu kubwa ya fundisho la maisha yajayo. Hivyo maisha ya duniani yana thamani kama yalivyo tu maisha yatakayokuja. Ndio maana kabla ya kuingia kule ilitupaswa kwanza tupitie hapa.
Zipo sehemu kadha wa kadha katika maandiko zinatuthibitishia kuwa tutatambuana kule mbinguni.
Tunaona Bwana wetu Yesu Kristo alipofufuka na mwili mpya wa utukufu, aliweza kutambuliwa . Kwamfano siku ile ya kwanza ya juma Mariamu Magdalena, akiwa pale kaburini alimtambua Bwana Yesu alipozungumza naye.
Yohana 20: 16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu).
Halikadhalika wakati ule Bwana Yesu anawachukua mitume wake watatu Petro, Yohana na Yakobo na kuwapeleka juu ya mlima ule mrefu, na kuwabadilikia sura, kama tunavyosoma watu wawili walitokea ambao ni Musa na Eliya.
Mitume waliweza kuwatambua ijapokuwa hawakuwahi kuwaona uso kwa uso hapo kabla.
Mathayo 17:3 Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.
1Wakorintho 15:42 Kadhalika na kiyama ya watu. Hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibika; 43 hupandwa katika aibu; hufufuliwa katika fahari; hupandwa katika udhaifu; hufufuliwa katika nguvu; 44 hupandwa mwili wa asili; hufufuliwa mwili wa roho. Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko
Mstari huo unatuonyesha kuwa hatutaondolewa uhalisia wetu Tutabakia kuwa sisi sisi., isipokuwa tutavikwa utukufu wa juu zaidi. Maana yake ni kuwa tutatambuana.
1Wathesalonike 4:16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana
hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.
Tutarejeshwa, na kuonana. Hivyo kwa mujibu wa vifungu hivyo katika ulimwengu ujao sote tutajuana na kufahamiana.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Sheria ni agizo la shuruti linalotolewa na mamlaka kuu…, na KANUNI ni mwongozo au utaratibu maalumu unaotolewa kuhusiana na utekelezaji wa sheria iliyowekwa au agizo lililotolewa..
Kwamfano katika biblia kulikuwa na Sheria ya “kuishika Pasaka” lakini ilikuwepo pia kanuni (ambayo ni mwongozo wa namna ya kuiadhimisha hiyo siku), kwamba ni lazima kwanza iwe siku ya 14 ya mwezi wa kwanza wa kalenda ya kiyahudi, na pia siku hiyo ni lazima achinjwe mwana kondoo na kumwoka motoni na aliwe pamoja na mboga zenye uchungu n.k (Soma Kutoka 12:1-12).
Sasa huo mwongozo wote wa jinsi ya kuiadhimisha hiyo siku ndio unaoitwa Kanuni, lakini sheria ni hiyo moja tu kwamba Waishike Pasaka..
Hesabu 9:14 “Na kama mgeni akiketi kati yenu ugenini, naye ataka kuishika Pasaka kwa Bwana; kama HIYO SHERIA YA PASAKA ILIVYO, na kama amri yake ilivyo, ndivyo atakavyofanya; MTAKUWA NA SHERIA MOJA, kwa huyo aliye mgeni, na kwa huyo aliyezaliwa katika nchi”.
Katika biblia kila Amri au sheria ilikuwa na Kanuni zake na hukumu zake.
Tunayo sheria na amri ya Kristo pia ambayo ni UPENDO, lakini huu upendo unao kanunini…ni lazima tuzitafutae kanuni za upendo na tuzijue.
Isaya 28:13 “Kwa maana ni amri juu ya amri, amri juu ya amri; kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; huku kidogo na huku kidogo”.
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini tarehe ya pasaka inabadilika kila mwaka?
PASAKA NI NINI? NA JE TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA?
Nini tofauti kati ya kileo na divai?
FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.
Je! kuna mwanamke mwingine aliyempaka Bwana marhamu (manukato) zaidi ya Mariamu ndugu yake Lazaro?
Jibu: Neno Utakatifu linatokana na Neno “utakaso”.. kitu lilichotakasika kinaitwa “kitakatifu”.. na kitu kilichotakasika/takata maana yake hakina uchafu.
Kwahiyo utakatifu kwa tafsiri rahisi maana yake ni “kuwa safi, (kutokuwa na uchafu)”.. Mtu anaweza kuwa msafi (mtakatifu) mwilini na rohoni.
Sasa kikawaida kitu chochote kinapokuwa safi, huwa kinatoa Mng’ao unaopendeza.. sasa ule mng’ao unaotafsiri usafi wa kitu kile ndio unaoitwa UTUKUFU, kwamfano dhahabu inaposafishwa na kuwa safi huwa inatoa mng’ao mzuri wa kipekee, sasa ule mng’ao ndio utukufu wa ile dhahabu au kito, na vitu vingine vyote ni hivyo hivyo.
Hali kadhalika mtu aliyetakaswa dhambi zake kwa damu ya YESU, na yeye mwenyewe kujilinda na kujitenga na uchafu wote wa rohoni na mwilini, basi mtu huyo ni mtakatifu na anao utukufu, ambao ni NURU inayong’aa, ambayo shetani na mapepo yake hayawezi kustahimili mwako wake.
Lakini zaidi sana MUNGU wetu aliyetuumba ndiye mwenye utukufu MKUU, ambao huo unatokana UTAKATIFU alionao, uzidio viumbe vyake vyote.. Mng’ao wa utukufu wake hata malaika wanainama mbele zake na kujifunika kwa mbawa zao, na utukufu wake unang’aa mpaka duniani.
Isaya 6:1 “Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu.
2 Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka.
3 WAKAITANA, KILA MMOJA NA MWENZAKE, WAKISEMA, MTAKATIFU, MTAKATIFU, MTAKATIFU, NI BWANA WA MAJESHI; DUNIA YOTE IMEJAA UTUKUFU WAKE”.
Naam nasi tuliompokea YESU ni lazima tufanane naye, na hatuwezi kuwa na utukufu bila kuwa watakatifu, na hatuwezi kukosa utukufu tukiwa watakatifu, na kuwa mtakatifu duniani inawezekana..
Zaburi 16:3 “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JE UMEUFIKIA ULE UTUKUFU HALISI WA MANA?
NYUMBANI MWA BABA YANGU MNA MAKAO MENGI.
Swali: Kuna tofauti gani kati ya Ahadi na Nadhiri, kwa mujibu wa Biblia?
Jibu: Ahadi ni Neno/tamko la hiari mtu analolitoa kwa mtu mwenzake, kwamba atalitenda katika wakati mfupi au mrefu ujao.
Kwamfano mtu anaweza kuahidi kuwa kesho atawasili katika hafla, na hiyo kesho kweli akafika kama alivyoahidi, hapo anakuwa ameitimiza ahadi yake, lakini asipowasili kama alivyoahidia anakuwa hajaitimiza ahadi, na ni dhambi ikiwa hakuwa na sababu za msingi za kuivunja ahadi yake.
Lakini katika upande wa Nadhiri, hii ni ahadi (yaani tamko ya hiari) mtu analolitoa kwa MUNGU, na si kwa mtu.
Kwamfano mtu anaweza kuahidi kuwa endapo akipona ugonjwa unaomsumbua atamtolea MUNGU sadaka ya shukrani, au endapo Mungu akimtendea jambo Fulani basi atamtolea MUNGU sadaka Fulani, hiyo inakuwa ni nadhiri.
Na mtu asipotimiza Nadhiri aliyomwekea MUNGU inakuwa ni dhambi..
Mhubiri 5:4 “Wewe ukimwekea Mungu nadhiri, usikawie kuiondoa; KWA KUWA YEYE HAWI RADHI NA WAPUMBAVU; BASI, UIONDOE HIYO ULIYOIWEKA NADHIRI.
5 Ni afadhali usiweke nadhiri, Kuliko kuiweka usiiondoe.
6 Usikiache kinywa chako kuukosesha mwili wako; wala usiseme mbele ya huyo malaika ya kwamba umepitiliwa; kwani Mungu akukasirikie sauti yako, na kuiharibu kazi ya mikono yako?”
Kwahiyo ni muhimu kuitimiza ahadi tunazozitoa na pia Nadhiri uliomwekea MUNGU.
Ikiwa kuna sababu zozote za msingi zilizojitokeza za kutotimiza ahadi basi ni vizuri kufanya mapatano na uliyemhadi mapema ili isigeuke kuwa uongo.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JE! USIPOTIMIZA NADHIRI ZAKO ZOTE KWA BWANA. HAWEZI KUKUSAMEHE?
Katika agano la kale dhambi ilitokea na kuhesabiwa katika maeneo mbalimbali.
Kwamfano
> Kulikuwa na makosa ya jamii nzima. Yaani taifa zima kuasi. (Kutoka 32,)
> Makosa ya mtu binafsi. Mfano kutenda uzinzi, Wizi, uuaji n.k.
> Makosa ya kuwatendea vibaya wanyonge: Mfano maskini, wageni, mayatima na wajane (Amosi 5:11-12),
> Makosa ya kukaidi sherehe za kidini (Walawi 11-15),
> Makosa ya kuvunja maagano (Yeremia 17:21-23),
> Makosa ya kuabudu miungu mingine (sanamu).
Lakini pia kulikuwa na aina nyingine mbili za makosa..
> Aina ya kwanza ni makosa ya kukusudia
> Aina pili ni yale ya kutokusudia.
Ikiwa mtu alitenda dhambi kwa kutojua, alihesabika kuwa ni dhambi, hivyo alilazimika atoe sadaka ya dhambi. Lakini kama alitenda dhambi ya makusudi kinyume na mwenzake, ili kuondoa kosa Ilipasa atoe sadaka ya hatia.
Aina ya sadaka hizi zinaelezwa kwa urefu kwenye kitabu cha Walawi 4:1 – 5:13
Dhambi za kutokusudia Mfano wake ilikuwa ni kama kuvunja amri bila kujua au kutojua Sheria ya vitu safi au najisi ilivyo. Hivyo mtu alijikuta tu anatenda kwa kukosa ufahamu.
Walawi 4:1-3
[1]BWANA akanena na Musa, na kumwambia,
[2]Haya, nena na wana wa Israeli, uwaambie, Kama mtu ye yote akifanya dhambi pasipo kukusudia, katika neno lo lote ambalo BWANA amelizuilia lisifanywe, na kutenda neno lo lote la maneno hayo;
[3]kama kuhani aliyetiwa mafuta akifanya dhambi, hata analeta hatia juu ya watu; ndipo na atoe kwa ajili ya dhambi yake aliyoifanya, na kumsongeza kwa BWANA ng’ombe mume mchanga mkamilifu, kuwa ni sadaka ya dhambi.
Dhambi za kukusudia ni zote ambazo zilitendwa kinyume na mtu mwingine au mambo matukufu mfano wa hizi ni kama kuiba, kusema uongo, viapo Vya uongo, hivyo iliambatana pia na kutoa fidia ya vitu hivyo.
Sio tu kusamehewa bali pia kuweka mambo sawasawa kwa kulipia fidia.
Mfano wa tendo hili, tunaona kwa Zakayo, alipofikiwa na wokovu, alitubu kwa kurejesha mara nne ya vyote alivyodhulumu. (Luka 19:8) huo ni mfano wa sadaka ya hatia.
Katika agano jipya dhambi Zote Za kukusudia na kutokusudia na nyingine zote zinaondolewa na sadaka moja tu ya daima nayo ni DAMU YA YESU (Waebr 9:26, Isaya 53:10, 1Petro 2:24). Hiyo tu ndio inafuta hatia zote.
Lakini pamoja na hayo, sadaka hizi hutukumbusha pia kila tuombapo rehema, (kwa unajisi tunaojitia kila siku), hatuna budi kuomba sio tu kwa dhambi tuzijuazo bali pia kwa zile tusizozijua.
Kwasasa dhambi tusizokusudia ni kama vile kumkwaza mwenzako bila kufahamu, Kutowaombea wengine(2Samweli 12:23), kuwaza vibaya, kutotumiza nadhiri zetu, au wajibu wetu N.k.
Bwana akubariki.
Je umesamehewa na kuondolewa dhambi zako? Kama ni la! basi wakati ndio sasa, unapomgeukia Bwana Yesu, anakuondolea kumbukumbu lote la makosa. Hivyo fungua hapa kwa msaada huo wa kumpokea yeye >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ndio kipi? (Matendo 21:25).
Nini maana ya dhabihu na matoleo hukutaka? (Waebrania 10:5).
Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?