Category Archive Uncategorized @sw-tz

Bafe ni nini (Mwanzo 49:17)

Neno hilo utalisoma katika ule utabiri wa Yakobo kwa watoto wake, alipokuwa anawabariki, na alipofikia kwa Dani, yeye alimfananisha na Bafe. Swali ni je Huyu bafe ni nani?

Tusome

Mwanzo 49:17 Dani atakuwa nyoka barabarani, Bafe katika njia, Aumaye visigino vya farasi, Hata apandaye ataanguka chali. 18 Wokovu wako nimeungoja, Ee Bwana.

Bafe ni nyoka aina ya kifutu. Hivyo Yakobo alimwona Dani kama nyoka, ambaye ijapokuwa maisha yake ni ya mavumbi, lakini ameng’ata farasi kisigo hatimaye farasi Yule akashindwa kuendelea na hapo hapo mpanda farasi naye akashindwa kuvifikia vita vyake.

Akimaanisha kuwa Dani anaweza dharaulika, lakini ana wokovu mkuu kwa watu wake, pale ambapo wangetarajia mpanda farasi arushiwe mikuki na majeshi ya watu, au avamiwe kijeshi, yeye anauma tu kisigo cha farasi wao, sumu inaingia na nguvu yao inaisha.

Ni kufunua kuwa kila mmoja wetu amepewa karama yake tofauti na mwingine, na kama ikitumika kifasaha huweza kumweka adui chini, sawa tu na zile karama ambazo huonekana zina heshima mbele ya macho ya watu kama vile, utume, uchungaji, uinjilisti n.k.

Kamwe usidharau karama yako, kumbuka sikuzote vile visivyoonekana  kwa urahisi ndio huwa vina umuhimu mkubwa. Unaweza usiwe mguu au mkono, lakini ukawa moyo, au figo, vilivyojificha ndani, ambavyo tunajua uthamani wake ulivyo.

Halikadhalika, katika Baraka zile, Yuda aliitwa simba, Isakari aliitwa punda, Dani aliitwa Bafe, Lakini wote waliitwa Israeli. Taifa la Mungu.

Je ! unaitumia vema karama yako, au umeidharau? Na kutamani za wengine?

Kwa msaada wa jinsi ya kuitambua karama yako fungua hapa >>> NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

UFUNUO: Mlango wa 6(Opens in a new browser tab)

Maana ya Mithali 11:17 Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake(Opens in a new browser tab)

(Opens in a new browser tab)MIHURI SABA(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

AINA SABA (7), ZA SIFA KIBIBLIA.

Katika biblia zipo aina mbalimbali za kumsifu Bwana, lakini kuna kuu saba ambazo zilitambuliwa na wayahudi kwa wakati wote. Hivyo ni vema kuzifahamu ili wigo wako uwe mpana zaidi katika eneo hili la sifa. Kwasababu ndio huduma kuu tuliyonayo duniani kwa Mungu wetu. Kumbuka chakula chetu ni Neno, lakini chakula cha Mungu wetu ni Sifa zetu. Hivyo ni lazima tujue tunamsifuje yeye kiufasaha kwa jinsi apendavyo.

Hizi ni aina saba za sifa.

1.) Kucheza: Kwa kiyahudi huitwa ‘Hallal’

Hii ni aina ya kumsifu Mungu ambayo, mwimbaji hujidai, hujigamba mbele za Mungu wake kwa kuuhusisha mwili wake, yaweza kuwa kuruka kuruka, au kucheza.

Agizo hilo lipo katika Zaburi 149:3 Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa matari na kinubi wamwimbie.

Ndio lile Daudi na Israeli wote walilolifanya walipokuwa wanalileta sanduku la Bwana Yerusalemu,

 2Samweli 6:14 Daudi akacheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote; na Daudi alikuwa amevaa naivera ya kitani.

15 Basi Daudi na nyumba yote ya Israeli wakalileta sanduku la Bwana kwa shangwe, na kwa sauti ya tarumbeta.

16 Ikawa, sanduku la Bwana lilipoingia mji wa Daudi Mikali, binti Sauli, akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi akiruka-ruka na kucheza mbele za Bwana; akamdharau moyoni mwake.

Hivyo na wewe kama mtu uliyeokolewa na Kristo, kujidai kwa ujasiri wote mbele ya Mungu wako usijizuie, angalizo tu ni kwamba usifanye kidunia, kana kwamba unacheza dansi, huku moyoni mwako hakuna ibada. Hiyo sio sawa, lakini kumwimbia Mungu kwa kucheza hakuna kosa lolote ikiwa ni jambo la kububujika  moja kwa moja kutoka moyoni mwako.

2) Kuinua mikono: Kwa kiyahudi huitwa ‘Yadah’.

Hii ni aina ya kumsifu Mungu kwa kuinua mikono juu, Kama ishara ya kutambua tegemeo lako kwake, kama mtoto mdogo kwa mzazi wako anapomlilia. Na kuonyesha upendo wako wa dhati kwa Mungu wako.

Zaburi 63: 3 Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; Midomo yangu itakusifu.  4 Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai; Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.

Kama mtakatifu jizoeze mara nyingi, kunyanyua mikono yako juu wakati unamwabudu Mungu, au wakati mwingine unapoomba. Binafsi, nimeona tofauti kubwa sana, niinuapo mikono yangu, pindi niombapo au nisifupo, najikuta nazama rohoni kwa haraka sana, zaidi ya napoweka mikono yangu chini. Kumbuka ile habari ya Musa, alipoinua mikono juu, Israeli ilishinda, lakini alipoweka mikono chini, Waamaleki walishinda. (Kutoka 17:11) Hivyo jifunze sana, kuiinua mikono yako juu, katika ibada zako.

3) Kuinama, kujusudu, kupiga magoti: Kwa kiyahudi huitwa ‘Barak’.

Hii ni aina ya kumsifu Mungu kwa kumbariki Mungu, lakini kwa kuonyesha heshima kubwa kama mfalme, kujishusha chini, kusujudu au kupiga magoti, kuonyesha yeye ni mkuu sana wa kuogofya zaidi ya wafalme wote na wakuu wote ulimwenguni.

Zaburi 5:7 Bali mimi, kwa wingi wa fadhili zako, Nitaingia nyumbani mwako; Na kusujudu kwa kicho, Nikilielekea hekalu lako takatifu.

Kama mwamini, sifa zako zisiwe za mdomo tu wakati wote, jifunze kupiga magoti, au kusujudu ni ishara ya unyenyekevu  wa hali ya juu. Fanya hivyo nyakati za sifa, nyakati za maombi.

4) Kusifu kusiko na maandalizi: Kwa kiyahudi huitwa Tehillah:

Aina ya kusifu moyoni mwako, kwa namna isiyo na maandalizi Fulani maalumu, mfano wa kwaya, ni nyimbo ambazo zitainuka  katikati ya mapito yako fulani, wakati mwingine unapopitia kutendewa mema mengi na Mungu, na hapo ghafla tu moyoni mwako unasikia kumsifu Mungu, kumpa utukufu.

Kwamfano Daudi alipokuwa anapitia magumu,au anashindaniwa na Mungu, akimtafakari Mungu, mara anaachilia kinywa chake, Mungu anaanza kububujisha nyimbo mpya ulimini mwake.

Mfano mwingine wa sifa kama hizi, ni pale Mungu alipowavusha wana wa Israeli, bahari ya Shamu, na kuona maadui zao wamefunikwa na habari, ndipo Israeli wote, pamoja na Miriamu na wanawake wakasimama kumwimbia Mungu nyimbo za Furaha (Kutoka 15).

Mfano mwingine ni pale Mariamu alipomtembelea Elizabeti, na kutolewa unabii kuwa atamzaa Masihi, alishangalia na ghafla  akafungua  kinywa chake kwa wimbo, kumsifu Mungu kwa namna hii,  (Luka 1:46-56)

Hivyo kila mkristo, katika majira yote, vipindi vyote, viwe vyepesi, viwe vingine, hana budi kutafakari na kufungua kinywa chake kumsifu Mungu kwa aina hii ya sifa ya Tehillah. Ni muhimu sana, na inampendeza, Mungu, hii haina maandalizi, haina mpangilio maalumu, hutoka moyoni mwako, kwasababu Fulani Mungu alizokuonekania.

5) Kusifu kwa vyombo vya muziki: Kwa kiyahudi huitwa “Zamar”.

Mungu aliwaagiza pia watu wake, wamwimbie si kwa vinywa vyao tu na makofi, lakini pia pamoja na kuchanganya zana mbalimbali za muziki.

Zaburi 150:3 Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;

4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;  5 Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6 Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya.

Ni wazi kuwa kuchanganya ala mbalimbali,kama vile gitaa, vinanda, filipi, tarumbeta, ngoma, zeze, marumba, n.k. Katika kumwimbia Mungu, huongeza ladha na hisia njema katika kumsifu, na hivyo hupendeza sana machoni pake. Wapo watu hawaamini katika matumizi ya vyombo. Lakini maandiko yanatuagiza tumsifu Mungu kwa hivyo.

6) Kusifu kwa kupaza sauti kuu: Kwa kiyahudi huitwa “Shabach”.

Aina hii ya sifa, ni kwa kupaza sauti yako juu sana kwa Mungu. Hii Huonyesha ujasiri wa Mungu unayemwabudu, na kuutangazia umati na ulimwengu kuwa yupo Mungu mahali hapo anayeabudiwa.

Zaburi 47:1 Enyi watu wote, pigeni makofi, Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe.

Sifa hizi zina nguvu sana, ndio zile ambazo ziliangusha kuta za Yeriko. Wana wa Israeli walipoambiwa wapaze sauti zao kwa Mungu. Zile sauti hayakuwa makelele tu, bali zilikuwa ni sauti za kumtukuza Mungu.(Yoshua 6:20).

Tumwimbiapo Mungu, hatupaswi tuwe kama mabubu, au tuimbe kinyonge, au kwa kutegea-tegea. Mungu anajivunia sana watu wale wanaomwabudu kwa ujasiri, kwa kufumbua vinywa vyao na kupaza sauti zao kwa nguvu  kumwadhimisha yeye.

7) Kusifu kwa ukiri, shukrani, kutoa: Kwa kiyahudi huitwa “Todah”.

Ni aina ya sifa inayofanana na ile ‘Yadah’,ya  kumwinulia Mungu mikono kumwimbia. Isipokuwa hii, ni kumwadhimisha Mungu, kwa matendo ambayo bado hujayaona kwa macho. Kutambua uweza wa Mungu, hata kama huoni matokeo yoyote, na kumshukuru katika hayo. Hata pale ambapo hujisikii.  .

Mfano ya sifa hizi, ni labda wewe ni mgonjwa, daktari amekuambia una siku chache za kuishi, ukiangalia umeombewa mara nyingi hakuna matokeo yoyote, lakini unakumbuka Neno la Bwana linalosema ‘kwa kupigwa kwake sisi tumepona’. Unaanza kufurahi, ukimwinulia mikono Mungu na kumshukuru ukisema asante, Bwana kwa kuniponya, huku ukimsifu katika hali yako hiyo hiyo ya udhaifu.

Sifa hizo ni muhimu sana kwetu, na zinaugusa moyo wa Mungu kwa namna ya kipekee, Kwasababu kamwe haziwezi kuwa na unafiki ndani yake.

Hizi zinapaswa ziwepo ndani yetu wakati wote. Unakumbuka ahadi za Mungu ambazo bado huoni zimetimia, unamsifu Mungu sana kwa furaha kana kwamba umekwisha vipata vyote sasa, umetafuta kazi umekosa, unamsifu Mungu kana kwamba umepokea ripoti ya kuajiriwa.

Hizi ndio aina saba za sifa, ambazo ukiziachilia katika maeneo yako yote ya kiibada. Utampendeza Mungu sana. Lakini pia zinapaswa ziwe katika Roho na Kweli, tafsiri yake, ni sharti mtu umsifuye Mungu uwe umeokoka, umeshatambua kazi ya Kristo ya ukombozi kwenye maisha yako ipoje. Tayari wewe ni  mfuasi wa Kristo. Ndipo sifa hizo zitakubalika. Vinginevyo haziwezi kumpendeza Mungu hata kama utazifanya zote kwa ufasaha.

Ikiwa bado hujaokoka, na upo tayari kufanya hivyo leo. Basi kwa msaada unaweza fungua hapa kwa msaada wa mwongozo huo wa kumkaribisha Yesu maishani mwako.>>>>  KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

SAFINA NI NINI?

Je kumwimbia Mungu kwa kucheza ni sahihi kibiblia?

(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Biblia ina mistari mingapi?

Agano la kale lina jumla ya mistari 23,145, na mistari 7957 kwenye agano jipya. Kuleta jumla ya mistari 31,102 kwa biblia nzima.

Ambapo tukileta katika eneo la wastani ni sawa na kusema biblia ina mistari 26 kwa sura.

Washirikishekishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Biblia ina sura na milango mingapi?

Je kumwimbia Mungu kwa kucheza ni sahihi kibiblia?

Mgawanyo wa Vitabu vya Biblia

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

Rudi Nyumbani

Print this post

Ni alama gani Mungu aliyomtia Kaini mwilini? (Mwanzo 4:15)

SWALI:Ni alama gani Mungu aliyomtia Kaini mwilini?


Tunaona Kaini baada ya kumuua ndugu yake Habili, Mungu alimpa adhabu kwa kumwambia maneno haya;

Mwanzo 4: 9 Bwana akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?

10 Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.

11 Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;

12 utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.

Lakini tukiendelea kusoma tunaona, Kaini anamlilia Mungu na kumwambia adhabu yangu ni kali sana, haichukuliki, kila mahali nitakapoenda nitakuwa mtu wa kuuliwa, ndipo Mungu akamuhakikisha ulinzi kwa kumwekea alama. Kama tunavyosoma kwenye vifungu vinavyofuata;

13 Kaini akamwambia Bwana, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.

14 Tazama, umenifukuza leo katika uso wa ardhi, nitasitirika mbali na uso wako, nami nitakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani; hata itakuwa kila anionaye ataniua.

15 Bwana akamwambia, Kwa sababu hiyo ye yote atakayemwua Kaini atalipizwa kisasi mara saba. Bwana akamtia Kaini alama, mtu amwonaye asije akampiga

Swali linakuja hii alama ni ipi?

Lakini kabla ya kufahamu alama yenyewe ni nini ni vizuri ukaelewa maana ya adhabu aliyopewa ya kuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani. Fungua hapa ufahamu tafsiri yake >>>> UTAKUWA MTORO NA MTU ASIYE NA KIKAO DUNIANI.

Hivyo tukirudi kwenye swali alama ni ipi?

Zipo nadharia nyingi, lakini tujifunze kwanza baadhi ya mambo.  Kumbuka kuwa adhabu ile Kaini aliitambua kabisa ilihusu kutengwa na fadhili na uso wa Mungu kabisa. Na mahali popote pasipo na mkono wa Mungu hapana usalama wowote, ni sawa na mwili unaokosa kinga, kila  ugonjwa unaopita pale utaushambulia, hata yale maradhi madhaifu kabisa,. Ndicho alichokigundua Kaini alijua pasipo Mungu duniani hata kwa sehemu ndogo, haiwezekaniki  kuishi, chochote chenye  uhai atakuweza tu, wanyama watakuweza, mapepo yatakuweza. Ndio maana ya kauli yake hiyo ‘kila anionaye ataniua’.

Lakini Mungu akamuhakikishia usalama, kwa kumwekea alama, ili yoyote akimwona asimuue Kaini. Sasa kufikiri alama hiyo ni mchoro(tattoo) Fulani mwilini, si rahisi kumfanya mtu asidiriki kumuua, kwani mchoro hauzuii mtu kuangamizwa.

Lakini kufikiria alama iliwekwa katika eneo la ki-mwonekano (ukubwa), au eneo la kuongezewa sifa/ufanisi Fulani uliotofauti na wengine yaweza kuwa jambo la kweli.

Kwanini?

Tunaweza kuona baada ya pale sifa za uzao wa Kaini jinsi zilivyokuwa, walikuwa ni watu wavumbuzi, watu wa elimu (Mwanzo 4:20-22) lakini pia Hodari na wengine wao wenye maumbo makubwa (Mwanzo 6:4),.  Kwahiyo sikuzote tunafahamu hata sasa walio na uwezo mkubwa wa kielimu na kiteknolojia si rahisi kuwaweza kivita, hata iweje. Tofauti na uzao wa Adamu kwa Sethi, walikuwa ni wakulima tu na wafugaji. Hawakuwa na ujuzi mwingi ijapokuwa walikuwa ni uzao wa Mungu.

Kwahiyo wana wa Kaini, waliitawala dunia, hawakuwa watu dhaifu dhaifu, na yoyote ambaye angejaribu kumuua mmojawapo, kisasi kingemrudia mara saba, kwa nguvu tu walizokuwa nazo, ijapokuwa hawakuwa na Mungu maishani mwao.

Ni kutufundisha nini?

Si jambo la ajabu Mungu kumuhakikisha ulinzi mtu mwovu, leo hii wengi watasema Bwana mbona wenye dhambi ndio wanaofanikiwa, mbona waovu ndio wenye nguvu duniani, wapo salama, ndio wenye mavumbuzi makubwa. Fahamu kuwa hiyo ni alama yao. Ambayo ilianzia tokea mbali kwa Kaini. Kwasababu wangekuwa waovu, halafu pia wanyonge, wangeishije kwenye hii dunia.

Kamwe usiitamani alama ya Kaini, usitamani kulindwa ndani ya uovu, kwasababu utadumu kwa kitambo tu, baadaye utaangamizwa kama ilivyokuwa kwa hawa, katika gharika. Yesu alitoa mfano wa magugu na ngano katika shamba, kama tunavyoifahamu ile habari, wale wakulima walitaka kwenda kuyang’oa magugu shambani ili waziache ngano. Lakini mwenye shamba akasema waache vyote vikue pamoja mpaka siku ya mavuno, ndipo yatakusanywa na kutupwa motoni.

Na tafsiri ya mfano ya ule mfano akasema shamba ni ulimwengu, na ngano ni wana wa ufalme, lakini magugu ni wana wa ibilisi, na wavunaji ni malaika. Kuonyesha duniani yapo mapando ya aina mbili, na yote yatashiriki mbolea, maji, matunzo yote kutoka kwa Mungu, na kimsingi magugu huwa ndio mepesi kustawi kwa haraka kuliko ngano.

Jiulize na wewe ambaye unastarehe katika dhambi na hauoni madhara yoyote, unaelekea wapi? Hujui umetiwa alama kwa muda, nguvu zako, utajiri wako, mafanikio yako, zaidi ya watu wa Mungu, usidhani ndio umebarikiwa unathamini na Mungu.  lakini wakati utafika kuzimu utaiona.  Embu kubali sasa kuwa mwana wa ufalme, kwa kumaanisha kutubu dhambi, na kumfanya Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako, ili akuondolee deni la dhambi uwe mtakatifu mbele zake kwa damu yake, akuepushe na hukumu inayokuja .

Ikiwa upo tayari kuokoka leo. Fungua hapa >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

Nitamjuaje nabii wa Uongo?

USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi wa kitabu cha Mithali ni nani?

SWALI: Mwandishi wa kitabu cha Mithali alikuwa nani?


Sulemani mwana wa Daudi, anajitaja mwenyewe kama mwandishi, katika mwanzo kabisa wa kitabu hiki

Mithali 1:1 Mithali za Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.2 Kujua hekima na adabu; kutambua maneno ya ufahamu

Kitabu hichi kinakadiriwa kuandikwa miaka mia tisa (900) kabla ya Kristo.Ni kitabu kilichojaa maneno ya hekima na kanuni, maagizo ya rohoni, vilevile maonyo mbalimbali yanayohusiana na maisha ya kawaida,  pamoja na maarifa na mafunzo yaliyo katika vitu vya asili.

Migawanyo yake:

Mithali 1-22:16, Iliandikwa na Sulemani mwenyewe.

Kuanzia Mithali 22:17-24:34, zilizojulikana kama kitabu cha Tatu, huwenda ziliandikwa na wengine lakini zikakusanywa na Sulemani mwenyewe.

Lakini Kuanzia Mithali 25-29, biblia inatuambia ziliandikwa na Sulemani, lakini watu wa mfalme Hezekia ndio waliozirekodi.

Na Mithali 30, Ambacho hujulikana kama kitabu cha Tano. Kiliandikwa na Aguri bin Yake.

Lakini Mithali 31 ambacho ni cha mwisho, kiliandikwa na mfalme Lemueli.

Japo wanazuoni wengine husema Aguri bin yake na Lemueli, yalikuwa  ni majina mengine ya Sulemani.

Kwa vyovyote, kitabu hichi kwa sehemu kubwa kimeandikwa na Sulemani. Ndio maana hujulikana kama kitabu cha Sulemani. Lakini pia hatuna uhakika asilimia zote  hekima zote ziliandikwa na yeye mwenyewe, kufuata na hao watu wawili wa mwisho wasiojulikana.

Kwa urefu wa chambuzi wa kitabu hichi fungua link hii >> VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)

Hizi ni baadhi ya fafanuzi ya hekima tuzisomazo katika kitabu hicho

Maana ya Mithali 21:17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini;

Fahamu maana ya Mithali 10:5 Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima; 

Fahamu maana ya Mithali 25:13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno; 

Nini maana ya Mithali 5:15-18 anaposema Unywe maji ya birika lako mwenyewe?

Nini maana ya  Mithali 21:1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana;

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! Sulemani alienda mbinguni?

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI

TAFUTA HEKIMA, MAARIFA, UFAHAMU NA BUSARA.

Print this post

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Wafalme

SWALI: Mwandishi wa kitabu cha Wafalme alikuwa nani?


Biblia haijaweka bayana aliyekuwa mwandishi wa kitabu hiki, lakini kufuatana na hadithi za kiyahudi huaminika kuwa nabii Yeremia ndiye alikuwa mwandishi wa vitabu hivi viwili vya wafalme.

Kitabu hichi kinaeleza kwa kina tawala za kifalme Kuanzia Mfalme Sulemani, na kugawanyika kwa  taifa la Israeli pande mbili, hadi kuanguka kabisa kwa taifa lote la Israeli  kwa kuchukuliwa  utumwani Ashuru na Babeli. Miongoni mwa Wafalme wapo waliosimama vema, lakini pia wapo wengi waliolikosesha taifa la Israeli, Wa kwanza alikuwa  ni Yeroboamu ambaye ndiye aliyeupokea ufalme uliogawanyika yeye aliunda  sanamu na kuzisimamisha kaskazini na kusini mwa Israeli, ili waisraeli wakamwabudu Mungu huko. Machukizo ambayo yaliendelea hivyo kwa muda mrefu, ijapokuwa zilikuja kuondolewa hizo sanamu na mfalme aliyeitwa Yosia, lakini bado hasira ya Mungu haikupoa kwa mambo mengi mabaya waliyokuwa wanayatenda wana wa Israeli, Hadi walipofikia hatua ya kuhamishwa.

Kwa urefu wa uchambuzi wa vitabu hivi waweza fungua hapa upate kujisomea  >>> VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 5

Bwana akubariki.

Je! Wewe umepokea wokovu wa Roho yako kwa Kristo Yesu? Kama ni la! Basi wakati ndio huu wa kufanya geuko la dhati, moyoni mwako. Ikiwa upo tayari basi fungua hapa kwa mwongozo huo>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WAFALME WALIOTAWALA ISRAELI.

Mwandishi wa kitabu cha Filemoni ni nani?

Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani?(Opens in a new browser tab)

Sala ya baraka (Hesabu 6:24-26).(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi wa kitabu cha Filemoni ni nani?

Mwandishi wa kitabu cha Filemoni

Kitabu cha Filemoni ni moja ya nyaraka ambazo mtume Paulo aliziandika akiwa kifungoni Rumi.  Waraka huu alimuandikia Filemoni mtu ambaye alimgeuza yeye mwenyewe katika injili yake. Baadaye akawa mtendakazi katika utumishi wa Bwana, katika nyumba yake mwenyewe. Na kuwa Baraka kwa watakatifu wengi huko Kolosai.

Filemoni 1:2 “na kwa Afia, ndugu yetu, na kwa Arkipo askari mwenzetu, na kwa kanisa lililo katika nyumba yako”

Kilichomsukuma hasaa mtume Paulo kuandika waraka huo ilikuwa ni kwa mtendakazi wake mpya aliyemzaa katika Kristo aliyeitwa Onesmo ambaye hapo mwanzo alikuwa ni mtumwa wa Filemoni aliyemwibia vitu vyake na kukimbia. Kwamba sasa ampokee na kumchukulia kama mtendakazi mwenzao, kwasababu ametubu na anafaa kwa utumishi. Kwa urefu wa mafunzo yaliyo ndani ya kitabu hichi cha Filemoni, Fungua hapa, ujifunze kwa kina >>>> MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA FILEMONI.

Je! Umempokea Kristo maishani mwako?

Kama ni la! Basi wakati ndio huu, bofya hapa kwa mwongozo wa namna ya kumpokea Kristo maishani mwako. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>   https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

NGUVU YA UPENDO WA KRISTO.

Mwandishi wa kitabu cha Zaburi ni nani?(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)

Maana ya Mithali 11:17 Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini wale askari walirudi nyuma, wakaanguka chini (Yohana 18:6)

Kijeshi kushindwa kumtambua adui yako mpaka adui yako anajitambulisha kwako tena mbele ya macho yako ni ishara kubwa ya kushindwa mapambano.

Ndivyo ilivyokuwa kwa wale askari, walipofika na ujasiri wao mwingi, wakiwa na wazo la kumkamata mlengwa wao, tunaona mambo yalikuwa ni tofauti, kwasababu viashiria na matarajio yaliyokuwa kichwani mwao, hayakuweza kumfunua ni nani miongoni mwao ndiye mlengwa, huwenda wengine walidhani hayupo amekimbilia mapangoni kama Daudi. Lakini Yesu baada ya kuona wanahangaika sana ndipo akawauliza mnamtafuta nani.. Na wao kwa ujasiri wakajibu Yesu Mnazareti.. Yesu akasema ni mimi hapa! Tusome;

Yohana 18:3-8

[3]Basi Yuda, akiisha kupokea kikosi cha askari na watumishi waliotoka kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, akaenda huko na taa na mienge na silaha.

[4]Basi Yesu, hali akijua yote yatakayompata, akatokea, akawaambia, Ni nani mnayemtafuta? 

[5]Wao wakamjibu, Ni Yesu Mnazareti. Yesu akawaambia, Ni mimi. Yuda naye aliyemsaliti alikuwa amesimama pamoja nao. 

[6]Basi alipowaambia, Ni mimi, walirudi nyuma, wakaanguka chini. 

[7]Basi akawauliza tena, Mnamtafuta nani? Wakasema, Yesu Mnazareti. 

[8]Yesu akajibu, Nimekwisha kuwaambieni ya kwamba ni mimi; basi ikiwa mnanitafuta mimi, waacheni hawa waende zao. 

Hivyo kibinadamu kwa taarifa hizo za ghafla nguvu lazima zikuishie, na kunyong’onyea ujikutapo kwenye mazingira kama hayo. Ni mfano tu wa ile habari ya Elisha (2Wafalme 6:8-23), Mfalme wa Shamu alituma majeshi kwenda kumkamata kwasababu alikuwa anatoa siri za ufalme wake kwa mfalme wa Israeli. Na hiyo ikapelekea washindwe sana mbele ya wayahudi. Lakini tunaona walipomfuata Elisha, alimwomba Mungu jeshi zima lipigwe upofu wasimtambue. Ndipo Elisha akalipeleka hilo jeshi katikati ya mji. Na baadaye akaomba wafumbiliwe macho, wakafumbuliwa wakagundua kumbe adui yao ndiye aliyekuwa kiongozi wao wa mbele. 

Nguvu ziliwaishia kujikuta katikati ya maadui zao, wakifahamu kinachofuata ni kifo. Lakini Elisha hakuagiza wauliwe, bali aliwaombea kwa mfalme wapewe chakula wale wanywe kisha waondoke. Ndipo walipoondoka, hawakurudi tena kuwasumbua Israeli kwa kipindi kirefu. Kwasababu waliwapaliwa makaa ya moto kichwani.

Inamfunua Kristo kwa wakati ule, maadui zao walipofika pale bustanini, hakuwaua kwasababu alikuwa na uwezo huo, lakini alipokatwa sikio, mmojawapo wa wale askari alikuwa radhi kumponya, (kumfanyia huduma). 

Na zaidi sana alikuwa tayari kuondoka na wale askari kuuawa nao, jambo ambalo Elisha hakufanya. Ili tu yeye afe taifa zima lipone..ni upendo wa namna gani huu usioweza kuelezeka aliuonyesha!.

Na kwa kifo chake hawakupona wayahudi tu, bali mpaka ni sisi watu wa mataifa kwa vizazi vyote, tumepona. Utukufu na heshima ni zake milele na milele.

Kwa hitimisho ni kuwa wale askari waliorudi nyuma wakaanguka chini, haikuwa bure hure, yote hiyo ilikuwa ni kufuatana na mwitikio wa Yesu kwao ambao hawakuutazamia. 

Ni kutufundisha kuwa mawazo ya Mungu, sio mawazo yetu, rehema zake na fadhili zake na huruma zake ni nyingi kiasi ambacho kinaweza kumfanya mwanadamu aanguke na kutetemeka, kwa mwitikio wake mkuu wa upendo kwa wenye dhambi.

Je! Umempokea Kristo? Kumbuka lengo lake ni kukuvuta ili usiangukie hukumu. Okoka leo

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Swali: Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.

Nini maana ya “Uweza wa kifalme utakuwa begani mwake” (Isaya 9:6)?.

Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?(Opens in a new browser tab)

(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?

Waraka wa kwanza na ule wa pili wa timotheo,mtume Paulo aliuandika akiwa gerezani kama mfungwa Rumi.

Kwa urefu wa maelezo ya nyaraka Paulo alizoziandika akiwa gerezani, fungua hapa >>> Je ni nyaraka zipi mtume Paulo aliziandikia gerezani?

Lakini swali linakuja je Timotheo alikuwa wapi kwa wakati huo nyaraka hizo mbili zinaandikwa. Jibu ni  kwamba alikuwa Efeso. Tunalithibitisha hilo kwa maneno ya Paulo mwenyewe. Tusome;

1Timotheo 1:3 Kama vile nilivyokusihi ukae Efeso, nilipokuwa nikisafiri kwenda Makedonia, ili uwakataze wengine wasifundishe elimu nyingine;

Amen

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Vihekalu vya fedha vya Artemi vilikuwaje? (Matendo 19:24).

MAMBO NANE (8), AMBAYO WEWE KAMA KIONGOZI UTAIGWA.(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)

Maana ya Mithali 11:17 Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Wagerasi ni nchi gani? (Luka 8:26-39)

Wagerasi ni watu waliokuwa wanaishi katika mji ulioitwa Gerasi ambao ulikuwa kusini mashariki mwa bahari ya Galilaya. (Tazama kwenye picha)

Ulikuwa ni moja ya miji ya Nchi ya Dekapoli. Nchi ya watu wa mataifa.

ndio kule ambako Yesu alivuka na kukatana na wale watu waliokuwa vichaa wakali, akawafungua.

Marko 5:1-3

[1]Wakafika ng’ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi. 

[2]Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu; 

[3]makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo; 

Urefu wa habari hii fungua hapa >>ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Mathayo 8:28-34, na Luka 8:26-39.

Ni nini ambacho Bwana anataka tujifunze kwa hawa wagerasi? 

Ni watu ambao walithamini, hazina zao, mali zao, utajiri wao, zaidi ya kufunguliwa kwao, ndio maana mara tu walipoona nguruwe wao wamekufa wote, jambo hilo liliwafanya wawe na hofu, na hiyo ikawapelekea kumsihi Yesu aondoke katika nchi yao, asije akaleta hasara zaidi.

hawakuona wokovu ule mkuu uliowafikia, waliona hasara waliyopata. Hiyo ni mbaya sana,  kwa urefu ya jambo hilo pitia hili somo.

Kamwe usiwe mgerasi.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine: 

HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI.

Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

Nini maana ya huu mstari? “Yeye mwenyewe ataokolewa lakini ni kama kwa moto”

Rudi Nyumbani

Print this post