Title August 2020

Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?

Mto Frati upo nchi gani,  na Umuhimu wake katika biblia ni upi, kwanini utajwe sana?


Mto Frati ni moja ya mito mikubwa na mirefu iliyopo Mashariki ya kati, Mto mwingine ukiwa ni Hidekeli (Tigris), mto huu unaanzia Uturuki na kutoka hapo unakatiza katika nchi ya  Syria na Iraq na kwenda kumwaga maji yake katika Ghuba ya uajemi.

Tazama picha.

Mto Frati na mto Hidekeli 

Mto Frati na Mto Hidekeli (Tigris) ni moja ya mito minne ambayo inatajawa kwenye biblia ilikuwa inatoa maji katika bustani ya Edeni.

Mwanzo 2:10 “Ukatoka mto katika Edeni wa kuitilia bustani maji, na kutokea hapo ukagawanyika kuwa vichwa vinne.

11 Jina la wa kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Havila, ambako kuna dhahabu;

12 na dhahabu ya nchi ile ni njema; huko kuna bedola, na vito shoham. 13 Na jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi.

14 Na jina la mto wa tatu ni Hidekeli; ndio unaopita mbele ya Ashuru. Na mto wa nne ni Frati”.

Lakini kingine cha kushangaza juu ya  mto Frati ni kuwa umetajwa pia  kitabu cha Ufunuo, Kama tu vile Babeli ilivyotajwa tangu kwenye kitabu cha Mwanzo hadi  Ufunuo. Kuonyesha kuwa kama vile ilivyo Babeli ya mwilini, hivyo hivyo pia ipo Babeli ya rohoni (Ufunuo 17 & 18). Halikadhalika na kwa mto Frati, sio tu ule unaouna pale Mashariki ya kati, hapana bali pia rohoni upo, na siku moja utakauka, na ukishakauka basi dunia itaingia katika vita kuu ya Tatu ya dunia

Ufunuo 9:14 ikimwambia yule malaika wa sita aliyekuwa na baragumu, Wafungue nao malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Frati.

15 Wale malaika wanne wakafunguliwa, waliokuwa wamewekwa tayari kwa ile saa na siku na mwezi na mwaka, ili kwamba waue theluthi ya wanadamu.

16 Na hesabu ya majeshi ya wapanda farasi ilikuwa elfu ishirini mara elfu kumi; nilisikia hesabu yao.

17 Hiyo ndivyo nilivyowaona hao farasi katika maono yangu, nao waliokaa juu yao, wana dirii kifuani, kama za moto, na za samawi, na za kiberiti; na vichwa vya farasi hao ni kama vichwa vya simba, na katika vinywa vyao hutoka moto na moshi na kiberiti.

18 Theluthi ya wanadamu wakauawa kwa mapigo matatu hayo, kwa moto huo na moshi huo na kiberiti hicho, yaliyotoka katika vinywa vyao.

19 Kwa maana nguvu za hao farasi ni katika vinywa vyao, na katika mikia yao; maana mikia yao ni mfano wa nyoka, ina vichwa, nao wanadhuru kwa hivyo”.

Unaona?. Watu wengi hawajui kuwa kipindi hicho kimekaribia sana,. Lakini kabla hilo halijatokea, kutatungulia kwanza Tukio la UNYAKUO, (kufahamu vizuri unyakuo utakuwaje kuwaje, tazama, masomo yaliyoorodheshwa chini).

Dalili zote zinaonyesha kizazi chetu kitaweza kushuhudia mambo hayo yote. Swali la kujiuliza Je! na wewe umejiwake tayari kwa tukio la kurudi kwa pili kwa Yesu Kristo? Je! Maisha yako yanauhakisi wokovu? Kama sivyo basi jitathimini sasa kwasababu ni kipindi kifupi cha neema tulichobakiwa nacho, Dunia hii inapumbaza kweli na wengi hawalijui hilo, Yesu atakuja kama mwivi usiku.

 Hivyo kama upo tayari kumpa Yesu leo maisha yako, hilo jambo la muhimu sana, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

 Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo ya Neno la Mungu  kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye  namba hii +255 789001312

Tazama chini vichwa vingine vya masomo.

Mada Nyinginezo:

MTO YORDANI UKO NCHI GANI KWA SASA?

MTO YORDANI UKO NCHI GANI KWA SASA?

UFUNUO: Mlango wa 9.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

MAONO YA NABII AMOSI.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

MTO YORDANI UKO NCHI GANI KWA SASA?

Mto Yordani uko nchi gani kwa sasa duniani?


Mto Yordani upo katika eneo la Mashariki ya kati, ni mto ambao unasimama kama mpaka wa mataifa mbalimbali, Ikiwemo Lebanoni, Syria, Israeli, na Yordani.

Ni kama vile ziwa Tanganyika lilivyo simama kama mpaka wa nchi 4, Congo, Burundi, Tanzania, na Zambia ndivyo ilivyo hata na kwa mto Yordani,

Nchi ya Yordani, unayoisikia leo hii pale mashariki ya kati, imechukua jina lake kutoka katika mto huu.

Mto huu chanzo chake ni kwenye chemchemi kadhaa zinazotiririka kutoka katika mlima Hermoni ulio mpakani mwa Lebanoni na Syria.Kisha kutoka hapo unateremsha maji yake mpaka Israeli kwenye bahari ya Galilaya/Tiberia/Genesareti. Na kutoka hapo unaibukia upande wa pili na kuendelea na safari yake moja kwa moja mpaka bahari ya Chumvi.

Tazama picha chini.

Chanzo cha mto Yordani Mashariki ya kati

Mto huu, umekuwa kitovu katika historia ya Israeli kuanzia agano la kale mpaka agano jipya. Yoshua aliusimamisha mto huu na wana wa Israeli wakavuka kuelekea Yeriko.

Vilevile mto huu huu katika agano jipya ndio makutano mengi yalikuwa yanavuka kumwendea Yesu ili waponywe.(Mathayo 19:1-2),  Na ni mto ambao Yesu mwenyewe  alibatiziwa.

Kuonyesha kuwa ili nawe upate wokovu na ushindi dhidi ya maadui zako,na ili uponywe nafsi yako, ni lazima Uvuke Yordani yako ya Rohoni..Ili ukakutane na Yesu ng’ambo ya pili huna budi kuvuka Yordani, Na Unavukaje Yordani? Ni kwa kubatizwa, kama Yesu alivyobatizwa kwenye mto ule.

Hivyo na wewe sharti ukishamwamini Yesu moja kwa moja ukabatizwe, mahali popote penye maji tele kama ishara ya kuwa umeokoka kweli kweli. Na kuwa unakwenda kuwashinda maadui zako.

Marko 16:16 “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.

Wengi wanapuuzia maagizo haya ya msingi, wanadhani kuamini tu inatosha, Ndugu kubatizwa ni tendo lenye maana kubwa sana kwako rohoni, aliyetupa maagizo hayo hakuwa amekosa cha kutuagiza bali alijua umuhimu wake.

Swali Nji wewe umebatizwa ipasavyo? Kama sivyo basi kafanye hivyo.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda masomo yetu yawe yanakufikia njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Israeli ipo bara gani?

Wafilisti ni watu gani.

 

MJUMBE WA AGANO.

Zile mbao mbili za mawe Musa alizoambiwa achonge zilikuwaje?

Mlima sinai upo nchi gani? Na Je unaijua Sinai yako ya rohoni?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mlima sinai upo nchi gani? Na Je unaijua Sinai yako ya rohoni?

Mlima sinai upo nchi gani? Na Je unaijua Sinai yako rohoni?


Mlima Sinai, au kwa jina lingine unajulikana kama Mlima Horebu, upo katika Rasi ya Sinai, Nchi ya Misri..Tazama katika picha.

sinai

Mlima huu, ni mlima ambao Mungu aliutumia kuwapa wana wa Israeli Torati na zile Amri 10. Ni mlima ambao wana wa Israeli waliutazama kwa muda mrefu kama mlima ambao unamtambulisha Mungu yupoje pale anapotaka kuzungumza na watu wake. Kufuatana na mstari huu;

Kutoka 19:16 “Ikawa siku ya tatu, wakati wa asubuhi, palikuwa na ngurumo na umeme, na wingu zito juu ya mlima, na sauti ya baragumu iliyolia sana. Watu wote waliokuwa kituoni wakatetemeka.

17 Musa akawatoa hao watu katika kituo, akawaleta ili waonane na Mungu; wakasimama pande za chini za kile kilima. 18 Mlima wa Sinai wote pia ukatoa moshi, kwa sababu Bwana alishuka katika moto; na ule moshi wake ukapanda juu kama moshi wa tanuu, mlima wote ukatetemeka sana.

19 Na hapo sauti ya baragumu ilipozidi kulia sana, Musa akanena, naye Mungu akamwitikia kwa sauti.

20 Bwana akaushukia mlima, juu ya kilele cha mlima; Bwana akamwita Musa aende hata kilele cha mlima; Musa akapanda juu”.

Unaona, wana wa Israeli walijiundia picha kuwa siku zote Mungu akishuka mahali kuzungumza na mtu/watu ni lazima kuwe na moto, na matetemeko, na upepo mkali n.k. .

Eliya naye alidhani vivyo hivyo, wakati mmoja alipokuwa anamkimbia Yezebeli, alienda kwenye mlima huu wa Musa, mlima Sinai (Horebu) kwa ajili ya kukutana na Mungu, Na yeye akidhani kuwa ili Mungu ashuke mahali Fulani ni lazima uwepo moto, na matetemeko ya ardhi. Lakini siku hiyo alipokwenda kwenye mlima huo ndio alijua ukweli wote wa Mungu.

Ni kweli kama ilivyo ada, Mungu alijifunua kwake kama alivyojifunua kwa Musa na Wana wa Israeli kwa radi, mingurumo n.k. Lakini Eliya aligundua mbona bado simwona MUNGU?

1Wafalme 19:8 “Akainuka, akala, akanywa, akaenda katika nguvu za chakula hicho siku arobaini mchana na usiku hata akafika Horebu, mlima wa Mungu.

9 Akafika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la Bwana likamjia, naye akamwambia, Unafanya nini hapa, Eliya?

10 Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu, waiondoe.

11 Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za Bwana. Na tazama, Bwana akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunja-vunja miamba mbele za Bwana; lakini Bwana hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini Bwana hakuwamo katika lile tetemeko la nchi;

12 na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu.

13 Ikawa, Eliya alipoisikia, alijifunika uso wake katika mavazi yake, akatoka, akasimama mlangoni mwa pango. Na tazama, sauti ikamjia, kusema, Unafanya nini hapa, Eliya”?

Unaona Eliya alipoisia tu ile sauti ya utulivu na upole. Hapo ndipo alipousikia uwepo wa Mungu ukibubujika ndani yake akajua sasa Mungu ameshuka kuzungumza na mimi.. Hapo ndipo alipofahamu  kuwa Mungu hakai katika milima, hakai katika tufani, hakai katika upepo wa kisulisuli, bali katika utulivu na upole.

Vivyo hivyo na wewe leo hii unahitaji kumwona Mungu, unahitaji kukutana na Mungu katika Sinai, yako..Basi jifunze kujinyenyekeza mbele zake, kaa katika utulivu mkubwa wa Roho, huku ukijifunza kanuni za Mungu katika maandiko, na hakika atajifunua kwako zaidi hata ya alivyojifunua kwa wana wa Israeli. Mungu ni mnyenyekevu na hivyo anajifunua kwa wanyenyekevu kwake, wanaolitii Neno lake.

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Israeli ipo bara gani?

Neno Korbani linamaanisha nini? (Marko 7:11)

SAYUNI ni nini?

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Neno Korbani linamaanisha nini? (Marko 7:11)

SWALI: Neno “Korbani” linalozungumziwa katika Marko 7:11 lina maana gani?


JIBU: Ili tupate picha nzuri ya Neno hilo embu tusome sehemu zote mbili zinazozungumzia jambo hilo hilo moja.

Mathayo 15 :1-6

1 “Ndipo Mafarisayo na waandishi toka Yerusalemu walipomwendea Yesu wakisema, 

2 Mbona wanafunzi wako huyahalifu mapokeo ya wazee, kwa maana hawanawi mikono walapo chakula. 

3 Akajibu, akawaambia, Mbona ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu? 

4 Kwa kuwa Mungu alisema, Mheshimu baba yako na mama yako, na Amtukanaye baba yake au mama yake kufa na afe. 

5 Bali ninyi husema, Atakayemwambia babaye au mamaye, Cho chote kikupasacho kusaidiwa na mimi ni wakfu, 

6 basi asimheshimu baba yake au mama yake. Mkalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu”.

Marko 7:8-13 

“8 Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu. 

9 Akawaambia, Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu. 

10 Maana Musa alisema, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Amtukanaye babaye au mamaye kufa na afe. 

11 Bali ninyi husema, Mtu akimwambia babaye au mamaye, NI KORBANI, yaani, wakfu, kitu changu cho chote kikupasacho kufaidiwa nacho, huwa basi; 

12 wala hammruhusu baada ya hayo kumtendea neno babaye au mamaye; 

13 huku mkilitangua neno la Mungu kwa mapokeo yenu mliyopokeana; tena mwafanya mambo mengi yaliyo sawasawa na hayo.

Kama tunavyosoma hapo, biblia imeshatoa tafsiri ya hilo Neno Korbani mbele  kidogo kuwa linaamanisha WAKFU.

Kitu chochote kilichowekwa wakfu ina maana kuwa hakitumiwi kwa mtumizi mengine yoyote isipokuwa kwa Mungu tu. Sasa katika habari hiyo, utaona Bwana Yesu alikuwa anawelenga sana sana Mafarisayo na waandishi kwa unafki wao kwa kujifanya kuwa wanaishika torati yote, wakati yapo mambo mengine mengi ya torati walikuwa wanayakaidi.

Na ndio hapo Bwana Yesu akawatolea mfano mmojawapo, ambao ulihusu  kuwaheshimu wazazi, kama mojawapo ya amri ambazo Mungu alizitoa zishikwe na watu wote. Na biblia iliposema kuwaheshimu wazazi, ilikuwa sio tu kuwaonyeshea heshima na utiifu, hapana ilikuwa ni zaidi ya hapo ikiwemo kuwahudumia kifedha, hususani wakiwa wazee.

Sasa hawa waandishi walikuwa wanayapindisha hayo maagizo, kwa kuwashurutisha watu, kuepuka majukumu yao ya kuwahudumia wazazi wao, kinyume chake walikuwa wanawaambia hayo wanayoyapata kwa ajili ya wazazi  wanaweza tu kuyafanya kuwa wakfu(Korbani) mbele za Mungu,  na ikawa ni sawa tu na kama wamewahudumia wazazi wao, isiwe dhambi mbele za Mungu.

Hivyo kama mtu alikuwa ametenga fedha yake kiasi kwa ajili ya matumizi ya baba yake au mama yake kule kijijini, basi walihimiziwa walizete Hekaluni kwa ajili ya Mungu kama wakfu..

Na mzazi akimuuliza, mbona huniletei matumizi, basi Yule kijana atasema, fedha hii au nafaka hii  niliyoivuna ni wakfu kwa Mungu.

Hivyo watu wengi wakawa wanawaacha wazazi wao katika hali ya shida na umaskini wa hali ya juu. Jambo ambalo Mungu hakuliagiza.

Ndipo Yesu anawakemea hawa waandishi kwa kuyapindua maagizo ya Mungu, ya kutotimiza majukumu yao ya kuwahudumia wazazi  kwa kanuni zao walizojitungia.

Nini tunajifunza?

Kumbuka biblia haifundishi watu wakimbie majukumu yao ya kifamilia kwa wazazi wao hususani pale wanapokuwa wazee kwa kisingizio kuwa wanamtolea Mungu.. Biblia inasema usipowahudumia watu wa nyumbani kwako, wewe ni kuliko hata mtu asiyeamini(1Timotheo 5:8).. Lakini pia biblia haifundishi kuwa watu waache kumtolea Mungu kwa kisingizio kuwa wanayo majukumu mengi ya kifamilia.

Lazima ujue kila utoaji una sehemu yake, na Baraka zake. Watu wa nyumbani kwako wana sehemu yao, maskini wana sehemu yao, na Mungu pia anayosehemu yake..Usipojua hilo utakuwa nawe pia unatangua torati kwa kufuata mawazo yako mwenyewe uliyojitungia. Kwasababu wapo watu wengi leo hii, wameacha kupeleka fedha zao kanisani, au kwenye huduma za Mungu, wanasema sitoi sadaka yangu, na ukiwauliza ni kwanini?, wanasema mbona hatuoni zikienda kuwahudumia maskini na wajane kama ilivyokuwa katika kanisa la kwanza la mitume…Lakini mtu huyo huyo hajui kuwa watakatifu wa kanisa la kwanza sio kama hawa wa sasahivi, wale walikuwa wapo tayari kuuza mashamba yao na viwanja vyao na kuleta kwa Mungu, hivyo kwa namna ya kawaida nishati ya kutosha ni lazima iwepo nyumbani kwa Mungu hata kuwahudumia mpaka wajane.

Lakini kama wewe unampelekea Mungu shilingi, wakati hiyo fedha hata gharama za umeme kanisani hazijitoshelezi, unapata wapi ujasiri wa kutaka kujua mfuko wa kanisa unatumikaje?? Fikiria tu. Je wewe unaweza kuuza shamba lako kule kijijini, umletee Mungu?

Bwana atusaidie,. 

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.

MIJI YA MAKIMBILIO.

JE KUVAA PETE NI DHAMBI?

MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.

YOTE NAMTOLEA YESU_Tenzi za Rohoni.

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Historia ya wimbo wa tenzi – Ndio dhamana Yesu wangu

Historia ya wimbo wa tenzi – Ndio dhamana Yesu wangu. (Blessed assuarance)


Wimbo huu ulindikwa na mwanamke mmoja aliyeitwa Fanny Crosby, Mwanamke huyu japo aliishi kwa miaka 95 akiwa kipofu,lakini hakuacha kuitumia neema Mungu aliyompa kutangaza injili kwa njia ya Nyimbo zenye muundo wa Tenzi za rohoni na nyinginezo, katika maisha yake alifanikiwa kuandika nyimbo zaidi ya 8000, Na hii nyimbo  “Ndio dhamana Yesu wangu” Ikiwa mojawapo, Nyingine inayojulikana sana mpaka leo ni “Usinipite mwokozi” yeye pia ndio aliyeiandika nyimbo hii alipokuwa amewatembelea wafungwa gerezani(angalia historia yake chini).

Phoebe Knapp

Phoebe Knapp

Sasa Siku moja  alipokuwa amemtembelea rafiki yake nyumbani kwake  aliyeitwa Phoebe Knapp, ambaye alikuwa ni mtunzi wa sauti za nyimbo, wakiwa  nyumbani kwake Phoebe alianza kupiga mdundo wake aliokuwa ameutunga, kisha baada ya muda alimuuliza Fanny, Je unaweza kuniambia mdundo huu ni wa nyimbo gani?

Ndipo Fanny akamwambia “Ndio dhamana Yesu wangu”. Basi hapo ndio pakawa mwanzo wa mdundo na utunzi wa wimbo huo (1873).

Ndio dhamana Yesu wangu.

Ndiyo dhamana, Yesu wangu;
Hunipa furaha za mbingu;
Mrithi wa wokovu wake,
Nimezawa kwa Roho wake.
 
Habari njema, raha yangu,
Yesu ndiye Mwokozi wangu,
Habari njema, raha yangu,
Yesu ndiye Mwokozi wangu.
 
Kumsalimu moyo wangu,
Mara namwona raha yangu;
Aniletea malaika,
Wananilinda, tutaokoka.
 
Habari njema, raha yangu,
Yesu ndiye Mwokozi wangu,
Habari njema, raha yangu,
Yesu ndiye Mwokozi wangu.
 
Sina kinyume; nashukuru,
Mchana kutwa huja kwangu;
Usiku kucha kuna nuru;
Mwokozi wangu; ndimi nuru.
 
Habari njema, raha yangu,
Yesu ndiye Mwokozi wangu,
Habari njema, raha yangu,
Yesu ndiye Mwokozi wangu.
 
Hali na mali; anitwaa!
Mara namwona anifaa,
Nami nangonja kwa subira;
Akiniita, nije mara.
 
Habari njema, raha yangu,
Yesu ndiye Mwokozi wangu,
Habari njema, raha yangu,
Yesu ndiye Mwokozi wangu.

*****

Uimbapo wimbo huu  kumbuka ni kipofu ndiye aliyeuandika, nawe pia unaposema “Ndio dhamana Yesu wangu” Basi awe kweli  wokovu wako. Mpende yeye bila unafki na kumtumikia kwasababu ndiye aliyekufa kwa ajili yako.

Je! Umeokoka? Unajua kuwa Unyakuo upo karibu sana, kwasababu tunaishi katika kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia? Na kwamba hatutakuwa na kanisa lingine zaidi ya hili? Siku hizi zimekwisha, Hivyo kama upo tayari kumpa Yesu maisha yako leo ili wimbo huu uwe na maana kweli kwako. Basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye  namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

USINIPITE MWOKOZI Lyrics

YOTE NAMTOLEA YESU_Tenzi za Rohoni.

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

CHA KUTUMAINI SINA lyrics

KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

MPINGA-KRISTO

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

UFUNUO: Mlango wa 1

Rudi Nyumbani:

Print this post

YOTE NAMTOLEA YESU_Tenzi za Rohoni.

Yote namtolea Yesu_tenzi za rohoni|Swahili hymn.


Wimbo huu uliandikwa na ndugu mmoja wa kimarekani aliyeitwa Judson W. Van DeVenter, Ndugu huyu alilelewa katika mazingira ya kikristo, aliokoka akiwa na miaka 17, kuanzia huo wakati wito wa kujitoa kikamilifu ulianza  kuita ndani yake,lakini bado hakufanya uamuzi huo. DeVenter alifanikiwa kusoma  mpaka chuo kikuu na kutunikiwa shahaba ya Sanaa, aliajiriwa kama mwalimu na mwongozaji katika shule za sanaa, hiyo ilimfanya aweze kusafiri sehemu nyingi mbalimbali katika bara la Ulaya kutokana na kazi yake ya sanaa.

Zaidi ya hilo alisomea pia na kufundisha elimu ya muziki, ilimchukua miaka 5 mpaka “Kumtolea yote Yesu”, Na hiyo ilikuwa ni baada ya marafiki zake kumshawishi sana, aingie katika kazi ya kumtumikia Mungu.

Mwaka 1896 Siku moja alipokuwa anafanya huduma ya muziki katika kanisani, hii ndio siku aliyoamua kuyasalimisha maisha yake ya ki-utumishi moja kwa moja kwa Kristo akiwa na miaka 41, aliamua kujitoa moja kwa moja kwa ajili ya kuifanya kazi ya unjilisti, na ndipo hapo huu wimbo “Yote namtolea Yesu” ulipozaliwa ndani ya moyo wake.

YOTE WA YESU.

Yote Namtolea Yesu.
Nampa moyo wote,
Nitampenda siku zote,
Namwandama kila saa.
 
Yote kwa Yesu,
Yote kwa Yesu,
Yote kwako, Ee Mwokozi,
Natoa sasa.
 
Yote namtolea Yesu,
Nainamia pake;
Nimeacha na anasa,
Kwako Yesu nipokee
 
Yote kwa Yesu,
Yote kwa Yesu,
Yote kwako, Ee Mwokozi,
Natoa sasa.
 
 Yote namtolea Yesu,
Nifanye niwe wako;
Nipe Roho yako, Bwana,
Anilinde daima,
 
Yote kwa Yesu,
Yote kwa Yesu,
Yote kwako, Ee Mwokozi,
Natoa sasa.
 
Yote namtolea Yesu,
Nami naona sasa;
Furaha ya ukombozi;
Nasifu jina lake. 
 
Yote kwa Yesu,
Yote kwa Yesu,
Yote kwako, Ee Mwokozi,
Natoa sasa.

*****

Je! Na sisi tunapouimba wimbo huu tunaweza kumtolea Yote Yesu?. Je! mali zetu tunaweza kumpa yeye, nguvu zetu tunaweza kuzielekeza kwake?, akili zetu tunaweza kuzitumia ziitende kazi ya Mungu? Kama sivyo basi wimbo huu tutauimba kinafki.

Bwana atutupe kutambua hayo.

Shalom.

Je! Umeokoka? Ikiwa bado hujaokoka na unahitaji kuokoka leo, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA


Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo mbalimbali ya Neno la Mungu, kwa njia ya whatsapp yako, basi tutumie ujumbe kwa namba hii :+255 789001312

Mada Nyinginezo:

YESU KWETU NI RAFIKI

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

MAONO YA NABII AMOSI.

 

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAANA YA KRISTO/ JINA KRISTO LINA MAANA GANI?

Neno Kristo, na Masihi ni kitu kimoja, isipokuwa kwa lugha ya Kiebrania linatamkwa kama Masihi, lakini kwa lugha ya kigiriki linatamkwa kama Kristo.

Yohana 1:41 “Huyo akamwona kwanza Simoni, ndugu yake mwenyewe, akamwambia, Tumemwona Masihi (maana yake, Kristo)”.

Hivyo Neno hili Kristo/Masihi linamaanisha mtiwa mafuta.

Mtiwa mafuta ni mtu yeyote aliyechaguliwa au aliyetengwa na Mungu kuwa wakfu kwa ajili ya kutimiza kusudi lake Fulani..Aidha na kuokoa, au kutawala, au kuchunga.

> Hivyo manabii wote unaowasoma katika biblia walikuwa ni masihi au Kristo kwa Mungu, kwa lengo la kuitabiria Israeli, na kuwaelekeza maagizo yatokayo kwa Mungu.

1Nyakati 16:22 “Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu”.

> Makuhani wote tunaowasoma katika biblia walikuwa ni masihi au maKristo wa Bwana wakifanya kazi ya upatanisho wa dhambi za watu na makosa yao.

> Waamuzi wote unaowasoma katika biblia walikuwa ni masihi wa Bwana waliotiwa mafuta kwa lengo la kuwakomboa wanadamu.Wakina Gideoni, Samsoni, Yeftha wote hao walikuwa ni masihi wa Bwana.

> Vilevile wafalme wote iwe ni wa wale waliotoka Israeli, au hawajatoka Israeli tunaowasoma katika biblia walikuwa ni masihi wa Bwana kwa ajili ya kuwaongoza watu wake.

1Samweli 24:5 “Lakini halafu, moyo wake Daudi ukamchoma, kwa sababu amekata upindo wa vazi lake Sauli.

6 Akawaambia watu wake, Hasha! Nisimtendee bwana wangu, masihi wa BWANA,neno hili,kuunyosha mkono wangu juu yake,kwa maana yeye ni masihi wa BWANA”.

 

Isaya 45:1 “Haya ndiyo Bwana amwambiayo Koreshi, masihi wake,ambaye nimemshika mkono wake wa kuume,ili kutiisha mataifa mbele yake,name nitalegeza viuno vya wafalme;ili kufungua milango mbele yake,hata malango hayatafungwa.

2 Nitakwenda mbele yako, na kupasawazisha mahali palipoparuza; nitavunja vipande vipande milango ya shaba, na kukata-kata mapingo ya chuma”;

Lakini hao wote walikuwa ni kivuli cha MASIHI/KRISTO MKUU NA HALISI atakayekuja, ambaye alitiwa mafuta mengi sana yasiyoelezeka kuliko wote, biblia inasema hivyo, na huyo si mwingine zaidi ya YESU.

Waebrania 1:8 “Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,Mungu,ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.

9 Umependa haki, umechukia maasi; KWA HIYO MUNGU, MUNGU WAKO, AMEKUTIA MAFUTA, MAFUTA YA SHANGWE KUPITA WENZIO”.

Na ndio maana haitwi tu Yesu peke yake, bali anaitwa YESU KRISTO.

Yesu Kristo ametiwa mafuta ya mengi sana ya kuwakomboa wanadamu. Yeye anayo mafuta yote ya kikuhani ndani yake, anayo mafuta ya kifalme ndani yake, anayo mafuta ya kinabii ndani yake, anayo mafuta ya kichungaji ndani yake.. Yaani kwa ufupi mafuta yote ya karama za Mungu yapo ndani yake.

Hivyo mtu akimwamini Yesu, basi amepata kila kitu, ikiwemo ukombozi wa roho yake.

Lakini tahadhari ni kuwa biblia imetabiri kuwa siku za mwisho kutatokea makristo wengi wa uongo ili kuwadanganya watu wengi.

Mathayo 24:24 “Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule.

25 Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele”.

Kumbuka anasema watatokea makristo, hasemi ma-yesu, ikiwa na maana kuwa watakuwa ni watiwa mafuta lakini ni watiwa mafuta ya uongo, watakuwa wanaweza kweli wakawaombea watu kwa jina la Yesu na wakapona lakini injili yao ni injili potofu isiyoweza kumwokoa yeye, wala hao anaowaongoza.

Na ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Hivyo je! Swali na  wewe umechukuliwa na hili wimbi la makristo wa uongo?

Tunaishi katika wakati mgumu na wa hatari kuliko yote katika historia, hivyo kama maisha yako yapo mbali na Kristo basi ujue upo hatarini sana kupotezwa.

Kwanini usimpe Kristo leo maisha yako ayabadilishe, kisha yeye mwenyewe akupe Roho wake Mtakatifu atakayekusaidia kuijua kweli yote ya kimaandiko, ambaye atakaa ndani yako kukulinda mitego yote ya ibilisi?. Kama leo upo tayari kufanya hivyo, na unasema sitaki tena maisha ya dhambi nataka Yesu aniokoe awe peke yake masihi ndani yangu. Basi fungua link hii kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

UPAKO NI NINI?

KUWA MWAMINIFU KWA MANENO YAKO MWENYEWE,

AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.

Yakobo alikuwa na watoto wangapi?

REKEBISHA YAFUATAYO ILI MAMBO YAENDE SAWA.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU UPENDO.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUWA MWAMINIFU KWA MANENO YAKO MWENYEWE,

Kuwa mwaminifu kwa maneno yako mwenyewe, ni muhimu sana!.


Jina la Bwana wetu Yesu libarikiwe. Karibu tujifunze biblia.

Mwinjilisti mmoja alichukuliwa katika maono mbinguni akakutana na Bwana Yesu, alionyeshwa mambo mengi yatakayotokea baada ya Maisha haya, kwa wema na waovu, lakini Pamoja na hayo kuna mambo mengine aliambiwa ambayo naamini leo tukiyatafakari yatatusaidia.

Na jambo mojawapo aliloambiwa lilikuwa ni kuhusu “uaminifu”…kulingana na maelezo yake, anasema Bwana Yesu alimwambia haya maneno;

Neno langu ni nguvu inayoshikilia vitu vyote. Kwa kiwango ambacho unavyoamini Neno langu ni kweli, ndivyo unavyoweza kufanya vitu vyote. Wale ambao wanaamini kwamba maneno Yangu ni kweli, basi watakuwa pia wakweli kwa maneno yao wenyewe, Ni asili yangu kuwa kweli, na uumbaji huliamini Neno Langu kwa sababu mimi ni mwaminifu na kwake.

Wale ambao ni kama mimi, pia huwa ni wakweli kwa maneno yao wenyewe. Neno lao ni hakika, na ahadi zao ni za kuaminika. ‘ndio’ yao inamaanisha ‘NDIO!’ na ‘hapana’ yao inamaanisha ‘HAPANA!’. Ikiwa maneno yako mwenyewe sio kweli, ni lazima pia utaanza kutilia shaka maneno Yangu, kwa sababu udanganyifu uko moyoni mwako. Ikiwa wewe sio mwaminifu kwa maneno yako mwenyewe, ni kwa sababu bado hujanijua kabisa mimi ni nani, mimi ni mwaminifu kwa maneno yangu. Ili kuwa na imani, lazima uwe mwaminifu kwa maneno yako. Nimekuita utembee kwa imani kwa sababu mimi ni mwaminifu. Hiyo ni asili yangu”.

**mwisho**

Ndugu moja ya tatizo kubwa linalowakabili wakristo wengi wa sasa, ni kukosa UAMINIFU. Na uaminifu unaanza kwa mtu kukosa uaminifu kwa mambo yake mwenyewe kwanza. Kwamfano mtu baada ya kumpa Yesu Maisha yake, akaahidi kwamba hatasengenya tena, hatatukana, hataiba, hatafanya hichi au kile anaahidi pia atamtumikia Mungu, au atakuwa mtu wa kumtolea Mungu sana n.k..lakini baada ya muda kupita anaanza kwenda kinyume na kile alichokisema au alichokipanga. Ndugu hiyo ni hatari sana.

Maneno hayo ya mwinjilisti huyo aliyoambiwa na Bwana, nayaamini asilimia mia kuwa ni kweli. Hata katika hali ya kawaida kama huwezi kuwa mwaminifu kwa mali yako mwenyewe ni Dhahiri kuwa haiwezekani kuwa mwaminifu kwa mali ya mwingine. Kama kiatu chako mwenyewe hukitunzi wala hukijali utakijali vipi kiatu cha mwingine aliyekuazima ukivae kwa muda tu!. Uaminifu wa mtu unaanza kwa kile alichonacho yeye mwenyewe, ndipo aweze kuwa mwaminifu kwa kitu cha mwingine.

Kadhalika huwezi kuwa mwaminifu kwa Maneno ya Mungu, kama sio mwaminifu kwa maneno yako mwenyewe.

Katika Luka 16:10 Bwana Yesu alisema maneno haya..

“Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia”.

Hivyo tujifunze kuyashika maneno yetu wenyewe..Ndipo tutakapoona Neno la Mungu likiwa na nguvu juu ya maisha yetu… Ukisema sitaki hichi au kile!, au nataka hichi!..basi kishikilie hicho kweli kweli usiwe na mawazo mawili mawili… Hiyo nguvu ya Maamuzi ndio chanzo cha nguvu zako za kiroho. Hata likitokea jambo mbele yako, na ukanukuu mstari Fulani kwenye biblia kwa Imani, basi jambo lile ulilolitamka kufuatia mstari huo uliounukuu, litatimia kama ulivyolisema kwasababu wewe pia huwa ni mkweli katika maneno yako…Hivyo Mungu atahakikisha na yeye analifanya neno lake kuwa kweli juu yako. Lakini tusipokuwa wakweli kwenye maneno yetu, basi kuna uwezekano pia neno la Mungu lisiwe kweli juu yetu. Tunaweza tukalinukuu sana na tusiona matokeo yoyote.. kwasababu sisi wenyewe sio waaminifu.

Bwana atusaidie, na atubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Ni ipi tarehe sahihi Evil-merodaki alimtoa Yekonia gerezani?

 

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

ZABURI 91, NI ZABURI YENYE NGUVU NYINGI.

SABATO TATU NI NINI?

Je! Mtume Paulo alikuwa ni Mrumi, Myahudi au raia wa Tarso?

JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?

NA UPEPO WA KUSI ULIPOANZA KUVUMA KIDOGO,

Hakuna mtu anenaye katika Roho,kusema Yesu amelaaniwa

Rudi Nyumbani:

Print this post

IS THERE ANY IMPORTANCE OF PAYING THE TITHES?

Blessed be the name of our Lord Jesus Christ, Today we will learn very briefly about paying tithes, Scripturally tithes are the 10th part, of one’s income to God. So tithing is one of the types of offerings.

Before we go to deeper to learn about the importance of paying tithes, whether it is necessary or not! Let’s learn first a little more about the history of tithes.

Tithing for the first time began to be paid by a man named Abraham, who is known as the Father of Faith.

We read about this in Genesis 14

Genesis 14:17 “And it came to pass, that, when Abram was returned from following Chedorlaomer, and the kings that were with him, then the king of Sodom went out to meet him in the valley of Shaveh, which is the king’s dale.

18 And Melchizedek king of Salem brought forth bread and wine: and he was the priest of the most high God.

19 And he blessed him, and said, Blessed be Abram of the most high God, possessor of heaven and earth:

20 And blessed be the most high God, which hath delivered thine enemies into thy hand. ABRAM GAVE HIM A TITHE OF ALL THINGS ”.

Abraham gave the tithes to this Melchizedek, remember this Melchizedek was God incarnate… and is also known as the High Priest, the image of the Son of God (Jesus Christ) having neither father nor mother, nor beginning of days or ending of days. So it was God Himself who came in human form.

It came to pass when Abram was come out to rescue his uncle Lot, who had been taken captive together with his sons, on the way back he met Melchizedek, and this Melchizedek was carrying Wine and Bread, and he gave it to Abram and because Abram loved God so much,  he did not consider it necessary to receive free gifts without giving…Above all God has appeared to him and succeeded him in the midst of his enemies and defeated them! So he was touched with it and he saw it was not right not to give anything back to his God, so he decided on his own without being told by anyone to give his God 10th part of his possessions!!! What kind of heart is that? Remember he was not even told by God to do that, only he himself had something in him that made him feel bad if he saw his God leave empty-handed, and that is nothing but the Holy Spirit in him.

Did the law work?

Now at that time there was no law, no 10 commandments and God did not enter into a Covenant with Abraham about tithes, the law of tithes came about 400 years later, it was necessary to pay tithes, if a person did not pay tithes it was considered a sin for him!, and before God he was like a thief (Malachi 3:8-9).

But now we are not living by the law but by faith, and the Faith we are talking about is the same Faith as that of Abraham, that is, the Faith of doing things without compulsion, and that Faith is the same as Abraham, of giving God 10 percent unconditionally! ..Abraham gave unconditionally, no law, no law! because the Law had not yet come, nor was it compelled, nor was it implanted or implored; nor inquiring God, he said God is my giver (Jehovah-YIRE), so if he has given me a large portion of these things, then why shouldn’t I repay him at least 10 percent of the things he has given me. And he made it his law always! Every 10th he gets he gives back to God.

Brethren, Abraham met Melchisedec, and even now this Melchisedec is with us and he is none other than our Lord Jesus Christ, the scripture proves that..

Hebrews 6:20 “When Jesus, who came before us, was our forerunner, he was a high priest for ever after the order of Melchizedek.”

Hebrews 7: 1 “For this Melchisedec, king of Salem, priest of the most high God, who met Abraham returning from the slaughter of the kings, and blessed him;

2 To whom also Abraham gave a tenth part of all; (The translation of his first name is King of Righteousness, and again, King of Salem, meaning, King of Peace;

3 He has no father, no mother, no parents, no beginning of days, nor end of life, but is likened to the Son of God); he remains a priest forever.

4 Now consider how great this man was, unto whom even the patriarch Abraham gave the tenth of the spoils.

Hebrews 5: 5 “So also Christ glorified not himself to be made an high priest; but he that said unto him, Thou art my Son, to day have I begotten thee.

6 As he saith also in another place, Thou art a priest for ever after the order of Melchisedec”.

You have seen that Christ was likened to Melchizedek, and as Melchizedek was given the 10th part by Abraham, so also Christ is entitled to the 10th part, because he is the Melchizedek of our Covenant, and just as Melchizedek fought for Abraham, so Christ now fights for us.

And just as Abraham gave Melchizedek the 10th verse without any conditions, or without law, or without law, or without any preaching, or without counsel, or without any other motive, so today we must offer JESUS CHRIST 10th part. without any law, without any restrictions, without any preaching, without being influenced by any man.

It should be a heartfelt expression that we recognize the presence of Jesus Christ in our lives and so we honor him by giving him 10th part, he is not after our money! But he is watching over our hearts! And the Lord Jesus Himself allowed that in (Matthew 23:23).

If you see someone objecting to pay TITHES! And to give to God, That’s proof that He doesn’t have the HOLY SPIRIT in him! It is one of the proofs of a man who lacked the Holy Spirit in him!.

Because it is clear that he does not love God, because he cannot thank God for giving even 10 percent of his possessions and giving them back to him, even though he inhales free of charge, tramples on land that is not his own, eats food that he does not know how to make! He does not appreciate even the Christ who gave his life for him. In short he is an ungrateful man.

And how can such a person thank God for giving 10 percent of his life to preach the Gospel ?, how can he give even his life for the sake of the Gospel ?, or how can he die for the Faith? If only 10 per cent of his money could not give it ?. How can that Person even give up everything and follow Christ if only tithe giving is war? Just think!

So TITHES are not something to be avoided at all! It is not given by law or by the law, nor is it written in the Bible, but by the heart like Abraham!

If you don’t have a job that gives you an income then you are free !, but whatever you get other than work give it away the 10th part of it, give it back to your God, you have no job but you have been given a certain amount of money make sure you give out the tithes, and give wholeheartedly without coercion, because our God is not a revenue collector! He wants us to give to Him wholeheartedly and joyfully, realizing the importance of giving to Him as Abraham did.

Now the question is what! If you don’t pay tithes will you go to hell?

What will send a person to hell is not the act of breaking the tithe or committing adultery, or stealing, or insulting no !! what will send a person to hell is the lack of the Holy Spirit in him,

where now the result of not having the Holy Spirit is that he will now be a thief, a fornicator, a blasphemer, a man without a heart to give, he will not be able to help others, and he will not contribute anything to the kingdom of heaven through his giving, he will also be unforgiving, Because A person with the Holy Spirit cannot do any of these things because the Holy Spirit will be speaking in him about sin and he will also be pushing him about why he do not give to God, so he cannot avoid paying tithes as he cannot help others or pray.

There is a saying that “I am perfect in every way! Except for tithes I do not give!”

That is a lie of the devil brother! it is impossible for a person to be perfect in all things and then miss one thing that does not pay tithes! There is no such thing!

If a person does not pay tithes while he can, then he must also be evil in other respects, it is the same as saying that this person is holy in everything but the only defect is an adulterer! That is a lie… One sin interacts with another, the adulterer must be greedy, resentful, a liar and a traitor, jealous, a competitor even if on the outside he will not be seen but in his heart he has all that.

So avoiding tithing is a sign of lack of the Spirit, and all those who do not have the Spirit of God the Bible says they are not His (read Romans 8: 9), and if they are not His then they will go to hell!

The Lord Bless you.


Related Articles:

Is it a sin to get a tattoo?

Is masturbation a sin?

Are all sins equal? and have the same punishment?

WHAT IS THE EVERLASTING GOSPEL?

Home:

Print this post

AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.

Kwanini Amelaaniwa aangikwaye msalabani?


Kutundikwa msalaba au kwa jina lingine kutundikwa mtini, ilikuwa ni adhabu iliyotekelezwa kwa watu wenye makosa ya hali ya juu sana.                               

Adhabu hii ilikuwa sio tu ilikuwa inatekelezwa na watu wa mataifa mengine kama wengi wanavyodhani ni Warumi tu, hapana bali pia ilikuwa inatekelezwa na Israeli pia.

Ni adhabu yenye mateso mengi sana, na vilevile ni adhabu ya aibu. Waliokuwa wanatundikwa msabani walikuwa sana sana ni wauaji. Makosa ambayo yalikuwa yanathibitisha kuwa wamelaaniwa na Mungu.

Kumbukumbu 21:22 “Akiwa mtu ametenda dhambi ipasayo kufa, akauawa, nawe ukamtundika juu ya mti;

23 mzoga wake usikae usiku kucha juu ya mti; lazima utamzika siku iyo hiyo; kwani aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu; usije ukatia unajisi katika nchi yako akupayo Bwana, Mungu wako, iwe urithi wako”.

Utasoma sehemu nyingi, katika biblia mifano ya watu waliangikwa msalabani. (Mwanzo 40:18-19, Esta 2:22-23, Esta 7:10)

Jambo hilo hilo tunaliona mpaka katika kipindi cha karibu na agano jipya, katika ule ufalme wa Rumi, wafungwa wote waliokuwa na kesi kubwa za mauaji au wizi, n.k. Adhabu yao ilikuwa ni kuangikwa/kutundikwa msalabani ukiwa hai.

Lakini cha ajabu ni kwamba, adhabu zilizokuwa zinawahusu watu waliolaaniwa, zilimkuta mtu ambaye hakuwahi kutenda dhambi hata moja..Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO

Wagalatia 3:13 “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, AMELAANIWA KILA MTU AANGIKWAYE JUU YA MTI;

14 ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani”.

Lakini ni kwanini yamkute hayo yote?

Je ni ilikuwa ni bahati mbaya tu? Au Mungu alishindwa kumzuia? Jibu ni la, ilitokea vile kwa makusudi kabisa, ili ile hati ya mashitaka ya waliolaaniwa ifutwe juu yetu, aliibeba yeye ile hati ya laana, na ndio maana pale ambapo Baraba muuaji alipopaswa auawe, Yesu aliuawa badala yake, pale ambapo wewe mzinzi ungepaswa uhukumiwe milele kwa makosa yako, Yesu aliichukua laana hiyo siku ile msalabani, pale ambapo wewe uliye na dhambi ambazo nyingine ni aibu kuzitaja, Yesu alizichukua, hatia zote kwako.

Lakini hizo haziwezi kufutika juu yako, hivi hivi tu, bali ni  mpaka uende kuzisalimisha msalabani.

Na ndio maana unahitaji kumpokea Yesu maishani mwako, vinginevyo hati ya mashitaka ya dhambi zako zitaendelea kubakia juu yako hadi siku ya mwisho, na utahukumiwa kama mkosaji.

Lakini ikiwa leo upo tayari kumpokea Yesu maishani mwako, basi leo leo atazifuta dhambi zako bure kabisa, haijalishi wewe ni mwenye dhambi kiasi gani.

Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.

5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.

Hivyo kama upo tayari leo kumpa Yesu maisha yako, basi uamuzi huo ni wa busara, hivyo fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba  >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali Share na wengine, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au katika namba hii hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

MASOMO MBALIMBALI YA NENO LA MUNGU.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

UTASIMAMA PEKE YAKO SIKU ILE.

USINIPITE MWOKOZI Lyrics

Rudi Nyumbani:

Print this post