Mithali 20:13 “Usipende usingizi usije ukawa maskini; Fumbua macho yako nawe utashiba chakula”.
Usingizi unaozidi unachelewesha utekelezaji wa majukumu ya muhimu. Kwamfano Mwanafunzi anayelala kupita kiasi ni lazima atakuwa mchelewaji wa shule, vilevile mfanyakazi alalaye kupita kiasi ni lazima atakuwa mchelewaji wa kazini, mfanya biashara anayealala kupita kiasi ni lazima atachelewa kuanza biashara yake.
Upo usemi usemao “biashara ni asubuhi” maana yake kwa mtu anayefanya biashara labda ya kuuza duka, asubuhi ndio wakati wa kufungua bishara maana watu wengi wanawahi kutafuta bidhaa asubuhi Zaidi ya mchana, hivyo alalapo sana hatapata zile faida za asubuhi, na hivyo yupo hatarini kufilisika.
Atapanga kweli kuwahi kuamka mapema kesho, lakini ifikapo asubuhi kitanda kinakuwa na nguvu kuliko maamuzi yake, atajiongezea muda wa kulala, na mwisho wa siku atashtukia kumeshapambazuka na jua linawaka..na hayo ni matokeo ya kusema “bado kulala kidogo”.
Mithali 6: 9 “Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaondoka lini katika usingizi wako?
10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi!
11 Hivyo umaskini wako huja kama mnyang’anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha”.
Sasa biblia ni kitabu kilichojaa hekima ya kumwongoza mtu hata katika maisha ya kawaida Zaidi yay ale ya rohoni…. ni kitabu kilichojaa mafunzo mengi mema yahusuyo kanuni za kimaisha na kitabu cha Mithali kimejaa mafunzo hayo.
Hivyo biblia inatufundisha wakristo tuwe na kiasi katika kulala, kwani usingizi unaozidi una matokeo mabaya.. Si kila changamoto inasababishwa na “wachawi”….. nyingine zinatokana na tabia zetu wenyewe.., na hivyo biblia inatufundisha jinsi ya kuepukana nazo, kwamba ni kubadili tu mienendo.
Maana yake ni kwamba, tukitaka kuepukana na “umasikini” kanuni sio tu “kufunga na kuomba” bali pia ni KUTOUPENDA USINGIZI!. Ukifunga na kuomba na huku unaendekeza usingizi kupita kiasi hakuna matokeo yoyote utakayoyaona.
Maana yake kama ni mfanyakazi basi usiwe mtu wa kupenda kulala mno..Ni kweli hatuwezi kuacha kulala kabisa, lakini kusizidi mipaka, kwani usingizi uliozidi ni zao la ibilisi.
Mithali 19:15 “Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa”
Lakini pia kiroho hatupaswi kulala kabisa, kwani usingizi wa kiroho matokeo yake ni mabaya kuliko ule wa kimwili.. Matendo yote ya giza mtu ayafanyayo ni matokeo ya usingizi wa kiroho..
Mtu anayefanya uzinzi, uasherati, anayelewa pombe, anayeiba, anayetukana, anayesengenya…huyo macho yake yamefumba kwa usingizi mzito.
Je na wewe umo miongoni mwa waliolala kiroho? Basi huu si wakati wa kuendelea kulala, bali wa kuamka na kuyaacha matendo ya giza.
Warumi 13:11 “Naam, tukiujua wakati, kwamba SAA YA KUAMKA KATIKA USINGIZI imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini
12 USIKU UMEENDELEA SANA, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru.
13 Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu”
Waefeso 5:14 “ Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza
15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;
16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu”.
Bwana atubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.
SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!
ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU.
Masomo maalumu kwa wahubiri.
Isaya 29:16 “NINYI MNAPINDUA MAMBO; Je! Mfinyanzi ahesabiwe kuwa kama udongo; kitu kilichofinyangwa kimnene yeye aliyekifinyanga, Hakunifinyanga huyu; au kitu kilichoumbwa kimnene yeye aliyekiumba, Yeye hana ufahamu?”
Kama Mtumishi/Mhubiri jihadhari na MAPINDUZI yasiyo na msingi!.
USIIPINDUE INJILI YA KRISTO KWASABABU YA TAMAA YA FEDHA.
Unapoanza kuwadanganya watu wa wenye nia ya kumtafuta Mungu, ili tu upate fedha kutoka kwao!.. unapoanza kuwatumainisha watu wa Mungu mambo ya uongo ili tu uwatoe fedha!.. Hiyo ni ishara mbaya na hatari kubwa sana kwako!. Bwana ataenda kukupindua nawe pia!.
Tito 1:11 “Hao WANAPINDUA watu wa nyumba nzima, wakifundisha yasiyowapasa kwa ajili ya mapato ya aibu”.
Ukilipindua Neno la Mungu na kuanza kufanya biashara katika nyumba ya Mungu (ambayo ni wewe mwili wako sawasawa na 1Wakorintho 3:16) kwa kuanza kufanya uasherati na uzinzi na ukahaba fahamu kuwa Bwana naye atakupindua (Soma 1Wakoritho 6:19).
Ukilipindua Neno la Mungu kwa kuiharibu nyumba yake (kama jengo) kwa kuanza kufanya biashara ndani yake na kufanya yasiyofaa Bwana YESU atazipindua meza zako (soma Mathayo 21:12)
Ukilipindua Neno la Mungu juu ya utakatifu wa mwilini na rohoni (sawasawa na 1Wathesalonike 5:23) na kuanza kufundisha/ kuhubiri kuwa Mungu haangalii mwili bali anaangalia roho tu peke yake ni kupindua maandiko ambako matokeo yake ni Mungu kuyapindua maneno yako na wewe kwa ujumla.
Mithali 22: 12 “Macho ya Bwana humhifadhi mwenye maarifa; Bali HUYAPINDUA MANENO YA MTU HAINI”
Ukilipindua Neno la Mungu na kuanza kuhubiri kuwa YESU KRISTO bado sana arudi, au kwamba hakuna mwisho wa dunia, huko ni kupindua mambo ambako matokeo yake ni mabaya kama ya Fileto na Himenayo.
2Timotheo 2:17 “na neno lao litaenea kama donda-ndugu. Miongoni mwa hao wamo Himenayo na Fileto,
18 walioikosa ile kweli, wakisema ya kwamba kiyama imekwisha kuwapo, hata KUIPINDUA imani ya watu kadha wa kadha”.
Kama Mhubiri Ni heri KUPINDUA ulimwengu kwa mambo ya kweli ya INJILI kama walivyofanya Mitume wa kanisa la kwanza kuliko kuigeuza/kuipindua injili kwa faida zetu wenyewe.
Matendo 17:6 “na walipowakosa, wakamkokota Yasoni na baadhi ya ndugu mbele ya wakubwa wa mji, wakipiga kelele, wakisema, Watu hawa WALIOUPINDUA ULIMWENGU WAMEFIKA huku nako”
Siku ya Mapinduzi makuu inakuja, ambapo Bwana ataipindua dunia yote kama alivyoipindua miji ya Sodoma na Gomora (soma Kumbukumbu 29:23) na kipindi cha gharika ya Nuhu (Soma Ayubu 12:15).
Ezekieli 21:27 “NITAKIPINDUA, NITAKIPINDUA, NITAKIPINDUA; hiki nacho hakitakuwa tena, hata atakapokuja yeye ambaye ni haki yake; nami nitampa”
Hegai 2:22 “nami nitakipindua kiti cha enzi cha falme, nami nitaziharibu nguvu za falme za mataifa; nami nitayapindua magari, na hao wapandao ndani yake; farasi na hao wawapandao wataanguka chini; kila mtu kwa upanga wa ndugu yake”.
Usipindue Mambo yaliyonyooka, bali pindua yale yaliyopotoka.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.
NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.
JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.
SWALI: Nini tafsiri ya Mithali 27:22
Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni pamoja na ngano; Upumbavu wake hautamtoka.
JIBU: Kama tunavyojua mtwangio na kinu ni vyombo vinavyotumika kuponda-ponda nafaka ngumu kuwa unga, au wakati mwingine mimea migumu kuwa milaini. Mfano wa kisamvu ambacho ili kiweze kulika, majani yake huwezi yapika hivyo hivyo huna budi kuyatwanga twanga kidogo, yalainike ndipo upike ule.
Na vivyo hivyo, nafaka kama mahindi, au ngano, ili viweze kulika zamani vilikuwa vinatwangwa kwenye vinu ,tofauti na sasa vinasagwa na mashine.
Sasa katika mithali hiyo, Mungu anatoa, asili ya mtu mpumbavu, kwamba hata akitwangwa, mfano wa ngano kinuni, huo upumbavu hauwezi kumtoka. Yaani njia gani ya lazima itumike bado hawezi kuacha upumbavu.
Sasa ni vizuri kufahamu, mpumbavu ni nani?
Mpumbavu kibiblia sio mtu Fulani mjinga tu hapana, bali ni Neno pana, linalolenga kuanzia
mtu anayesema hakuna Mungu (zaburi 14:1)
Mtu mgomvi (Mithali 9:13),
Mtenda maovu (Mithali 10:23)
Anayejiona njia yake ni sawa machoni pake (Mithali 12:15)
Mwenye kiburi (Mithali 14:3)
Mwenye dharau (Mithali 15:5)
Yaani kwa kifupi mpumbavu ni mtu ambaye hana Mungu ndani yake. Kwasababu dhambi ndani ya mtu ndio chanzo cha Upumbavu wote.
Sasa mtu kama huyu, hakuna kitu kinachoweza kuutoa upumbavu huo ndani yake, waweza kusema elimu, lakini ni watu wangapi wameelimika, lakini walevi, watukanaji, mashoga. Hata atwangwe vipi kinuni hawezi lainika, ikiwa hajui ni kipi sahihi kinachoweza kutoa upumbavu huo.
Kumfunga mwizi, hakumfanyi wizi au tamaa ya kuiba itoke ndani yake, mara ngapi unasikia mwizi katoka jela, karudia wizi wake, au ni kiongozi ambaye anaaminiwa awe kielelezo cha kupambana na ufisadi, lakini yeye ndio anakamatwa katika ufisadi, au teja ametolewa hospitalini karudia, tena madawa la kulevya. Ndio maana jamii ijapojaribu kudhibiti vitendo viovu, bado haviishi, bali hubadilika tu maumbile. Kwasababu mpumbavu hata atwangwe kinuni, hawezi geuka, hakuna nidhamu inayoweza mbadilisha. Huwezi acha mwenendo wake mbovu kwa semina za kijamii, au kuwekewa sheria
Je! Ni kipi kinachoweza kumgeuza?
Ni Yesu Kristo tu. Yeye ndiye aliyetiwa mafuta, na Mungu kuwaokoa watu wa Mungu na kuwafungua. Amwaminiye na kudhamiria moyoni mwake kumfuata, basi atageuzwa moja kwa moja na kuwa mtu mwingine, huo ni uhakika.
Alisema.
Yohana 1:12 Bali wote waliompokea aliwapa UWEZO wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.
Ni ahadi yake kuwa Ukimwamini jambo la kwanza ni kukusamehe dhambi zako, kwasababu ndio jambo lililomfanya aende msalabani kwa ajili yako miaka elfu mbili iliyopita,. Unakuwa huhesabiwi dhambi tena, unahesabiwa haki bure kwa neema yake. Lakini sambamba na hilo anakupa UWEZO wa kuwa kama yeye kwa nguvu za Roho wake Mtakatifu atakayemwachia ndani yako, pindi tu unapoamini.
Na baada ya hapo utashangaa tu unavyoanza kubadilika moyoni mwako.
Zingatia tu toba ya kweli, pamoja na ubatizo sahihi (kuzamishwa katika maji mengi kwa jina la Yesu Kristo). Na kumtii yeye.
Upumbavu utakutoka.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Fahamu Maana ya Mithali 18:13 Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.
Nini maana ya Mithali 9:13 Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu?
SWALI: Nini maana ya Mithali 26:2
Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake, Na kama mbayuwayu katika kuruka kwake; Kadhalika laana isiyo na sababu haimpigi mtu.
JIBU: Mungu anafananisha laana isiyo na sababu na ndege wanaotanga-tanga angani.
Kama tunavyojua ndege hawa aina ya shomoro na mbayuwayu, kila siku tunawaona wanaruka angani, kila siku tunawaona wapo hari-hari, wanaonekana kama wapo buzy, lakini katika kazi zao zote, na juhudi zao zote, na mikakati yao yote, kamwe huwezi ona yanaleta madhara yoyote kwa mwanadamu. Hata kama utawaharibia viota vyao, hata kama watakauwa na hasira na wewe, huwezi ona wanamshambulia mwanadamu, kwasababu uwezo huo hawana. Huwezi wafikiria na kila wanapokuona wanakimbia. Wewe mwenyewe ukiwaona huwezi kuwaogopa, tofauti na ukimwona nyoka, utajidhatiti asikuume. Lakini ndege huvai ‘chapeo’ kichwani kujilinda naye asikuume, kwasababu hana madhara.
Ndivyo Mungu anavyotufundisha, laana zisizo na sababu, haziwezi kukupata ni kama ndege tu angani, zitapita, na kuendelea na shughuli zake, kamwe haziwezi kukupata ikiwa wewe ni mtakatifu, Hii ni kutufundisha kuwa hatupaswi kuwa waoga wa maneno ya watu (laana) ambayo hayana sababu.
Ukiona laana imekupata basi ujue kulikuwa na sababu nyuma yake, (lakini sio tu maneno matupu mtu anayoyatoa), mfano wa laana hizi ni ile ya Elisha aliyowalaani wale vijana 42, walioraruliwa na dubu. Kwasababu walimdhihaki. (2Wafalme 2:22-25)
Lakini mfano wa laana zisizo na sababu, ni ile Goliathi aliyomlaani Daudi kwa miungu yake, ambayo ilikuwa ni kazi bure..
1Samweli 17:42 Hata Mfilisti alipotazama huku na huku, akamwona Daudi akamdharau; kwa kuwa ni kijana tu mwekundu, tena ana sura nzuri. 43 Mfilisti akamwambia Daudi, Je! Mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake
Ni mfano mwingine ni ile Balaamu mchawi alivyojaribu kuwalaani Israeli ikashindakana, kwasababu huwezi laani vilivyobarikiwa. (Hesabu 23)
Hata leo, ikiwa wewe umeokoka, hupaswi kuogopa, maneno yoyote iwe ya waganga au wanadamu. Kwasababu wewe tayari ni mbarikiwa. Ni ajabu sana kuona mkristo, analia na kutetemeka, eti! Mchawi kamwambia mwaka huu hautaisha atakuwa watoto wake wote watakuwa wamekufa!!. Mzee wa mila kamwambia atapata ajali kwasababu hakutambika kijijini mwaka huu.
Mwingine anawaza, mzazi kamwambia hatafanikiwa kwasababu kaamua kuokoka. Haa! Unaogopa nini hapo?. Hizo ni laana zisizo na sababu. Ishi kwa amani zione tu kama ndege wa angani ambao hukai kuwafikiria kama watakushambulia siku moja.
Ukiokolewa na Kristo umebarikiwa, wewe sio wa kunenewa maneno ovyo ovyo tu, na yakatokea. Wewe ni uzao wa kifalme usiotetemeshwa, ngome imara isiyoangushwa. Mwamba mgumu usiogharikishwa. Yatambue mamlaka na nguvu ulizopewa ndani ya Kristo. Usiogope!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Elewa maana ya Mithali 26:2 Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake,
Maana yake nini, Mwe na hofu wala msitende dhambi? (Zaburi 4:4)
Katika Ayubu 41, tuona Mungu akieleza kwa urefu sifa ya mnyama mamba.
Ametumia taswira ya mamba huyu tunayemwona, kumwelezea mamba wake wa rohoni, ambaye hasaa Ayubu alionyeshwa habari zake kwa urefu kupitia sura hii.
Na ndio maana kuna sifa nyingine ukizisoma hapo, huwezi kuziona kwa mamba huyu tuliye naye sasa, lakini Mungu hupenda kutumia mifano halisi walau tupate taswira wa kile alichokimaanisha. Ndio maana akaweka sifa chache kwenye mambo wetu huyu ili tumwelewe.
Sasa katika sura hii, Mungu anaanza kwa kumwonyesha Ayubu jinsi anavyomtofautisha sana mnyama mamba na viumbe vingi mbalimbali vilivyopo duniani, kuanzia vya kwenye maji kama vile samaki, mpaka vile vile vya angani kama vile ndege, hadi wanyama wa kufugwa kama ng’ombe na wale wa mwituni kama vile simba.. Hawa wote hakuna aliyelinganishwa naye.
Mungu anamwonyesha ukali mwingi alionao, nguvu alizonazo, ugumu ulio katika ngozi yake, kiasi cha mkuki wowote kushindwa kupenya kwenye ngozi yake, zaidi sana ujasiri alioumbiwa. Kwa ufupi kulingana na habari hii hakuna mnyama aliyeweza kulinganishwa na huyu duniani kote.
Sasa embu soma hizi sifa, na mwishoni utamjua mamba huyo ni nani, na uzao wake ni upi. (Zingatia maneno yaliyoandikwa kwa herufi kubwa)
Ayubu 41
1 Je! Waweza wewe KUMVUA MAMBA KWA NDOANA? Au, kuufunga ulimi wake kwa kamba? 2 Je! Waweza kutia kamba puani mwake? Au kutoboa taya yake kwa kulabu?
3 JE! ATAKUSIHI SANA? Au, atakuambia maneno ya upole? 4 Je! Atafanya agano pamoja nawe, UMTWAE KUWA MTUMISHI WAKO milele?
5 Je! UTAMCHEZEA kama ndege? Au, kumfunga kwa ajili ya wasichana wako? 6 Je! Vikosi vya wavuvi watamfanyia biashara? WATAMGAWANYA kati ya wafanyao biashara?
7 Je! Waweza kuijaza ngozi yake na vyuma vyenye ncha, Au kichwa chake kwa vyusa? 8 Mwekee mkono wako; Vikumbuke vile vita, wala usifanye tena.
9 Tazama, kumtamani ni bure; Je! Hatambwaga chini huyo atakayemtazama? 10 HAPANA ALIYE MKALI HATA AKATHUBUTU KUMWAMSHA; Bali ni nani awezaye kusimama mbele yangu mimi? 11 Ni nani aliyetangulia kunipa hata nimlipe? Kila kilicho chini ya mbingu nzima ni changu.
12 Sitanyamaa kusema habari za via vyake, Wala nguvu zake kuu, wala umbo lake zuri. 13 Ni nani AWEZAYE KUMBAMBUA MAGAMBA YAKE? NI NANI ATAKAYEPENYA DIRII YAKE MARADUFU? 14 Ni nani awezaye kuifungua milango ya uso wake? Meno yake yatisha kandokando yake.
15 Magamba yake yenye nguvu ndiyo fahari yake, Yamefungamana pamoja kama kwa kufungwa kwa muhuri. 16 Jinsi yalivyoshikamana Hata upepo hauwezi kupita kati. 17 Yamefungamana pamoja; Yameshikamana, hata hayawezekani kutengwa.
18 Kwa kuchemua kwake mwanga humemetuka, Na macho yake yanafanana na makope ya alfajiri. 19 MIENGE IWAKAYO HUTOKA KINYWANI MWAKE, NA MACHECHE YA MOTO HURUKA NJE. 20 MOSHI HUTOKA KATIKA MIANZI YA PUA YAKE, Kama nyungu ikitokota, na manyasi yawakayo.
21 Pumzi zake huwasha makaa, Na miali ya moto hutoka kinywani mwake. 22 Katika shingo yake hukaa nguvu, Na utisho hucheza mbele yake. 23 Manofu ya nyama yake hushikamana; Yanakazana juu yake; hayawezi kuondolewa.
24 MOYO WAKE UNA IMARA KAMA JIWE; Naam, imara kama jiwe la chini la kusagia. 25 Anapojiinua, mashujaa huogopa; Kwa sababu ya woga wao huvunjwa moyo. 26 Mtu AKIMPIGA KWA UPANGA, HAUMWINGII; Wala fumo, wala mshale, wala mkuki wenye ncha.
27 Yeye huona chuma kuwa kama nyasi, Na shaba kama mti uliooza. 28 Mshale hauwezi kumkimbiza; Na mawe ya teo kwake hugeuka kuwa kama makapi. 29 Marungu huhesabiwa kama mabua; Naye hucheka mshindo wa mkuki ukitupwa.
30 Pande zake za chini ni kama vigae vikali; Hutandika malazi kama kuweka chombo cha kupuria nafaka juu ya matope. 31 Yeye huchemsha kilindi mfano wa nyungu; Hufanya bahari kuwa kama mafuta.
32 Hufanya mapito yake kung’aa nyuma yake Hata mtu angedhani kilindi kina mvi. 33 JUU YA NCHI HAPANA ALIYEFANANA NAYE, ALIYEUMBWA PASIPO OGA. 34 Yeye hutazama kila kitu kilicho juu; Ni mfalme juu ya wote wenye kiburi.
Mamba huyu si mwingine zaidi ya BWANA YESU KRISTO.!
Hakuna ufalme, au mwanadamu, au mamlaka iliyoweza au inayoweza kuutetemesha ufalme wa Kristo, zaidi dunia nzima humuhofu. Yeye sio samaki, yeye ni zaidi ya mamba.
Lakini pia anao uzao wake tofauti na uzao wa viumbe vingine. Na watoto wake watafanana na yeye, ndio wale waliomwamini. Ndio maana ukimpokea Kristo kwa kuzaliwa mara ya pili, unakuwa mtu mwingine kabisa duniani, kwasababu asili yake inakaa ndani yako.
Ndugu, utaishi kinyonge hapa duniani, mapepo yatakusumbua, dunia itakusumbua kwasababu wewe ni dhaifu, na utaendelea kuwa dhaifu tu kama visamaki vingine vinavyovuliwa-vuliwa tu ovyo na ndoano. Lakini ukimpokea Kristo maishani mwako. Wewe ni mtu mwingine.Rohoni unaogopeka mno.
Embu leo tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, mwambie Yesu naufungua moyo wangu, ingia ndani yangu, na hakika ataingia, na kukusamehe dhambi zako zote, kama hakikisho la uzima wa milele . Atakufanya kiumbe kipya, hakikisha tu unamaanisha kusema kimatendo kuanzia leo YESU ni wangu, mimi ni wake. Hilo tu, kisha nenda ukabatizwe ikiwa hukubatizwa. Baada ya hapo asili yako itabadilishwa. Uwe mamba, umiliki na kutawala sio samaki.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Neno “Via” linamaanisha nini katika biblia?
KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?
Waefeso 2:10
MAANA TU KAZI YAKE, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.
Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, karibu tujifunze maneno ya uzima.
Mimi na wewe kama vile maandiko yanavyosema hapo, ni “kazi ya Mungu”..Hivyo ni lazima kujua kama ni kazi ya Mungu basi ni lazima pia tumekusudiwa kutimiza jukumu fulani hapa duniani.
Kwamfano unapoona gari, unasema lile ni kazi ya mtu sio mbuzi.. Na kama ni kazi yake, basi kuna wajibu fulani nyuma yake ambao liliumbiwa lifanye. Na wajibu wenyewe ni kumsafirisha mtu au vitu kwa haraka na wepesi.
unapoona nyumba, tunasema ni kazi ya mtu, imejengwa kuwa makao ya kupumzika, haijajengwa tu, bila kusudi lolote duniani.
hata unapoona kiota, ile ni kazi ya ndege kakijenga sio kiwe tu pale kama takataka, bali aishi ndani yake.
Vivyo hivyo na sisi ni kazi ya Mungu tuliumbwa kutimiza kusudi fulani. Hivyo ni lazima ujue, na kusudi lenyewe ni KUTENDA MATENDO MEMA.
Sisi ni vyombo mahususi, Mungu alivyovikusudia kudhihirisha matendo mema, ambayo aliyaumba tangu mwanzo yatendwe, hakuna chombo chochote chenye uwezo wa kufanya hivyo isipokuwa mwanadamu.
Waefeso 2:10
MAANA TU KAZI YAKE, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.
Sasa wewe kama mtu usipojua wajibu wako hapa duniani, utakuwa hatarini kuangamizwa. Ni sawa na TV isiyoonyesha kitu, gari lisilotembea, pasi isiyotoa moto. ni wazi kuwa vitatupwa kama sio kuwekwa kwenye karakana.
Na wewe vivyo hivyo, fahamu kuwepo kwako duniani ni kutenda matendo mema. ndio kusudi lako
Sasa, si matendo mema, ilimradi matendo mema…hapana…yapo matendo mema, lakini yasiwe na nguvu mbele za Mungu, hayo ndio yale ambayo mataifa huyafanya..lakini matendo mema tunayoyazungumzia hapa ni yale yaliyo ndani ya YESU KRISTO. Ndio maana hapo anasema tuliumbwa katika Kristo Yesu, sio katika Adamu, au Ibrahimu, au nabii fulani bali Kristo Yesu..maana yake matendo ya Yesu, (au kwa namna nyingine tabia za Yesu) ambayo hakuna mwingine awezaye kuyatenda isipokuwa mtu huyo amezaliwa mara ya pili.
Hivyo leo tutatazama aina ya matendo hayo mema ambayo wewe kama mwana wa Mungu huna budi kuyadhirisha uwapo duniani.
Upendo wa Kristo, sio kama upendo wa kiulimwengu, ule ambao, unawapenda wakupendao hapana..mbele za Mungu hapo bado hujafanya tendo la upendo, huo ni mwanzo tu.
bali ni ule wa kupenda wanaokuudhi, lakini sio kupenda tu, unafikia hatua ya kuwaombea, na unapofikia kilele chake unaweza hata kuutoa uhai wako kwa ajili yao.
Mathayo 5:43-48
[43]Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
[44]lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
[45]ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
[46]Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
[47]Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?
[48]Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.
Huu unaitwa upendo wa agape. Mimi na wewe lazima tufanye bidii tuudhihirishe. Ndio ulioumbiwa tangu mwanzo uuonyeshe kwa wengine. Epuka mafundisho ya piga adui zako, kumbuka wewe ni kazi ya Mungu, kuonyesha upendo.
Yesu alisema haki yenu isipozidi ya waandishi na mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.
Mathayo 5:20
[20]Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.
Mafarisayo walikuwa hawana Roho Mtakatifu, hivyo mambo yote waliyatimiza kwa nguvu lakini haikusaidia kuondoa tamaa za mwili. walikuwa hawazini lakini mioyo yao ilikuwa na tamaa. Lakini Yesu alitoa mizizi ya uzinzi, ndani ya mtu kwa Roho wake mtakatifu anayempa.
Ndio maana kwanini unapaswa ujazwe Roho, lakini pia utembee kwa Roho Mtakatifu ili uweze kuushinda mwili, vinginevyo hutaweza kwa nguvu zao, utafanya kinafiki. Biblia inasema..
Wagalatia 5:16-17
[16]Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
[17]Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.
Ni lazima ujifunze utii wa Neno la Mungu, kwa kujikana nafsi, na kumfuata Yesu, wakristo wengi hawajikani nafsi, wanakiri wokovu lakini gharama zake hawataki kuingia, wamesilibiwa kweli msalabani lakini hawataki kufa, hawataki kuvunjwa vunjwa miguu yao wafe,. Ukiingia kwa Kristo kubali kufa ili akuhuishe, ndivyo utakavyoweza kuushinda ulimwengu, kubali kusema bye! bye! kwa ulimwengu. Utaona tu jinsi gani utakavyoweza kuishi maisha matakatifu bila shida yoyote. Roho Mtakatifu huwa anapata nguvu ya kumbadilisha mtu pale ambapo anakubali kujikana kweli nafsi. lakini kama hataki, Mungu kidogo, udunia kidogo, utaendelea kuwa vilevile tu kama mafarisayo na waandishi, ambao vikombe vyao havijasafishwa kwa ndani.
Wewe ni kazi ya Mungu umeumbwa uwe mtakatifu kama yeye alivyo mtakatifu. Kubali tu kuongozwa na Roho kwa kujikana nafsi.
1 Petro 1:16
[16]kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.
Yesu alipokuja duniani, alitambua kuwa vinywa vyetu viliumbwa mahususi, kuwafundisha na kuwaekeza wengine njia iliyo sahihi. Ndio maana mapema tu, alianza kuhubiri na kufundisha katikati ya vijiji na miji, habari za ufalme..Huoni hayo ni matendo mema?
Warumi 10:15
[15]Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema!
Halikadhalika hatuna budi kufahamu agizo la sisi kuhubiri, ndilo tuliloumbiwa na Mungu tangu mwanzo tulifanye..ndio agizo kuu. Jambo ambalo lipo kwa wakristo tu. Ni mpango ambao Mungu amekusudia kuutumia kuzungumza, kuponya, kufungua watu kupitia watu hao hao.
Sasa ikiwa wewe umeokoka halafu, huna habari ya kuwashuhudia wengine Injili, fahamu kuwa wewe, sio kazi ya Mungu, uliyeumbwa katika Kristo Yesu. Bali ni kazi ya mwingine.
Amka sasa, ondoa woga na uvivu wa kuwatangazia wengine Kristo, usiwe chombo kibovu, anza kuwatangazia wengine wokovu, uwezo huo upo ndani yako, kushuhudia hakuhitaji elimu yoyote ya biblia au vifungu elfu vya kwenye maandiko, ni kueleza ushuhuda wa maisha yako matendo makuu Kristo aliyokutendea, ushuhuda huo unatosha kumgeuza mwingine, kabla hujafikiria kutoa vifungu anzia kwanza hapo. Ndicho alichokifanya yule kichaa aliyetolewa pepo, Yesu alimwambia nenda kwenu kawashuhidie watu matendo makuu Mungu aliyokutendea, na kwa kupitia ushuhuda wake taifa zima la Dekapoli likamwamini Kristo, mwanamke msamaria, kusikia tu habari zake zinafichuliwa akaenda kuwaleza watu, samaria yote ikaamini. Hakuna haja ya kuwa na hofu, anza sasa kuwashuhudia ndugu zako.
Wewe ni kazi ya Mungu, umeumbwa ili uhubiri.
Vilevile Matendo ya imani, tuliumbiwa sisi tangu mwanzo tuyadhihirishe, na ndio maana hatumwoni Mungu kwa macho, tofauti na malaika, kwasababu tumetengenezwa kwa namna hii, haiwezekani wewe kumpendeza Mungu pasina imani.
Waebrania 11:6
[6]Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.
Lakini imani yetu, haina budi kuzidi ile ya watu wa kidunia, ya kwetu huzaliwa na Neno la Mungu, nguvu ya Mungu iliyo katika msalaba wa Yesu.
tukiumwa tunaamini hakika, Yesu alishayachukua magonjwa yetu, huzuni zetu, umaskini, hatuna mashaka kwasababu Yesu alishayamaliza yote. Hatupaswi kuwa na hofu ya maisha, Yesu mwokozi wetu ameshayamaliza.
Kuwa mtu wa imani, liweke Neno la Mungu kwa wingi ndani yako. Mtegemee Kristo, amini kazi zake. Usiishi kwa kuona.
Maombi ni mawasiliano. Sisi kama kazi yake anatazamia, tuwe watu wa kumtegemea kwa asilimia mia, maombi yapo ya aina mbalimbali, sifa ni moja ya maombi, ibada ni aina ya maombi,
Ndio maana Yesu alipokuja duniani, maombi yalikuwa ni sehemu ya maisha yake. Aliomba zaidi ya watu wa kidini, alikesha, akawataka na mitume wake wafanye vile, alisema ombeni nanyi mtapewa, ombeni bila kukoka, dumuni katika sala. (Mathayo 26:41, Wakolosai 4:2)
Wewe ni manukato ya Mungu, Mungu anataka kusikia harufu yako nzuri. Na harufu yenyewe ni Maombi yako.
Ufunuo 5:8 Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele za Mwana-Kondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni maombi ya watakatifu
Vilevile fahamu maombi ni mahali ambapo unampa Mungu nafasi ya kukukarabati wewe kama chombo chake uweze kuzifanya kazi zake vyema. Vilevile Haiwezekani mwanadamu uliyeumbwa kwa mfano wa Kristo kwa wokovu uepuke maombi. Ukifa kimaombi, ni umekufa kiroho, huwezi kuzitenda kazi za Mungu.
Jambo lingine ambalo Mungu anatazamia alione kwako, ni wewe kudhihirisha umoja wa Roho ndani ya mwili wa Kristo. (Waefeso 4:3)
Yesu alisema .
Yohana 17:11, 21
[11]Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. … [21]Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ILI ULIMWENGU UPATE KUSADIKI YA KWAMBA WEWE NDIWE ULIYENITUMA.
Lengo la kufikia umoja ni ili ulimwengu umwamini Kristo. Mahali ambapo tunashindwa kupaelewa sisi kama kazi ya Mungu ndio hapo, yaani kila mtu anataka awe kivyake, au wazo lake liwe bora, tukidhani ndio tuliombwa tuishi hivyo..
halitawezekana, endapo hutatambua nafasi zetu katika mwili wa Kristo ni ipi, kama Mungu hajakupa uongozi, kwanini ung’ang’anie nafasi hiyo?
kuwa katika utumishi wa chini, hakukufanyi karama yako kudidimia, Mungu alimtoa Daudi mazizini, vivyo hivyo yule aliyemkusudia atamwinua tu popote lakini sio kugombani au kumwonea wivu mwenzako awapo kwenye nafasi fulani, hivyo ili tuufikie umoja wa Roho ni kukubali kujishusha kwa kuongozwa, na kufundishwa, na kuridhika na ulichokirimiwa na Bwana.
Tukizangatia matendo hayo. Basi tutakuwa ni vyombo bora, vinavyostahili kutumika kwa kazi rasmi za Mungu ambazo bado hazijafuniliwa..Zitafunuliwa katika huo ulimwengu ujao, Huko ambako jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.
Jiulize je! Wewe ni chombo kamilifu cha Kristo?
2 Timotheo 2:20-21
[20]Basi katika nyumba kubwa havimo vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali na vya mti, na vya udongo; vingine vina heshima, vingine havina.
[21]Basi ikiwa mtu amejitakasa kwa kujitenga na hao, atakuwa chombo cha kupata heshima, kilichosafishwa, kimfaacho Bwana, KIMETENGENEZWA KWA KILA KAZI ILIYO NJEMA.
Hayo ndio matendo yetu mema, yatokayo kwa Kristo Yesu, sio ulimwengu. Fanya bidii kuyatoa ndani yako.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Ni kama machungwa katika vyano vya fedha.
“Vya Kaisari mpeni kaisari” ni vipi hivyo tunavyopaswa tumpe?.
Jina la Bwana na Mwokozi wetu, (Mkuu wa Uzima na Mfalme wa wafalme), YESU KRISTO libarikiwe. Karibu tujifunze Neno la Mungu wetu lililo taa na Mwanga wa njia zetu (Zab. 119:105).
Kiashiria cha Kwanza ni UTAKATIFU:
kwamba Roho Mtakatifu yupo ndani yako (au umebatizwa na Roho Mtakatifu) ni UTAKATIFU, angalia maisha yako, je dhambi imekuwa hafifu kiasi gani, ukijilingalisha na kipindi cha nyuma.. Ukiona kuna nguvu kubwa ndani yako ya kushinda dhambi, basi tambua kuwa si wewe, bali ni uwepo wa nguvu za Roho Mtakatifu ndani yako.
Kiashairia cha Pili ni KARAMA:
Karama maana yake ni ile shauku/msukumo wa kumtumikia Mungu katika eneo Fulani, ambao unakutofautisha na mwingine.. Ukiona una shauku kubwa ya kumtumikia Mungu, na ukiangalia shauku hiyo huioni kwa mwingine aliye karibu na wewe, au ukijaribu kumweleza mwingine ni kama hakuelewi, basi fahamu kuwa hiyo shauku si wewe, bali ni Nguvu/msukumo wa Roho Mtakatifu ndani yako. (ndio maana zinaitwa karama za roho, 1Wakorintho 12:1)
Kiashiria cha Tatu ni KUCHUKIWA/KULAUMIWA BILA SABABU:
Si kila lawama ni ishara mbaya: Ukiona kila unalolifanya la KiMungu linazua lawama, au shida mahali ulipo..basi hiyo pia ni ishara nyingine ya uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yako..
1Petro 4:14 “MKILAUMIWA kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia”.
Kiashiria cha Nne: KUPUNGUA KWA HOFU NDANI YAKO.
Ukiona hofu imeisha ndani yako, kiasi kwamba wakati wengine wana wasiwasi kuhusiana na mambo Fulani wewe huna wasiwasi hata kidogo, na unajihisi kabisa kuwa Mungu yupo na wewe, basi fahamu kuwa kuna uwepo wa Nguvu za Roho Mtakatifu ndani yako, na si wewe kwa akili zako (kwasababu kwa akili za kawaida, hakuna mtu mwenye akili timamu asiyetishwa na misukosuko ya maisha).
Kiashiria cha Tano: FURAHA.
Ukiona kuna furaha isiyoelekeza ndani yako kila unapofikiria habari za YESU, na wakati mwingine unatamani kumweleza mwingine, na ukijaribu ni kama haoni kama unavyoona, basi fahamu kuwa si wewe hisia zako, bali ni nguvu za Roho Mtakatifu ndani yako, Wagalatia 5:22.
Kiashiria cha Sita: MFULULIZO WA MAFUNUO.
Ukiona kila unapotembea unamwona YESU katika neno lake, au unauona uweza wa YESU, ambao unakuletea changamko Fulani, na msisimko wa kipekee, ambao huoni kwa mwingine, basi tambua kuwa ni kazi za Roho Mtakatifu hizo ndani yako.. kwani kwa kawaida macho yaliyofumbwa hayawezi kumwona YESU popote wala kuuona uweza wake.
Vile vile ishara hii inaambatana na kupata ufahamu wa maandiko kwa namna ya kipekee sana.
SASA UFANYE NINI UNAPOGUNDUA KUWA ROHO MTAKATIFU YUPO NDANI YAKO?
Kumzimisha Roho Mtakatifu ni kitendo cha kumfanya Roho Mtakatifu aondoke ndani yako na kukaa mbali nawe aidha kwa muda kwa muda au moja kwa moja.. na vitu vinavyomzimisha Roho Mtakatifu ni dhambi za makusudi…kama uzinzi, wizi, ibada za sanamu na kupenda mambo ya kidunia.
Mambo haya mtu akiyafanya Roho Mtakatifu anaondoka ndani yake, na ile nguvu ya kushinda dhambi inaondoka ndani yake, vile vile ile nguvu ya kushinda hofu pia inaondoka ndani yake.
Kumhuzunisha Roho sawasawa na Waefeso 4:30, ni kitendo cha kumfanya Roho Mtakatifu asifurahiwe na wewe, na matokeo ya kumhuzunisha Roho Mtakatifu kwa muda mrefu, ni kuondoka ndani ya mtu.
Mambo yafuatayo yanaweza kuwa sababu ya Roho Mtakatifu kuhuzunika ndani yetu..
1. Tabia ya kukosa Imani…kama vile Bwana YESU alivyohuzunishwa na wanafunzi wake mara kadhaa, pale walipokuwa wanapungukiwa na Imani, mpaka kufikia hatua ya kuwaambia mara kwa mara “Imani yenu iko wapo”
Vile vile na sisi tunapopungukiwa na Imani katika mazingira tukutanayo hiyo Roho Mtakatifu anaugua ndani yetu, hivyo hatuna budi kuwa watu wa Imani daima.
Na Imani chanzo chake ni kusikia Neno la Mungu, (ambayo tafsiri yake ni kusoma na kujifunza biblia). Neno la MUNGU linapokaa kwa wingi ndani yetu pamoja na maombi basi viwango vyetu vya Imani vinakuwa na hivyo tunakuwa katika hali ya kumpendeza Roho Mtakatifu.
2. Tabia ya uvivu wa kiroho.. Ukiwa mlegevu kutenda yakupasayo, Roho Mtakatifu anaugua kwasababu hutumii kile ulichopewa,
Kama viashiria hivyo havipo ndani yako basi huenda Roho MTAKATIFU bado hajaingia ndani yako, au amesogea pembeni, na hiyo si kwasababu wewe ni mbaya, au una kasoro, au wengine ni bora kuliko wewe mbele zake, LA!..bali ni kwasababu bado hujafungua mlango, au ulikuwa hujui jinsi ya kuufungua mlango..kwasababu yeye anatamani aingie ndani yako Zaidi hata ya wewe unavyotamani.
Sasa swali la msingi, unaufunguaje mlango ili aingie ndani yako?
Kanuni ni rahisi sana, isiyogharimu hata theluthi ya senti moja.. na kanuni yenyewe ni kukiri tu makosa yako, kwamba wewe ni mwenye dhambi na hivyo unahitaji msaada wake (kutubu) kwa kumaanisha kabisa kuacha mambo yote mabaya.., na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU, kama bado ulikuwa hujabatizwa, baada ya hapo yeye mwenyewe ataingia ndani yako, na utaona matunda hayo na mengine Zaidi ya hayo..
Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”
Kama haujabatizwa na utahitaji msaada huo, basi waweza wasiliana nasi kwa namba zilizoanishwa hapa chini na tutakusaidia juu ya hilo.
Ubarikiwe sana.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
FAHAMU VIASHIRIA VYA MTU ALIYESAMEHEWA DHAMBI ZAKE.
JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.
Mtu yeyote aliyeokoka, ndani ya moyo wake kunatokea chemchemi ya maji yaliyo hai (Mithali 4:23). Na maji hayo huwa hayakauki, kwasababu yanatoka kwenye chanzo chenyewe halisi ambacho ni Yesu Kristo,
Na Kama vile tunavyojua maji hufanya kazi zisizopungua nne.
Ndivyo ilivyo kazi ya maji haya katika moyo wa mtu, hukata kiu ya mambo maovu(Ufunuo 21:6, Yohana 4:14), humeesha mambo mema ya Mungu , husafisha moyo wa mtu, lakini pia hugharikisha kazi za Yule mwovu.
Ndio maana maandiko yanasema pepo limtokapo mtu hupitia mahali pasipo na maji, ni kwanini? Ni kwasababu eneo lenye maji rohoni, pepo hawezi kukaa anaona gharika, na mafuriko makubwa hawezi kusogelea hapo. Na eneo lenye maji ni moyo wa mtu aliyeokoka.
Luka 11:24 Pepo mchafu amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika; asipoona, husema,
25 Nitairudia nyumba yangu niliyotoka
26 Hata afikapo, akaiona imefagiwa na kupambwa, ndipo huenda akachukua pepo wengine saba, walio waovu kuliko yeye mwenyewe, wakaingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza
Sasa wengi wetu hatujui kuwa hayo maji, yanakuwa kama maji ya “KISIMA” tu, ambayo hutulia pale pale, ni neema ya bure ambayo kila mwamini amepewa. Lakini ili ayafanye maji hayo kuwa “MITO” yaani yatiririke mbali. Si jambo la kusema tu nimeokoka. Bali kitu cha ziada lazima kifanyike kwenye maisha ya mtu.
Kama tunavyojua mito, huenda mbali kuwasaidia, hata watu wasiojua chanzo chake kilianzia wapi, Kwamfano mamilioni ya wakazi wa mji wa Kilimanjaro, kutegemea maji yanayotiririka kutoka katika mlima wa Kilimanjaro, Na ni wazi wengi wao hawajui chanzo ni mwamba gani. Lakini wananufaika. Hata Pale Edeni Mungu alitoa mto katikati ya bustani, lakini haukuishia pale bali ulitoka mpaka nje ya bustani, kuyanufaisha mataifa. (Mwanzo 2: 10-14)
Vivyo hivyo ili na wewe yale maji uliyoyapokea siku ulipookoka, kama chemchemi ya kisima, unataka yatoke nje, huna budi kufanya jambo lingine la ziada.
Ndio maana mitume walishindwa kulitoa lile pepo sugu, wakijiuliza kwanini, ndipo Bwana Yesu alisema maneno haya
Mathayo 17:21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]
Ni nini hiyo haitoki?
Ni maji yaliyo ndani yako. Kubadilika na kuwa mito, ni lazima uingie gharama za kuwa mwombaji. Si kuomba tu bali Kuomba bila kukoma. Mwombaji yoyote huuvutia uwepo wa Mungu maishani mwake. Maombi ni ‘pump ‘ya Mungu inayoyavuta yale maji nje! Yakawasaidie wengine. Huwezi kuwa mtu wa mafunuo kama huna desturi ya kuomba, huwezi kuwasaidia wengine rohoni, hata kuwaombea wasaidike, kama wewe si mtu wa kuomba. Unatazamia mumeo aache pombe, halafu sio mwombaji, utapona tu wewe peke yako, lakini hutaweza kumponya mwingine. Unatazamia familia yako iokoke, halafu wewe mwenyewe huingii gharama za mifungo na maombi, yasiyo koma, mara kwa mara, zitakuwa ni ndoto tu, labda Mungu awaguse kwa njia zake mwenyewe, lakini sio kwa matamanio yako.
Na si tu katika eneo la kuwasaidia wengine, bali hata katika maeneo ya maisha yako ambayo unataka uone maingilio Fulani ya Mungu makubwa. Huna budi kuyatoa hayo maji yaende kuponya hayo maeneo.
Maandiko yanasema imetupasa kumwomba Mungu sikuzote bila kukata tamaa (Luka 18). Hiyo ndio njia pekee itakayoleta majibu.
Yohana 7:38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.
Na Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Luka 14:27 “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU”.
Je unaelewa maana ya kuwa Mwanafunzi?
Zifuatazo ni sifa za mwanafunzi.
1. KUFUNDISHWA
2. KUJIFUNZA.
3. KUFANYA MITIHANI.
4. KUHITIMU.
Mtu akikosa hizo sifa basi sio mwanafunzi.
Na kwa upande wa BWANA wetu YESU KRISTO ni hivyo hivyo (Tutazame moja baada ya nyingine).
1. KUFUNDISHWA
Hakuna mwanafunzi yoyote anayejifundisha mwenyewe, ni lazima awe na mwalimu
Na vile vile Ili ukidhi vigezo vya kufundishwa na BWANA YESU mwenyewe ni “lazima ujikane nafsi”.. Na matokeo ya kukosa kufundishwa na Bwana ni kushindwa mitihani ya maisha ikiwemo VIPINDI VYA KUPUNGUKIWA na VIPINDI VYA KUWA NA VINGI.
Katika biblia tunaona mtu aliyefundishwa Vizuri na Bwana YESU na kuelewa ni Paulo… Yeye alifundishwa jinsi ya kuishi vipindi vyote vya (njaa na kutokuwa na njaa, vya kupungukiwa na kuongezekewa).
Wafilipi 4:12 “Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.
13 Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”
2. KUJIFUNZA.
Hii ni sifa ya pili ya Mwanafunzi yoyote, ni lazima awe anajifunza. Na kwa upande wa Imani ni lazima kujifunza kama mwanafunzi wa Kristo…
Na tukitaka tuweze kujifunza biblia na kuielewa vizuri ni lazima tujikane Nafsi na kubeba misalaba yetu na kumfuata Bwana YESU. (hakuna njia nyingine tofauti na hiyo).
Si ajabu leo hii inakuwa ngumu sana kuweza kuielewa biblia, pindi tuisomapo…sababu pekee ni kutojikana nafsi na kubeba msalaba na kumfuata Bwana YESU, tunapenda ule ukristo laini laini, ambao hauna matokeo yoyote kiroho.
3. KUFANYA MITIHANI.
Hii ni sifa ya tatu ya mwanafunzi yoyote anayesoma, ni lazima awe na vipindi vya kujaribiwa kwa mitihani.
Vivyo hivyo ili tuwe wanafunzi wa YESU wa Bwana ni lazima tupitishwe katika vipindi vya kujaribiwa na Bwana YESU mwenyewe….. Na lengo la mitihani hiyo (au majaribu hayo) ni kumwimarisha mtu huyo kiimani.
Yakobo 1:2 “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;
3 mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi”.
Na madhara ya kukosa kujaribiwa kwa mitihani ya BWANA YESU ni kushindwa kuhitimu na hatimaye kukosa cheti.
4. KUHITIMU.
Mwanafunzi anayehitimu ni yule aliyemaliza mitihani yote na kufaulu, (huwa anapewa cheti) kile cheti ni kibali maalumu, na fursa pamoja na heshima ya daima kwa mwanafunzi yule.
Vile vile na mtu aliye mwanafunzi wa BWANA YESU, akiisha kumaliza majaribu yote na kuyashinda, atahitimu kwa kupewa cheti ambacho ni TAJI YA UZIMA..
Yakobo 1:12 “ Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao”.
Jiulize je wewe ni Mwanafunzi wa BWANA YESU au ni mfuasi tu?…. Waliokuwa wanamfuatilia Bwana YESU ni wengi lakini waliomfuata na kuwa wanafunzi wake walikuwa wachache sana.. Wengine wote walikuwa ni washabiki tu aidha wa miujiza au wa siasa, lakini waliojiunga na chuo cha Bwana YESU walikuwa ni wachache sana.
Na kanuni ya kujiunga na chuo hicho cha Bwana YESU na kuwa mwanafunzi wake si nyingine Zaidi ya hiyo ya “KUJIKANA NAFSI NA KUBEBA MSALABA”.
Luka 14:27 “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU”.
Na kumbuka hakuna tafsiri nyingine ya UKRISTO au kuwa MKRISTO Zaidi ya UANAFUNZI..
Matendo 11:26 “….Na WANAFUNZI waliitwa WAKRISTO kwanza hapo Antiokia”.
Hivyo ukitaka kujijua kama wewe ni Mkristo au la!.. sipime tu kama umeshakuwa Mwanafunzi wake, kama huna sifa hizo hapo juu za uanafunzi bado hujawa MKRISTO.
Bwana YESU atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Bwana alimaanisha nini kusema “Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake”?
Mtu akija kwangu naye HAMCHUKII baba yake hawezi kuwa mwanafunzi wangu?
Leo hii kumekuwa na hofu nyingi katikati ya watu, juu ya historia na machimbuko ya familia zao. Wengine wameona maisha yao au tabia zao za sasa zimeathiriwa na chimbuko la familia zao, au koo zao, au mababu yao. Na hivyo hawajui wafanyeje.
Lakini ukweli ni kwamba hakuna hata mmoja wetu ambaye, chimbuko lake halijaathiriwa, Tukianzia na la Bwana wetu Yesu Kristo, na ndio maana biblia imeandikwa tukapewa, ili kutuonyesha sisi njia, ya kusimama na shindana na nguvu za Yule mwovu kwa ujasiri wote bila woga.
Kitabu cha Mathayo, kinaanza na kueleza ukoo wa Yesu. Kulikuwa na sababu ya kutangulizwa historia ya ukoo wake, ili Mungu kutufundisha sisi jambo. Watu wengi wakiangalia ule mtiririko, wanadhani Mungu anatuonyesha jinsi Yesu alivyotokea katika ukoo hodari, mashuhuri. Lakini Hapana. Ukweli ni kwamba hakukuwa na umuhimu wowote, kwa wengi walioorodheshwa katika ukoo wake.
Lakini nataka tuone, jinsi ukoo ule ulivyovurugwa, kiasi kwamba kama Mungu angetazama usafi basi, usingestahili hata kidogo kumleta mkombozi duniani. Katika ukoo wake hakukuwa tu na wema, lakini kulikuwa na “makahaba” kulikuwa na pia “wazinzi-waliokubuhi”, kulikuwa na “makafiri” . Kwamfano Yule Rahabu, alikuwa ni kahaba, tena kahaba kweli kweli. Tena Kulikuwa na Ruthu, mwanamke wa kimataifa, ambaye Mungu aliwakataza kwa nguvu sana, wayahudi wasitwae wanawake wa kimataifa kuwaoa, mbegu takatifu zisichangamane na mbegu nyingine (Ezra 9:2) ni unajisi, lakini hapa ikawa tofauti, mwanamke wa kimataifa akaingizwe kwenye ukoo. kama huyo haitoshi alikuwepo mzinzi Tamari, ambaye, yeye alifanya hila akalala na mkwe wake, kumzaa Peresi,..Jambo lisilofikirika kiakili, vilevile, alikuwepo Bersheba mke wa wizi, wa Mfalme Daudi, ambaye miongoni mwa wake halali wa Daudi hakuwepo, lakini alichaguliwa yeye, kuupitisha uzao wa Kristo, na wale wasafi wakaachwa.
Tusome..
Mathayo 1:1 Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo, mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu.
2 Ibrahimu alimzaa Isaka; Isaka akamzaa Yakobo; Yakobo akamzaa Yuda na ndugu zake;
3 Yuda akamzaa Peresi na Zera KWA TAMARI; Peresi akamzaa Esromu; Esromu akamzaa Aramu;
4 Aramu akamzaa Aminadabu; Aminadabu akamzaa Nashoni; Nashoni akamzaa Salmoni;
5 Salmoni akamzaa Boazi KWA RAHABU; Boazi akamzaa Obedi KWA RUTHU; Obedi akamzaa Yese;
6 Yese akamzaa mfalme Daudi. Daudi akamzaa Sulemani KWA YULE MKE WA URIA ;
7 Sulemani akamzaa Rehoboamu; Rehoboamu akamzaa Abiya; Abiya akamzaa Asa;
8 Asa akamzaa Yehoshafati; Yehoshafati akamzaa Yoramu; Yoramu akamzaa Uzia;
9 Uzia akamzaa Yothamu; Yothamu akamzaa Ahazi; Ahazi akamzaa Hezekia;
10 Hezekia akamzaa Manase; Manase akamzaa Amoni; Amoni akamzaa Yosia;
11 Yosia akamzaa Yekonia na ndugu zake, wakati wa ule uhamisho wa Babeli.
12 Na baada ya ule uhamisho wa Babeli, Yekonia akamzaa Shealtieli; Shealtieli akamzaa Zerubabeli;
13 Zerubabeli akamzaa Abihudi; Abihudi akamzaa Eliakimu; Eliakimu akamzaa Azori;
14 Azori akamzaa Sadoki; Sadoki akamzaa Akimu; Akimu akamzaa Eliudi;
15 Eliudi akamzaa Eleazari; Eleazari akamzaa Matani; Matani akamzaa Yakobo;
16 Yakobo akamzaa Yusufu mumewe Mariamu aliyemzaa YESU aitwaye Kristo.
17 Basi vizazi vyote tangu Ibrahimu hata Daudi ni vizazi kumi na vinne; na tangu Daudi hata ule uhamisho wa Babeli ni vizazi kumi na vinne; na tangu ule uhamisho wa Babeli hata Kristo ni vizazi kumi na vine.
Hivyo ukoo wa Bwana wetu Yesu Kristo, ulivurugwa-vurugwa, tunaweza kusema haukuwa msafi, kulinganisha na koo za wayahudi wengine. Lakini huyo ndiye aliyekuja kumpendeza Mungu kuliko wote, ijapokuwa alitokea katika chimbuko lililokorongoka, huyo ndiye aliyekuja kuwa mkombozi, huyo ndiye aliyekuja kuwafungua watu na kukata mizizi yote ya laana, na kuwa Baraka kwa ulimwengu.
Usiogope, yawezekana kweli, chimbuko lenu ni bovu, ni makahaba tu, ni walevi tu, mna magonjwa ya kurithi yanatembea, mnaudhaifu Fulani, maskini wa kupindukia, hamuoelewi, hamzai. Nataka nikuambie wacha kuhangaika kuufikiria ukoo wako. Kwasababu hata iweje hakuna aliyewahi kutokea mwenye chimbuko safi hapa duniani. Wewe mtazame Kristo tu, aliyemaliza yote pale msalabani. Amini tu kazi yake aliyoimaliza kwako.
Unapookoka, huna laana yoyote ndani yako, haijalishi ukoo mzima walizindika, haijalishi mna mizimu na mikoba ndani.. Hiyo ndio bye! Bye!, imeisha!. Haina nguvu ndani yako, wala usiipe kibali, mwamini Yesu aliyekukomboa.
Usiwe mtu wa kuzunguka huku na huko kuvunja laana za ukoo, utavunja ngapi? Ni mababu wangapi wamepita huko nyuma, itakupasa basi urudi sasa mpaka Adamu. Uvunje laana zote. Hivyo kua kiroho, mwamini Yesu aliyekukomboa. Matatizo ya kifamilia mliyonayo, wanayo hata wale watumishi wa Mungu, isipokuwa kwa namna tu nyingine. Lakini wao wamemwamini Kristo aliyewakomboa, ndio maana hawana laana yoyote. Lakini kaulizie huko kwao kukoje watakuambia. Ndugu ukiokoka, Ya kale yamepita tazama, yamekuwa mpya. Unachopaswa kufanya baada ya kuokoka tu , ni kuendelea kumjua zaidi Kristo ili uwe na amani,sio kuchimbua tena ya kale, jifunze kwa ukoo wa Yesu .
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini vizazi vya ukoo wa Yesu vinajipinga katika Mathayo na Luka.