Category Archive maswali na majibu

Maana ya Mhubiri 10:15 Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja,

SWALI: Je, mstari huu tunaousoma kwenye Mhubiri 10:15 una maana gani?

Mhubiri 10:15

[15]Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja, Maana hajui hata njia ya kuuendea mji.


JIBU: Kwa namna ya kawaida ya kibinadamu tunajua watu wengi hutamani kuishi mijini kuliko mashambani. Kwasababu mijini huduma zote hupatikana, na ni mahali pa raha. Hata kazi, mtu anazozifanya mashambani, wengi wao ni ili matunda yake wakayafurahie mjini, Au wakaziuze bidhaa zao huko wawe matajiri.

lakini tengeneza picha mtu, ambaye anajitaabiisha kufanya kazi kwa lengo la kuzifurahia mjini, halafu hajui njia ya kufika huko, kinyume chake ndio anakwenda mbali zaidi na mji, anaelekea majangwani au mabondeni?  ni wazi kuwa mtu kama huyo  hawezi kuwa na raha katika kazi yake, kwasababu taabu yake haina faida, alikosa malengo au hakuwa na maarifa sahihi.

Ni ufunuo gani upo nyuma yake?

Na sisi pia tuliomwamini Kristo. Tuna mji ambao tunatarajia kuungia, ndio ule Yerusalemu mpya ishukayo kutoka mbinguni kwa Baba..

Ufunuo  21:2-3

[2]Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe. 

 [3]Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. 

Anaendelea kusema…

Ufunuo  22:14-15

[14]Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake. 

[15]Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.

Huo ndio ule mji halisi ambao hata Ibrahimu aliona, ikamfanya aishi maisha kama ya mpitaji hapa duniani.

Waebrania 11:8-10

[8]Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako. 

 [9]Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile. 

 [10]Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu. 

Umeona na sisi ili tuweze kuonekana tumestahili kuuingia katika mji huo wa mbinguni hatuna budi tuwe tumeokolewa na YESU KRISTO. Kwasababu yeye ndio NJIA ya kuuingia mji.

Ukiwa nje ya Kristo tafsiri yake wewe ni mpumbavu, kwasababu taabu yako yote ya hapa duniani, haikufikishi popote haikuepeki mjini mwa Mungu, itakuchosha tu, utakuwa na magorofa, utaijaza akaunti fedha, utakuwa ni miradi mikubwa lakini mwisho utakufa, na kwenda kaburini. Lakini ukiiona njia na kuifuata Yerusalemu basi hufanyi kazi ya bure, unapojiwekea hazina kule hufanya kazi ya kushosha, ni uzima baada ya kifo. Utafaidi matunda yake

Je umeokoka?

Ikiwa bado na unatamani kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo >>>  KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yerusalemu ni nini?

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)Maana ya Mhubiri 1:9 “wala jambo jipya hakuna chini ya jua”. (Opens in a new browser tab)

MJI WENYE MISINGI.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Naliazimu nisijue neno lolote kwenu?” (1Wakorintho 2:2).

Jibu: Turejee..

1Wakorintho 2:2 “Maana naliazimu nisijue neno lo lote kwenu ila Yesu Kristo, naye amesulibiwa”

Haya ni maneno ya Mtume Paulo aliyowaambia watu wa kanisa la Korintho… sasa tunaweza kuyaweka katika lugha rahisi namna hii…. “Nilipokuja kwenu (ninyi Watu wa Korintho) nilikusudia kufahamu yale mnayoyajua kumhusu YESU KRISTO, ambaye amesulubiwa na si jambo lingine lolote”.

Maana yake Paulo alitaka kuelewa ni nini Wakorintho wanaelewa kumhusu YESU aliyesulubiwa, hicho tu ndicho alicholenga kujua, na hakutaka kujua mambo mengine..

Kwanini alitaka kujua ufahamu wao kuhusu YESU?…

Ni kwasababu alijua kama wakimfahamu YESU kama inavyopaswa kufahamika, basi Imani yao itakuwa katika msingi thabiti.. Lakini kama wakimfahamu Yesu kwa ushawishi wa Maneno, basi Imani yao itakuwa katika hekima za kibinadamu.

1Wakorintho 2:1 “Basi, ndugu zangu, mimi nilipokuja kwenu, sikuja niwahubiri siri ya Mungu kwa ufasaha wa maneno, wala kwa hekima.

2  Maana naliazimu nisijue neno lo lote kwenu ila Yesu Kristo, naye amesulibiwa.”

Vile vile kama watamfahamu YESU wa ishara na miujiza tu, basi Imani yao itakuwa katika miujiza  na ishara kama wale Wasamaria (Yohana 6:26) na si katika Imani thabiti ya YESU ALIYESULIBIWA

Lakini kama wakimfahamu YESU kama Mwokozi aliyesulibiwa kwaajili ya makosa yao na dhambi zao, basi Imani yao itakuwa thabiti, na yenye uhakika.. Itakayowapelekea kuungama dhambi, na kutafuta kuyafanya mapenzi ya Mungu, jambo ambalo ni msingi sana, na ambalo ndio tiketi ya kumwona Mungu (Mathayo 7:21-23)

Hivyo na sisi kilicho kikubwa na cha Msingi ni kuishikilia ile Imani ya Msingi (ambayo ndio Imani mama), ambayo inatupeleka/kutusukuma kujitakasa na kujiepusha na uchafu(dhambi).

Bwana atusaidie, na Bwana atubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! Kiongozi wa dini anaouwezo wa kusamehe dhambi?

LAKINI HAITAKUWA HIVYO KWENU.

MSIJISUMBUE KWA NENO LOLOTE.

Je! dhambi zote ni sawa Kuna dhambi kubwa na ndogo?

MSINGI WA NYUMBA YA MUNGU, NI JINA LA MUNGU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! Malaika wanazaliana?

Wapo wanaodhani kuwa malaika wanao uwezo wa kuzaliana sawasawa na habari ya wana wa Mungu na binti za wanadamu inayozungumzwa  katika kitabu cha Mwanzo.

Mwanzo 6:1-3,  Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.

3 Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.

Kwa habari hiyo wengi hufikiri, hao wana wa Mungu walikuwa ni malaika, ukweli ni kwamba hawakuwa malaika bali wanadamu. Yesu alisema, tutakapofika mbinguni, hatutaoa wala kuolewa, tutafanana na malaika, Kuonyesha kuwa malaika hawazaliani. (Mathayo 22:30)

Vilevile katika habari hiyo hatuoni kwamba malaika wakiadhibiwa, bali wanadamu, kuonyesha kuwa ni jambo la kibinadamu. Kwa urefu wa fundisho hilo, fungua hapa >>> WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

Viungo vya uzazi viliumbwa mahususi kwa viumbe wa ulimwenguni, kwa lengo la kuijaza nchi. Lakini vya mbinguni havikuumbwa kwa utaratibu kama huu wa kwetu.

Hivyo kwa hitimishi ni kuwa malaika watakatifu hawazaliani. Kwasababu wao ni viumbe vya rohoni, waishio milele. Hivyo hawahitaji kuzaliana.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! mbinguni kuna malaika wa kike?. Na je! tukifika mbinguni tutafanana wote?

Je malaika wote wana wabawa?

KUNDI LA MALAIKA WALETAO MABAYA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je malaika wote wana wabawa?

Katika maandiko tunaona, Malaika wakionekana kwa mifano ya viumbe mbalimbali vya duniani, ikiwemo wanadamu. Kwamfano wale wenye uhai wanne, wapo waliokuwa na uso kama wa tai, wengine simba, wengine ndama na wengine wanadamu(Ufunuo 4:7). Maserafi na Makerubi walionekana kuwa ni malaika wenye mabawa. (Kutoka 25:20, Isaya 6, Ezekieli 10).

Lakini wapo pia walionekana kwa mfano wa wanadamu kabisa, mfano wa hawa ni wale waliomtembelea Ibrahimu wakala naye, kisha wakaenda Sodoma. (Mwanzo 18 &19)

Kwahiyo si malaika wote waliokuwa na mwonekano wa mabawa. Lakini ni vema kufahamu kuwa mabawa au mionekano si vitu ambavyo vinawafanya watembee au wawe na uwezo ule, wale ni viumbe vya rohoni hivyo hawategemei kanuni za kidunia kutembea, ijapokuwa wataonekana kama wanadamu bado sio wanadamu, hawawezi kuzaliana, wataonekana na mifano ya ndege sio ndege wala akili zao hazipo vile.

Kwahiyo kujua kama malaika wote wana mabawa au hawana, si muhimu. Muhimu ni kufahamu ni kwamba wamewekwa kutuhudumia sisi tutakaourithi wokovu. Hivyo tumtiipo Kristo maana yake ni tunaruhusu huduma yao kutenda kazi katikati yetu, hapa ulimwenguni.

Waebrania 1:13  Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? 14  Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?

Lakini kinyume chake ni kweli umtiipo shetani, tafsiri yake ni kuwa unayaruhusu mapepo kufanya kazi hapa duniani.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MALAIKA NI WALIMU WA SIFA KWETU, TUJIFUNZE KWAO!

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

(Opens in a new browser tab)HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Tafsiri ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;

SWALI: Maana ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake; Naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa.


JIBU: Mstari huo una vipengele viwili cha kwanza ni Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake

Na cha pili ni naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa.

Tukianzana na hicho cha kwanza. Tufahamu kuwa Mungu ameiandika injili yake sio tu kwenye kitabu chake, bali pia kwenye vitu vya asili, ndio maana Yesu alitumia mifano mingi ya namna hiyo, kuzungumza nao habari zake mwenyewe. Kuanzia wakulima, mimea, wanyama, wafanya biashara, wafalme n.k.

Sasa hapa anasema yeye atunzaye mtini atakula matunda yake. Kumbe kula matunda ni “kutunza”. Usipotunza huwezi pata chochote. Ili uone kazi yako, utaiwekea mbolea, utaipalilia, utaipiga dawa n.k. Na mwisho utakuwa mvumilivu aidha miaka mitatu/ minne ukisubiri  mazao.

Halidhalika rohoni. Sisi kama watoto wa Mungu (tuliookolewa), kila mmoja wetu anao “mtini” moyoni mwake, na huo si mwingine zaidi ya Yesu Kristo. Wengi wasichojua ni kwamba Kristo huanza kama kichanga, kisha huwa kijana mdogo, baadaye huwa mtu mzima, na mwisho huanza kutenda kazi zake. Kama tu alivyokuwa hapa duniani alivyoishi na Mariamu na Yusufu, hakuanza kufanya chochote pindi anazaliwa.

Hivyo usipomlea ipasavyo hutafaidi matunda yake vema. Ndio mfano wa mpanzi ambao Yesu mwenyewe aliutoa, akasema zile mbegu ziliporushwa nyingine zikaishia njiani, nyingine kwenye miamba, nyingine kwenye miiba, na nyingine kwenye udongo mzuri, moja ikazaa thelathini, nyingine sitini, nyingine mia. Akatoa ufafanuzi wake, kwamba zile zilizofanikiwa kuzaa, ni kwamba zilichangiwa na KUVUMILIA (Luka 8:15). Sasa kuvumilia nini? Kuvumilia  hatua zote tatu za mwanzo, yaani dhiki kwa ajili ya Kristo, kujiepusha na anasa, udanganyifu wa mali, na uvivu wa kulitendea kazi Neno.

Ukuaji wa kiroho tafsiri yake ni ‘Kristo kukua ndani yako’. Ukiona upo  ndani ya wokovu kwa miaka mingi, halafu huoni matunda yoyote ya wokovu wako, katika ufalme wa Mungu, tatizo linakuwa hapo, hukuwa na nafasi ya kuutunza mtini wako.

Ukiokoka, ni lazima bidii ya kusoma Neno iwe ndani yako kila siku, usiwe mvivu wa maombi, vilevile epuka maisha ya kidunia, na ubize uliopitiliza, ambao unakufanya hata nafasi ya Mungu wako unakosa. Ukizingatia hayo, baada ya kipindi Fulani utaona Kristo anavyojengeka nafsini mwako , na kukutumia.

Lakini pia sehemu ya pili inasema naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa,. Ni hekima ya kawaida, ukiwa mfanyakazi mwema kwa bwana wako, hawezi kukuchikia kinyume chake atakupa heshima yako, lakini pia na watu wengine wote wa nyumbani kwake watafanya hivyo.

Si zaidi Mungu?

Heshima hasaa kwa Mungu wako, sio kumwambia “Shikamoo” au kuomba kwa sauti ya unyenyekevu, au kuinamisha kichwa uwapo ibadani. Heshima yake hasaa ni pale unapomtumikia, unapotii agizo lake la kuwaeleza wengine habari za injili, na pale naposimama katika nafasi yako kwenye mwili wa Kristo.

Tutafute kuheshimiwa na Bwana kwa kuwashuhudia wengine injili.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MTINI, WENYE MAJANI.

Biblia imemaanisha nini kusema Nyoka atakula mavumbi?(Opens in a new browser tab)

(Opens in a new browser tab)Je ile habari ya mtini kunyauka inajichanganya?(Opens in a new browser tab)

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo.

SWALI: Nini maana ya mstari huu Yohana 12:35

Basi Yesu akawaambia, Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako.

JIBU:  Yesu alipokuwa duniani, alijilinganisha na Nuru ya uimwengu huu (jua), Yohana 11:9-10…Na hivyo mara kwa mara katika mafundisho yake aliwasisitiza wayahudi juu ya jambo hilo, lakini hawakulielewa.

kwa kawaida jua huwa halizimi, lakini pia huwa halitulii mahali pamoja(kwa jinsi ya kawaida). Litachomoza, litazama,.litaendelea hivyo hivyo katika mzunguko wake. Wakati linaangaza upande mmoja, upande mwingine wa dunia ni giza.

Sasa wayahudi walipomwona Kristo, wengine walimpokea, wengine walimpinga, wengine walimwonea wivu, wengine walimwita mchawi.

Lakini wote hawa, Neema bado ilikuwa juu yao. Bado Kristo alikuwa anawakusanya kama vile kuku akusanyaye vifaranga vyake chini ya mbawa zake (Luka 13:34). Yesu hakudhubutu kwenda kuhubiri kwenye mataifa mengine ambayo yalihitaji hata kumfanya mfalme, ijapokuwa walikuwa wanampinga vikali.

Sasa ndio hapa akawaambia..kwambo hili halitaendelea sana…kuna wakati pia nuru hii  mnayoiona sasa itawafikie na wengine..

ndio hapo akawaambia..

“Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako”.

Maana yake ni kuwa anawaambia aminini mapema, kwasababu nguvu hii inayowalilia mioyoni mwenu itaondoka … Mkikataa neema, mkikataa kujazwa Roho,  Kamwe hamtaweza kulishinda giza kwa nguvu zenu.

Na tunaona ni kweli, jambo hilo liliendelea kwa kipindii kifupi, baada ya Kristo kufufuka, na kupaa, injili kidogo kidogo ikaanza kutoka kwa wahayudi.ikaenda kwa watu wa mataifa yaani mimi na wewe..

Tangu ule wakati, wa mitume, mpaka leo hii inakaribia sasa miaka 2000, wayahudi bado hawajafumbuliwa macho, kwasababu wokovu ni neema kuamini. Sio utashi wa mtu.

Sasa leo hii sisi watu wa mataifa tunayo injili, lakini kanuni ya Nuru ni ileile, huzunguka. Na kwetu pia haitadumu milele. Mungu aliahidi ule mwisho unapokaribia kufika (ambao ndio huu) atawarudia tena Israeli kwa kipindi kifupi. na hivyo kwa upande wetu, hakutakuwa na neema tena ya wokovu itakayokuwa imesalia..

Warumi 11:25-26

[25]Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

[26]Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa,

Mwokozi atakuja kutoka Sayuni;

Atamtenga Yakobo na maasia yake.

Hii ni kutufunisha pia Bwana hasemi na wayahudi tu, bali na anasema sisi pia…

Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako.

Je unaenda katika nuru hiyo? Kama bado wasubiri nini. Geuka leo uoshwe dhambi zako upokee uzima wa milele, usipofanya hivyo kamwe huwezi kulishinda giza.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.

Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,

(Opens in a new browser tab)Mistari ya biblia kuhusu maombi.(Opens in a new browser tab)

AGIZO LA UTUME.(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

TUJIHADHARI NA KUKANWA!.

Mathayo 10:33 “Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni”

Jina la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze biblia.

Hebu tulitafakari kwa upana kidogo  hili neno “kukanwa”.

Kukanwa ni ile hali ya kukataliwa na mtu unayemjua, unayetembea naye daima, uliyeweka matumaini yako kwake, mnayekubaliana  au uliye na mahusiano naye ya karibu”

Na ipo tofauti ya “kukana na kusaliti”…kwa urefu juu ya tofauti ya maneno haya mawili fungua hapa 》》Tofauti kati ya kukana na kusaliti ni ipi?

Sasa Bwana YESU anasema kuwa tukimkana mbele ya watu naye atatukana mbele ya Baba yake kule mbinguni.

Hebu tengeneza unafika kule, halafu unakanwa na yule ambaye ulikuwa unaona anatembea na wewe kila siku, anakuponya, anakulinda, ukiliita jina lake maajabu yanatokea, pepo zinatoka na miujiza mingi inafanyika.

Halafu huyu huyu ambaye ulipokuwa duniani alikuwa haonyeshi dalili ya kukukataa lakini unafika kule anakukana anasema hakujui!..ni jambo gumu sana kuamini!.

Lakini ndivyo itakavyokuwa siku ile..

Mathayo 7:22 “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.”

Hatuna budi kukaza mwendo daima na kila siku tukihakiki ni lipi limpendezalo Bwana (Waefeso 5:10).

Mtume Paulo ijapokuwa alikuwa na wingi wa mafunuo lakini alisema maneno haya..

1 Wakorintho 9:26 “Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;

27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.

Na pia alisema…

Wafilipi 3:12 “Si kwamba nimekwisha kufika, au nimekwisha kuwa mkamilifu; la! Bali nakaza mwendo ili nipate kulishika lile ambalo kwa ajili yake nimeshikwa na Kristo Yesu.

13 Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele;

14 nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MFALME ANAKUJA.

JINA LAKO NI LA NANI?

UWEZA WA MUNGU NJE YA WAKATI.

Kulabu ni nini katika biblia?(2Wafalme 19:27)

JE UNAMHUBIRI KRISTO KATIKA KWELI YOTE?.

Rudi Nyumbani

Print this post

Bwana YESU KRISTO anatuombeaje kule juu mbinguni? (Warumi 8:34)

Swali: Maandiko yanasema KRISTO ameketi kutuombea, hata tufanyapo dhambi?


Jibu: Tafadhali soma taratibu na kwa umakini…

Warumi 8:34 “Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; TENA NDIYE ANAYETUOMBEA”.

Ni kweli Neno la Mungu linasema BWANA WETU YESU KRISTO, katika mstari huo na linazidi kututhibitishia tena katika 1Yohana 2:1.

1Yohana 2:1 “Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi TUNAYE MWOMBEZI KWA BABA, Yesu Kristo mwenye haki”

Lakini ni vizuri kuzijua lugha za kiroho na namna ya kuzitafsiri, vinginevyo itatuwia vigumu sana kuielewa biblia na hata wakati mwingine kujikuta tunaabudu sanamu kwa kushindwa kuzipambanua lugha za kiroho,

Kwamfano kuna mahali Bwana YESU alisema Mtu asipoula mwili wangu, na kuinywa damu yangu hana uzima ndani yake (soma Yohana 6:53), sasa tukiuchukua huo mstari kama ulivyo na kwenda kutafuta mwili wa Bwana kama nyama, na Damu yake kama ilivyo na kuinywa, tutakuwa tumeshindwa kutafsiri vyema lugha ya biblia, na hivyo tutakuwa tumefanana na waganga na wachawi walao nyama na kunywa damu!.

Lakini kama tukiweza kuelewa maana ya mwili wake Bwana Yesu na damu yake kuwa ni ule mkate na kile kikombe, sawasawa na (Mathayo 26:26-27) tutakuwa tumeenda sawasawa na Neno la Mungu.

SASA KWA MSINGI HUU, TUTAKUWA TAYARI KUJIFUNZA NI KWA NAMNA GANI KRISTO ANATUOMBEA KWA BABA.

Katika hiko kitabu cha Warumi mlango wa 8:34 tuliposoma kuwa KRISTO ndiye anayetuombea, hebu turudi mistari kadhaa nyuma mpaka ule mstari wa 26, tuone jambo..

 Warumi 8:26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini ROHO MWENYEWE HUTUOMBEA KWA kuugua kusikoweza kutamkwa.

27  Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu”

Angalia hapa; Katika ule mstari wa 34 tumesoma kuwa ni BWANA YESU ndiye anayetuombea, lakini tena katika mstari wa 26 ndani ya sura hiyo hiyo, tunasoma kuwa ni ROHO MTAKATIFU ndiye anayetuombea.. Sasa swali ni yupi kati ya hawa wawili anayetuombea kwa Baba?… ni Roho Mtakatifu au ni Bwana YESU??.

Sasa jibu la swali hili ni rahisi sana na ndio tunaelekea katika kiini cha mada hii.

Jibu la swali hili tunalipata katika kitabu kile cha 2Wakorintho 3:17, sikiliza Neno la Mungu linavyosema…

2Wakorintho 3:17  “Basi Bwana ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru”.

Hapo anasema lakini “Bwana” (yaani YESU)..ndiye “Roho”(yaani Roho Mtakatifu).. kumbuka hapo Roho imeanza kwa herufi kubwa kuwakilisha Roho Mtakatifu. (Popote pale Roho inapoanza kwa herufi kubwa inamaanisha Roho wa Mungu).

Hivyo kulingana na hayo maandiko, ni sahihi kabisa kusema BWANA YESU ndiye ROHO MTAKATIFU, na Roho mtakatifu ndiye Bwana YESU.. Kwahiyo mahali popote asemapo Roho Mtakatifu ni Bwana YESU ndiye kasema..

Ndio maana utaona katika kile kitabu cha Ufunuo Mlango wa 2 na wa 3 katika jumbe za yale makanisa saba, utaona ujumbe unaanza YESU ANASEMA, na unamaliza ROHO AYAAMBIA MAKANISA, ikiwa na maana kuwa Roho ndiye huyo huyo Bwana.

Vile vile Roho Mtakatifu akiomba ni  Bwana ameomba.

Sasa swali la mwisho ambalo litahitimisha Mada hii, ni je!, Kama Bwana YESU ndiye Roho Mtakatifu, je huyo Roho Mtakatifu anatuombeaje sawasawa na huo mstari wa 26?

Roho Mtakatifu (ambaye ndiye Bwana mwenyewe) hatuombei kama sisi tunavyoombeana!.. La! Yeye anaomba ndani yetu.. Maana yake tuombapo sisi, basi yale maombi yetu anayachukua na kuyapeleka mbele za Baba katika lugha nzuri Zaidi, katika maelezo mazuri Zaidi.

Lakini si kwamba tumelala au tunacheza, au tunafanya mambo yetu mengine basi wakati huo huo yeye kule anatuombea, hapana! Hiyo si tafsiri yake kabia..

Kwa urefu jinsi Roho Mtakatifu anavyotuombea fungua hapa utapata kuelewa vizuri sana >>ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba jinsi Bwana YESU anavyotuombea ni kwajinsi ya Roho Mtakatifu, na Roho Mtakatifu anachukua yale maombi yetu na kuyapeleka kwa Baba kwa lugha kamilifu Zaidi.. Hivyo kamwe usiwaze kuwa Bwana  YESU yupo mbinguni mbele za Baba, akisali kwaajili yetu, bali ni kwa njia ya Roho wake mtakatifu ndani yetu, ndipo anapotuombea.

Kwanini tunajifunza haya?.

Ni kwasababu zipo Imani zilizoanzishwa na ibilisi mwenyewe zisemazo kuwa “hatuna haja ya kuomba, kwasababu Bwana YESU yupo mbinguni anatuombea usiku na mchana”…

Kamwe usidanganyike na hayo mafundisho kwani ni mafundisho ya Adui, ibilisi… Tusipoomba na Roho Mtakatifu hawezi kuomba, na Roho Mtakatifu asipoomba ni Bwana hajaomba.. Lakini tuombapo, Roho Mtakatifu ni kipaza sauti chetu kwa Baba..kwahiyo maombi ni lazima… (Pitia tafadhali somo la jinsi Roho Mtakatifu anavyotuombea).

Na mwisho kabisa, hakuna mtakatifu yoyote aliyekufa au aliyenyakuliwa anayetuombea… NI YESU TU PEKE YAKE, kwa NJIA YA ROHO WAKE MTAKATIFU, ndiye anayetuombea.. Hivyo Mtakatifu Mariamu, hawezi kutuombea, wala Eliya, wala Musa, wala Henoko, wala mtu mwingine yoyote aliye hai wala aliyekufa…(Hawana na hatuna hivyo vigezo).

Kwahiyo lililo kubwa na la msingi sana, ni kutafuta Roho Mtakatifu kwasababu kwa kupitia huyo ndio maombi yetu yatafika na kukubaliwa, na tena mtu asiyekuwa na Roho Mtakatifu huyo si wake kulingana na biblia (Warumi 8:9)

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)

NJIA/BARABARA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Roho Mtakatifu ni nani?.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! Ni dhambi kutumia njia za kisasa za uzazi wa mpango.

Kwanza ni vema kufahamu uzazi wa mpango ni nini na kama ni dhambi au la!.

Uzazi wa mpango ni kuzaa kwa mpangilio ulioutaka wewe, kwamfano ukijiwekea malengo ya kuzaa watoto 30, huo ni uzazi wa mpango maadamu yalikuwa ni malengo yako, au ukijiwekea malengo ya  kuzaa mmoja maisha yako yote huo pia ni uzazi wa mpango. Kinyume chake uzao usio wa mpango, ni ule wa  kutojali idadi ya watoto utakaouzaa, wala kutojali muda wa uzaaji wako.

Lakini je! Jambo hili linaruhusiwa na Mungu?

Ukweli ni kwamba uzazi wa mpango si dhambi. Kwasababu gani?

Licha ya kwamba Mungu ameweka maagizo yake kupitia biblia takatifu, lakini pia, ameweka hekima yake kupitia mambo ya asili (1Wakorintho 11:14, Warumi 1:20), Hivyo mambo ya asili yanatufundisha pia agizo la Mungu .

Si kila wakati mama atashika ujauzito, bali upo wakati wa hatari na wakati usio wa hatari. Sasa kwa hekima huo tayari ni utaratibu Mungu kamwekea mtu, atambue majira yake, achukue tahadhari. Umeona? Kwa namna nyingine Mungu anasema, kuna majira utapata mtoto, na kuna majira hutapata mtoto. Hivyo uamuzi ni wako, ukitaka kuzingatia mazunguko huo, ni wewe, usipojali pia ni wewe.

Sasa mtu ambaye anayechagua kuzingatia mzunguko huo wa asili wa Mungu, huyo tayari yupo katika uzazi wa mpango. Na pia ni agizo la Mungu tuwe na uwezo wa kuwatunza wale wa nyumbani kwetu (1Timotheo 5:8)

Lakini je! Vipi ambao wanatumia njia za kisasa za uzazi wa mpango je na wao wapo sawa?

Tukisema njia za kisasa, ni kama zile za kutumia vidonge, kutumia sindano, kutumia vizuizi kama mipira (kwa wanaume na wanawake), kuweka kitanzi, na kuweka vipandiki/vijiti.  Zote hizi ni njia za kisasa.

Hapa ni lazima tufahamu pia lengo ni nini?. Bila shaka lengo ni lile lile moja la uzazi wa mpango kwa wanandoa, na si vinginevyo. Lakini mwanadamu ameamua kutumia njia zake za kisasa, ili kufanikisha hilo?

Je! Ni kosa?

Ili kujibu swali hilo, tufikirie pia mambo mengine ya kisasa, leo hii tuna vitu vingi vya kisasa vimebuniwa na wanadamu, kwamfano kuna kuku wa kienyeji lakini pia wapo wa kisasa, kuna mchicha wa kienyeji lakini pia ipo ya kisasa, kuna matunda ya kienyeji lakini pia yapo ya kisasa. Je! Ni dhambi kutumia vitu hivyo, kwasababu vimebuniwa na mwanadamu?

Jibu ni hapana.

Lakini vinaweza kuwa na madhara yake, kwasababu mwanadamu hawezi kuumba kitu kiukamilifu. Ndio maana asilimia kubwa ya vitu hivi vya kisasa, huwa si vizuri kiafya. Vivyo hivyo katika matumizi ya njia za kisasa za uzazi wa mpango. Yaweza isiwe dhambi kwako kutumia. Lakini madhara ya kiafya, pia waweza kukumbana nayo. Wengine hupata shida ya vizazi, wengine ugumba kabisa kulingana na njia iliyotumika, lakini wengine hawapatwi na madhara. Hivyo amani ya Kristo iamue ndani yako.

Lakini ile y asili ni bora zaidi. Ukitumia njia ya kalenda, ni salama lakini pia Mungu ametubunia hiyo, ukijizoesha kuifuatilia utaweza tu kupangilia uzazi wako.

Lakini fahamu pia uzazi wa mpango, maadamu amani ya Kristo imeamua moyoni mwako, si dhambi mbele za Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je ni halali kwa mkristo kufanya biashara ya Forex?

JE! KUBET NI DHAMBI?

Je Kutoa Mimba ni dhambi?

Rudi Nyumbani

Print this post

Misunobari ni miti gani?

Jibu: Miti ya Misunobari tunaisoma katika kitabu cha Isaya 55:13 na sehemu nyingine baadhi katika biblia.

Isaya 55:13 “Badala ya michongoma utamea MSUNOBARI, Na badala ya mibigili, mhadesi; Jambo hili litakuwa la kumpatia Bwana jina, Litakuwa ishara ya milele isiyokatiliwa mbali”

“Misonubari” ni jamii moja na miti ya “Mierezi”. Tofauti ya Msonubari na mwerezi ni kwamba Misonubari yenyewe haiwi mirefu kama mierezi, na pia ina matawi myembamba kuliko mierezi, lakini kwa sehemu kubwa inafanana kimatumizi na mierezi, ndio maana sehemu karibia zote panapotajwa miti ya Mierezi basi na Misunobari pia inatajwa..

Zekaria 11:2 “Piga yowe, MSUNOBARI, maana mwerezi umeanguka, Kwa sababu miti iliyo mizuri imeharibika; Pigeni yowe, enyi mialoni ya Bashani, Kwa maana msitu wenye nguvu umeangamia”.

Soma pia 2Wafalme 19:23,  Isaya 14:8, Isaya 37:24,  Ezekieli 27:5 na Ezekieli 31:8.

Miti ya Misonubari na Mierezi ilitumika katika ujenzi wa nyumba za thamani na ilipatikana sana katika nchi ya Lebanoni..

Sasa kwa urefu kuhusu miti ya Mierezi na matumizi yake fungua hapa >>>Mwerezi ni nini?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI LAZIMA KUISHIKILIA IMANI MPAKA MWISHO.

Sala ya baraka (Hesabu 6:24-26).

Fahamu maana ya Mhubiri 10:9 Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo;

FAHAMU SEHEMU NNE (4)  APANDWAPO MWAMINI.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Rudi Nyumbani

Print this post