Category Archive Uncategorized @sw-tz

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Petro.(1Petro)

Kichwa cha kitabu hichi kinasema “Waraka wa kwanza wa Petro kwa watu wote” Kutuonyesha kuwa Petro Ndiye mwandishi.

Waraka huu mfupi aliuelekeza kwa watakatifu wote waliotawanyika, na kuishi kama wageni maeneo ya Asia ndogo ambayo kwasasa ni nchi ya Uturuki.

Maudhui makuu ya waraka huu tunaweza kuyagawanya katika sehemu kuu nne(4):

1) Ni kuwafariji watakatifu kwa kuwaeleza juu ya utukufu walioandaliwa mbinguni utakaofunuliwa siku ya mwisho. Na kwamba kwa kulitambua hilo basi wafurahi Katika majaribu mbalimbali ya imani, yaliyo ya kitambo tu.

2) Lakini pia unalenga kuwahimiza kuishi maisha ya utakatifu ya kumpendeza Mungu katika wakati wao wa kuishi hapa duniani.

3) Vilevile wajibu wakuishi maisha ya nidhamu katika Jamii ya wasioamini inayowazunguka.

4) Halikadhalika wajibu wa viongozi kulichunga kundi la Kristo kwa uaminifu wotena wajibu wa kanisa lote kumpinga shetani.

Haya ni maelezo mafupi juu ya kila kipengele:

1) Faraja katika dhiki mbalimbali.

Petro anawahimiza watakatifu kwamba wafurahi katika majaribu mbalimbali (kuliko kuhuzunika) kwa sababu ya uthamani mkuu wa imani yao itakayolipwa siku ile ya mwisho ambayo Yesu atafunuliwa kwetu.

1 Petro 1:6-7

[6]Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;

[7]ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.

> Petro Anahimiza kuiga kielelezo cha Kristo ambaye yeye alikubali kuteswa ijapokuwa hakutenda Dhambi, hata alipotukanwa hakurudisha majibu. Vivyo hivyo na sisi tukubali teso lolote kwa ajili yake katika upole wote, uvumilivu na ustahimilivu.

1 Petro 2:19-21

[19]Maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki.

[20]Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu.

[21]Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.

1 Petro 4:12-16

[12]Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.

[13]Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.

[14]Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia.

[15]Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.

[16]Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.

2) Wito wa kuishi maisha matakatifu.

Sehemu hii ya pili Mtume Petro anawahimiza watakatifu, kuwa kwasababu wanatazamia neema itakayofunuliwa siku ya mwisho ya kuja kwake Yesu Kristo (1:13), hivyo hawana budi kuishi maisha ya kiasi na utakatifu hapa duniani.

1 Petro 1:13-16

[13]Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.

[14]Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu;

[15]bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;

[16]kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.

1 Petro 2:1-2

[1]Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.

[2]Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu;

> Petro anaendelea kuwasihi watakatifu waishi kama wapitaji duniani, kwa kuziepuka tamaa za mwili.

1 Petro 2:11

[11]Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho.

1 Petro 4:2-3

[2]Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.

[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;

> Anaeleza pia Wajibu wa kupendana kuhurumiana, kunyenyekeana, tuwe watu wasiolipa baya kwa baya, bali wenye kubariki(3:8-12, 4:7)

> Kadhalika pia anaeleza wajibu wa wanandoa. Kwamba wake wawatii Waume zao, na kujipamba kwao kunapaswa kuwe kwa mapambo ya rohoni, Lakini pia waume kuishi na wake zao kwa akili. (3:1-7)

3) Mwenendo wa nidhamu kwa watu walio nje

Katika sehemu hii ya tatu anahimiza watakatifu kuwa na mwenendo unaopasa kwa watu wasioamini, ili wakose nafasi ya kutushitaki au kutulaumu kwa lolote.

> Anagusia katika eneo la watumwa Kwamba wawatii bwana zao, si wale tu wapole bali pia wale wakali.(2:18)

> Lakini pia Watakatifu waitii kila kilichoamriwa na mamlaka.

1 Petro 2:13-15

[13]Tiini kila kiamriwacho na watu, kwa ajili ya Bwana; ikiwa ni mfalme, kama mwenye cheo kikubwa;

[14]ikiwa ni wakubwa, kama wanaotumwa naye ili kuwalipiza kisasi watenda mabaya na kuwasifu watenda mema.

[15]Kwa sababu ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba kwa kutenda mema mzibe vinywa vya ujinga vya watu wapumbavu;

> Lakini pia anahimiza watakatifu wawaheshimu watu wote(2:17)

4) Wito kwa viongozo wa kanisa.

Mwishoni Petro anatoa wito wa waangalizi wa kanisa la Mungu (wazee), kwamba walichunge kundi kwa hiari, sio kwa kulazimishwa au kutazamia malipo ya kifedha, bali kwa moyo.

1 Petro 5:1-3

[1]Nawasihi wazee walio kwenu, mimi niliye mzee, mwenzi wao, na shahidi wa mateso ya Kristo, na mshirika wa utukufu utakaofunuliwa baadaye;

[2]lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo.

[3]Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao, bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi.

> Pamoja na hayo anasisitiza watakatifu wote wawe na kiasi na kukesha, kwasababu adui yetu ibilisi ni mfano wa simba angurumaye akitafuta mtu ammeze, hivyo wana wajibu wa kumpinga sikuzote.(5:8-9)

Hitimisho: 

Hivyo kwa maelezo machache ni kwamba Petro analihimiza kanisa kutembea katika uvumilivu wote na uthabiti Wa imani, pamoja na utakatifu, na kutimiza wajibu wao katika utakatifu na adabu kwa wanadamu wote, katika wakati ambao kanisa linasubiria neema kuu itakayofunuliwa siku ya mwisho Yesu atakaporudi.

Na ndivyo ambavyo sote tunapaswa tuishi hivyo sasa.

Kama mkristo je unaendelea kufurahi katika majaribu? Unaishi maisha matakatifu? Unaishi vema na jamii yako? unaifanya kazi ya Mungu? Unampinga shetani kwa kudumu katika sala?

Ikiwa hayo, unayazingatia basi, wewe ni mshirika wa neema hiyo kuu ya Mungu itakayofunuliwa siku ya mwisho.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Epafra ni nani katika biblia? (Wakolosai 1:7)

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.

JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE

Print this post

USIRUDI NYUMA KATIKA IMANI

Tukiwa bado tupo mwanzo wa mwaka, ni wakati wa kushika sana vile tulivyo navyo na kuendelea mbele, wala si wakati wa kurudi nyuma kabisa.

Usiyarudie mambo ya kale uliyoyaacha, usiyatamani mambo ya kale uliyoyakimbia, usiirudie njia  ya kale uliyoikataa…

Ulikuwa upo mbali na anasa mwaka jana, basi huu si mwaka wa kuzirudia tena, usirudie ulevi uliouacha miaka ya nyuma, usirudie uzinzi ulioushinda miaka ya nyuma, usirudie kujichua ulikokuacha miaka ya nyuma,

Usirudie mavazi yasiyo na staha uliyoyaacha miaka ya nyuma, usirudie wala kuitamani mitindo ya kidunia uliyoiacha mwaka jana.

Usirudie starehe za kidunia, mwanzo huu wa mwaka ni wakati ambao shetani anafanya kazi kubwa sana kuwarudisha watu nyuma kiroho, na atashambulia mambo yafuatayo ili kuhakikisha mwamini anarudi nyuma kiroho.

    1. Afya.

Atajaribu kukuletea mashambulizi katika eneo la afya, kwa kuitikisa afya yako au ya watu wako wa karibu, ikiwemo pia afya ya uzazi.. Simama endelea mbele usirudi nyuma!.

     2. Uchumi.

Atajaribu kutikisa uchumi wako lakini, hawezi kuondoa baraka zako za mwaka, hivyo usitishwe na vimitikisiko vya uchumi vya ibilisi vya hapa na pale, ni vya muda tu wewe endelea mbele usirudie biashara haramu wala tamaa za mali ulizoziacha huko nyuma endelea mbele kwani Bwana anakujua.

     3. Ndoa.

Atakuletea vimitikisiko vya kifamilia vya hapa na pale, pia visikutishe kwani ni kawaida yake kutishia, lakini wewe endelea mbele na imani usirudie magomvi uliyoyaacha miaka ya nyuma, usirudie anasa za kupunguza mawazo ulizoziacha huko nyuma…yapo mambo mazuri mbele yako kwaajili ya huu mwaka.

Pia ondoa hofu ya kesho…kwamba itakuwaje kesho, itakuwaje disemba…ndio usijizuie kutafakari yajayo, lakini usiufanye moyo wako kuwa mzito kwaajili ya hayo, kwani huo pia ni mlango mwingine wa ibilisi kumrudisha mtu nyuma.

Ukiwa ndani ya Kristo fahamu kuwa mambo yote yatakuwa sawa, haijalishi itachukua muda gani au mambo yanaanzaje…kushinda ni lazima! na ni AMRI.

Usirudi nyuma Baba, usirudi nyuma Mama, usirudi nyuma kaka, usirudi nyuma dada, usirudi nyuma mtoto…kwani matokeo ya kurudi nyuma ni kumfadhaisha Bwana.

1 Samweli 15:11”Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia BWANA usiku kucha”.

Utakapofika mwisho wa mwaka tena uwe na sababu ya kumshukuru Bwana kama amekulinda hujarudi nyuma.

Ayubu 23:12 “Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu”.

Lakini kama ulikuwa umeshaanza kurudi nyuma, bado hujachelewa hebu kataa hiyo njia na leo mwombe Bwana rehema na kuziacha hizo njia utaona maajabu ya Bwana, kwani atakutia nguvu na utaendelea mbele kwa mbio kubwa, Bwana atakurehemu na utamfurahia.

Hosea 14:4 “Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha”.

Isaya 50:5 “Bwana MUNGU amenizibua sikio langu, wala sikuwa mkaidi, wala sikurudi nyuma

Lakini usipojali na kuendelea katika njia hiyo ya kurudi nyuma, ipo hatari mbele yako..

Mithali 1:32  “Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua,

Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza”

USIRUDI NYUMA! USIRUDI NYUMA!…USIRUDI NYUMA!.

Ukiwa utahitaji msaada wa maombezi ili uzidi kusimama, basi piga namba hizi 0789001312.

Bwana anakupenda, na Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

NI LAZIMA KUISHIKILIA IMANI MPAKA MWISHO.

SHIKA SANA ULICHO NACHO, ASIJE MTU AKAITWAA TAJI YAKO.

USIIGE TABIA YA NAAMANI

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha Wafilipi.

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha wafilipi

Kama pale mwanzo kinavyojitambulisha “Waraka wa Paulo mtume kwa wafilipi”.

Paulo ndiye mwandishi wa kitabu hiki. Ni moja ya nyaraka ambazo Paulo aliziandika akiwa kama mfungwa, aidha kule Rumi.

Maudhui makuu ya waraka huu mfupi wenye sura nne(4) yalikuwa ni kuwatia moyo watakatifu na kuwahimiza waiendeleze furaha ya Mungu ndani yao,bila kukwamishwa na dhiki za aina yoyote, lakini pia sehemu ya pili ni kuwataka wapige hatua katika mwenendo wao ndani ya injili waliyoipokea.

Tukianza na hiyo sehemu ya kwanza:

1) Furaha ndani ya Kristo

Paulo anahimiza watakatifu kufurahi katika dhiki zote, ikizingatiwa kuwa Kanisa hili lilishuhudia vifungo na mapigo mengi ya Paulo. Kama tunavyosoma kwenye Matendo 16:16-40, Kule ambapo Paulo na Sila walipigwa sana na kutupwa gerezani, biblia inatuambia kulikuwa ni huku Filipi. Lakini hata katika waraka huu bado anashuhudia kuwa dhiki zake, zimekuwa wazi kwa maaskari, na watu wote wa huko (1:12-13).

Hivyo Paulo alijua watu wa Filipi huwenda wakawa na huzuni nyingi juu yake, au juu ya injili, kutokana na dhiki nyingi walizoziona kupitia yeye.

Lakini hapa anawaeleza kuwa yeye anafuraha sikuzote katika Kristo.

> Anaendelea kueleza furaha yake haiathiriwi na watu wanaomzushia fitna ili apitie mateso, maadamu anayeathirika ni yeye si Kristo. Basi bado anafurahi..(1:17-18)

> Anasema hata akihukumiwa kifo kwa ajili ya watakatifu, bado furaha yake itazidi zaidi wala haiwezi kuathiriwa..

Wafilipi 2:17-18

[17]Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote.

[18]Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.

Hivyo anawahimiza pia na wafilipi wafurahi kama yeye, wala wasione huzuni kwasababu ya dhiki hizi, kwasababu tumewekewa kuwa sehemu yetu katika ushuhuda wa injili.

Wafilipi 1:29

[29]Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;

Hizi ni sehemu nyingine kadha wa kadha Paulo akihimiza jambo hilo hilo,

Wafilipi 3:1

[1]Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana.

Wafilipi 4:4

[4]Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.

Sehemu ya Pili:

2) Mwenendo upasao injili

Katika sehemu ya pili Paulo anahimiza watakatifu kuwa na mwenendo unaipasa injili waliyopokea. Na hiyo ni ili wasiwe na ila na lawama,na udanganyifu. Kuonyesha kuwa injili, inayo na taratibu zake..Sio kuamini tu na kusema nimeokoka…bali pia kutii agizo lake.

Wafilipi 1:27

[27]Lakini mwenendo wenu na uwe kama inavyoipasa Injili ya Kristo, ili, nikija na kuwaona ninyi, au nisipokuwapo, niyasikie mambo yenu, kama mnasimama imara katika roho moja, kwa moyo mmoja mkiishindania imani ya Injili;

Anaendelea kusema watakatifu wana wajibu wa kunia mamoja, kutenda mambo yote bila majivuno,wala manung’uniko, wala mashindano, wanapaswa kutenda yote bila ubinafsi bali na ya wengine..

Anasisitiza watakatifu wanapaswa wawe wanyenyekevu, wenye nia ya Kristo..ambaye yeye hapo mwanzo alikuwa kama Mungu lakini alijishusha kwa kukubali kuachia nafasi yake, akawa kama mtumwa, akajinyenyekeza mpaka mauti ya msalaba,lakini Mungu akamkweza zaidi ya vitu vyote..Na sisi tulioipokea injili tunapaswa tuwe na nia hiyo hiyo ya unyenyekevu.(2:1-16)

Anasisitiza zaidi Wakristo wanapaswa wawe wapole, pia wawe waombaji na wenye shukrani.(4:5)

Halikadhalika ni wajibu wetu sote kuutumiza wokovu tulioupokea kwa kuogopa na kutetemeka, kwasababu ndiye Mungu atendaye kazi ndani yetu.(2:12-13)

Pamoja na hayo Watakatifu wana wajibu pia wa kuyahakiki mambo yote yaliyo mazuri na kuyaiga, (2:1-2)

Wafilipi 4:8

[8]Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.

Lakini pia anawatahadharisha kujiepusha na wahubiri wa uongo akianzana na wayahudi (watu wa tohara), ambao wanahubiri wokovu kwa njia ya torati zaidi ya ile tuipatayo ndani ya Kristo Yesu kwa njia ya imani. (3:1–16,)

Pamoja watumishi ambao fundisho lao ni la mambo ya duniani tu, na sio yale ya kumwelekeza mtu mbinguni (3:17-21).

Mwisho, Paulo anatoa salamu zake, na shukrani kwa huduma ya utoaji kanisa hilo lililomfanyia, na linaloendelea kumfanyia.

Hivyo kwa hitimisho, waraka huu maudhui kuu ni kuwafariji watakatifu wafurahi katika mambo yote, tukizingatia tunda la Roho ni furaha. Yesu alisema tufurahi na kushangalia pale tunapoudhiwa, kwa ajili ya jina lake. Hivyo, hakuna eneo lolote furaha ya Mungu ndani yetu ,inastahili kukatishwa. Tupitiapo magonjwa kama Epafrodito(2:25-30), shida, njaa, tumefundishwa kuyaweza yote ndani ya Kristo(4:12-3). Hivyo furaha yetu haiwezi kuathiriwa..Ilinde furaha yako.

Lakini anahimiza mwenendo upasao injili. Kwamba huo utaweza kufanikiwa pale tunapokubali kuwa na nia kama ile ya Kristo, ya unyenyekevu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Watu wa nyumbani mwa Kaisari ni watu gani? (Wafilipi 4:22).

Epafrodito ni nani kwenye biblia?

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakolosai

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakolosai

Kama kinavyoanza kwa utambulisho wake, ‘Waraka wa Paulo mtume kwa Wakolosai’.

Paulo ndiye mwandishi wa waraka huu.

Madhumuni makuu ya waraka huu ulikuwa ni kuwasisitiza Wakolosai  jinsi Yesu alivyo UTOSHELEVU WOTE, ambaye kwa kupitia yeye Uumbaji wote umekamilishwa ndani yake, lakini si hilo tu bali na  utimilifu  wote wa ki-Mungu unapatikana ndani yake, pamoja na hazina zote za hekima na maarifa.

Akiwa na maana kuwa mtu akimpata Kristo, hahitaji kitu kingine cha pembeni kumkamilisha yeye, Utoshelevu wote upo kwake.

Hivi ni vifungu mama,

1:15-17

“15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. 16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. 17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye”.

2:3

ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.

 

2:9

 “Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili”.

Lakini Sababu ya kusisitiza jambo ni ipi?

Anaeleza kwa undani katika sura ile ya pili, kwamba ni kutokana na uwepo wa watu waliolivamia kanisa na kuwadanganya kwa maneno ya ushawishi, nia zao ni kuwafanya mateka kwa elimu isiyo na matunda, ya mapokeo ya kibinadamu, yasiyo ya Kristo (2:8). Kwamba mtu akishika hayo, ndio utimilifu wote unapatikana.

Vilevile kuonekana kwa baadhi ya desturi za kiyahudi ndani ya kanisa, kama vile kushika sikukuu, tohara,  sabato, na mwandamo wa mwezi. Vikidhaniwa kuwa vitu hivyo vinaweza kuleta ukamilifu wote pamoja na Kristo (2:11-23)

Na pia kuzuka kwa ibada bandia za kuabudu viumbe vya rohoni (malaika), kwa mawazo kuwa mtu ataupokea ukamilifu.(2:18)

Paulo anaeleza yote hayo hayana wokovu, isipokuwa kwa njia ya haki tuliyoipokea kwa msalaba wake uliofuta hati ya mashtaka yetu, kwa mateso yake pale msalabani ambayo kwa kupitia njia hiyo tumepokea msamaha wa dhambi, pale tu tunapoamini na kubatizwa (2:12-17)

Maisha mapya ndani ya Kristo.

Sehemu ya tatu Paulo anaeleza kwamba kuamini ni pamoja na kuuvaa utu upya wa Kristo. Hivyo huyu mtu hatarajiwi kuendelea kuishi hivi hivi tu, kisa Kristo amemkamilisha kwa kila kitu, bali anapaswa aenende kwa Kristo mwenyewe, ayafikiri yaliyo juu, (3:1-17),

Kwa namna gani?

Kwa kuzifisha tabia za mwilini, kama uasherati, uchafu, kutamani, mawazo mabaya, ghadhabu, matusi. Lakini pia kujivika utu wema, moyo wa rehema, unyenyekevu, upole, uvumilivu, kusameheana, upendo, ibada. Vilevile si tu katika mambo ya rohoni , bali mpaka kwenye ngazi za kifamilia, kwamba wake kuwatii waume zao, na waume kuwapenda wake zao, na watoto kuwatii wazazi. Hizo ndio tabia za utu mpya.

Katika sura ya 4.

Bado Paulo aendelea kueleza huo mwenendo ndani ya Kristo, unapaswa uonekane mpaka kwa mabwana, kwa watumwa wao. Kwamba mabwana wawape watumwa haki zao, Lakini pia watakatifu wote, wanapaswa kudumu katika maombi, na kuenenda kwa hekima kwa watu wasioamini, katika usemi bora, na kujifunza kuukomboa wakati.

Na mwisho.

Paulo anawasilisha salamu za washirika wenzake wa injili, kwa Wakolosai ikiwemo, Epafra, Luka, Dema, marko, Aristarko, Yusto.

Hitimisho.

Kwa ufupi waraka huu, hueleza kwamba utoshelevu wote upo ndani ya Kristo tu na sio zaidi ya hapo, hatuhitaji kitu kingine cha pembeni kutukamilisha sisi, Lakini ni wajibu wa huyu mkristo kutembea katika maisha mapya ndani yake. Kwasababu mambo yote mawili yanakwenda sambamba hayatengani. Kristo huokoa na kutakasa wakati huo huo. Unapookolewa, saa hiyo hiyo umevikwa utu upya. Huwezi kuendelea katika dhambi.

Ni kipi cha ziada tunachoweza kujifunza katika waraka huu?.

Maombi ya Paulo na Eprafa yasiyokoma kwa kanisa hili(1:3, 9, 4:12):

Hatuna budi kujijengea desturi ya sikuzote kuliombea kanisa la Bwana, hususani mahali tulipo, pamoja na watakatifu wengine tuwajuao. Kwasababu kusimama kwa kanisa hutegemea sana maombi yasiyokoma.

                                        Bwana akubariki.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                     ||kiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii. Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya kuabudu malaika? (Wakolosai 2:18)

Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,

Tafsiri ya Wakolosai 2:18 Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu,

Epafra ni nani katika biblia? (Wakolosai 1:7)

Uchambuzi na Mwandishi wa kitabu cha Wagalatia

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini biblia iwasifu wenye kutumia shoto zaidi ya wanaotumia kulia? (Waamuzi 20:16).

Kwanini biblia iwasifu wenye kutumia shoto zaidi ya wanaotumia kulia? (Waamuzi 20:16).


Swali: Je kuna jambo gani la ziada katika mkono wa kushoto hata watajwe kama mahodari katika vita?.

Jibu: Turejee…

Waamuzi 20:16 “Katika watu hao wote walikuwako watu waume mia saba waliochaguliwa, wenye shoto; kila mmoja alikuwa anaweza kuutupia unywele mawe kwa teo, wala asikose”.

Ni kweli zipo tafiti zinazoonyesha kuwa mkono wa kushoto una nguvu (uwezo) kuliko ule wa kuume (kulia).

Lakini hiyo si sababu biblia iliyoitumia kuusifiia mkono huo(wa kushoto) zaidi ya ule wa kulia…kwasababu pia walikuwepo mahodari waliotumia mikono yote miwili na walionekana sawa tu..

1Nyakati 12:2 “Walikuwa wenye kupinda upinde, nao walikuwa hodari wa kutumia mkono wa kuume na wa kushoto, kwa kutupa mawe ya teo, na kwa kupiga mishale ya upinde; walikuwa wa nduguze Sauli, wa Benyamini”.

Sasa ni sababu gani inayowafanya wanaotumia shoto kuonekana mashujaa zaidi?.

Jibu, Sababu kuu ni mbinu za upiganaji.

 Kawaida ni kuwa idadi ya askari wanaotumia mkono wa kulia (kuume)…ni kubwa kuliko ile ya wanaotumoa shoto.

Sasa kikawaida inakuwa ni ngumu sana kupambana na mtu anayetumia mfumo mwingine tofauti na wa kwako, lakini mfumo unaofanana na wewe ni rahisi kumsoma, na kumwingia.

Ni rahisi sana mashoto kupambana na mashoto wenzake na kulia kupambana na kulia mwenzake..lakini inapotokea kinyume na hapo, basi vita vinakuwa vigumu kwasababu ni mifumo miwili tofauti.

Na kwasababu mashoto ni wachache na wengi wanaokutana nao wakati wa vita ni watu wanaotumia mkono wa kuume (kulia), basi wanapata mzoefu mkubwa wa kupambana na watu wa tofauti na mikono yao, na kuwafanya kuwa hodari zaidi..

Lakini wale wanaotumia kulia, wanakuwa na uhodari hafifu kwasababu ni mara chache sana wanakutana na wasiotumia mashoto, hiyo inawafanya uzoefu wa kupigana na jamii hiyo ya watu kuwa mdogo, na kuwafanya kuanguka (kupigwa) wanapokutana na watu wanaotumia mashoto, hiyo ndio sababu kuu…

Na sababu nyingine inayowafanya watu wanaotumia mashoto kuwa hodari zaidi katika biblia, ni uwezo wa kuficha jambo bila kujulikana..

Kikaiwaida askari anajulikana kwa kuhifadhi upanga wake upande wa paja lake la kushoto, lakini wale wanaotumia mashoto huficha panga zao upande wa kuume, jambo linalowafanya wasifahamike kwa haraka kama ni maaskari..

Jambo hilo tunaliona kwa Ehudi aliyekuwa mwamuzi wa Israeli.

Waamuzi 3:14 “Wana wa Israeli walimtumikia Egloni mfalme wa Moabu muda wa miaka kumi na minane.

15 Lakini wana wa Israeli walipomlilia BWANA, BWANA akawainulia mwokozi, Ehudi, mwana wa Gera, Mbenyamini, mtu aliyekuwa mwenye shoto; nao wana wa Israeli walimpelekea Egloni mfalme wa Moabu tunu mkononi mwa huyo Ehudi.

16 Ehudi alijifanyia upanga uliokuwa na makali kuwili, urefu wake ulipata dhiraa moja; akaufunga huo upanga ndani ya nguo yake katika paja lake la MKONO WA KUUME…………

20 Basi Ehudi akamwendea; naye alikuwa anaketi peke yake katika chumba chake cha baridi. Ehudi akasema, Mimi nina ujumbe utokao kwa Mungu kwako wewe. Basi akainuka katika kiti chake.

21 Ehudi akaunyosha mkono wake wa kushoto, akaushika huo upanga kuutoa hapo katika paja lake la kuume, akamtia tumboni mwake;

22 hicho kipini nacho kikaingia ndani pamoja na huo upanga wenyewe; nayo mafuta yakashikamana tena juu ya upanga, kwani hakuutoa tena upanga tumboni; nao ukatokea kwa nyuma”

Bwana atupe kutumia mashoto mbele ya adui wetu ibilisi, tupiganapo vita vya kiroho.

Waefeso 6:14 “Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani……..

17 tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu”

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

LIPO LA KUJIFUNZA KWA WALE MASHUJAA 37 WA DAUDI.

Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?

Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu (Zekaria 13:7-9)

MAANA ROHO HUCHUNGUZA YOTE, HATA MAFUMBO YA MUNGU.

TUTAMPIGA KWA NDIMI ZETU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Warumi.

Kitabu hichi kama kinavyojitambulisha, “Waraka wa Paulo kwa Warumi” mwandishi wake ni Mtume Paulo.

Kitabu hiki alikiandika akiwa Korintho mahali palipoitwa Kenkrea (Warumi 16:1)

Tofauti na nyaraka nyingine ambazo Paulo aliziandika kwa makanisa ambayo alikuwa tayari ameshayatembelea/ameyapanda hapo nyuma. Waraka huu tunaonyeshwa Paulo hakuwahi kufika Rumi. Lakini alisikia mwitikio wao wa injili, hivyo likawa ni tamanio lake pia awafikie na wao, lengo likiwa sio kupanda juu ya msingi wa watu wengine bali wajengane kiimani.(1-18),

Na kweli tamanio lake tunaona lilikuja kutimia baadaye, kama tunavyosoma kwenye kitabu cha matendo ya mitume, katika ile ziara yake ya mwisho kama mfungwa, alifika Rumi, na huko akafanikiwa kuhubiri injili sawasawa na tamanio lake (Matendo 27-28).

Hichi ni kitabu kinachoeleza misingi ya imani  ki-mpangilio . Kuanzia asili ya wokovu wetu, haki ya Mungu, na mwenendo wa kikristo. Hivyo kuna umuhimu mkubwa sana kwa mkristo yoyote kukielewa vema kitabu hichi.

Migawanya mikuu ya kitabu hichi.

     1) Nguvu ya injili? (1: 1-17)

Baada ya Paulo, kueleza tamanio lake la kuwafikia katika utangulizi wake, tunaona katika mistari hiyo anasisitiza kwanini afanye hivyo? Ni kwasababu ya ‘Nguvu ya Injili yenyewe’, Akisema Injili ni uweza wa Mungu uuletao wokovu. Na hivyo haionei haya kuihubiri kwa watu wote..kwa wayahudi na watu wa mataifa pia.

  1. Hatia kwa wanadamu wote (1:18- 3:20)

Sehemu ya pili Paulo anaeleza jinsi wanadamu wote walivyopungikiwa na utukufu wa Mungu kuanzia watu wa mataifa ambao wameshindwa kuitii kweli ya Mungu iliyofunuliwa kwao kwa mambo yake yaliyo dhahiri kabisa yanayotambulika hata pasipo sheria, kwamba mambo ya asili yanafundisha haki ya Mungu, lakini walikataa kutii. Vilevile na wayahudi  pia ambao walikuwa na sheria lakini walishindwa kuyatenda yote kulingana na yaliyoandikwa. Hivyo hakuna hata mmoja mwenye haki,  wote wamewekwa chini ya hukumu ya ghadhabu ya Mungu, kwa kushindwa kutenda haki yote.

  1. Haki kwa Imani (3:21-5:21)

Kwa kuwa wanadamu wameshindwa kuwa wakamilifu, Paulo anaeleza njia ambayo Mungu ameitoa kwa  mwanadamu kuweza  kuhesabiwa haki. Ni njia ambayo inadhihirishwa bila matendo ya sheria, tunayoipata kwa kumwamini tu Yesu Kristo. Yaani pale mtu anapomwamini Bwana Yesu kwamba kifo chake kimeleta ukombozi wa roho yake, basi mtu huyo anakuwa amehesabiwa haki kuwa ni Mtakatifu mbele za Mungu.

Kulithibitisha hilo Paulo akaendelea kueleza  kwa mfano wa Ibrahimu jinsi Mungu alivyomhesabia haki bila sheria yoyote, na kwamba sisi pia tutahesabiwa kwa njia hiyo hiyo.

  1. Maisha mapya ndani ya Kristo (6:1-8:39)

Katika sehemu hii Paulo anaeleza maisha baada ya kuhesabiwa haki, kwamba mkristo anapaswa aendelee kutakaswa na kuwa kama Kristo. Lakini kutokana na mashindano kati ya mwili na roho. Ili aweze kuushinda mwili anapaswa ajifunze kuishi kwa Roho, kwa kuruhusu utendaji kazi wake ndani yake. Maneno hayo ameyarudia pia katika waraka wake kwa Wagalatia (Wagatia 5:16). Kwamba mtu anayeenenda kwa Roho kamwe hawezi kuzitimiza tamaa za mwili.

Lakini mbele kidogo anaendelea kuhimiza upendo wa milele wa Mungu, uliodhihirishwa kwetu kupitia Yesu Kristo, ambao hauwezi kutenganishwa na kitu chochote tukijuacho duniani au mbinguni.

  1. Uhuru wa Mungu wa kuchagua, na kusudi lake kwa Waisraeli (9:1- 11:36)

Kwenye sura hizi, Paulo anaeleza uhuru wa Mungu wa kuchagua, na siri iliyokuwa nyuma ya Israeli kukataa injili. Anaeleza mpango wake wa wokovu kwa mataifa na waisraeli, kwamba iliwapasa wao wakatae injili ili sisi watu wa mataifa tuipokee injili. Na hivyo anaeleza sisi pia tunapaswa tuupokee wokovu kwa unyenyekevu wote kwasababu tusipokaa katika kuamini tutakatwa, kama wao walivyokatwa.

  1. Tabia ya maisha mapya katika Kristo (Warumi 12:1- 15:3 )

Paulo anaeleza jinsi tunavyopaswa kuitoa miili yetu kama dhabihu iliyo hai takatifu yenye kumpendeza Mungu, tunawajibu wa kupendana sisi kwa sisi, tusiwe watu wa kulipa kisasi, tuishi kwa heshima, tuhudumiane katika karama mbalimbali tulizokirimiwa na Mungu, tutii mamlaka zilizowekwa, vinywa vyetu vitoe baraka, tumtumikie Mungu kwa bidii, tudumu katika sala, tuishi kwa amani sisi kwa sisi, pia tuweze kuchukiliana katika viwango mbalimbali vya imani bila kuhukumiana.

Kwa ufupi sura hizi zinaeleza tabia zetu zinapaswa ziweje baada ya wokovu.

  1. Hitimisho  (15:14- 19:27)

Paulo anaeleza mpango wake wa kuwafikia Warumi pindi atakapokuwa anasafiri kwenda Spania kuhubiri injili. Akiomba akumbukwe katika maombi dhidi ya watu wabaya, na mwisho anatoa salamu kwa watakatifu wote walio Rumi, pamoja na angalizo kwa watu waletao fitna katika injili waliyoipokea wajiepushe nao

KWA UFUPI.

Kitabu hichi kinaeleza

Haki ya Mungu ikoje, ambapo hapo mwanzo ilidhaniwa inapatikana kwa sheria au matendo ya mwanadamu, kumbe sio, hayo yalishindwa bali kwa njia ya Yesu Kristo, lakini pia kinaeleza namna ambavyo tunaupokea wokovu huo kwa neema kwa njia ya Imani, na pia jinsi Mkristo anavyopaswa aishi kulingana na wokovu alioupokea. Kwamba sio kwasababu amehesabiwa haki bure bila matendo, basi aishi maisha kama atakayo, hapana vinginevyo atakufa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NJIA/BARABARA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.

Uchambuzi na Mwandishi wa kitabu cha Wagalatia

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Rudi Nyumbani

Print this post

TUTAMPIGA KWA NDIMI ZETU.

Silaha ya Mwisho mwisho kabisa ya adui  kumshambulia Mtu ni “ULIMI WA UOVU”.. Ukiona Maneno ya uongo kuhusu wewe, au ya vitisho au ya uchonganishi yanatembea huku na huko basi fahamu kuwa adui ndio yupo katika hatua za mwisho mwisho, kukuacha!..(Ni wakati wa kumaliza jaribu).

Na kama ukiweza kusimama katika hiko kipindi bila hofu, wala kutetereka wala kurudi nyuma, basi shetani unaweza usimwone tena baada ya hapo, kwa kipindi kirefu sana.

Mfano katika biblia tunamwona Nabii Yeremia,

Adui alimtafuta mara nyingi kwa njia mbalimbali ili amnyamazishe asitoe unabii, lakini kila alichojaribu ili kumzuia Yeremia asitoe unabii, kilishindikana, na ndipo akatumia silaha yake ya mwisho ya NDIMI ZA UOVU, ili yamkini amtishe Yeremia, lakini pia haikusaidia,

Yeremia 18:18 “Hapo ndipo waliposema, Njoni na tufanye mashauri juu ya Yeremia; maana sheria haitampotea kuhani, wala shauri halitampotea mwenye hekima, wala neno halitampotea nabii. Njoni, na TUMPIGE KWA NDIMI ZETU, wala tusiyaangalie maneno yake yo yote.

19 Niangalie, Ee Bwana, ukasikilize sauti ya wanaoshindana nami”.

Wakati huo kilitokea kikundi kiovu na kuanza kumtisha Yeremia kwa maneno mengi, na pia kumzushia mambo mengi na zaidi ya yote, ya uchonganishi na kumchafua mbele ya Mfalme, ili tu Yeremia akamatwe asiendelee kutoa unabii.

Yeremia 38: 4 “Ndipo wakuu wakamwambia mfalme, Twakuomba, mtu huyu auawe, kwa kuwa aidhoofisha mikono ya watu wa vita, waliobaki katika mji huu, na mikono ya watu wote, kwa kuwaambia maneno kama hayo; maana mtu huyu hawatafutii watu hawa heri, bali shari.

5 Naye mfalme Sedekia akasema, Tazama, yu mikononi mwenu; maana mfalme siye awezaye kufanya neno lo lote kinyume chenu”.

Mtu mwingine aliyepigwa kwa NDIMI  OVU ni nabii Danieli, soma Danieli 6..

Sasa kwanini Adui, aiweke hii silaha ya ulimi kama chaguo lake la mwisho?… Ni kwasababu anajua ulimi wa mtu unaweza kuwasha moto mkubwa, na kama mtu hatakuwa na Imani ya kutosha basi anaweza kuanguka kabisa…

Yakobo 3:6 “Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum”

Hivyo shetani anaweza kukuwashia tu moto kupitia ulimi wa mtu au ndimi za watu, na moto huo ukawa mkubwa sana, kiasi kwamba kama huna imani na ujasiri wa kutosha, unaweza kurudi nyuma kabisa.

Shedraka, Meshaki na Abednego walijikuta wapo katika tanuru la Moto, kwasababu tu ya baadhi ya watu waliotumia ndimi zao kupeleka mashitaka kwa mfalme kuwa hawataki kuisujudia ile sanamu.(Danieli 3:8-12).

Danieli naye alijikuta katika tundu la simba kwasababu tu ya vinywa vya watu, na Yeremia naye alijikuta katika lile shimo refu lenye giza lililojaa matope kwasababu ya maneno ya watu(Yeremia 38:6)..

Lakini wote hao walishinda, kwani moto ule uliokusudiwa juu yao uliwala maadui zao, na mashimo yale na matundu yale yaliyokusudiwa juu yao yaliwaharibu maadui zao, lakini kama wangetetemeka na kuogopa na kurudi nyuma bila shaka wangepotea kwa kuharibiwa na ibilisi!.

Na sisi hatuna budi kusimama Imara bila hofu, kwa ujasiri mwingi pale ambapo adui anatumia NDIMI za watu kama silaha yake…

Hiko ni kipindi cha kuwa na imani na ujasiri….mipango inapopangwa ya vitisho au uchonganishi, havitasimama endapo wewe utasimama.

Ni wakati kusimama na kuamini huku tukiomba, na silaha za ndimi zao zitaanguka, na Bwana atatukuzwa.

Ifuatayo ni mistari inayozungumzia hatari ya NDIMI ZA UOVU…

Zaburi 57:4 “Nafsi yangu i kati ya simba, Nitastarehe kati yao waliowaka moto. Wanadamu meno yao ni mikuki na mishale, Na ndimi zao ni upanga mkali.”

Zaburi 64: 2 “Utanificha mbali na shauri la siri la watenda mabaya, Mbali na ghasia ya watu wafanyao maovu;

3 Waliounoa ulimi wao kama upanga, Wameielekeza mishale yao, maneno ya uchungu,

4 Wapate kumpiga mkamilifu faraghani, Kwa ghafula humpiga wala hawaogopi.

5 Walijifanya hodari katika jambo baya; Hushauriana juu ya kutega mitego; Husema, Ni nani atakayeiona”

Zaburi 140:1 “Ee Bwana, uniokoe na mtu mbaya, Unihifadhi na mtu wa jeuri.

2 Waliowaza mabaya mioyoni mwao, Kila siku huondokesha vita.

3 Wamenoa ndimi zao kama nyoka, Sumu ya fira i chini ya midomo yao”.

Lakini pamoja na kwamba adui anatumia ndimi kutushambulia, vile vile na sisi tunaweza kutumia ndimi hizo hizo, kumharibu.

Mithali 18:21 “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake”

Tunampiga shetani kwa ndimi zetu, kwa njia ya KUOMBA, na hususani maombi yanayohusisha mfungo.

Bwana atubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Kughafilika ni nini? (Wagalatia 6:1)

Swali: Kughafilika maana yake nini?


Jibu: Turejee…

Wagalatia 6:1  “Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.

2  Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo”

Kughafilika maana yake ni  “Kuchukuliwa na jambo fulani baya”.. Mtu aliyeghafilika anakuwa amezama katika Uovu na anakuwa haoni tena kama ni kosa kufanya uovu ule  (kiasi kwamba ufahamu wake unakuwa kama umefungwa)..

Kwamfano mtu aliyezama katika anasa ambao hapo kwanza alikuwa anaukataa, mtu huyo anakuwa “Ameghafilika katika anasa za dunia” n.k

Biblia inatufundisha kuwa watu kama hawa ni kuwarejesha kwa roho ya upole, Maana yake kwa kuwafundisha taratibu na kuwaombea mpaka watakaporudi katika mstari, na hiyo ndiyo tafsiri ya kuchukua mzigo wa mwingine, (yaani  ni kumrejesha katika kweli, mtu aliyekengeuka, na si kumwombea baada ya kufa!)

Mtu aliyekufa hakuna mtu anayeweza kuuchukua mzigo wake wa dhambi, bali atasimama nao mbele ya kile kiti cha hukumu..

Wagalatia 6:5 “Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe”

Na sio tu mtu, bali hata Bwana mwenyewe hatamchukulia mtu mzigo wa dhambi, baada ya kifo….

Yohana 8:21  “Basi akawaambia tena, Mimi naondoka, nanyi mtanitafuta; NANYI MTAKUFA KATIKA DHAMBI YENU; mimi niendako ninyi hamwezi kuja…….

24  Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU”.

Je umeokoka?.. una uhakika Bwana YESU akirudi leo utakwenda naye?.

Maran atha..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Uchambuzi na Mwandishi wa kitabu cha Wagalatia

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU

Je, kama hauna ubatizo sahihi hauwezi kuwa na Roho Mtakatifu?

Ni uchafu gani unaozungumziwa katika Wagalatia 5:19?

je! Paulo aliwalaani Wagalatia na Wakorintho?

Rudi Nyumbani

Print this post

MHESHIMU MCHUNGAJI WAKO.

Kila mahali pana mamlaka yake, na mamlaka hizo huwa ni  wajibu kwa walio chini yake kuzitii. Kwamfano katika familia Mungu ameweka mamlaka, Baba awe kichwa, na mama msaidizi wake, hivyo ni wajibu wa watoto kuwatii wazazi wao . Familia haiwezi kusimama,.kama mtoto atataka nafasi ya baba, kwamba yeye ndio atoe maamuzi ya mwisho, au ajiamulie la kufanya, awapangie wazazi wake majukumu ya ndani. hilo haliwezekani.

Vilevile katika ngazi ya utawala wa kidunia, Mungu kaziweka mamlaka na anataka watu wote wazitii, kwasababu hazijaamuriwa na mwanadamu bali yeye Mungu mwenyewe..

Warumi 13:1-2

[1]Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu.

[2]Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.

Tito 3:1-2

[1]Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema; [2]wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wema, wakionyesha upole wote kwa watu wote.

Sasa hizi ni mamlaka za kidunia. Zipi kuhusu Mungu, unadhani hana mamlaka?

Mungu pia ameweka mamlaka yake duniani, ambayo ni kuu kupita hizo zote, na kupitia hiyo huwahudumia watu wake. Na anataka tuitii na kuitetemekea kwasababu ni yeye mwenyewe atendaye kazi kupitia hiyo.

Je mamlaka hiyo kaiweka kupitia nani?

Bila shaka kupitia wachungaji wetu/waangalizi wetu, ndani ya kanisa

Ni vema kufahamu kuwa kiongozi yoyote wa kiroho (anayeisimamia kweli). Hakujiteua mwenyewe kwenye nafasi hiyo.  Mitume wa Yesu hawakujichagua wao. Bali walichaguliwa na Mungu mwenyewe.

Mtu yeyote aliyepewa maono ya kuanza kanisa, na ukajikuta upo chini yake, au kateuliwa na Roho Mtakatifu mwenyewe ndani ya kanisa (Matendo 14:23), Huyo ni wa kumtii sana. Kama vile unavyowatii watawala au mazazi wako kwenye familia, haijalishi atakuwa na mapungufu kiasi gani, au umri wake ni mdogo au mkubwa kiasi gani, awe mwenye uwezo au asiye na uwezo kiasi gani.

Kwanini uwaheshimu.

1) Wanajitaabisha kwa ajili yako kukuchunga, kukuonya na kukuombea.

Hivyo wajibu ni wako kurudisha moyo wa upendo, na kuwasikiliza.

1 Wathesalonike 5:12-13

[12]Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni; [13]mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi.

2) Watasimama mbele ya kiti cha hukumu siku ya mwisho kutoa hesabu juu yako.

Hivyo ni wajibu kuonyesha moyo wa kunyenyekea kwao.

Waebrania 13:17

[17]Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.

Madhara ya kutowasikiliza/ kutowatii.

i) Watafanya kazi ya Mungu kwa kuugua.

Hapo kwenye Waebrania 13:17b anasema..

..ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi

Na matokeo yake utendaji kazi ndani ya kanisani utakuwa hafifu. Ukishaanza kuonyesha tabia ya kutosikiliza unachoelekezwa, unapewa jukumu hutekelezi, hurudishi mrejesho, unafanya tofauti na wengine, yeye anataka uende kulia wewe unaenda kushoto, , yeye anafundisha hiki wewe unafundisha kile. Fahamu kuwa jambo hilo litamhuzunisha kiongozi wako. Na hivyo kupelekea hamasa ya kuhudumu kupungua. Na madhara yake ni kuwa Mungu kukata utendaji kazi wake mahali hapo,

ii) Dhara lingine ni kuwa utajisababishia adhabu kwa Mungu.

Wakati ule Haruni na Miriamu dada yake. walimnenea Musa maneno mabaya kwasababu na mke wake ambaye hakuwa myahudi. Mungu aliwaadhibu kwa kumpiga ukoma Miriamu kwasababu tu hiyo ya kutoonyesha adabu kwa mtumishi wake.

Hesabu 12:7-8

[7]Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote;

[8]Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la BWANA yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?

Ni kosa kumnenea vibaya mchungaji wako. Epuka masengenyo na uasi na matabaka ndani ya kanisa. Uonapo kosa mwombee, au mfuate mweleze  uwapo naye peke yake. Hilo litamjenga zaidi ya kutoa malaumu na manung’uniko. Adui hutumia sana njia hii kuleta mafarakano na magomvi, na mapigo kanisani.

Mheshimu mchungaji wako, zaidi ya raisi wa nchi kwasababu yeye ni balozi wa mbinguni na Mungu atakuinua (1Petro 5:1-6)

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi

Ipi tofauti kati ya KUHANI na MCHUNGAJI.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Rudi Nyumbani

Print this post