Category Archive Mafundisho

FUNDISHA NENO KANISANI NA NYUMBANI.

(Masomo maalumu kwa wazazi/walezi).

Ni nini unafanya kama mzazi uwapo nyumbani?.. Je maisha yako ndani ya kanisa ni sawa na yale nje ya kanisa?..Je kile unachokifanya kanisani ndicho unachokifanya nyumbani?…je nyumbani kwako ni sehemu ya kuishi tu au ni sehemu pia ya ibada?.

Kama wewe ni mwalimu kanisani, ni lazima pia uwe mwalimu nyumbani kwako…kama wewe ni kiongozi katika nyumba ya Mungu ni lazima pia uwe kiongozi katika nyumba yako, kama wewe ni mchungaji katika nyumba ya Mungu ni lazima pia uwe mchungaji katika nyumba yako mwenyewe…Ndivyo biblia inavyotufundisha.

Mitume wa Bwana YESU ni kielelezo kwetu, wao walikuwa wakihubiri Neno HEKALUNI NA NYUMBANI, kama maandiko yanavyosema, hivyo kama na sisi tumejengwa juu ya msingi wao ni lazima tufanye kama wao walivyofanya..

Matendo 5:42 “Na kila siku, NDANI YA HEKALU na NYUMBANI MWAO, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo”.

Umeona?.. Si hekaluni tu!, bali hata nyumbani…. Uharibifu mkubwa shetani anauanzia nyumbani… Hivyo ni lazima uwe na AMRI, katika nyumba yako mwenyewe… Ni lazima pafanyike ibada nyumbani kila siku, ni lazima pafanyike maombi, ni lazima watoto na wengine wanaoishi katika nyumba yako wajue kuomba na kuombea wengine.

Ni lazima watoto wajifunze biblia na kufundisha biblia tangu wakiwa wadogo, ni lazima pia wajifunze kutoa.. ni lazima wote wawe wa kiroho, ni lazima uwafundishe wawe vipaumbele katika Imani wawapo shuleni, maana yake wakiwa shuleni wawe vipaumbele katika kuongoza maombi kwa wanafunzi wenzao, na kuomba vile vile kufunga… Na si kuwaacha jumapili kwa jumapili  tu wafundishwe kanisani hayo mambo..

Jenga tabia ya kuwafuatilia mienendo yao ya kiimani wakiwa mashuleni, fuatilia sifa zao za kiimani wawapo mashuleni, (na si tu taaluma yao)..wapo watoto taaluma zao zinaonekana nzuri lakini shetani kashawaharibu kitabia muda mrefu (matokeo yake yatakuja kuonekana baadaye).

Hivyo kama mzazi au mlezi, simama katika hiyo nafasi… kiasi kwamba NENO LA MUNGU nyumbani kwako ni AMRI sio OMBI!. Kama Nabii Yoshua alivyoazimia zamani zile..

Yoshua 24:15 “Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia Bwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng’ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; LAKINI MIMI NA NYUMBA YANGU TUTAMTUMIKIA BWANA.

16 Hao watu wakajibu wakasema, Hasha! Tusimwache Bwana, ili kuitumikia miungu mingine”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUOTA UPO KANISANI.

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

YESU HAYUPO KATIKA MAZINGIRA YALEYALE TU SIKUZOTE, USIJISAHAU.

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

Rudi Nyumbani

Print this post

Lalama kwa uhai wa watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa(Maombolezo 2:19)

Mafundisho maalumu kwa watumishi wa Mungu na Watenda kazi wote katika shamba la Bwana.

Maombolezo 2:19

[19]Inuka, ulalamike usiku, Mwanzo wa makesha yake; Mimina moyo wako kama maji usoni pa Bwana; Umwinulie mikono yako; KWA UHAI WA WATOTO WAKO WACHANGA WAZIMIAO KWA NJAA, Mwanzo wa kila njia kuu. 

Ikiwa wewe ni mzazi au mlezi unaelewa ni uchungu mwingi kiasi gani  unakupata  pale unapoona mtoto wako anaangamia kwa kukosa mahitaji yake muhimu, mfano  wa chakula. Ndicho kilichotokea kwa mama Hajiri siku alipofukuzwa kwa Ibrahimu, akiwa kule jangwani amepotea hali ilikuwa mbaya sana, kwani chakula na maji viliwaishia kabisa, huwenda zilipita siku kadhaa hawakuona dalili yoyote ya kupata msaada. Hivyo alichokifanya Hajiri, ni kwenda mbali kidogo na kumlilia sana Mungu wake, na Mungu akasikia, akaonyeshwa palipo na maji, akaenda kumpa mwanae, kuonyesha ni jinsi gani alivyouthamini uhai wa Ishmaeli.

Mwanzo 21:14 Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba. 

15 Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja. 

16 Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, AKAPAZA SAUTI YAKE, AKALIA. 

17 Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko. 

18 Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa. 

19 Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana. 

Umeona kama Hajiri asingemtafuta Mungu katika hali ile, ni wazi kuwa Yule kijana ambaye alikuwa amekusudiwa awe taifa kubwa angefia jangwani na yale maono yasingetokea.

Ndicho tunachojifunza katika vifungu hivyo, kwenye kitabu cha Maombolezo, anasema kesha, ulie, kwa ajili ya watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa. Leo hii tuna watu wengi ambao wameokoka kwa kuisikia injili yetu. Lakini je, watu hao wanasimama au wanakufa?, Unapomhubiria mtu, hatutakiwi kusema yaliyobaki namwachia Mungu, bali ni kuhakikisha hafi kiroho kwa kukosa chakula cha uzima. Na hiyo inakuja kwa kuendelea kumfuatilia kumfundisha, Lakini zaidi sana KUMWOMBEA kwa Mungu usiku na mchana akue kiroho.

Tukiiga mfano wa Epafra jinsi alivyokuwa akiwaombea sana watu wa kolosai walioamini kwa injili yao.

Wakolosai 4:12  Epafra, aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu Kristo, awasalimu, akifanya bidii siku zote kwa ajili yenu katika maombi yake, ili kwamba msimame wakamilifu na kuthibitika sana katika mapenzi yote ya Mungu.

Umeona? Ukomavu wa watu walio wachanga wa kiroho hutegemea sana maombi ya kina kwa waliowazaa. Hivyo wewe kama mtenda kazi hakikisha unakuwa na maombi mengi kwa ajili ya wale uliowahubiria injili wakaokoka vinginevyo watakufa kiroho, katika ulimwengu huu wa njaa na kiu ya Neno la Mungu, tenga masaa kuwaombea. Na maombi hayo yawe ya rohoni kabisa, sio ya juu juu, bali ya kuzama, ili Mungu awakuze, na matokeo ya kazi yako utayaona tu baada ya kipindi fulani, jinsi watakavyozidi kubadilika na kukomaa kidogo kidogo, hatimaye kuwa watumishi imara katika shamba la Mungu.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

NJAA ILIYOPO SASA.

LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu 

SWALI: Nini maana ya

Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu, Ndivyo ilivyo habari njema itokayo katika nchi ya mbali.

JIBU: Biblia inalinganisha burudiko kubwa mtu analolipata pale anaposikia habari fulani njema na mfano wa mtu mwenye kiu halafu ghafla akaletewa kikombe cha maji ya baridi, sasa katika mazingira kama hayo ni wazi kuwa maji yale atayafurahia sana kwasababu yupo katika kiu.

lakini kiini cha mstari huo ni hapo anaposema ni habari njema ITOKAYO KATIKA NCHI YA MBALI.

Tukumbuke kuwa zipo habari njema nyingi..kwamfano habari za kupewa tenda fulani ya kibiashara ni habari njema, habari za kufaulu darasani ni habari njema, habari za kuzaliwa mtoto duniani ni habari njema, habari za kupandishwa cheo ni habari njema n.k…lakini zote hizi hazina jipya kwasababu ni za hapa hapa tu duniani.

Bali zipo habari njema zinazotoka katika nchi ya mbali na huko si kwingine zaidi ya MBINGUNI, hizo ndizo watu wana kiu nazo, wakizisikia tu ni lazima mioyo yao ni lazima iburudike sana.

Na habari zenyewe ni zile zinazomuhusu  Yesu Kristo.

Alisema.

Yohana 6:33-35

[33]Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.

[34]Basi wakamwambia, Bwana, sikuzote utupe chakula hiki. 

[35]Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.

Yesu ndio maji yakatao kiu, alileta habari njema iliyotoka mbinguni, alikuja kutuletea ukombozi na msamaha wa dhambi, alikuja kutufungua katika vifungo vyetu, na shida zetu mbalimbali, na kutumwagia karama za rohoni, mambo ambayo mwingine yoyote hawezi kutoa. Lakini zaidi sana alikuja kutuambia habari za ufalme wake, kwa habari ya mambo yanayokuja, kuhusu mbingu mpya na nchi mpya, na Yerusalemu mpya, na umilele, na uzuri na thawabu alizotuandalia sisi tuliomwamini. Mambo ambayo ukisikia kama wewe unapenda kweli maisha…utayafurahia sana.

hivyo yatupasa mimi na wewe tuwe na mwitikio huu, wa habari hizi njema kwa kuwashuhudia pia na wengine maji haya, kwasababu ni wazi kuwa wengi wana kiu, na hivyo wanahaja ya kuzisikia hizi habari njema zimuhusuyo Yesu Kristo.

Sote kwa pamoja tuamke tukahubiri injili. Tukijua kuwa inahitajiwa sana.

shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

INJILI NI NINI?

Maana ya Mithali 17:22 Moyo uliochangamka ni dawa nzuri;

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

Rudi Nyumbani

Print this post

AINA TATU ZA IBADA ZA SANAMU.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu, lililo Taa ya njia zetu na Mwanga wa njia yetu (Zab. 119:105).

Zipo aina tatu (3) za sanamu zinazoabudiwa na watu.

1.Sanamu zenye mfano wa Mtu

2.Sanamu-watu

3.Sanamu-vitu

Tutazame moja baada ya nyingine.

      1.SANAMU ZENYE MFANO WA MTU.

Hivi ni vitu vyote visivyo na uhai vyenye mfano wa mtu, ambavyo vinatengenezwa na watu kwa lengo la kuabudiwa.

Tabia ya hizi sanamu kulingana na biblia ni kwamba zina midomo lakini hazisemi, zina macho lakini hazioni, zina masikio lakini hazisikii, zina pua lakini hazinusi..na wanaoziabudu wanafanana na hizo kiroho.

Zaburi 115:4 “Sanamu zao ni fedha na dhahabu, Kazi ya mikono ya wanadamu.

5 Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho lakini hazioni,

6 Zina masikio lakini hazisikii, Zina pua lakini hazisikii harufu,

7 Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi, Wala hazitoi sauti kwa koo zake.

8 Wazifanyao watafanana nazo, Kila mmoja anayezitumainia”

Hizi ndio zile zote zinazoabudiwa na wapagani, pamoja na baadhi ya madhehebu yajiitayo ya kikristo. Utakuta sanamu imewekwa ndani ya nyumba ya ibada, na watu wanakwenda kuiangukia na kuisujudia, hata kuitolea sadaka na kuiomba, jambo ambalo ni machukizo makubwa..

Ni dhambi kubwa kusujudia sanamu yoyote ile, Kasome Kutoka 20:1-6.

2. SANAMU-WATU.

Hii ni aina  ya pili ya sanamu ambayo ni tofauti kidogo na ile ya kwanza… ile ya kwanza ina midomo lakini haisemi, ina macho lakini haioni, ina masikio lakini haisikii…. Hii ya pili nayo ni hivyo hivyo, ina macho lakini haioni, ina masikio lakini haisikii, ina macho lakini haioni..tofauti tu ni kwamba ile ya kwanza ile ya kwanza haipumui ila hii ya pili inapumua, ile ya kwanza imetengenezwa kwa miti, udongo, chuma, fedha au dhahabu lakini hii ya pili ni Wanadamu.

Sasa tunaisoma wapi katika biblia…

Ezekieli 12: 1 “Neno la Bwana likanijia tena, kusema,

2 Mwanadamu, wewe unakaa kati ya nyumba iliyoasi, WATU AMBAO WANA MACHO YA KUONA, ILA HAWAONI, WANA MASIKIO YA KUSIKIA, ILA HAWASIKII; kwa maana ni nyumba iliyoasi”.

Umeona? Kumbe sanamu sio tu mawe na udongo vinavyoweza kuwa sanamu bali hata watu..

Kama hujamaanisha kumfuata YESU wewe ni SANAMU.. Kwasababu una macho lakini huoni mambo ya rohoni, una masikio lakini husikii sauti ya MUNGU, Una kinywa lakini hakineni mambo ya Mungu, Hivyo wewe ni sanamu pamoja na viungo vyako vyote.

“KICHWA” chako ni sanamu/mungu wako, ndio maana unakitumikia kwa vitu vya kidunia kama YEZEBELI..

“MASIKIO” yako ni sanamu/mungu wako, ndio maana unayatumikia kwa kubadilisha vipuli kila siku.

“MACHO” yako ni sanamu/mungu wako, ndio maana unayatumikia usiku na mchana kupaka uwanja, na kupadilisha kope pamoja na kuchonga nyusi.

“MDOMO” wako ni sanamu/mungu wako, ndio maana unautumika kwa rangi na kila aina ya lipstick

“MIKONO” yako na “MIGUU” ni sanamu/mungu wako, ndio maana unaitumika kwa bangili na kucha za bandia..

“TUMBO” lako ni mungu wako ndio maana unalitumikia kwa kulinywesha pombe na kuliburudisha kwa kila linachohitaji usiku na mchana… Huna muda wa kufunga na kuomba walau kwa wiki mara moja, kwako kufunga ni adhabu kubwa!!..

Wafilipi 3:19  “mwisho wao ni uharibifu, MUNGU WAO NI TUMBO, utukufu wao u katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani”.

Ikiwa hujamaanisha kumfuata YESU kila kiungo katika mwili wako ni sanamu/mungu.. Ndio maana biblia inasema tuvifishe viungo vyetu vilivyo katika nchi, maana kwa hivyo huzaa dhambi na NDIO ibada ya sanamu.

Wakolosai 3:5 “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;

6  kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu”.

     3. SANAMU-VITU.

Hizi ni sanamu zote zisizo na mwonekano au maumbile ya mwanadamu lakni zinaabudiwa.

Mfano wa hizi ni kazi, fedha, umaarufu, Elimu, Mali kama nyumba, magari, ardhi n.k. Mtu akiwa na hivi na hana KRISTO maishani mwake ni mwabudu sanamu tu!

KUMBUKA: Usipomwabudu MUNGU  WA KWELI, basi unaabudu sanamu, na usipoabudu sanamu basi unamwabudu MUNGU WA KWELI, Hakunaga hapo katikati! Ni aidha uwe wa shetani au wa Mungu.

Kama kazi yako inaheshima kuliko Mungu kiasi kwamba unakosa hata siku moja ya wiki kumtolea Mungu wako, hiyo kazi ni sanamu/mungu kwako.

Kama elimu yako, au umaarufu wako au cheo chako kina nguvu kuliko Neno la MUNGU, basi hicho ulichonacho tayari ni mungu wako.

Je umeokoka?…Kumbuka wote wanaoabudu sanamu sehemu yao ni katika lilwe ziwa liwakalo moto na kiberiti kulingana na biblia.

Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, NA HAO WAABUDUO SANAMU, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

Biblia inamaanisha nini kusema Yeye aliye na sikio, na asikie?

USIMWABUDU SHETANI!

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

DANIELI: Mlango wa 3

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 17:22 Moyo uliochangamka ni dawa nzuri;

SWALI: Nini maana ya

Mithali 17:22 Moyo uliochangamka ni dawa nzuri; Bali roho iliyopondeka huikausha mifupa.


JIBU: Mstari huu unatuonyesha jinsi gani hali ya moyo inavyoweza kuathiri hali za nje za mwili. Si kila wakati dawa itatibu, ikiwa moyo umepondeka afya inaweza kuathiriwa pia. Kwamfano labda mtu yupo katika nyumba au makazi ambayo hana amani, anateswa, anaudhiwa, anaabishwa, muda wote anakuwa mnyonge, utaona pia kwa namna Fulani afya yake itaathirika, labda atasumbuliwa na ugonjwa Fulani ambao hauna sababu wala chanzo.

Lakini moyo ukichangamka, hata kama huyo mtu yupo katika hali/mazingira magumu kiasi gani, mwili wake pia baada ya mda utaitikia hali ya roho yake. Na hivyo atakuwa na afya yake.

Sasa Nitaufanyaje moyo wangu uchangamke?

1)    Kwa kutembea ndani ya ahadi za Mungu katika Neno lake. Mara kadhaa katika maandiko Bwana Yesu alisema” jipeni moyo”. Unapojipa moyo katika ahadi za Mungu ukijua kabisa, ni hakika atatenda,hasemi uongo, Fahamu kuwa utakuwa ni mwanzo wa kuchangamka kwako. Kwamfano ukikumbuka kuwa alisema hatatuacha wala kutupungukia, unakuwa na amani wakati wote, nyakati zote, ukiwa na vingi ukiwa umepungukiwa yote yatakuwa sawa tu, kwasababu sikuzote yupo pamoja na wewe. Furaha inakutawala.

Hata upitiapo magonjwa, ukikumbuka ahadi zake kuwa atakuponya, ukaendelea kuzishika kwa imani, afya yako hurejea.

Yeremia 30:17 Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana, kwa sababu wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni Sayuni, ambao hapana mtu autakaye. 

18 Bwana asema hivi, Tazama, nitarudisha tena hema za Yakobo zilizohamishwa, na kuyahurumia makao yake; nao mji huo utajengwa juu ya magofu yake wenyewe, nalo jumba litakaliwa, kama ilivyokuwa desturi yake. 

19 Tena kwao itasikiwa shukrani, na sauti yao WACHANGAMKAO; nami nitawazidisha, wala hawatakuwa wachache; tena nitawatukuza, wala hawatakuwa wanyonge.

Hivyo ishi kwa kushikilia ahadi za Mungu kwenye Neno lake, zipo nyingi sana, na zimefika katika kila Nyanja ya maisha yetu. Hakuna sababu ya kutochangamka, wakati Neno la ahadi lipo. Aliyekuahidia ni Mungu wa miungu muumba wa mbingu na nchi hakuna lolote linalomshinda, kwanini uogope?

2) Pili, kwa kupenda ushirika na wengine. Kamwe usiishushe wala kuipuuzia  nguvu iliyopo ndani ya ndugu katika Kristo. Zipo nyakati utahitaji kutiwa nguvu na wenzako, hata kukaa pamoja tu, kutafakari Neno la Mungu na kumwimbia Mungu ni tiba nzuri sana, itakayochangamsha moyo wako, tofauti na kama ungekuwa mwenyewe mwenyewe tu wakati wote.

Ndivyo ilivyokuwa hata kwa Paulo, wakati ule..

Matendo 28:15  Na kutoka huko ndugu, waliposikia habari zetu, wakaja kutulaki mpaka Soko la Apio na Mikahawa Mitatu. Paulo alipowaona alimshukuru Mungu, AKACHANGAMKA.

Chuma hunoa chuma, tuwapo pamoja, tunajengana nafsi, na matokeo ya kufanya hivyo yataonekana mpaka nje.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

PALE AHADI ZA MUNGU ZINAPOKUJARIBU.

JE! UNAIONA ILE NCHI NZURI YA KUMETA-META MBELE YAKO?

Je sisi wakristo tunaruhusiwa kufanya 40 za marehemu?

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 10:12 Kuchukiana huondokesha fitina

Elewa maana ya mstari huu;

Mithali 10:12 Kuchukiana huondokesha fitina; Bali kupendana husitiri makosa yote.

Mstari huu unalenga kutufundisha sifa za kipekee sana za upendo. Ambazo zinazungumziwa pia sehemu mbalimbali.

Kwamfano hapo anasema kuchukiana hakuzai kingine zaidi ya fitina,( yaani uchongezi, na kudhuriana), lakini upendano husitiri MAKOSA YOTE.  Anaposema yote. Ni kweli yote. Endapo upendo utatoka kwelikweli katika kilele chake. Hiyo ndio sifa ya ajabu ya upendo ambayo kitu kingine chochote chema hakiwezi kutoa, kwamfano imani, nguvu, mamlaka, uweza n.k. haviwezi kusitiri “makosa yote”. Ni upendo tu peke yake.

Neno hilo hilo pia limerudiwa katika agano jipya.

1Petro 4:8  Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi

Ndio maana Bwana Yesu alisema Torati yote imelalia hapo, katika kumpenda mwenzako kama nafsi yako, alisema  vile unavyotaka wewe utendewe watendee wenzako. Utashangaa tu, wivu unayeyuka wenyewe, hasira inakufa, vinyongo vinaondoka, mashindano yanapotea, wizi, uzinzi unafutika, kwasababu umegundua kuwa mwenzako ni kama hiyo nafsi yako mwenyewe, kama vile wewe unavyopenda kufanikiwa vivyo hivyo usichukie kuona mwenzako amefanikiwa.

Lakini Jambo hili linaweza kutoka ndani yetu kwa njia tatu. Ya kwanza ni kujazwa Roho Mtakatifu.  Kwasababu tunda mojawapo la Roho Mtakatifu ni upendo (Wagalatia 5:22). Hivyo unapokuwa mwombaji sana, hususani wa “masaa” sio dakika, unajazwa Roho Mtakatifu vema. Na matokeo yake ni kuwa urahisi wa kuudhihirisha upendo unakuja.

Lakini hilo peke yake halitoshi, unapaswa  uambatanishe na usomaji  wa Neno kila siku. Neno ni njia nyingine ya Roho Mtakatifu kukukumbusha, yale unayopaswa kufanya, kwamfano ukidhihirisha hasira ukisoma Neno utajifunza uvumilivu, utajifunza unyenyekevu, kuachia, na madhara ya kutokusamehe. Hivyo litakufanya uweze kurejea  kwenye mstari haraka pale unapokaribia kuteleza. Usipuuzie kusoma Neno kila siku.

Tatu, ni kutendea kazi. Lazima ujiwekee malengo. Kwasababu ukiwa mwombaji tu, na msomaji peke yake bado  haitakusaidia sana , kama huna mikakati ya kukifanyia kazi. Ndio maana hapo anasema iweni na JUHUDI nyingi katika kupendana,.Juhudi ni lazima yaani unaanza kuchukua hatua ya kushindana na vipinga-upendo, na hapo hapo utaanza kuona, wepesi umekuja ndani yako,

Sisi kama watoto wa Mungu, tumeagizwa tukue kila siku kuufikia upendo wa ki-Mungu ndani yetu. Ndio ukomavu wetu na kilele cha imani yetu. Kwasababu hii ndio dawa ya dhambi zote.(2Petro 1:5-11)

Bwana atuongezee neema.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

UMETEKWA NA UPENDO WA KRISTO?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

Rudi Nyumbani

Print this post

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA MATHAYO.

(Hotuba za Yesu)

Kitabu cha Mathayo ni moja ya vitabu vinne (4), vya injili. Yapo mambo mengi ya kujifunza ndani yake, lakini katika makala hii, tutaona mambo muhimu ya kufahamu ambayo yatakusaidia katika usomaji wako.

Tukiachia mbali matukio, na huduma mbalimbali ikiwemo za uponyaji alizozifanya Yesu. Tunafahamu kuwa Bwana “ALIFUNDISHA” pia. Na hapa ndipo kiini cha kujifunza kwetu.

Hivyo katika kufundisha kwake, kuligawanyika mara mbili. Kuna taarifa ambazo alizotoa bila kutolea maelezo mengi, lakini pia kuna taarifa alizitoa kama hotuba.

Sasa tutaangazia hizo HOTUBA, ambazo zimerekodiwa kwenye kitabu hichi.

Zipo tano (5), Nazo ni

  1. Hotuba ya Mlimani. (Mathayo 5-7)
  2. Hotuba ya utume (Mathayo 10)
  3. Hotuba ya ufalme wa mbinguni (Mathayo 13)
  4. Hotuba ya kanisa (Mathayo 18)
  5. Hotuba ya siku za mwisho (Mathayo 24)

Kabla ya kuziangalia kwa upana kidogo. Tufahamu kwanza hapo tusemapo “hotuba” tunamaanisha nini.

Hotuba ni mahubiri/mafundisho aliyoyasema Yesu kwa upana, yaliyolenga mada Fulani maalumu.

Ni mazungumzo marefu ya Bwana Yesu. kukazia jambo lile lile moja. Sasa embu Tuangalie kiini cha kila hotuba.

1) Hotuba ya mlimani. (Mwenendo wa Mkristo)

Hii tunaisoma katika sura ile ya 5,6,7. Ni wakati ambapo Bwana Yesu alipanda mlimani, kisha wanafunzi wake wakamfuata, akaanza kuwafundisha mambo mengi. Sasa kiini cha hotuba hii, kilikuwa ni kuwafundisha mwenendo sahihi wa Mkristo, unaokubaliwa na Mungu.

Anaanza kwa kusema HERI, HERI, HERI, maskini wa roho, wapole, wenye rehema, wapatanishi, wenye moyo safi, wenye kiu na njaa ya haki, n.k. anaendelea jinsi tunapavyopaswa tuwapende maadui, tusamehe, tusilipize kisasi, akafundisha usahihi wa kuomba, kufunga, kutoa sadaka, usafi wa moyo, na upendo, na mambo mengine kadha wa kadha.

Ni maneno ambayo kama wewe ni mwamini basi unapaswa uyasome na kuyatafakari kila inapoitwa leo. Kwasababu Huu ndio uliokuwa mwenendo wa Yesu duniani. Akahesabiwa kumpendeza Mungu kabla hata hajaanza huduma yake ya kuhubiri, kwasababu aliishi aliyokuwa anayasema. Hivyo siri iliyopo hapa ni kwamba alikuwa anasema mwenendo wa maisha yake yalivyokuwa.

Na sisi pia tukitaka tufanane, na Kristo kimwenendo na tabia, basi tuzingatie sana, kuyaaishi haya tunayoyasoma katika sura hizi tatu yaani 5,6,7, Ni muhimu sana, sio kuimba “natamani kufanana na wewe”, lakini hatujui tunafananaje na yeye.

2) Hotuba ya Utume (Mathayo 10)

Katika mahubiri haya, Bwana Yesu aliwaita wanafunzi wake na kuanza, kuwapa maelezo ya namna ya kuhubiri kule atakapowatuma. Akawaeleza kwa upana jinsi mazingira ya kuhubiri yalivyo, kwamba kuna mahali pia hawatakubalika, akawafundisha pia jinsi ya kuhubiri, akawaondoa hofu ya wanadamu, na hofu ya kusumbukia mahitaji kwamba huko huko mbele ya safari Bwana atakuwa nao, akawafundisha pia mahali pa kuanzia kuhubiri, akawafundisha hekima ya kuhubiri, na kuponya watu. Na mambo mengine kadha wa kadha.

Kiasi kwamba, wewe kama mtendakazi katika shamba la Bwana ukisoma habari hizi, zitakusaidia katika ustahimilivu wako shambani mwa Bwana, tukikumbuka kuwa kila mmoja wetu ameitwa na Bwana kwenda kuwafanya wengine kuwa wanafunzi. Hivyo, Usomapo habari hii ya kitume, itakusaidia kunoa vema utumishi wako, katika eneo la upelekaji kazi ya Mungu mbali. Pata nafasi pitia wewe mwenyewe kwa utulivu sura yote ya kumi. Bwana atakupa kuelewa mengi ndani yake. Na hivyo utakuwa mtume, kama mitume wako walivyokuwa.

3) Hotuba ya ufalme wa mbinguni (Mathayo 13)

Hii ni hotuba, iliyohusu siri za ufalme wa Mbingu. Ambapo Bwana Yesu alitumia mifano (mafumbo), kuulezea. Biblia inaposema ufalme wa mbinguni, inamlenga YESU mwenyewe, na kazi yake aliyokuja kuifanya duniani (Luka 4:18-19).

Katika sura hii ya 13, alieleza mifano mikuu saba (7), japokuwa kulikuwa na mengine aliyokuwa iliyohusu ufalme wa mbinguni isipokuwa haijarekodiwa katika kitabu hichi. Mfano wa kwanza ulikuwa ni wa mpanzi, kisha magugu na ngano, kisha chembe ya haradali, kisha chachu katika unga, kisha hazina iliyositirika katika shamba, kisha mfano wa mfanyabiashara na lulu, na juya lililotupwa baharini.

Katika mifano hii yote, maudhui ni kuonyesha ukubwa ulio ndani ya Kristo Yesu, pale mtu anapomwamini na kustahimili kumfuata ukweli ni kwamba ataanza kama chenye ya haradali, lakini ataishia mti mkubwa, ni kama aliyepata hazina na lulu kubwa sana, akaenda kuuza akawa tajiri,.

Hivyo usomapo kwa makini mifano hii, utakuwa na kila sababu ya kuutafuta sana ufalme wa Mungu (yaani Kumuhufadhi Kristo sana moyoni mwako). Kwasababu unajua ulichokitapata ni zaidi ya vitu vyote duniani. Ambavyo utakuja kuvifurahia vema uendapo kule ng’ambo mbinguni.

4) Hotuba ya kanisa (Mathayo 18)

Hotuba hii inalenga, namna ya kuchukuliana sisi kwa sisi (Kanisa), tuliomwamini Yesu katika eneo la kujishusha na kunyenyekeana, kutokwazana, kutokupuuziana, lakini pia kuwa tayari kuwatafuta wale waliopotea na kuwarudisha kundini, ni muhimu sana, akatoa mfano wa mtu aliyeacha kondoo wake tisini na tisa, na kwenda kumtafuta Yule mmoja aliyepotea. Na sisi yatupaswa tuwe na moyo huo wa kichungaji.

Vilevile kusameheana sisi kwa sisi hata saba mara sabini akatoa mfano wa Yule mtu aliyesamehewa talanta elfu kumi, lakini yeye hakuwa tayari kumsamehe aliyemdai dinari mia, pia alifundisha njia nzuri ya kuonyana kingazi kufatana na utaratibu kwa kikanisa.

Hivyo usomapo hotuba hii, utafahamu namna ambavyo Bwana anataka sisi tuishi kama ndugu tuwapo pamoja kama kanisa lake.

5) Hotuba ya siku za mwisho (Mathayo 24)

Hii ni hotuba inayohusu, matukio yote ya siku za mwisho wa dunia, na kurudi kwa Yesu kutakavyokuwa, anaeleza kwa urefu dalili zake, mabadiliko ya kimwenendo ya watu, yatakavyokuwa, majanga ya asili, na vita vitakavyofuata baadaye, anatoa tahadhari ya manabii wa uongo, unyakuo wa kanisa, dhiki kuu na mapigo ya Mungu, Na mwisho anatoa angalizo ni nini tunapaswa tufanye. Kwamba “Tukeshe”, kwasababu hatujui siku wala saa.

Hotuba hii ni vizuri ukaisoma kwa urefu, na kuelewa kwa undani, kwasababu nyakati tulizopo sasa, tupo katika “mwisho wa siku za mwisho.” Dalili nyingi zilizotabiriwa zilishatimia. Jiulize umejiandaaje kwa yaliyo mbele yetu?

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa, ufahamupo Mahubiri hayo (Hotuba), utapata uelewa wa undani kimaudhui ndani ya kitabu cha Mathayo, Jifunze kusoma sana, na kurudia rudia, hotuba hizi, kulikuwa na sababu kwanini Bwana atoe habari zake kwa urefu, kwasababu ndio “Fundisho” la mwamini. Zingatia hayo na Bwana akubariki.

Tutakuwa na uchambuzi wa vitabu vingine..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

ANGUKO LA UFALME WA SHETANI:

Rudi Nyumbani

Print this post

NIONDOLEENI KELELE ZA NYIMBO ZENU (Amosi 5:23)

Amosi 5:23 “Niondoleeni KELELE ZA NYIMBO ZENU; kwa maana sitaki kuzisikia sauti za vinanda vyenu”.

Je ni kwamba Mungu wetu hapendezwi na nyimbo tunazomwimbia??

Jibu ni la! Yeye anapendezwa na nyimbo na tena anaketi katika SIFA.

Zaburi 22:3 “Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za Israeli”.

Lakini kwanini aseme “niondoleeni kelele za nyimbo zenu?”… Ni wazi kuwa kuna nyimbo ambazo kwa Mungu ni kama kelele.

Sasa ni aina gani za nyimbo ambazo kwa Mungu ni kelele?.

1. NYIMBO ZA UNAFIKI.

Nyimbo za kinafiki ni zile mtu anazoimba kwa kupaza sauti, lakini maisha yake hayaendani na kile anachokiimba, kuanzia, uzungumzaji, uvaaji, utendaji na maisha yake yake siri. Mtu mwenye tabia hiyo halafu akasimama na kuimba nyimbo za kumtukuza Mungu, iwe ni nyimbo alizozitunga yeye, au za mwingine, mtu huyo anapiga kelele mbele za Mungu na hivyo anafanya dhambi.

2. NYIMBO ZENYE MIDUNDO YA KIDUNIA.

Kuna nyimbo ambazo zinafanana sana na za kidunia, kiasi kwamba mtu akisikiliza anafananisha na nyimbo Fulani ya kidunia ambayo alishawahi kuisikia mahali fulani. Nyimbo za namna hiyo ni kelele, na si kelele tu, bali pia ni machukizo… mfano wa hizo ni nyimbo aina ya rege, rap, pop, taarabu na nyingine zinazofanana na hizo, Nyimbo za namna hii zinajulikana kama nyimbo za upuuzi (Amosi 6:5). Hivyo wakristo hatupaswi kutumia midundo hiyo kumwimbia MUNGU.

3. NYIMBO ZINAZOSHIRIKISHA WASANII WA KIDUNIA.

Wasanii wa kidunia ni watu wanaoimba nyimbo za zinazotukuza na kusifia mambo ya ulimwengu huu, na ulimwengu upo chini ya shetani, sasa mtu anayewashirikisha waimbaji hao wa kidunia, waliozoea kumwimbia shetani, kisha wakapewa mashairi ya kumsifu Mungu pamoja na watu wa kiMungu, hizo ni kelele na machukizo mbele za Mungu, haijalishi nyimbo hiyo itakuwa na beti nzuri kiasi gani na ujumbe mzuri kiasi gani, au zenye kumsifia MUNGU kwa kiasi gani,  bado ni kelele mbele za Mungu na hazina matunda yoyote.

Nyimbo zenye kumtukuza Mungu ni zile zilizobeba ushuhuda wa Neno kuanzia kwa MWIMBAJI, beti na mdundo. Na zinapoimbwa zinamtukuza Mungu na kuwabariki wasikiao.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAONO YA NABII AMOSI.

WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.

Nini maana ya Mithali 9:13 Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu?

Fahamu maana 1Wakorintho 14:20  “Ndugu zangu msiwe watoto katika akili zenu;

LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.

Rudi Nyumbani

Print this post

NI MAJIRA YAPI YA NEEMA WEWE UPO?

Kuna wakati wa kukokotwa-kokotwa, lakini kuna majira ya  kuachwa ufanye maamuzi mwenyewe, na usipofanya unakufa. Mtu aliye mchanga kiroho, ni rahisi Mungu kuchukuliana naye katika mambo yasiyofaa kutokana na uchanga wake kwa siku zile za awali, lakini haiwezi kuwa hivyo siku zote, kwa jinsi siku zinavyokwenda, kusukumwa sukumwa hakutakuwepo, ni kuwa makini sana!.

Ukitafakari habari ya Mke wa Lutu, unaweza kupata picha halisi jambo hili lilivyo, yeye alidhani ataendelea kuvutwa-vutwa tu nyakati zote, lakini walipofikishwa mahali Fulani, nje kidogo ya mji wameshaijua njia, waliambiwa wajiponye wenyewe nafsi zao, lakini yeye akageuka nyuma, na wakati ule ule akawa jiwe la chumvi.

Mwanzo 19:15 Hata alfajiri ndipo malaika wakamhimiza Lutu, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu. 

16 AKAKAWIA-KAWIA; nao wale watu wakamshika mkono, na mkono wa mkewe, na mkono wa binti zake wawili, KWA JINSI BWANA ALIVYOMHURUMIA, wakamtoa wakamweka nje ya mji. 

17 Ikawa walipomtoa nje, mmoja alisema, JIPONYE NAFSI YAKO USITAZAME NYUMA, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea.

Hatari tuliyonayo sisi tuliopo katika siku hizi za mwisho, katika kanisa hili la Laodikia (Ufunuo 3:14-21), ni kwamba tunafahamu mambo mengi, na tumeshaona mifano mingi kwenye maandiko na kwenye historia, lakini geuko la dhati ndani ya wengi halipo, tukifikiri  tutalinganishwa na wale watu wa zamani. Neema kwako wewe haifanyi kazi katika kukokotwa tena, bali katika kukimbia. Ilifika wakati Yesu hakuwaambia tena wanafunzi wake “nifuate”, aliwaambia na “ninyi mnataka kuondoka?”

Halikadhali, kama umeshaokoka, jichunge sana, dhambi usiifanye rafiki kwako, ukidhani kila kosa tu utakalolifanya upo msamaha, acha hayo mawazo, unajitafutia kuwa mke wa lutu. Neno la Mungu linasema;

Waebrania 6:4  Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

5  na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,

6  wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

7  Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu; 8  bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.

Ni kusimama imara, sio tena kumbelezewa injili, sio tena kukumbushwa-kumbushwa wajibu wako wewe kama mkristo, na kuambiwa kaombe, nenda ibadani, mtafute Mungu, acha anasa, soma biblia. Ni wakati wa kujitambua kuwa sasa umeshatolewa nje ya mji, changamka, zama ndani ya Kristo. Acha kuwa vuguvugu utatapikwa, zama hizi ni zama za uovu. Wokovu wa mawazo mawili sio sasa, neema hiyo haipo kwetu mimi na wewe siku hizi za mwisho. Injili ya maneno laini, isikupumbaze, fanya Imara uteule wako na wito wako.

Ufunuo 22:10  Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

11  Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa

12  Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

Kimbia, usiangalie nyuma.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! “majira na sheria” mpinga-kristo atakayokuja kubalisha ni kupindua siku ya sabato na kuwa jumapili?

Nini tofauti ya Majira na Wakati?

UMEJIANDAAJE KWA NYAKATI ZA KUWA PEKE YAKO?

WAKATI ULIOKUBALIKA NALIKUSIKIA

Rudi Nyumbani

Print this post

UTAJUAJE UFAHAMU WAKO UMECHUKULIWA?

Swali: Utajuaje ufahamu wako umetekwa au ni viashiria gani vitakavyotambulisha kuwa ufahamu umetekwa na adui?


Jina la Bwana YESU libarikiwe.

Kabla ya kujipima kama ufahamu umechukuliwa au la!..Ni vizuri kwanza tukajua kibiblia mtu mwenye ufahamu anatafsiriwaje?

Turejee kile kitabu cha Ayubu 28:28.

Ayubu 28:28 “Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, kumcha Bwana ndiyo hekima, NA KUJITENGA NA UOVU NDIO UFAHAMU

Kwahiyo kumbe Mtu anayeweza kujitenga na Uovu ndiye mwenye ufahamu…maana yake kinyume chake yule asiyeweza kujitenga na uovu hana Ufahamu…au kwa lugha nyingine “UFAHAMU WAKE UMETEKWA”.

Na hapo neno linasema “kujitenga na uovu” na sio  “kujizuia na uovu”… maana yake “unakaa nao mbali”... Kama ni ulevi mtu anakaa nao mbali, kuanzia mazingira ya kulewa mpaka makundi ya walevi (wote anajitenga nao).

Kama ni uasherati na uzinzi, mtu anakaa nao mbali kuanzia mawasiliano, mavazi, makundi…vile vile anajitenga na mazingira yote yanayochochea hiyo dhambi ikiwemo mazungumzo na mitandao.

Kama ni usengenyaji, mtu anajitenga na mazingira hayo na makundi yote..

Kama ni utukanaji vivyo hivyo, Kama ni wizi/ufisadi au utukanaji na hasira ni hivyo hivyo..

Lakini kinyume chake mtu asiyeweza kujitenga na hayo yote basi UFAHAMU WAKE UMECHUKULIWA (UMETEKWA)!!...Upo chini ya Milki ya mkuu wa giza. Anatumikishwa na mamlaka za giza.

Haijalishi kama ni mchungaji, au askofu, au Nabii, au Mtume, au mwimbaji wa kwaya, au Papa, au Raisi wa nchi, au mtu mwingine yoyote mwenye kuheshimika katika jamii au kanisa.

Mtu asiyeweza kujiepusha na UOVU  ufahamu wake haupo (Umefungwa na kamba za kuzimu)., haijalishi ana uwezo mkubwa kiasi gani wa kupambanua mambo ya kimwili, haijalishi ana elimu kubwa kiasi gani na anategemewa na watu wengi kiasi gani katika kutatua mambo…bado ufahamu wake haupo!.

UTAURUDISHAJE UFAHAMU WAKO?.

Hakuna mtu ambaye kwa nguvu zake ana uwezo wa kuurudisha ufahamu wake!… Isipokuwa kwa msaada wa Mungu tu…Na msaada huu unaanza pale tunapoamua kufanya mageuzi katika maisha yetu kwa kutubia dhambi zetu na kumkiri Mwokozi YESU.

Ambapo kama tutatubu kwa kumaanisha kweli basi atatupa kipawa cha Roho wake mtakatifu ambaye kupitia huyo basi ataurejesha ufahamu uliochukuliwa na ile nguvu ya kuushinda uovu na kujitenga nao itakuwa juu yetu.

Faida ya kwanza ya ufahamu wa mtu kurudi ndani yake ni UZIMA WA MILELE lakini pia UZIMA WA MAISHA ya duniani, kwani ufahamu wa roho ndio unaofungua kufahamu mambo mengine yote.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post