Title 2025

Je Malaika wana viongozi?.

Swali: Je Malaika watakatifu walioko mbinguni wanao uongozi, kama sisi wanadamu tulivyo na viongozi wanaotuongoza?.


Jibu: Kama vile sisi binadamu tulivyo na Uongozi duniani biblia inatuonyesha pia Malaika wanao uongozi mbinguni,  maana yake wapo walio viongozi na wasio viongozi.

Kwa mfano tukisoma kitabu cha Ufunuo 12, tunaona Mikaeli anatajwa akiwa pamoja na malaika zake, hiyo ni kuonyesha kuwa Mikaeli ni kiongozi.

Ufunuo 12:7 “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;

8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni”.

Soma pia Yuda 1:9, utaona Mikaeli anatajwa tena kama Malaika Mkuu..

Na pia wakati ule Yoshua anakutana na yule Malaika wa Bwana baada ya kuvuka Yordani, Malaika yule alijitambulisha kuwa ni AMIRI wa jeshi la Bwana…Sasa Amiri maana yake ni kiongozi wa jeshi.

Yoshua 5:13 “Ikawa hapo Yoshua alipokuwa karibu na mji wa Yeriko, akavua macho yake na kuangalia, na tazama, mtu mume akasimama kumkabili mbele yake, naye alikuwa na upanga wazi mkononi mwake; Yoshua akamwendea, na kumwambia, Je! Wewe u upande wetu, au upande wa adui zetu?

14 Akasema, La, lakini nimekuja sasa, nili amiri wa jeshi la BWANA. Yoshua akapomoka kiusouso hata nchi, naye akasujudu, akamwuliza, Bwana wangu aniambia nini mimi mtumishi wake?

15 Huyo amiri wa jeshi la BWANA akamwambia Yoshua, Vua viatu vyako miguuni mwako; kwa kuwa mahali hapo usimamapo ni patakatifu. Yoshua akafanya vivyo”

Hivyo huyu Malaika alikuwa ni kiongozi wa Malaka wengine wa vita mbinguni, ndio maana akajitambulisha kama “Amiri”.

Lakini pamoja na kwamba upo uongozi katikati ya Malaika, hiyo bado haiwafanyi waabudiwe au wasujudiwe au kusifiwa.

Anayestahili kusifiwa na kusujudiwa duniani na mbinguni ni MUNGU peke yake.

Wakolosai 2:18 “Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, NA KUABUDU MALAIKA, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili”.

YESU KRISTO anarudi mwamini na mtumikie.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Je Malaika wana maamuzi binafsi?

Swali: Je Malaika wa mbinguni wana maamuzi binafsi kama tuliyonayo sisi wanadamu, mfano wakiamua kufanya jambo fulani wanafanya pasipo kuongozwa wala kuamuliwa?


Jibu: Maandiko yanatuonyesha kuwa viumbe pekee walioumbwa na Mwenyezi MUNGU walio na utashi ni Wanadamu pamoja na Malaika.

Na kama vile wanadamu tulivyo na utashi pamoja na maamuzi binafsi, (kwamba kuna mambo tunaweza kuamua wenyewe na mengine kuamuliwa) vile vile na malaika nao waliumbwa kwa mfumo huo huo,  wanayo maamuzi yao binafsi, na mengine kuamuliwa na MUNGU…

Na tena maamuzi mengine ya Malaika ni magumu kuliko hata yetu wanadamu..

Kwamfano tukirejea kabla ya Uasi wa shetani kule juu mbinguni, wakati ambao alikuwa ni malaika mkuu (Kerubi), biblia inatuambia kuwa ilifika wakati moyo wake ulinyanyuka na kuanza uasi, wa kutaka kuwa kama MUNGU, (yaani kuabudiwa).. sasa kitendo cha kuchukua hatua ya kutaka kuabudiwa hayo sio maamuzi madogo, na wala si hisia za kawaida… Kwahiyo malaika wa mbinguni na wale walioasi (yaani mapepo) wanayo maamuzi na hisia..

Sasa na malaika wengine wote wa mbinguni ni hivyo hivyo, wanayo maamuzi na hisia, na wana akili timamu…Ndio maana Bwana katika kutufundisha kuomba alisema tuombea “mapenzi ya yake yafanyike duniani kama kule juu mbinguni (Mathayo 6:10)”.

Ikiwa na maana kuwa mbinguni kuna shughuli zinaendelea, na malaika waliosalia mbinguni wanayafanya mapenzi ya MUNGU kila siku, na si kwamba wapo tu wamekaa wakisubiri amri Fulani!.. La wanaendelea na shughuli zao ambazo nyingi ya hizo sisi wanadamu hatuzijui, (lakini zote zipo ndani ya mapenzi ya MUNGU).

Zaidi tunaweza kusoma maandiko machache yanayozidi kutuonyesha kuwa Malaika wanayo maamuzi binafsi na ya kipekee..

Kutoka 23:20 “Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea. 

21 Jitunzeni mbele yake, mwisikize sauti yake; wala msimtie kasirani; maana, hatawasamehe makosa yenu; kwa kuwa jina langu limo ndani yake”.

Hapo anasema “huyo malaika” hatawasamehe, kuonyesha kuwa yeye si robot.. bali anatafakari na kapewa mamlaka na Mungu juu ya watu hao..soma tena Waamuzi 2:2-3.

Waamuzi 2:1 “Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi; 

2 nanyi msifanye agano lo lote na hawa wenyeji wa nchi hii; zipomosheni nchi madhabahu zao; lakini hamkuisikia sauti yangu; je! Mmefanya haya kwa sababu gani?

3 Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu.

 4 Ikawa, hapo huyo malaika wa Bwana alipoyanena maneno haya, kuwaambia wana wa Israeli wote, ndipo hao watu wakainua sauti zao na kulia”.

Tusome tena habari za Balaamu na Punda…

Hesabu 22:31 “Ndipo Bwana akafunua macho ya Balaamu akamwona malaika wa Bwana amesimama njiani, ana upanga mkononi mwake, umekwisha kufutwa naye akainama kichwa, akaanguka kifudifudi. 

32 Malaika wa Bwana akamwambia, Mbona umempiga punda wako mara tatu hizi? Tazama mimi nimekuja ili kukupinga, KWA SABABU NJIA YAKO IMEPOTOKA MBELE ZANGU,

 33 punda akaniona, akageuka upande mbele zangu mara tatu hizi; kama asingejiepusha nami, bila shaka ningalikuua wewe, nikamwacha yeye hai”.

Hapo Malaika anamwambia Balaamu kuwa njia za Balaamu zimepotoka mbele zake (huyo Malaika)

Lakini pamoja na na kwamba Malaika waliopo mbinguni wanayo maamuzi, lakini bado maamuzi yao hayavuki Neno la MUNGU,.. kwahiyo hawawezi kufanya lolote lililo kinyume na Neno la MUNGU, na wanafanya kazi pamoja na watu wa Mungu katika kuwahudumia (Soma Waebrania 1:14), na wanafurahi wanadamu wanapookoka.

Luka 15:10 “Nawaambia, Vivyo hivyo kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye”.

Malaika walioasi, yaani shetani na mapepo yake hao wanafanya maamuzi yao, yaliyo kinyume na mapenzi ya MUNGU na ndio chanzo cha matatizo yote ya wanadamu leo.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Ni kwa namna gani Bwana YESU alikula Siagi na Maziwa? (Isaya 7:15)

Swali: Tunasoma unabii wa Bwana YESU kuwa atakula siagi na maziwa, je ni kwa namna gani hilo lilitimia?


Jibu: Turejee..

Isaya 7:14 “Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli. 

15 Siagi na ASALI ATAKULA, wakati ajuapo kuyakataa mabaya na kuyachagua mema”. 

Siagi inayozungumziwa hapo ni ile inayotokana na maziwa..

Mithali 30:33 “Kwa maana kupiga maziwa HULETA SIAGI….”.

Kwahiyo kusema “Siagi na Asali” ni sawa kabisa na kusema “Maziwa na Asali”.. Hivyo unabii unaonyesha kuwa Mtoto YESU atakula Maziwa na Asali sawasawa ahadi Bwana aliowapa wana wa Israeli kipindi anawapandisha kutoka Misri..

Hesabu 14:8 “Ikiwa Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali”.

Lakini kabla ya kuangalia kwa undani ni kwa namna gani Bwana alikula Maziwa/siagi na Asali, tujifunze kwanza hatua wana wa Israeli walizopitia mpaka kuingia nchi imiminikayo maziwa na asali.

   1.KUITWA KUTOKA MISRI.

Hosea 11:1 “Israeli alipokuwa mtoto, nalikuwa nikimpenda, nikamwita mwanangu atoke Misri”.

Kutoka 3:17 “Nami nimesema, Nitawapandisha kutoka katika mateso ya Misri na kuwaingiza katika nchi ya Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, nchi ijaayo maziwa na asali.”

Na tukirudi kwa upande wa mtoto YESU naye pia aliitwa kutoka Misri, na kupandishwa mpaka nchi ya Israeli wakati akiwa mchanga..

Mathayo 2:14  “Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri;

15  akakaa huko hata alipokufa Herode; ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii, akisema, KUTOKA MISRI NALIMWITA MWANANGU.”

    2. KUFANYA MAPENZI YA MUNGU.

Ili ahadi ya kufaidi maziwa na asali katika nchi ya ahadi ni lazima wawe wanamcha MUNGU na kumpendeza, kwa kufanya mema, lakini kama watafanya mabaya basi hiyo nchi itawatapika..

Kumbukumbu 6:18 “Nawe fanya yaliyo sawa, na mema, machoni pa Bwana; ili mpate kufanikiwa, nawe upate kuingia na kuimiliki nchi nzuri Bwana aliyowaapia baba zako”

Kwa upande wa wana wa Israeli wapo waliofanya mema wakafanikiwa, na wako waliofanya mabaya na wakaikosa ahadi hiyo ya maziwa na asali, Lakini kwa upande wa Bwana YESU baada ya kupanda kutoka Misri maandiko yanasema alichagua MEMA, na kuyakataa MABAYA hivyo basi akashiriki ahadi ya kula Siagi na Maziwa sawasawa na ahadi ya Bwana..

Isaya 7:14 “Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli. 

15 SIAGI na ASALI ATAKULA, wakati ajuapo kuyakataa mabaya na kuyachagua mema”. 

Umeona?.. kumbe Kristo alijifunza kuyakaa mabaya tangu utoto wake na kuchagua mema?..na hiyo ikawa sababu ya kubarikiwa sana katika nchi ile aliyokuwepo, Kristo hakuishi maisha ya tabu, wala hakuwa na haja na kitu, vyote alipewa na Baba na alishabarikiwa tangu utoto, hakutawaliwa na magonjwa ya Misri, wala shida za kiMisri.

Sasa swali lingine ni hili, ni kwanini hatumsomi Bwana akiwa na mali nyingi?.. sababu kuu ni kwamba hakuwa anajilimbukizia, vyote alivyobarikiwa alivitoa kwa watu, na vingine hakutaka kuchukua, lakini haimaanishi kwamba alikosa, laiti angefungua mlango wa kupokea  vyote vya mwilini alivyopewa na Baba na kujilimbikizia, huenda ndani ya siku moja angekuwa mtu tajiri Zaidi ya mtu yeyote aliyewahi kutokea.

Lakini alijiweka katika hali hiyo kwasababu alijua upo utajiri mkuu Zaidi ya huu wa duniani, ambao ataupokea hapo baadaye,  

Kwahiyo Siagi na Asali inawakilisha Baraka zote za rohoni na mwilini katika nchi mtu aliyepo, ijapokuwa alijiweka katika hali ya umasikini lakini alikuwa ni tajiri sana, na rohoni alibarikiwa sana kwa Roho Mtakatifu zaidi ya mtu mwingine yoyote, miujiza aliyoifanya ni ya kupita kawaida na neema aliyoibeba ni kubwa sana kiasi cha kumtoa mwanadamu katika hukumu ya milele na kumwingiza katika uzima wa milele.

Na tunapomwamini na sisi tunaingia katika mkondo huo wa Baraka zake, kwanza tutapata uzima wa milele na pili tutapata baraka za mwilini.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Maana ya Mithali 30:33 Kwa maana kupiga maziwa huleta siagi

Print this post

Uchambuzi wa kitabu cha pili cha Paulo kwa Timotheo (2Timotheo).

Huu ni waraka wa Pili ambao mtume Paulo aliuandika kwa mwanae Timotheo akiwa kama mfungwa kule Rumi (2Timotheo 1:17)

Ni waraka wa Kitume zaidi, akimweleza Timotheo mambo mengi anayopaswa ayafanya, na ayaelewe kuhusiana na kazi ya Mungu.

Maudhui makuu ya Paulo yalikuwa ni haya;.

  1. Kumtaka Timotheo ajithibitishe vema katika huduma, 
  2. Lakini pia kumjuza juu ya tabia za wahudumu mbalimbali atakaokutana nao katika kazi ya Mungu, 
  3. Tabia zitakazoonekana siku za mwisho, jinsi asili ya watu itakavyokuwa na namna ya kukabiliana nazo.

Haya ni maelezo mafupi katika maeneo hayo makuu:

1) Wito kwa Timotheo kuwa kamili Na thabiti Katika huduma.

> Paulo Anaanza kwa kumtaka Timotheo aichochee karama iliyo ndani yake, aliyoipokea kwa kuwekewa mikono na yeye. Akionyesha kuwa huduma ni kama moto ambao ili kuufanya uendelee kuwaka inahitaji wakati wote uchochewe.(2Timotheo 1:6-8)

> Anamsihi kama askari mwema, ajikite katika kazi moja ya injili, Asipeleke fikra zake katika shughuli za kidunia, akimtaka afahamu hilo ili aweze kuvipiga vita vizuri vya imani, bila kuvutwa na mambo mengi.

2 Timotheo 2:3-7

[3]Ushiriki taabu pamoja nami, kama askari mwema wa Kristo Yesu.

[4]Hakuna apigaye vita ajitiaye katika shughuli za dunia, ili ampendeze yeye aliyemwandika awe askari.

[5]Hata mtu akishindana katika machezo hapewi taji, asiposhindana kwa halali.

[6]Yampasa mkulima mwenye taabu ya kazi kuwa wa kwanza wa kupata fungu la matunda.

[7]Yafahamu sana hayo nisemayo, kwa maana Bwana atakupa akili katika mambo yote.

> Anamtaka pia ajionyeshe Kuwa amekubaliwa na Mungu, Mtu awezaye kuligawanya Neno la Mungu vema, (2:15)

> Azikimbie tamaa za ujanani (2:22)

> Awe tayari kuhubiri injili Wakati wote  ufaao na usiofaa.(4:1-2)

> Awe na kiasi katika mambo yote, avumilie mabaya, atimize huduma yake. (4:5)

> Akumbuke pia akikubali kuishi maisha ya utauwa ataudhiwa.(3:12)

2) Tabia mbalimbali za wahudumu wenza.

Paulo anatoa habari za tabia alizokutana nazo kwa baadhi wa wahudumu wenza,

makundi hayo ni kama yafuatayo;

> Walioshirika na yeye nyakati zote kwa uaminifu,  mfano wa hawa ni Onesiforo na watu wa nyumbani mwake, pamoja na Luka(1:16).

> Waliotengana naye  kwasababu njema za mtawanyiko wa kihuduma mfano wa hawa ni Kreste na Tito,(4:9b)

> Lakini wapo ambao walimwacha kwa kupenda dunia mfano wa hawa ni Dema.(4:9)

> Na wengine kwa kujiingiza kwenye mafundisho ya uongo mfano wa hawa ni Himenayo na Fileto.(2:17-18)

> Na wengine walifanyika kabisa wapinzani wake. Mfano wa hawa ni Iskanda mfua shaba.(4:14)

Lengo la Paulo kumjuza juu ya watu hawa ni kumtaka ajifunze kuvumilia, na pia kujiepusha nao hususani wale wapingamizi, na kuweka misingi ya kimafundisho kwa kuwatahadharisha watu wasiyafuatishe mafundisho mengine, kwani makundi hayo atakutana nayo, na yatakuwepo.

3) Nyakati za hatari, katika siku za mwisho.

Paulo anampasha habari Timotheo uhalisia juu ya nyakati za mwisho, ambazo tangu wakati ule zilikuwa tayari zimeshaanza..

2 Timotheo 3:1-5

[1]Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.

[2]Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi,

[3]wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema,

[4]wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu;

[5]wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.

makusudi yake ni kumtaka avumilie, na kusimama  imara katika huduma, kwasababu nyakati ngumu atakutana nazo za watu wengi kujiepusha na mafundisho ya uzima.

Anasema pia kutazuka wimbi la waalimu wa uongo,  wapinzani wa injili mfano wa Yane na Yambre, ambao watashindana na kweli, (3:8-9).

Hatua za kuchua:

> Adumu katika mafundisho na mwenendo wote alioupokea kwake (3:10, 14)

> Awakabidhi wengine mapokeo hayo. .(2:1)

> Ajiepushe na mashindano ya kidini, na maneno yasiyokuwa na maana (2:16, 23-26)

Mwisho.

Paulo anaeleza mwisho wake, na sababu ya kuvipiga vita vema na kusimama imara katika Imani,  ni kwasababu aliiona ile  taji ya haki aliyowekewa Na Mungu mbinguni. Akitumai na Timotheo atasukumwa kuvipiga vita vema kwa kuiona thawabu hiyo hiyo aliyowekewa mbinguni.

2 Timotheo 4:6-8

[6]Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika.

[7]Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;

[8]baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Paulo kwa Timotheo (1Timotheo)

MAMBO NANE (8), AMBAYO WEWE KAMA KIONGOZI UTAIGWA.

UNALITUMIA KWA HALALI NENO LA KWELI?.

Print this post

Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?

Jibu: Biblia haijata umri wa Mariamu kipindi ametembelewa na Malaika Gabrieli na kupewa taarifa za kubeba ujauzito wa Bwana YESU kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

Na si miaka yake tu ambayo haijatajwa bali hata kabila lake Mariamu, wala ukoo wake….Na kwanini biblia haijarekodi mambo hayo yamhusuyo Maramu?….Jibu: Ni kwasababu si wa muhimu sana sisi kuujua…

Tunachojua ni kuwa Mariamua alikuwa ameshafikia umri wa kutosha wa kujitambua ndio maana tayari alikuwa ametolewa posa.. Hivyo alikuwa na umri wa kutosha na alikuwa mnyenyekevu na aliyemcha MUNGU.

Umri wa Mariamu, au familia aliyotokea au kabila alilotokea havikuwa vya umuhimu sana sisi kuvijua, kwasababu Mariamu alikuwa ni mwanamke tu kama wanawake wengine, alipata tu neema ya kumzaa Bwana YESU lakini hakuwa na utofauti na wanawake wengine waliomcha MUNGU.

Kwahiyo kilichokuwa cha muhimu sana sisi kujua ni kwamba “bikira atachukua mimba”…sawasawa na unabii wa Isaya.

Isaya 7:14 “Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli”.

Na hapo hasemi… “ bikira atachukia mimba akiwa na miaka 20 au 25 au 30”.. La! haisemi hivyo.. ikimaanisha kuwa lililo la msingi kwetu kulifahamu ni hilo la bikira kuchukua mimba basi, hayo mengine hayana umuhimu hivyo yanabaki kuwa ya Mungu na ya wale waliokuwepo wakati Mariamu anachukua ujauzito..

Kumbukumbu 29:29 “Mambo ya siri ni ya BWANA, Mungu wetu; lakini mambo yaliyofunuliwa ni yetu sisi na watoto wetu milele, ili tuyafanye maneno yote ya sheria hii”.

Wapo wanaomwona Mariamu kama mwanamke aliye tofauti na wanawake wengine wote, kwamba anaweza kusimama katika nafasi ya kutuombea au hata kutubariki, na hivyo anapaswa apewe heshima ya kipekee, na hata inaaminika pia kwa baadhi ya watu kuwa alipaa, jambo ambalo pia ni uongo.

Dhana ya kuwaamini manabii na watu waliopokea neema kwenye biblia kuwa ni watu wakuu sana wa kusimama katika nafasi ya kuombwa au kutukuzwa ilianza tangu zamani kabla hata ya ujio wa Bwana YESU.

Wapo waliokuwa wanamwabudu Henoko aliyetwaliwa, wapo waliokuwa wanamwabu Musa, wengine Eliya wengine Daudi, na sasa wapo wanamwabudu Mariamu n.k, lakini hawa wote biblia inasema ni watu kama sisi tu..

Yakobo 5:17 “Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita”.

Sasa kama Eliya aliyepaa mbinguni biblia inasema alikuwa ni mtu kama sisi vipi hao wengine ambao walikufa??…

Ambaye hakuwa mtu wa kawaida ni Bwana YESU tu na huyo ndiye maandiko yanasema anastahili kuabudiwa kwa kuwa alimwaga damu yake kwaajili yetu..

Ufunuo wa Yohana 5:8 “Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele za Mwana-Kondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni maombi ya watakatifu.

9 Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa”.

Je umempokea Bwana YESU…Umebatizwa katika ubatizo sahihi?.

Kama bado basi fanya uamuzi leo, kwasababu hizi ni siku za mwisho na YESU yupo mlangoni.

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 27:19 Kama uso katika maji ndivyo mtu na mwenzake

Mithali 27:19 Kama uso ufananavyo na uso katika maji; Kadhalika moyo wa mtu na mwenzake.


JIBU: Anaanza kwa kutoa mfano halisi, ili kueleza vema jambo la kitabia. Anasema kama vile maji yanavyoweza kuwa kioo kiakisicho, vivyo hivyo mioyo ya watu walio pamoja.

Kama tunavyojua ukiyatazama maji, utauona uso wako vilevile kama ulivyoyatazama, wala hayawezi kudanganya, ukiyaangalia umekunja sura, utaonekana hivyo hivyo, ukiyaangalia umevaa kofia, utajiona hivyo hivyo.

Ndivyo Mungu anavyowaona watu wawili waliojiungamanisha katika kitu kimmoja,(urafiki),  tabia ya mmoja itamwakisi mwingine, mwisho wa siku watafanana tu na kuwa na mwenendo sawa. Akiwa mmoja ni mwizi, Yule mwingine atakuwa kama yeye tu, akiwa mmoja ni mwamini mwombaji Yule mwenzake atakuwa naye mwombaji, akiwa ni mkarimu, mwenzake naye atakuwa hivyo hivyo.

Ndio sababu biblia inasema wawili hawawezi kukaa pamoja isipokuwa wamepatana (Amosi 3:3). Hivyo vifungu hivi vinatukumbusha umuhimu wa kuchagua watu sahihi wa kuambatana nao, imesisitiza tusifungwe nira ya watu wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa, kwasababu kwa njia hiyo watatuambukiza tabia zao.

Hata katika kuoa/kuolewa, ikiwa umeokoka, tafuta wa kufanana na wewe, au mbadilishe kwanza awe kama wewe ndio umwoe/uolewe naye vinginevyo, unajiandaa kugeuzwa tabia kama ilivyokuwa kwa Sulemani kuoa wake wa kimataifa.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI UTUKUFU WA MUNGU KUFICHA JAMBO.

Na alaaniwe ampigaye mwenzake kwa siri.

Amali, na kila kazi ya ustadi, inatokana na mtu kupingana na mwenzake.

Print this post

NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?

Je ni nani unayemwona zaidi usomapo biblia?..Je ni Musa?, au Eliya? au Elisha au nabii gani mwingine?..


Je ni habari za nani unapenda kuzihubiri zaidi katika biblia?…

Kama ni taswira za wanadamu ndizo zinazokujia zaidi basi kuna uwezekano macho yako bado hayajafunguka vizuri..

Leo nataka tuangalie ni nani tunayepaswa kumwona zaidi na kumhubiri zaidi kila tusomapo biblia…

Tuyarejee maneno yafuatayo ya Bwana YESU..

Luka 24:25 “Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii!

26 Je! Haikumpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake?

27 AKAANZA KUTOKA MUSA NA MANABII WOTE, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe”.

Hapa Bwana YESU hakuanza kuwafunulia maandiko kwa kuanza kumtukuza Musa au Eliya na uhodari wao…La! Bali alianza kuelezea habari zinazomhusu yeye mwenyewe..

Wala kumsifu Samson na ushujaa wake, bali kupitia habari za Samson alijionyesha nafasi yake..

Vile vile hakuanza kumsifia na kumtukuza Sulemani na wake zake na mke wake, bali kupitia maisha ya Sulemani alielezea habari zake zaidi..na hivyo hivyo kwa manabii wengine wote, kupitia maisha yao na nyaraka zao alijielezea yeye mwenyewe…

Tuangalie maandiko machache ya manabii yaliyomhusu yeye

》  Nabii Musa aliandika habari za Bwana YESU!!..

Kumbukumbu 18:15 “BWANA, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye”.

》 Nabii Samweli naye aliandika naye habari za Bwana YESU!!..

1Samweli 2:1 “Nami nitajiinulia kuhani mwaminifu, atakayefanya sawasawa na mambo yote niliyo nayo katika moyo wangu, na katika nia yangu; nami nitamjengea nyumba iliyo imara; naye atakwenda mbele ya masihi wangu milele”.

》 Na Nabii Isaya naye aliandika habari za mkuu wa uzima YESU, 

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani”

Soma pia Isaya 7:14.

》 Pia Nabii Mika aliandika habari za YESU..

Mika 5:2 “Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele”

》 Bila kumsahau na Daudi naye aliandika habari za YESU.

Zaburi 22:18 “Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu wanalipigia kura”.

Linganisha na Mathayo 27:35..

》 Nabii Hosea naye hakuacha kumtaja YESU..

Hosea 11:1 “Israeli alipokuwa mtoto, nalikuwa nikimpenda, nikamwita mwanangu atoke Misri”.

Linganisha na Mathayo 2:14-15.

》 Na Yeremia naye alimzungumzia YESU KRISTO.

Yeremia 31:15 “BWANA asema hivi, Sauti imesikiwa Rama, kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake; asikubali kufarijiwa kwa watoto wake, kwa kuwa hawako”

Linganisha na Mathayo 2:18.

》Na nabii Zekaria ni hivyo hivyo..

Zekaria 9:9 “Furahi sana, Ee binti Sayuni; Piga kelele, Ee binti Yerusalemu; Tazama, mfalme wako anakuja kwako; Ni mwenye haki, naye ana wokovu; Ni mnyenyekevu, amepanda punda, Naam, mwana-punda, mtoto wa punda”.

Linganisha na Mathayo 21:5.

》 Bila kumsahau Danieli naye alimwona YESU

Danieli 7:13 “Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye.

14 Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa”.

》 Na malaki alimwona pia..

Malaki 3:1 “Angalieni, namtuma mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu; naye Bwana mnayemtafuta atalijilia hekalu lake ghafula; naam, yule mjumbe wa agano mnayemfurahia, angalieni, anakuja, asema BWANA wa majeshi”

》 Nabii Yona naye ni hivyo hivyo aliandika habari za YESU..Soma Mathayo 12:40.

》 Nabii Ezekieli alieleza habari zake YESU…Soma Ezekieli 36:26-27 linganisha na Yohana 15:26.

》  Nabii Amos aliandika mahubiri ya yake YESU…Soma  Amosi 8:9 linganisha na Mathayo 24:29.

》 Nabii Yoeli naye alizigusia kazi zake..

Soma Yoeli 2:28-32

》 Ayubu naye alimwona Soma Ayubu 19:25.

Na manabii wengine wote walimwona YESU kabla ya wakati na kuandika habari zake.

Hiyo ni kuonyesha jinsi YESU KRISTO alivyo kiini cha Imani, na kiini cha mafundisho..

Tukiweza kufikia kiwango cha kumwona Bwana YESU zaidi katika biblia zaidi ya mtu mwingine yeyote sisi ni watu wengine na wenye akili, na hapo ndipo tunapoweza kusema kuwa tunaijua biblia..

Luka 24:44 “Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi.

45 Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko”.

Bwana atufune akili zetu tumjue sana Mwana wa Mungu.

Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo”.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Nini Maana ya kauli “atakatiliwa mbali na watu wake”. (Walawi 7:27)

SWALI: Kwanini sehemu kadha wa kadha wana wa Israeli walipoonekana wanakwenda kinyume na Torati hutumia kauli ya 

“atakatiliwa mbali na watu wake”. Nini maana ya hii kauli?

Mambo ya Walawi 7:27

[27]Mtu ye yote alaye damu, mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake.


JIBU: Ni kauli ya ujumla inayomaanisha huyo mtu atatengwa na kusanyiko la Israeli. Kutengwa huko kunaweza kuwa Kwa namna mbalimbali kutegemeana na aina ya kosa.

Hizi ndio aina kuu tatu za kukatiliwa mbali

 

1) Kifo.

Kifo kilihusika katika baadhi ya hukumu, ambazo Nyingine ni Mungu mwenyewe aliyezitekeleza (Walawi 20:3-6). Na nyingine Wanadamu. Kwamfano mtu yeyote aliyefumaniwa katika uzinzi, adhabu yake ilikuwa ni kupigwa Mawe Mpaka kufa. 

Vivyo hivyo katika kuihalifu sabato, adhabu ilikuwa ni hiyo soma;

Kutoka 31:14

[14]Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake. 

 

2) Kutengwa na jamii ya watu.

Hii nayo ilikuwa ni aina nyingine ya kukatiliwa mbali, ambapo ulifutwa katika hesabu ya waisraeli, inayokufanya kupoteza haki ya kushiriki Ibada yoyote katika makusanyiko, au vipaumbele.

Hesabu 19:20

[20]Lakini mtu atakayekuwa najisi, naye hataki kujitakasa, mtu huyo atakatiliwa mbali katika mkutano, kwa sababu amepatia unajisi mahali patakatifu pa BWANA; hayo maji ya farakano hayakunyunyizwa juu yake; yeye yu najisi. 

 

3) Kupoteza baraka za maagano

Maana yake ni kuwa hauwi mshirika tena wa baraka za maagano ya Mungu, kama vile ulinzi na ahadi.

Mwanzo 17:14

[14]Na mwanamume mwenye govi asiyetahiriwa nyama ya govi lake, mtu yule atatengwa na watu wake; amelivunja agano langu. 

 Hata leo, katika agano jipya mambo mambo tunaweza kufanya yakatusababishia kukatiliwa mbali na rehema za Mungu. 

Na adhabu hizo zinaweza kutekelezwa na wanadamu(watakatifu), na nyingine Mungu mwenyewe.

Kwamfano Biblia inatoa ruhusu kanisa kumtenga mtu ambaye anazoelea dhambi, (1Wakorintho 5:1-5)

Mungu mwenyewe anaweza kutekeleza hukumu hiyo, kwamfano tunaweza kuona kwa Anania na Safira, ambao walitumia njia ya hila katika mapatano ya Roho.(Matendo 5:1-11). Lakini pia kwa mtu ambaye anakusudia kuurudia ulimwengu baada ya kuipokea neema, hukumu kama hii huweza kumkuta. (Waebrania 10:26-27)

Kwahiyo jambo hili halikuwa tu kwa wana wa Israeli, lakini lipo hata sasa rohoni. Tusiwe watu wa kuzoelea dhambi tukidhani kuwa wakati wote Mungu ataturehemu. Usidanganyike ukishakatiliwa mbali si rahisi tena kumgeukia Mungu wako.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Tofauti kati ya makuhani na walawi ni ipi?

Maana ya Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu 

ALIPOKUWA ANGALI MBALI, BABA YAKE ALIMWONA.

Print this post

Swali: Je Kula nyama mbichi ni dhambi?.

Swali: Je kula nyama mbichi ni dhambi kibiblia?…Maana zamani tulikuwa tunakula maini mabichi na utumbo mbichi ule wa taulo.


Jibu: Hakuna maelezo ya moja kwa moja katika biblia yanayoonyesha kuwa kula nyama mbichi ni dhambi,

Lakini vipo vielelezo vichache katika maandiko vinavyoonyesha kuwa si vizuri/si sahihi kula nyama mbichi.

Wakati wana wa Israeli wanatolewa Misri, ule usiku Bwana MUNGU aliwaambia waile pasaka, ambapo waliagizwa wamtwae mwanakondoo na kumooka motoni, wamle pamoja na mboga chungu lakini wasimle mbichi.

Kutoka 12:8 “Watakula nyama yake usiku ule ule, imeokwa motoni, pamoja na mkate usiotiwa chachu; tena pamoja na mboga zenye uchungu.

9 MSIILE MBICHI, wala ya kutokoswa majini, bali imeokwa motoni; kichwa chake pamoja na miguu yake, na nyama zake za ndani”.

Kwa asili Ulaji wa nyama mbichi ni hatari kwa afya ya mwili, kwani nyama mbichi ina minyoo na wadudu wengi wasiionekana kwa macho ambao ni hatari kwa afya na tumepewa maagizo ya kuitunza hii miili..lakini nyama iliyopikwa inakuwa salama kwani inaea vimelea hivyo…

Na pia ulaji wa nyama mbichi unaweza kuashiria uwepo wa roho nyingine ndani ya mtu, na mara nyingi roho ya ukatili inawaingia watu walao nyama mbichi (kwani wanyama ndio walao nyama mbichi).

Na pia ulaji wa nyama mbichi unahusiana na imani za kishirikina na imani nyingine potofu…

Hivyo si vyema kula nyama mbichi kama wanyama.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Paulo kwa Timotheo (1Timotheo)

Tofauti na nyaraka nyingi za mtume Paulo, ambazo aliziandika kwa Makanisa, waraka huu aliuelekeza kwa Timotheo ambaye alisimama sio tu kama msaidizi wake wa kihuduma bali pia kama mwanae Katika vifungo vya injili. Ni waraka wa kichungaji zaidi ya wa kimafundisho,

Katika waraka huu Paulo anamwagiza Timotheo namna ambavyo kanisa linapaswa likae katika utaratibu, Mungu alioukusudia.(1Timotheo 3:15)

Maudhui makuu ya Paulo kwa Timotheo yalikuwa ni haya;

  1. Kujilinda na waalimu wa uongo.
  2. Namna ya ‘jinsia na marika’ mbalimbali yanavyopaswa yaenende/ kuhudumu ndani ya nyumba ya Mungu.
  3. Vigezo vya viongozi thabiti wa kuliongoza Kanisa.
  4. Agizo kwa Timotheo kuwa kamili katika utumishi wake.

Haya ni maelezo mafupi Kwa kila kipengele.

1) Kujilinda na waalimu wa Uongo.

Paulo anamhiza Timotheo lengo kubwa la kumtaka abaki Efeso ni ili awazuie watu wasifundishe elimu nyingine.

1 Timotheo 1:3

[3]Kama vile nilivyokusihi ukae Efeso, nilipokuwa nikisafiri kwenda Makedonia, ili uwakataze wengine wasifundishe elimu nyingine;

Elimu hiyo potofu aliyoina iliegemea kuwazuia watu wasile aina ya vyakula, Wasioe, pamoja na kuhubiriwa Hadithi za kizee, na nasaba (1:4, 4:7)

Kwa urefu wa mafundisho Hayo bofya hapa >>> HADITHI ZA KIZEE.

1 Timotheo 4:1-3

[1]Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

[2]kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;

[3]wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.

2) Namna ‘jinsia na marika’ mbalimbali yanavyopaswa yaenende ndani ya Kanisa la Mungu.

Kwa wanaume: Paulo anatoa agizo la kwamba wao wanajukumu la kusalisha kila mahali, lakini bila hasira wala majadiliano, yaani wawe safi kiibada (2:8)

Kwa Wanawake: Paulo anatoa agizo kuwa hawana ruhusa ya kufundisha katika kanisa (2:12), halikadhalika wanawajibu wa kuvaa mavazi ya kujisitiri, mapambo yao yawe yale ya rohoni na sio ya mwilini (2:9-10).

Anaendelea kusema Wanawake ambao ni wajane waandikwe katika kanisa ili Wahudumiwe kimahitaji, lakini wale ambao si wajane kwelikweli hawapaswi kuandikwa (5:4-16)

Wazee, na vijana wafanyapo makosa wasikemewe, Bali Waonywe kwa upole Kulingana na marika yao(5:1), lakini pale wafanyapo dhambi. kwa kukusudia au kuzoelea wakemewe mbele ya wote. (5:20),

Watumwa wote wanawajibu wa kuwaheshimu mabwana zao, si tu kwa wale wasiamini bali pia kwa wale waaminio wawaheshimu wote. (6:1)

Kanisa lina wajibu wa kuwaombea watu wote, na watawala, ili liishi katika utulivu, na amani, katika utauwa wote.(2:1-4)

3) Kuchagua viongozi thabiti wa kulichunga kanisa

Sehemu hii Paulo anamwagiza Timotheo juu ya vigezo vya maaskofu, na Mashemasi namna wanavyopaswa wawe, kwamba wawe watu wasio laumika, wameshuhudiwa mema na watu wa nje, waume wa wake mmoja mmoja, si watu wa kupenda fedha,si walevi, si waongofu wapya, wanapaswa wawe wakaribishaji,, wastahivu, wenye kiasi, waaminifu, wawasimamiao watoto wao vema, na wake zao, (3:1-13).

Lakini pia anawahimiza wazee wanaotawala vema wahesabiwe kuwa wamestahili heshima mara dufu (5:17).

4) Agizo la Paulo kwa Timotheo kuwa kamili katika utumishi wake.

Paulo anamwagiza Timotheo wajibu wake kama mwangalizi kuwa na upendo, Imani isiyo na unafki, na dhamiri njema, upole, saburi, na haki (1:5, 18-20, 6:11),

Anamwagiza afanye mambo yote bila upendeleo (1Timotheo 5:21).

Ajizoeshe kupata utauwa (4:8).

Awe kielelezo katika usemi na mwenendo (4:12)

Asiwaekee watu mikono kwa haraka,(5:22)

Akimbie tamaa ya fedha, na mashindano ya kidini (6:20).

Hitimisho.

Hivyo kwa ufupi, waraka huu ni wa kikanisa zaidi, na kwamba vigizo hivyo vikisimamiwa vema kanisa litakuwa imara, lenye heshima lisiloshitakiwa mabaya nje.

Ikiwa viongozi watachaguliwa hodari, na kila rika na jinsia likahudumu katika nafasi yake, yaani wanawake Kudumu katika upole, kujisitiri na kiasi na wanaume kuhudumu bila hasira wala majadiliano, huku waangalizi wakihakikisha mafundisho potofu hayapati nafasi. Ni ukweli kwamba kanisa hilo litakuwa imara sana.

Bwana akubariki

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mada nyingine:

Nasaba ni nini kibiblia?(1Nyakati 9:1, Tito 3:9)

Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE

Print this post