Title Devis

YONA: Mlango wa 4

Bwana wetu YESU KRISTO atukuzwe.

Tunamshukuru Mungu kwa kutupa neema hii mpya ya kujifunza Neno lake. Leo tukiwa ukingoni kabisa wa kitabu cha Yona ile sura ya nne. Kama tulivyojifunza katika sura zilizotangulia, Nabii Yona anawakilisha kundi la wakristo pamoja na wahubiri walio vuguvugu wa Imani biblia inawaita wanawali wapumbavu, ambao walipaswa kuingia na Bwana wao katika karamu lakini kwasababu Taa zao hazikuwa na mafuta ya ziada wakaachwa. Kwasababu walikisia tu kwamba yale mafuta yaliyokuwa katika taa zao yangewatosha mpaka wakati wa Bwana wao kuja (Mathayo 25). Ni Mfano dhahiri wa wakristo wa kanisa hili la mwisho la Laodikia.

Na kiini cha sura hii ya mwisho tunaona ni Yona kutoa SABABU YA YEYE KUTOKWENDA NINAWI. Na haya yote tunayaona ni baada ya Bwana kughahiri mabaya yote aliyokuwa ameyakusudia kuyaleta juu ya Mji wa Ninawi, baada ya kuona kuwa matendo yao yamebadilika na kutubu, Tunasoma:

Yona 4

“1 Lakini jambo hili lilimchukiza Yona sana, naye akakasirika.

2 Akamwomba Bwana, akasema, Nakuomba, Ee Bwana; sivyo hivyo nilivyosema, hapo nilipokuwa katika nchi yangu? HII NDIYO SABABU NALIFANYA HARAKA KUKIMBILIA TARSHISHI; KWA MAANA NALIJUA YA KUWA WEWE U MUNGU MWENYE NEEMA, UMEJAA HURUMA, SI MWEPESI WA HASIRA, U MWINGI WA REHEMA, NAWE WAGHAHIRI MABAYA.

3 Basi, sasa, Ee Bwana, nakuomba, uniondolee uhai wangu; maana ni afadhali nife mimi kuliko kuishi.

4 Naye Bwana akasema, Je! Unatenda vema kukasirika?

5 Ndipo Yona akatoka mjini, akaketi upande wa mashariki wa mji, akajifanyia kibanda huko, akakaa chini yake uvulini, hata aone mji ule utakuwaje.

6 Na Bwana Mungu aliweka tayari mtango, akaufanya ukue juu ya Yona, ili uwe kivuli juu ya kichwa chake, na kumponya katika hali yake mbaya. Basi Yona akafurahi sana kwa sababu ya ule mtango.

7 Lakini siku ya pili kulipopambazuka, Mungu akaweka tayari buu, nalo likautafuna ule mtango, ukakatika.

8 Basi ikawa, jua lilipopanda juu, Mungu akaweka tayari upepo wa mashariki, wenye hari nyingi; jua likampiga Yona kichwani, hata akazimia, naye akajitakia kufa, akasema, Ni afadhali nife mimi kuliko kuishi.

9 Mungu akamwambia Yona, Je! Unatenda vema kukasirika kwa ajili ya mtango? Naye akasema, Ndiyo, natenda vema kukasirika hata kufa.

10 Bwana akamwambia, Wewe umeuhurumia mtango, ambao hukuufanyia kazi, wala kuuotesha; uliomea katika usiku mmoja, na kuangamia katika usiku mmoja;

11 na mimi, je! Haikunipasa kuuhurumia Ninawi, mji ule mkubwa; ambao ndani yake wamo watu zaidi ya mia na ishirini elfu, wasioweza kupambanua katika mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto; tena wamo wanyama wa kufugwa wengi sana?”

Kama tunavyosoma maandiko hapo juu, sababu pekee iliyomfanya YONA akaidi njia za Mungu, ni kumkadiria Mungu kwamba yeye anaweza yote, Yona alimsoma Mungu kwa muda mrefu akaona jinsi alivyokuwa analirehemu taifa la Israeli pindi walipokuwa wanamuudhi sana Mungu, na kutaka kuangamizwa lakini Mungu alikuwa akighahiri mabaya yote. Hata wakati Yona alipokuwa anaishi katika Taifa lake, uovu wa wana wa Israeli ulikuwa ni mwingi sana, lakini Bwana alikuwa akiwahurumia kwa kuwatumia manabii wake kuwaonya watubu. Hivyo Yona kwa kuyajua hayo yote, Neno la Mungu lilipomjia na kuambiwa aende Ninawi kawahubiria watu watubu vinginevyo wataangamizwa, yeye akajisema ndani ya moyo wake, ..’aa Mungu najua siku zote ni wa rehema, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa huruma, huwa anaghahiri mabaya, ni mwema, anatupenda sana. mwisho wa siku atasamehe tu!.Yona hakuona sababu ya kwenda kuwapa watu presha, wakati mwisho wa siku anajua wataponywa tu! Mungu ni mwingi wa rehema. Hivyo Yona kwa kulijua hilo akalifanya lile Neno kuwa jepesi sana, na kuendelea na mambo yake mwenyewe, na kama tunavyosoma habari yakamkuta mabaya yale pale alipopitia dhiki isiyokuwa ya kawaida tumboni mwa samaki siku tatu usiku na mchana….

Ndivyo ilivyo kwa wahubiri wa leo na wakristo walio vuguvugu, Wahubiri wengi mwanzoni walitumwa na Mungu kweli wawahubirie watu habari za TOBA, na kwamba wamgeukie Mungu na kuacha njia zao mbaya kwasababu hukumu ya Mungu inakuja. Lakini wengi wamegeuka sasa wanawahubiria watu mahubiri ya faraja angali wanajua kabisa Hakuna amani kwa mtu ambaye hajatubu kwa kumaanisha kuziacha dhambi zake na kujazwa Roho Mtakatifu, Mahubiri yao siku zote ni …”Mungu ni wa rehema”…”Yote ni mema, “Haijalishi”..”Mungu ni Mungu wa upendo” “Hawezi kuteketeza dunia leo wala kesho,… tunaishi chini ya neema”..”Mungu haangalii mavazi, anaangalia moyo”n.k.

Wahubiri hawa kiini cha mafundisho yao ni faraja na mafanikio ya ulimwengu huu tu!..TOBA inatupiliwa nyuma kama kitu kisichokuwa na umuhimu sana. kwamba kwao laana kubwa ni mtu ambaye hajafanikiwa kimaisha, na sio mtu ambaye hajatubu dhambi zake. Lakini hawakusoma kwamba Neno la kwanza Yohana mbatizaji alilohubiri katika huduma yake ni TOBA, pia Hubiri la kwanza lililotoka katika kinywa cha Bwana wetu YESU KRISTO ni TUBUNI! kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia. Lakini wao neno lao la kwanza ni NJOO UPOKEE!!.. Na kundi kubwa la wakristo limeungana na hawa watu hawajui kuwa wote kwa pamoja wanaelekea Tarshishi kwa NJIA YA BAHARI ambapo humo yumo yule mnyama atokaye baharini mwenye vichwa 7 na pembe 10 (Ufunuo 13&17) aliyewekwa tayari kuwameza, katika kile kipindi cha dhiki kuu. Wakati huo unyakuo wa Bibi-arusi wa kweli wa Kristo utakuwa umeshapita.

Lakini ni kwasababu gani watayapata hayo yote?. Ni kwasababu walikisia kuwa Mungu ni Mungu wa rehema, si mwepesi wa hasira, kwani kuna watoto wasiojua mema na mabaya, kuna wanyama, kuna mimea, n.k. Bwana hawezi kuangamiza vyote hivyo. Lakini ndugu nataka nikuambie Bwana anaweza kama alifanya kwa wakati wa Nuhu, na wakati wa Luthu atafanya pia katika siku za mwisho kama watu wasipotubu.

Kuna wakati kilele cha maovu ya Israeli kilifika na Bwana akakusudia Yuda kuchukuliwa utumwani (BABELI). Na Bwana alimtumia nabii Yeremia kutoa unabii huo kwa mfalme wa Israeli na wakuu wake, na kuwaambia baada ya siku ambazo si nyingi watachukuliwa mateka waende Babeli, lakini alizuka nabii mmoja anayeitwa HANANIA yeye alinyanyuka na kutabiri kuwa Bwana ameghahiri mabaya hawataenda tena utumwani zaidi ya yote vile vitu vyao vilivyochukuliwa kabla vitarudishwa. Hivyo Israeli wote wakafurahi na kustarehe na kufarijika sana, wakijua ni habari njema, kumbe hawajui Hanania hakutumwa na Mungu ni nabii wa uongo. Na baada ya miezi 2 Mungu alimuua kwa kuwatumainisha watu uongo.

Yeremia 28: 15 ” Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, Sikia sasa, Ee Hanania; Bwana hakukutuma; lakini UNAWATUMAINISHA WATU HAWA MANENO YA UONGO.

16 Basi Bwana asema hivi, Tazama, nakutuma uende zako toka juu ya uso wa nchi; mwaka huu utakufa, kwa sababu umenena maneno ya uasi juu ya Bwana.

17 Basi nabii Hanania akafa, mwaka uo huo, mwezi wa saba.”

Hivyo ndugu usidanganyike na Injili za matumaini kana kwamba hakuna hukumu inayokuja mbeleni. Tunaishi katika siku za mwisho hizi, Bwana Yesu yupo mlangoni kurudi, wakati umeenda sana, ishi maisha ya TOBA, na utakatifu, jiepushe na ibada za sanamu, uasherati, ulevi, anasa, mavazi ya kikahaba, rushwa, usengenyaji n.k.(Waebrania 12:14) ubatizwe katika ubatizo sahihi kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako, ujazwe na Roho wa Mungu. Huko ndiko kufanikiwa kwa kwanza kwa mkristo ndipo mafanikio mengine ya mwilini yafuate.

Mungu akubariki sana.

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Tafadhali share ujumbe huu kwa wengine na Mungu atakubariki!.


Mada Nyinginezo:

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

DHAMBI YA MAUTI

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

BWANA ALIPOSEMA “SIKUJA KUTANGUA TORATI BALI KUITIMILIZA” ALIKUWA ANAMAANISHA NINI?

PAULO ALIMWAMBIA TIMOTHEO ATUMIE MVINYO KIDOGO KWA AJILI YA TUMBO LAKE, JE! TUNARUHUSIWA KUTUMIA POMBE?


Rudi Nyumbani:

Print this post

YONA: Mlango wa 3

Bwana wetu YESU KRISTO ahimidiwe milele na milele. AMEN.

Karibu tujifunze Neno la Mungu, leo tukiwa katika ile sura ya 3 ya kitabu cha Nabii Yona. Katika sura zilizotangulia tuliona jinsi taabu na dhiki alizopitia Yona zinafananishwa na dhiki watakazokuja kupitia wakristo waliovuguvugu (wanawali wapumbavu mathayo 25) watakaokosa unyakuo. Pia tuliona kama vile Yona alivyomezwa na Yule samaki mkubwa atokaye baharini na kukaa muda wa siku tatu katika lile tumbo, hawa nao watamezwa na Yule mnyama atokaye baharini mwenye vichwa 7 na pembe 10 (ambaye ni Mpinga-kristo na mfumo wake) kwa muda wa miaka mitatu na nusu katika ile dhiki kuu.(soma Ufunuo 13&17). Hivyo habari ya Yona ni unabii halisi wa mambo yatakayokuja kutokea mwishoni.

Lakini tukiendelea katika hii sura ya 3 tunasoma:

Yona 3 “Neno la Bwana likamjia Yona mara ya pili, kusema,

2 Ondoka, uende Ninawi, mji ule mkubwa; ukaihubiri habari nitakayokuamuru.

3 Basi Yona akaondoka, akaenda Ninawi, kama Bwana alivyonena. Basi Ninawi ulikuwa mji mkubwa mno, ukubwa wake mwendo wa siku tatu.

4 Yona akaanza kuuingia mji mwendo wa siku moja, akapaza sauti yake, akasema, BAADA YA SIKU AROBAINI NINAWI UTAANGAMIZWA.

5 Basi watu wa Ninawi WAKAMSADIKI MUNGU; WAKATANGAZA KUFUNGA, wakajivika nguo za magunia, tangu yeye aliye mkubwa hata aliye mdogo.

6 Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu.

7 Naye akapiga mbiu, akatangaza habari katika mji wa Ninawi, kwa amri ya mfalme na wakuu wake; kusema, Mwanadamu asionje kitu, wala mnyama wala makundi ya ng’ombe, wala makundi ya kondoo; wasile, wala wasinywe maji;

8 bali na wafunikwe nguo za magunia, mwanadamu na mnyama pia, nao wakamlilie Mungu kwa nguvu, naam, NAWAGEUKE, kila mtu AKAACHA NJIA YAKE MBAYA, na udhalimu ulio mikononi mwake.

9 Ni nani ajuaye kwamba Mungu hatageuka na kughairi, na kuiacha hasira yake kali, ili msiangamizwe?

10 MUNGU AKAONA MATENDO YAO, YA KUWA WAMEIACHA NJIA YAO MBAYA. Basi BAADA YA SIKU AROBAINIneno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende”.

Kama tunavyosoma habari hii baada ya Yona kutapikwa na yule samaki, Bwana alimtuma tena kwa mara ya pili Ninawi akawahubirie watu habari za Toba na kwamba wasipotubu baada ya siku 40, Ninawi itaangamizwa. Lakini tunaona watu wale walitii sauti ya Mungu na kutubu.

Lakini ni kitu gani kilichowafanya watubu kirahisi rahisi hivyo?.

Kumbuka kwa wakati ule Ninawi haikuwa na tofauti sana na mji wa Sodoma au Gomora, kwasababu ilikuwa yote ni miji ya kimataifa, watu wasiozijua sheria za Mungu wa mbinguni, ni mataifa yaliyoabudu maelfu ya miungu, yaliyojaa maovu ya kila namna, hivyo ingekuwa ni ngumu sana mtu kujizukia asiye na kitu na asiyejulikana na kuanza kuhubiri habari za kuteketezwa mji wao na mahubiri ya kubadilisha mtindo wa maisha yao. Hivyo ilihitajika kitu kingine cha ziada kuwashawishi wale watu waamini kuwa ni Mungu kweli wa mbinguni anazungumza na wao.

Hivyo Bwana kwa kulijua hilo akaruhusu Yona kwa makusudi akae katika tumbo la samaki siku tatu usiku na mchana bila kufa, kabla ya kwenda Ninawi. Pengine wale watu wa Ninawi walimuuliza Yona ni Ishara gani aliyonayo ili wasadiki kwamba ametumwa na Mungu wa mbinguni?. Na Yona akawasimulia ushuhuda wa maisha yake kwa muda wa siku tatu katika ule mji. Na pia mashuhuda wa jambo hilo walikuwepo, ambao ni wale mabaharia waliosafiri na Yona, ambao ndio baadaye walikuja kumtupa baharini, pengine baadaye walimwona ng’ambo ya pili akihubiri na kuwathibitishia watu kwamba ni kweli alikaa tumboni mwa samaki siku tatu. ndipo watu wa Ninawi wakaogopa sana, na kuchukua hatua ya kulia na kuomboleza juu ya dhambi zao, hivyo wakageuka na kuacha njia zao mbaya.

Vivyo hivyo hukumu ya Mungu ilipokaribia ya kuuteketeza ulimwengu wote tena, kwamba baada ya kipindi kisichokuwa kirefu kutokana na maovu ya watu ghadhabu ya Mungu itamwagwa juu ya ulimwengu mzima kama watu wasipotubu, Hivyo Mungu kwa kuwa ni wa rehema alianza kutanguliza kwanza manabii wake kuhubiri habari za TOBA kwa watu wote ambapo hapo kabla zilikuwa hazihubiriwi kama kiini cha wokovu, ndipo tunamwona Yohana mbatizaji akiwaonya watu watubu kwasababu hukumu ya Mungu imekaribia. Kadhalika na mwisho ya yote akamtuma nabii mfano wa Yona, mwenye ishara kama ya Yona, yamkini watu wa ulimwengu wakiiona hiyo WATUBU kama walivyofanya watu wa Ninawi lakini wasipotubu hukumu ya Mungu inakuja juu yao.

Ndipo Mungu akamtuma mwanae mpendwa Bwana Yesu ambaye kiini cha ujumbe wake kilikuwa ni TOBA ilioambata na ISHARA KUU. Tunasoma katika Mathayo 12:38 mafarisayo walio mfano wa watu wa Ninawi walimuuliza kwa ishara gani unatuonyesha tuamini kuwa hiyo hukumu inayokuja unayoizungumzia ni kweli, ili tupate kutubu…Tunasoma:

“38 Hapo baadhi ya waandishi na Mafarisayo wakamjibu, wakasema, Mwalimu, twataka kuona ishara kwako.

39 Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.

40 Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi.

41 Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona. “

Umeona hapo? hukumu ya huu ulimwengu ilishatamkwa siku nyingi, na Yona wetu ni Bwana Yesu Kristo kitendo cha kufa na kufufuka kwake haikuwa bure, baada ya kumaliza kazi yake hapa duniani angepaswa apae juu moja kwa moja kama Eliya au Henoko, lakini kizazi hichi kingesadiki vipi kama kisingepewa ISHARA KAMA HIYO?. Hivyo kitendo cha kufa kwake na kukaa siku tatu kaburini na kufufuka ni ishara tosha ya kumfanya kila mwanadamu atubu kwa kuvaa magunia na kuomboleza kama watu wa Ninawi na kuacha njia zake mbaya. Lakini Bwana Yesu alisikitika sana na kusema katika siku ya hukumu watu watakaokihukumu kizazi hiki watakuwa ni wale watu wa Ninawi, Jaribu kutafakari Yona hakufanya miujiza wala kuponya watu, zaidi ya ile ishara ya kumezwa na samaki lakini watu wa Ninawi walitubu, lakini sisi watu wa kizazi hiki tumeona Ishara nyingi za Yesu Kristo licha ya hiyo ya kufa na kufufuka kwake, kuna miujiza na uponyaji wa kiungu vinaambatana naye kila siku lakini bado watu hawataki kutubu. Alisema pia..

Mathayo 11: 20 “Ndipo akaanza kuikemea miji ile ambamo ndani yake ilifanyika miujiza yake iliyo mingi, KWA SABABU HAIKUTUBU.

21 Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, WANGALITUBU ZAMANI kwa kuvaa magunia na majivu.

22 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zao siku ya hukumu kuliko ninyi.

23 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.

24 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe”.

Na kumbuka pia watu wa Ninawi walipewa muda wa kutubu, nao ni siku 40, na si zaidi, baada ya hapo hakuna tena wokovu ghadhabu ikishamiminwa hakuna tena Toba. Vivyo hivyo na sisi tumewekewa muda wa kutubu, sio kila siku tutaliliwa Tubu! tubu! hapana, kuna muda utafika mlango wa neema utakuwa umefungwa, pale Bwana Yesu atakaposimama na kuufunga mlango.

Luka 13: 23 “Mtu mmoja akamwuliza, Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache? Akawaambia,

24 Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, EE BWANA, TUFUNGULIE; yeye atajibu na kuwaambia, SIWAJUI MTOKAKO;

26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.

28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje”.

Ndugu huu ulimwengu unakaribia kutimiza 40 zake, na dalili zote zinaonyeshwa huu ni wakati wa siku za mwisho, utafika wakati hutaisikia tena injili ya Toba, na hata ukisikia haitakufaidia chochote kilichobaki kwako ni siku ile ya hukumu kusimama mbele ya watu wa Ninawi wakikuhukumu kwanini hukutubu kwa Ishara kuu kama hizi, na zaidi ya yote utakutana na watu wa sodoma na Gomora nao pia watakuhukumu kwamba umestahili adhabu kubwa kuliko wao kwa kuwa uliona ishara nyingi na miujiza mingi kuliko wao na bado haukutubu. Siku hiyo yatakuwa ni maombolezo na majuto kiasi gani.Na siku hiyo inakaribia.

 

TUBU leo ndugu angali muda upo kumbuka Kutubu maana yake ni KUGEUKA na kuacha njia mbaya, sio kusali sala ya toba tu, halafu basi, ndio maana tunasoma pale Mungu aliyatazama MATENDO ya watu wa Ninawi kama kweli wamegeuka au la!! . na sio maombolezo yao peke yake na alipoona matendo yao wamegeuka alighahiri mabaya yale.,Na wewe fanya vivyo hivyo, Kristo bado hajaja, ila hivi karibuni anakuja kumnyakua yule aliyekuwa tayari kwenda nae.

Mungu akubariki.

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Kwa mwendelezo >>> YONA: Mlango wa 4


Mada Nyinginezo:

MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA.

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

CHUKIZO LA UHARIBIFU

SAUTI NYUMA YA ISHARA.

MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!

Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?


Rudi Nyumbani:

Print this post

YONA: Mlango wa 2

Jina la mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe.

Karibu katika mwendelezo wetu wa kitabu cha nabii Yona. Tukiwa katika sura ya pili, tulishaona katika sura iliyopita jinsi Yona alivyojitenga na mapenzi ya Mungu kwa kukataa kwenda katika njia zake, na kujikuta akingukia mambo mabaya badala ya mema kwa kumezwa na yule nyangumi mkubwa, na tukaona kuwa habari hiyo inafunua siri ya kanisa la Kristo katika wakati wa siku hizi za mwisho, kwa wale wakristo vuguvugu wa kanisa la mwisho la Laodikia ambalo ndilo tunaloliishi kuwa wataangukia katika tumbo la yule mnyama anayezungumziwa katika (Ufunuo 13&17) hapo itakuwa ni baada ya unyakuo kupita ambacho ndicho kile kipindi cha Dhiki kuu kitakachodumu kwa muda wa miaka mitatu na nusu ya mwisho.

Lakini tunaona katika sura hii ya pili baada ya Nabii Yona kumezwa, kilichofuata akiwa ndani ya lile tumbo la samaki ilikuwa ni mapambano akiishindania NAFSI yake, isiteketee kabisa ndani ya lile tumbo la yule samaki, tunasoma Yona alipitia kipindi kilichokuwa kifupi lakini kigumu sana, kiasi kwamba kilimfanya awe katika MAJUTO makubwa sana, na MAOMBOLEZO yasiyoelezeka… Tusome.

Mlango wa 2

1 Ndipo Yona akamwomba Bwana, Mungu wake, katika tumbo la yule samaki,

2 Akasema, Nalimlilia Bwana KWASABABU YA SHIDA YANGU, Naye akaniitikia; Katika tumbo la kuzimu NALIOMBA, Nawe ukasikia sauti yangu.

3 Maana ULINITUPA VILINDINI, Ndani ya moyo wa bahari; Gharika ya maji ikanizunguka pande zote; Mawimbi yako yote na gharika zako zote zimepita juu yangu.

4 Nami nikasema, Nimetupwa mbali na macho yako; Lakini nitatazama tena kukabili hekalu lako takatifu.

5 Maji yalinizunguka, hata nafsini mwangu; Vilindi vilinizunguka; MWANI ulikizinga kichwa changu;

6 NALISHUKA HATA PANDE ZA CHINI ZA MILIMA; HIYO NCHI NA MAPINGO YAKE YALINIFUNGA HATA MILELE; Lakini umeipandisha nafsi yangu kutoka shimoni, Ee Bwana, Mungu wangu,

7 Roho yangu ilipozimia ndani yangu, Nalimkumbuka Bwana; Maombi yangu yakakuwasilia, Katika hekalu lako takatifu.

8 WATU WAANGALIAO MAMBO YA UBATILI NA UONGO HUJENGA NA REHEMA ZAO WENYEWE;

9 Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani; Nitaziondoa nadhiri zangu. Wokovu hutoka kwa Bwana.

10 Bwana akasema na yule samaki, naye akamtapika Yona pwani.

Amen. Hapo tunaweza kuona ni jinsi gani Yona alipitia taabu sana, ni rahisi kuisoma kama habari tu, lakini jaribu kutafakari kwa kina uelewe ni mateso ya namna gani, mtu kukaa kwenye tumbo la kiumbe ambacho hakijui, na kibaya zaidi kipo baharini ingekuwa heri kama kingekuwa ni cha nchi kavu, Yona anasema alipelekwa mpaka katika moyo wa bahari katikati ya vilindi, kwenye baridi kali huko chini, jaribu kifikiria mazingira ya tumboni, biblia inasema yule samaki alikuwa anakula pia na magugu ya baharini(mwani), ambayo yalikuwa yanamsumbua sana kule tumboni, jenga picha ni shida kiasi gani, kumbuka tumboni hamna mwanga, hata hewa yenyewe tunajiuliza alikuwa anapataje pataje katika tumbo lile, alikuwa hali wala hanywi muda wa siku tatu usiku na mchana, na tunafahamu kuna kemikali maalumu za kumeng’enya chakula ambazo ni lazima ziwepo ndani ya matumbo ya wanyama, hivyo mambo hayo yote yalimpata Yona. Na zaidi ya yote alifahamu kabisa hayo yote yalimpata kwasababu ya upumbavu wake, na ndio maana alipokuwa analia na kuomboleza alisema.. “8 WATU WAANGALIAO MAMBO YA UBATILI NA UONGO HUJITENGA NA REHEMA ZAO WENYEWE;”. Yona alijitenga na Rehema zake mwenyewe na ndio maana yakampata mambo hayo,

Mfano kamili wa mambo yatakayokuja kulipata hili kanisa la mwisho tunaloishi, siku ile Unyakuo utakapokuwa umepita, Kumbukua watu watakaonyakuliwa watakuwa wachache sana na sio watu wote wa dunia watafahamu kama wengi wanavyodhania, kwasababu zitaonekana kuwa kama habari za kutunga machoni pa watu wengi, na pia hakutaonekana mabadiliko yoyote mbinguni wala duniani, wala hakutakuwa na maajali, au viashiria vyovyote kwamba unyakuo umepita kwasababu litakuwa ni kundi ndogo sana litakalonyakuliwa.

Watakaokuja kufahamu kuwa unyakuo umepita na wao wameachwa, ni wale wakristo wapumbavu ambao nao pia watakuwa wachache, Hawa ndio wale waliokuwa wanajua kabisa unabii wa siku za mwisho, wanafahamu kabisa kuwa Bwana wao yupo karibuni kurudi lakini hawakutaka kujiweka tayari (wapo vuguvugu) leo wanamwabudu Mungu, kesho wanatenda maovu, mfano wa wale wanawali 5 wapumbavu (Mathayo 25) ambao hawakubeba mafuta ya ziada pindi Bwana wao alipokuja awachukue waende karamuni Hivyo kundi hili ndilo litakalolia na kuomboleza mfano wa Yona. Kumbuka hawatukuwa waislamu, au watu wasiomjua Mungu, au wasiojua unabii wa biblia kuhusu habari za siku za mwisho (hawa watapokea chapa ya mnyama kwasababu hawafahamu chochote). Lakini Itakaye muhusu ni yule mkristo anayejua sana maandiko kama wewe unayesoma ujumbe huu na hautaki kugeuka, siku ile mpinga-kristo atatafuta watu wa namna hii ili awameze pale watakapojaribu kukataa mfumo wake(Chapa ya Mnyama).

Kama vile Yona alivyopitia dhiki kuu ndani ya lile tumbo kadhalika hawa nao watapitia dhiki isiyo ya kawaida kama Bwana alivyosema kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijawahi kutokea tangu ulimwengu kuwako na wala hatakaa iwako. Usidhani itakuwa ni rahisi kuikataa ile chapa, usidanganyike ni heri usiwepo hicho kipindi kwasababu hutasalimika, kumbuka hutaweza kuajiriwa, kujiajiri kuuza wala kununua bila hiyo chapa, sasa utakula nini usipoweza kununua wala kuuza!..na utajifichia wapi katika jamii ya leo ni dhahiri kuwa mwisho wa siku utashikwa tu,(maana ule mfumo wa mpinga-kristo utashirikiana na vyombo vya dola,) na kupelekwa katika magereza maalumu ya mateso, huko hutakufa leo wala kesho, leo hii hayo magereza yapo tayari, kwasababu ni kikundi kidogo tu kitakacho kamatwa wengine wote watakuwa wanamfurahia mpinga-kristo kama mtu wa amani aliyekuja kuwaondolea watu waovu na wavuruga amani miongoni mwao, wakati huo wanawali wapumbavu walioachwa watakuwa wanalia na kuomboleza kwenye matumbo ya yule mnyama.

KAMA ILIVYOKUWA KATIKA SIKU ZA NUHU:

Siku hizo Bwana alizifananisha na kama zile za Nuhu, kumbuka kabla ya gharika haijaja duniani, HENOKO aliyekuwa mtu wa SABA (7) baada ya Adamu, alinyakuliwa juu asione uharibifu biblia inasema hivyo. Na aliyepata ufunuo wa kuondoka kwa HENOKO alikuwa ni Nuhu pekee yake, hivyo akalazimika kuingia katika ile SAFINA ili aiponye nafsi yake katika mawimbi na misukosuko ya MAJI MENGI kabla ya pepo hazijaanza kuvuma na madirisha ya mbinguni kufunguka.

Vivyo hivyo Henoko anawakilisha watu wa kanisa la 7, ambalo ndilo la mwisho, wakristo waliojiweka tayari bikira safi watakaoenda na Bwana kwenye unyakuo. Hawa Bwana atawaepusha na ile dhiki inayokuja. Lakini Nuhu na familia yake akiwakilisha Wale wanawali waliosalia wasiokuwa werevu iliwabidi waingie kwenye ile NYAMBIZI(SAFINA),hivyo wakagharimika kupitia misukosuko ya mafuriko makubwa katikati ya vilindi vya maji kama tu Yona alivyopitia misukosuko katika tumbo la yule mnyama. Wengi tunadhani Nuhu na familia yake walikuwa wamestarehe kwenye safina wakipata raha, kuna raha gani! kukaa katika kijumba kile chenye giza kwa siku 150, huku mkirushwarushwa na tufani na mafuriko,radi na mingurumo huko nje?..Ni dhahiri kuwa hofu ya Mungu iliwaangukia, kila siku ilikuwa ni kulia na kuomboleza, yamkini Mungu asiwajumuishe pamoja na wale wengine katika adhabu ile.Kumbuka pia ile safina ilikuwa haielei tu muda wote, kutoka na tufani kubwa ilikuwa inazamishwa chini ya maji na kupandishwa juu, na ndio maana biblia inasema ilipigwa LAMI NDANI na NJE, ili maji yasipenye ndani. Kadhalika kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu ndivyo itakavyokuwa katika siku zetu, ni mmoja tu aliyeenda kwenye unyakuo ikifunua ni kundi dogo sana litakalonyakuliwa, na pia ni wachache tu waliostahimili misukosuko ambao ni watu 8 tu, ikifunua kuwa wataostahimili dhiki ya siku ile watakuwa ni watu wachache sana.

Hivyo ndugu usitamani uwepo kule, anza kuweka mambo yako sawa, hizo siku zimekaribia sana, ulimwenguni wote umeshadanganywa na shetani, ni kundi dogo la wakristo ndilo analolitafuta, na shabaha yake sio kukufanya uwe baridi la! bali ni kukufanya uwe vuguvugu na ndio tabia iliyotabiriwa kwa kanisa la LAODIKIA kwasababu anajua Bwana anamchukia zaidi mtu aliyevuguvugu kuliko aliye baridi kabisa. Tubu umgeukie Mungu, epuka ibada za sanamu, injili za mafanikio tu huku roho yako unaicha nyuma inaangamia zitakupoteza, acha mavazi ya kutokujisitiri hayo hayamfai kabisa bibi-arusi wa Kristo, tafuta utakatifu, ambao pasipo huo hakuna atakayemwona Mungu asipokuwa nao.Shika NENO la Mungu kwa kudumu katika mafundisho ya biblia tu.

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Pia washirikishe na wengine mambo haya.

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Kwa mwendelezo >>>> YONA: Mlango wa 3


Mada Nyinginezo:

MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

SIKU YA HASIRA YA BWANA.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

UAMSHO MKUU UMEKARIBIA!!


Rudi Nyumbani:

Print this post

YONA: Mlango 1

Yona alikuwa mmoja wa manabii wa Israeli wakati wa utawala wa Yeroboamu Mfalme wa Israeli, ambaye Mungu alimtumia sana kutoa unabii kadha wa kadha katika Israeli, kama tunavyomsoma katika (2Wafalme 14:21-25). Lakini ilifika wakati BWANA akataka kumtuma kwa watu wa Mataifa, Mji wa NINAWI uliokuwa mji mkuu wa Taifa la ASHURU ambalo kwa wakati ule lilikuwa ni moja ya ngome yenye nguvu duniani ndilo lililokuja baadaye kuhusika kuwachukua wana wa Israeli utumwani (2Wafalme 18:11), Mataifa mengine yakiwemo BABELI pamoja na MISRI. Kumbuka taifa la Ashuru liliyachukua yale makabila 10 na kuyapeleka Ashuru, na makabila mawili ya Israeli yaliyosalia (Yaani YUDA na BENYAMINI) Mfalme Nebukadneza, alikuja kuyachukua utumwani Babeli.

Hivyo mji wa NINAWI uliokuwa mji mkuu katika Ashuru ulijaa maovu mengi sana, mfano wa Sodoma na Gomora, mpaka kufikia wakati Bwana kutaka kuuangamiza mji wote na watu wote waliokuwepo kule, lakini Mungu alivyo wa rehema hawezi kufanya jambo lolote kabla hajawaonya kwanza watu wake, ili pengine waghahiri uovu wao wasiangamizwe, na ndivyo alivyofanya kwa kumtuma YONA nabii katika mji ule Mkubwa uliokuwa mbali sana na taifa la Israeli.

Lakini tunasoma habari haikuwa hivyo kwa nabii YONA, badala ya kwenda NINAWI mji wa ASHURU alioagizwa na Bwana, yeye akaamua kuubuni mji wake yeye alioupenda ili akakae huko, ndipo akakimbilia TARSHISHI mji uliokuwa nchi ya Lebanoni ili tu AJIEPUSHE NA MAPENZI YA MUNGU.

Lakini alisahau kuwa ili afikie malengo yake hana budi kupitia “NJIA YA BAHARI”.. Hivyo akaamua kupanda Merikebu zinazoelekea Tarshishi, Na kama tunavyosoma habari alipokuwa katikati ya safari yake bahari ilichafuka na mambo yakaanza kuharibika..

 
Yona 1: 4 “Lakini Bwana alituma upepo mkuu baharini, ikawa tufani kubwa baharini, hata merikebu ikawa karibu na kuvunjika.

5 Basi wale mabaharia wakaogopa, kila mtu akamwomba mungu wake; nao wakatupa baharini shehena iliyokuwa merikebuni, ili kuupunguza uzito wake. Lakini Yona alikuwa ameshuka hata pande za ndani za merikebu; akajilaza, akapata usingizi.

6 Basi nahodha akamwendea, akamwambia, Una nini, Ewe ulalaye usingizi? Amka, ukamwombe Mungu wako; labda Mungu huyo atatukumbuka, tusipotee.

7 Wakasemezana kila mtu na mwenzake, Haya, na mpige kura, mpate kujua mabaya haya yametupata kwa sababu ya nani. Basi wakapiga kura, nayo kura ikamwangukia Yona.

8 Ndipo wakamwambia, Tafadhali utuambie, wewe ambaye mabaya haya yametupata kwa sababu yako; kazi yako ni kazi gani? Nawe umetoka wapi? Nchi yako ni nchi ipi? Nawe u mtu wa kabila gani?

9 Akawaambia, Mimi ni Mwebrania; nami namcha Bwana, Mungu wa mbingu, aliyeziumba bahari na nchi kavu.

10 Ndipo watu wale wakaogopa mno, wakamwambia, Ni jambo gani hili ulilolitenda! Kwa maana watu wale walijua ya kuwa amekimbia, ajiepushe na uso wa Bwana, kwa sababu alikuwa amewajulisha.

11 Basi wakamwambia, Tukutende nini, ili bahari itulie? Kwa maana bahari ilikuwa inazidi kuchafuka.

12 Naye akawaambia, Nikamateni, mnitupe baharini; basi bahari itatulia; kwa maana najua ya kuwa ni kwa ajili yangu tufani hii imewapata.

13 Lakini wale watu wakavuta makasia kwa nguvu, ili wapate kurudi pwani, wasiweze; kwa maana bahari ilizidi kuwachafukia sana.

14 Basi wakamlilia Bwana, wakasema, Twakuomba, Ee Bwana, twakuomba, tusiangamie kwa ajili ya uhai wa mtu huyu, wala usitupatilize kwa ajili ya damu isiyo na hatia; kwa maana wewe, Bwana, umefanya kama ulivyopenda.

15 Basi wakamkamata Yona, wakamtupa baharini, nayo bahari ikaacha kuchafuka.

16 Ndipo wale watu wakamwogopa Bwana mno, wakamtolea Bwana sadaka, na kuweka nadhiri.

17 Bwana akaweka tayari samaki mkubwa ili ammeze Yona, naye Yona akawa ndani ya tumbo la samaki yule muda wa siku tatu, mchana na usiku”.

Basi wakamkamata  nabii Yona, wakamtupa baharini, nayo bahari ikaacha kuchafuka.

Bwana aliyaruhusu yote haya yampate YONA ili kutuonya sisi kwamba tusipotaka kuenda katika njia ambayo Mungu kaikusudia tuiendee,yatatukuta kama hayo hayo. Kama biblia inavyosema
 
1Wakoritho 10: 11 “Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ILI KUTUONYA SISI, tuliofikiliwa na miisho ya zamani. Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.”
 

SWALI NI JE! NJIA YA BAHARI NI SALAMA?

Kibiblia BAHARI inawakilisha nini?…Ili kufahamu jambo hili ni vizuri tujue ni kitu gani kimo humo ndani yake .tukisoma. 

Ufunuo 13: 1 “KISHA NIKAONA MNYAMA AKITOKA KATIKA BAHARI, mwenye pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru.

2 Na yule mnyama niliyemwona alikuwa mfano wa chui, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya dubu, na kinywa chake kama kinywa cha simba, yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi.”

Unaona hapo?.

Kumbuka YONA anawakilisha kundi la wakristo wasiotaka kudumu katika mapenzi ya Mungu (yaani VUGUVUGU).leo wanaenda na Mungu, kesho wanaenda katika akili zao, leo anafanya ibada kesho anakula rushwa. N.k. Sasa Kama vile  nabii YONA alivyokimbia uso wa Mungu na kuelekea njia ya BAHARINI na hatimaye kumezwa na yule SAMAKI MKUBWA, vivyo hivyo na kundi hili la wakristo wasiotaka kutengeneza mambo yao sasa vizuri na Mungu, hawajui kama wanakimbilia baharini pasipo wao kujua, ambapo kule kuna Yule mnyama mwenye vichwa saba na pembe kumbi ameandaliwa kuwameza.

Na bahari inawakilisha nini?

Tukirudi kusoma Ufunuo 17: 15 Kisha akaniambia, YALE MAJI ULIYOYAONA, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha.” Kumbuka huyu kahaba anayezungumziwa hapa ameketi juu ya Yule mnyama aliyetoka baharini ambaye tumemsoma katika Ufunuo 13.

Kwahiyo bahari au maji mengi inawakilisha mahali penye mkusanyiko wa watu wengi, hivyo Yule mnyama anatoka mahali penye mkusanyiko wa watu wengi, mahali ambapo amekubaliwa na wengi, tukizungumza katika roho leo hii mfumo wa mpinga-kristo unatenda kazi katikati ya mataifa, na dini nyingi za uongo.

Kama vile Yona alivyoiacha njia ya Mungu na kuchagua Njia ya BAHARI akidhani kuwa ni salama, vivyo hivyo na wakristo wa leo walio vuguvugu, wanamsahau Mungu na kushikimana na mambo maovu ya ulimwengu huu, nabii Yona alisinzia pale alipoona kuna utulivu mwanzoni mwa safari yake, kadhalika kundi hili la wakristo vuguvugu wanasinzia kwasababu wanajiona wapo salama, wanaona hata wakifanya hivyo hakuna dhara lolote wanatakalolipata lakini hawajui kuwa kuna mnyama ameshaandaliwa kwa ajili yao chini ya Merikebu yao. Pale PEPO zitakapovuma ndipo watakapotambua kwamba hawapo salama, wakati huo unyakuo umeshapita, ndugu unajiona upo salama katika ulimwengu, hata ukitenda dhambi unaona hakuna dhara lolote linalokupata, angali unafahamu kabisa moyoni mwako umeukimbia uso wa Mungu na unayoyafanya sio sahihi na bado unajiita Mkristo, hujui kwamba ni NEEMA ya Mungu tu, imekushikilia dhidi ya Yule Mnyama utubu, ugeuze njia uepuke madhara yaliyopo mbeleni ambayo yapo karibuni kuupata ulimwengu mzima. Ipo siku NEEMA inayokushikilia itakwisha na moja ya siku hizi PEPO ZITAANZA KUVUMA BAHARINI. Kama biblia inavyosema katika..

Danieli 7: 1 “Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza, mfalme wa Babeli, Danieli aliona ndoto, na maono ya kichwa chake, kitandani mwake; basi akaiandika ndoto, akatoa habari ya jumla ya mambo hayo.

2 Danieli akanena, akisema, Naliona katika maono yangu wakati wa usiku; na tazama, HIZO PEPO NNE ZA MBINGUNI ZILIVUMA KWA NGUVU JUU YA BAHARI KUBWA.

3 Ndipo wanyama wakubwa wanne wakatoka baharini, wote wa namna mbalimbali”………

Wanyama hao Nabii Danieli alionyeshwa, watatu wa kwanza walishapitia na Yule wa mwisho wanne, ndiye aliyeko sasa chini ya MERIKEBU(NEEMA), na moja ya hizi siku pepo zitamwamsha kutenda kazi tukiendelea kumsoma:

“7 Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama,MNYAMA WA NNE, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi, naye alikuwa na meno ya chuma, makubwa sana; alikula na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; na umbo lake lilikuwa mbali kabisa na wale wa kwanza, naye alikuwa na pembe kumi.

8 Nikaziangalia sana pembe zake, na tazama, pembe nyingine ikazukia kati yao, nayo ilikuwa ndogo, ambayo mbele yake pembe tatu katika zile za kwanza zikang’olewa kabisa; na tazama, katika pembe hiyo mlikuwa na macho kama macho ya mwanadamu, na kinywa kilichokuwa kikinena maneno makuu”.

Kama vile Nabii Yona alikaa ndani ya tumbo la samaki siku tatu usiku na mchana, kadhalika Huyu mnyama atokaye baharini atalimeza hili kundi la watu, kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu ndio kile kipindi cha dhiki kuu, mpinga-kristo atakaponyanyuka na kuanza kuleta dhiki isiyoelezeka kwa wale waliouvuguvugu kwa kuupenda ulimwengu huu, na kuiacha njia Mungu aliyowawekea wao waiendee.

Hichi kipindi kipo karibuni kutokea, Yule mnyama sasa anatenda kazi katika siri na watu wa Mungu wanasinzia hawaoni kuwa wapo katika hatari, wanadanganyika na utulivu uliopo sasa hivi kama vile nabii Yona alivyodhani lakini biblia inasema 

1Wathesalonike 5: 2 “Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile MWIVI ajavyo usiku. Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Ndugu usileweshwe na ulevi wa hii dunia hata kulala usingizi, Bwana yupo karibu kulichukua kanisa lake BIBI-ARUSI WA KWELI anayedumu katika Neno lake na UTAKATIFU, Na hatua za unyakuo zimeshaanza Bwana anawakusanya watu wake toka kila mahali, watu ambao macho yao yapo mbinguni, duniani wao ni kama wapitaji tu, hao ndio watakaofunuliwa siri za unyakuo lakini wengine wote ikiwemo wakristo vuguvugu, hawatajua lolote isipokuwa kumtazamia Yule mpinga-kristo mnyama atokaye baharini. Utajisikiaje siku ile wenzako wapo mbinguni kwenye KARAMU YA MWANA-KONDOO na wewe upo katika dhiki kuu na zaidi ya yote watakuja kutawala na Kristo milele na milele kama wafalme na makuhani wa Mungu na wewe upo kwenye ziwa la moto??. Ni vizuri utengeneze mambo yako sasa hivi kabla siku ile haijafika. Tubu ukabatizwe kwa Jina la BWANA YESU upate ondoleo la dhambi zako na uanze kuishia wokovu..

Mungu akubariki..

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Kwa mwendelezo >>> YONA: Mlango wa 2

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: MLANGO WA 13

UFUNUO: MLANGO WA 17

DANIELI: MLANGO WA 7

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA


Rudi Nyumbani:

Print this post

ESTA: Mlango wa 8, 9 & 10. (SIKU KUU YA PURIMU)

Jina la YESU KRISTO BWANA wetu lisifiwe.

Karibu kwenye mwendelezo wa kitabu cha Esta, leo tukiwa katika sura za mwisho, yapo mambo mengi ya kujifunza yahusuyo safari yetu ya ukristo tunapopitia kitabu hichi, tunaona mara baada ya Hamani adui wa watu wa Mungu kuuawa, Malkia Esta ananyanyuka tena kumwomba mfalme ayaondoe madhara aliyokusudia juu ya wayahudi wote waliandikiwa kuuawa, tunasoma;

Mlango 8

“ 1 Siku ile mfalme Ahasuero alimpa malkia Esta nyumba yake Hamani, yule adui ya Wayahudi. Mordekai naye akahudhuria mbele ya mfalme; kwa maana Esta alikuwa amedhihirisha alivyomhusu.

2 Basi mfalme akaivua pete yake, aliyompokonya Hamani, akampa Mordekai. Naye Esta akamweka Mordekai kuwa juu ya mlango wake Hamani.

3 Tena Esta akasema na mfalme mara ya pili, akaanguka miguuni pake, akamsihi kwa machozi ayaondoe madhara ya Hamani, Mwagagi, na shauri alilowafanyia Wayahudi.

4 Ndipo mfalme alipomnyoshea Esta fimbo yake ya dhahabu. Basi Esta akaondoka, akasimama mbele ya mfalme.

5 Akasema, Mfalme akiona vema, nami nikiwa nimepata kibali machoni pake, na neno likionekana jema mbele ya mfalme, nami nikimpendeza machoni pake, iandikwe kuzitangua barua za Hamani bin Hamedatha, Mwagagi, alizotunga na kuziandika ili kuwaangamiza Wayahudi walioko katika majimbo yote ya mfalme.

6 Kwa maana niwezeje kuyaona mabaya yatakayowajia watu wangu? Au niwezeje kuyatazama maangamizo ya jamaa zangu?

7 Mfalme Ahasuero akawaambia malkia Esta na Mordekai, Myahudi, kusema, Tazama, nimekwisha kumpa Esta nyumba yake Hamani, naye mwenyewe wamekwisha kumtundika juu ya mti, kwa sababu aliwatia mikono Wayahudi.

8 Basi waandikieni Wayahudi pia vyo vyote mpendavyo, kwa jina la mfalme, mkatie muhuri kwa pete ya mfalme; kwa kuwa andiko lililoandikwa kwa jina la mfalme na kutiwa muhuri kwa pete ya mfalme hakuna awezaye kulitangua.

9 Basi, waandishi wa mfalme wakaitwa pale pale, siku ya ishirini na tatu ya mwezi wa tatu, ndio mwezi wa Siwani; na kama vile Mordekai alivyoamuru, Wayahudi wakaandikiwa, pamoja na maakida na maliwali, na wakuu wa majimbo toka Bara Hindi mpaka Kushi, majimbo mia na ishirini na saba, kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake; na Wayahudi kwa mwandiko wao na kwa lugha yao”.

Kama tunavyosoma ule msiba mkuu na uchungu ambao ulikuwa juu ya wayahudi wote duniani Bwana aliugeuza na kuwa furaha na shangwe kwao, ile nyumba ya Hamani pamoja na cheo chake walipewa Mordekai na watu wake, wale walioonekana hawana heshima katikati ya mataifa Bwana aliwapa heshima kuliko jamii za watu wote duniani. wale walioonekana wadogo wakawa wakuu katikati ya mataifa. Biblia inasema kukawa nuru na furaha kwao;

Hata ile siku waliyopanga kuwaangamiza wayahudi wote tarehe 13 mwezi wa 12, ndio ikawa tarehe hiyo hiyo ya wayahudi wote duniani kuwaangamiza maadui zao waliowazunguka na kuwatawala. Hivyo tarehe 14. na 15 ya mwezi huo huo wa 12 wakaifanya kuwa sikukuu yao ya ushindi Bwana aliowapa dhidi ya maadui zao, wakaifanya kuwa sikukuu ya kupelekeana zawadi, pamoja na karamu na furaha waliyoiita sikukuu ya PURIMU.

Esta 8: 15 “Naye Mordekai akatoka usoni pa mfalme, amevaa mavazi ya kifalme, ya rangi ya samawi na nyeupe, mwenye taji kubwa ya dhahabu, na joho ya kitani safi na rangi ya zambarau. Mji wa Shushani wakapaza sauti, wakashangilia.

16 IKAWA NURU na FURAHA na SHANGWE na HESHIMA kwa Wayahudi.

17 Na katika kila jimbo, na kila mji, po pote palipowasili amri ya mfalme na mbiu yake, Wayahudi wakapata FURAHA, na SHANGWE, KARAMU na SIKUKUU. HATA WENGI WA WATU WA NCHI WAKAJIFANYA WAYAHUDI, KWA KUWA HOFU YA WAYAHUDI IMEWAANGUKIA. “

Hivyo Bwana akawapa wayahudi wote kustarehe na kufurahi siku zote za ufalme wa Ahasuero.

Kumbuka habari yoyote tunayoisoma katika agano la kale ni kivuli cha mambo yatakayokuja kutokea mbeleni. Wakati wote shetani alipojaribu kuwaletea mateso na dhiki watu wa Mungu, Bwana alitolea wokovu na ushindi mkuu kwao, tunasoma habari ya wana wa Israeli jinsi walivyopiganiwa na Bwana dhidi ya maadui zao walipokuwa wanatoka Misri, wakati wa-Misri walipoona njia pekee iliyosalia ni kuwateketezea katika zile kingo za bahari ya shamu, kinyume chake, wao ndio walioteketezwa katika ile habari, ikawa shangwe kwa wayahudi, huo ulikuwa ni mfano wa PURIMU kwao.

Vivyo hivyo na sehemu nyingine zote, tunaona wakati wa wafilisti walipokuja kupigana na Israeli, wakati wa akina Shedraki, Meshaka, na Abadnego walipotupwa katika tanuru la moto, wakati wa Danieli alipotupwa katika tundu la simba, n.k. hata kwa Bwana wetu Yesu, tunaona jambo lile lile shetani alijaribu kumuua akidhani ameshinda, lakini ufufuo ulidhihirisha ushindi wake, wote hawa maangamizi yao yaligeuka kuwa wokovu mkubwa kwao…ikawa kama mfano wa PURIMU kwao.

Vivyo hivyo katika siku za mwisho shetani anashindana na UZAO wa Mungu, yaani wayahudi wa mwilini na wayahudi wa rohoni (wakristo), kama alivyofanya katika siku za kale, kumbuka HAMANI ni mfano wa mpinga-kristo atakayekuja, na Esta ni mfano wa BIBI-ARUSI wa Kristo. Kama vile HAMANI alivyokusudia kuwaangamiza wayahudi wote duniani, isipokuwa Esta kwasababu yeye alikuwa ni malkia..Vivyo hivyo na mpinga-kristo atakapotafuta kuwaua wayahudi wote (wa-mwilini na wa-rohoni) hatoweza kwa BIBI-ARUSI wa Kristo kwasababu wakati huo atakuwa ameshakwenda katika unyakuo yupo kwenye Jumba la kifalme mbinguni mfano wa Esta. Hivyo hayo madhara hayatamkuta yeye.

Mpinga-kristo (ambaye atakuwa ni PAPA wa wakati huo), atakusudia kuundoa uzao wote wa Mungu duniani kwa njia ya hila, kwa kisingizio cha kuleta amani duniani kama Hamani alivyofanya kuwasingizia wayahudi kwamba wamefarakana na watu wote wa dunia nzima, jambo ambalo si kweli. Hivyo katika siku hizo wayahudi wote, na wale wakristo wote waliokuwa vuguvugu waliokosa unyakuo watagharimika kuingia katika ile dhiki kuu Bwana aliyoizungumzia.

Japokuwa mpinga-kristo atafanikiwa kuua watu wengi, lakini haitakuwa kwa wote, kwasababu biblia inasema wapo watakaofichwa mbali naye,(Ufunuo 12) mpaka siku ile MFALME WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA, YESU KRISTO Atakapokuja na mawingu pamoja na bibi-arusi wake, kuwaokoa wateule wake walioko duniani, na kila jicho litamwona, atakaposhuka na kukusanya watu wake(wayahudi) toka pembe nne za dunia, hapo ndipo mataifa yote yatakapoomboleza kwa maana atakuja na upanga kinywani mwake, kama vile maadui wa wayahudi walivyoomboleza siku yao ilipofika, mbele ya Mordekai na Esta ndivyo itakavyokuwa siku ile mbele ya Bwana Yesu na watakatifu wake. Mataifa yaliyowatesa watu wa Mungu yataomboleza sana mbele zake.

Ufunuo 19:11 “Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 NA MAJESHI YALIYO MBINGUNI WAKAMFUATA, WAMEPANDA FARASI WEUPE, NA KUVIKWA KITANI NZURI, NYEUPE, SAFI.

15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA”.

Umeona hapo, ukirudi kwenye..
 Mathayo 24: 29 inasema….; Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika;
30 ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi.
31 Naye atawatuma malaika zake pamoja na sauti kuu ya parapanda, nao watawakusanya wateule wake toka pepo nne, toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu”.

PURIMU KWA WATU WA MUNGU.

Katika sura ya tisa ya kitabu cha Esta, kama vile tulivyoona jinsi wayahudi walivyosheherekea sikukuu ya PURIMU baada ya ushindi dhidi ya maadui zao, mpaka wale wasiokuwa wayahudi walijifanya kuwa kama wayahudi, kadhalika na katika siku hizo mpinga-kristo na mifumo yake yote mibovu pamoja na mataifa yote yaliyosalia wataangamizwa kwa maangamizo makuu katika vita vya Har-Magedoni. Wakati huo wengi watatamani kuwa kama watu wa Mungu lakini haitawezekana tena, kwao itakuwa ni MSIBA mkuu, wakati huo watoto wa Mungu kwao itakuwa ni KARAMU ya PURIMU. Kufarijiwa na kuburudishwa milele, na kufutwa machozi. Pale watakapomwona BWANA wao uso kwa uso akija kuwapigania na kuleta utawala mpya wa AMANI wa miaka 1000 usio wa shida wala uchungu.

Ufunuo 19:17 “Kisha nikaona malaika mmoja amesimama katika jua; akalia kwa sauti kuu, akiwaambia ndege wote warukao katikati ya mbingu, Njoni mkutane KWA KARAMU YA MUNGU ILIYO KUU;

18 mpate kula nyama ya wafalme, na nyama ya majemadari, na nyama ya watu hodari, na nyama ya farasi na ya watu wawapandao, na nyama ya watu wote, waungwana kwa watumwa, wadogo kwa wakubwa.

19 Kisha nikamwona huyo mnyama, na wafalme wa nchi, na majeshi yao, wamekutana kufanya vita na yeye aketiye juu ya farasi yule, tena na majeshi yake.

20 Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wangali hai katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti;

21 NA WALE WALIOSALIA WALIUAWA KWA UPANGA WAKE YEYE ALIYEKETI JUU YA YULE FARASI, upanga utokao katika kinywa chake. Na ndege wote wakashiba kwa nyama zao.”

Unaona hapo ndugu hii roho ya mpinga-kristo ilishaanza kutenda kazi tangu zamani, na shabaha yake si kwa kila mtu duniani bali ni kwa wale walio uzao wa Mungu tu.Iliwauwa wakristo wengi wakati wa zama za giza zaidi ya milioni 68, Na chombo chake teule anachotumia na atakachokuja kutumia kuyalaghai mataifa yote ulimwenguni ni dini na madhehebu huku akihubiri injili yake bandia yenye kivuli cha amani lakini nia yake sio kuleta amani bali kuangamiza uzao mteule wa Mungu. Hivyo ndugu ni wakati wa kujitathimini, je! Wewe ni mfuasi wa kweli wa Kristo au mfuasi wa dini au dhehebu?, je! Wewe ni mtakatifu au vuguvugu,.je! unahuakika wa kwenda mbinguni au unahisi tu?. Je! Wewe ni bibi-arusi wa kweli kama Esta au kama Vashti. Jibu lipo moyoni mwako. Kumbuka ndani ya kanisa yapo magugu na ngano, wapo wanawali wapumbavu na werevu..Je! wewe ni yupi kati ya hayo?.

Bwana wetu yuaja.

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312


Mada Nyinginezo:

NIFANYE NINI ILI NIIKWEPE HUKUMU.

NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!

UPUMBAVU WA MUNGU.

JE! MUNGU ATAIANGAMIZA DUNIA TENA BAADA YA GHARIKA YA NUHU?

MANENO HAYA YANA MAANA GANI? “..KWA SABABU HAMTOI ROHO KWA KIPIMO. (YOHANA3:34)”


Rudi Nyumbani

Print this post

ESTA: Mlango wa 5, 6 & 7

Jina la mwokozi wetu YESU KRISTO litukuzwe.

Huu ni mwendelezo wa kitabu cha Esta. Katika sura hizi tatu (5,6 na 7), tunaona Malkia Esta akienda kijihudhurisha mbele ya mfalme kinyume cha taratibu ili awaombee watu wake dhidi ya adui wao Hamani aliyekusudia kuwaangamiza wayahudi wote waliokuwa dunia nzima. Lakini tunasoma badala ya Esta kuuliwa kinyume chake alipata kibali mbele ya mfalme kuwasilisha haja zake, na mfalme alipomuuliza Haja zake, Malkia Esta hakumweleza pale pale bali alimwalika kwanza kwenye karamu alizomwandalia, yeye na Hamani adui wa wayahudi. Tunasoma;

Esta 5: 2 “Ikawa, mfalme alipomwona malkia Esta amesimama uani, yeye akapata kibali machoni pake; naye mfalme akamnyoshea Esta fimbo ya dhahabu aliyokuwa nayo mkononi. Basi Esta akakaribia, akaigusa ncha ya fimbo.

3 Mfalme akamwambia, Malkia Esta, wataka nini? Nayo ni haja gani uliyo nayo? Utapewa hata nusu ya ufalme.

4 Esta akasema, Mfalme akiona vema, na aje leo, mfalme na Hamani, kwenye karamu niliyomwandalia.

5 Basi mfalme akasema, Mhimize Hamani, ili ifanyike kama Esta alivyosema. Hivyo mfalme na Hamani wakafika katika karamu ile aliyoiandaa Esta.”

Hivyo Mfalme alipofurahishwa sana na sherehe aliyoandaliwa na Malkia Esta, alirudia tena kumuuliza ni nini anachohitaji kufanyiwa?..Lakini Esta hakumweleza mfalme chochote badala yake alimwandalia karamu nyingine nzuri zaidi na kumwalika mfalme pamoja na Hamani. Na Mfalme alipokula na kunywa na kufurahi ndipo akamuuliza kwa mara nyingine tena Esta ni nini haja ya moyo wake. Tunasoma;

 

Esta 7:2-10 “

2 Mfalme akamwambia Esta tena siku ya pili pale pale penye karamu ya divai, Malkia Esta, dua yako ni nini? Nawe utapewa; na haja yako ni nini? Hata nusu ya ufalme utafanyiziwa.

3 Ndipo malkia Esta alipojibu, akasema, Mfalme, ikiwa nimepata kibali machoni pako, na mfalme akiona vema, nipewe maisha yangu kuwa dua yangu, na watu wangu kuwa haja yangu.

4 Maana tumeuzwa, mimi na watu wangu, ili tuharibiwe, na kuuawa, na kuangamia. Kama tungaliuzwa kuwa watumwa na wajakazi, ningalinyamaza; ila hata hivyo msiba wetu haulinganishwi na hasara ya mfalme.

5 Ndipo mfalme Ahasuero aliponena, akamwambia malkia Esta, Ni nani huyu, tena yuko wapi, ambaye moyoni mwake alithubutu kufanya hivi?

6 Esta akasema, Ni mtesi, tena ni adui, ndiye huyu Hamani, mtu mbaya kabisa. Mara Hamani akaingiwa na hofu mbele ya mfalme na malkia.

7 Mfalme akaondoka katika ghadhabu yake kutoka kwenye karamu ya divai, akaingia bustani ya ngome. Hamani naye akasimama ili ajitakie maisha yake kwa malkia Esta; kwa kuwa aliona ya kwamba amekusudiwa madhara na mfalme.

8 Kisha mfalme akarudi kutoka katika bustani ya ngome hata mahali pa karamu ya divai. Ikawa Hamani amejitupa chini penye kitanda alipokuwapo Esta. Mfalme akasema, Namna gani! Je! Atamfanyia malkia jeuri hata machoni pangu nyumbani mwangu? Na neno lilipotoka kinywani mwa mfalme, wakamfunika uso Hamani.

9 Ndipo aliposema Harbona, msimamizi-wa-nyumba mmojawapo wa wale waliohudhuria mbele ya mfalme, Tazama, basi, mti wa mikono hamsini urefu wake, Hamani aliomwekea tayari Mordekai, ambaye alinena vema kwa ajili ya mfalme, upo umesimamishwa nyumbani kwa Hamani. Mfalme akasema, Mtundikeni juu yake.

10 Basi wakamtundika Hamani juu ya mti aliomwekea tayari Mordekai. Ghadhabu ya mfalme ikatulia. ”

Esta kama mfano wa Bibi-arusi wa Kristo, habari yake inatufundisha jinsi ya kumwendea Mfalme wetu (ambaye ni Bwana YESU) pale tunapokuwa na mahitaji yetu. Tunamwona Esta japokuwa alikuwa na uchungu mkubwa na shida kubwa ndani ya moyo wake, hakukimbilia moja kwa moja kuzungumza haja zake, japokuwa mfalme alifahamu kuwa ana mahitaji fulani. Lakini alitumia Hekima kwa kuufurahisha kwanza moyo wa mfalme, kwa kumuandalia karamu mbili, za thamani nzuri. Ndipo baadaye afunue yaliyokuwa ndani ya moyo wake.

Vivyo hivyo na sisi tunapomwendea Mungu ni vizuri kumfanyia kitu kwanza kinachompendeza moyo wake, kama Esta alivyomfanyia mfalme, swali ni je! katika wingi wa maombi unayompelekea Mungu kila siku je! ulishawahi kumfanyia kitu kinachompendeza kwanza?. Mfano kujitolea kwa ajili ya kazi yake?, au kumtolea Sadaka nzuri katika mali zako? au kuwasaidia wahitaji na maskini au mayatima?, au kuwavuta watu kwa Mungu? au kwenda kuwatazama wagonjwa?hususani wakristo wenzako? kumtolea shukrani kwa kumsifu na kumwabudu kwa bidii? n.k…kisha ndipo upeleke mahitaji yaako?. Kumbuka biblia inasema Mungu anafahamu haja zetu hata kabla hatujamwomba, kama tu vile mfalme alivyokuwa anajua kuwa Esta ana haja kabla hata hajamwomba. Hivyo tunapoenda mbele za Mungu tujifunze kuanza kumwandalia “karamu” impendezayo kwanza, na ndipo tuwasilishe mahitaji yetu. Kama alivyofanya Nuhu baada ya kumtolea Mungu sadaka nzuri Bwana akaibariki tena nchi na kuahidi hataiangamiza tena kwa maji.

Jambo lingine tunaona pia Esta hakujiombea ufahari bali alijiombea uhai wake pamoja na ndugu zake wayahudi. Ndipo akapewa alivyoviomba na zaidi ya alivyoviomba. Na sisi pia tunapomwendea Mungu ni vizuri kutanguliza kuwaombea watu wa Mungu na kanisa la Kristo kwa ujumla, kwasababu hao ndio ndugu zako wa daima, shetani akilidhuru kanisa, nawe pia ni lazima udhurike. Mungu anapendezwa na watu wanamwendea kwa namna hiyo, mfano Danieli alipomwendea Mungu kwa ajili ya makosa yake na watu wake Israeli tunaona Mungu alimsikia. Hivyo hivyo hata Bwana wetu Yesu aliomba siku zote kwa ajili yetu sisi na si kwa ajili yake peke yake, kadhalika na sisi tunapaswa tuchukue madhaifu ya wengine. Ili na sisi Bwana ayachukue madhaifu yetu.Wagalatia 6: 2 Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.

Biblia .inasema pia Kisasi ni juu ya Mungu yeye mwenyewe atalipa. Tunaona yule Hamani mti aliouchonga kumtundika Mordekai mtu aliyekuwa na haki ndio uliomtundikia yeye mwenyewe. Cheo alichokuwa anajisifia mbele ya Mordekai ndicho alichopewa Mordekai, Heshima aliyotafuta kutoka kwa Mordekai ndiyo yeye mwenyewe aliyokuja kumpa Mordekai pale alipoambiwa na Mfalme amchukue na kumzungusha mjini,pale alipotaka kumwangamiza Mordekai na watu wake, Mungu akageuza uteka yeye ndiye aliyeangamizwa pamoja na watu wake.

Mthali 26: 27 Achimbaye shimo atatumbukia mwenyewe; Naye abingirishaye jiwe litamrudia.

Kadhalika dhambi atendayo mtu itamrudia mwenyewe wewe unayestarehe katika maisha ya dhambi na anasa, huku unajidhania unanawiri kwa kuwa na afya, mali, cheo au umaarufu, hujui kuwa uharibifu wako utakuja kwa ghafla ndani ya siku moja kama Hamani, leo hii unakejeli injili, unasema wokovu ni kwa watu waliokosa uelekeo wa maisha, biblia ni hadithi zilizotungwa na watu, hakuna mtu kuokoka duniani n.k. Injili inahubiriwa kila mahali lakini unabakia kuwa vile vile kwasababu mafanikio yako yanakudanganya fahamu kuwa utaanguka kama Hamani kama usipotubia uovu wako. Neno la Mungu linasema.

kufanikiwa kwa mpumbavu kutamwangamiza, ziwa la moto lipo halishibi kupokea watu..

Tubu umgeukie Bwana ukabatizwe katika ubatizo sahihi kwa jina lake YESU KRISTO upate ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Kwa mwendelezo >>>> ESTA: Mlango wa 8, 9 & 10. (SIKU KUU YA PURIMU)


 

Mada Nyinginezo:

SIKUKUU YA VIBANDA.

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

EPUKA KUTOA UDHURU.

FUVU LA KICHWA.

NJIA MUNGU ALIYOIWEKA KWA KILA JAMBO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

ESTA: Mlango wa 4

BWANA wetu YESU KRISTO atukuzwe.

Karibu katika uchambuzi wa kitabu cha Esta. Leo tukiwa katika sura ya 4, hivyo ni vizuri kama utapitia binafsi kwanza kusoma sura hii na zilizotangulia ili upate picha halisi iliyojificha katika kitabu hichi cha Esta kwa msaada wa Roho Mtakatifu.

Tunaona baada ya Hamani kutoa amri ya wayahudi wote kuuawa katika majimbo yote yaliyokuwa ulimwenguni, ambayo iliwafadhaisha sana wayahudi, na kumbuka hii ilikuwa ni sheria kwa umedi na Uajemi kwamba amri yoyote itakayopitishwa na mfalme isitanguke kwa namna yeyote ile, kama ilivyokuwa katika kipindi cha Danieli ilipotuolewa amri ya yeye kutupwa katika lile tundu la Simba, ilipaswa iwe hivyo hata mfalme mwenyewe alipotaka kujaribu kumwokoa Danieli haikuwezekana,

kwasababu ilikuwa ni sheria kwa Wamedi na Waajemi kwamba Amri yoyote itakayopitishwa na mfalme haiwezi kugeuzwa.

Hivyo kwa kuyafahamu hayo na Kwa tukio hilo Mordekai pamoja na Wayuhudi wote walilia sana na kuomboleza kama biblia inavyosema.

Esta 4: 1 “Basi Mordekai alipojua mambo yote yaliyofanyika, alizirarua nguo zake, akajivika gunia pamoja na majivu, akatoka hata kufika katikati ya mji, akalia kwa sauti kuu ya uchungu.

2 Pia akafika hata mbele ya mlango wa mfalme; maana hakuna awezaye kuingia ndani ya mlango wa mfalme hali amevaa magunia.

3 Na katika kila jimbo, ambako amri ya mfalme na mbiu yake imewasili, palikuwako msiba mkuu kwa Wayahudi, na kufunga, na kulia, na kuomboleza; hata na wengi wakalala juu ya gunia na majivu.”

Hivyo Mordekai akaona mlango pekee wanaoweza kuutumia kutafuta ukombozi wao ni kwa kupitia Malkia Esta, Ndipo akamweleza Esta mambo yote Hamani aliyoyapanga dhidi ya wayahudi wote, na kumsihi akamwombe mfalme ili aweze kugeuze shauri hilo. Lakini jibu la Esta lilikuwa ni tofauti alimwambia hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia katika Ua wa mfalme pasipo kuitwa, na kwamba yeyote atakaye kwenda kinyume na amri hiyo ilikuwa ni kifo.

Esta 4: 10 “Ndipo Esta akasema na Hathaki, akamtuma tena kwa Mordekai, kusema,

11 Watumwa wote wa mfalme wanajua sana, hata na watu wa majimbo ya mfalme, ya kwamba mtu ye yote, akiwa mwanamume au mwanamke, atakayemjia mfalme katika ua wa ndani, wala hakuitwa, kuna sheria moja kwake, ni kwamba auawe; isipokuwa yeye ambaye mfalme atamnyoshea fimbo ya dhahabu, ili aishi; wala mimi sikuitwa niingie kwa mfalme yapata siku thelathini”.

Lakini tunasoma Mordekai alizidi kumsisitiza Esta na kumwambia: 14 “Kwa maana wewe ukinyamaza kabisa wakati huu, ndipo kutakapowatokea Wayahudi msaada na wokovu kwa njia nyingine; ila wewe utaangamia pamoja na mlango wote wa baba yako; WALAKINI NI NANI AJUAYE KAMA WEWE HUKUUJIA UFALME KWA AJILI YA WAKATI KAMA HUO?.

Na ndipo malkia Esta tunasoma akachukua hatua ya kwenda kumuona mfalme kinyume na sheria, lakini kabla ya kufanya hivyo aliwaamuru wayahudi wote wafunge siku tatu kwa ajili yake ili apate kibali cha kusikilizwa. Na tunasoma alipozimaliza zile siku na kwenda kwa mfalme, Mungu alimpa kibali mbele ya mfalme na badala ya kufa alipata kibali kikubwa zaidi kufikia hata kuahidiwa kupewa nusu ya ufalme wa mfalme kama angetaka.

Tunajifunza nini hapo? Esta anayesimama kama Bibi-Arusi wa Kristo, alidhubutu kuhatarisha hata maisha yake kwa ajili ya wokovu wa ndugu zake, hii inatufundisha na sisi wakristo kujitoa kwa ajili ya wokovu wa watu wengine pasipo kujali ni mambo mangapi tutakayoyapoteza kwa kufanya hivyo, Esta alikuwa tayari kupoteza maisha yake, Lakini Bwana Yesu anasema Mathayo 10: 39 “Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”. Mungu ni mwema japo Esta aliyahatarisha maisha yake lakini mwisho wa siku aliyapata kwasababu alifanya hivyo kwa ajili ya ndugu zake.

Kadhalika na sisi tunaojiita bibi-arusi katika nafasi za kiroho Mungu alizotuweka na katika mahali popote tulipo tunapaswa tuwe mashahidi waaminifu wa Kristo pasipo kujali madhara yatakayotukuta, tuwalete watu kwa Kristo ili watoke katika mitego ya mauti ya shetani. Shetani ni mfano wa Hamani amewakusudia mabaya watu wa Mungu, lakini ni nani aliyetayari kujitoa kwa ajili yao? Bila shaka ni wewe uliyepewa hii neema na Bwana ya kumjua yeye.

Mordekai alimwambia Esta “WALAKINI NI NANI AJUAYE KAMA WEWE HUKUUJIA UFALME KWA AJILI YA WAKATI KAMA HUU?”.Vivyo hivyo katika nafasi uliyopo wewe iwe ni katika kanisa, familia, jamii, ofisi, madaraka, uongozi n.k. popote pale , ni nani ajuaye kuwa Mungu kakuweka mahali hapo kwa wakati kama huo kwa ajili ya wokovu wa watu wake?.(nazungumza na wewe uliye mkristo)

Anza kufanya hivyo uone kama hautapa kibali mbele za Mungu, pale ambapo unaona kama ukijaribu kufanya hivyo utapoteza kazi yako, au heshima yako, fahamu tu pale unapomuheshimu Mungu, Mungu naye atakuheshimu na kukutokezea njia pale pasipokuwa na njia., anza leo kuwa shahidi wa Kristo, wahurumie watu wake kwa jinsi wanavyoangamia, naye atakukirimia.

Chochote Mungu alichokupa nacho uwezo kitumie kwa Bwana kwa ajili ya injili, iwe ni cheo, iwe ni mali, iwe ni ujuzi, iwe ni elimu, iwe ni umashuhuri, iwe ni ukubwa, iwe ni kipaji, iwe ni ujana, iwe ni muda, vitumie kwa BWANA maana ni nani ajuaye kuwa umepewa hayo kwa wakati kama huu ili watu wa Mungu waokolewe?.

Unaweza ukasema mahali nilipo hapastahili mkristo kuwepo hapo au hapastahili kufanyia kazi ya Mungu, lakini ni nani ajuaye Mungu kakuweka hapo kwa kusudi maalumu la kuwaokoa watu kwake?. Kumbuka hata Esta mahali alipokuwepo sio kwamba palikuwa ni sehemu nzuri sana inayompendeza Mungu, hapana Torati yao ilishakataza kwa myahudi yoyote kutoa binti yake na kuolewa na watu wa mataifa (watu wasio wayahudi), ni machukizo mbele za Mungu. Lakini ilipotokea kwa Esta ni nani ajuaye ilikuwa vile kwa ajili ya ukombozi wa watu wa Mungu baadaye?.

Hivyo ndugu popote ulipo fanya kitu kwa Mungu, naye atakupa kibali chema.

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Kwa mwendelezo >>> ESTA: Mlango wa 5, 6 & 7

Mada Nyinginezo:

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU.

RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO.

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

SAYUNI NI NINI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

ESTA: Mlango wa 3

Jina la Bwana wetu YESU KRISTO aliye mkuu wa uzima wote litukuzwe.

Karibu katika kujifunza NENO la Mungu ili tukue toka utukufu hata utukufu mpaka tutakapofikia kile kilele cha kumjua sana huyu mwokozi wetu Yesu. Leo tukiendelea na ile sura ya 3 ni vizuri ukaipitia habari hii kwanza peke yako katika biblia ndipo tuende pamoja.

Kwa maelezo mafupi kitabu hichi kinaelezea unabii wa mambo yatakayokuja kutokea baadaye licha ya kwamba tunaisoma kama hadhithi iliyo nyepesi kuielewa lakini ndani yake imebeba maana kubwa zaidi ambayo kila mkristo ni vema akaifahamu kwa haya majira tunayoishi, kwa mfano laiti ile historia ya YONA ingeeleweka machoni pa watu wengi kwa wakati ule kwamba sio tu ilikuwa ni hadithi ya Yona kutokutii maagizo ya BWANA, bali pia ilikuwa inamwelezea Bwana wetu Yesu kufa na kufufuka kwake, kuwa atakuja kukaa siku tatu kaburini kama vile Yona alivyokaa siku tatu usiku na mchana katika tumbo la samaki. Unaona Hivyo hadithi hizi zote zinaelezea unabii wa mambo yanayokuja kutokea mbeleni na ndivyo ilivyo hata katika kitabu hichi cha Esta.

Katika sura ya 3 tunasoma habari ya HAMANI ambaye alikuja kupandishwa cheo na mfalme Ahasuero na kuwa juu ya maakida wote waliokuwa katika ufalme wake uliotawala dunia nzima, (Esta 3:1-2) Alitukuzwa sana kiasi kwamba watu wote waliokuwa chini yake waliamiriwa wamsujudie, Lakini tunasoma haikuwa hivyo kwa watu wote, alionekana mtu mmoja myahudi aliyeitwa Mordekai alikataa kuanguka chini yake na kumpa heshima yake. Na habari ilipomfikia Hamani alikasirika sana, na alipomjaribu tena aone kama atamwangukia amsujudie kama wale wengine wanavyofanya, msimamo wa Mordekai ulikuwa ni ule ule hakudhubutu kumsujudia..Hivyo Hamani tunasoma alizidi kuchukia zaidi akaona si shani kumwangamiza Mordekai peke yake bali hata na watu wake wote (yaani WAYAHUDI).

Esta 3:2 “Nao watumishi wote wa mfalme, walioketi mlangoni pa mfalme, wakainama na kumsujudia Hamani, maana ndivyo alivyoamuru mfalme kwa habari zake. Bali Mordekai hakuinama, wala kumsujudia.
3 Basi watumishi wa mfalme walioketi mlangoni pa mfalme wakamwambia Mordekai, Mbona wewe waihalifu amri ya mfalme?

Lakini swali la kujiuliza ni hili; kwanini Mordekai aliyahalifu maagizo ya mfalme juu ya kusujudiwa kwa Hamani angali tunamsoma Mordekai alikuwa ni mtu mkamilifu aliyemuheshimu mfalme na kumtii?. Kumbuka neno kusujudia linavyotumika hapo sio kumsujudia kama Mungu bali ni kuanguka na kumpa Heshima yake kama mkuu wa nchi, ni kama tu vile kwasasa mahali ambapo Raisi anapita watu wote mnapaswa kusimama ili kumpa heshima yake, ndivyo Mordekai alivyokuwa anafanya kwa mfalme na kwa wakuu wote waliokuwa juu yake..lakini haikuwa hivyo kwa Hamani yeye alienda kinyume na wengine, hakumsujudia.

Ni dhahiri kuwa kuna jambo Mordekai aliliona ndani ya HAMANI ambalo sio sawa na ndio maana hakumpa Heshima yake. Biblia haijaeleza moja kwa moja ni mambo mangapi aliyaona kwa yule mtu. Lakini tukichunguza biblia tunaweza tukapata dondoo za kwanini Mordekai asimuheshimu HAMANI kama wakuu wengine wa Uajemi.

Tukirejea nyuma kidogo katika ile ya sura ya pili mwishoni tunaona kulikuwa na watu wawili waliotaka kumfanyia hila mfalme Ahausero na kutaka kumuua. (Esta 2:21-23). Lakini Mordekai alipogundua ya kwamba madhara yamepangwa kinyume cha Mfalme alikwenda kumuarifu jambo hilo na wale watu wakauliwa. Hivyo tukichunguza tunaona kuwa katika ule utawala fitna nyingi zilikuwa zinapangwa dhidi ya mfalme na ufalme wake. Na Mordekai kwasasa tunaweza kusema alikuwa ni mtu wa USALAMA,

Hivyo alichunguza mambo yote waliyokuwa yanaendelea kwa siri pasipo hata wakuu wengine kujua. Hivyo kitendo cha kutokumpa heshima HAMANI ni kwasababu aliziona HILA zake mbaya tokea mbali. Pengine hata wale watu waliotaka kumuua mfalme walikuwa na mahusiano ya karibu na Hamani. Na Mordekai kwa kutokupenda UNAFKI alidhihirisha moja kwa moja kuwa huyu mtu hastahili heshima ya ukuu japokuwa amri imetoka kwa mfalme watu wote wamwangukie.

Lakini tunavyozidi kuendelea kusoma tunakuja kuona jinsi Hamani alivyoomba kibali cha Mfalme kuwateketeza hata watu wasiokuwa na hatia (WAYAHUDI). Aliwachukia mpaka akatenga siku rasmi kuwaangamiza wayahudi wote walioko duniani. Mpaka biblia inamtaja kama “Adui wa wayahudi”. Na japokuwa ni mfalme mwenyewe aliyemnyanyua lakini alikuja kuwa adui hata wa mfalme kwa kujaribu kuwaangamiza ndugu wa mke wake (Malkia Esta). Lakini utawala wake wa hila haukudumu kwa muda mrefu tutakuja kuona mbeleni tunavyozidi kusoma..

Habari hii inatoa picha halisi ya mambo yatakayokuja kutokea katika siku za mwisho. Kumbuka moja ya siku hizi atanyanyuka MFALME ambaye Mungu atamruhusu atende kazi kwa kipindi kifupi.

Tukisoma Ufunuo 13:5-7 ” 5 Naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya makufuru. AKAPEWA UWEZO wa kufanya kazi yake MIEZI AROBAINI NA MIWILI.

6 Akafunua kinywa chake amtukane Mungu, na kulitukana jina lake, na maskani yake, nao wakaao mbinguni.

7 Tena AKAPEWA KUFANYA VITA NA WATAKATIFU na kuwashinda, AKAPEWA UWEZO JUU YA KILA KABILA NA JAMAA NA LUGHA NA TAIFA. “

Hamani ni mfano wa mpinga-kristo atakayeanza kufanya kazi moja ya siku hizi. Yeye alipewa amri kutoka kwa mfalme ahausero naye huyu vivyo hivyo atapewa uwezo kutoka kwa Mungu mwenyewe kutawala dunia kama biblia inavyosema. Na kama vile watu wote wa dunia nzima walimsujudia Hamani isipokuwa Mordekai peke yake. Vivyo hivyo mpinga-kristo atasujudiwa na watu wote wa dunia nzima pale atakapoanza kutenda kazi yake isipokuwa kikundi cha watu wachache sana watakaomdhihirisha maovu yake (miongoni mwao watakuwepo wale mashahidi wawili wa ufunuo 11, pamoja na wale wayahudi 144,000 watakaotiwa muhuri na Mungu katika Ufunuo 7&14.) kumbuka wakati huo kanisa litakuwa limeshanyakuliwa.

Jambo lile lile lililotokea kwa Hamani la kumchukia Mordekai kisa tu hajapendezwa naye na kukusudia kumwangamiza yeye pamoja na watu wake wote (wayahudi), vivyo hivyo MPINGA-KRISTO naye atawaghadhibikia wale MASHAHIDI WAWILI pamoja na wale 144000 na kutaka kuwaua na sio wao tu..bali mpaka wayahudi wengine waliozagaa duniani kote na baadhi ya masalia ya wakristo waliokosa unyakuo. Wote hawa atatafuta kuwaua kwa bidii (Ufunuo 12).

Wale mashahidi wawili wa ufunuo 11 watamhubiri kuwa huyu mfalme anayejitukuza sasa kana kwamba yeye ni Mungu sio rafiki wa Mungu bali ni MPINGA-KRISTO aliyetabiriwa, na watu waache kumwabudu wamgeukia Mungu wa mbinguni, wakithibitisha hilo kwa zile Ishara na yale mapigo yaliyoandikwa kule. Hivyo mpinga-kristo (PAPA kwa wakati huo) ataghadhibika sana na kufanya vita nao. Na kwasababu atakuwa ana nguvu duniani kote, atatoa amri kuundwe ustaarabu mpya wa dunia (NEW WORLD ORDER). Kwa kisingizio cha kuleta amani duniani lakini nia yake sio hiyo bali ni kuwakamata na kuwauwa watu wote watakaenda kinyume na uongozi wake na hawa watakuwa si wengine zaidi ya wayahudi na masalia ya waliokosa unyakuo. kama vile HAMANI alivyofanya.

Kumbuka sio watu wote watajua kuwa ni kiongozi mbaya kama vile Hamani sio watu wote waliojua kuwa ni kiongozi mbaya wengi walijua amepewa heshima na mfalme mpaka mwishoni kabisa walipokuja kujua kumbe alikuwa ni adui wa mfalme pia.

Vivyo hivyo na huyu MPINGA-KRISTO hatajulikana na watu wote, wengi watamwona kama kateuliwa na Mungu kama tu kivuli cha huyu wa sasa watu wasivyoweza kuona ni roho gani iliyopo ndani yake. Biblia inasema watu ambao hawakuandikwa majina yao tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu ndio watakaomsujudia (Ufunuo 17:8). Pale atakapotaka kukaa katika Hekalu la Mungu na kutaka kuabudiwa kama Mungu (2Thesalonike 2).

Hivyo atakuja kwa kivuli cha AMANI, na kuunda chapa yake itakayomtambulisha kila mtu IMANI yake. Vitu kama Micro-chips,lDS, N.k vitatumika kutakuwa hakuna “kujiajiri wala kuajiriwa” bila kuwa na vitambulisho maalumu, hivi vitatumika kutambulisha Dini/ dhehebu lililosajiliwa na UMOJA WAKE ALIOUUNDA (Ekumene). Kumbuka usajili huu hautakwepeka mahali popote usipokuwepo kwenye kitambulisho cha taifa utakutana nao kwenye leseni ya biashara au kitambulisho cha kazi au leseni au ATM card ..Hivyo lile neno hakuna atakayeweza kuuza wala kununua litatimia kwa namna hiyo. Sasa kwa wale ambao watakataa kupokea utambulisho wake ndio watakaopitia DHIKI ambayo haijawahi kuwepo.

Unaona hii roho ya shetani inavyojirudia rudia..ilianzia kwenye utawala wa Babeli wakati wa akina shedraki, Meshaki na Abednego, walipolazimishwa kuabudu ile sanamu, ukaja katika huu utawala wa Uajemi na Umedi, Hamani anataka kuwateketeza tena wayahudi, Ilitokea pia katika utawala wa Uyunani Antiokia IV Epifane alipowauwa baadhi ya wayahudi na kuwaondolea sadaka ya kuteketezwa ya daima. Na utawala wa mwisho ambao ni RUMI ndio uliopo sasa uliohusika kwa mauaji mengi ya wakristo waaminifu kwa Mungu zaidi ya milioni 68. Umetabiriwa utapata nguvu tena katika siku hizi za mwisho utahusika na mauaji makubwa ambayo biblia inasema haijawahi kutokea mfano wake.

Hivyo ndugu majira haya sio ya kuchezea kabisa Bwana yupo mlangoni kurudi, kulinyakuwa kanisa lake, na siku atakapolinyakua watakaojua ni bibi-arusi tu, lakini wengine haitajulikana kwao. Je! umejiwekaje tayari, Bwana akirudi leo utasema sijasikia?. Mtafute Muumba wako angali muda unao tubu weka mbali uasherati, ibada za sanamu, nguo zisizo na maadili, ulevi, usengenyaji n.k. ukabatizwe upate ondoleo la dhambi zako. Umwishie Mungu ili uwe na uhakika wa maisha yako ya milele.

Ubaikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Kwa mwendelezo >>>  ESTA: Mlango wa 4

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: MLANGO WA 14

CHAPA YA MNYAMA.

DANIELI: MLANGO WA 7

NINI MAANA YA ELOHIMU?

WALE MANABII 400 WALIOMTABIRIA MFALME AHABU WAKATI WA MIKAYA WALIKUWA NI MANABII WA MUNGU KWELI?

JE! NI SAHIHI KWA MKRISTO KUOA/KUOLEWA NA MTU WA IMANI NYINGINE?


Rudi Nyumbani:

Print this post

ESTA: Mlango wa 1 & 2

MFALME wa WAFALME YESU KRISTO Bwana wetu, atukuzwe daima

Karibu kwa neema za Mungu tujifunze kitabu cha Esta leo tukianza na ile sura ya 1 na ya 2.Ni vizuri ukiwa na biblia yako pembeni uipitie habari hii kwanza ndipo tuende pamoja. Kama tunavyofahamu Agano la Kale ni kivuli cha Agano jipya hivyo kila habari inayozungumzwa katika agano la kale, inafunua jambo fulani linaloendelea katika roho kwa wakati tunaoishi sasa.

Kitabu hiki kwa ufupi kinaelezea habari ya Mfalme Ahasuero wa Ufalme wa Umedi & Uajemi aliyekuwa tajiri sana na mwenye nguvu ni mfalme aliyetawala mataifa 127, biblia inasema kuanzia India mpaka taifa la Kushi (Ethiopia), kote huku alimiliki na kwa wakati ule alikuwa ni kama Mfalme wa dunia. Kwasababu Umedi na Uajemi ndio zilikuwa zinatawala dunia kwa wakati huo.

Hivyo ilifika wakati mfalme Ahasuero aliandaa sherehe kubwa sana kwa wakuu wake wote, pamoja na watu wote waliokuwapo katika mji wake (huko Shushani ngomeni), wakubwa kwa wadogo walihudhuria, watu walikula na kunywa jinsi wapendavyo, na kwa fahari yake aliamua kumuwasilisha malkia aitwaye VASHTI, mbele za wakuu wote wauone uzuri wake, maana biblia inasema Vashti alikuwa ni mzuri sana wa uso, kwasababu hata tafsiri ya jina Vashti linamaanisha “mwanamke mzuri”.

Lakini mambo hayakuwa kama yalivyotarajiwa, Badala ya Vashti kumtii mume wake, na zaidi ya yote alikuwa ni MFALME, alikaidi amri ile kwa KIBURI cha Uzuri wake na kuamua kutokwenda, Jambo hili lilionekana kuwa ni aibu kubwa kwa Uajemi yote, kwasababu hakukuwa na desturi ya mwanamke kumvunjia heshima mfalme, Na tunasoma Vashti alikuja kuvuliwa umalkia wake na kutafutwa mwengine “ALIYE MWEMA KULIKO YEYE”.

 

Esta 1:19 “Basi mfalme akiona vema, na itoke kwake amri ya kifalme, nayo iandikwe katika sheria za Waajemi na Wamedi isitanguke, ya kwamba Vashti asifike tena mbele ya mfalme Ahasuero; na umalkia wake mfalme ampe mwingine aliye mwema kuliko yeye.”

Hivyo moja kwa moja, ikaanza kupangwa mipango ya kumtafuta malkia mwingine mahali pa Vashti, mbiu zikapigwa katika mataifa yote duniani (127) aliyokuwa anayamiliki, walikuja MABIKIRA vijana wengi na ESTA alikuwa mmoja wapo. Kumbuka wote hawa walitokea katika machimbuko tofauti tofauti, wengine katika familia za kitajiri, wengine katika koo za kifalme, wengine walikuwa mabinti za maakida, wengine familia za kisomi, wengine familia za mabinti warembo n.k. Kwahiyo walikusanyika wengi sana pengine mabinti 30,000 au zaidi.

Lakini tukiendelea kusoma habari tunaona kwamba kila mmoja alipewa uhuru wa kujipamba kwa jinsi atakavyo, apewe chakula atakacho, au lolote atakalolitaka apewe ili tu siku atakapopelekwa mbele ya mfalme Ahasuero isionekane kasoro yoyote kama walivyofanyiwa wakina Danieli, Shedraka, Meshaki na Abednego mbele ya mfalme Nebukadreza. Hivyo mabikira wote na Esta akiwa miongoni mwao waliwekwa chini ya msimamizi mmoja wa nyumba ya mfalme Ahasuero aliyeitwa “HEGAI”.

Kazi ya huyu HEGAI ilikuwa ni kuhakikisha kuwa anawahudumia na kuwapa mahitaji yao kwa jinsi watakavyo. Tukisoma;

 

Esta 2:1-4 “ 1 Baada ya hayo, hasira yake mfalme Ahasuero ilipotulia, alimkumbuka Vashti, na vile alivyotenda, na yale yaliyoamriwa juu yake.

2 Basi watumishi wa mfalme waliomhudumu walimwambia, Mfalme na atafutiwe mabikira vijana wazuri;

3 naye mfalme aweke wasimamizi katika majimbo yote ya ufalme wake, ili wakusanye pamoja mabikira vijana wazuri wote waende Shushani ngomeni, kwenye nyumba ya wanawake mikononi mwa HEGAI, MSIMAMIZI-WA-NYUMBA WA MFALME, mwenye kuwalinda wanawake; tena wapewe VIFAA VYA UTAKASO.

4 Naye yule msichana atakayempendeza mfalme na awe malkia badala ya Vashti. Neno hilo likampendeza mfalme, naye akafanya hivyo.”

 

LAKINI NI SIRI IPI ILIYOMFANYA ESTA AKUBALIKE KULIKO MABIKIRA WENGINE?.

Biblia haimtaji Esta kama alikuwa ni mwanamke mzuri kuliko wote waliohudhuria, hapana biblia inasema alikuwa na Uso mwema tu, wala hakutokea katika familia ya kitajiri kama wenzake, wala hakuwa na elimu kama wale wengine pengine ingekuwa chachu ya kumfanya mfalme Ahasuero avutiwe naye lakini vyote hivyo hakuwa navyo. Bali kuna jambo lingine lililomfanya mfalme avutiwe naye. Na hili tunalipata kwa HEGAI, YULE MSIMAMIZI WA NYUMBA YA MFALME na MORDEKAI mjomba yake.

Wakati wengine wakimwendea Hegai na kumlazimisha awape vitu wanavyotaka wao ili wamwendee mfalme, Esta hakuwa hivyo, bali alijinyenyekeza kwa Hegai, Huku akishikilia maagizo aliyopewa na mjomba wake Mordekai kuwa ASIJIONYESHE KABILA LAKE HUKO AENDAKO, hivyo kwa jambo hilo tu ilimpelekea Hegai avutiwe naye sana kwasababu hakupeleka sifa yoyote imuhusuyo yeye mbele zake, na kwa kuwa Hegai alikuwa ni msimamizi wa nyumba ya mfalme Ahasuero, kwa uzoefu wa miaka mingi aliokuwa nao kule alitambua mfalme huwa anapenda msichana wa tabia gani au huwa hapendi msichana wa tabia gani, kwasababu yeye ndiye aliyekuwa msimamizi wa Vashti kabla hajawa malkia. Kwahiyo alitambua tabia ya mfalme kuwa anapenda mwanamke katika mwonekano upi, na katika tabia ipi. Na siri hiyo HEGAI alimfunulia Esta peke yake.Akamtenga Esta na wale wengine na kumpa matunzo ya kipekee kwa msaada wa vijakazi wengine saba.

Esta 2:8-9 “Basi ikawa, wakati iliposikiwa amri ya mfalme na mbiu yake, wasichana wengi wakakusanyika huko Shushani ngomeni mikononi mwa Hegai; Esta naye aliingizwa katika nyumba ya mfalme, mikononi mwa Hegai mwenye kuwalinda wanawake.

9 Yule mwanamwali akampendeza, akapokea fadhili kwake; naye akampa upesi vifaa vya utakaso, pamoja na posho zake, na vijakazi saba walio haki yake, wa nyumbani mwa mfalme. Pia akamhamisha yeye na vijakazi wake akawaweka mahali pazuri katika nyumba ya wanawake.

10  Walakini Esta hakudhihirisha kabila yake wala jamaa yake, kwa maana ndivyo alivyomwagiza Mordekai asiwadhihirishe.”

Kwahiyo baada ya ule muda wa utakaso kuisha ambao ulikuwa ni miezi 12 tu, Esta na wenzake waliingizwa mbele za mfalme kila mmoja akijionyesha ujuzi wake na uzuri wake, na utashi wake, kila mmoja kwa namna yake, pengine wengine walionyesha familia za kitajiri walizotokea, wengine tamaduni zao za kujua kucheza vizuri na urembo wao, wengine pamoja na uzuri wao juu ya hilo walionyesha elimu zao kubwa mbele ya mfalme, pengine wengine walionyesha kuwa wametoka kabila moja na mfalme, hivyo wangestahili, na mambo kadha wa kadha.

Lakini tukirudi kwa Esta yeye hakuonyesha chochote, isipokuwa vile tu alivyopewa na Hegai aende navyo mbele za mfalme. Na badala yake hakuonekana aliyekuwa mfano wa Esta mbele ya mfalme.

JE! BIBI-ARUSI WA KRISTO ANAPATIKANAJE?

Tunaposoma habari hii tunajifunza kwa Bwana Yesu jinsi alivyoanza kumtafuta BIBI-ARUSI wake bikira safi tangu vizazi vya kale hadi sasa, Kwahiyo mambo haya tafsiri yake kwa kanisa ni;

>Mfalme Ahasuero anamwakilisha BWANA YESU,

>malkia VASHTI ambaye baadaye alikuja kutolewa katika Umalkia wake anawakilisha taifa la ISRAELI,

>ESTA anamwakilisha BIBI-ARUSI wa kweli aliyekubaliwa na Kristo,

> Wale mabikira wengine ; Wanawakilisha MADHEHEBU.

>Hegai na Mordekai wanawakilisha NENO LA MUNGU na Roho Mtakatifu.

Israeli kama taifa teule la Mungu, lilifananishwa na mke wa Mungu(Yeremia 3:14), na ndivyo lilivyokuwa kwa miaka yote, Lakini Mfalme wake (YESU KRISTO) alipokuja ili afanye nao karamu, walimkataa kwa kiburi na zaidi ya yote wakamzalilisha pale kalvari mbele ya dunia yote ni mfano tu wa Vashti alivyomwaibisha mfalme Ahasuero mbele ya dunia yote. Japo Bwana Yesu alikuja kwa upole kwa mke wake Israeli wao walimkataa na kumpinga, Na ndio maana tunaona Bwana Yesu aliwaambia Ee Yerusalemu, Yerusalem “Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!”

Mathayo 23:38 “Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.

39 Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana.”

Unaona hapo baada ya wayahudi kumkataa aliye mfalme wao na mume wao, walikuja kukatwa(Warumi 11) na kutolewa katika nafasi yao ya umalkia, na ndipo Mungu akaanza kutafuta malkia mwingine mahali pake, Ndipo NEEMA ikatugeukia sisi mataifa, akitafuta BIBI-ARUSI safi atakayekaa mahali pa Israeli.

Na kama vile tunavyoona walijihudhurisha mabinti wengi mbele za mfalme kutoka maeneo mbali mbali duniani kote. Hawa mabinti si wengine zaidi ya madhehebu mbalimbali na kila moja linajiona kuwa limestahili kuwa bibi-arusi wa BWANA YESU zaidi ya lenzake. Huoni leo hii Kanisa Katoliki linajiona kanisa pekee mama ambalo Mungu amelipokea?, walutheri nao vivyo hivyo, Waanglikana wanajiona wao ndio wapo sawa, wasabato nao vivyo hivyo wao ndio kanisa litakalokwenda kumlaki Bwana mawinguni, mashahidi wa Yehova nao vivyo hivyo, wapentekoste nao wanajiona kuwa wamestahili kuwa bibi-arusi wa KRISTO, na madhehebu mengine yote yanafanya ivyo hivyo..kumbuka leo hii duniani kuna madhehebu ya kikristo zaidi ya 40,000 na yote wanadai kuwa yapo sahihi zaidi ya mengine?. Lakini tujiulize je! Wote hawa watakuwa bibi-arusi wa Kristo??.

Jibu ni hapana bibi-arusi ni mmoja tu na ni ESTA basi. Yule tu atakayekidhi vigezo vya mfalme ndiye atakayekuwa malkia.

 

JE! ESTA NI MFANO WA DHEHEBU GANI SASA HIVI?

Tabia ya kwanza ya Esta aliyoonywa na Mordekai mjomba yake(aliye mfano wa Roho Mtakatifu) ni “KUTOKUFUNUA KABILA YAKE” mahali aendapo . Hiyo ni sifa iliyomfanya Esta apate kibali kwanza kwa HEGAI na kisha kwa Mfalme. Ukitaka kufahamu kwamba jambo la kujisifia, au kueleza chimbuko lako lilikuwa ni harufu mbaya mbele za mfalme, utaona kuwa japo Esta alikuwa ni malkia kwa muda mrefu mfalme alioishi naye hakuwahi hata siku moja kumuuliza Esta yeye ni kabila gani au jamaa zake ni nani?, au watu wake ni watu na namna gani!!, mpaka baadaye sana matatizo yalipotokea, hii ilionyesha kuwa mfalme alikuwa havutiwi na chimbuko la mtu unapokuja mbele zake, Yeye alimtaka Esta kama Esta tu katika unyenyekevu wake wote yeye kama alivyo, bila kujihesabia haki mbele zake. Na ndivyo Kristo anavyotaka watu wamwendee mbele zake.

Na jambo lingine lililomfanya Esta akubalike mbele za mfalme ni kumsikiliza HEGAI, ambaye ni Mfano wa mitume na manabii (yaani NENO LA MUNGU), Esta alipata ujuzi wa taratibu za kumwendea mfalme tofauti na wale mabinti wengine kwa kudumu katika maagizo ya HEGAI.

Na sasa hivi maana ya “KUFUNUA KABILA NI NINI?”. Pale unapomwendea Kristo na desturi za kimadhehebu; Ukatoliki, ulutheri, usabato, uanglikana, u-JW,n.k. pale unapoulizwa je! Wewe Ni MKRISTO? unasema mimi ni mlutheri, au mimi ni mbranhamite au mimi ni mpentekoste n.k…mpaka hapo hizo ni hatua za awali za wewe kutokidhi vigezo vya wewe kutokuwa bibi-arusi wa Kristo. Kwasababu pale utakapokwenda kukutana na HEGAI wako(yaani NENO LA MUNGU), na kuambiwa vitu visivyoendana na dhehebu lako.. utaishia kupinga na kujikuta unamfuata Bwana Yesu kwa desturi zako mwenyewe na sio desturi zilizopo katika NENO LAKE.

Hivyo ndugu ili uwe bibi-arusi aliyekubaliwa jambo la kwanza ondoa udhehebu ndani ya fikra zako, toka kwenye kamba za kidini na za kimadhehebu, halafu mfuate yeye kama ulivyo, unaona mafarisayo walimfuata Yesu na madhehebu yao wakaishia kukatwa, vivyo hivyo ukishikilia dhehebu na kumfuata YESU utakatwa kama wao. Mgeukie HEGAI wako yaani INJILI YA MITUME NA MANABII.. BIBLIA TAKATIFU.. mfuate MFALME YESU KWA NJIA HIYO ndipo utakapomwona.

Biblia inasema Tokeni kwake enyi watu wangu..kumbuka udhehebu ni chapa ya mnyama, alama hii ukiikumbatia itakusabibishia usimuone Bwana siku ile ya unyakuo itakapofika..bibi-arusi wa kweli wa Kristo ni mnyenyekevu aliyekaa chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu peke yake na kudumu katika kile NENO LINACHOSEMA na SIO KILE KANISA LINACHOSEMA.

Neno la Mungu linaposema “mwanamke avae mavazi ya kujisitiri(1Timotheo 2:9)” na wewe unasema haijalishi dhehebu letu halihimizi hivyo, ni sawa na kukataa maagizo ya Hegai na bado unataka uwe bibi-arusi hiyo haiwezekani..pia NENO linaposema “usijifanyie sanamu za kuchonga na kuziabudu (kutoka 20)” na wewe anaenda kuchukua sanamu ya mtakatifu Fulani na kuiabudu na kusema dhehebu letu linatufundisha hivyo..Na bado unasubiri siku ile uchaguliwe na Bwana uende mbinguni…Nataka nikuambie ndugu yangu siku ile utaikosa licha ya juhudi zako zote za kujionyesha kukubaliwa siku ile utalia na kuomboleza kama wale wanawali wapumbavu wa kwenye Mathayo 25 walivyokuwa. Kwasababu tu ya kuyadharau maagizo ya HEGAI (NENO LA MUNGU).

Hivyo maombi ni Bwana akupe kuliona hilo, na kuwa Bibi-arusi safi aliyestahili kwenda katika KARAMU YA MWANA-KONDOO. Mfuate Bwana kama ulivyo bila kuwa na utambulisho wowote unaokufuata hapo nyuma.

Mungu akubariki.Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001 312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Kwa mwendelezo >>> ESTA: Mlango wa 3


Mada Nyinginezo:

MUNGU NDIYE ANAYEISHAWISHI MIOYO.

MAFUTA YA ZIADA WALIYOKUWA NAO WALE WANAWALI 10 YANAWAKILISHA NINI?

HUDUMA YA (ELIFAZI, BILDADI, NA SOFARI).

MAJI YA UZIMA.

KIKOMBE CHA GHADHABU YA MUNGU KINAJAA…TUBU UMGEUKIE MUNGU


Rudi Nyumbani:

Print this post