Swali: Maana ya Madhali ni nini kama ilivyotumika hapo katika Zaburi 21:11
Jibu: Turejee…
Zaburi 21:11 “Madhali walinuia kukutenda mabaya, Waliwaza hila wasipate kuitimiza”.
Neno “Madhali” limeonekana mara moja tu kwenye biblia yote, na maana yake ni “Ingawa” Hivyo Kiswahili kingine cha neno “Ingawa” ni “Madhali” …
Kwahiyo maandiko hayo yanaweza kuweleweka pia hivi…“Ingawa walinuia kukutenda mabaya, Waliwaza hila wasipate kuitimiza”.
Madhara yanayonuiwa na watu wabaya, ikiwa tupo ndani ya Kristo, hayataweza kushinda juu yetu, haijalishi yataonekana yamekomaa kiasi gani.
Je umempokea BWANA YESU?..
Unao wokovu ndani yako?
Waebrania 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia”.
Maran atha
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Tunasoma Simeoni alipomwona mtoto YESU, Alikiri kuuona Wokovu wa MUNGU, sasa swali ni Wokovu gani huo alioupata?
Jibu: Tuanzie ule mstari wa 25 ili tuweze kuelewa vyema…
Luka 2:25 “Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.
27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,
28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,
29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;
30 KWA KUWA MACHO YANGU YAMEUONA WOKOVU WAKO,
31 Uliouweka tayari machoni pa watu wote;
32 Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli”
Sasa hapo hajasema AMEUPATA WOKOVU..La! bali anasema “MACHO YANGU YAMEUONA WOKOVU”.. kuuona wokovu na kuupata wokovu ni vitu viwili tofauti…
Wokovu wa Mungu unapatikana kupitia mmoja tu, naye ni YESU KRISTO (Matendo 4:12),..Baada ya YESU kusulibiwa ndipo watu wakaanza kuupata wokovu, lakini kabla ya hapo waliusikia na kuuona tu,…waliousikia ni manabii wa kale na watu wote wa agano la kale, na waliouona ni watu waliokuwepo kipindi BWANA YESU anazaliwa, na walioupata ni wote waliomwamini baada ya kufufuka kwake.
Sasa utauliza vipi waliokufa katika haki wakati wa agano la kale, je hawakupata wokovu kabisa katika kipindi chao?… Jibu ni kwamba baada ya kufa kwao wokovu wao ulikuwa haujakamilika, lakini KRISTO aliposhuka kuzimu na kuchukua mamlaka yote ya walio hai na waliokufa, ndipo wokovu wao ukakamilika (maana yake wakaupata wokovu).
1Petro 1:10 “Katika habari ya wokovu huo manabii walitafuta-tafuta na kuchunguza-chunguza, ambao walitabiri habari za neema itakayowafikia ninyi.
11 Wakatafuta ni wakati upi, na wakati wa namna gani ulioonywa na Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, ambaye alitangulia kuyashuhudia mateso yatakayompata Kristo, na utukufu utakaokuwako baada ya hayo.
12 Wakafunuliwa ya kuwa si kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yenu walihudumu katika mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiri ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Mambo hayo malaika wanatamani kuyachungulia”.
Kwahiyo Simoni aliuona Wokovu, kwakuwa anayebeba wokovu (YESU KRISTO) yupo pale.
Na wote tunaomwamini sasa, tunapokea wokovu wa roho zetu.
Je umempokea YESU?… Je umeoshwa dhambi zako kwa damu yake?
Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
FAHAMU KANUNI ZA KUZISUBIRIA AHADI ZA MUNGU?
Nini tofauti ya haya maneno. 1) KUOKOKA, 2) WOKOVU, 3) KUONGOKA.?
Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?
UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA.
Musa alikuwa na sababu kadha wa kadha za yeye kufanye vile, ikiwemo
Kutoka 3:11
[11]Musa akamwambia Mungu, Mimi ni nani, hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa Israeli watoke Misri?
Musa aliogopa, kwenda kuwahubiria watu juu ya Mungu Ambaye hakulijua jina lake, kwani zamani zile, miungu yote ilifahamika kwa majina, hivyo alijiona kama kwenda kuwaambia watu habari za Mungu asiyejulikana jina lake, ni kama anawafedhehi.
Kutoka 3:13 Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n’nani? Niwaambie nini?
Kutoka 4:1
[1]Musa akajibu akasema, Lakini, tazama, hawataniamini, wala hawataisikia sauti yangu; maana watasema, BWANA hakukutokea.
Kwasababu alikuwa hana ishara yoyote ya ki-Mungu ndani yake.
Kutoka 4:10
[10]Musa akamwambia BWANA Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito.
Pamoja na Mungu kumwakikishia kuwa atakuwa naye na kumsaidia lakini Musa bado akakataa, ndipo Mungu akaghadhibika na kumletea nduguye Haruni, kama msaidizi wake.
Jambo ambalo halikuwa mpango wa awali wa Mungu, kwani uongozi wa Haruni hakuwa kusudi kamilifu la Bwana. Sababu kadha wa kadha zilizowapelekea wana wa Israeli kupata adhabu, zilikuwa ni pamoja na uongozi dhaifu wa Haruni. Utakumbuka wakati Musa amepanda juu mlimani kuchukua zile mbao mbili za amri 10, Haruni aliachiwa uongozi kwa muda, watu walipomfuata Kwa ajili ya hatma zao, akasikiliza mapendekezo yao akawaundia sanamu ya ndama ili waiabudu, ikapelekea Mungu kuwaangamiza wana wa Israeli wengi sana, (Kutoka 32:1-6) mzizi huo ni kutokana na kutokutii kwa Musa, halikadhalika sababu ya Musa kutoiona nchi ya ahadi ilichangiwa pia na uongozi hafifu wa Haruni, kwani kule Meriba kosa alilofinya Musa la kuchukua utukufu wa Mungu, alihusika na Haruni pia. (Hesabu 20:10-12)
Hivyo ni wazi kama angekuwa na imani na Mungu, mengi yasingetokea mbeleni. Hata wakati huu wa sasa, wengi wetu tumejikuta katika machaguzi ya pili ya Mungu kwasababu tu, ya kumpotezea imani, kuwa anaweza kutenda kusudi lake lote hata katika Madhaifu yetu.
Mwamini Mungu mtegemee yeye tu.
Shikilia vifungu hivi vikusaidie.
Mithali 3:5
[5]Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
Isaya 6:8
[8]Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi.
2 Timotheo 1:7
[7]Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini Mungu alimchagua Musa, na si mtu mwingine?
Je ni sala gani inahitajika kabla ya kumchinja mnyama katika ukristo?
Je maombi ya mlimani yana ulazima wowote kwa mkristo?
Mungu hakumchagua Musa kwasababu ya wema, au kipawa, au ujuzi fulani aliokuwa nao tofauti na wengine. Hapana almchagua ili ‘kutumiza kusudi lake la kuchagua’ ambalo tunalisoma kwa urefu katika (Warumi 9:11-17). Linalomaanisha Mungu humchagua mtu na kumfanya awe kama anavyotaka mwenyewe, na sio kwa jinsi Yule mtu atakavyo. Kwamfano alimchagua Farao, kisha akamwekea moyo mgumu,ili atimize kusudi lake mwenyewe, kujichotea utukufu kwa mapigo yale kumi,aliyoyaachia kwa wamisri, vivyo hivyo na kwa Musa alimchagua na kumpa neema ile kubwa ya hofu ya Ki-Mungu na upole ili atimize kusudi lake la kuwakomboa wana wa Israeli.
Lakini hakuwa na tendo lolote jema alilowahi kutenda lililomshawishi Mungu amchague yeye tofauti na wengine.
Na ndivyo anavyofanya hata sasa kwa wanadamu wote. Tunaokolewa na kutumiwa na Mungu kwa neema tu, na si kwasababu ya matendo Fulani mema tuliyowahi kumtendea Mungu.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nini tofauti ya Majira na Wakati?
Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?
NAAM, HATA WABAYA KWA SIKU YA UBAYA.
Swali: Je sisi wakristo tunapaswa tuombe sala gani kabla kumchinja mnyama?, maana Imani nyingine tunaona kabla kuchinja wanatanguliza sala.
Jibu: Katika biblia hatujapewa maagizo yoyote ya kuomba sala, au kukiri maneno Fulani kabla ya kumchinja mnyama. Ndio zipo Imani zinazoelekeza kufanya hivyo, lakini si Biblia takatifu.
Maagizo tu yaliyopo katika biblia ni kushukuru kabla ya kula..lakini kupiga sala kabla ya kuchinja hatujapewa kwani hatuendi kutoa sadaka kwa miungu bali ni kwaajili ya kitoweo.
Katika agano la kale, wanyama waliombewa kabla ya kuchinjwa iwapo wanaenda kutolewa kama sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana (dhabihu).
Walawi 4:32 “Naye akileta mwana-kondoo kuwa sadaka ya dhambi, ataleta wa kike mkamilifu.
33 Naye ataweka mkono wake kichwani mwake sadaka ya dhambi, kisha atamchinja awe sadaka ya dhambi, mahali hapo wachinjapo sadaka ya kuteketezwa”.
Lakini katika agano jipya dhabihu ya mwili wa YESU ilishatolewa, (hiyo ndio dhabihu kamilifu)…sasa wanyama wanachinjwa kwaajili ya vitoweo, na si kwaajili ya sadaka.. na hakuna sala yoyote inayotangulia, na hata wanaoomba hizo dua bado kuna viumbe vitawafunga katika sheria hiyo, kwamaana samaki au dagaa au wadudu kama kumbikumbi au senene unawaombeaje dua kabla ya kutoa uhai wao?… utaombea dagaa mmoja mmoja??..ni jambo lisilowezekana vinginevyo hatutakula kabisa.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba hakuna sala inayotangulia kabla ya kuchinja au kuutoa uhai wa kiumbe chochote kwaajili ya chakula.. Na kufahamu kwa urefu kama wakristo anaruhusiwa kula nyama ya mnyama aliyechinjwa kwa dua, basi fungua hapa >>UKWELI KUHUSU UISLAMU Sehemu ya Pili: (Jiwe/Jabali la Kaaba).
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SWALI: Yusufu aliwezaji kutafsiri ndoto? Je ni kwa hekima aliyokuwa nayo au kwa kuangalia ishara fulani, au kwa usomaji wa vitabu, au kwa saikolojia?
JIBU: Biblia inatuonyesha sifa kuu, ya Yusufu iliyokuwa ndani yake ni uwezo wa kutafsiri ndoto.
Lakini swali linaloulizwa je uwezo huo alitolea wapi, ulikuwa ndani yake mwenyewe au ulitoka kwingine.
Tukisoma Mwanzo 41:15, tunaweza kupata majibu;
Farao akamwambia Yusufu, Nimeota ndoto, wala hakuna awezaye kunifasiria; nami nimesikia habari zako, ya kwamba, usikiapo ndoto, waweza kuifasiri.16 Yusufu akamjibu Farao, akisema, Si mimi; Mungu atampa Farao majibu ya amani.
Hapo Yusufu anasema si mimi, Mungu atampa Farao majibu. Kuonyesha kuwa uwezo huo ulitoka kwa Mungu wala sio katika akili zake, elimu , saikolojia , au hekima ya kibinadamu.
Alimtegemea Mungu asilimia mia kumfunulia, mfano tu wa Danieli alipokwenda kuomba juu ya tafsiri ya ndoto ya Nebukadreza katika sala akafunuliwa. Ndivyo ilivyokuwa kwa Yusufu, katika kutafsiri ya ndoto ya Farao, pamoja na za wale watumishi wawili wa mfalme waliokuwa wanahudumu mezani pa mfalme. Hakubuni tu tafsiri kulingana na mazingira, bali alifunuliwa moja kwa moja aidha kwa ndoto au kuona maono.
Lakini ni kwanini Yusufu apokee neema hiyo kirahisi kwa Mungu, tofauti na wengine.
Jibu lipo katika TABIA yake, Ni wazi Roho ya Mungu huvutika sana katika tabia njema ya mtu. Yusufu tangu udogo alijitahidi kujiepusha na tabia zisizofaa, jambo lililopelekea mpaka ndugu zake kumchukia kwasababu alikuwa anatoa siri za mambo yao mabaya, hata alipouzwa kwa akida wa Farao, bado aliendeleza tabia yake ileile, pale mke wa Potifa alipomtamani akakataa, mwishowe akatupwa gerezani. Kwa njia hiyo Yusufu hakuacha kulitunza joto la ROHO ndani yake. Mfano tu wa Danieli naye, ambaye hakutaka kujitia unajisi kwa vyakula vya kifalme, na ndani ya hakukuonekana kosa lolote (Danieli 6:3).
Akashuhudiwa na mfalme kuwa Roho njema sana, na iliyo bora inakaa ndani yake.
Danieli 5:12 kwa kuwa roho njema kupita kiasi, na maarifa, na ufahamu, na uwezo wa kufasiri ndoto, na kufunua maneno ya fumbo, na kufungua mafundo, zilionekana katika Danieli huyo, ambaye mfalme alimwita Belteshaza. Basi na aitwe Danielii, naye ataionyesha tafsiri.
Hivyo ili na sisi tushiriki sehemu bora na njema za vipawa mbalimbali vya Roho Mtakatifu, hatuna budi kujijenga kimwenendo, katika maisha matakatifu yampendezayo Mungu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?
KWA KUWA ROHO BORA ILIKUWA NDANI YAKE.
JIBU: Safina ya Nuhu ilikuwa ni mfano wa Meli kubwa iliyojengwa katika deka tatu, ambayo vipimo vyake vilikuwa ni mikono mia tatu urefu wake, na mikono hamsini upana, na mikono thelathini kwenda juu.
Mwanzo 6:13 Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia.14 Ujifanyie safina ya mti wa mvinje; fanya na vyumba ndani ya safina, ukaifunike ndani na nje kwa lami. 15 Hivi ndivyo utakavyoifanya; mikono mia tatu urefu wa safina, mikono hamsini upana wake, na mikono thelathini kwenda juu kwake.
Ambayo kwa vipimo vya sasa ni sawa na makadirio ya;
> Mita 137 urefu
> Mita 23 upanda
> Mita 14 kimo.
Ukubwa wa ile Safina, kwa sasa tunaweza kuifananisha na hizi meli kubwa za mizigo.
Yapo mambo manne ya kufahamu;
1). Jambo la kwanza ni kuwa hawakuingizwa wengi wengi, bali wawili wawili, na wengine saba saba, hivyo ni idadi ndogo tu ya kila jamii ndio iliyoingizwa.
2) Lakini pia kuna uwezekano Nuhu aliwaingiza wale wadogo wadogo tu, na sio wale wakubwa, Hivyo ikaachilia nafasi ya wanyama wote kujitosheleza ndani ya safina.
3) Tatu alipoambiwa awaingize wanyama kwa “namna” zao, (Mwanzo 6:20). Kwa lugha ya kibiblia si lazima imaanishe kila familia za wanyama ziingie, mfano familia mbalimbali za mbwa, wenye manyoya marefu, wenye asili ya ufupi, wawindaji, n.k. hapana, bali walipoingizwa mbwa, ni namna moja tu, iliwakilisha wote, Na baadaye walipoongozeka waliweza kuonekana wa maumbile tofauti tofauti tena, hilo linawezekana, ni sawa na sisi wanadamu tulitoka katika asili ya baba mmoja na mama mmoja, lakini leo hii kuna waafrika, wazungu, wachina, waarabu n.k. Hivyo ikiwa aliwaingiza kwa njia hiyo basi kisayansi inawezekana kabisa.
4) Lakini hoja ya mwisho iliyo na nguvu kuliko zote, ni kuwa hata kama ni namna zote na familia zao waliingia, bado Mungu anaweza kufanya mambo ambayo mwanadamu hawezi kuyafanya, ikiwa katika uzazi wa mwanaume mmoja Mungu amehifadhi mamilioni ya mbegu za kibinadamu, na ndani ya tumbo la mwanamke mmoja hadi watoto tisa wanakaa kwa ujauzito mmoja. Hivyo hatuwezi kushangaa, Mungu kuvihifadhi viumbe vyote katika meli ile, inayoonekana haijitoshelezi. Kwasababu yeye ni Mungu asiyeshindwa na chochote.
Ni kwa yeye haathiriwi na nafasi ya udogo au ukubwa, kusudi lake litasimama tu. Kwa vile vichache vilivyokuwa kwenye safina, ulimwengu leo umejawa na viumbe vingi na watu wengi. Wengine wanasema mimi nabanwa na muda hivyo siwezi kumtumikia Mungu, mimi nabanwa na masomo hivyo siwezi kufanya kitu kwa Mungu, mimi nimefungwa gerezani, siwezi kulitimiza kusudi lolote la Mungu. Ndugu Neno la Mungu halifungwi.
Ndugu Paulo alifungwa gerezani akazuiwa kwenda kuhubiri injili katika mataifa kama ilivyo desturi yake, lakini akiwa gerezani aliandika nyaraka ambazo mpaka leo hii zinaendelea kuhubiri injili, zaidi hata ya ziara zake.
Amini uweza wote wa Mungu mahali popote ulipo, bila kuathiriwa na mazingira.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NUHU ALIJENGA SAFINA KWA MIAKA MINGAPI?
SAFINA NI NINI?
Mvinje ni mti gani? (Mwanzo 6:14)
Swali: Je mtu akifanya dhambi katikati ya mfungo, mfano dhambi ya uzinzi, je ule mfungo unakuwa umeharibika?
Jibu: Awali ya yote ni vizuri kufahamu kuwa kufunga ni kitendo cha kuyatiisha chini mapenzi ya mwili na kuruhusu mapenzi ya roho yaje juu, kwasababu roho siku zote hushindana na mwili..
Wagalatia 5:16 “Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka”
Sasa unapokula chakula katikati ya mfungo, huo mfungo unakuwa umeharibika, kwasababu unakuwa umeyaruhusu mapenzi ya mwili, hali kadhalika unapofanya dhambi kama ya uzinzi katikati ya mfungo, pia mfungo huo unakuwa umeharibika kwasababu uzinzi ni dhambi inayohusisha mwili kwa asilimia zote.
1Wakorintho 6:18 “Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe”.
Kwahiyo mtu anayefanya zinaa anakuwa ameuharibu mfungo wake, na hivyo anapaswa atubu kwa kumaanisha kuacha hiyo dhambi kisha kwa uongozo wa Roho Mtakatifu apange mfungo mwingine.
Kwa urefu kuhusiana na njia bora ya kufunga, fungua hapa >>>NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea.
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
Jibu: Turejee…
Walawi 24:3 “Hapo nje ya pazia la ushahidi, ndani ya hema ya kukutania, Haruni ataitengeza tangu jioni hata asubuhi mbele za BWANA daima; ni amri ya milele katika vizazi vyenu”.
“Pazia la ushahidi” au kwa lugha nyingine “Pazia la Sitara” lilikuwa ni pazia lililotenga “patakatifu” na “Patakatifu pa patakatifu”.
Pazia hili lilisitiri eneo la ndani kabisa ya hema mahali palipokuwepo sanduku la Agano au sanduku la ushahidi.
Kipindi wana wa Israeli wapo jangwani wakitaka kuondoka eneo moja kwenda lingine walikuwa hawana budi kulivunja hema, na ili kulisitiri sanduku la agano mbali na macho ya watu wakati wanatembea, Bwana aliwaambia watumie pazia hilo la ushahidi linalotenga patakatifu na patakatifu pa patakatifu kulifunika hilo sanduku.
Na walipopiga makambi tena walilitengeneza hema na kilitumia hilo pazia kusitiri sehemu hizo mbili, hiyo ndiyo ilikuwa desturi yao.
Hesabu 4:5 “hapo watakapong’oa safari, Haruni ataingia ndani, na wanawe, nao watalishusha pazia la sitara, na kulifunika sanduku la ushahidi kwa hilo pazia”
Sasa Pazia la sitara kiroho liliwakilisha kiambazi kulichotutenga sisi na rehema za Mungu, kwamba hapo kwanza hakuna mtu yeyote ambaye angeweza kupaingia patakatifu (ndani ya pazia) na kudai rehema isipokuwa kuhani mkuu tu, tena mara moja kwa mwaka, na dhambi zilifunikwa tu na hazikuondolewa.
Lakini Kristo alipokufa pale msalabani maandiko yanaonyesha kuwa hili Pazia la sitara lilipasuka kati kwa kati, vipande viwili.
Mathayo 27:50 “Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.
51 Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka”.
Hiyo nikufunua kuwa sasa watu wote tunaweza kukikaribia kiti cha neema kupata rehema..
Waebrania 4:14 “Basi, iwapo tunaye kuhani mkuu aliyeingia katika mbingu, Yesu, Mwana wa Mungu, na tuyashike sana maungamo yetu”
Ni neema kubwa sana tuliyonayo sasa ambayo haikuwepo zamani, watu wa kale walitamani kuipata neema hii tuliyonayo lakini hawakuipata.
Lakini swali kuu linabaki kwetu…Je tunaithamini hii Neema, au tunaichukulia tu kama kitu cha kawaida?.
Waebrania 10:29 “Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”.
Bwana atusaidie tusimame imara.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Jibu: Turejee…
Walawi 7:9 “Na kila sadaka ya unga iliyookwa MEKONI, na yote yaliyoandaliwa chunguni, au kaangoni, yote yatakuwa ya huyo kuhani aliyeyasongeza”.
Mekoni ni jiko la kuokea mikate kwa lugha ya kiingereza ni “oven”.
Katika agano la kwanza sadaka zote za unga zilizotengenezwa kwa kupikwa ….Bwana Mungu aliagiza ziwe ni riziki za makuhani wanaofanya kazi yake katika nyumba yake.
Walawi 7:10 “Na kila sadaka ya unga, kama umeandaliwa na mafuta, au kama ni mkavu, watautwaa wana wote wa Haruni kuutumia, kila mtu sawasawa”
Katika agano jipya pia Bwana ameruhusu wanaohudumu madhabahu wale kupitia madhabahu..
1 Wakorintho 9:13 “Hamjui ya kuwa wale wazifanyao kazi za hekaluni hula katika vitu vya hekalu, na wale waihudumiao madhabahu huwa na fungu lao katika vitu vya madhabahu?
14 Na Bwana vivyo hivyo ameamuru kwamba wale waihubirio Injili wapate riziki kwa hiyo Injili”
Unapotoa riziki kwa wanahubiri injili unafanya jambo lenye thawabu kwasababu ni maagizo ya Bwana na si sheria.
Shetani kaliharibu hilo eneo la matoleo na kuwafanya watu wasitoe kabisa wakiamini kuwa ni biashara zinafanyika..
Ni kweli wapo wanaofanya injili kama biashara lakini si wote, hatuwezi kuacha kutimiza majukumu kwa Bwana kwasababu ya uharibifu wa shetani, tutaendelea mbele kwasababu Ukristo ni mapambano.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine: