Neno Maganjo linamaanisha nini katika biblia?

Neno Maganjo linamaanisha nini katika biblia?

Maganjo ni kitu kilichoharibiwa, kwa mfano jengo likiharibiwa labda tuseme kwa  kombora, lile gofu linalobakia ndio maganjo. Au mji unapochomwa moto, yale masalia salia ya mji, ndio maganjo.

Mungu amekuwa akitumia Neno hili kuonyesha jinsi adhabu yake itakavyokuwa kwa wasiomcha yeye.

Hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utaweza kukutana na Neno hilo;

Walawi 26:30 “Nami nitapaharibu mahali penu palipoinuka, na kuziangusha sanamu zenu za jua, nami nitaitupa mizoga yenu juu ya mizoga ya sanamu zenu; na roho yangu itawachukia.

31 NAMI NITAIFANYA MIJI YENU IWE MAGANJO, na mahali penu patakatifu nitapatia ukiwa; wala sitasikia harufu ya manukato yenu yapendezayo.

32 Nami nitaitia hiyo nchi ukiwa; na adui zenu watakaokaa huko wataistaajabia”.

Ezekieli 6:14 “Nami nitanyosha mkono wangu juu yao, na kuifanya nchi kuwa MAGANJO, tena ukiwa mbaya kuliko jangwa upande wa Dibla, katika makao yao yote; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana”.

Yeremia 51:42 “Bahari imefika juu ya Babeli, Umefunikwa kwa wingi wa mawimbi yake.

43 Miji yake imekuwa MAGANJO; Nchi ya ukame, na jangwa; Nchi asimokaa mtu ye yote, Wala hapiti mwanadamu huko”.

Yeremia 4:7 “Simba ametoka katika kichaka chake, ndiye aangamizaye mataifa; ameanza kushika njia, ametoka katika mahali pake; ili aifanye nchi yako kuwa ukiwa, miji yako ifanywe MAGANJO, asibaki mwenyeji ndani yake. 8 Kwa sababu hiyo jifungeni nguo za magunia; ombolezeni na kulia kwa uchungu; kwa maana hasira kali ya Bwana haikugeuka na kutuacha”.

Som pia Ezekieli 12:20, 29:12, Amosi 9:14

Hata sasa, huu ulimwengu, utakwenda kufanywa maganjo kipindi si kirefu, haijalishi umejengwa vizuri kiasi gani, haijalishi umeshafikia hatua ya kuwa ustaarabu mzuri namna gani,..Bwana Yesu alisema kuwa hakuna jiwe litakalosalia juu ya jiwe. Kila kitu unachokiona leo hii kitateketezwa, siku ile ya Bwana itakapofika. Kila kitu kitafumuliwa, moto utaisafisha kweli kweli hii dunia, kama vile gharika ilivyoisafisha dunia ya kwanza wakati ule wa Nuhu.

Soma.

2Petro 3:10 “Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.

11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,

12 mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka”?

Swali ni je! Mimi na wewe tumeekeza wapi maisha yetu?  Je ni duniani au mbinguni?..Kumbuka duniani ni tunapita, yapo maisha ya milele huko mbeleni yanatungojea.. Ni wajibu wetu kutambua lililo la muhimu kwanza, ambalo ni wokovu wetu, Lengo la Mungu kuifanya hii dunia kuwa maganjo si kwamba ni mbaya hapana, bali sisi ndio tumeifanya kuwa mbaya kwa dhambi zetu, na hivyo ni lazima iteketezwe tu.

Hivyo sisi sote tusiwe washirika wa hiyo ghadhabu ya Mungu. Kumbuka Unyakuo upo mlangoni. Na haya mambo hatutashangaa kuyaona yakitimia hata kwenye kizazi chetu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

KWA WALE WALIO NJE “YOTE” HUFANYWA KWA MIFANO.

UFUNUO: Mlango wa 14

Sodoma ipo nchi gani?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Cleven Nassary
Cleven Nassary
2 years ago

Amen