Title February 2024

Mafuta mabichi ni mafuta ya aina gani? (Zaburi 92:10)

Swali: Mafuta Mabichi yapoje, na yanafunua nini kiroho?


Jibu: Tureje..

Zaburi 92:10 “Bali pembe yangu umeiinua kama pembe ya nyati, Nimepakwa MAFUTA MABICHI”.

Mafuta mabichi yanayozungumziwa hapo si mafuta ambayo hayajapitishwa kwenye moto yakaiva na kuchemka… La!.. bali ni mafuta yaliyo mapya (yaani freshi) ambayo yayajakaa muda mrefu.

Nyakati za biblia na hata sasa wayahudi wanatumia mafuta ya Mizeituni kwa matumizi ya chakula na ibada.

Asilimia kubwa ya vyakula vya wayahudi na baadhi ya jamii za mashariki ya kati wanatumia mafuta ya Mizeituni kama kiungo cha mboga, na wakati jamii nyingine mbali na hizo wanatumia mafuta ya Alizeti au mimea mingine katika mapishi.

Chakula kilichoandaliwa kwa mafuta mabichi (yaani mapya) ya Mizeituni kinakuwa ni kitamu na chenye ladha… utaona hata ile MANA jangwani, ladha yake ilifananishwa na ladha ya mafuta mapya. (soma Hesabu 8:11).

Vile vile katika shughuli za kiibada, pale ambapo mtu anatawazwa kuwa mfalme basi alipakwa Mafuta haya ya mizeituni kama ishara ya kuruhusiwa kuchukua madaraka hayo,

1Samweli 9:15 “Basi Bwana alikuwa amemfunulia Samweli, siku moja kabla Sauli hajamwendea, akisema,

16 Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mtu kutoka nchi ya Benyamini, NAWE MTIE MAFUTA ili awe mkuu juu ya watu wangu Israeli, naye atawaokoa watu wangu na mikono ya Wafilisti; maana nimewaangalia watu wangu, kwa sababu kilio chao kimenifikilia”

Soma pia1Wafalme 16:12, 1Wafalme 1:34, na 1Wafalme 19:15-16 utaona jambo hilo hilo..

Vile vile makuhani walitiwa mafuta kama ishara ya kuchaguliwa na Mungu kutumika katika nyumba yake.

Zaburi 133:2 “Ni kama mafuta mazuri kichwani, Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni, Yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake”.

Sasa ilikuwa ni heshima na jambo jema kutiwa mafuta ambayo ni mapya.. Kwani Mafuta ya Mizetuni kama yamehifadhiwa vizuri yanadumu kwa miaka 2 tu, ukipita huo muda yanaharibika na kutoa harufu nyingine. Kwahiyo chakula kilichoandaliwa kwa mafuta yaliyokaa kinakuwa hakina ladha na pia kinatoa harufu mbaya…

Vile vile mtu aliyepakwa mafuta yaliyokaa sana au kuharibika si jambo la utukufu… lakini mafuta mabichi ilikuwa ni jambo la utukufu kwasababu ni freshi.

Sasa mafuta mabichi (yaani mapya) na yale yaliyokaa (yaani ya zamani) yanawakilisha nini sasa kiroho?..

Mafuta yanamwakilisha ROHO MTAKATIFU. Hivyo mafuta yaliyokaa (ya zamani) yanawakilisha utendaji kazi wa Roho Mtakatifu katika Agano la kale… na Mafuta mapya ni utendaji wa ROHO MTAKATIFU katika agano jipya.

Na sisi tunayahitaji mafuta mabichi katika UTUMISHI WETU,  na si yale yaliyokaa… kwasababu hayatatufaa sana..

Mafuta mapya yanatufundisha kuwa wakamilifu zaidi na katika kuyafanya mapenzi ya Mungu..kuliko yale ya zamani.

Mathayo 5:27  “Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini;

28  lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.

29  Jicho lako la kuume likikukosesha, ling’oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.

30  Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.

31  Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka;

32  lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.

33  Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako;

34  lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu”.

Je umempokea YESU KRISTO, aliye mjumbe wa Agano jipya?, kumbuka huwezi kuwa na ROHO MTAKATIFU, kama YESU KRISTO hayupo ndani ya maisha yako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza

Je tunaruhusiwa kujipaka mafuta au kujipulizia marashi?

MAANA YA KRISTO/ JINA KRISTO LINA MAANA GANI?

 Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako,katika kufanya maombezi?

Mfano wa wanawali kumi(Mathayo 25), unaelewekaje?

Rudi nyumbani

Print this post

BWANA ANA NGUVU KAMA ZA NYATI! USIOGOPE UCHAWI!

Kama umeokoka kikweli kweli kwanini uchawi uwe na nguvu kwako??


Hesabu 23:22 “Mungu amewaleta kutoka Misri, Naye ana nguvu kama NGUVU ZA NYATI.

23 Hakika HAPANA UCHAWI juu ya Yakobo, WALA HAPANA UGANGA juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!”

Umewahi kujiuliza kwanini Nguvu za Mungu zifananishwe an za NYATI kipindi anawatoa wana wa Israeli Misri na kuwapeleka nchi ya ahadi??..Je unajua tabisa za nyati ni zipi mpaka zifananishwe na za Mungu?

NYATI ni Mnyama jamii ya Ng’ombe, na anafanana sana na Ng’ombe… lakini ana nguvu nyingi kuliko Ng’ombe.. Lakini tabia za huyu mnyama ni kwamba HAKUBALI KUFUNGWA NA MTU na ANAWAPIGA WOTE WANAOJARIBU KUMSOGELEA.. Laiti angekubali kufungwa na mwanadamu basi angekuwa nyenzo moja bora sana ya kazi.. kwani ana nguvu kuliko Ng’ombe.

Kwa nguvu alizonazo huenda matrekta ya kulimia yangekosa soko, kama angekubali kufungwa NIRA kama Ng’ombe!..Lakini hakubali kufugika ingawa ni Ng’ombe, mwenye sifa zote za kufugika lakini hafungiki….Nguvu zake anazimalizia kutishia na kudhuru maadui zake na wote wanaomsogelea, wakati Ng’ombe ni mnyenyekevu na mwenye kukubali NIRA. .

Ayubu 39:9 “Je! Nyati atakubali kukutumikia? Au atakaa katika zizi lako?

10 Je! Waweza kumfunga nyati kwa kamba matutani? Au, yeye atayalima mabonde nyuma yako?

11 Je! Utamtumaini kwa sababu ana nguvu nyingi? Au, utamwachia yeye kazi yako?

12 Je! Utamtumaini kwamba ataileta mbegu yako nyumbani. Na kukusanya nafaka ya kiwanja chako cha kupuria?”

Sasa tabia hiyo ya NYATI ya kukataa KUFUNGWA Nira, na BADALA YAKE KUWADHURU WANAOMSOGELEA KWA NGUVU ZAKE..ndiyo ilikuwa ndani ya WANA WA ISRAELI, walipokuwa wanasafiri jangwani.. Hakuna aliyewafunga tena Nira ya utumwa tena, na walikuwa wanawapiga maadui zao.

Pale ambapo Balaamu aliyekuwa mchawi (Yoshua 13:22) alipojaribu kuwalaani (yaani kuwafunga nira kichawi/kuwaloga), Ilishindaka kwasababu wanatembea na NGUVU ZA NYATI, ASIYEKUBALI NIRA!. Balaamu alipojaribu kuwafunga Mafundo kiroho ili wawe wanyonge mbele ya Balaki alishindwa, ule uchawi uligota.

Na Balaamu-mchawi alipoona kwamba mambo hayawezekaniki…Ndipo akasema, “HAKUNA UCHAWI WALA UGANGA JUU YA YAKOBO” Maana yake hakuna Nira ya kichawi wala ya kiganga kwa wana wa Israeli wanatembea kwa nguvu kama za NYATI…

Hesabu 23:22 “Mungu amewaleta kutoka Misri, Naye ana nguvu kama NGUVU ZA NYATI.

23 Hakika HAPANA UCHAWI juu ya Yakobo, WALA HAPANA UGANGA juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!”

Je umeokoka na hizi nguvu zinatembea nawe?

Kama bado hujaokoka kikamilifu basi ni haki yako kuuogopa uchawi tena uugope sana!!. Lakini ukitaka usiuogope wala usiwe na nguvu juu yako suluhisho si kutafuta maji, au mafuta ya upako.. bali suluhisho ni wewe kuwa Israeli wa kiroho..Ukiwa Isreali wa kiroho uchawi unadunda, kwasababu utakuwa unatembea na NGUVU ZA NYATI ndani yako.

Na unafanyikaje Israeli wa kiroho?..Si kwa njia nyingine Zaidi ya kutubu na kubatizwa katika ubatizo sahihi na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Ikiwa utahitaji msaada wa kuongozwa namna ya kumpokea Bwana Yesu na kubatizwa basi waweza wasiliana nasi kwa namba zetu.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU

JE! WEWE NI MFUNGWA WA BWANA?

YESU ANA KIU NA WEWE.

Rudi nyumbani

Print this post

Je kuwashwa mkono ni ishara ya kupata pesa?

Swali: Je ni kweli kwamba kiganja cha mkono wa kushoto au wa kulia kikiwasha basi ni ishara ya kupata pesa?


Jibu ni LA!.. hakuna uhusiano wowote  kiganja kuwasha na fedha kumjia mtu. Labda kama mtu huyo ana pepo la utambuzi ndani yake..

Kama mtu ana pepo la utambuzi basi anaweza kuhisi kitu Fulani kikimjia, ikiwemo pesa kutoka katika chanzo kisicho cha kiMungu, au akahisi hatari kutoka katika upande wa maadui zake (maana yake upande wa Mungu), na ishara hizo anaweza kuzihisi kwa njia kama hizo za kuwashwa mkono, au kuwashwa sehemu nyingine ya mwili.

Lakini mtu mwenye Roho wa Mungu hisia zake zipo katika Neno la Mungu..Anaposoma Neno la Mungu na kudumu katika uwepo huo basi anaweza kuhisi Baraka zijazo, au hatari ijayo.

Kwamfano Neno hili katika biblia linaweza kukupa hisia za Baraka zijazo…

Mithali 13:11 “Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa”.

Mtu akilisoma hili Neno la kulishika, tayari atakuwa anajua ni nini kitafuta katika shughuli anayoifanya.. lakini si kukisikilizia kiganja kinasema nini!.. Na maneno mengine yote ya Mungu ni hivyo hivyo..

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba,  Elimu ya kusoma viungo vya mwili na kutabiri mambo yajayo ni elimu ya adui na ya kupotosha..

Lakini pia kumbuka si kila anayewashwa mkono basi ana pepo la utambuzi!.. La!, mkono unaweza kuwasha kwa sababu nyingine yoyote ya kibaolojia, na mtu asiwe na pepo!.. (Hata hivyo asilimia kubwa ya wanaowashwa mikono hawana mapepo). Hivyo kilicho kikubwa na cha msingi ni kudumu katika Neno la Mungu.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KUOTA UNAPEWA PESA, KUNA MAANISHA NINI?

Pesa za bindoni ni nini?(Marko 6:8)

Je! fedha ni jawabu la mambo yote? (Mhubiri 10:19).

MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA.

Biblia inaposema Yesu ameketi mkono wa kuume inamaana gani?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya kurarua mavazi? (Mwanzo 37:34).

Kurarua mavazi ni utamaduni wa wayahudi na watu wa zamani kuonyesha hisia zao kwa kuyararua (kuchana) sehemu ya mavazi yao kama isha ya Toba (kujishusha) au  maombolezo au majuto.

      1. Ishara ya kushuka (kunyenyekea) na kutubu.

Mfalme Yosia alipokiona kitabu cha Torati alitambua Israeli wamefanya dhambi kulingana na yaliyoandikwa kule, hivyo akajishusha mbele za Mungu Soma 2Wafalme 22:11-15..

Vile vile Mfalme Ahabu baada ya kutamkiwa hukumu yake na Mungu kwaajili ya shamba la Nabothi alilomdhulumu na tena kumwua..Ahabu alijishusha mbele za Mungu kwa kuyararua mavazi yake..

1Wafalme 21:27 “Ikawa, Ahabu alipoyasikia maneno hayo, akayararua mavazi yake, akavaa magunia mwilini mwake, akafunga, akajilaza juu ya magunia, akaenda kwa upole”.

      2. Maombolezo.

Kwamfano utaona baada ya Yakobo kupokea taarifa za kifo cha mwanae Yusufu (ambaye kimsingi hakufa) aliyararua mavazi yake kama ishara ya kuhuzunika na kumwombolezea..

Mwanzo 37:34 “Yakobo akararua mavazi yake, akajivika gunia viunoni, na kumlilia mwanawe siku nyingi”

Utasoma tena tukio kama hilo katika Mwanzo 37:29 pale Rubeni alipopata taarifa za kifo cha ndugu yake. Na pia 2Samweli 13:29-31, Esta 4:1, na Ayubu 1:20.

      3.Majuto

Utaona Mwamuzi Yeftha baada ya kukutana na mwanae, anaijutia nadhiri aliyoiweka kwa kurarua mavazi yake..

Waamuzi 11:35 “Ikawa alipomwona akayararua mavazi yake, akasema, Ole wangu! Mwanangu, umenitweza sana, nawe u mmoja miongoni mwa hao wanisumbuao; kwa kuwa mimi nimemfunulia Bwana kinywa changu, nami siwezi kurejea nyuma”.

Lakini je kiroho kurarua mavazi ni kufanya nini? Na je mpaka sasa tunapaswa tuyararue mavazi yetu kwa namna ya kimwili kama walivyofanya wayahudi zamani pindi tunapopitia maombolezo, au tunapotaka kutubu au kunyinyenyekeza kwa Mungu?

Jibu tunalipata katika kitabu cha Yoeli 2:13.

Yoeli 2:13 “Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea;

13 RARUENI MIOYO YENU, WALA SI MAVAZI YENU, MKAMRUDIE BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya.

14 N’nani ajuaye kwamba hatarudi na kugeuka, na kutuachia baraka nyuma yake, naam, sadaka ya unga, na sadaka ya kinywaji, kwa Bwana, Mungu wenu?”

Umeona?.. Kumbe kurarua mavazi ni kutubu!.. Na kwamba tunapotubu na kugeuka na kubadili njia zetu, mbele za Mungu ni sawa na tumeyararua mavazi yetu!.

Je leo umeurarua moyo wako?,  Umetubu kwa kumaanisha kabisa kuacha njia ile mbovu?…

Isaya 66: 2 “….lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu”.

Kujua maana ya “Kuvaa mavazi ya magunia” basi fungua hapa >>Nguo za magunia katika biblia ni zipi?

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

MAVAZI YAPASAYO.

USIYAACHE MAVAZI YAKO NA KWENDA UCHI!

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

YEYE AJAYE ATAKUJA WALA HATAKAWIA.

Rudi nyumbani

Print this post

YEYE AJAYE ATAKUJA WALA HATAKAWIA.

Waebrania 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, YEYE AJAYE ATAKUJA, wala hatakawia”.

Angalia muda unavyokimbia, angalia majira yanavyobadilika, angalia maasi yanavyoongezeka kwa kasi.. Je! yote haya unajua ni ishara ya nini?..Si ya kitu kingine bali  ya YEYE AJAYE!!.. Ndio! Yupo mmoja anayekuja! na yupo karibu sana..

Gari likipita huwa linaacha vumbi!, lakini ikitokea vumbi linatangulia kabla ya gari kufika basi ni upepo unavuma kuelekea mbele, na una mbio kuliko gari lenyewe!.

Na YESU KRISTO anakuja, na ishara zake zinatangulia mbele yake!..zina mbio kabla ya kuwasili kwake, Uvumi wa ujio wake unatufikia kabla ya yeye kuwasili.

Zifuatazo ni sifa za “Yeye ajaye”

        1. Yeye ajaye anakuja kutoka Juu mbinguni.

Yohana 3:31 “YEYE AJAYE kutoka juu, huyo yu juu ya yote. Yeye aliye wa dunia, asili yake ni ya dunia, naye anena mambo ya duniani. Yeye ajaye kutoka mbinguni yu juu ya yote”.

       2. Yeye ajaye ana nguvu kuliko manabii wote.

Mathayo 3:11 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali YEYE AJAYE nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake…”.

      3. Yeye ajaye Ni Mbarikiwa na amejaa utukufu.

Mathayo 21:9 “Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, YEYE AJAYE kwa jina la Bwana; Hosana juu mbinguni”.

      4. Yeye ajaye Anakuja Upesi wala hakawii.

Waebrania 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, YEYE AJAYE ATAKUJA, wala hatakawia”.

>Jiulize!…Utajisikiaje siku umeamka asubuhi unajiandaa kwenda kazini, halafu ghafla unapokea taarifa za kuwa KRISTO kashawachukua watu wake, na wewe umebaki?

> Utajisikiaje umeamka vizuri na unaelekea shuleni, halafu unapata taarifa kuwa unyakuo wa kanisa umepita na wewe umeachwa?

> Utajisikiaje ule muda unapewa taarifa kuwa Kanisa limenyakuliwa na jana tu uliyasikia mahubiri na hukuzingatia??..

>Tafakari utakuwa katika hali gani utakapoanza kutafakari mambo yatakayoupata ulimwengu baada ya hapo?..Kwamaana maandiko yanasema baada ya hapo itakuwa ni dhiki kuu na  hukumu kwa wanadamu na mlango wa rehema utakuwa umefungwa!.

Isaya 26:21 “Kwa maana, tazama, Bwana anakuja kutoka mahali pake, ili kuwaadhibu wakaao duniani, kwa sababu ya uovu wao…”.

Zaburi 96:13 “Mbele za Bwana, kwa maana anakuja, Kwa maana anakuja aihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, Na mataifa kwa uaminifu wake”

Wakati huo watu watatamani kuingia katika mlango wa Neema lakini watakuwa wamechelewa…kwasababu mwenye nyumba (YESU) atakuwa ameshasimama na ameufunga mlango, hakuna anayeingia wala anayetoka..

Luka 13:23  “Mtu mmoja akamwuliza, Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache? Akawaambia,

24  Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba WENGI WATATAKA KUINGIA, WASIWEZE.

25  Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;

26  ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

27  Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.

28  Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje”.

Kwanini leo usijitahidi kuingia katika mlango ulio mwembaba???… hao marafiki watakusaidia nini siku ile au watakushauri nini utakapoukosa unyakuo?.. hizo mali zitakutetea vipi wakati huo?… hizo fasheni za kidunia na huo urembo utakupa kibali gani nyakati hizo?… Kumbuka YEYE AJAYE, ANAKUJA WALA HATAKAWIA!!

Ni heri ukayasalimisha maisha yako kwa YESU leo, maana hizi ni nyakati za hatari!.. na muda wowote parapanda inalia!.

Ufunuo 22:20 “Yeye mwenye kuyashuhudia haya asema, Naam; naja upesi. Amina; na uje, Bwana Yesu”

Ikiwa unahitaji kumpokea YESU basi fungua hapa kwa mwongozo >>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

ANAKUJA KAMA “MWIVI” NA SI KAMA “ASKARI” FANYIKA CHOMBO CHA THAMANI.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.

LIITE JINA LA BWANA KATIKA NYAKATI MBALIMBALI ZA MAISHA.

Rudi nyumbani

Print this post

Isaya 40:12 ‘maji kwa konzi ya mkono, na mbingu kwa shubiri’

SWALI: Naomba kufahamu nini maana ya Isaya 40:12 inaposema maji kwa konzi ya mkono, na mbingu kwa shubiri?

Isaya 40:12 “Ni nani aliyeyapima maji kwa konzi ya mkono wake, na kuzikadiri mbingu kwa shubiri, na kuyashika mavumbi ya dunia katika pishi, na kuipima milima kwa uzani, na vilima kama kwa mizani”?


 JIBU: Ukianzia kusoma vifungu vya juu na kuendelea vile vya chini, utaona Mungu anawaambia watu wake Israeli kuwa atawajilia kama mchungaji awachungaye kondoo wake , na kuwalisha, na kuwakuongoza, na kuwakusanya kifuani mwake, hata wale walio wachanga, ndivyo atakavyowatendea watu wake na hilo litawezekana.

Lakini Israeli waliona kama jambo hilo linaweza lisiwe rahisi, Ndio hapo akawaambia sasa katika vifungu vifuatavyo maneno hayo. Kwamba “Ni nani aliyeyapima maji kwa konzi ya mkono wake”? Maji anayoyazungumzia hapo ni maji mengi, mfano wa bahari, na maziwa Je! Kuna mtu yeyote anayeweza kuyakusanya maji mengi namna hiyo kwenye viganja vyake? Jibu ni hapana! Lakini kwa Mungu ni jambo dogo sana.

Vilevile anawauliza ni nani awezaye ‘kuzikadiri mbingu kwa shubiri’?. Shubiri ni kipimo cha urefu, wa kiganja, toka kidole gumba mpaka kile cha katikati vinaponyooshwa. Na ni wazi hakuna mtu anayeweza kupima ukubwa wa mbingu, toka sayari moja hadi sayari nyingine, kwa kipimo chochote kile cha kibinadamu. Lakini kwa Mungu hilo ni jambo dogo sana, ni kama kuzipima kwa shubiri.

Halikadhalika anauliza  ni nani awezaye kuyashika mavumbi ya dunia katika pishi?. Pishi ni kopo dogo, je kuna mwanadamu anaweza kuyakusanya mavumbi yote duniani, kama vile akusanyavyo yale machache kwenye kopo lake. Ni wazi hakuna awezaye kuwa na pipa la uwezo huo.

Vilevile anauliza ni nani anayeweza kuipima milima kwa uzani, na vilima kama kwa mizani?. Je! Kuna mizani yoyote ya kibinadamu inaweza kuiweka milima juu yake, na kutoa vipimo?. Jibu ni hakuna. Lakini kwa Mungu ni jambo dogo sana. Milima ni kama vipunje vidogo sana vya mchanga.

Ikiwa haya yanaonekana magumu kwa mwanadamu, lakini kwa Mungu ni mepesi. Vivyo hivyo jambo la kuwakusanya watu wake, au kuwasaidia, lisitizamwe kibinadamu, kwasababu uweza wa Mungu ni mkuu sana usioweza kufikirika kibinadamu. Maswali ya namna hii ndio kama yale Mungu aliyokuwa anamuuliza Ayubu, (Ayubu 38-41), na katika Mithali 30:4

Yesu kama mchungaji wetu mkuu, anauwezo wa kutukusanya kama kondoo wake. Haijalishi tutaonekana tumetawanyika mbali kiasi gani, lakini akisema jambo ni lazima liwe. Halikadhalika na katika mambo yetu yote ya kiroho na kimwili.

Hivyo kitabu cha Isaya sura ya 40 yote, kinaeleza uweza wa Mungu, usiopomika kibinadamu. Lakini Swali ni Je! Kristo amekusamehe dhambi zako? Kama ni la! Basi nafasi bado unayo leo. Mwamini yeye akuokoe. Na kukupa ondoleo la dhambi zako.

Kwa mwongozo wa namna ya kupokea wokovu basi fungua hapa>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Nini maana ya mbingu na nchi zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe? (Mathayo 24:35).

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)

Kuna Mbingu ngapi?

Mbinguni ni sehemu gani?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya 1Wakorintho 4:7?

SWALI: Naomba kufahamu maana ya 1Wakorintho 4: 7 

Maana ni nani anayekupambanua na mwingine? Nawe una nini usichokipokea? Lakini iwapo ulipokea, wajisifia nini kana kwamba hukupokea?


JIBU: Ukianza kusoma tokea sura ya kwanza utaona Paulo, anakemea sana baadhi ya tabia ya matengano ambayo ilionekana katika kanisa hili la wakorintho. Iliyozuka kutokana na aina ya mafundisho au utendaji kazi wa waasisi wa huduma, au waliowabatiza, na sana sana kati ya Paulo na Apolo.

Hivyo matabaka haya yakawafanya wajivunue wanadamu, na mafundisho yao. Bila kufahamu kuwa kanisa ni la Kristo na si la wanadamu.

Ndipo Paulo, akaweka wazi kuwa kila mmoja aliitwa kwenye utumishi wa Kristo Yesu, ambao una mchango wake katika kanisa, lakini si kwamba huduma ya mmoja ni bora kuliko nyingine. Akasema mmoja anapanda mwingine anatia maji, lakini mkuzaji ni Mungu.

Sasa katika vifungu hivi anaendelea kuwaambia tabia ya kupambanua watumishi, au huduma, si sawa.  Ndio hapo anasema “Nawe una nini usichokipokea?. Akiwa na maana je! Kuna kipawa gani, au kitu gani chema katika kanisa ambacho hawakukipokea kutoka kwa Mungu,?

Lakini anasema..

Iwapo ulipokea, wajisifia nini kana kwamba hukupokea?. Yaani kama vyote vilitoka kwa Mungu na sio kwa wanadamu, mbona basi mnajisifia kana kwamba vimekuja kwa uweza wa kibinadamu?.

Kama tumepewa kwa neema iweje sasa tujisifie, kana kwamba tumevipokea kwa nguvu zetu na utashi wa watumishi wetu, na ukuu wao, na uwezo wao wa kuhubiri vizuri? Karama hizi za rohoni hakuna hata mmoja imetoka kwa mwanadamu, wenyewe wamefanyika vyote tu. Hivyo wa kujivunia hapo na kusifiwa hapo ni Mungu wala si Paulo au Apolo.

Jambo ambalo hata leo huonekana kwa baadhi ya watu wa kanisa la leo. Ikiwa tuna msingi katika Kristo, iweje kujivunia makanisa au huduma, na kujiona sisi ndio bora zaidi ya wale wengine?

Ni kweli zipo huduma ambazo si za kweli, hazina msingi sahihi wa Kristo Yesu. Lakini ikiwa wote Injili yetu ni ya Kristo aliyesulubiwa kutukomboa sisi, basi tofauti za kiutendaji kazi, au kiujuzi, zisitufanye tujione bora, kwasababu sio hao wanadamu walitoa hivyo vipawa bali ni Roho Mtakatifu. Na anatenda kazi kama apendavyo yeye, anampa huyu hiki, anampa Yule kile.

Mmoja atapanda, mwingine atatia maji, mwingine mbolea, mwingine mvunaji, lakini atakuzaye ni Mungu mmoja, katika shina la Yesu Kristo Bwana wetu.

Kama mkristo ukijiona una vita vya kiuhuduma, ujue bado ni mchanga kiroho, bado unatabia za mwilini.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Mwanazuoni ni mtu gani kibiblia?

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

MAUMIVU  NYUMA-YA-HUDUMA.

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Rudi nyumbani

Print this post