Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Fahamu maana ya Mithali 28:20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;
KILA MTU NA AMCHE BABA YAKE NA MAMA YAKE.
MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.
Akaabudu akiegemea kichwa cha fimbo yake.
Waebrania 11:21
[21]Kwa imani Yakobo, alipokuwa katika kufa, akambariki kila mmoja wa wana wa Yusufu, akaabudu akiegemea kichwa cha fimbo yake.
Ulishawahi kujiuliza ni kitu gani Yakobo alikuwa anawaonyesha wana wake siku ile alipokuwa anakaribia kufa.. kitendo cha yeye kusujudu kwa kuegemea kichwa cha fimbo?
Kwanini biblia iseme akaegemea fimbo na sio ukuta, au kitanda au au kiti au isikae tu kimya, bila kueleza chochote?
Yakobo alikuwa na maana kubwa kufanya vile, kwasababu hata alipokuwa akiwabariki watoto wa Yusufu (Efraimu na Manase) alipishanisha mikono..wakidhani kuwa amekosea, akawaambia sijakosea naelewa ninachokifanya, leo ndio tunajua kumbe alikuwa anaunda msalaba, ambao kwa kupitia huo neema inawafikia mataifa kwanza.
Vivyo hivyo na alipokuwa anakufa alisujudu kwa kuegemea kichwa cha fimbo, na huwenda watoto wake walistaajabishwa na kusujudu kule, pengine walijaribu kumwondoa pale ili asujudu vema, lakini akawaambia niacheni naelewa…
Fimbo kibiblia inafunua mamlaka ya mfalme, mchungaji na safari.
Yakobo hakuishi bila tegemeo la mchungaji…udhihirisho Ulikuwa ndio ile fimbo..kwasababu sikuzote alijiona kama kondoo wa Mungu, hakutaka kuiacha fimbo ya mchungaji wake, popote alipokuwepo kwasababu ndio faraja yake.
Daudi alisema…Bwana ndiye mchungaji wangu…gongo lake, na fimbo yake vyanifariji..
Zaburi 23:1-4
[1]BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.
[2]Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
[3]Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
[4]Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.
Kwa ufupi ni kuwa palipo na fimbo ya mchungaji hapo hapo utaona Na kondoo wamejilaza. Yakobo alitembea na Kristo, Mpaka dakika ya mwisho wa maisha yake.
Lakini pia Fimbo inamfunua msafiri…zamani wasafiri walikuwa wanasafiri na fimbo kuwasaidia kutembea..
Wana wa Israeli walipokuwa wanajiandaa na safari ya kutoka Misri, utakumbuka usiku ule walipewa maagizo kila mmoja kushika fimbo yake.
Kutoka 12:11
[11]Tena mtamla hivi; mtakuwa mmefungwa viuno vyenu, mmevaa viatu vyenu miguuni, na fimbo zenu mikononi mwenu; nanyi mtamla kwa haraka; ni pasaka ya BWANA.
Kristo pia alipokuwa anawatuma wanafunzi wake katika ziara za injili aliwaagiza Kubeba fimbo zao..
Marko 6:8
[8]akawakataza wasichukue kitu cha njiani isipokuwa fimbo tu; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni;
Hii ni kutufunulia kuwa Yakobo alikataa kuishi kama mwenyeji duniani.. bali msafiri..
Hivyo alitamani urithi wake ujue jumla ya mwenendo wa maisha yake hapa duniani ulikuwaje..
Hiyo ndio sababu kwanini historia za maisha ya watu kama hawa Mungu kazihifadhi tuzisome hadi leo.
Hata sasa, ujiulize je na Mimi je! fimbo ya mchungaji wangu(YESU KRISTO), ipo pamoja nami? ujiulize je mimi ni msafiri hapa duniani?
Fahamu tu Wazao wote wa Mungu huwakosi na fimbo ya Mungu, hiyo ndio alama yetu.
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Yakobo alimaanisha nini kusema ‘ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu’ Mwanzo 28:21
Kwanini Yakobo alimshinda Mungu, Je! Mungu huwa anashindwa na wanadamu?
Ni kwanini mifugo ya Yakobo iliongezeka kwa wingi kiasi kile?
Biblia inamaana gani inaposema “Mungu wa neema yote”
1 Petro 5:10
[10]Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu.
Tafsiri ya Neema ni kukubaliwa kusikostahili.. au upendeleo usio na sababu. Kwamfano pale mtu anapomwajiri mtu asiye na ujuzi kisha akampa nafasi au mshahara mkubwa wa kiwango cha sawasawa na yule mwenye elimu nyingi na uzoefu..hiyo tunaiita neema.
Hivyo katika ukristo msingi mkuu wa wokovu wetu unategemea neema ambayo ililetwa na Bwana wetu Yesu Kristo(Yohana 1:17).
Yaani Tunakubaliwa na Mungu kuwa sisi tumestahili kuingia katika ufalme wa Mungu na kuwa watoto wake, kwa kumwamini tu Yesu Kristo bila kutegemea matendo yetu wenyewe kama kigezo cha sisi kufikia kiwango hicho.
Neema hiyo hujulikana kama neema ya wokovu. Ambayo ndio neema kuu, iliyomfanya Kristo aje duniani kufa kwa ajili yetu kama fidia ya dhambi ili sisi tuitwe waliostahili. (Waefeso 2:8-9)
Lakini pamoja na hayo Mungu hana mipaka kwamba anatoa neema ya aina moja tu yaani ya wokovu peke yake…hapana anazo Neema nyingi, ambazo zinaingia katika nyanja mbalimbali za maisha ya mwanadamu.
Sehemu nyingine katika biblia huitwa. Neema juu ya neema..
Yohana 1:16
[16]Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema.
Neema hii unamwezesha mtu, kuwa na matokeo katika Huduma na ustahimilivu wote. Ndiyo ambayo Paulo na Barnaba walipewa, iliyowafanya waweze kukichukua kijiti cha injili na kufanikiwa kukipeleka kwa mataifa.
Matendo ya Mitume 13:2
[2]Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.
Mbeleni utaona maandiko yanasema..
Matendo ya Mitume 14:26
[26]Na kutoka huko wakaabiri kwenda Antiokia. Huko ndiko walikoombewa neema ya Mungu kwa ile kazi waliyokwisha kuitimiza.
Hivyo wewe kama mtakatifu ukitaka mafanikio katika huduma au karama yako. Kujifunza kuomba neema ya Mungu katika huduma ni liwe ni sehemu ya maisha yako. Kwasababu hiyo Ipo kukusaidia…Na utapata matokeo ambayo hayategemei zaidi nguvu zako. Ndicho walichokuwa wanakiomba sana mitume.
Matendo ya Mitume 15:40
[40]Lakini Paulo akamchagua Sila, akaondoka, akiombewa na wale ndugu apewe neema ya Bwana. Neema ya kupokea vitu.
2 Wakorintho 9:8
[8]Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;
Kumbukumbu la Torati 8:18
[18]Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.
Hata kupata vitu kiwepesi, hasaa hutegemea neema ya Mungu, kama mkristo ni lazima ujifunze kumwomba Mungu neema ya kufanikishwa, katika mambo yako yote ya kimaisha, isizitegemee tu nguvu zako au akili zako, hata kama jambo ni jepesi vipi, ikiwa ni kazi Omba Mungu akupe neema ya mafanikio, ikiwa ni biashara omba Akupe neema ya kupata Faida Zaidi, ikiwa ni elimu omba Mungu akuongezee akili zaidi.
Zaburi 68:9
[9]Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema; Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu.
Ni sifa ya Mungu kauchilia neema yake kwa watu wake pale wanapochoka huwatia nguvu mpya, wao wenyewe wanashangaa wanainuka tena na kuendelea mbele.. Ndio maana tunasema Mtu anayedumu katika wokovu maisha yake yote, hata anapopitia katika tufani, Pepo na mawimbi, bado hatetereki.. Ni neema ya Kristo inakuwa imehusika hapo kumvusha, si nguvu Zake.
Jifunze kuiomba hii namna ya neema.
Matendo ya Mitume 6:8
[8]Na Stefano, akijaa neema na uwezo, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa katika watu.
Karama za Roho, mfano miujiza, uponyaji, lugha, unabii, utume, uchungaji, n.k, ni vipawa ambavyo hutolewa bure na Roho Mtakatifu, Hakuna jitihada Yoyote ambayo mtu atafanya aweze kukunua nguvu za kumfufua mfu, au kuona mambo ya mbeleni Ayatolee unabii, au kuundoa Ukimwi kwenye damu Ya mtu, isipokuwa kwa neema za Mungu, kutembea na yeye.
Ni neema ambayo tunapaswa tuiombe, ambayo inamfanya Mungu aachilie mafuta mengi ndani yako ya kutembea katika vipawa hivyo, ili kulijenga kanisa.
1 Petro 4:10
[10]kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu.
2 Wakorintho 1:12
[12]Kwa maana kujisifu kwetu ni huku, ushuhuda wa dhamiri yetu, ya kwamba kwa utakatifu na weupe wa moyo utokao kwa Mungu; si kwa hekima ya mwili, bali kwa neema ya Mungu; tulienenda katika dunia, na hasa kwenu ninyi.
Inategemea nguvu ya Mungu (neema), kutembea katika hali ya kutimiza mapenzi yote ya Mungu katika utakatifu… maana yake ni kuwa mwanadamu Akijifunza kumpa Nafasi Roho Mtakatifu ndani yake. Atajaliwa kuishi Maisha yote yampendezayo Mungu, sawasawa na Wagalatia 5:16
2 Wakorintho 8:1-3
[1]Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia;
[2]maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na umaskini wao uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao.
[3]Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao;
Hii ni uwezo wa kutoa vitu/ maisha/ chochote kwa wengine bila kujali nafsi yako mwenyewe.
Jifunze kumwomba Mungu neema ya utoaji. inafaida kubwa sana kwa wengine, kwa binafsi lakini pia katika kukua kwa ufalme wa Mungu.
2 Wakorintho 8:9
[9]Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.
1 Petro 1:13
[13]Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.
Yapo mambo Mengi mema tusiyoyajua, ambayo tutapewa tukifika kule ng’ambo Kristo atakaporudi.. ni mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia, biblia imehitimisha kwa kuyaita “neema”
Je Umepokea neema zote? Lakini zaidi ya yote neema ya wokovu?. Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari leo Yesu akusamehe dhambi zako, basi tawasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya chapisho hili upate msaada huo.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NI MAJIRA YAPI YA NEEMA WEWE UPO?
TAHADHARI YA NEEMA YA MUNGU.
UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?
Swali: Huwa tunasema.. “tusome maandiko” na wakati mwingine “tusome Neno”..ipi tofauti ya maneno haya mawili?.
Jibu: Tuanze na Neno au Neno la Mungu.
“Neno” ni sauti ya MUNGU yenye ujumbe inayokuja kwa mtu kwa njia ya maono au ndoto au njozi..
Kwamfano katika biblia utaona lugha iliyotumika kwa manabii wote waliojiliwa na sauti ya Mungu iliyobeba ujumbe ni hiyo ya “Neno la Mungu”
Mwanzo 15:1 “Baada ya mambo hayo NENO LA BWANA likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.
Soma pia 1Wafalme 17:8, Isaya 38:4, Yeremia 1:11, Ezekieli 1:3, Ezekieli 12:21, Hosea 1:1, Yona 1:1, Mika 1:1, Sefania 1:1 n.k
Hata sisi wakati mwingine tunapotaka kuzungumza na mtu, tunaweza kutumia lugha hiyo kwa kumwambia “nina neno nataka kusema nawe”… au kama kuna mtu amekuambia jambo unaweza kusema “mtu Fulani kaniambia neno”.. kwahiyo ni hivyo hivyo hata katika biblia, Neno la Mungu ni sauti ya MUNGU.
Sasa kama “Neno” tafsiri yake ndio hiyo, vipi kuhusu “Andiko”?
Andiko ni Neno la Mungu lililo katika maandishi… Kwamfano; hilo Neno lililomjia Abramu, kwake yeye ni Neno la Mungu lakini kwetu sisi ni andiko, ndio maana tunalisoma.. Na Nguvu ya andiko na Neno ni ile ile.
Hivyo maneno ya Mungu yote yaliyoandikwa katika Biblia ni “MAANDIKO”.. Hata wewe maneno yako unayoyasema unaweza kuyaandika katika kitabu, na yakawa ni maandiko kwasababu ni maneno yaliyoandikwa.. Hali kadhalika, kila Neno la Mungu kwenye Biblia ni andiko.
Hivyo mtu anayesema “tusome maandiko” na Yule anayesema “tusome Neno la Mungu” ni kitu kimoja.. na nguvu ni ile ile..
Na kila Andiko lenye pumzi ya Mungu linafaa kwa mafundisho, kuonya, kuongoza na kuadibisha..
2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema”
Kwa urefu kuhusiana na kazi ya MAANDIKO inayofanya kwa mtu fungua hapa >>MAMBO MANNE(4) YAFANYAYO NENO LA MUNGU.
Je umempokea YESU?, Umebatizwa katika ubatizo sahihi?..una uhakika Bwana YESU akirudi unaenda naye?.
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?
TUUTAZAME PIA MWISHO WA UJENZI WETU.
ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.
Swali: Katika Mathayo 27:31-32 tunasoma kuwa Simoni Mkirene alimsaidia Bwana kuubeba msalaba wakati anaelekea mahali pa kusulibishwa, lakini tukirudi katika Yohana 19:17-18 tunasoma kuwa hakusaidiwa na mtu badala yake aliubeba mwenyewe mpaka Golgotha, je mwandishi yupi yupo sahihi?.
Jibu: Turejee mistari hiyo..
Mathayo 27:31 “Hata walipokuwa wakitoka, wakamwona mtu Mkirene, jina lake Simoni; huyu wakamshurutisha auchukue msalaba wake.
33 Na walipofika mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa”
Hapa ni kweli Simoni Mkirene alimsaidia Bwana kuubeba msalaba..
Lakini hebu tusome tena Yohana 19:17-18..
Yohana 19:16 “Basi ndipo alipomtia mikononi mwao ili asulibiwe; nao wakampokea Yesu.
17 Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, au kwa Kiebrania, Golgotha.
18 Wakamsulibisha huko, na wengine wawili pamoja naye, mmoja huku na mmoja huku, na Yesu katikati”.
Hapa inaonyesha ni kama hakusaidiwa na mtu mpaka alipofika Golgotha..
Je kwa mantiki hiyo biblia inajichanganya?…
Jibu ni La! Biblia ni kitabu kisicho na makosa wala mkanganyiko mahali popote, isipokuwa fahamu zetu na pambanuzi zetu ndizo zinazojichanganya.
Sasa tukirejea katika habari hizo mbili, ni kwamba Mwandishi wa kitabu cha Yohana (ambaye ni Yohana mwenyewe) alijaribu kueleza safari ya Bwana kwenda Golgotha kwa ujumla, bila kuhusisha matukio madogo madogo yaliyokuwa yanatokea njiani.
Kwamfano utaona yeye kasema tu Bwana alijichukulia msalaba wake mpaka Golgotha, pasipo kutaja matukio kama ya kutemewa mate njiani, au wale wanawake kumlilia na Bwana kuwajibu kwamba wajililie nafsi zao na watoto wao (Luka 13:26-28).. Sasa matukio kama haya Yohana hajayataja lakini haimaanishi kuwa amesema hayapo, la! Bali ni kwamba kafupisha tu habari.. hata wewe/mimi tunaweza kuelezea jambo kwa urefu au ufupi kutegemea na mapenzi yetu.
Lakini sasa tukirudi kwa Mathayo yeye kataja safari ya Bwana kwa urefu kidogo, akihusisha matukio madogo madogo yaliyokuwa yanaendelea njiani katika safari yake..na mojawapo ya tukio ndio hilo la Simoni Mkirene aliyekuwa anatokea shamba na akashurutishwa kuubeba msalaba wa Bwana YESU.
Na utaona pia ijapokuwa Mathayo alirekodi tukio la Simoni Mkirene kumsaidia Bwana msalaba, lakini pia hakutaja tukio la wanawake waliomlilia Bwana njiani, ambapo tukio hilo linakuja kutajwa na mwandishi mwingine wa kitabu kingine ambaye ni Luka..
Luka 23:26 “Na walipokuwa wakimwondoa walimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa ametoka shamba, wakamtwika msalaba, auchukue nyuma yake Yesu.
27 Mkutano mkubwa wa watu wakamfuata, na wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea.
28 Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu.
29 Kwa maana tazama, siku zitakuja watakaposema, Heri walio tasa, na matumbo yasiyozaa, na maziwa yasiyonyonyesha”.
Umeona kwahiyo habari ya Bwana YESU kujichukulia msalaba mpaka Golgotha kama ilivyoandikwa na Yohana haipingani na ile iliyoandikwa na Luka, Mathayo au Marko.. kinachotofautisha habari hizo ni kwamba moja imeandikwa kwa urefu nyingine kwa ufupi.
Je umempokea YESU, je umeubeba msalaba wako na kumfuata?.. Je unajua ni kwanini Simoni Mkirene aliruhusiwa kubeba msalaba nyuma ya YESU?.. ni ufunuo kuwa tukitaka kumfuata YESU ni lazima tubebe msalaba tumfuate YESU nyuma.
Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.
35 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha”.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MANENO SABA YA YESU MSALABANI.
YESU MNAZARETI, ANWANI YA MSALABA.
MSALABA NI ZANA YA UJENZI WA MAISHA YAKO.
Je! Bwana Yesu alisulubiwa juu ya msalaba au juu ya mti uliokuwa wima?
Waefeso 6:16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu
Waefeso sura ya 6, inaeleza mapambano ambayo yapo rohoni kati ya sisi na ufalme wa giza, na namna ambavyo tunapaswa tusimame kushinda vita hivyo, kwa kuvaa zile silaha zote za haki zinazotajwa pale. Kama vile chapeo ya wokovu, dirii ya haki, kweli kiunoni, upanga wa Roho, na ngao ya Imani,.
Lakini pia katika vifungu hivyo tunaelezwa mojawapo ya silaha ya adui, nayo ni “mishale ya moto”. Swali Je hii mishale ya moto ni ipi?
Mishale ni silaha zilizotumika zamani, za kumshambulia adui kwa mbali, na hivyo ili kuziboresha waliweka moto kwa mbele ili zitakapomfikia adui basi zilete madhara zaidi ya yale tu ya kutoboa, bali kuunguza kama sio kumuharibu kabisa adui.
Tofauti na silaha kama rungu, au upanga ambavyo vinahitaji uso kwa uso kutumika. Kwa mbali havina matokeo.
Tukirudi katika ulimwengu wa sasa mishale ya vita ni makombora, Kwanini hapo shetani anaonekana akirusha mishale kutokea mbali? Ni kwasababu kwa karibu hamwezi mwamini, kwani nguvu zilizo ndani yake ni nyingi kuliko alizonazo.
Shetani hutumia sana ulimi kuleta, aidha udanganyifu, mafarakano, vita n.k. Ndio maana maandiko yanasema;
Yakobo 3:5 Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.
6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum.
7 Maana kila aina ya wanyama, na ya ndege, na ya vitambaavyo, na ya vitu vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha kufugwa na wanadamu.
8 Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.
9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu.
10 Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo.
Hawa alidanganywa na Nyoka kwa ulimi, Mafundisho ya uongo, huanzia katika maneno. Hivyo sisi kama watoto wa Mungu ni lazima tuijue silaha hii na kuidhibiti kwanza sisi wenyewe ndani yetu, kuhakikisha hatutumiki kama warusha mishale, kwa kusema yasiyopasa, lakini pia kusimama kwa imani kuhakikisha, tunakuwa thabiti kiimani, kwa kupuuzia, au kutokuweka moyoni kila Neno linalosemwa kinyume chetu, sambamba na kuwa makini kwa kupima kila neno tunaloambiwa kama kweli ni la Mungu au la!.
Mkristo usipojua silaha hii ya adui, utajikuta kila kukicha unaishi kwa machungu ya maneno ya watu, huna raha, una mashindano, au utajikuta unaanguka katika mikono ya manabii wa uongo, na hatimaye shetani anakuwa amekupata.
1Petro 4:12 Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.
13 Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.
14 Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia
Majaribu yote hutoka kwa Yule mwovu, lengo lake ni kumwangusha mwamini ili amwasi Mungu, hata wakati ule Bwana Yesu anakaribia kusulubiwa, alimwombea Petro ili imani yake isitindike, kwasababu alijua wataingia kwenye majaribu makubwa, kwa upungufu wa maombi yao. Vivyo na sisi yatupaswa tuwe waombaji ili tuizime mishale ya majaribu mbalimbali ya adui tusiyojua pembe ipi yanatokea. Na pia tunapojikuta ndani ya hayo majaribu, yatupasa kuishikilia imani yetu hasaa, kwa kuamini kuwa Bwana yupo pamoja nasi kutengeneza njia ya kutokea.
Shetani akijua kuwa hana nguvu ya kumshinda mwamini moja kwa moja, hivyo hupenda kuinua ujasiri wake kama silaha, na akiwa mbali anajua akirusha mishale yake kisha Yule mtu akiiogopa basi anamwangusha. Ndio hapo huleta vitisho, mfano wa kipindi kile cha wana wa Israeli walipopewa agizo la kwenda kumjengea Mungu nyumba Yerusalemu, tunasoma baada ya kipindi kifupi maadui zao wakainuka, na kuwasemelea kwa mfalme, hatimaye marufuku ikatoka, wasiendeleze ujenzi, hivyo mahali pa Mungu pakabaki gofu tu la msingi kwa muda mrefu, kisa hofu ya utalawa mpya. Lakini baada ya muda mwingi sana, tunaona Mungu akawaamsha mioyo Hagai pamoja na Zekaria, na kuwaambia Israeli kwanini wameacha kuijenga nyumba ya Bwana. (Hagai 1:1-9), walipogundua makosa yao, kwa kuruhusu hofu, Ndipo walipoamka kwa ujasiri tena na kuijenga, Mungu akawafanikisha sana.
Vivyo hivyo na sisi, tumepewa agizo la kuhubiri injili, ikiwa itapingwa, au tutatishiwa kuuawa au kufungwa, ikiwa tutapitishwa kwenye miiba au miamba hatupaswi kuogopa mishale hiyo, bali tusimame kwa imani kama akina Shedraki na Danieli, wakiwa katika matanuru ya moto, na matundu ya simba hawakutetereka. Bali walimtumaini Mungu anayewaokoa, na hatimaye kweli ikawa vile.
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba ipo kweli mishale mingi ya moto, ya adui lakini hiyo mitatu ndio mikuu. Na tukiweza kusimama kwa imani basi shetani pande zote anakuwa ameshindwa kabisa kabisa, (Akiwa karibu na vilevile akiwa mbali) linda kinywa chako /puuzia/ pima maneno unayoyasikia, vilevile kuwa mwombaji ili usiingie majaribuni/ uyashinde majaribu, Lakini zaidi sana kamwe usiogope vitisho vya adui, kwasababu hawezi kufanya lolote kwa ihari yake mwenyewe.
Mungu akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi
Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?
Kamwe usifundishe kitu ambacho wewe mwenyewe hukitendi.. Usiwafundishe wengine kumcha MUNGU ilihali wewe mwenyewe uko mbali na MUNGU!.. Usiwafundishe wengine umuhimu wa kuomba ilihali wewe mwenyewe hufanyi hivyo..
Kuna madhara makubwa ya kuwafundisha watu kitu ambacho wewe mwenyewe hukifanyi au hukiwezi.. Katika Biblia walikuwepo Mafarisayo ambao walikuwa wanawatwika watu mizigo ambao wao wenyewe hawakuiweza..
Mathayo 23:2 “Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa;
3 basi, yo yote watakayowaambia, myashike na kuyatenda; lakini kwa mfano wa matendo yao, msitende; maana wao hunena lakini hawatendi.
4 Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao”.
Na tena kitabu cha Warumi kinazidi kuliweka hilo vizuri zaidi…
Warumi 2:21 “basi wewe umfundishaye mwingine, je! Hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kwamba mtu asiibe, waiba mwenyewe?
22 Wewe usemaye kwamba mtu asizini, wazini mwenyewe? Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?
23 Wewe ujisifuye katika torati, wamvunjia Mungu heshima kwa kuiasi torati?
24 Kwa maana jina la Mungu latukanwa katika Mataifa kwa ajili yenu, kama ilivyoandikwa”.
Mitume wa Agano jipya pamoja na Manabii wa agano la kale, hawakuwahubiria watu vitu wasivyoviishi wao, bali waliwafundisha watu yale wanayoyaishi ili wawe vielelezo..
Ezra 7:10 “Kwa maana huyo Ezra alikuwa ameuelekeza moyo wake KUITAFUTA sheria ya Bwana, na KUITENDA, na KUFUNDISHA maagizo na hukumu katika Israeli”.
Hapa Ezra kwanza alianza kwa KUITAFUTA sheria ya Bwana, na AKAITENDA na ndipo AKAWAFUNDISHA wengine.. Ni lazima na sisi tupitie hizi hatua tatu; KUTAFUTA, KUTENDA na KUFUNDISHA.
Tukiiruka ile ya kwanza na ya pili na kuifanya hiyo ya Tatu ya kufundisha, hatutakuwa mashahidi wazuri, na wala ushuhuda wetu hautakuwa na nguvu, tutakuwa ni mashabiki wa injili na si wahubiri wa Injili.. Injili inahubiriwa kwanza katika matendo ndipo mafundisho, hatuwezi kufundisha tusichokitenda!, hapo tutakuwa waongo, au watu wa kutafuta faida zetu.
Bwana YESU atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MWOMBENI BWANA WA MAVUNO APELEKE WATENDA KAZI.
TENDA AGIZO LA YESU, HILO NDIO LITAKALOKULINDA.
MATENDO YETU YANAPIMWA KATIKA MIZANI.
Mtande ni nini? Ni funzo gani lipo nyuma yake?
Utakuwa Kichwa na si Mkia maana yake nini? (Kumbukumbu 28:13).
Jibu: Turejee Matendo
Matendo 16:6 “Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, WAKIKATAZWA NA ROHO MTAKATIFU, WASILIHUBIRI LILE NENO KATIKA ASIA.
7 Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa,
8 wakapita Misia wakatelemkia Troa”.
Biblia haijataja sababu za moja kwa moja kwanini Roho Mtakatifu awazuie wasiingie Asia kuhubiri injili lakini zifuatazo zinaweza kuwa sababu za Roho Mtakatifu kuwazuia Paulo na wenzake wasiingie hiyo miji kuhubiri injili.
1. WAKATI WA INJILI KWA HIYO MIJI ULIKUWA HAUJAFIKA.
Kila mahali pana wakati wake wa kuhubiri injili kulingana na mapenzi ya Mungu, kwamfano kuna wakati ambao injili ilikuwa haijaruhusiwa kuhubiriwa kwa watu wa mataifa isipokuwa wayahudi tu peke yao, na kipindi hiko ni kile ambacho Bwana YESU alikuwa yupo bado duniani.
Mathayo 10:5 “Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akawaagiza, akisema, Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie.
6 Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
7 Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia”.
Maneno hayo ya Bwana Yesu yanaonyesha kuwa wakati wa injili kwa watu wa mataifa ulikuwa haujafika, lakini haikumaanisha kuwa Mataifa hawakuwa katika mpango wa Mungu wa kupokea Injili, walikuwepo lakini muda wao ulikuwa bado haujafika.
Na hapa katika Asia ni hivyo hivyo, huwenda muda wao wa kufikishiwa injili ulikuwa bado.
2. WATUMISHI WENGINE WALIKUWEPO WAKIHUBIRI INJILI.
Kama muda wao wa kupokea Injili ulikuwa umefika na bado Roho Mtakatifu akawazuia akina Paulo kufika miji hiyo, sababu nyingine ni kwamba labda walikuwepo watumishi wengine wakihubiri katika hiyo miji, hivyo hakukuwa na haja ya akina Paulo kwenda huko tena wasije wakajenga juu ya msingi wa wengine kama Neno la Mungu linavyosema katika Warumi 15:20.
Warumi 15:20 “kadhalika nikijitahidi kuihubiri Injili, nisihubiri hapo ambapo jina la Kristo limekwisha kutajwa, nisije nikajenga juu ya msingi wa mtu mwingine”
3. WATUMISHI WENGINE WAMEKUSUDIWA KWENDA KUHUBIRI KATIKA HIYO MIJI.
Na kama hakukuwa na watumishi wengine waliokuwa wanahubiri katika miji hiyo, basi sababu nyingine ya Roho Mtakatifu kumzuia Paulo na wenzake kufika huko Asia huwenda ni kwasababu Roho Mtakatifu alikuwa amepanga/kusudia watumishi wengine ndio wakahubiri kwenye hiyo miji mbali na Paulo na wenzake.
Kikawaida Roho Mtakatifu ndiye anayepanga watu na mahali watakapokwenda..Paulo asingeweza kwenda miji yote peke yake, ni wazi kuwa ipo miji mingine ilikusudiwa kupelekewa injili na watumishi wengine/mitume.
4. WALIIKATAA INJILI.
Hii yaweza kuwa sababu ya mwisho ya Roho Mtakatifu kuzuia injili isiingie Asia kupitia Paulo na wenzake… Inawezekana Roho Mtakatifu alishatanguliza watu huko waliohubiri Neno la Mungu lakini wakaikataa ile injili.. na matokeo yake ni kufungiwa dhambi sawasawa na Yohana 20:22-23..
Yohana 20:22 “Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.
23 Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa”.
Kufungiwa dhambi kunakuja pale ambapo Neno la Mungu linahubiriwa kwa watu na wale watu wanalikataa kwa makusudi na hata kuwaua au kuwafukuza watumishi wa MUNGU, inapotokea wale watumishi wanakung’uta mavumbi kwenye miguu yao na kuondoka hapo wanakuwa wameufungia dhambi ule mji au mtaa, matokeo yake ni kwamba Roho Mtakatifu hawezi tena kupeleka wahubiri hapo mahali, wale watu watabaki vile vile kwasababu walishamkataa Roho Mtakatifu.
Mathayo 10:14 “Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, KUNG’UTENI MAVUMBI YA MIGUUNI MWENU.
15 Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule”.
Tunachoweza kujifunza ni kuwa Injili sio kitu kinachoweza kupatikana kila wakati, upo wakati ambapo Neema ikishaondoka mahali hairudi, au hata ikirudi yaweza kuchukua muda sana, hivyo hatuna budi kuiheshimu sana Neema ya Mungu.
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je Paulo, alihimiza kusikiliza nyimbo za kidunia kulingana na Matendo 17:28
Paulo aliwapaje watu karama ya rohoni?
Je ni sawa kuukubali udhaifu kama mtume Paulo alivyojisifia kwa huo? (2Wakorintho 12:9-10)
Kwanini Paulo, alihukumu wakati hukumu hairuhusiwi?
Paulo alikuwa anamaanisha nini kusema “Mnatenda vema kuvumiliana naye” (2Wakorintho 11:4).
SWALI: Biblia inasema maziwa ni kwa watoto wachanga, lakini chakula kigumu ni cha watu wazima. Mfano wa chakula hichi kigumu ni kipi?
Waebrania 5:12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu. 13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga. 14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya
JIBU:
Kabla ya kufahamu hicho chakula kigumu, ni vema kujua kwanza maziwa ni yapi.
Hivyo ukiendelea kusoma vifungu vinavyofuata anasema..
Waebrania 6:1 Kwa sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu, 2 na wa mafundisho ya mabatizo, na kuwekea mikono, na kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele. 3 Na hayo tutafanya Mungu akitujalia.
Sasa hayo mafundisho ya kwanza ya Kristo ndio maziwa. Yaani Mafundisho ya toba, imani kwa Mungu, ubatizo, kuwekewa mikono, kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele ni mafundisho ya watoto wachanga..kiroho hujulikana kama maziwa..
Kimsingi mtoto akiendelea kunywa maziwa tu peke yake daima, kitakachotokea baadaye ni kudumaa kama sio kufa kabisa, hivyo itafika wakati tu atahitaji chakula kingine ili aendelee kuishi. Vivyo hivyo na sisi, vipo vyakula ambavyo tunapaswa tule, kwa jinsi tunavyoendelea kukua kiroho.
Vifuavyo ndio vyakula vigumu vya kiroho vya watu wazima:
Mathayo 5:44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
Kwanini ni chakula kigumu?. Kwasababu jambo hilo linaenda kinyume na asili ya mwanadamu, linafunua asili ya ndani kabisa ya Kristo, ambayo si rahisi mtu aliyemchanga kiroho, kuielewa, au kulipokea nyakati za mwanzoni, yaani kumwombea na kumpenda Yule ambaye anaiwinda roho yake au aliyemjeruhi, ..
Wafilipi 1:29 Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;
Kwanini ni chakula kigumu?. Kwasababu mwamini mchanga, mara nyingi atapenda kuambiwa maneno ya faraja, baraka, na mafanikio, awapo kwa Kristo, lakini mkristo aliyekomaa, anayaona mapenzi ya Mungu pia hata katika majaribu na kuyashangalia.
1Wathesalonike 3:3 mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo
Soma pia 1Petro 1:6-8, 4:13, Wakolosai 1:24, Luka 6:22-23
Waebrania 5:14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya
Mkristo aliyekomaa kiroho, anafundishwa na Mungu kutambua na kugawanya vema mambo yote, kujua vilivyo najisi na visivyo najisi, mafundisho ya kweli na yale ya uongo, anafundishwa, busara, ujuzi na hekima hata katika kuhubiri injili kwa makundi yote, bila kuanguka na kunajisika, kwasababu amepewa roho ya upambanuzi ambayo huja kwa kuzoeshwa na Mungu kwa kipindi Fulani cha muda kupitia Neno lake.
1Wakorintho 9:20 Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria.
21 Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria. 22 Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.
Soma pia, 1Wakorintho 8:6-13, Yohana 2:1-12, Mathayo 11:19.
Kwanini ni chakula kigumu? Kwasababu mtu ambaye ni mchanga kiroho, akijihusisha katika viwango hivyo, hupotea na kunajisika kama sio kupotea kabisa. Ndicho kilichowatokea Adamu na Hawa kuuvamia mtu wa ujuzi wa mema na mabaya nje ya ratiba ya Mungu, matokeo yake wakayavuna mabaya, wala sio mema.
Katika wokovu ipo fimbo ya Mungu; Mzazi yoyote huwa hatoi zawadi tu, sikuzote, hacheki na mwanawe siku zote, lakini pia kuna wakati fimbo hutumika, Vivyo hivyo Mungu ni Baba yetu, huadhibu, pale tunapokosea..
Waebrania 12:11 Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.
Kwanini ni kigumu? Kukubali marekebisho kwa kuadhibiwa kama sehemu ya kutengenezwa na Mungu, si jambo rahisi mtu kulikubali mkristo ambaye hajakomaa. Yeye atakachojua tu, kuwa Mungu ni upendo.
Luka 9:23 Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.
Kwanini ni chakula kigumu? Aliye mchanga kiroho kukubali kukataa mapenzi , kuingia gharama kuacha vyote na kuyakubali ya Mungu tu, si jambo rahisi kwa mwanafunzi wa ngazi ya chini.
Wafilipi 2:3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.
4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;
8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba
Kwanini ni chakula kigumu?.
Mkristo mchanga kiroho, si rahisi kuangalia mambo ya wengine, mfano wa Kristo, si rahisi kujinyenyekeza na kukubali kutembea kama mtumwa ili kuwatumikia wengine.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Kama mwamini mpya ni lazima ufahamu kuwa kanisa sio jengo, bali kanisa ni watu wa Mungu waliookolewa na kuwekwa pamoja ili kumwabudu Mungu, na kuhudumiana.
1 Wakorintho 12:27
[27]Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.
Kama vile viungo vinavyoshirikiana, vivyo hivyo na wewe huna budi kuwa na ushirika wote wa kanisa, sio kuwa mtembeleaji. Kila mwamini ni kiungo Katika mwili huo.
Waefeso 5:25-27
25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; 26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;
Kristo anataka ujue kuwa unapookoka, unakuwa katika kifungo chake, mfano tu wa mwanamke aliye katika ndoa. Bwana mmoja, mwili mmoja, huku akimtii yeye katika yote. Vivyo hivyo na wewe, tangu huu wakati uliokoka ni wajibu wako, kumtumikia Kristo tu, na kumtii katika yote atakayokuagiza ndani ya kanisa.
Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu”.
Kama mwanafamilia unakuwa na haki ya kupokea na kurithi ahadi zote ambazo Mungu alizoahidi kwa watu wake, kwasababu wewe tayari umeshafanywa kuwa mwana wake.
1Wakorintho 3:16 -17
16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? 17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.
Kwamba ukishaokoka, wewe na waamini wenzako mnaitwa nyumba ya Mungu, hivyo ni wajibu wako kuifanya nyumba hiyo safi sikuzote kwa kuishi maisha ya utakatifu, kwasababu Mungu haishi mahali pachafu, bali pasafi. Wewe ni nyumba ya Mungu, iheshimu nyumba yake.
Kwa kupitia mafundisho, mahubiri, madara ya uanafunzi, uyapatayo ndani ya kanisa, pamoja na madhihirisho mbalimbali ya karama za Mungu, utajikuta unajengeka kwa haraka sana na Matokeo yake utajengwa na kukua kiroho, tofauti Na kama ungekuwa peke yako. (Waefeso 4: 11-13)
Mahali Bora pa kumwabudu, na kumsifu Mungu kwa uhuru na nguvu, ni Pale uwapo katika mkusanyiko. Daudi alisema;
Zaburi 95:6
[6]Njoni, tuabudu, tusujudu, Tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.
Kanisa lina misingi ya maombi na Maombezi. Bwana Yesu alisema;
Yakobo 5:16
[16]Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.
Huwezi kusaidika pale unapoishiwa na nguvu, kama huna jamii ya watu nyuma yako kukushika mkono kimaombi au kihali usimame. Kanisa la kwanza, lilipokusanyika, lilisaidiana katika mahitaji, lakini pia lilitatua migogoro, mbalimbali iliyozuka katikati yao. Hivyo mtu anayekosa kanisa, ukweli ni kwamba anaishi kama yatima wa kiroho.
Kanisa Ni kama karakana ya Mungu inayowaandaa watu, kuwa watendakazi. Ni mahali ambapo utatambua Karama yako. Kisha kuitumia hiyo kuwahudumia wengine na kuipeleka mbele kazi ya Mungu.
Matendo 2:41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali
Mengi kwa jinsi uwezavyo..
Biblia inatuambia tuonyana kila inapoitwa leo (yaani kila siku).
Waebrania 3:13 Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa udanganyifu wa dhambi. 14 Kwa maana tumekuwa washirika wa Kristo, kama tukishikamana na mwanzo wa uthabiti wetu kwa nguvu mpaka mwisho;
Pamoja na hilo, atakatifu wa zamani, ukiachilia mbali makusanyiko ya katikati ya wiki, ilikuwa ni lazima siku ya kwanza ya juma wote wakusanyike. (1Wakorintho 16:2). Yaani kila jumapili ilikuwa ni siku ya Bwana.
Kanisa ni kama Shule kwa mwanafunzi. Tunajua Shule kama Shule sio elimu. Bali shule hutoa elimu. Kwasababu ndani yake wapo waalimu, zipo nidhamu, wapo wanafunzi wenzako , yapo majaribio, Vipo vitabu n.k. ambavyo vinakusaidia Kufaulu vizuri katika masomo yako.
Halikadhalika wewe kama mwamini mpya, ni lazima uwe na kanisa. Mwamvuli wako, ujengwe ukue, uandaliwe. Kanisa ni chombo maalumu alichokiunda Mungu, siku ile ya pentekoste ili watu wake wamwone yeye.
Zingatia sio kila mkusanyiko unaosema ni wa-kikisto ni kweli ni kanisa la Mungu. Kwasababu manabii, na wapinga-Kristo wapo sasa duniani.
> Epuka mikusanyiko isiyo mfanya YESU KRISTO kama ndio msingi, na wokovu wa mahali hapo.
> Epuka mikusanyiko isiyokurejeza katika maisha haki na utakatifu.
> Epuka mikusanyiko isiyokukumbusha juu ya hatma ya maisha yajayo, yaani kuzimu na mbinguni
> Epuka mikusanyiko isiyoamini katika utendaji kazi wa karama za Roho Mtakatifu.
Omba, kwanza, kisha fanya maamuzi.
Ikiwa bado hujawa na uhakika wa pa kukusanyika. Basi wasiliana na sisi tukusaidie mahali sahihi pa kukusanyika..
Vifungu hivi visitoke akilini mwako:
Waebrania 10:25
[25]wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.
Mhubiri 4:9-10
[9]Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.
[10]Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!
Zaburi 122:1
[1]Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa BWANA.
WALA TUSIACHE KUKUSANYIKA PAMOJA
WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU
KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.
KAMA MKRISTO NI LAZIMA UWE NA DESTURI HII.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.