Category Archive Mafundisho

NIONDOLEENI KELELE ZA NYIMBO ZENU (Amosi 5:23)

Amosi 5:23 “Niondoleeni KELELE ZA NYIMBO ZENU; kwa maana sitaki kuzisikia sauti za vinanda vyenu”.

Je ni kwamba Mungu wetu hapendezwi na nyimbo tunazomwimbia??

Jibu ni la! Yeye anapendezwa na nyimbo na tena anaketi katika SIFA.

Zaburi 22:3 “Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za Israeli”.

Lakini kwanini aseme “niondoleeni kelele za nyimbo zenu?”… Ni wazi kuwa kuna nyimbo ambazo kwa Mungu ni kama kelele.

Sasa ni aina gani za nyimbo ambazo kwa Mungu ni kelele?.

1. NYIMBO ZA UNAFIKI.

Nyimbo za kinafiki ni zile mtu anazoimba kwa kupaza sauti, lakini maisha yake hayaendani na kile anachokiimba, kuanzia, uzungumzaji, uvaaji, utendaji na maisha yake yake siri. Mtu mwenye tabia hiyo halafu akasimama na kuimba nyimbo za kumtukuza Mungu, iwe ni nyimbo alizozitunga yeye, au za mwingine, mtu huyo anapiga kelele mbele za Mungu na hivyo anafanya dhambi.

2. NYIMBO ZENYE MIDUNDO YA KIDUNIA.

Kuna nyimbo ambazo zinafanana sana na za kidunia, kiasi kwamba mtu akisikiliza anafananisha na nyimbo Fulani ya kidunia ambayo alishawahi kuisikia mahali fulani. Nyimbo za namna hiyo ni kelele, na si kelele tu, bali pia ni machukizo… mfano wa hizo ni nyimbo aina ya rege, rap, pop, taarabu na nyingine zinazofanana na hizo, Nyimbo za namna hii zinajulikana kama nyimbo za upuuzi (Amosi 6:5). Hivyo wakristo hatupaswi kutumia midundo hiyo kumwimbia MUNGU.

3. NYIMBO ZINAZOSHIRIKISHA WASANII WA KIDUNIA.

Wasanii wa kidunia ni watu wanaoimba nyimbo za zinazotukuza na kusifia mambo ya ulimwengu huu, na ulimwengu upo chini ya shetani, sasa mtu anayewashirikisha waimbaji hao wa kidunia, waliozoea kumwimbia shetani, kisha wakapewa mashairi ya kumsifu Mungu pamoja na watu wa kiMungu, hizo ni kelele na machukizo mbele za Mungu, haijalishi nyimbo hiyo itakuwa na beti nzuri kiasi gani na ujumbe mzuri kiasi gani, au zenye kumsifia MUNGU kwa kiasi gani,  bado ni kelele mbele za Mungu na hazina matunda yoyote.

Nyimbo zenye kumtukuza Mungu ni zile zilizobeba ushuhuda wa Neno kuanzia kwa MWIMBAJI, beti na mdundo. Na zinapoimbwa zinamtukuza Mungu na kuwabariki wasikiao.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAONO YA NABII AMOSI.

WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.

Nini maana ya Mithali 9:13 Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu?

Fahamu maana 1Wakorintho 14:20  “Ndugu zangu msiwe watoto katika akili zenu;

LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.

Rudi Nyumbani

Print this post

NI MAJIRA YAPI YA NEEMA WEWE UPO?

Kuna wakati wa kukokotwa-kokotwa, lakini kuna majira ya  kuachwa ufanye maamuzi mwenyewe, na usipofanya unakufa. Mtu aliye mchanga kiroho, ni rahisi Mungu kuchukuliana naye katika mambo yasiyofaa kutokana na uchanga wake kwa siku zile za awali, lakini haiwezi kuwa hivyo siku zote, kwa jinsi siku zinavyokwenda, kusukumwa sukumwa hakutakuwepo, ni kuwa makini sana!.

Ukitafakari habari ya Mke wa Lutu, unaweza kupata picha halisi jambo hili lilivyo, yeye alidhani ataendelea kuvutwa-vutwa tu nyakati zote, lakini walipofikishwa mahali Fulani, nje kidogo ya mji wameshaijua njia, waliambiwa wajiponye wenyewe nafsi zao, lakini yeye akageuka nyuma, na wakati ule ule akawa jiwe la chumvi.

Mwanzo 19:15 Hata alfajiri ndipo malaika wakamhimiza Lutu, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu. 

16 AKAKAWIA-KAWIA; nao wale watu wakamshika mkono, na mkono wa mkewe, na mkono wa binti zake wawili, KWA JINSI BWANA ALIVYOMHURUMIA, wakamtoa wakamweka nje ya mji. 

17 Ikawa walipomtoa nje, mmoja alisema, JIPONYE NAFSI YAKO USITAZAME NYUMA, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea.

Hatari tuliyonayo sisi tuliopo katika siku hizi za mwisho, katika kanisa hili la Laodikia (Ufunuo 3:14-21), ni kwamba tunafahamu mambo mengi, na tumeshaona mifano mingi kwenye maandiko na kwenye historia, lakini geuko la dhati ndani ya wengi halipo, tukifikiri  tutalinganishwa na wale watu wa zamani. Neema kwako wewe haifanyi kazi katika kukokotwa tena, bali katika kukimbia. Ilifika wakati Yesu hakuwaambia tena wanafunzi wake “nifuate”, aliwaambia na “ninyi mnataka kuondoka?”

Halikadhali, kama umeshaokoka, jichunge sana, dhambi usiifanye rafiki kwako, ukidhani kila kosa tu utakalolifanya upo msamaha, acha hayo mawazo, unajitafutia kuwa mke wa lutu. Neno la Mungu linasema;

Waebrania 6:4  Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

5  na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,

6  wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

7  Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu; 8  bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.

Ni kusimama imara, sio tena kumbelezewa injili, sio tena kukumbushwa-kumbushwa wajibu wako wewe kama mkristo, na kuambiwa kaombe, nenda ibadani, mtafute Mungu, acha anasa, soma biblia. Ni wakati wa kujitambua kuwa sasa umeshatolewa nje ya mji, changamka, zama ndani ya Kristo. Acha kuwa vuguvugu utatapikwa, zama hizi ni zama za uovu. Wokovu wa mawazo mawili sio sasa, neema hiyo haipo kwetu mimi na wewe siku hizi za mwisho. Injili ya maneno laini, isikupumbaze, fanya Imara uteule wako na wito wako.

Ufunuo 22:10  Akaniambia, Usiyatie muhuri maneno ya unabii wa kitabu hiki, kwa maana wakati huo umekaribia.

11  Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa

12  Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

Kimbia, usiangalie nyuma.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! “majira na sheria” mpinga-kristo atakayokuja kubalisha ni kupindua siku ya sabato na kuwa jumapili?

Nini tofauti ya Majira na Wakati?

UMEJIANDAAJE KWA NYAKATI ZA KUWA PEKE YAKO?

WAKATI ULIOKUBALIKA NALIKUSIKIA

Rudi Nyumbani

Print this post

UTAJUAJE UFAHAMU WAKO UMECHUKULIWA?

Swali: Utajuaje ufahamu wako umetekwa au ni viashiria gani vitakavyotambulisha kuwa ufahamu umetekwa na adui?


Jina la Bwana YESU libarikiwe.

Kabla ya kujipima kama ufahamu umechukuliwa au la!..Ni vizuri kwanza tukajua kibiblia mtu mwenye ufahamu anatafsiriwaje?

Turejee kile kitabu cha Ayubu 28:28.

Ayubu 28:28 “Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, kumcha Bwana ndiyo hekima, NA KUJITENGA NA UOVU NDIO UFAHAMU

Kwahiyo kumbe Mtu anayeweza kujitenga na Uovu ndiye mwenye ufahamu…maana yake kinyume chake yule asiyeweza kujitenga na uovu hana Ufahamu…au kwa lugha nyingine “UFAHAMU WAKE UMETEKWA”.

Na hapo neno linasema “kujitenga na uovu” na sio  “kujizuia na uovu”… maana yake “unakaa nao mbali”... Kama ni ulevi mtu anakaa nao mbali, kuanzia mazingira ya kulewa mpaka makundinya walevi (wote anajitenga nao).

Kama ni uasherati na uzinzi, mtu anakaa nao mbali kuanzia mawasiliano, mavazi, makundi…vile vile anajitenga na mazingira yote yanayochochea hiyo dhambi ikiwemo mazungumzo na mitandao.

Kama ni usengenyaji, mtu anajitenga na mazingira hayo na makundi yote..

Kama ni utukanaji vivyo hivyo, Kama ni wizi/ufisadi au utukanaji na hasira ni hivyo hivyo..

Lakini kinyume chake mtu asiyeweza kujitenga na hayo yote basi UFAHAMU WAKE UMECHUKULIWA (UMETEKWA)!!...Upo chini ya Milki ya mkuu wa giza. Anatumikishwa na mamlaka za giza.

Haijalishi kama ni mchungaji, au askofu, au Nabii, au Mtume, au mwimbaji wa kwaya, au Papa, au Raisi wa nchi, au mtu mwingine yoyote mwenye kuheshimika katika jamii au kanisa.

Mtu asiyeweza kujiepusha na UOVU  ufahamu wake haupo (Umefungwa na kamba za kuzimu)., haijalishi ana uwezo mkubwa kiasi gani wa kupambanua mambo ya kimwili, haijalishi ana elimu kubwa kiasi gani na anategemewa na watu wengi kiasi gani katika kutatua mambo…bado ufahamu wake haupo!.

UTAURUDISHAJE UFAHAMU WAKO?.

Hakuna mtu ambaye kwa nguvu ake ana uwezo wa kuurudisha ufahamu wake!… Isipokuwa kwa msaada wa Mungu tu…Na msaada huu unaanza pale tunapoamua kufanya mageuzi katika maisha yetu kwa kutubia dhambi zetu na kumkiri Mwokozi YESU.

Ambapo kama tutatubu kwa kumaanisha kweli basi atatupa kipawa cha Roho wake mtakatifu ambaye kupitia huyo basi ataurejesha ufahamu uliochukuliwa na ile nguvu ya kuushinda uovu na kujitenga nao itakuwa juu yetu.

Faida ya kwanza ya ufahamu wa mtu kurudi ndani yake ni UZIMA WA MILELE lakini pia UZIMA WA MAISHA ya duniani, kwani ufahamu wa roho ndio unaofungua kufahamu mambo mengine yote.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

JE! UNATAKA UITWE MSOMI NA MUNGU?

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, Karibu katika kuyatafakari maneno ya uzima.

Sulemani, mtoto wa Daudi, katika kitabu chake cha mhubiri, kilichojawa na utafiti wa hali ya juu wa mambo mengi ya kimaisha yamuhusuyo mwanadamu, Tunaona mwishoni kabisa mwa utafiti wake alihitimisha kwa maneno haya;

Mhubiri 12:11 “Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; HAKUNA MWISHO WO WOTE WA KUTUNGA VITABU VINGI; NA KUSOMA SANA HUUCHOSHA MWILI. 

13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.

12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili. 

13 Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu”.

Sulemani alikuwa ni mtafiti sana, na kama kusoma na kutunga vitabu, basi alitunga vingi sana, na katika vyote (viwe Vya ki-Mungu na visivyo wa ki-Mungu ) alijaribu kutafuta siri, na mwongozo sahihi wa mwanadamu. Lakini tunaona akapata jawabu, ambalo ni rahisi sana kwa wote. Na jawabu lenyewe ni hili “kumcha Mungu na kuzishika amri zake”.

Akasema unaweza ukakesha kusoma vitabu vingi sana katika huu ulimwengu, na matokeo ya kusoma sana, ni kudhoofika, Na bado usipate ukweli mwingine zaidi ya ule ule “kumcha Mungu na kuzishika amri zake”. Ndio maana akahitimisha kwamba Mtu akizingatia sana hilo, laweza kuzidi usomaji mwingi tuuona hapa duniani.

Sasa kumcha Mungu na kuzishika amri zake maana yake ni nini?

Kumbuka biblia nzima inazungumzia habari za Yesu Kristo mwokozi wetu. Hivyo hapo ni sawa na kusema “Kumcha Yesu na kuzishika amri zake”. Hiyo Ni zaidi ya kuwa na maarifa ya vitabu milioni moja, au elimu za shahada elfu,. Ikiwa na maana yule mtu aliyemwamini Yesu, kisha akawa anaishi kwa kulifuata Neno lake, na kuitimiza amri yake kuu, ambayo alisema ni UPENDO. Huyo ni zaidi ya Msomi yoyote aliyewahi kutokea duniani. Au mtunzi yoyote mwenye hekima aliyewahi kuandika vitabu vingi. Ni mtu aliyemaliza kusoma vitabu vyote.

Yohana 13:34  Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.

35  Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.

Hivyo, usisumbukie maarifa  mengi, ukadhani kuwa ndio utamwelewa Mungu, sumbukia Kristo moyoni mwako, sumbukia upendo wa agape moyoni mwako. Kwasababu huko kote utakapokwenda kutakurudisha hapo hapo, ndicho alichokigundua sulemani katika usomaji wake mwingi, hakuna jipya ndani yake Ni kujisumbua tu, ndio maana biblia inasema, yapo mambo mengi aliyoyafanya Yesu na kama yangeandikwa basi vitabu vyote visingetosha duniani.

Yohana 21:25  Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa.

Umeona? Vitabu visingetosha kuandika mambo yote ya Yesu, kwasababu maudhui yake ndio yaleyale, tunayoyasoma katika maneno machache ya kwenye biblia. Ambayo ni wokovu na Upendo wa Mungu. Tukiyatimiza hayo ni sawa na kusoma vitabu vyote duniani.

Hivyo mimi na wewe tuanze kuweka juhudu, kimatendo, kutendea kazi Neno lake, zaidi ya kuhangaika kutafuta maarifa mengi. Kwasababu anasema mwenyewe chanzo cha maarifa ni kumcha yeye, na sio chanzo cha kumcha yeye ni maarifa.

Kumbuka pia asemapo kusoma kwingi huuchosha mwili, hamaanishi uwe mjinga usiwe msomaji kabisa hapana, Lakini anakupa shabaha ni wapi uweke juhudi zako nyingi ili ufanikiwe kuwa na Maarifa ya kweli ya kisomi, Usije ukawa unaufuata upepo.

Tumia nguvu nyingi kuyatendea kazi yale yaliyopo kwenye biblia tu, zaidi ya mihangaiko mingi huku na kule, na elimu nyingi za kidunia.  Utaitwa Msomi na Mungu.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Uchaji ni nini kama tunavyosoma katika 1Timotheo 2:10?

NI NANI ANAYEUFUNGA MLANGO WA MAARIFA?

Rudi Nyumbani

Print this post

FAHAMU KURUDI KWA YESU KUKO KWA NAMNA NGAPI?

Wengi, tumeshasikia kuwa Yesu atarudi, lakini mpaka mtu anasema atarudi, maana yake ni kuwa alishawahi kuja hapo nyuma. Na kama tunavyojua Bwana wetu Yesu Kristo alikuja mara moja tu, miaka karibu elfu mbili iliyopita, akaishi, akafa,akazikwa, akafufuka, akapaa mbinguni. Lakini wakati wote alipokuwa hapa duniani aliwaahidi wanafunzi wake kuwa atarudi tena.

Hivyo somo hili, ni muhimu kufahamu,  namna ambazo Yesu alisema atarudi, ili usikose maarifa, kwasababu wengi hapa wanakosa shabaha katika kutambua kauli za Yesu. Naomba Soma kwa utulivu somo hili mpaka mwisho.

Sasa kuhusu kurudi kwake duniani, alizungumza katika nyakati tofuati tofauti kurudi kwa namna mbili.

  1. Namna ya kwanza, ni kama Roho
  2. Namna ya pili ni kama Mwizi

Tuangalie kwa undani, namna hizi mbili. Husasani tutailenga hiyo ya pili.

Je! ni kwa namna gani, alirudi kama Roho,Aliwaambia hivi mitume wake;

Yohana 14:18  “Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu. 19  Bado kitambo kidogo na ulimwengu haunioni tena; bali ninyi mnaniona. Na kwa sababu mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai.

20  Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu”.

Soma pia, katika Yohana 16:16, amerudia maneno hayo hayo,

Unaona? Mitume walidhani hawatamwona tena, lakini siku ile aliyopaa mbinguni,siku kumi baadaye, biblia inasema walikuwa wamekusanyika wote mahali pamoja, akawajilia Roho Mtakatifu akawakalia wote, wakajazwa Roho Mtakatifu. Na kama tunavyojua tangu huo wakati na kuendelea, kila mmoja alijua anaye Yesu moyoni mwake, hakuna mtu aliyeuliza Yesu yupo wapi.

Uyatima uliondoka kabisa, kabisa, ndipo wakatambua maana ya yale maneno. Hivyo tumeshaona kurudi kwake kwa kwanza duniani, kulikuja kwa namna hiyo ya Roho Mtakatifu, na mpaka sasa Kristo yupo ndani ya mioyo ya waliomwamini, na kupokea Roho Mtakatifu.

Lakini pia katika maneno yake mengine, alisema atarudi kama mwizi.

Soma,

Mathayo 24:43  Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.

44  Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.

Unaona tena?, Hajasema, atarudi kama askari, au mfanya biashara, bali kama mwizi. Sasa ni vema tujue sifa za mwizi, ni zipi kibiblia, ndipo tuelewe jinsi kurudi kwake kwa namna hiyo kutakavyokuwa.

Ukisoma Yohana 10:10  Yesu anasema hivi;  Mwivi haji ila AIBE na KUCHINJA na KUHARIBU; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele”.

Kumbe mwizi hasaa, anayezungumziwa ni mfano wa jambazi, na sio wale wadokozi, ni wale wanaobeba silaha, ili kuharibu na kuua wanaowaona, wachukue mali yao waondoke.

Na Yesu ndivyo atakavyokuja katika siku za mwisho hizi, atatimiza sifa hizo zote tatu.

1.) Jambo la kwanza Atakuja saa tusiyodhani, Kisha ATAIBA kitu chake cha thamani duniani. Ni hicho si kingine zaidi ya watakatifu wake. Hapo ndio suala la unyakuo linapoibukia.

Mathayo 24:40  Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa; 41  wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.

2) Lakini pamoja na hilo, kuja kwake kutaambatana na KUCHINJA.

Maana yake ni kwamba, kama unyakuo utakupita, dunia itakuwa inajiandaa kuingia katika siku ile ya mapigo ya ghadhabu ya Mungu, ambayo mwisho wake utaishia na Kristo kuonekana katika umbile la kibinadamu kabisa, kuwaua mataifa yote ambayo yatakusanyika kupigana naye katika ile vita kuu ya Harmagedoni.

Ufunuo 19:11  Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

12  Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13  Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14  Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15  NA UPANGA MKALI hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16  Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANAWA MABWANA.

Huu ni wakati ambao Yesu, atauangamiza  ulimwengu, mfano wa mwizi, asiyekuwa na huruma. Usitamani uwepo wakati huo ndugu, ni majuto vilio na kusaga meno.

3) Lakini mwisho kabisa, ATAHARIBU.

Tunafahamu kuwa mwizi, huvunja, mahali ili aingie, huvuruga kila kitu anachokiona, vivyo hivyo na hii dunia itafumuliwa yote, mifumo yote itaangushwa, itafinyangwa upya, yote hayo yatatokea katika siku hiyo hiyo ya Bwana, ambayo itaharibu kila kitu.

2Petro 3:10  Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. 11  Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa, 12  mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka?

Soma pia,(Ufunuo 16:17-21), kuongeza maarifa..

Hivyo ndugu, wakati huu wa Yesu kurudi kama mwizi umekaribia sana, ambao utaanza  Kwanza kwa tukio la unyakuo. Bwana anatutaka sisi tukeshe(rohoni), asitukute tumelala. Ili Siku hiyo isitujilie ghafla, tukabaki hapa duniani.

1Wathesalonike 5:1  Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

2  Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3  Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.

4  Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.

5  Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.

6  Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.

7  Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku. 8  Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.

Bwana atupe macho ya kuona haya.

Je! Umempokea Yesu maishani mwako, Je! Ameziondoa dhambi zako? Kama jibu ni la, unasubiri nini? Hujui kesho kama utakuwepo, hujui kama leo atarudi. Hivyo tubu sasa, mwamini Yeye upate ondoleo la dhambi zako, kisha utapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Ikiwa utapenda kupokea wokovu basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii bure. Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.

KAMA MWIZI USIKU WA MANANE.

Kuna tofauti gani kati ya “Mwivi” na “Mwizi”?

Fahamu Namna ya Kuomba.

Rudi Nyumbani

Print this post

BWANA NITIE NGUVU TENA. (Waamuzi 16:28)

Waamuzi 16:28 “Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili”.

Samsoni haombi kujilipiza kisasi kwaajili ya Nywele zake zilizokatwa, bali kwajili ya “MACHO YAKE MAWILI”.. Maana yake macho yake yalikuwa ni bora kuliko nguvu zake… Laiti angeambiwa achague nguvu ziondolewe na macho yabaki, ni Dhahiri kuwa angechagua macho  yabaki.. Na huo ungeweza kuwa uchaguzi wa kila mtu.

Macho ni Zaidi ya mikono, ni Zaidi ya miguu, ni Zaidi ya nguvu za mwili.. Na ndicho shetani alikitafuta kwa SAMSONI.. Macho yake!!!!… lakini ni jinsi gani angeyatoa?? Inahitajika kuziondoa kwanza nguvu zake za mwili.. Shetani alikuwa haziogopi nguvu za Samsoni, alichokuwa anakiogopa ni macho yake…

Kwani baada ya kumtoa macho alizitumia nguvu zake kusaga ngano za wafilisti…

Na leo hii adui anatafuta macho ya watu kama shabaha yake ya kwanza.. na macho anayoyatafuta si ya kimwili, bali yale ya kiroho..na anaanza kwanza kwa kudhoofisha nguvu za kiroho za mtu na kisha anamaliza kwa kumpofusha Macho ya kiroho … (hapo anakuwa amemaliza kazi!).. na hapo anaanza kumtumikisha kama alivyomtumikisha Samsoni.

2Wakorintho 4:4 “ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.

Lakini habari njema ni kwamba ipo NEEMA kuu juu yetu Zaidi ya ile iliyokuwa juu ya Samsoni. Kwani Samsoni alipomwomba Mungu amrejezee Nguvu zake alirejeshewa kweli na kuwaaharibu maadui zake lakini bado aliendelea kuwa kipofu..

Lakini katika wakati huu wa agano jipya tunaponyenyekea kwa Baba na kuomba msaada, kwa kumaanisha kabisa mbele zake, basi zile nguvu zetu adui alizoziteka zinarejea tena upya na pia macho yetu yanatiwa nuru.. Hiyo ndio faida ya kuwa ndani ya KRISTO.

Je nguvu zako za Kuomba zimeisha???, nguvu zako za kufunga zimeisha??..Nguvu za kumtumikia Mungu zimeisha??…. Kama ndio jua hiyo pia ni dalili ya kupofushwa macho na Ibilisi… Hivyo huwezi kuona mbele wala kutafakari yaliyopita… unahitaji msaada wa Mungu, kwa nguvu zako huwezi!!!

Huu ni wakati wa wewe kunyenyekea kwa Mungu kama Samsoni ili Bwana azirejeshe nguvu zako upya na macho yako yatiwe nuru.

Waamuzi 16:28 “Samsoni akamwita Bwana, akasema, Ee Bwana MUNGU, unikumbuke, nakuomba, ukanitie nguvu, nakuomba, mara hii tu, Ee Mungu, ili nipate kujilipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili”.

Omba kwa kumaanisha, na ikiwezekana funga! Ili Toba yako iwe na nguvu.. Na matokeo utayaona!

Waefeso 1:18  “macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?

KITENDAWILI CHA SAMSONI

UMEFUNULIWA AKILI?

BUSTANI YA NEEMA.

Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?

Rudi Nyumbani

Print this post

MADHARA YA KIBURI KATIKA MAISHA YA MTU.

Kiburi ni hali ya moyo wa mtu kuinuka kutokana na kitu fulani alichonacho, au alichokipata au atakachokipata ambacho kinamtofautisha au kitamtofautisha yeye na mwingine.

Hali hii inamfanya mtu anakuwa na majivuno, dharau na jeuri na asiyetii na hata kukosa staha.

Mtu huyu anakuwa ni mgumu kushaurika, na wakati wote yeye ndio anajiona yupo sahihi  na wengine wote wana kasoro.

Vifuatavyo ni vitu vichache ambavyo vinatengeneza kiburi ndani ya mtu.

1.MALI

Hiki ni kitu cha kwanza ambacho kinatengeneza kiburi ndani ya mtu, na kiburi chenyewe ni “kiburi cha uzima” tunachokisoma katika 1Yohana 2:16.

Hapa mtu anakuwa anaamini anao uzima au maisha kupitia vile alivyonavyo.. Hivyo hahitaji kuambiwa kingine chochote ambacho kitampa yeye uzima, tayari yeye anakuwa anaamini mali alizonazo ndizo jawabu la mambo yote..hivyo hata ukimpelekea Neno la Mungu ambalo ndilo uzima hawezi kukusikiliza…

Na kiburi hiki pia kwa sehemu kipo kwa watu wasio na mali, wanaozisaka wakiamini kuwa watakapozipata zintawapa majibu yote…na hawa ndio wale ukiwapelekea Neno la Mungu wanadharau na kukejeli na kuulizia pesa.

Lakini Bwana YESU alisema kuwa uzima wa mtu haupo katika wingi wa vitu mtu alivyonavyo..(Luka 12:15).

2. ELIMU

Maarifa hususani ya kidunia ni mlango wa pili wa kuzalisha kiburi ndani ya mtu.

Hapa ni pale mtu kapata elimu ambayo ni ya juu kuliko wengi..moyo wake unanyanyuka na kuona wengine wote hawawezi kumzidi akili au uwezo wa kutafakari..

Hivyo anapoletewa Neno la Mungu basi anaanza kumpima yule aliyemletea na anapogundua kuwa ana elimu ndogo ya kidunia kuliko yake, basi hamsikilizi akiamini kuwa atakuwa na upambanuzi hafifu…pasipo kujua kuwa elimu ya mbinguni haipatikani katika shule za wanadamu..kwani hata Mitume wa Bwana Yesu hawakusoma isipokuwa Mathayo tu..lakini leo mafunuo yao tunayasoma na kutusaidia.

3. KIPAWA/KARAMA

Kipawa/kipaji/Karama mtu alichonacho ni mlango wa tatu wa kuzalisha kiburi ndani ya mtu.

Hapa ni pale mtu anapotambua kuwa anao uwezo pengine wa kuimba kuliko wengine, anauwezo wa kufundisha kuliko wengine, ana uwezo wa kutenda jambo fulani kuliko wengine, na badala atumie uwezo huo kujaza pale palipopunguka, kinyume chake anautumia uwezo huo kujisifia au kujionyesha yeye ni bora na hivyo hata kusikiliza wengine au kushawishwa na wengine inakuwa ni ngumu.

4. CHEO/NAFASI.

Cheo au nafasi ni mlango wa nne wa kiburi kuzalika ndani ya mtu..

Hapa ni pale mtu anapopata nafasi fulani katika kanisa, au jamii au kazi…na kuona wote walio chini yake hawawezi kumwongezea chochote.

5. MWONEKANO

Huu ni mlango wa tano ambao unatengeneza kiburi ndani ya mtu..

Hapa ni pale mtu inatokea kujiona anavutia kimwonekano kuliko wengine, na kuamini kuwa yeye ni mzuri/mrembo zaidi ya wote na hakuna wa kumzidi..

Na kiburi hiki kinazalika pale anapopokea maoni ya kusifiwa na mtu mmoja au wawili.. Mtu kama huyu anapotokea mtu mwingine na kutaka kuzungumza naye inakuwa ni ngumu kumsikiliza kwasababu alijiona kama atachafuliwa mwonekano wake.

Sasa yafuatayo ni madhara ya kiburi juu ya mtu kibiblia.

1.Kiburi kinaondoa Neema ya Mungu.

Petro 5:5 “Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema”.

Neema ya Mungu inapokuwa juu ya mtu inamwongezea kibali kwake Mungu na kwa wanadamu…

Mtu mwenye neema ya Mungu tele juu yake, inakuwa ni vyepesi kwake kushinda dhambi tofauti na yule ambaye amepungukiwa neema, vike vile inakuwa vyepesi kwake kufanya jambo likafanikiwa.

2. Kiburi kinamletea mtu Aibu.

Mithali 11:2 “Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu…”

Watu wengi wenye kiburi wanaishia kuabika, kutokana na majivuno yao na dharau zao hivyo mwisho wake huwa hawapati vile wanavyovitafuta na hivyo wanakuja kuaibika baadaye.

3. Kiburi kinaharibu Nyumba

Mzazi mmoja au wote wanapokuwa na kiburi wanaiharibu familia yao wenyewe…

Mithali 15:25 “BWANA ataing’oa nyumba ya mwenye kiburi..”

4. Kiburi kinamshusha mtu chini (kimaisha).

Wote wenye kiburi Mungu anawashusha chini..

Mithali 29:23 “Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa”.

5. Kiburi kitamshusha mtu kuzimu.

Wote wenye kiburi hawataurithi uzima wa milele.

Isaya 2:12 “Kwa maana kutakuwa siku ya BWANA wa majeshi juu ya watu wote wenye kiburi na majivuno, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini……..

17 Na majivuno ya mwanadamu yatainamishwa, na kiburi cha watu kitashushwa; naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo”

Tabia nyingine ya mtu wenye kiburi pia ni mashindano na ubishi

Mithali 21:24 “Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi; Hutenda mambo majivuno ya kiburi chake”.

Mithali 13:10 “Kiburi huleta mashindano tu…”

Jihadhari na kiburi..Na tunajihadhari nacho kwanza kwa kuokoka kisha kujazwa Roho Mtakatifu katika maisha yetu na kujitahidi kwa bidii kukaa mbali na mazingira yote yanayochochea kiburi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kiburi cha Uzima ni nini? (1Yohana 2:16)

MUNGU HUWAPINGA WENYE KIBURI.

Unyenyekevu ni nini?

Babeli ni nchi gani kwasasa?

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

Rudi Nyumbani

Print this post

NA SISI TUTOKE TUMWENDEE NJE YA KAMBI.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, Karibu tujifunze maneno ya uzima.

Katika agano la kale ilikuwa ni sheria, ili sadaka ya upatanisho, au ya dhambi ambayo ilihusisha kafara za wanyama, kuwa kamili, ni lazima uhusishwe na sehemu kuu mbili, ya kwanza ni ndani ya kambi, na ya pili ni nje ya kambi.

Ndani ya kambi au ndani ya lango, ndio ilichukuliwa damu ya mnyama huyo na kuingizwa kwa ajili ya upatanisho kwa kunyunyizwa. Lakini ilikuwa ni sharti pia viungo, ngozi na vinyesi, vya mnyama huyo vikateketezwe mbali nje ya kambi. Na kama jambo hilo lisipofanyika, haijalishi damu ya kunyunyiza ya mnyama  huyo itakuwa ni njema kiasi gani, utapatanisho hauwezi kutokea.

Ndani ya kambi ni mahali patakatifu, lakini je! Ya kambi ni mahali pa uovu.

Sasa tukirudi kwenye agano jipya, tunaona mwokozi wetu Yesu Kristo, anafananisha na mnyawa huyo wa upatanisho, Hivyo ilimbidi, ahusishwe pia na sehemu zote mbili, yaani ndani ya kambi na nje ya kambi.

Alimwaga damu yake, ambayo kwa kupitia hiyo, ameingia nayo  patakatifu pa patakatifu kule mbinguni, kutuombea sisi, Lakini hilo lisingewezekana, kama asingeteketezwa nje ya kambi.

Ndio Hapo tunaona Bwana wetu, ilimpasa, aache enzi na mamlaka mbinguni, (Atoke nje ya kambi), akutane na waovu huku duniani, ateketezwe kabisa mahali pa aibu pa waovu pale Golgota, ili sasa damu yake ipatikane kufanya upatanisho wetu kule mbinguni, kwa Baba ambapo ndio ndani ya kambi.

Na matokeo yake ndio haya tunayoyaona sasa hivi, sote kupata neema na ondoleo la dhambi zetu.

Lakini sasa maandiko yanasema..

Waebrania 13:11  Maana wanyama wale ambao damu yao huletwa ndani ya patakatifu na kuhani mkuu kwa ajili ya dhambi, viwiliwili vyao huteketezwa nje ya kambi.

12  KWA AJILI HII YESU NAYE, ILI AWATAKASE WATU KWA DAMU YAKE MWENYEWE, ALITESWA NJE YA LANGO.

13  BASI NA TUTOKE TUMWENDEE NJE YA KAMBI, TUKICHUKUA SHUTUMU LAKE.

14  Maana hapa hatuna mji udumuo, bali twautafuta ule ujao.

Umeona hapo? Kumbe na sisi, hatuna budi kumfuata Yesu nyayo zake, kwasababu alisema mimi nilipo na mtumishi wangu atakuwepo.  Sasa hapo anasema, na sisi tutoke nje ya kambi, tuchukue shutumu lake. Akiwa na maana, tukubali kujitoa sadaka na sisi, nje ya lango, waovu walipo ili tuwavute wengine kwa mwokozi.

Kama mashahidi  wa kweli wa Kristo, ni lazima tuwe tayari kuhatarisha maisha yetu, kwa ajili ya wengine. Tusiwe tu ndani ya lango, walipo watakatifu, ni kweli ni vizuri kufanya semina za ndani makanisani zina nafasi yake, ni vizuri kuhubiri mikutano ya ndani. Lakini je! Tunaweza tukawa tayari pia kwenda katikati ya watu wa dini nyingine kuwahubiria Kristo, tukawa tayari kwenda mahali pa jamii zenye vita na kuzitangaza habari za Yesu. Kanisa la Kwanza la mitume lilikuwa tayari kutoka nje ya kambi, kukutana na ukinzani wa wayahudi, kuburutwa, kupigwa mawe hata kuawa, walikuwa tayari kuwaendea wapagani sugu, na jamii za wachawi kuwatangazia Kristo. Vivyo hivyo na sisi hatuna budi kutoka nje ya kambi, kuliendea na kundi lingine ambalo halijamjua Kristo.

Hatuna budi kuwa tayari hata kuhatarisha afya zetu, fedha zetu, kazi zetu,  vyeo vyetu, elimu zetu inapobidi ili wengine waokoke, wamjue Kristo. Huko ndiko kutoka nje ya kambi. Bwana Yesu ilimpasa aache enzi na mamlaka juu mbinguni, awaendee makahaba na watoza ushuru, awaendee waliosumbuliwa na ibilisi na mapepo, na sio kwa makuhani na waandishi, ijapokuwa na hao pia alikuja kuwafia, lakini nguvu zake nyingi zilikuwa kwa wenye dhambi.

Bwana atupe neema hiyo.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

UWEZA WA MUNGU NJE YA WAKATI.

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

USIWE ADUI WA BWANA

Rudi Nyumbani

Print this post

Je biblia inajichanganya kwa habari za Yohana kuwa Eliya?

Swali: Tunaona sehemu moja Bwana YESU akimshuhudia Yohana Mbatizaji kuwa yeye ndiye Eliya ajaye (Mathayo 11:14), lakini sehemu nyingine Yohana Mbatizaji anakataa jambo hilo kuwa yeye si Eliya, (Yohana 1:19-21) je ni yupi yupo sahihi, Bwana Yesu au Yohana Mbatizaji?.. au je biblia inajichanganya?

Jibu: Turejee mistari hiyo..

Mathayo 11:13 “Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana.

14  Na ikiwa mnataka kukubali, yeye ndiye Eliya atakayekuja”.

Ni kweli hapa Bwana YESU anasema “Yohana Mbatizaji ndiye Eliya ajaye”. Lakini kumbuka kuwa Bwana YESU hakumlenga Eliya kama Eliya, kwamba atarudi tena na kutokea duniani kuhubiri!.. La! Bali alimaanisha “roho ya Eliya/ huduma ya Eliya” ipo ndani ya Yohana Mbatizaji.

Ni sawa na kwenye ule mfano wa Lazaro na Tajiri Bwana YESU aliowaambia watu, pale Ibrahimu aliposema “Wanaye Musa na Manabii (Luka 16:29)” hakumaanisha Musa yupo sasahivi, bali alimaanisha kuwa watumishi wa Mungu wanaohubiri leo ndio akina Musa..

Hivyo Bwana YESU aliposema Yohana Mbatizaji ndiye Eliya alimaanisha ile roho iliyokuwa inatenda kazi ndani ya Eliya sasa ipo juu ya Yohana Mbatizaji. Sawasawa na ujumbe wa Malaika, aliompa Zakaria baba yake Yohana, kuwa mtoto atakayezaliwa atatangulia mbele za Bwana katika roho ya Eliya, lakini hatakuwa Eliya.

Luka 1:13 “Lakini yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohana.

14  Nawe utakuwa na furaha na shangwe, na watu wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.

15  Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana; hatakunywa divai wala kileo; naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye.

16  Na wengi katika Waisraeli atawarejeza kwa Bwana Mungu wao.

17  NAYE ATATANGULIA MBELE ZAKE KATIKA ROHO YA ELIYA, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, na kuwatilia waasi akili za wenye haki, na kumwekea Bwana tayari watu waliotengenezwa.”

Hapo mstari wa 17 unasema, “Atatangulia katika roho ya Eliya”…na si kwamba atakuwa Eliya mwenyewe yule aliyepaa.. (Yule alishaondoka na hawezi kurudi tena).. Hivyo Yohana Mbatizaji, alijijua kuwa roho ya Eliya inatenda kazi ndani yake, lakini yeye si Eliya, na ndio maana walipomwuliza kama yeye ni Eliya akajibu siye.

Kwanini alijibu vile?..kwasababu ni kweli hakuwa Eliya, isipokuwa Huduma ya Eliya/roho iliyokuwa juu ya Eliya inatenda kazi ndani yake.

Yohana 1:19 “Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani?

20  Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo.

21  Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kuwa Yohana Mbatizaji hakuwa Eliya aliyerudi… bali ni mtu ambaye roho ya Eliya ilikuwa inatenda kazi ndani yake. Hivyo biblia haijichanganyi mahali popote.

Je umeokoka?.. Kama bado basi fahamu kuwa unyakuo wa kanisa upo karibu sana, na Kristo amekaribia kulichukua kanisa lake. Hivyo fanya uamuzi sahihi leo wa kumkabidhi Bwana YESU maisha yako kabla ya ule mwisho.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

YEYE AJAYE ATAKUJA WALA HATAKAWIA.

Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?

Je! ile habari ya Herode kutaka kumwua Yohana mbatizaji inajichanganya?(Mathayo 14:5 na Marko 6:20).

ROHO YA ELIYA KATIKA AGANO JIPYA INATENDAJE KAZI?.

YOHANA MBATIZAJI

Rudi Nyumbani

Print this post

Je Bwana YESU alimjibu Pilato au hakumjibu? Je biblia inajichanganya?

Swali: Je biblia inajichanganya kwa habari ya Bwana YESU kumjibu Pilato? Maana katika (Yohana 18:33-34) inasema alimjibu lakini katika (Mathayo 27:13-14)..  inasema hakujibu chochote alipoulizwa? Je lipi ni sahihi?


Jibu: Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa biblia haijichanganyi mahali popote pale, isipokuwa kinachojichanganya ni tafakari zetu, na fahamu zetu… Lakini biblia ni kitabu kikamilifu na kilichovuviwa na Roho Mtakatifu wa Mungu, hivyo hakina kasoro yoyote.

Sasa tukirejea habari hiyo katika Yohana 18:33-37.

Yohana 18:33 “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?

34  Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?

35  Pilato akajibu, Ama! Ni Myahudi mimi! Taifa lako na wakuu wa makuhani ndio waliokuleta kwangu. Umefanya nini?

36  Yesu akajibu, Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa.

37  Basi Pilato akamwambia, Wewe u mfalme basi? Yesu akajibu, Wewe wasema, kwa kuwa mimi ni mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu”

Hapa ni kweli tunasoma Bwana YESU alimjibu Pilato alipoulizwa kuhusu habari zake mwenyewe… Lakini tukirejea kitabu cha Mathayo ni kama tunasoma habari tofauti kidogo.

Mathayo 27:11 “Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, WEWE WASEMA.

12  Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno.

13  Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia?

14  Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana”.

Hapa tunasoma Bwana YESU hamjibu Pilato.. Sasa swali je! Biblia inajichanganya??..Jibu ni la! Haijichanganyi.

Tukisoma vizuri habari hizo mbili zinaelezea kisa kimoja lakini katika mazingira manne tofauti..

  1. Mazingira ya Kwanza:

Wakati Bwana anafikishwa kwa Pilato, alitangulia liwali kumhoji Bwana YESU kama yeye ndiye mfalme wa Wayahudi hapo alijibu “wewe wasema (maana yake ndio mimi ndiye)” Huyo ni Liwali anahoji na anajibiwa na Bwana bila maficho yoyote.

Mathayo 27:11 “Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, WEWE WASEMA…”

  1. Mazingira ya pili:

Lakini wakati ambao Wazee wa makuhani wanamshitaki Bwana YESU kwa Pilato yeye hakujibu chochote..

Kumbuka hapa wazee wa makuhani hawakuwa wanamhoji kuhusiana na swali alilouliza Liwali kwamba kama yeye ni mfalme wa Wayahudi…LA! Bali wazee wa makuhani wenyewe walikuwa wanamshitaki kwa mambo mengine ikiwamo habari ya kulivunja hekalu pamoja na kujiita mwana wa Mungu.. Soma Mathayo 26:62-68..Na sasa wanataka wamsikie Bwana YESU akijitetea mbele ya Pilato. Lakini Bwana YESU hakujibu chochote.

Mathayo 27:12  “Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno”.

  1. Mazingira ya tatu:

Pilato aliposimama na kumwuliza Bwana YESU ajitetee, mbele ya wazee wa makuhani kuhusiana na mashtaka hayo (ya kulivunja hekalu na kujiita mwana wa Mungu).. yeye hakujibu chochote mpaka Liwali akashangaa!!..

Mathayo 27:13 “Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia?

14  Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana”

Na kwanini Bwana YESU hakumjibu hapa Pilato lolote?.. JIbu ni kwasababu Wazee wa Makuhani ambao waliokuwa ni wanafiki walikuwepo pale wakitafuta neno litokalo kinywani mwake ili waanze kuzusha maneno mengi juu yake..hivyo Bwana hakumjibu Pilato wala makuhani.

  1. Mazingira ya nne

Pilato alipoona hapati jibu lolote kuhusiana na mashtaka ya wayahudi juu ya Bwana.. alimchukua Bwana YESU ndani ya Praitorio na kumwoji akiwa peke yake swali lile lile aliloulizwa na Liwali! (Je wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi?)..na Bwana YESU akampa jibu kama lile lile alilompa Liwali.

Yohana 18:33  “Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?

34  Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?…”

Umeona?… Kwahiyo biblia haijichanganyi yenyewe.. Ni kwamba Bwana YESU hakujibu mashtaka ya Wazee wa Wayahudi lakini alijibu maswali ya Pilato na Liwali.

Na kwanini Bwana YESU asijibu mashtaka ya wazee wa makuhani? Na amjibu Liwali pamoja na Pilato peke yao?…ni kwasababu wale wazee walikuwa wamemkusanyikia kwa shari, wapate kumwongezea dhiki….

Maswali yao si ya lengo la kutaka kujua, bali kutafuta sababu za kumshitaki..kwani tayari alishawajibu huko nyuma lakini bado waliendelea kumtafuta kwa maswali mengine mengi (Mathayo 26:62-68).

Kwahiyo na sisi tunachoweza kujifunza ni utulivu na kunyamaza katika vipindi ambavyo adui anatumia vinywa vya watu kutujaribu.. Ukishajibu swali mara ya kwanza, na mtu haelewi badala yake anatafuta tu kasoro, basi kinachofuata baada ya hapo ni kukaa kimya.

Kwasababu yapo maswali ambayo ukijibu hayatamsaidia yule anayeuliza badala yake yatampa kila sababu za kukusumbua wewe ziaidi, kwasababu lengo lake si kutaka kujua bali ni kubishana au kukudhuru wewe au kukushambulia. Hivyo ni muhimu kuwa makini.

Tito 3:9  “Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana.

10  Mtu aliye mzushi, baada ya kumwonya mara ya kwanza na mara ya pili, mkatae”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini maandiko yanajichanganya yenyewe kwenye habari ya Paulo alipotokewa na Yesu alipokuwa anakwenda Dameski?

Habari ile ya Pilato kuchanganya zile damu za wayahudi na pamoja na dhabihu zao,(Luka 13) ilihusu nini?

NENO LA MUNGU NI UFUNUO MKAMILIFU.

Liwali ni nani?

UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.

Rudi Nyumbani

Print this post