Category Archive Mafundisho

NYUMBANI MWA BABA YANGU MNA MAKAO MENGI.

Bwana Yesu karibu na kuondoka alizungumza maneno haya;

Yohana 14:1  Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.

2  Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.

3  Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.

Kwa mara ya kwanza anawafunuliwa wanafunzi wake, kuhusu mambo yaliyo kwa Baba yake tuliyoandaliwa sisi. Na hapo anasema huko kuna “makao mengi”. Hasemi kuna “kao”kana kwamba ni moja, bali “makao” tena mengi.. Hatujui idadi labda ni mia, au elfu, au milioni, au bilioni. Yesu kusema mengi, amini ni mengi kwelikweli.

Ndio maana kumaliza mambo mema Mungu aliyotuandalia inahitaji umilele.

Sasa kibiblia tumepewa kuyajua makao ya aina tatu tu.

Moja, alituletea tayari, Lakini Mengine mawili yatakuja baadaye.

Kao la kwanza: Lilikuwa ni yeye kutukaribisha ndani yake.

Hilo lilitimia muda mfupi sana, baada ya kuondoka, Tunaona baada ya siku 10, siku ile ya pentekoste, alirudi tena juu yetu kama Roho Mtakatifu. Akaingia ndani yetu, Kwa mara ya kwanza sisi ndio tulipokea mahusiano binafsi ya moja kwa moja na Mungu, tukaingia nyumbani mwake.

Matendo 2:1  Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.

2  Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.

3  Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.

4  Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.

Mtu aliye na Roho Mtakatifu, huishi tofauti na mtu ambaye hana Roho. Kwasababu ulimwengu wake ni mwingine kabisa na ule wa kwao, Kao lako ni kuu zaidi ya kao lao la kidunia. Raha na pumziko analolipata, walimwengu hawawezi kulipata. Hekima na upeo ulionao wewe,wale hawana, Hakika kao hili ni zuri sana. Unapojazwa Roho vema, ndio unaona uzuri wa kao hilo maishani mwako.

Kao la pili: Ni kao la roho zetu.

Kumbuka roho hizi zipo ndani ya miili hii ya mavumbi. Lakini Yesu aligundua udhaifu wa miili hii hivyo, alikwenda kutundalia miili ya utukufu itokayo juu, ambayo hiyo tutavishwa, siku ile ya unyakuo itapofika, miili ambayo haijatengenezwa kwa malighafi za duniani, bali zile za kimbinguni. Miili isiyozeeka, isiyougua, isiyo sikia njaa, wala isiyokufa. Haleluya. Ni kao zuri ambalo hakuna hata mmoja wetu anapaswa alikose.

2Wakorintho 5:1  Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele mbinguni.

2  Maana katika nyumba hii twaugua, tukitamani sana kuvikwa kao letu litokalo mbinguni;

3  ikiwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tu uchi.

4  Kwa sababu sisi tulio katika maskani hii twaugua, tukilemewa; si kwamba twataka kuvuliwa, bali kuvikwa, ili kitu kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima.

Kao la Tatu: Ni mazingira mapya ya watakatifu, ndio ile mbingu mpya na nchi mpya.

Na ule mji wa kimbinguni, Yerusalemu mpya ishukayo kutoka juu kwa Baba. Uzuri ulioko huko hauna kifani. Ni mji unawaka na kumeta-meta utufukufu wa Mungu.

Ufunuo 21:15  Na yeye aliyesema nami alikuwa na mwanzi wa dhahabu, apate kuupima huo mji, na milango yake, na ukuta wake.

16  Na ule mji ni wa mraba, na marefu yake sawasawa na mapana yake. Akaupima mji kwa ule mwanzi; ulikuwa kama maili elfu na mia tano; marefu yake na mapana yake na kwenda juu kwake ni sawasawa.

17  Akaupima ukuta wake, ukapata dhiraa mia na arobaini na nne, kwa kipimo cha kibinadamu, maana yake, cha malaika.

18  Na majenzi ya ule ukuta wake yalikuwa ya yaspi, na mji ule ulikuwa wa dhahabu safi, mfano wa kioo safi.

19  Na misingi ya ukuta wa mji ilikuwa imepambwa kwa vito vya thamani vya kila namna. Msingi wa kwanza ulikuwa yaspi; wa pili yakuti samawi; wa tatu kalkedoni; wa nne zumaridi;

20  wa tano sardoniki; wa sita akiki; wa saba krisolitho; wa nane zabarajadi; wa kenda yakuti ya manjano; wa kumi krisopraso; wa kumi na moja hiakintho; wa kumi na mbili amethisto.

21  Na ile milango kumi na miwili ni lulu kumi na mbili; kila mlango ni lulu moja. Na njia ya mji ni dhahabu safi kama kioo kiangavu.

22  Nami sikuona hekalu ndani yake; kwa maana Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo, ndio hekalu lake.

23  Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-Kondoo.

24  Na mataifa watatembea katika nuru yake. Na wafalme wa nchi huleta utukufu wao ndani yake.

25  Na milango yake haitafungwa kamwe mchana; kwa maana humo hamna usiku.

26  Nao wataleta utukufu na heshima ya mataifa ndani yake.

27  Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo

Haya ni matatu tu! Vipi kuhusu hayo mengine ambayo hatujafunuliwa? Ukiyajua hayo, hutauchukulia wokovu kirahisi-rahisi, utafanya bidii uingie ndani ya Kristo. Mfuate Kristo akupe uzima wa milele. Ikiwa upo tayari kuokoka leo, basi wasiliana  nasi kwa mawasiliano unayoyapata mwisho wa makala hii, bure

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

Nini maana ya Mithali 19:21Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.

Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.

TUMAINI NI NINI?

Rudi Nyumbani

Print this post

UKWELI KUHUSU UISLAMU, Sehemu ya Tatu: Kisima cha Zamzam.

Kisima cha Zamzam ni nini, na ukweli wake ni upi?


Angalizo: Makala hii haina lengo la kushambulia Imani Fulani, wala kushabikia Imani Fulani, pia haina lengo la kumchafua mtu yoyote, wala kumdhalilisha, bali kutoa elimu sahihi kuhusiana na tunayoamini na yanayoaminiwa.


Kisima cha “Zamzam”, ni kisima kilichopo katika msikiti wa Al Haram uliopo Makka, katika nchi ya Saudi Arabia. Kisima hiki kipo umbali mfupi kutoka katika jiwe/jabali jeusi la Kaaba. (umbali wa mita 20 mashariki mwa jiwe hilo).

Kulingana na Uislamu, kisima hiko kilijitokeza hapo kimiujiza kipindi kile Hajiri kijakazi wa Sara alipoachwa na Abramu katika lile jangwa (katika vilima vya Safa na Marwah) na akakosa maji ya kunywa yeye na mwanae Ismaili.

Na Hajiri alipoona mwanae anakaribia kufa, akaanza kuzunguka vilima hivyo vya Safa na Marwah mara saba, na alipokuwa katika mzunguko wa saba, ndipo Malaika Jibra’il (Gabrieli) akatokea na kukitokeza kisima hiko kimiujiza na kilipotokea, Hajiri akaanza kusema zamzam, maana yake “acha kutiririka”

Hadithi za kiislamu zinazidi kusema kuwa kisima hiko kilikauka, lakini kikaja kuvumbuliwa tena na babu yake Muhamad aliyeitwa Muttalib katika karne ya sita(6).

Lakini pia binamu yake Muhamad aliyeitwa “Ibn Abbas” alisema “Maji ya zamzam yanafaa kwa nia yoyote ile, mtu akinywa kwa lengo la kupona ugonjwa basi mungu atamponyesha kupita maji hayo, kama mtu atakunywa kwa lengo la kuondoa njaa, basi mungu ataiondoa njaa yake, kama mtu atayanywa kwa lengo la kukata kiu basi mungu ataikata kiu yake kwasababu hata Ismail alikunywa maji hayo na kukata kiu yake kali”.

Na kwasababu hiyo maelfu ya watu wanayatumia maji hayo wakiamini yamebeba uponyaji wa kimungu ndani yake??. (Je ukweli wa mambo haya ni upi)?

Awali ya yote tufahamu kuwa Ishamaeli, mwana wa Hajiri hakuwa mwana wa Ahadi kulingana na biblia, hali ISAKA, mwana wa Sara ndiye aliyekuwa mwana wa Ahadi.  Hadithi zote zilizopo na zinazotungwa zinazoshinikiza kuwa Ishamaeli ndiye mwana wa Ahadi, si za kweli.

Ishmaeli aliahidiwa Baraka nyingine za Mungu lakini si za Mzaliwa wa kwanza. Baraka za mzaliwa wa kwanza zilikuwa kwa Isaka aliyekuwa mwana wa Sara.

Sasa ukweli wa kisima hiko kibiblia ni upi na je kuna muujiza wowote katika kisima hiko?

Habari ya kisima hiko, ambako biblia haisemi kwamba kinaitwa “Zamzam” inapatikana katika kitabu kile cha Mwanzo 21, Hebu tuianzie ile habari mbali kidogo katika ule mstari wa 9 ili tuielewe habari..

Mwanzo 21:9 “Sara akamwona yule mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alimzalia Ibrahimu, anafanya dhihaka.

10 Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka.

11 Na neno hilo lilikuwa baya sana machoni pa Ibrahimu, kwa ajili ya mwanawe.

12 Mungu akamwambia Ibrahimu, Neno hili lisiwe baya machoni pako, kwa ajili ya huyo mwana, na huyo mjakazi wako. Kila akuambialo Sara, sikiza sauti yake, kwa maana katika Isaka uzao wako utaitwa.

13 Naye mwana wa mjakazi nitamfanya kuwa taifa, maana huyu naye ni uzao wako.

14 Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba.

15 Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja.

16 akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, akapaza sauti yake, akalia.

17 MUNGU AKASIKIA SAUTI YA KIJANA. MALAIKA WA MUNGU AKAMWITA HAJIRI KUTOKA MBINGUNI, AKAMWAMBIA, UNA NINI, HAJIRI? USIOGOPE, MAANA MUNGU AMESIKIA SAUTI YA KIJANA HUKO ALIKO.

18 ONDOKA, UKAMWINUE KIJANA, UKAMSHIKE MKONONI MWAKO, KWA KUWA NITAMFANYA KUWA TAIFA KUBWA. 

19 mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana.

20 mungu akawa pamoja na huyo kijana, naye akakua, akakaa katika jangwa, akawa mpiga upinde.

21 akakaa katika jangwa la parani; mama yake akamtwalia mke katika nchi ya misri”.

Sasa kulingana na maandiko hayo matakatifu, ni Dhahiri kuwa Ishmaeli (au Ismail), hakuwa mwana wa ahadi ndio maana aliondolewa katika hema ya Sara, na Mungu alikuwa upande wa Sara. Lakini kwasababu Mungu ni wa rehema asingeweza kumwacha kabisa Hajiri na Ishamaeli kwani nao pia ni uzao wa Ibrahimu, ndio maana akawaokoa na mauti katika jangwa lile lisilo na maji.

Na utaona Malaika wa Mungu alimfumbua macho Hajiri ili akione kisima, na si kwa “alikitokeza kisima kile kimiujiza”.. Maana yake ni kwamba kisima kile tayari kilikuwepo pale, isipokuwa macho ya Hajiri hayakukiona, na yalipofumbuliwa ndipo akakiona na kumshukuru Mungu.

Sasa swali la Msingi ni hili, je kisima hiko kiliendelea kuwepo?, na je Mungu aliagiza chochote juu ya kisima hiko, kwamba watu waende huko kuchota maji yake?

Jibu ni kwamba kisima hiko kiliendelea kuwepo, kwasababu kilikuwepo kabla ya hapo pia!..na ulipofika wakati kilipotea kama tu visima vingine vilivyopotea… Na wala maji yake hayakuwa na muujiza wowote kwa Ishmaeli Zaidi ya maji mengine yoyote.

Yale yalikuwa ni maji ya kawaida tu, ambayo mtu akinywa anakata kiu, na ndilo lililokuwa lengo la Mungu, kwa Hajiri na Ishmaeli, kwamba wanywe wakate kiu basi, waweze kuokoka na mauti ya kukosa maji, na si kwamba wakifanye kuwa kisima kitakatifu cha kufanyia ibada.

Sasa kulingana na hadithi za kiislamu, wanakiri kuwa kilipotea hiko kisima, lakini ajabu ni kwamba kimekuja kugunduliwa na kufukuliwa karne ya 6, (Jambo hilo si kweli, ni uongo wa adui).

Huenda hiko kisima kilichopo sasahivi ni kisima tu kilichoibuliwa na watu, na zaidi hata kama kingekuwa ni chenyewe (halisi) kile alichoonyeshwa Hajiri na Malaika, kisingekuwa na Uungu wowote ndani yake kwani Mungu hajawahi kuweka agano lake katika visima! Au mito au bahari.

Ingekuwa ndivyo basi ule mto Yordani ambao Naamani-Mkoma aliokwenda kuoga mara saba na ukoma wake kuondoka basi hata leo wakoma na wagonjwa wangetiririka pale kuoga ili kupona magonjwa yao…

2Wafalme 5:9 “Basi Naamani akaja na farasi wake na magari yake, akasimama mlangoni pa nyumba ya Elisha.

10 Naye Elisha akampelekea mjumbe, akisema, Enenda ukaoge katika Yordani mara saba, na nyama ya mwili wako itakurudia, nawe utakuwa safi………………

14 Ndipo akashuka, akajichovya mara saba katika Yordani, sawasawa na neno lake yule mtu wa Mungu; nayo nyama ya mwili wake ikarudi ikawa kama nyama ya mwili wa mtoto mchanga, akawa safi”.

Sasa huo ni mto Yordani ambao mpaka leo upo! Na ndio mto Bwana YESU aliobatizwa na Mbingu zikafunuka juu yake kumshuhudia.. Lakini maji yake leo hayawezi kutumika kama maji ya kiungu.. Vipi hayo mengine?.

Na pia kisima hiko cha Hajiri hakikuwepo Saudi Arabia, bali kilikuwepo Parani katika jangwa la Sinai.

Kwahiyo maji hayo ya zamzam, yanayotoka huko Saudi Arabia, (Makka), si maji ya kiungu na  mkristo/asiye mkristo hapaswi kuyatumia kwa matumizi yoyote, matokeo ya kutumia maji hayo kwa lengo la kupata uponyaji, au utatuzi wa tatizo lingine lolote ni KUONGEZA TATIZO HILO!.

Inasadikika pia maji haya yanatumika katika baadhi ya misiba, (yanatiwa katika vyakula vya misibani), na katika baadhi ya vyakula vya biashara, na matumizi mengine,

Ikiwa unahudhuria mazishi yoyote yale (yawe ya kikristo au sio ya kikristo), hakikisha unatakasa vyakula vyote kwa Imani kwa damu ya YESU kabla ya kula!.. Usile tu!..Vile vile kila ununuacho kama bidhaa ya chakula, pasipo kujua asili ya utengenezaji wake, kabla ya matumizi, takasa kwa Imani kwa damu ya YESU.

Lakini si maji ya zamzam tu yenye shida kiroho, bali pia na maji yajulikanayo kama “ya upako yauzwayo katika baadhi ya makanisa”..yote yanabeba sifa moja na haya ya ZAMZAM.

Ukiona maji yanauzwa kwa kivuli cha upako, kwamba uyatumiapo utapata uponyaji au ufunguzi!, kuwa makini sana!.

Watumishi wa kweli wa Mungu, wanatumia maji kwa uongozo maalumu wa Roho Mtakatifu, na si kama utaratibu au mwenendo wa mara zote, kwamba kila tatizo ni maji na tena yanauzwa!, na tena yanaaminishwa kuwa ndio kitu kiponyacho!, hayo ni mafundisho ya ibilisi, ambayo ni muhimu kuwa nayo makini!.

Ukikuta maji yanauzwa usinunue!, ukikuta mafuta yanauzwa usinunue!..Ibilisi ni yule yule, anayefanya kazi kwenye kila kitu kilicho kinyume na Neno la Mungu.

Usikose Makala zijazo…

Je umempokea YESU kama Bwana na Mwokozi wa maisha yako?..kumbuka yeye pekee ndiye Njia ya kufika mbinguni, na si mwanadamu yoyote aliye hai au aliyekufa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UKWELI KUHUSU UISLAMU Sehemu ya kwanza: (Msikiti wa AL-Aqsa).

HAJIRI NI KAMA MLIMA SINAI ULIOKO ARABUNI.

JE! NI CHEMCHEMI IPI INATOKA NDANI YAKO, YA MITO AU YA KISIMA?

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

Rudi Nyumbani

Print this post

KILINDI CHAPIGIA KELELE KILINDI.

Zaburi 42:7

[7]Kilindi chapigia kelele kilindi kwa sauti ya maboromoko ya maji yako, Gharika zako zote na mawimbi yako yote yamepita juu yangu.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tutafakari pamoja Neno la Mungu.

Biblia inatuambia kila jambo tunalolifanya lina matokeo sawa rohoni. Ikiwa wewe ni mwizi malipo ya wizi utayapata rohoni, ikiwa wewe ni muuaji, malipo ya uuwaji utayapokea vilevile rohoni, mito ya maji inapoelekea huko huko ndipo inaporudia.

Ufunuo 13:10

Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye subira na imani ya watakatifu.

Sasa hapo tumeona katika eneo la ubaya, je vipi katika upande wa Mema?

Maandiko hayo hayo yanatuambia kwamba Kilindi hupigia kelele kilindi.

maana yake ni nini?

kilindi ni mahali pa katikati kabisa mwa bahari. Sasa mwandishi wa zaburi  anatumia mifano ya kitu halisi kana kwamba kinaongea… anasema Kinaita chapigia kelele kilindi. Na cha kushangaza ni kwamba hakiiti eneo lingine lolote la maji labda ufukweni.. au kwenye rasi, au ghuba.. hapana bali kinapigia kelele kilindi chenzake.

Kilindi chapigia kelele kilindi

Maana yake ni nini?

Tukitaka mambo ya ndani ya Mungu, mambo ya vilindini, lazima na sisi tuwe vilindini. Ni muunganiko wa ki-Mungu. kila kiwango kina sauti yake. kamwe hizo sauti haziingiliani, ni sawa na mbwa amwite tai kwa sauti yake ya kubweka, haiwezekani kuja inahitaji, ajifunze sauti yake ili yule tai aelewe, vinginevyo atakuwa anapiga kelele tu.

Na sisi vivyo hivyo kwa Mungu, wengi tunatamani tumwone Mungu kwa undani katika maisha yetu, lakini hatutaki tuzame ndani yake.

Mwandishi wa Zaburi mwanzoni kabisa kabla hajasema maneno hayo kwenye hiyo sura 42 anasema

Zaburi 42:2-3

[2]Nafsi yangu inamwonea kiu MUNGU, Mungu aliye hai, Lini nitakapokuja nionekane mbele za Mungu?

[3]Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku, Pindi wanaponiambia mchana kutwa, Yuko wapi Mungu wako.

Kuonyesha ni mtu ambaye alimtamani sana Mungu wake.

Sehemu nyingine Daudi anasema..

Zaburi 63:1-8

[1]Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema,

Nafsi yangu inakuonea kiu, Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji.

[2]Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu, Nizione nguvu zako na utukufu wako.

[3]Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; Midomo yangu itakusifu.

[4]Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai; Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.

[5]Nafsi yangu itakinai kama kushiba mafuta na vinono; Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha.

[6]Ninapokukumbuka kitandani mwangu, Nakutafakari Wewe makesha yote ya usiku.

[7]Maana Wewe umekuwa msaada wangu, Na uvulini mwa mbawa zako nitashangilia.

[8]Nafsi yangu inakuandama sana; Mkono wako wa kuume unanitegemeza.

Umeona, usiku kucha, anamtafakari Mungu, kuonyesha ni mtu ambaye moyo wake upo kwa Mungu asilimia mia..unategemea vipi mtu kama huyo Mungu asijifunue kwake kwa viwango vile?

Nafasi hii pia mimi na wewe tunayo. Tumfuate Mungu wetu vilindini, ili ajifunue kwetu katika viwango vingine..

Na hiyo inakuja kwa kile Bwana Yesu alichosema..Tujitwike misalaba yetu tumfuate, tuwe tayari kuacha vyote visivyompendeza yeye na kumtii. Na kwa kufanya hivyo rohoni tunatafsirika kuwa tunamwita Mungu wa vilindini.

Anza sasa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.

Ni kelele gani zinazozungumziwa hapo katika Waefeso 4:31.

NIONDOLEENI KELELE ZA NYIMBO ZENU (Amosi 5:23)

Nini maana ya Mithali 9:13 Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu?

Rudi Nyumbani

Print this post

UKWELI KUHUSU UISLAMU Sehemu ya Pili: (Jiwe/Jabali la Kaaba).

Je “Kaaba” ni nini na ipo kwenye biblia?, Na wanyama wanaochinjwa kuelekea Kaaba je tunaruhusiwa kuwala?.

Angalizo: Makala hii haina lengo la kushambulia Imani Fulani, wala kushabikia Imani Fulani, pia haina lengo la kumchafua mtu yoyote, wala kumdhalilisha, bali kutoa elimu sahihi kuhusiana na tunayoamini na yanayoaminiwa.


Kama hujapitia sehemu ya kwanza ya Makala hii, inayohusu msikiti wa Al-Aqsa uliopo Yerusalemu pamoja na unabii wake basi waweza fungua hapa >>> UKWELI KUHUSU UISLAMU Sehemu ya kwanza: (Msikiti wa AL-Aqsa).

Leo tunaendelea na sehemu ya pili, na tutalitazama “Jiwe la Kaaba” na uhusiano wake na Imani ya kikristo.

“Kaaba” au kwa jina lingine al-Ka’ba al-Musharrafa ni jengo la “Jiwe Jeusi” lililopo katikati ya msikiti uitwao “Masjid al-Haram” uliopo mahali pajulikanapo kama “Makka”, huko nchini Saudi Arabia.

Jiwe hili linaaminika na dini ya kiislamu kuwa “nyumba ya mungu”. Na pia linaaminika kuwa ni ufunuo Mungu aliompa Abramu (Ibrahimu) pamoja na Ishaeli mwanae kama mahali pekee na sahihi alipopachagua Mungu pa kuabudia, kulingana na Quran, Al Imran 3:96 (Sasa kujua ukweli wa jambo hili kibiblia soma Makala hii mpaka mwisho).

Zaidi inaaminika kuwa mahali hapo “Kaaba (hapo Makka)” ndipo mahali ambapo Malaika walikuwa wakimwabudu Mungu kabla ya mwanadamu kuubwa, na baadaye mwanadamu alipoumbwa ndipo Adamu akapajenga tena mahali hapo kama sehemu ya kumwabudu Mungu, na baadaye baada ya mafuriko ya Nuhu mahali hapo pakapotea, pakawa hapajulikani, na alipotokea Ibrahimu ndio akapata ufunuo wa mahali hapo (kujua usahihi na ukweli wa jambo hili kibiblia soma Makala hii mpaka mwisho).

Baadaye kulingana na imani ya kiislamu, Abramu (Ibrahimu), aliambiwa awaambie wageni wote kutoka uarabuni na kila mahali wasafiri na kufika hapo kuhiji, na hiyo ndio sababu ya watu wa Imani ya kiislamu kuwasili huko Makka kuhiji kila mwaka.

Na si tu watu kuwasili pale, bali pia wanyama wachinjwapo wanaelekezwa (kibla) huko Maaka palipo na Kaaba.

Swali?.. Je ukweli wa mambo huu ni upi?

Awali ya yote ni muhimu kufahamu kuwa Mwana wa Ahadi alikuwa ni Isaka mzao wa Sara, na si Ishmaeli aliyekuwa mzao wa kijakazi Hajiri.. Ingawa Mungu alimbariki pia Ishmaeli mwana wa Hajiri, lakini hakuwa amekusudiwa kubeba ahadi yoyote ya urithi wa mzaliwa wa kwanza, kwanini?.. kwasababu hakuwa mwana wa mke halali wa kwanza wa Abramu, na hiyo ndio sababu ya Sara kumfukuza Hajiri, na Mungu akawa upande wa Sara.

Mwanzo 21:9 “Sara akamwona yule mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alimzalia Ibrahimu, anafanya dhihaka.

10 Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka.

11 Na neno hilo lilikuwa baya sana machoni pa Ibrahimu, kwa ajili ya mwanawe.

12 Mungu akamwambia Ibrahimu, Neno hili lisiwe baya machoni pako, kwa ajili ya huyo mwana, na huyo mjakazi wako. Kila akuambialo Sara, sikiza sauti yake, kwa maana katika Isaka uzao wako utaitwa.

13 Naye mwana wa mjakazi nitamfanya kuwa taifa, maana huyu naye ni uzao wako.

14 Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba”.

Sasa Imani ya kiislamu inaamini kuwa Ishmaeli(au Ismail) ndiye mwana wa ahadi halali wa Abramu, na biblia haisemi hivyo, na hapa ndipo MAKOSA YALIPOANZIA!!!!...Ndipo adui alipoanza kutengeneza MTI WAKE!!.

Na kwasababu hiyo, ya kuamini kuwa Ishmaeli ndiye mwana wa ahadi na si Isaka, basi ndipo zikazuka habari nyingine zisizo za kweli kwamba Abramu alishuka mpaka Makka na kupewa ufunuo uliopotea zamani kuwa mahali pa kuabudia ni hapo Makka, na pia zikatengenezwa habari nyingine kuhusiana na kisima maarufu kijulikanacho kama ZAMZAM, ambacho tutakuja kukiangalia katika Makala inayofuata na hatari yake kiroho.

Ukweli ni kwamba Abramu baada ya kumruhusu Hajiri aondoke na Ishmaeli, hakuendelea kufuatilia habari zake kwani Mungu alishamwambia amsikilize Sara, na ajihusishe na Isaka Zaidi ya Ishmaeli, hivyo si kweli kwamba Abramu aliwahi kushuka Saudi Arabia akiwa na Ishmaeli na kupewa ufunuo wa mahali hapo Makka, na hata biblia haionyeshi mahali popote jambo hilo.

Zaidi biblia inaeleza wazi kuwa baada ya Isaka kumzaa Yakobo, na Yakobo kulizaa Taifa la Israeli, kupitia Taifa hilo la Israeli alitokea Mfalme Daudi, ambaye baada ya kumpendeza sana Mungu, ndipo Mungu akauchagua mji wake Daudi (yaani Yerusalemu) uwe mahali pa kuweka nyumba yake na jina lake, na mahali pa kuabudia mpaka nyakati zake Masihi (yaani YESU).

2Nyakati 6:5 ”Tangu siku ile nilipowatoa watu wangu katika nchi ya Misri, sikuchagua mji wo wote wa kabila zote za Israeli ili kujenga nyumba, jina langu liwe humo; wala sikumchagua mtu ye yote awe mkuu juu ya watu wangu Israeli;

6 LAKINI NIMEUCHAGUA YERUSALEMU, JINA LANGU LIWE HUMO; NA DAUDI NIMEMCHAGUA AWE JUU YA WATU WANGU ISRAELI”.

Na tangu wakati ambapo Hekalu la Mungu lijengwe na Sulemani, mwana wa Daudi pale Yerusalemu, wenye Imani ya kiyahudi ndio walikuwa wanatoka Mataifa mbali mbali kwenda kuabudu pale, kwamaana ndio mahali alipopachagua Mungu aliweke jina lake.

Na hata watu wakiwa mbali walikuwa wanaabudu kuelekea Yerusalemu mahali hekalu lile lilipojengwa, mfano wake ni nabii Danieli katika Danieli 6:10, soma pia 1Wafalme 8:29-30.

Hivyo watu waliendelea kuwasili Yerusalemu mahali pale ambapo Mungu alipachagua, kwa miaka mingi ndio maana hata kibla ya kwanza ya uislamu ilikuwa ni hapo hapo Yerusalemu, walipokuja kujenga msikiti,  mahali hekalu lilipojengwa, ingawa walikuja kugeuza na kusema si hapo tena bali ni Makka, penye “Kaaba”.

Na Masihi alipokuja (YAANI YESU KRISTO) ndipo atakapoonyesha sehemu sahihi ya kuabudia, alipopachagua MUNGU kabla ya kuwekwa misingi ya Ulimwengu, na kwamba watu wote wakusanyike hapo ili wamwabudu MUNGU sawasawa na mapenzi yake.

Kwani watu wote walijua kuwa siku Masihi atakapokuja atasahihisha mambo yote, na kuonyesha njia sahihi, sasa njia hiyo ni ipi?? Tusome maandiko yafuatayo..

Yohana 4:19 “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!

20  Baba zetu waliabudu katika mlima huu, NANYI HUSEMA YA KWAMBA HUKO YERUSALEMU NI MAHALI PATUPASAPO KUABUDIA.

21  Yesu akamwambia, MAMA, UNISADIKI, SAA INAKUJA AMBAYO HAMTAMWABUDU BABA KATIKA MLIMA HUU, WALA KULE YERUSALEMU.

22  Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23  Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo WAABUDUO HALISI WATAMWABUDU BABA KATIKA ROHO NA KWELI. KWA MAANA BABA AWATAFUTA WATU KAMA HAO WAMWABUDU

24  Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

25  Yule mwanamke akamwambia, Najua ya kuwa yuaja Masihi, (aitwaye Kristo); naye atakapokuja, yeye atatufunulia mambo yote.

26  Yesu akamwambia, Mimi ninayesema nawe, ndiye”.

Umeona mahali sahihi alipopachagua Mungu pa Ibada?.. Si Yerusalemu tena, wala mahali pengine popote bali ni katika Roho Mtakatifu, na katika kweli ya MUNGU.

Maana yake kama mtu hana Roho Mtakatifu ndani yake basi hawezi kuwa na ibada halisi, kama hawezi kuutunza mwili wake na roho yake, basi hakuna mahali pengine popote duniani atakapoweza kumfanyia Mungu ibada akaikubali, kwasababu maandiko yanasema miili yetu ni HEKALU la ROHO MTAKATIFU (Soma 1Wakorintho 3:16 na 1Wakorintho 6:19).

Na Hekalu tafsiri yake ni sehemu ya nyumba ya ibada, hivyo ibada ya kwanza inaanza ndani ya mtu, hiyo ikiharibiwa mtu huyo hata aende wapi hawezi kumwona MUNGU wala kukutana na MUNGU, hata apae juu ya sayari zote, bado atakuwa mbali na Mungu na maombi yake hayasikilizwi.

Lakini kama akitakasika katika utu wake wa ndani na wa nje, basi mahali popote pale alipo ibada itakuwa inabubujika ndani yake, na hiyo ndio siri ya agano jipya.

Sasa swali ni je!, Wanaoenda Yerusalemu au Makka wanafanya makosa?

Kama mtu ataenda Yerusalemu kwa lengo la utalii, au kujifunza mambo, na pengine kumshukuru Mungu kwa atakayojifunza…hafanyi makosa lakini kama ni kwa lengo la Ibada, akiamini kuwa ile ni ardhi takatifu, hivyo atakokea kitu cha ziada, anakosea sana kwasababu Bwana Yesu alishasema.. saa yaja, nayo ipo, kwamba waabuduo halisi hawataenda tena Yerusalemu, bali watamwabudu katika roho na kweli.

Vile vile wanaoenda kuhiji Makka, wapo nje ya Imani kabisa, kwasababu hata huko Makka hapajaagizwa kabisa na Mungu, ni ufunuo wa ibilisi uliosambaa ili kuwafanya watu wasimwabudu MUNGU WA KWELI katika roho na kweli, badala yake katika makosa makubwa. Hivyo wanaokwenda kuhiji Makka wanahitaji msaada wa kumjua YESU, na NEEMA yake, ili watoke katika hayo makosa.

Hali kadhalika hakuna agizo lolote la mnyama achinjwapo basi aelekezwe Yerusalemu wala Makka, hayo pia ni maagizo ya ibilisi, ambayo yanalengo la kuingiza roho katika vile tuvilavyo.

Ikiwa nyama inauzwa buchani, Mkristo anaweza kuinunua akiongozwa na Amani ya Roho mtakatifu, na baada ya kuinunua anaweza kuitakasa kwa maombi, kisha akaitumia, lakini kama katika bucha hilo, wauzaji wamekiri waziwazi kuwa nyama hiyo imechinjwa kwa kuelekezwa kibla yoyote ile iwe ya Yerusalemu au Makka au penginepo popote nyama hiyo usinunue wala usile, kwasababu ya Dhamiri, ndivyo maandiko yasemavyo..

1Wakorintho 10:25 “Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni, bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri;

26  maana, Dunia ni mali ya Bwana na vyote viijazavyo

27  Na mtu asiyeamini akiwaalika, nanyi mnataka kwenda, kuleni kila kitu kiwekwacho mbele yenu bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri.

28  Lakini mtu akiwaambia, Kitu hiki kimetolewa kiwe sadaka, msile, kwa ajili yake yeye aliyeonyesha, na kwa ajili ya dhamiri.

29  Nasema, dhamiri, lakini si yako, bali ya yule mwingine. Maana kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?”

Usikose mwendelezo wa sehemu inayofuata wa Kisima cha Zamzam, na mengineyo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

MJUE SANA YESU KRISTO.

DANIELI: Mlango wa 9

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Rudi Nyumbani

Print this post

UKWELI KUHUSU UISLAMU Sehemu ya kwanza: (Msikiti wa AL-Aqsa).

Je msikiti wa Al-Aqsa ni nini, na unahusikaje katika unabii wa biblia?

Angalizo: Makala hii haina lengo la kushambulia Imani Fulani, wala kushabikia Imani Fulani, pia haina lengo la kumchafua mtu yoyote, wala kumdhalilisha, bali kutoa elimu sahihi kuhusiana na tunayoamini na yanayoaminiwa.

MSIKITI WA Al-Aqsa

Msikiti wa Al-Aqsa ni msikiti uliopo katika mji wa YERUSALEMU, ndani ya Nchi ya Israeli, Msikiti huu unaaminika kuwa ni sehemu ya tatu ya utakatifu kulingana na dini ya kiislamu, Sehemu ya kwanza ikiwa ni Makka (au Mecca), ya pili ni Al-masjid an Nabawi iliyopo Medina (nchini Saudi Arabia), na ya tatu ndio hii Al-Asqa.

Msikiti wa Al-Aqsa umejengwa pembezoni mwa jengo maarufu kama “Kuba ya Mwamba” (au Dome of Rock), tazama picha chini.

kuba ya mwamba

Msikiti huu wa Al-Aqsa unaaminika ulijengwa na mtu aliyeitwa Umayyad caliph Abd al-Malik kati ya Karne ya saba (7) na ya nane (8), baada ya KRISTO. Na kulingana na dini  ya kiislamu, inaaminika kuwa Muhamad ndipo alipopaa mbinguni na kwenda kupewa ufunuo wa kitabu cha Quran (Sasa kujua kama ni kweli au si kweli soma Makala hii mpaka mwisho)..

Mbali na kwamba katika msikiti huu ndio panaaminika kuwa mahali Muhamad alipopaa lakini pia zamani paliaminika na waislamu wa kwanza kuwa ndio maahali pa kutazama wakati wa sala, maarufu kama “kibla”. Hebu tuielezee hii Kibla kidogo..

Kibla ni neno la kiaramu lenye maana ya “Uelekeo”, Waislamu wanaposali kulingana na Imani yao, wanapaswa waelekee upande Fulani, sasa zamani Kibla ilikuwa ni katika huu msikiti wa Al-Aqsa uliopo Yerusalemu Israeli, lakini baadae walikuja kubadilisha kulingana na kuwa mahali pajulikanapo kama Makka (Mecca) huko Saudi Arabia, ambapo ndipo Muhamad alipozaliwa.

Hivyo sasa waslamu wote wanaposali wanaelekea kibla huko Makka Saudi Arabia na si tena Yerusalemu, na pia mtu anapozikwa anaelekezewa huko Makka, na vile vile mnyama anapochinjwa anaelekezewa huko huko Makka (kujua usahihi wa jambo hili na kama wakristo wanaruhusiwa kushiriki vyakula hivyo endelea kufuatilia Makala hizi)..

Sasa swali ni je! Huu msikiti ambao sasahivi upo pale Yerusalemu, unaoaminika na watu Zaidi ya Bilioni 1.9, kuwa ndio sehemu ya Tatu kwa utakatifu, je msikiti huu utaendelewa kuwepo pale milele au utakuja kuondolewa?.

Jibu: Kujua kama utaondolewa au la! Turejee Biblia..

Maandiko yanasema lile Hekalu la Kwanza lililojengwa na Sulemani, lilitengenezwa juu ya Mlima Moria, ambapo ni eneo lile lile Abrahamu alipotaka kwenda kumtoa mwanae Isaka kama sadaka ya kuteketezwa, na sasa ndio eneo hili hili ambalo msikiti wa Al-Aqsa umejengwa.

Na ilikuwaje Hekalu kuondolewa na msikiti kujengwa?..

Sababu iliyofanya Msikiti huo kujengwa mahali pale pale Hekalu lilipokuwepo… ni kuvunjwa kwa hekalu hilo mara ya kwanza na ya pili…na wayahudi (yaani waisraeli), kuondolewa katika nchi yao na kutapanywa katika mataifa yote mwaka ule wa 70 Baada ya Kristo.

Wayahudi walipoondolewa katika nchi yao kutokana na makosa yao kwa Mungu, ndipo Ngome ya kiarabu ikateka na kujenga msikiti huo.

Adhabu ya Mungu kwa Israeli, haikuwa ya milele, kwani aliahidi atawarudia tena, na kuwarudisha katika nchi yao, na tena watalijenga Hekalu. (soma Ezekieli 40-48), na kufikia mwaka 1948, Israeli walirejea nchini kwao na mpaka sasa wapo pale.

Na hatua ya kwanza ya matengenezo ni wao kuirudia torati waliyopewa na Musa, hivyo watalijenga Hekalu kama lile la kwanza na baadaye, watamwagiwa Neema na macho yao kufumbuliwa Zaidi kwa kumwamini Masihi YESU, aliye hekalu halisi, sawasawa na Warumi 11 (kwani kwasasa wengi wao hawaamini hivyo).

Warumi 11:1 “Basi, nauliza, Je! Mungu aliwasukumia mbali watu wake? Hasha! Kwa kuwa mimi nami ni Mwisraeli, mmoja wa wazao wa Ibrahimu, mtu wa kabila ya Benyamini.

2  Mungu hakuwasukumia mbali watu wake aliowajua tokea awali. Au hamjui yale yaliyonenwa na maandiko juu ya Eliya? Jinsi anavyowashitaki Waisraeli mbele za Mungu………………………

25  Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

26  Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake”.

Sasa kabla ya huo wakati wa Israeli kufumbuliwa macho,na kumjua Kristo kama Hekalu halisi, watasimamisha kwanza Hekalu la damu na nyama, na mahali litakapojengwa ni palepale lilipojengwa hekalu la kwanza. Na hapo si pengine bali ni eneo lile lile Msikiti wa Al-aqsa ulipo.

Maswali yafuatayo yananyanyuka:

Je! Ni ni kitatokea?..na je huo msikiti utaondolewa kupisha ujenzi wa Hekalu, na kama utaondolewa je utaondolewaje?..na ni lini?.

Jibu ni  kwamba Msikiti ule ni lazima utaondolewa pamoja na ile Kuba ya Mwamba (Dome of Rock)!!, kwasababu Neno la Mungu limeshasema hivyo kwamba Hekalu litajengwa…na Neno la Mungu halijawahi kupita (kilichotabiriwa katika Ezekieli 40-47  kitatimia kama kilivyo), hakuna shaka juu ya hilo, haijalishi ni muda gani utapita!!.. Wakati utakapofika wa unabii huo kutimia msikiti wa Al-Aqsa utaondoka.

Ni kwa njia gani utaondolewa?.. hakuna anayejua kama ni kwa njia ya Amani, au kwa njia nyingine, lakini dunia nzima itatii tu kwasababu ni Bwana ndiye aliyeyasema hayo, na kuyapanga si MTU, wala WATU wala Taifa la Israeli, bali ni MUNGU mwenyewe!!, hivyo hata wakati wa kuondolewa hakuna atakayejisifu kuwa ni nguvu zake, bali Mungu mwenyewe ndiye atakayehusika hapo.

Na dalili zote zinaonyesha kuwa tumekaribia sana hicho kipindi, kwani waisraeli wameshakusanya utajiri mkubwa na utaalamu mwingi, kiasi kwamba endapo ikitokea ukaanza leo, basi hakuna kizuizi chochote cha kifedha wala kiutalaamu.

Na ujenzi huo unauhusiano mkubwa sana na mpinga-Kristo ajaye, ambapo biblia inasema atatafuta kuingia katika hekalu hilo, ili atafute kuabudiwa yeye kama Mungu (2Wathesalonike 2:4), na maandalizi ya mpinga-kristo yapo ukingoni..nafasi yake ipo tayari, kinachongojewa ni parapanda.

HOJA NYINGINE ZISIZO SAHIHI.

  1. Je Muhamad alipaa??..

Je ni kweli Muhamad alipaa, na je ni kweli Qurani ni kitabu cha Mwenyezi Mungu?

Jibu ni la! Hakupaa!!..Kwasababu Biblia inatuambia manabii waliopaa ni wawili tu, Henoko na Eliya.. na BWANA YESU ambaye ndiye Mkuu wa Uzima. Hao ndio waliopaa, na wengine watakaopaa ni watu watakaofufuliwa na kwenda mbinguni siku ya unyakuo, na watakatifu watakaokuwa hai siku ya kurudi kwa Bwana, pamoja na wale manabii wawili waliotajwa katika Ufunuo 11, basi!

Na pia Quran sio kitabu cha mwenyezi Mungu chenye kumfikisha mtu mbinguni. Kinaweza kuwa kitabu chenye baadhi ya maonyo yaliyo sahihi ambayo mtu akiyafuata anaweza kuwa mzuri katika jamii, lakini si kuurithi uzima wa milele…Kwa ujumla kitabu hiko hakina mafundisho ya Uzima wa milele, kwasababu kinamkataa YESU kama NJIA PEKEE ya WOKOVU wa mwadamu.

Na kitabu chochote kisichoelekeza moja kwa moja Uzima wa milele uliopo ndani ya YESU, au  mtu yeyote yule asiyeamini kuwa YESU ndiye BWANA, na Mwokozi, na ndiye njia pekee ya UZIMA, huyo mtu hana uzima wa milele haijalishi atakuwa anafanya mambo mengine yanayoonekana mazuri machoni pa watu, lakini kama hatamwamini Bwana YESU baada ya kumsikia, matendo yake hayo hayatamsaidia chochote, kwasababu hakuna mwanadamu atakayeweza kusimama kwa matendo yake peke yake.

Yohana 3:18 “ Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu”.

Usikose mwendelezo kuhusiana na Kibla ya wanyama na “Kaaba”, na kama wakristo tunaruhusiwa kushiriki vyakula hivyo.. Pia usikose kufuatilia Makala hizi pamoja na nyingine nyingi, juu ya ukweli kuhusiana na Uislamu na Imani nyingine.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je!Sisi kama wakristo Tunaruhusiwa kuchangia ujenzi wa Imani nyingine?

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

JE! UNA MASIKIO YANAYOSIKIA?

UFUNUO: Mlango wa 11

Je! Wapalestina ni watu gani, na sehemu yao katika biblia ni ipi?

Rudi Nyumbani

Print this post

NIFANYE NINI NIMSHINDE SHETANI?

1) WOKOVU: 

Hilo ndio jambo la kwanza. Kamwe huwezi kumshinda shetani ikiwa upo nje ya Kristo, Ndicho kilichowakuta wale wana wa Skewa, walipotaka kutoa pepo kwa jina la Yesu. Lakini Yule pepo akawaambia Yesu namjua, na Paulo namfahamu, lakini je ninyi ni akina nani?

Matendo 19:13  Baadhi ya Wayahudi wenye kutanga-tanga, nao ni wapunga pepo, wakajaribu kutaja jina la Bwana Yesu juu yao waliopagawa na pepo wachafu, wakisema, Nawaapisha kwa Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo.

14  Walikuwako wana saba wa mtu mmoja Skewa, Myahudi, kuhani mkuu, waliofanya hivyo.

15  Yule pepo mchafu akawajibu, akawaambia, Yesu namjua na Paulo namfahamu, lakini ninyi ni nani? 16  Na yule mtu aliyepagawa na pepo mchafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.

Wokovu, ni Kristo ndani yako, na kwa huo nguvu za adui zote huyeyuka mara moja. Mtu aliyempokea Yesu, shetani kamwe hamwezi, kwasababu anamwona Kristo ndani yake.

2) MAOMBI: huharibu mipango ya ibilisi.

Unaweza ukawa umeokoka, lakini shetani akapata nguvu za kukusumbua kwa majaribu, kwasababu unashindwa kutumiza baadhi ya wajibu wako kwa mwamini, Yesu alisema..

Mathayo 26:41  Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.

Yesu ijapokuwa alikuwa ni mkamilifu hana dhambi, alijaribiwa na adui, wewe ni nani usikutane na hayo? Usipokuwa mwombaji, uvivu ukakumeza, unaona shida kuomba kila siku, kuhudhuria mikesha ujue tayari upo majaribuni. Hata kama utajiona upo sawa, fahamu tu hapo ulipo kuna eneo Fulani adui anakusumbua, utakuja kugundua pindi utakapoanza kuwa mwombaji. Na ndio maana maisha ya wokovu hayatengwi na maombi. Shetani akimwangalia mwombaji anaona moto umemzunguka mkali, hawezi jiamulia tu kufanya analotaka kwake.

3) KUBALI KUWA MJINGA: Utamweka chini shetani.

Warumi 16:19  Maana utii wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya. 20  Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. [Amina.]

Hapo anasema tuwe wajinga katika mambo mabaya. Ni nafasi kubwa kwa Mungu kumweka shetani chini ya miguu yetu. Kwamfano, unapokuwa hujui kuhusu mitindo mipya ya kidunia, sio mfuatiliaji wa miziki ya kidunia, muvi mpya mpya zilizotoka duniani, yaani kwa ufupi unapitwa na mambo ya kidunia yasiyokuwa na maana kwako, kinyume chake, unakuwa na ujuzi na hekima katika mambo ya rohoni jua hapo umemshinda shetani kwa sehemu kubwa. Hana kitu kwako, kwasababu bidhaa zake, huna mpango nazo, hununui chochote kwake.  Kuipenda dunia ni kuwa adui wa Mungu, na rafiki wa shetani.

4) WEKA NENO LA MUNGU NDANI: Utamfukuza shetani.

Kuweka Neno sio, kukariri vifungu vingi vya biblia, hapana, bali ni kufahamu “ukweli” (ufunuo)  wa kila Neno unaloliweka moyoni mwako. Pale jangwani, Yesu alipokutana na shetani, alimjaribu kwa Neno hilo hilo,lakini Yesu akamwambia kweli yote ipoje.

Mathayo 4:6  akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 7  Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.

Ni muhimu ukalifahamu Neno la Mungu katika kweli yake, na hiyo huchangiwa na kufundishwa kwa ufasaha Neno la Mungu na waalimu, kwasababu Roho Mtakatifu atasema na wewe kupitia wao. Lakini pia kumpa Roho Mtakatifu nafasi ya moja kwa moja kukufundisha. Vinginevyo adui atakudanganya sana, hususani kupitia manabii wa uongo, kwasababu hulijui Neno vema.

 5) LITII NENO: Utaweza yastamili majaribu yake yote.

Kulifahamu Neno, na kuijua kweli, ni jambo muhimu lakini bado shetani anaweza pata mianya ya kukunasa endapo hutaweza kulitii Neno. Penda utakatifu, penda kutendea kazi kile unachofundishwa. Yesu alisema, wapo watu wasikiao tu, lakini wapo wasikiao na kuyatendea kazi. Wote hujaribiwa kwa pepo, mafuriko na mvua za shetani. Sasa Yule aliyejijenga  juu ya fundisho tu, na sio kutendea kazi fundisho, ndio huyo anayechukuliwa na mafuriko.

Mathayo 7:26  Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

27  mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.

Mateso mengine huwapata watu kwasababu ya dhambi. Kuishi maisha matakatifu, humnyima adui mlango wa kukushambulia kwa namna yoyote. Liishi Neno.

6) HUBIRI NENO: Utamwangusha adui kutoka juu.

Watu wengi hudharau ushuhudiaji. Tunapokuwa na moyo mmoja wa kuitenda kazi ya Mungu, adui hawezi kukaa juu ya anga hili, kutupinga. Tunalisoma wapi hilo? Utakumbuka wakati ule Bwana alipowatuma wanafunzi  wake wawili wawili kuhubiri, waliporudi kwa furaha, huku wakimwambia Bwana  hata mapepo yanawatii. Yesu akawaambia nalimwona shetani akianguka kutoka juu kama umeme. Kuonyesha kuwa kitendo cha wao kuhubiri adui alikuwa anaporomoka kwa kasi sana.

Mathayo 10:17  Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. 18  Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.

Hivyo ukizingatia mambo  hayo sita (6), Utakuwa sio tu umemdhibiti adui kila Nyanja, bali pia umemteka. Ni wajibu wako mimi na wewe kuboresha mahali ambapo hapako sawa, ili kwa pamoja tukaujenge ufalme wa Mungu na kuziangusha kazi za shetani.

Yakobo 4:7  Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ZIFAHAMU KAZI KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

USIWE ADUI WA BWANA

Rudi Nyumbani

Print this post

Ijapokuwa amekufa, angali akinena(Waebrania 11:4)

SWALI: Maandiko yanaposema Habili ijapokuwa amekufa angali akinena, je! Ananenaje, wakati yeye ni marehemu. Je! Hiyo inamaana wazee wetu wa zamani wanaweza kunena na sisi?

Waebrani 11:4  Kwa imani Habili alimtolea Mungu dhabihu iliyo bora kuliko Kaini; kwa hiyo alishuhudiwa kuwa ana haki; Mungu akazishuhudia sadaka zake, na kwa hiyo, ijapokuwa amekufa, angali akinena


JIBU: Kibiblia ni kweli kabisa watakatifu waliokufa kale hunena nasi. Lakini kunena kwao ni tofauti na huku kunakodhaniwa, kwamba mzimu unakutokea kwenye ndoto, au unasikia sauti ya petro makaburini ikizungumza na wewe,  Hapana, ukiona hivyo ujue huzungumzi na huyo mtu, bali ni pepo.

Sasa watakatifu waliokufa wanazungumzaje na sisi?

Ni kwa ushuhuda waliouacha. Maisha yao na maagizo yao, ndio huzungumza nasi, sikuzote, kana kwamba tupo nao sasa, kwa mafundisho yao yaliyopo  mpaka sasa kana kwamba tunawaona wenyewe kumbe wamekufa.

Ndio maana ile habari ya Yule tajiri wa Lazaro, tunaambiwa alipofika kule kuzimu akaomba mtu atolewe kwa wafu awahubirie injili, akakataliwa, kuonyesha kuwa hakuna mtu aliyekufa mwenye uwezo wa  kuja tena kuzungumza na sisi, nafasi hiyo haipo kwao. Lakini waliambiwa WANAO MUSA NA MANABII, WAWASIKILIZE.

Luka 16:29  Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.

Maana yake ni kuwa sio kwamba Musa kweli alikuwepo duniani, au manabii wa kale kama Isaya walikuwa duniani kwa wakati huo, anaambiwa hayo maneno. Lakini shuhuda zao na mahubiri yao, huwawakilisha wao. Tunaweza kusema “ijapokuwa wamekufa wangali wakinena”

Ndivyo ilivyo kwa Habili, ijapokuwa aliuliwa na ndugu yake, lakini IMANI yake inasema nasi mpaka leo. Mitume wa Kristo ijapokuwa hawapo duniani lakini sauti zao tunazisikia hadi sasa.

Lakini pia kuna mahali pengine biblia inasema damu ya Yesu hunena mema kuliko ya Habili (Waebrania 12:24). Kufahamu kwa kina damu ya mtakatifu  hunenaje? Pitia somo hili. >>> DAMU YA ZAKARI BIN BARAKIA.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

KUOTA MTU AMEKUFA/NDUGU AMEKUFA.

ALIPOKUWA ANGALI MBALI, BABA YAKE ALIMWONA.

Rudi Nyumbani

Print this post

TABIA SITA (6) ZA WANAFUNZI WA YESU.

Zifuatazo ni baadhi ya tabia za kuigwa walizokuwa nazo wanafunzi wa Bwana YESU ambazo nasi tunapaswa tuzionyeshe.

1. WALIJIKANA NAFSI ZAO.

Hii ni sifa ya kwanza waliyokuwa nayo wanafunzi wa YESU, Kwani mtu aliyekosa hii sifa hakuweza kuwa mwanafunzi wake.

Luka 14:27 “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.

Halikadhalika na sisi kama wanafunzi wa Bwana ni sharti tujikane nafsi kila siku, na kubeba msalaba. (Zingatia hilo neno, “Kila siku”), na si siku moja tu..

Luka 9:23 “Akawaambia wote, Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate”.

2. WALIKAA KUFUNDISHWA NA BWANA.

Maana ya kuwa mwanafunzi ni kuketi na kufundishwa mpaka kuhitimu. Na wanafunzi wa Bwana YESU walilijua hilo, hivyo walikuwa walijiunga na chuo hicho cha Bwana ili kupokea mafunzo.

Na leo ni hivyo hivyo, Mwalimu wetu ni ROHO MTAKATIFU na chuo chetu ni Biblia. Na kila mtu ni lazima apite chini ya chuo hicho, ili aweze kuwa mwanafunzi wa Bwana.

3. WALIMFUATA BWANA KILA ALIKOKWENDA.

Maisha ya Bwana YESU hayakuhusisha kukaa mahali pamoja, bali kuzunguka huku na kule, katika miji na vijiji kuhubiri injili.

Mathayo 9:35 “Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina”.

Hata wanafunzi wasomao chuo, upo wakati wanaenda katika mafunzo kwa njia ya vitendo kabla ya kuhitimu (maarufu kama mafunzo ya field).

Na vivyo hivyo na sisi kama wanafunzi  ni lazima tuifanye kazi ya Bwana kwa yale tuliyoyapokea hata kama hatubobea katika hayo..

Lakini utaona leo, mtu hataki kuwahubiria wengine kwa hofu ya kwamba yeye hajui….Ni kweli usifundishe usichokijua lakini kile kidogo ambacho umeshakijua, usikifukie chini bali kawape wengine wasiokijua kabisa.

4. WALIMTII BWANA.

Tabia nyingine ya mwanafunzi Halisi ni UTII na NIDHAMU.

Wanafunzi wa Bwana YESU wale 11 walimtii Bwana kwakila jambo, kuanzia maagizo ya ubatizo, kuhubiri, meza ya Bwana na mengineyo.

Na wote walimwogopa Bwana (hakuna aliyedhubutu kuhojiana naye wala kushindana naye) Luka 9:45.

5. WALIMWAMINI BWANA.

Wanafunzi halisi wa Bwana YESU hawakuwa na mashaka mashaka na Bwana YESU…walimwamini moja kwa moja…

Yohana 2:11 “Mwanzo huo wa ishara Yesu aliufanya huko Kana ya Galilaya, akaudhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini”

6. WALIMVUMILIA BWANA

Hata kama yalikuwepo mambo ambayo yalikuwa ni magumu kueleweka kwa katika hali yao.ya uchanga…lakini walivumilia wakiamini siku moja watakuja kuelewa vizuri..

Yohana 6:67 “Basi Yesu akawaambia wale Thenashara, Je! Ninyi nanyi mwataka kuondoka?

68 Basi Simoni Petro akamjibu, Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.”

Na sisi kama wanafunzi wa YESU hatupaswi kurudi nyuma,  tunapokutana na mambo tusiyoyaelewa katika imani au maandiko..badala yake tunapaswa kuwa wavumilivu kwa matumaini mazuri yajayo.

Na kumbuka maana ya kuwa MRISTO ni kuwa MWANAFUNZI…Huwezi kusema ni mkristo na sio mwanafunzi.

Matendo ya Mitume 11:26 “hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo ANTIOKIA”.

BWANA ATUSAIDIE.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU.

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

Rudi Nyumbani

Print this post

NDOA TAKATIFU NI MKE MMOJA/MUME MMOJA.

Ndoa za wake wengi ni za ibilisi!..ndoa za wake wengi ni za ibilisi!!… ndoa za wake wengi ni za ibilisi!!!. Hali kadhalika ndoa za waume wengi ni za ibilisi, kama tu zilivyo za jinsi moja (zote ni zao la ibilisi).

Zipo hoja kuwa kwasababu Daudi, Sulemani na manabii wengine wakale walioa wake wengi, basi hata leo ni halali kuoa wake wengi.. tena zipo hoja zifananishazo wanyama wa porini na wa kufungwa na uhalali wa kuoa wake wengi.

Hoja zote hizi ni za ibilisi… Ndugu, usiongeze wake, wala wala usiongezee waume.

Bwana YESU alipokutana na yule mwanamke Msamaria kisimani hakumwambia akawalete WAUME ZAKE!.. Ingawa alikuwa ana wanaume wengi (na Bwana alilijua hilo), lakini alimwambia nenda “kamlete mumeo”… ikimaanisha kuwa ndoa halali na takatifu ni ya mume mmoja na mke mmoja.

Sasa Kristo alikuwa anamjua Sulemani, na Daudi..

Yohana 4:15 “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.

16  Yesu akamwambia, NENDA KAMWITE MUMEO, uje naye hapa.

17  Yule mwanamke akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume;

18  kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli”.

Bwana YESU kabla ya kukutana na huyu mama, alikuwa anamjua Daudi pamoja na Sulemani na idadi ya wake wake waliooa!.. Lakini tunaona hakumwambia huyu mwanamke Msamaria, kwamba akawalete waume zake!!.. Bali alimwambia kamlete mumeo! (maana yake mmoja tu).. bado huoni tu, kuwa ndoa za mitara ni batili na za ibilisi!.

Na tena biblia inasema hapo Mwanzo Mungu alimwumba mwanaume na mwanamke, na si mwanaume na wanawake, au mwanamke na wanaume (soma Mwanzo 1:27 na Mathayo 19:4).

Huoni kuwa ndoa hizo za wake wengi zitakukosesha maji ya uzima!.. Na pia fahamu kuwa ndoa za wake wengi sio zile tu zinazohusisha mtu kuwa na wake wengi katika boma moja kwa wakati mmoja…la! Hata zile za kuacha na kuoa mwingine ilihali yule wa kwanza bado yupo hai.. hiyo ni mitara! Ndicho kilichokuwa kwa huyu mwanamke Msamaria.

Huyu mwanamke msamaria alikuwa na wanaume watano kulingana na darubini ya kimbingu! Ingawa haishi nao, lakini alikuwa nao watano, na anayeishi naye ni wa 6, vile vile kuna watu leo hii wamecha wake zao na kuoa wengine, na kuacha tena na kuoa wengine, (hawa hawana tofauti na wale waliooa wake wawili na kuishi nao wote kwa pamoja).

Na madhara ya ndoa za mitara ni “KUKOSA MAJI YA UZIMA”..

Yapo maji ya Uzima tuyanywayo hapa Duniani, na yapo yale tutakayoyanywa katika mbingu mpya na nchi mpya.

Maji ya Uzima duniani ni YESU KRISTO, tumpatapo yeye tunapata uzima wa milele (Yohana 4:14), lakini ukijiunganisha na hizi ndoa za mitara hawezi kuingia ndani yako!.. vile vile maji ya uzima baada ya maisha haya tutayanywa kutoka katika ule mto wa maji ya Uzima katika mbingu mpya na nchi mpya.

Ufunuo 22:1 “Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung’aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo,

2  katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa.

3  Wala hapatakuwa na laana yo yote tena. Na kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwamo ndani yake. Na watumwa wake watamtumikia;

4  nao watamwona uso wake, na jina lake litakuwa katika vipaji vya nyuso zao.

5  Wala hapatakuwa na usiku tena; wala hawana haja ya taa wala ya nuru ya jua; kwa kuwa Bwana Mungu huwatia nuru, nao watatawala hata milele na milele”.

Neema ya Bwana YESU itufunike.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAFUNDISHO YA NDOA.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

VIGEZO VYA KUWA KARIBU NA YESU KRISTO KATIKA ULIMWENGU UJAO.

NDOA NI NINI?

KUWA NA  MAFUTA YOTE YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO.

Rudi Nyumbani

Print this post

FUNDISHO LA BWANA JUU YA KUZALIWA MARA YA PILI.

Jina la BWANA wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze biblia neno la Mungu wetu ambalo ni Taa na Mwanga wa njia yetu (Zab.119:105).

Hebu tuangalie uzito wa kuzaliwa mara ya pili kupitia maneno ya BWANA WETU YESU KRISTO.

Yohana 3:1 “Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.

2  Huyo alimjia usiku, akamwambia, RABI, TWAJUA YA KUWA U MWALIMU, UMETOKA KWA MUNGU; KWA MAANA HAKUNA MTU AWEZAYE KUZIFANYA ISHARA HIZI UZIFANYAZO WEWE, ISIPOKUWA MUNGU YU PAMOJA NAYE.

3  Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.

4  Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

5  Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, MTU ASIPOZALIWA KWA MAJI NA KWA ROHO, HAWEZI KUUINGIA UFALME WA MUNGU”.

Hapa Nekodemo anataja vigezo vya Mtu kuwa na MUNGU kuwa ni “Ishara azifanyazo”…na anamthibitisha Bwana kwa ishara hizo, lakini Bwana anamrekebisha, kuwa “MTU asipozaliwa mara ya pili hawezi kuurithi ufalme wa Mungu (maana yake hawezi kuwa na MUNGU)”… Je! na sisi leo tunalijua hilo??????….Je unalijua hilo??? .

Nikodemo anaona ISHARA ni tiketi ya kuwa na MUNGU,… Bwana YESU anataja KUZALIWA MARA YA PILI ndio TIKETI.. Sasa tuchukue ya nani tuache ya nani?.. Bila Shaka maneno ya BWANA YESU ni hakika, na tena ndio uzima.

Ndugu haijalishi tutakuwa na uwezo wa kufanya miujiza mingi na mikubwa kiasi gani, kama HATUJAZALIWA MARA YA PILI (Maana yake kwa maji na kwa Roho) hatuwezi kuwa na Mungu, kutembea naye wala hatutamwona siku ile.

Mtu anapozaliwa mara ya pili anakuwa kiumbe kipya, maana yake yale maisha ya kwanza ya dhambi yanakuwa hayapo tena maishani mwake.

Kuzaliwa kwa maji ni Ubatizo wa Maji mengi na kwa jina la Bwana YESU na kuzaliwa kwa Roho ni ubatizo wa Roho Mtakatifu (Matendo 2:37-38), mambo haya ndiyo yanamkamilisha mtu baada ya kutubu.

Na anayetuzaa mara ya si mtu bali ni Mungu mwenyewe, na Mungu ni Roho (sawasawa na Yohana 4:24), na tunapozaliwa na Roho, basi tunakuwa watu wa rohoni.

Yohana 3:6 “Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho”

Na kuwa mtu wa rohoni, si kuona maono, au mapepo, bali ni kuzaliwa katika Roho, na Maji. Na sifa kuu ya mtu wa rohoni ni kuushinda ulimwengu (dhambi na mambo mengine ya kidunia).

1Yohana 5:4  “Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu”.

Soma pia 1Yohana 3:9 na 1Yohana 5:18.

Hivyo ukiona tamaa za kidunia bado zinakusumbua kuna uwezekano kuwa bado hujazaliwa mara ya pili, kwasababu wote waliozaliwa mara ya pili wanayo nguvu ndani yao ya kuushinda ulimwengu na ndio watu wa rohoni.

Je ishara ni uthibitisho wa mtu kuwa na Mungu??..jibu ni ndio!, lakini si uthibitisho wa kwanza… bali uthibithsho wa kwanza wa mtu kuwa na Mungu ni KUZALIWA MARA YA PILI. Kwasababu wapo watakaotenda miujiza na kufanya ishara nyingi lakini wasimwone Bwana siku ile sawasawa na Mathayo 7:22.

Kwahiyo kilicho cha msingi kuliko vyote ni “KUZALIWA MARA YA PILI (kuwa kiumbe kipya)”  na mengine ndio yafuate.

Wagalatia 6:15 “Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya“.

1Petro 1:23 “Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.

JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?.

UMUHIMU WA KUZALIWA MARA YA PILI.

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

Rudi Nyumbani

Print this post