Category Archive Mafundisho

Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu (Zekaria 13:7-9)

SWALI: Nini maana ya hivi vifungu?

Zekaria 13:7-9

[7]Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu, na juu ya mtu aliye mwenzangu, asema BWANA wa majeshi; mpige mchungaji, nao kondoo watatawanyika; nami nitaugeuza mkono wangu juu ya wadogo.

[8]Hata itakuwa, ya kwamba katika nchi yote mafungu mawili yatakatiliwa mbali, nao watakufa, asema BWANA; lakini fungu la tatu litabaki humo.

[9]Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo; wataliitia jina langu, nami nitawasikia; mimi nitasema, Watu hawa ndio wangu; nao watasema, BWANA ndiye Mungu wangu.


JIBU: Unabii huu ulimtabiri Yesu, wakati wa kukamatwa kwake na wayahudi ili auawe, ukisoma Mathayo 26:31 utaona Bwana alinukuu yeye mwenyewe maneno hayo kwa kusema..

“Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote mtachukizwa kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika”.

Na kweli tunaona baada ya Yesu kukamatwa mwanafunzi wake wote wakamkimbia.

Kama mstari wa nane unavyosema mafungu mawili yatakatiliwa mbali, nao watakufa, lakini fungu la tatu litabaki humo.

Ni kuonyesha kwa lugha ya mifano kuwa ni idadi ndogo tu ya wanafunzi ambao hawakumuacha kabisa kabisa, mfano wa “theluthi moja”, lakini theluthi mbili zote zilirejea nyuma moja kwa moja. Na ndio maana utaona siku ile ya pentekoste ni watu 120 tu waliokuwepo pale kuingojea ahadi ya roho. Lakini yale maelfu ya makutano yaliyokuwa yakimfuata yalitawanyika.

Lakini katika mstari wa 9, anasema;

“Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo; wataliitia jina langu, nami nitawasikia; mimi nitasema, Watu hawa ndio wangu; nao watasema, BWANA ndiye Mungu wangu.”

na hao ndio waliopitishwa katika moto, wakabatizwa na Roho, wakawa vyombo vikamilifu vimfaavyo Mungu kwa kazi ya uvuvi.

Lakini adui hakujua ulikuwa ni mpango wa Mungu iwe vile kwamba mchungaji afe, ili wokovu mkuu zaidi ya ule wa kwanza uje kwa kupitia kifo chake.Angelijua hilo hata asingedhubutu kumgusa.

Ndio hapo shetani hakuamini alipoona wale wachache waliojazwa Roho, wakivuta maelfu kwa mamilioni ya watu  kwa kipindi kifupi mpaka dunia nzima ikawa imepinduliwa. Shetani hakujua misheni ya mchungaji ilikuwa ni kuingia ndani ya kondoo, sio kuwachunga tena kwa nje, kama hapo mwanzo.

Je nini tunajifunza?

Je! Wewe ni kundi lipi? Lile la tatu, au yale mawili ya kwanza. Ambayo yanapoona mtikisiko kidogo tu wa kimaisha hurudi nyuma, yanapoona kuyumba kidogo tu kwa kanisa hutoroka, yanapoona kutetereka kidogo kwa kiongozi wao yanarudi Misri? Kumbuka ni kusudi la Kristo wote tupitishwe katika moto, ili tuimarishwe tufae kwa ajili ya kazi njema ya utumishi wake.

Aliwapitisha wana wa Israeli jangwani, ili kuwaimarisha kabla ya kwenda kuwaangusha maadui zao kule Kaanani. Aliwapitishwa mitume wako, kwanini na wewe usipitishwe?

Vivyo hivyo ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, ambaye utapenda Bwana akutumie, basi liweke kichwani kwamba kuna mahali fulani utapitishwa ili kuimarishwa, huo ndio ubatizo wa Moto ulio wa Roho Mtakatifu. Wakati huo usimwache Bwana, kuwa fungu la tatu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI KRISTO AFE?

Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?

(Opens in a new browser tab)MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.(Opens in a new browser tab)

AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.

Rudi Nyumbani

Print this post

NAYE NENO ALIFANYIKA MWILI.

Je unaielewa vyema hii sentensi? “..Naye Neno alifanyika Mwili”.

Yohana 1:14 “Naye NENO alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli”.

Je ulishawahi kuzungumza na mtu kwa simu?.. Je anapozungumza na wewe huwa unamwona?? Au unayasikia MANENO YAKE TU?.. Ni wazi kuwa humwoni ila unasikia MANENO YAKE.

Lakini atakapokujia na kusema nawe ana kwa ana..hapo utakuwa UNAMWONA na pia UNAYASIKIA MANENO YAKE YANAYOTOKA KATIKA KINYWA CHAKE.

Hivyo tunaweza kusema kuwa wakati anaongea nawe kwenye simu yalikuwa ni Maneno tu (Pasipo yeye kumwona), lakini alipokujia na kusema nawe ana kwa ana yalikuwa ni Maneno yale yale isipokuwa yanatoka ndani ya mwili unaoonekana..KWA LUGHA NYINGINE TUNAWEZA KUSEMA NI MANENO YALIYOUVAA MWILI.

Na siri ya UUNGU wa YESU, inaanzia hivyo hivyo… Kwamba hapo Mwanzo Mungu alisema nasi kwa NENO LAKE pasipo yeye kuonekana… Lakini baadaye yeye mwenyewe akaja katika mwili na kuonekana na kusema MANENO YALE YALE kupitia mwili unaoonekana…

Mtume Paulo kaielezea vizuri hiyo siri katika 1Timotheo 3:16

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. MUNGU ALIDHIHIRISHWA KATIKA MWILI, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.

Lakini sio tu Mtume Paulo aliyefunuliwa hiyo siri, bali pia Mtume Yohana, aliyekuwa mwanafunzi wa BWANA YESU, alifunuliwa hiyo siri ya MUNGU kudhihirika katika mwili..

Yohana 1:1 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.

2  Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.

3 Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika…………

14 NAYE NENO ALIFANYIKA MWILI, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.”

Na huyu Neno aliyevaa mwili alikuwa si mwingine Zaidi ya BWANA YESU KRISTO, MKUU WA UZIMA!!!.

Tena Mtume huyu huyu Yohana kazidi kuliweka hili wazi katika nyaraka yake nyingine aliyoiandika kwa watu wote.. na kusema kuwa lile NENO lililokuwa linasikiwa zamani, limefanyika mwili, na wakaushika ule mwili na kuupapasapasa (yaani mwili wa BWANA YESU).

1Yohana 1:1 “Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima”

Kumbe hili Neno lilianza kwa kusikiwa, baadaye likaonekana (maana yake lilivaa mwili)..na Mitume wakalipapasa (maana yake waliushika mwili wa BWANA YESU) kabla na baada ya kufufuka.

Kwahiyo KRISTO ni Neno la MUNGU na ni MUNGU pia aliyeuvaa mwili, ni Mungu pamoja nasi (Imanueli) ndio maana katukuka kuliko vitu vyote na viumbe vyote.

Je umemwamini na kumpokea maishani mwako?..kama bado fahamu kuwa hakuna njia nyingine yoyote ya kufika mbinguni isipokuwa kwa njia ya yeye. Na pia hakuna mtu wala malaika, wala kiumbe kingine chochote kitakachoweza kukupenda wewe au mimi katika viwango atupendavyo BWANA YESU.

Sasa ni heri umtumainie huyu YESU ambaye si mnafiki katika upendo, mwanadamu anaweza kukunafikia, mchungaji anaweza kukunafikia, lakini YESU, ni wa UPENDO USIO NA UNAFIKI NDANI YAKE. Yasikilize maneno yake, yakubali na yapokee.

BWANA AKUBARIKI.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

“WOKOVU WETU U KARIBU NASI KULIKO TULIPOANZA KUAMINI”

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

Roho Mtakatifu ni nani?.

Rudi Nyumbani

Print this post

MAMBO SITA, AMBAYO MUNGU HUTUMIA KUONDOA UOVU NDANI YA MTU.

Nakusalimu katika jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo, karibu katika kujifunza Neno la Mungu. Leo tutaona mambo Makuu sita (6), ambayo Mungu anatumia kuondoa uovu ndani ya mtu, na kumfanya awe mtakatifu kabisa kama yeye alivyo. Ikiwa wewe umemfuata Kristo basi tarajia mambo haya matano atayatumia katika maisha yako, kukukamilisha.

  1. Damu
  2. Maji
  3. Moto
  4. Fimbo
  5. Pepeto
  6. Dawa

Tukianza na

DAMU:

Kumbuka sisi sote tulizaliwa na deni la dhambi. Hivyo tulistahili hukumu ya mauti, (Warumi 6:23), Lakini deni hilo lilikuja kulipwa na Bwana wetu Yesu kwa kifo chake pale msalabani (Warumi 5:8). Kumwagika kwa damu yake, sote tumepokea “msamaha wa dhambi” bure kwa neema. Hakuna mwanadamu yoyote anayeweza kukubaliwa na Mungu, kwa uweza wake mwenyewe. Kwahiyo damu ya Yesu imekuwa hatua ya kwanza ya sisi kukubaliwa na Mungu.

Sasa tunaweza kupokea msamaha kweli, tukasemehewa, lakini dhambi bado ikawepo ndani yetu. Na hilo sio kusudu la Mungu atusemehe tu, halafu atuache tuendelee kuwa watumwa wa dhambi ndani kwa ndani. Si lengo la Mungu, hata mtu mwenye upendo wa dhati wa Yule aliyekosewa naye, anapoona amemsamehe, huwa hamwachi tena kesho arudie kosa lile lile ili, amsamehe, hapana, bali humwonyesha njia ya kuepuka makosa ili yeye mwenyewe aweze kusimama kwa ujasiri mbele zake. Na ndivyo ilivyo kwa Mungu mara baada ya kupokea msamaha wa dhambi, huyo mtu anaanza hatua ya utakaso wa Mungu ambao sasa hufanywa na Roho Mtakatifu aliyeingia ndani yake, Ndio hapo inakuja hatua ya pili,

NENO:

Biblia inasema Neno ni kama maji, ambayo yanasafisha.

Waefeso 5:26  ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; 27  apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.

Umeona, Kristo hulisafisha kanisa lake, kwa Neno, ndio maana wewe kama mtu uliyempokea Yesu, Ni lazima uwe na juhudu nyingi sana za kusoma Neno la Mungu kila siku, usikie maonyo, fundisho, agizo,  njia, (2Timotheo 3:16), Na kwa jinsi unavyojifunza sana, ndivyo unavyosafishwa moyo wako na roho yako, hatimaye unaanza kujiona mtu ambaye huna hatia ndani yako. Na hapo ndipo unapojikuta unaacha baadhi ya mambo uliyokuwa unafanya huko nyuma. Kumbuka biblia uliyonayo sio kitambulisho cha mkristo au pambo la mkoba, bali ni maji hayo ya kukusafisha, hivyo oga kila siku, uwe msafi. Kwasababu usipofanya hivyo utakuwa mchafu tu sikuzote.

MOTO:

Kwa kawaida sio kila uchafu hutoka kwa maji, mwingine huitaji moto ili kuundoa. Kwamfano ukiupata mwamba wenye dhahabu ndani yake ukipitisha maji huwezi toa uchafu uliogandamana nao,hivyo wale wafuaji, wanaupitisha kwenye moto, kisha unayeyuka na baada ya hapo uchafu na dhahabu hujitenga kisha wanaikusanya dhahabu. Ndivyo ilivyo na Mungu kwa watoto wake. Upo moto ambao wewe kama mwana wa Mungu ni lazima tu utapitishwa hata iweje, kuondoa mambo sugu yaliyogandamana na wewe yasiyoweza kutoka kwa Neno tu bali kwa hatua ya kimaisha, ndio huo unaoitwa “ubatizo wa moto”. Mfano wa huu ndio ule uliompata mfalme Nebukadreza (Danieli 4), kukaa miaka saba maporini kula majani ili tu aondolewe kiburi ndani yake. Ni aina Fulani ya maisha ambayo kwako yatakuwa kama moto, lakini mwisho wake hukuletea faida ya roho yako.

1Petro 1:6  Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;7  ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.

FIMBO:

Zipo tabia nyingine ambazo Mungu anaona mwanawe anakuwa nazo kwa ujinga tu, hivyo, ili kuundoa ujinga huo, haihitaji maji wala moto, bali kiboko. Anapoona unafanya jambo Fulani kwa makusudi na alishakukataza hapo awali fahamu pia kiboko kitapita juu yako.

Waebrania 12:6  Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye.

7  Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye?

8  Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali. 9  Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi?

10  Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake.

Biblia inasema pia..

Mithali 22:15 Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.

PEPETO:

Yohana mbatizaji kwa uvuvio wa Roho aliandika maneno haya kuhusu  Bwana Yesu..

Mathayo 3:11  Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.

12  Ambaye pepeto lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya ngano yake ghalani, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.

Yesu akija kwako, fahamu kuwa mkononi ameshika pepeto pia, na wewe utawekwa juu yake, Anajua kabisa ulipo wewe makapi pia yapo, uliyotoka nayo huko shambani (ulimwenguni), hivyo ili kukutenga nayo, ataanza kukupepeta, kama vile ngano, utarushwa juu, utashushwa chini, utarushwa juu utashushwa chini, huwezi kuachwa utulie, lengo ni kuhakikisha makapi yote yanapeperushwa na upepo, iwe ni watu, vitu, utaona tu unapelekwa mbele, unarudishwa nyuma..baadaye akishaona ni ngano tu imebakia chini, hapo ndipo anapokuacha, unaanza kuona ushwari. Hii ilimkuta Ibrahimu, Bwana anamtoa Uru, anampeleka kaanani, mara anakimbilia Misri, mara anarudisha, lakini baadaye Mungu alimpa pumziko, baada ya kuona wote waliokuwa wameshikamana naye hawapo naye.

Usishangae kutokuwa na utulivu katika nyakati fulani za maisha yako wokovu, wakati Fulani unafanikiwa, halafu unarudi chini, wakati Fulani unapata amani kotekote, gafla inaondoka, unapata, ghafla tena unapoteza, tulia tu, kuwa na amani ndani ya Kristo, utakuwa tu, imara, wala hiyo misukosuko haitakuwepo tena, ni kwanini iwe hivyo? Ni kwasababu makapi yanapeperushwa na upepo.

DAWA:

Kaa ukifahamu Yesu anajulikana pia kama tabibu,(Marko 2:17) na anajua maovu mengine unayoyafanya yanatokana na magonjwa na majeraha ya rohoni, anajua hali yako ilivyo hivyo anachokifanya ni kukutibu yeye mwenyewe, ndio hapo unashangaa tu mwingine anatokwa na mapepo yaliyokuwa yanamsumbua na kumpelekea kutenda dhambi mwingine anapona udhaifu fulani, uliokuwa unamfanya amkosee Mungu, mwingine anapokea faraja, amani, utulivu usio wa kawaida, anashangaa kuona tofauti kubwa  ya sasa na hapo kabla. Hili nalo mtu aliyempokea Kristo ataliona kwenye maisha yake. Na atimaye anakuwa mwema yeye tu mwenyewe, asukumwi tena na presha ya dhambi fulani. Kwasababu tabibu mkuu ameshamponya, ambaye akikuweka huru, unakuwa huru kwelikweli.

Ufunuo 3:18

Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na DAWA ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

Hivyo, wewe kama mwana wa Mungu, tambua yote hayo yatapita katika sehemu Fulani ya maisha yako. Usidhani kusafishwa tu na damu ya Yesu ndio basi, utatakaswa na hiyo ni katika maisha yako yote. Haiwezekani mtu aliyeokoka ambaye amepokea Roho maisha yake yote awe Yule Yule wa zamani, hizo sio kanuni za wokovu, wala sio kusudi la Mungu. Ukubali utakaso, au usiwe mkristo kabisa. Kwasababu hivi viwili huenda sambamba wala haviwezi kutenganishwa. Huo ndio upendo wa Mungu.

Utukufu na heshima ni vyake  milele na milele.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> hhttps://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

(Opens in a new browser tab)UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.

Ipi tofuati kati ya UTAKATIFU na UKAMILIFU?

Rudi Nyumbani

Print this post

UTUKUFU WA MUNGU, UPO KATIKA UMOJA

Umoja katika Ukristo ni jambo linalokimbiwa na wengi lakini ndilo jambo pekee lililobeba UTUKUFU WA MUNGU wa moja kwa moja. Na maana ya Utukufu wa Mungu ni “MUNGU KUTUKUZWA”.. Maana yake Mungu anatukuzwa katika Umoja.

Labda utauliza ni kwa namna gani?.. Tusome maandiko yafuatayo..

Yohana 17:22 “Nami UTUKUFU ULE ULIONIPA nimewapa wao; ILI WAWE NA UMOJA kama sisi tulivyo umoja.

23  Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”

Kumbe Utukufu Kristo aliotuachia lengo lake la kwanza ni ili tuwe na UMOJA.. Na si kutenda miujiza, na maajabu.. Maana yake Mungu anatukuzwa Zaidi katika UMOJA kuliko katika MIUJIZA na ISHARA. Na ndicho kitu pekee kilicho na nguvu ya kuwafanya watu wamwamini Mungu kuliko ishara na miujiza.

Watu watakapoona umoja wetu katika Mungu, ndipo watavutwa kumwamini Mungu kuliko hata kuona ishara na miujiza halafu hamna Umoja… Na ndicho kitu pekee kinachotufanya sisi tumwamini BWANA YESU, ni kwasababu alikuwa na Umoja na Baba.

Laiti Bwana YESU asingelikuwa na umoja na Baba, ingelikuwa ngumu kumwamini kwa ishara na miujiza pekee, lakini ule Umoja wa Roho kati yake na Baba, umetutengenezea sisi Upendo wa ajabu, na Imani kuu kwa BWANA YESU KRISTO, Kwamba yeye ni kweli na hamna uongo ndani yake.

Na vile vile sisi tukiwa na Umoja na Mungu, na tukiwa na umoja sisi kwa sisi ndipo USHUHUDA WETU UTAKAPOTHIBITIKA ZAIDI kuliko kukaa katika matengano.

Yohana 17:21 “WOTE WAWE NA UMOJA; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ILI ULIMWENGU UPATE KUSADIKI YA KWAMBA WEWE NDIWE ULIYENITUMA.

22  Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.

23  Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.

Hapo mstari wa 21 anasema.. “WOTE WAWE NA UMOJA ….ILI ULIMWENGU UPATE KUSADIKI YA KWAMBA WEWE NDIWE ULIYENITUMA”.

Kumbe UMOJA WETU ndio utakaowaaminisha watu kuwa KRISTO ni BWANA! Na si mahubiri yetu kuwa mengi, au miujiza yetu kuwa mingi…ni UMOJA TU!.

Tukilikataa Neno hili, na kufuata njia zetu za matengano, tutakuwa tunajipunguzia wenyewe utukufu wa Mungu, kwasababu KRISTO hakujitenga na Baba, wala hakujitenga na wanafunzi wake.

> Unapochagua kuomba peke yako kila mara na huku ipo nafasi ya kuomba na mwingine mmoja au wawili ni roho ya matengano inayoondoa utukufu wa Mungu. (Bwana wetu YESU KRISTO mara nyingi alipanda mlimani kuomba na wanafunzi wake, na hata katika sehemu za faragha soma Mathayo 17:1, na Marko 14:33-34).

> Unapochagua kila mara kwenda kuhubiri peke yako na wakati kuna nafasi ya kwenda na mwingine mmoja au wawili, ni roho ya matengano ambayo inapunguza utukufu wa Mungu juu yako (Bwana YESU aliwatuma wawili wawili kuhubiri katika miji na vijiji soma Luka 10:1 na Matendo 13:2).

> Unapochagua kila mara kutosema na ndugu yako, kumfariji, au kumtia moyo au kukaa karibu naye, ili hali ni mtu wa Imani moja nawe, mnamwamini Bwana mmoja, mmepokea roho mmoja, na hata ubatizo mmoja hiyo ni roho ya matengano inayoharibu utukufu wa Mungu juu yetu.

Hivyo ni lazima tuuhifadhi Umoja wa Roho kama Neno la Mungu linavyotufundisha ili tusipungukiwe na utukufu wa Mungu.

Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.

4  Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.

5  Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.

6  Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”

Bwana atusaidie na kutuwezesha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TUUTAFUTE UMOJA WA ROHO.

JE UNAMHUBIRI KRISTO KATIKA KWELI YOTE?.

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

MARINDA KATIKA BIBLIA NI KITU GANI?

BWANA ni mtu wa vita,  BWANA ndilo jina lake.(Kutoka 15:3)

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 21:30 Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri,  juu ya Bwana.

SWALI: Nini maana ya Mithali 21:30 Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri,  juu ya Bwana ?


JIBU: Mstari huo unaweza ukasemwa hivi; “Hapana hekima, wala ufahamu, wala shauri linaloweza kufanikiwa/kusimama kinyume na Mungu”.

Ikiwa na maana iwe ni mwanadamu au malaika, atumie uwezo wake wote, kufanya jambo la hila kinyume na yeye haliwezi kufichika kwasababu yeye ni mkuu zaidi ya vyote. Mpango wa shetani kuliharibu kanisa huawezi kufanikiwa hata azidishe kufanya kazi mara elfu zaidi ya mwanzo hilo haliwezekani kama lilivyoshindikana mbinguni.

Mambo yote yanayotokea hayafiki kwake ghafla tu bila hodi, kama ilivyo kwetu sisi wanadamu. Elimu ya darasani haiwezi pindua ukweli wake wa uungu, wajaposema mwanadamu ametokana na nyani, mwishoni wanarudia kule kule kwenye ukweli wa uumbaji wa kiungu, kwasababu atabakia kusimama kuwa Mungu wa daima, na ataabudiwa vizazi vyote haijalishi dunia itaelimika kiasi gani.

Mungu Anajua mawazo yetu yote tokea mbali, wewe kama mwanadamu huwezi mficha dhambi zako, ukajifanya  mbele zake umesahau, au ulikuwa hujui, hata utumie hekima nyingi kiasi gani kuficha ukweli bado anatambua nia ya mioyo yetu.

Anasema;

Zaburi 50:17 Maana wewe umechukia maonyo, Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.  18 Ulipomwona mwivi ulikuwa radhi naye, Ukashirikiana na wazinzi.

19 Umekiachia kinywa chako kinene mabaya, Na ulimi wako watunga hila.  20 Umekaa na kumsengenya ndugu yako, Na mwana wa mama yako umemsingizia.

21 NDIVYO ULIVYOFANYA, NAMI NIKANYAMAZA; UKADHANI YA KUWA MIMI NI KAMA WEWE. Walakini nitakukemea; Nitayapanga hayo mbele ya macho yako.

22 Yafahamuni hayo, Ninyi mnaomsahau Mungu, Nisije nikawararueni, Asipatikane mwenye kuwaponya.

Pale tunapomwona Mungu ni kama sisi ndio unakuwa mwanzo wa kuto-mhofu  yeye. Unapokuwa na udhuru wa kuifanya kazi yake halafu unasingizia sina muda, lakini una muda wa kufanya mambo yako, ukidhani yeye hajui nia yako ya ndani, unajidanganya mwenyewe. Unapoepuka maombi, kwa kisingizio umechoka, na bado unataka Mungu akuhudumie, fahamu Mungu anakuelewa vizuri sana, atakuonyesha ambao wanachoka zaidi yako, lakini hawana udhuru. Jambo lolote tulifanyalo, tutambue kwanza kwa Mungu halifichiki.

Kwasababu Hapana hekima, wala ufahamu, wala shauri litakalosimama kinyume cha Mungu

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya Mithali 19:21Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.(Opens in a new browser tab)

Je shauri la kuipepeleza Kanaani lilitoka kwa wana wa Israeli au kwa BWANA?(Opens in a new browser tab)

Tofauti kati ya Hekima, ufahamu na maarifa, ni ipi?

(Opens in a new browser tab)Maana ya Mithali 11:17 Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 21:17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini;

SWALI: Nini maana ya  Mithali 21:17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini; Apendaye mvinyo na mafuta hatakuwa tajiri.


JIBU: Mstari huo unamaana mbili.

Maana ya kwanza ni ya mwilini, ni ukweli watu wanaopenda maisha ya anasa, mwisho wao huwa ni kutofanikiwa. Kwasababu kile wanachokipata ambacho kingepaswa kiwekwe akiba kwa wakati wa baadaye au kiwekezwe kizalishe zaidi, wao hutumia chote katika starehe mfano wa pombe, uasherati, na kununua vitu vya gharama kubwa, lengo tu asionekane amepitwa na wakati, au aonekane wa kisasa.

Hapo anaposema apendaye mvinyo na mafuta, hayo mafuta yanayozungumziwa hapo ni marashi ya gharama ambayo zamani waliokuwa wananunua ni matajiri. Ni sawa na leo labda mwajiriwa analipwa mshahara wa laki tatu (3) kwa mwezi, halafu anakwenda kununua perfume (marashi), ya  laki 2, ili tu aonekane wa kisasa, hiyo ni anasa, na mwisho wake ni umaskini.

Anasa ni tunda la majivuno, na kukosa adabu. Hivyo biblia inamfundisha mwanadamu yoyote kuwa, anasa ni kinyume cha mafanikio.

Lakini pia rohoni, anasa ni zao la ufukara wa ki-Mungu. Mtu wa anasa, hutumia muda wake vibaya, kwasababu nyakati zake za ziada huishia kwenye starehe za kimwili na sio kwenye mambo ki-Mungu.

Bwana alisema;

Luka 8:14  Na zilizoanguka penye miiba ni wale waliosikia, na katika kuenenda kwao husongwa na shughuli na mali, na anasa za maisha haya, wasiivishe lo lote.

Umeona? Anasa husonga mbegu ya Mungu ndani yako.

Katika kizazi cha sasa anasa ni pamoja na kushinda kwenye tv kutazama muvi kila kukicha, ni pamoja na kushinda mitandaoni kufuatilia vipindi vinavyokupa raha za kimwili na kihisia lakini havikujengi rohoni,  ni kuwekeza muda wako katika matanuzi ya mijini na kwenye sherehe-sherehe za kila mara ambazo hazina mpangalio. Muda wote akili yako ipo katika kile kitu wanachosema “ku-party weekend” na marafiki. Ushikapo simu yako, usiku wote ni kuchat, na wale wanaowaita ma-boyfriend na ma-girlfriend. Muda ambao ungepaswa kusoma Neno na kuomba.

Sasa ikiwa wewe umeokoka, na una mwenendo huo wa maisha, usitazamie hapo utazalisha kitu. Utabakia kuwa Yule Yule milele. Biblia inasema ni heri kuona kwa macho kuliko kutangatanga kwa tamaa(Mhubiri 6:9). Sio kila taarifa uifuatilie, sio kila kitu ukitende, viache vingine vikupite, ili upate nafasi ya kuwa karibu na Mungu wako, uwe mtu wa matunda. Komboa wakati.

Shalom..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa.

(Opens in a new browser tab)APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 4)(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 18:22 Apataye mke apata kitu chema

SWALI: Je andiko hili humaanisha nini? kupata mke ni kujipatia kibali cha kumkaribia Mungu tofauti na  hapo mwanzo?

Mithali 18:22

Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa BWANA. 

JIBU: Andiko hili hutafsiriwa vibaya na watu wengi, wakiamini kuwa pale mtu anapoingia kwenye ndoa basi ndio amejizidishia kibali cha kukubaliwa na Mungu katika maisha yake. Jibu ni hapana, kibali kwa Mungu sio ndoa, kibali kwa Mungu ni “kufanya vema mapenzi ya Mungu” .

Mungu alimwambia kaini maneno haya

Mwanzo 4:7

[7]Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde. 

Zaidi pia, maandiko yanaeleza ipo nafasi kubwa kwa mtu  kumkaribia Mungu anapokuwa hajaoa/kuolewa kuliko yule aliyeoa au kuolewa.Kwasababu ambaye hajaoa/ olewa hupata nafasi ya kutosha kumtafuta Bwana na kumfikiria yeye ampendezeje.

1 Wakorintho 7:32-33

[32]Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana; 

[33]bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe. 

Lakini je! andiko hilo humaanisha kibali gani?

“Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa BWANA”. 

Tafsiri ya Neno hilo ni kuwa Mungu analikubali jambo hilo(Ndoa), analibariki, na pia analiona ni jema. Hivyo mtu asidhani kuwa aingiapo katika ndoa atamkosea Mungu, au Mungu atapunguza ukaribu naye. Hapana, kinyume chake atapata kibali tu. Hivyo awe na furaha na amani afanyavyo hivyo.

Makala Yanayofadhiliwa Tafuta kitu kwa kila mtu katika mkusanyiko wetu wa soksi za rangi, http://www.swisswatch.is best replica watches angavu na maridadi. Nunua kibinafsi au kwa vifurushi ili kuongeza rangi kwenye droo yako!

kwasababu pia zipo faida zinazoambata na mtu aliyeoa, mojawapo ni kujiongezea heshima kwa jamii lakini pia kuaminiwa zaidi. Na hilo ni jema husasani katika utumishi & huduma.

Lakini haimaanishi kuwa unapooa ndio Mungu anakukubali zaidi ya ule wakati ambao ulikuwa hujaoa/kuoelewa, au zaidi ya yule mtu ambaye hafikirii kuoa.

Mtume Paulo, Barnaba hawakuoa na zaidi mwokozi wetu Yesu Kristo hakuoa lakini tunaona ni jinsi gani walivyojirahisishia nafasi zao  kwa Mungu. 

kwa mafundisho zaidi kuhusu ndoa pitia masomo chini;

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAFUNDISHO YA NDOA.

MWANAMKE UKITAKA KIBALI, USIWE MTU WA KUPENDA VITU. (Esta 2:17)

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 10:5 Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima; 

SWALI: Nini maana ya;

Mithali 10:5 Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima; Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha. 

JIBU: Kwa kawaida kipindi cha hari ( kiangazi), huwa ndio kipindi cha mavuno mengi. kwasababu mavuno yanakuwa yameshakomaa na kukauka.

Hivyo wakulima wengi kwa nyakati hizo wanakuwa mashambani kuvuna, kama vile tu walivyokuwa wakati wa masika walipokuwa wanapanda..

Na ni kipindi ambacho mkulima hufurahi pia kwasababu anakwenda kuona matunda ya kazi yake wakati si mwingi.

Lakini ni ajabu kuona, mtu ambaye hajasumbukia kupanda, halafu anaambiwa tu yeye akavune, tena kwa faida yake mwenyewe akauze, anaona uvivu kwenda kuvuna, hataki kabisa kwenda kujishughulisha na kazi hiyo, mpaka msimu mwingine unakuja, mazao yanaharibikia yote shambani. Mtu kama huyo utamchukuliaje? Ni sawa tu akiitwa  “mwana mwenye kuaibisha”, Kwasasababu ni uvivu wa makusudi.

Sasa jambo kama hili kwasasa lipo pia rohoni.

Na lipo kwa namna mbili.

1.) Katika kazi ya Mungu.

Bwana Yesu alisema..

Yohana 4:35-38

[35]Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno. 

[36]Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele, ili yeye apandaye na yeye avunaye wapate kufurahi pamoja. 

[37]Kwa maana hapo neno hilo huwa kweli, Mmoja hupanda akavuna mwingine. 

[38]Mimi naliwatuma myavune yale msiyoyataabikia; wengine walitaabika, nanyi mmeingia katika taabu yao. 

Umeona? Kufuatana na vifungu hivyo Bwana anatuonyesha kuwa tupo wakati wa mavuno sasa, wakati wa hari, wa kiangazi, mashamba yamekwisha kuwa meupe,  Hivyo sote kwa pamoja kwa moyo mmoja yatupasa tutoke tuanze kuifanya kazi ya Mungu bila ulegevu kwasababu Yesu alishatupa agizo kuu kuwa tutoke tuenende ulimwenguni kote kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi.

Lakini ukilala na kusema huu si wakati, ndugu ni sawasawa na hilo neno unakuwa mwana mwenye kuaibisha. Kila mmoja wetu ameitwa kuwahubiria wengine habari njema za wokovu wa Yesu Kristo, haijalishi upo ofisini, shuleni, ugenini, jeshini, una wajibu wa kuvuna. Shika mundu yako washuhudie wengine habari njema, kwasababu huu ni wakati  sahihi, na hautadumu milele.Hivyo tumia muda vizuri.

2) Katika kipindi cha maisha ulichopo.

Neno la Mungu linasema..

Mhubiri 12:1

[1]Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya,  Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo. 

na pia linasema..

1 Yohana 2:14

[14]Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.

Katika umri wako wa ujana ambao una nguvu ndio wakati wa kwenda shambani kumtumikia Bwana wako. ndio wakati wako wa hari, lakini unapokuwa mlegevu, hujishughulishi na Mungu wako, unachowaza ni anasa, starehe, mihangaiko, unasema nitamtumikia Mungu uzeeni, fahamu kuwa wewe ni sawa na mwana mwenye kuaibisha, kwasababu wakati huo utakuwa umeshapita.

Komboa wakati wako, thamini majira uliyopo, etende kazi ya Bwana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

Maana ya Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu 

Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;

Rudi Nyumbani

Print this post

Kuhani wa Oni alikuwa nani?

Swali: Huyu Kuhani wa Oni ambaye binti yake aliolewa na Yusufu, tunayemsoma katika Mwanzo 41:45  je alikuwa ni kuhani wa Mungu au wa kuhani wa miungu ya kiMisri?

Jibu: Terejee mistari hiyo…

Mwanzo 41:45 “Farao akamwita Yusufu, Safenath-panea; akamwoza Asenathi, binti POTIFERA, KUHANI WA ONI, kuwa mkewe Yusufu akaenda huko na huko katika nchi yote ya Misri”.

“Oni” lilikuwa ni eneo katika nchi ya Misri, kama vile ilivyo Mwanza, au Lindi nchini Tanzania au Nakuru Kenya.

Mji huu (wa Oni) Ulikuwa ni mji wa miungu ya kiMisri, na nchi ya Misri yote ilikuwa ni nchi inayoabudu miungu mingi,  ikiwemo Bethshemeshi (soma Yeremia 43:13), sanamu za ng’ombe (1Wafalme 12:28) na mingine mingi (soma Yoshua 24:14).

Hivyo huyu kuhani “Potifera” hakuwa kuhani wa Mungu wa mbingu nan chi (YEHOVA), bali alikuwa ni kuhani wa miungu ya kimisri iliyokuwepo hapo “Oni”, na Yusufu alipofika kule alipewa binti yake awe mkewe.

Na Kwanini ulikuwa hivyo?(yaani kwanini Farao amchagulie mke na si Yusufu ajitafutie mwenyewe?)..

Jibu ni kwamba Farao aliona njia pekee ya kumheshimisha Yusufu na kumfanya apate kibali katikati ya waMisri ni kumuunganisha yeye na familia za watu wa kubwa na wenye hadhi wa nchi ya Misri.(wenye hadhi za kiimani), kwasababu naye Yusufu alikuwa mtu wa kiimani.

Hivyo na mtu wa kiimani na kidini aliyekuwa mkubwa huko ni huyo kuhani wa Oni, ndipo akapewa binti yake aliyeitwa Asenathi. Lakini hata baada ya Yusufu kupewa mwanamke huyo bado hakufuata miungu hiyo ya kiMisri, na Farao alilijua hilo, na wala hakumpatia huyo binti kwa lengo la kugeuza Imani ya Yusufu, bali kumheshimisha.

Lakini kwasababu pia ilikuwa ni mpango wa Mungu iwe hivyo (Yusufu aoe mwanamke wa kimataifa) basi hata mke aliyempata alikuwa ni sahihi kwake na wala hakumsumbua Yusufu baada ya hapo (huwenda hata alimtumikia Mungu wa Israeli baada ya hapo), na Zaidi sana tendo la Yusufu kumwoa Asenathi (binti wa kimataifa) limebeba ufunuo mkubwa juu ya Bwana  YESU KRISTO na BIBI-HARUSI WAKE (yaani kanisa).

Kwa urefu marefu juu ya ufunuo wa maisha  ya Yusufu fungua hapa >>>Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Musa aliua lakini bado Mungu alimchangua kuwaongoza wana wa Israeli, je! Mungu anaruhusu mauaji?

ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.

UNAMFAHAMU MUNGU WA KWELI?

Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.

Ni lini na wapi Ibrahimu aliiona siku ya Bwana akashangilia?.

Rudi Nyumbani

Print this post

TEMBEA KATIKA NJIA KUU

Jina la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe daima. Karibu katika mafundisho ya biblia, Neno la Mungu wetu lililo Taa na Mwanga wa Njia zetu (Zab.119:105).

Zipo njia Mbili tu zilizowekwa mbele ya kila mwanadamu, Nazo ni njia ya UZIMA, na njia ya MAUTI.

Yeremia 21:8 “Nawe waambie watu hawa, Bwana asema hivi, Tazama naweka mbele yenu NJIA YA UZIMA, na NJIA YA MAUTI”.

Njia ya Uzima, inamwongoza mtu “Uzimani”..na Njia ya Mauti inamwongoza mtu “Mautini (ziwa la moto)”.

Njia ya Uzima imenyooka haina migawanyiko mingi (sawasawa na Yohana 14:6), ambapo Bwana YESU alisema yeye ndio hiyo “Njia”, na mtu hafiki kwa Baba isipokuwa kwa njia yake yeye.

Yohana 14:6  “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”

(Maana yake hakuna njia mkato wala njia mbadala ya kumfikia Baba)…Ni moja tu! Tena iliyonyooka, nayo ni YESU KRISTO, na si kupitia mtu mwingine yoyote mashuhuri, au mtakatifu mwingine yoyote aliye hai au aliyekufa au nabii yoyote katika biblia.

Lakini ile ya Mauti inamigawanyiko mingi, inaanza kama njia moja lakini mwisho wake inamigawanyiko,

Mithali 14:12 “IKO NJIA ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni NJIA ZA MAUTI”

Hapo anamaliza na kusema mwisho wake ni “NJIA ZA MAUTI” na si “NJIA YA MAUTI” kana kwamba ni moja, bali nyingi. Na njia ya Mauti si mwingine Zaidi ya “shetani”…Kama jinsi njia ya UZIMA ilivyo Bwana YESU kadhalika njia ya Mauti ni “shetani”.

Na shetani anaabudiwa kupitia vitu vingi, anaweza kuabudiwa kupitia miti, mawe, udongo, au kupitia vitu vitu vingine kama fedha, watu, dini n.k..ndio maana hapo biblia inasema hiyo Njia (shetani) mwisho wake ni “Njia za Mauti” (maana yake zipo nyingi).

Na hiyo ndio sababu pia kwanini biblia inataja uwepo wa milango mingi ya kuzimu (Soma Mathayo 16:18). Milango ya kuzimu ndio hizo njia zote zinazoweza kumpeleka mtu kuzimu.

Nabii Isaya amezidi kuziweza vizuri njia hizi kwa ufunuo wa Roho… Amezitofautisha kama “NJIA” pamoja na “NJIA KUU”..

Isaya 35:8 Na hapo patakuwa na NJIA KUU, na NJIA….”

“Njia Kuu” ni “Njia ya Uzima”…. Na “Njia” pekee yake “Ni njia ya Mauti”..

Lakini anaendelea kusema… hiyo “Njia kuu” itaitwa Njia ya utakatifu, na ya watu wasafirio..

Isaya 35:8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio….”

Maana yake wote wanaiendea hiyo njia ya Uzima (YESU) Ni lazima “utakatifu” uwe muhuri wao sawasawa na kitabu kile cha Waebrani 12:14.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”.

Vile vile ni lazima wawe “wasafiri”.. Tabia ya msafiri huwa anadumu katika chombo cha usafiri awapo safarini, na hawezi kujishikisha na mambo akutanayo njiani au barabarani…. na chombo chetu cha usafiri ni NEEMA YA MUNGU.  Tuwapo katika safari hii ya kwenda mbinguni kupitia njia ya Bwana YESU, mambo ya ulimwengu hayapaswi yashikamane  na sisi.

1Petro 2:11  “Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho”.

Na mwisho anasema.. “wajapokuwa wajinga hawatapotea katika njia hiyo”

Isaya 35:8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, WAJAPOKUWA WAJINGA, HAWATAPOTEA KATIKA NJIA HIYO”. 

Ikiwa utaonekana mjinga kwa kuwa umeamua kuifuata NJIA KUU ya UTAKATIFU na umeamua kuishi kama MSAFIRI duniani, basi biblia inasema “hautapotea/hatutapotea” katika njia hiyo..

Haijalishi dunia nzima itakuona kama umepotea, umerukwa na akili, umechanganyikiwa…Mungu yeye anakuona upo katika njia sahihi na una hekima nyingi.. kwasababu mwisho wa njia hiyo ni UZIMA WA MILELE, Na Utakutana na Bwana naye atakufuta machozi.

Ufunuo 7:15 “Kwa hiyo wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, nao wanamtumikia mchana na usiku katika hekalu lake, na yeye aketiye katika kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao

16  Hawataona njaa tena, wala hawataona kiu tena, wala jua halitawapiga, wala hari iliyo yote.

17  Kwa maana huyo Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha enzi, atawachunga, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji yenye uhai, na Mungu atayafuta machozi yote katika macho yao.”

Je wewe leo umechagua njia ipi??… Njia kuu ya Uzima? Au Njia ya Mauti..

Kumbukumbu 30:14 “Lakini neno li karibu nawe sana, li katika kinywa chako na moyo wako, upate kulifanya.

15 ANGALIA, NIMEKUWEKEA LEO MBELE YAKO UZIMA NA MEMA, NA MAUTI NA MABAYA”.

CHAGUA NJIA YA UZIMA, na TEMBEA KATIKA NJIA KUU YA UTAKATIFU.

BWANA AKUBARIKI.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

HATARI YA KUTOKUITAFAKARI BIBLIA VIZURI?

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

Rudi Nyumbani

Print this post