Category Archive Mafundisho

UTUKUFU WA MUNGU, UPO KATIKA UMOJA

Umoja katika Ukristo ni jambo linalokimbiwa na wengi lakini ndilo jambo pekee lililobeba UTUKUFU WA MUNGU wa moja kwa moja. Na maana ya Utukufu wa Mungu ni “MUNGU KUTUKUZWA”.. Maana yake Mungu anatukuzwa katika Umoja.

Labda utauliza ni kwa namna gani?.. Tusome maandiko yafuatayo..

Yohana 17:22 “Nami UTUKUFU ULE ULIONIPA nimewapa wao; ILI WAWE NA UMOJA kama sisi tulivyo umoja.

23  Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”

Kumbe Utukufu Kristo aliotuachia lengo lake la kwanza ni ili tuwe na UMOJA.. Na si kutenda miujiza, na maajabu.. Maana yake Mungu anatukuzwa Zaidi katika UMOJA kuliko katika MIUJIZA na ISHARA. Na ndicho kitu pekee kilicho na nguvu ya kuwafanya watu wamwamini Mungu kuliko ishara na miujiza.

Watu watakapoona umoja wetu katika Mungu, ndipo watavutwa kumwamini Mungu kuliko hata kuona ishara na miujiza halafu hamna Umoja… Na ndicho kitu pekee kinachotufanya sisi tumwamini BWANA YESU, ni kwasababu alikuwa na Umoja na Baba.

Laiti Bwana YESU asingelikuwa na umoja na Baba, ingelikuwa ngumu kumwamini kwa ishara na miujiza pekee, lakini ule Umoja wa Roho kati yake na Baba, umetutengenezea sisi Upendo wa ajabu, na Imani kuu kwa BWANA YESU KRISTO, Kwamba yeye ni kweli na hamna uongo ndani yake.

Na vile vile sisi tukiwa na Umoja na Mungu, na tukiwa na umoja sisi kwa sisi ndipo USHUHUDA WETU UTAKAPOTHIBITIKA ZAIDI kuliko kukaa katika matengano.

Yohana 17:21 “WOTE WAWE NA UMOJA; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ILI ULIMWENGU UPATE KUSADIKI YA KWAMBA WEWE NDIWE ULIYENITUMA.

22  Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.

23  Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.

Hapo mstari wa 21 anasema.. “WOTE WAWE NA UMOJA ….ILI ULIMWENGU UPATE KUSADIKI YA KWAMBA WEWE NDIWE ULIYENITUMA”.

Kumbe UMOJA WETU ndio utakaowaaminisha watu kuwa KRISTO ni BWANA! Na si mahubiri yetu kuwa mengi, au miujiza yetu kuwa mingi…ni UMOJA TU!.

Tukilikataa Neno hili, na kufuata njia zetu za matengano, tutakuwa tunajipunguzia wenyewe utukufu wa Mungu, kwasababu KRISTO hakujitenga na Baba, wala hakujitenga na wanafunzi wake.

> Unapochagua kuomba peke yako kila mara na huku ipo nafasi ya kuomba na mwingine mmoja au wawili ni roho ya matengano inayoondoa utukufu wa Mungu. (Bwana wetu YESU KRISTO mara nyingi alipanda mlimani kuomba na wanafunzi wake, na hata katika sehemu za faragha soma Mathayo 17:1, na Marko 14:33-34).

> Unapochagua kila mara kwenda kuhubiri peke yako na wakati kuna nafasi ya kwenda na mwingine mmoja au wawili, ni roho ya matengano ambayo inapunguza utukufu wa Mungu juu yako (Bwana YESU aliwatuma wawili wawili kuhubiri katika miji na vijiji soma Luka 10:1 na Matendo 13:2).

> Unapochagua kila mara kutosema na ndugu yako, kumfariji, au kumtia moyo au kukaa karibu naye, ili hali ni mtu wa Imani moja nawe, mnamwamini Bwana mmoja, mmepokea roho mmoja, na hata ubatizo mmoja hiyo ni roho ya matengano inayoharibu utukufu wa Mungu juu yetu.

Hivyo ni lazima tuuhifadhi Umoja wa Roho kama Neno la Mungu linavyotufundisha ili tusipungukiwe na utukufu wa Mungu.

Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.

4  Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.

5  Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.

6  Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”

Bwana atusaidie na kutuwezesha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TUUTAFUTE UMOJA WA ROHO.

JE UNAMHUBIRI KRISTO KATIKA KWELI YOTE?.

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

MARINDA KATIKA BIBLIA NI KITU GANI?

BWANA ni mtu wa vita,  BWANA ndilo jina lake.(Kutoka 15:3)

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 21:30 Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri,  juu ya Bwana.

SWALI: Nini maana ya Mithali 21:30 Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri,  juu ya Bwana ?


JIBU: Mstari huo unaweza ukasemwa hivi; “Hapana hekima, wala ufahamu, wala shauri linaloweza kufanikiwa/kusimama kinyume na Mungu”.

Ikiwa na maana iwe ni mwanadamu au malaika, atumie uwezo wake wote, kufanya jambo la hila kinyume na yeye haliwezi kufichika kwasababu yeye ni mkuu zaidi ya vyote. Mpango wa shetani kuliharibu kanisa huawezi kufanikiwa hata azidishe kufanya kazi mara elfu zaidi ya mwanzo hilo haliwezekani kama lilivyoshindikana mbinguni.

Mambo yote yanayotokea hayafiki kwake ghafla tu bila hodi, kama ilivyo kwetu sisi wanadamu. Elimu ya darasani haiwezi pindua ukweli wake wa uungu, wajaposema mwanadamu ametokana na nyani, mwishoni wanarudia kule kule kwenye ukweli wa uumbaji wa kiungu, kwasababu atabakia kusimama kuwa Mungu wa daima, na ataabudiwa vizazi vyote haijalishi dunia itaelimika kiasi gani.

Mungu Anajua mawazo yetu yote tokea mbali, wewe kama mwanadamu huwezi mficha dhambi zako, ukajifanya  mbele zake umesahau, au ulikuwa hujui, hata utumie hekima nyingi kiasi gani kuficha ukweli bado anatambua nia ya mioyo yetu.

Anasema;

Zaburi 50:17 Maana wewe umechukia maonyo, Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.  18 Ulipomwona mwivi ulikuwa radhi naye, Ukashirikiana na wazinzi.

19 Umekiachia kinywa chako kinene mabaya, Na ulimi wako watunga hila.  20 Umekaa na kumsengenya ndugu yako, Na mwana wa mama yako umemsingizia.

21 NDIVYO ULIVYOFANYA, NAMI NIKANYAMAZA; UKADHANI YA KUWA MIMI NI KAMA WEWE. Walakini nitakukemea; Nitayapanga hayo mbele ya macho yako.

22 Yafahamuni hayo, Ninyi mnaomsahau Mungu, Nisije nikawararueni, Asipatikane mwenye kuwaponya.

Pale tunapomwona Mungu ni kama sisi ndio unakuwa mwanzo wa kuto-mhofu  yeye. Unapokuwa na udhuru wa kuifanya kazi yake halafu unasingizia sina muda, lakini una muda wa kufanya mambo yako, ukidhani yeye hajui nia yako ya ndani, unajidanganya mwenyewe. Unapoepuka maombi, kwa kisingizio umechoka, na bado unataka Mungu akuhudumie, fahamu Mungu anakuelewa vizuri sana, atakuonyesha ambao wanachoka zaidi yako, lakini hawana udhuru. Jambo lolote tulifanyalo, tutambue kwanza kwa Mungu halifichiki.

Kwasababu Hapana hekima, wala ufahamu, wala shauri litakalosimama kinyume cha Mungu

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya Mithali 19:21Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.(Opens in a new browser tab)

Je shauri la kuipepeleza Kanaani lilitoka kwa wana wa Israeli au kwa BWANA?(Opens in a new browser tab)

Tofauti kati ya Hekima, ufahamu na maarifa, ni ipi?

(Opens in a new browser tab)Maana ya Mithali 11:17 Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 21:17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini;

SWALI: Nini maana ya  Mithali 21:17 Mtu apendaye anasa atakuwa maskini; Apendaye mvinyo na mafuta hatakuwa tajiri.


JIBU: Mstari huo unamaana mbili.

Maana ya kwanza ni ya mwilini, ni ukweli watu wanaopenda maisha ya anasa, mwisho wao huwa ni kutofanikiwa. Kwasababu kile wanachokipata ambacho kingepaswa kiwekwe akiba kwa wakati wa baadaye au kiwekezwe kizalishe zaidi, wao hutumia chote katika starehe mfano wa pombe, uasherati, na kununua vitu vya gharama kubwa, lengo tu asionekane amepitwa na wakati, au aonekane wa kisasa.

Hapo anaposema apendaye mvinyo na mafuta, hayo mafuta yanayozungumziwa hapo ni marashi ya gharama ambayo zamani waliokuwa wananunua ni matajiri. Ni sawa na leo labda mwajiriwa analipwa mshahara wa laki tatu (3) kwa mwezi, halafu anakwenda kununua perfume (marashi), ya  laki 2, ili tu aonekane wa kisasa, hiyo ni anasa, na mwisho wake ni umaskini.

Anasa ni tunda la majivuno, na kukosa adabu. Hivyo biblia inamfundisha mwanadamu yoyote kuwa, anasa ni kinyume cha mafanikio.

Lakini pia rohoni, anasa ni zao la ufukara wa ki-Mungu. Mtu wa anasa, hutumia muda wake vibaya, kwasababu nyakati zake za ziada huishia kwenye starehe za kimwili na sio kwenye mambo ki-Mungu.

Bwana alisema;

Luka 8:14  Na zilizoanguka penye miiba ni wale waliosikia, na katika kuenenda kwao husongwa na shughuli na mali, na anasa za maisha haya, wasiivishe lo lote.

Umeona? Anasa husonga mbegu ya Mungu ndani yako.

Katika kizazi cha sasa anasa ni pamoja na kushinda kwenye tv kutazama muvi kila kukicha, ni pamoja na kushinda mitandaoni kufuatilia vipindi vinavyokupa raha za kimwili na kihisia lakini havikujengi rohoni,  ni kuwekeza muda wako katika matanuzi ya mijini na kwenye sherehe-sherehe za kila mara ambazo hazina mpangalio. Muda wote akili yako ipo katika kile kitu wanachosema “ku-party weekend” na marafiki. Ushikapo simu yako, usiku wote ni kuchat, na wale wanaowaita ma-boyfriend na ma-girlfriend. Muda ambao ungepaswa kusoma Neno na kuomba.

Sasa ikiwa wewe umeokoka, na una mwenendo huo wa maisha, usitazamie hapo utazalisha kitu. Utabakia kuwa Yule Yule milele. Biblia inasema ni heri kuona kwa macho kuliko kutangatanga kwa tamaa(Mhubiri 6:9). Sio kila taarifa uifuatilie, sio kila kitu ukitende, viache vingine vikupite, ili upate nafasi ya kuwa karibu na Mungu wako, uwe mtu wa matunda. Komboa wakati.

Shalom..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa.

(Opens in a new browser tab)APENDAYE FEDHA HASHIBI FEDHA.

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 4)(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 18:22 Apataye mke apata kitu chema

SWALI: Je andiko hili humaanisha nini? kupata mke ni kujipatia kibali cha kumkaribia Mungu tofauti na  hapo mwanzo?

Mithali 18:22

Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa BWANA. 

JIBU: Andiko hili hutafsiriwa vibaya na watu wengi, wakiamini kuwa pale mtu anapoingia kwenye ndoa basi ndio amejizidishia kibali cha kukubaliwa na Mungu katika maisha yake. Jibu ni hapana, kibali kwa Mungu sio ndoa, kibali kwa Mungu ni “kufanya vema mapenzi ya Mungu” .

Mungu alimwambia kaini maneno haya

Mwanzo 4:7

[7]Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde. 

Zaidi pia, maandiko yanaeleza ipo nafasi kubwa kwa mtu  kumkaribia Mungu anapokuwa hajaoa/kuolewa kuliko yule aliyeoa au kuolewa.Kwasababu ambaye hajaoa/ olewa hupata nafasi ya kutosha kumtafuta Bwana na kumfikiria yeye ampendezeje.

1 Wakorintho 7:32-33

[32]Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana; 

[33]bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe. 

Lakini je! andiko hilo humaanisha kibali gani?

“Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa BWANA”. 

Tafsiri ya Neno hilo ni kuwa Mungu analikubali jambo hilo(Ndoa), analibariki, na pia analiona ni jema. Hivyo mtu asidhani kuwa aingiapo katika ndoa atamkosea Mungu, au Mungu atapunguza ukaribu naye. Hapana, kinyume chake atapata kibali tu. Hivyo awe na furaha na amani afanyavyo hivyo.

Makala Yanayofadhiliwa Tafuta kitu kwa kila mtu katika mkusanyiko wetu wa soksi za rangi, http://www.swisswatch.is best replica watches angavu na maridadi. Nunua kibinafsi au kwa vifurushi ili kuongeza rangi kwenye droo yako!

kwasababu pia zipo faida zinazoambata na mtu aliyeoa, mojawapo ni kujiongezea heshima kwa jamii lakini pia kuaminiwa zaidi. Na hilo ni jema husasani katika utumishi & huduma.

Lakini haimaanishi kuwa unapooa ndio Mungu anakukubali zaidi ya ule wakati ambao ulikuwa hujaoa/kuoelewa, au zaidi ya yule mtu ambaye hafikirii kuoa.

Mtume Paulo, Barnaba hawakuoa na zaidi mwokozi wetu Yesu Kristo hakuoa lakini tunaona ni jinsi gani walivyojirahisishia nafasi zao  kwa Mungu. 

kwa mafundisho zaidi kuhusu ndoa pitia masomo chini;

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAFUNDISHO YA NDOA.

MWANAMKE UKITAKA KIBALI, USIWE MTU WA KUPENDA VITU. (Esta 2:17)

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Mithali 10:5 Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima; 

SWALI: Nini maana ya;

Mithali 10:5 Akusanyaye wakati wa hari ni mwana mwenye hekima; Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha. 

JIBU: Kwa kawaida kipindi cha hari ( kiangazi), huwa ndio kipindi cha mavuno mengi. kwasababu mavuno yanakuwa yameshakomaa na kukauka.

Hivyo wakulima wengi kwa nyakati hizo wanakuwa mashambani kuvuna, kama vile tu walivyokuwa wakati wa masika walipokuwa wanapanda..

Na ni kipindi ambacho mkulima hufurahi pia kwasababu anakwenda kuona matunda ya kazi yake wakati si mwingi.

Lakini ni ajabu kuona, mtu ambaye hajasumbukia kupanda, halafu anaambiwa tu yeye akavune, tena kwa faida yake mwenyewe akauze, anaona uvivu kwenda kuvuna, hataki kabisa kwenda kujishughulisha na kazi hiyo, mpaka msimu mwingine unakuja, mazao yanaharibikia yote shambani. Mtu kama huyo utamchukuliaje? Ni sawa tu akiitwa  “mwana mwenye kuaibisha”, Kwasasababu ni uvivu wa makusudi.

Sasa jambo kama hili kwasasa lipo pia rohoni.

Na lipo kwa namna mbili.

1.) Katika kazi ya Mungu.

Bwana Yesu alisema..

Yohana 4:35-38

[35]Hamsemi ninyi, Bado miezi minne, ndipo yaja mavuno? Tazama, mimi nawaambieni, Inueni macho yenu myatazame mashamba, ya kuwa yamekwisha kuwa meupe, tayari kwa mavuno. 

[36]Naye avunaye hupokea mshahara, na kukusanya matunda kwa uzima wa milele, ili yeye apandaye na yeye avunaye wapate kufurahi pamoja. 

[37]Kwa maana hapo neno hilo huwa kweli, Mmoja hupanda akavuna mwingine. 

[38]Mimi naliwatuma myavune yale msiyoyataabikia; wengine walitaabika, nanyi mmeingia katika taabu yao. 

Umeona? Kufuatana na vifungu hivyo Bwana anatuonyesha kuwa tupo wakati wa mavuno sasa, wakati wa hari, wa kiangazi, mashamba yamekwisha kuwa meupe,  Hivyo sote kwa pamoja kwa moyo mmoja yatupasa tutoke tuanze kuifanya kazi ya Mungu bila ulegevu kwasababu Yesu alishatupa agizo kuu kuwa tutoke tuenende ulimwenguni kote kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi.

Lakini ukilala na kusema huu si wakati, ndugu ni sawasawa na hilo neno unakuwa mwana mwenye kuaibisha. Kila mmoja wetu ameitwa kuwahubiria wengine habari njema za wokovu wa Yesu Kristo, haijalishi upo ofisini, shuleni, ugenini, jeshini, una wajibu wa kuvuna. Shika mundu yako washuhudie wengine habari njema, kwasababu huu ni wakati  sahihi, na hautadumu milele.Hivyo tumia muda vizuri.

2) Katika kipindi cha maisha ulichopo.

Neno la Mungu linasema..

Mhubiri 12:1

[1]Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya,  Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo. 

na pia linasema..

1 Yohana 2:14

[14]Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.

Katika umri wako wa ujana ambao una nguvu ndio wakati wa kwenda shambani kumtumikia Bwana wako. ndio wakati wako wa hari, lakini unapokuwa mlegevu, hujishughulishi na Mungu wako, unachowaza ni anasa, starehe, mihangaiko, unasema nitamtumikia Mungu uzeeni, fahamu kuwa wewe ni sawa na mwana mwenye kuaibisha, kwasababu wakati huo utakuwa umeshapita.

Komboa wakati wako, thamini majira uliyopo, etende kazi ya Bwana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

Maana ya Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu 

Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;

Rudi Nyumbani

Print this post

Kuhani wa Oni alikuwa nani?

Swali: Huyu Kuhani wa Oni ambaye binti yake aliolewa na Yusufu, tunayemsoma katika Mwanzo 41:45  je alikuwa ni kuhani wa Mungu au wa kuhani wa miungu ya kiMisri?

Jibu: Terejee mistari hiyo…

Mwanzo 41:45 “Farao akamwita Yusufu, Safenath-panea; akamwoza Asenathi, binti POTIFERA, KUHANI WA ONI, kuwa mkewe Yusufu akaenda huko na huko katika nchi yote ya Misri”.

“Oni” lilikuwa ni eneo katika nchi ya Misri, kama vile ilivyo Mwanza, au Lindi nchini Tanzania au Nakuru Kenya.

Mji huu (wa Oni) Ulikuwa ni mji wa miungu ya kiMisri, na nchi ya Misri yote ilikuwa ni nchi inayoabudu miungu mingi,  ikiwemo Bethshemeshi (soma Yeremia 43:13), sanamu za ng’ombe (1Wafalme 12:28) na mingine mingi (soma Yoshua 24:14).

Hivyo huyu kuhani “Potifera” hakuwa kuhani wa Mungu wa mbingu nan chi (YEHOVA), bali alikuwa ni kuhani wa miungu ya kimisri iliyokuwepo hapo “Oni”, na Yusufu alipofika kule alipewa binti yake awe mkewe.

Na Kwanini ulikuwa hivyo?(yaani kwanini Farao amchagulie mke na si Yusufu ajitafutie mwenyewe?)..

Jibu ni kwamba Farao aliona njia pekee ya kumheshimisha Yusufu na kumfanya apate kibali katikati ya waMisri ni kumuunganisha yeye na familia za watu wa kubwa na wenye hadhi wa nchi ya Misri.(wenye hadhi za kiimani), kwasababu naye Yusufu alikuwa mtu wa kiimani.

Hivyo na mtu wa kiimani na kidini aliyekuwa mkubwa huko ni huyo kuhani wa Oni, ndipo akapewa binti yake aliyeitwa Asenathi. Lakini hata baada ya Yusufu kupewa mwanamke huyo bado hakufuata miungu hiyo ya kiMisri, na Farao alilijua hilo, na wala hakumpatia huyo binti kwa lengo la kugeuza Imani ya Yusufu, bali kumheshimisha.

Lakini kwasababu pia ilikuwa ni mpango wa Mungu iwe hivyo (Yusufu aoe mwanamke wa kimataifa) basi hata mke aliyempata alikuwa ni sahihi kwake na wala hakumsumbua Yusufu baada ya hapo (huwenda hata alimtumikia Mungu wa Israeli baada ya hapo), na Zaidi sana tendo la Yusufu kumwoa Asenathi (binti wa kimataifa) limebeba ufunuo mkubwa juu ya Bwana  YESU KRISTO na BIBI-HARUSI WAKE (yaani kanisa).

Kwa urefu marefu juu ya ufunuo wa maisha  ya Yusufu fungua hapa >>>Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Musa aliua lakini bado Mungu alimchangua kuwaongoza wana wa Israeli, je! Mungu anaruhusu mauaji?

ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.

UNAMFAHAMU MUNGU WA KWELI?

Ni kosa gani lililowafanya wana wa israeli wawe watumwa miaka 400 Misri?.

Ni lini na wapi Ibrahimu aliiona siku ya Bwana akashangilia?.

Rudi Nyumbani

Print this post

TEMBEA KATIKA NJIA KUU

Jina la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe daima. Karibu katika mafundisho ya biblia, Neno la Mungu wetu lililo Taa na Mwanga wa Njia zetu (Zab.119:105).

Zipo njia Mbili tu zilizowekwa mbele ya kila mwanadamu, Nazo ni njia ya UZIMA, na njia ya MAUTI.

Yeremia 21:8 “Nawe waambie watu hawa, Bwana asema hivi, Tazama naweka mbele yenu NJIA YA UZIMA, na NJIA YA MAUTI”.

Njia ya Uzima, inamwongoza mtu “Uzimani”..na Njia ya Mauti inamwongoza mtu “Mautini (ziwa la moto)”.

Njia ya Uzima imenyooka haina migawanyiko mingi (sawasawa na Yohana 14:6), ambapo Bwana YESU alisema yeye ndio hiyo “Njia”, na mtu hafiki kwa Baba isipokuwa kwa njia yake yeye.

Yohana 14:6  “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”

(Maana yake hakuna njia mkato wala njia mbadala ya kumfikia Baba)…Ni moja tu! Tena iliyonyooka, nayo ni YESU KRISTO, na si kupitia mtu mwingine yoyote mashuhuri, au mtakatifu mwingine yoyote aliye hai au aliyekufa au nabii yoyote katika biblia.

Lakini ile ya Mauti inamigawanyiko mingi, inaanza kama njia moja lakini mwisho wake inamigawanyiko,

Mithali 14:12 “IKO NJIA ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni NJIA ZA MAUTI”

Hapo anamaliza na kusema mwisho wake ni “NJIA ZA MAUTI” na si “NJIA YA MAUTI” kana kwamba ni moja, bali nyingi. Na njia ya Mauti si mwingine Zaidi ya “shetani”…Kama jinsi njia ya UZIMA ilivyo Bwana YESU kadhalika njia ya Mauti ni “shetani”.

Na shetani anaabudiwa kupitia vitu vingi, anaweza kuabudiwa kupitia miti, mawe, udongo, au kupitia vitu vitu vingine kama fedha, watu, dini n.k..ndio maana hapo biblia inasema hiyo Njia (shetani) mwisho wake ni “Njia za Mauti” (maana yake zipo nyingi).

Na hiyo ndio sababu pia kwanini biblia inataja uwepo wa milango mingi ya kuzimu (Soma Mathayo 16:18). Milango ya kuzimu ndio hizo njia zote zinazoweza kumpeleka mtu kuzimu.

Nabii Isaya amezidi kuziweza vizuri njia hizi kwa ufunuo wa Roho… Amezitofautisha kama “NJIA” pamoja na “NJIA KUU”..

Isaya 35:8 Na hapo patakuwa na NJIA KUU, na NJIA….”

“Njia Kuu” ni “Njia ya Uzima”…. Na “Njia” pekee yake “Ni njia ya Mauti”..

Lakini anaendelea kusema… hiyo “Njia kuu” itaitwa Njia ya utakatifu, na ya watu wasafirio..

Isaya 35:8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio….”

Maana yake wote wanaiendea hiyo njia ya Uzima (YESU) Ni lazima “utakatifu” uwe muhuri wao sawasawa na kitabu kile cha Waebrani 12:14.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”.

Vile vile ni lazima wawe “wasafiri”.. Tabia ya msafiri huwa anadumu katika chombo cha usafiri awapo safarini, na hawezi kujishikisha na mambo akutanayo njiani au barabarani…. na chombo chetu cha usafiri ni NEEMA YA MUNGU.  Tuwapo katika safari hii ya kwenda mbinguni kupitia njia ya Bwana YESU, mambo ya ulimwengu hayapaswi yashikamane  na sisi.

1Petro 2:11  “Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho”.

Na mwisho anasema.. “wajapokuwa wajinga hawatapotea katika njia hiyo”

Isaya 35:8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, WAJAPOKUWA WAJINGA, HAWATAPOTEA KATIKA NJIA HIYO”. 

Ikiwa utaonekana mjinga kwa kuwa umeamua kuifuata NJIA KUU ya UTAKATIFU na umeamua kuishi kama MSAFIRI duniani, basi biblia inasema “hautapotea/hatutapotea” katika njia hiyo..

Haijalishi dunia nzima itakuona kama umepotea, umerukwa na akili, umechanganyikiwa…Mungu yeye anakuona upo katika njia sahihi na una hekima nyingi.. kwasababu mwisho wa njia hiyo ni UZIMA WA MILELE, Na Utakutana na Bwana naye atakufuta machozi.

Ufunuo 7:15 “Kwa hiyo wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu, nao wanamtumikia mchana na usiku katika hekalu lake, na yeye aketiye katika kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao

16  Hawataona njaa tena, wala hawataona kiu tena, wala jua halitawapiga, wala hari iliyo yote.

17  Kwa maana huyo Mwana-Kondoo, aliye katikati ya kiti cha enzi, atawachunga, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji yenye uhai, na Mungu atayafuta machozi yote katika macho yao.”

Je wewe leo umechagua njia ipi??… Njia kuu ya Uzima? Au Njia ya Mauti..

Kumbukumbu 30:14 “Lakini neno li karibu nawe sana, li katika kinywa chako na moyo wako, upate kulifanya.

15 ANGALIA, NIMEKUWEKEA LEO MBELE YAKO UZIMA NA MEMA, NA MAUTI NA MABAYA”.

CHAGUA NJIA YA UZIMA, na TEMBEA KATIKA NJIA KUU YA UTAKATIFU.

BWANA AKUBARIKI.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

TABIA ZA NJIA YA MUNGU KWA MKRISTO

HATARI YA KUTOKUITAFAKARI BIBLIA VIZURI?

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

Rudi Nyumbani

Print this post

FUNDISHA NENO KANISANI NA NYUMBANI.

(Masomo maalumu kwa wazazi/walezi).

Ni nini unafanya kama mzazi uwapo nyumbani?.. Je maisha yako ndani ya kanisa ni sawa na yale nje ya kanisa?..Je kile unachokifanya kanisani ndicho unachokifanya nyumbani?…je nyumbani kwako ni sehemu ya kuishi tu au ni sehemu pia ya ibada?.

Kama wewe ni mwalimu kanisani, ni lazima pia uwe mwalimu nyumbani kwako…kama wewe ni kiongozi katika nyumba ya Mungu ni lazima pia uwe kiongozi katika nyumba yako, kama wewe ni mchungaji katika nyumba ya Mungu ni lazima pia uwe mchungaji katika nyumba yako mwenyewe…Ndivyo biblia inavyotufundisha.

Mitume wa Bwana YESU ni kielelezo kwetu, wao walikuwa wakihubiri Neno HEKALUNI NA NYUMBANI, kama maandiko yanavyosema, hivyo kama na sisi tumejengwa juu ya msingi wao ni lazima tufanye kama wao walivyofanya..

Matendo 5:42 “Na kila siku, NDANI YA HEKALU na NYUMBANI MWAO, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo”.

Umeona?.. Si hekaluni tu!, bali hata nyumbani…. Uharibifu mkubwa shetani anauanzia nyumbani… Hivyo ni lazima uwe na AMRI, katika nyumba yako mwenyewe… Ni lazima pafanyike ibada nyumbani kila siku, ni lazima pafanyike maombi, ni lazima watoto na wengine wanaoishi katika nyumba yako wajue kuomba na kuombea wengine.

Ni lazima watoto wajifunze biblia na kufundisha biblia tangu wakiwa wadogo, ni lazima pia wajifunze kutoa.. ni lazima wote wawe wa kiroho, ni lazima uwafundishe wawe vipaumbele katika Imani wawapo shuleni, maana yake wakiwa shuleni wawe vipaumbele katika kuongoza maombi kwa wanafunzi wenzao, na kuomba vile vile kufunga… Na si kuwaacha jumapili kwa jumapili  tu wafundishwe kanisani hayo mambo..

Jenga tabia ya kuwafuatilia mienendo yao ya kiimani wakiwa mashuleni, fuatilia sifa zao za kiimani wawapo mashuleni, (na si tu taaluma yao)..wapo watoto taaluma zao zinaonekana nzuri lakini shetani kashawaharibu kitabia muda mrefu (matokeo yake yatakuja kuonekana baadaye).

Hivyo kama mzazi au mlezi, simama katika hiyo nafasi… kiasi kwamba NENO LA MUNGU nyumbani kwako ni AMRI sio OMBI!. Kama Nabii Yoshua alivyoazimia zamani zile..

Yoshua 24:15 “Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia Bwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng’ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; LAKINI MIMI NA NYUMBA YANGU TUTAMTUMIKIA BWANA.

16 Hao watu wakajibu wakasema, Hasha! Tusimwache Bwana, ili kuitumikia miungu mingine”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUOTA UPO KANISANI.

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

YESU HAYUPO KATIKA MAZINGIRA YALEYALE TU SIKUZOTE, USIJISAHAU.

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

Rudi Nyumbani

Print this post

Lalama kwa uhai wa watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa(Maombolezo 2:19)

Mafundisho maalumu kwa watumishi wa Mungu na Watenda kazi wote katika shamba la Bwana.

Maombolezo 2:19

[19]Inuka, ulalamike usiku, Mwanzo wa makesha yake; Mimina moyo wako kama maji usoni pa Bwana; Umwinulie mikono yako; KWA UHAI WA WATOTO WAKO WACHANGA WAZIMIAO KWA NJAA, Mwanzo wa kila njia kuu. 

Ikiwa wewe ni mzazi au mlezi unaelewa ni uchungu mwingi kiasi gani  unakupata  pale unapoona mtoto wako anaangamia kwa kukosa mahitaji yake muhimu, mfano  wa chakula. Ndicho kilichotokea kwa mama Hajiri siku alipofukuzwa kwa Ibrahimu, akiwa kule jangwani amepotea hali ilikuwa mbaya sana, kwani chakula na maji viliwaishia kabisa, huwenda zilipita siku kadhaa hawakuona dalili yoyote ya kupata msaada. Hivyo alichokifanya Hajiri, ni kwenda mbali kidogo na kumlilia sana Mungu wake, na Mungu akasikia, akaonyeshwa palipo na maji, akaenda kumpa mwanae, kuonyesha ni jinsi gani alivyouthamini uhai wa Ishmaeli.

Mwanzo 21:14 Ibrahimu akaamka asubuhi na mapema akatwaa mkate na kiriba cha maji, akampa Hajiri akimtwika begani pake, na kijana, akamruhusu; naye akatoka, akapotea katika jangwa la Beer-sheba. 

15 Yale maji yakaisha katika kiriba, akamlaza kijana chini ya kijiti kimoja. 

16 Akaenda akakaa akimkabili, mbali naye kadiri ya mtupo wa mshale; maana alisema, Nisimwone kijana akifa; naye akakaa akimkabili, AKAPAZA SAUTI YAKE, AKALIA. 

17 Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, Una nini, Hajiri? Usiogope, maana Mungu amesikia sauti ya kijana huko aliko. 

18 Ondoka, ukamwinue kijana, ukamshike mkononi mwako, kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa. 

19 Mungu akamfumbua macho, naye akaona kisima cha maji; akaenda akakijaza kiriba maji, akamnywesha kijana. 

Umeona kama Hajiri asingemtafuta Mungu katika hali ile, ni wazi kuwa Yule kijana ambaye alikuwa amekusudiwa awe taifa kubwa angefia jangwani na yale maono yasingetokea.

Ndicho tunachojifunza katika vifungu hivyo, kwenye kitabu cha Maombolezo, anasema kesha, ulie, kwa ajili ya watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa. Leo hii tuna watu wengi ambao wameokoka kwa kuisikia injili yetu. Lakini je, watu hao wanasimama au wanakufa?, Unapomhubiria mtu, hatutakiwi kusema yaliyobaki namwachia Mungu, bali ni kuhakikisha hafi kiroho kwa kukosa chakula cha uzima. Na hiyo inakuja kwa kuendelea kumfuatilia kumfundisha, Lakini zaidi sana KUMWOMBEA kwa Mungu usiku na mchana akue kiroho.

Tukiiga mfano wa Epafra jinsi alivyokuwa akiwaombea sana watu wa kolosai walioamini kwa injili yao.

Wakolosai 4:12  Epafra, aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu Kristo, awasalimu, akifanya bidii siku zote kwa ajili yenu katika maombi yake, ili kwamba msimame wakamilifu na kuthibitika sana katika mapenzi yote ya Mungu.

Umeona? Ukomavu wa watu walio wachanga wa kiroho hutegemea sana maombi ya kina kwa waliowazaa. Hivyo wewe kama mtenda kazi hakikisha unakuwa na maombi mengi kwa ajili ya wale uliowahubiria injili wakaokoka vinginevyo watakufa kiroho, katika ulimwengu huu wa njaa na kiu ya Neno la Mungu, tenga masaa kuwaombea. Na maombi hayo yawe ya rohoni kabisa, sio ya juu juu, bali ya kuzama, ili Mungu awakuze, na matokeo ya kazi yako utayaona tu baada ya kipindi fulani, jinsi watakavyozidi kubadilika na kukomaa kidogo kidogo, hatimaye kuwa watumishi imara katika shamba la Mungu.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

NJAA ILIYOPO SASA.

LISHA KONDOO WANGU, LISHA WANA-KONDOO WANGU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu 

SWALI: Nini maana ya

Mithali 25:25 Kama vile maji ya baridi kwa mtu mwenye kiu, Ndivyo ilivyo habari njema itokayo katika nchi ya mbali.

JIBU: Biblia inalinganisha burudiko kubwa mtu analolipata pale anaposikia habari fulani njema na mfano wa mtu mwenye kiu halafu ghafla akaletewa kikombe cha maji ya baridi, sasa katika mazingira kama hayo ni wazi kuwa maji yale atayafurahia sana kwasababu yupo katika kiu.

lakini kiini cha mstari huo ni hapo anaposema ni habari njema ITOKAYO KATIKA NCHI YA MBALI.

Tukumbuke kuwa zipo habari njema nyingi..kwamfano habari za kupewa tenda fulani ya kibiashara ni habari njema, habari za kufaulu darasani ni habari njema, habari za kuzaliwa mtoto duniani ni habari njema, habari za kupandishwa cheo ni habari njema n.k…lakini zote hizi hazina jipya kwasababu ni za hapa hapa tu duniani.

Bali zipo habari njema zinazotoka katika nchi ya mbali na huko si kwingine zaidi ya MBINGUNI, hizo ndizo watu wana kiu nazo, wakizisikia tu ni lazima mioyo yao ni lazima iburudike sana.

Na habari zenyewe ni zile zinazomuhusu  Yesu Kristo.

Alisema.

Yohana 6:33-35

[33]Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.

[34]Basi wakamwambia, Bwana, sikuzote utupe chakula hiki. 

[35]Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.

Yesu ndio maji yakatao kiu, alileta habari njema iliyotoka mbinguni, alikuja kutuletea ukombozi na msamaha wa dhambi, alikuja kutufungua katika vifungo vyetu, na shida zetu mbalimbali, na kutumwagia karama za rohoni, mambo ambayo mwingine yoyote hawezi kutoa. Lakini zaidi sana alikuja kutuambia habari za ufalme wake, kwa habari ya mambo yanayokuja, kuhusu mbingu mpya na nchi mpya, na Yerusalemu mpya, na umilele, na uzuri na thawabu alizotuandalia sisi tuliomwamini. Mambo ambayo ukisikia kama wewe unapenda kweli maisha…utayafurahia sana.

hivyo yatupasa mimi na wewe tuwe na mwitikio huu, wa habari hizi njema kwa kuwashuhudia pia na wengine maji haya, kwasababu ni wazi kuwa wengi wana kiu, na hivyo wanahaja ya kuzisikia hizi habari njema zimuhusuyo Yesu Kristo.

Sote kwa pamoja tuamke tukahubiri injili. Tukijua kuwa inahitajiwa sana.

shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

INJILI NI NINI?

Maana ya Mithali 17:22 Moyo uliochangamka ni dawa nzuri;

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

Rudi Nyumbani

Print this post