Title Devis

ANZA MWAKA NA KUSAMEHE

Maandiko yanasema Makwazo hayana budi kuja (Luka 17:1)

Unapofanyiwa jambo baya na Mtu wako wa karibu au wa Mbali, huwa ni ngumu kusahau…

Kama umeshaokoka na ni mtu uliye mwepesi kusamehe na kusahau, basi Bwana amekutengeneza kwelikweli na umetengenezekeka, Lakini kama ndani yako kuna UGUMU wa kusamehe, fahamu kuwa hilo ni tatizo ambalo unapaswa ulitafutie ufumbuzi haraka sana, mwanzoni mwa mwaka.

Umeumizwa na Ndugu, umeumizwa na Mpendwa mwenzako, umeumizwa na Rafiki, umeumizwa na Mke, Umeumizwa na Mume, umeumizwa na watoto, mchungaji, mshirika wako, mkufunzuki wako au mtu mwingine yeyote, leo itoe hiyo sumu..

Fanya jambo  hili  moja ili ushinde hali hiyo ya kutokusamehe na hatimaye uachilie msamaha.

UTAFAKARI MSAMAHA WA YESU.

Tafakari ni mambo mangapi mabaya uliyoyafanya au unayoyafanya kwa MUNGU, unaweza ukawa hujawahi kumfanyia mtu ubaya, lakini vipi MUNGU?.. Je hujawahi kumfanyia ubaya kabisa?..huna dhambi kabisa??, huna kasoro kabisa??.. Hilo ni jambo lisilowezekana. (2Nyakati 6:36)

Tafakari tu mawazo yako kwa siku yanavyo vuka na kuwa machafu, na MUNGU anakutazama tu!, tafakari ni vipindi vingapi umewaka hasira moyoni na Mungu anakutazama tu, tafakari ni mangapi amekusamehe, na ni mangapi unayohitaji ukusamehe.

Hayo yote uliyoyafanya na unayoyafanya Mungu anayatazama tu, na yupo tayari kukusamehe, au huenda ameshakusamehe, sasa kama wewe umesamehewa mengi hivyo bure kabisa, vipi na wewe kwanini usimsamehe yule aliyekokosea mwaka jana, au mwezi jana, au siku ya jana??.

Wakati mwingine si lazima yeye akuombe msamaha,  Wewe samehe tu hata kama hajaja kukuomba msamaha, maana hata BWANA aliwasamehe wale wasiomwomba msamaha..

Luka 23:34 “Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.

35  Watu wakasimama wakitazama. Wale wakuu nao walikuwa wakimfanyia mzaha, wakisema, Aliokoa wengine; na ajiokoe mwenyewe, kama ndiye Kristo wa Mungu, mteule wake.”

Wengine watakukosea na daima wataendelea kujiona wapo sawa, na wengine wataendelea kukukosea  tu!.. Lakini kanuni ni ile ile KUSAMEHE..

Hivyo kwa kuutafakari mambo ya maisha yako, na kasoro zako mbele za MUNGU, Huwezi kukosa sababu za wewe kutosamehe.

Kwa kumalizia hebu tafakari kwa undani maandiko yafuatayo…

Mathayo 18:21  “Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?

22  Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.

23  Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.

24  Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.

25  Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.

26  Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

27  Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.

28  Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho.

29  Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

30  Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.

31  Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka”.

Kumbe tusipokuwa na TAFAKARI ya kutosha kwa msamaha BWANA aliotupa, yaweza kuwa sababu ya sisi pia kutosamehewa!. Lakini kama tukifakari kwamba na sisi tumeshafanya mengi mabaya, ambayo hayakustahili msamaha basi na sisi pia tutasamehe.

Mhubiri 7:20 “Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ambaye afanya mema, asifanye dhambi.

21 Tena, usitie moyoni mwako maneno yote yaliyosemwa; usije ukamsikia mtumwa wako mwenyewe ali anakutukana.

22 Kwa kuwa mara nyingi moyo wako pia unajua ya kwamba wewe mwenyewe umewatukana watu wengine”.

Mwombe Bwana katika mwanzo wa mwaka huu akuumbie  “Moyo wa kusamehe”.. Ni yeye ndiye anayetoa huo moyo, ikiwa tutamwomba, kwa kumaanisha kabisa, Hivyo jifungie chumbani kwako, au tafuta sehemu yoyote yenye utulivu na mwambie Bwana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TAFAKARI SANA KABLA YA KUAMUA HATIMA YAKO.

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

Maana ya Mithali 19:11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake.

Je! Kiongozi wa dini anaouwezo wa kusamehe dhambi?

BWANA ANASAMEHE.

Rudi Nyumbani

Print this post

Shetani alitoka wapi?

Swali: Je shetani yule audanganyaye ulimwengu alitoka wapi?


Jibu: shetani kwa asili aliumbwa na Mungu, na kabla ya kuwa shetani alikuwa akiitwa “Kerubi afunikaye”

Ezekieli 28:14 ” Wewe ulikuwa KERUBI MWENYE KUTIWA MAFUTA AFUNIKAYE; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto”.

Na MUNGU alimwumba akiwa mkamilifu (asiye na dosari) kama tu MAKERUBI wengine, lakini baadaye moyo wake uliinuka akajidanganya mwenyewe kuwa anaweza kuwa kama MUNGU (aabudiwe kama MUNGU) Na ndipo Uovu huo ukaonekana ndani yake, na hakutaka kubadilika.

Ezekieli 28:15 “Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako”

Na baadaye alipoasi ndipo akawa shetani, na maana ya shetani ni Mshitaki/Mchongezi, maana yake anawashitaki wanadamu mbele za MUNGU mchana na usiku.

Ufunuo 12:9 “Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.

10  Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana AMETUPWA CHINI MSHITAKI WA NDUGU ZETU, YEYE AWASHITAKIYE MBELE ZA MUNGU WETU, MCHANA NA USIKU”.

Kwahiyo shetani aliumbwa na MUNGU, na akaasi na  ataharibiwa na MUNGU katika ziwa la MOTO baada ya hukumu ya kile kiti cheupe.

Ufunuo 20:10 “Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele”.

Bwana atuepushe na ibilisi.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

NYOTA YA ASUBUHI.

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wathesalonike wa kwanza.

Kitabu hichi kama kinavyojitambulisha katika mwanzo wake  ‘Waraka wa kwanza wa Paulo mtume kwa Wathesalonike’.

Paulo ndiye mwandishi wa waraka huu. Aliuandika akiwa Korintho. Tumelijua hilo  kufuatana na ujio wa Timotheo kutoka Makedonia na kumpa ripoti nzuri ya maendeleo yao ya kiroho,  kuanzia eneo la imani, upendo na tumaini, ambazo tunazisoma katika kitabu cha Matendo ya mitume sura ya 18.

Kwasababu ya ugumu wa kuwafikia uliochangiwa na shetani,  Akasukumwa kuandika nyaraka hizi mbili kwa watakatifu hawa, kuwajenga katika maeneo kadha wa kadha,  ambazo zilipishana kwa miezi kadhaa tu.

Kitabu hichi kina sura tano (5)

Maudhui kuu ya waraka huu ni matatu(3)

  1. kwanza ni kuwahimiza watakatifu kudumu katika imani  husasani katika nyakati za dhiki.
  2. Pili kuwapa mwongozo wa mwenendo sahihi upasao ndani ya imani.
  3. Tatu, kuwapa majibu ya maswali yahusuyo ujio wa pili wa Yesu Kristo na kiyama ya wafu ambayo walikuwa nayo.

Tuyaangalie hayo maeneo matatu kwa ufupisho;

1) Kuhusu kudumu katika Imani.

Paulo anaanza kwa kuwashuhudia kwa maneno mengi dhiki alizozipata katika kuieneza injili kwao, na jinsi alivyoweza kustahimili, Na kwamba wao pia wanapopitia dhiki za namna mbalimbali kutoka kwa watu wa taifa lao, wasivunjike moyo na kuiacha imani. Wajue kuwa dhiki pia wamewekewa watakatifu.

1 Wathesalonike 2:14

[14]Maana ninyi, ndugu, mlikuwa wafuasi wa makanisa ya Mungu yaliyo katika Uyahudi, katika Kristo Yesu; kwa kuwa mlipata mateso yale yale kwa watu wa taifa lenu wenyewe, waliyoyapata na hao kwa Wayahudi;

[15]ambao walimwua Bwana Yesu, na hao manabii, na kutuudhi sisi; wala hawampendezi Mungu, wala hawapatani na watu wo wote;

1 Wathesalonike 3:3

[3]mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo.

2) Sehemu ya pili ambayo inahusu mwenendo upasayo wa imani.

Paulo anagusia maeneo mengi kuanzia upendo hadi utakatifu kwamba wana wajibu wa kuongezeka katika hivyo ili wasionekane katika lawama katika siku ile ya kuja Bwana wetu Yesu Kristo kutoka mbinguni.

1 Wathesalonike 3:12-13

[12]Bwana na awaongeze na kuwazidisha katika upendo, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;

[13]apate kuifanya imara mioyo yenu iwe bila lawama katika utakatifu mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote.

> Anagusia pia katika eneo la kudhibiti miili yetu katika utakatifu na heshima na sio katika tamaa mbaya(4:1-5),

> Halikadhalika wakristo kuonyesha mwenendo wa adabu kwa walio nje, kwa kutenda shughuli zetu wenyewe ili tusiwe na uhitaji wa vitu vyao (4:11-12)

> Pia kama watakatifu ni mwiko kulipana baya kwa baya (5:15),

> Tunapaswa sikuzote tudumu katika kuomba, kufurahi, kushukuru kwa kila jambo, tusimzimishe Roho, tusipuuzie unabii, tujitenge na ubaya wa kila namna.(5:16-23)

> Lakini Paulo anahimiza mwenendo wetu unapaswa uende mpaka kwa wale wanaotusimamia na kutuchunga kwamba tuwastahi.

1 Wathesalonike 5:12-13

[12]Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni;

[13]mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi.

> Na katika yote ni wajibu wetu sote kufarijiana na kuonyana na kuvumiliana na kutiana nguvu(5:14-15)

3) Sehemu ya tatu ambayo anatoa majibu ya maswali yahusuyo ujio wa pili wa Kristo, na kiyama ya wafu

Paulo anawafiriji kwa kuwaambia wafu waliolala katika Kristo, siku ya mwisho wataamshwa wote..wasidhani kuwa hawatawaona wapendwa wao waliotangulia.

1 Wathesalonike 4:13-16

[13]Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.

[14]Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.

[15]Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.

[16]Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

Sambamba na hilo, anawafumbua macho juu ya nyakati na majira ya kurudi kwa Yesu kwamba hakutakuwa na taarifa zozote au viashiria vyovyote kwa watu wa dunia. Bali itawajilia kwa ghafla tena katika nyakati ambazo wanasema kuna amani na shwari.

Hivyo anawatahadharisha watakatifu nao kuwa macho wakati wote.

1 Wathesalonike 5:1-11

[1]Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

[2]Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

[3]Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.

[4]Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi.

[5]Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.

[6]Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.

[7]Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku.

[8]Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu.

[9]Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo;

[10]ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, kwamba twakesha au kwamba twalala.

[11]Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya.

Hivyo kwa ufupi ni kuwa waraka huu. Unawataka wakristo kuthibitika katika imani, haijalishi ni changamoto gani za kimaisha au ugumu gani watakutana nao kwa wapinga-kristo, Wanapaswa waendelee kusimama hivyo hivyo  mpaka mwisho katika Kristo Yesu.

Lakini pia wajue  Bwana anarudi, na atakuja ghafla, Hivyo yawapasa  wawe watu wa mchana sikuzote wasilale usingizi kwa kuhakikisha wanaishi maisha ya utakatifu, na adabu, ili atakaporudi Bwana wasiwe na lawama yoyote.

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Kama ni la, fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya wokovu. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha Wafilipi.

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Yakobo.

Print this post

Ufidhuli ni nini (2Wakorintho 12:10).

Swali: Ufidhuli ni nini kama tunavyosoma katika 2Wakorintho 12:10?


Jibu: Turejee..

2 Wakorintho 12:10 “Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na UFIDHULI, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu”

Maana ya “Ufidhuli” kama ilivyotumika hapo ni “Matukano”

Hivyo Mtume Paulo kwa ujasiri katika Roho Mtakatifu alidiriki kusema kuwa “anapendezwa na madhaifu”  katika Kristo maana yake ni kwamba pale anapojiona kuwa ni mdhaifu basi alijiona mwenye heri.

Lakini pia anapendezwa na UFIDHULI (Matukano). Yaani pale anapotukanwa kwaajili ya Kristo basi jambo hilo kwake alilipenda zaidi.

Sasa kujua kwa marefu kama ni sahihi kwa Mtume Paulo kujisifia udhaifu fungua hapa >>> Je ni sawa kuukubali udhaifu kama mtume Paulo alivyojisifia kwa huo? (2Wakorintho 12:9-10)

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya 2 Wakorintho 8:9 alikuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.

SWALI: Nini maana ya 2 Wakorintho 8:9

isemayo alikuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.

2 Wakorintho 8:9

[9]Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.


JIBU: Katika sura hii mtume Paulo anawaandikia wakorintho juu ya huduma ya utoaji kwa watakatifu walio maskini katika makanisa mengine, ya mbali

Na hapa anawasisitiza kukubali kutoa kwa kufuata kielelezo cha Kristo katika eneo la neema yake..Jinsi alivyokubali kuwa maskini, kwa kuacha enzi na utukufu na mamlaka juu mbinguni, na kuja duniani, katika hali ya chini sana (ijapokuwa hakuwa duni), ili tu atukomboe sisi tulio katika hali ya ufukara wa roho. 

Kwasababu kama asingeweza kujishusha vile, na kukubali kuhesabiwa si kitu (ijapokuwa alikuwa na nguvu), matokeo yake ni kwamba asingekwenda msalabani kusulubiwa kwa ajili yetu tena uchi, na mwisho wake kusingekuwa na  msamaha wa dhambi.

Isaya 53:3

[3]Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. 

 

Lakini sasa tumepokea neema na utajiri wote wa rohoni kupitia yeye kujishusha kwake.

 

Waefeso 1:3

[3]Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo; 

Vivyo hivyo Mtume Paulo anawahimiza  Wakorintho waige mfano huo huo, katika eneo la kuwahudumia watakatifu wengine. Akitumia mfano wa Wamakedonia ambao walikuwa ni maskini, na wenye dhiki lakini walikuwa tayari kutoa kwa moyo na furaha kwa watakatifu maskini waliokuwa Yerusalemu.

2 Wakorintho 8:1-3

[1]Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia; 

[2]maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na umaskini wao uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao. 

[3]Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao; 

Halikadhalika Bwana anataka na sisi tuhudumiane katika ufahamu wa Kristo, yaani kuwa tayari kuwasaidia watakatifu wengine hata katika hali zetu za dhiki.

Lakini mtazamo ambao si sahihi kuhusiana na vifungu hivi ni kudhani kwamba andiko hilo moja kwa moja linamaanisha  lengo la Bwana Yesu kuwa maskini duniani ni ili sisi tuwe matajiri kifedha. Ni kweli kupitia Yesu, tunabarikiwa mwilini, lakini hicho sio kinachozungumziwa hapo.  Bwana Yesu kuwa maskini ni kutupa utajiri wa roho zetu, pamoja na ule wa ulimwengu ujao.

Bwana akubariki.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)

Kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi ( 1 Wakorintho 7:14)

Nini maana ya waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo? (Matendo 11:23)

Rudi Nyumbani

Print this post

Kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi ( 1 Wakorintho 7:14)

 SWALI: Je! kulingana na mstari huu, watoto wa wapagani hawataokolewa?

1 Wakorintho 7:14

[14]Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.


JIBU: Ukianzia juu utaona andiko hilo linazungumzia juu ya wandoa wanaoishi pamoja lakini mmojawapo hajaamini. Bwana anatoa agizo kwamba ikiwa bado huyo ambaye hajaamini anaona sawa kuendelea kuishi naye, basi yule aliyeamini asimwache.

Kwasababu kwa kupitia njia hiyo, yule asiyeamini hutakaswa na yule aliyeamini Pamoja na watoto wake pia.

Lakini je mstari huo unamaanisha kuwa mwanandoa mmoja katika familia akiokoka, basi ameiponya familia yote mpaka watoto wake?

Jibu ni la! andiko hilo halikumaanisha hivyo.

Bali linamaanisha kuwa, kwa kupitia yeye, ni rahisi wao kuambukizwa imani na hatimaye kufanya uamuzi wa kuokoka.

Wokovu hauji kwa kurithishana au kwa ‘niaba-ya’ bali kwa mtu mwenyewe kufanya maamuzi binafsi mara baada ya kushawishwa na injili.

Hata sasa tumeona shuhuda nyingi watu wakiwavuta ndugu zao kwa Kristo, aidha kwa injili au mienendo yao, na hatimaye wote kugeuka.

1 Petro 3:1-2

[1]Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; 

[2]wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. 

Hivyo kwa hitimisho, watu wote, haijalishi wakubwa au wadogo, aidha wa waamini au wapagani, wote wanahitaji kumwamini Yesu ndipo waokolewe dhambi zao. Lakini hiyo huja kwa ushawishi wetu, kwa jinsi tunavyosema nao, tunavyoenenda katika mwenendo wetu mzuri, tunapozifanya nyumba zetu kuwa makao ya ibada, ni njia rahisi ya kuwashawishi.

Bwana akubariki.

Washirikishena akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

je! Paulo aliwalaani Wagalatia na Wakorintho?

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

Matasa ni nini? (1Nyakati 28:17)

Rudi Nyumbani

Print this post

CHAGUA UTAKATIFU MWAKA HUU.

Zaburi 93:5 “Shuhuda zako ni amini sana; UTAKATIFU NDIO UFAAO NYUMBA YAKO, Ee BWANA, milele na milele”.

Ni kitu gani umekichagua kwenye nyumba ya MUNGU katika mwaka huu?..Je nafasi fulani, au cheo, au umaarufu, au nini?.

Kumbuka Nyumba ya MUNGU ni zaidi ya jengo la Ibada, bali pia Miili yetu ni nyumba ya MUNGU.

Yohana 2:20 “Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu?

21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake”.

1 Wakorintho 3:16 “Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?”

Soma pia 1Wakorintho 6:19, utazidi kuelewa vyema.

Sasa kama Miili yetu ni HEKALU LA MUNGU, yaani NYUMBA YA MUNGU ni kipi umekiamua juu ya Mwili wako katika mwaka huu mpya?, kwamaana Neno linasema Utakatifu ndio ufaao nyumba ya MUNGU, na tena haufai siku moja tu, bali milele…..

Zaburi 93:5 “Shuhuda zako ni amini sana; UTAKATIFU NDIO UFAAO NYUMBA YAKO, Ee BWANA, milele na milele”.

Chagua utakatifu wa mwilini na rohoni huu Mwaka, usiishi tena kwa kuuchafua mwili wako kama ilivyouchafua mwaka jana, au miaka iliyopita, anza mwaka na mambo mapya.

Anza kujenga ushuhuda mpya, badilika kimwonekano, watu watakapokutazama waone waseme hakika yule ni mkristo, na watakapokuuliza usema “UMECHAGUA UTAKATIFU KWA MAANA NDIO UFAAO NYUMBA YA MUNGU”.

Sema mwaka huu sio mwaka wa Kushindana na mtu kimavazi ndani ya nyumba ya MUNGU, sema mwaka huu ni wakati wa kuipamba nyumba ya MUNGU kwa utakatifu.

Sema mwaka huu ni mwaka wa kuhubiri UTAKATIFU kila mahali, kwamaana pasipo huo hakuna mtu atakayemwona Mungu (Waebrania 12:14).

2 Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”.

Hili ni neno fupi la mwaka kwako.

Bwana atusaidie sana..

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Ni kipawa kipi hicho tusichoweza kukisifu jinsi ipasavyo?(2Wakorintho 9:15)

SWALI: Ni kipawa kipi hicho tusichoweza kukisifu jinsi ipasavyo?

2 Wakorintho 9:15

[15]Mungu ashukuriwe kwa sababu ya kipawa chake, tusichoweza kukisifu kama ipasavyo.


 JIBU: Mungu alitupa mwana wake (Yesu Kristo), kama zawadi kwetu, ambaye anakaa ndani yetu kwa Roho wake Mtakatifu. 

Warumi 5:17

[17]Kwa maana ikiwa kwa kukosa mtu mmoja mauti ilitawala kwa sababu ya yule mmoja, zaidi sana wao wapokeao wingi wa neema, na kile kipawa cha haki, watatawala katika uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo. 

Yesu (kupitia Roho Mtakatifu), ni kipawa kikubwa ambacho hatuwezi kukielezea uzuri wake(kukisifu), jinsi ipasavyo.

 Ndani ya Yesu ni hakika tunapata vitu vyote (vya rohoni na mwilini)

Hivyo kulingana na vifungu hivyo ukianzia tokea juu katika sura hiyo ya tisa (9), anaegemea hasaa  katika eneo la kubarikiwa na Mungu katika baraka za mwilini. ambazo huja ndani ya kipawa hichi cha Mungu.

2 Wakorintho 9:11

[11]mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu. 

Ni kweli hatuwezi kueleza kwa maneno haya jinsi gani Yesu alivyoleta ukombozi katika maeneo mengi zaidi ya yale tunayoyadhani, si tu katika roho zetu, bali mpaka miili yetu, dunia yetu, uchumi wetu, familia zetu, magonjwa yetu, wanyama wetu, jamii yetu, ardhi zetu,  n.k. kipawa hichi kila mahali kinatibu.

Hivyo si rahisi kukisifu kwa jinsi ipasavyo. Ndio maana kwa Yesu tumetia nanga, yeye ndio utoshelevu wetu wote, hatuna haja kwa mtu mwingine yeyote zaidi yake, na ndivyo ilivyo. Hekima ya Mungu iliona hilo ndio maana hakutupa sisi wanadamu kitu kingine zaidi ya Yesu Kristo tu.

 Ashukuriwe Mungu kwa zawadi hii. Utukufu heshima na shukrani vimrudie yeye mile na milele. Amina.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Maana ya 2Wakorintho 9:11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote

Kiti cha Musa ni kipi? (Mathayo 23:2)

USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya 2Wakorintho 9:11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote

SWALI: Nini tafsiri  ya 2 Wakorintho 9:11-12

[11]mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu.


JIBU: Katika sura hii mtume Paulo analillsisitiza kanisa la Wakorintho, uthamani wa huduma ya utoaji kama njia mojawapo ya utiifu katika kuikiri wa injili (9:13).

Na hapa anaongezea kuwa Mungu hutoa utajiri katika vitu vyote (si tu vya rohoni tu, bali pia vya mwilini). Na kwamba yeye ndiye huwapa watu mbegu za kupanda na chakula.

Hivyo atutajirishapo lengo lake ni tutumie utajiri huo kwa kutenda mema (9:8), (yaani kuwapa maskini hususani watakatifu), kwasababu ndivyo ilivyokuwa kwa Kristo(9:9). Na si tutumie katika anasa na ufahari, na ubinafsi.

Ndio hapo anasema “mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote”. Na kama tukifanya hivyo, mitume wanasema shukrani zinamfikia Mungu kwa kutii kazi yao hiyo ya kutuhimiza sisi kutoa.

2 Wakorintho 9:11-12

[11]mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu. 

[12]Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu; 

Hivyo Bwana anatutaka kila atufanikishapo tujue amekusudia tuwasidie wengine walio maskini husasani watakatifu, kwasababu kwa njia hiyo shukrani nyingi humfikia Mungu.

Zaidi vifungu hivi vinasisitiza pia jinsi Mungu anavyoongeza baraka pale tunapotoa sana, akisema atoaye haba hatavuna haba,(9:6). kile tupandacho ndicho tutakachovuna kwake. 

Bwana atusaidie tuwe watoaji katika hali zote.

ubarikiwe.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> 

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FAIDA NYINGINE MUHIMU YA KUMTOLEA MUNGU.

USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.

Mistari ya biblia kuhusu shukrani.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je ni kweli Bwana YESU hajui siku ya kuja kwake? (Mathayo 24:36)

Swali: Ni kwanini siku/saa ya kuja kwa Bwana YESU anaijua Baba peke yake na mwana haijui?, na ilihali pia YESU ni Mungu?


Jibu: Turejee..

Mathayo 24:36 “Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.”

Kipindi Bwana YESU yupo duniani, alikuwa hana budi kuwa kama wanadamu wengine, ingawa alikuwa na uungu ndani yake,  Hivyo alikuwa anahisi maumivu kama watu wengine,… alikuwa anasikia huzuni kama tu watu wengine,  na pia ilimpasa amtafute Mungu kama tu wanadamu wengine wanavyomtafuta, ndio maana alifunga na kukesha milimani kuomba kwa machozi, ili aweze kupokea mafunuo kutoka kwa Baba, kwaajili ya huduma yake na watu wake.

Waebrania 5:7 “Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu.

Hivyo Bwana YESU hakuzaliwa anajua vyote, ilimpasa ajifunze vitu.. alizaliwa hajui kutembea na hivyo ikampasa ajifunze kutembea kama watoto wengine, vile vile alizaliwa hajui kusoma na hivyo ilimpasa ajifunze kusoma na pia ajifunze torati.

Luka 2:46 “na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta.

46  Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.”

Hivyo kwa tabia hiyo ya kuendelea kujifunza, ni wazi kuwa si vyote alikuwa anavijua kipindi yupo duniani, ndio maana akasema “ile siku hata yeye haijui”

Lakini alipokufa na kufufuka, mambo yakageuka… ALIJUA YOTE!!, kwani baada ya kufufuka alisema, amepewa mamlaka yote ya mbinguni na duniani.

Mathayo 28:16 “Na wale wanafunzi kumi na mmoja wakaenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu.

17  Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka.

18  Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani”.

Sasa hawezi kupewa mamlaka yote mbinguni, halafu asijue saa ya kuja kwake, ni jambo lisilowezekana…

Kiashiria kingine kinachoonesha kuwa Bwana YESU aliijua saa  ya kurudi kwake, baada ya kufufuka ni lile neno alilomwambia  Petro kumhusu Yohana kwamba “ikiwa anataka akae hata ajapo” soma Yohana 21:22.

Soma pia Ufunuo 3:3, Ufunuo 16:15, Ufunuo 22:12, na Ufunuo 22:20.. Utaona mamlaka ya YESU kuhusiana na kurudi kwake.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Bwana YESU KRISTO sasahivi anajua kila kitu, ikiwemo siku ya kurudi kwake mara ya pili, na mwisho wa dunia (Si wa kawaida kabisa!!)

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MCHE MWORORO.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

TUNAPASWA TUWEJE WAKATI WA KUJA KWAKE  BWANA YESU?.

Maana ya Mhubiri 10:15 Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja,

Kwanini Mungu anajifanya kama hajui mambo?

Rudi Nyumbani

Print this post