Mathayo 21:12 Yesu akaingia ndani ya hekalu, akawafukuza wote waliokuwa wakiuza na kununua hekaluni,akazipindua meza za wabadili fedha, na viti vyao waliokuwa wakiuza njiwa;
13 akawaambia, Imeandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala; bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.
Bwana aliwaagiza wana wa Israeli, kwamba waendapo mbele zake mahali patakatifu alipopachagua wakusanyike kwa ajili ya upatanisho. Kila mtu mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi atatoa nusu shekeli kama kodi, ambapo fedha hiyo ilitumika kwa ajili ya shughuli mbalimbali za hekaluni . Hivyo watu wote walipokwenda hekaluni kwa ajili ya ibada, walihakikisha wanabeba sadaka hiyo kwa ajili ya gharama za hekalu.
Utalisoma hilo katika vifungu hivi;
Kutoka 30:11 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
12 Utakapowahesabu wana wa Israeli, kama itakavyotokea hesabu yao, ndipo watakapompa Bwana kila mtu ukombozi kwa ajili ya roho yake, hapo utakapowahesabu; ili kwamba yasiwe maradhi kati yao, hapo utakapowahesabu.
13 Nacho watakachotoa ni hiki, kila mtu apitaye kwa wale waliohesabiwa atatoa nusu shekeli kwa kuiandama shekeli ya mahali patakatifu; (shekeli ni gera ishirini;) nusu shekeli kwa sadaka ya Bwana.
14 Kila mtu apitaye kwa wale waliohesabiwa tangu huyo ambaye umri wake ni miaka ishirini, au zaidi, atatoa hiyo sadaka ya Bwana.
15 Matajiri hawataleta zaidi, wala maskini hawataleta kilichopungua, katika hiyo nusu shekeli, watakapotoa hiyo sadaka ya Bwana, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya roho zenu.
16 Nawe utapokea hizo fedha za upatanisho mikononi mwa hao wana wa Israeli, na kuziweka kwa ajili ya utumishi wa hema ya kukutania; ili kwamba ziwe ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli mbele ya Bwana, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya roho zenu.
Lakini sasa kwa sababu fedha hiyo ilipaswa itolewe kwa fedha ya kiyahudi, na si za kigeni, ikizingatiwa kuwa watu walikuwa wanatoka mataifa mbalimbali ulimwenguni kote kuja kumwabudu Mungu pale Yerusalemu, Sasa hawa wanaoitwa wabadili fedha ndio wakapatia hapo fursa ya kuanzisha biashara hiyo pale hekaluni.
Lakini badala ya kufanya kama huduma, kuwasaidia watu kazi hiyo bila riba, wao wakageuza pale kuwa ni mahali pao pa kujipatia faida, pakawa kama kiini cha soko la fedha ukanda ule wote. Watu walipokuja na fedha zao, waliwageuzia kwa riba ya juu.
Hiyo ndio sababu Yesu kuchukizwa na wale watu, na kwenda kuzipindua meza zao, pamoja na wale wauza njiwa
Hata sasa, desturi hii ya adui inatenda kazi katika nyumba nyingi za Mungu duniani.
Watu hutumia mambo ya kiibada kama njia ya kujipatia faida. Si ajabu hata Mtume Paulo aliliona hilo akasema,
wakidhani ya kuwa utauwa ni njia ya kupata faida. (1Timotheo 6:5).
Utakuta mtu anafanya biashara ya biblia, kando kando ya kanisa. Atakuwa radhi kuzitoza bei zaidi ya kiwango stahiki ili ajinufaishe, kwasababu anajua watu wenye uhitaji wa vitabu hivyo kwa watu huo ni wengi. Mwingine atakuwa anauza maji au mafuta (wayaitayo ya upako), lengo sio kuwasaidia hao watu wapokee huduma, bali ni kujipatia faida.
Injili ya Kristo imekuwa biashara, kumwona mtumishi uombewe, ni lazima uandikiwe kuponi ya fedha, vinginevyo huwezi kumwona.
Sas watu kama hawa Yesu hawezi waonea huruma atazipindua meza zao, kama tu vile alivyozipundua za wale hekaluni. Maana yeye ni yeye Yule jana, na leo na hata milele.
2Timotheo 3:9 Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa dhahiri.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je! Habari iliyo katika 1Nyakati 21:25, na 2Samweli 24:24, ya Daudi kununua kiwanja inajichanganya?
Rudi Nyumbani
SWALI: Kwanini wale wayunani, walimfuata Filipo na kumwambia tunataka kumwona Yesu, maudhui ya tukio lile ni nini, mpaka lirekodiwe?
JIBU: Kipindi cha Bwana Yesu hadi kipindi chote cha mitume, yalikuwepo makundi mawili ya watu ambayo yalijikita kwa umakini sana katika kutafuta uhalisia na ukweli wote kuhusu masuala ya Mungu.
kundi la kwanza lilikuwa ni wayahudi, na kundi la pili ni wayunani. Tofauti ya wayahudi na wayunani ni kwamba. Wayahudi walijikita kuthibitisha kwa njia ya ishara. Lakini wayunani kwa hekima.
1 Wakorintho 1:22-23
[22]Kwa sababu Wayahudi wanataka ishara, na Wayunani wanatafuta hekima; [23]bali sisi tunamhubiri Kristo, aliyesulibiwa; kwa Wayahudi ni kikwazo, na kwa Wayunani ni upuzi;
Hivyo Yesu ambaye ni jibu lao wote alipokuja, baadhi ya hawa wayahudi walipomwona Kristo wakaanza kumthibitisha kwa ishara kwa walivyotarajia, kwamba ndiye masihi na mkombozi waliyemtarajia la!.(wakitaka wafanyiwe matendo fulani ya ajabu mbele ya macho yao, waamini)
Ijapokuwa Mungu hathibitishwi kwa ishara, bado Kristo aliwapa ishara.. Na ishara hiyo ilikuwa ni ile ya Yona. kukaa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana na hatimaye kutoka mzima.
Mathayo 12:38 Hapo baadhi ya waandishi na Mafarisayo wakamjibu, wakasema, Mwalimu, twataka kuona ishara kwako.
39 Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.
40 Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi.
Hilo lilipokuja kutimia…tunaona wayahudi wengi waliamini, ikiwemo mitume (akina Tomaso). Na ndio ukawa mwanzo wa kumuhubiri Yesu aliyefufuka.
Lakini wale waliotazamia ishara walizoziwaza kwa akili zao, mfano za kushusha moto, kama Eliya, na kusahau ile ya kufufuka ambayo imezidi zote, bado Kristo akabakia kikwazo kwao.
Halikadhalika na kwa wayunani. Walimtafuta Mungu kwa njia ya hekima, ya elimu, ya maarifa, walimtafuta Mungu mwenye siri zote za uumbaji, na ujuzi, na utashi zaidi ya wanadamu wote na viumbe vyote.Ambaye atawazidi wanafalsa wao kama Plato, Socrates, Aristotle.
Kwa muda mrefu hawakufanikiwa mpaka baadhi yao, wakaishia kumwabudu tu, huku wakikiri hawamjui.
Matendo 17:22-23
[22]Paulo akasimama katikati ya Areopago, akasema, Enyi watu wa Athene, katika mambo yote naona ya kuwa ninyi ni watu wa kutafakari sana mambo ya dini.
[23]Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua.
Yaani wakiwa na maana tunasikia miungu mingi,.lakini katika hiyo yote bado hatujaona mwenye hekima ya kuitwa Mungu wa ulimwengu. Wote akili zao ni kama za kibinadamu tu.
Sasa tukirudi kipindi cha Yesu, tunaona tukio jipya linajitokeza,
sio tu wayahudi walimwamini, bali hadi hawa wayunani watafuta-hekima wengi wao waliposikiliza maneno ya Yesu, na kupima kwa jicho la hekima, wakaona hakika hajawahi tokea anayeweza kuelezea ukweli wote wa uumbaji kama Yesu.
Hilo liliwashawishi na kuwafanya kukiri kuwa huyu ndiye suluhisho la utata wetu kuhusu Mungu na elimu.
Hivyo wakaamini, ndio sababu ya wao kumfata Filipo kumwomba wamwone Yesu. Hiyo ilikiwa ni heshima kubwa sana kwa Yesu (kidini) mbele ya macho makuhani na mafarisayo wote, kwamba Mungu kathibitishwa kifalsafa. Kumbuka wayunani hawa waliokwenda hawakuwa watu tu wa kawaida. Bali ni watu wenye heshima ya juu sana na hadhi.
Hiyo ndio sababu Bwana Yesu kusema saa imefika mwana wa Adamu atukuzwe.
Yohana 12:20-26
[20]Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu.
[21]Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu.
[22]Filipo akaenda, akamwambia Andrea; kisha Andrea na Filipo wakamwambia Yesu.
[23]Naye Yesu akawajibu, akasema, Saa imefika atukuzwe Mwana wa Adamu.
[24]Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi.
[25]Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele.
[26]Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.
Hata leo, Yesu anathibitika katika mambo yote endapo tu tutamaanisha kumwona katika namna hizo. Ndio maana katika makundi yote ya watu ni lazima utakuta waamini.
Katika ya wanasayansi utawaona, katikati ya wanajeshi utawaona, katikati ya watawala utawaona,katikati ya mamajusi utawaona, katikati ya matajiri utawaona, katikati ya maskini utawaona, kati ya wanazuoni utawaona, kati ya madaktari utawaona,
Ukiuliza imekuwaje katika hali zao/ nafasi zao ambazo ni mbaya, na nyingine zenye majaribu, au zenye kumkana Mungu waziwazi, lakini wao wamemwamini Mungu?.
Ni kwasababu YESU anathibitika kila mahali.
Mtu kutokuamini ni yeye mwenyewe kataka. Hakuna atakayekuwa na udhuru siku ya mwisho, kwasababu Yesu amefunuliwa kila mahali.
Swali ni je! umemwamini Kristo? kama ni la! unasubiri nini. Mwamini leo kwa kuikubali kazi aliyoikamilisha juu yako ya kuondoa dhambi kwa kifo na kufufuka kwake. Ambayo hiyo huambatana na toba ya kweli na ubatizo.
Baada ya hapo utakuwa umepokea ondoleo la dhambi zako bure, mpokee Yesu sasa
Mungu akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
Maandiko yanaonyesha kuwa kitu pekee cha asili kinachoweza kutenganisha watu wawili walio katika Ndoa ni KIFO.
Warumi 7:2 “Kwa maana mwanamke aliye na mume amefungwa na sheria kwa yule mume wakati anapokuwa yu hai; bali akifa yule mume, amefunguliwa ile sheria ya mume.
3 Basi wakati awapo hai mumewe, kama akiwa na mume mwingine huitwa mzinzi. Ila mumewe akifa, amekuwa huru, hafungwi na sheria hiyo, hata yeye si mzinzi, ajapoolewa na mume mwingine.”
Lakini inapotokea Mtu anachukua nafasi ya KIFO, yaani anaivunja ndoa yake mwenyewe au ya Mtu mwingine iliyo ya Halali, basi mtu huyo kibiblia ni MFU, au jina lake lingine ni KIFO/MAUTI..Sasa utauliza KIFO kinaweza kuwa MTU jibu ni Ndio!.
Ufunuo 6:8 “Nikaona, na tazama, farasi wa rangi ya kijivujivu, na yeye aliyempanda JINA LAKE NI MAUTI, na Kuzimu akafuatana naye…”
Kwahiyo Mtu anayechukua nafasi ya KIFO, katika ndoa yake mwenyewe au ya mwingine, huyo jina lake ni MAUTI kibiblia, awe mwanamke au mwanaume, huyo ni MAUTI, ni Mfu anayetembea.
Utauliza ni wapi tena katika maandiko, panaonyesha mtu aliyeharibu ndoa ya mwingine aliitwa MFU?
Mwanzo 20:2 “Ibrahimu akamnena Sara mkewe, Huyu ni ndugu yangu. Basi Abimeleki mfalme wa Gerari akapeleka watu akamtwaa Sara.
3 Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, UMEKUWA MFU WEWE kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu”.
Umeona hapo?.. MUNGU anamwambia Abimeleki kuwa yeye ni MFU kwa kitendo tu cha kumchukua mke wa Ibrahimu.
Hebu jiulize hapo kwanini Mungu hajamwambia Mfalme Abimeliki kuwa umekuwa Najisi, au umekuwa Mjinga, au umekuwa Mpumbavu.. badala yake anamwambia amekuwa MFU!!!.. Maana yake pale alipo alikuwa ni Marehemu anayeishi.. Siku yoyote anashuka kaburini, na kila atakachojihusisha nacho kitakufa pia.
Hiyo pia ni hali ya Mtu anayeharibu ndoa yake mwenyewe au ya mwingine, kiroho jina lake ni MFU/MAUTI.
Na kumbuka maandiko yanasema Mauti anafuatana na Kuzimu.. Ufunuo 6:8 “Nikaona, na tazama, farasi wa rangi ya kijivujivu, na yeye aliyempanda JINA LAKE NI MAUTI, na Kuzimu akafuatana naye…”
Maana yake huyu mtu anayeitwa MAUTI, anakwenda sambamba na kuzimu, na mwisho ni ZIWA LA MOTO.
Ufunuo 20:14 “Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto”.
Je Mke au Mume uliye naye ni wako? Au wa mtu mwingine?… Unajua ni maumivu gani unayasababisha kwa mwingine unapomchukua Mke wake au Mume wake??..
Labda ulimchukua pasipo kujua maandiko au enzi bado hujaokoka, lakini sasa umejua …Mrudishe huyo mwanamke/mwanamume kwa aliyewake wake hata kama una watoto naye, (weka naye tu mipango ya namna ya kuwatunza watoto), lakini usiendelee kuishi naye kwani unafanya UZINZI, mrudishe kwa mume wake/mke wake, akikataa Mwache aishi mwenyewe, wewe utakuwa umejifungua katika kifungo cha Mauti….Vunja agano na Mauti kwa namna hiyo…
Isaya 28:18 “Na agano lenu mliloagana na mauti litabatilika, tena mapatano yenu mliyopatana na kuzimu hayatasimama; pigo lifurikalo litakapopita, ndipo ninyi mtakapokanyagwa nalo”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)
Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu Yesu Kristo, karibu tuyatafakari maneno ya uzima. Leo napenda tujifunze tabia nyingine ya Bwana Yesu. Kwasababu yeye mwenyewe alituambia ‘tujifunze kwake’. Hivyo naamini tuna mengi ya kuyajua kuhusu yeye.
Habari hiyo tunaisoma katika vifungu hivi;
Luka 9:51 Ikawa, siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu;
52 akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.
53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.
54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?
55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]
56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine.
Kama wewe ni msomaji mzuri wa biblia utakumbuka kuwa kuna wakati ulifika, ilikuwa wazi kwa watu wote, kuwa Yesu anatafutwa ili auawe, (hususani kule Yerusalemu). Na hilo lilimfanya mara kadha wa kadha asitembee kwa uwazi wote mbele ya makutano (Yohana 7:10), kwasababu, saa yake ya kuuawa ilikuwa bado haijafika.
Yohana 11:54 Kwa hiyo Yesu hakutembea tena kwa wazi katikati ya Wayahudi; bali alitoka huko, akaenda mahali karibu na jangwa, mpaka mji uitwao Efraimu; akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
Lakini mambo yalikuja kubadilika baadaye, hilo halikuendelea kwa wakati wote. Alipoona sasa kazi aliyopewa na Mungu ameimaliza, alionyesha tabia nyingine ambayo haikuwa ya kawaida. Biblia inatuambia, “aliukaza uso wake kuelekea Yerusalemu”, kule kule alipokuwa anatafutwa auawe.
Jambo ambalo lilileta mshtuko hata kwa mitume wake;
Yohana 11:7 Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, Twendeni Uyahudi tena.
8 Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe, nawe unakwenda huko tena?
9 Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.
Walishangaa, ujasiri huo ni wa namna gani? Ni sawa na wanajeshi waliokwenda vitani, halafu maadui wakawaua wanajeshi wote, akabakia mmoja tu, halafu huyo mmoja anasema nitakwenda kupambana na jeshi lote hilo peke yangu sitajificha. Ukweli ni kwamba inahitaji nguvu nyingine ya ziada ndani ya huyo mtu.
Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu, aliukaza uso wake, kwenda kututetea sisi. Embu Fikiria kama angeulegeza, na kuendelea kuzunguka mahali pengine na sio kule uyahudi(Yerusalemu), wokovu wetu tungeupatia wapi?
Ilibidi, alazamishe mambo, japo mwili wake ulikuwa hautaki, ndio maana akiwa pale bustanini, anaomwomba Baba, akisema ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke, ni kuonyesha kuwa hata mwili wake ulikuwa unagoma kuwepo kule Yerusalemu, na si mwili tu, bado mazingira pia hayakutaka, alipokuwa anakatiza kwa Wasamaria wenyeje wa pale hawakutaka kumruhusu akae kwao, kwasababu waliona kama anawaletea matatizo, ikumbukwe kuwa watu hao hao ndio waliokuwa wanataka kumfanya mfalme hapo mwanzo. Kuonyesha kuwa mazingira yalimgomea. Si mazingira peke yake, hata mitume wake nao, walifanya kama kumsindikiza tu, lakini mioyo yao walishajiandaa kuchukua hatua yoyote lolote litakapotokea, ndio maana pale bustanini, wale watu walipokuja kila mmoja akakimbia na njia yake.
Kwa ufupi kila kitu kilikataa, isipokuwa roho yake tu. Ndio sababu ya kwanini maandiko yanatuambia ‘aliukaza uso wake’ kwasababu haikuwa rahisi, si jambo tena la kuomba, au kubembeleza, au kushawishi, au kusubiri msimu mzuri. Bali ni kujitoa tu wote wote, katika hayo. Watu wengi tunadhani Yesu aliuchukua msalaba wake siku ile alipobebeshwa ule mti, hapana, aliuchukua msalaba wake Kwa kitendo hichi cha kuamua kuukaza uso wake, kuelekea kifoni. Hata aliposema tujitwike misalaba yetu, alilenga, eneo hilo.
Ni nini na sisi tunapaswa tukipokee kwa Bwana Yesu?
Kwa kuwa Roho wake naye yupo ndani yetu, hatuna budi kufahamu kuwa yapo majira katika safari yetu ya wokovu, hatutahitaji mazingira yawe mazuri, ndio tulitimize kusudi la Mungu, au ndugu kutukubalia, au marafiki kuafikiana na sisi, au miili kutuambia sasa ndio wakati, hapana..bali ni kujitwika misalaba yetu, “kwa kukaza nyuso zetu” na kumfuata Yesu.
Tukingoja vikwazo viondoke, au viondoshwe, tutajidanganya, na tutangoja sana, kwani vita vitaendelea kuwepo mpaka mwisho, mapambano hayaishi, tutashinda tu kwa kukaza tu nyuso zetu. Na Bwana atakuwa pamoja na sisi, ijapokuwa itaonekana ni kujipoteza lakini mwisho wake utakuwa ni uzima kama ulivyokuwa kwa Bwana Yesu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?
Rudi Nyumbani
Msingi ni chimbuko, au mwanzo au kiini cha kitu fulani.
Ni wazi kuwa kila jambo lina msingi wake. taifa lina msingi wake, taasisi ina msingi wake, kabila lina msingi wake vilevile pia imani ina msingi wake.
Hivyo tukirudi katika ukristo. Msingi wa imani yake ni upi?
Msingi wa ukristo ni YESU KRISTO mwenyewe, na kazi yake aliyoikamilisha ya kufa na kufufuka kwake. Na sio kanisa, au dhehebu, au mapokeo fulani, au kikundi fulani cha wanaharakati.
Pasipo Yesu hakuna ukristo.
Yeye anafananishwa na lile jiwe kuu la pembeni, ambalo hakuna mjenzi aliyeweza kusimamisha jengo bila kuliweka hilo.
1 Petro 2:6
[6]Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika.
Habari kamili za Yesu, na kazi yake aliyokuja kuifanya duniani unaipata katika kitabu kimoja tu kiitwacho BIBLIA. Hivyo huwezi kutenganisha biblia na Yesu Kristo.
Ili mtu ashawishwe kuipokea imani, ni sharti, aisikie kwanza injili yake ambayo hiyo utaipata katika Neno la Mungu yaani biblia..(Warumi 10:17)
Mpaka mtu aitwe mkristo ni lazima amtambue kwanza Kristo ni nani, na nini amekileta duniani, vinginevyo hawezi kuwa mkristo, hata kama atajiunga na kanisa, au dhehebu na kuyashika mapokeo yote aliyoyakuta huko, au kuisoma biblia yote, huyo bado hajawa mkristo.
Ni muhimu sana kumtambua Yesu ni nani kwetu. Kumtambua Yesu kama mwana wa Mungu bado inaweza isikupe wokovu, hata kumtambua Yesu kama Mungu bado inaweza isikupe wokovu (ijapokuwa vyote hivyo ni vyeo vyake). Lakini vyeo hivyo sio kiini cha ukristo.
Yesu ni nani na ni nini alikileta duniani?
Yesu ni MKOMBOZI, kama tafsiri ya jina lake linavyojieleza( Mathayo 1:21)
mkombozi wa nini?
Alikuja kutukomboa roho zetu, nafsi zetu na miili yetu, Na kama ilivyo kanuni ya kiroho ili jambo hilo liweze kukamilika ilipasa itolewe kafara isiyo na kasoro yoyote(yaani dhambi). Na aliyeweza kukidhi vigezo hivyo ni Yesu pekee.
Ndio maana ilimgharimu afe, kama fidia ili sisi tupokee ondoleo la dhambi na msamaha wa dhambi kwa kifo chake. Hivyo yoyote anayeamini(yaani anayeupokea wokovu huo aliouleta).
kwa toba ya kweli na ubatizo, Basi anakuwa ameokoka, hivyo ile ghadhabu ya Mungu kwa wenye dhambi wote haiwi tena juu yake, tangu huo wakati anaitwa mbarikiwa, au mkristo, kwasababu dhambi zake zinakuwa zimefutwa kabisa.
Na zaidi ya hayo mtu huyu moja kwa moja anapewa zawadi ya Roho Mtakatifu, ambaye tangu huo wakati na kuendelea anakuwa ndani yake kama msaidizi, kumsaidia madhaifu yake, katika kuomba, kuijua kweli, kumkumbusha aliyoyasema Yesu, kumpasha habari ya mambo yajayo, na kumtia nguvu ya kumtumikia Mungu, pamoja na kumpa nguvu ya kushinda dhambi.
Huyu ndiye mkristo.
Swali ni je! umemwamini ipasavyo? au umempokea kwa namna ile ya kidini?
Usifikiri kuhama dini, wewe ni Kristo, au kuzaliwa kwenye familia ya kikristo wewe ndio mkristo, au kusomea theolojia, hapana hizo ni kampeni tu, ukristo halisi huja kwa kumwelewa Kristo ni nani na ni nini amekifanya kwako.
Ikiwa bado hujaokoka na unataka kumpokea leo ili upate ondoleo la dhambi zako. Basi uamuzi huo ni bora sana kwako. Wasiliana nasi namba uzionazo chini kwa mwongozo wa sala ya toba.
Ubarikiwe.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
+255693036618/ +255789001312
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?
Rudi Nyumbani
Biblia kitabu kikamilifu, na kitakatifu kimeandikwa na waandishi Zaidi ya 40 kwa Uvuvio wa Roho Mtakatifu. Ndani ya biblia kuna taarifa zinazohusu maisha ya watu zilizobeba sauti ya Mungu nyuma yake, pia kuna taarifa za Mataifa mbalimbali pia zenye kubeba sauti ya Mungu nyuma yake, lakini Zaidi sana kuna Nabii za wakati ujao.
Ifuatayo ni orodha ya waandishi 40 wa Biblia kuanzia Agano la kale hadi Agano jipya.
Agano la kale.
Agano Jipya.
Kwanini waandishi wapo Zaidi ya 40 na si 40 kamili?.. Ni kwasababu biblia pia imewataja wana wa Kora, ambao hatujui walikuwa ni wangapi, zaidi sana yupo mwandishi wa kitabu cha Waebrania, ambaye hajatajwa ni nani, huenda akawa ni Mtume Paulo, lakini kama si yeye bali ni mwingine, basi ataongezeka katika idadi ya walioiandika biblia.
Kumbuka tena, biblia ni kitabu cha Mungu kilichoandikwa na WATU, kwa uvuvio wa ROHO MTAKATIFU, Hivyo maneno yaliyoandikwa ndani ya Biblia, yana uzima.
2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema”.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.
Mwandishi wa kitabu cha Matendo ya mitume.
Mwandishi wa kitabu cha Mithali ni nani?
Hosea 2:13 “Nami nitamwadhibu kwa sababu ya siku za Mabaali, aliowafukizia uvumba; hapo alipojipamba kwa PETE MASIKIONI MWAKE, na kwa vito asema Bwana”.
Kabla ya kuvaa kitu, au kuiga mtindo fulani, hebu tenga muda kwanza kufuatilia asili ya kitu hiko kibiblia, kwasababu kuna vitu vingine asili yake ni mbaya, na isiyo na baraka kwa Mungu.
Hebu jiulize swali hili.. Mungu akuumbe na masikio yaliyo kamili, halafu akwambie au akuruhusu ukayatoboe masikio hayo, eti ili tu upendeze?..hivi jambo hilo ni kweli Mungu kaliagiza au kaliruhusu??.. au ni ujanja tu wa akili za watu! (walionyanyuliwa na ibilisi, Waefeso 4:14).
Sasa sikuhukumu wewe uliyetobolewa masikio, huenda si wewe kwa hiari ulifanya hivyo, bali walikutoboa tu ukiwa mchanga..na pia waliokutoboa huenda nao pia walipokea tu kwa waliotangulia, hivyo huenda kosa si lako wala la wazazi, bali la yule wa kwanza kuanzisha makosa hayo..
Lakini sasa baada ya kuelewa, si sawa kuendeleza hayo makosa kwa vizazi vyako, vile vile si sawa kuweka chuma au dhahabu katika matundu ya masikio yaliyotobolewa, kwani kwa kufanya hivyo bado utakuwa unaendeleza desturi hiyo.
Hebu tusome tena…
Hosea 2:13 “Nami nitamwadhibu kwa sababu ya siku za Mabaali, aliowafukizia uvumba; hapo alipojipamba kwa pete masikioni mwake, na kwa vito asema Bwana”.
Asili ya kujipamba kwa pete za masikioni (yaani kuweka hereni) ilikuwa NI KUJIWEKA TAYARI KWA KUVUKIZA UVUMBA KWA MABAALI… na baali si mwingine zaidi ya shetani mwenyewe/kusifa katika kinyago chake kingine.
Kwahiyo zamani mtu akijipamba kwa kutoboa masikio na kuweka hereni alikuwa aidha ametoka kuvukiza uvumba kwa baali au ndio anaenda kuvukiza uvumba kwa baali, na hereni zamani hazikuwa zinavaliwa tu na wanawake, bali hata na wanaume, na lengo lilikuwa ni hilo hilo kumvukizia uvumba baali.
Labda utauliza ni wapi tena pengine panapoonyesha hereni, zinahusishwa na ibada za miungu..
Mwanzo 35:2 “Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake, na wote waliokuwa pamoja naye, ONDOENI MIUNGU MIGENI ILIYOKO KWENU, mjisafishe mkabadili nguo zenu. .
4 NAO WAKAMPA YAKOBO MIUNGU MIGENI YOTE ILIYOKUWA MIKONONI MWAO, NA PETE ZILIZOKUWA MASIKIONI MWAO, naye Yakobo akazificha chini ya mwaloni ulioko Shekemu”.
Sasa shetani ni yule yule, na ibada zake ni zile zile, hazijabadilika……kama bado yupo kwenye makafara ya mang’ombe mpaka leo, na mambuzi, na bado waganga wake ni wale wale, na mavazi yao ni yale yale, na uchawi wake ni ule ule, unadhani uchawi wake katika HERENI (pete za masikioni) utakuwa umebadilika??.. Jibu ni la! Utakuwa ni ule ule tu.
Tafakari, tafakari mama, tafakari dada, tafakari kaka unayevaa hereni, kuambiwa usivae hereni sio kwamba unawekwa chini ya sheria, hapana!.. bali kinyume chake ndio UNAKUWA HURU… Lakini kuvaa hereni ndio sheria, kwani itakulazimu kila siku kuivaa kabla ya kutoka nje, na kubadilisha aina ya hereni leo hii kesho ile, sasa huoni kama hiyo ndio SHERIA???, na kutokuvaa hereni ndio uhuru??.
Ni kweli ukiacha kuzivaa utaonekana si mrembo kwa baadhi ya watu, lakini utakuwa umejiepusha na ibada za sanamu, ambazo zitakuzalia madhara mengine makubwa kiroho.
Miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, sawasawa na 1Wakorintho 3:16, na 1Wakorintho 6:19.
Kwa jinsi tunavyozidi kuiweka kuwa mitakatifu, ndivyo Roho Mtakatifu anavyokaa ndani yetu, na ndivyo tunavyomfaidi Roho Mtakatifu kwa matunda yake yaliyotajwa katika Wagalatia 5:22.
Bwana akubariki sana.
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je unaijua anwani ya msalaba?…na je unajua nguvu yake? Kama bado hujaifahamu basi leo ifahamu na anza kuitumia katika maombi yako, badala ya vitendea kazi vingine kama maji,chumvi na mafuta.
Yohana 19:19 “Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI.
20 Basi anwani hiyo waliisoma wengi katika Wayahudi; maana mahali pale aliposulibiwa Yesu palikuwa karibu na mji; nayo iliandikwa kwa Kiebrania, na Kirumi, na Kiyunani”
Jina la YESU WA NAZARETI ndio ANWANI ya maombi ya kila Mkristo.
Umeahi kujiuliza kwanini haijaandikwa YESU MGALILAYA, au YESU MBETHLEHEMU mji ule aliozaliwa, badala yake imeandikwa YESU MNAZARETI?..na tena kwa lugha zote tatu (3), zilizokuu za dunia.
Kuna nini katika Nazareti?
Nazareti ndio mji uliotabiriwa na manabii kubeba utambulisho wa Masihi Mkuu ajaye… hivyo huo ni mji wa UTAMBULISHO KIBIBLIA.
Mathayo 2:23 “akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo”.
Kwahiyo tunapotaja jina la YESU na kuelekeza yule wa NAZARETI tumelenga kwenye shabaha yenyewe hivyo mashetani yanaondoka, magonjwa yanaondoka, dhambi inaisha nguvu, kwasababu ndiye Masihi halisi aliyetajwa.
Hebu tulione hili zaidi…
Wakati Bwana YESU anamtokea Sauli alipokuwa anaenda Dameski kwa ajili ya kuwaua wakristo, utaona hakujitambulisha kama YESU wa Galilaya, au YESU aliye mbinguni, badala yake alijitambulisha kama YESU Mnazaeti ijapokuwa yupo mbinguni.
Matendo 22:6 “Ikawa nilipokuwa nikisafiri, nikikaribia Dameski, wakati wa adhuhuri, ghafula nuru kuu ilitoka mbinguni, ikanimulikia pande zote.
7 Nikaanguka nchi, nikasikia sauti ikiniambia, Sauli, Sauli, mbona unaniudhi?
8 Nikajibu, Wewe u nani, Bwana? Akaniambia, MIMI NI YESU MNAZARETI, ambaye wewe unaniudhi”.
Utaona pia Mitume wa Bwana YESU waliitumia hii anwani popote walipokwenda katika huduma zao.
Petro aliitumia alipokutana na yule kiwete aliyezaliwa katika hali ile..
Matendo 3:6 “Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende.
7 Akamshika mkono wa kuume, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu.
8 Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda; akaingia ndani ya hekalu pamoja nao, akienda, akiruka-ruka, na kumsifu Mungu.
9 Watu wote wakamwona akienda, akimsifu Mungu”.
Soma pia Matendo 2:22, Matendo 3:6, Matendo 4:10, Matendo 10:38, Matendo 26:9, Marko 1:24, Marko 16:6, Marko 10:47, Luka 24:9, Yohana 1:45, utazidi kuona jambo hilo.
Na hiyo pia ndio sababu Mungu aliruhusu Pilato aandike anwani ile juu ya msalaba… “YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI”. Kwa lugha zote kuu, ikimaanisha kuwa anwani ya wokovu wa msalaba kwa mataifa yote na lugha zote ni jina la YESU WA NAZARETI.
Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”
Maana yake njili inayohubiri msalaba pasipo kuhusisha anwani ya jina la YESU ni uchawi, maombi yoyote yasiyohusisha anwani ya jina la YESU ni unashiri na ibada za sanamu.
Kama anwani hiyo ya jina la YESU WA NAZARETI hata baada ya Bwana kupaa bado anaitumia akiwa mbinguni, sisi ni akina nani tuifanye iieshe matumizi katika zama zetu?, na kuweka mafuta, chumvi, maji au majina yetu kama mbadala??.
Tumia jina la YESU, liamini jina la YESU WA NAZARETI epuka matapeli, na jina la YESU HALIUZWI, EPUKA MATAPELI!.
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mithali 29:17 “Mrudi mwanao naye atakustarehesha”.
Kumrudi mtoto sio “kumwadhibu tu”. Bali pia kumrekebisha (Kauli zake na njia zake).
Ni kweli maandiko yanaruhusu kumwadhibu mtoto kwa kiboko pale anapokosea, lakini hiyo iwe hatua ya mwisho baada ya kuona harekebishiki kwa maneno..
Katika hatua hiyo maandiko yameruhusu kutumia mapigo kwa huyo mtoto, ili kuiokoa roho yake na kuzimu.
Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.
14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.
Soma pia Mithali 22:15.
Wengi wanaogopa kuwaadhibu watoto wao kwa mapigo wakiamini kuwa watapata madhara ya kisaikolojia na hata kiafya.. pasipo kujua kuwa hapo biblia imesema ukimpiga “hatakufa”..maana yake Mungu atazuia madhara yote ya kiafya, ikiwa lengo lako si lingine zaidi ya kumjenga.
Lakini kabla ya kufikia hatua hiyo ya matumizi ya fimbo, ni muhimu kuanza na maonyo, na makemeo.
Maana yake kama mtoto amekosea kusema ni lazima arekebishwe kusema kwake mapema, kwasababu watoto wanasikia mambo mengi na kuyachukua tu pasipo kupambanua.
Tuliwahi kufanya maombi sehemu fulani, tukakuta mtoto wa miaka 5 anatukana matusi makubwa na anarudia tusi hilo hilo moja, mara ya kwanza tulidhani ni mtoto ana mapepo, lakini baadae tuligundua kuwa hana mapepo na hata matusi aliyokuwa anayatamka alikuwa hajui maana yake, alitamka tu akidhani kuwa ni maneno ya kawaida, pasipo kujua kuwa alikuwa anatukana.
Sasa mtoto ni kwamba alisikia hayo matusi pengine kwa watoto wenzake anaocheza nao, wasio na maadili na yeye akidhani ni neno la kawaida akalichukua na kulitumia popote alipoona mazingira hayampendezi.
Sasa mzazi hakuchukua jukumu sahihi la kumrekebisha, badala yake tu alianza kumpiga kila alipotaja hilo neno akidhani kuwa anafanya makusudi, na hata sisi tulipofika alitukana na mamaye alimfinya, lakini alipolia bado aliendelea kutukana.
Mama alidhani mtoto anakiburi na mkorofi, kumbe mtoto alilia akijitetea kwa kudhani kuwa lile neno ni sahihi kutamka mahali pale.
Sasa laiti kama mzazi angepata wasaa wa kumketisha na kumwonya na kumwambia anachokisema si sahihi na hakifai, kabla ya mapigo… mtoto angeelewa na kubadilika.
Kwahiyo ni muhimu kuwasikiliza watoto wanasema nini na kuzirekebisha kauli zao mapema,
Ni vizuri kuangalia watoto wako wanachokiangalia na kukikosoa mbele yao kama hakifai…
Pia ni muhimu kufuatilia michezo yao wanayoicheza na kuikemea mapema mbele yao,…..kwani wao ni kuiga tu siku zote…ni vichache wanabuni wenyewe..
Vingi wanaiga kutoka kwa watu pasipo kupambanua, na wanajifunza kutoka kwa watu wanaowazunguka, ikiwemo wanafunzi wenzao mashuleni na pia kupitia Tv.
Kwahiyo kagua maisha ya watoto wako, na “warudi mapema”..wala hawatakuchukia, au kuwashusha kisaikolojia bali utawajenga kwa maisha yao ya baadae..
usipowarudi mapema na wakikua katika misingi hiyo itakuwa ni ngumu kubadilika ukubwani, kwani ile dhambi wameanza kuifanya tangu utotoni na hivyo hawawezi kushawishika kuona madhara yake ukubwani, na ili hali hawakuona madhara yake utotoni.
Mtoto akiwa na kiburi au mtukutu basi mkanye kila wakati, na panapobidi basi tumia kiboko ila usimwache akakua na hiyo tabia.
Na pia akiwa hasikii, tafuta kila namna awe anasikia, usiache na kusema huyu karithi hiyo tabia kwa watu fulani waliotangulia..
Na pia mfundishe kauli za kibiblia, na kuomba, mfundishe
salamu za kibiblia, na misemo ya kibiblia…akue katika hiyo hata kama bado hajaweza kuipambanua lakini mfanye akariri hivyo hivyo kwani itakuja kumsaidia mbeleni kwasababu itakuwa moyoni mwake.
Kwa kumlea hivyo biblia inasema baadaye atakustarehesha..
Mithali 29:17 “Mrudi mwanao naye atakustarehesha”.
Kustarehesha maana yake “hatakuja kukusumbua huko mbeleni”…
Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!
WAISRAELI WENGI SANA WANARUDI KWAO SASA.
BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.
Jina tukufu la Bwana YESU KRISTO libarikiwe.
Je umewahi kutafakari kwanini mapigo yote tisa (9) aliyopigwa Farao bado moyo wake ulikuwa mgumu? Na kwanini lile pigo moja la mwisho la kufa wazaliwa wa kwanza ndipo akawaruhusu wana wa Israeli?.
Sasa hakuna mahali popote maandiko yanasema kuwa “Mungu aliufanya moyo wa Farao kuwa mlaini”.
Maana yake Farao aliendelea kuwa na moyo mgumu mpaka alipoingia kwenye ile bahari ya Shamu, na hapo ndio ikawa mwisho wake.
Sasa ni nini kilitokea mpaka Farao akawaachia wana wa Israeli?… Si kingine bali ni ule msiba alioupata,
Na huku bado moyo wake ukiendelea kuwa mgumu, alivunja sheria ya moyo wake na kuwafukuza wana wa Israeli kwa muda. (Lakini moyo wake bado ulikuwa mgumu tu).
Kutoka 11:1 “BWANA akamwambia Musa, Liko pigo moja bado, nitakaloleta juu ya Farao na juu ya Misri; baadaye atawapa ninyi ruhusa mtoke huku; naye hapo atakapowapa ruhusa, atawafukuza mtoke huku kabisa kabisa”
Sasa ni siri gani iliyokuwepo ndani ya wazaliwa wa kwanza wa Misri hata kumfanya Farao awafukuze wana wa Israeli?…Kwani ni wazi kuwa hata Farao angepigwa kwa mapigo gani ya asili asingewaachia wana wa Israeli.
Ila ni nini kilikuwa kwa wazaliwa wa kwanza wa kiMisri?
Kilichokuwa ndani ya wazaliwa wa kwanza wa Misri, ikiwemo mwana wa Farao si kingine zaidi ya “miungu ya kimisri”..
Hivyo kifo cha wazaliwa wa kwanza ilikuwa ni hukumu kubwa kwa miungu yao pamoja kudhalilika kwa miungu yao ambao waliamini ina nguvu nyingi.
Ndio maana MUNGU aliposhuka kuwaharibu wazaliwa wa kwanza pia alisema ataiharibu na miungu yao (ambayo kiuhalisia ilikuwa inaishi ndani ya hao wazaliwa wa kwanza).
Kutoka 12:12 “Maana nitapita kati ya nchi ya Misri usiku huo, namij nitawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, wa mwanadamu na wa mnyama; nami nitafanya hukumu juu ya miungu yote ya Misri; Mimi ndimi BWANA.”
Zamani katika nchi ya Misri na hata katika mataifa mengine ya dunia, wazaliwa wa kwanza wa kiume waliaminika kama miungu ya familia na ya nchi.
Na wanyama wa kwanza kuzaliwa, ndio waliotumika kwa kafara za miungu yao.
Hivyo watoto wote wa kwanza wa kiume walikuwa wanabeba ukuhani wa miungu, na roho zote za miungu zilikuwa zinakaa ndani yao.
Kwahiyo kilichomwumiza zaidi Farao si msiba wa mtoto, bali ni kuhukumiwa kwa miungu yao iliyokuwepo ndani ya wale watoto!!..
Kwaufupi Farao alichanganyikiwa kidogo, hakuelewa ni nini kimetokea katika eneo lake la imani.
Na hata waMisri wote walichanganyikiwa vivyo hivyo, hakuna ambaye hakulia..wote walilia na kuhofu na kutoelewa ni nini cha kufanya, waliyeyuka mpaka kufikia hatua ya wana wa Israeli kuwateka nyara.
Kutoka 12:33 “Wamisri nao wakawahimiza watu, kuwatoa katika nchi kwa haraka, maana walisema, Tumekwisha kufa sote.
34 Watu wakauchukua unga wa mikate yao kabla haijatiwa chachu, na vyombo vyao vya kukandia wakavitia ndani ya nguo zao mabegani.
35 Wana wa Israeli wakafanya kama neno lile la Musa; wakataka kwa Wamisri vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu, na mavazi.
36 BWANA akawajalia kupendelewa na Wamisri hata wakawapa kila walichokitaka. Nao wakawateka Wamisri nyara”
Ni ujumbe gani tunapata hapo?..au ni kitu gani kilichokuwa kimewafunga wana wa Israeli?
Si utajiri wala hazina zilizoko Misri kwamaana Bwana aliuharibu utajiri wake wote kwa zile mvua za mawe na nzige, vile vile si uzuri wa Misri, kwasababu Bwana aliharibu uzuri wake kwa zile mvua za mawe lakini bado wana wa Israeli walikuwa kifungoni.
Wala si ushujaa wa waMisri kwasababu Bwana aliwapiga kwa chawa, na majipu na aliwanyima maji ya kunywa kwa siku saba, hivyo walikuwa dhaifu..lakini bado wana wa Israeli walikuwa kifungoni.
Ni nini kilichokuwa kimewashikilia wana wa Israeli???…..jibu ni “miungu ya kimisri” iliyokuwa inaabudiwa ndani ya watu.
Hiyo ilipopigwa pamoja na makuhani wake (ambao ndio wazaliwa wa kwanza)..vifungo vikalegea, wana wa Israeli wakaachiwa.
Laiti Bwana Mungu angelileta hilo pigo mwanzoni kabla ya yote, Farao angeshaawaachia Israeli kitambo sana pamoja na moyo wake kuwa mgumu, lakini Mungu aliliruhusu liwe mwisho wa kusudi lake maalumu.
Na ukiendelea kusoma mbele utaona Bwana anawapa amri wana wa Israeli wawatakase wazaliwa wa kwanza na kwamba kila mzaliwa wa kwanza atakuwa ni wa Bwana, maana yake atakuwa kuhani wa Bwana kwa lazima (kwasababu kulikuwa na kitu katika wazaliwa wa kwanza).
Maana yake kila mzaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli alipaswa kutolewa kwa Bwana kama Hana alivyomtoa Samweli kwa Bwana (hiyo ilikuwa ni amri).
Lakini sheria hiyo ilikuja kubadilika, na ukuhani wa wazaliwa wa kwanza likapewa kabila la Lawi.
Hesabu 3:12 “Mimi, tazama, nimewatwaa Walawi na kuwatoa kati ya wana wa Israeli badala ya wazaliwa wa kwanza wote wafunguao tumbo katika wana wa Israeli; na hao Walawi watakuwa wangu;
13 kwa kuwa hao wazaliwa wa kwanza wote ni wangu; katika siku ile niliyowapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri nikajiwekea wakfu wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, wa wanadamu na wa wanyama; watakuwa wangu; mimi ndimi BWANA”.
Hivyo wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli wanaozaliwa ilikuwa ni sharti wakombolewe kwa sadaka ili watokane na kiapo hiko cha Bwana cha kuwa makuhani.
Na maana ya kukombolewa si kutolewa katika vifungo vya laana, kama mafundisho ya siku hizi za mwisho yanavyofundisha.
Bali ukombozi ilikiwa ni ile hali ya mtoto kutolewa katika nafasi ya kikuhani ambayo angepaswa kuitumikia maisha yake yote.
Hivyo anapokombolewa anakuwa huru kama watu wengine wasio na utumishi wa kikuhani (kwa ufupi anafunguliwa kutoka katika vifungo vya ukuhani)
Na mtoto wa kwanza asipokombolewa anabaki katika kifungo cha dhambi ya nafasi ya kikuhani.
Sasa swali je hata sasa katika agano jipya tunasheria hizo za kukomboa mzaliwa wa kwanza?.
Jibu ni la!..katika agano jipya hatuna sheria za kumkomboa mzaliwa wa kwanza au wa mwisho, kwasababu sote tuliomwamini Bwana YESU na kutakaswa kwa damu yake tunafanyika kuwa makuhani wa Bwana.
Ufunuo wa Yohana 1:6 “na kutufanya kuwa ufalme, na makuhani kwa Mungu, naye ni Baba yake; utukufu na ukuu una Yeye hata milele na milele. Amina”.
Hivyo sote tunayo huduma ya kikuhani na mbele za Mungu, na ukishakuwa tu kuhani tayari ni mzaliwa wa kwanza pasipo kujali rika…Hivyo kanisa la Kristo ni wazaliwa wa kwanza.
Waebrania 12:23 “mkutano mkuu na kanisa la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni, na Mungu mwamuzi wa watu wote, na roho za watu wenye haki waliokamilika”.
Kwahiyo hakuna sadaka yoyote ya ukombozi kwa wazaliwa wa kwanza kwa jinsi ya mwili.
Mafundisho na maombi ya kukombolewa kwa wazaliwa wa kwanza si ya kiMungu, bali ni ya ibilisi.
Ndio tunaweza kuwaombea wazaliwa wetu wa kwanza na kuwaweka wakfu kwa Bwana, dhidi ya roho zinazofuatilia, lakini si kuwakomboa….uwakomboe na nini?…je uwakomboe uwatoe katika ukuhani?…maana ndio lengo la ukombozi hilo kibiblia lililokuwepo juu ya wana wa Israeli juu ya wazaliwa wa kwanza.
Zaidi sana watoto wetu wa kwanza wanapaswa wawe wazaliwa wa kwanza kiroho kwa kumwamini YESU na kutakaswa ndipo wanapofanyika makuhani kama wengine wote waliomwamini YESU.
Mwisho, fahamu kuwa kilichowafuga wana wa Israeli ni miungu ya misri, iliyokuwa inaabimudiwa ndani ya kila kiumbe kilichokuwa cha kwanza.
Hali kadhalika vile vitu vinavyojiinua katika maisha yetu vilivyo vya kwanza ndivyo ni lazima tuwe navyo makini kwani hivyo ibilisi anaweza kuvitumia kama mlango wa kutufunga.
Je cha kwanza kwako ni nini?…je ni kazi uliyonayo?…au ni cheo ulicho nacho?..au ni uzuri au ni Bwana YESU?..
Ni heri BWANA YESU akawa wa kwanza kwako, kwani yeye ndiye njia, kweli na Uzima.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Waliouawa Shitimu kwa pigo walikuwa ni watu Elfu 23 au elfu 24?.