Category Archive maswali na majibu

Masheki ni akina nani? (Ayubu 29:10).

Swali: Masheki ni watu gani kama tusomavyo katika Ayubu 29:10?

Jibu: Turejee..

Ayubu 29:10 “Sauti yao masheki ilinyamaa, Na ndimi zao zilishikamana na makaakaa yao”.

Masheki ni jina lingine la “Wana wa wafalme”

Hivyo hapo aliposema.. “Sauti yao masheki ilinyamaa..”  ni sawa na kusema “sauti zao wana wa wafalme zilinyamaa”.

Neno hili pia tunalisoma katika..Zaburi 68:31, Zaburi 83:11 na Zaburi 105:22, na zote zina maana ile ile moja (wana wa wafalme ambao ni wakuu wa nchi).

Zaburi 68:31 “]Masheki watakuja kutoka Misri, Kushi itamnyoshea Mungu mikono yake mara”.

Je umempokea YESU Mwokozi?. na kukamilisha haki yote kwa ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU? (sawasawa na Matendo 2:38)?

Kama bado basi tengeneza mambo yako hayo kabla ule mwisho haujafika.

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Shetani alitoka wapi?

Swali: Je shetani yule audanganyaye ulimwengu alitoka wapi?


Jibu: shetani kwa asili aliumbwa na Mungu, na kabla ya kuwa shetani alikuwa akiitwa “Kerubi afunikaye”

Ezekieli 28:14 ” Wewe ulikuwa KERUBI MWENYE KUTIWA MAFUTA AFUNIKAYE; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto”.

Na MUNGU alimwumba akiwa mkamilifu (asiye na dosari) kama tu MAKERUBI wengine, lakini baadaye moyo wake uliinuka akajidanganya mwenyewe kuwa anaweza kuwa kama MUNGU (aabudiwe kama MUNGU) Na ndipo Uovu huo ukaonekana ndani yake, na hakutaka kubadilika.

Ezekieli 28:15 “Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako”

Na baadaye alipoasi ndipo akawa shetani, na maana ya shetani ni Mshitaki/Mchongezi, maana yake anawashitaki wanadamu mbele za MUNGU mchana na usiku.

Ufunuo 12:9 “Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.

10  Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana AMETUPWA CHINI MSHITAKI WA NDUGU ZETU, YEYE AWASHITAKIYE MBELE ZA MUNGU WETU, MCHANA NA USIKU”.

Kwahiyo shetani aliumbwa na MUNGU, na akaasi na  ataharibiwa na MUNGU katika ziwa la MOTO baada ya hukumu ya kile kiti cheupe.

Ufunuo 20:10 “Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele”.

Bwana atuepushe na ibilisi.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

NYOTA YA ASUBUHI.

ZIFAHAMU KAZI TATU ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA ULIMWENGU.

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Ufidhuli ni nini (2Wakorintho 12:10).

Swali: Ufidhuli ni nini kama tunavyosoma katika 2Wakorintho 12:10?


Jibu: Turejee..

2 Wakorintho 12:10 “Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na UFIDHULI, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu”

Maana ya “Ufidhuli” kama ilivyotumika hapo ni “Matukano”

Hivyo Mtume Paulo kwa ujasiri katika Roho Mtakatifu alidiriki kusema kuwa “anapendezwa na madhaifu”  katika Kristo maana yake ni kwamba pale anapojiona kuwa ni mdhaifu basi alijiona mwenye heri.

Lakini pia anapendezwa na UFIDHULI (Matukano). Yaani pale anapotukanwa kwaajili ya Kristo basi jambo hilo kwake alilipenda zaidi.

Sasa kujua kwa marefu kama ni sahihi kwa Mtume Paulo kujisifia udhaifu fungua hapa >>> Je ni sawa kuukubali udhaifu kama mtume Paulo alivyojisifia kwa huo? (2Wakorintho 12:9-10)

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya 2 Wakorintho 8:9 alikuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.

SWALI: Nini maana ya 2 Wakorintho 8:9

isemayo alikuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.

2 Wakorintho 8:9

[9]Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.


JIBU: Katika sura hii mtume Paulo anawaandikia wakorintho juu ya huduma ya utoaji kwa watakatifu walio maskini katika makanisa mengine, ya mbali

Na hapa anawasisitiza kukubali kutoa kwa kufuata kielelezo cha Kristo katika eneo la neema yake..Jinsi alivyokubali kuwa maskini, kwa kuacha enzi na utukufu na mamlaka juu mbinguni, na kuja duniani, katika hali ya chini sana (ijapokuwa hakuwa duni), ili tu atukomboe sisi tulio katika hali ya ufukara wa roho. 

Kwasababu kama asingeweza kujishusha vile, na kukubali kuhesabiwa si kitu (ijapokuwa alikuwa na nguvu), matokeo yake ni kwamba asingekwenda msalabani kusulubiwa kwa ajili yetu tena uchi, na mwisho wake kusingekuwa na  msamaha wa dhambi.

Isaya 53:3

[3]Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. 

 

Lakini sasa tumepokea neema na utajiri wote wa rohoni kupitia yeye kujishusha kwake.

 

Waefeso 1:3

[3]Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo; 

Vivyo hivyo Mtume Paulo anawahimiza  Wakorintho waige mfano huo huo, katika eneo la kuwahudumia watakatifu wengine. Akitumia mfano wa Wamakedonia ambao walikuwa ni maskini, na wenye dhiki lakini walikuwa tayari kutoa kwa moyo na furaha kwa watakatifu maskini waliokuwa Yerusalemu.

2 Wakorintho 8:1-3

[1]Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia; 

[2]maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na umaskini wao uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao. 

[3]Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao; 

Halikadhalika Bwana anataka na sisi tuhudumiane katika ufahamu wa Kristo, yaani kuwa tayari kuwasaidia watakatifu wengine hata katika hali zetu za dhiki.

Lakini mtazamo ambao si sahihi kuhusiana na vifungu hivi ni kudhani kwamba andiko hilo moja kwa moja linamaanisha  lengo la Bwana Yesu kuwa maskini duniani ni ili sisi tuwe matajiri kifedha. Ni kweli kupitia Yesu, tunabarikiwa mwilini, lakini hicho sio kinachozungumziwa hapo.  Bwana Yesu kuwa maskini ni kutupa utajiri wa roho zetu, pamoja na ule wa ulimwengu ujao.

Bwana akubariki.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)

Kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi ( 1 Wakorintho 7:14)

Nini maana ya waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo? (Matendo 11:23)

Rudi Nyumbani

Print this post

Kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi ( 1 Wakorintho 7:14)

 SWALI: Je! kulingana na mstari huu, watoto wa wapagani hawataokolewa?

1 Wakorintho 7:14

[14]Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.


JIBU: Ukianzia juu utaona andiko hilo linazungumzia juu ya wandoa wanaoishi pamoja lakini mmojawapo hajaamini. Bwana anatoa agizo kwamba ikiwa bado huyo ambaye hajaamini anaona sawa kuendelea kuishi naye, basi yule aliyeamini asimwache.

Kwasababu kwa kupitia njia hiyo, yule asiyeamini hutakaswa na yule aliyeamini Pamoja na watoto wake pia.

Lakini je mstari huo unamaanisha kuwa mwanandoa mmoja katika familia akiokoka, basi ameiponya familia yote mpaka watoto wake?

Jibu ni la! andiko hilo halikumaanisha hivyo.

Bali linamaanisha kuwa, kwa kupitia yeye, ni rahisi wao kuambukizwa imani na hatimaye kufanya uamuzi wa kuokoka.

Wokovu hauji kwa kurithishana au kwa ‘niaba-ya’ bali kwa mtu mwenyewe kufanya maamuzi binafsi mara baada ya kushawishwa na injili.

Hata sasa tumeona shuhuda nyingi watu wakiwavuta ndugu zao kwa Kristo, aidha kwa injili au mienendo yao, na hatimaye wote kugeuka.

1 Petro 3:1-2

[1]Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; 

[2]wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. 

Hivyo kwa hitimisho, watu wote, haijalishi wakubwa au wadogo, aidha wa waamini au wapagani, wote wanahitaji kumwamini Yesu ndipo waokolewe dhambi zao. Lakini hiyo huja kwa ushawishi wetu, kwa jinsi tunavyosema nao, tunavyoenenda katika mwenendo wetu mzuri, tunapozifanya nyumba zetu kuwa makao ya ibada, ni njia rahisi ya kuwashawishi.

Bwana akubariki.

Washirikishena akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

je! Paulo aliwalaani Wagalatia na Wakorintho?

UTAYAFIKIAJE MANENO SAFI YA MUNGU?

Matasa ni nini? (1Nyakati 28:17)

Rudi Nyumbani

Print this post

Ni kipawa kipi hicho tusichoweza kukisifu jinsi ipasavyo?(2Wakorintho 9:15)

SWALI: Ni kipawa kipi hicho tusichoweza kukisifu jinsi ipasavyo?

2 Wakorintho 9:15

[15]Mungu ashukuriwe kwa sababu ya kipawa chake, tusichoweza kukisifu kama ipasavyo.


 JIBU: Mungu alitupa mwana wake (Yesu Kristo), kama zawadi kwetu, ambaye anakaa ndani yetu kwa Roho wake Mtakatifu. 

Warumi 5:17

[17]Kwa maana ikiwa kwa kukosa mtu mmoja mauti ilitawala kwa sababu ya yule mmoja, zaidi sana wao wapokeao wingi wa neema, na kile kipawa cha haki, watatawala katika uzima kwa yule mmoja, Yesu Kristo. 

Yesu (kupitia Roho Mtakatifu), ni kipawa kikubwa ambacho hatuwezi kukielezea uzuri wake(kukisifu), jinsi ipasavyo.

 Ndani ya Yesu ni hakika tunapata vitu vyote (vya rohoni na mwilini)

Hivyo kulingana na vifungu hivyo ukianzia tokea juu katika sura hiyo ya tisa (9), anaegemea hasaa  katika eneo la kubarikiwa na Mungu katika baraka za mwilini. ambazo huja ndani ya kipawa hichi cha Mungu.

2 Wakorintho 9:11

[11]mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu. 

Ni kweli hatuwezi kueleza kwa maneno haya jinsi gani Yesu alivyoleta ukombozi katika maeneo mengi zaidi ya yale tunayoyadhani, si tu katika roho zetu, bali mpaka miili yetu, dunia yetu, uchumi wetu, familia zetu, magonjwa yetu, wanyama wetu, jamii yetu, ardhi zetu,  n.k. kipawa hichi kila mahali kinatibu.

Hivyo si rahisi kukisifu kwa jinsi ipasavyo. Ndio maana kwa Yesu tumetia nanga, yeye ndio utoshelevu wetu wote, hatuna haja kwa mtu mwingine yeyote zaidi yake, na ndivyo ilivyo. Hekima ya Mungu iliona hilo ndio maana hakutupa sisi wanadamu kitu kingine zaidi ya Yesu Kristo tu.

 Ashukuriwe Mungu kwa zawadi hii. Utukufu heshima na shukrani vimrudie yeye mile na milele. Amina.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Maana ya 2Wakorintho 9:11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote

Kiti cha Musa ni kipi? (Mathayo 23:2)

USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya 2Wakorintho 9:11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote

SWALI: Nini tafsiri  ya 2 Wakorintho 9:11-12

[11]mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu.


JIBU: Katika sura hii mtume Paulo analillsisitiza kanisa la Wakorintho, uthamani wa huduma ya utoaji kama njia mojawapo ya utiifu katika kuikiri wa injili (9:13).

Na hapa anaongezea kuwa Mungu hutoa utajiri katika vitu vyote (si tu vya rohoni tu, bali pia vya mwilini). Na kwamba yeye ndiye huwapa watu mbegu za kupanda na chakula.

Hivyo atutajirishapo lengo lake ni tutumie utajiri huo kwa kutenda mema (9:8), (yaani kuwapa maskini hususani watakatifu), kwasababu ndivyo ilivyokuwa kwa Kristo(9:9). Na si tutumie katika anasa na ufahari, na ubinafsi.

Ndio hapo anasema “mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote”. Na kama tukifanya hivyo, mitume wanasema shukrani zinamfikia Mungu kwa kutii kazi yao hiyo ya kutuhimiza sisi kutoa.

2 Wakorintho 9:11-12

[11]mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu. 

[12]Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu; 

Hivyo Bwana anatutaka kila atufanikishapo tujue amekusudia tuwasidie wengine walio maskini husasani watakatifu, kwasababu kwa njia hiyo shukrani nyingi humfikia Mungu.

Zaidi vifungu hivi vinasisitiza pia jinsi Mungu anavyoongeza baraka pale tunapotoa sana, akisema atoaye haba hatavuna haba,(9:6). kile tupandacho ndicho tutakachovuna kwake. 

Bwana atusaidie tuwe watoaji katika hali zote.

ubarikiwe.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> 

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

FAIDA NYINGINE MUHIMU YA KUMTOLEA MUNGU.

USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.

Mistari ya biblia kuhusu shukrani.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je ni kweli Bwana YESU hajui siku ya kuja kwake? (Mathayo 24:36)

Swali: Ni kwanini siku/saa ya kuja kwa Bwana YESU anaijua Baba peke yake na mwana haijui?, na ilihali pia YESU ni Mungu?


Jibu: Turejee..

Mathayo 24:36 “Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.”

Kipindi Bwana YESU yupo duniani, alikuwa hana budi kuwa kama wanadamu wengine, ingawa alikuwa na uungu ndani yake,  Hivyo alikuwa anahisi maumivu kama watu wengine,… alikuwa anasikia huzuni kama tu watu wengine,  na pia ilimpasa amtafute Mungu kama tu wanadamu wengine wanavyomtafuta, ndio maana alifunga na kukesha milimani kuomba kwa machozi, ili aweze kupokea mafunuo kutoka kwa Baba, kwaajili ya huduma yake na watu wake.

Waebrania 5:7 “Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu.

Hivyo Bwana YESU hakuzaliwa anajua vyote, ilimpasa ajifunze vitu.. alizaliwa hajui kutembea na hivyo ikampasa ajifunze kutembea kama watoto wengine, vile vile alizaliwa hajui kusoma na hivyo ilimpasa ajifunze kusoma na pia ajifunze torati.

Luka 2:46 “na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta.

46  Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.”

Hivyo kwa tabia hiyo ya kuendelea kujifunza, ni wazi kuwa si vyote alikuwa anavijua kipindi yupo duniani, ndio maana akasema “ile siku hata yeye haijui”

Lakini alipokufa na kufufuka, mambo yakageuka… ALIJUA YOTE!!, kwani baada ya kufufuka alisema, amepewa mamlaka yote ya mbinguni na duniani.

Mathayo 28:16 “Na wale wanafunzi kumi na mmoja wakaenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu.

17  Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka.

18  Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani”.

Sasa hawezi kupewa mamlaka yote mbinguni, halafu asijue saa ya kuja kwake, ni jambo lisilowezekana…

Kiashiria kingine kinachoonesha kuwa Bwana YESU aliijua saa  ya kurudi kwake, baada ya kufufuka ni lile neno alilomwambia  Petro kumhusu Yohana kwamba “ikiwa anataka akae hata ajapo” soma Yohana 21:22.

Soma pia Ufunuo 3:3, Ufunuo 16:15, Ufunuo 22:12, na Ufunuo 22:20.. Utaona mamlaka ya YESU kuhusiana na kurudi kwake.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Bwana YESU KRISTO sasahivi anajua kila kitu, ikiwemo siku ya kurudi kwake mara ya pili, na mwisho wa dunia (Si wa kawaida kabisa!!)

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MCHE MWORORO.

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

TUNAPASWA TUWEJE WAKATI WA KUJA KWAKE  BWANA YESU?.

Maana ya Mhubiri 10:15 Kazi yao wapumbavu huwachosha kila mmoja,

Kwanini Mungu anajifanya kama hajui mambo?

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini pawekwe MITI pale bustanini na si kitu kingine?.

Swali: Kwanini pale Edeni pawekwe MITI, isimamie uzima au Mauti na si kiti kingine kama JIWE?.


Jibu: Ijapokuwa zipo sifa nyingi za MITI zinazoipa vigezo vya kuweza kuwakilisha UZIMA au MAUTI…Lakini sifa kuu inayoweza kusimamia nafasi hiyo ni UREFU wa MAISHA.

Mti ndio kiumbe hai pekee kilichoumbwa na MWENYEZI MUNGU kinachoishi muda mrefu kuliko vyote.

Tembo ni kiumbe hai lakini miaka yake ya kuishi ni 80 tu, Kasuku ni miaka 90, kunguru ni miaka 90, kobe ni miaka 200 lakini MITI inafika mpaka miaka 2,000..

Ipo miti yenye miaka zaidi ya elfu chini ya Jua, na bado inaendelea kuzaa matunda yenye ubora ule ule, na zaidi ya yote MITI haisogei ipo palepale, lakini unaishi muda mrefu.

Tofauti na Jiwe, lenyewe Lipo kwa muda mrefu (hata miaka elfu) lakini haliishi (halina uhai), halizai wala haliongezeki liko vile vile siku zote…kama tu mifupa ya mfu iliyopo kaburini kwa mamia ya miaka.

Sasa kwa sifa hiyo ya MTI kuishi muda mrefu, ikiwa bado inaendelea kuzaa matunda yale yale na ikiwa bado ipo eneo lile lile moja..ndio inayoifanya ichukue sifa ya kusimamia UZIMA wa Daima au MAUTI ya daima.

Kwamba tunapotafakari maisha ya MTI (jinsi yalivyo marefu na usivyosogea). Hali kadhalika Mauti ya mtu aliye katika dhambi ni ya DAIMA, na hukumu yake ni ya Daima, vile vile UZIMA wa MTU aliye ndani ya MUNGU ni wa daima na usio badilika.

Sasa huu MTI wa uzima ni nini? Au upo wapi?..

MTI wa uzima ni YESU KRISTO, leo lifahamu hili, Nitakuhakikishia hilo kimaandiko.

Maandiko yanasema Kristo ndiye hekima ya MUNGU.

1 Wakorintho 1:23 “bali sisi tunamhubiri Kristo, aliyesulibiwa; kwa Wayahudi ni kikwazo, na kwa Wayunani ni upuzi;

24 bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni KRISTO, nguvu ya Mungu, na HEKIMA YA MUNGU”.

Umeona hapo?..KRISTO ni HEKIMA ya MUNGU na kama Kristo ni Hekima ya MUNGU, basi yeye ni MTI wa UZIMA kama maandiko yasemavyo katika Mithali 3:18.

Mithali 3:13 “Heri mtu yule aonaye HEKIMA, Na mtu yule apataye ufahamu……

18 Yeye ni MTI WA UZIMA kwao wamshikao sana; Ana heri kila mtu ashikamanaye naye”

Kumbe YESU KRISTO ni MTI wa UZIMA, na ana heri kila amshikaye!!!… naam si ajabu tuonapo anatajwa kama Mkuu wa Uzima (Matendo 3:15).

Si ajabu tusomapo kuwa hakuna mwingine mwenye Uzima zaidi yake yeye (Yohana 10:10) na yeye lpekee ndiye njia na Uzima (Yohana 14:6).

Si ajabu kusikia kuwa kila anayemkimbilia anapata uzima wa milele (Yohana 3:16, Yohana 6:47).

Kwaufupi hakuna UZIMA nje ya YESU KRISTO, aliyekufa na kufufuka na kupaa mbinguni, yeye ndiye MTI uishio Milele, na kwake yeye kuna Uzima.

Je unao uzima wa milele?…je umeupata huu Mti?..kama bado mkaribishe YESU maishani mwako na akufanye kiumbe kipya na ukabatizwe kwa maji tele na kwa jjina lake YESU.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

JE UMEUFIKIA ULE UTUKUFU HALISI WA MANA? 

Uzima wa milele ni nini?

MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.

CHAGUA UPANDE WA UZIMA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini mke wa Ayubu hakupitia matatizo?

SWALI: Kwanini mke wa Ayubu hakupitia matatizo?


JIBU: Ni vema kufahamu kibiblia si kila tendo au jambo lililoandikwa lina umuhimu kulijengea hoja, kana kwamba usipolijua litakupunguzia sehemu  katika roho yako. Hapana, Kwamfano maswali kama Yohana alibatizwa na nani, Au mke wa Petro aliitwa nani au kaburi la Yesu lipo wapi kwasasa,  haya hayatusaidii sana kwasababu sio fundisho au agizo tuliloamuriwa tulishike.

Lakini ikiwa ni kutanua upana wa fikra zetu, basi tunaweza jifunza mambo kadhaa kuhusu matukio kama haya mfano wa hili la  mke wa Ayubu, kutohusishwa katika majaribu.

Ni swali ambalo watu huuliza, mbona watoto wote wa Ayubu, walikufa mifugo na mali pia viliondoka, lakini hatuoni mke wa Ayubu kuguswa.

Tukumbuke kuwa hakukuwa na agizo kwamba vyote alivyonavyo Ayubu ni LAZIMA viathiriwe…Hapana. Kwani tunaona hata miongoni mwa watumwa wake wapo walionusurika kifo. Na hao waliachwa wawe kama mashahidi wa yaliyotokea.

Ayubu 1:16

[16]Huyo alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Moto wa Mungu umeanguka kutoka mbinguni na kuwateketeza kondoo, na wale watumishi, na kuwaangamiza; mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari. 

Vivyo hivyo hata katika eneo la familia ya Ayubu hwenda ilipasa  abakie shahidi wa kueleza hali ya moyoni iliyokuwa inaendelea katika nyumba hiyo.

Mke wa Ayubu anatufunulia machungu yaliyowapata kiasi cha mwanadamu wa kawaida kushindwa kuvumilia, isipokuwa tu kumkufuru Mungu. Kikawaida mpaka mtu kufikia hatua ya kutoa maneno ya matusi, na kufuru kwa muumba wake, ujue kabisa jambo lililomkuta limeijeruhi sana nafsi yake mpaka kushindwa kuvumilia.

Ni Ayubu tu peke yake ndiye aliyeweza kustahimili hivyo, hata mke wake alipomshauri alikataa. Hii ni kutuonyesha jinsi gani mtu huyu alivyo mwogopa Mungu, zaidi ya matatizo yake. Kama tusingesikia aliyoyafanya mkewe, hakika tusingejua-fika hali waliyokuwa nayo Ayubu, na nguvu aliyojaliwa hata kutoa majibu kinyume na uhalisia wa kibinadamu.

habari ya Ayubu hutupa sisi funzo kubwa la uvumilivu katika Imani. Kwasababu tunapostahimili, sikuzote mwisho wake Mungu huwa anatupa faraja kubwa zaidi ya mwanzo.

Yakobo 5:11

[11]Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma. 

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

HUJAPEWA MBAWA ZA KUKIMBIA MATATIZO

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Kuguguna maana yake nini? (Ayubu 30:3 )

Rudi Nyumbani

Print this post