Category Archive maswali na majibu

Je gharika ya Nuhu iliangamiza hadi samaki wa baharini na nyangumi?.

Jibu:  Jibu la swali hili tutalipata katika ule mstari wa 22, sura ya 7 ya kitabu cha Mwanzo…

Mwanzo 7:22 “kila kitu chenye pumzi ya roho ya uhai puani mwake kikafa, kila kilichokuwako katika nchi kavu”.

Hapo yanatajwa mambo mawili, 

 1. Kila chenye roho ya uhai puani kikafa.

Kufuatia andiko hili, ni wazi kuwa samaki hawapumui kupitia pua kwasababu wao wapo chini ya maji..

2. Pia Kila kilichokuwako katika nchi kavu.

Kupitia maneno haya ni wazi kuwa gharika haikuwahusu viumbe wa majini  au baharini, kwasababu hao hawaishi nchi kavu.

Vile vile hatusomi popote kuwa Nuhu aliingiza nyangumi, au kambale ndani ya safina, badala yake tunaona ni wanyama tu peke yao, na tena walimfuata Nuhu mwenyewe na wala Nuhu hakwenda kuwatafuta, sasa kwa mantiki hiyo nyangumi wangemfuataje Nuhu safinani?.

Kwahiyo ni wazi kuwa gharika ile ilihusu viumbe waliooishi nchi kavu, ambao ni wanadamu ndege, wanyama na wadudu.

Mwanzo 7:20 “Maji yakapata nguvu, hata ikafunikwa milima kiasi cha mikono kumi na mitano. 

21 Wakafa wote wenye mwili waendao juu ya nchi, na ndege, na wanyama wa kufugwa, na kila mnyama wa mwitu, na kila kitambaacho chenye kutambaa juu ya nchi, na kila mwanadamu”

Sasa kama ni hivyo, basi samaki walihifadhiwa wapi wakati wa gharika?

Jibu ni kwamba samaki waliendelea kubaki majini wakati wa gharika.

Lakini pamoja na hayo biblia inatabiri ujio wa gharika nyingine ambayo si ya maji tena bali ya moto, ambapo viumbe vyote vitafumuliwa na hakuna kitakachosalia..

2 Petro 3:6 “kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia. 

7 Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu. 

8 Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja. 

9 Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba. 

10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. 

11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa”.

Bwana atusaidie tukae katika mwenendo wa UTAKATIFU na UTAUWA.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NAYE AKASIMAMA JUU YA MCHANGA WA BAHARI.

NUHU WA SASA.

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

KWANINI NI NUHU, AYUBU NA DANIELI?

Makasia ni nini? (Yona 1:13).

Rudi Nyumbani

Print this post

Bwana alimaanisha nini kusema “Yeye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo”? (Mathayo 23:20)

Jibu: Ili tuweze kuelewa vizuri, turejee mistari hiyo (kuanzia ule mstari wa 16 -22).

Mathayo 23:16  “Ole wenu viongozi vipofu, ninyi msemao, Mtu atakayeapa kwa hekalu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa dhahabu ya hekalu, amejifunga.

17  Wapumbavu ninyi na vipofu; maana ni ipi iliyo kubwa, ile dhahabu, au lile hekalu liitakasalo dhahabu?

18  Tena, Mtu atakayeapa kwa madhabahu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa sadaka iliyo juu yake, amejifunga.

19  Vipofu ninyi; maana ni ipi iliyo kubwa, ile sadaka, au ile madhabahu iitakasayo sadaka?

20  Basi yeye aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hiyo, na kwa vitu vyote vilivyo juu yake.

21  Naye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo, na kwa yeye akaaye ndani yake.

22  Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa yeye aketiye juu yake”.

Shabaha kubwa ya Bwana YESU hapo si kuhalalisha VIAPO, Kwamba ni halali Mtu kuapa kwa Hekalu au kwa maadhahabu!.. La! Hiyo haikuwa shabaha yake kwani tayari alishaonya kuhusu viapo katika Mathayo 5:33-37.

Mathayo 5:33 “Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako;

34  lakini mimi nawaambia, USIAPE KABISA; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu;

35  wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa Yerusalemu, kwa maana ndio mji wa Mfalme mkuu.

36  Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi. 37  Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu”.

Na Pia Mtume Yakobo akaliandika jambo hilo hilo katika Yakobo 5:12.

Kwahiyo lengo la Bwana YESU halikuwa kuhalalisha viapo, bali ni kuonyesha UOVU na UNAFIKI wa viongozi hao wa kiyahudi (Mafarisayo na Masadukayo na waandishi) kupitia viapo vyao!. Kwamba wanavipa nguvu viapo vya sadaka Zaidi ya viapo vya Hekalu ambalo ndani yake lina Mungu na sadaka pia…Lakini wenyewe wanatazama sadaka tu!.

Maana yake ni kwamba kama Mtu ameapa kutoa sadaka (dhahabu au kitu kingine chochote) basi amejifunga (maana yake ni lazima atimize kiapo chake hicho, na asipotimiza ni dhambi kubwa)..lakini kama ameapa tu kwa kwa hekalu (labda kuabudu siku hiyo hekaluni, na asiabudu), basi sio kosa kubwa sana!!..

Ila kwa upande wa dhahabu (sadaka), ni kosa kubwa! Pasipo kuona kuwa Hekalu/Madhabahu ni kuu kuliko sadaka! Kwamba aliyeapa kwa Hekalu kaapa jambo kubwa sana kuliko yule aliyeapa kwa sadaka (dhahabu) peke yake itolewayo Hekaluni… kwasababu ndani ya Hekalu ndiko kwenye taratibu zote za matoleo, na si ndani ya matoleo ndio kwenye Hekalu…Ila Mafarisayo walikuwa hawalioni hilo, na ndio maana Bwana YESU anawaita vipofu.

Na kwanini walikuwa wamevipa hadhi kubwa viapo vya sadaka kuliko vya Hekalu??… Hakuna sababu nyingine Zaidi ya kwamba walikuwa wanapenda fedha!!!, walijua ya kwamba wakiwabana watu katika matoleo basi watanufaika Zaidi, hivyo walijali matoleo kuliko Hekalu la Mungu pamoja na madhabahu yake..

Na jambo hilo hilo utaona Bwana YESU alilirudia juu ya “vile vipasavyo kuwasaidia wazazi”..ambapo Mafarisayo walisema endapo mtu akipata chochote na kile anaweza kukifanya chote wakfu (yaani Korbani) na wala asiwape chochote wazazi, na isiwe dhambi!… jambo ambalo ni baya sana! (soma Marko 7:11).. na kwa maelezo marefu juu ya habari hiyo ya Korbani fungua hapa >>>>Neno Korbani linamaanisha nini? (Marko 7:11)

Mfano kamili wa baadhi ya viongozi wa kiimani wa leo??…. Utaona wanathamini Matoleo Zaidi ya Hekalu la Mungu na taratibu zake. Utaona mtu akiahidi kuja kanisani na asije, haiwi shida….lakini hebu mtu aahidi kutoa halafu asitoe!, inakuwa ni vita vikali na ni laana kubwa!…pasipo kujua kuwa nyumba ya Mungu ni kuu kuliko sadaka, kwasababu ndani ya nyumba ya Mungu kuna matoleo!.. (Na mtu akiiheshimu nyumba ya Mungu ataheshimu pia matoleo).

Bwana atusaidie sana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ipi tofauti kati ya matoleo na sadaka?

WEWE NI HEKALU LA MUNGU.

JE! UNA MASIKIO YANAYOSIKIA?

UJIO WA BWANA YESU.

CHACHU YA MAFARISAYO NA CHACHU YA HERODE.

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya  Yakobo 1:17 Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu,

SWALI: Naomba kufahamu tafsiri ya Yakobo 1:13-17, hususani pale anaposema “Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu”

Yakobo 1:13-17,

[13]Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu. 

[14]Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa. 

[15]Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti. 

[16]Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike. 

[17]Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka. 


JIBU: Katika hiyo mistari ya juu kabisa, tunasoma mtume Yakobo akitoa ufafanuzi wa mawazo ya watu kuhusu Mungu ambayo sio sahihi. Wakidhani kuwa majaribu yampatayo mtu hutolewa na Mungu, kwasababu chanzo chake ni Mungu.

Chukulia mfano labda mpendwa kabarikiwa na Mungu kwa shamba la mizabibu, likawa linasitawi sana, hata kumfanya afungue kiwanda chake cha juisi na kuuza na kupata faida nyingi..Sasa baada muda fulani watu wakamfuata na kuulizia bidhaa ya mvinyo, mwanzoni alikataa, lakini baadaye alipopiga hesabu na kuona faida itakuja mara nne,.akaingiwa na tamaa akaanza kutengeneza divai akauza na yeye mwenyewe akaanza kuwa mlevi, hatimaye maisha yake ya wokovu yakaporomoka akawa amekufa kabisa kiroho. Mwishowe akaanza kumlaumu Mungu amemletea jaribu la kumpa shamba la mzabibu na kumbariki sana, ndio maana akawa mlevu.  Sasa mtu wa jinsi hii Mtume Yakobo anasema asiseme amejaribiwa na Mungu.

Ni sawa na tamaa za mwili,.Mungu aliziweka mahususi kwa ajili ya furaha ya wanandoa lakini imebadilika na kuwa uzinzi, na watu hutumia kisingizio kuwa Mungu ameziweka kama jaribu kwao. kumbe Mungu alichowapa ni chema isipokuwa wao wenyewe wamekigeuza kuwa uovu.

ndo maana sasa ya vifungu vinavyofuata vinasema. “kila kutoa kuliko kwema na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu. Kwa lugha rahisi anamaanisha chochote kitolewacho kilicho chema hutoka kwa Mungu, lakini tu sio kilicho chema bali pia chochote kilicho kikamilifu, hutoka juu kwa Baba yetu.

Mungu sikuzote hutupa sisi vitu vizuri. Na si vizuri tu bali pia vilivyo vikamilifu hutoka kwake. tujengwe na tufurahie, isipokuwa sisi huvipindua na kuvitumia kwa tamaa zetu. 

Pesa ni kitu kizuri, chakula ni kitu kizuri, usingizi ni kitu kizuri, ndoa ni kitu kizuri, kazi ni kitu kizuri, muziki ni kitu chema.

Lakini watu wanapovitumia kinyume ndio huzaa uzinzi, anasa, ulevi, uvivu, ufisadi.n.k.

Vitu vyote vyema vimetoka kwa Mungu na hajatupa ili kutujaribu..anaendelea kusema..

“hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka”. 

Baba wa mianga, akijifananisha na jua ambalo huangaza kotekote, isipokuwa yeye amelizidi jua, hana misimu wala majira ya kuangaza, yeye wakati wote hutoa vilivyo vyema, hifadhili majira yote kwa watu wake.

Hata leo, uonapo Mungu amekupa kitu chema, halafu baadaye kikakuletea matatizo makubwa.. Tafakari hapo kuna mahali ulimpa nafasi shetani kukujaribu. Kwasababu Mungu hawezi kumpa mtu jiwe aliyemwomba mkate.

“kila kutoa kuliko kwema na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu.

Ubarikiwe.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

YAFAHAMU MAPENZI KAMILI YA MUNGU KWA MAADUI ZAKO.

EPUKA KUTOA UDHURU.

SI KILA KILICHO HALALI KINAFAA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Yakobo 1:5 inasema tuombapo hekima, Mungu hakemei, maana yake ni nini.

SWALI: Katika Yakobo 1:5 inasema tuombapo Mungu hakemei, maana yake ni nini.


JIBU:

Yakobo 1:5

[5]Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa. 

Kabla ya kuona maana hilo neno “wala hakemei naye atapewa”. Tuone kwanza tafsiri ya kifungu chote.

Hapa mtume Yakobo kwa uongozo wa Roho, anandika juu ya suluhisho la kupungukiwa kwa jambo muhimu sana ndani ya mwanadamu. Nalo ni Hekima.

Haandiki ikiwa mtu amepungukiwa na mali, au na umaarifu au na fursa, au watoto…hapana bali na hekima, na aombe dua.

Lakini hekima aisemayo sio hekima ya duniani, bali hekima ya ki- Mungu. Ambayo ni ufahamu wa Ki-Mungu unaoingia moyoni mwa mtu kumsaidia aweze kupambanua vema mambo yote, katika ufasaha wote ili kuleta matokeo aliyoyatarajia.

Hivyo sisi wote tunaihitaji hekima katika yote tuyatendayo. Vinginevyo hatutaweza kuzalisha chochote. 

Lakini bado anatoa kanuni ya kuipata, hasemi tukae chini tuwaze, au tukahubiri, au tukatoe sadaka, au tuende kwenye shule za biblia. Hapana anasema na tuombe dua kwa Mungu.

Tunaipata kwa kuomba. Kwa kuchukua muda kupiga magoti na kuomba. Sio kuomba dakika mbili, na kusema Amen au yale maombi ya kumalizia siku unapokwenda kulala. Hapana bali ni maombi yaliyochanganyikana na kiu ya dhati kupata hekima ya Ki-Mungu katika eneo fulani, unalotaka Bwana akusaidie.

Vilevile hatupaswi kuomba bila dira. Kwamfano kusema.. “Mungu naomba unipe hekima”.. Hapana tunaomba tukielekeza eneo ambalo tunataka Bwana atusaidie kupata hiyo hekima ya kupambanua.

Kwamfano hekima katika kuyaelewa maandiko, hekima katika kuhubiri, hekima katika kufundisha, katika kuombea wagonjwa, katika kufanya biashara, katika kuimba. n.k.

Na hapo ndipo Mungu mwenyewe anaongeza ufahamu wake juu ya hicho unachokiomba na hatimaye utaona tu, mabadiliko, au njia ya kitu hicho unachotaka akusaidie.

Sasa tukirudi kwenye swali, pale anaposema

“awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa”

Maana yake, kwasababu Mungu ana ukarimu, basi hachagui wa kumpa, anawapa wote. Hii ahadi yake kuwa kila aombaye humpa. Haleluya.

Na tena anasema “hakemei”. Tofauti na sisi wanadamu

Kwamfano sisi tuwafuatapo wazazi wetu na kuwaomba kitu, wakati mwingine, hutugombeza, au huwa wakali, au kutaka utoe kwanza hesabu ya kile cha nyuma ulikitumiaje, kabla ya kukupa hichi kingine. Na ndio maana ulikuwa na hofu, kujifikiria mara mbili mbili hicho unachotaka kwenda kuomba, ukiulizwa hivi, ujibu vipi. Sio tu kwa wazazi, lakini kwa wanadamu wote, sifa hiyo wanayo tuwafuatapo kuwaomba kitu, si kivyepesi vyepesi kama tunavyodhani.

Lakini kwa Mungu wetu sio, hakemei, haangaali ya nyuma kukushutumu, hakuuliza makosa yako. Anakupa tu, bila sharti lolote.

Ni furaha iliyoje. Mimi na wewe tuliomwamini tunapokwenda kumwomba Mungu hekima, hatushutumiwi kwa lolote, au kwa madhaifu yetu. Bali kinachohitajika tu ni kumwamini  yeye asilimia mia, bila kutia shaka katika hilo unaloomba, kwasababu ukitia shaka, maombi hayo hayaendi kwake bali kwa mungu mwingine asiyeweza yote. 

ndio maana anataka tumfuatapo tusiwe na shaka ya kutojibiwa, ili maombi yetu yafike kwake kwelikweli, yeye aliyemweza wa yote.

Anasema hivyo katika vifungu vya mbeleni.

Yakobo 1:6-8

[6]Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.

[7]Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.

[8]Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote. 

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je Elisha alimdanganya Ben-hadadi kuwa hatakufa kwa ugonjwa wake?

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI

IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Ayubu alimaanisha nini kusema ‘nami nitarudi tena huko uchi vilevile;?

SWALI: Ayubu alimaanisha nini kusema..Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; Aliwezaje kurudi tena tumboni mwa mama yake tena uchi je hilo jambo linawezekana?


JIBU: Kauli hiyo aliisema Ayubu baada ya kupotelewa na familia yake na mali zake. Lakini Kwa ujasiri akamtukuza Mungu katika hali hiyo pia, kwa kusema maneno hayo; 

Ayubu 1:21

[21]akasema, Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA na libarikiwe. 

Lakini swali lipo hapo, katika kurudi tumboni mwa mama yake uchi. maana yake ni nini?

Ikumbukwe kuwa sisi hatukutoka tu  katika tumbo la wanamke bali pia katika tumbo la ardhi, hiyo ndio mama wa ulimwengu. yaani mama wetu wa kwanza.

soma; 

Zaburi 139:15

[15]Mifupa yangu haikusitirika kwako, 

Nilipoumbwa kwa siri, Nilipoungwa kwa ustadi pande za chini za nchi; 

Mhubiri 12:7

[7]Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, 

Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa. 

Hivyo Ayubu aliposema nami nitarudi tena huko huko hakumaanisha mama yake mzazi, bali mama wa ulimwengu wote yaani ardhi.

Na ndivyo ilivyo kwa kila mmoja wetu, hukuja na kitu, utaondoka bila kitu chochote. Ukiwa uchi vilevile.

lakini jambo lingine la kufahamu kuwa, wale walio ndani ya Kristo, wafikapo kule ng’ambo hawataonekana uchi, bali watapewa vazi jipya la rohoni la Kristo Yesu, ndio ile miili mipya ya utukufu isiyoona uharibifu idumuyo milele.

2 Wakorintho 5:1-3

[1]Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele mbinguni. 

[2]Maana katika nyumba hii twaugua, tukitamani sana kuvikwa kao letu litokalo mbinguni; 

[3]ikiwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tu uchi. 

Swali ni je! Umeandaliwa vazi lako baada ya kuondoka?

Kumbuka unalipokea kwa kumwamini Yesu Kristo leo, okoka tubu dhambi zako, ubatizwe, kisha upokee kipawa cha Roho Mtakatifu. vazi lako liwe limekamilika., ili siku ile usionekane uchi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

SIFA ZA MAMBA YULE MKUBWA WA AYUBU.

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MFUNGO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je Daudi aliwachukia viwete na vipofu? (2Samweli 5:6-9)

SWALI: Je Daudi aliwachukia viwete na vipofu? Kama tunavyosoma katika 2Samweli 5:6-9. Je! habari hiyo tunaielewaje?


JIBU:

2 Samweli 5:6-9

[6]Kisha mfalme na watu wake wakaenda Yerusalemu ili kupigana na Wayebusi, wenyeji wa nchi ile; hao ndio waliomwambia Daudi, wakisema, Usipowaondoa vipofu, na viwete, hutaingia humu kamwe; huku wakidhania ya kuwa Daudi hawezi kuingia humo.

[7]Lakini Daudi aliipiga ngome ya Sayuni; huu ndio mji wa Daudi.

[8]Naye Daudi alisema siku hiyo, Yeye atakayewapiga Wayebusi, na apande kwenye mfereji wa maji, na kuwapiga viwete, na hao vipofu, ambao roho yake Daudi inawachukia. Kwa sababu hii watu husema, Wako vipofu na viwete hawawezi kuingia nyumbani.

[9]Basi Daudi akakaa ndani ya ngome hiyo, akaiita mji wa Daudi. Kisha Daudi akajenga toka Milo na pande za ndani.

Habari hii inazungumzia wakati ule ambao Daudi alikwenda kuiteka Yerusalemu na kuufanya kuwa mji wa Mungu.

Alipofika na kukutana na wenyeji wa mji huo, walimdharau na kumsema kimafumbo kwa kauli ya mzaha kumwambia “Usipowaondoa vipofu, na viwete, hutaingia humu kamwe;”

Wakiwa na maana vita yake ni ya kupambanishwa na watu dhaifu kabisa wa mji, mfano wa vipofu na viwete, hao ndio apambane nao, lakini sio majemedari wa nchi ile. Akiweza hao walau ndio aingie sasa kujaribu kuuteka, huku wakijua kuwa hata hilo Daudi hataweza kwasababu walimwona ni dhaifu.

Na ukweli wakati huo Daudi hakuwa na nguvu yoyote, kwasababu ndio kwanza ametoka kuupokea ufalme. Hawakujua kuwa nguvu zake tangu zamani zina Mungu, ndio zile zilizomwangusha Goliathi ni silaha zake kwa jiwe moja.

Lakini Daudi aliipowafuatia na kuwapiga, na kuwaangamiza, naye alitumia pia jina hilo hilo la vipofu na viwete kimizaha akiwaita wayebusi waliomwonyeshea dharau..pamoja na hilo Daudi alionyesha kuwachia sana.

Lakini mistari hiyo hakumaanisha kuwa anawachukia viwete na vipofu. Hapana Kama ingekuwa hivyo asingemkaribisha Mefiboshethi mtoto wa Yonathani katika nyumba yake ya kifalme kuketi mezani pake daima..(2Samweli 9). Na ikumbukwe kuwa Daudi alikuwa anamcha Mungu na kuwakumbuka sana wanyonge.

Lakini pale inaposema….

“Kwa sababu hii watu husema, Wako vipofu na viwete hawawezi kuingia nyumbani”.

Ni kwamba kufuatana na Daudi kuwasema viwete na vipofu akiwarejea wayebusi, ukazuka msemo huo, ‘vipofu na viwete hawana ruhusu kuingia nyumbani mwa Mungu;. Lakini haikuwa hivyo’..

Misemo na namna hii ilikuwepo tangu zamani hata kuhusu ile habari ya mfalme Sauli, ya kutabiri (1Samweli 19:24), na kuhusu ike habari za mtume Yohana, pale wale mitume wengine waliposikia Kauli ya Bwana Yesu inayosema ikiwa nataka huyu awepo mpaka nijapo, wakadhani kuwa Yohana hata onja mauti kamwe, mpaka Yesu atakaporudi kumbe hawakumuelewa Bwana Yesu, hakumaanisha vile.(Yohana 21:22-23)

Na ndivyo ilivyodhaniwa kwa Daudi kwamba anawachukia vipofu na viwete, kumbe aliwamaanisha wayebusi.

Lakini ni nini hasaa tunaweza jifunza..katika tukio hilo?

Ni kawaida ya adui yetu anapokaribia kushindwa hunyanyua ujasiri wake kwa kiwango cha juu sana. Mji ambao uligeuzwa kuwa wa Bwana, na mwema kuliko yote, ulitanguliwa na dhihaka nyingi za kukatisha tamaa. Hata ukuta aliokuwa anaujenga Nehemia, ambao sehemu yake iliendelea kudumu kwa mamia ya miaka mbeleni ulitanguliwa na dhihaka nyingi za kuvunjishwa moyo. wakisema hata mbweha akipita juu yake utaanguka.

Silaha hiyo hiyo anaitumia adui leo, unapoona maono makubwa ya kuitenda kazi ya Bwana ndani yetu, vitisho vya adui huanzia hapo, aah wewe huna upako, wewe huwezi kuhubiri, huna pesa, huna elimu ya kukutosha, huna uzoefu, utafungwa..hizo zote ni dhihaka, Daudi alishazitambua toka kwa Goliathi, ndio maana akawashinda wayebusi.

Hivyo ni kusimama imara kuitetea injili, kwa imani tukijua hakuna linaloshindikana kwake yeye aaminiye. Na palipo na dhihaka nyingi ndipo palipo na mafanikio makubwa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Wayebusi walikuwa ni watu gani?

Hanithi ni nini katika biblia? (kumbukumbu 23:17)

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

Rudi Nyumbani

Print this post

Kusanyiko la makini/ mkutano wa makini ni upi?

Katika agano la kale, Israeli walikuwa na makusanyiko mengi, ambapo walikutanika kumfanyia Mungu ibada, na kuzishika sikukuu. Lakini pia yalichaguliwa makusanyiko mengine yaliyoitwa mikutano/makusanyiko ya makini. Makusanyiko haya yalifanyika  katika siku ya saba ya sikukuu ya Pasaka, na siku ya nane, baada ya sikukuu ya vibanda. Katika siku hiyo hawakuruhusiwa kufanya kazi yoyote. Bali ilitengwa kwa ajili ya kujitakasa, au kujisogeza karibu na Mungu,

Hivi ni vifungu baadhi vinavyoielezea siku hiyo;

Hesabu 29:35 Tena siku ya nane mtakuwa na kusanyiko la makini sana; hamtafanya kazi yo yote ya utumishi;

36 lakini mtasongeza sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kusongezwa kwa moto, harufu ya kupendeza kwa Bwana; ng’ombe mume mmoja, na kondoo mume mmoja, na wana-kondoo waume wa mwaka wa kwanza wakamilifu saba.

Walawi 23:34 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Siku ya kumi na tano ya mwezi huo wa saba ni sikukuu ya vibanda muda wa siku saba kwa Bwana.

35 Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu; msifanye kazi yo yote ya utumishi.

36 Mtamsongezea Bwana sadaka kwa moto siku saba; siku ya nane kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka kwa moto; ni mkutano wa makini huu; msifanye kazi yo yote ya utumishi

Kumbukumbu 16:8 Siku sita utakula mikate isiyotiwa chachu; na siku ya saba na uwe mkutano mtukufu kwa Bwana, Mungu wako, usifanye kazi yo yote.

Huo mkutano mtukufu ndio kusanyiko la makini.

Hekalu la kwanza pia lilipomalizika liliwekwa wakfu katika siku hii ya kusanyiko la makini

2Nyakati 7:9 Hata siku ya nane wakaita kusanyiko la makini; kwa maana walishika kuitakasa madhabahu siku saba, na sikukuu siku saba.

Sehemu  nyingine mikusanyiko hii iliitishwa rasmi, kwa lengo la kujimimina kwa Mungu kuomba, kwa ajili ya maovu na majanga ambayo yanaipata nchi. (Yoeli 1:14 – 2:15). Kusanyiko hili liliitwa pia kama kusanyiko  kuu.

Je! Ufunuo wake ni upi leo?

Kama vile tulivyo na mikusanyiko ya aina mbalimbali leo, mfano  ya shule ya jumapili, ya semina, ya injili n.k. Vivyo hivyo hatuna budi kuwa na makusanyiko ya makini. Ambayo ni mikusanyiko ya mifungo na maombi. Ambapo tunapata muda wa kujimimina kwa undani kabisa uweponi mwa Mungu, kumtaka aingilie kati mambo yetu.

Je! unaithamini? Mungu aliyesema tusiache kukusanyika pamoja (Waebrania 10:25). Hakumaanisha tu mikusanyiko ya jumapili, lakini pia ya mifungo na maombi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.

SWALI: 2Timotheo 3:7, ina maana gani inaposema;

wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.


JIBU: Katika kitabu cha 2Timotheo sura ya tatu(3), kuanzia mstari 1-9. Kinaeleza sifa za watu watakaozuka katika siku za mwisho.  Tabia ambazo hapo mwanzo hazikuwepo. Sasa ukisoma pale utaona zimeorodheshwa baadhi ikiwemo kutokea watu wenye kupenda fedha, watu wakali, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu,..na nyinginezo

Lakini ipo sifa nyingine inatajwa pale, kuwa litazuka kundi la watu wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake..ndio hao ambao anaeleza sasa mbeleni, wanajifunza sikuzote ila wasiweze kuufikia ujuzi wa kweli.

Tusome;

2 Timotheo 3:5-9

[5]wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao.

[6]Kwa maana katika hao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu, na kuchukua mateka wanawake wajinga wenye mizigo ya dhambi, waliochukuliwa na tamaa za namna nyingi;

[7]wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.

[8]Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani.

[9]Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa dhahiri.

Maana ya ujuzi;

Ujuzi maana yake ni ufanisi au kukifanya kitu kwa utashi wote. Mtu anaweza akafanya jambo lakini akiwa hana ujuzi nalo litakuwa ni kituko kama sio hasara kabisa. Kwamfano mtu atasema, mimi naweza kujenga (na hajasomea ujenzi). Hivyo akaenda kununua tofali na kuanza kupandisha, unajua ni nini kitamkuta? kwasababu hajui kanuni za ujenzi anaenda  kufanana na yule mtu aliyejenga nyumba yake juu ya machanga.

Ndivyo ilivyokuwa kwa hawa watu, hawakuufikia huo ujuzi wa kweli, kwasababu walikuwa na nia zao wenyewe za tofauti na sio ya Kristo, walilenga kuwakusanya wanawake waliokuwa na mizigo ya dhambi, kama daraja lao, na hifadhi yao ya kihuduma, ili watumize malengo yao. Sasa Kwa urefu wa tabia za wanawake hao bofya link hii  uwasome >>> Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?

Lakini huo ujuzi wa kweli ni upi?

ujuzi wa kweli ni UTAUWA/ UTAKATIFU. Mtu anayefikia kilele cha kuifahamu kweli ya Kristo huishia katika utakatifu wa kweli. Tunalisoma hilo katika;

Tito 1:1

[1]Paulo, mtumwa wa Mungu, na mtume wa Yesu Kristo; kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu, na ‘ujuzi wa kweli’ ile iletayo utauwa;

Umeona ujuzi wa kweli, lazima ulete utauwa.

Lakini watu hawa walikuwa na mfano wa utauwa lakini walizikana nguvu zake kimatendo, ndio maana hawakufikia..waliitwa wakristo lakini wakristo jina, waliitwa mitume, wainjilisti, manabii, waalimu, watakatifu, lakini nia zao zipo penginepo. Walikuwa na elimu za vyuoni, wanajua kuyachambua maandiko, na vifungu vyote, lakini maisha ya utakatifu yapo mbali na wao.

Ndilo linalotendeka leo hii, maarifa tuliyonayo kuhusu Mungu ni mengi, zaidi hata watu wa kale, tuna wingi wa vyuo vya theolojia, na makanisa, na mafudisho mengi. Lakini maisha ya wengi hayamwakisi Kristo katika utakatifu wa kweli.

ndio hili neno linatimia,

wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli

Ni swali la kujiuliza na sisi, je! wokovu wetu umefikia ujuzi wa kweli? Kumbuka hizi ni siku za mwisho, mafundisho uliyonayo yanakusukuma kwenye nini? FUATA UTAKATIFU.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

MWE NA HASIRA, ILA MSITENDE DHAMBI.

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mathayo 6:34 ‘Yatosha kwa siku maovu yake’ 

SWALI: Bwana Yesu alikuwa anamaanisha nini kusema.. “Yatosha kwa siku maovu yake”.

Mathayo 6:34

[34]Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.


JIBU: Bwana, hataki tuwe na hofu ya vitu vya huko mbeleni (ambavyo bado havijafikiwa), si mpango wa Mungu tubebe mizigo mingi kwa wakati mmoja, kwasababu hatujaumbiwa asili hiyo, ndio maana hata katika ile sala ya Bwana tunasema; utupe “siku kwa siku” rikizi yetu.

Hasemi utupe riziki ya “mwaka mzima” kana kwamba tukikosa vyote leo hatutaishi.. bali siku kwa siku..

Kwanini iwe hivyo?

Sasa katika hali yetu ya kibinadamu tunajua kabisa mihangaiko yetu, taabu zetu, shughuli zetu za kila siku, mara nyingi huwa haziwi safi kama tunavyotarajia, wakati mwingine kama sio kujikwaa, basi tunakutana na mambo mengi pia ya kukosesha yasiyompendeza Mungu. Hayo ndio maovu yake.

Tunakutana na watukanaji, na wazinzi, na waharibifu, wenye mizaha, wasumbufu, n.k. hivyo kiuhalisia katika mambo yetu mema, maovu pia hutokea. Hivyo kitendo cha kuyataabikia sana ya mbeleni, tafsiri yake ni kuwa tunayaleta na maovu yake pia leo. Na matokeo yake tutalemewa na maovu kichwani Na kujikuta tunamkosea Mungu.

Bwana anataka tupambane kwanza na yale ya leo, ya kesho tutapewa nguvu ya kushindana nayo. Kwa tafsiri nyingine ikiwa wewe ni wa kubeba mambo mengi ya mbeleni, dhambi itakulemea na kukushinda.

Yatosha kwa siku maovu yake.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni kwa jinsi gani Mungu anapatiliza maovu ya baba zetu sawasawa na Kutoka 20:5-6?

Nilikuwa naomba kujua utofauti kati ya DHAMBI, UOVU na KOSA kibiblia.asante!!

HAMJAFAHAMU BADO?

Rudi Nyumbani

Print this post

Munyu ni nini? (Wakolosai4:6).

Jibu: Turejee..

Wakolosai 4:6 “Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea MUNYU, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu”.

“Munyu” ni kiswahili kingine cha “chumvi”. Neno hili limeonekana mara moja tu katika biblia..

Hivyo hapo maandiko hayo yanaweza kusomeka hivi…

“Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea CHUMVI, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu”.

Sasa swali; Maneno yaliyokolea Munyu/chumvi ndio maneno gani?.

Kabla ya kuyaangalia haya maneno hebu tujifunze matumizi ya chumvi.

Mbali na kwamba chumvi ni kiungo cha kuongeza ladha ya chakula, lakini pia ilitumika kwaajili ya kuhifadhia vitu ili visiharibike.

Enzi za zamani hakukuwa na friji kama tulizo nazo sasa, hivyo kitu pekee kilichotumika kuhifadhia chakula ambacho hakijapikwa ilikuwa ni chumvi?.

Kwahiyo chakula kilichotiwa chumvi kilidumu muda mrefu, na kitu kingine chochote..

Soma zaidi kuhusu Agano la chumvi hapa》》Agano la Chumvi ni nini? (2Nyakati 13:5)

Sasa tukirudi katika “maneno” ni hivyo hivyo… “maneno yaliyokolea chumvi/munyu” mbali na kwamba ni maneno yaliyokolea ladha za kiroho..Lakini pia ni “maneno yenye kidumu muda mrefu”…yasiyopita!

Ni maneno yenye kidumu si mengine zaidi ya yale yenye kutangaza habari za uzima wa milele.

Ni maneno yenye kutangaza tumaini lililopo ndani ya YESU..maneno yenye kumpa mtu hamasa ya kumtumikia Mungu ili awe na nafasi katika ule mji mtakatifu..

Ni maneno yote yaliyonenwa na YESU mwenyewe…

Mathayo 24:35 “Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”.

Lakini maneno yasiyo na munyu ni yale yote yenye kunia na kutukuza mambo ya duniani ambayo yapo leo na kesho hayapo..

Yakobo 4:13 “Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida; 

14 walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka”.

Bwana atusaidie maneno yetu yakolee munyu daima.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

IMANI YENYE MATENDO

Agano la Chumvi ni nini? (2Nyakati 13:5)

Ninyi ni chumvi ya dunia, Andiko hilo lina maana gani?

HAMJAFAHAMU BADO?

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani

Print this post