SWALI: Nini maana ya Yeremia 31:30 “Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi”.
JIBU: Zamani za agano la kale katika taifa la Israeli, kulikuwa na usemi maarufu, unaosema “Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi”.
Kikawaida zabibu au matunda mengine yenye asidi nyingi mtu alapo , huwa meno yanatia ganzi, lakini kamwe haiwezekani mtu mwingine akatiwa ganzi kwa ulaji wa mwingine.
Hapa Waisraeli wakiwa wanamaanisha kuwa adhabu za Mungu huwa zinatembea hata kwa kizazi cha watu, Lakini Mungu kwa kinywa cha Yeremia anawasahihisha kuwa hilo si jambo lake..Anawaambia kila mtu ataadhibiwa sawasawa na uovu wake, wala watoto hawatauchukua uovu wa wazazi wao..Jambo ambalo alilirudia pia kwa kinywa cha Nabii Ezekieli (Ezekieli 18:20).
Lakini pia ukisoma muktadha wa vifungu hivyo, utaona anatoa unabii wa agano jipya ambalo atalifanya na watu wake kupitia Yesu Kristo, akimaanisha kuwa wokovu wake pia , utakuwa ni wa mtu binafsi, mmoja mmoja. Tusome habari yote tokea juu.
Yeremia 31: 27 Tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapoipanda nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda, mbegu ya mwanadamu na mbegu ya mnyama. 28 Tena itakuwa, kwa kadiri nilivyowaangalia, ili kung’oa, na kubomoa, na kuangusha, na kuangamiza, na kutesa; kwa kadiri iyo hiyo nitawaangalia, ili kujenga, na kupanda, asema Bwana. 29 Siku zile, hawatasema tena, Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi. 30 Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi. 31 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda. 32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana. 33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
Hivyo vifungu hivi, vinatupa kutambua kuwa wajibu wa kulitunza agano la Mungu ni la mtu binafsi, sawasawa na alivyokuja kulifunua katika agano jipya kupitia Yesu Kristo, kwamba ijapokuwa wokovu umeachiliwa kwa wote, lakini haupokelewi kijumuiya, kifamilia, au kikabila, bali kibinafsi.
Kila mtu atalibeba furushi lake mwenyewe. (Wagalatia 6:5)
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tafsiri ya Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.
Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?
Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?
Print this post
SWALI: Je! Ni sahihi kwa mkristo kujifunza, au kufundishwa na AI (Artificial Inteligence), mfano wa Chatgpt, deepseek n.k.
JIBU: Ili kujibu swali hili ni vema, kutambua mashine hizi za akili bandia (AI), zinafanya kazi gani.
Kwa ufupi ni kuwa AI, inafanya kazi ya kuchakata taarifa nyingi, kutoka katika vyanzo vingi vilivyopo mitandaoni, mfano vitabu, makala, sauti, machapisho n.k, na hivyo inazichanganya taarifa hizo zote kwa kuangalia muktadha unaofanana na kuzifupisha, na kukujibu.
Hivyo kimsingi, ni chombo ambacho kinatoa msaada mkubwa katika ulimwengu wa sasa, na ndio ukweli usiopingika..Kwasababu kinarahisisha utafutaji wa taarifa. Lakini pamoja na hayo haimaanishi kuwa kinatoa kwa ufasaha wote.
Sasa tukija kwenye eneo la kiroho. Je ni vema mkristo kwenda kuuliza AI, au kuandaa maombi au masomo kupitia hiyo, n.k.
Ukweli ni kwamba Imani, sio taarifa, ni zaidi ya taarifa.. Hizi AI, zinatoa tu taarifa lakini hazitoi mafunuo. Hazina pumzi ya Roho Mtakatifu ndani yake.
Ikiwa unataka kuongeza maarifa kwa sehemu fulani zinaweza kukusaidia, lakini sio kukujenga nafsi, kwani inahitaji pumzi ya Mungu na miongozo ya Mungu wewe kujengwa nafsi, na sio taarifa.
Kwamfano ikiwa wewe ni mchungaji halafu, kila inapokaribia jumapili unachowaza ni kwenda chatgpt, kuiambia ikuandalie somo la kufundisha jumapili, ndugu hapo hesabu kuwa umepotea kama sio kukengeuka… Tumia hiyo kwenye biashara zako, masomo yako, projekti zao lakini sio kwenye mambo ya kiroho. Hilo liepuke kabisa.
Kufundisha Neno inahitaji ‘Neno’ mwenyewe (Yesu) akae ndani yako, kwasababu ni UHAI sio taarifa (Waebrania 4:12) ndio hapo itakupasa kupiga magoti kwanza uombe, kwa muda mrefu, utafakari moyoni mwako, ukae kwenye utulivu wa kutosha, ndipo Mungu alipande somo lake moyoni mwako. Ambalo yeye mwenyewe anajua litakuwenda kuwagusa vipi watu wake, wenye changamoto mbalimbali, kwamfano, pengine mtu mmoja alikuwa anakaribia kwenda kujinyonga kwasababu ya ugumu wa maisha na mateso fulani, na Mungu kamwona anataka amsaidie, kwa kuliweka somo linalohusiana na mapito ya Ayubu ili ainuliwe imani. Kinyume chake kwasababu ya uvivu wako wewe unakwenda kuiambia chatgpt (akili bandia), ikuandalie somo. Halafu jumapili utakwenda na taarifa zao sio mafunuo. Badala uokoe roho inayokwenda kujinyonga, unaiambia, “leo tunajifunza kanuni kumi za kudumisha ndoa na mahusiano kibiblia”. Hapo unafanya nini sasa?
Au Neno fulani Bwana anataka kukupa la wakati wako, sasa ikiwa unakimbilia AI ikusaidie, hutaki kuchukua muda wako binafsi kutafakari na kuomba ‘jiandae kukutana na ukame wa kiroho.
Visaidizi hivi, hatupaswi kuvifanya ndio sehemu ya imani yetu, kwamba kila kitu tutegemee kule, hivi ni tone dogo sana kati ya bahari kubwa. Roho Mtakatifu alishatuandalia njia zake, kuu za kujengwa na yeye.
Wekeza zaidi, kuomba msaada kwa wakufunzi wako, viongozi wako, ndugu zako katika Kristo, wekeza katika maombi, mifungo, tafakari, na kujisomea mwenyewe Neno. kwa njia hizi hakika Bwana atasema nawe na kujengwa zaidi kuliko visaidizi. Lakini pia ikiwa pana umuhimu wa kujiongezea taarifa kwa vile unavyovijua, visaidizi hivi vitakufaa (Katika uangalizi maalumu), vinginevyo utajidumaza kiroho.
Karismatiki ni nini?
Uinjilisti kama agizo kuu la Bwana.
Vita vya kiroho, na mwamini Mpya.
WhatsApp
Kama mwamini ni lazima ujue kila kitakachotekea siku za mwisho, na kile Mungu alichokiahidi kuhusu maisha yajayo
Siku za mwisho zilianza wakati ule wa pentekoste Roho alipomiminwa duniani, kwa watu wote, na hizo zinaendelea hadi sasa mpaka wakati ambapo Kristo atatokea ulimwengu kwa mara ya pili kuleta hukumu na ufalme wake mpya.
Ni ukweli usiopingika kwamba tupo ukiongoni kabisa mwa siku za mwisho.Ingawa Biblia haitupi tarehe kamili (Mathayo 24:36), inatupa ishara na maagizo ya kuwa macho na wenye tumaini wa siku hiyo kuu.
Hii inaonyesha kwamba historia inaelekea kwenye mwisho ulioamriwa na Mungu.
Yesu aliahidi atarudi tena (Yohana 14:3). Kurudi kwake hakutakuwa kwa siri, bali kutakuwa kwa utukufu, nguvu na hukumu.
[11]Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni. . — Matendo 1:11
Hili si tumaini la kubahatisha — ni matumaini ya hakika yaliyowekwa juu ya ahadi za Mungu.
“Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu.” — Wakolosai 1:27
Kimaandiko, utukufu humaanisha:
Uwepo wa Mungu unaoonekana (Kutoka 33:18-20)
Utakatifu wake ulio mkuu na mkamilifu (Isaya 6:3)
Hali ya mwisho ya waamini — kufanana na Kristo milele (Warumi 8:17; 2 Wakorintho 3:18)
1 Wakorintho 15:52 [52]kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.
Hakutakuwa na ugonjwa, uchovu, wala mauti tena. Tutakuwa na miili kama wa Yesu baada ya kufufuka kwake (Wafilipi 3:20-21).
ii) Makao ya Milele
Yesu amekwenda kutuandalia makao (Yohana 14:2). Mbingu mpya na dunia mpya hazitakuwa na huzuni, machozi wala laana (Ufunuo 21:1-5).
iv) . Kumwona Mungu Uso kwa Uso
Hatutamtazama tena kwa imani bali tutamwona moja kwa moja (Ufunuo 22:4). Tutamtumikia na kumtukuza milele (Ufunuo 22:5).
🔸Kuwa Macho
Kanisa la kwanza liliishi kwa umakini mkubwa. Wakijua kuwa Yesu anaweza kurudi wakati wowote (Tito 2:13).
→ Usicheleweshe toba wala kuwa mzembe kiroho.
🔸Ishi Maisha Matakatifu
“Kila mwenye tumaini hilo ndani yake hujitakasa, kama Yeye alivyo mtakatifu.” — 1 Yohana 3:3
Ufahamu wa kurudi kwa Kristo unapaswa kutuchochea kuishi maisha ya utakatifu na utii.
🔸 Kuwa na Tumaini
Tufahamu kuwa Majaribu haya ni ya muda. Tumaini letu ni nanga ya roho zetu (Waebrania 6:19).
🔸 Tembea na Ujumbe kwa wengine.
Milele ni halisi. Ndio maana tunahubiri Injili—kwa sababu maisha ya watu yana hatma ya milele.
“Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo!” — Ufunuo 22:17
“Amina. Njoo, Bwana Yesu.” — Ufunuo 22:20
Sauti ya kanisa si hofu, bali ni shauku. Nyakati za mwisho si mwisho wa matumaini, bali ni mwanzo wa utukufu wa milele kwa wote waliomo ndani ya Kristo.
Mafundisho ya ziada kuhusu Siku za Mwisho.
KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.
NYUMBANI MWA BABA YANGU MNA MAKAO MENGI.
SIFA SITA (6), ZINAZOIKAMILISHA ILE SIKU YA BWANA ITISHAYO.
Jehanamu ni nini?
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Biblia unapozungumzia kuhusu kupewa jina jipya inamaanisha nini?
MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.
Vita vya kiroho ni mapambano yasiyoonekana kwa macho ya kawaida, yanayofanyika katika ulimwengu wa roho kati ya ufalme wa Mungu na ufalme wa giza (Shetani na mapepo yake).
Ingawa hayaonekani, lakini vita vyao ni vibaya zaidi ya vile vinavyoonekana, kwani vinamuathiri mwanadamu kotekote, mwilini lakini pia rohoni katika mawazo yetu, hisia, tabia, ndoa, huduma, na hata afya.
Biblia inasema:
Waefeso 6:12
Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho
Mfano:
Mtu anayeokoka anaweza ghafla kuanza kupata majaribu makubwa ya kuudhiwa na watenda dhambi, jambo ambalo huko nyuma hakuwahi kuliona, mpaka anawaza kwamba maisha wa wokovu ni magumu. Hili ni shambulio la kiroho, linalolenga kumrudisha nyuma kiroho.
Ulipompokea Yesu, uliingia katika Ufalme wa Mungu. Na moja kwa moja ulifanyija adui wa Shetani.
Shetani alikupoteza na sasa anafanya kila juhudi kukurudisha, kukuzuia usikue kiroho, au kukushawishi uishi maisha yasiyo ya ushindi.
“Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake.” (Wakolosai 1:13)
Maandiko yanatuambia Shetani alikuwa malaika aliyeasi (Isaya 14:12–15).
Anaendesha vita kwa kutumia uongo, hofu, mashaka, tamaa, magonjwa, migawanyiko, na kushambulia akili zetu.
Uongo – Anapandikiza mawazo kama: “Hujasamehewa” au “Mungu hajasikia maombi yako.”
Vishawishi – Hutumia tamaa za mwili, pesa, au kiburi kukushawishi.
Kuchosha kiroho – Anakufanya uchoke au kupoteza hamu ya kusoma Biblia au kuomba.
Kuvuruga mahusiano – Kupitia fitina, chuki, au hasira isiyoisha.
“Yeye ni mwongo na baba wa huo.” (Yohana 8:44)
Waefeso 6:10–18 inatupa silaha saba za kiroho za kujilinda na kushambulia nguvu za giza:
3.1 Kweli kiunoni.
Kuwa na ujuzi wa kweli ya Neno la Mungu na kuiishi.
Hii inasaidia kutambua uongo wa Shetani.
Mfano: Unapofikiri “Mungu hanipendi,” Neno la Mungu linasema “Hakika amekupenda kwa upendo wa milele.” (Yeremia 31:3)
3.2 Dirii ya Haki
Maisha ya uadilifu na kutokubaliana na dhambi.
Haki hii inatoka kwa Yesu, sio kwa matendo yako.
“Yeye asiyemjua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika Yeye.” (2 Wakorintho 5:21)
3.3 Viatu vya Injili ya Amani (utayari miguuni)
Kuwa tayari kueneza habari njema na kuishi kwa amani.
Mtu aliye tayari kushuhudia haogopi mapambano.
3.4 Ngao ya Imani
Imani huuzima mishale ya hofu, mashaka, na huzuni.
Unaposema, “Mungu atanitetea,” hata wakati hali ni ngumu, hiyo ni imani.
3.5 Chapeo ya Wokovu
Linda mawazo yako kwa kufikiri mambo yanayohusiana na wokovu wako.
Kukumbuka kwamba umeokolewa hukufanya usiyumbishwe na hila za adui.
3.6 Upanga wa Roho (Neno la Mungu)
Neno la Mungu ni silaha ya kushambulia.
Yesu alilitumia aliposhambuliwa na Shetani (Mathayo 4:1–11).
3.7 Maombi
Maombi ni silaha ya nguvu inayoweza kubadilisha hali yoyote.
Omba kwa ajili yako, familia yako, kanisa, na hata waliopotea.
Waefeso 6:18
[18]kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;
Soma Biblia kila siku – Neno la Mungu hukujenga kiroho.
Omba kila siku – Ushindi unapatikana kwa kusali daima.
Kataa dhambi kimaamuzi – Usingojee hisia, fanya uamuzi wa kiroho.
Tembea na Wakristo wengine – Ushirika hukupa nguvu.
Fanya ibada (Sifu na abudu) – Hukuza uwepo wa Mungu na huvunja vifungo vya giza.
Tubu haraka unapokosea – Usimpe shetani nafasi ya kukushitaki.
5.1 Vita vya Kiroho Sio:
Kila shida ni mapepo – Baadhi ya mambo ni matokeo ya maamuzi au mazingira. Hivyo ni wajibu kuchunguza chanzo cha tatizo ni je Adui kweli au!
Kukemea tu– Mamlaka ya kiroho hutegemea maisha ya utii kwa Kristo. Utiifu wako
Kuwa na hofu – Kwamba tuigope, au tuishi kwa mashaka, kana kwamba tuwezekeze nguvu zetu zote kupamba a nayo. Hapana Tuna mamlaka kupitia Yesu.
“Nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge, na kushinda nguvu zote za adui; wala hakuna kitakachowadhuru.” (Luka 10:19)
Ukiwa ndani ya Kristo, huna sababu ya kuogopa. Mapambano yapo, lakini ushindi ni wako kupitia Yesu Kristo.
“Katika mambo haya yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.” (Warumi 8:37)
Waefeso 6:11 – “Vaeni silaha zote za Mungu…”
Yakobo 4:7 – “Mtiini Mungu, mpingeni ibilisi naye atawakimbia.”
2 Wakorintho 10:4 – “Silaha za vita vyetu si za mwili…”
1 Petro 5:8 – “Muwe na kiasi na kukesha… ibilisi yenu… hutafuta mtu wa kummeza.”
Masomo ya ziada kukusaidia kuvishinda vya kiroho
NGUVU YA “KUKATAA” UNAPOPAMBANA VITA VYA KIROHO
Maana ya Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita;
JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
BWANA ni mtu wa vita, BWANA ndilo jina lake.(Kutoka 15:3)
Mishale ya moto ya mwovu inayozungumziwa kwenye Waefeso 6:16 ni ipi?
Nini maana ya huu mstari ” Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;”?(2Timotheo 4:7)
Kila mwamini ameitwa kuieneza injili ya Yesu Kristo. Ambayo huitwa habari njema.
Mathayo 28:19-20
[19]Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; [20]na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
[19]Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
[20]na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Habari njema ni nini? Ni habari za wokovu kwa mwanadamu, ulioletwa na kupitia mtu mmoja Yesu Kristo kwa tendo la kufa na kufufuka kwake kaburini.
Kama tulivyotangulia kuona hapo juu, kuwa siku Yesu alipoondoka hakutuacha bila wajibu, bali kila mmoja wetu alipewa sehemu ya huduma katika shamba lake. Ya kuenenda ulimwenguni kote kuwafanya watu kuwa wanafunzi wake.
Kazi hii sehemu nyingine anaifananisha na talanta, ambayo amempa kila mwamini na anataka kila mmoja aizalishe (Mathayo 25:14-30), sehemu nyingine anaifananisha na matunda, anasema sisi ni matawi na yeye ni mzabibu kwamba tumzalie matunda, (Yohana 15:1-7),sehemu nyingine nyingine anaiita posho, huku yeye akijiita bwana, na sisi mawakili wake, akitutaka tutoe posho kwa wakati kwa watu wake, (Luka 12:42-48)
Sasa ukiangalia utaona sehemu zote hizo tunazofananishwa nazo, kama mtu hajafanya chochote au hajazalisha chochote, haachwi hivi hivi, bali kuna aidha kuondolewa sehemu ya thawabu yake, au kukataliwa kabisa.
Ndio maana ni lazima tujue mwamini yoyote yule, ni lazima aishi maisha ya kuwashuhudia wengine injili.
Warumi 10:14 Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo mhubiri?
Ni lazima ujue kuwa hukumu ipo na kuzimu pia ipo, na inawameza wengi, Na watu hawawezi kuokoka tu wenyewe hivi hivi bila kusikia injili kama wewe ulivyosikia. Tengeneza picha unamwona baba yako, au mama yako kwenye ziwa la moto, halafu anakuambia laiti ningelijua ukweli nisingekuwa huku, utajisikiaje? Ukilijua hili basi huruma ya ki-Mungu itakujaa tu ndani yako, na utasukumwa kujitoa kuwaendea wenye dhambi, kama Kristo alivyotujia sisi, kutoka mbinguni, na kama mitume walivyowaendea watu, ili kuhakikisha wanaokoka.
Luka 15:7 Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu
Mungu hufurahi malaika pia hufurahi, wanapoona roho za watu zinaokoka,duniani, Hivyo sisi kama wana wa Mungu ni wajibu wetu kuyatenda yale tu ambayo yanamfanya Baba yetu afurahi, na hilo si lingine zaidi ya kutoka na kwenda kuwashuhudia watu injili.Hapo tunaufanya moyo wa Mungu hufurahi sana.
Ni ukweli usiopingika kuwa kila mmoja wetu kuna mahali Mungu amemtoa mpaka hapo alipomfikisha, anayo mengi ya kushuhudia kuhusu uzuri wa Kristo.
Wazia yule kichaa ambaye alikuwa katika hali mbaya kule makaburini, uchi, usiku na mchana, ameshindikana kwa vifungo vyote. Lakini Yesu alipokutana naye saa ile ile alipona, akataka kuambatana na Yesu, lakini Yesu akamwambia nenda nyumbani kwa watu wako uwasimulie matendo makuu ambayo Mungu amekutendea, Na tunaona alikwenda kusimulia yote mji ule, na watu wengi wakamwamini Kristo, kwa ushuhuda wake tu.
Marko 5:20 Akaenda zake, akaanza kuhubiri katika Dekapoli, ni mambo gani makuu Yesu aliyomtendea; watu wote wakastaajabu
Hata wewe, wazia uzuri ulioupata pindi ulipompokea Kristo, utamani pia mwingine aupate, na huo ndio upendo, umeonja uzuri wa Kristo unakwenda kuwaambia na wengine mfano tu wa yule mwanamke pale kisimani.
Sawasawa na agizo ambalo Yesu alimwagiza yule mtu ambaye aliteswa Na mapepo akamfungua. (Marko 5:19-20)
Hii ni njia bora, ambayo utapata nguvu ya kikanisa, kwasababu mule akutanapo na vipawa mbalimbali vya Mungu, hurahisisha zaidi moyo wake, kuamini ujumbe uliompelekea.
Ishi maisha yanayomuhakisi Kristo. Kwasababu matendo yako ni injili kuwa wengine kumgeukia Kristo. (1Petro 3: 1-2)
Hivi Ni kama vitabu, kanda, luninga, na kwa dunia ya sasa, Vitu kama whatsapp, websites, panaweza pakawa mahali Ambapo injili yetu kupaa sana na kuwavuta wengi ndani ya ufalme. Ulimwengu wa sasa, upo mtandaoni, hivyo tumia fursa hiyo, kushea mafundisho, mahubiri sahihi ya Neno la Mungu kwa marafiki zako, familia, ndugu, majirani, huko huko Mungu ataanza kazi ya wokovu ndani yao.
Haya ni mambo ya kukumbuka kila uendapo kushuhudia, ili usishindwe na hofu.
Usiwe na hofu ikiwa huoni mwitikio wowote, kwa yule unayemweleza habari ya wokovu, fahamu kuwa ipo mbegu imemwingia ambaye itakuja kumea tu kwa wakati wake.
Uinjilisti wa wawili huwa mrahisi zaidi ya ule wa mmoja (isipokuwa unao uzoefu). Yesu aliwatuma wanafunzi wake wawili wawili, alijua ujasiri utaongezeka lakini wangeweza kufanya zaidi, pale mmoja anapochoka anamtia nguvu mwenzake. Vivyo hivyo na wewe katika hatua za awali ongozana na kiongozi wako, au mshirika mwenza katika kazi ya injili.
Yohana 3:16
Warumi 3:23
Warumi 6:23
Warumi 10:9–10
2 Wakorintho 5:17
Kwa mwongozo wa namna ya kutembea katika baadhi ya vifungu hivyo, pitia hili fundisho >>> NJIA/BARABARA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.
Mafundisho ya ziada
KWANINI TUNAPASWA KWENDA KUIHUBIRI INJILI KWA UJASIRI WOTE?
IHUBIRI INJILI, KILA MAHALI KWASABABU AKUZAYE NI MUNGU.
HEKIMA NANE(8) ZA KIUINJILISTI, KATIKA KUWAVUA WATU KWA KRISTO.
JE UDHAIFU WANGU UNAWEZA KUZUIA INJILI?
KUTOKUIHUBIRI INJILI,KUNA MADHARA GANI?
KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI
Baraka yaweza kutokana na matendo mtu aliyoyatenda au maombi aliyoyaomba.
Kwamfano utamwona mtu anayeitwa Yabesi alimwomba Mungu ambariki na Mungu akasikia na kumbariki.
1Nyakati 4:10 “Huyo Yabesi akamlingana Mungu wa Israeli, akisema, Lau kwamba ungenibarikia kweli kweli, na kunizidishia hozi yangu, na mkono wako ungekuwa pamoja nami, nawe ungenilinda na uovu, ili usiwe kwa huzuni yangu! Naye Mungu akamjalia hayo aliyoyaomba”
Baraka za MUNGU zimegawanyika katika makundi makuu mawili;
1. BARAKA ZA ROHONI.
Hizi ni baraka zinazoinufaisha roho ya mtu na ndizo zenye umuhimu sana kuliko zile nyingine.
Baraka ya kwanza ya rohoni ni “WOKOVU”. Mtu aliyepata Neema ya kumwamini YESU na kuoshwa dhambi zake huyo amebarikiwa, kwasababu anao uzima wa milele.
Waefeso 1:3 “Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa BARAKA ZOTE ZA ROHONI, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo”.
Baraka ya rohoni inazaa Furaha, amani, utulivu na utakatifu kwa ujumla.
Watu waliobarikiwa rohoni hata wakose vyote vya mwilini bado wanaishi maisha ya raha, kwasababu roho zao zimebarikiwa kuwa ndani ya YESU ambaye kila kitu.
2. BARAKA ZA MWILINI.
Baraka za mwilini ni vyote ambavyo mtu anavipokea kutoka kwa MUNGU vyenye manufaa ya mwili, ikiwemo afya, cheo, uzao au mali.
Mfano wa watu waliobarikiwa kwa baraka za mwilini ni Sulemani, alipewa utajiri mkubwa hata baada yake hakukuwa na mtu kama yeye,
Na wengine kwenye Biblia agano la kale ni Abramu na Ayubu hawa walibarikiwa vingi na MUNGU.
Lea naye alibarikiwa kuwa na watoto wengi, Samsoni alibariwa nguvu za mwilini n.k
Katika Agano jipya walikuwepo akina Yusufu wa Arimathaya, (Mathayo 27:57), na wanawake si haba, akina Yoana, Suzana na wengine wengi (Luka 8:3).
Na waliobarikiwa kwa vyeo, waliomwamini Bwana YESU walikuwa wengi sana wanaume na wanawake (soma Matendo 17:12-14).
Na kubarikiwa mwilini kunaweza kuwa ishara ya kubarikiwa pia rohoni, lakini sio ishara pekee kwasababu wapo matajiri wasiomwamini YESU na walikuwepo matajiri kabla ya Bwana YESU,
Na watakuwepo matajiri wengi katika ziwa la moto (Soma Luka 16:20-34).
Na tena Bwana Yesu alisema itamfaidia nini mtu apate kila kitu halafu apate hasara ya nafsi yake (Marko 8:34).
Na pia wapo maskini ambao hawajabarikiwa baraka za mwilini lakini wamebarikiwa mambo ya rohoni..
Yakobo 2:5 “Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao?”.
Kwahiyo tukiwa wote ndani ya Kristo, hatupaswi kudharauliana kwa hali zetu, bali tunapaswa tuhudumiane kwa viwango vya baraka tulivyobarikiwa..
kwasababu yule unayemwona ni maskini wa vya mwilini huenda ni tajiri wa vya rohoni sana, ndivyo Neno la Mungu linavyosema..
Ufunuo 2:9 “Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri)…”
Na yule unayemwona hana vya rohoni kama ulivyo navyo wewe basi amebarikiwa vya mwilini, ambavyo kupitia hivyo vinahitajika kwaajili ya injili, ili mambo yote yakae katika uwiano na wote tuheshimiane.
Na pia inawezekeana mtu akabarikiwa kwa vyote vya rohoni na mwilini, kwa mapenzi ya MUNGU, lakini haiwezekani mtu aliyemwamini YESU akakosa vyote..
Ikitokea dalili ya kukosa vyote basi kuna kasoro katika imani, hivyo mtu huyo anapaswa aangalie jinsi alivyosikia na anavyoenenda.
Je umempokea YESU?..huo uchungu na hofu na wasiwasi ni ishara ya kupungukiwa baraka za rohoni.
Leo hii mpokee YESU ili uanze kula matunda ya baraka za rohoni.
MAOMBI YA YABESI.
Fahamu maana ya Mithali 28:20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;
KILA MTU NA AMCHE BABA YAKE NA MAMA YAKE.
MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.
TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.
Swali: Huwa tunasema.. “tusome maandiko” na wakati mwingine “tusome Neno”..ipi tofauti ya maneno haya mawili?.
Jibu: Tuanze na Neno au Neno la Mungu.
“Neno” ni sauti ya MUNGU yenye ujumbe inayokuja kwa mtu kwa njia ya maono au ndoto au njozi..
Kwamfano katika biblia utaona lugha iliyotumika kwa manabii wote waliojiliwa na sauti ya Mungu iliyobeba ujumbe ni hiyo ya “Neno la Mungu”
Mwanzo 15:1 “Baada ya mambo hayo NENO LA BWANA likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.
Soma pia 1Wafalme 17:8, Isaya 38:4, Yeremia 1:11, Ezekieli 1:3, Ezekieli 12:21, Hosea 1:1, Yona 1:1, Mika 1:1, Sefania 1:1 n.k
Hata sisi wakati mwingine tunapotaka kuzungumza na mtu, tunaweza kutumia lugha hiyo kwa kumwambia “nina neno nataka kusema nawe”… au kama kuna mtu amekuambia jambo unaweza kusema “mtu Fulani kaniambia neno”.. kwahiyo ni hivyo hivyo hata katika biblia, Neno la Mungu ni sauti ya MUNGU.
Sasa kama “Neno” tafsiri yake ndio hiyo, vipi kuhusu “Andiko”?
Andiko ni Neno la Mungu lililo katika maandishi… Kwamfano; hilo Neno lililomjia Abramu, kwake yeye ni Neno la Mungu lakini kwetu sisi ni andiko, ndio maana tunalisoma.. Na Nguvu ya andiko na Neno ni ile ile.
Hivyo maneno ya Mungu yote yaliyoandikwa katika Biblia ni “MAANDIKO”.. Hata wewe maneno yako unayoyasema unaweza kuyaandika katika kitabu, na yakawa ni maandiko kwasababu ni maneno yaliyoandikwa.. Hali kadhalika, kila Neno la Mungu kwenye Biblia ni andiko.
Hivyo mtu anayesema “tusome maandiko” na Yule anayesema “tusome Neno la Mungu” ni kitu kimoja.. na nguvu ni ile ile..
Na kila Andiko lenye pumzi ya Mungu linafaa kwa mafundisho, kuonya, kuongoza na kuadibisha..
2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; 17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema”
2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema”
Kwa urefu kuhusiana na kazi ya MAANDIKO inayofanya kwa mtu fungua hapa >>MAMBO MANNE(4) YAFANYAYO NENO LA MUNGU.
Je umempokea YESU?, Umebatizwa katika ubatizo sahihi?..una uhakika Bwana YESU akirudi unaenda naye?.
Maran atha.
EPUKA KUJIFANYA HUJUI.
MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?
TUUTAZAME PIA MWISHO WA UJENZI WETU.
ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.
NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?
Swali: Katika Mathayo 27:31-32 tunasoma kuwa Simoni Mkirene alimsaidia Bwana kuubeba msalaba wakati anaelekea mahali pa kusulibishwa, lakini tukirudi katika Yohana 19:17-18 tunasoma kuwa hakusaidiwa na mtu badala yake aliubeba mwenyewe mpaka Golgotha, je mwandishi yupi yupo sahihi?.
Jibu: Turejee mistari hiyo..
Mathayo 27:31 “Hata walipokuwa wakitoka, wakamwona mtu Mkirene, jina lake Simoni; huyu wakamshurutisha auchukue msalaba wake. 33 Na walipofika mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa”
Mathayo 27:31 “Hata walipokuwa wakitoka, wakamwona mtu Mkirene, jina lake Simoni; huyu wakamshurutisha auchukue msalaba wake.
33 Na walipofika mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa”
Hapa ni kweli Simoni Mkirene alimsaidia Bwana kuubeba msalaba..
Lakini hebu tusome tena Yohana 19:17-18..
Yohana 19:16 “Basi ndipo alipomtia mikononi mwao ili asulibiwe; nao wakampokea Yesu. 17 Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, au kwa Kiebrania, Golgotha. 18 Wakamsulibisha huko, na wengine wawili pamoja naye, mmoja huku na mmoja huku, na Yesu katikati”.
Yohana 19:16 “Basi ndipo alipomtia mikononi mwao ili asulibiwe; nao wakampokea Yesu.
17 Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, au kwa Kiebrania, Golgotha.
18 Wakamsulibisha huko, na wengine wawili pamoja naye, mmoja huku na mmoja huku, na Yesu katikati”.
Hapa inaonyesha ni kama hakusaidiwa na mtu mpaka alipofika Golgotha..
Je kwa mantiki hiyo biblia inajichanganya?…
Jibu ni La! Biblia ni kitabu kisicho na makosa wala mkanganyiko mahali popote, isipokuwa fahamu zetu na pambanuzi zetu ndizo zinazojichanganya.
Sasa tukirejea katika habari hizo mbili, ni kwamba Mwandishi wa kitabu cha Yohana (ambaye ni Yohana mwenyewe) alijaribu kueleza safari ya Bwana kwenda Golgotha kwa ujumla, bila kuhusisha matukio madogo madogo yaliyokuwa yanatokea njiani.
Kwamfano utaona yeye kasema tu Bwana alijichukulia msalaba wake mpaka Golgotha, pasipo kutaja matukio kama ya kutemewa mate njiani, au wale wanawake kumlilia na Bwana kuwajibu kwamba wajililie nafsi zao na watoto wao (Luka 13:26-28).. Sasa matukio kama haya Yohana hajayataja lakini haimaanishi kuwa amesema hayapo, la! Bali ni kwamba kafupisha tu habari.. hata wewe/mimi tunaweza kuelezea jambo kwa urefu au ufupi kutegemea na mapenzi yetu.
Lakini sasa tukirudi kwa Mathayo yeye kataja safari ya Bwana kwa urefu kidogo, akihusisha matukio madogo madogo yaliyokuwa yanaendelea njiani katika safari yake..na mojawapo ya tukio ndio hilo la Simoni Mkirene aliyekuwa anatokea shamba na akashurutishwa kuubeba msalaba wa Bwana YESU.
Na utaona pia ijapokuwa Mathayo alirekodi tukio la Simoni Mkirene kumsaidia Bwana msalaba, lakini pia hakutaja tukio la wanawake waliomlilia Bwana njiani, ambapo tukio hilo linakuja kutajwa na mwandishi mwingine wa kitabu kingine ambaye ni Luka..
Luka 23:26 “Na walipokuwa wakimwondoa walimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa ametoka shamba, wakamtwika msalaba, auchukue nyuma yake Yesu. 27 Mkutano mkubwa wa watu wakamfuata, na wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea. 28 Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu. 29 Kwa maana tazama, siku zitakuja watakaposema, Heri walio tasa, na matumbo yasiyozaa, na maziwa yasiyonyonyesha”.
Luka 23:26 “Na walipokuwa wakimwondoa walimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa ametoka shamba, wakamtwika msalaba, auchukue nyuma yake Yesu.
27 Mkutano mkubwa wa watu wakamfuata, na wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea.
28 Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu.
29 Kwa maana tazama, siku zitakuja watakaposema, Heri walio tasa, na matumbo yasiyozaa, na maziwa yasiyonyonyesha”.
Umeona kwahiyo habari ya Bwana YESU kujichukulia msalaba mpaka Golgotha kama ilivyoandikwa na Yohana haipingani na ile iliyoandikwa na Luka, Mathayo au Marko.. kinachotofautisha habari hizo ni kwamba moja imeandikwa kwa urefu nyingine kwa ufupi.
Je umempokea YESU, je umeubeba msalaba wako na kumfuata?.. Je unajua ni kwanini Simoni Mkirene aliruhusiwa kubeba msalaba nyuma ya YESU?.. ni ufunuo kuwa tukitaka kumfuata YESU ni lazima tubebe msalaba tumfuate YESU nyuma.
Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate. 35 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha”.
Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.
35 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha”.
MANENO SABA YA YESU MSALABANI.
YESU MNAZARETI, ANWANI YA MSALABA.
MSALABA NI ZANA YA UJENZI WA MAISHA YAKO.
Je! Bwana Yesu alisulubiwa juu ya msalaba au juu ya mti uliokuwa wima?
Kwanini Bwana Yesu alisema pale msalabani naona kiu?
SWALI: Biblia inasema maziwa ni kwa watoto wachanga, lakini chakula kigumu ni cha watu wazima. Mfano wa chakula hichi kigumu ni kipi?
Waebrania 5:12 Kwa maana, iwapasapo kuwa waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu. 13 Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga. 14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya
JIBU:
Kabla ya kufahamu hicho chakula kigumu, ni vema kujua kwanza maziwa ni yapi.
Hivyo ukiendelea kusoma vifungu vinavyofuata anasema..
Waebrania 6:1 Kwa sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu, 2 na wa mafundisho ya mabatizo, na kuwekea mikono, na kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele. 3 Na hayo tutafanya Mungu akitujalia.
Sasa hayo mafundisho ya kwanza ya Kristo ndio maziwa. Yaani Mafundisho ya toba, imani kwa Mungu, ubatizo, kuwekewa mikono, kufufuliwa wafu, na hukumu ya milele ni mafundisho ya watoto wachanga..kiroho hujulikana kama maziwa..
Kimsingi mtoto akiendelea kunywa maziwa tu peke yake daima, kitakachotokea baadaye ni kudumaa kama sio kufa kabisa, hivyo itafika wakati tu atahitaji chakula kingine ili aendelee kuishi. Vivyo hivyo na sisi, vipo vyakula ambavyo tunapaswa tule, kwa jinsi tunavyoendelea kukua kiroho.
Vifuavyo ndio vyakula vigumu vya kiroho vya watu wazima:
Mathayo 5:44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
Kwanini ni chakula kigumu?. Kwasababu jambo hilo linaenda kinyume na asili ya mwanadamu, linafunua asili ya ndani kabisa ya Kristo, ambayo si rahisi mtu aliyemchanga kiroho, kuielewa, au kulipokea nyakati za mwanzoni, yaani kumwombea na kumpenda Yule ambaye anaiwinda roho yake au aliyemjeruhi, ..
Wafilipi 1:29 Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;
Kwanini ni chakula kigumu?. Kwasababu mwamini mchanga, mara nyingi atapenda kuambiwa maneno ya faraja, baraka, na mafanikio, awapo kwa Kristo, lakini mkristo aliyekomaa, anayaona mapenzi ya Mungu pia hata katika majaribu na kuyashangalia.
1Wathesalonike 3:3 mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo
Soma pia 1Petro 1:6-8, 4:13, Wakolosai 1:24, Luka 6:22-23
Waebrania 5:14 Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya
Mkristo aliyekomaa kiroho, anafundishwa na Mungu kutambua na kugawanya vema mambo yote, kujua vilivyo najisi na visivyo najisi, mafundisho ya kweli na yale ya uongo, anafundishwa, busara, ujuzi na hekima hata katika kuhubiri injili kwa makundi yote, bila kuanguka na kunajisika, kwasababu amepewa roho ya upambanuzi ambayo huja kwa kuzoeshwa na Mungu kwa kipindi Fulani cha muda kupitia Neno lake.
1Wakorintho 9:20 Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria. 21 Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria. 22 Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.
1Wakorintho 9:20 Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria), ili niwapate walio chini ya sheria.
21 Kwa wale wasio na sheria nalikuwa kama sina sheria, (si kwamba sina sheria mbele za Mungu, bali mwenye sheria mbele za Kristo), ili niwapate hao wasio na sheria. 22 Kwa wanyonge nalikuwa mnyonge, ili niwapate wanyonge. Nimekuwa hali zote kwa watu wote, ili kwa njia zote nipate kuwaokoa watu.
Soma pia, 1Wakorintho 8:6-13, Yohana 2:1-12, Mathayo 11:19.
Kwanini ni chakula kigumu? Kwasababu mtu ambaye ni mchanga kiroho, akijihusisha katika viwango hivyo, hupotea na kunajisika kama sio kupotea kabisa. Ndicho kilichowatokea Adamu na Hawa kuuvamia mtu wa ujuzi wa mema na mabaya nje ya ratiba ya Mungu, matokeo yake wakayavuna mabaya, wala sio mema.
Katika wokovu ipo fimbo ya Mungu; Mzazi yoyote huwa hatoi zawadi tu, sikuzote, hacheki na mwanawe siku zote, lakini pia kuna wakati fimbo hutumika, Vivyo hivyo Mungu ni Baba yetu, huadhibu, pale tunapokosea..
Waebrania 12:11 Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani.
Kwanini ni kigumu? Kukubali marekebisho kwa kuadhibiwa kama sehemu ya kutengenezwa na Mungu, si jambo rahisi mtu kulikubali mkristo ambaye hajakomaa. Yeye atakachojua tu, kuwa Mungu ni upendo.
Luka 9:23 Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.
Kwanini ni chakula kigumu? Aliye mchanga kiroho kukubali kukataa mapenzi , kuingia gharama kuacha vyote na kuyakubali ya Mungu tu, si jambo rahisi kwa mwanafunzi wa ngazi ya chini.
Wafilipi 2:3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. 4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine. 5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; 6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; 7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; 8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba
Wafilipi 2:3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.
4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;
8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba
Kwanini ni chakula kigumu?.
Mkristo mchanga kiroho, si rahisi kuangalia mambo ya wengine, mfano wa Kristo, si rahisi kujinyenyekeza na kukubali kutembea kama mtumwa ili kuwatumikia wengine.
Kama mwamini mpya ni lazima ufahamu kuwa kanisa sio jengo, bali kanisa ni watu wa Mungu waliookolewa na kuwekwa pamoja ili kumwabudu Mungu, na kuhudumiana.
1 Wakorintho 12:27
[27]Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.
Kama vile viungo vinavyoshirikiana, vivyo hivyo na wewe huna budi kuwa na ushirika wote wa kanisa, sio kuwa mtembeleaji. Kila mwamini ni kiungo Katika mwili huo.
Waefeso 5:25-27
25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; 26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;
Kristo anataka ujue kuwa unapookoka, unakuwa katika kifungo chake, mfano tu wa mwanamke aliye katika ndoa. Bwana mmoja, mwili mmoja, huku akimtii yeye katika yote. Vivyo hivyo na wewe, tangu huu wakati uliokoka ni wajibu wako, kumtumikia Kristo tu, na kumtii katika yote atakayokuagiza ndani ya kanisa.
Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu”.
Kama mwanafamilia unakuwa na haki ya kupokea na kurithi ahadi zote ambazo Mungu alizoahidi kwa watu wake, kwasababu wewe tayari umeshafanywa kuwa mwana wake.
1Wakorintho 3:16 -17
16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? 17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.
Kwamba ukishaokoka, wewe na waamini wenzako mnaitwa nyumba ya Mungu, hivyo ni wajibu wako kuifanya nyumba hiyo safi sikuzote kwa kuishi maisha ya utakatifu, kwasababu Mungu haishi mahali pachafu, bali pasafi. Wewe ni nyumba ya Mungu, iheshimu nyumba yake.
Kwa kupitia mafundisho, mahubiri, madara ya uanafunzi, uyapatayo ndani ya kanisa, pamoja na madhihirisho mbalimbali ya karama za Mungu, utajikuta unajengeka kwa haraka sana na Matokeo yake utajengwa na kukua kiroho, tofauti Na kama ungekuwa peke yako. (Waefeso 4: 11-13)
Mahali Bora pa kumwabudu, na kumsifu Mungu kwa uhuru na nguvu, ni Pale uwapo katika mkusanyiko. Daudi alisema;
Zaburi 95:6
[6]Njoni, tuabudu, tusujudu, Tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.
Kanisa lina misingi ya maombi na Maombezi. Bwana Yesu alisema;
Yakobo 5:16
[16]Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.
Huwezi kusaidika pale unapoishiwa na nguvu, kama huna jamii ya watu nyuma yako kukushika mkono kimaombi au kihali usimame. Kanisa la kwanza, lilipokusanyika, lilisaidiana katika mahitaji, lakini pia lilitatua migogoro, mbalimbali iliyozuka katikati yao. Hivyo mtu anayekosa kanisa, ukweli ni kwamba anaishi kama yatima wa kiroho.
Kanisa Ni kama karakana ya Mungu inayowaandaa watu, kuwa watendakazi. Ni mahali ambapo utatambua Karama yako. Kisha kuitumia hiyo kuwahudumia wengine na kuipeleka mbele kazi ya Mungu.
Matendo 2:41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali
Mengi kwa jinsi uwezavyo..
Biblia inatuambia tuonyana kila inapoitwa leo (yaani kila siku).
Waebrania 3:13 Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa udanganyifu wa dhambi. 14 Kwa maana tumekuwa washirika wa Kristo, kama tukishikamana na mwanzo wa uthabiti wetu kwa nguvu mpaka mwisho;
Pamoja na hilo, atakatifu wa zamani, ukiachilia mbali makusanyiko ya katikati ya wiki, ilikuwa ni lazima siku ya kwanza ya juma wote wakusanyike. (1Wakorintho 16:2). Yaani kila jumapili ilikuwa ni siku ya Bwana.
Kanisa ni kama Shule kwa mwanafunzi. Tunajua Shule kama Shule sio elimu. Bali shule hutoa elimu. Kwasababu ndani yake wapo waalimu, zipo nidhamu, wapo wanafunzi wenzako , yapo majaribio, Vipo vitabu n.k. ambavyo vinakusaidia Kufaulu vizuri katika masomo yako.
Halikadhalika wewe kama mwamini mpya, ni lazima uwe na kanisa. Mwamvuli wako, ujengwe ukue, uandaliwe. Kanisa ni chombo maalumu alichokiunda Mungu, siku ile ya pentekoste ili watu wake wamwone yeye.
Zingatia sio kila mkusanyiko unaosema ni wa-kikisto ni kweli ni kanisa la Mungu. Kwasababu manabii, na wapinga-Kristo wapo sasa duniani.
> Epuka mikusanyiko isiyo mfanya YESU KRISTO kama ndio msingi, na wokovu wa mahali hapo.
> Epuka mikusanyiko isiyokurejeza katika maisha haki na utakatifu.
> Epuka mikusanyiko isiyokukumbusha juu ya hatma ya maisha yajayo, yaani kuzimu na mbinguni
> Epuka mikusanyiko isiyoamini katika utendaji kazi wa karama za Roho Mtakatifu.
Omba, kwanza, kisha fanya maamuzi.
Ikiwa bado hujawa na uhakika wa pa kukusanyika. Basi wasiliana na sisi tukusaidie mahali sahihi pa kukusanyika..
Vifungu hivi visitoke akilini mwako:
Waebrania 10:25
[25]wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.
Mhubiri 4:9-10
[9]Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao. [10]Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!
[9]Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao.
[10]Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua!
Zaburi 122:1
[1]Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa BWANA.
Kwanini tunakwenda kanisani?
WALA TUSIACHE KUKUSANYIKA PAMOJA
WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU
EPUKA KUCHELEWA IBADA.
KATAA KUWA EUTIKO, WA KUSINZIA IBADANI.
KAMA MKRISTO NI LAZIMA UWE NA DESTURI HII.