Title Devis

KUOTA NYOKA.

Nakusalimu katika jina la mwokozi wetu YESU KRISTO, Suala la upambanuzi wa ndoto ni moja ya mambo ambayo yanawasumbua wengi, lakini kwa bahati mbaya watu wengi wamekosa kujua tafsiri ya ndoto zao, kulingana na maandiko…

Hivyo kabla ya mtu hukimbilia kupewa au kutafuta tafsiri ya ndoto yake ni vizuri kwanza akafahamu kuwa ndoto zimegawanyika katika makundi makuu matatu, kundi la kwanza ni zile ndoto zinazotokana na Mungu, kundi la pili ni zile zinazotokana na shetani na kundi la tatu ni ndoto zinazotokana na mtu mwenyewe, na hizi ndizo zinazochukua sehemu kubwa ya ndoto tunazoziota karibu kila siku, na aina hii ya tatu huwa inakuja kutokana na shughuli zetu tunazozifanya kila siku au mazingira yanayotuzunguka kila siku..

Ndoto za namna hii huwa hazibebi ujumbe wowote, hivyo hazihitaji kutafsiriwa, mara nyingi zinapaswa zipuuziwe..ikiwa hujafahamu vizuri namna ya kuitambua ndoto yako kulingana na makundi haya basi bofya somo hii ulipitie kisha ukishamaliza tuendelee…>> NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?

Watu wengi wamekuwa wakiniuliza tafsiri ya ndoto hii ya kuota nyoka, sasa ikiwa ni ndoto ambayo inajirudia rudia, basi izingatie sana..kumbuka Nyoka katika maandiko tangu mwanzo anasimama kama ishara mbaya,

Na nyoka amebeba tabia kuu tatu, ya kwanza ni kudanganya kama tunavyomsoma pale Edeni alivyomdanganya Hawa (Mwanzo 3:1-5), tabia ya Pili ni kuuma kama biblia inavyotuambia atakugonga kisigino (Mwanzo 3:15), na ya tatu ni kumeza, kama tunavyosoma katika kitabu cha Ufunuo 12:4), pale alipotaka kummeza mtoto yule alipotaka kuzaliwa,..Na tabia hizi zote Shetani anazo na ndio maana kila mahali alifananishwa na joka, na sio kiumbe kingine chochote kama vile kondoo au njiwa.

Hivyo ndoto za namna hii nyingi zinatoka kwa shetani, na chache sana zinakuja kutoka kwa Mungu, lakini tukianza kuchambua upande mmoja mmoja hatutamaliza, wengine wanaota wanakimbizwa na nyoka, wengine wanaota wanaumwa na nyoka, wengine wanaota wameviringishwa na nyoka, wengine wanaota wapo karibu na ziwa au bahari na lijoka likubwa linatoka huko, wengine wanaota wanamezwa na joka, wengine wanaongea nayo n.k. n.k. vyovyote vile chamsingi ambacho mtu anapaswa kufahamu hapo ni kuwa ziwe zinatoka upande wa Mungu au upande wa shetani,..Ni kwamba ADUI YUPO MBELE YAKO.

Hapo Shetani yupo karibu na wewe kutimiza kazi hizo tatu au aidha mojawapo,

Jambo la kwanza ni  kukudanganya au tayari ameshakudanganya: Sasa Ikiwa upo nje ya Kristo yaani hujaokoka basi fahamu kuwa upo chini ya udanganyifu wa shetani tayari, hivyo hapo unaonyeshwa hali yako ilivyo rohoni, Jambo unalopaswa kufanya ni kurudi kwa Kristo haraka sana kabla udanganyifu haujawa mkubwa zaidi ukakuzalia matunda ya mauti, hapo ulipo tayari umepofushwa macho pasipo hata wewe kujijua. Hivyo tubu umgeukie Mungu haraka sana, maadamu muda bado upo.

Au kwa namna nyingine shetani anakaribia kukushawishi kuingia katika kosa au dhambi ambayo itakugharimu sana, hata maisha yako, hivyo angalia njia zako, uchukue tahadhari, funga milango yote ambayo unaona itakupeleka mbali na Kristo, acha kufanya vitu ambavyo sasa hivi unavifanya unaona kabisa havimpendezi Mungu, acha haraka sana, upo mtego wa shetani nyuma yake.

Pili shetani anakutegea mtego au anataka kukuletea madhara aidha katika huduma yako, au afya yako,au familia yako au shughuli yako, anataka kukugonga kisigino chako usisonge mbele, hapo unapaswa uongeze kiwango chako cha maombi kama Bwana Yesu alivyosema ombeni msije mkaingia majaribuni..Hivyo ili kumshinda silaha uliyonayo ni kuomba sana.

Tatu shetani anataka kukimeza kile ambacho Mungu amekipanda ndani yako:

Na jambo la kwanza huwa anakimbilia ni NENO LA MUNGU hilo ndilo huwa anafanya bidii sana kupambana nalo kwasababu anajua likishakuwa ndani ya mtu litakwenda kuleta madhara makubwa sana katika ufalme wake hivyo anasimama hapo karibu na wewe ili akimeze kile ulichokisikia.. inafananishwa na zile mbegu ambazo zilingukia njiani ndege wakaja kuzila,

Mathayo 13:18 “Basi ninyi sikilizeni mfano wa mpanzi.

13.19 Kila mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia.”

Hivyo kwa ufupi ikiwa upo nje ya Kristo fanya hima uingie ndani, na ikiwa upo ndani ya Kristo chukua tahadhari uimarishe uhusiano wako na Kristo kwasababu shetani yupo karibu na wewe kushindana nawe kwa kila hali..

Ubarikiwe.

Group la whatsapp Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU.

JE! WEWE NI MWANA WA IBRAHIMU?

USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.

UZAO WA NYOKA.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini wakristo wengi ni maskini?.

Mtu anayeuliza swali hili ninaamini kabisa anauliza kutoka katika dhana hii “Kama Mungu ni tajiri, kwanini basi na watu wake wasiwe matajiri kama yeye”…Na ndio maana swali kama hili la kwanini wakristo wengi ni maskini linajengeneza kichwani mwake…Lakini laiti kama angejiuliza kwa kulinganisha wakristo na watu wengine, au kuulinganisha ukristo na dini nyingine basi swali hili ninauhakika lingeshajijibu lenyewe kichwani mwake..

Kwani bila shaka hakuna asiyejua idadi ya matajari na maskini duniani haiwezi kuwa sawa na wala haitakaa ikaribiane daima, karibu katika kila Nyanja na kila eneo na kila sekta, utakuta maskini au watu wenye uchumi wa kati ni wengi kuliko matajiri, hata ukienda katika mataifa yanayojiona kuwa ni matajiri, hata ukirudi mataifa maskini, hata ukienda katika dini zote, sio tu katika ukristo, ukienda pia kwa waislamu utakuta waislamu wengi ni maskini kuliko matajiri, ukienda kwa wahindu utakuta hivyo hivyo, ukienda kwa wasio na Mungu jambo ni lile lile kwahiyo ukitazama kwa jicho hilo utagundua kuwa  hilo sio jambo la kushangaza sana.

Lakini kwasababu tunataka kuwalinganisha sawasawa na Mungu wao wanayemtumikia, naomba ubofye somo hili ulipitie taratibu naamini utapata majibu yote yaliyojibiwa kulingana na maandiko..…>>>  JE! UKRISTO UNAMPA MTU DHAMANA YA KUWA TAJIRI?

Mada Nyinginezo:

BIBLIA INAPOSEMA “HERI WALIO MASKINI WA ROHO MAANA UFALME WA MBINGUNI NI WAO”JE HATUNA RUHUSA YA KUWA MATAJIRI KATIKA ROHO?.

 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wakatoliki wanaabudu sanamu?

Kulingana na Biblia, Wakatoliki ni kweli wanaabudu sanamu…

Biblia inasema, katika

Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao”,

Sasa tatizo sio kutengeneza sanamu, wala kuning’iniza picha manyumbani mwetu za watakatifu au za wanafamilia wetu, bali tatizo ni “kuzisujudia” na “kuzitumikia”…Hivyo vitu viwili ndio tatizo.

Sasa Kanisa katoliki linafundisha watu kusujudia sanamu pamoja na kutumikia sanamu. Na kumbuka sanamu haimaanishi tu lisanamu likubwa kama lile la Nebkadneza, bali sanamu  hata ndogo tu kama punje ya harage pia ni sanamu…mbele za Mungu zote ni sawa!

Sasa Waumini wa kanisa katoliki wanafundishwa kuzipa hizi sanamu heshima fulani kana kwamba zimebeba kitu cha kiungu ndani yake..Kitendo tu cha kuzipa heshima fulani, kama kwamba ni kitu cha Kiungu hiyo tayari ni Ibada ndani ya moyo wa Mtu, na ndio kitu kinachomchukiza Mungu..

Kadhalika, kutumikia maana yake ni kukiwekea hicho kitu utaratibu fulani ambao ni kama sheria fulani inayokufanya wewe kuwa mtumwa wa hicho kitu…Kwamfano kusali rozari kila siku asubuhi, mchana na jioni na kuogopa hata kuikanyaga kwa bahati mbaya  hiyo ni kuitumikia rozari….ambapo kwako inakufanya kuwa mtumwa..Jambo hilo ni machukizo mbele za Mungu.

Sasa si wakatoliki wote wanajua hilo, na si wakatoliki wote wana nia mbaya katika kwenda kuabudu katika kanisa hilo, wengi wana nia ya kweli ya kwenda kumtafuta Mungu, isipokuwa Mfumo wa Udini umewafunga hata hawawezi kuiona kweli tena!..Lakini wale Bwana aliowachagua wakati ukifika wanapokutana na Ukweli wanafunguka macho na kurekebisha njia zao, kwa kutoka katika mifumo ya kanisa hilo na kugeukia kumwabudu Mungu katika roho na Kweli.


Mada Nyinginezo:

JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?

JE BIKIRA MARIAMU ALIZAA WATOTO WENGINE?

JE! NI SAHIHI KUMUITA MARIA MAMA WA MUNGU?

JE! BIKIRA MARIA NI MALKIA WA MBINGUNI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Mtume Paulo alioa?

Mtume Paulo, hapo kwanza alikuwa akiitwa SAULI, Alikuja kuitwa Paulo baada ya kukutana na Bwana Yesu, na kubadilishwa….Alizaliwa mahali panapoitwa Tarso, huko Kilikia,…Kwasasa ni eneo la nchi ya UTURUKI.

Matendo 21:39 “Paulo akasema, Mimi ni mtu wa Kiyahudi, mtu wa Tarso, mji wa Kilikia, mwenyeji wa mji usiokuwa mnyonge”.

Kwa asili Paulo alikuwa ni Myahudi (yaani Muisraeli) alikuwa ni wa kabila la Benyamini na alikuwa ni Farisayo.

(Wafilipi 3.5 Nalitahiriwa siku ya nane, ni mtu wa taifa la Israeli, wa kabila ya Benyamini, Mwebrania wa Waebrania, kwa habari ya kuishika torati, ni Farisayo,)

Mtume Paulo hakuoa mke, Alijizuia kuoa ili aihubiri Injili pasipo kuvutwa na mambo mawili, yaani mambo ya kumpendezesha mke na kumpendezesha Mungu..

1Wakorintho 7 :32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;

33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe”.

kama alivyokuwa Yohana Mbatizaji na Eliya Nabii hao pia hawakuoa. Na hivyo kuwafanya Injili yao kuwa na matunda mengi kuliko wengine wote.

Biblia inasema hakuna Nabii aliyetokea aliye Mkuu kuliko Yohana Mbatizaji, kadhalika Eliya ni nabii pekee ambaye hakuonja mauti..Na Mtume Paulo ni Mtume pekee ambaye alifanya kazi kuliko wote waliomtangulia.


Mada Nyinginezo:

YOHANA MBATIZAJI NI NANI?

YESU NI NANI?

SIRI YA KUFANIKIWA KWA MTUME PAULO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNASAFIRI.

Napendelea kabla mtu hajakimbilia kutafuta tafsiri ya ndoto yake, ni vizuri kwanza apate  elimu juu  ya aina za ndoto, hiyo itamsaidia kujua ndoto yake inaangukia katika kundi la aina gani, hivyo atapata wepesi wa kuweza yeye mwenyewe kuzitafsiri ndoto pasipo hata kutegemea msaada wa mtu mwingine.

Ikiwa utapenda kujua aina hizi za ndoto bofya hapa >>  NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?   ukishamaliza kusoma kisha tuendelee…

Sasa kama ndoto yako sio ile inayotokana na shughuli za kila siku au mazingira yanayokuzunguka na unaiota mara kwa mara, basi fahamu kuwa kuna jambo Mungu anazungumza na wewe hapo zingatia sana..Biblia inasema..

Ayubu 33:14 “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.

15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;

16 Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao,”

Mungu anakukumbusha kuwa upo safarini hapa duniani, kwamba kila jambo unalolifanya ukumbuke kuwa upo safarini hakuna na chochote utashikamana nacho hapa duniani milele,..

Na kama tunavyojua safarini, hata mkishuka kupumzika pengine kula au kujisaidia basi  ni dakika chache tu 10 au 15 basi safari inaendelea, hakuna muda wa kuzurura zurura au kuanza kujihangaisha na mambo ya hapo mlipokuwa mnapita, utakuwa ni mjinga kama utawaza kuwekeza eneo hilo, au kwenda kufanya shughuli hapo, gari litaondoka na kukuacha, na mwisho wa siku kule ulipokuwa unatazamia kwenda hutafika..

Hivyo Mungu kukuonyesha hivyo ni kukuonya usiangalie sana mambo ya ulimwengu huu yanayopita bali angalia vya kule mbele vinavyodumu na ukumbuke kuwa upo safarini, inamaanisha kuwa kwa namna moja au nyingine ulishawahi kuyatazama mambo ya kule, ishi kama maisha ya mpitaji, kwasababu watu wote wa Mungu ndivyo wanavyoishi..

Isaya 35:8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, wajapokuwa wajinga, hawatapotea katika njia hiyo.”

Hivyo angalia ni vitu gani vinavyokusonga katika maisha yako, Je! Ni shughuli za ulimwengu huu mpaka hauna muda na Mungu? Je! Ni tamaa ya mambo ya ulimwenguni huu, Je ni anasa? Biblia inasema:

1Petro 2:11 “Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho.

12 Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.”

Hivyo Fahamu kuwa Mungu anakupenda na ndio maana amekuonyesha ndoto za namna hiyo, basi usipuuzie sauti yake, anza sasa kumtazama YESU ikiwa bado upo mbali naye, Unachopaswa kufanya ni kutubu sasa mkabidhi yeye maisha yako upya, nenda kabatizwe kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako, kisha yeye mwenyewe atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu…nawe utakuwa na uhakika wa kuwa salama katika safari yako fupi iliyobakia hapa duniani… Aidha kama utakuwa upo tayari ndani ya Kristo na unajihisi huna kando lolote basi fahamu kuwa Mungu anataka uzidi kuiangalia safari yako zaidi kuliko kitu kingine chochote, kwasababu ipo thawabu kubwa amekuandalia mbele.

Ubarikiwe.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

MFALME ANAKUJA.

NINI MAANA YA KUISHI KWA KUUKOMBOA WAKATI?.

CHANZO CHA MAMBO.

UNYAKUO.

SIKU YA HUKUMU ITAKUWAJE?


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNA MIMBA.

Usipokuwa na uelewa wa kutosha  juu ya ndoto, unaweza ukajikuta unatoka nje ya kusudi la Mungu ambalo amekukusudia wewe uishi kwalo hapa duniani..

Na hiyo imewafanya watu wengi wazunguke huko na huko, kutafuta tafsiri ya ndoto zao..Lakini jambo la kwanza na la msingi sana kufahamu ni kuwa, tunapaswa kujua kuwa ndoto yoyote ni lazima iwepo katika mojawapo ya  makundi haya matatu:

> Kundi la kwanza ni ndoto zinazotokana na Mungu,

> Kundi la Pili ni ndoto zinazotokana na shetani,

> na kundi la tatu ni ndoto zinazotokana na mtu mwenyewe.

Sasa ndoto hizi zinazotokana na mtu mwenyewe huwa zinaathiriwa sana na mambo mbalimbali aidha kutokana na mazingira ya mtu yanayomzunguka au shughuli anazozifanya mara kwa mara,  au mambo anayoyawaza kila wakati..Na aina hii ya ndoto ndiyo inayochukua asilimia kubwa sana ya ndoto watu tunazoziota kila siku, naweza kusema hata asilimia 95 ya ndoto tunazoziota kila siku na hizi huwa hazina maana sana, lakini watu kwa kukosa ufahamu imefanya wahangaike kutwa kuchwa kutafuta tafsiri ya kila ndoto yanazoziota mpaka inawafanya kuwa watumwa wa ndoto…Kumbe kiuhalisia sio kila ndoto ina ujumbe wa kutufaa..

Hivyo mtu akishakuwa na uelewa wa namna ya kuzigawanya ndoto hizi katika makundi haya hatapata shida kuitafsiri ndoto yake..Hivyo nakuashuri pitia kwanza somo hili kisha ndio tuendelee.  >> NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI? 

Sasa ukiota una mimba: Ikiwa ndoto hiyo haitokani na shughuli zako mwenyewe au mazingira yanayokuzunguka, au mawazo unayoyawaza kila mara, kwasababu kumbuka ndoto kama hizi huwa zinawatokea mara nyingi wanawake, kwahiyo uwezekano wa kuangukia katika  kundi hilo la tatu la ndoto ni mkubwa kwasababu wanawake maisha yao tangu wakiwa watoto wanawaza siku moja ni kuwa na mtoto kwahiyo kuota wamebeba mimba si jambo la kushangaza, au utakuta mwingine maisha yake yote anatamani sana kuwa na mtoto, hana watoto, moja kwa moja mtu kama huyo ni rahisi kuota ni mjamzito au mwingine utakuta anaishi na mwanamke mjamzito  karibu na mazingira yake au jana amemwona mwanamke mmoja barabarani akipita akiwa mjamzito akajikuta usiku anaota kabeba mimba akadhani kuwa ndoto hiyo inamaana sana kwake..,

Ikiwa ni hivyo, basi zipuuzie tu, ni ndoto zinazokuja kutokana na mawazo yako. Hizo hazibebi ujumbe wowote kwako.

Lakini hapa tunadhania kuwa ndoto hiyo haijatoka katika vyanzo vya namna hiyo, 

Sasa fahamu kuwa tendo lolote kuchukua mimba liwe ni jema au liwe ni baya, liwe limekuja kwa  njia ya uzinzi au kwa njia ya haki ni lazima tu kiumbe kipya kije duniani mwisho wa siku hakuna namna!..Na kabla hakijaja lazima dalili Fulani zionekane…Hivyo kama ndoto yako  imekuwa ni ya kujirudia rudia basi itilie maanani zaidi kwasababu inaweza kuwa imebeba ujumbe kutoka kwa Mungu,..

Utakumbuka Farao alipoota ndoto ile ihusuyo miaka saba na njaa na miaka saba ya neema, ilikuja mara mbili, hata kama ilichukua taswira nyingine lakini ujumbe ulikuwa ni mmoja..ndipo akawa na uhakika wa kuwa ndoto ile ni ya kuizingatia..Vivyo hivyo na wewe ikiwa unaota mara kwa mara una mimba, ni mjamzito izingatie sana ndoto hiyo.

Kwahiyo jambo unalopaswa kufanya hapo kwa kuwa wewe ndiye unayeyafahamu maisha yako zaidi kuliko mtu mwingine yeyote , kaa chini kwa utulivu mwingi utafakari maisha yako na njia yako unayoiendea sasa hivi..iwe ni katika huduma yako, iwe ni katika familia yako, iwe ni katika shughuli yako unayoifanya sasa, kuna uamuzi uliuchua, au kuna jambo ulilifanya  ambalo hivi karibuni utakwenda kuona matokeo yake..

Hivyo kama ulimwomba Mungu juu ya kitu Fulani, kwa muda mrefu akupatie basi kaa katika matarijio ya kukipata, au kama ulijitaabisha katika kitu ambacho kwasasa faida yake haionekana kaa katika matarajio ya kukipata muda si mrefu..

Sara alikuwa katika matarajio ya kupata mtoto kwa muda mrefu, lakini wakati ulipofika malaika alimjia na kumwambia panapo wakati kama huu mwakani utalea mtoto..VIvyo hivyo na wewe kama upo katika mstari ulionyooka na Mungu wako basi tarajia Mungu kukupa kile ulichokuwa unakitafuta. Kwasababu mimba sikuzote ni matokeo ya ile mbegu iliyoingia ndani yako..Kama ni mbegu njema uliipanda basi utavuna kilicho chema.

Vile vile kama ulikuwa ni mwovu unafanya mambo yasiyompendeza Mungu nawe pia kaa katika matarajio ya kukipata hicho ulichokuwa unakifanya, ikiwa ulikuwa mchawi jiandae kuvuna matunda ya uchawi wako, ikiwa ulikuwa ni tapeli au mla rushwa jiandae kukumbana na ulichokihangaikia, kama ulikuwa ni mrushi vile vile jiandae kukutana na malipo yake hivi karibuni…

Usishangae kukutana na mabaya, kwasababu biblia inasema dhambi nayo huwa inapitia hatua hizo hizo mpaka kufikia mauti.

Yakobo 1:14 “Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.

15 Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.”

Zaburi 8:14 “Tazama, huyu ana utungu wa uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.”

Isaya 59:3 “Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong’ona ubaya.

4 Hapana adaiye kwa haki, wala hapana atetaye kwa kweli; hutumainia ubatili, hunena uongo; hupata mimba ya madhara, na kuzaa uovu.”

Hivyo kama unatenda maovu sasa, acha mara moja, Tubu dhambi zako, umegukie muumba wako YESU KRISTO kabla huo wakati wa mabaya haujafika, lakini kama unajijua upo katika njia iliyonyooka na umekuwa katika dua ya kumwomba Mungu kwa ajili ya kitu Fulani chema..Basi kuwa katika matarajio ya kukipata siku za hivi karibuni.

Ubarikiwe.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

USHUHUDA WA RICKY:

MTETEZI WAKO NI NANI?

KUOTA UNAPEWA PESA.

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Mtakatifu ni Nani?

 JIBU: Tafsiri ya kibiblia ya MTU MTAKATIFU ni tofauti na tafsiri ya kiulimwengu.
 
Ulimwengu unatafsiri Mtu mtakatifu ni mtu yeyote anayetenda matendo mema! mtu asiyetenda dhambi!..mtu anayekubalika na asiye na mawaa,
 
Lakini Biblia haitafsiri hivyo, kwasababu hakuna mwanadamu yeyote anayeweza kusimama mbele za Mungu kwa Matendo yake, na kujigamba mbele zake, wanadamu wote tunatenda dhambi kwa namna moja au nyingine aidha kwa kujua au kwa kutokujua. Na hivyo wakati unapojiona upo sawa, kumbe haupo sawa..wakati unajiona ni msafi kumbe ni mchafu n.k
 
Sasa Biblia inamtaja mmoja tu ambaye hakuwa na dhambi hata moja na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO peke yake! huyo ndiye biblia imemtaja kuwa mtakatifu, kwasababu alizaliwa bila dhambi na aliondoka duniani bila dhambi hata moja. Huyo peke yake ndiye anayeweza kusimama mbele za Mungu kwa matendo yake. Na ndiye pekee Mungu anayemwangalia kuwa ni Mtakatifu. Wengine wote tumetenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
 
Warumi 3: 23 “kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;
24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu”
 
Sasa Kwa kupitia huyo sisi wengine tutakaomwamini yeye ndio tutahesabiwa kuwa ni watakatifu,. Kama mtu yeyote hatakuwa ndani ya YESU hawezi kuonekana mtakatifu mbele za Mungu, hata kama anajiona ni mkamilifu kiasi gani, hata kama atatenda matendo ya haki kiasi gani…mbele za Mungu ni kama Uchafu tu!
 
Yesu ni kama vazi letu la nje sisi tulio wachafu! Ukimvaa Yesu mbele za Mungu hakuoni wewe, bali anamwona Yesu mwanawe ambaye ni Mtakatifu, hivyo na wewe unaonekana mtakatifu kwa ajili yake. Hiyo ndio maana ya NEEMA, Tunahesabiwa HAKI (yaani tunahesabiwa kuwa watakatifu) bure kwa njia tu ya kumwamini YESU KRISTO. Hapo ndipo mtu unaouna umuhimu wa YESU kuja duniani, Kwahiyo watakatifu ni wale walio ndani ya YESU tu!.
 
Hivyo wale wanaosema duniani hakuna watakatifu, ni kweli kwa mtazamo wa kibinadamu, lakini kwa mtazamo wa Mungu duniani wapo watakatifu maandiko yanatumabia hivyo katika:
 
Zaburi 16:3 “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao”.
 
Na hawa ndio wale wale wote walio ndani ya YESU KRISTO.
Sasa utauliza! Ina maana tukiwa ndani ya Yesu hata kama tukitenda dhambi za makusudi, tutazidi kuonekana NI watakatifu mbele za Mungu? jibu ni la! hakuna mtu yeyote aliye ndani ya Kristo, akawaza tena kutenda dhambi za makusudi, hakuna mtu aliye ndani ya Kristo akafanya uasherati, au akalawiti au akaua..ukiona mtu anatenda dhambi za Makusudi huyo bado hajawa ndani ya YESU, bado ni wa Ulimwengu. (Soma 1Yohana 3:9 na Warumi 6:1-2 )..
 
Kwasababu mtu yeyote aliyempokea YESU huwa anapokea hapo hapo kipawa cha Roho Mtakatifu, ambaye huyo kazi yake ni kumwongoza, kumfundisha na kumpasha habari ya mambo yote..kwahiyo mtu wa namna hiyo moja kwa moja atajikuta anatamani kupiga hatua mbele kila siku kuelekea ukamilifu na sio nyuma…Hata ile tamaa ya kufanya dhambi huwa inakufa yenyewe ndani yake, na hivyo hawezi kutenda dhambi mwenyewe za makusudi.
 
Ubarikiwe.

 


Mada Nyinginezo:

JEHANAMU NI NINI?

MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?

ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU.

USITAFUTE FAIDA YAKO MWENYEWE BALI YA WENGINE.

NJAA ILIYOPO SASA.

JIKANE NAFSI MTEULE WA MUNGU.


Rudi Nyumbani:

Print this post

CHAGUA UPANDE WA UZIMA.

Kama ukichunguza kwa makini, utaona Mungu kaumba kila kitu katika sehemu kuu mbili…Kwamfano utaona mtu katengenezwa kwa vipande viwili, kushoto na kulia, na vipande hivyo vinafanana..kila kimoja ni taswira ya mwenzake….Mkono wa kushoto unafanana na mkono wa kulia..lakini kimaumbile upo kinyume na mwenzake kadhalika mguu wa kushoto kimaumbile ni kinyume cha mguu wa kulia…
 
Na pia ukitazama, kuna pande mbili za mwangaza…Kuna upande wa Nuru, na upande wa Giza, hivi navyo kila kimoja ni kinyume na mwenzake…Ndio maana urefu wa usiku ni sawa na wa mchana.
 
Lakini pia zipo pande mbili nyingine zilizo pacha zenye sehemu kubwa sana katika maisha…ambazo nazo zinafanana isipokuwa kimaumbile ni kinyume na mwenzake…nazo si nyingine Zaidi ya UZIMA na KIFO. Hivi vitu viwili ili Maisha yawe na maana ni lazima viwepo. Wengi hawafahamu kuwa Kifo ni sehemu ya uumbaji wa Mungu…Na kifo Mungu hakukiumba kwa bahati mbaya au kwa makusudi mabaya…Wala giza Mungu hakuliumba kwa madhumuni mabaya…Giza Lilivyoumbwa lilikuwa na kazi yake maalumu ya kiMungu na takatifu….Kadhalika Kifo kilivyoumbwa kilikuwa na kazi yake ya muhimu na takatifu, kifo kisingekuwepo Maisha yasingekamilika hapa duniani…Ni kama tu mkono wa kushoto ulivyoumbwa!…huwezi kusema mkono wa kushoto hauna kazi yeyote katika mwili wako, au mguu wa kushoto! Kadhalika Kifo kiliumbwa kwa kusudi maalumu..
 
Kifo kisingekuwepo, zile mboga na zile mbegu za matunda Adamu na Hawa walizokuwa wanakula pale bustanini zingemea tumboni mwao, kwasababu zingekuwa bado na uzima, hivyo ilimpasa aliue kwanza lile tunda kwa kulichuma kutoka katika shina la mti kisha alile lote…kadhalika Adamu na Hawa wasingeweza kuilima na kuitunza bustani ambayo Mungu aliwaambia waiilime na kuitunza, kwasababu hata nyasi ambazo wangezilima, zingekuwa mbichi vile vile daima, zisingekauka, na kufa na kupotea… hivyo miti na nyasi zingeendelea kuota duniani na dunia nzima ingekuwa ni misitu tu, ambayo inaendelea kuota na kuota, hata maana ya kulima ingekuwa haipo tena…
 
Kwahiyo ili kuweka usawa..dunia iweze kujisafisha na kulimika na kutunzika, Bwana Mungu alikiumba Kifo… kwamba ni lazima vitu vingine vife ili viache nafasi ya vingine vipya kuja lakini kwa utaratibu…kuwe na mzunguko wa namna hiyo…mti atapata uzima, lakini utapata pia kifo pia..n.k
Sasa Mwanadamu hakuumbiwa hicho kifo tangu Edeni, yeye alipoumbwa alipewa zawadi ya upande mmoja tu wa UZIMA. Kwamba ataishi milele…Lakini baada ya anguko Adamu na Mkewe Hawa, kuvunja maagizo ya Mungu…Kifo nao kikawaingia ambacho hakikupasa kiwe kwao, uzio ukaondoka wa wao kutopenya upande wa kifo…jambo ambalo halikuwa mpango wa Mungu…kwamba Mwanadamu aje na kupita…hivyo nao wakawa wanakufa kama mimea.
 
Lakini Yesu Kristo alipokuja, kwa kupitia Msalaba alikikomesha kifo…alisema katika
Yohana 11:25 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; 26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele”.
 
Na Yesu Kristo huyo huyo ndio NJIA YA UZIMA..Hakuna mwanadamu yeyote, wala mungu yeyote anayeweza kutibu kifo! Wala awezaye kumfufua mtu…usidanganyike kwamba kuna mungu wa dini yeyote duniani, ambaye anaweza kutoa tumaini la ufufuo wa wafu! Hakuna! Ni Yesu Kristo pekee, ambaye alikufa na akafufuka! Huyo ndiye anayeweza kufufua wafu na kukikomesha kifo…Yeye peke yake ndiye aliyetabiriwa kuwa atamweka adui wa mwisho chini ya miguu yake, ambaye adui huyo ni mauti. (1 Wakorintho 15:25-26).
 
Na hakuna namna yeyote tunaweza kuishi katika haya Maisha kama hatutakuwa na uhakika wa UZIMA WA MILELE…hivyo huu ni wakati wetu wa chagua uzima au mauti, lakini kumbuka Itatufaidia nini tuwe matajiri wa kupindukia, halafu tujue baada ya miaka 70 tunakufa! Na biashara yetu itakuwa imeishia hapo?…Ni heri kutafuta kwanza uzima wa Milele, na hayo mengine yatakuja…Ni heri sasa kutafuta mabilioni na mabilioni ya miaka isiyoisha ya kuishi…na hayo mengine nitayafanya nikishapata hayo mabilioni ya miaka isiyoisha…ndani ya hayo mabilioni ya mamiaka nitakuwa na muda wa kutosha pengine hata kutafuta hizo mali, kama kutakuwa na kutafuta mali…Lakini kutafuta mali na huku nina miaka 70 tu ya kuishi na baada ya hapo ni ziwa la moto! Hiyo sio akili wala hekima.
 
Tafuta uzima wa milele! Ambao huo unapatikana kwa Yesu Kristo pekee! Baada ya kifo.
 
Bwana akubariki sana.

Mada Nyinginezo:

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

JE, KAMA HAUNA UBATIZO SAHIHI HAUWEZI KUWA NA ROHO MTAKATIFU?

SANDUKU LA AGANO LILIKUWA LINAWAKILISHA NINI KATIKA AGANO JIPYA?

BWANA YESU ALIKUWA NA MAANA GANI KUSEMA CHAKULA CHA WATOTO USIWAPE MBWA KATIKA MATHAYO 15:21-28?


Rudi Nyumbani:

Print this post

ASIYEFANYA KAZI NA ASILE

Biblia ina maanisha nini iliposema “Asiyefanya kazi na asile”?

Maandiko hayo yanapatikana kutoka katika kitabu cha 2 Wathesalonike 3:10 “Kwa kuwa hata wakati ule tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula”.

Mstari huo unatafsiriwa isivyopaswa na wengi wanaousoma..

Lakini mstari huo, unawahusu Wakristo! yaani watu wanaokusanyika  pamoja kanisani.

Katika Kanisa la Kwanza ulikuwepo utaratibu wa Waumini wote kufanya vitu kwa shirika,  ikiwemo kila mmoja kutoa sehemu ya mali zake na kuzileta kanisani ili zitumike katika kusaidiana pamoja na kunyanyuana..hususani kwa wale wenye mahitaji…. Hilo tunalisoma katika kitabu cha Matendo ya Mitume 2

Matendo 2:44 “Na wote walioamini walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika,

45 wakiuza mali zao, na vitu vyao walivyokuwa navyo, na kuwagawia watu wote kama kila mtu alivyokuwa na haja.

46 Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,

47 wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa”.

Sasa kilichokuwa kinatokea ni kwamba, kulikuwepo na watu wachache ambao, walikuwa na uwezo wa kwenda kufanya kazi, lakini kwasababu wanaona kuna ofa hiyo ya kugawiwa baadhi ya vitu bure ikiwemo chakula kanisani, wakawa hawaendi kufanya kazi, na kukaa kusubiria hilo fungu la kanisa lifike wapewe, hivyo hiyo ikawa inasababisha kanisa kulemewa, kwa kuongezeka kwa watu wasio na shughuli zao na huku bado wanataka kupewa fungu kutoka kanisani.

Nakala hii inataja unayopenda kwa bei ya chini sana. Chagua kutoka kwa usafirishaji wa siku hiyo hiyo, https://www.swisswatch.is/product-category/tag-heuer/ uwasilishaji wa gari au kuchukua agizo.

Sasa kulitatua tatizo hilo, Ndipo Mtume Paulo kwa Uwezo wa Roho akaagiza katika makanisa yote kwamba watu wakafanye kazi, wale chakula chao wenyewe ili kanisa lisilemewe…Wabakie tu wale wanaostahili kweli kweli kupata fungu kutoka kanisani…Na wengi wa hao wanaostahili walikuwa ni wajane wenye umri wa miaka 60 na kuendelea, tena wasio na ndugu wa kuwasaidia, wameachwa wenyewe, na pia wana rekodi nzuri ya kuifanya kazi ya Mungu kanisani…hao ndio waliostahili kupokea sehemu ya fungu… na watu wasio na uwezo kabisa..Lakini wengine waliosalia wasipewe kitu chochote hata chakula kutoka kanisani, wakafanye kazi ili kanisa lisilemewe.


Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

TUNAPOSEMA TUISHI KWA NENO, INAMAANISHA TUISHI MAISHA YA NAMNA GANI?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

JE! KUBET NI DHAMBI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Fahamu Namna ya Kuomba.

Wengi wa wanaompa Yesu Kristo maisha yao kwa mara ya kwanza, ndio maswali ya kwanza kwanza kujiuliza…nitaombaje! namna gani ya kuomba ili Mungu anisikie!

Kiuhalisia hakuna fomula fulani maalumu ya kuomba wala chuo fulani maalumu cha kujifunzia kuomba, Kwasababu Mungu wetu si mwanadamu wala hana udhaifu wa kutuelewa…Sehemu nyingine katika maandiko inasema “Baba yetu wa mbinguni anajua tujayohitaji hata kabla sisi hatujamwomba”

Unaona? kwa sentensi tu hiyo inaonesha kuwa Mungu si dhaifu wa kutuelewa sisi, kiasi kwamba tunahitaji course fulani tukasome ndipo atuelewe au kutusikia. Kitendo cha Kuwa mwanadamu tu! tayari Mungu anakuelewa kuliko unavyojielewa.

Hivyo mbele za Mungu, hatuendi na mpangilio mzuri wa Maneno kama tunavyoandaa hotuba kwenda kuisoma mbele za Mkuu wa Nchi…Isipokuwa tunakwenda na hoja zenye nguvu...Na hoja hizo ndio zile Bwana alizotufundisha wakati wa kuomba..katika Mathayo 6

“9 Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,

10 Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.

11 Utupe leo riziki yetu.

12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.

13 Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina”.

Kwamba tuombapo tuhakikishe tunaomba toba, na pia tuhakikishe nawasamehe wengine ili na sisi pia tusamehewe…Kadhalika tunapoomba tuhakikishe tunalitukuza jina la Yesu, na pia tunaomba ufalme wake uje…Na pia tusisahau kusema mapenzi yake yatimizwe…kwasababu sio kila kitu tunachokiomba ni mapenzi ya Mungu…Pia tunapaswa tumwombe Mungu atupe riziki zetu za kila siku, kama chakula, mavazi, malazi pamoja na fursa.

Kadhalika tunamwomba asitutie majaribuni hiyo inahusisha kumwomba Bwana atuepushe na yule mwovu katika maisha yetu, imani yetu, familia zetu, kazi zetu, huduma zetu za kila siku za kuwaleta watu kwa Kristo, tunazungukwa na nguvu za yule adui kila mahali, hivyo ni muhimu kumwomba Bwana atuepushe na mitego yake yote.

Na bila kusahau kurudisha utukufu, na kutambua kuwa uweza, nguvu na mamlaka vina yeye milele na milele…Hivyo hakuna kama yeye, na yeye ndiye mwanzo na mwisho.

Hizo ndio hoja zenye nguvu…usitazame ni maneno kiasi gani umekosea kuongea, wala ni lugha gani umezungumza wakati wa kuomba, hakikisha tu maombi yako yanahusisha hivyo vipengele.

Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye
namba hizi: +255789001312/ +255693036618


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU

FAIDA ZA MAOMBI.

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

TUMEAMBIWA TUNAPOSALI TUSIPAYUKE-PAYUKE, JE! HUKO KUPAYUKA PAYAUKA NDIO KUPI?

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?


Rudi Nyumbani:

Print this post