Kwa kiyahudi huitwa ‘Tevat’, ni chombo cha majini kilichotumika mahususi kwa ukombozi. Ni mfano wa meli iliyotumika kuokoa watu/wanyama kutoka katika maangamizi fulani. Kwamfano katika biblia tunaona Nuhu aliagizwa atengeneze safina, ambayo ataingia yeye pamoja na familia yake, na wanyama wa nchi.
Ukisoma Mwanzo 6-8, utapata kufahamu vipimo vya safina hiyo vilivyokuwa na vigezo vyake, japokuwa biblia haijatueleza mahususi umbo la chombo kile kilivyokuwa.
Lakini pia wakati Musa anazaliwa, tunaona wazazi wake walimtengeneze a naye kisafina kidogo, akafichwa ndani yake, ili kunusuriwa na maangamizi ya Farao.
Kutoka 2:1 Mtu mmoja wa nyumba ya Lawi akaondoka akaoa binti mmoja wa Lawi.
2 Yule mwanamke akachukua mimba akazaa mwana, na alipoona ya kuwa ni mtoto mzuri akamficha miezi mitatu.
3 Na alipokuwa hawezi kumficha tena, akampatia kisafina cha manyasi akakipaka sifa na lami, akamtia mtoto ndani yake, akakiweka katika majani kando ya mto.
Jambo la muhimu kufahamu ni kuwa safina hizo ilikuwa ni lazima zipakwe LAMI ndani na nje. Lami hizo ni mfano wa gundi nzito zilizopakwa, lengo lake likiwa ni kuzuia maji yasiweze kupenya sehemu yoyote ndani ya Safina, (Mwanzo 6:14, Kutoka 2:3). Safina zilikuwa na sifa kama za “nyambizi” tulizonazo sasa, ambazo hazihathiriwi na maji mahali popote ziwapo juu au chini ya maji.
Ni Kristo Yesu, yeye ndiye mwokozi wetu dhidi ya ghadhabu ya Mungu juu ya ulimwengu huu kwa wenye dhambi. Na DAMU yake ndiyo ile LAMI. Inayonyunyizwa kwetu sisi. Mtu yeyote ambaye hajamwamini Yesu, ni dhahiri kuwa ghadhabu ya Mungu ipo juu yake, hawezi kuiepuka. Kwasababu amekataa msamaha wa dhambi, tuliopewa bure kwa kifo chake pale msalabani.
Je! Unaichezea neema? Kumbuka ulimwengu huu unafikia mwisho. Kristo amekaribia kurudi, kuwanyakua watu wake. Je! Bado upo kwenye dhambi? Ikiwa utataka kuupokea wokovu leo bure, basi uamuzi huo ni bora kwako, Hivyo waweza, fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa sala hiyo ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JIHADHARI NA ROHO ZIDANGANYAZO.
Mvinje ni mti gani? (Mwanzo 6:14)
Unaweza kuuliza je! Mwamini anaweza kufungwa na adui?. Jibu ni ndio anaweza kufungwa. Utauliza tena, kama anafungwa sasa kazi ya Yesu msalabani ilikuwa ni nini ikiwa hajawekwa huru kweli kweli.
Jibu ni kwamba mwamini yeyote, hawezi kuwa na kifungo katika roho yake, yaani hawezi kufungwa roho aidha na mapepo, au wanadamu au chochote kile. Hawezi kuwa na laana yoyote ndani yake, aidha ya ukoo au ya mabibi. Kwasababu yeye ni mbarikiwa amewekwa huru na Yesu, na ndio kazi Yesu aliyokuja kuifanya kuwaweka huru walioonewa na ibilisi.Hivyo mtu yeyote aliyemwamini Yesu kwa ‘TOBA’, ubatizo na kupokea Roho. Huyo hana kifungo chochote kwasababu uhai wake unakuwa umefichwa ndani ya Kristo.
Lakini Shetani anauwezo wa kumzuia, katika mambo mengi, asipojua ni nini anapaswa afanye. Na hicho ndicho kifungo cha nje akifanyacho adui. Kukuzuia wewe mwamini, ndicho alichokifanya kwa Paulo wakati Fulani alipotaka kwenda kuhubiri injili kwa Wathesalonike akasema shetani alinizuia (1Wathesalonike 2:8).
Lakini pia tunamwona Mtume mwingine aliyeitwa Petro.
sasa hebu tuangalie kisa hiki kwenye maandiko Kilichomhusu yeye, tuone ni maeneo gani huwa adui analenga mahususi.
Matendo 12:4 Alipokwisha kumkamata, akamweka gerezani akamtia mikononi mwa vikosi vinne vya askari wanne wanne, wamlinde, akitaka baada ya Pasaka kumtoa na kumweka mbele ya watu.
5 Basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamwomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake.
6 Hata wakati Herode alipotaka kumtoa, usiku ule ule Petro alikuwa analala katikati ya askari wawili, amefungwa minyororo miwili; walinzi mbele ya mlango wakalilinda gereza.
7 Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye, nuru ikamulika kule chumbani, akampiga Petro ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi. MINYORORO YAKE IKAMWANGUKA MIKONONI.
8 Malaika akamwambia, Jifunge, KAVAE VIATU VYAKO. Akafanya hivyo. Kisha akamwambia, JIVIKE NGUO YAKO, ukanifuate.
9 Akatoka nje, akamfuata; wala hakujua ya kuwa ni kweli yaliyofanywa na malaika; bali alidhani kwamba anaona maono.
Umeona maeneo aliyofungwa Petro?
Wafungwa wa zamani, ilikuwa ili aitwe mfungwa, ni lazima mambo hayo matatu yakamilishwe juu yake; nayo ni.
1) Kufungwa, Minyororo mikononi
2)Kuondolewa Mavazi, na kupewa mengine ya gerezani.
3)Kuondolewa viatu miguuni
Na hiki ndicho kitu anachokifanya pia adui kwa mwamini. Anaanza kwa kukufunga mikono yako rohoni, kisha kuyaondoa mavazi yako, na mwisho viatu vyako miguuni. Baada ya hapo unakuwa tayari huna nguvu ya kumshinda.
Mikono ni nini?
Ni “maombi na mifungo”
Mikono ni viungo mama katika mwili. Husaidia viungo vingi kufanya shughuli zake. Silaha hushikwa na mikono, hata ngumi hurushwa kwa mikono. Hivyo adui anajua akizuia mikono yako. Huwezi kufanya lolote. Mikono ya mwamini, ni “maombi na mifungo”.
Mtu ambaye ni mwombaji, kiwango cha Roho ndani yake huwa ni kikubwa, na hivyo hakuna mnyororo wowote, unaoweza kumshika. Ndio maana utaona baada ya kanisa kumwombea Petro kwa juhudi, akafunguliwa. Vilevile Paulo na Sila walipokuwa wamefungwa kipindi kile, hawakulala tu, bali usiku wa manane walikuwa wakiomba, na matokeo yake vifungo vikawaachia.
Matendo 16:25 Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. 26 Ghafla pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa.
Umeona, maombi, huondoa minyororo mikononi. Kuwa mwombaji, uzishinde nguvu za mwovu. Shetani anawaogopa waombaji
Mavazi ni nini?
Ufunuo 19:8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu
Mavazi, ni matendo mema. Ukikosa matendo mema,(Utakatifu), si rahisi kumshinda adui, utakuwa mwamini asiye na matunda yoyote, itaishi tu kama mwanadamu ambaye anamapungufu ya akili rohoni, hutaweza kufanya lolote.Ndani una makunyanzi, mawaa, ambazo katika hizo shetani anakuwa na haki ya kukulaumu.
Ishi kama mkristo, ukiwa rafiki wa dunia, fahamu kuwa unajifanya adui kwa Mungu moja kwa moja. Nuru yako isipoangaza nje, huwezi mshinda shetani. Ni lazima uwe kikombe safi, nje na ndani. Huwezi kusema umeokoka halafu matendo yako hayaendani na imani yako.Unajidanganya, bado hujaifahamu neema ya Mungu.
Miguu ni nini?
Waefeso 6:14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani, 15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani.
Miguu ni utayari, wa kuhubiri. Adui anapenda kukawiisha nia za watu, kwa kuwavuta katika mambo yao mengine, na kusahau yaliyo ya msingi kwao, ndio hapo atawasonga kwa anasa, udanganyifu wa mali, na shughuli za ulimwengu huu. Na mwisho wa hapo wanabakia kuwa hawana matunda.
Hivyo ndugu uliyeokoka, usiruhusu adui kukuzuia popote. Jijengee desturi ya kuwa mwombaji wa kila siku. Mikono yako isifungwe. Penda kuishi maisha matakatifu, vazi lako lisibadilishwe, kuwa tayari kuhubiri injili wakati wowote, ukifaao na usiokufaa, epuka udhuru wa mwili au kazi, pinga sana hapo jiwekee ratiba yako, ili upate sehemu ya kuwaeleza wengine habari za Yesu Kristo anayewaokoa wanadamu.
Tukizingatia hayo. Tutakuwa tumemshinda shetani ndani na nje. Hatujafungwa ndani wala nje.
Bwana akubariki
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?
Kongwa ni nini kwenye biblia?(Wagalatia 5:1)
Swali: Njia ya msalaba ni nini na Ipi historia ya njia ya msalaba?
JIBU..
Njia ya Msalaba ni Desturi iliyoanzishwa na kanisa Katoliki ambapo waumini wanapita katika mitaa ile Bwana YESU aliyosulubiwa, kuanzia alipotoka kwa Pilato mpaka mwili wake ulipowekwa kaburini.
Kulingana na kanisa Katoliki, kuna vituo 14 ambavyo Bwana YESU alipitia, ambapo kila inapofika Ijumaa kuu (ile ya pasaka) wakatoliki hupita katika vituo hivyo huko YERUSALEMU kuanzia mahali pajulikanapo kama “ngome ya Antonia” mpaka “kanisa la Roma la ufufuo” (karibia na mahali ambapo Kaburi la Bwana YESU lilikuwepo)..matembezi hayo ni ya mita 600.
Na wale wasiokuwepo Israeli basi watapita karibu na picha kumi na nne (14) zilizochorwa katika kuta za makanisa hayo ya Roma na kusema baadhi ya sala.
Vifuatavyo ni vituo hivyo kulingana na kanisa katoliki.
1. Yesu anahukumiwa kuuawa.
2. Yesu anapewa msalaba na maaskari wa kiroma
3. Yesu anaanguka chini kwa mara ya kwanza.
4. Yesu anakutana na mama yake (Mariamu)
5. Simoni Mkirene anashurutishwa kuubeba msalaba wa Yesu.
6. Veronika anapangusa damu katika uso wa Bwana Yesu.
7. Yesu anaanguka kwa mara ya pili.
8. Yesu akutana na wanawake wa Yerusalemu.
9. Yesu anaanguka mara ya tatu
10. Yesu anavuliwa mavazi yake
11. Bwana Yesu anagongomelewa msalabani
12. Yesu anaisalimu roho yake
13. Mwili wa Bwana Yesu unaondolewa msalabani.
14. Mwili wa Bwana Yesu wawekwa kaburini.
Hivyo ndivyo vituo 14, Bwana Yesu alivyovipitia kulingana na kanisa katoliki.
Lakini vituo baadhi hapo hatuvioni katika maandiko, kwamfano kituo cha 3,7 na 9 cha Bwana YESU kuanguka chini mara ya kwanza, na ya pili na ya tatu havipo katika maandiko..
Vile vile kituo cha 6 kinachomtaja Veronika kufuta damu katika uso wa Bwana YESU hakipo katika biblia..na hata kituo cha 4 cha Bwana YESU kukutana na mama yake hakipo katika biblia!.
Hivyo kama habari hizo hazipo katika biblia hatupaswi kuziamini wala kuzishika kwani huenda ni habari za kutungwa! au zimetolewa katika vyanzo visivyo sahihi, ambavyo havijahakikiwa na Roho Mtakatifu.
Kitabu cha biblia chenye vitabu 66, hiyo ndiyo iliyohakikiwa na Roho Mtakatifu lakini vitabu vingine nje na hivyo vya kwenye biblia ni potofu na vina udanganyifu.
Na Zaidi hatujapewa amri ya kuadhimisha vituo vya Bwana YESU alivyopitia, ndio! Tunaweza kutafakari lakini si kufanyia ibada,..sala za namna hiyo ni ibada za sanamu, kwani zinamfanya mtu aanguke katika zile picha au katika ile mitaa huko Yerusalemu, jambo ambalo ni machukizo.
Kufahamu njia ya Msalaba hasa kibiblia ni ipi fungua hapa >>> NJIA YA MSALABA
Shalom..
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.
Matuoni ni nini katika biblia?
MSALABA NI ZANA YA UJENZI WA MAISHA YAKO.
UTHAMINI WITO WA PILI WA YESU ZAIDI YA ULE WA KWANZA.
Swali: Muujiza wa kwanza wa Bwana YESU ulikuwa ni upi?
Jibu: Mwujiza wa kwanza wa Bwana YESU ni ule wa Kana ya Galilaya, ambapo aligeuza maji kuwa Divai.
Yohana 2:1 “Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.
2 Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.
4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia.
5 Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni.
6 Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu.
7 Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu.
8 Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka.
9 Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi,
10 akamwambia, Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa.
11 MWANZO HUO WA ISHARA YESU ALIUFANYA HUKO KANA YA GALILAYA, akaudhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini”.
Mstari huo wa 11 unatudhihirishia wazi kuwa hiyo ndio iliyokuwa ishara ya kwanza kufanywa na BWANA YESU mbele ya wanafunzi wake.
Sasa kujua kwa mapana ujumbe uliopo nyuma ya muujiza wa kwanza wa Bwana YESU wa Kana ya Galilaya fungua hapa >>Kwanini Bwana YESU ageuze maji kuwa Divai? Na ni ujumbe gani tunapata?
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NI NINI BWANA ANATAKA KUTOKA KATIKA MUUJIZA ALIOKUFANYIA?
JE UMEJIANDAA KUTIMIZA UNABII UPI?
Kumaka ni nini katika biblia? (Mathayo 8:27)
Swali: Kuna nini katika Divai mpaka Bwana YESU ayageuze maji kuwa Divai?
Jibu: Hakukuwa na chochote maalumu au cha kipekee katika Divai.
Sababu ya Bwana YESU kuyageuza maji kuwa Divai na si kinywaji kingine ni kwasababu ndicho kinywaji kilichokuwa kimepunguka pale! (Kulingana na zile taarifa alizoletewa na mama yake).. Endapo kama ingekuwa ni chakula ndicho kilichopunguka basi Bwana YESU angefanya muujiza wa chakula kuongezeka cha kuutosha ule umati wote, huenda angefanya muujiza kama ile ya Mikate na Samaki, alipolisha maelfu ya watu. (Marko 6:38-44 na Luka 9:13-17).
Sasa kabla ya kuangalia ni ujumbe gani tunapata kwa mwujiza ule, hebu kwanza tuangalie matokeo ya kukosa Divai katika ile Harusi.
Kufahamu kwa kina matumizi ya Divai katika biblia fungua hapa >>MATUMIZI YA DIVAI.
Kulingana na Desturi za kiyahudi ilikuwa ni aibu kubwa sana arusi ikose Divai, au chakula…Hivyo ni aibu kubwa sana kwa wanafamilia, sawasawa tu sasa sherehe ikipungukiwa na chakula inakuwa ni aibu kubwa kwa walioandaa na huzuni na karaha!..
Sasa kitendo cha Bwana YESU kubadili yale maji na kuwa Divai, tena yenye kuwatosha watu wote ni kitendo KILICHOWAONDOLEWA AIBU WANA ARUSI NA WAZAZI.. vile vile ni kitendo kilichowaondolewa huzuni, na masononeko na fadhaa.. na ni kitendo kilichowapa heshima. Ndio maana utaona yule mkuu wa Meza alimfuata Bwana arusi kumsifu badala ya Bwana YESU.
Sasa ni ujumbe gani mkuu tunaupata hapo?
Ujumbe mkuu si upekee wa Divai.. bali ni Faida ya BWANA YESU ndani yetu au katikati yetu. Kuwa yeye anapoingia ndani yetu anazichukua aibu zetu, na fadhaa zetu na masikitiko yetu, na kutuheshimisha na kutuondolea aibu zetu..
Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.
5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.
Unauona upendo wa YESU kwetu pale tunapomkaribisha na kumtwika fadhaa zetu?.. Wale wanaharusi waliona thamani ya YESU na kumwalika katika sherehe yao, na pale walipopungukiwa ndipo Kristo alipozuchukua fadhaa zao na aibu yao..
Wenye harusi , (wao hawakumwalika Bwana kwasababu walijua divai itaisha ili baadaye wamwite awageuzie maji kuwa Divai).. La! Ile ilitokea tu kama dharura na ndipo Bwana akafanya miujiza.. Wao lengo lao kubwa lilikuwa ni kumwitaji YESU ndani ya harusi yao, na si wamtumie.
Na sisi leo hatupaswi kumfuata BWANA YESU kwasababu tu tunataka uponyaji, au heshima au kuinuliwa kimaisha (watu wote waliomfuata Bwana YESU kwa haja kama hizo aliwakimbia Soma Yohana 6:25-26)..Lakini tumfuate Bwana YESU kwasababu tunataka uzima kwanza, na kuyafanya mapenzi yake na hayo mengine yawe ni dharura tu, kama wale waliomwalika.
Ukishahikiki kwamba uzima upo ndani yako, ndipo tumtwike hayo mengine..
1Petro 5:7 “huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu”.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Manabii walisema “Neno la Mungu likanijia” ..Maana ya hili neno ni nini?.
Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.
WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.
Bwana YESU KRISTO alizaliwa katika Nchi/Taifa la ISRAELI, lililopo mashariki ya kati. Na mji aliozaliwa ni Bethlehemu ambao ulikuwa katika urithi wa kabila la YUDA.
Mika 5:2 “Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele”.
Pamoja na kwamba Bwana YESU alizaliwa Bethlehemu kulingana na unabii huo wa Mika, lakini hakulelewa katika huo mji wa Bethlehemu badala yake wazazi wake waliishi mahali palipojulikana kama NAZARETI, Mji mdogo sana uliopo kaskazini mwa Taifa hilo la Israeli, na huko ndiko Kristo alikokulia, ndio maana mahali pengine anajulikana kama Mnazorayo (yaani mtu wa Nazareti).
Mathayo 2:23 “akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo”.
Lakini pia Mji huo wa Nazareti ulikuwa ndani ya Wilaya iitwayo Galilaya, wakati mji wa Bethlehemu aliozaliwa Bwana YESU ulikuwa katika Wilaya iliyoitwa Yudea au Uyahudi.
Wilaya ya Galilaya ndio uliyojumuisha miji mingine midogo midogo kama Kapernaumu na Korazini na Bethsaida, ambapo wanafunzi wengi wa Bwana YESU walitokea katika hiyo miji, na ndio miji ambayo iliona miujiza mingi ya Bwana YESU lakini haikutubu (Mathayo 11:21)…. Wakati Wilaya ya Uyahudi ndio iliyobeba miji ya Bethlehemu pamoja na Yerusalemu.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba BWANA YESU alizaliwa Bethlehemu ya Uyahudi na kulelewa Nazareti ya Galilaya, na alifia YERUSALEMU na kuzikiwa hapohapo, na kufufuka hapo hapo YERUSALEMU. Na sasa yupo hai na atarudi tena mara ya pili na siku hizo zimekaribia kulingana na unabii wa biblia.
Je umeokoka?
Bwana YESU ANARUDI.
Kama unatamani kuokoka basi fuatiliza sala hii >>KUONGOZWA SALA YA TOBA
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Bwana Yesu alizaliwa mwaka gani?
Raheli aliwalilia vipi watoto wake?
BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA
Jibu: Turejee,
Walawi 19:32 “Mwondokeeni mtu mwenye mvi; heshimuni uso wa mtu mzee; nawe mche Mungu wako, Mimi ndimi Bwana”.
Maana ya kumwondokea ni “kumsogelea au kumkaribia ili kumsikiliza”. Hivyo biblia iliposema mwondokeeni mtu mwenye mvi, maana yake “tumsogeleeni mtu mwenye mvi na kumsikiliza”..
Na kwanini tumsogelee mtu/watu wenye mvi?..Ni kwasababu “kuna hekima katika wazee, kwani wameishi muda mrefu na kukutana na mengi na kujifunza mengi”. (wazee walio ndani ya KRISTO).
Ayubu 12:12 “Wazee ndio walio na hekima, Na katika kuishi siku nyingi iko fahamu”.
Soma pia Ayubu 32:6-7 na Mithali 23:22.
Hivyo ukitaka mashauri sahihi kuhusu maisha basi watafute walio na mvi, (yaani wazee) walio ndani ya Kristo, watakuambia au ukutahadharisha na mengi…
> Vile vile ukitaka maarifa na ushauri sahihi kuhusu ndoa, kazi au elimu watafute wenye mvi walio ndani ya KRISTO watakushauri na kukutahadharisha mambo yaliyo sahihi na yale yasio sahihi.
> Vile vile ukitaka mashauri sahihi ya kiroho watafute wenye mvi za kiroho watakushauri mambo sahihi.
Na mambo mengine yote ni hivyo hivyo, wenye mvi wanafahamu Zaidi kuliko vijana.
Lakini hasemi tu! Kumwondokea mwenye mvi… bali pia anasema “heshimuni uso wa mzee”. Maana yake mzee/wazee wanapaswa kuheshimiwa sana…. ni kosa kumvunjia mzee heshima, hata kama kafanya jambo lisilo sahihi mbele ya macho yako. Si ruhusa kumkemea mzee kama wanavyokemewa vijana au watoto.
1Timotheo 5:1 “Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu;
2 wanawake wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote”.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
TUTAMKARIBIA MUNGU KWA IDADI YA MVI ZETU ROHONI.
HATA WAKATI WENU WA MVI NITAWACHUKUENI. (Isaya 46:3)
UTAKAPOKUWA MZEE, UTAINYOSHA MIKONO YAKO. NA MWINGINE ATAKUFUNGA
WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?
Huwenda ukawa unajiuliza, Bwana Yesu alikuwa na maana gani kusema, Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru? . Je huko gizani ni wapi, na sirini ni wapi? Je yeye huwa anazungumza gizani.
Mathayo 10:26 “Basi, msiwaogope, kwa maana hakuna neno lililositirika, ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa, ambalo halitajulikana.
27 Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba”
JIBU: Ni vema tukaifahamu tabia ya Bwana wetu Yesu Kristo, katika kufundisha jinsi ilivyokuwa alipokuwa anazungumza na watu mbalimbali. Yapo maneno au mafundisho au mafunuo aliyoyaweka wazi kwa watu wote, lakini yapo ambayo hakuyaweka wazi kwa kila mtu.
Mahubiri yake mengi aliyazungumza hadharani, lakini mengine haikuwa hivyo, kwamfano upo wakati alijitenga akapanda milimani, na wale waliomfuata ndio aliowafundisha (Mathayo 5:1), wakati mwingine aliingia nyumbani, hakutana kujulikana kwasababu alikuwa akitaka kuwafundisha wanafunzi wake tu, peke yao (Marko 9:29-31), wakati mwingine aliwaponya watu akawataka wasimdhihirishe, (Marko 1:44), wakati mwingine alijifunua utukufu wake, kwa wale tu waliokwenda naye kuomba mlimani, uso wake ukawa unameta meta, kama jua, alipomaliza akawakataza wasimwambie mtu, mpaka atakapofufuka (Mathayo 16).
Hayo ni mazingira mbalimbali, ambayo Yesu alisema nao bila kujulikana na kila mtu, Sasa mazingira hayo ndio aliyaita “Gizani, au sirini”
Hii ni kufunua kuwa hata sasa Yesu anazungumza hadharani, lakini pia anazungumza sirini. Na yale ya sirini huwa ni makubwa zaidi na ndio maana haitaji yajulikane na kila mtu.
Watu wengi wanamsikia Yesu hadharani, lakini hawamsikii sirini. Hadharani, ni pale unaposikia mafundisho kanisani, mahubiri, semina, mkutano n.k. Ni kweli Yesu atakufundisha mengi kupitia matumishi wake mbalimbali, na yatakujenga na ni muhimu ufanye hivyo.
Lakini lazima pia sirini pa Yesu uwe napo.
Je hapo ni wapi?
“Ni eneo lako la utulivu la kimaombi na kutafakari”.
Ni muhimu sana kila mkristo, awe na wakati wake maalumu kila siku alioutenga wa kuzama uweponi, katika maombi, kusoma Neno na kutafakari shuhuda za Mungu maishani mwake. Ni muhimu sana.
Zaburi 91:1 AKETIYE MAHALI PA SIRI PAKE Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.
Mathayo 6:6 Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
Hapa Yesu anataka uingie gharama, kidogo ili umsikie, au akuhudumie, au akufundishe. Ndio mfano wa wale waliomfata milimani. Vivyo hivyo na wewe, ingia gharama ya kudumu uweponi mwa Mungu. Ukiona mchana pana usumbufu, usiku ni muda mzuri sana, kuamka, tena masaa yako kadhaa kila siku,. Kumpa Bwana nafasi ya kukufundisha.
Ukiwa wa namna hii, hutamkosa Bwana popote pale. Kaa mahali pake pa siri. Kwasababu yupo pia sirini, akupe mambo mambo utayasema hadharani wakati fulani.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Neno sulubu huzaa kusulibisha/kusulubisha,
Maana ya Sulubu, ni kuadhibisha kwa kuning’iniza kwenye mti wa msalaba, au nguzo iliyonyooka, kwa kufungwa au kugongelewa miguu na mikono, na kuacha hapo mpaka ufe.
Hii ni aina ya adhabu ya kifo, ambayo ilitumika zamani, kwenye falme zilizokuwa na nguvu na katili kama Rumi.
Watu walioshitakiwa kwa makosa makubwa ikiwemo uhaini, au uuaji, uvunjaji amani, hawakupewa adhabu ya kawaida ya kifo kama vile kukatwa kichwa na kufa mara moja,. Bali walipewa adhabu kali kama hii, lengo lake ni kumfanya Yule mshitakiwa kupitia mateso makali ya muda mrefu kabla ya kufa, kwasababu, baada ya kuning’inizwa kwake pale msalabani itamchukua siku tatu mpaka wakati mwingine wiki hadi kufa. Hivyo kipindi chote hicho unatakuwa unateseka tu pale mtini.
Hiyo ndio adhabu waliyoichagua kwa mwokozi wetu Yesu Kristo, ambaye hakuwa na hatia yoyote, wala kosa, jambo ambalo hata mtawala yule Pilato alilishuhudia kuwa hakukuwa na uovu wowote ndani yake. (Luka 23:4). Lakini kwasababu ilipasa maandiko yatimie ili sisi tupate ukombozi mkamilifu, ndio maana ilimpasa Yesu aadhibiwe vikali, ili mimi na wewe tupokee ONDOLEO LA DHAMBI. Kwa kifo chake.
Gharama aliyoilipa ni kubwa sana, kusulubiwa uchi wa mnyama, bila nguo, kudhalilishwa na kupigwa, na kuharibiwa mwili wote. Ni kwasababu mimi na wewe tupokee msamaha wa dhambi, tuepushwe na hukumu ya milele ya jehanamu ya moto.
Ndio maana maandiko yanasema..
Waebrania 2:3 sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia.
Je! Umempokea Yesu maishani mwako?
Ikiwa ni la! Basi waweza kufanya hivyo sasa, kwa kubofya hapa ili upate mwongozo wa sala hiyo. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
ALIFANYIKA SADAKA KWA AJILI YETU!
Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?
Nyakati tunazoishi ni za hatari kubwa, zaidi hizo zinazokuja wakati si mwingi ndio za hatari mno. Watu wengi hawajui kuwa mwisho umekaribia sana, dunia imekwisha, na kwamba SIKU YA BWANA, ipo mlangoni.
Siku ya Bwana ni nini?
Siku ya Bwana ni kipindi fulani maalumu ambacho Mungu amekiandaa ili kuuharibu huu ulimwengu pamoja na watu wote waovu waliopo duniani, na mifumo yao mibovu. Na hiyo itakuja baada ya kanisa la Kristo kunyakuliwa
Tukisoma katika kitabu cha Sefania tunaelezwa kwa urefu juu ya sifa kuu za siku hiyo itakavyokuja.
Ametaja sifa zake sita (6), kwa kuziita “siku ya”..”siku ya”…”siku ya”
Tusome..
Sefania 1:14-16
[14]Hiyo siku ya BWANA iliyo kuu i karibu; I karibu, nayo inafanya haraka sana; Naam, sauti ya siku ya BWANA; Shujaa hulia kwa uchungu mwingi huko!
[15]Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu,
[16]Siku ya tarumbeta na ya kamsa, Juu ya miji yenye maboma, Juu ya buruji zilizo ndefu sana.
Ghadhabu ni zao la hasira, na hasira hufuatana na mapigo. ndio hapo tunaposoma kitabu cha ufunuo 16, tunaona kipindi hicho kikifika wale malaika saba watavimimina vile vibakuli vyao saba vya ghadhabu ya Mungu juu ya nchi. na kitakachofuata kwa tendo lile ni mapigo, ndio hapo utaona majipu mabovu, yanawatokea wanadamu, na tena jua linashushwa na kiwaunguza watu, mpaka wanafikia hatua ya kumtukana Mungu.
Ufunuo 16:8-9
[8]Na huyo wa nne akakimimina kitasa chake juu ya jua, nalo likapewa kuwaunguza wanadamu kwa moto.
[9]Wanadamu wakaunguzwa maunguzo makubwa, nao wakalitukana jina la Mungu aliye na mamlaka juu ya mapigo hayo; wala hawakutubu wala kumpa utukufu. .
Dhiki na fadhaa ni taabu ambazo mtu anazipata hususani kutoka katika mazingira ya nje. Ukiendelea kusoma sura ile ya 16, utaona mito, chemchemi na bahari zote zinageuzwa kuwa damu, wanadamu wanakosa maji. hofu na mashaka ya mabadiliko ya nchi. Duniani hatakuwa ni mahali penye utulivu, tengeneza picha unaishi katika dunia ya namna hii, utastahimili vipi. Bwana anasema wanadamu watafuta kifo, lakini kifo kitawakimbia.
Ufunuo 16:3 Na huyo wa pili akakimimina kitasa chake juu ya bahari, ikawa damu kama damu ya mfu, na vitu vyote vyenye roho ya uhai katika bahari vikafa.
4 Na huyo wa tatu akakimimina kitasa chake juu ya mito na chemchemi za maji; zikawa damu. 5 Nami nikamsikia malaika wa maji akisema, Wewe u mwenye haki, uliyeko na uliyekuwako, Mtakatifu, kwa kuwa umehukumu hivi;
6 kwa kuwa walimwaga damu ya watakatifu na ya manabii, nawe umewapa damu wainywe; nao wamestahili
Sio tu mapigo na dhiki, lakini pia kuharibiwa kwa huu ulimwengu na mifumo yake kutafuata, kwasababu biblia inasema siku hiyo kutatokea tetemeko kubwa la ardhi ambalo halijawahi kutokea tangu dunia kuumbwa, mpaka visiwa kuhama, inasema moto utatokea kuharibu huu ulimwengu, mfano wa sodoma na gomora na mfano wa kipindi cha gharika.
2 Petro 3:10-12
[10]Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.
[11]Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,
[12]mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka?
Giza na utusitusi unaozungumziwa hapa ni ule wa rohoni. ni kipindi ambacho watu watautafuta uso wa Mungu lakini hawatauona, ndio maana Yesu alisema imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyetupeleka maadamu ni mchana, usiku waja asioweza mtu kufanya kazi. watu watamwita Mungu, lakini hakutakuwa na majibu yoyote.
Mithali 1:27 Hofu yenu ifikapo kama tufani, Na msiba wenu ufikapo kama kisulisuli, Dhiki na taabu zitakapowafikia. 28 Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika; Watanitafuta kwa bidii, wasinione. 29 Kwa kuwa walichukia maarifa, Wala hawakuchagua kumcha Bwana. 30 Hawakukubali mashauri yangu, Wakayadharau maonyo yangu yote
Vilevile kwa jinsi dunia hii itakavyoharibiwa jua na mwezi na nyota vitazuiliwa.. duniani kutakuwa na giza ambalo halijawahi kutokea, na hayo ndio yatakuwa yale mapigo ya mwisho mwisho kabisa yatakayokuwa yanaukaribisha ujio wa pili wa Yesu duniani.
Vilevile wingu zito litatandaa angani, mawe mazito yatashuka duniani kama talanta, jiwe lenye uzito wa kg 34, hatujui itakuwa ni mvua ya namna gani, hiyo.
Ufunuo 16:18-21
[18]Pakawa na umeme na sauti na radi; na palikuwa na tetemeko la nchi kubwa, ambalo tangu wanadamu kuwako juu ya nchi hapakuwa namna ile, jinsi lilivyokuwa kubwa tetemeko hilo.
[19]Na mji ule mkuu ukagawanyikana mafungu matatu, na miji ya mataifa ikaanguka; na Babeli ule mkuu ukakumbukwa mbele za Mungu, kupewa kikombe cha mvinyo ya ghadhabu ya hasira yake.
[20]Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena.
[21]Na mvua ya mawe kubwa sana, ya mawe mazito kama talanta, ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu. Wanadamu wakamtukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe; kwa maana pigo lake ni kubwa mno.
Kamsa ni kelele za vita. Maana yake katika kipindi hicho cha siku ya Bwana, vita vitakuwepo, ndio ile vita ya mwisho ijulikanayo kama Harmagedoni.Mataifa yote yatahusika. lakini Bwana awataua watu wengi sana. damu nyingi sana zitamwagika. ni nyakati ambayo hakutakuwa na shujaa, kila mtu ataomboleza mpaka mashujaa, wafalme na matajiri wote hao watalia sana, pesa zao hazitawasaidia wataomba milima iwaangukie wafe haraka, kuliko kushuhudia huo mfululizo wa mapigo ya Mungu mwenyezi.
Na ndio maana ukimalizia kusoma mistari inayofuata pale kwenye kitabu cha Sefania anasema
Sefania 1:17-18
[17]Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda BWANA dhambi; na damu yao itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi.
[18]Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya BWANA; bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu wote wakaao katika nchi hii, naam, ukomo wa kutisha.
Ndugu yangu, ikiwa unyakuo ukipita leo, fahamu haya utayashuhudia, wakati huu si wa kumbelelezewa wokovu, ni kuamka na kuikimbilia neema, nyakati mbaya zimekaribia, haya mambo ya duniani yatakufikisha wapi? uhai wako umefichwa wapi? Ukifa leo huko uendako utakuwa mgeni wa nani.Kwasababu huko nako kuna mateso makali vilevile kama hapa.
Embu dhamiria kutubu na kumgeukia Bwana Yesu leo, akupe msamaha wa dhambi bure. Hukumu ya Mungu inatisha.
Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu maishani mwako. Na unatamani leo Yesu akutue hiyo mizigo ya dhambi. Basi waweza kusali sala hii kwa imani. Ukijua Kristo wakati wote yupo kutuokoa. Kumbuka kinachotangulia ni kuamini. Kisha ndipo kukiri.
Hivyo
Hapo ulipo piga magoti, kisha dhamiria moyoni mwako kuyasema maneno haya, na moja kwa moja leo, utapokea msamaha wa dhambi zako hapo hapo ulipo,
Sema.
Ee Bwana Yesu asante kwa kuja kwako duniani, kutukomboa sisi wanadamu tuliokuwa tumepotea, kwa kifo chako pale msalabani na kufufuka kwako. Ninaamini kuwa wewe ndio Bwana na mwokozi, nami napokea neema uliyonipa bure ya ondoleo la dhambi, tangu leo ninakubali kufanyika mwana wako, na kugeuka kuacha njia mbaya za kale. Asante kwa kuwa unanipa nguvu hiyo na kuliandika leo jina langu katika kitabu cha uzima. Nami nafanyika kiumbe kipya. Asante kwa kunipokea, asante kwa kunisamehe, Asante kwa kunifanya mwana wako. Ninaomba nikiamini katika jina la Yesu Kristo Amen.
Basi ikiwa umesema sala hiyo toka moyoni kwa imani. Tayari umeshaupokea wokovu. Na hivyo hatua zilizobakia kwako ili kuitimiza haki yote, ni wewe kubatizwa. Tafuta mahali wabatizwapo kwa maji tele, na kwa jina la Yesu Kristo. Ikiwa utahitaji msaada pia waweza kuwasiliana nasi kwa namba zetu chini.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)