Category Archive Home

IKIWA MWENYE HAKI AKIOKOKA KWA SHIDA, MWENYE DHAMBI ATAONEKANA WAPI?

Siku ile unapofanyika kuwa mtoto wa Mungu, yaani siku ile unayotubu kwa kuamua kabisa kuyasalimisha maisha yako kwa Bwana Yesu, siku ambayo unageuka na kusema maisha yangu sasa ni kwa Bwana, ya kale yamepita. Na ukazingatia kufuata maagizo yote yanayoambata na wokovu wako yaani kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO. siku hiyo ambayo Roho wa Mungu anaangia ndani yako na kukushuhudia kuwa wewe ni mwana wake. Basi kuanzia siku hiyo unauhakika kuwa jina lako lipo katika kitabu cha uzima na umevuka toka mautini na kuingia uzimani (1Yohana 3:14), na kufanyika kuwa mrithi wa ahadi zote za Mungu.

Lakini ili uonekane kuwa umestahili kupokea URITHI huo utakaokuja kufunuliwa kwa wana wote wa Mungu siku ile ya mwisho ya unyakuo, ni lazima kwanza kwa namna moja au nyingine upitie njia kama aliyopitia BWANA YESU KRISTO alivyokuwa hapa duniani. Ni lazima Bwana aisafishe kwanza nyumba yake, na mambo yote machafu. Hatuwezi kuwa warithi na tabia zetu chafu tulizotoka nazo huko ulimwenguni. Hatuwezi kuwa wasengenyaji, halafu kule tukawe warithi wa uzuri Mungu aliwaandalia watakatifu wake, hatuwezi tukawa na viburi halafu tuingie uzimani hivi hivi kiwepesi, hatuwezi tukawa watukanaji, wawakaji wa tamaa, waabudu sanamu, waongo halafu tukamilikishwe mambo matukufu makuu namna ile kiwepesi wepesi tu. Ni sharti kwanza hayo yote yasafishwe. Na yakishasafishwa sasa hatuna budi kukionja kikombe cha mateso kama kile alichokinywa Bwana.

Kama YESU alikuwa ni mkamilifu bila dhambi yoyote [yeye aliyekuwa mti mbichi] lakini alionja sehemu ya HUKUMU YA MUNGU kwa ajili ya makosa yetu, itakuwaje kwa sisi tulio miti mikavu?. Hatuwezi kuikwepa hukumu yake. Hivyo kwa mtu yeyote aliye mwaminio wa kweli HUKUMU hii pia lazima ipite juu yake. Ambayo hiyo inakuja hapa hapa duniani. Tofuati na Hukumu ya watu waovu, yao itakuja baada ya kifo. Ambapo huko hakuna kutubu, mtu akishaonekana amesimama mbele ya Kiti cheupe cha Enzi cha mwanakondoo basi jua mtu huyo moja kwa moja ni kwenye ziwa la moto, kwasababu huko hakuna tena msamaha.

Hivyo hukumu hii ya Mungu itakuja juu ya mwaminio kwa namna zote mbili: Yaani pale ATAKAPOFANYA KOSA kadhalika na pale ATAKAPOISHI MAISHA MASAFI YA HAKI. Katika zote mbili hukumu ya Mungu lazima itamfiikia.

1) MTAKATIFU ATAKAPOISHI MAISHA YA HAKI:

“1Petro 4: 4.13 Lakini kama MNAVYOYASHIRIKI MATESO YA KRISTO, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.

14 MKILAUMIWA KWA AJILI YA JINA LA KRISTO NI HERI YENU; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia.

15 Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.

16 Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.

17 KWA MAANA WAKATI UMEFIKA WA HUKUMU KUANZA KATIKA NYUMBA YA MUNGU; na ikianza kwetu sisi, mwisho wao wasioitii injili ya Mungu utakuwaje?

18 NA MWENYE HAKI AKIOKOKA KWA SHIDA, YULE ASIYEMCHA MUNGU NA MWENYE DHAMBI ATAONEKANA WAPI?

19 Basi wao wateswao kwa mapenzi ya Mungu na wamwekee amana roho zao, katika kutenda mema, kama kwa Muumba mwaminifu”.

Unaona? Kama vile Bwana Yesu alivyopitia makwazo, na majaribu mazito namna ile mpaka kufikia hatua ya kudhihakiwa na kutukanwa, na kutemewa mate, na huku hajafanya jambo lolote listahililo kutendewa mambo hayo, hakutenda dhambi yoyote kustahili msalaba, hakumdhulumu mtu yeyote kustahili kupigwa makofi, lakini aliyapitia hayo, sio kwamba alimkosea Mungu, hapana, bali Mungu aliridhika kumfanya ayapitie yale, ili aitimize HUKUMU ile juu yake ili mbele zake aonekane kama amestahili kuzipokea Ahadi zote alizokuwa amemwahidia za kumfanya awe mrithi wa vyote. Biblia inasema..

Isaya 53: 4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; LAKINI TULIMDHANIA YA KUWA AMEPIGWA, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.

5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu;……..

9 Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya; Na pamoja na matajiri katika kufa kwake; Ingawa hakutenda jeuri, Wala hapakuwa na hila kinywani mwake.

10 LAKINI BWANA ALIRIDHIKA KUMCHUBUA; AMEMHUZUNISHA; Utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi, Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi, Na mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake;

11 Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika. Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki Atawafanya wengi kuwa wenye haki; Naye atayachukua maovu yao”.

Kama tunavyoona maandiko yanasema “TULIMDHANIA KUWA AMEPIGWA NA MUNGU”..Bwana Yesu kupitia majaribu kama yale mpaka kusulibiwa kwa aibu msalabani watu walidhani kuwa Mungu ndiye aliyemlipizia maovu yake, ya kujifanya kuwa yeye ni sawasawa na Mungu. Lakini Mungu alimuhukumia adhabu ile kwa ajili yetu, “Mungu aliridhika kumchubua na kumuhuzunisha” ili mwisho wa siku aje kuona wingi wa uzao Mungu alimwandalia kwa kupitia yeye, ili baadaye aje kuona matunda ya taabu yake biblia inasema hivyo, jinsi atakavyomiliki mataifa mengi na wafalme wengi. Na ndio maana mpaka sasa unaweza kuona ni jinsi gani KRISTO anamiliki kila kitu sasa hivi, Jina lake linaitwa kila mahali duniani kote, katika vizazi vyote na hapo bado ufalme wake haujaanza, siku ukija kuanza duniani ndipo tutamwelewa vizuri yeye ni kwanini anaitwa BWANA WA MABWANA na MFALME WA WAFALME.

Vivyo hivyo na sisi ambao tutakuwa warithi pamoja na yeye. Kusudi kwamba tuonekane tumestahili kuzirithi hizo ahadi nono ambazo Mungu kawaandalia watoto wake, yapo mambo tutayapitia kwa ajili ya imani yetu. Ni kweli inajulikana kila mahali kuwa mtu akiwa mwenye haki, hawezi kuudhiwa au kushitakiwa kwa namna yoyote ile, lakini kwa mkristo ni kinyume chake. Mungu kaiweka hivyo kwa makusudi yake, hiyo ndiyo HUKUMU yake kwa wana wake.

Kwa mfano unaweza ukashangaa hapo mwanzo ulikuwa ni fisadi, lakini ulipomwamini Kristo tu na kuacha ufisadi, badala ya wale wanaoupinga wakufurahie ghafla unashangaa ndio wanaanza kukuchukia, ulikuwa ni mhubiri feki, wa injili za juu juu tu, za kuwachekesha watu madhabahuni, lakini ulipoamua kuchukua uamuzi wa kusimama katika imani, na kuanza kuihubiri ile injili ya mitume,sasa badala ya kufurahiwa ghafla makasisi wenzako wanaanza kukuangalia vibaya na kukutenga, na kukukataza kuhubiri mbele ya makanisa yao. Ulipokuwa katika dhambi ndugu na marafiki hawakuwa na neno lolote juu yako. Lakini siku ulipoamua kumfuata Kristo badala wakufurahie umekuwa mtu mwema, ndio kwanza wanaanza kukuzungumzia vibaya, wanaanza kukuchukia bila sababu, wanaanza kukuwekea vinyongo, wanaanza kukuwekea mitego isiyo na sababu ukitazama kosa lako hulioni.

Mtume Paulo aliliona hilo tangu zamani na kusema

2Timotheo 3:12 “Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu WATAUDHIWA”.

Wafilipi 1: 29 “Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;”

 Hivyo ndugu mkristo, usishangae wala usiogope unapoyapitia haya, kwasababu ya Imani yako, unapopigwa, unapofungwa, unapotengwa, unapoachwa jua tu hiyo ni hukumu ya Mungu inapita juu yako, hata mitume walipitia kadhalika na wakristo wenzako duniani wanapitia hivyo hivyo ili siku ile uonekane kuwa umestahili kupata vinono vya ufalme ule usikuwa na mwisho kama Bwana Yesu yalivyomkuta ni sharti upitie hapo..Jua tu hivyo ni vya kukutengenezea TAJI bora utakapoingia katika ufalme ule. Wakati mwingine utashangaa kuona misiba ya watu wako wa karibu, au utapoteza vile uvipendavyo kwasababu umeamua tu kumfuata Kristo, utapitia njaa, utapitia shida, n.k. Lakini kuwa na uhakika kuwa hujapoteza lolote, hiyo ni hukumu ya Mungu itakayopita juu yako kwa muda.

Sasa biblia ndio inakuja kusema IKIWA MWENYE HAKI ATAOKOKA KWA SHIDA NAMNA HIYO?. Asiye mcha Mungu na mwenye dhambi ataonekania wapi?. Ndugu hukumu za Mungu si za kuzitamani kabisa. Ikiwa huyu ambaye anamcha Mungu leo hii unamwona yupo katika dhiki,na pengine taabu. Ikiwa watakatifu ndio unawaona kuwa wenyewe ndio watu wa bahati mbaya. Wewe ambaye sasa huna habari na Mungu siku ile utaonekania wapi? Ni nani atakayasimama badala yako kukutetea siku ile?.

Leo hii watu wanaowadhihaki watakatifu na kusema hawana uelekeo wowote, wana shida, wamepoteza dira ya maisha, maisha yao ni ya dhiki, hawana mbele wala nyuma, hawajui hata wale wayahudi walimwambia hivyo hivyo Bwana Yesu. Walisema ngoja sasa tumuue tuone huyo baba yake kama atakuwa na uwezo wa kumshusha msalabani, . Na walipoona hajashushwa msalabani waliendelea kudhihaki, hakisema huyo Mungu mbona hamsaidii? lakini hawakujua kuwa Mungu ndiye aliyeridhika kumchubua,.Ikiwa Bwana Yesu ambaye hakuwa na dhambi aliupata ule ufalme kwa taabu vile, sisi ambao leo hii tunaudharau wokovu na njia ya msalaba tutaonekania wapi siku ile.?.

2) MTAKATIFU ATAKAPOMKOSEA MUNGU.

Leo hii watakatifu wakimkosea Mungu kwa kosa linaloweza kuonekana kuwa dogo, inawagharimu adhabu kubwa sana hata wakati mwingine kupoteza maisha yao kama ilivyokuwa kwa Hanania na safira (Matendo 5), kwa kosa kutokutimiza tu nadhiri zao walikufa wote wawili pale pale.

Kumbukumbu 8: 5 “Nawe fikiri moyoni mwako, ya kuwa kama vile baba amrudivyo mwanawe, ndivyo Bwana, Mungu wako, akurudivyo”.

Sasa hao walio waasherati, na waabudu sanamu, na washirikina, na wenye dhambi wote ambao hawataki sasa kuyasalimisha maisha yako kwa Bwana. siku ile watastahimili vipi ile hukumu?. Pengine utatoka leo kuzini na usione chochote, utatoka leo kuua na jambo lolote baya lisikutokee, utakwenda kulawiti na ubaya wowote usikupate. Utakwenda kuloga na usikutwe na ubaya wowote, Sio kwasababu Mungu hakuoni au wewe ni mtu wa kipekee sana kwake zaidi ya Yule anayemcha yeye na kupitia mabaya. Hapana fahamu tu jambo moja, Hukumu ya waovu sio sasa. Bali ni baada ya dunia hii yote kuisha. Siku ile mataifa yote yatakaposimama mbele ya kiti cha huku cheupe cha enzi cha mwanakondoo na kila mmoja atakapotoa hesabu ya mambo yake yote aliyokuwa anayafanya hapa duniani. Sio kutamani kuwepo siku hiyo. Kumbuka watakatifu wale walimwamini Kristo wakati huo hawatakuwepo.

Huu si wakati wa kuchekezea maisha yako, Kila mtu anajua kuwa haya ni majira ya kurudi kwa Bwana Yesu mara ya pili duniani, Kila mtu anajua kuwa dhiki kuu ipo mlangoni kuanza, na Yule mpinga-kristo kunyanyuka. Sasa unasubiri nini usitengeneze maisha yako sasa?.

Ikiwa mwenye haki akiokoka kwa shida, yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi?.

Ni furaha yangu, ukigeuka sasa angali muda upo.

Tafadhali hubiri habari njema hizi kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

AYUBU 28 : HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

‘’MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI’’..NA NDIVYO ILIVYO KWA UASHERATI

JE! WEWE NI MBEGU HALISI?


Rudi Nyumbani

Print this post

BARUA INAYOSOMWA

2 Wakorintho 3:2 “NINYI NDINYI BARUA YETU, iliyoandikwa mioyoni mwetu, INAJULIKANA NA KUSOMWA NA WATU WOTE;”

Maisha tunayoishi sisi ni BARUA ya Kristo, watu watutazamapo, wanapata ujumbe hata kabla ya sisi kuzungumza lolote,. Na matendo yetu ndiyo maandishi, na siku zetu ndizo kurasa, Tangu tulipompa Bwana maisha yetu, siku hiyo hiyo tunaanza kuandika kurasa njema za barua zetu.

Injili yenye matunda Kristo anayoyataka haihubiriwi kwa maneno matupu! Hapana bali inahubiriwa kwa matendo..Matendo yetu ndiyo yanayohubiri injili kuliko kingine chochote, Matendo yetu ndiyo yanayomtangaza Kristo kuliko kitu kingine chochote. Tunaweza tukawa na uwezo mzuri wa kuhubiri au kuongea lakini kama matendo yetu hayaendani na tunachokizungumza basi injili tunayoihubiri ni BURE!!.

Unaweza ukawa unahudhuria kanisani kila siku, unasaidia watu, lakini kama maisha yako ya siri ni machafu, kama maisha yako ya pembeni ni ya kiasherati, au ni mtazamaji wa pornography, au mfanyaji masturbation au mtukanaji, au mwizi, au mwuaji, au unacheza kamari, au mtu wa hasira usiyesamehe basi wewe ni barua yako ni mbaya, haijalishi unalitaja jina la Kristo mara ngapi..

Maisha yetu yanapaswa yahubiri injili kwa watu wa nje kiasi kwamba mtu akikuona tu anajua moja kwa moja Yule ni Mkristo hata kabla hujazungumza lolote, akikuona juzi, jana na leo maisha yako ni yale yale masafi, hata kabla hajazungumza na wewe Neno moja anakiri moyoni kwamba wewe ni mwanafunzi wa Kristo.

Sio lazima tuonekane tumebeba biblia, au tumevaa kanzu, au tumevaa kama watu wa dini au tusikiwe tunaimba mapambio, au tuonekane tunaenda kanisani kila siku, au tusikiwe tukisali kila siku hapana! Hiyo ni vizuri lakini hata pasipo hayo mambo, pasipo watu kutusikia tukisali, au tukiimba, au tukienda kanisani n.k inapaswa wakituona tu, ndani ya muda mfupi wameshajua sisi ni watu wa namna gani, washajua kuwa sisi milki ya Yesu Kristo.

Unaweza usiwe unaongea kama watu wa kidini, lakini inapasa mtu akikutazama tu maisha yako, siku mbili tatu,lazima kuwe kuna kitu ndani yake kinamshuhudia kwamba wewe ni mwana wa Mungu. Kwa jinsi maisha yako yanavyoangaza Nuru, na kuonekana Barua inayosomeka vyema.

Mathayo 5:16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona MATENDO YENU mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni…

Unaona? Kitu Bwana Yesu anachosema hapo ni kwamba nuru ya mtu inaangaza kwa matendo yake, na si kitu kingine na hichi ndicho watu wanachokitazama.

Hebu tujifunze kidogo Kitabu cha ESTA.

Esta alikuwa ni Myahudi lakini alizaliwa katika nchi ya Babeli, wakati wana wa Israeli wapo utumwani, hakuwahi kufika nchi yake Israeli.. aliishi na Kaka yake aliyeitwa Mordekai, baada ya wazazi wake kufa (ambapo Baba yake Esta alikuwa ni mjomba wake Mordekai). Walikuwa wanamcha Mungu yeye na Mordekai, lakini ilipofika wakati Mfalme wa Uajemi anatafuta malkia mwingine sehemu ya Malkia Vashti aliyemvunjia heshima Mfalme, Mordekai alimpandisha Esta kwenda kushindania hiyo nafasi ya umalkia miongoni mwa wanawali watakaochaguliwa na mfalme, Lakini jambo la kimiujiza ni kwamba Mordekai wala Esta hawakujitambulisha kuwa wao ni watu kutoka taifa gani wala Imani yao ni Imani gani…Na chakushangaza ni kwamba japo kuwa Esta hakuidhihirisha Imani yake mbele ya nyumba ya Mfalme wa Uajemi, lakini kwa matendo yake TAYARI WALE WALIOKUWA WANAWACHAGUA WANAWALI, WALISHAMSOMA ESTA NA KUGUNDUA KUWA NI MTU WA KIMUNGU, MWENYE TABIA NJEMA. Na kama ni msomaji wa Biblia utaona kuwa Ni Esta peke yake ndiye aliyepata kibali mbele ya Mfalme kuwa MALKIA kati ya wale wanawali wengine.

Sasa Ni nini tunachoweza kujifunza hapo?? Hata pasipo Kutaja DINI YAKO,WALA DHEHEBU LAKO, WALA IMANI YAKO, watu wanaweza kukusoma tu na kugundua wewe ni mtu wa namna gani? Watu wanaweza wakakusoma tu na kugundua Barua yako ni barua ya namna gani. Kwa mwenendo wako tu hata pasipo kusema BWANA ASIFIWE! au BWANA ATUKUZWE!

Sasa tukirudi kwenye kitabu cha Esta, tunaweza tukajifunza jambo lingine kubwa sana..

JE! Unajua kuwa kitabu cha ESTA ndio kitabu pekee cha Biblia ambacho kuanzia mwanzo wake hadi mwisho wake hakuna Neno “BWANA” wala neno “MUNGU”? Kama hujui hilo nenda kapitie tena biblia yako na utaligundua hilo. Sasa Jambo hilo linafunua nini? Japokuwa kitabu cha Esta hakijamtaja mahali popote Bwana wala neno Mungu halionekani, lakini tukisomapo kile kitabu tunamwona Mungu kwa sehemu kubwa sana na uwezo wake, na bila shaka watu wote tunafahamu kuwa ni kitabu takatifu cha Mungu…ikifunua jambo lile lile kwamba unaweza usionekane unalitaja jina la Bwana Mahali popote pale lakini watu WASOMAPO BARUA YAKO WANAMWONA MUNGU kwa kiwango kikubwa. Na hicho ndicho Mungu anachotaka. Simaanishi kuwa usilitaje jina la Bwana mahali popote hapana, ni wajibu wetu sote kufanya pia na hayo.

Mungu Hataki tuwe kama wanafki kama mafarisayo, ambao kwa nje, tunaonekana ni wakidini lakini kwa ndani ni wachafu. Malkia Esta hakubeba Torati na kuingia nayo kwa Mfalme ndipo akubalike, hakujidhihirisha kwamba yeye ni Myahudi, mwana wa Ibrahimu, na kwamba anamwabudu Mungu wa aliyeziumba Mbingu na nchi..hakufanya hayo yote, yeye aliingia tu mbele ya mfalme na barua ya maisha yake, na utii wake, unyenyekevu wake, upole wake, usikivu wake, na utulivu wake, na tabia yake njema, aliingia na tabia yake ya kuwa na kiasi, ya mtu asiye na majivuno, asiye na kiburi, asiyekuwa na tamaa, aliingia na tabia yake ya kuridhika, na kutotamani mambo makubwa, aliingia na tabia yake ya kutokusengenya, ya kutokuwa mwashetati, hiyo ndiyo iliyomfanya apendwe na Mfalme, hiyo ndiyo iliyomfanya akubalike..Hiyo ndiyo iliyomfanya Barua yake isomeke vyema mbele za Mfalme, na Ufalme wa Uajemi wote, na hiyo ndiyo iliyomfanya KITABU CHAKE JAPOKUWA HAKINA JINA LA BWANA MAHALI POPOTE LAKINI KIMEINGIA KATI YA VITABU 66 VYA BIBLIA.

Kaka/Dada uliye mkristo usomaye ujumbe huu, ifanye barua yako isomeke vyema, kusudi kwamba watu wakishauona mwenendo wako, roho zao zipate kuponywa. Mwenendo tu wa mtu ni nguvu tosha ya kumgeuza mtu kama vile Neno linavyoweza kumgeuza mtu. Wakati mwingine ndoa yako inamatatizo na umehangaika huku na kule, umefunga na kusali, lakini bado mume wako anazidi kuwa mwovu, anazidi kuwa mlevi, mke wako hana nidhamu, hamchi Mungu, watoto wako ni watukutu hawataki kukutii, wazazi wako ni waashirikina, wanagombana, wametengana..Na wewe ni mkristo umejaribu kuomba, hata wakati mwingine kuwashuhudia lakini bado hakuna mabadiliko..Tatizo linaweza kuwepo katika mwenendo wako, wanapokutazama hawaoni kitu cha kuwavutia kuwa kama wewe. Lakini ikiwa mwenendo wako utaubalishwa na kuishi maisha ya nidhamu na utakatifu na kumcha Mungu, basi fahamu kuwa hiyo ni injili tosha ya kuwafanya wao wabadilike. Embu soma vifungu hivi vinavyosema juu ya familia.

1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;

2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.”

Unaona hapo? Hivyo ndugu ikiwa bado hujamkabidhi Bwana Yesu maisha yako, mpe leo, Tubu mgeukie kwasababu yeye ndiye Njia ya kufika mbinguni, hakuna mwingine, njia nyingine za kidini, kidhehebu, mtu binafsi, n.k zote zinaishia mautini..Yesu ndiye mwokozi, Siku tunazoishi ni siku za Mwisho, zilizotabiriwa. Na Neema inakaribia kurudi Israeli, na Kristo kulichukua kanisa lake, je! umo miongoni mwa watakaoenda na Bwana??

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo izidi kuwa nawe!!

Tafadhali “share” kwa wengine,

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO.

HADITHI ZA KIZEE.

UFUFUO WA UZIMA NA WA HUKUMU.

MADARAKA YA WAKATI MKAMILIFU.

LULU YA THAMANI


Rudi Nyumbani

Print this post

JAWABU LA MAISHA YA MTU.

Kwa muda mrefu Mfalme Sulemani aliingia katika kuchunguza hekima ya viumbe vyote duniani, mimea yote na kazi zote za wanadamu zinazofanywa chini ya jua hili ili kutoa jawabu moja ambalo kwa hilo litamfanya mwanadamu aweze kufungua milango yote ya BARAKA,na MAARIFA na UZIMA na AMANI katika siku zake zote aishizo hapa duniani. Mfalme Sulemani aliingia katika utafiti huo wa hali ya juu kwa wa muda mrefu sana, tangu ujana wake akiongozwa na ile hekima iliyokuwa ndani yake, biblia inasema alijaribu hata “upumbavu” mambo yasiyopaswa kufanywa na mtu yeyote wa Mungu, lakini yeye alifanya kwa kusudi tu la kulivumbua hilo jawabu pengine linaweza likawa limejificha ndani yake.. Jawabu ambalo litampa mwanadamu wepesi wa maisha, amani, furaha ya kudumu, utulivu, kuridhika,uzima, upendo n.k.

Uchunguzi huu wa Sulemani tunaweza kuusoma katika kitabu cha Mhubiri tukianzia mwanzoni kabisa tunaona Sulemani akieleza jinsi alivyoutia moyo wake kutafuta na kuchunguza hekima ili kupata jawabu hilo moja, hivyo ilimgharimu kujaribu kitu kimoja kimoja kinachoweza kutamanika hapa duniani, na kila alichokijaribu na kuona sio chenyewe chenye ufunguo wa maisha kwa kwa mwanadamu alisema ni UBATILI, hivyo akaendelea na kingine, kadhalika alipoona hicho nacho hakiwezi kumsaidia mwanadamu alisema ni UBATILI..hivyo akakiacha akaendelea na kingine, hivyo hivyo mpaka alipofanikiwa kujaribu kila kitu unachoweza kukifahamu hapa chini ya jua, hakuna ambacho hakukijaribu, mpaka kwa wachawi na miungu migeni alifika, hakuna kitu ambacho hakukijaribu Sulemani, alijaribu vyote, lakini vyote aliona ni ubatili na upotevu ni sawa na kuufuata na kujilisha Upepo, mpaka tunapokuja kusoma sasa kwenye sura ya mwisho kabisa ya kitabu cha Mhubiri baada ya Sulemani kwenda huku na kule, kufanya hichi na kile, kujaribu hichi na kile, ndipo mwisho wa siku anakuja kulipata JAWABU lenyewe alilokuwa analitafuta kwa muda mrefu, tangu ujana wake, lililomgharimu hata kuipoteza nafsi yake katika mambo yasiyompasa kuyafanya ili tu alipate na hatimaye akalipata jawabu hilo..Haikuwa kazi rahisi..

Ni sawa na wewe leo unakwenda kutafuta nguo yenye nyuzi za rangi 10 iliyoandikwa karatu katika soko la mitumba, itakugharimu kuchambua mtumba mmoja hadi mwingine mpaka uipate, na hiyo haitakuwa kazi ya kuisha ndani ya siku moja, utafukua mitumba na mitumba soko zima na pengine unaweza usiipate.

Ndicho kilichomgharimu Sulemani kuipata hiyo kanuni ya mwanadamu ya kuishi hapa duniani kwa wepesi na furaha na amani, kwa lugha ya kisayansi tunaweza kusema FORMULA ya maisha ya mwanadamu ambayo katika hiyo mwanadamu atakuwa na uwezo wa kufungua milango yote migumu ya maisha yake ya sasa na ya baadaye ambayo hapo kwanza kwa kuikosa hiyo ndio iliyomfanya mwanadamu awe mtu wa kutangatanga huko na kule, ajisumbue kwa hili na lile, ajitese kwa hichi na kile. Lakini sasa akishaifahamu hii kanuni basi maisha yake yatakuwa matamu yenye raha na mafanikio.

Na jawabu hili tunakuja kuliona mwishoni kabisa mwa kitabu alichokiandika SULEMANI cha Mhubiri..Sulemani anasema

Mhubiri 12: 13 “Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; MCHE MUNGU, NAWE UZISHIKE AMRI ZAKE, MAANA KWA JUMLA NDIYO IMPASAYO MTU.

14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni KILA KAZI, pamoja na KILA NENO LA SIRI, likiwa jema au likiwa baya”.

Unaona jumla mambo yote yampasayo mtu ni hii KUMCHA MUNGU, NA KUZISHIKA AMRI ZAKE.Basi!!..kwa hilo kila mlango utafunguka, ambao mwanadamu alikuwa anajitesa kwayo.

Sasa sisi tunaoishi kizazi hiki, tumesharahisishiwa mambo yote, leo hii unahangaika kutafuta mali ukidhani kuwa huko ndiko utapata jawabu la maisha yako, ndugu Sulemani alizitafuta sana tena kwa lengo la kupata jawabu kama hilo hilo unalolitafuta wewe, lakini hakuliona mwisho wa siku akasema ni UBATILI na UONGO..

Mhubiri 7: 27 “Tazama, asema Mhubiri, mimi nimeyaona hayo kwa kulinganisha hili na hili, ili kuitafuta jumla;

28 ambayo bado nafsi yangu nikali nikiitafuta, nisiione;….”

Leo hii unatafuta kuzitii tamaa zako za macho na anasa,kila mwanamke mzuri unataka awe wako, kila mwanaume mwenye utajiri unataka awe mume wako, ukidhani kuwa utapata raha nafsini mwako, na hivyo maisha yako yatakuwa mepesi ukidhani kuwa hiyo ndio maana ya maisha. dada/kaka Sulemani alishalijaribu hilo nalo kwa ajili yetu, ili aone kama kweli humo ndani yake kuna jambo la maana sana la kumfaa mwanadamu lakini alingundua ndani yake kuna ubatili na mauti, yeye alikuwa na mamia ya wake na Masuria lakini hata kimoja hakuona kama kinao uwezo wa kutoa jawabu la maisha ya mtu hapa duniani.

Unadhani siku ukishajenga nyumba na kuwa na familia nzuri ndio siku utakayofurahia maisha yako?. Na hivyo leo hii unazunguka huku na kule unajitabisha kwa hili na lile ili uifikie hiyo furaha?. Ndugu ni vizuri kufanya hivyo lakini fahamu kuwa hilo sio jawabu la maisha yako.

Unaona kuwa ulevi ndio furaha ya maisha ya mwanadamu, hilo nalo lilishajaribiwa lakini alisema halina manufaa yoyote ya kumwokoa mwanadamu. Embu sikiliza walau kidogo maneno haya ya Sulemani aliyosema:

Mhubiri MLANGO 2

“1 Nikauambia moyo wangu, Haya, nitakujaribu kwa njia ya furaha basi ujifurahishe kwa ANASA. Na tazama, hayo nayo yakawa ubatili.

2 Nikasema juu ya kicheko, Ni wazimu; na juu ya furaha, Yafaa nini?

3 Moyoni mwangu nikapeleleza jinsi ya kuuburudisha mwili KWA MVINYO, na (moyo wangu ukali ukiniongoza kwa hekima) jinsi ya kushikana na upumbavu, HATA NIYAONE YALIYO MEMA YA KUWAFAA WANADAMU, ILI WAYAFANYE HAYO CHINI YA MBINGU SIKU ZOTE ZA MAISHA YAO.

4 Nikajifanyizia kazi zilizo kubwa; nikajijengea nyumba; nikajipandia mashamba ya mizabibu;

5 nikajifanyizia bustani na viunga, na kuipanda humo miti yenye matunda ya kila namna;

6 nikajifanyizia birika za maji, ya kuunyweshea mwitu mlimopandwa miti michanga.

7 Nami nikanunua watumwa na wajakazi, nikawa na wazalia nyumbani mwangu; tena nikawa na mali nyingi za ng’ombe na kondoo, kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu;

8 TENA NIKAJIKUSANYIA FEDHA NA DHAHABU, NA TUNU ZA KIFALME NA ZA KUTOKA KATIKA MAJIMBO. Nikajipatia waimbaji, waume kwa wake, nao wale ambao wanadamu wanawatunuka, masuria wengi sana.

9 Basi nikawa mkuu, nikaongezeka kupita wote walionitangulia katika Yerusalemu; pia hekima yangu nikakaa nayo.

10 Wala sikuyanyima macho yangu cho chote yalichokitamani; wala sikuuzuia moyo wangu katika furaha yo yote; maana moyo wangu ulifurahi kwa sababu ya kazi yangu yote, na hii ilikuwa sehemu yangu katika kazi yangu yote.

11 Kisha nikaziangalia kazi zote zilizofanywa kwa mikono yangu, na taabu yote niliyotaabika katika kuzitenda; na tazama, YOTE NI UBATILI NA KUJILISHA UPEPO, WALA FAIDA HAKUNA CHINI YA JUA”.

Unaona hapo ndugu mimi na wewe hatupaswi kuyajaribu hayo yote ambayo tayari yalishajaribiwa na kuonekana kwamba hayawezi kutupatia sisi furaha na uzima wowote ndani yetu. Tuufuate ushauri wa wenye hekima, tuufuate ushauri wa mababa, tuufuate ushauri wa walitutanguliza zamani wazee wetu ambao kwa hekima za Mungu waliona na kufundishwa mengi Ndio maana Suleimani akaitwa akaitwa MUHUBIRI.. Usidanganyike na wahubiri wengine wanaokutumainisha katika mambo ya ulimwengu huu, Tumsikilize Muhubiri huyu aliyetiwa mafuta na Mungu mwenyewe na kuitwa MUHUBIRI,na ndio maana Sulemani alisisitiza sana katika mithali zake akisema..

Mithali 7: 1 “Mwanangu, yashike maneno yangu, Na kuziweka amri zangu akiba kwako.

2 Uzishike amri zangu ukaishi, Na sheria yangu kama mboni ya jicho lako.

3 Zifunge katika vidole vyako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako”.

Mithali 4: 10 “Mwanangu, sikiliza, na kuzipokea kauli zangu; Na miaka ya maisha yako itakuwa mingi.

11 Nimekufundisha katika njia ya hekima; Nimekuongoza katika mapito ya unyofu.

12 Uendapo, hatua zako hazitadhiikika, Wala ukipiga mbio hutajikwaa”.

Yesu pekee ndio jawabu la maisha yako, haijalishi utahangaika wapi, utasumbuka wapi, utajitaabisha na nini, leo ni rahisi kupuuzia lakini utafika wakati ambao utaona hivyo vitu ulivyovitaabikia havikukupa jawabu la maisha yako hapo ndipo utapozikumbuka zile hekima ulizopewa na mababa ukazikataa. Na kumbuka ukishafika huo wakati huwezi tena kuwa na raha, utajikuta tu unayachukia maisha yako. Kwasababu umeshachelewa, na wala huna nguvu tena ya kumshinda yule mwovu kwasababu siku za maisha yako zimeshakwenda..

Mwanadamu huwa akishafika hatua hiyo ni ngumu tena kumgeukia Mungu kwasababu anakuwa ameshachanganyikiwa rohoni hajui ni wapi tena pa kuanzia,ni wapi pa kumalizia, japo atajifanya kuwa anafuraha kwa nje lakini ndani yake huzuni na hofu vimemjaa kwasababu alipuuzia hekima za mababa angali akiwa kijana, hakumkumbuka muumba wake siku za ujana wake, hata hekima za kidunia zinasema Samaki mkunje angali mbichi..Akishakauka ukijaribu kufanya hivyo atavunjika kama kijiti badala ya kukunjika..ndivyo itakavyokuwa hali yake mtu yule anayeupuuzia wokovu sasa..

Sulemani anasema tena “1 Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo.(Mhubiri 12:1)”.

Unaona hapo zipo siku ZILIZO MBAYA, kadhalika zipo siku ZISIZO NA RAHA ndani yake zitakuja huko mbeleni kwa kila mwanadamu ambaye hamkumbuki muumba wake katika siku za ujana wake.

Wewe ni kijana unayesoma hii habari, yatafakari yote ambayo yalimgharimu Sulemani kuyafanya wakati mwingine hata mambo yasiyompendeza Mungu ili kusudi kwamba tu avumbue jumla ya maisha yako, unende katika kanuni ya maisha iliyo sahihi..

Na sasa JUMLA hiyo ipo wazi mbele ya macho yetu, siku ile hutakuwa na udhuru tena, ukisema nilitanga tanga kutafuta raha na amani na ndio maana niliingia katika anasa na ushirikina, Sulemani atakuhukumu siku ile kwa kutokutii sauti ya Mungu inayozungumza na wewe kupitia injili yake.

TUBU sasa, mpe YESU KRISTO maisha yako, acha dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kutozifanya tena na sio kimazoea, kisha ukabatizwe katika ubatizo ulio sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi katika jina la YESU ili upate ondoleo la dhambi zako, kisha kuanzia hapo Bwana mwenyewe atakupa Roho wake Mtakatifu kukusaidia kuushinda ulimwengu na kumcha Yeye kila siku. Na maisha yako yatakuwa SALAMA katika mikono yake yeye aliyekupa huo uzima, siku zako zilizobakia hapa duniani.

Ni maombi yangu utafanya hivyo leo.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

UMEFUNULIWA AKILI?

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

TUSIFUNGWE NIRA PAMOJA NA WASIOAMINI.

KWANINI TUWE WENYE BUSARA KAMA NYOKA?

DHAMBI YA ULIMWENGU


Rudi Nyumbani

Print this post

FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

Mhubiri 12: 1 “MKUMBUKE MUUMBA WAKO SIKU ZA UJANA WAKO, KABLA HAZIJAJA SIKU ZILIZO MBAYA, Wala HAIJAKARIBIA MIAKA utakaposema, MIMI SINA FURAHA KATIKA HIYO”.

Biblia inasema “Mkumbuke” ikiwa na maana kuwa ni wakati ambao kuna “kusahau” wakati wa kupumbazwa na mambo mengi, …Na huo wakati si mwingine zaidi ya wakati wa UJANA. Na biblia inasema pia zitakuja nyakati au siku zilizo mbaya, ambazo zitakuwa sio za furaha, nyakati zisizofaa tena kumgeukia yeye,..

Tafakari kwa makini hiyo sentesi “Mkumbuke muumba wako kabla hazijaja siku !!” Ina maana sio kila wakati unafaa katika kumgeukia Mungu..Ni rahisi kusema nitakapokuwa MZEE nitamgeukia Mungu, au nitakapofikia kipindi Fulani au nitakapokuwa nimezidiwa sana, au nitakapokuwa nimefilisika sana, au nitakapokuwa katika ugonjwa wa kufisha, au siku nitakayokaribia kufa ndiyo nitakuwa karibu na Mungu. Ndugu hiyo ni hatari sana neema ya Mungu haiotewi. yeye anasema “mkumbuke Muumba wako kabla hazijaja siku zilizo mbaya”..zingatia hilo neno kabla!! Kabla!!,.Kumbuka Wengi wanaopata Neema ya kuokolewa katika hizo nyakati zilizo mbaya ni wale tu ambao hawajawahi kabisa kuisikia injili hapo nyuma, mfano wa Yule muhalifu aliyesulibiwa na Kristo pale Msalabani. Hivyo usiliweke hilo akilini kwa sisi wa kizazi hiki ambacho injili ya Kristo inahubiriwa kila siku barabarani lakini hatutaki kusikia au tunapuuzia tukitumaini itafika siku tu tumtafuta Mungu..Hilo tuliondoe akilini.

SASA HIZO SIKU ZILIZO MBAYA(au siku za matatizo) NI ZIPI? AMBAZO TUMEONYWA TUMKUMBUKE MUUMBA WETU KABLA HAZIJAFIKA??

Ukizidi kusoma mistari inayofuata utaona hizo siku siku mbaya zinazozungumziwa hapo ni zipi. Ukiwa na nafasi binafsi utasoma, sura yote ya 12,lakini kwasasa tutaangalia vipengele hivyo vikuu.

1)KABLA JUA, NA NURU, NA MWEZI, NA NYOTA, HAVIJATIWA GIZA; (Mhubiri 12:1-14)

Hapo anazungumzia siku ya Bwana inayotisha, ambayo ipo mbioni kuijilia dunia nzima,.Biblia inasema tumkumbuke Bwana kabla hiyo siku haijafika, siku ambayo Jua litatiwa giza, na mwenzi hautatoa nuru yake, na nyota za mbinguni zitakapoanguka…Siku ya kutisha ya hasira ya Mungu mwenyezi.

Amosi 5: 18 “Ole wenu! Ninyi mnaoitamani siku ya Bwana; kwani kuitamani siku ya Bwana? NI GIZA, WALA SI NURU.

19 Ni kama mtu aliyemkimbia simba, akakutana na dubu; au aliingia katika nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, nyoka akamwuma.

20 Je! SIKU YA BWANA HAITAKUWA GIZA, WALA SI NURU? Naam, yenye giza sana, wala haina mwanga” 

Amosi 8: 9 “Tena itakuwa siku hiyo, asema Bwana MUNGU, nitalifanya JUA LITUE WAKATI WA ADHUHURI, NAMI NITAITIA NCHI GIZA WAKATI WA NURU YA MCHANA.

10 Nami nitazigeuza sikukuu zenu kuwa maombolezo, na nyimbo zenu zote kuwa vilio; nami nitatia nguo za magunia katika viuno vyote, na upaa katika kila kichwa; nami nitayafanya haya kuwa kama maombolezo kwa ajili ya mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.”

Unaona sisi watu wa kizazi hichi, tunaishi karibu na siku hizo, mambo yote yanathibitisha hilo, siku yoyote mwisho unafika, kwani katika kalenda ya kibiblia tunaishi katika kanisa la mwisho linalojulikana kama Laodikia (Ufunuo 3).Na ndio kanisa hilo litakaloshuhudia mambo yote. Unyakuo pamoja na dhiki kuu.

2) KABLA YA KURUDI MAWINGU BAADA YA MVUA; (Mhubiri 12:2)

Kabla ya kurudi mawingu baada ya Mvua, inafunua “kipindi cha njaa kuanza” Kama vile Farao alivyoambiwa na Bwana itakuja miaka 7 ya neema, ya mvua tele na kisha baada ya hiyo itaanza miaka mingine 7 ya njaa, isiyokuwa na Mvua, kupanda wala kuvuna. Ndio kitu kile kile Biblia inachokizungumzia hapa, kwamba baada ya mvua mawingu yatarudi na kuanza vipindi vya njaa, Biblia inatabiri pia siku za mwisho Bwana ataleta njaa juu ya nchi, si njaa ya chakula bali njaa ya KUKOSA KUYASIKIA MANENO YA MUNGU.

Amosi 8: 11 “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Bwana.

12 Nao watatanga-tanga toka bahari hata bahari; na toka upande wa kaskazi hata upande wa mashariki; watapiga mbio, wakienda huko na huko, kulitafuta neno la Bwana, wasilione.

13 Siku hiyo wanawali wazuri na wavulana watazimia kwa kiu”.

Neno la Mungu linatuonya TUMKUMBUKE MUUMBA WETU KABLA HIZO SIKU HAZIJAFIKA, Na hizo siku zimeshaanza kujitokeza duniani…Tunaona sasa Njaa ya Neno la Mungu imeanza kuongezeka..

3) KABLA HAIJAKATIKA KAMBA YA FEDHA; (Mhubiri 12:6)

Kabla ya uchumi wako binafsi kuanguka, Unaona hapo?? usiseme siku nitakapoishiwa fedha au nitakapokuwa naumwa sana ndipo nitakapomgeukia Mungu, au siku nitakapokaribia kufa..Bwana hadhihakiwi, yeye anasema TUMKUMBUKE KABLA HIZO SIKU HAZIJAFIKA, ikiwa na maana kuwa kama tutamkataa leo kwa makusudi tukiwa katika hali nzuri, hatakuwa na sisi wakati wa matatizo. Tukimkana leo yeye wakati wa ujana wetu, na yeye atatukana sisi wakati wa matatizo yetu, kumbuka Watakaompata katika hali za matatizo ni wale tu ambao hawakuwahi kuisikia injili hapo kabla, lakini kama ulishawahi kuisikia na unaipuuzia hakutakuwa na nafasi ya pili wakati matatizo yatakapokukumba.

4) KABLA MAVUMBI KUIRUDIA NCHI KAMA YALIVYOKUWA, NAYO ROHO KUMRUDIA MUNGU ALIYEITOA. (Mhubiri 12:7)

Biblia inasema katika Waebrania 9:27 “MTU AMEANDIKIWA KUFA MARA MOJA NA BAADA YA KIFO HUKUMU”..Ndugu, hakuna maombi yoyote yanayoweza kumsaidia mtu baada ya kufa, Mafundisho ya Toharani hayapo katika biblia takatifu, ni mafundisho ya Yule mwovu, ili kuwafariji watu kuwa baada ya kufa unaweza ukaombewa na ukatolewa katika maumivu ya moto, hakuna kitu kama hicho, baada ya kifo ni hukumu ndivyo Neno linavyosema, ndio maana hapa Bwana anatuonya

“mkumbuke Muumba wako kabla roho yako haijamrudia yeye” ikiwa na maana kuwa baada ya kufa hakuna nafasi yoyote ya kumgeukia Mungu, au kuokoka na lile ziwa la Moto, kama ulimkataa yeye katika enzi za uhai wako.

Ujana wako unaweza usiwe tu ujana wa mwili wako, bali hata ujana wa akili yako, Na ujana wa akili yako ndio huu, ambao unaweza ukapata nafasi ya kusikiliza Neno la Mungu, Siku ile hutasema hukusikia, Leo hii mkumbuke Muumba wako, kabla ya siku za matatizo kufika, kabla ya vipindi vya njaa, shida, mauti, kabla ya kurudi kwa pili kwa Kristo, kabla ya Mpinga-Kristo kunyanyuka, kabla ya siku ya ghadhabu ya Mungu kumiminwa, uukumbuke msalaba, usiwe miongoni mwa hao wanaodhihaki ambao biblia inasema “Mungu amewaletea nguvu ya upotevu” wauamini uongo ili wapotee. Ujana wako unautumiaje?, nguvu zako unampa nani?.

Biblia inasema nimewaandikia ninyi vijana kwasababu mna nguvu ya kumshinda shetani, hii ikiwa na maana kuwa utafika wakati hizo nguvu hutakuwa nazo za kumpinga shetani maisha mwako kama hutakuwa ndani ya Kristo. Embu jaribu kifikiria unapata faida gani leo unavyoishi katika hayo maisha ya dhambi?. Huoni kama upo katika hatari kubwa sana. Tubu angali bado upo katika siku njema, siku za neema, siku ambazo bado hazijawa mbaya, tuipishe ghadhabu ya Mungu ambayo hivi karibuni inakwenda kumiminwa katika dunia nzima.

Ni maombi yangu kuwa Bwana atakujali kufanyika kiumbe kipya.

Tafadhali “share” kwa wengine, 

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

CHUKIZO LA UHARIBIFU

JE! WEWE NI MWANA WA IBRAHIMU?.

UMUHIMU WA KUZALIWA MARA YA PILI.

JIRANI YAKO NI NANI?

UMUHIMU WA KUISHI MAISHA YAMPENDEZAYO MUNGU SASA.


Rudi Nyumbani

Print this post

UPENDO

Upendo ni kiini cha ukristo na pia ni KILELE CHA UKRISTO. Mungu hajaufunua Upendo kama moja ya tabia zake, kwa mfano hajasema mahali popote kuwa yeye ni mwenye upendo kama anavyosema juu ya tabia zake nyingine alizonazo, mfano Mungu muweza yote, au Mungu mwenye nguvu, Mungu wa rehema, au Mungu mwenye mamlaka n.k. hapana bali anapofikia kwenye suala la Upendo anasema “MIMI NI UPENDO”, yaani yeye kama alivyo ni UPENDO na si kama moja ya tabia zake..Hivyo hulifanya hili Neno upendo katika mtazamo wa rohoni kuwa na tafsiri pana zaidi kuliko sisi tunavyoweza kulichukulia.

1Yohana 4:16 “Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. MUNGU NI UPENDO, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake”.

Upendo ule unaozungumziwa kwenye biblia sio upendo wa kusema nakupenda kimdomo na wala si upendo wa kihisia bali ni upendo UNAOTENGENEZWA ndani ya moyo wa mtu, kwasababu chanzo chake si mwanadamu bali ni Mungu. Hivyo sio wa kutokea tu ndani ya siku moja, pale mtu anapozaliwa mara ya pili. Na ndio maana ukisoma katika kitabu cha 2Petro 1:1-10, utaona kuwa Upendo unachukua hatua ya mwisho kabisa baada ya mtu kupita hatua zote sita za kuelekea ukamilifu, upendo ndio unatokea mwishoni,

2 Petro 1: 5 “Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na WEMA, na katika wema wenu MAARIFA,

6 na katika maarifa yenu KIASI, na katika kiasi chenu SABURI, na katika saburi yenu UTAUWA,

7 na katika utauwa wenu UPENDANO WA NDUGU, na katika upendano wa ndugu, UPENDO.

8 Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana wetu Yesu Kristo”.

huwezi kurukia hatua ya mwisho ukasema kuwa unao upendo wakati hatua zile 6 bado hujazikamilisha ndani yako.Maana ile hatua ya mwisho ni Mungu mwenyewe. Hivyo ili kufikia hatua hiyo ya juu kabisa kileleni Mungu alipo, mahali ambapo utakuwa karibu sana na Mungu katika roho kuliko pengine popote ni hapo utakapoufikia Upendo wa Mungu ndani yako. Na hivyo ili kufika hapo inahitaji BIDII na si vinginevyo. Hiyo haiji kwa kuombewa wala kwa kuwekewa mikono. Biblia inasema ni kwa jitihada na bidii. Kama inavyosema:

1Petro 1: 1.22 “Mkiisha kujitakasa roho zenu kwa kuitii kweli, hata kuufikilia upendano wa ndugu usio na unafiki, basi JITAHIDINI kupendana kwa moyo.  Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele”.

“Zaidi ya yote iweni na JUHUDI NYINGI katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.” (1Petro 4:8).

Unaona biblia inasema pia katika:

1Yohana 4:20. “Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona. NA AMRI HII TUMEPEWA NA YEYE, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake”.

Pamoja na hayo biblia inatuambia hata tukiwa na uwezo wa kuzungumza lugha za malaika hata tukiwa na imani timilifu ya kuweza kuhamisha milima, hata tukitoa mali zetu kuwapa maskini, hata tukitoa miili yetu iungue kwa moto lakini kama hatutakuwa na huo Upendo unaozungumziwa kwenye Neno la Mungu..hatuwezi kuwa kitu mbele za Mungu.

Ukiangalia hayo kwa ukaribu utaona upendo ni kitu cha utofauti na kile tunachokidhania Upendo wa Mungu ni jambo linalojengeka ndani ya mtu katika kipindi cha muda, hivyo inahitaji bidii ya kulipalilia ili liumbike, vinginevyo itakuwa ni ngumu kulifikia..Embu turudi pale kwenye 1Wakoritho 13 tuone biblia inasema nini juu ya Upendo mkamilifu..

“4 Upendo HUVUMILIA, HUFADHILI; UPENDO HAUHUSUDU; upendo HAUTAKABARI; HAUJIVUNI;

5 HAUKOSI KUWA NA ADABU; HAUTAFUTI MAMBO YAKE; HAUONI UCHUNGU; HAUHESABU MABAYA;

6 HAUFURAHII UDHALIMU, BALI HUFURAHI PAMOJA NA KWELI;

7 HUVUMILIA YOTE; HUAMINI YOTE; HUTUMAINI YOTE; HUSTAHIMILI YOTE.

8 Upendo HAUPUNGUI NENO WAKATI WO WOTE; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika”.

Unaona unaweza kutoa mali zako zote kuwapa maskini, lakini je! uvumilivu upo ndani yako?, Tumaini lipo ndani yako? kustahimili mabaya kwa ajili ya Kristo kupo ndani yako? Adabu njema ipo ndani yako? majivuno yameondoka ndani yako?. Kuamini yote unayoambiwa na Mungu kupo ndani yako,? Unaweza ukasaidia maskini sana lakini je! Uchungu upo ndani yako? Unaweza ukawa na karama ya kunena kwa lugha na kuona maono, na kutabiri, lakini je! Unahesabu mabaya kwa ndugu yako n.k??.

Sasa hivi vyote vikiungana na kuonekana ndani ya mtu ndio Neno Upendo wa Mungu linaumbika. Lakini huwezi kusema wewe hauhusudu kama hutaonyesha bidii ya kutokufanya hivyo..kama wewe ni wa kukaa kuwazungumzia vibaya wengine, na bado ni mkristo, hata kama utakuwa una karama kubwa kiasi gani basi mbele za Mungu wewe si kitu ndivyo biblia inavyosema. Kama hutaonyesha bidii katika uvumilivu kwenye mambo yote kwanza kwa ajili ya imani yako na kwa ajili ya kudhulumiwa au kuonewa huwezi kusema upendo wa Mungu upo ndani yako.

Hivyo ni wajibu wetu sisi sote (mimi na wewe), kuonyesha bidii kuutafuta upendo kwasababu ndio kifungo cha ukamilifu, ndio kilele cha ukristo wetu. Na hii inakuja Kwa kuvitunza kwa bidii hivyo vigezo vilivyotelewa hapo juu, mpaka kufikia hatua ya vyenyewe kujengeka ndani yetu na kuwa ni TABIA yetu. Sasa tukishafikia hatua hiyo biblia inasema hapo sisi ni watu wakamilifu sana.

Wakolosai 3:14 “Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu”.

Tunapaswa tuyatawale maisha yetu kwa kanuni za Neno la Mungu, kwa bidii, kuonyesha zile tabia zinazoambatana na Upendo wake. Kila siku tukiyarekebisha maisha yetu, na kutengeneza upya pale tulipojikwaa jana, ikiwa tulishindwa kuwavumilia ndugu zetu au marafiki zetu kwa mabaya waliyotutenda na kukataa kuwasamehe, ni wakati wa kujirekebisha, kufanya bidii kusamehe, ikiwa tulikuwa tunatafuta mambo yetu wenyewe, tunapaswa tufanye bidii kubadilika, ikiwa tulikuwa hatufadhili tunapaswa pia tufanye bidii kufadhili, na kuwa na adabu ili tuonekane kuwa ni watoto wa Mungu. Na kufikia hatua ya kupendana sisi kwa sisi pasipo unafki,

1Yohana 4: 12 “Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote.

Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, NA PENDO LAKE LIMEKAMILIKA NDANI YETU”.

Hivyo sisi sote tuzidi kuonyesha bidii katika kupendana mpaka tumfikie Bwana mwenyewe ambaye ni UPENDO.Kama Bwana wetu Yesu alivyofikia.

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

LENGO LA SHETANI KWA WATOTO WA KIZAZI HIKI.

UKOMA NA UJANE ULIO NDANI YAKO, UMEUPATIA TIBA?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

USIACHE KUJIFUNZA NENO LA MUNGU

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.


Rudi Nyumbani

Print this post

NJIA YA MSALABA

Yohana 19: 16 “Basi ndipo alipomtia mikononi mwao ili asulibiwe; nao wakampokea Yesu.

17 Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, au kwa Kiebrania, Golgotha.

18 Wakamsulibisha huko, na wengine wawili pamoja naye, mmoja huku na mmoja huku, na Yesu katikati.

19 Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI”

Bwana Yesu alisema mimi ndimi NJIA, na KWELI na UZIMA..mtu haji kwa Baba ila kwa njia ya mimi (Yohana 14:6). Litafakari hilo neno “ILA KWA NJIA YA MIMI” Kumbuka aliposema ILA KWA NJIA YA MIMI hakumaanisha kuwa wafuasi wake au washabiki wake.Hapana alimaanisha kitu kingine kabisa tofauti na hicho.

Tuchukue mfano leo hii, mwanariadha maarufu duniani, ambaye amepokea tuzo bora kuliko wote duniani…atoe sentensi aseme “mtu hawezi kuifikia tuzo niliyo nayo mimi isipokuwa kwa njia yangu mimi” je! Kwa sentensi hiyo unadhani atakuwa anamaanisha  kuwa ili mtu awe kama yeye anapaswa awe mshabiki wake au mfuasi wake??…Ni wazi hamaanishi hivyo, utagundua kuwa anamaanisha kwamba mtu akitaka kuwa kama yeye, ni lazima kwanza awe mwanariadha kama yeye, na pili awe na bidii kama za kwake, ajue mbinu anazozitumia za yeye kufanikiwa..

Unaona kwahiyo NJIA ya mwanariadha sio kuwa mshabiki wake wala mfuasi wake bali ni kuwa na bidii kama ya kwake, kufanya mazoezi magumu kama aliyoyafanya yeye, kujitoa kama alivyojitoa yeye, kutokata tama kama yeye asivyokata, kukubali kupitia changamoto zote kama alizozipitia yeye pasipo kukata tamaa n.k…Kwahiyo utagundua kuwa kumbe Kupata tuzo kama aliyoipata yeye sio jambo jepesi ni zaidi na kuwa mshabiki wake au kuwa mfuasi wake.

Kadhalika na Bwana Yesu aliposema mtu haji kwa Baba ila kwa njia yake yeye…hakumaanisha tuwe wafuasi wake, au washabiki wake, kwamba tumshabikie kila mahali tueleze sifa zake na umahiri wake tu, halafu inatosha, hapana alimaanisha kuwa ili mtu afike kwa Baba kama yeye atakavyofika, hana budi kupitia njia kama alizopitia yeye, na si njia nyingine yeyote.. Ilikuwa ili aipate tuzo iliyo bora ilimpasa, kudharaulika, kutukanwa, kutemewa mate kwa ajili ya Imani, kutengwa, kuchukiwa pasipo sababu na zaidi ya yote ilimpasa siku moja ABEBE MSALABA WAKE aelekee Golgotha.

“17 AKATOKA, HALI AKIJICHUKULIA MSALABA WAKE, mpaka mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, au kwa Kiebrania, Golgotha.”

Na yeye akasema mtu yeyote akitaka kumfuata na apitie njia hiyo hiyo, akubali kuchukiwa, akubali kutemewa mate, akubali kudharaulika kwa ajili ya Imani, akubali kukataliwa, akubali kuyaacha mambo ya ulimwengu hata ikiwezekana ndugu, wazazi na jamii na Mwisho wa yote na yeye pia akubali KUBEBA MSALABA WAKE kuelekea Golgotha yake kama yeye alivyofanya. Kwasababu hawezi kuwaambia watu wabebe misalaba yao na wakati yeye mwenyewe habebi.

 Ni njia ngumu lakini ndio Mungu aliyoichagua, tukitaka kufika kwa Baba mbinguni hatuna budi tupitie hiyo…hakuna njia nyingine ya Mkato, ni lazima tubebe Misalaba yetu. Ndio maana Bwana Yesu alisema mara nyingi kila mahali..

Mathayo 16: 24 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, MTU YE YOTE AKITAKA KUNIFUATA, NA AJIKANE MWENYEWE, AJITWIKE MSALABA WAKE, ANIFUATE. Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona”.

Na kama Mungu, alivyompa Bwana wetu Yesu Kristo nguvu ya kushinda majaribu mazito kama yale, nguvu hiyo hiyo atatupa sisi endapo tutakubali kumfuata yeye kwa mioyo yetu yote na kwa roho zetu zote. Endapo tutaikubali hii njia ya msalaba iliyodharaulika..

Bwana baada ya kudharaulika kwa ajili ya Imani, mwisho wa siku aling’aa kama jua, Biblia inasema aliidharau aibu,na hivyo Mungu akamuadhimisha mno, akamkirimi jina lile lipitalo kila jina.

Wafilipi 2: 8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.

9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;

10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;

11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba”.

Bwana atusaidie tusiwe WASHABIKI WAKE au WAFUASI WAKE, bali tuwe watu tunayoiendea njia yake, tukiwa ni walevi na bado tunajiita wakristo sisi bado ni washabiki, tukiwa tunaenda kanisani na bado tunasengenya sisi bado tu ni washabiki, gharama za mbio hatuzijui, ikiwa bado tunavaa nusu uchi na mavazi yasiyostahili mbele za Mungu, bado sisi ni washabiki hatutaweza kufika kwa Baba wanaofika kwa Baba ni wale wanaoiendea NJIA YA BWANA YESU KRISTO, yeye hakuwa mlevi, hakuwa mtukanaji, hakuwa mwizi, hakuwa mwabudu sanamu, hakuwa mwasherati, hakuwa mfuasi wa mambo ya ulimwengu huu. Hiyo ndiyo njia tunayowekewa tuifuate, kama Mwana wa Mungu kapitishwa kwa hiyo, unadhani sisi wengine tutatengenezewa njia nyingine mbadala ya mkato?? Hapana njia ni moja tu, na imeshawekwa na kuthibitishwa na Mungu nayo ni njia ya YESU KRISTO.

Hivyo kama hujampa Bwana Yesu Maisha yako, usikawie kufanya hivyo, nyakati hizi tunazoishi ni za hatari, muda unakaribia kusimamishwa, na umilele kuanza, Bwana asirudi leo na kukukuta upo hivyo ulivyo, asikukuta katika hali hiyo ya uvuguvugu uliyo nayo, Mkabidhi leo maisha yako kikamilifu, kwa kudhamiria kabisa kutoka moyoni mwako, Kuanza maisha mapya na UKAIFUATE NJIA YA MSALABA, na yeye mwenyewe atakuwezesha kuiendea, Na kuumaliza mwendo salama. Ili siku ile uwe na ujasiri wa kusimama mbele zake.

Wafilipi 1: 6 “..yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;

Bwana akuangazie Neema yake.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Print this post

NJIA YA BWANA INATENGENEZWA WAPI?

Kabla Bwana YESU kuanza huduma yake ya wokovu hapa duniani, Ilimpendeza Mungu amtangulizie kwanza mtu atakayemwandalia mazingira mazuri ya yeye kufanyia huduma yake, mtu atakayemtengenezea njia ya kupendeza iliyonyooka ili apate kupita juu yake. Mungu hakuona vema mwanawe mpendwa afanye kazi katika mazingira ambayo hayajaandaliwa kwa namna yoyote, hivyo kwa hekima zake nyingi akaona ni vema amtangulize kwanza mtu atakayeanza kuzungumzia habari za kuja kwake kabla ya yeye kufika, kusudi kwamba atakapofika watu wawe tayari kumpokea kwa furaha, kadhalika awe mtu atakayeigusia habari ya injili ambayo yeye atayaokuja kuihubiri mbeleni na ndio hapo tunakuja kumuona Yohana mbatizaji akihubiri habari za ubatizo na toba pamoja na ufalme wa mbinguni mambo ambayo hayakujulikana na wayahudi hapo mwanzo.

Na injili hiyo hiyo ya ufalme wa mbinguni ndiyo YESU aliyoanzana nayo katika huduma yake. Jambo lililomfanya Yohana kuonekana mtu MKUU sana katika ufalme wa mbinguni kuliko hata wote waliomtangulia katika agano la kale. Kwasababu yeye pekee ndiye aliyefanikiwa kumtengenezea Mungu NJIA ya kutembelea hapa duniani hakukuwa na mwingine yeyote aliyefanikiwa kufanya vile au kufikia viwango vile kabla yake.

Marko 1: 1 “Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.

2 Kama ilivyoandikwa katika nabii Isaya, Tazama, namtuma mjumbe wangu Mbele ya uso wako, ATAKAYEITENGENEZA NJIA YAKO.

3 Sauti ya mtu aliaye nyikani, Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni mapito yake.

4 Yohana alitokea, akibatiza nyikani, na kuuhubiri ubatizo wa toba liletalo ondoleo la dhambi.

5 Wakamwendea nchi yote ya Uyahudi, nao wa Yerusalemu wote, wakabatizwa katika mto wa Yordani, wakiziungama dhambi zao.

6 Na Yohana alikuwa amevaa singa za ngamia na mshipi wa ngozi kiunoni mwake, akala nzige na asali ya mwitu”.

Lakini swali la kujiuliza hapo ni kwanini Yohana alionekana kuwa ni mtu azungumzaye kutoka NYIKANI. Tunapaswa tujue maana ya maisha yake ya nyikani na jangwani, ili kwamba tufahamu ni kitu gani kilichompelekea awe mtu wa namna ile, kumbuka Mungu huwatumia manabii wake kuwa ISHARA kwa ajili ya Neno lake ili kufunua mambo ya rohoni. Sasa kama tukisoma Isaya 40:3 inasema..

Isaya 40:3 “Sikiliza, ni sauti ya mtu aliaye, ITENGENEZENI NYIKANI njia ya Bwana; NYOSHENI JANGWANI njia kuu kwa Mungu wetu.

4 Kila bonde litainuliwa, Na kila mlima na kilima kitashushwa; Palipopotoka patakuwa pamenyoka, Na palipoparuza patasawazishwa;

5 NA UTUKUFU WA BWANA UTAFUNULIWA, Na wote wenye mwili watauona pamoja; Kwa kuwa kinywa cha Bwana kimenena haya.”

Unaona hapo?. Isaya anasema NJIA YA BWANA haitengenezwi mahali pengine popote isipokuwa nyikani, kadhalika NJIA KUU YAKE hainyooshwi mahali pengine popote isipokuwa jangwani..Hivyo JANGWANI na NYIKANI ni mahali ambapo njia ya Bwana inapotengenezewa..

Na ndio maana tunaomwona mtu kama Yohana Mungu alimtumia kama ishara ya wazi kuwa mtu wa majangwani na nyikani kuonyesha kuwa huko ndiko Njia ya Mungu inapotengenezewa..Yeye aliufahamu ujumbe huo ambao nabii Isaya aliuhubiri kwa miaka zaidi ya 700 iliyopita, akajua hilo Neno si la mtu Fulani pekee tu, bali ni kwa yeyote atakayeliishi, na hilo Neno linaishi kwa kila kizazi na ndio maana utamwona japo Yohana alikuwa ndiye mtu aliyemtengenezea Bwana njia lakini bado aliwahubiria watu na makutano kuwa wao nao WAMTENGENEZEE BWANA NJIA YA KUSHUKIA..

Ukiendelea kusoma hapo katika Isaya utaona inasema:

“4 Kila bonde litainuliwa, Na kila mlima na kilima kitashushwa; Palipopotoka patakuwa pamenyoka, Na palipoparuza patasawazishwa;

5 NA UTUKUFU WA BWANA UTAFUNULIWA, Na wote wenye mwili watauona pamoja; Kwa kuwa kinywa cha Bwana kimenena haya.”

Sasa mabonde yanayozungumziwa hapo ni mabonde yote yanayoweza kukwamisha kusudi la Mungu lisifunuliwe kwa watu wake kupitia wewe, hayo yote yataondolewa si pengine zaidi ya jangwani na nyikani, milima yote, na makando kando yote yanayoweza kukwamisha utukufu wa Mungu usifunuliwe juu ya watu wote yataondolewa pale tu mtu atakapokubali kuipitia njia ya nyikani na jangwani.

Kumbuka wana wa Israeli wasingeweza kumjua Mungu wa Yakobo ni nani na anataka nini katika maisha yako kama ingekuwa ni kutoka tu Misri na moja kwa moja kufika Kaanani, japo waliuona kweli mkono wa Mungu ukiwapigania na kuwashindania dhidi ya maadui zao, kwa ishara nyingi na miujiza mingi lakini bado wangefika nchi ya ahadi pasipo kumjua Mungu wanayemtumikia. Iliwapasa kwanza wapitie njia ya JANGWA NA NYIKA muda mrefu ili Mungu awape amri zake na sheria zake. Iliwapasa wapitie kule ili Mungu aondoe vinyago vilivyokuwa ndani ya mioyo yao. Walikaa nyikani mbali na mataifa mengine kwa muda mrefu wakilishwa tu mana siku zote walizokuwa kule jangwani. Mungu hakuwaruhusu wafanye biashara yoyote na mataifa ya pembeni, wala shughuli zozote za kimaisha, yeye pekee ndiye aliyekuwa anawalisha mana. Aliwatenga mbali sana na tamaa za ulimwengu na macho mahali ambapo ukiangalia mkono wa kulia huoni miji wala majengo mazuri isipokuwa milima na mabonde tu kwa muda wa miaka mingi, mahali pakame sana, walisahau anasa na vitu vitamaniwavyo vya ulimwengu huu, Mungu aliwaua kwa habari ya dunia, aliwanyenyekeza kiasi kwamba vile viburi walivyotoka navyo Misri hawakuingia navyo Kaanani.

Na huko ndiko walipotoka na sheria na kanuni za kutembea na Mungu katika hiyo nchi waliyokuwa wanaiendea. Huko ndipo walipomtengenezea Mungu NJIA KUU ya kutembelea kwa utukufu wake.

Milima yote ya kiburi ilishushwa kule jangwani, mabonde yote ya ouvu yalisafishwa walipokuwa kule jangwani. Walipokuwa wanasua sua kwa kutokumwamini Mungu walitengenezwa upya Hivyo walipokuwa wakiingia katika nchi ya ahadi walikuwa tayari kwa kumtumikia Mungu na kwa kupitia wao MUNGU KUONYESHA UTUKUFU WAKE KWA MATAIFA YOTE YA DUNIA NZIMA.

Mwangalie Musa, mwanzoni alidhani kuwa anaweza kuwaokoa wana wa Israeli,kwa siasa na elimu yake na cheo chake alichokuwa nacho Misri, lakini haikuwa hivyo badala yake ndio alijitafutia matatizo, mpaka pale alipokimbilia jangwani huko nchi isiyokuwa na raha zile alizokuwa anazipata katika jumba la kifalme Misri, na kukaa huko muda mrefu kumtafakari na kuulizia juu Mungu wa baba yake Ibrahimu. Mungu alimtweza huko kwa muda wa miaka 40, akiiua ile asili ya kidunia iliyokuwa ndani yake, akiishusha milima yote ya majivuno iliyokuwa imejificha ndani yake, akitoa elimu yake ya kipagani iliyokuwa imeujaza moyo wake kwa muda wa miaka 40 alikuwa anamwandalia tu Mungu njia ya kupitia, mpaka pale alipokamilishwa biblia inasema alikuwa ni mjuzi wa usemi na kunena [mwanasiasa mzuri] (Matendo 7:22) lakini alipokutana na Bwana hata ule ujuzi wake wa kuongea hakuwa nao tena ndani yake ulishakufa, Bwana pia anamshuhudia Musa na kusema kuwa yeye ndio alikuwa mtu MPOLE kuliko wote duniani(Hesabu 12:3), jaribu kufikiria jambo hilo, utagundua kuwa kutembea na Mungu au kuwa karibu na Mungu sio kiwango cha upako ulichonacho, hapana bali ni jinsi gani moyo wako umeandaliwa katika kanuni azitakazo yeye. Sasa baada ya Musa kufikia viwango hivyo ndipo UTUKUFU WA MUNGU ULIPOFUNULIWA JUU YAKE. NA WATU WOTE WAKAUONA.

Mambo yanatupa mwongozo gani katika Roho?.

Kumbuka Wana wa Israeli katika mwili ndio sisi(Wakristo) katika roho. Kwasababu hata Bwana wetu aliandikiwa hivyo..katika Mathayo 2:15 ikisema…Kutoka Misri nalimwita mwanangu..Unaona maneno hayo yalikuwa ni ya wana wa Israeli, baadaye yakaja kuwa ya Bwana wetu Yesu Kristo kadhalika pia ni ya kwetu sisi leo hii kama tukitii KUTOKA MISRI MUNGU ALITUITA..Na kama tuliitwa kweli kutoka Misri hatuna budi kupitia njia ya nyikani na jangwani ili kuifikia nchi ambayo Mungu ataachilia UTUKUFU WAKE kuwaokoa wengine.

SASA NYIKANI NA JANGWANI NI WAPI KWA SASA?.

Unapopompa Bwana maisha yako kwa mara ya kwanza, hauna budi kuwa radhi kusalimisha kila kitu chako kwake ili aweze kukufanya kuwa mwanafunzi wake, ili Mungu baadaye aweze kukutumia wewe kuachilia utukufu wake uwaangazie wengine ni sharti ukubali kutii kupitia madarasa ya Mungu na ndio maana Bwana Yesu aliwaambia maneno haya wale wote ambao walitaka kuwa wanafunzi wake.

Luka 14.25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,

26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.

27 MTU YE YOTE ASIYEUCHUKUA MSALABA WAKE NA KUJA NYUMA YANGU, HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU.

28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia?

29 Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki,

30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza.

31 Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini?

32 Na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali.

33 BASI, KADHALIKA KILA MMOJA WENU ASIYEACHA VYOTE ALIVYO NAVYO, HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU.”

Unaona hapo?. Zipo gharama za kuwa mwanafunzi, kumbuka sio watu wote wanaweza wakawa wanafunzi wa Kristo,. Kama Usipokuwa tayari kupoteza kila kitu ulichonacho kwa ajili ya Kristo, kama vile mwanafunzi shuleni, anasahau kabisa dunia ikoje anakaa bweni miaka kadhaa akisoma tu,asijishughulishe na kitu kingine na kusahau tamaa za nje alizokuwa anaziona, na ndivyo ilivyo kwa wale wanaopenda kuwa wanafunzi wa Kristo, usipokubali kupita katika njia ya jangwa na kuishi maisha ya kumwangalia yeye tu, hutaweza kuwa mwanafunzi wake, usipokuwa tayari kuichukia hata nafsi yako kwa ajili ya Kristo, usipokuwa tayari kuacha anasa zako, usipokuwa tayari kuacha hizo biashara haramu kwa ajili ya Kristo, na usipokuwa tayari kuchukiwa na ndugu, hata wakati mwingine wazazi kwa ajili ya Kristo, huwezi kuwa mwanafunzi wake, usipokuwa tayari kuishi kwa kumtegemea Mungu tu, akufundishe, kama wana wa Israeli jangwani, kama Yohana jangwani, kama Musa jangwani, kama Eliya jangwani, kama Elisha nyikani, huwataweza kumwandalia Mungu njia ya kushukia. Usipokuwa tayari kupoteza vitu uvipendavyo kwa ajili ya madarasa ya Kristo hutaweza kumtengenezea njia ya yeye kushukia.

Isaya 40:3 “Sikiliza, ni sauti ya mtu aliaye, ITENGENEZENI NYIKANI njia ya Bwana; NYOSHENI JANGWANI njia kuu kwa Mungu wetu.

Hivyo yeye atakayeshinda kulivuka hilo jangwa na hiyo nyika ambayo Mungu atampeleka huko makusudi kwa ajili ya kumfundisha hapo ndipo atatiwa mafuta na Mungu mwenyewe ili kuwahudumia watoto wake.

Bwana Yesu anasema mtu wa namna hiyo ni mkuu zaidi ya nabii yoyote yule. Mtu yoyote Yule ambaye atamtengenezea Bwana njia iliyonyooka, huyo ni mkuu kushinda nabii yoyote Yule alishawahi kutokea duniani Bwana YESU anasema hivyo.

Mathayo 11:9…..Naam, nawaambia, na aliye mkuu zaidi ya nabii.

10 Huyo [mtu huyo] ndiye aliyeandikiwa haya, Tazama, mimi namtuma mjumbe wangu Mbele ya uso wako, Atakayeitengeneza njia yako mbele yako.

Hivyo kama na sisi tunataka tuwe wajumbe watakaomtangulia mbele yake, inatupasa tumwandalie njia kwanza kabla ya kufika, na njia haiandaliwi mahali popote tu isipokuwa NYIKANI NA JANGWANI.

Tusijidanganye tunasema sisi ni watumishi wa Mungu, sisi tuna nena kwa lugha, sisi tuna upako, sisi tunatoa pepo, sisi tunaponya magonjwa, na huku madarasa ya Mungu tumeyakwepa, na huku ndani ya mioyo yetu tuna viburi, ndani ya mioyo yetu tuna sanamu, ndani ya mioyo yetu hatujaumbiwa saburi na unyenyekevu, ndani ya mioyo yetu ni wanung’unikaji, tusijidanganye ikiwa tumelikwepa hilo jangwa ambalo kwa hilo tungefundishwa sheria na kanuni za Mungu,

Na maombi yangu, tusikwepe madarasa ya Mungu yanapoletwa mbele yetu, pale tunapoteremshwa jangwani tusipindishe njia na kutaka kurukia moja kwa moja Kaanani siku hiyo hiyo, Mungu huwa anatembea katika kanuni zake, ikiwa wewe ni mtoto kweli wa Mungu siku inakuja Mungu atakapeleka nyikani tu, hilo ni darasa lisilokwepeka. vinginevyo mbele za Mungu tutaonekana watoto wachanga tusiomjua yeye. Hawakuwa na bahati mbaya mitume wa Kristo kupoteza vyote walivyonavyo kwa ajili ya Kristo, kadhalika haitakuwa bahati mbaya kwetu nasi tukipoteza vyote tulivyonavyo kwa ajili ya Kristo, kwasababu hiyo ndiyo njia pekee ya kuwa WAKUU MBELE ZA MUNGU na kuwa wanafunzi wake.

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

MELKIZEDEKI NI NANI?.

MWEZI NI ISHARA GANI KWETU?.

SEHEMU YA MAANDIKO ILIYOFICHWA.

MAVAZI YAPASAYO


Rudi Nyumbani

Print this post

UMEFUNGWA KATIKA GIZA NA UVULI WA MAUTI?

Ni rahisi kudhani kuwa watu wote walio waovu, au wauaji au wanaofanya vitendo vya giza kama vile uchawi ni mambo ambayo walizaliwa kuyapenda, na hiyo wakati mwingine inapelekea hata maombi yetu kwa Mungu tunayoyaelekeza kwao ni ya kifo tu, na si kingine. Lakini hatujui kuwa wengi wao wanaofanya mambo kama hayo mwanzoni hawakuwa na nia ya kuwa wachawi, au wauaji, bali ilitokea kuna wakati waliingiwa na tamaa ya kitu Fulani labda tuseme mali, na ndani ya mawazo yao wanafikiria mali tu na si kingine, huo ndio mtengo mkubwa shetani anaowanasia watu kwasababu biblia ilishasema katika..

1Timotheo 6.10 “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni KUPENDA FEDHA; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.”

Unaona sasa katika kuhangaika kwao ndio wanajikuta kidogo kidogo wanaanza kwenda kwa waganga, na kule kwa mganga anapewa labda masharti Fulani ambayo yanamgharimu kuwa mshirikina, na kwa jinsi siku zinavyozidi kuendelea, kwa kuwa lengo la shetani ni kumvuta kwake ili awe mtumishi wake wa UHARIBIFU hivyo anampa vitu anavyovihitaji kwa muda na baadaye analazimishwa kuwa mchawi na huko ndiko anapopewa majukumu makubwa hata ya kutoa roho za watu ili tu aendelee kuishi na kwamba asipofanya hivyo yupo katika hatari ya kuuliwa yeye naye, sasa hatua hiyo aliyofikia hata akijaribu kutoka hawezi, haoni pa kukimbilia, hivyo anajikuta anamalizia kuendelea tu hivyo hivyo huku dhamira yake ikiugua kila siku akifahamu kuwa anayofanya sio sahihi, lakini hawezi kutoka kwasababu ameshaingia katika mtego asioweza kujinasua tena..

Na sisi kwa kuwa hatuna jicho lingine la mbali katika ulimwengu wa roho tunawaombea kifo,.Hatujui kuwa chanzo cha mambo yote ni ibilisi. Kadhalika unakuta na mtu mwingine alijiingiza katika kazi za ujambazi, lengo lake halikuwa kuuwa watu, hapana bali ni kupata mali, sasa hajui kuwa kumbe ni lengo la shetani kumfanya awe muuaji, pasipo kufahamu yeye anaingia huko, na mwisho wa siku katika harakati zake za wizi, siku moja pale anapoona kuwa anakaribia kukamwata analazimika kutoa bunduki na kumpiga mtu na kumuua pasipo yeye mwenyewe kupenda kwa lengo la kujilinda. Lakini sisi huku tunasema Yule jambazi ni katili sana, hana hata huruma.

Kadhalika wapo watu wengine ambao sio wachawi na wala sio wafanyaji wa vitendo viovu, lakini shetani naye anafanikiwa kuwanasa katika mitego yake ya uharibifu.

Kwamfano ngoja nikupe kisa kimoja ambacho kimetokea hapa mtaani kwetu wiki hii.

Kuna kijana mmoja mdogo tu kama miaka 18, ni kijana ambaye ni mtulivu, hakuwa mlevi wala mtumiaji wa sigara, wala hakuwa katika vikundi vya vijana waporaji wa mitaani, lakini ghafla siku ya jumapili tulipata habari kuwa amejinyonga kwa kamba ndani kwao. Na kule kwenye msiba kulikuwa na mtu mwingine aliyehudhuria msibani naye anasema ndugu yake wiki hii hii kajinyonga. Sasa Kama ukichunguza watu wa namna hii vyanzo vinavyowapelekea wao mpaka kufikia hatua hiyo ngumu namna hiyo za kujitoa uhai hazijulikani..

Kwamfano huyu kijana wa kwanza alishawahi kujaribu kujiua mara mbili, haukufanikiwa moja alijaribu kumvamia dereva wa dalala ili aachie usukani gari lipinduke watu wafe pamoja naye kwenye gari, lakini alishikiliwa na watu, na baadaye kupigwa sana nusu kuuawa, na mara ya pili tena alikunywa sumu lakini walimuwahi akapona.

Sasa kwa namna ya kawaida kwa nje, ni rahisi kusema hawa watu ni WAJINGA, WAUAJI, au WANA DHAMBI NYINGI, WAKATILI, MASHETANI n.k. pasipo kujua kuwa wamenaswa katika mitego ambayo hawawezi kutoka kiuwepesi kama wewe unavyodhani na ndio maana wamelazimika kufanya hivyo, sio kwa hiari yao bali ni sababu ya vifungo vya giza kutoka kwa yule adui zimewafanya kuwa hivyo au kufanya vitendo kama hivyo.

Nguvu hiyo hiyo ilimnasa hata mmoja wa mtume wa BWANA wetu YESU KRISTO, naye ni Yuda, ambaye yeye ndio kabisa alikuwa anakula na kutembea na Bwana kila mahali je! Si zaidi kutunasa na sisi watu wa kawaida tusipokuwa makini?. kumbuka lengo la Yuda halikuwa kumsaliti Bwana ili auawe, hapana bali lilikuwa ni fedha tu basi, lakini kwasababu shetani alikuwa anaona mbali akijua kabisa Yuda atajutia kwa tendo lile na kisha baadaye amshawishi ajinyonge hivyo akatumia udanganyifu wa mali kumvuta kwake, na aliponaswa, akiona kuwa maji tayari yameshamwagika hayawezi tena kuzoleka. sasa ile nguvu ya adui ndipo ilipoanza kufanya kazi ndani yake kumpa sababu ya yeye kujiondoa uhai wake..Usidhani ni rahisi kujinasua unapofika katika hatua kama hiyo..Ni ngumu sana hapo inahitaji mkono wa Mungu ulio hodari..Lakini Yuda alizidiwa mpaka kufikia hatua ya KUJINYONGA.

Watu wa namna hii wapo wengi, wamenaswa katika mitego ya adui ya namna mbali mbali na hawawezi kutoka, inawezekana wewe unayesoma habari hii ni mmojawapo. Imefika hatua umezama kwenye uchawi na ushirikina wa viwango vya juu na unaona ni ngumu kutoka tena huko, umezama katika uuaji, umetoa mimba nyingi, umeua watu na shetani anakuambia kuwa wewe dhambi yako haiwezi kusameheka tena, na hivyo unahitaji njia ya kuutoa uhai wako, pengine umekata tamaa ya kuishi baada ya kugundua kuwa umeambukizwa ukimwi au unaugonjwa wa kufisha kama saratani, hivyo kila siku unatamani roho yako itoke usiendelee kuishi tena unatamani hata upate ajali ufe. Ndugu usifanye hivyo yupo tabibu anayeweza kuuganga moyo wako na kukufanya kuwa upya tena kana kwamba hukuwahi kutenda dhambi yoyote, kana kwamba hukuwahi kuumwa, au kumkosea Mungu.

Kama yeye mwenyewe anasema WENYE AFYA HAWAHITAJI TABIBU, BALI WALIO HAWAWEZI.(Mathayo 9:12).Huhitaji kudhani kuwa tatizo lako halina mtetezi..Kumbuka moja ya makusudi maalumu Bwana YESU yaliyomleta duniani ni pamoja na hiyo ya kuwaganga waliovunjika mioyo, na waliofungwa kufunguliwa kwao. Na hakuna yoyote mwingine zaidi yake anayeweza kuwa na hiyo Taaluma.

Isaya 61: 1 “Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao”.

Yeye pekee ndiye anayeweza kukupa wewe tumaini la uzima, haijalishi umeasi kiasi gani, haijalishi umefungwa katika vifungo vikubwa kiasi gani haijalishi umeshajiunga katika vikundi vya kichawi (occultic groups) vingi kiasi gani, haijalishi umeloga au umehudhuria kwa waganga wengi kiasi gani, haijalishi umeuwa na umetoa mimba nyingi kiasi gani, haijalishi una ugonjwa wa mauti kiasi gani ambao uliupata kwa kutokana na uzembe wako wa kuzini ovyo, hiyo haijalishi embu soma hapa:

Zaburi 107: 10 “Waliokaa katika giza na uvuli wa mauti, Wamefungwa katika taabu na chuma,

11 KWA SABABU WALIYAASI MANENO YA MUNGU, WAKALIDHARAU SHAURI LAKE ALIYE JUU.

12 Hata akawadhili moyo kwa taabu, Wakajikwaa wala hakuna msaidizi.

13 WAKAMLILIA BWANA KATIKA DHIKI ZAO, AKAWAPONYA NA SHIDA ZAO.

14 ALIWATOA KATIKA GIZA NA UVULI WA MAUTI, AKAYAVUNJA MAFUNGO YAO.

15 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.

16 Maana ameivunja milango ya shaba, Ameyakata mapingo ya chuma.”

17 WAPUMBAVU, KWA SABABU YA UKOSAJI WAO, Na kwa sababu ya maovu yao, hujitesa.

18 Nafsi zao zachukia kila namna ya chakula, Wameyakaribia malango ya mauti.

19 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.

20 HULITUMA NENO LAKE, HUWAPONYA, HUWATOA KATIKA MAANGAMIZO YAO”.

Bwana leo atalituma Neno lake na kukuponya kama utakuwa tayari kumruhusu yeye ayabadilishe maisha yako. Uwe tu tayari kutubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha kabisa, uwe tayari kusema kuanzia leo mimi na ulimwengu basi, mimi na shetani basi, mimi na dhambi basi namgeukia Bwana Yesu, tumaini langu, kisha ukishatubu hatua inayofuata ni kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO ili upate ondoleo la dhambi zako, popote pale upendapo. Na kuanzia hapo na kuendelea Bwana atakupa uwezo wa kipekee wa kumshinda adui, hayo mapepo yaliyokufunga na yaliyokuwa yanakutishia kukuua yataondolewa na YESU mwenyewe,bila hata kutumia nguvu. huo ugonjwa wa mauti wanaosema hauponyeki YESU KRISTO atakuponya, hiyo hofu ya kutokusamehewa iliyo ndani yako na inayokutaka ujiue,jua tu ni ibilisi ndio kaiweka na Yesu pekee ndio ataiondoa.. Hivyo chukua uamuzi sasa maadamu damu ya Yesu ipo kukuganga, usisubiri baadaye au kesho, saa ya wokovu ni sasa.

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; NANYI MTAPATA RAHA NAFSINI MWENU;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.”

RAHA YA NAFSI YAKO UTAIPATA KWA YESU TU PEKEE.

Ubarikiwe sana.Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Print this post

MAFUNDISHO YA MASHETANI

1 Timotheo 4 : 1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;”

Biblia inasema, nyakati za mwisho wengine, watajitenga na IMANI, Imani inayozungumziwa hapo si imani nyingine zaidi ya Imani katika Yesu Kristo.

Mungu alimuumba mwanadamu na sehemu mbili, Sehemu ya Roho na Sehemu ya mwili.

Sehemu ya mwili ndio hii tunayoiona kwa macho, milima, mabonde, miti, nyumba, bahari, wanadamu, wanyama n.k. Na sehemu ya Roho hatuioni kwa macho, imefungwa kwetu wanadamu.

Sehemu hii ya Roho ndio mahali Mungu, anapoonekana, na ndio mahali malaika wanapoonekana na ndio mahali shetani na malaika zake wanapoonekana, ndio mahali vita vinapopiganwa na ndio mahali vyanzo vya mambo yote vinapotokea.

Sasa baada ya Adamu kuanguka, Bwana hajaruhusu tuingie katika ulimwengu wa Roho, hakuruhusu macho yetu ya Roho yafumbuliwe tuone kila kitu kinachoendelea katika ulimwengu wa Roho.Na endapo tungefumbuliwa macho tuone mambo gani yanaendelea katika ulimwengu wa Roho duniani kusingekuwa mahali pa kukalika, kwasababu tungekuwa tunaona mambo mengi mno ya ajabu, na kila siku tungekuwa tunaona mambo mapya. Tungekuwa tunaona mambo mengine ambayo yangekuwa hata hayatusaidii..Ingekuwa ni dunia iliyojaa vurugu mno. Kwasababu ulimwengu wa Roho umejaa mambo mengi.

Tuchukue mfano, wakati ule Nabii Elisha alipomwomba Mungu amfungue macho Yule mtumwa wake, na alipofunguliwa macho aliona kilima chote kimejaa jeshi la malaika wenye upanga..Sasa kumbuka malaika hata siku moja hawapigani na wanadamu, bali wanashindana na majeshi ya mapepo wabaya.. kwahiyo kama kulikuwa na majeshi ya malaika wa mbinguni, ni wazi kuwa yalikuwepo pia majeshi ya mapepo yaliyokuwa tayari kushindana na lile jeshi la malaika, kwahiyo kama Bwana angeruhusu Yule mtu aendelee kuona yale mambo ya rohoni ni wazi kuwa angeona vita viwili vinaendelea, vya kwanza vya malaika na vya pili vya wanadamu.

2 Wafalme 6: 15 “Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule mtu wa Mungu alipoondoka, na kwenda nje, kumbe! Pana jeshi la watu, na farasi na magari, wameuzingira mji ule. Mtumishi wake akamwambia, Ole wetu! Bwana wangu, tufanyeje?

16 Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.

17 Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote”.

mafundisho ya mashetani

Kwahiyo unaweza ukaona kuwa ulimwengu wa Roho, wa malaika upo, na una mambo mengi mno, yasiyoelezeka na mengine ni magumu kuyatambua, yamekaa kimafumbo jaribu kufikiri Yohana aliyeandika kitabu cha ufunuo anaona malaika wana Uso wa TAI, mwingine ana kichwa cha NDAMA, mwingine ana kichwa kama cha SIMBA na bado wana mabawa, na wana kwato!! Umewahi kujiuliza hivyo viumbe endapo tukiwa tunaviona kila siku duniani kutakuwaje?? Nabii Ezekieli naye alionyeshwa mambo hayo hayo,Nabii Isaya naye alionyeshwa mambo hayo hayo, lakini hawakuyaelewa kwa undani mambo hayo kwasababu ni mambo ya Rohoni.

Kwahiyo ni wazi kuwa Sio mpango wa Mungu, tuwe na uwezo kila dakika kuyaona mambo ya rohoni, vinginevyo maisha yatakuwa hayana maana.

Lakini maandiko yanasema Yohana 4.23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu. 24 MUNGU NI ROHO, NAO WAMWABUDUO YEYE IMEWAPASA KUMWABUDU KATIKA ROHO NA KWELI.”

Sasa hapa ndipo pa kuzingatia sana, maana pasipoeleweka vizuri, ni rahisi shetani kumzamisha mtu katika MAFUNDISHO YA MASHETANI.

Biblia inasema “saa yaja ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli”

Biblia iliposema “katika roho na kweli” haikumaanisha kuwa itafika wakati tutakuwa tunazama katika ulimwengu wa roho na kufikia kumwona Mungu na malaika, na hatimaye kumwabudu tukiwa tunamwona wazi kama tunavyowaona mwanadamu wenzetu.. Hapana haikumaanisha hivyo…

Na Shetani ndipo alipoanzia hapa kupandikiza mafundisho yake ya mashetani.

Nini maana ya kumwabudu Mungu katika ROHO NA KWELI?

Kabla ya kujua maana ya kumwabudu Mungu katika roho na kweli, hebu turudi nyuma kidogo…Kumbuka kama tulivyosema ulimwengu wa Roho ni ulimwengu wa Malaika, ikiwa na maana kuwa vita vyote na mambo yote yanayoendelea katika ulimwengu wa Roho Mungu huwa anawatumia malaika zake kuyafanikisha, mambo hayo namna ya kuyafanya na jinsi ya kuyafanya hayamuhusu mwanadamu hata kidogo sio sehemu ya mwanadamu..Ni kazi ya malaika Kwamfano Mungu alipomtuma Malaika Gabrieli kwa Mariamu kumpa taarifa za kuzaliwa kwa Mwokozi Bwana Yesu Kristo namna ya kuitengeneza ile mimba tumboni mwa Mariamu pasipo Mwanaume kuhusika haikuwa kazi ya Mariamu, au mwanadamu yoyote yule bali ilikuwa ni kazi ya Malaika wa Mungu katika uwezo wa Roho.

Mungu alipoyaleta yale mapigo yote kwa farao, na kuwaongoza katika lile jangwa kimiujiza haikuwa kazi ya mwanadamu kuyatengeneza yale mapigo..mwanadamu alikuwa na kazi yake tutakuja kuiona mbele kidogo.

Kadhalika kazi ya kuleta tauni katikati ya watu wakati wa Mfalme Daudi haikuwa kazi ya wanadamu bali ilikuwa ni kazi ya Malaika wakifanya kazi katika ulimwengu wa roho..Hao ndio Bwana aliowatia mafuta kuweza kufanya mambo makubwa yasiyowezekana kwa namna ya kawaida.

Sasa mwanadamu ambaye anamcha Mungu hajapewa maarifa hayo, mwanadamu anayemcha Mungu hajapewa uwezo wa kuingia kwenye ulimwengu wa roho na kutengeneza mambo au kuingia na kupambana na roho za malaika walioasi.

Sasa uwezo mwanadamu anayemcha Mungu aliopewa na Mungu ni mwongozo wa namna ya kuwafanya hawa malaika waweze kumhudumia yeye. Mwongozo wa namna ya kutembea na kundi hili la malaika watakatifu.

Ni sawasawa na mwanadamu na Farasi, mwanadamu hajapewa uwezo wa kukimbia kwa kasi kama farasi, hajapewa mapafu kama ya farasi, lakini amepewa uwezo wa kumwongoza Yule farasi amtii yeye ampeleke katika mwendo anaotaka..

Na huo mwongozo mwanadamu aliopewa utakaomsaidia yeye kutembea na malaika walio na nguvu na uwezo katika ulimwengu wa Roho ni BIBLIA TAKATIFU (yaani NENO LA MUNGU). Ni kama tu Mtu asiyekuwa na MANUAL ya kuendesha gari, hataweza kuliendesha gari hilo hata iweje, kadhalika mtu ambaye hajafundishwa namna ya kumpanda farasi na kumwendesha hataweza kumwendesha, badala yake anaweza akajikuta hata akajeruhiwa na Yule farasi farasi.

Naamini kidogo kidogo utakuwa umeshaanza kuelewa nini maana ya kuingia katika ROHO…Kwahiyo maana ya kuingia katika roho sio kugeuka na kuanza kujifananisha na malaika, au mapepo hapana bali ni kuelewa uwezo uliopewa wa kutembea na malaika ambao hao ndio wanaojua namna ya kutengeneza mambo katika ulimwengu wa roho.

Kwasababu hiyo basi Mwanadamu anayemcha Mungu hawezi akajua njama za adui zote na elimu yake kwa mapana na marefu, hawezi akajua idadi ya mapepo yaliyopo, hawezi akajua yanafanyaje fanyaje kazi..malaika watakatifu ndio wanaojua (wamepewa uwezo huo na Mungu mwenyewe) ..Sisi tunachojua tu tukitaka tulindwe na Yule adui Kwanza tumwamini Bwana Yesu Kristo, kisha tukabatizwe kisha tuishi maisha matakatifu na ya uangalifu, tukidumu katika kusali na ushirika. Hiyo inatosha kabisa kuwafanya wale malaika watakatifu watupiganie dhidi ya mapepo wabaya.

Tukitaka tusife tuishi maisha marefu, wale malaika Bwana aliowapaka mafuta katika ulimwengu wa Roho wanajua namna ya kumzuia shetani na mapepo wake wasituguse mpaka tutakapotimiza umri wa kuondoka duniani, hivyo kama maandiko yanavyosema “waheshimu baba yako na mama yako upate siku nyingi na za heri” hivyo wale malaika watakatifu wanatembea na mtu anayelishika neno hilo, na mtu Yule anajikuta anakingiwa na ajali na dhiki za Yule mwovu na kutimiza umri wa maisha yake..Sasa huyu mtu tayari kashaingia katika roho. Anakuwa anamwabudu Mungu katika roho na kweli. Kwasababu maneno ya Yesu Kristo ndio Roho. (Yohana 6:63)

Au mtu wa Mungu anapoumwa wale malaika wanaohusika na uponyaji, waliohusika na kuitengeza mimba ya Mariamu pasipo mwanamume kwa uwezo wa roho ndio hao hao pia wana uwezo wa kuondoa ugonjwa pasipo daktari lakini wanafanya kazi na mtu anayeliaimi neno hili “kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.

Kwahiyo hizo ndizo silaha zetu sisi katika ulimwengu wa Roho, kulishika NENO la Mungu pamoja Na kuwa na IMANI katika Neno lake.

Na ndio maana Mtume Paulo alisema katika..

Waefeso 4: 11 “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.

12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14 Basi simameni, hali mmejifunga KWELI VIUNONI, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

16 zaidi ya yote mkiitwaa NGAO YA IMANI, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni NENO LA MUNGU;”

Unaona hapo? Ukilijua Neno la Mungu kwa undani,wewe tayari ni Mtu wa rohoni, ambaye unashindana vita visivyoonekana kwa macho na unashinda, hauna haja ya kuona mapepo, hauna haja ya kuona wachawi, hauna haja ya kuona majini, vibwengo, hauna haja ya kumwona hata shetani mwenyewe,..na zaidi ya yote hauna haja ya kuwaona hata malaika..Wao wanafanya kazi zao katika ulimwengu wa roho ambao wewe ndio unaoupalilia kwa kulishika na kuliamini Neno la Mungu..

Sasa mafundisho ya mashetani leo ni yapi?

Mafundisho ya mashetani ni yale yanayokufundisha kwamba unaweza ukaingia katika ulimwengu wa roho na wewe ukashindana na mapepo kama wanavyofanya malaika…Ndio hapo shetani anatumia nguvu kubwa kuwavuta watu wasilijue Neno la Mungu, na kuwafanya wakeshe kutafuta kujua elimu za mapepo, utakuta anawafundisha watu aina za mepepo na majini, na utendaji wao kazi. Wengine wanawafundisha watu wasile vyakula Fulani au wasipande miti Fulani majumbani mwao, kwasababu vina uhusiano wa moja kwa moja na mapepo n.k.

Wengine wanafundisha watu kwamba usiende kuogelewa baharini au mtoni saa 7 au kabla ya kuogelea baharini, kemea kwanza pepo la maji, kwamba kabla ya kupita karibu na makaburi kemea kwanza pepo la mauti lisije likakuingia, unapokaribishwa kwa mtu usiyemjua usile kwanza chakula Fulani, kwamba ukiona mtu kakuamkia na kukuonyesha ishara Fulani, kemea hilo ni pepo la mauti, unapougua kichomi basi umetumiwa jini Fulani n.k..

Unapofika mahali Fulani usipende kutenda wema, nyota yako itachukuliwa n.k nataka nikwambie ndugu hizo zote ni ELIMU ZA MASHETANI.!!

Sisi tuliompa Bwana Yesu Kristo maisha yetu tunafahamu Neno moja tu!! Nalo ni hili “Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Hesabu 23:23”. Hiyo ndio silaha tuliyo nayo sisi..Ni namna gani inatenda kazi?? Hatujui Malaika ndio wanaojua…wao ndio wanaojua kuna aina ngapi za vibwengo, na wachawi, na mapepo na namna ya kuwashughulikia sisi sio kazi yetu kujua aina za mapepo na utandaji kazi wao…

Tunapotenda wema na kuambiwa nyota zetu zitachukuliwa…hilo hatulijui sisi tunachojua ni kwamba.. “hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyetu utakaopotea, na nywele zetu zote zimehesabiwa Luka 21:18” Ni kwa namna gani hilo linatenda kazi? Hiyo sio kazi yetu kujua, Malaika watakatifu ndio waliobobea katika mambo ya rohoni hao ndio wanazo hizo teknolojia ya kuzihifadhi nyota zetu kama zipo, sisi hatuna huo uwezo. Sisi kazi zetu ni kulishika Neno lake tu!

Biblia inatuonya hizi elimu/mafundisho siku za mwisho yatakuwa mengi, yakiwatoa watu katika Imani lengo ni kuwafanya watu wajitenge na Imani, . Na badala ya kumfungua mtu, utakuta ndio zinamfunga na kumfanya awe mwoga wa wokovu wake, Hata siku moja Mungu hamletei mtu hofu, bali ujasiri, utakuta watu wamehama nyumba zao kwa kuogopa zimezindikwa na wanahubiriwa hivyo na wanaojiiita watumishi. Wengine kila kukicha ni kufundishwa utendaji kazi wa mapepo tu!! Kila kitu kitakachokuja mbele yako ni kukemea, ukiingia hospitali kemea, kabla ya kulala mwaga damu ya Yesu chooni, mapepo yasikuvae, saa kumi jioni majini aina Fulani yanafunguliwa hivyo usipende kula kitu Fulani huo wakati. Na mambo mengine mengi yanayofanana na hayo, kila kitu ni mapepo mapepo tu!!

Dada/Kaka unayesoma haya, tafuta kulijua Neno la Mungu na kuliamini, hayo mengine sio kazi yetu kujua, Mtafute Bwana alisema katika Neno lake Maneno yake ndiyo Roho na Uzima(Yohana 6:64)…na maneno yake sio mengine zaidi ya Biblia takatifu, kwahiyo kwa lugha nyingine unaweza kusema biblia takatifu ndio Roho na uzima..Hivyo kuwa mtu wa rohoni ni kuyaishi na kuyaamini maneno ya Yesu Kristo 100% na si kingine.

Kama unataka leo hii uwe mtu wa rohoni, mtii leo maneno yake anayokuambia, kwa kukusudia kutubu dhambi zako kabisa kwa kumaanisha kuacha uasherati wako, kwa kukusudia kuacha pombe zako, uvaaji wako mbaya {vimini, surali,wigi,wanja,lipstick, herein n.k}, kwa kumaanisha kuacha wizi wako, utukanaji wake, rushwa zako, usengenyaji wako n.k Ili uwe na uhakika wa kuurithi ufalme wa mbinguni na kuruhusu Malaika wa Bwana watembee na wewe siku zote za maisha yako, na kuepukana na mafundisho ya mashetani

Mungu akubariki

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kama umempa Bwana maisha yako, tafadhali tangaza habari zake kwa kadri uwezavyo kwa watu wengine wasiomjua yeye.


Mada zinazoendana


SHETANI NI NANI?

 DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI NI IPI?

HUDUMA KUMI (10) ZA SHETANI DUNIANI NI ZIPI?


Rudi Nyumbani

Print this post

JE! UMEFUNDISHWA?

Wafilipi 4.10 “Nalifurahi sana katika Bwana, kwa kuwa sasa mwisho mmehuisha tena fikira zenu kwa ajili yangu, kama vile mlivyokuwa mkinifikiri hali yangu lakini hamkupata nafasi.

11 Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali yo yote niliyo nayo.

12 Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, NIMEFUNDISHWA kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.

13 Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”.

Katika maandiko haya Mtume Paulo, anasema AMEFUNDISHWA kushiba na kuona njaa…Hebu litafakari hilo neno kwa undani “NIMEFUNDISHWA”. Kufundishwa maana yake ni kupewa maarifa ambayo ulikuwa huyajui, hivyo ni wazi kuwa Mtume Paulo kuna wakati alikuwa hajafundishwa baadhi ya mambo mpaka ulipofika wakati Fulani wa kupokea mafundisho za dizaini hiyo..

Na moja ya mambo hapa ambayo Mtume Paulo anasema amefundishwa ni hili la “KUSHIBA NA KUONA NJAA”. Ikiwa na maana kuwa kuna wakati Mungu alimpitisha katika kipindi cha uhitaji mkubwa (kipindi kikali cha kuona njaa) ili amfundishe huko.. Na kuna wakati pia Mungu alimpitisha katika kipindi cha kushiba ili pia ajifunze.

Kwahiyo tunaona kuwa mojawapo ya tabia ya Mungu ni kumpitisha Mtu katika VIPINDI VIWILI, vya KUSHIBA na KUONA njaa. Vipindi vya KUPUNGUKIWA na KUWA NA VINGI, Vipindi vya kupandishwa juu na vipindi vya kushushwa.(Mhubiri 3). NIA NA MADHUMUNI YA MUNGU..NI ILI TUFIKIE MAHALI TUWE RADHI NA VITU TULIVYONAVYO. Tufikie mahali tusipepesuka na hali yoyote tutakayokutana nayo katika siku za usoni.

Unajua kuna tabia moja Fulani ambayo baadhi ya majeshi mengi duniani wanayo,  pindi wanapomsajili mwanachama mpya katika jeshi huwa wanamchukua Yule mtu kwasababu ndio kajiunga kwa mara ya kwanza,hajui kanuni cha jeshi, wanamchukua na kuanza kumwonea au kumfanyia mambo ya kumuudhi…utaona kafika tu kesho yake, anaanza kupigwapigwa pasipo sababu, pengine ametulia tu hajafanya kosa lolote anajikuta  mtu anatokea na kuanza kumtukana pasipo sababu na kumshurutisha kufanya jambo Fulani, utakuta kalala na mtu anakuja kumwamsha na kumpiga bila sababu, na mambo mengi mabaya ya kuudhi hapo hakuna wa kumsaidia. Sasa huo ndio umekuwa utaratifu wa majeshi mengi duniani kufanya hivyo, nia na makusudi yao sio kumtesa Yule mgeni, au kumwonea hapana bali kumtolea ndani yake “ile hasira ya asili (kupanic) ambayo kila mtu anakuwa amezaliwa nayo ” Ili kumpa uwezo wa kustahimili mambo magumu atayoweza kukutana nayo katika vita.

Kwahiyo utaona mara za kwanza anapigwa, na kuanza kunung’unika saa hiyo hiyo, na wakati mwingine kurudisha mapigo au matusi au kununa kwa muda mrefu, na kutengeneza kinyongo lakini siku zinavyozidi kwenda anakuwa anazoea zile hali hivyo hata akifanyiwa hayo mambo mara nyingi vipi  anajikuta  hapaniki tena kama zamani, anakuwa kawaida, haumii moyo tena kama alivyokuwa anaumia..Hiyo inamsaidia Yule mwanajeshi akiwa vitani atumie AKILI ZAIDI KULIKO HISIA. Kwahiyo hayo ni moja ya mafundisho tu ya majeshi ya watu wa Ulimwengu huu. Hicho ndicho kinachomtofautisha mwanajeshi na raia wa kawaida. Utashangaa ni kwanini anaweza akaona ndugu yake  mpendwa vitani labda kaka yake kapigwa risasi na kuuliwa, badala ya kuvunjika moyo na kulia pale, yeye ndio atambeba na kumuhifadhi kisha kuendelea na vita kana kwamba hajafiwa..Lakini ukirudi kwa watu wa kawaida mfano msiba umetokea kidogo tu utaona watu wanaanza kupiga mayowe  na wengine hata kukufuru..Ni kwasababu gani? Ni kwasababu hawajafundishwa. Hilo tu.

Lakini Kristo naye ana mafunzo yake, kabla ya kumpeleka mtu, katika vita vya kiroho..Na mojawapo ya mafundisho ndio hayo “KUFUNDISHWA KUONA NJAA na KUSHIBA”.

Wana wa Israeli kabla ya kufika nchi ya Ahadi, Bwana aliwapitisha jangwani na wakati mwingine alikuwa anawaacha waone njaa na kiu kwa muda mrefu ili awafundishe. Ili Watakapoingia nchi ya Kaanani wasilalamike watakapopitia mitikisiko kidogo tu. Walikuwa wanatembe jangwa masiku hawaoni maji.

Kumbukumbu 8: 1 “Amri hii ninayokuamuru leo mtaishika kuitenda, mpate kuishi na kuongezeka, na kuingia katika nchi ile ambayo Bwana aliwaapia baba zenu; nanyi mtaimiliki.

2 Nawe utaikumbuka njia ile yote Bwana, Mungu wako ALIYOKUONGOZA MIAKA HII AROBAINI KATIKA JANGWA, ili akutweze, kukujaribu kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo.

3 Akakutweza, AKAKUACHA UONE NJAA, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa MWANADAMU HAISHI KWA MKATE TU, BALI HUISHI KWA KILA LITOKALO KATIKA KINYWA CHA BWANA”.

Unaona! Wana wa Israeli kuna kipindi Mungu aliwaacha makusudi waone njaa lakini walikuwa hawafi wala hawaumwi, Ili wajue tu kuwa Mtu anaweza kuishi bila kula vyakula vya kimwilini na asife bali akaishi kwa Neno la Mungu tu.

Na ndio maana Bwana Yesu naye vivyo hivyo alipokwenda mlimani alifunga siku 40 usiku na mchana bila kula, na mwovu alipomjia na kumjaribu ageuze  jiwe kuwa mkate..alimpa jibu lile lile kuwa “MTU HATAISHI KWA MKATE TU BALI KWA KILA NENO LINALOTOKA KATIKA KINYWA CHA BWANA”..Kwasababu gani alimjibu vile ni kwasababu “HUKO NYUMA ALISHAFUNDISHWA KUSHIBA NA KUONA NJAA” kwahiyo kwake yeye AWE NACHO au ASIWE nacho vyote ni sawasawa. Awe na chakula asiwe na chakula kwake yeye ni sawa sawa..Anayaweza mambo yote kwa yeye AMTIAYE Nguvu. Anachojua ni kwamba Mungu hatamtupa kabisa.

Na ndio Mtume Paulo naye, hakuwahi kutamani fungu kutoka kwenye makanisa aliyoyazaa yeye kiroho, ingawa angestahili kupata fungu kutoka huko, lakini badala yake ndio anawaambia watu wa kanisa la Filipi ambalo walitamani sana kumuhudumia kwa mali zao..

Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; MAANA NIMEJIFUNZA KUWA RADHI NA HALI YO YOTE NILIYO NAYO. 

12 Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, NIMEFUNDISHWA kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.

13 Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”.

Hiyo ina maana kuwa HAHUBIRI INJILI YA KRISTO kwasababu anataka FEDHA, au kwasababu ANA FEDHA, hapana Bali anahubiri injili ya Kristo kwasababu ana NIA YA KRISTO NDANI YAKE, AWAVUTE WENGI KWAKE…AWE NACHO ASIWE NACHO KWAKE YEYE NI SAWASAWA Injili ya KRISTO ataendele kuihubiri.

Na sisi je! Tumefundishwa KUWA RADHI NA VITU TULIVYO NAVYO? Kwamba ifikie mahali hatumfuati Bwana Yesu kwasababu tunatafuta utajiri, au mali kutoka kwake, au hatumfuati kwasababu Tuna mali., Yaani ifikie hatua tunasema TUMEFUNDISHWA KUWA RADHI NA VITU TULIVYO NAVYO. Tumefundishwa kuridhika na vitu tulivyo navyo..viwe vingi au vichache tutamtumikia Bwana, tuwe tuna  Elimu tusiwe na Elimu kwetu iwe ni mamoja, tuwe matajiri tuwe maskini Thamani ya Kristo Kwangu ni ile ile. Niwe na chochote nisiwe na chochote tutaihubiri injili ya Kristo.

Kama hatujafunzwa hivyo Basi tumwombe Bwana atufundishe masomo hayo ili tuweze kutembea naye pasipo manung’uniko wala malalamiko Kama alivyotembea na Mtume Paulo..Hiyo itatusaidia sisi tunapopitia vipindi vya kupungukiwa tusijione wanyonge, na kuanza kutanga huku na huko, bali tujue ni vya muda tu, sisi tusonge mbele na Imani mpaka kuja kwake YESU KRISTO ambapo yeye mwenyewe atatufariji kwa taabu zetu hapa duniani.

Tafadhali wahubirie wengine habari njema ya Msalaba kwa kadri uwezavyo.

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KARAMA ILIYO KUU NI IPI?

MOYO ULIOELEKEA KWA MUNGU.

ROHO MBAYA KUTOKA KWA BWANA.

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?


Rudi Nyumbani

Print this post