Shetani ni nani?…Tafsiri ya Jina shetani ni ‘mshitaki’ au ‘mchongezi’. Kazi yake ni kuwashitaki watakatifu mbele za Mungu.
Jina lingine la shetani ni “LUSIFA” Maana yake ‘NYOTA YA ALFAJIRI’. (Isaya 14:12) Jina hili Lusifa aliitwa kabla hajaasi, baada ya kuasi ndio akawa shetani.
Alikuwa ni Malaika wa Sifa (Kerubi) huko mbinguni, alikuwa ni Mzuri kwa mwonekano na mkamilifu katika njia zake zote, aliishi katika taratibu za Mungu, na katika njia za Mungu, na hivyo akapata heshima kubwa mbinguni zaidi ya Malaika wengi (Ezekieli 28:14).. Alikuwa mkamilifu mpaka siku uovu ulipoonekana ndani yake (Ezekieli 28:15).
Kwasababu ya uzuri wake Moyo wake ukainuka, akataka kujiinua awe kama Mungu, aabudiwe kama Mungu na kwa ujuzi wake mwingi akawashawishi theluthi ya Malaika mbinguni (1/3) waambatane naye.
Vita, vikali vikatokea Mbinguni kati ya Malaika waliokataa kuungana na Lusifa na malaika waliokubali kuungana naye. Biblia haisema vita hivyo vilipiganwa kwa muda gani, lakini inasema mwisho wa siku lusifa pamoja na malaika wake walishindwa vita vile, na kutupwa chini duniani (Ufunuo 12:7).
Na vita hivyo bado havijaisha, vita vya kwanza vilipiganwa mbunguni, kati ya Malaika walio upande wa shetani na wale walio upande wa Mungu na Malaika waliokuwepo Upande wa Mungu wakavishinda, lakini vita vya pili na vya mwisho vinapiganwa hapa duniani na hata sasa bado vinaendelea..Na vitaisha mwisho wa dunia. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
1. Je! Ni nani aliyemdanganya shetani?
2. Huduma 10 za shetani sasahivi duniani ni zipi?
3. Mpango wa shetani kwa watoto katika siku hizi za mwisho.
4. Agenda kubwa ya shetani kwa kanisa hili la siku za mwisho
5. Mafundisho ya Mashetani ni yapi katika siku hizi za mwisho?
Swali: Je Bwana YESU alipanda mlimani na wanafunzi wake baada ya siku ngapi?..ni Sita au Nane?, Kwa maana katika Mathayo 17:1 na Marko 9:2 panaonyesha ni baada ya siku sita (6) lakini tukisoma Luka 9:28 panaonyesha ni siku ni nane (8) Je ukweli ni upi?.
Jibu: Turejee mistari hiyo..
Mathayo 17:1 “Na baada ya SIKU SITA Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani”
Hapa ni kweli tunasoma “Siku sita” na Marko 9:2 tunasoma vile vile ni siku sita (6).
Tusome tena Luka 9:28..
Luka 9:28 “Baada ya maneno hayo yapata SIKU NANE, aliwatwaa Petro na Yohana na Yakobo, akapanda mlimani ili kuomba”.
Hapa tunasoma ni siku nane (8) na si sita tena, swali ni je! Biblia inajichanganya?, au mwandishi mmoja amekosea?
Jibu ni La! Biblia haijichanganyi na wala hakuna mwandishi aliyekosea, wote wapo sawa na maneno yote ni hakika, kwasababu biblia ni kitabu kilichohakikiwa na Roho Mtakatifu mwenyewe na hakina makossa (Mithali 30:5).
Sasa kama ni hivyo kwanini panaonekana kuna tofauti ya siku?..
Mwandishi wa kitabu cha Luka alionyesha jumla ya siku walizokaa mlimani, na Mwandishi wa kitabu cha Mathayo na Marko wakaonyesha siku walizoondoka katika makazi yao na kuelekea mlimani.
Sasa ni kwamba baada ya Bwana kuwaambia wanafunzi wake kuwa wapo ambao hawataonja mauti hata watakapoona ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu, zilipita siku sita akawachukua wanafunzi wake baadhi (ambao ni Petro, Yohana na Yakobo) akapanda nao mlimani.
Na biblia haijaeleza katika hizo siku sita kabla ya kupanda mlimani walikuwa wanafanya nini au walikuwa wapi, pengine waliachana kidogo, au walikuwa katika huduma zilizowatenga kwa muda siku sita, mpaka ilipofika siku hiyo ya kupanda mlimani….hiyo yote haijaeleza lakini inasema tu baada ya siku sita alipanda nao mlimani, na ndicho Mwandishi Mathayo na Marko walichokieleza.
Lakini sasa Luka yeye hakulenga kuelezea siku waliyopanda mlimani, kwamba ni baada ya siku sita za yale maneno, bali yeye alisema “YAPATA SIKU NANE”… Hilo Neno “Yapata” ni neno la ujumla, likielezea Muda wa safari Nzima, kuwa ni SIKU NANE (8), Maana yake baada ya siku sita walipanda mlimani sawasawa na Mwandishi Mathayo na Marko na kule mlimani walikaa siku mbili (2), na kufanya jumla ya siku kuwa nane, ndicho mwandishi alichokilenga. (kwahiyo muda waliokaa mlimani ni siku mbili, lakini walipanda baada ya siku sita).
Kwahiyo biblia haijajichanganya hapo, bali ni uelewa wetu ndio unaojichanganya.
Je umempokea BWANA YESU?.. Na je unajua kuwa dalili zote zinaonyesha kuwa kizazi tulichopo ni cha mwisho?..Je umejiandaaje? Taa yako inawaka?
Luka 12:35 “Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;
36 nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na
Je bado unaendelea na maisha ya dhambi?, bado unakunywa pombe?, bado unazini, bado unajichua, bado unavaa kidunia?
Muda umeisha, msikilize Roho Mtakatifu, na usizisikilize roho zidanganyazo.
1Timotheo 4:1“Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani”
Maran tha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
TABIA SITA (6) ZA WANAFUNZI WA YESU.
KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?
Je maombi ya mlimani yana ulazima wowote kwa mkristo?
SWALI: Wanawake wenye cheo wanaotajwa kwenye biblia ni akina nani? (Matendo 17:12)
JIBU: Mitume walipoanza kulitekeleza agizo kuu la Bwana Yesu la kuenenda ulimwenguni kote kuhubiri injili, biblia inatuonyesha walikutana na makundi mbalimbali ya walioamini.
Sasa mojawapo ya kundi hilo ambalo liliipokea injili, walikuwa ni hawa wanawake wenye cheo.
Kwamfano tunaweza kuona jambo hilo katika ziara ya mtume Paulo kule Beroya.. alipofika kule alikutana wa wanawake wa namna hii, na akawahubiria wakaipokea injili.
Matendo ya Mitume 17:10-12
[10]Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi.
[11]Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.
[12]Basi watu wengi miongoni mwao wakaamini, na wanawake wa Kiyunani wenye cheo, na wanaume si wachache.
Wanawake wenye cheo ni wanawake waliokuwa na sifa ya aidha nafasi za juu za kiutalawa, au ushawishi mkubwa kwenye jamii zao au wenye mali nyingi.
Wengi wao walipokutana na injili ya kweli ya Bwana Yesu Kristo waliipokea na kugeuka.
Lakini tunaona mahali pengine, mtume Paulo alipokwenda, wayahudi walimfanyia fitina kwa kuwatumia watu wa namna hii ili kuwataabisha..Kwamfano alipofika kule Antiokia mji wa Pisidia, na kuhubiri injili kwa ushujaa na wengi kuokoka. Wayahudi kwa sababu ya wivu wakawashawishi baadhi ya wanawake na wanaume wa namna hii..Ili wawapinge akina Paulo. Kwasababu walijua nguvu yao kijamii ni kubwa kiasi gani, hivyo itakuwa rahisi kutekeleza adhma yao.
Matendo ya Mitume 13:50
[50]Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao.
Hivyo hiyo ni kututhibitishia hata sasa, Watu wenye vyeo wana nafasi ya kuwa washirika wa injili. Hivyo tusibague wa kumuhubiria, kwasababu wote Kristo amewafia msalabani. awe ni mbunge, au waziri, awe ni tajiri, au maskini, msomi, au asiye na elimu,. wote ni wa Mungu na wanastahili wokovu, wasipotumiwa na Mungu wao, shetani atawatumia. Hivyo nguvu zetu za injili ziwe sawasawa kwa watu wote.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Wale waliowekewa tayari ufalme ni akina nani?. (Mathayo 20:23).
Rudi Nyumbani
Je unaijua anwani ya msalaba?…na je unajua nguvu yake? Kama bado hujaifahamu basi leo ifahamu na anza kuitumia katika maombi yako, badala ya vitendea kazi vingine kama maji,chumvi na mafuta.
Yohana 19:19 “Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI.
20 Basi anwani hiyo waliisoma wengi katika Wayahudi; maana mahali pale aliposulibiwa Yesu palikuwa karibu na mji; nayo iliandikwa kwa Kiebrania, na Kirumi, na Kiyunani”
Jina la YESU WA NAZARETI ndio ANWANI ya maombi ya kila Mkristo.
Umeahi kujiuliza kwanini haijaandikwa YESU MGALILAYA, au YESU MBETHLEHEMU mji ule aliozaliwa, badala yake imeandikwa YESU MNAZARETI?..na tena kwa lugha zote tatu (3), zilizokuu za dunia.
Kuna nini katika Nazareti?
Nazareti ndio mji uliotabiriwa na manabii kubeba utambulisho wa Masihi Mkuu ajaye… hivyo huo ni mji wa UTAMBULISHO KIBIBLIA.
Mathayo 2:23 “akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo”.
Kwahiyo tunapotaja jina la YESU na kuelekeza yule wa NAZARETI tumelenga kwenye shabaha yenyewe hivyo mashetani yanaondoka, magonjwa yanaondoka, dhambi inaisha nguvu, kwasababu ndiye Masihi halisi aliyetajwa.
Hebu tulione hili zaidi…
Wakati Bwana YESU anamtokea Sauli alipokuwa anaenda Dameski kwa ajili ya kuwaua wakristo, utaona hakujitambulisha kama YESU wa Galilaya, au YESU aliye mbinguni, badala yake alijitambulisha kama YESU Mnazaeti ijapokuwa yupo mbinguni.
Matendo 22:6 “Ikawa nilipokuwa nikisafiri, nikikaribia Dameski, wakati wa adhuhuri, ghafula nuru kuu ilitoka mbinguni, ikanimulikia pande zote.
7 Nikaanguka nchi, nikasikia sauti ikiniambia, Sauli, Sauli, mbona unaniudhi?
8 Nikajibu, Wewe u nani, Bwana? Akaniambia, MIMI NI YESU MNAZARETI, ambaye wewe unaniudhi”.
Utaona pia Mitume wa Bwana YESU waliitumia hii anwani popote walipokwenda katika huduma zao.
Petro aliitumia alipokutana na yule kiwete aliyezaliwa katika hali ile..
Matendo 3:6 “Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende.
7 Akamshika mkono wa kuume, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu.
8 Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda; akaingia ndani ya hekalu pamoja nao, akienda, akiruka-ruka, na kumsifu Mungu.
9 Watu wote wakamwona akienda, akimsifu Mungu”.
Soma pia Matendo 2:22, Matendo 3:6, Matendo 4:10, Matendo 10:38, Matendo 26:9, Marko 1:24, Marko 16:6, Marko 10:47, Luka 24:9, Yohana 1:45, utazidi kuona jambo hilo.
Na hiyo pia ndio sababu Mungu aliruhusu Pilato aandike anwani ile juu ya msalaba… “YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI”. Kwa lugha zote kuu, ikimaanisha kuwa anwani ya wokovu wa msalaba kwa mataifa yote na lugha zote ni jina la YESU WA NAZARETI.
Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”
Maana yake njili inayohubiri msalaba pasipo kuhusisha anwani ya jina la YESU ni uchawi, maombi yoyote yasiyohusisha anwani ya jina la YESU ni unashiri na ibada za sanamu.
Kama anwani hiyo ya jina la YESU WA NAZARETI hata baada ya Bwana kupaa bado anaitumia akiwa mbinguni, sisi ni akina nani tuifanye iieshe matumizi katika zama zetu?, na kuweka mafuta, chumvi, maji au majina yetu kama mbadala??.
Tumia jina la YESU, liamini jina la YESU WA NAZARETI epuka matapeli, na jina la YESU HALIUZWI, EPUKA MATAPELI!.
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Je Bwana YESU alikuwa amemfunga shetani wakati wa kuzaliwa kwake Kulingana na Mathayo 12:29?
Jibu: Turejee.
Mathayo 12:29 “Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, ASIPOMFUNGA KWANZA yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake”.
Jibu ni kwamba shetani hakuwa amefungwa wakati wa kuzaliwa Bwana YESU, na hata sasa shetani hajafungwa!, kwani Ingekuwa shetani amefungwa wakati wa kuzaliwa Bwana, basi Herode asingetafuta kumwua mtoto..
Mathayo 2:13 “Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize”.
Tukio hilo linaeleweka vizuri katika Ufunuo 12:1-6.
Vile vile Ibilisi asingesimama kumjaribu Bwana kule jangwani..
Mathayo 4:1 “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ILI AJARIBIWE NA IBILISI.
2 Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa.
3 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate”
Na ikiwa shetani amefungwa leo, maasi yasingeendelea kuwepo na maandiko yasingetuonya kuwa tusimpe nafasi..
Waefeso 4:28 “wala msimpe Ibilisi nafasi.
28 Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji”.
Maandiko yametabiri shetani kuja kufungwa katika ule utawala wa miaka elfu wa Bwana wetu YESU hapa duniani. Na utawala huo utaanza baada ya dhiki kuu kuisha, na hukumu ya Mungu kwa mataifa kupita (Ufunuo 16), hapo ndipo utawala wa miaka elfu moja utakapoanza na shetani (pamoja na majeshi yake) kufungwa kwa kipindi hiko.
Ufunuo 20:1 “Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake.
2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu;
3 akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache”.
Kwahiyo shetani kwasasa yupo na hakuwahi kufungwa wakati wowote huko nyuma, lakini atakuja kufungwa baada ya hukumu ya Mungu kwa mataifa inayotajwa katika Ufunuo 16.
Sasa swali kama ni hivyo je! Maandiko hayo katika Mathayo 12:29 yana maana gani?….
Turejee tena..
Mathayo 12:29 “Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, ASIPOMFUNGA KWANZA yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake”.
Haya ni maneno ambayo Bwana YESU aliyasema, akifundisha nguvu iliyo kuu/kubwa inapoingia mahali basi inateka au inafunga ile nguvu iliyo dhaifu.
Na ukisoma kuanzia juu kidogo utaona ni wakati ambapo Mafarisayo walimwona akitoa pepo kwa uweza wa Mungu, lakini wakasema yeye hatoi kwa uweza wa Mungu bali kwa uwezo wa Pepo mkuu aitwaye Beelzebuli, ambaye ni shetani mwenyewe.
Na Bwana akawahoji, akiwauliza yawezekanaje Shetani amtoe shetani mwenzake?..jambo ambalo haliwezekani!, vinginevyo ufalme wa giza hauwezi kusimama, lakini kama wakiona pepo katolewa maana yake katolewa kwa uweza wa Mungu, kwasababu kamwe shetani hawezi kumtoa shetani mwenzake.
Na ili kulifanya hilo lizidi kueleweka vizuri ndipo akatoa mfano mwingine kwamba… “Awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, ASIPOMFUNGA KWANZA yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake”
Ikifunua kuwa Bwana anapotoa pepo, kwanza anauteka ule ufalme wa giza (maana yake wote unakuwa chini ya amri yake) halafu ndipo anaamrisha pepo zitoke na kwenda atakako yeye soma Mathayo 8:28-32.
Sasa kitendo cha Bwana YESU kusimama na kuamrisha, maana yake mamlaka yake ni KUU inayoteka, na kufunga, na kuhamisha.. Na mamlaka hiyo hajabaki kwake tu pake yake, bali pia amewapa na wale wote wanaomwamini na kufanya mapenzi yake, kwamba kwa jina lake wanateka, na wanafunga na kuhamisha kila falme za giza.
2Wakorintho 10:4 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; NA TUKITEKA NYARA KILA FIKIRA IPATE KUMTII KRISTO;
6 tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”.
Kwahiyo mantiki ya Bwana YESU hapo ya KUFUNGA, haikuwa ya kumfunga shetani asiwepo duniani, bali katika kuzifunga kazi za ibilisi na majeshi yake zisisimame mbele yetu. (lakini shetani yupo, na ataendelea kuwepo na kuwasumbua wale wote wasiomwamini na kumfuata Bwana YESU), lakini walio na Bwana shetani hana nguvu juu yao.
Mathayo 18:18 “Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni”.
Je umeokoka??..Hizi ni siku za hatari na BWANA anarudi. Na shetani anajua wakati wake uliobaki ni mchache sana, hivyo anafanya kazi kwa kasi sana kusudi asiende kwenye lile ziwa la moto peke yake.
Ufunuo 12:12 “Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu”
Je bado wewe ni rafiki wa dunia?, bado ni mshabiki wa mipira, bado unacheza Kamari, bado unavaa kidunia na kuupenda ulimwengu?
1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.
16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.
17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je YUDA alikuwa ni shetani kulingana na Yohana 6:70?
NIFANYE NINI NIMSHINDE SHETANI?
Je! Yesu aliwezaje kuchukuliwa na shetani juu ya kinara cha hekalu kujaribiwa?
Nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.
Swali: Neno la Mungu linasema Katika Yohana 3:18 na 36 ..amwaminiye mwana anao uzima wa milele, asiyemwamini hana uzima? .. Je kuna haja ya kutafuta jambo lingine tena baada ya kumwamini Bwana YESU?.
Jibu: Yapo maandiko katika biblia yanayokamilishwa na maandiko mengine, yako maandiko ambayo hayahitaji kukamilishwa na mengine kwani yanakuwa yamejitosheleza lakini yapo ambayo yanaelezwa kwa ufupi hivyo ni lazima yakamilishwe na maandiko mengine…
kwamfano andiko hilo la Yohana 3:18 na 36 ni kweli maandiko yanatuonyesha kuwa “tukimwamini Bwana YESU hatutahukumiwa bali tutapata uzima wa milele”.
Yohana 3:18 “AMWAMINIYE YEYE HAHUKUMIWI; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu…..
36 Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia.
Lakini tukirejea Marko 16:16 tunaona kuna jambo lingine linaongezeka..
Marko 16:16 “Aaminiye na KUBATIZWA ATAOKOKA; asiyeamini, atahukumiwa”.
Hapa kinachoongezeka ni “UBATIZO” Kwamba mtu akiamini pasipo kubatizwa bado hataurithi uzima wa milele, (ikiwa amesikia habari za ubatizo na hajataka kubatizwa).
Na ubatizo unaozungumziwa hapo sio ule wa MAJI TU, bali hata ule wa ROHO MTAKATIFU soma Luka 3:16.
Ili tuzidi kuelewe vizuri lugha hii, hebu tafakari kauli hizi mbili… “Ukipanda maharage utavuna maharage”… na kauli ya pili “Ukipanda maharage na kuyamwagilia maji utavuna maharage”.. Je kwa ni kauli ipi ipo sahihi kuliko nyingine?.. Ni wazi kuwa kauli zote zipo sahihi, isipokuwa ya pili imefafanua vizuri.. na inayofaa Zaidi ni hiyo ya pili, kwasababu ndio imekamilisha kauli ya kwanza.
Vivyo hivyo Neno linasema katika Yohana 3:18 kuwa amwaminiye YESU hatahukumiwa, lakini Marko 16:16, inakamilisha vizuri Zaidi kwamba Amwaminiye YESU na kubatizwa hatahukumiwa..Kwahiyo ya pili ni ya nzito Zaidi kwasababu imeikamilisha ile ya kwanza.
Sasa kwanini Imani pekee yake haitoshi ni lazima kubatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu??
Jibu: Kwasababu hata Mashetani yanaamini lakini bado hayana wokovu..
Yakobo 2:19 “Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda VEMA MASHETANI NAO WAAMINI NA KUTETEMEKA.
20 Lakini wataka kujua, wewe mwanadamu usiye kitu, kwamba imani pasipo matendo haizai”
Kwa hitimisho ni kwamba “IMANI YA KUMWAMINI BWANA YEESU ni LAZIMA IENDE NA MATENDO”.. Na tendo la kwanza ni hatua ya ubatizo wa Maji na nyingine ni ya Roho Mtakatifu.
Mtu anapomwamini Bwana YESU na kubatizwa kwa maji na kwa Roho anakuwa amekamilika, na kukidhi vigezo vya kuuona ufalme wa Mungu, kwani maana pia ya kuzaliwa mara ya pili ni kuzaliwa kwa maji na kwa ROHO.
Yohana 3:4 “Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?
5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, MTU ASIPOZALIWA KWA MAJI NA KWA ROHO, HAWEZI KUUINGIA UFALME WA MUNGU.
6 KILICHOZALIWA KWA MWILI NI MWILI; NA KILICHOZALIWA KWA ROHO NI ROHO.
7 Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?
TUMEPEWA, SI KUMWAMINI TU KRISTO, ILA NA KUTESWA KWA AJILI YAKE;
Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, alimaanisha hakuwa na wengine?
Danieli 2:2
[2]Ndipo mfalme akatoa amri kuwaita waganga, na wachawi, na wasihiri, na Wakaldayo, wapate kumweleza mfalme ndoto zake. Basi wakaingia, wakasimama mbele ya mfalme.
Wasihiri ni kundi la wachawi, lililojikita kwenye mazingaumbwe. Linatumia uchawi kubadili vitu kwa hila, mbele ya macho ya watu kuwafanya waone kama ni muujiza umetendeka, na wakati mwingine kutumia njia hiyo kuleta madhara kwa watu.
kwamfano wale yane na yambre kipindi cha Musa walikuwa ni wasihiri, walijaribu kubadili fimbo kuwa nyoka, na kuleta vyura.(Kutoka 8:7)
Mfano mwingine ni yule Simoni mchawi, tunayemsoma katika;
Matendo 8:9-11
[9]Na mtu mmoja, jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa.
[10]Wote wakamsikiliza tangu mdogo hata mkubwa, wakisema, Mtu huyu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu.
[11]Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake.
Tofauti na waganga ambao, wenyewe wanajifanya kama matabibu, na wachawi na wale wakaldayo ambao ni wanajibu(wasoma nyota)…hawa wasihiri kazi yao hasaa ni ile ya kiini macho.
Lakini Mungu anathibitisha kwamba makundi yote haya, hakuna hata moja lenye uwezo wa kufikia hekima ya Mungu ipitayo vyote Hayana nguvu ya kupambanua mambo. au kufanya miujiza. Hakuna mganga wala wachawi, mwenye uwezo wa kufanya muujiza.
Sasa utauliza ni nini kile wanachokifanya kama sio miujiza?
Awezaye kutenda miujiza ni Mungu tu. wasihiri na waganga wanafanya kazi ya kulaghai fikra za watu kwa elimu ambayo ni ya siri (ya mashetani), ndio maana wanaofanya hizo kazi huenda kujifunza kufanya hivyo, namna ya kuchezea fikra za watu, na si kingine.
Sasa wewe kwasababu hujaijua hiyo elimu unaweza ukasema umeona muujuza kumbe ni uongo tu..wamekudanganya.
ni sawa na leo unapoona mtu akiwasiliana na mtu mwingine akiwa mbali na kuiona sura yake kwenye kioo, kama huijui elimu ya darasani, utasema ni muujiza lakini kumbe ni maarifa tu ya kibinadamu.
vivyo hivyo na hawa wachawi na wasihiri, hawana jipya kusema wanafanya muujiza fulani, ni elimu zao tu za kipepo
Hawawezi kuumba chochote. wale vyura waliofanya kutokea kipindi cha Farao, hawakuumba vyura wao wapya kimiujiza..Vinginevyo mpaka leo shetani angekuwa na uwezo wa kuumba na angeumba vyura wake wengi tu na viumbe vyake vimwabudu. Alichokifanya pale ni kuchukua vyura walioumbwa na Mungu, na kuwapumbaza watu macho, waone ni mawe yamegeuzwa vyura kumbe hakuna kitu. Ndio maana ujinga wao ulikuwa wazi baadaye…walipodhani kila eneo ni kiini macho, walipojaribu kwa chawa wakashindwa, kibao kikawageukia, wakakiri ni Mungu tu awezaye.
Kwahiyo wewe uliye na Yesu, shetani anakuona kama mungu duniani, mwenye nguvu nyingi sana, hekima mamlaka zaidi ya yeye. Wewe unaweza kutenda muujiza kabisa kwa jina la Yesu. yeye hawezi
mwamini Yesu mtegemee yeye tu, kwanini kutafuta msaada kwa vitu dhaifu, ukamtia Mungu wivu?. Kwenda kwa waganga ni kupungukiwa akili, ni kujitenga na fadhili zako, mwenyewe, ni kumdharau muumba wa mbingu na nchi, Yehova, atupaye vyote.
Okoka sasa, mpokee Yesu, upate uzima wa milele. Wachawi waliokutana na Yesu walisalimu amri na kuchoma mikoba yao. sasa wewe unaenda kufanya nini huko?
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Falaki ni elimu gani? (Isaya 47:13).
JIHADHARI NA ROHO YA YEZEBELI.
Rudi Nyumbani
Zipo kanuni za ki-Mungu tunaweza kuzifuata na zikaleta matokeo kabisa halisi, lakini zisiwe na manufaa kwetu katika suala la wokovu. Sasa kabla ya kuangalia ni kwa namna gani?
chukulia mfano wa kawaida.
Mwanamke yeyote anaweza kubeba ujauzito katika mazingira mbalimbali, kwamfano anaweza akatwezwa nguvu (akabakwa), na akapata ujauzito, lakini pia anaweza kwenda kujiuza kama kahaba na bado akapata ujauzito, vilevile anaweza akasubiri aolewe kwanza katika ndoa halali ndipo apokee ujauzito na likafanikiwa vilevile tu, kuleta kiumbe duniani, kama angefanya hayo kabla ya ndoa, au atokapo nje ya ndoa yake.
Sasa unaweza jiuliza, katika njia zote hizo ambazo angepata ujauzito ni ipi iliyo halali inayokubalika mbele za Mungu na wanadamu. Bila shaka ni hiyo njia ya mwisho ambayo ni ya kuolewa kwanza, ndipo apokee ujauzito kutoka kwa mume wake mmoja wa halali. Na ndio mtoto huyo hujulikana kama halali sio haramu.
Lakini cha ajabu ni kuwa ijapokuwa njia halali ipo lakini feki pia huleta matokeo yaleyale mfano wa halali. Kwasababu gani? Kwasababu kanuni ya kupata mtoto, si kanuni ya uhalali. Hivyo ni vitu viwili tofauti,
Hata Ibrahimu, alikuwa na watoto wengi, alitangulia Ishmaeli, kisha baadaye wakazaliwa na watoto wengine sita kwa suria mwingine, mbali na Isaka. Wote walikuwa wanadamu, viumbe wa Mungu, wenye akili na nguvu na baraka, wasio na hatia. Lakini lilipokuja suala la urithi, ndipo kubaguliwa kulipokuja, Watoto wote wa masuria walifukuzwa wakapewa zawadi tu bali Isaka alipewa vyote.
Mwanzo 25:5-6
[5]Ibrahimu akampa Isaka yote aliyokuwa nayo.
[6]Lakini wana wa masuria aliokuwa nao Ibrahimu, Ibrahimu akawapa zawadi, naye akawaondoa katika mahali alipokaa Isaka mwanawe, wakati wa uhai wake, waende pande za mashariki, mpaka nchi ya Kedemu.
Zipo kanuni nyingi sana za kiroho ambazo mtu yeyote, hata ambaye hajamwamini Yesu anaweza zitumia na zikatoa matokeo yaleyale sawa tu na mtu ambaye ameokoka.
Kwamfano, kufanya miujuza na ishara kwa jina la Yesu. Watu hawajui kuwa jambo hili huhitaji imani tu, katika jina lake. Hivyo wale wafikiao kiwango hicho haijalishi ni mwizi, ni mpagani, anaweza pokea muujiza na akafanya pia muujiza sawa tu na yule aliyeokoka.
Kwasababu gani? kwasababu amefanikiwa kufuata kanuni ambayo ni Imani.
Akijua lile neno linalosema ‘yote yawezekana kwake yeye aaminiye’’ (Marko 9:23). Ndio maana walikuwepo watu wengi wasiokuwa wayahudi kipindi kile cha Yesu walipokea miujiza mikubwa, zaidi ya wayahudi kwasababu tu ya ukubwa wa imani zao. Na sio haki zao.
Vivyo hivyo hata katika kuomba. Mtu yeyote aombaye hupokea. Ni kanuni ya asili ya rohoni, haijalishi ni nani.
Mathayo 7:8
[8]kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.
Watu hawajui hata kufanikiwa kwa shetani hutegemea maombi, na yeye pia huenda mbele za Mungu kuomba na hupewa..hajiamulii tu mambo yake ovyo ovyo bila idhini ya Mungu, kwasababu hii dunia si yake… utauliza kwa namna gani, ? unamkumbuka shetani kipindi cha Ayubu, yeye naye alikwenda kujihudhurisha mbele za Mungu, ndipo akaleta uharibifu. Akapeka haja zake akasikiwa, dua zake na magoti yake.
Ayubu 1:6
[6]Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za BWANA, Shetani naye akaenda kati yao.
Watu wengi wanapoona wanamwomba Mungu wanajibiwa wanadhani, ndio wamekubaliwa na Mungu. Kumbe unaweza kuomba kama mwana-haramu usiyekuwa na urithi wa uzima wa milele, bali haki ya kupokea tu unachokiomba.
Unaweza ukafanya miujiza kama mwana-haramu. Lakini usiende mbinguni.
Mathayo 7:22-23
[22]Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
[23]Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.
Unaweza ukamwamini Yesu, na kumuhofu, lakini ukaamini kama mashetani.
Yakobo 2:19
[19]Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka.
unaweza ukawavuta watu kwa Kristo na wakaokoka, lakini ukawa mtu wa kukataliwa kama tu Paulo alivyosema katika;
1 Wakorintho 9:27
[27]bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.
Kanuni Mungu anayoitazama kwetu ni Wokovu uliokamilishwa kwa matendo yake.
Angalia mwishoni pale kwenye Mathayo 7:23 Bwana Yesu alichokisema;
“ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”
Umeona je unaishi maisha gani?. hicho ndio kipimo cha ki-Mungu,
Alisema pia.
Yakobo 2:24
[24]Mwaona kwamba mwanadamu huhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo yake; si kwa imani peke yake.
Hakikisha maisha yako yanaendana na ukiri wako, wa imani yako, usiishi tu kama mtu ambaye hajaamini ukijitumainisha, kuona maombi yako yanajibiwa, karama yako inafanya kazi, imani yako inatenda kazi..hizo ni kanuni za kupokea lakini sio kanuni za uhalali wa kuurithi uzima wa milele. Ishi kama mtu ampendezaye Bwana wake kimwenendo, ndipo hayo mengine yakifuata huna hasara.
Nyakati hizi za mwisho, adui anaweka uzito kwenye mioyo ya watu wasipende kutafuta maisha matakatifu, kinyume chake wabakie tu kwenye miujiza, uponyaji, utabiri…Siku ile hivyo vitu havitafuata na wewe ndugu, bali matendo yako.
Ufunuo wa Yohana 14:13
[13]Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.
Tuanze sasa kujipima mienendo yetu. Kisha tutumie nguvu nyingi hapo kujirekebisha, sawasawa na imani tuliyoipokea, ili tuwe wana halali waliozaliwa kweli ndani ya Kristo, watakaorithi uzima wa milele.
Wokovu wa kweli hufunuliwa kwa mwenendo mzuri. Tuitazame sana kanuni hii.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”.
Je unaelewa maana ya kukaa ndani ya YESU (kuwepo ndani ya YESU) ??kwasababu ipo tofauti ya Bwana YESU kukaa ndani yako, na wewe kukaa ndani yake.
Kukaa ndani si Kumpa YESU maisha yako!!!…Ni zaidi ya hapo!.
Je ulishawahi kusikia mtu akisema “fulani nimemtoa ndani yangu kabisa au moyoni”..??
Utakuwa unaelewa maana ya hiyo kauli kwamba huenda katendewa kitendo kibaya sana, au cha kuumiza au kudhalilisha…ikasababisha kumtoa huyo mru moyoni kabisa.
Vile vile kuna mtu utamsikia akisema “mtu fulani yupo sana moyoni mwangu”…
Maana yake mpaka kusema hivyo huenda huyo mtu kamfanyia jambo jema sana au la kugusa moyo wake, au la kumvutia, mpaka kufanya aingie moyoni mwake.
Na Bwana YESU ni hivyo hivyo, kuna watu wapo ndani yake (moyoni mwake)..na kuna watu hawapo kabisa moyoni mwake ijapokuwa wanaweza kukiri wanaye…
Kwanini?..
Jibu: Kwasababu hawajawahi kuugusa moyo wa Bwana hata kumfanya Bwana awaweke moyoni mwake..watu hawa kibiblia hawapo ndani ya YESU na Kristo ingawa wanaweza kukiri kwamba wanaye Kristo moyoni, na Bwana atawakana siku ile kwamba hawajui.
Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.
Yafuatayo ni mambo (Matendo) ambayo mtu anaweza kuyafanya yakaugusa moyo wa Bwana YESU , hata kumfanya mtu huyo awe ndani ya KRISTO (moyoni mwake).
Hili ni jambo la kwanza linalomzamisha mtu kwenye moyo wa KRISTO.
Yohana 6:56 “Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake.
57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi”.
Kamwe usiidharau meza ya Bwana, lakini pia hakikisha unashiriki kulingana na Neno lake..Kwa kufanya hivyo utauteka moyo wa Bwana kwa kiwango kikubwa sana.
2.UMOJA.
Hili ni jambo la pili linalouteka moyo wa Bwana sana na kumzamisha mtu ndani ya moyo wake.
Yohana 17:21 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.
23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Hivyo jenga sana desturi ya kutafuta Umoja wa Roho, usipende kukaa peke yako peke yako (huendi kanisani, hushirikiani na wengine..ni hatari kubwa sana).
3. MATOLEO.
Kumtolea Mungu kwa hiari pasipo kulazimishwa wala kushinikizwa, ni kitendo cha tatu kinachougusa sana Moyo wa Bwana (hauwezi kutoka moyoni mwake daima).
Mathayo 26:12 “Maana kwa kunimwagia mwili wangu marhamu hiyo, ametenda hivyo ili kuniweka tayari kwa maziko yangu.
13 Amin, nawaambieni, Kila patakapohubiriwa Injili hii katika ulimwengu wote, tendo hilo alilolitenda huyu litatajwa pia kwa kumbukumbu lake”.
Huyu mwanamke amekuwa ndani ya moyp wa Kristo kwa vizazi vyote, mpaka sasa tunavyozungumza.
Usikwepe matoleo (sadaka) shetani amevuruga sana eneo hili la matoleo kwasababu anajua endapo mtu akipata ufunuo mkamilifu basi ataingia ndani ya Kristo moja kwa moja.
Unyenyekevu ni wa kukiri makosa, na kurudi kitubu na kuyokurudia rudia machafu, ni tendo kubwa sana linamwingiza mtu ndani ya YESU.
Luka 23:40 “Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?
41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.
42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”
Na yapo mambo mengine mengi katika maandiko yanayomwingiza mtu na kumdumisha ndani ya KRISTO.
Zifuatazo ni faida za kuwa ndani ya KRISTO.
Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”
2.Tunakuwa viumbe vipya.
2 Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya”.
Hasara za kutokuwa ndani ya KRISTO ni kinyume cha faida hizo.
Bwana atusaidie tuingie na kudumu ndani yake.
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!
USIWE MKRISTO WA KUKAA TU GHALANI,
JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.
JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.
Yubile, wengine huiita yubilei, au yubilii.
Ni mwaka wa hamsini (50), katika kalenda ya miaka ya kiyahudi. Mungu aliwaagiza wana wa Israeli, wahesabu miaka saba, kisha waizidishe mara saba, 7×7=49.
Na ule unaofuata wa 50, uliitwa mwaka wa yubile.
Ni mwaka ambao Mungu aliwaagiza wapumzike kabisa, hawakuruhusiwa kupanda wala kuvuna. Kwa miaka miwili mfululizo(yaani mwaka wa 49 na ule wa 50), kwasababu ule wa 49 ni sabato ya kila mwaka wa 7, ndio maana miaka miwili inatokea hapo. Sasa swali la kujiuliza wangewezaje kuishi miaka yote miwili bila kufanya kazi? Jibu ni kwamba Mungu aliwabariki mara dufu katika mwaka wa 48, hivyo wakafanikiwa kukusanya vingi vya kuwatosha miaka yote hiyo miwili ijayo bila kazi.
Lakini pia ulikuwa ni mwaka wa kusamehe madeni sambamba na hilo ulikuwa mwaka pia wa kuwaachilia huru watumwa.
Walawi 25:8 Nawe utajihesabia Sabato saba za miaka, maana, miaka saba mara saba; zitakuwa ni siku za Sabato saba za miaka kwenu, maana miaka arobaini na kenda.
9 Ndipo utakapoipeleka pande zote hiyo baragumu yenye sauti kuu, siku ya kumi ya mwezi wa saba; katika siku hiyo ya upatanisho mtaipeleka baragumu katika nchi yenu yote.
10 Na mwaka wa hamsini mtautakasa, na kupiga mbiu ya kuachwa mahuru katika nchi yote kwa watu wote wanayokaa; itakuwa ni yubile kwenu, nanyi kila mtu atairudia milki yake mwenyewe, nanyi mtarejea kila mtu kwa jamaa yake.
11 Mwaka huo wa hamsini utakuwa ni yubile kwenu; msipande mbegu, wala msivune kitu hicho kimeacho chenyewe, wala msizitunde zabibu za mizabibu isiyopelewa.
12 Kwa kuwa ni yubile; utakuwa mwaka mtakatifu kwenu; mtakula maongeo yake yatokayo shambani. 13 Mwaka huo wa yubile mtairudia kila mtu milki yake.
14 Tena kama ukimwuzia jirani yako cho chote, au kununua cho chote mkononi mwa jirani yako, msidanganyane wenyewe kwa wenyewe;
15 kwa hesabu ya miaka iliyo baada ya yubile, ndivyo utakavyonunua kwa jirani yako, na kama hesabu ya miaka ya mavuno ndivyo atakavyokuuzia wewe
Yubile, ilifunua kazi ya msalaba baadaye. Kwani Bwana wetu Yesu ndiye aliyekuja kutimiza kazi hii rohoni.
Kwanza ndani yake tunapokea pumziko kamili la utumwa wa dhambi. Pili tunasamehewa deni zetu (dhambi zetu), Na Tatu tunafanywa huru, katika vifungo vya shetani. Yaani Magonjwa na mapepo.
Huo ndio mwaka wa Bwana uliokubaliwa, ndio Yubile yetu halisi.
lakini pia sisi kama waamini katika mwenendo wetu, tuna mambo ya kujifunza tuipatazampo Yubile?.
Kwanza ni umuhimu wa kupumzika, kuahirisha mambo yetu kupata muda na Mungu. Si tupate tu siku moja kwa wiki kuwa karibu na Mungu. Wakati mwingine Mungu anataka kipindi kirefu. Wewe kama mfanyakazi, au umejiajiri, jiwekee utaratibu baada ya kipindi fulani uwe na likizo ndefu ambayo unaitenga kwa Mungu wako,kuutafuta uso wake, ni muhimu sana.
pili tunajifunza kusamehe watu madeni yao. Si kila tunayemdai lazima atulipe, fikiria juu ya hilo. Yesu alisema achilieni nanyi mtaachiliwa. Hujui ni wapi na wewe sikumoja utakwama, na utatamani.uachiliwe.
na mwisho kuwapa uhuru watumwa wetu ikiwa wewe ni mwajiri, fikiria kuwa mfanyakazi wako anahitaji pumziko refua, mpatie, bila kumpunguzia mshahara wake. Bwana ataona umeitunza yubilee yake pia kimwili. Na sio kufanya kumbukizi ya ndoa, au kuzaliwa, hiyo sio yubilei.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!