Title shetani ni nani?

Shetani ni nani?

Shetani ni nani?…Tafsiri ya Jina shetani ni ‘mshitaki’ au ‘mchongezi’.  Kazi yake ni kuwashitaki watakatifu mbele za Mungu.

Jina lingine la shetani ni “LUSIFA” Maana yake ‘NYOTA YA ALFAJIRI’. (Isaya 14:12) Jina  hili Lusifa aliitwa kabla hajaasi, baada ya kuasi ndio akawa shetani.

Alikuwa ni Malaika wa Sifa (Kerubi) huko mbinguni, alikuwa ni Mzuri kwa mwonekano na mkamilifu katika njia zake zote, aliishi katika taratibu za Mungu, na katika njia za Mungu,  na hivyo akapata heshima kubwa mbinguni zaidi ya Malaika wengi (Ezekieli 28:14).. Alikuwa mkamilifu mpaka siku uovu ulipoonekana ndani yake (Ezekieli 28:15).

Kwasababu ya uzuri wake Moyo wake ukainuka, akataka kujiinua awe kama Mungu, aabudiwe kama Mungu na kwa ujuzi wake mwingi akawashawishi theluthi ya Malaika mbinguni (1/3) waambatane naye.

Vita, vikali vikatokea Mbinguni kati ya Malaika waliokataa kuungana na Lusifa na malaika waliokubali kuungana naye. Biblia haisema vita hivyo vilipiganwa kwa muda gani, lakini inasema mwisho wa siku lusifa pamoja na malaika wake walishindwa vita vile, na kutupwa chini duniani (Ufunuo 12:7).

Na vita hivyo bado havijaisha, vita vya kwanza vilipiganwa mbunguni, kati ya Malaika walio upande wa shetani na wale walio upande wa Mungu na Malaika waliokuwepo Upande wa Mungu wakavishinda, lakini vita vya pili na vya mwisho vinapiganwa hapa duniani na hata sasa bado vinaendelea..Na vitaisha mwisho wa dunia. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

1. Je! Ni nani aliyemdanganya shetani?

2. Huduma 10 za shetani sasahivi duniani ni zipi?

3. Mpango wa shetani kwa watoto katika siku hizi za mwisho.

4. Agenda kubwa ya shetani kwa kanisa hili la siku za mwisho

5. Mafundisho ya Mashetani ni yapi katika siku hizi za mwisho?

6. Kazi ya Malaika watakatifu sasa ni nini?

HOME

Print this post

Merikebu ya Iskanderia kwanini itajwe jina lake ‘Ndugu Pacha’?

SWALI: Je kulikuwa na umuhimu wowote wa ile merikebu ya Iskanderia  walioipanda Paulo na wafungwa wengine kutajwa jina lake ‘ndugu Pacha’,?

Matendo 28:11  Baada ya miezi mitatu tukasafiri katika merikebu ya Iskanderia iliyokuwa imekaa pale kisiwani wakati wa baridi; na alama yake ni Ndugu Pacha. 12  Tukafika Sirakusa, tukakaa siku tatu. 13  Kutoka huko tukazunguka tukafikia Regio; baada ya siku moja upepo wa kusi ukavuma, na siku ya pili tukawasili Puteoli. 14  Huko tukakuta ndugu, wakatusihi tukae nao siku saba; na hivi tukafika Rumi.


JIBU: Safari ya mtume Paulo kama mfungwa, kutoka Kaisaria kwenda Rumi kuhukumiwa, haikuwa rahisi, iligubikwa na misuko suko mikubwa ambayo ilihatarisha maisha yao ukisoma Matendo 27, utaona mtume Paulo alionywa na Roho Mtakatifu kuhusu hatari hiyo lakini alipomwambia akida na manahodha, walipuuzia agizo lake, kwasababu watu wale hawakuamini habari za “miungu kabisa”. Maandiko yanasema walipoona upepo wa kusi umevuma kidogo tu, unaoruhusu kusafiri, wakadhani itakuwa hivyo mbeleni.

Lakini tunaona walipofika katikati, ghafla ile bahari iliwachafukia sana, upepo wa nguvu ukavuma merikebu yao ikawa karibu na kuzama, baadaye ilivunjika kabisa, na wakaokoka kwa shida kwasababu Mungu alimuhakikishia Mtume Paulo kuwa hakuna hata mmoja wao atakayeangamia.

Walipookoka na kufika kisiwa kile kilichoitwa Melita, walikaa miezi mitatu pale, kuruhusu hali ya hewa kutulia, kabla ya kuondoka. Lakini tunaona walipotaka kuondoka, safari hii wale mabaharia pamoja na maakida, hawakuichukulia safari yao kirahisi rahisi, yaani hivi hivi tu bila uongozo wowote. Ndipo walipojifunza kuchagua merikebu yenye “ulinzi wa kiroho”. Wakaipata hiyo ya Iskanderia iliyokuwa na nembo ya “Ndugu Pacha” kwa mbele.

Ndugu Pacha ni miungu ya kipagani ya kiyunani, ukisoma tafsiri nyingine za biblia imewataja moja kwa moja miungu hiyo kama Castor na Pollux. Ni miungu ambayo waliamini inahusika na ulinzi wa  safari za majini. Hivyo kwa imani yao ya kipagani, wakachukua nembo yao kuonyesha tunaiabudu na kuiheshimu hii miungu, na kutaka iwaongoze  salama katika safari yao, hawategemei tena elimu zao na nadharia zao.

Sasa tukirudi kwenye swali, linalouliza, kulikuwa ni umuhimu gani, hiyo merikebu ya Iskanderia kutajwa hadi nembo yake ya ndugu Pacha. Sababu ndio hiyo, Sio kwamba biblia inatufundisha, na sisi tukaweke miungu ya kipagani, kwenye vyombo vyetu vya usafiri kutuhakikishia ulinzi, hapana!

Bali inatufundisha Safari ya maisha hapa duniani. Kila mwanadamu anasafiri, lakini Je! Katika safari yako ni kitu gani kinakuongoza na kukulinda ili kukufikia ng’ambo yako salama?

Hakuna mwanadamu ambaye anaweza kujiongoza mwenyewe. Na ndio maana utaona hawa kwasababu hawakumjua Mungu wa kweli iliwabidi wakatafuta vinyago visivyoweza kuwasaidia kitu viwaongoze, na kama sio mtume Paulo kuwepo ndani ya Merikebu ile, safari yao ndio ingekuwa mbaya mara mbili zaidi. Hawakujua tu waliongozwa na Kristo Yesu pasipo wao kujua kwa neema tu!. Kwasababu watumishi wa Mungu walikuwa ndani.

Na sisi, hapa tulipo, fahamu kuwa maisha yako, bila KRISTO ni mauti mbele. Shetani hakuwazii mema, wala akili zako mwenyewe hazikusaidii ndugu, hiyo elimu ni kazi bure, huo uzoefu na ujuzi ulionao ni bure rafiki. Unamuhitaji Kristo, yeye ndio awe nembo  ya maisha yako. Mwamini leo akupe msamaha wa dhambi, mwamini leo akuokoe, safari yako iwe salama hapa duniani. Ukifa leo katika hali hiyo, fahamu ni jehanamu moja kwa moja. Umesikia injili ikihubiriwa mara ngapi, kwamba Yesu ni mwokozi lakini unapuuzia? Walio kuzimu wanatamani hata dakika moja, watubu hawawezi kwasababu kule hakuna maisha ya kuishi. Lakini wewe unaishi.

Usikiapo maneno haya, ugeuze moyo wako, umruhusu Kristo leo akuokoe, ikiwa upo tayari kumgeukia Bwana Yesu , na unatamani upate mwongozo wa kimaombi kwa ajili ya wokovu wako. Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii, bure.

Bwana akubariki.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NA UPEPO WA KUSI ULIPOANZA KUVUMA KIDOGO,

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

Kalafati ni nini? (Ezekieli 27:9)

KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Roho ya Malipizi/ roho za malipizi ni nini?

Swali: roho za Malipizi ni nini na mtu anawezaje kuzifunga?


Jibu: roho ya Malipizi au roho za malipizi ni roho zinazojilipiza kisasi baada ya kushindwa vita.

Maandiko yanasema vita vyetu sisi si juu ya damu na nyama, bali juu ya falme na mamlaka za giza katika ulimwengu wa roho.

Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho”.

Sasa hizi roho za mapepo na za wakuu wa giza, zinaposhindwa vita dhidi ya mtu, au watu, au kanisa basi, huwa zina tabia ya kukimbilia kutafuta sehemu nyingine iliyo dhaifu ya huyo mtu, au watu au kanisa na kushambulia ili kumwumiza yule aliyekuwa anashindana nazo.

Tuchukue mfano, mtu mmoja aliyeokoka ameomba kwaajili ya familia yake (Labda kwajili ya Mke wake au Mume au watoto), na katika kuomba kwake, ameomba ulinzi, na neema ya kumjua Mungu, na Zaidi sana amezikemea roho zote zinazopambana na familia yake, (roho za kurudi nyuma, roho za magonjwa na matatizo mengine) na amezishinda kwa maombi na kuziadhibu sawasawa na 2Wakorintho 10:6.

Sasa roho hizo (za mapepo na wakuu wa giza) zinapoanguka na kushindwa namna hiyo, huwa zina tabia ya kulipiza kisasi…kwa wakati huo zinaondoka na kwenda kutafuta sehemu nyingine ya maisha ya huyo mtu zilizo dhaifu na kuzivamia au kufanya nazo vita kutokana na uchungu na hasira za kushindwa..

Ndio hapo zitaacha kushughulika na familia ya huyo mtu kwa muda, na kwenda kupiga marafiki wa karibu wa huyo mtu, au wazazi, au watu wengine wowote walio wa muhimu katika maisha ya huyo mtu, lengo ni ili kumwumiza huyo mtu au kumsumbua na zinaweza kwenda kupiga kwa magonjwa, hasara au hata mauti kabisa..

Hivyo ni muhimu sana kumalizia maombi kwa kuomba ulinzi kwa watu wote walio karibu nawe ili wazidhurike na ghadhabu za hizo roho.

Hiyo siku zote ndio tabia ya shetani na majeshi yake, “kujilipiza kisasi”

Sasa  pengine utauliza ni wapi katika biblia jambo kama hilo limetokea?..tusome maandiko yafuatayo..

Ufunuo 12:7 “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;

8  nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.

9  Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.

10  Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.

11  Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.

12  Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! KWA MAANA YULE IBILISI AMESHUKA KWENU MWENYE GHADHABU NYINGI, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu”.

Umeona hapo mstari wa 12, maandiko yanasema yule ibilisi aliposhindwa alitupwa chini mwenye ghadhabu nyingi, na anashuka kujilipiza kisasi kwa kufanya vita na hao wakaao juu ya nchi na bahari kutokana na kushindwa kwake vita mbinguni. Na hapa tumeshapata jibu kwanini shetani anafanya vita na sisi wanadamu?.. sababu si nyingine Zaidi ya kisasi alichonacho, lakini ashukuriwe Kristo YESU Bwana wetu yupo katika mkono wa kuume akituombea (Warumi 8:34) .

Lakini tukizidi kusoma maandiko hayo mpaka ule mstari wa 17  bado tunaendelea kuona kisasi cha shetani baada ya kushidwa tena vita dhidi ya yule ya yule mtoto (YESU KRISTO) na dhidi ya yule mwanamke (Israeli).

Ufunuo 12:13 “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

14  Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.

15  Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.

16  Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.

17  Joka akamkasirikia yule mwanamke, AKAENDA ZAKE AFANYE VITA JUU YA WAZAO WAKE WALIOSALIA, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari”.

Umeona tena hapo?.. baada ya Ibilisi kumshindwa “mtoto na yule mwanamke” anapanga tena malipizi juu ya uzao wake, hiyo yote ni kuonyesha roho mbaya ya kisasi aliyonayo adui.

Vivyo hivyo, mpaka leo hiyo roho anayo pamoja na mapepo yake, yakishindwa vita yanaenda kutafuta wengine kumalizia hasira zao, kwahiyo ni muhimu sana pia kuomba maombi ya kufunga na kuzuia hizo roho zisiende kuleta madhara sehemu nyingine ya maisha ya watu unaohusiana nao!.

Na huu ndio umuhimu wa kuwaombea wengine, na pia ndio umuhimu wa kuomba.. Usipokuwa mwombaji na kusubiri kuombewa tu mara kwa mara, upo katika hatari ya kuvamiwa na maroho ya malipizi kutoka katika kila kona (kutokana na maombi ya wengine) endapo hawatafunga hizo roho. Kwahiyo ni muhimu sana kuomba na kuwaombea wengine.

2Wakorintho 10:4 “(maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5  tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;

6  tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”

Bwana akubariki.

Maran atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.

USILIPIZE KISASI.

UFUNUO: Mlango wa 12

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?

Rudi nyumbani

Print this post

Roho ya kukata tamaa ni nini na inatendaje kazi?

Swali: Roho ya kukata tamaa ipoje na inatendaje kazi na inawezaje kumtoka mtu?


“Roho ya kukata tamaa” ni roho inayomwingia mtu na kumfanya asiweze kuendelea mbele Zaidi. Roho hii inapomwingia mtu inamfanya asiwe na nguvu ya kufanya au kutafuta jambo lolote lile lililo zuri. Ndio hapo utaona mtu anakata tamaa ya kuendelea kusubiri jambo Fulani au kuendelea kuomba au kuendelea kutafuta.

Roho hii inasababishwa na “shetani” kwasababu kamwe MUNGU hawezi kumkatisha mtu tamaa kwa jambo lolote jema mtu apangalo kulifanya au kulitafuta. Yeye (Mungu) anasema maneno yafuatayo..

Luka 18:1  “Akawaambia mfano, ya kwamba IMEWAPASA KUMWOMBA MUNGU SIKUZOTE, WALA WASIKATE TAMAA”.

Mathayo 7:7 “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;

8  kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa”

Lakini adui kazi yake ni kukatishata tamaa, aidha kwa njia ya mawazo, ndoto au maneno ya watu.

Zifuatazo ni njia za kushughulika na roho ya kukata tamaa.

   1. MPOKEE YESU

Kama bado hujaokoka, fahamu kuwa wewe ni windo tosha la adui, na moyo wako ni malango ya maskani za roho zote chafu zikiwemo za kukatisha tamaa, hivyo maisha yako yatatawaliwa na kuvunjika moyo na kutokusonga mbele.

     2. SOMA NENO.

Soma sana Neno la MUNGU (Biblia) kwasababu ndani yake limejaa maneno ya Faraja, ambayo yanaweza kukufaa na kukutia nguvu katika nyakati zote utakayopitia za kukatisha tamaa, Kama magonjwa ndiyo yaliyokukatisha tamaa ndani ya biblia ipo mistari mingi ya kutia moyo wa kuendelea mbele.

Kama ni Ndoa ndio iliyokukatisha tamaa, yapo maneno ya faraha na kutia nguvu yahusuyo ndoa ndani ya biblia, kama ni anguko Fulani limetokea na likakukatisha tamaa, ndani ya biblia ipo mistari ya kutia nguvu ya kukunyanyua tena katika hali unayopitia. N.k

    3. MAOMBI

Fanya maombi kila siku, hii utakusaidia kukuweka katika lile joto la kiroho, na hivyo kufunga milango yote ya roho za adui za vitisho na kukatisha tamaa. Ukiwa mwombaji utakuwa katika usalama wa Roho daima.

Kwa njia hizo tatu basi waweza kujifungua na kila kifungo cha kukata tamaa, au kukatishwa tamaa.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NI JAMBO GANI LINALOMTAMANISHA SANA BWANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?

KWANINI UKATE TAMAA?

Nini maana ya kupiga Kite! Katika biblia.

Maana yake nini, Mwe na hofu wala msitende dhambi? (Zaburi 4:4)

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

Rudi nyumbani

Print this post

NI LAZIMA NIWE MBWEHA WA KRISTO!

Kama mwamini hizi si nyakati za kuishi kilegevu, unapoona, watu wanakufa katika dhambi na kwenda jehanamu bila kumjua Kristo, unajisikiaje, unapoona kazi za shetani zinasitawi, na kuwaharibu watu unawezaje kutujulia moyoni mwako?

Ni Funzo gani unalipata nyuma ya hasira ya Samsoni? Alipoona mke wake ameuzwa kwa wageni na baba-mkwe wake, je alitulia, na  kusema basi tu hii sio bahati yangu? Kinyume chake Alinyanyuka kwa hasira akasema ninakwenda kulipiza kisasi, kwa hawa wafilisti.

Unajua alifanya nini?

Alikwenda kuwachukua mbweha mia tatu (300), Akawafunga wawili wawili mikia yao, kisha, akawafungia mienge ya moto, na kuwaachia waingie kwenye mashamba ya ngano ya wafilisti. Baada ya hapo ni jambo gani akawa analifanya? Ni kuwaangalia tu wale mbweha walivyokuwa wanayateketeza mashamba ya ngano hekari kwa mahekari. Jambo lililowafanya wafilisti waamke wote kwenye majumba yao wamtafute huyu Samsoni ni nani?

Waamuzi 15:3 “Samsoni akasema, Safari hii nitakuwa sina hatia katika habari za hawa Wafilisti, hapo nitakapowadhuru.  4 Samsoni akaenda akakamata mbweha mia tatu; kisha akatwaa vienge vya moto akawafunga mbweha mkia kwa mkia, akatia kienge kati ya kila mikia miwili.  5 Alipokwisha kuviwasha moto vile vienge, akawaachia mbweha kati ya ngano ya Wafilisti, akayateketeza matita, na ngano, hata na mashamba ya mizeituni”

Akimfunua nani?

Ni Yesu Kristo,

Bwana alipoona kazi za adui zinapaswa ziharibiwe pale Israeli. Alichofanya ni kuwachukua wanafunzi wake pia, akawatuma wawili-wawili akawaambia waende mahali alipotaka yeye kwenda, akawapa amri ya kutoa pepo, kupooza magonjwa na kuhubiri habari njema. Na unajua ni nini kilitokea baada ya pale, ndani ya kipindi kifupi, waliporudi?

Yesu alikuwa akiwaangalia “MBWEHA WAKE” katika roho wakiziharibu kazi za shetani, akasema, nalimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme.. Ha! ha! ha! ha! Mbweha wamfanya kazi.

Luka 10:17  “Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. 18  Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. 19  Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru”.

Na sisi (yaani mimi na wewe), tuliokoka, Ikiwa umeshajazwa “Roho Mtakatifu” wewe tayari ni mbweha, Sijui unasubiri nini kwenda kuziharibu kazi za shetani, kwa kumuhubiri Kristo, na wokovu wake? Unasubiri nini mpendwa?

Angalia Yesu alichokisema..

Luka 12:49  “Nimekuja kutupa moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi?

Moto umekwisha kuwekwa kwenye mkia wako, angalia usije ukazima kabla haujafanya kazi yake. Ndio huo moto wa Roho Mtakatifu unaochoma ndani yako, kukuagiza uhihubiri neema ya Kristo kwa ndugu zako na watu wengine ili waokoke.

Kwa pamoja tunaweza upindua ulimwengu. Tumuhubiri Kristo, hilo ndio agizo kuu kwa wanadamu wote. Kila mmoja wetu ni mbweha wa Kristo. Simama sasa, pokea ujasiri, kamuhubiri Kristo, watu waokoke.

Bwana akubariki

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?

KITENDAWILI CHA SAMSONI

HUDUMA YA MALAIKA WAWILI.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Sadaka ya Kaini ilikataliwa? (Mwanzo 4:5).

Swali: Kwanini sadaka ya Kaini ya Mazao ilikataliwa na ile ya Habili ya wanyama ilikubaliwa? Je ni kwamba “wanyama” ni bora kuliko “mazao” mbele za Mungu?


Jibu: Turejee,

Mwanzo 4:4 “Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake;

5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana”.

Sababu ya sadaka  ya Kaini kukataliwa si kwasababu Mungu anapendezwa sana na wanyama kuliko mazao.. LA! Zaidi sana Mazao yanaweza kuwa bora kuliko wanyama kwasababu hayahusishi umwagaji wa damu.

Lakini sababu kuu ya Sadaka ya Kaini kukataliwa ni hiyo tunayoisoma katika mstari wa  3 na wa 4..

“Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa Bwana. Habili naye akaleta WAZAO WA KWANZA wa wanyama wake na SEHEMU ZILIZONONA za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake;”

Habili alileta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona… Lakini Kaini hakupeleka sehemu za kwanza za mazao yake!..bali alipeleka sehemu dhaifu,  kama ni mahindi pengine alipeleka yale yaliyoharibika haribika, kama ni matikiti alipeleka yale yaliokaribia kuoza! N.k..na zile njema na nzuri aliona zinamfaa yeye na si Mungu anayempa pumzi, na uhai na maisha.

Hivyo alimfanya Mungu wapili katika mali zake, na Mungu naye akamfanya wa pili mbele ya ndugu yake Habili.

Lakini Mungu ni wa upendo, huwenda alifanya vile kwa kukosa maarifa.. hivyo alimwonya na kumfundisha njia iliyobora ya kutoa sadaka ili sadaka yake ikubaliwe kama ya nduguye, lakini kwa kiburi alishupaza shingo, na akaenda kumwua ndugu yake, ikawa dhambi kubwa sana kwake.

Mwanzo 4:3 “Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa Bwana.

4 Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake;

5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana.

6 Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?

7 Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.

8 Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani]Ikawa walipokuwapo uwandani,Kaini akamwinukia Habili nduguye,akamwua.

9 Bwana akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu? “

Ni jambo gani tunajifunza hapo?

Jambo kuu tunalojifunza ni kuwa Mungu anaziangalia sadaka zetu, na kupitia hizo anatuhukumu nazo!.. Maandiko yanasema “hazina ya mtu ilipo ndipo na moyo wake utakapokuwepo (Mathayo 6:21)”.. Kama hazina yako ya kwanza haipo kwa Mungu, na Moyo wako hauwezi kuwa kwa Mungu, na ndicho kilichokuwa kwa Kaini.. Hazina yake kamilifu haikuwa kwa Mungu ndio maana hata Moyo wake haukumwelekea Mungu baada ya pale.

Lakini kama sehemu ya kwanza ya Hazina yako (sadaka) ipo kwa Mungu hata moyo wako utakuwa kwa Mungu..

Na kama unataka kujipima kama moyo wako kweli upo kwa Mungu “jiangalie utoaji wako”..(Hicho ndio kipimo kirahisi sana cha kujitambua wewe ni mtu wa namna gani).. Kwasababu hiyo basi ni dhambi kubwa sana kukwepa matoleo, haihitaji elimu kubwa kufahamu hilo….mtolee Bwana Zaka, mtolee Bwana sehemu zilizonona wala usimwibie, na moyo wako utakuwa kwake na utabarikiwa pia.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

Biblia inaposema Kaini akatoka mbele za uso wa Bwana, Inamaana gani?

SISI NI WINDO BORA SANA, LA DHAMBI.

DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?

SADAKA INAHARIBU NGUVU ZA MADHABAHU ZA MASHETANI.

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI MUNGU HAJIBU MAOMBI?

Kawaida MUNGU huwa anajibu maombi, isipokuwa Majira yake mara nyingi ni tofauti na Majira yetu.. Sisi uwa tunapenda tujibiwe maombi muda ule ule tunapoomba!.. Hiyo inaweza kutokea ikiwa ombi uliloomba linastahili kujibiwa wakati huohuo..

Lakini ikiwa si mapenzi ya Mungu upate hiko ulichokiomba kwa wakati huo, basi itakupasa usubiri mpaka wakati wa Bwana, na hiyo haimaanishi kuwa Mungu hajakujibu!.. Ameshakujibu isipokuwa jibu lako hajaliweka leo, bali kaliweka kesho, au mwezi ujao au mwaka ujao, au miaka kadhaa ijayo..Kwasababu majibu mengine yanahitaji kwanza mtu aandaliwe ndipo apokee alichokiomba.

Haiwezekanani mtoto ambaye hajaanza hata shule amwombe baba yake amnunulie gari ili aendeshe kwasababu tu baba yake ana uwezo, halafu yule mzazi amjibu kwa kumnunulia hilo gari na kumpa aendeshe siku ile ile alipoomba..Ni kitu ambacho hakiwezekani! Kwa mzazi mwenye akili timamu.

Badala yake mzazi atalichukua lile ombi la mwanae na kuliweka akiba, mpaka atakapokuwa mtu mzima, amekomaa kiakili na kielimu ndipo ampe zawadi ile ya gari, ambayo aliomba miaka kadhaa nyuma…kwasababu wakati huo atakuwa anajua jinsi ya kuliendesha na amekomaa kiakili. Lakini mtoto huyo huyo akiomba peremende kutoka kwa baba yake ni rahisi kupewa wakati ule ule alioomba, kwasababu ombi lake ni dogo, na halihitaji maandalizi yoyote.

Vile vile na kwa upande wa Mungu wetu (ambaye tunamwita BABA)..yapo maombi ambayo anayajibu papo kwa hapo na mengine yatachukua muda, mpaka mtu ajibiwe…

Ndio maana baada ya kuomba ni vizuri kuruhusu mapenzi ya MUNGU yatimie kama Daudi alivyosema katika..

Zaburi 69:13 “Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana, Wakati ukupendezao; Ee Mungu, Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, Katika kweli ya wokovu wako.

14 Uniponye kwa kunitoa matopeni, Wala usiniache nikazama. Na niponywe nao wanaonichukia, Na katika vilindi vya maji”.

LAKINI PAMOJA NA HAYO YAPO MAOMBI AMBAYO MUNGU HAJIBU KABISA!!. NA MAOMBI HAYO NI KAMA YAFUATAYO.

   1. MAOMBI YA TAMAA.

Mfano wa maombi ya tamaa ni yale mtu anaomba kitu si kwasababu ana haja na hiko kitu, bali kwasababu anataka kukitumia kwa anasa, au kwa mashindano, au kwa maonesho.

Mfano mtu ataomba Mungu ampe pesa, si kwasababu anataka atokane na changamoto Fulani za msingi, bali lengo lake ni ili awe nazo ili awaoneshe watu, au ajivune mbele za watu, au azitumie kwa anasa.. Mtu huyu anaweza asiseme kwa kinywa lakini moyo wake ndivyo vitu unavyovitamani.. Sasa maombi ya mtu wa namna hiyo biblia imesema huwa hayajibiwi.

Yakobo 4:3 “Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.

Kwahiyo ni muhimu sana, kuzichunguza NIA zetu, (kwamba kwanini tunaomba)..tuhakikishe nia zetu ni safi, na kweli tuna haja na hiko kitu tukiombacho kwa NIA njema.

    2. MAOMBI YA MTU MWOVU.

Mtu ambaye hamtaki Mungu moyoni mwake, lakini anataka vya Mungu (anataka kupokea kutoka kwa Mungu), maombi yake mtu huyo hayajibiwi!.

Ni muuaji na hataki wala hana mpango wa kuacha uuaji wake, ni mwizi wala hana mpango wa kuacha wizi wake, ni mzinzi na mwasherati wala hana mpango wa kuacha uasherati wake ijapokuwa anasikia mahubiri yahusuyo hayo kila siku, maombi yake mtu huyu hayajibiwi kulingana na biblia.

Isaya 1:15 “Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.

16 Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu; acheni kutenda mabaya;

17 jifunzeni kutenda mema; takeni hukumu na haki; wasaidieni walioonewa; mpatieni yatima haki yake; mteteeni mjane”.

    3. MAOMBI YA MANUNG’UNIKO NA MALALAMIKO.

Maombi ya Manung’uniko na malalamiko ni yale mtu anaomba kwa kulaumu, na kunung’unika kana kwamba kaonewa au kadhulumiwa, maombi kama haya majibu yake mara nyingi ni kinyume.. badala ya mtu kupokea anachokinung’unikia kinyume chake anaweza kupoteza hata kile kidogo alicho nacho.

1Wakorintho 10:10 “Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu.

11  Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani”.

Epuka manung’uniko wakati wa maombi.. badala yake kuwa mtu wa shukrani, na mtu wa kumsihi Mungu kwa unyenyekevu na heshima.

    4. MAOMBI YA KUMJARIBU MUNGU.

Mfano wa maombi haya ni yale, shetani aliyompelekea Bwana YESU kule jangwani.

Luka 4:9  “Akamwongoza mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini;

10  kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake wakulinde;

11  na ya kwamba,mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

12  Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako”.

Usiombe maombi ya kumwangalia BWANA atafanya nini… maombi ya nama hiyo hayana majibu, na zaidi wakati mwingine yanaishi kupokea adhabu badala ya Baraka.

1Wakorintho 10:9 “Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka”

Jihadhari na aina hizo nne (4) za Maombi ili upokee majibu ya Maombi yako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

FAIDA ZA MAOMBI.

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?

NDUGU,TUOMBEENI.

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Rudi nyumbani

Print this post

Ni mtu yupi aliyeishi miaka mingi kwenye biblia?

Swali: Je mtu aliyeishi miaka mingi kwenye biblia alikuwa nani?..na Mtu aliyeishi miaka mingi duniani ni nani?.


Jibu: Katika biblia mtu aliyeishi miaka mingi kuliko wote, ni METHUSELA, mwana wa Henoko aliyetwaliwa na Mungu..Biblia inasema huyu Methusela aliishi miaka 969, na hakuna mwingine aliyerekodiwa kuishi miaka mingi kuliko yeye.

Mwanzo 5:25 “Methusela akaishi miaka mia na themanini na saba, akamzaa Lameki.

26 Methusela akaishi baada ya kumzaa Lameki miaka mia saba na themanini na miwili, akazaa wana, waume na wake.

27 Siku zote za Methusela ni miaka MIA KENDA NA SITINI NA KENDA, AKAFA”.

Wengine walioishi miaka mingi katika biblia ni pamoja na;

  1. Yaredi, aliishi miaka 962, (Soma Mwanzo 5:20).
  2. Nuhu, Miaka 950 (Soma Mwanzo 9:29)
  3. Adamu, Miaka 930 (Soma Mwanzo 5:5)
  4. Sethi, Miaka 912 (Soma Mwanzo 5:8)
  5. Kenani, Miaka 910 (Soma Mwanzo 5:14)
  6. Enoshi, Miaka 905 (Soma Mwanzo 5:11)
  7. Mahalaleli, Miaka 895 (Soma Mwanzo 5:17)
  8. Lameki, Miaka 777 (Soma Mwanzo 5:31)
  9. Henoko, Miaka 365 (Soma Mwanzo 5:18-24)

Baada ya “Gharika ya Nuhu” miaka ya wanadamu ilishushwa mpaka kufikia miaka 120.. Ambapo ni wachache sana walivuka miaka hiyo, wengi waliishi chini ya hiyo..

Mwanzo 6:3 “Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini”.

Lakini kwajinsi siku zinavyozidi kwenda Miaka ya mwanadamu kuishi duniani ilizidi kushuka.. kutoka 120 mpaka 80

Zaburi 90:9 “Maana siku zetu zote zimepita katika hasira yako, Tumetowesha miaka yetu kama kite.

10 Siku za miaka yetu ni MIAKA SABINI, NA IKIWA TUNA NGUVU MIAKA THEMANINI; Na kiburi chake ni taabu na ubatili, Maana chapita upesi tukatokomea mara”.

Lakini swali kuu ni hili; kwanini miaka ya wanadamu inazidi kupungua siku baada ya siku? Je ni kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa au mabadiliko ya vyakula?

Jibu rahisi ni kwasababu ya “kuongezeka kwa Maasi”. Wala si mabadiliko ya hali ya hewa! Bali ni DHAMBI!.. Kitu cha kwanza kilichopunguza miaka ya Adamu na Hawa kutoka kuishi MILELE mpaka kufikia kuishi miaka 930 si kingine Zaidi ya DHAMBI!.. wala si kwasababu walikuwa hawazingatii mazoezi au milo kamili!..La!! bali ni dhambi!..

Na kanuni hiyo hiyo ndiyo inayopunguza maisha ya mwanadamu inaendelea mpaka sasa… Na wakati huo huo upande wa pili shetani anajaribu kuwaaminisha watu kuwa ni “Milo wanayokula ndiyo inayopunguza miaka” kwamba wapunguze ulaji wa nyama, na mafuta, na wazingatie mazoezi wataishi miaka mingi.

Mambo hayo ni mazuri, na yanafaa..lakini hayafai katika kuongeza UREFU WA MAISHA YA MTU, Kwani kuna wengi ambao wamezingatia hayo yote lakini wamewahi kuondoka duniani!.. na kuna ambao hawajazingatia hayo yote lakini wanayo miaka mingi duniani.

Kanuni ya kuishi miaka mingi na ya heri NI KUMCHA MUNGU NA KUEPUKANA NA UOVU, hiyo tu… Zishike Amri, fanya mapenzi ya Mungu, maisha yako yatakuwa marefu, hapa na katika ulimwengu ujao.

Kutoka 20: 12 “Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako”.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.

NIFANYE NINI ILI NISILALE NINAPOSOMA BIBLIA.

MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.

Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Mtande ni nini? Ni funzo gani lipo nyuma yake?

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi.

Waamuzi 16:13 Delila akamwambia Samsoni, Hata sasa umenidhihaki, umeniambia maneno ya uongo; niambie sasa, waweza kufungwa kwa kitu gani? Akamwambia, Ukivifuma hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo. 

14 Basi akazifunga kwa msumari, akamwambia Samsoni, Wafilisti wanakujia. Naye akaamka usingizini, akaung’oa ule msumari, na ule mtande. 

15 Mwanamke akamwambia, Wawezaje kusema, Nakupenda; na moyo wako haupo pamoja nami? Umenidhihaki mara hizi tatu, wala hukuniambia asili ya nguvu zako nyingi.

Mtande ni kifaa maalumu kinachotumika kufumia nyuzi za nguo, kwa kuzisokota pamoja ili kuunda nguo. Tazama mfano wa picha.

Hivyo nyuzi za nguo zilipitishwa katikati ya kamba hizo ngumu za mtande, kisha kuvutwa na kukazwa na mfumaji.

Katika habari hiyo tunaona Delila kazi yake huwenda ilikuwa ni ya ufumaji. Kwasababu ya uwepo wa kifaa hicho katika nyumba yake. Lakini katika harakati zake za kutaka kujua asili ya nguvu za Samsoni, biblia inatuambia, Samsoni alimdanganya kwa kumwambia ikiwa atavifuma vishungi vyake saba vya nywele katika mtande ule, basi, hatakuwa na nguvu za kujinasua, mahali pale.

Delila kusikia vile akaamini ni kweli, kwasababu kwa kawaida mtu ukishikwa tu nywele zako, si rahisi kuleta vurugu kwasababu utakuwa unajiumiza mwenyewe. Delila akizingatia kuwa alijua pia namna ya kufuma nyuzi vizuri. Hivyo alijihakikishia kuwa hilo linawezekana. Na cha kuongezea akapigilia na msumari kabisa, ili atakapojaribu kuzivuta nyewe zake, kutoka pale ashindwe. Kisha wafilisti waje kumchukua.

Lakini bado tunaona hilo halikuwezekana. Samsoni aling’oa misumari ile na kuuvunja mtande ule, Delila alipomwamsha.

Ni nini Tunajifunza katika habari hiyo kama waaminio?

KATIKA USINGIZI MUNGU ANAUMBA, NA SHETANI NAYE ANANASA.

Jiulize kwanini majaribio hayo yote Delila aliyafanya wakati ambao Samsoni amelala?. Alijua kabisa wakati akiwa macho Samsoni hawezi kukubali. Lakini pia swali lingine watu wanalojiuliza, iweje Samsoni, asisikie lolote wakati anatendewa vitendo vile. Kwamfano mpaka Delila anachukua nywele zake na kuziingiza kwenye mtande na kuzibana na kuzipigia misumari, asisikie chochote, ni usingizi wa namna gani?

Ndugu Mitego ya shetani, si rahisi kuigundua, kwasababu anaoutashi wa kuiweka kiasi cha kukufanya wewe usiwe mwepesi kuitambua, au kuisikia. Utashutukia tu umeshanaswa. Hivyo kama mwaminio ni kukimbia usingizi wowote wa kiroho kwa hali zote. Kwa kumtazama na kumfuata Yesu wakati wote. Unapomtazama Yesu, na kumtii kwa kuyakimbia machafu ya dunia. Hapo hujalala kiroho.

Lakini Pia katika usingizi Mungu pia hufanya jambo, na hilo si lingine zaidi ya kuumba. Utalithibitisha hilo kipindi kile alipomuumba Adamu, Mungu anasema.

Mwanzo 2:21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, 

22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. 

23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.

Umeona? Ukitulia kwa Bwana, akapumzika kwa Bwana, ukalala kwake. Jiandae kuumbiwa jambo lako bora kuliko yote katika maisha yako. Kama vile Mungu alivyomuumbia Adamu, msaidizi bora kuliko wote.

Kulala kwa Bwana ni kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yako, akupe ondoleo la dhambi. Kisha kuamua kuacha mambo yote ya kidunia na kumfuata yeye kwa uaminifu kwa kulitii Neno lake baada ya hapo. Na hapo ndipo unakuwa umelala kwake.

Hivyo chagua leo “Kuumbwa” badala ya “Kunaswa”. Mpokee Yesu sasa, ikiwa upo tayari kufanya hivyo. Basi fungua hapa kwa mwongozo huo wa sala ya Toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

KITENDAWILI CHA SAMSONI

JE! NYWELE ZAKO ZINAOTA AU ZIMESIMAMA?

Je Bwana Yesu alikuwa na nywele ndefu?

Rubani ni nani katika biblia? (Ezekieli 27:8)

Rudi nyumbani

Print this post

Machukizo ni nini?

Machukizo au Chukizo ni nini? kama tunavyosoma katika biblia?


Machukizo linatokana na neno “chukizo” na chukizo ni kitu kinachosababisha chuki/hasira. Kwa Mungu kitu chochote kinachoipandisha ghadhabu yake kinaitwa “chukizo”.

Na vitu vifuatavyo ndivyo vilivyokuwa machukizo kwa MUNGU.

   1. Ibada ya Sanamu.

Sanamu ya aina yoyote ile ilikuwa ni machukizo kwa Mungu na hicho ndicho kitu cha kwanza kilichokuwa kinaletea wivu kwa Mungu.

Kumbukumbu 27:15 “Na alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga, au ya kusubu, machukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi, akaisimamisha kwa siri. Na watu wote wajibu, waseme, Amina”.

Kumbukumbu 32:16 “Wakamtia wivu kwa miungu migeni, Wakamkasirisha kwa machukizo.

17 Walitoa sadaka kwa pepo, si Mungu, Kwa miungu wasiyoijua, Kwa miungu mipya iliyotokea siku zilizo karibu, Ambayo baba zenu hawakuiogopa”.

Soma pia Kumbukumbu 27:15, na 2Wafalme 23:24

   2. Uasherati na ulawiti.

Walawi 18: 22 “Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo”.

Soma tena Mambo ya Walawi 20:13

   3. Mavazi yasiyopasa.

Kumbukumbu 22:5 “Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanamume, wala mwanamume asivae mavazi ya mwanamke; kwa maana kila afanyaye mambo hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”

Mfano wa mavazi yasiyopasa, ni suruali kwa mwanamke, na nguo mfano wa magauni kwa wanaume.

   4. Sadaka yenye kasoro.

Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.

Kumbukumbu 17:1 “Usimchinjie Bwana, Mungu wako, ng’ombe wala kondoo aliye na kilema, wala neno ovu lo lote; kwa kuwa hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”.

Na yapo machukizo mengine mengi!.

Lakini pia lipo chukizo moja KUU na KUBWA ambalo litatokea kule YERUSALEMU, ambalo ni CHUKIZO LA UHARIBIFU, linalomhusu Mpinga-kristo.

Kwa upana juu ya CHUKIZO LA UHARIBIFU, basi fungua hapa >>CHUKIZO LA UHARIBIFU

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

VIPIMO MBALIMBALI VYA KIBIBLIA.

Kemoshi ni nani? (Yeremia 48:46)

Kwanini kuwe na kitabu Cha kumbukumbu la Torati na kwanini kiitwe vile?

Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post