Title shetani ni nani?

Shetani ni nani?

Shetani ni nani?…Tafsiri ya Jina shetani ni ‘mshitaki’ au ‘mchongezi’.  Kazi yake ni kuwashitaki watakatifu mbele za Mungu.

Jina lingine la shetani ni “LUSIFA” Maana yake ‘NYOTA YA ALFAJIRI’. (Isaya 14:12) Jina  hili Lusifa aliitwa kabla hajaasi, baada ya kuasi ndio akawa shetani.

Alikuwa ni Malaika wa Sifa (Kerubi) huko mbinguni, alikuwa ni Mzuri kwa mwonekano na mkamilifu katika njia zake zote, aliishi katika taratibu za Mungu, na katika njia za Mungu,  na hivyo akapata heshima kubwa mbinguni zaidi ya Malaika wengi (Ezekieli 28:14).. Alikuwa mkamilifu mpaka siku uovu ulipoonekana ndani yake (Ezekieli 28:15).

Kwasababu ya uzuri wake Moyo wake ukainuka, akataka kujiinua awe kama Mungu, aabudiwe kama Mungu na kwa ujuzi wake mwingi akawashawishi theluthi ya Malaika mbinguni (1/3) waambatane naye.

Vita, vikali vikatokea Mbinguni kati ya Malaika waliokataa kuungana na Lusifa na malaika waliokubali kuungana naye. Biblia haisema vita hivyo vilipiganwa kwa muda gani, lakini inasema mwisho wa siku lusifa pamoja na malaika wake walishindwa vita vile, na kutupwa chini duniani (Ufunuo 12:7).

Na vita hivyo bado havijaisha, vita vya kwanza vilipiganwa mbunguni, kati ya Malaika walio upande wa shetani na wale walio upande wa Mungu na Malaika waliokuwepo Upande wa Mungu wakavishinda, lakini vita vya pili na vya mwisho vinapiganwa hapa duniani na hata sasa bado vinaendelea..Na vitaisha mwisho wa dunia. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

1. Je! Ni nani aliyemdanganya shetani?

2. Huduma 10 za shetani sasahivi duniani ni zipi?

3. Mpango wa shetani kwa watoto katika siku hizi za mwisho.

4. Agenda kubwa ya shetani kwa kanisa hili la siku za mwisho

5. Mafundisho ya Mashetani ni yapi katika siku hizi za mwisho?

6. Kazi ya Malaika watakatifu sasa ni nini?

HOME

Print this post

Wasihiri ni akina nani?

Danieli 2:2
[2]Ndipo mfalme akatoa amri kuwaita waganga, na wachawi, na wasihiri, na Wakaldayo, wapate kumweleza mfalme ndoto zake. Basi wakaingia, wakasimama mbele ya mfalme.

Wasihiri ni kundi la wachawi, lililojikita kwenye mazingaumbwe. Linatumia uchawi kubadili vitu kwa hila, mbele ya macho ya watu kuwafanya waone kama ni muujiza umetendeka, na wakati mwingine kutumia njia hiyo kuleta madhara kwa watu.

kwamfano wale yane na yambre kipindi cha Musa walikuwa ni wasihiri, walijaribu kubadili fimbo kuwa nyoka, na kuleta vyura.(Kutoka 8:7)

Mfano mwingine ni yule Simoni mchawi, tunayemsoma katika;

Matendo 8:9-11

[9]Na mtu mmoja, jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa.

[10]Wote wakamsikiliza tangu mdogo hata mkubwa, wakisema, Mtu huyu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu.

[11]Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake.

Tofauti na waganga ambao, wenyewe wanajifanya kama matabibu, na wachawi na wale wakaldayo ambao ni wanajibu(wasoma nyota)…hawa wasihiri kazi yao hasaa ni ile ya kiini macho.

Lakini Mungu anathibitisha kwamba makundi yote haya, hakuna hata moja lenye uwezo wa kufikia hekima ya Mungu ipitayo vyote Hayana nguvu ya kupambanua mambo. au kufanya miujiza. Hakuna mganga wala wachawi, mwenye uwezo wa kufanya muujiza.

Sasa utauliza ni nini kile wanachokifanya kama sio miujiza?

Awezaye kutenda miujiza ni Mungu tu. wasihiri na waganga wanafanya kazi ya kulaghai fikra za watu kwa elimu ambayo ni ya siri (ya mashetani), ndio maana wanaofanya hizo kazi huenda kujifunza kufanya hivyo, namna ya kuchezea fikra za watu, na si kingine.

Sasa wewe kwasababu hujaijua hiyo elimu unaweza ukasema umeona muujuza kumbe ni uongo tu..wamekudanganya.

ni sawa na leo unapoona mtu akiwasiliana na mtu mwingine akiwa mbali na kuiona sura yake kwenye kioo, kama huijui elimu ya darasani, utasema ni muujiza lakini kumbe ni maarifa tu ya kibinadamu.

vivyo hivyo na hawa wachawi na wasihiri, hawana jipya kusema wanafanya muujiza fulani, ni elimu zao tu za kipepo

Hawawezi kuumba chochote. wale vyura waliofanya kutokea kipindi cha Farao, hawakuumba vyura wao wapya kimiujiza..Vinginevyo mpaka leo shetani angekuwa na uwezo wa kuumba na angeumba vyura wake wengi tu na viumbe vyake vimwabudu. Alichokifanya pale ni kuchukua vyura walioumbwa na Mungu, na kuwapumbaza watu macho, waone ni mawe yamegeuzwa vyura kumbe hakuna kitu. Ndio maana ujinga wao ulikuwa wazi baadaye…walipodhani kila eneo ni kiini macho, walipojaribu kwa chawa wakashindwa, kibao kikawageukia, wakakiri ni Mungu tu awezaye.

Kwahiyo wewe uliye na Yesu, shetani anakuona kama mungu duniani, mwenye nguvu nyingi sana, hekima mamlaka zaidi ya yeye. Wewe unaweza kutenda muujiza kabisa kwa jina la Yesu. yeye hawezi

mwamini Yesu mtegemee yeye tu, kwanini kutafuta msaada kwa vitu dhaifu, ukamtia Mungu wivu?. Kwenda kwa waganga ni kupungukiwa akili, ni kujitenga na fadhili zako, mwenyewe, ni kumdharau muumba wa mbingu na nchi, Yehova, atupaye vyote.

Okoka sasa, mpokee Yesu, upate uzima wa milele. Wachawi waliokutana na Yesu walisalimu amri na kuchoma mikoba yao. sasa wewe unaenda kufanya nini huko?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Falaki ni elimu gani? (Isaya 47:13).

 

JIHADHARI NA ROHO YA YEZEBELI.

Rudi Nyumbani

Print this post

IFUATE KANUNI SAHIHI YA MUNGU

Zipo kanuni za ki-Mungu tunaweza kuzifuata na zikaleta matokeo kabisa halisi, lakini zisiwe na manufaa kwetu katika suala la wokovu.  Sasa kabla ya kuangalia ni kwa namna gani? 

chukulia mfano wa kawaida.

Mwanamke yeyote anaweza kubeba ujauzito katika mazingira mbalimbali, kwamfano anaweza akatwezwa nguvu (akabakwa), na akapata ujauzito, lakini pia anaweza kwenda kujiuza kama kahaba na bado akapata ujauzito, vilevile anaweza akasubiri aolewe kwanza katika ndoa halali ndipo apokee ujauzito na likafanikiwa vilevile tu, kuleta kiumbe duniani, kama angefanya hayo kabla ya ndoa, au atokapo nje ya ndoa yake.

Sasa unaweza jiuliza, katika njia zote hizo ambazo angepata ujauzito ni ipi iliyo halali inayokubalika mbele za Mungu na wanadamu. Bila shaka ni hiyo njia ya mwisho ambayo ni ya kuolewa kwanza, ndipo apokee ujauzito kutoka kwa mume wake mmoja wa halali. Na ndio mtoto huyo hujulikana kama halali sio haramu.

Lakini cha ajabu ni kuwa ijapokuwa njia halali ipo lakini feki pia huleta matokeo yaleyale mfano wa halali. Kwasababu gani? Kwasababu kanuni ya kupata mtoto, si kanuni ya uhalali. Hivyo ni vitu viwili tofauti, 

Hata Ibrahimu, alikuwa na watoto wengi, alitangulia Ishmaeli, kisha baadaye wakazaliwa na watoto wengine sita kwa suria mwingine, mbali na Isaka. Wote walikuwa wanadamu, viumbe wa Mungu, wenye akili na nguvu na baraka, wasio na hatia. Lakini lilipokuja suala la urithi, ndipo kubaguliwa  kulipokuja, Watoto wote wa masuria walifukuzwa wakapewa zawadi tu bali Isaka alipewa vyote.

Mwanzo 25:5-6

[5]Ibrahimu akampa Isaka yote aliyokuwa nayo. 

[6]Lakini wana wa masuria aliokuwa nao Ibrahimu, Ibrahimu akawapa zawadi, naye akawaondoa katika mahali alipokaa Isaka mwanawe, wakati wa uhai wake, waende pande za mashariki, mpaka nchi ya Kedemu. 

Hii ni kutufundisha nini hasaa katika maisha yetu ya wokovu.

Zipo kanuni nyingi sana za kiroho ambazo mtu yeyote, hata ambaye  hajamwamini Yesu anaweza zitumia na zikatoa matokeo yaleyale sawa tu na mtu ambaye ameokoka.

Kwamfano, kufanya miujuza na ishara kwa jina la Yesu. Watu hawajui kuwa jambo hili huhitaji imani tu, katika jina lake. Hivyo wale wafikiao kiwango hicho haijalishi ni mwizi, ni mpagani, anaweza pokea muujiza na akafanya pia muujiza sawa tu na yule aliyeokoka.

Kwasababu gani? kwasababu amefanikiwa kufuata kanuni ambayo ni Imani.

Akijua lile neno linalosema  ‘yote yawezekana kwake yeye aaminiye’’ (Marko 9:23). Ndio maana walikuwepo watu wengi wasiokuwa wayahudi kipindi kile cha Yesu walipokea miujiza mikubwa, zaidi ya wayahudi kwasababu tu ya ukubwa wa imani zao. Na sio haki zao.

Vivyo hivyo hata katika kuomba. Mtu yeyote aombaye hupokea. Ni kanuni ya asili ya rohoni, haijalishi ni nani.

Mathayo 7:8

[8]kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. 

Watu hawajui hata kufanikiwa kwa shetani hutegemea maombi, na yeye pia huenda mbele za Mungu kuomba na hupewa..hajiamulii tu mambo yake ovyo ovyo bila idhini ya Mungu, kwasababu hii dunia si yake… utauliza kwa namna gani, ? unamkumbuka shetani kipindi cha Ayubu, yeye naye alikwenda kujihudhurisha mbele za Mungu, ndipo akaleta uharibifu. Akapeka haja zake akasikiwa, dua zake na magoti yake.

Ayubu 1:6

[6]Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za BWANA, Shetani naye akaenda kati yao. 

Watu wengi wanapoona wanamwomba Mungu wanajibiwa wanadhani, ndio wamekubaliwa na Mungu. Kumbe unaweza kuomba kama mwana-haramu usiyekuwa na urithi wa uzima wa milele, bali haki ya kupokea tu unachokiomba.

Unaweza ukafanya miujiza kama mwana-haramu. Lakini usiende mbinguni.

Mathayo 7:22-23

[22]Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? 

[23]Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu. 

 Unaweza ukamwamini Yesu, na kumuhofu,  lakini ukaamini kama mashetani.

Yakobo 2:19

[19]Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka. 

unaweza ukawavuta watu kwa Kristo na wakaokoka, lakini ukawa mtu wa kukataliwa kama tu Paulo alivyosema katika; 

1 Wakorintho 9:27

[27]bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa. 

Sasa kanuni sahihi ya Mungu ni ipi ili tuonekane kamili na halali?

Kanuni Mungu anayoitazama kwetu ni Wokovu uliokamilishwa kwa matendo yake.

Angalia mwishoni pale kwenye Mathayo 7:23 Bwana Yesu alichokisema;

“ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”

Umeona je unaishi maisha gani?. hicho ndio kipimo cha ki-Mungu, 

Alisema pia.

Yakobo 2:24

[24]Mwaona kwamba mwanadamu huhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo yake; si kwa imani peke yake. 

Hakikisha maisha yako yanaendana na ukiri wako, wa imani yako, usiishi tu kama mtu ambaye hajaamini ukijitumainisha, kuona maombi yako yanajibiwa, karama yako inafanya kazi, imani yako inatenda kazi..hizo ni kanuni za kupokea lakini sio kanuni za uhalali wa kuurithi uzima wa milele. Ishi kama mtu ampendezaye Bwana wake kimwenendo, ndipo hayo mengine yakifuata huna hasara.

Nyakati hizi za mwisho, adui anaweka uzito kwenye mioyo ya watu wasipende kutafuta maisha matakatifu, kinyume chake wabakie tu kwenye miujiza, uponyaji, utabiri…Siku ile hivyo vitu havitafuata na wewe ndugu, bali matendo yako.

Ufunuo wa Yohana 14:13

[13]Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao. 

Tuanze sasa kujipima mienendo yetu. Kisha tutumie nguvu nyingi hapo kujirekebisha, sawasawa na imani tuliyoipokea, ili tuwe wana halali waliozaliwa kweli ndani ya Kristo, watakaorithi uzima wa milele.

Wokovu wa kweli hufunuliwa kwa mwenendo mzuri. Tuitazame sana kanuni hii.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KANUNI JUU YA KANUNI.

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI AU KUTOA TALAKA?

Print this post

JE UPO NDANI YA YESU?

Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”.

Je unaelewa maana ya kukaa ndani ya YESU (kuwepo ndani ya YESU) ??kwasababu ipo tofauti ya Bwana YESU kukaa ndani yako, na wewe kukaa ndani yake.

Kukaa ndani si Kumpa YESU maisha yako!!!…Ni zaidi ya hapo!.

Je ulishawahi kusikia mtu akisema “fulani nimemtoa ndani yangu kabisa au moyoni”..??

Utakuwa unaelewa maana ya hiyo kauli kwamba huenda katendewa kitendo kibaya sana, au cha kuumiza au kudhalilisha…ikasababisha kumtoa huyo mru moyoni kabisa.

Vile vile kuna mtu utamsikia akisema “mtu fulani yupo sana moyoni mwangu”…

Maana yake mpaka kusema hivyo huenda huyo mtu kamfanyia jambo jema sana au la kugusa moyo wake, au la kumvutia, mpaka kufanya aingie moyoni mwake.

Na Bwana YESU ni hivyo hivyo, kuna watu wapo ndani yake (moyoni mwake)..na kuna watu hawapo kabisa moyoni mwake ijapokuwa wanaweza kukiri wanaye…

Kwanini?..

Jibu: Kwasababu hawajawahi kuugusa moyo wa Bwana hata kumfanya Bwana awaweke moyoni mwake..watu hawa kibiblia hawapo ndani ya YESU na Kristo ingawa wanaweza kukiri kwamba wanaye Kristo moyoni, na Bwana atawakana siku ile kwamba hawajui.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Yafuatayo ni mambo (Matendo) ambayo mtu anaweza  kuyafanya yakaugusa moyo wa Bwana YESU , hata kumfanya mtu huyo awe ndani ya KRISTO (moyoni mwake).

  1. KUSHIRIKI MEZA YA BWANA.

Hili ni jambo la kwanza linalomzamisha mtu kwenye moyo wa KRISTO.

Yohana 6:56 “Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake.

57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi”.

Kamwe usiidharau meza ya Bwana, lakini pia hakikisha unashiriki kulingana na Neno lake..Kwa kufanya hivyo utauteka moyo wa Bwana kwa kiwango kikubwa sana.

2.UMOJA.

Hili ni jambo la pili linalouteka moyo wa Bwana sana na kumzamisha mtu ndani ya moyo wake.

Yohana 17:21 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.

22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.

23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.

Hivyo jenga sana desturi ya kutafuta Umoja wa Roho, usipende kukaa peke yako peke yako (huendi kanisani, hushirikiani na wengine..ni hatari kubwa sana).

3. MATOLEO.

Kumtolea Mungu kwa hiari pasipo kulazimishwa wala kushinikizwa, ni kitendo cha tatu kinachougusa sana Moyo wa Bwana (hauwezi kutoka moyoni mwake daima).

Mathayo 26:12 “Maana kwa kunimwagia mwili wangu marhamu hiyo, ametenda hivyo ili kuniweka tayari kwa maziko yangu.

13 Amin, nawaambieni, Kila patakapohubiriwa Injili hii katika ulimwengu wote, tendo hilo alilolitenda huyu litatajwa pia kwa kumbukumbu lake”.

Huyu mwanamke amekuwa ndani ya moyp wa Kristo kwa vizazi vyote, mpaka sasa tunavyozungumza.

Usikwepe matoleo (sadaka) shetani amevuruga sana eneo hili la matoleo kwasababu anajua endapo mtu akipata ufunuo mkamilifu basi ataingia ndani ya Kristo moja kwa moja.

  1. UNYENYEKEVU.

Unyenyekevu ni wa kukiri makosa, na kurudi kitubu na kuyokurudia rudia machafu, ni tendo kubwa sana linamwingiza mtu ndani ya YESU.

Luka 23:40 “Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?

41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.

42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.

43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”

Na yapo mambo mengine mengi katika maandiko yanayomwingiza mtu na kumdumisha ndani ya KRISTO.

Zifuatazo ni faida za kuwa ndani ya KRISTO.

  1. Lolote tuombalo tunapata.

Yohana 15:7 “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa”

    2.Tunakuwa viumbe vipya.

2 Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya”.

Hasara za kutokuwa ndani ya KRISTO ni kinyume cha faida hizo.

Bwana atusaidie tuingie na kudumu ndani yake.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!

USIWE MKRISTO WA KUKAA TU GHALANI,

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

JINSI YA KUEPUKA KUUMIZWA MOYO KUSIKOKUWA NA SABABU.

Rudi Nyumbani

Print this post

yubile ni nini kwenye maandiko?

Yubile, wengine huiita yubilei, au yubilii.

Ni mwaka wa hamsini (50), katika kalenda ya miaka ya kiyahudi. Mungu aliwaagiza wana wa Israeli, wahesabu miaka saba, kisha waizidishe mara saba,  7×7=49.

Na ule  unaofuata wa 50, uliitwa mwaka wa yubile.

Ni mwaka ambao Mungu aliwaagiza wapumzike kabisa, hawakuruhusiwa kupanda wala kuvuna. Kwa miaka miwili mfululizo(yaani mwaka wa 49 na ule wa 50), kwasababu ule wa 49 ni sabato ya kila mwaka wa 7, ndio maana miaka miwili inatokea hapo. Sasa swali la kujiuliza wangewezaje kuishi miaka yote miwili bila kufanya kazi? Jibu ni kwamba Mungu aliwabariki mara dufu katika mwaka wa 48, hivyo wakafanikiwa kukusanya vingi vya kuwatosha miaka yote hiyo miwili ijayo bila kazi.

Lakini pia ulikuwa ni mwaka wa kusamehe madeni sambamba na hilo ulikuwa mwaka pia wa kuwaachilia huru watumwa.

Walawi 25:8 Nawe utajihesabia Sabato saba za miaka, maana, miaka saba mara saba; zitakuwa ni siku za Sabato saba za miaka kwenu, maana miaka arobaini na kenda.

9 Ndipo utakapoipeleka pande zote hiyo baragumu yenye sauti kuu, siku ya kumi ya mwezi wa saba; katika siku hiyo ya upatanisho mtaipeleka baragumu katika nchi yenu yote.

10 Na mwaka wa hamsini mtautakasa, na kupiga mbiu ya kuachwa mahuru katika nchi yote kwa watu wote wanayokaa; itakuwa ni yubile kwenu, nanyi kila mtu atairudia milki yake mwenyewe, nanyi mtarejea kila mtu kwa jamaa yake.

11 Mwaka huo wa hamsini utakuwa ni yubile kwenu; msipande mbegu, wala msivune kitu hicho kimeacho chenyewe, wala msizitunde zabibu za mizabibu isiyopelewa.

12 Kwa kuwa ni yubile; utakuwa mwaka mtakatifu kwenu; mtakula maongeo yake yatokayo shambani.  13 Mwaka huo wa yubile mtairudia kila mtu milki yake.

14 Tena kama ukimwuzia jirani yako cho chote, au kununua cho chote mkononi mwa jirani yako, msidanganyane wenyewe kwa wenyewe;

15 kwa hesabu ya miaka iliyo baada ya yubile, ndivyo utakavyonunua kwa jirani yako, na kama hesabu ya miaka ya mavuno ndivyo atakavyokuuzia wewe

Yubile, ilifunua  kazi ya msalaba baadaye. Kwani Bwana wetu Yesu ndiye aliyekuja kutimiza kazi  hii rohoni.

Kwanza ndani yake tunapokea pumziko kamili la utumwa wa dhambi. Pili tunasamehewa deni zetu (dhambi zetu), Na Tatu tunafanywa huru, katika vifungo vya shetani. Yaani Magonjwa na mapepo.

Huo ndio mwaka wa Bwana uliokubaliwa, ndio Yubile yetu halisi.

lakini pia sisi kama waamini katika mwenendo wetu, tuna mambo ya kujifunza tuipatazampo Yubile?.

Kwanza ni umuhimu wa kupumzika, kuahirisha mambo yetu kupata muda na Mungu. Si tupate tu siku moja kwa wiki kuwa karibu na Mungu. Wakati mwingine Mungu anataka kipindi kirefu. Wewe kama mfanyakazi, au umejiajiri, jiwekee utaratibu baada ya kipindi fulani uwe na likizo ndefu ambayo unaitenga kwa Mungu wako,kuutafuta uso wake, ni muhimu sana.

pili tunajifunza kusamehe watu madeni yao. Si kila tunayemdai lazima atulipe, fikiria juu ya hilo. Yesu alisema achilieni nanyi mtaachiliwa. Hujui ni wapi na wewe sikumoja utakwama, na utatamani.uachiliwe.

na mwisho kuwapa uhuru watumwa wetu ikiwa wewe ni mwajiri, fikiria kuwa mfanyakazi wako anahitaji pumziko refua, mpatie, bila kumpunguzia mshahara wake. Bwana ataona umeitunza yubilee yake pia kimwili. Na sio kufanya kumbukizi ya ndoa, au kuzaliwa, hiyo sio yubilei.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Sikukuu ya kutabaruku ni ipi?

SIKUKUU YA VIBANDA.

JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?.

Rudi Nyumbani

Print this post

Tafsiri ya Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.

Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.

13 Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.

14 Nami nitaonekana kwenu, asema Bwana, nami nitawarudisha watu wenu waliofungwa, nami nitawakusanya ninyi, nikiwatoa katika mataifa yote, na katika mahali pote, nilikowafukuza, asema Bwana; nami nitawaleta tena, hata mahali ambapo kutoka hapo naliwafanya mchukuliwe mateka

Huu ni utabiri ambao Mungu aliwaambia Israeli, pindi tu walipochukuliwa utumwani Babeli, akiwaahidia atawarudisha tena kwenye nchi yao baada ya miaka sabini. Na zaidi ya hayo akawapa pia na Neno la ahadi kwamba wakati huo wakimtafuta kwa mioyo yao yote, watamwona, watamwomba atawasikia, na wote watarejeshwa nyumbani ijapokuwa walichukuliwa mbali sana.

Na kweli utabiri huo ulikuja kutumia, kwani mwishoni mwa hiyo miaka sabini, mbiu ilipigwa waisraeli wote warudishwe kwao. Na aliwaonekania sana pindi waliporejea.

Ni neno la ahadi hata kwetu,

Kwamba tukimtafuta yeye kwa mioyo yetu yote, tutamwona. Kumbuka anasema “MIOYO YETU YOTE”. Kosa linatokea pale tunapompenda Mungu kwa sehemu, leo kwake kesho kwa shetani. Ndio Inayopelekea tusimwone Mungu katika ukamilifu wake wote. Mungu anahitaji vyako vyote vielekee kwake, ndipo tumwombe na kumwita ili atuitikie..

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine

Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,

Nini Maana ya Adamu?

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

Rudi Nyumbani

Print this post

NIFANYE NINI NIMSHINDE SHETANI?

1) WOKOVU: 

Hilo ndio jambo la kwanza. Kamwe huwezi kumshinda shetani ikiwa upo nje ya Kristo, Ndicho kilichowakuta wale wana wa Skewa, walipotaka kutoa pepo kwa jina la Yesu. Lakini Yule pepo akawaambia Yesu namjua, na Paulo namfahamu, lakini je ninyi ni akina nani?

Matendo 19:13  Baadhi ya Wayahudi wenye kutanga-tanga, nao ni wapunga pepo, wakajaribu kutaja jina la Bwana Yesu juu yao waliopagawa na pepo wachafu, wakisema, Nawaapisha kwa Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo.

14  Walikuwako wana saba wa mtu mmoja Skewa, Myahudi, kuhani mkuu, waliofanya hivyo.

15  Yule pepo mchafu akawajibu, akawaambia, Yesu namjua na Paulo namfahamu, lakini ninyi ni nani? 16  Na yule mtu aliyepagawa na pepo mchafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.

Wokovu, ni Kristo ndani yako, na kwa huo nguvu za adui zote huyeyuka mara moja. Mtu aliyempokea Yesu, shetani kamwe hamwezi, kwasababu anamwona Kristo ndani yake.

2) MAOMBI: huharibu mipango ya ibilisi.

Unaweza ukawa umeokoka, lakini shetani akapata nguvu za kukusumbua kwa majaribu, kwasababu unashindwa kutumiza baadhi ya wajibu wako kwa mwamini, Yesu alisema..

Mathayo 26:41  Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.

Yesu ijapokuwa alikuwa ni mkamilifu hana dhambi, alijaribiwa na adui, wewe ni nani usikutane na hayo? Usipokuwa mwombaji, uvivu ukakumeza, unaona shida kuomba kila siku, kuhudhuria mikesha ujue tayari upo majaribuni. Hata kama utajiona upo sawa, fahamu tu hapo ulipo kuna eneo Fulani adui anakusumbua, utakuja kugundua pindi utakapoanza kuwa mwombaji. Na ndio maana maisha ya wokovu hayatengwi na maombi. Shetani akimwangalia mwombaji anaona moto umemzunguka mkali, hawezi jiamulia tu kufanya analotaka kwake.

3) KUBALI KUWA MJINGA: Utamweka chini shetani.

Warumi 16:19  Maana utii wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya. 20  Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. [Amina.]

Hapo anasema tuwe wajinga katika mambo mabaya. Ni nafasi kubwa kwa Mungu kumweka shetani chini ya miguu yetu. Kwamfano, unapokuwa hujui kuhusu mitindo mipya ya kidunia, sio mfuatiliaji wa miziki ya kidunia, muvi mpya mpya zilizotoka duniani, yaani kwa ufupi unapitwa na mambo ya kidunia yasiyokuwa na maana kwako, kinyume chake, unakuwa na ujuzi na hekima katika mambo ya rohoni jua hapo umemshinda shetani kwa sehemu kubwa. Hana kitu kwako, kwasababu bidhaa zake, huna mpango nazo, hununui chochote kwake.  Kuipenda dunia ni kuwa adui wa Mungu, na rafiki wa shetani.

4) WEKA NENO LA MUNGU NDANI: Utamfukuza shetani.

Kuweka Neno sio, kukariri vifungu vingi vya biblia, hapana, bali ni kufahamu “ukweli” (ufunuo)  wa kila Neno unaloliweka moyoni mwako. Pale jangwani, Yesu alipokutana na shetani, alimjaribu kwa Neno hilo hilo,lakini Yesu akamwambia kweli yote ipoje.

Mathayo 4:6  akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 7  Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.

Ni muhimu ukalifahamu Neno la Mungu katika kweli yake, na hiyo huchangiwa na kufundishwa kwa ufasaha Neno la Mungu na waalimu, kwasababu Roho Mtakatifu atasema na wewe kupitia wao. Lakini pia kumpa Roho Mtakatifu nafasi ya moja kwa moja kukufundisha. Vinginevyo adui atakudanganya sana, hususani kupitia manabii wa uongo, kwasababu hulijui Neno vema.

 5) LITII NENO: Utaweza yastamili majaribu yake yote.

Kulifahamu Neno, na kuijua kweli, ni jambo muhimu lakini bado shetani anaweza pata mianya ya kukunasa endapo hutaweza kulitii Neno. Penda utakatifu, penda kutendea kazi kile unachofundishwa. Yesu alisema, wapo watu wasikiao tu, lakini wapo wasikiao na kuyatendea kazi. Wote hujaribiwa kwa pepo, mafuriko na mvua za shetani. Sasa Yule aliyejijenga  juu ya fundisho tu, na sio kutendea kazi fundisho, ndio huyo anayechukuliwa na mafuriko.

Mathayo 7:26  Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

27  mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.

Mateso mengine huwapata watu kwasababu ya dhambi. Kuishi maisha matakatifu, humnyima adui mlango wa kukushambulia kwa namna yoyote. Liishi Neno.

6) HUBIRI NENO: Utamwangusha adui kutoka juu.

Watu wengi hudharau ushuhudiaji. Tunapokuwa na moyo mmoja wa kuitenda kazi ya Mungu, adui hawezi kukaa juu ya anga hili, kutupinga. Tunalisoma wapi hilo? Utakumbuka wakati ule Bwana alipowatuma wanafunzi  wake wawili wawili kuhubiri, waliporudi kwa furaha, huku wakimwambia Bwana  hata mapepo yanawatii. Yesu akawaambia nalimwona shetani akianguka kutoka juu kama umeme. Kuonyesha kuwa kitendo cha wao kuhubiri adui alikuwa anaporomoka kwa kasi sana.

Mathayo 10:17  Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. 18  Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.

Hivyo ukizingatia mambo  hayo sita (6), Utakuwa sio tu umemdhibiti adui kila Nyanja, bali pia umemteka. Ni wajibu wako mimi na wewe kuboresha mahali ambapo hapako sawa, ili kwa pamoja tukaujenge ufalme wa Mungu na kuziangusha kazi za shetani.

Yakobo 4:7  Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ZIFAHAMU KAZI KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

USIWE ADUI WA BWANA

Rudi Nyumbani

Print this post

Nyota ya bahati yangu ni ipi?

Je ni kweli kuna watu wenye nyota ya bahati? Na je nitaipate nyota hiyo maishani mwangu?


JIBU: Nyota ya bahati inasadikika ni pale mtu anapobahatika kupata kitu kwa haraka au kwa wepesi, au bila matarajio yake,au nguvu zake nyingi katika kukipata tofauti na wengine. Kwamfano labda mtu ni mchimba madini, mara ghafla anatapa dhahabu nyingi tofauti na wachimbaji wengine. Au mwingine amehitimu chuo, mara anapata kazi nzuri, yenye cheo, zaidi hata ya wengine wengi waliomtangulia. Au ni mfanya-biashara mara anapata tenda kubwa ambayo inainua biashara yake kwa kasi zaidi ya wengine. N.k.

Sasa mtu kama huyu wengi husema ana nyota ya bahati. Lakini je ni kweli?

Ukweli ni kwamba twaweza kusema ana-bahati –tu, lakini hana nyota-ya-bahati. Kwavipi.

Kwasababu mafanikio hayo, yanaweza kuondoka tena kwake, na kama yakibaki, bado bahati hiyo hainunui tunu za rohoni. Mfano amani, upendo, utu wema,  imani, adili, unyenyekevu, na uzima baada ya kifo. N.k., Ni mafanikio ambayo hata mashetani huyatoa.

Lakini ni lazima ujue nyota halisi ya bahati ni ipi? Ambayo katika hiyo unaweza kupata vyote, Kisha uifuate.

Hiyo si nyingine zaidi ya YESU KRISTO. Vitabu vitakatifu vinasema hivyo, Vilevile Watu wote wanalijua hilo, ikiwemo wachawi wote, wanajimu wote, malaika wote, na mashetani yote.

Soma hapa;

Mathayo 2:1  Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, MAMAJUSI WA MASHARIKI walifika Yerusalemu, wakisema,

2  Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana TULIIONA NYOTA YAKE MASHARIKI, nasi tumekuja kumsujudia.

3  Basi mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, na Yerusalemu pia pamoja naye. 4  Akakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, akatafuta habari kwao, Kristo azaliwa wapi?

5  Nao wakamwambia, Katika Bethlehemu ya Uyahudi; kwa maana ndivyo ilivyoandikwa na nabii,

6  Nawe Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, Hu mdogo kamwe katika majumbe wa Yuda; Kwa kuwa kwako atatoka mtawala Atakayewachunga watu wangu Israeli.

7  Kisha Herode akawaita wale mamajusi faraghani, akapata kwao hakika ya muda tangu ilipoonekana ile nyota.

8  Akawapeleka Bethlehemu, akasema, Shikeni njia, mkaulize sana mambo ya mtoto; na mkiisha kumwona, nileteeni habari, ili mimi nami niende nimsujudie.

9  Nao waliposikia maneno ya mfalme, walishika njia; na tazama, ile nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, hata ikaenda ikasimama juu ya mahali alipokuwapo mtoto.

10  NAO WALIPOIONA ILE NYOTA, WALIFURAHI FURAHA KUBWA MNO.

11  Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane.

Ikiwa Yesu yupo moyoni mwako. Ikiwa umemwamini, kisha ukamfanya Bwana na kiongozi wa maisha yako. Jambo la kwanza analolifanya ndani yako ni kuondoa laana yote ya dhambi, ambayo humfanya mwanadamu aende kuzimu, ambayo kila mwanadamu anayo. Na wakati huo huo huyo mtu anaitwa mbarikiwa, anaitwa mtakatifu, makosa yake yote yanakuwa yamefutwa, hahesabiwi dhambi tena.

Na moja kwa moja anapewa, Roho Mtakatifu. Sasa Kazi ya huyu Roho Mtakatifu, ni kumtengeneza roho yake,kumsafisha kutoka katika ubaya kumweka katika wema, na kumfanya aweze kushinda dhambi na maovu yote.

Ndio hapo kama alikuwa mlevi, kiu hiyo inaondolewa, alikuwa mzinzi, hamu ya mambo hayo yanakufa ndani yake, alikuwa ana uchungu, furaha inaanza kujengeka, alikuwa ni mwenye hasira, upendo wa ki-Mungu unaumbika sana moyoni mwake, anaanza kupenda watu wote.

Na zaidi sana, anapokea uzima wa milele, hata akifa ghafla, haendi kuzimu, hapotei, bali anakuwa amelala tu, anasubiri siku ya ufufuo, aamshwe aende mbinguni.

Pamoja na hilo, hata yale mengine ambayo alikuwa anayatafuta au anayapata kwa shida, Yesu anampa mafanikio pia  kiwepesi kwasababu aliahidi hivyo. Zile bahati ambazo anatamani azipate, Yesu anamletea mara mia (100), katika maisha yake.

Mathayo 19:28  Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.

29  NA KILA MTU ALIYEACHA NYUMBA, AU NDUGU WA KIUME AU WA KIKE, AU BABA, AU MAMA, AU WATOTO, AU MASHAMBA, KWA AJILI YA JINA LANGU, ATAPOKEA MARA MIA, NA KUURITHI UZIMA WA MILELE.

Umeona, mwisho wa siku unakuwa umepata vyote, kwasababu kwa Yesu vipo vyote.

Huoni kuwa hiyo ni NYOTA nzuri sana ya bahati? Kwanini uende wa waganga wa kienyeji, kutafuta laana, huko? Kwasababu wale wanakurushia mapepo, ambayo mafanikio yao ni batili, ni kitanzi, mwisho wa siku ni kukuangamiza, sasa unakuwa umepata faida gani? Wakati mafanikio ya Yesu Kristo, hutajirisha wala hayana huzuni ndani yake, biblia inasema hivyo;

Mithali 10:22 Baraka ya Bwana hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo

Ungoja nini usimpokee Yesu leo? Ikiwa umedhamiria kwa dhati kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa namna ya kuokoka leo >>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Falaki ni elimu gani? (Isaya 47:13).

NYOTA YA ASUBUHI.(Opens in a new browser tab)

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

Rudi Nyumbani

Print this post

KILA SILAHA ITAKAYOFANYIKA JUU YAKO HAITAFANIKIWA.

Jina la BWANA wetu YESU KRISTO lihimidiwe daima.

Neno la Mungu linasema..

Isaya 54:17 “KILA SILAHA ITAKAYOFANYIKA JUU YAKO HAITAFANIKIWA Kila na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema Bwana”.

Hapo anasema “kila silaha itakayofanyika haitafanikiwa” na si “kila shambulizi halitafanikiwa”.. Maana yake katika tu mwanzo wa maandalizi ya silaha, huo ndio hautafanikiwa!..

Kivipi?

Silaha za zamani zilikuwa ni Mikuki, Panga na Mishale na nyinginezo baadhi ambazo zote zilikuwa zinatengenzwa kwa vyuma na Wahunzi..(Sasa kufahamu mengi kuhusu Wahunzi na jinsi wanavyofua vyuma basi fungua hapa >>> Mhunzi ni nani? (Isaya 54:16) ).

Hivyo Wahunzi walikuwa wanayeyusha chuma kisha wanakitengeneza kwa umbile la silaha waitakayo kama ni panga, au kisu au mkuki.. Sasa hapa biblia inasema silaha yoyote inayotaka kutengenezwa na hawa wahunzi, haitafanikiwa..

Maana yake wahunzi wakiwa katika zile hatua za kuyeyusha chuma, basi hawafanikiwa kufikia hitimisho la kuikamilisha  ile silaha, maana yake shughuli yao itaishia katikati na hakuna silaha yoyote itakayozaliwa. (aidha wakiwa katika utengenezaji wataungua moto, au watapungukiwa na malighafi, au watapata hitilafu nyingine yoyote ambayo itawafanya wasilamize ile kazi).

Watabaki na chuma kisicho na umbile lolote la kisu, au sime, au panga au mkuki..

Isaya 54:16-17 “Tazama, nimemwumba MHUNZI avukutaye moto wa makaa, akatoa silaha kwa kazi yake; nami nimemwumba mharibu ili aharibu…kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa”

Vile vile na agano Mungu analoingia na watumishi wake ni agano la namna hiyo hiyo, maana yake hawataona hata dalili ya silaha juu ya maisha yao kwani Bwana ataziharibu kabla hazijakamilika…

Kama ni uchawi ndio silaha ya adui, basi wakati tu unapikwa huko kwenye vibuyu na miti, na makaburini na habarini au katika madhabahu za baali basi utaungua moto kabla haujakamilika (wala hutajua kama kuna mashambulizi yalikuwa yameandaliwa dhidi yako, hutaona hata hiyo dalili..mambo yanaharibika kabla hayakamilika)… baadaye sana ndio utakuja kusikia ushuhuda kwamba kuna njama zilipangwa juu yako na zikashindikana (kama Bwana ataruhusu ujue).

Kama magonjwa ndio silaha ya adui anayoisuka juu yako, akiwa katika kiwanda chake cha kukutengenezea hayo, Bwana atasimama kinyume chake na kuziharibu hizo hila, na hutaona chochote na wala kujua chochote kwani hata dalili haitaonekana.

Kama ni kuondolewa kazi ndio silaha ya adui, basi kabla hata hiyo mipango kukamilika, itafutwa na Bwana na kuharibiwa..(utakuja kujua tu baadaye kama Bwana ataruhusu ujue).

Na hiyo ndio sababu kwanini kuna umuhimu wa kumshukuru Mungu kila wakati kwani kuna vitu vingi sana Bwana anatuepusha navyo pasipo hata kuona dalili yake..

Kama ni visa ndio silaha ya adui ili upotezi hiki au kile Bwana alichokupa, basi kabla hivyo visa havijakamilika Bwana ataviharibu.. Hiyo ndio maana ya “kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa”.

Lakini hiyo ni kama wewe ni mtumishi wa Mungu (Maana yake unayempendeza Mungu na kuyafanya mapenzi yake)

Isaya 54:17 “SILAHA ITAKAYOFANYIKA JUU YAKO HAITAFANIKIWA Kila na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema Bwana”

Lakini kama upo nje ya Kristo, basi fahamu kuwa kila silaha itakayofanyika juu yako itafanikiwa na itakudhuru.. Hivyo usiruhusu silaha yoyote ifanikiwe juu yako… Ni sharti iharibiwa ikiwa katika hatua zake za matengenezo, na wenye nguvu za kuweza kuharibu silaha hizo ni wale tu walio ndani ya imani.

Je umempokea Bwana YESU?.. Kama bado huu si wakati wa kupoteza muda, wala kungoja ngoja..ni wakati wa kujiokoa nafsi yako, wala si wakati wa kutazama nyuma, kama mke wa Lutu, bali ni wakati wa kupiga mbio na kuikimbia Sodoma..

Luka 17:32  “Mkumbukeni mkewe Lutu.

33  Mtu ye yote atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza; na ye yote atakayeiangamiza ataiponya”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

TUZIDI KUWA HODARI KATIKA BWANA.

Mata ni nini (Mwanzo 27:3).

Kombeo ni nini? Teo ni nini katika biblia?

Fahamu ni nani aliye mwandishi wa kitabu cha Mathayo.

Rudi Nyumbani

Print this post

Siri za Mungu ni zipi? (1Wakorintho 4:1)

Swali: Biblia inataja siri za Mungu katika 1Wakorintho 4:1, je hizi siri ni zipi na zipo ngapi?

Jibu: Turejee,

1Wakorintho 4:1 “Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu”

Awali ya yote tujue maana ya uwakili unaozungumziwa hapo?…. Uwakili unaozungumziwa hapo sio mfano wa ule wa “mahakamani” La! bali unamaanisha “Usimamizi”… Kibiblia mtu aliyepewa usimamizi wa nyumba au kazi Fulani, aliitwa “Wakili”..soma Luka 12:43-48 na Luka 16:1-13

Hivyo hapo Mtume Paulo, aliposema “.. sisi ni mawakili wa siri za Mungu” maana yake “wameweka kuisimamia nyumba ya Mungu kwa kuzifundisha siri za Mungu”….Kwa urefu Zaidi kuhusu Uwakili katika biblia fungua hapa >>> Wakili ni nani kibiblia? Uwakili ni nini?

Sasa tukirudi katika swali letu, SIRI ZA MUNGU NI ZIPI na ZIPO NGAPI?

Jibu ni kwamba “SIRI ZA MUNGU” zimetajwa MBILI TU (2), katika biblia. Ambazo ni 1)YESU NI MUNGU.   2) MATAIFA NI WARITHI WA AHADI ZA MUNGU… Tutazame moja baada ya nyingine.

  1.YESU NI MUNGU.

Wakolosai 2:2 “ili wafarijiwe mioyo yao, wakiunganishwa katika upendo, wakapate utajiri wote wa kufahamu kwa hakika, WAPATE KUJUA KABISA SIRI YA MUNGU, YAANI, KRISTO;

3  ambaye ndani yake yeye HAZINA ZOTE ZA HEKIMA NA MAARIFA ZIMESITIRIKA”.

Kwanini au kivipi “KRISTO” ni “SIRI YA MUNGU”?.. Kwasababu ndani yake hazina zote na hekima na maarifa zimesitirika..maana yake yeye ndio kila kitu, NDIYE MUNGU MWENYEWE katika mwili wa kibinadamu!!!!..Kiasi kwamba laiti Pilato angelijua hilo, asingeruhusu hukumu ipite juu yake, laiti wale makuhani na maaskari wangelijua hilo wasingepitisha misubari katika mikono yake na miguu yake, lakini walifumbwa macho ili tupate wokovu.

1Wakorintho 2:7 “bali twanena hekima ya Mungu KATIKA SIRI, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;

8  AMBAYO WENYE KUITAWALA DUNIA HII HAWAIJUI HATA MMOJA; MAANA KAMA WANGALIIJUA, WASINGALIMSULIBISHA BWANA WA UTUKUFU”.

Siri hii ya kwamba KRISTO NI MUNGU, inaanzia katika Isaya 9:6, na kisha Yohana 1:1, Yohana 14:9, Yohana 20:28, Tito 2:13, 1Timotheo 3:16 na Ufunuo 22:13-13.

Siri ya Bwana YESU Kuwa MUNGU, inajulikana pia kama “Siri ya Utauwa/Uungu” ambayo Mtume Paulo aliitaja katika 1Timotheo 3:16..

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka SIRI YA UTAUWA NI KUU. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.

Kwahiyo BWANA YESU KRISTO ni MUNGU ALIYEDHIHIRISHWA KATIKA MWILI, na wote tunaomwamini tunapaswa tuwe mawakili wa SIRI HIYO, Maana yake “KUIAMINI na KUIHUBIRI KWA WENGINE, wasiofahamu” .

  2. MATAIFA NI WARITHI WA AHADI ZA MUNGU.

Hii ni Siri ya pili (2) ambayo ilifichwa kwa vizazi vingi, lakini ikaja kufunuliwa baada ya KRISTO kupaa juu mbinguni.. Tangu wakati wa Musa mpaka wakati wa Yohana, manabii wote na wayahudi wote walikuwa wanajua na kuamini kuwa “hakuna namna yoyote, wala njia yoyote” itakayofanyika kwa watu wa mataifa wakubaliwe na MUNGU.

Wote walijua Taifa Teule la Mungu ni ISRAELI peke yake, na mataifa mengine yote ni watu najisi, lakini baada ya Bwana YESU kuondoka alianza kumfunulia Petro siri hiyo kuwa hata mataifa ni warithi sawa tu na wayahudi, kupitia msalaba wake (Bwana YESU).. Na alimfunulia siri hiyo wakati ule alipokwenda nyumbani kwa Kornelio aliyekuwa mtu wa mataifa (Matendo 10)..

Na baadaye Bwana YESU akaja kumfunulia Mtume Paulo siri hiyohiyo kuwa Mataifa nao ni warithi, tena wa ahadi moja na wayahudi, hivyo wanastahili injili, na kuhubiriwa habari njema..

Waefeso 3:5 “Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;

6  YA KWAMBA MATAIFA NI WARITHI PAMOJA NASI WA URITHI MMOJA, NA WA MWILI MMOJA, NA WASHIRIKI PAMOJA NASI WA AHADI YAKE ILIYO KATIKA KRISTO YESU KWA NJIA YA INJILI;

7  Injili hiyo ambayo nalifanywa mhudumu wake, kwa kadiri ya kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa kadiri ya utendaji wa uweza wake”.

Na sisi lazima tuwe wahudumu (Mawakili) wa siri hii kwamba “Wokovu ni haki ya watu wote” na Mungu anawapokea watu wote, ikiwa tu watakubali kutii na kunyenyekea mbele zake.

Kwahiyo kwa hitimisho, ni kwamba “Siri za Mungu” Si zile siri za kanisa, au zile za watumishi, au wapendwa kanisani…La! Bali ni hizo zilizotajwa hapo katika maandiko…Na kumbuka, shetani naye ana siri yake ijulikanayo kama “Siri ya Kuasi” iliyotajwa katika biblia ambayo inafanya kazi kwa kasi sana nyakati hizi…

Je umempokea YESU?..Kumbuka kipindi tulichopo ni cha Neema, lakini hii neema haitadumu milele, itafika wakati itaisha.. baada ya unyakuo hakuna neema tena, vile vile baada ya kifo hakuna Neema tena. Ni heri ukayasalimisha maisha yako kwa Bwana YESU maadamu unaishi, baada ya kifo hakuna nafasi ya pili.

Warumi 10:8 “Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo.

9  Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.

10  Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.

11  Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika

12  Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao;

13  KWA KUWA, KILA ATAKAYELIITIA JINA LA BWANA ATAOKOKA”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.

Hazina za gizani ni zipi? (Isaya 45:3).

SIRI YA KUASI KATIKA KANISA LA MUNGU.

UFUNUO: Mlango wa 10.

KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.

Rudi Nyumbani

Print this post