Category Archive Mafundisho

Maana ya Mithali 10:1 Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;

SWALI: Naomba kuelewa tafsiri halisi ya maneno tuyasomayo kwenye Mithali 10:1.

Mithali 10:1

[1]Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.


JIBU: Mpumbavu kibiblia ni mtu yeyote aliyemkosa Mungu ndani yake, ambaye kwa njia hiyo anaweza kuonyesha tabia yoyote mbaya, aidha wizi, au kiburi, au umalaya, au uchawi, au hasira, mwingine atakuwa mlevi, mtukanaji, mwongo, jambazi, mchoyo, mbinafsi, mkorofi n.k.

Chimbuko ni kumkosa Mungu ndani yako.

Sasa mwana wa namna hii kibiblia sio tu anaiathiri roho yake lakini pia hata waliomzaa.

Mithali 10:1

[1]Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.

Lakini kauli hiyo inapaswa eleweke vizuri, sio kwamba mwana akiwa na hekima ni furaha ‘tu’ kwa baba, mama hausiki, au akiwa mpumbavu ni mzigo tu kwa mama baba hausiki.

Hapana, mambo hayo yanawapata wote.. akiwa na hekima wote hufurahi, vilevile akiwa mpumbavu wote huhuzunika.. Ndio maana sehemu nyingine anasema..

Mithali 17:25

[25]Mwana mpumbavu ni huzuni kwa babaye, Na uchungu kwa mamaye aliyemzaa.

Wazazi wote hufurahishwa au huhuzunishwa kwa tabia husika za watoto wao.

Lakini alipoonyesha kama kuwatenganisha, ni kuelezea ‘hisia za juu zaidi’ zitokeazo kulingana na mzazi na mzazi.

Kimsingi mtoto akiwa na hekima, baba huwa anajivunia sana mtoto huyo, utaona baba anajigamba kwa ajili ya mwanae..Mfano tu wa Sulemani kwa Daudi, hekima yake ilikuwa ni fahari ya babaye Daudi.

Lakini akiwa ni mpumbavu, tengeneza picha mtoto ni teja, na kibaka, na mlevi, kiuhalisia utaona akina mama ndio wanateseka zaidi na kuumia juu ya watoto wao. Wanapatwa na mzigo mzito sana moyoni. Na hiyo huwa inawasukuma kuzunguka huku na huko kutafuta msaada. Tofauti na wababa, watamwonya, mara ya kwanza, mara ya pili, mara ya tatu wakiona haonyeshi geuko lolote, ni rahisi kuachana nao.

Ni nini tunaonyeshwa rohoni?

Si mwilini tu. Rohoni Kristo anafananishwa na Baba, na Kanisa lake ni Mama.

Wote sisi ni watoto ambao Kristo ametuzaa ndani ya kanisa lake, tuwapo na hekima (tunamcha), tunatembea katika misingi ya Neno lake, kwa kuzingatia viwango vya upendo na utakatifu, tujue kuwa Kristo hutukuzwa na hujivunia sana sisi. Lakini tuwapo wapumbavu, tunajiumiza zaidi sisi wenyewe. Kwamfano sababu mojawapo ipelekeayo makanisa kupoteza furaha na amani,  ni kukosekana umoja na upendo.

Bwana atusaidie.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.

MJUE SANA YESU KRISTO.

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

Rudi Nyumbani

Print this post

USIKOSE MAZIKO (Mhubiri 6:3)

SWALI: Naomba kufahamu nini maaana ya mhubiri 6:3?

Mhubiri 6:3

[3]Mtu akizaa watoto mia, akaishi miaka mingi, nazo siku za maisha yake ni nyingi, lakini nafsi yake haikushiba mema; tena ikiwa, zaidi ya hayo, amekosa maziko; mimi nasema, Heri mimba iliyoharibika kuliko huyo;


JIBU: Mhubiri katika jicho la kibinadamu anaelezea jinsi inavyoonekana kama ni hasara kubwa sana, kwa mtu ambaye amejitaabisha maisha yake yote, kutengeneza heshima, kwanza kwa kuwa na watoto wengi, lakini pia kwa kujinyima raha, kuwekeza vema vitu vyake ili siku za kufa iwe heshima kubwa kwake, hata baada ya hapo aache jina kwa uzao wake wote.

Lakini mambo yanatokea kinyume chake, anakufa kama mtu asiye na kitu, au kwa aibu,  hata baada ya hapo anasahaulika kabisa ijapokuwa aliwekeza muda wake mwingi kujijengea jina.. Sasa mhubiri anasema ni heri mimba iliyoharibika kuliko huyu kwasababu kimsingi mimba huwa inasahaulika kweli muda mfupi,na haiwi na maziko ya watu, lakini haijatabika kwa lolote, kuliko huyu ambaye ametabika sana maisha yake yote, kuacha kumbukumbuku , halafu amesahaulika mfano ule ule wa kama mimba iliyoharibika.

Mfano wa watu kama hawa alikuwa ni Ahabu, ambaye alikuwa na watoto sabini, na ufalme mkubwa lakini alikufa kwa aibu, damu yake ililambwa na mbwa. Pamoja na mkewe Yezebeli ambaye mzoga wake uliliwa kabisa na mbwa, hakuwa na maziko. Ikawa ni fedheha kubwa sana kwao (1Wafalme 22),

Lakini maana hasaa ya huo mstari rohoni ni ipi?

Maziko halisi ni yale ya Mungu. Kukosa maziko ya kibinadamu, hakuwezi kukufanya udharauliwe milele. Lakini ukikosa maziko ya Mungu ni aibu na kudharaliwa milele.

Ukipata fedha zote duniani, ukazaa watoto wengi ambao watalirithi jina lako, ukawa mtu maarufu, mpaka ukawa mfalme wa nchi, jina lako likakumbukwa hata vizazi elfu baadaye, kama hujafa ndani ya Kristo. Ni heri mimba iliyoharibika kuliko wewe. Huna kumbukumbu lolote mbinguni

Mwamini Kristo leo, akuoshe dhambi zako. Jiulize ukifa leo katika dhambi, huko uendako utakuwa mgeni wa nani? Wokovu ni sasa, saa iliyokubaliwa ni leo. Fungua moyo wako mpokee Yesu, hata kufa kwako kuwe kuna thamani.

Zaburi 116:15

[15]Ina thamani machoni pa BWANA Mauti ya wacha Mungu wake.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Maana ya Mhubiri 1:9 “wala jambo jipya hakuna chini ya jua”. 

Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Rudi Nyumbani

Print this post

MHESHIMU MCHUNGAJI WAKO.

Kila mahali pana mamlaka yake, na mamlaka hizo huwa ni  wajibu kwa walio chini yake kuzitii. Kwamfano katika familia Mungu ameweka mamlaka, Baba awe kichwa, na mama msaidizi wake, hivyo ni wajibu wa watoto kuwatii wazazi wao . Familia haiwezi kusimama,.kama mtoto atataka nafasi ya baba, kwamba yeye ndio atoe maamuzi ya mwisho, au ajiamulie la kufanya, awapangie wazazi wake majukumu ya ndani. hilo haliwezekani.

Vilevile katika ngazi ya utawala wa kidunia, Mungu kaziweka mamlaka na anataka watu wote wazitii, kwasababu hazijaamuriwa na mwanadamu bali yeye Mungu mwenyewe..

Warumi 13:1-2

[1]Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu.

[2]Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.

Tito 3:1-2

[1]Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema; [2]wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wema, wakionyesha upole wote kwa watu wote.

Sasa hizi ni mamlaka za kidunia. Zipi kuhusu Mungu, unadhani hana mamlaka?

Mungu pia ameweka mamlaka yake duniani, ambayo ni kuu kupita hizo zote, na kupitia hiyo huwahudumia watu wake. Na anataka tuitii na kuitetemekea kwasababu ni yeye mwenyewe atendaye kazi kupitia hiyo.

Je mamlaka hiyo kaiweka kupitia nani?

Bila shaka kupitia wachungaji wetu/waangalizi wetu, ndani ya kanisa

Ni vema kufahamu kuwa kiongozi yoyote wa kiroho (anayeisimamia kweli). Hakujiteua mwenyewe kwenye nafasi hiyo.  Mitume wa Yesu hawakujichagua wao. Bali walichaguliwa na Mungu mwenyewe.

Mtu yeyote aliyepewa maono ya kuanza kanisa, na ukajikuta upo chini yake, au kateuliwa na Roho Mtakatifu mwenyewe ndani ya kanisa (Matendo 14:23), Huyo ni wa kumtii sana. Kama vile unavyowatii watawala au mazazi wako kwenye familia, haijalishi atakuwa na mapungufu kiasi gani, au umri wake ni mdogo au mkubwa kiasi gani, awe mwenye uwezo au asiye na uwezo kiasi gani.

Kwanini uwaheshimu.

1) Wanajitaabisha kwa ajili yako kukuchunga, kukuonya na kukuombea.

Hivyo wajibu ni wako kurudisha moyo wa upendo, na kuwasikiliza.

1 Wathesalonike 5:12-13

[12]Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni; [13]mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi.

2) Watasimama mbele ya kiti cha hukumu siku ya mwisho kutoa hesabu juu yako.

Hivyo ni wajibu kuonyesha moyo wa kunyenyekea kwao.

Waebrania 13:17

[17]Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.

Madhara ya kutowasikiliza/ kutowatii.

i) Watafanya kazi ya Mungu kwa kuugua.

Hapo kwenye Waebrania 13:17b anasema..

..ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi

Na matokeo yake utendaji kazi ndani ya kanisani utakuwa hafifu. Ukishaanza kuonyesha tabia ya kutosikiliza unachoelekezwa, unapewa jukumu hutekelezi, hurudishi mrejesho, unafanya tofauti na wengine, yeye anataka uende kulia wewe unaenda kushoto, , yeye anafundisha hiki wewe unafundisha kile. Fahamu kuwa jambo hilo litamhuzunisha kiongozi wako. Na hivyo kupelekea hamasa ya kuhudumu kupungua. Na madhara yake ni kuwa Mungu kukata utendaji kazi wake mahali hapo,

ii) Dhara lingine ni kuwa utajisababishia adhabu kwa Mungu.

Wakati ule Haruni na Miriamu dada yake. walimnenea Musa maneno mabaya kwasababu na mke wake ambaye hakuwa myahudi. Mungu aliwaadhibu kwa kumpiga ukoma Miriamu kwasababu tu hiyo ya kutoonyesha adabu kwa mtumishi wake.

Hesabu 12:7-8

[7]Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote;

[8]Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la BWANA yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?

Ni kosa kumnenea vibaya mchungaji wako. Epuka masengenyo na uasi na matabaka ndani ya kanisa. Uonapo kosa mwombee, au mfuate mweleze  uwapo naye peke yake. Hilo litamjenga zaidi ya kutoa malaumu na manung’uniko. Adui hutumia sana njia hii kuleta mafarakano na magomvi, na mapigo kanisani.

Mheshimu mchungaji wako, zaidi ya raisi wa nchi kwasababu yeye ni balozi wa mbinguni na Mungu atakuinua (1Petro 5:1-6)

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi

Ipi tofauti kati ya KUHANI na MCHUNGAJI.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Rudi Nyumbani

Print this post

Ni vitu vipi hivyo tumekirimiwa vitupasavyo uzima na utauwa? (2Petro 1:3)

SWALI: Ni vitu vipi hivyo tumekirimiwa vitupasavyo uzima na utauwa? (2Petro 1:3)

2 Petro 1:3

[3]Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia “vitu vyote” vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.


JIBU: Andiko hilo linatufundisha kuwa Mungu anao uweza wake, ambao una nguvu ya kumfanya mtu kuwa kama anavyotaka. Sasa hapo tunafunuliwa kuwa uweza huo ameuachilia katika maeneo mawili makuu la kwanza ni UZIMA la pili UTAUWA. Uzima ni maisha ya milele, na utauwa ni utakatifu.

Sasa swali linauliza ni vitu gani hivyo ambavyo Mungu ametukirimia vinavyozungumziwa hapo vitufanyavyo  kuufikia huo uzima na utauwa, anaousema?

Vitu vyenyewe ni kama vifuatavyo

1) Mwana wake (Yesu).

Bila Yesu Kristo kuja duniani, kuwa fidia ya dhambi zetu kwa kifo chake, tusingeweza kupokea uzima wa milele. Kwasababu ilihitajika kumwagika kwa damu isiyokuwa na dhambi ili kutuondolea sisi dhambi zetu tupokee uzima wa milele. Hivyo uweza huu wa uungu, umetukirima Yesu Kristo, kutuondolea dhambi ndani yetu.

Tuna kila sababu za kumshukuru Mungu sikuzote, kwa huruma zake hizi. Tunaye mkombozi ambaye kila amwaminiye tu. Uzima anao. (Yohana 3:16)

2) Roho Mtakatifu.

Roho wa Mungu ni msaidizi wetu, bila yeye, ni kweli tungesamehewa dhambi lakini tusingeweza kuwa watakatifu. Hivyo yeye anapokuja juu yetu na kujaa vizuri tunajikuta tunaweza enenda katika mwenendo wa utakatifu. Hivyo huu ni uweza wa Mungu mwenyewe.

Yohana 14:16

[16]Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;

Wagalatia 5:16

[16]Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

3) Biblia.

Hichi ni kitu kingine ambacho Mungu ametukirimia kwa uweza wake, kwa kuisoma tunatambua wazo lote la Mungu, na hivyo kuturahisishia kuisikia sauti ya Mungu. Tusomapo biblia tunabadilishwa tabia zetu, kwa maonyo, mafundisho, faraja, shuhuda n.k.

2 Timotheo 3:16

[16]Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

4) Kanisa.

Kanisa ni uweza wa Mungu kwetu, hekima ya Mungu ambayo aliibuni yeye mwenyewe siku ile ya pentekoste. Kuwakusanya watakatifu wake na kuwahudumia kwa karama mbalimbali. Kanisa humlinda mwamini, kanisa humwombea mwamini, humsaidia mwamini, humfariji mwamini na kumwongoza.

Sikuzote  Uthabiti wa mwamini hutegemea kanisa. Mtu asiye na kanisa (ushirika), ameukana uweza huu wa Mungu, ambao Mungu huutumia kutukamilisha sisi.(Waebrania 10:25)

1 Wakorintho 12:27-28

[27]Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.

[28]Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha.

5) Malaika

Bwana huwatuma malaika wake, kumlinda mwamini asijikwae. Huu ni uweza wa Mungu pia.

Waebrania 1:14

[14]Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?

Zaburi 91:11-12

[11] Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote. [12] Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

Kama si Mungu kutuagizia malaika zake, bila shaka adui angepata penyo nyingi sana za kutuletea majaribu na kutuangusha. Ukiwa ndani ya Kristo adui hana nguvu juu yako, kwasababu unalindwa na jeshi lake. Unapiganiwa kwa namna usiyojua wewe.

Na hivyo kuishi maisha ya utauwa kwako inakuwa ni vyepesi zaidi ya mtu mwingine yeyote aliye nje.

Swali ni je umepokea vitu hivi vyote?

Ukipungukiwa kimoja wapo, ni lazima tu eneo lako la utauwa  au uzima litakuwa na kasoro. Kumbuka Bwana ameshatukirimia ni sisi tu kukubali na kupokea.

Wokovu upo bure, biblia ipo wakaki wote, Roho yupo, kanisani lipo, malaika wapo. Amini tu na  kutubu dhambi zako, kwa Kumaanisha kabisa kugeuka na kumfuata Yesu, akupaye ondoleo la dhambi. Kisha ukabatizwe, upokee Roho. Na baada ya hapo, shiriki sasa vitu hivyo vya ki-ungu kwasababu vimewekwa tayari kwa ajili yako na mimi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Rudi Nyumbani

Print this post

JINSI YA KUMFANYA MUNGU MWONGO.

Wazia jambo hili, raisi amepewa taarifa na wataalamu wake wa hali ya hewa kwamba kuna kimbunga kikubwa kinatokea bahari. 

Hivyo akachukua hatua ya kuwatahadharisha wananchi wake wasifike maeneo yote ya pwani. akawaelekeza na namna ya kujilinda, na mazingira yote hatarishi, akawajuza na madhara ambayo tayari kimbunga hicho kimeshaleta, akawaonya sana wakae ndani mpaka hicho kipindi chote cha hatari kitakapokwisha.

Lakini cha kushangaza kesho yake wakaonekana watumishi wa raisi na mawaziri , pamoja na watumishi wote wa serikalini wakiwa ufukweni wakiogolea na kufurahi na kustareheka..kana kwamba hakuna hatari yoyote mbeleni.

Unadhani ni wazo gani litajengeka kwa wananchi juu ya raisi wao?

Watasema raisi ni mwongo. Ametulaghai, mbona mamlaka yake haichukui hatua ya janga lililotangazwa?

Lakini heri na hapo, unadhani raisi naye atajisikiaje moyoni, kwa wale watu waliomtendea hivyo?

Sasa hilo ndilo watu wanalolifanya kwa Mungu sasa mpaka anaonekana ni mwongo.

Neno la Mungu linasema…

1 Yohana 5:10-12

[10]Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu anao huo ushuhuda ndani yake. Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe.

[11]Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe.

[12]Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima.

Mungu alimtuma Yesu duniani, kuushuhudia ulimwengu kuwa una dhambi, Na mwana wake kuja duniani ni kwa lengo hilo kuu la kuwaokoa watu dhambini.

Hivyo Mungu akamshuhudia kwa sauti kutoka mbinguni, kwa ishara na miujiza mingi,.kwa Roho Mtakatifu aliyetuachia, lakini bado watu wakapuuzia, wakaendelea na mambo yao. Sasa huko ndiko kumfanya Mungu mwongo. Yaani kufikiri kuwa sisi hatukutenda dhambi, tunamfanya yeye kuwa mwongo.

1 Yohana 1:10

[10]Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu.

Hivyo mtu yeyote anayekataa injili, ni kwamba anamfanya yeye aonekane mwongo. Ushuhuda wake ni uongo, kazi aliyoifanya ni bure, ni kuthibitisha mtu anaweza kuishi tu mwenyewe apendavyo na akawa na maisha ya milele?

Je! umempokea Yesu, kama Bwana na mwokozi wa maisha yako. Kama ni La! ndugu Kamwe usimfanye Mungu mwongo.

Amini ushuhuda wake kupitia mwana wake kwasababu ni kweli usipookolewa na yeye. Uzima wa milele haupo ndani yako. Dhambi ipo, na bado itaendelea kuwepo juu yako, hata kama utakuwa na matendo mazuri kiasi gani.

Fanya uamuzi sasa ya kuokoka. Hukumu ipo mbele na inatisha.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JINSI YA KUUHARIBU UJANA WAKO.

NI NJIA GANI MTU AITUMIE AWEZE KUSHINDA TAMAA NA VISHAWISHI?

NINYI AKINA BABA MSIWACHOKOZE WATOTO WENU

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Yakobo.

Kitabu hiki kama kinavyoanza na utambulisho wake. Kiliandikwa na Yakobo aliye mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo. (Yakobo 1:1).

Yakobo huyu sio yule mmoja wa mitume kumi na mbili wa Yesu, (yaani ndugu yake Yohana wana wa Zebedayo)..Hapana bali ni mmoja wa ndugu  za Yesu wa kunyonya aliozaliwa nao (kimwili) kupitia Mariamu. Na huyu ndiye baadaye aliyekuwa kama moja ya nguzo ya kanisa la Yerusalemu. Wengine wakiwa ni Petro na Yohana.

Inaonekana wakati Petro alipotoka na kwenda kusimamisha makanisa katika mataifa ya mbali, yeye ndiye aliyebakia kama msimamizi mkuu kwa kanisa la Yerusalemu,

Vilevile majaribu na dhiki mbalimbali zilizolikumba kanisa hili tukiachia mbali janga la njaa kubwa lililotokea wakati ule, mpaka wakapelekewa misaada kutoka kwa makanisa mengine (Matendo 11:28–30), lakini pia na dhiki walizozipata kwa wayahudi wasioamini, mtume huyu Yakobo alizifahamu sana.

Ndio maana katika sehemu kadha wa kadha za waraka huu Yakobo anayazungumzia majaribu,

Huku yeye akiyachukulia katika taswira nyingine, tofauti na kama yangepaswa kuchukuliwa, akielezea  kwamba Majaribu na dhiki, sio jambo la kukaa na kuhuzunika, kinyume chake tuyaone kama ni fursa nzuri ya sisi kuimarishwa na kuthibitishwa kiimani.

Lakini Maudhui kuu ya waraka huu, ni kueleza mahusiano kamili yaliyo katika imani, na matendo yake. Kwamba hivi vitu viwili haviwezi kutenganishwa.

Waraka huu aliuelekeza kwa wayahudi wote waliotawanyika ulimwenguni kote (kwa wakati ule). Ambao kwasasa unatuhusu sote.

Huu ndio ufupisho wake katika maeneo makuu SITA (6).

Yakobo anaeleza.

 1) Imani iliyo kamili huvumilia majaribu na dhiki (1:2-18)

  • Inapopita katika majaribu haivunjiki moyo bali hufurahi na kustahimili (1:2-4,),
  • Lakini pia hutambua kuwa chanzo cha majaribu si Mungu, bali ni tamaa za mtu mwenyewe. Hivyo asiwe na fikra kuwa Mungu anawajaribu watu kwenye dhambi (1:13-15)

 

2) Imani kamilifu huonekana katika hekima ya ki-Mungu.

  • Hekima ya ki-Mungu huwa ni safi, ya amani na upole, haiwi katika wivu, uchungu na ugomvi (3:13-17)
  • Hivyo pale tunapopungukiwa hekima tunapaswa tuombe (1:5-8),

3) Imani/Dini ya kweli huwachukulia watu kwa usawa bila kujali matabaka yao

  • Matajiri wanapaswa wasiwakandamize maskini katika kazi zao(Yakobo 5:1-6),
  • Vilevile katika kanisa kusiwe na upendeo kwa watu matajiri zaidi ya maskini (2:1-13)

4) Imani ya kweli huiweka huthibitika kwa matendo yake (1:19-2:26)

  • Tunapaswa tuwe wepesi wa kusikia, zaidi ya kuongea (1:19-20)
  • Tuzitumie ndimi zetu vema. Yatokea yaliyo sahihi tu (1:26, Yakobo 3:1-12)
  • Tusiwe msikiaji tu wa Neno bali pia mtendaji (1:21-27).Kwa kwenda kuwatazama wajane, yatima (1:26)
  • Kuonyesha kimatendo wokovu tuliopokea, vinginevyo ni imani mfu ijulikanayo kama ya mashetani (2:14-26)

5) Imani ya kweli inazalika katika kujinyenyekeza (4:1-17)

  • Kwa kukataa kuwa rafiki wa dunia, (4:1-6)
  • kwa kujisogoza karibu na Mungu, kwa maombolezo, kulia, (4:7-17)
  • Kwa kuepuka kuwahukumu wengine (4:11-12)
  • Kwa kukataa kujivunia kesho (4:13-16)

6) Imani ya kweli huthibitika katika Maombi, upendo na uvumilivu (5:1-20)

  • Kuna baraka katika kuwa wavumilivu mpaka kutokea kwake Bwana (mfano wa Ayubu 5:7-12)
  • Kuna heri kuwa waombaji wenye bidii kama Eliya (5:13-18)
  • Kuna heri kuonyesha upendo kwa waliopotea, kwasababu tunaponyeka pia sisi (5:19-20).

Kwa ufupi mtume Yakobo kwa uvuvio wa Roho alilenga kuimarisha watakatifu katika eneo la utendeaji kazi imani. Na hiyo pengine ilidhaniwa au kufikiriwa kuwa wokovu ni kuamini tu, bila kuonyesha matendo yoyote. Lakini katika waraka huu analiweka sawa kwa kuonyesha matendo na imani hivitenganiki, kama mtu akijaribu kuacha kimoja, basi ni kifo mfano wa roho na mwili visivyoweza kutenganika.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA MATHAYO.

Uchambuzi na Mwandishi wa kitabu cha Wagalatia

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo? (Matendo 11:23)

SWALI:  Mitume walikuwa na maana gani kuwasihi wanafunzi kule Antiokia, waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo? Ni maana ya hiyo kauli?

Matendo 11:22 Habari hizo za watu hao zikafika masikioni mwa kanisa lililokuwako katika Yerusalemu; wakamtuma Barnaba, aende hata Antiokia.

23 Naye, alipokwisha kufika na kuiona neema ya Mungu akafurahi, akawasihi wote waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo.

24 Maana alikuwa mtu mwema amejaa Roho Mtakatifu na imani; watu wengi wakaongezeka upande wa Bwana.

JIBU: Kauli hiyo inamaanisha kwa “kusudi sahihi la moyo” sawasawa na imani waliyoipokea, Kwasababu Mitume walijua madhumuni ya wao kumfuata Yesu yakiwa sio sahihi, kusimama kwao kunaweza kusidumu. Kwasababu walijua wapo wanaomfuata Kristo kwa sababu ya fitna, wengine fedha, wengine watu, wengine vyeo, wengine kuajiriwa n.k.. Na hiyo haipaswi. Kwasababu Mungu huuchunguza kwanza moyo wako kilichokupelekea  kumfuata ni nini?. Ikiwa sio kwa lile kusudi lake sahihi, hauwezi kusimama.

Sifa hizo za Mungu kuchunguza makusudi ya moyo tunazisoma kwenye vifungu hivi;

Waebrania 4:12 Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukataokuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.

Hivyo hata sasa, Mungu anataka tuipokee imani kwa kusudi la kweli la moyo, ili tuweze kudumu, na kuona utendaji kazi wake bora, katika maisha yetu ya rohoni, na pia tuweze kusimama hadi mwisho .

Kusudi sahihi la moyo ni kumfuata Yesu ili akuokoe dhambini, kumtazama Kristo kama dhabihu kamilifu ya Mungu iliyotolewa kwa ajili ya kuondoa dhambi zetu, na sio atupe utajiri, au atuponye magonjwa, au atupe mke/mume.

Kwanini  iwe hivyo?

Kwasababu hayo yasipokuja kwa wakati  utamwacha Kristo, au yakipatikana basi Kristo hawezi kuwa tena na thamani moyoni mwako, kwasababu kusudi lako moyoni lilikuwa utatuliwe tu changamoto yako, si zaidi. Na ndio maana ni rahisi leo kuona watu wengi makanisani, lakini wasiwe wote wameokoka.

Mitume waliliona hili kama ni jambo muhimu sana kufundishwa mwanzoni kabisa mwa imani kwa waongofu wapya. Vivyo hivyo na sisi tuige fundisho hilo pindi tunapowajenga waongofu wapya.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.

NAAM, HATA WABAYA KWA SIKU YA UBAYA. 

Nini tofauti ya Majira na Wakati?

Rudi Nyumbani

Print this post

Wabadili fedha ni watu gani kwenye biblia? (Mathayo 21:21)

Mathayo 21:12 Yesu akaingia ndani ya hekalu, akawafukuza wote waliokuwa wakiuza na kununua hekaluni,akazipindua meza za wabadili fedha, na viti vyao waliokuwa wakiuza njiwa;

13 akawaambia, Imeandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala; bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.

Bwana aliwaagiza wana wa Israeli, kwamba waendapo mbele zake mahali patakatifu alipopachagua wakusanyike kwa ajili ya upatanisho. Kila mtu mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi atatoa nusu shekeli kama kodi, ambapo fedha hiyo ilitumika kwa ajili ya shughuli mbalimbali za hekaluni .  Hivyo watu wote walipokwenda hekaluni kwa ajili ya ibada, walihakikisha wanabeba sadaka hiyo kwa ajili ya gharama za hekalu.

Utalisoma hilo katika vifungu hivi;

Kutoka  30:11 Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

12 Utakapowahesabu wana wa Israeli, kama itakavyotokea hesabu yao, ndipo watakapompa Bwana kila mtu ukombozi kwa ajili ya roho yake, hapo utakapowahesabu; ili kwamba yasiwe maradhi kati yao, hapo utakapowahesabu.

13 Nacho watakachotoa ni hiki, kila mtu apitaye kwa wale waliohesabiwa atatoa nusu shekeli kwa kuiandama shekeli ya mahali patakatifu; (shekeli ni gera ishirini;) nusu shekeli kwa sadaka ya Bwana.

14 Kila mtu apitaye kwa wale waliohesabiwa tangu huyo ambaye umri wake ni miaka ishirini, au zaidi, atatoa hiyo sadaka ya Bwana.

15 Matajiri hawataleta zaidi, wala maskini hawataleta kilichopungua, katika hiyo nusu shekeli, watakapotoa hiyo sadaka ya Bwana, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya roho zenu.

16 Nawe utapokea hizo fedha za upatanisho mikononi mwa hao wana wa Israeli, na kuziweka kwa ajili ya utumishi wa hema ya kukutania; ili kwamba ziwe ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli mbele ya Bwana, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya roho zenu.

Lakini sasa kwa sababu fedha hiyo ilipaswa itolewe kwa fedha ya kiyahudi, na si za kigeni, ikizingatiwa kuwa watu walikuwa wanatoka mataifa mbalimbali ulimwenguni kote kuja kumwabudu Mungu pale Yerusalemu, Sasa hawa wanaoitwa wabadili fedha ndio wakapatia hapo fursa ya kuanzisha biashara hiyo pale hekaluni.

Lakini badala ya kufanya kama huduma, kuwasaidia watu kazi hiyo bila riba, wao  wakageuza pale kuwa ni mahali pao pa kujipatia faida, pakawa  kama kiini cha soko la fedha ukanda ule wote. Watu walipokuja na fedha zao, waliwageuzia kwa riba ya juu.

Hiyo ndio sababu Yesu kuchukizwa na wale watu, na kwenda kuzipindua meza zao, pamoja na wale wauza njiwa

Hata sasa, desturi hii ya adui inatenda kazi katika nyumba nyingi za Mungu duniani.

Watu hutumia mambo ya kiibada kama njia ya kujipatia faida. Si ajabu hata Mtume Paulo aliliona hilo akasema,

wakidhani ya kuwa utauwa ni njia ya kupata faida. (1Timotheo 6:5).

Utakuta mtu anafanya biashara ya biblia, kando kando ya kanisa. Atakuwa radhi kuzitoza bei zaidi ya kiwango stahiki ili ajinufaishe, kwasababu anajua watu wenye uhitaji wa vitabu hivyo kwa watu huo ni wengi. Mwingine atakuwa anauza maji au mafuta (wayaitayo ya upako), lengo sio kuwasaidia hao watu wapokee huduma, bali ni kujipatia faida.

Injili ya Kristo imekuwa biashara, kumwona mtumishi uombewe, ni lazima uandikiwe kuponi ya fedha, vinginevyo huwezi  kumwona.

Sas watu kama hawa Yesu hawezi waonea huruma atazipindua  meza zao, kama tu vile alivyozipundua za wale hekaluni. Maana yeye ni yeye Yule jana, na leo na hata milele.

2Timotheo 3:9 Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa dhahiri.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je! Habari iliyo katika 1Nyakati 21:25, na 2Samweli 24:24, ya Daudi kununua kiwanja  inajichanganya?

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

SI KWA FAIDA YA MWENYEZI, BALI KWA FAIDA YETU.

Rudi Nyumbani

Print this post

BWANA, SISI TUNATAKA KUMWONA YESU.

SWALI: Kwanini wale wayunani, walimfuata Filipo na kumwambia tunataka kumwona Yesu, maudhui  ya tukio lile ni nini, mpaka lirekodiwe?


JIBU: Kipindi cha Bwana Yesu hadi kipindi chote cha mitume, yalikuwepo makundi mawili ya watu ambayo yalijikita kwa umakini sana katika kutafuta uhalisia na ukweli wote kuhusu masuala ya Mungu.

kundi la kwanza lilikuwa ni wayahudi, na kundi la pili ni wayunani. Tofauti ya wayahudi na wayunani ni kwamba. Wayahudi walijikita kuthibitisha kwa njia ya ishara. Lakini wayunani kwa hekima.

1 Wakorintho 1:22-23

[22]Kwa sababu Wayahudi wanataka ishara, na Wayunani wanatafuta hekima;  [23]bali sisi tunamhubiri Kristo, aliyesulibiwa; kwa Wayahudi ni kikwazo, na kwa Wayunani ni upuzi;

Hivyo Yesu ambaye ni jibu lao wote alipokuja, baadhi ya hawa wayahudi walipomwona Kristo wakaanza kumthibitisha kwa ishara kwa walivyotarajia, kwamba ndiye masihi na mkombozi waliyemtarajia la!.(wakitaka wafanyiwe matendo fulani ya ajabu mbele ya macho yao, waamini)

Ijapokuwa Mungu hathibitishwi kwa ishara, bado Kristo aliwapa ishara.. Na ishara hiyo ilikuwa ni ile ya Yona. kukaa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana na hatimaye kutoka mzima.

Mathayo 12:38 Hapo baadhi ya waandishi na Mafarisayo wakamjibu, wakasema, Mwalimu, twataka kuona ishara kwako.

39 Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.

40 Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi.

Hilo lilipokuja kutimia…tunaona wayahudi wengi waliamini, ikiwemo mitume (akina Tomaso). Na ndio ukawa mwanzo wa kumuhubiri Yesu aliyefufuka.

Lakini wale waliotazamia ishara walizoziwaza kwa akili zao, mfano  za kushusha moto, kama Eliya, na kusahau ile ya kufufuka ambayo imezidi zote, bado Kristo akabakia kikwazo kwao.

Halikadhalika na kwa wayunani. Walimtafuta Mungu kwa njia ya hekima, ya elimu, ya maarifa, walimtafuta Mungu mwenye siri zote za uumbaji, na ujuzi, na utashi zaidi ya wanadamu wote na viumbe vyote.Ambaye atawazidi wanafalsa wao kama Plato, Socrates, Aristotle.

Kwa muda mrefu hawakufanikiwa mpaka baadhi yao, wakaishia kumwabudu tu, huku wakikiri hawamjui.

Matendo  17:22-23

[22]Paulo akasimama katikati ya Areopago, akasema, Enyi watu wa Athene, katika mambo yote naona ya kuwa ninyi ni watu wa kutafakari sana mambo ya dini.

[23]Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua.

Yaani wakiwa na maana tunasikia miungu mingi,.lakini katika hiyo yote bado hatujaona mwenye hekima ya kuitwa Mungu wa ulimwengu. Wote akili zao ni kama za kibinadamu tu.

Sasa tukirudi kipindi cha Yesu, tunaona tukio jipya linajitokeza,

sio tu wayahudi walimwamini, bali hadi hawa wayunani watafuta-hekima wengi wao waliposikiliza maneno ya Yesu, na kupima kwa jicho la hekima, wakaona hakika hajawahi tokea anayeweza kuelezea ukweli wote wa uumbaji kama Yesu.

Hilo liliwashawishi na kuwafanya kukiri kuwa huyu ndiye suluhisho la utata wetu kuhusu Mungu na elimu.

Hivyo wakaamini, ndio sababu ya wao kumfata Filipo kumwomba wamwone Yesu. Hiyo ilikiwa ni heshima kubwa sana kwa Yesu  (kidini) mbele ya macho makuhani na mafarisayo wote, kwamba Mungu kathibitishwa kifalsafa. Kumbuka wayunani hawa waliokwenda hawakuwa watu tu wa kawaida. Bali ni watu wenye heshima ya juu sana na hadhi.

Hiyo ndio sababu Bwana Yesu  kusema saa imefika mwana wa  Adamu atukuzwe.

Yohana 12:20-26

[20]Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu.

[21]Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu.

[22]Filipo akaenda, akamwambia Andrea; kisha Andrea na Filipo wakamwambia Yesu.

[23]Naye Yesu akawajibu, akasema, Saa imefika atukuzwe Mwana wa Adamu.

[24]Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi.

[25]Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele.

[26]Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.

Ni nini cha tunafundishwa katika habari hii ya wayunani?

Hata leo, Yesu anathibitika katika mambo yote endapo tu tutamaanisha kumwona katika namna hizo. Ndio maana katika makundi yote ya watu ni lazima utakuta waamini.

Katika ya wanasayansi utawaona, katikati ya wanajeshi utawaona, katikati ya watawala utawaona,katikati ya mamajusi utawaona, katikati ya  matajiri utawaona, katikati ya maskini utawaona, kati ya wanazuoni utawaona, kati ya madaktari utawaona,

Ukiuliza imekuwaje katika hali zao/ nafasi zao ambazo ni mbaya, na nyingine zenye majaribu, au zenye kumkana Mungu waziwazi, lakini wao wamemwamini Mungu?.

Ni kwasababu YESU anathibitika kila mahali.

Mtu kutokuamini ni yeye mwenyewe kataka. Hakuna atakayekuwa na udhuru siku ya mwisho, kwasababu Yesu amefunuliwa kila mahali.

Swali ni je! umemwamini Kristo?  kama ni la! unasubiri nini. Mwamini leo kwa kuikubali kazi aliyoikamilisha juu yako ya kuondoa dhambi kwa kifo na kufufuka kwake. Ambayo hiyo huambatana na toba ya kweli na ubatizo.

Baada ya hapo utakuwa umepokea ondoleo la dhambi zako bure, mpokee Yesu sasa

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nawiwa na Wayunani na wasio Wayunani.

Utawanyiko wa Wayunani ulikuwaje?

ALIYOKUTANA NAYO YESU, YERIKO.

SAUTI NYUMA YA ISHARA.

Rudi Nyumbani

Print this post

USIFANYIKE KIFO KATIKATI YA NDOA YA MWINGINE.

Maandiko yanaonyesha kuwa kitu pekee cha asili kinachoweza kutenganisha watu wawili walio katika Ndoa ni KIFO.

Warumi 7:2 “Kwa maana mwanamke aliye na mume amefungwa na sheria kwa yule mume wakati anapokuwa yu hai; bali akifa yule mume, amefunguliwa ile sheria ya mume.

3  Basi wakati awapo hai mumewe, kama akiwa na mume mwingine huitwa mzinzi. Ila mumewe akifa, amekuwa huru, hafungwi na sheria hiyo, hata yeye si mzinzi, ajapoolewa na mume mwingine.”

Lakini inapotokea Mtu anachukua nafasi ya KIFO, yaani anaivunja ndoa yake mwenyewe au ya Mtu mwingine iliyo ya Halali, basi mtu huyo kibiblia ni MFU, au jina lake lingine ni KIFO/MAUTI..Sasa utauliza KIFO kinaweza kuwa MTU jibu ni Ndio!.

Ufunuo 6:8 “Nikaona, na tazama, farasi wa rangi ya kijivujivu, na yeye aliyempanda JINA LAKE NI MAUTI, na Kuzimu akafuatana naye…”

Kwahiyo Mtu anayechukua nafasi ya KIFO, katika ndoa yake mwenyewe au ya mwingine, huyo jina lake ni MAUTI kibiblia, awe mwanamke au mwanaume, huyo ni MAUTI, ni Mfu anayetembea.

Utauliza ni wapi tena katika maandiko, panaonyesha mtu aliyeharibu ndoa ya mwingine aliitwa MFU?

Mwanzo 20:2 “Ibrahimu akamnena Sara mkewe, Huyu ni ndugu yangu. Basi Abimeleki mfalme wa Gerari akapeleka watu akamtwaa Sara.

3 Lakini Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto ya usiku, akamwambia, UMEKUWA MFU WEWE kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemtwaa, maana ni mkewe mtu”.

Umeona hapo?.. MUNGU anamwambia Abimeleki kuwa yeye ni MFU kwa kitendo tu cha kumchukua mke wa Ibrahimu.

Hebu jiulize hapo kwanini Mungu hajamwambia  Mfalme Abimeliki kuwa umekuwa Najisi, au umekuwa Mjinga, au umekuwa Mpumbavu.. badala yake anamwambia amekuwa MFU!!!.. Maana yake pale alipo alikuwa ni Marehemu anayeishi.. Siku yoyote anashuka kaburini, na kila atakachojihusisha nacho kitakufa pia.

Hiyo pia ni hali ya Mtu anayeharibu ndoa yake mwenyewe au ya mwingine, kiroho jina lake ni MFU/MAUTI.

Na kumbuka maandiko yanasema Mauti anafuatana na Kuzimu.. Ufunuo 6:8 “Nikaona, na tazama, farasi wa rangi ya kijivujivu, na yeye aliyempanda JINA LAKE NI MAUTI, na Kuzimu akafuatana naye…”

Maana yake huyu mtu anayeitwa MAUTI, anakwenda sambamba na kuzimu, na mwisho ni ZIWA LA MOTO.

Ufunuo 20:14 “Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto”.

Je Mke au Mume uliye naye ni wako? Au wa mtu mwingine?… Unajua ni maumivu gani unayasababisha kwa mwingine unapomchukua Mke wake au Mume wake??..

Labda ulimchukua pasipo kujua maandiko au enzi bado hujaokoka, lakini sasa umejua …Mrudishe huyo mwanamke/mwanamume kwa aliyewake  wake hata kama una watoto naye, (weka naye tu mipango ya namna ya kuwatunza watoto), lakini usiendelee kuishi naye kwani unafanya UZINZI,  mrudishe kwa mume wake/mke wake, akikataa Mwache aishi mwenyewe, wewe utakuwa umejifungua katika kifungo cha Mauti….Vunja agano na Mauti kwa namna hiyo…

Isaya 28:18 “Na agano lenu mliloagana na mauti litabatilika, tena mapatano yenu mliyopatana na kuzimu hayatasimama; pigo lifurikalo litakapopita, ndipo ninyi mtakapokanyagwa nalo”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

MATESO YA KUZIMU.

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)

NDOA NA IHESHIMIWE NA WATU WOTE.

Rudi Nyumbani

Print this post