Musa alizaliwa huko Misri, miaka mingi kidogo baada ya Yusufu mwana wa Yakobo kufariki. Wakati wa kuzaliwa kwake, mama yake alimhifadhi mtoni kutokana na hofu ya amri ya Mfalme juu ya kuuawa kwa wazaliwa wote wa jinsia ya kiume.
Jina la Baba yake Musa ni Amramu na Mama yake ni Yokebedi. (Hesabu 26:59).
Musa alikuwa na Kaka yake wa damu aliyeitwa Haruni waliokuwa wamepishana miaka 3, Haruni alikuwa mkubwa kwa Musa, na ndiye yule aliyekuja kuwa Kuhani Mkuu, pia alikuwa na dada yake aliyeitwa Miriamu ambaye naye pia alikuwa ni Nabii wa Bwana.
Bithiani aliyekuwa Binti wa Farao alimwokota akiwa kwenye kijisafina kidogo, pembezoni mwa mto wakati akiwa anaoga. Musa aliishi katika Nyumba ya kifalme mpaka alipofikisha umri wa miaka 40, Baadaye aliasi nyumba ya Farao kutokana na kumsaidia mmoja wa ndugu zake wa Kiebrania, akakimbilia nchi ya Midiani. Huko alipata mke kutoka kwenye nyumba ya kuhani mmoja wa Midiani aliyeitwa Yethro.
Alikaa miaka 40 nyumbani kwa Yethro, akichunga mifugo yake, mpaka siku moja Bwana alipomtokea katika mwali wa moto, ndani ya kile kijiti, alipokuwa anachunga kundi la Yethro, Alipewa maagizo ya kuwaokoa Israeli waliokuwa wanateswa chini ya utawala mkali wa Farao.
Kwa Ishara nyingi na miujiza mingi Musa aliwaongoza wana wa Israeli miaka 40 mingine, na Alifariki akiwa na miaka 120, akiwa na nguvu zake zote. Macho yake hayakupofuka wala mwili haukupungua nguvu (Kumbukumbu 34:7)
Musa pekee ndiye Nabii aliyezungumza na Mungu uso kwa uso, wala baada yake hakuinuka nabii mfano wake yeye (Kumbukumbu 34:10-12)
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
1.Utaji uliokuwepo juu ya uso wa Musa ulikuwa unaashiria nini?
SWALI: Katika ule mlima mrefu, aliopanda Yesu na wanafunzi wake kuomba, kwanini atokewe na Musa na Eliya na sio manabii wengine? Mfano wa Isaya au Samweli?
JIBU: Awali ya yote yeye kutokewa na wale watu halikuwa Kwa lengo lake. Bali Kwa lengo la wale wanafunzi aliokuwa nao, Ili kutimizi mambo yafuatayo.
a) Unabii wa kwanza ni ule alioutoa Musa kuwa atakuja Nabii mwingine kama yeye na kwamba watu wamsikilize..
Kumbukumbu la Torati 18:15
[15]BWANA, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye.
Soma pia Matendo 3:22-25,. Hivyo wayahudi walikuwa na matarajio ya kuona mtu anayefanana na Musa atakayeleta Sheria mpya akija duniani, lakini akiwa na nguvu na uweza mwingi mfano wa Musa..
Ndio sababu ya Musa kutokea mbele ya wanafunzi wake, ili Mungu awathibitishie huyu ndio yule Musa aliyemnenea habari zake.
b) Lakini pia unabii uliohusu kutangulia Kwa Eliya kabla ya Kuja kwake duniani.
Wanafunzi walikuwa na dukuduku kama huyu, ndiye Kristo aliyetabiriwa au sio, na kama ndio mbona Eliya hajatangulia mbele yake tukamwona? Kwasababu waliambiwa hivyo na waandishi. Lakini sasa walipomwona Eliya mwenyewe amesimama mbele ya Yesu wakaamini lakini bado hawakuelewa..Sasa walipokuwa wanashuka ndio wakapata nguvu ya kumuulizia hilo swali.. Na hili ndio likawa jibu lake.
Mathayo 17:9-13
[9]Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, Msimwambie mtu ye yote habari ya maono hayo, hata Mwana wa Adamu atakapofufuka katika wafu.
[10]Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, Basi kwa nini waandishi hunena ya kwamba imempasa Eliya kuja kwanza?
[11]Naye akajibu, akawaambia, Kweli Eliya yuaja kwanza, naye atatengeneza yote,
[12]ila nawaambia, ya kwamba Eliya amekwisha kuja, wasimtambue, lakini wakamtenda yote waliyotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu naye yuaenda kuteswa kwao.
[13]Ndipo wale wanafunzi walipofahamu ya kuwa amesema nao habari za Yohana Mbatizaji.
Utakumbuka kabla ya kupanda mlimani aliwaliza watu kuwa wanamzungumzia kuwa yeye ni nani? Wanafunzi wakamjibu kuwa wanasema yeye ni Eliya, wengine mmojawapo wa manabii wa Kale.n.k. Hivyo kulikuwa na utata mwingi. Lakini siku hiyo alitoa utata huo Soma.Mathayo 16:13-18.
Mitume walipoona sura za manabii wao wa kale wamesimama mbele ya Yesu, mwenye utukufu mwingi sana kupitia wao. Wakaamini yeye ni zaidi ya manabii wote wakubwa Kwa wadogo waliowahi kutokea katika historia.
Musa alikufa, lakini Eliya alipaa.
Yesu ndio mtu pekee miongoni mwa wanadamu, aliyekufa, Kisha akazikwa, kisha akafufuka.na mwisho akapaa. Kwa hiyo Ile ilikuwa ni lugha ya kinabii, kueleza hatma yake na ndio maana hata manabii Hao walikuwa wakizungumza mambo yahusuyo kufa kwake na kufufuka.(Luka 9:31).
Hizo ndio zilikuwa sababu kuu za Bwana kutokewa na manabii wale wawili na sio wengine. Na walipokuwa wanashuka Akawaambia wanafunzi wake wasimwambie mtu mpaka atakapofufuka katika wafu.
Kufunua nini?
SI wote watamwona Yesu katika kilele Cha utukufu wake, isipokuwa wale tu walio na kiu na yeye. Ambao watakuwa tayari kuwa karibu naye wakati wote mfano wa Hawa wanafunzi watatu yaani Yohana, Petro na Yakobo.
Ukimpenda Yesu tumia muda mwingi kuwepo uweponi mwake. Utamjua sana Kwa mapana na marefu yake.
Je! Umeokoka? Je unatambua kuwa hizi ni siku za mwisho na Kristo yupo mlangoni kurudi? Dalili zote zimeshatimia, unasubiri nini usimpe Bwana maisha yako, embu fanya uamuzi leo. Tubu dhambi zako, mgeukie Yesu, Unyakuo usikupite. Ikiwa utapenda upate mwongozo huo, wasiliana nasi kwa namba zetu hizi bure +255693036618 /+255789001312
Shalom
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.
Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?
Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?
Je! Umeona asali? Kula kadiri ya kukutosha;
KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.
Swali: Katika kitabu cha Mathayo 17:4 Mtume Petro na wenzie waliwezaje kufahamu kuwa wale ni Musa na Eliya?
Jibu: Turejee habari hiyo kuanzia ule mstari wa kwanza..
Mathayo 17:1 “Na baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani;
2 akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang’aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru.
3 Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.
4 Petro akajibu akamwambia Yesu, Bwana, ni vizuri sisi kuwapo hapa; ukitaka, nitafanya hapa vibanda vitatu, kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya”.
Biblia haijaeleza kama Musa na Eliya walijitambulisha katika maono yale, ikiwa na maana kuwa kuna njia nyingine iliyowafanya Petro na wenzie kujua kuwa wale ni manabii Musa na Eliya na si wengine.
Sasa njia Pekee iliyomfanya Petro na wenzie kufahamu kuwa wale walikuwa ni Musa na Eliya na si wengine, ni UFUNUO WA ROHO MTAKATIFU.
Kama vile ufunuo wa Roho Mtakatifu ulivyomjia Petro kumhusu YESU.
Mathayo 16.15 “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”.
Umeona hapo?, aliyemwambia Petro kuwa YESU ni KRISTO tena ni MWANA WA MUNGU aliye juu sio YESU mwenyewe!, bali ni ufunuo wa alioupokea kutoka kwa Baba.
Na hiyo sio ajabu kwani walikuwa wameenda mlimani kuomba.. ni kawaida kwa watumishi wa MUNGU kupokea mafunuo ya mambo yaliyopo, au yajayo wanapokuwa katika maombi, hususani kama hayo ya mlimani.
Kwahiyo Mtume Petro na wenzie walipata ufunuo wa ujio au uwepo wa manabii hao wawili wakiwa katika maombi, utaona jambo kama hilo lilishatokea tena kwa Petro wakati yupo kwa Yule Simoni mtengenezaji wa ngozi wa kule Yafa, wakati ambapo Roho Mtakatifu alimfunulia alipokuwa katika maombi kuwa kuna watu watatu wanamwulizia, hivyo aende nao asiogope!, na kweli ikawa hivyo..
Matendo 10:17 “Hata Petro alipokuwa akiona shaka ndani ya nafsi yake, maana yake ni nini maono hayo aliyoyaona, wale watu waliotumwa na Kornelio, wakiisha kuiulizia nyumba ya Simoni, wakasimama mbele ya mlango,
18 wakaita; wakauliza kwamba Simoni aitwaye Petro anakaa humo.
19 Na Petro alikuwa akiyafikiri yale maono. Roho akamwambia, Wako watu watatu wanakutafuta.
20 Basi ondoka ushuke ufuatane nao, usione tashwishi, kwa maana ni mimi niliyewatuma.
21 Petro akawashukia wale watu, akanena, Mimi ndiye mnayemtafuta. Mmekuja kwa sababu gani?”
Kwa namna hiyo hiyo, huenda Petro na wenzake walipokea ufunuo kuwa wale ni Musa na Eliya, labda walipokea ufunuo huo muda mchache kabla hawajawatokea, au wakati ule ule walipotokea.
Kikubwa tunachoweza kujifunza ni kuwa tuwapo katika uwepo wa MUNGU kama katika maombi, ni rahisi kupokea ufunuo wa Roho Mtakatifu kwani tunakuwa tupo katika roho, na mtu anapokuwa katika roho anayatambua mambo yote ya rohoni pasipo kuambiwa!
Hivyo ni muhimu sana kuwa waombaji, na wasomaji wa Neno la MUNGU, endapo akina Petro wangekuwa si watu wa kusoma maandiko, ni dhahiri kuwa wasingemjua Musa wala Eliya na hiyo ingezuia Roho kuwafunulia watu hao, kwani Roho Mtakatifu anamfunulia mtu kitu ambacho kinahusiana na Neno la MUNGU.
Je na wewe ni mtu wa kudumu uweponi mwa MUNGU? Je KRISTO YESU?..Je unao uhakika kwamba akirudi unaenda naye?
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini Eliya afunge Mbingu miaka mitatu na nusu? (1Wafalme 17:1)
TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?
Je! Tutatambuana tukifika mbinguni?
Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?
Swali: Inakuwaje manabii wa uongo wanakuwa na uwezo wa kutoa pepo kwa jina la YESU?, na ilihali hawana mahusiano na Mungu wa kweli? je ni nguvu gani wanazitumia? Za Mungu au shetani?.
Jibu: Zipo aina mbili za manabii wa uongo. Aina ya kwanza ni ile inayotumia nguvu za giza asilimia mia moja (100%), kundi hili halihusishi kabisa jina la YESU katika huduma zake, wala halimhubiri YESU wa kweli bali shetani.
Hawa wanakuwa ni wachawi waliovaa suti na kushika biblia, na Neno la MUNGU linasema tutawatambua kwa matunda yao, na si mwonekano wao wa nje.
Kundi la Pili: la manabii wa Uongo, ni wale ambao sio wachawi lakini halina mahusiano na MUNGU, maana yake aidha wanamtumikia MUNGU kwa faida za matumbo yao, au walishamwacha MUNGU na kufuata akili zao, kundi hili ndio hatari zaidi kwasababu bado linaweza kutumia jina la YESU na miujiza ikatendeka.
Mtu anakuwa kashapoteza mahusiano na MUNGU lakini bado upako anao!.. utauliza hilo linawezekanaje?.. Mkumbuke MUSA!.. Bwana MUNGU alimwambia auambie mwamba utoe maji, lakini yeye pamoja na ndugu yake Haruni, hawakumsikiliza MUNGU wakaenda kufanya kinyume na walivyoagizwa, na jambo la ajabu ni kwamba ijapokuwa walikuwa wameenda kinyume na agizo la MUNGU (wapo nje na mpango wa Mungu) lakini walipouchapa mwamba ulitoa maji, binafsi ningetegemea maji yasitoke mwambani kwasababu walikuwa nje na agizo la MUNGU, lakini haikuwa hivyo.
Hesabu 20:6 “Musa na Haruni wakatoka pale palipokuwa mkutano, wakaenda hata mlangoni pa hema ya kukutania, wakaanguka kifudifudi; utukufu wa Bwana ukawatokea.
7 Bwana akasema na Musa, akinena,
8 Twaa ile fimbo, ukawakusanye mkutano, wewe na Haruni ndugu yako, ukauambie mwamba mbele ya macho yao utoe maji yake, nawe utawatokezea maji katika mwamba, na hivyo utawanywesha maji mkutano na wanyama wao.
9 Musa akaitwaa hiyo fimbo kutoka mbele za Bwana kama alivyomwamuru.
10 Musa na Haruni wakawakusanya kusanyiko mbele ya mwamba, akawaambia, Sikieni sasa, enyi waasi; je! Tuwatokezee maji katika mwamba huu?
11 Musa akainua mkono wake akaupiga ule mwamba kwa fimbo yake mara mbili; maji yakatoka mengi, mkutano wakanywa na wanyama wao pia.
12 Bwana akamwambia Musa na Haruni, Kwa kuwa hamkuniamini mimi, ili kunistahi mbele ya macho ya wana wa Israeli, basi kwa sababu hiyo, hamtawaingiza kusanyiko hili katika ile nchi niliyowapa”.
Umeona hapo?.. ijapokuwa Musa alikuwa anatembea nje ya agizo la MUNGU, lakini bado upako alikuwa nao, na manabii wa uongo ni hivyo hivyo, wanaweza kuwa wanatembea na upako wa MUNGU wa kweli lakini hawana MUNGU maishani mwao, na mwisho wao ni mbaya…na hawa tumeambiwa tutawatambua kwa matunda yao na si upako wao, wala mwonekano wao.
Mfano mwingine ni Yule nabii mzee tunayemsoma katika biblia, aliyemwambia uongo nabii mwenzake, na badala nguvu za MUNGU zimwondoke baada ya kusema kwake uongo, kinyume chake ndio kwanza anapokea unabii mwingine kumhusu mwenzie. Soma habari hiyo katika 1Wafalme 12:11-30.
Ikifunua kuwa unabii, au muujiza au upako mtu/mtumishi alionao sio kipimo cha kwanza cha kumtambua nabii/mtumishi wa Mungu wa kweli, bali ni mtu kuwa na mahusiano mazuri na MUNGU, kwani maandiko yanasema Yohana Mbatizaji hakufanya ishara wala muujiza hata mmoja lakini mbinguni alihesabika kuwa mkuu kuliko manabii wote na watu wote wa agano la kale (Yohana 10:41 na Mathayo 11:11).
Na tena Bwana YESU alisema wengi watakuja siku ile wakisema, hatukutoa pepo na kufanya unabii kwa jina lako?.. na yeye atasema siwajui mtokako! (Mathayo 7:21-22).
Ili kumtambua kuwa huyu ni Nabii wa kweli na si wa uongo, ni matunda anayoyatoa.. Maana yake Matunda ya maisha yake, na matunda ya kazi yake.
Matunda ya maisha yake ni jinsi anavyoishi, je anazaa matunda ya Roho mtakatifu tunayoyasoma katika Wagalatia 5:22?.. au ni mtu wa namna gani?..kama maisha yake si kulingana na Neno la MUNGU bali ni mtenda dhambi, basi huyo hata kama anauwezo wa kusimamisha jua, bado hatupaswi kudanganyika kwake.
Vile vile kama matunda anayoyazaa kutokana na kazi yake (maana yake watu anao wahubiria) hawawi wasafi mwilini na rohoni, hiyo ni ishara nyingine ya kumtambua nabii huyo kuwa si wa MUNGU. Kwani kama watu anaowatengeneza hawana tofauti na wa ulimwengu, maana yake matunda yake si matunda ya kiMungu bali ya adui.
Hiyo ndio namna pekee ya kuwapima manabii au wachungaji au waalimu au mitume wa kweli na wale wa uongo, na tunapowafahamu biblia imetuonya tujihadhari nao.
Mathayo 7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? 17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.
18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.
19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.
20 Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.
21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Ni mji gani mtakatifu shetani aliomchukua Bwana YESU? (Mathayo 4:5)
SADAKA INAHARIBU NGUVU ZA MADHABAHU ZA MASHETANI.
SADAKA INAHARIBU NGUVU ZA MADHABAHU ZA MASHETANI.
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Kwanini Nabii Musa amtake Hobabu (shemeji yake) kama dira yake ya kuelekea Kaanani na tayari Mungu alishawafunulia juu yao nguzo ya wingu wakati wa mchana na Nguzo ya moto wakati wa usiku kama dira yao na kama kitu cha kuwaongozea?
Jibu: Lipo jambo kubwa sana hapa la kujifunza..
Awali ya yote kama bado hujamfahamu Hobabu ni nani na inakuwaje awe shemeji yake Musa fungua hapa >>>Huyu Mkeni shemeji yake Musa alikuwa ni mtu wa namna gani? (Waamuzi 1:16)
Sasa kwa muhtasari ni kwamba kipindi wana wana wa Israeli wanatoka Misri kuelekea Kaanani, ni kweli Bwana aliwapa wingu na nguzo ya moto iwaongoze mchana na usiku.
Lakini Zaidi ya hayo Musa alitafuta tena mtu ambaye atamwongoza njia yao kuelekea nchi ya ahadi.. sasa swali ni alifanya makosa?… na tena akataka kumfanya kama “Macho” katika safari hiyo..
Waamuzi 10:28 “Ndivyo zilivyokuwa safari zao wana wa Israeli kwa majeshi: yao; nao wakasafiri kwenda mbele.
29 Kisha Musa akamwambia Hobabu, mwana wa Reueli Mmidiani, mkwewe Musa, Sisi twasafiri kwenenda mahali ambapo Bwana amenena habari zake hivi, Nitawapa ninyi mahali hapo; uje pamoja nasi, nasi tutakufanyia mema; kwa kuwa Bwana ametamka mema juu ya Israeli.
30 Naye akamwambia, Siendi mimi; ila nitairudia nchi yangu mwenyewe, na kwa jamaa zangu mwenyewe.
31 NAYE AKAMWAMBIA, USITUACHE, TAFADHALI; KWA KUWA WEWE WAJUA JINSI TUTAKAVYOPANGA NYIKANI, NAWE UTAKUWA KWETU BADALA YA MACHO.
32 Itakuwa, ukienda pamoja nasi, naam, itakuwa mema yo yote Bwana atakayotutendea sisi, tutakutendea wewe vivyo
34 NA WINGU LA BWANA LILIKUWA JUU YAO MCHANA HAPO WALIPOSAFIRI KWENDA MBELE KUTOKA KAMBINI.
35 Ilikuwa, hapo sanduku liliposafiri kwenda mbele, ndipo Musa akasema, Inuka, Ee Bwana, adui zako na watawanyike; na wakimbie mbele zako hao wakuchukiao”.
Jibu ni La!.. Musa hakuwa Mjinga, wala hakuwa mtu wa kumtegemea Mwanadamu.. Daima alijua Mungu ndiye Ngao yake na watu wake, na wala hakuna mtu yeyote awezaye kumsaidia kazi. Lakini Nabii Musa alifikiri Zaidi, Alijua watu aliona ni watu wenye mioyo migumu, na shingo ngumu.
Alijua Imani yao kwa Mungu ilikuwa ni ndogo, na wengi wao ni watu wa mwilini, na alijua wasipopata mtu wa kuwapanga vyema kule nyikani, aliyemzoefu wa jangwa na njia, zitanyanyuka shida nyingi na hatimaye watamkufuru Mungu na kuadhibiwa wote.
Hivyo kwa faida ya watu wasiangamia aliwatafutia mwalimu wa mwilini ili awaongoze, na kuwafundisha jinsi ya kukaa jangwani, na hiyo ikawa dawa kwa sehemu kubwa sana.
Na utaona hii familia ya Yethro (babamkwe wake Musa na mashemeji zake), ilikuwa msaada mkubwa sana kiushauri katika safari ya wana wa Israeli jangwani na kwa Musa kwa ujumla. Kwani kipindi ambacho Musa alikuwa anawaamua watu wote peke yake kuanzia asubuhi mpaka jioni, alipokuja huyu babamkwe wake alimpa ushauri bora sana wa kuweka wakuu wa maelfu, wakuu wa mahamsini na wakuu wa mamia na wakuu wa makumi (Soma Kutoka 18:12-27).
NINI TUNAJIFUNZA KWA MUSA:
Musa alikuwa na “Macho juu” ambaye ni Roho Mtakatifu juu (kama wingu likimwongoza na watu wake) lakini pia alikuwa na “macho chini” (Hobabu, shemeji yake) kwaajili ya watu wake. Mambo haya yanaenda pamoja..
Wewe kwama Mzazi, unaye Roho Mtakatifu anayekuongoza wewe na familia yako kama Macho ya Juu, lakini hayo hayatoshi pekee, ni lazima watoto wako uwapatie waalimu watakaowafundisha njia za Roho Mtakatifu katika mashule yao waliopo, katika makanisa yao, katika shughuli zao n.k
Ukisema utawaacha na kuongozwa na Roho Mtakatifu kama wewe uongozwavyo, utawapoteza…wawekee waalimu.
Vilevile Mtumishi wa Mungu weka waalimu kwa watoto wako wa kiroho, weka wachungaji watakaowaangalia, itakuwa afya na heri kwao.
Bwana atusaidie
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
KAZI ZA ROHO MTAKATIFU
Je Musa kumwoa Sipora, Mkushi alifanya dhambi?
Jibu: Tusome,
Waefeso 2:20 “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni”
Hapo maandiko yanasema tumejengwa juu ya “Msingi wa Mitume na Manabii “na si juu ya “Mitume na Manabii” .. Na pia inasema tumejengwa juu ya “Msingi” na si juu ya Misingi ya mitume na manabii. Ikiwa na maana kuwa Msingi ni mmoja tu, ambao tumejegwa juu yake, (mbele kidogo tutakuja kuuona huo msingi ni nini).
Sasa yapo maswali mawili hapo ya kujiuliza; 1) Hawa Mitume na Manabii ni akina nani na 2) Huo msingi ni nini?
1) Mitume na Manabii:
Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapa katika Waefeso 2:20 sio hawa waliopo sasa, Bali ni wale walioandika biblia, kama Musa, Yeremia, Hosea, Ezekieli na Malaki vile vile mitume wale 12 wa Bwana pamoja na wengine kama akina Paulo, ambao waliandika biblia.
Mtu yeyote aliyepo sasa, au atakayekuja kutokea na kujiita mtume au nabii, basi afahamu kuwa andiko hilo la Waefeso 2:20 halimhusu hata kidogo. Na shetani amewapandikiza watu wengi kiburi (watu wanaojulikana kama mitume na manabii wa leo), na kuanza kujivuna kuwa wao ndio Msingi wa kanisa.. Jambo ambalo si la kweli hata kidogo.
2) Msingi
Msingi ambao sisi tumejengwa juu yake ni ule waliokuwa nao Mitume, ikiwa na maana kuwa kile Mitume walichokifanya msingi, ndicho hicho hicho sisi (kanisa la Mungu) tunajengwa juu yake. Sasa ni kitu gani Mitume na Manabii wa kwenye biblia walikifanya msingi?… Hicho si kingine zaidi ya YESU KRISTO MWENYEWE!!!. Huyu ndiye Msingi wa kanisa na ndiye aliyekuwa msingi wa mitume, na ndio msingi wetu sisi na bado ataendelea kuwa msingi siku zote.
1Wakorintho 3:11 “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, YESU KRISTO”.
YESU KRISTO ndio Mwamba ule ambao yeye mwenyewe alisema kuwa kanisa lake litajengwa juu yake.
Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?
14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.
15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
16 Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.
18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”.
Umeona? Mwamba unaonenewa hapo sio Petro bali ni yeye YESU MWENYEWE!.. yaani huo Ufunuo Petro alioupata wa YESU KUWA MWANA WA MUNGU Ndio MSINGI, na NDIO MWAMBA ambao kanisa litajengwa juu yake.
Kanisa lolote leo ambao YESU sio kiini cha Imani hiyo, hilo sio kanisa la kweli, vile vile imani yoyote ile isiyomweka YESU kama msingi badala yake inawemweka mwanadamu mwingine au mnyama au sanamu basi imani hiyo ni imani ya Uongo n.k
Mahubiri yoyote yasiyomweka YESU msingi, hayo ni mahubiri kutoka kwa Yule adui.
Mtumishi yoyote Yule, awe mchungaji, mwalimu, mtume, nabii au mwinjilisti asiyemweka YESU kama kiini na kitovu cha Mafundisho huyo si wa kweli, kwa mujibu wa maandiko.
Vile vile mtu yeyote ajiitaye Mkristo na Yesu si msingi wa maisha yake, huyo ni mkristo jina tu wa uongo.
Bwana atusaidie tumweke Yesu msingi wa maisha yetu.
Maran atha!.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?
Nitamjuaje nabii wa Uongo?
Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?
Swali: Katika biblia tunasoma sehemu kadha wa kadha zikiwataja “wana wa manabii”.. Je! Hawa wana wa manabii walikuwa ni watu gani?, na kazi yao ilikuwa ni ipi? Na kwanini waliitwa hivyo?.. Na je hata leo kuna wana wa manabii?
Jibu: Ni kweli Katika Agano la kale lilikuwepo kundi la watu waliojulikana kama Wana wa Manabii. (Soma 1Wafalme 20:35, 2Wafalme 6:1, 2Wafalme 4:1, na 2Wafalme 2:5).
Watu hawa walikuwa ni “manabii wa Mungu”, ambao walijitia katika kifungo cha kujifunza juu ya Nabii zilizotangulia kabla yao..
Kumbuka sio kujifunza jinsi manabii wanavyoishi au wanavyokula au wanavyoona maono!… La! Hakuna mwanadamu yeyote anayeweza kumfundisha mtu mwingine namna ya kuona maono!…hivyo ni vipawa vya Mungu ambayo ni Mungu mwenyewe anaviweka ndani ya mtu, na hatujifunzi wala hatufundishwi.. Ni sawa na ndoto…
Hakuna mtu anayeweza kumfundisha mwenzake jinsi ya kuota!.. Ndoto zinakuja zenyewe, kwasababu ni vipawa vya asili ambavyo Mungu kaviweka kwetu sote.. Na nabii za Mungu, zinawajia watu maalumu ambao Bwana kawachagua, na si kupitia kujifunza!.
Kwahiyo hawa wana wa manabii, au kwa lugha nyingine “Wanafunzi wa manabii” walikuwa ni watu waliojikita kujifunza Nyakati na Majira, Pamoja na Nabii zilizotangulia kutolewa na manabii wengine waliowatangulia..(kumbuka walikuwa wanajulikana kama wana wa manabii, na sio wana wa NABII!)..
Na lengo la kufanya hivyo (yaani kupokea maarifa hayo) ni ili wawe salama, na wawe na uhakika wa Nabii watakazozitoa isije wakapotoka na kutoa unabii wa uongo.
Kwa mfano Nabii anaweza kuona maono au kupata ujumbe kuhusu Taifa la Israeli, sasa ili authibitishe ujumbe ule au ono lile kama kweli ni kutoka kwa Bwana, ni sharti awe na Nabii nyingine za kutosha, za waliomtangulia zinazosapoti ono lake hilo jipya!.. Na akija kugundua kuwa Nabii mwingine, mkuu aliyetangulia alishatabiri jambo kama hilo au linalokaribiana na hilo… basi ndipo Ono lake hilo linathibitika… lakini akija kukuta ono lake linakinzana na maono ambayo manabii wakuu waliyatoa, ndipo analiacha, kwasababu sio kutoka kwa Bwana… (kwasababu kamwe Bwana hawezi kujipinga katika maneno yake).
Hivyo ndio maana ilihitajika shule ya manabii, ambayo lengo lake ni kujifunza kujua Nabii zilizotangulia juu ya watu, na mataifa…
Ili tuzidi kuelewa vizuri, utakumbuka kipindi cha Nabii Yeremia wakati anatabiri kwamba Israeli watachukuliwa utumwani kwenda Babeli.. utaona Yeremia alikuwa ni mtu mwenye elimu ya kutosha kuhusu Nabii zilizotangulia, alihakiki jumbe anazozipokea katika maono, kwa nabii za waliomtangulia kama wakina Isaya, na wengineo..
Na jambo moja utaona alilojifunza ni kuwa “Manabii karibia wote, hawakuwahi kutabiri juu ya amani kwa mataifa, manabii wengi walikuwa wanatabiri juu ya Vita na Mabaya na Tauni”.. Na Yeremia alijua Mungu hawezi kujipinga.. Hivyo maono yake aliyahakiki kwa namna hiyo..
Lakini utaona alitokea mtu anaitwa Hanania, ambaye alijitokeza na kuanza kutabiri juu ya Amani kwa Israeli kwamba hawataenda utumwani, watakuwa salama, ni ilihali Taifa zima limemwacha Mungu..jambo ambalo linakinzana na Nabii Mungu alizozitoa kupitia manabii wakuu waliotangulia… Na Yeremia kuliona hilo akamwambia Hanania maneno yafuatayo…
Yeremia 28:7 “Lakini lisikilize sasa neno hili nilisemalo, masikioni mwako, na masikioni mwa watu wote,
8 MANABII WALIOKUWAKO KABLA YA ZAMANI ZANGU, NA ZAMANI ZAKO, WALITABIRI JUU YA NCHI NYINGI, NA JUU YA FALME KUBWA, HABARI YA VITA, NA YA MABAYA, NA YA TAUNI”.
Umeona jambo Yeremia alilomwambia huyu Hanania?…
Yeremia alikuwa ni Mwana wa manabii, lakini Hanania alikuwa ni mtu tu aliyejizukia na kujiita Nabii, hana elimu yoyote ya Nabii za Mungu.. na akaanza kuwafariji watu kwa maneno ya uongo!..Jambo ambalo lilimchukiza sana Mungu, na hata kumwua Hanania.
Yeremia 28:15 “Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, Sikia sasa, Ee Hanania; Bwana hakukutuma; lakini unawatumainisha watu hawa maneno ya uongo.
16 BASI BWANA ASEMA HIVI, TAZAMA, NAKUTUMA UENDE ZAKO TOKA JUU YA USO WA NCHI; MWAKA HUU UTAKUFA, KWA SABABU UMENENA MANENO YA UASI JUU YA BWANA.
17 BASI NABII HANANIA AKAFA, MWAKA UO HUO, MWEZI WA SABA”.
Lakini leo hii shetani kaligeuza hili Neno “Wana wa Manabii”. Leo hii kuna watu wamefungua vyuo vyao, wakiwa wenyewe wanajiita Manabii wakuu, na vijana wao wanawaita “wana wao (yaani wana wa manabii)”.. Lakini ukiingia katika madara yao na kusikia wanachofundishwa, ni huzuni tupu!.
Utasikia wanachofundishwa ni jinsi ya kuona maono, jinsi ya kutumia na kutengeneza mafuta na chumvi na mengineyo, utaona wanafundishwa mtindo wa maisha na mtindo wa kuongea, na kuvaa kama nabii mkuu wao, na jinsi ya kumwogopa na kumtukuza baba yao, nabii mkuu..
Na watasomea hata miaka 5 na wakitoka hapo wanapewa na vyeti, tayari wakufunzi!!!..
Ndugu! Huo ni uongo wa shetani…
Wana wa manabii katika Agano la kale, hawakufundishwa wala hawakuwa wanajifunza mitindo ya kuongea ya manabii waliowatangulia…wala walikuwa hawajifunzi jinsi ya kuona maono! (kwasababu tayari walikuwa na hiyo karama, ndio maana wakaitwa manabii)..Walichokuwa wanajifunza ni Nabii zilizotangulia zinazohusu wakati waliopo wao, na za mataifa mengine, kuanzia zilizoandikwa katika Torati ya Nabii Musa, mpaka wakati waliopo wao, ili kusudi wasije wakapotoka na maono waliyokuwa wanayapokea.
Na sisi leo hii wote ni wana wa Manabii.. ambao manabii wetu si baba zetu wa kiroho!!! Wala si maaskofu wetu, bali ni MITUME WA KWENYE BIBLIA, na MANABII WA KWENYE BIBLIA!!!...Tunatembea katika Nabii walizozitoa hao, wakina Musa, Isaya, Yeremia, Habakuki, na mitume wakina Petro, Yohana, Paulo n.k.. (Na nabii zao hazijawahi kukinzana),Kwasababu walikuwa na Roho mmoja.
Kwamfano Nabii Isaya alitoa unabii ufuatao..
Isaya 13:6 “Pigeni kelele za hofu; maana siku ya Bwana i karibu; itanyesha kama maangamizi yatokayo kwa Mwenyezi Mungu”.
Nabii Yoeli naye alitoa unabii kama huo huo katika Yoeli 3:14, na manabii wengine wote walitabiri hayo hayo…
Kwahiyo ili sisi tuhesabike kuwa “Wana wa manabii” ni lazima maono yetu tunayoyaona katika ndoto, au kwa wazi, ni lazima yapatane na huo unabii wa Isaya, na Yoeli na wengineo katika biblia!… usipopatana na huo unabii wa Isaya basi hilo Ono au huo Unabii ni wa UONGO!!! Ni kutoka Kuzimu!!!...
Tukiota au tukiona maono ambayo yanatuonyesha au kutuambia kuwa “Tufurahi, tupige kelele za shangwe, kwasababu siku ya Bwana bado sana”..basi hilo ni Ono kutoka kuzimu!!!..
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba wana wa manabii, ni manabii ambao walikuwa wamejikita katika kusoma Nabii za manabii wa Mungu waliowatangulia, ili wasifanye makosa katika kutoa nabii zao.
Na sisi ni lazima tuwe wanafunzi wa biblia, turejee biblia katika kuhakiki kila kitu, na hatupaswi kuamini tu kila jambo ambalo tunalipokea katika ndoto au maono.
Bwana Yesu na atusaidie sana.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.
Nini maana ya “Torati na manabii”?
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze maneno ya Uzima wa Mungu wetu..
Yapo maswali kadhaa ambayo tunaweza kujiuliza, juu ya tukio la Bwana Yesu kutokewa na Musa na Eliya siku ile alipopanda mlimani kuomba pamoja na wale wanafunzi wake watatu (Petro, Yohana na Yakobo)..
Na maswali yenyewe ni haya..
1) Iweje Bwana Yesu atokewe na Musa ambaye tayari alishakufa miaka mingi?, na Zaidi ya yote maandiko yanasema alizikwa, tena na Mungu mwenyewe?..
2) Kwanini Musa na Eliya wamtokee?.. kulikuwa na umuhimu gani wa wao kumtokea Bwana?
Sasa ili tupate majibu ya maswali hayo vizuri, Labda tusome habari yenyewe kwa ufupi kisha tuendelee
Luka 9:28 “Baada ya maneno hayo yapata siku nane, aliwatwaa Petro na Yohana na Yakobo, akapanda mlimani ili kuomba.
29 Ikawa katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka, mavazi yake yakawa meupe, yakimeta-meta.
30 Na tazama, watu wawili walikuwa wakizungumza naye, nao ni MUSA NA ELIYA;
31 walioonekana katika utukufu, WAKANENA HABARI ZA KUFARIKI KWAKE ATAKAKOTIMIZA YERUSALEMU”
Kiini cha majibu ya maswali yetu tutakipata katika huu mstari wa 31.. “walioonekana katika utukufu, WAKANENA HABARI ZA KUFARIKI KWAKE ATAKAKOTIMIZA YERUSALEMU”
Kumbe Sababu ya Musa na Eliya kumtokea Bwana, ilikuwa ni kuzungumza kuhusu Kufa kwake Bwana Yesu, ambako atakutimiza Yerusalemu.
Sasa swali linakuja?, je ni kwamba Bwana Yesu alikuwa hajui kwamba atakwenda kufa mpaka atokewe na watu hao wawili, wamweleze kuhusu kufa kwake?.. Jibu ni la!.. alikuwa anajua, lakini zipo siri nyingine zihusuzo kufa kwake na kufufuka kwake na kupaa kwake, ambazo hizo Baba alimfunulia siku hiyo kupitia manabii hao wawili.
Kumbuka kabla ya Kristo kufa, roho za watakatifu zilikuwa chini, na shetani alikuwa na uwezo wa kuzileta juu, kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka lile tukio la Samweli kuletwa juu ya yule mwanamke mwenye pepo la utambuzi, na baada ya kuletwa juu, Samweli aliweza kutoa unabii wa mambo yajayo, ijapokuwa alikuwa ameshakufa na kuzikwa, kwani tunasoma, alimtolewa Unabii Mfalme Sauli kuhusu KUFA KWAKWE, AMBAKO KUTAKWENDA KUTIMIA KIPINDI SI KIREFU KUTOKA PALE. Unaweza kusoma Habari hiyo kwa urefu katika kitabu cha 1Samweli 28:1-19.
Sasa Biblia haijaeleza Musa alikuwa anamweleza nini Bwana Yesu, lakini tunajua kabisa ni kuhusu Habari za kufunguliwa kwao wafu, na kwamba Bwana Yesu atakwenda kusulibiwa na kushuka sehemu ya wafu wao (akina Musa na wengine walipo na kuwaweka huru, na kwamba siku ya tatu atafufuka).
Kwahiyo kumbe kabla ya Bwana Yesu kufa, Wafu waliendelea kuishi, na pia iliwezekana kuwaleta baadhi yao juu na kutoa unabii, kwa njia yoyote ile!..
Kwasababu hiyo basi tumeshapata jibu ni kwanini MUSA, aliletwa juu na Mungu, ili kutoa unabii (Habari za kufa kwake Bwana Yesu, ijapokuwa Musa alikuwa ameshakufa kitambo na kuzikwa)…Ni kama tu vile, Nabii Samweli alivyoletwa juu na yule mwanamke mwenye pepo la utambuzi. (Kumbuka jambo hilo liliwezekana tu kipindi kabla ya Bwana Yesu kufa, lakini baada ya Bwana Yesu kufa na kufufuka, hakuna mchawi yeyote anayeweza kumleta juu mtu aliyekufa, kwasababu Kristo alizichukua funguo za Mauti na kuzimu).
Hapo tumepata jibu kuhusu Musa, sasa vipi kuhusu ELIYA?
Tunajua kabisa Eliya hakufa, bali alipaa..Maana yake Eliya anayajua yaliyo ya Mbinguni.. kama Nabii, Bwana alimtoa huko na kuja kumpasha Habari Bwana Yesu, kuhusu kupaa kwake, na enzi na mamlaka zinazomngojea Mbinguni (labda na siku hiyo alimpa na tarehe ya kupaa kwake, hatujui).
Kwasababu ijapokuwa Eliya alikuwa amepaa mbinguni, lakini bado alikuwa ni Nabii. Kwahiyo ujio wa Eliya ulikuwa ni wa muhimu sana kwa Bwana, kupata taarifa kuhusu kupaa kwake.
Kwahiyo kwaufupi ni kwamba Mungu aliwatumia manabii hawa wawili kama Manabii wa Ushahidi. Na Ushahidi huo ni wa KUFA kupitia Musa, na Kupaa kupitia ELIYA. Kwasababu Kristo naye atakufa kama Musa aliye nabii mkuu, na vile vile atapaa mbinguni kama ELIYA.
Kwahiyo baada ya tukio lile, Bwana Yesu alipokea Ufunuo mkuu kuhusu Mauti yake na kufufuka kwake, na kupaa kwake.. Zaidi sana na kurudi kwake kutakavyokuwa..ndio maana tunaona pia Uso wake uling’aa kama jua, kuashiria siku ya kurudi kwake kutakavyokuwa.
Na wakati ulipofika kweli Bwana Yesu, alikufa, akafufuka, na akapaa mbinguni.. imesalia hatua moja tu!.. nayo ni KURUDI KWAKE KUTUCHUKUA!..
Je! Umejiandaaje?.. Kama Nabii hizo mbili za kufa na kufufuka kwake na kupaa kwake zilitimia.. Basi hata kurudi kwake kutatimia. Na tupo katika majira ya kurudi kwake, dalili zote zimeshaonekana, muda wowote mambo yanakwisha, Kristo anakuja kuwachukua watakatifu wake, na kitakachokuwa kimesalia kwa wale watakaobaki ni majuto na dhiki kuu.
Je umejiandaaje? Je umemwamini Yesu na kutubu dhambi zako? Je umebatizwa katika ubatizo sahihi?…kama bado unangoja nini?.. Ukiikataa leo injili siku hiyo hutakuwa na la kujitetea. Mpokee Yesu leo, na ukabatizwe na kujazwa Roho Mtakatifu.
Bwana akubariki.
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?
Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?
Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;
SWALI: Tukisoma katika maandiko tunaona sehemu kadha wa kadha likitajwa neno “Torati na manabii”. Sasa hii torati na manabii maana yake ni nini? Kwamfano Mathayo 7:12 inasema
“Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii”.
JIBU: Bwana Yesu aliposema Torati na manabii, alimaanisha Agano la kale, ambalo ndio limeundwa na vitabu vya Musa (Torati), ambavyo ni vitano (5), Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na Kumbukumbu la Torati. Pamoja na vitabu vyote vya manabii, kama vile, Yeremia, Isaya, Danieli, Ezekieli, Hababuki, Amosi, n.k. hapa ikijumuisha pia, vile vingine kama Waamuzi, Zaburi, Ayubu, Wafalme, Mithali, Ruthu n.k. Ambavyo sio moja kwa moja vya manabii, lakini vimebeba nabii za Mungu ndani yake.
Kwahiyo torati na manabii kwa ufupi ni lile agano lote la kale. Hivyo Pale Bwana Yesu alipokuwa anawafundisha juu ya kanuni za kufuata, alirejea biblia yao, akiwaambia kuwa kiini cha biblia hiyo ni UPENDO. Wala hakuna siri nyingine nyuma yake, Torati yote, pamoja manabii wote, walichokuwa wanahubiri ni Upendo, (Ambao umegawanyika, wa Mungu na wanadamu)
Hata sisi wa leo tulio katika agano jipya, tunaposoma biblia yote tujue Ujumbe mkuu tunaoupata katika agano letu ni ule ule UPENDO. Na ndio maana Mtume Paulo alisema.
1Wakorintho 13:1 “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.
3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu”.
Hivyo na sisi, tunapaswa tuutafute huu, kwa bidii zote, ili tuonekane kuwa wakamilifu mbele za Mungu.
Shalom
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo: