Title NABII MUSA

NABII MUSA.

Musa alizaliwa huko Misri, miaka mingi kidogo baada ya Yusufu mwana wa Yakobo kufariki. Wakati wa kuzaliwa kwake, mama yake alimhifadhi mtoni kutokana na hofu ya amri ya Mfalme juu ya kuuawa kwa wazaliwa wote wa jinsia ya kiume.

Jina la Baba yake Musa ni Amramu na Mama yake ni Yokebedi. (Hesabu 26:59).

Musa alikuwa na Kaka yake wa damu aliyeitwa Haruni waliokuwa wamepishana miaka 3, Haruni alikuwa mkubwa kwa Musa, na ndiye yule aliyekuja kuwa Kuhani Mkuu, pia alikuwa na dada yake aliyeitwa Miriamu ambaye naye pia alikuwa ni Nabii wa Bwana.

Bithiani aliyekuwa Binti wa Farao alimwokota akiwa kwenye kijisafina kidogo, pembezoni mwa mto wakati akiwa anaoga. Musa aliishi katika Nyumba ya kifalme mpaka alipofikisha umri wa miaka 40, Baadaye aliasi nyumba ya Farao kutokana na kumsaidia mmoja wa ndugu zake wa Kiebrania, akakimbilia nchi ya Midiani. Huko alipata mke kutoka kwenye nyumba ya kuhani mmoja wa Midiani aliyeitwa Yethro.

Alikaa miaka 40 nyumbani kwa Yethro, akichunga mifugo yake, mpaka siku moja Bwana alipomtokea katika mwali wa moto, ndani ya kile kijiti, alipokuwa anachunga kundi la Yethro, Alipewa maagizo ya kuwaokoa Israeli waliokuwa wanateswa chini ya utawala mkali wa Farao.

Kwa Ishara nyingi na miujiza mingi Musa aliwaongoza wana wa Israeli miaka 40 mingine, na Alifariki akiwa na miaka 120, akiwa na nguvu zake zote. Macho yake hayakupofuka wala mwili haukupungua nguvu (Kumbukumbu 34:7)

Musa pekee ndiye Nabii aliyezungumza na Mungu uso kwa uso, wala baada yake hakuinuka nabii mfano wake yeye (Kumbukumbu 34:10-12)

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

1.Utaji uliokuwepo juu ya uso wa Musa ulikuwa unaashiria nini?

2.Haruni ni nani?

3. Miriamu ni nani?

HOME

Print this post

Yesu alipopanda kuomba kwanini atokewe na Musa na Eliya na sio manabii wengine?

SWALI: Katika ule mlima mrefu, aliopanda Yesu na wanafunzi wake kuomba, kwanini atokewe na Musa na Eliya na sio manabii wengine? Mfano wa Isaya au Samweli?


JIBU: Awali ya yote yeye kutokewa na wale watu halikuwa Kwa lengo lake. Bali Kwa lengo la wale wanafunzi aliokuwa nao,  Ili kutimizi mambo yafuatayo.

1 ) Kutimiza unabii mkuu uliomuhusu yeye.

a) Unabii wa kwanza ni ule alioutoa Musa kuwa atakuja Nabii mwingine kama yeye na kwamba watu wamsikilize..

Kumbukumbu la Torati 18:15

[15]BWANA, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye.

Soma pia Matendo 3:22-25,. Hivyo wayahudi walikuwa na matarajio ya kuona mtu anayefanana  na Musa atakayeleta Sheria mpya  akija duniani, lakini akiwa na nguvu na uweza mwingi mfano wa Musa..

Ndio sababu ya Musa kutokea mbele ya wanafunzi wake, ili Mungu awathibitishie huyu ndio yule Musa aliyemnenea habari zake.

b) Lakini pia unabii uliohusu kutangulia Kwa Eliya kabla ya Kuja kwake duniani.

Wanafunzi walikuwa na dukuduku kama huyu, ndiye Kristo aliyetabiriwa au sio, na kama ndio mbona Eliya hajatangulia mbele yake tukamwona? Kwasababu waliambiwa hivyo na waandishi. Lakini sasa walipomwona Eliya mwenyewe amesimama mbele ya Yesu wakaamini lakini bado hawakuelewa..Sasa walipokuwa wanashuka ndio wakapata nguvu ya kumuulizia hilo swali.. Na hili ndio likawa jibu lake.

Mathayo 17:9-13

[9]Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, Msimwambie mtu ye yote habari ya maono hayo, hata Mwana wa Adamu atakapofufuka katika wafu.

[10]Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, Basi kwa nini waandishi hunena ya kwamba imempasa Eliya kuja kwanza?

[11]Naye akajibu, akawaambia, Kweli Eliya yuaja kwanza, naye atatengeneza yote,

[12]ila nawaambia, ya kwamba Eliya amekwisha kuja, wasimtambue, lakini wakamtenda yote waliyotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu naye yuaenda kuteswa kwao.

[13]Ndipo wale wanafunzi walipofahamu ya kuwa amesema nao habari za Yohana Mbatizaji.

2) Na Pili ni Kutoa utata Kuwa yeye sio mmojawapo wa manabii wakubwa wa kale wanaodhaniwa.

Utakumbuka kabla ya kupanda mlimani aliwaliza watu kuwa wanamzungumzia kuwa yeye ni nani? Wanafunzi wakamjibu kuwa wanasema yeye ni Eliya, wengine mmojawapo wa manabii wa Kale.n.k. Hivyo kulikuwa na utata mwingi. Lakini siku hiyo alitoa utata huo Soma.Mathayo 16:13-18. 

Mitume walipoona sura za manabii wao wa kale wamesimama mbele ya Yesu, mwenye utukufu mwingi sana kupitia wao. Wakaamini yeye ni zaidi ya manabii wote wakubwa Kwa wadogo waliowahi kutokea katika historia.

3) Lakini pia alikuwa na Lengo la kuwafunulia kuwa atakufa kama mmojawapo wa manabii wakubwa, lakini pia atapaa kama mmojawapo wa manabii wakubwa.

Musa alikufa, lakini Eliya alipaa.

Yesu ndio mtu pekee miongoni mwa wanadamu, aliyekufa, Kisha akazikwa, kisha akafufuka.na mwisho akapaa. Kwa hiyo Ile ilikuwa ni lugha ya kinabii, kueleza hatma yake na ndio maana hata manabii Hao walikuwa wakizungumza mambo yahusuyo kufa kwake na kufufuka.(Luka 9:31).  

Hizo ndio zilikuwa sababu kuu za Bwana kutokewa na manabii wale wawili na sio wengine. Na walipokuwa wanashuka Akawaambia wanafunzi wake wasimwambie mtu mpaka atakapofufuka katika wafu.

Kufunua nini?

SI wote watamwona Yesu katika kilele Cha utukufu wake, isipokuwa wale tu walio na kiu na yeye. Ambao watakuwa tayari kuwa karibu naye wakati wote mfano wa Hawa wanafunzi watatu yaani Yohana, Petro na Yakobo.

Ukimpenda Yesu tumia muda mwingi kuwepo uweponi mwake. Utamjua sana Kwa mapana na marefu yake.

Je! Umeokoka? Je unatambua kuwa hizi ni siku za mwisho na Kristo yupo mlangoni kurudi? Dalili zote zimeshatimia, unasubiri nini usimpe Bwana maisha yako, embu fanya uamuzi leo. Tubu dhambi zako, mgeukie Yesu, Unyakuo usikupite. Ikiwa utapenda upate mwongozo huo, wasiliana nasi kwa namba zetu hizi bure +255693036618 /+255789001312

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

Je! Umeona asali? Kula kadiri ya kukutosha;

KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.

LAKINI MAKINDA WAWEZA KUYATWAA UWE NAYO.

Rudi nyumbani

Print this post

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

Jibu: Tusome,


Waefeso 2:20 “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni”

Hapo maandiko yanasema tumejengwa juu ya “Msingi wa Mitume na Manabii “na si juu ya “Mitume na Manabii” .. Na pia inasema tumejengwa juu ya “Msingi” na si juu ya Misingi ya mitume na manabii. Ikiwa na maana kuwa Msingi ni mmoja tu, ambao tumejegwa juu yake, (mbele kidogo tutakuja kuuona huo msingi ni nini).


Sasa yapo maswali mawili hapo ya kujiuliza; 1) Hawa Mitume na Manabii ni akina nani na 2) Huo msingi ni nini?


1) Mitume na Manabii:


Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapa katika Waefeso 2:20 sio hawa waliopo sasa, Bali ni wale walioandika biblia, kama Musa, Yeremia, Hosea, Ezekieli na Malaki vile vile mitume wale 12 wa Bwana pamoja na wengine kama akina Paulo, ambao waliandika biblia.


Mtu yeyote aliyepo sasa, au atakayekuja kutokea na kujiita mtume au nabii, basi afahamu kuwa andiko hilo la Waefeso 2:20 halimhusu hata kidogo. Na shetani amewapandikiza watu wengi kiburi (watu wanaojulikana kama mitume na manabii wa leo), na kuanza kujivuna kuwa wao ndio Msingi wa kanisa.. Jambo ambalo si la kweli hata kidogo.


2) Msingi


Msingi ambao sisi tumejengwa juu yake ni ule waliokuwa nao Mitume, ikiwa na maana kuwa kile Mitume walichokifanya msingi, ndicho hicho hicho sisi (kanisa la Mungu) tunajengwa juu yake. Sasa ni kitu gani Mitume na Manabii wa kwenye biblia walikifanya msingi?… Hicho si kingine zaidi ya YESU KRISTO MWENYEWE!!!. Huyu ndiye Msingi wa kanisa na ndiye aliyekuwa msingi wa mitume, na ndio msingi wetu sisi na bado ataendelea kuwa msingi siku zote.


1Wakorintho 3:11 “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, YESU KRISTO”.


YESU KRISTO ndio Mwamba ule ambao yeye mwenyewe alisema kuwa kanisa lake litajengwa juu yake.


Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?
14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.
15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
16 Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.
18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”.


Umeona? Mwamba unaonenewa hapo sio Petro bali ni yeye YESU MWENYEWE!.. yaani huo Ufunuo Petro alioupata wa YESU KUWA MWANA WA MUNGU Ndio MSINGI, na NDIO MWAMBA ambao kanisa litajengwa juu yake.


Kanisa lolote leo ambao YESU sio kiini cha Imani hiyo, hilo sio kanisa la kweli, vile vile imani yoyote ile isiyomweka YESU kama msingi badala yake inawemweka mwanadamu mwingine au mnyama au sanamu basi imani hiyo ni imani ya Uongo n.k


Mahubiri yoyote yasiyomweka YESU msingi, hayo ni mahubiri kutoka kwa Yule adui.
Mtumishi yoyote Yule, awe mchungaji, mwalimu, mtume, nabii au mwinjilisti asiyemweka YESU kama kiini na kitovu cha Mafundisho huyo si wa kweli, kwa mujibu wa maandiko.
Vile vile mtu yeyote ajiitaye Mkristo na Yesu si msingi wa maisha yake, huyo ni mkristo jina tu wa uongo.
Bwana atusaidie tumweke Yesu msingi wa maisha yetu.


Maran atha!.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?

Nitamjuaje nabii wa Uongo?

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

Kiti cha Rehema kilikuwaje? (Kutoka 40:20)

Rudi nyumbani

Print this post

Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?

Wingu la Mashahidi
Wingu la Mashahidi
Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?
/

Swali: Katika biblia tunasoma sehemu kadha wa kadha zikiwataja “wana wa manabii”.. Je! Hawa wana wa manabii walikuwa ni watu gani?, na kazi yao ilikuwa ni ipi? Na kwanini waliitwa hivyo?.. Na je hata leo kuna wana wa manabii?

Jibu: Ni kweli Katika Agano la kale lilikuwepo kundi la watu waliojulikana kama Wana wa Manabii. (Soma 1Wafalme 20:35, 2Wafalme 6:1, 2Wafalme 4:1, na 2Wafalme 2:5).

Watu hawa walikuwa ni “manabii wa Mungu”, ambao walijitia katika kifungo cha kujifunza juu ya Nabii zilizotangulia kabla yao..

Kumbuka sio kujifunza jinsi manabii wanavyoishi au wanavyokula au wanavyoona maono!… La! Hakuna mwanadamu yeyote anayeweza kumfundisha mtu mwingine namna ya kuona maono!…hivyo ni vipawa vya Mungu ambayo ni Mungu mwenyewe anaviweka ndani ya mtu, na hatujifunzi wala hatufundishwi.. Ni sawa na ndoto…

Hakuna mtu anayeweza kumfundisha mwenzake jinsi ya kuota!.. Ndoto zinakuja zenyewe, kwasababu ni vipawa  vya asili ambavyo Mungu kaviweka kwetu sote.. Na nabii za Mungu, zinawajia watu maalumu ambao Bwana kawachagua, na si kupitia kujifunza!.

Kwahiyo hawa wana wa manabii, au kwa lugha nyingine “Wanafunzi wa manabii” walikuwa ni watu waliojikita kujifunza Nyakati na Majira, Pamoja na Nabii zilizotangulia kutolewa na manabii wengine waliowatangulia..(kumbuka walikuwa wanajulikana kama wana wa manabii, na sio wana wa NABII!)..

Na lengo la kufanya hivyo (yaani kupokea maarifa hayo) ni ili wawe salama, na wawe na uhakika wa Nabii watakazozitoa isije wakapotoka na kutoa unabii wa uongo.

Kwa mfano Nabii anaweza kuona maono au kupata ujumbe kuhusu Taifa la Israeli, sasa ili authibitishe ujumbe ule au ono lile kama kweli ni kutoka kwa Bwana, ni sharti awe na Nabii nyingine za kutosha, za waliomtangulia zinazosapoti ono lake hilo jipya!..  Na akija kugundua kuwa Nabii mwingine, mkuu aliyetangulia alishatabiri jambo kama hilo au linalokaribiana na hilo… basi ndipo Ono lake hilo linathibitika… lakini akija kukuta ono lake linakinzana na maono ambayo manabii wakuu waliyatoa, ndipo analiacha, kwasababu sio kutoka kwa Bwana… (kwasababu kamwe Bwana hawezi kujipinga katika maneno yake).

Hivyo ndio maana ilihitajika shule ya manabii, ambayo lengo lake ni kujifunza kujua Nabii zilizotangulia juu ya watu, na mataifa…

Ili tuzidi kuelewa vizuri, utakumbuka kipindi cha Nabii Yeremia wakati anatabiri kwamba Israeli watachukuliwa utumwani kwenda Babeli.. utaona Yeremia alikuwa ni mtu mwenye elimu ya kutosha kuhusu Nabii zilizotangulia, alihakiki jumbe anazozipokea katika maono, kwa nabii za waliomtangulia kama wakina Isaya, na wengineo..

Na jambo moja utaona alilojifunza ni kuwa “Manabii karibia wote, hawakuwahi kutabiri juu ya amani kwa mataifa, manabii wengi walikuwa wanatabiri juu ya Vita na Mabaya na Tauni”.. Na Yeremia alijua Mungu hawezi kujipinga.. Hivyo maono yake aliyahakiki kwa namna hiyo..

Lakini utaona alitokea mtu anaitwa Hanania, ambaye alijitokeza na kuanza kutabiri juu ya Amani kwa Israeli kwamba hawataenda utumwani, watakuwa salama, ni ilihali Taifa zima limemwacha Mungu..jambo ambalo linakinzana na Nabii Mungu alizozitoa kupitia manabii wakuu waliotangulia… Na Yeremia kuliona hilo akamwambia Hanania maneno yafuatayo…

Yeremia 28:7 “Lakini lisikilize sasa neno hili nilisemalo, masikioni mwako, na masikioni mwa watu wote,

8 MANABII WALIOKUWAKO KABLA YA ZAMANI ZANGU, NA ZAMANI ZAKO, WALITABIRI JUU YA NCHI NYINGI, NA JUU YA FALME KUBWA, HABARI YA VITA, NA YA MABAYA, NA YA TAUNI”.

Umeona jambo Yeremia alilomwambia huyu Hanania?…

Yeremia alikuwa ni Mwana wa manabii, lakini Hanania alikuwa ni mtu tu aliyejizukia na kujiita Nabii, hana elimu yoyote ya Nabii za Mungu.. na akaanza kuwafariji watu kwa maneno ya uongo!..Jambo ambalo lilimchukiza sana Mungu, na hata kumwua Hanania.

Yeremia 28:15 “Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, Sikia sasa, Ee Hanania; Bwana hakukutuma; lakini unawatumainisha watu hawa maneno ya uongo.

 16 BASI BWANA ASEMA HIVI, TAZAMA, NAKUTUMA UENDE ZAKO TOKA JUU YA USO WA NCHI; MWAKA HUU UTAKUFA, KWA SABABU UMENENA MANENO YA UASI JUU YA BWANA.

17 BASI NABII HANANIA AKAFA, MWAKA UO HUO, MWEZI WA SABA”.

Lakini leo hii shetani kaligeuza hili Neno “Wana wa Manabii”. Leo hii kuna watu wamefungua vyuo vyao, wakiwa wenyewe wanajiita Manabii wakuu, na vijana wao wanawaita “wana wao (yaani wana wa manabii)”.. Lakini ukiingia katika madara yao na kusikia wanachofundishwa, ni huzuni tupu!.

Utasikia wanachofundishwa ni jinsi ya kuona maono, jinsi ya kutumia na kutengeneza mafuta na chumvi na mengineyo, utaona wanafundishwa mtindo wa maisha na mtindo wa kuongea, na kuvaa kama nabii mkuu wao, na jinsi ya kumwogopa na kumtukuza baba yao, nabii mkuu..

Na watasomea hata miaka 5 na wakitoka hapo wanapewa na vyeti, tayari wakufunzi!!!..

Ndugu! Huo ni uongo wa shetani…

Wana wa manabii katika Agano la kale, hawakufundishwa wala hawakuwa wanajifunza mitindo ya kuongea ya manabii waliowatangulia…wala walikuwa hawajifunzi jinsi ya kuona maono! (kwasababu tayari walikuwa na hiyo karama, ndio maana wakaitwa manabii)..Walichokuwa wanajifunza ni Nabii zilizotangulia zinazohusu wakati waliopo wao, na za mataifa mengine, kuanzia zilizoandikwa katika Torati ya Nabii Musa, mpaka wakati waliopo wao, ili kusudi wasije wakapotoka na maono waliyokuwa wanayapokea.

Na sisi leo hii wote ni wana wa Manabii.. ambao manabii wetu si baba zetu wa kiroho!!! Wala si maaskofu wetu, bali ni MITUME WA KWENYE BIBLIA, na MANABII WA KWENYE BIBLIA!!!...Tunatembea katika Nabii walizozitoa hao, wakina Musa, Isaya, Yeremia, Habakuki, na mitume wakina Petro, Yohana, Paulo n.k.. (Na nabii zao hazijawahi kukinzana),Kwasababu walikuwa na Roho mmoja.

Kwamfano Nabii Isaya alitoa unabii ufuatao..

Isaya 13:6 “Pigeni kelele za hofu; maana siku ya Bwana i karibu; itanyesha kama maangamizi yatokayo kwa Mwenyezi Mungu”.

Nabii Yoeli naye alitoa unabii kama huo huo katika Yoeli 3:14, na manabii wengine wote walitabiri hayo hayo…

Kwahiyo ili sisi tuhesabike kuwa “Wana wa manabii” ni lazima maono yetu tunayoyaona katika ndoto, au kwa wazi, ni lazima yapatane na huo unabii wa Isaya, na Yoeli na wengineo katika biblia!… usipopatana na huo unabii wa Isaya basi hilo Ono au huo Unabii ni wa UONGO!!! Ni kutoka Kuzimu!!!...

Tukiota au tukiona maono ambayo yanatuonyesha au kutuambia kuwa “Tufurahi, tupige kelele za shangwe, kwasababu siku ya Bwana bado sana”..basi hilo ni Ono kutoka kuzimu!!!..

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba wana wa manabii, ni manabii ambao walikuwa wamejikita katika kusoma Nabii za manabii wa Mungu waliowatangulia, ili wasifanye makosa katika kutoa nabii zao.

Na sisi ni lazima tuwe wanafunzi wa biblia, turejee biblia katika kuhakiki kila kitu, na hatupaswi kuamini tu kila jambo ambalo tunalipokea katika ndoto au maono.

Bwana Yesu na atusaidie sana.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.

Nini maana ya “Torati na manabii”?

Nini maana ya “Roho za manabii huwatii manabii?

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

Rudi nyumbani

Print this post

TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze maneno ya Uzima wa Mungu wetu..

Yapo maswali kadhaa ambayo tunaweza kujiuliza, juu ya tukio la Bwana Yesu kutokewa na Musa na Eliya siku ile alipopanda mlimani kuomba pamoja na wale wanafunzi wake watatu (Petro, Yohana na Yakobo)..

Na maswali yenyewe ni haya..

 1) Iweje Bwana Yesu atokewe na Musa ambaye tayari alishakufa miaka mingi?, na Zaidi ya yote maandiko yanasema alizikwa, tena na Mungu mwenyewe?..

2) Kwanini Musa na Eliya wamtokee?.. kulikuwa na umuhimu gani wa wao kumtokea Bwana?

Sasa ili tupate majibu ya maswali hayo vizuri, Labda tusome habari yenyewe kwa ufupi kisha tuendelee

Luka 9:28 “Baada ya maneno hayo yapata siku nane, aliwatwaa Petro na Yohana na Yakobo, akapanda mlimani ili kuomba.

29 Ikawa katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka, mavazi yake yakawa meupe, yakimeta-meta.

30 Na tazama, watu wawili walikuwa wakizungumza naye, nao ni MUSA NA ELIYA;

31 walioonekana katika utukufu, WAKANENA HABARI ZA KUFARIKI KWAKE ATAKAKOTIMIZA YERUSALEMU”

Kiini cha majibu ya maswali yetu tutakipata katika huu mstari wa 31.. “walioonekana katika utukufu, WAKANENA HABARI ZA KUFARIKI KWAKE ATAKAKOTIMIZA YERUSALEMU”

Kumbe Sababu ya Musa na Eliya kumtokea Bwana, ilikuwa ni kuzungumza kuhusu Kufa kwake Bwana Yesu, ambako atakutimiza Yerusalemu.

Sasa swali linakuja?, je ni kwamba Bwana Yesu alikuwa hajui kwamba atakwenda kufa mpaka atokewe na watu hao wawili, wamweleze kuhusu kufa kwake?.. Jibu ni la!.. alikuwa anajua, lakini zipo siri nyingine zihusuzo kufa kwake na kufufuka kwake na kupaa kwake, ambazo hizo Baba alimfunulia siku hiyo kupitia manabii hao wawili.

Kumbuka kabla ya Kristo kufa, roho za watakatifu zilikuwa chini, na shetani alikuwa na uwezo wa kuzileta juu, kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka lile tukio la Samweli kuletwa juu ya yule mwanamke mwenye pepo la utambuzi, na baada ya kuletwa juu, Samweli aliweza kutoa unabii wa mambo yajayo, ijapokuwa alikuwa ameshakufa na kuzikwa, kwani tunasoma, alimtolewa Unabii Mfalme Sauli kuhusu KUFA KWAKWE, AMBAKO KUTAKWENDA KUTIMIA KIPINDI SI KIREFU KUTOKA PALE. Unaweza kusoma Habari hiyo kwa urefu katika kitabu cha 1Samweli 28:1-19.

Sasa Biblia haijaeleza Musa alikuwa anamweleza nini Bwana Yesu, lakini tunajua kabisa ni kuhusu Habari za kufunguliwa kwao wafu, na kwamba Bwana Yesu atakwenda kusulibiwa na kushuka sehemu ya wafu wao (akina Musa na wengine walipo na kuwaweka huru, na kwamba siku ya tatu atafufuka).

Kwahiyo kumbe kabla ya Bwana Yesu kufa, Wafu waliendelea kuishi, na pia iliwezekana kuwaleta baadhi yao juu na kutoa unabii, kwa njia yoyote ile!..

Kwasababu hiyo basi tumeshapata jibu ni kwanini MUSA, aliletwa juu na Mungu, ili kutoa unabii (Habari za kufa kwake Bwana Yesu, ijapokuwa Musa alikuwa ameshakufa kitambo na kuzikwa)…Ni kama tu vile, Nabii Samweli alivyoletwa juu na yule mwanamke mwenye pepo la utambuzi. (Kumbuka jambo hilo liliwezekana tu kipindi kabla ya Bwana Yesu kufa, lakini baada ya Bwana Yesu kufa na kufufuka, hakuna mchawi yeyote anayeweza kumleta juu mtu aliyekufa, kwasababu Kristo alizichukua funguo za Mauti na kuzimu).

Hapo tumepata jibu kuhusu Musa, sasa vipi kuhusu ELIYA?

Tunajua kabisa Eliya hakufa, bali alipaa..Maana yake Eliya anayajua yaliyo ya Mbinguni.. kama Nabii, Bwana alimtoa huko na kuja kumpasha Habari Bwana Yesu, kuhusu kupaa kwake, na enzi na mamlaka zinazomngojea Mbinguni (labda na siku hiyo alimpa na tarehe ya kupaa kwake, hatujui).

Kwasababu ijapokuwa Eliya alikuwa amepaa mbinguni, lakini bado alikuwa ni Nabii. Kwahiyo ujio wa Eliya ulikuwa ni wa muhimu sana kwa Bwana, kupata taarifa kuhusu kupaa kwake.

Kwahiyo kwaufupi ni kwamba Mungu aliwatumia manabii hawa wawili kama Manabii wa Ushahidi. Na Ushahidi huo ni wa KUFA kupitia Musa, na Kupaa kupitia ELIYA. Kwasababu Kristo naye atakufa kama Musa aliye nabii mkuu, na vile vile atapaa mbinguni kama ELIYA.

Kwahiyo baada ya tukio lile, Bwana Yesu alipokea Ufunuo mkuu kuhusu Mauti yake na kufufuka kwake, na kupaa kwake.. Zaidi sana na kurudi kwake kutakavyokuwa..ndio maana tunaona pia Uso wake uling’aa kama jua, kuashiria siku ya kurudi kwake kutakavyokuwa.

Na wakati ulipofika kweli Bwana Yesu, alikufa, akafufuka, na akapaa mbinguni.. imesalia hatua moja tu!.. nayo ni KURUDI KWAKE KUTUCHUKUA!..

Je! Umejiandaaje?.. Kama Nabii hizo mbili za kufa na kufufuka kwake na kupaa kwake zilitimia.. Basi hata kurudi kwake kutatimia. Na tupo katika majira ya kurudi kwake, dalili zote zimeshaonekana, muda wowote mambo yanakwisha, Kristo anakuja kuwachukua watakatifu wake, na kitakachokuwa kimesalia kwa wale watakaobaki ni majuto na dhiki kuu.

Je umejiandaaje? Je umemwamini Yesu na kutubu dhambi zako? Je umebatizwa katika ubatizo sahihi?…kama bado unangoja nini?.. Ukiikataa leo injili siku hiyo hutakuwa na la kujitetea. Mpokee Yesu leo, na ukabatizwe na kujazwa Roho Mtakatifu.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

Ngome ni nini?  Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Torati na manabii”?

SWALI: Tukisoma katika maandiko tunaona sehemu kadha wa kadha likitajwa neno “Torati na manabii”. Sasa hii torati na manabii maana yake ni nini? Kwamfano  Mathayo 7:12  inasema

“Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii”.

JIBU: Bwana Yesu aliposema Torati na manabii, alimaanisha Agano la kale, ambalo ndio limeundwa na vitabu vya Musa (Torati), ambavyo ni vitano (5), Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na Kumbukumbu la Torati.  Pamoja na vitabu vyote vya manabii, kama vile, Yeremia, Isaya, Danieli, Ezekieli, Hababuki, Amosi, n.k. hapa ikijumuisha pia, vile vingine kama  Waamuzi, Zaburi, Ayubu, Wafalme,  Mithali, Ruthu n.k. Ambavyo sio moja kwa moja vya manabii, lakini vimebeba nabii za Mungu ndani yake.

Kwahiyo torati na manabii kwa ufupi ni lile agano lote la kale. Hivyo Pale Bwana Yesu alipokuwa anawafundisha juu ya kanuni za kufuata, alirejea biblia yao, akiwaambia kuwa kiini cha biblia hiyo ni UPENDO. Wala hakuna siri nyingine nyuma yake, Torati yote, pamoja manabii wote, walichokuwa wanahubiri ni Upendo, (Ambao umegawanyika, wa Mungu na wanadamu)

Hata sisi wa leo tulio katika agano jipya, tunaposoma biblia yote tujue Ujumbe mkuu tunaoupata katika agano letu ni ule ule UPENDO. Na ndio maana Mtume Paulo alisema.

1Wakorintho 13:1 “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.

2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.

3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu”.

Hivyo na sisi, tunapaswa tuutafute huu, kwa bidii zote, ili tuonekane kuwa wakamilifu mbele za Mungu.

Shalom

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Je aliyezungumza na Musa kule jangwani ni Mungu mwenyewe au malaika wake?

Katika kitabu cha Kutoka 3:2, tunasoma ni Malaika wa Mungu ndiye aliyemtokea Musa, lakini tukiendelea mbele katika Mstari wa 4, tunaona ni Mungu ndiye anayezungumza na Musa, na si Yule malaika tena, hapo imekaaje?

Jibu: Tuisome habari hiyo…

Kutoka 3: 2 “Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea

3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei.

4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.

5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.

 6 Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu”.

Aliyemtokea Musa ni Malaika wa Mungu, na si Mungu mwenyewe… na malaika huyo alimtokea katika mwonekano wa Moto.. (kumbuka malaika wanaweza kuchukua mfano wa umbile lolote, wanaweza kuchukua umbile la mtu, au moto, au mwanga), wanapochukua umbile la kibinadamu wanaonekana kama wanadamu, mfano wa yule aliyemtokea Yoshua katika kitabu cha Yoshua 5:14, wanapokuja katika maumbile haya wanakuwa kama watu kabisa, wanaweza kuonekana na kuzungumza. Kadhalika wanaweza kuja katika maumbile kama ya mwanga au moto..katika maumbile haya, unaweza kusikia sauti tu na usione mtu..ukaona tu huo mwanga au moto!. N.k

Sasa Malaika huyu alitumwa na Mungu kwa Musa akiwa amebeba ujumbe wa Mungu, na alimtokea Musa katika umbile la Moto, maana yake Musa aliona moto tu kwenye kile kijiti na kusikia sauti lakini hakuwa anaona mtu.

Sasa jambo moja la kujifunza ni kwamba, Malaika wanapobeba ujumbe wa Mungu, na Mungu anapoweka jina lake ndani yako,na kuwatuma, wanaweza kutoa ujumbe kana kwamba ni Mungu mwenyewe ndiye anasema ndani yao..Sasa katika huyu Malaika aliyezungumza na Musa, Mungu alikuwa ameweka neno lake ndani yake, kiasi kwamba lolote atakalozungumza ni Mungu ndio kazungumza…(Sasa sio kwamba ni lolote atakalojiamulia tu yeye kusema!..hapana..bali ni lile ambalo Mungu atakalomwambia alifanye na kulisema ndilo atakalolisema).. Tunaweza kusoma hilo vizuri…

Kutoka 23:20 “Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea.

 21 Jitunzeni mbele yake, MWISIKIZE SAUTI YAKE; wala msimtie kasirani; maana, hatawasamehe makosa yenu; kwa kuwa JINA LANGU LIMO NDANI YAKE.

22 LAKINI UKIISIKIZA SAUTI YAKE KWELI, NA KUYATENDA YOTE NINENAYO MIMI; ndipo mimi nitakuwa ni adui wa adui zako, na mtesi wa hao wakutesao”.

Hapo mstari wa 22, anasema “lakini ukiisikiza sauti yake kweli, na kuyatenda yote ninenayo mimi”..Maana yake “Bwana atanena kupitia yule malaika, chochote Yule malaika atakachokisema ni Bwana kakisema”. Jambo hilo liliwezekana kwa malaika tu! ila kwa sehemu ndogo! (si wakati wote Mungu alizungumza na watu kupitia malaika wake kama alivyofanya kwa Musa hapo)..…

Lakini zamani hizi limewezekana kwa asilimia zote kupitia mmoja tu YESU KRISTO!! MKUU WA UZIMA.. Huyo amefanyika bora kupita malaika, akisema ni Mungu kasema asilimia 100!, Maneno yake ni Maneno ya Mungu,..kwasababu amefanyika Bora kupita malaika haleluya!!! (Tutakuja kuliona hilo vizuri mbeleni kidogo!!).

Lakini tukirudi katika upande wa Malaika aliyezungumza na Musa, tunaona baadaye, mbeleni kabisa wana wa Israeli walipoanza kuzembea kuwafukuza wale wenyeji wa miji ile, tunaona Yule malaika aliyepewa maneno ya Bwana kinywani mwake, akitokea na kuanza kuzungumza, kana kwamba ni Bwana mwenyewe ndiye anayezungumza…

Waamuzi 2:1 “Kisha malaika wa Bwana alikwea juu kutoka Gilgali kwenda Bokimu. Akasema, Mimi nimewaleta ninyi mkwee juu kutoka nchi ya Misri, nami nimewaleta hata nchi niliyowaapia baba zenu; nami nilisema, Mimi milele sitalivunja hilo agano langu nililoagana nanyi;

2 nanyi msifanye agano lo lote na hawa wenyeji wa nchi hii; zipomosheni nchi madhabahu zao; lakini hamkuisikia sauti yangu; je! Mmefanya haya kwa sababu gani?

 3 Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu.

4 Ikawa, hapo huyo malaika wa Bwana alipoyanena maneno haya, kuwaambia wana wa Israeli wote, ndipo hao watu wakainua sauti zao na kulia

5 Nao wakaliita jina la mahali pale Bokimu; nao wakamchinjia Bwana sadaka huko”.

Umeona hapo?..aliyewatoa wana wa Israeli Misri kuwapeleka Kaanani ni Bwana, na si malaika, lakini Bwana alimpa Malaika wake jukumu zima, na vile vile, aliweka maneno yake ndani ya Yule malaika, kiasi kwamba atakachokinena Malaika yule, ni Bwana kakinena, na atakachokifanya malaika Yule ni Bwana kakifanya, vile vile Agano lake aliliweka ndani ya Yule malaika, kiasi kwamba atakayevunja agano lile la Yule malaika, ni sawa kalivunja agano la Mungu..kwasababu Neno lake limejaa ndani ya Malaika yule, anakuwa si yeye tena, bali ni Mungu anazungumza ndani yake.

Sasa katika agano hilo la kwanza, Mungu alizungumza ndani ya Malaika, lakini si wakati wote,(wakati mwingine Bwana alisema pasipo kuwatumia hao malaika).. lakini katika agano jipya, Mungu amejitwalia chombo chake, ambacho ametia maneno yake yote ndani yake, na agano lake lote ndani yake, zaidi ya alivyofanya kwa malaika…Chombo hicho hakina pumziko, wakati wote kikinena ni Mungu kanena..na chombo hicho si kingine zaidi ya Bwana Yesu…Huyu kafanyika bora kuliko malaika!!..

Waebrania 1:1  “Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi,

2  mwisho wa siku hizi AMESEMA NA SISI KATIKA MWANA, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.

3  Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu;

4  AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA, KWA KADIRI JINA ALILOLIRITHI LILIVYO TUKUFU KULIKO LAO”

Umeona sauti ya Mungu leo ipo wapi?..umeona agano la Mungu leo lipo wapi?..si kwa mwingine zaidi ya kwa YESU!.. Huyo ni zaidi ya Yule malaika aliyezungumza na Musa pale kwenye ule mwali wa Moto.. Na kama agano la kwanza ambalo Bwana alinena kupitia malaika lilikuwa na utukufu mkubwa vile, kiasi kwamba yeyote atakayelivunja neno la malaika Yule alikufa,. hili la pili ni mara nyingi zaidi..biblia inasema hivyo..

Waebrania 2:1 “Kwa hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa.

2  Kwa maana, IKIWA LILE NENO LILILONENWA NA MALAIKA LILIKUWA IMARA, na kila kosa na uasi ULIPATA UJIRA WA HAKI,

3  sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? AMBAO KWANZA ULINENWA NA BWANA, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia”.

Je umempokea Yesu?.. Je! Umeyakabidhi maisha yako yote kwake?..fahamu kuwa Mamlaka yote ya mbinguni na duniani kapewa yeye..na yeye ndiye sauti ya Mungu kwetu!, ukimkataa yeye umemkataa Mungu, ukimkubali yeye umemkubali Mungu..

Kama bado hujamwamini, nafasi yako ya kumpokea ndio sasa, unachopaswa kufanya hapo ulipo ni kujitenga kwa muda, kisha kupiga magoti binafsi na kumkiri Yesu kwa kinywa chako kuwa ndiye Bwana na mwokozi wa ulimwengu, na kisha kukiri makosa yako kwa kutubu, huku umedhamiria kutofanya tena dhambi hizo, na baada ya hapo haraka sana bila kuchelewa tafuta ubatizo sahihi kama bado hujabatizwa ubatizo sahihi, kumbuka ubatizo ulioagizwa na Bwana Yesu ni ule wa maji mengi na kwa jina la YESU (Matendo 2:38), na baada ya hapo, Roho Mtakatifu atakuongoza katika yote yaliyosalia, ikiwemo kukupa uwezo wa kushinda dhambi.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.

Ni kweli Waliolala Katika Kristo Wamepotea?(1Wakor 15:18)

NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA!

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Je Musa yupo anawashitaki watu..kulingana na Yohana 5:45?

Tusome,

Yohana 5:45  “Msidhani kwamba mimi nitawashitaki kwa Baba; yuko anayewashitaki, ndiye Musa, mnayemtumaini ninyi.

46  Kwa maana kama mngalimwamini Musa, mngeniamini mimi; kwa sababu yeye aliandika habari zangu.

47  Lakini msipoyaamini maandiko yake, mtayaamini wapi maneno yangu?”

Mstari huo haumzungumzii Musa kama Musa, kwamba yupo mahali Fulani mbinguni, anawashitaki watu..hapana!! bali unazungumzia maneno ya Musa (yaani mahubiri yake). Hayo ndiyo yayowashitaki watu sasa, na yatakayowashitaki watu siku ya hukumu, ndio maana hapo katika mstari wa 47 unamalizia kwa kusema.. “Lakini msipoyaamini maandiko yake, mtayaamini wapi maneno yangu?”.

 Sasa Ni kwa namna gani maneno ya Musa yanawashitaki watu sasa?, tutakuja kuona mbele kidogo, lakini sasa tuangalie kwa ufupi ni jinsi gani yatawashitaki watu siku ya hukumu…

Bwana Yesu alisema mahali Fulani maneno haya..

Yohana 12:47  “Na mtu akiyasikia maneno yangu, asiyashike, mimi simhukumu; maana sikuja ili niuhukumu ulimwengu, ila niuokoe ulimwengu

48  Yeye anikataaye mimi, asiyeyakubali maneno yangu, ANAYE AMHUKUMUYE; NENO HILO NILILOLINENA NDILO LITAKALOMHUKUMU SIKU YA MWISHO.

49  Kwa sababu mimi sikunena kwa nafsi yangu tu; bali Baba aliyenipeleka, yeye mwenyewe ameniagiza nitakayonena na nitakayosema.”

Umeona? hapo Bwana Yesu anasema..”Neno analolihubiri ndilo litakalohumu siku ya mwisho”.

Hivyo hata Musa naye, hasimami kumhukumu mtu, bali injili yake ndiyo itakayohukumu watu siku ya mwisho..Kama Musa alitabiri kwamba “Atakuja Masihi”, na Masihi alipokuja kweli kulingana na huo unabii, watu wakamkataa Masihi huyo, basi siku ile ya hukumu, Unabii ule alioutoa kwa uwezo wa Roho utawahukumu wale watu, waliomkataa Masihi. Kwasababu Musa alisema kitu alichoonyeshwa na Mungu, na wala si kwa nafsi yake.

Na si maneno ya Musa tu peke yake, bali na ya Mitume wote wa Mungu na Manabii katika biblia takatifu.

 Kwamfano utaona mahali Fulani Mtume Paulo alisema maneno yafuatayo kwa uwezo wa Roho…

1Wakorintho 6:9  “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? MSIDANGANYIKE; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,  wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”

Na mtu akausikia mstari huo aliouzungumza Paulo kwa ufunuo wa Roho, lakini akaudharau, na kuona kama kasema hayo kwa akili zake, siku ile ya hukumu, Maneno hayo ya Mtume Paulo yatamhukumu. Ndio maana Mtume Paulo mwenyewe alisema tena maneno yafuatayo..

Warumi 2: 16 “katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, SAWASAWA NA INJILI YANGU, kwa Kristo Yesu”.

Hapo anasema “sawasawa na Injili yangu”.. maana yake tutahukumiwa kulingana na Injili ya Paulo, na mitume wengine kwenye biblia, ndio maana nyaraka za Mitume, Roho Mtakatifu kazifanya leo kuwa ni Neno lake.  Chochote kilichozungumzwa na Mtume Paulo katika biblia, au Mtume Petro, au Yohana, au Mathayo kimekuwa ni NENO LA MUNGU KAMILI, na wala si la huyo mtume, na ndicho siku ile ya hukumu, kitakacho hukumu watu.

Mtume Paulo alisema  kwa ufunuo wa Roho…“  Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika kama sina upendo mimi si kitu”. Maana yake kama hatutatafuta upendo kwa bidii, na kujitumainisha kwa karama tulizo nazo, kama lugha au unabii,  siku ile hatutaurithi uzima wa milele, kwasababu Neno hili litasimama kutuhukumu, kwamba tulipaswa tuwe na upendo na si karama tu peke yake.

Lakini pamoja na hayo, Maneno yote ya Watumishi wa Mungu waliopo katika Biblia, yanasimama pia kutuhukumu leo, Maana yake ni kwamba Injili ya Musa, Paulo, Petro, Yohana, na wengine wengi katika biblia, yapo yanatuhukumu wakati huu.

Sasa yanatuhukumu kwa namna gani?

Jibu ni rahisi, kwa njia ya MASHITAKA!.

Mtu anayejiita ameokoka, na huku anajua kabisa katika biblia Mtume Paulo aliandika kwa uwezo wa Roho katika..

1Wakorintho 6:16  “Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja”

Na kwa kulijua hili neno, akakaidi na kwenda kufanya uasherati makusudi, moja kwa moja Shetani analichukua hili andiko na kwenda nalo mbele za Mungu, kumshitaki mtu huyo, atakachosema ni hichi>> “Bwana Mungu Yule mtu, anayesema amekupokea wewe, tazama anafanya uzinzi na kahaba makusudi na ilihali anajua kabisa katika maandiko yako umesema, yeye ajiunganishaye na kahaba ni mwili mmoja naye,”.

Kwa mashitaka kama hayo, shetani anashinda hoja juu yako, na hivyo unahesabika kuwa na hatia juu ya hilo andiko… Ni heri ungekuwa hujaokoka halafu unafanya hayo, shetani asingekuwa na hoja nyingi juu yako, lakini unasema umempokea Yesu lakini unafanya uasherati, hapo ndipo unakabidhiwa shetani na Adui yako shetani anaweza kukufanya lolote kuhakikisha kuwa unakuwa mwili mmoja na Yule unayezini naye… Maana yake matatizo yake yote na laana anazobeba huyo unayezini naye, zinakuja kwako (kwasababu mmeshakuwa mwili mmoja), hata kama anamapepo basi na wewe ni rahisi kuyashiriki. Ndio maana kuna hatari kubwa sana ya kulipuuzia Neno la Mungu, hata tukiwa hapa duniani, kabla hata ya kufika siku ya hukumu.

Hivyo ni muhimu sana kulifuata na kulishika Neno la Mungu, na wala si la kulidharau, kwasababu  ndilo tutakalohukumiwa nalo siku za Mwisho na ndilo linalotushitaki sasa kupitia adui yetu shetani. Na neno la Mungu linapatikana katika kitabu kimoja tu! Kinachoitwa Biblia yenye vitabu 66, na si kwenye kitabu kingine chochote.

Kama hujampokea Yesu leo, huu ndio wakati wako, shetani hakupendi kama unavyodhani, anachokitaka kwako ni ufe katika dhambi zako, siku ile ukahukumiwe na kutupwa katika lile ziwa la Moto. Huko tumwache aende peke yake, lakini sisi tujiokoe roho zetu kwa kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo, na kutubu dhambi zetu, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu, na kupokea Roho Mtakatifu, ili tujiweka salama na tuwe na uhakika wa uzima wa milele.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?

MMESIKIA KWAMBA IMENENWA?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post

Wewe u nabii yule akajibu la!..swali huyu ‘nabii yule’ ni nani?

SWALI: Ukisoma Yohana 1:19-26 inaelezea habari za Yohana mbatizaji akijitambulisha yeye ni nani! Napata shida katika mstari wa 21, alipoulizwa ” wewe u nabii yule” akajibu la!.

Huyu nabii yule, ambaye wayahudi walimtegemea kuja, ni nani?

Maana Yohana alishaulizwa kama yeye ni KRISTO, au ELIYA mwanzoni na akakanusha kuwa yeye si hao…Sasa huyu nabii yule ni nani?


JIBU: Tusome..

Yohana 1:19 “Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani?

20  Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo.

21  Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La.

22  Basi wakamwambia, U nani? Tuwape majibu wale waliotupeleka. Wanenaje juu ya nafsi yako”?

Mstari huu umetafsiriwa vibaya hususani kwa watu wasio wakristo wanaosema huo ni unabii unaomzungumzia mtume Mohamedi, kuwa atakuja baada ya Kristo kuwarejeza watu kwa Mungu

Lakini biblia haitabiri jambo lolote kuhusu kuja kwa mtu mwingine baada ya Kristo, yeye ndiye Alpha na Omega, hakuna nabii au mtume mwingine yoyote ambaye atatumwa baada ya Kristo, kuwaongoza watu katika njia ya kweli..Kama mtu atajiita mtume au Nabii basi ajue huduma yake italenga katika kuwaelekeza watu kwa  huyu nabii mkuu Yesu Kristo,..Lakini sio kupokea maagizo yake tofauti yanayodai kuwa yanawaongoza watu kwa Mungu.

Sasa swali ni nani aliyekuwa anazungumziwa pale?

Kabla ya kufahamu ni nani aliyekuwa anazungumziwa pale, ni vizuri kufahamu Unabii Musa aliutoa huko nyuma kuhusu nabii mwingine ambaye Mungu atamnyanyua kama yeye, (Kumbukumbu 18:15-22)..Sasa biblia inaweka wazi kabisa nabii huyo aliyezungumziwa ni Yesu Kristo na hilo tunalithibitisha katika (Matendo 3:22-23) ukipata nafasi unaweza kuvisoma kwa muda wako vifungu hivyo…

Sasa Je hawa wayahudi walimaanisha nabii gani tena huyu? Ambaye walimuulizia Yohana..?

Jibu ni kwamba enzi zile wayahudi walikuwa na mitazamo mingi ambayo mengine haikuwa sahihi, na hiyo ni kutokana na kuwa na ukimya wa miaka mingi bila kuzukiwa na nabii yoyote Israeli, tangu nabii wa mwisho ambaye aliyejulikana kama Malaki..Hiyo ikawafanya wengi wao waamini kuwa wapo manabii wa kale kama Yeremia watafufuka au watashushwa kwa ajili ya kuwatolea unabii na maneno ya Mungu..

Na ndio maana utaona pale Bwana Yesu alipowauliza mitume wake, kuwa yeye ni nani walimjibu hivi..

Mathayo 16:13 “ Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? 14  Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.

Soma tena..

Luka 9:7 “Na Herode mfalme akasikia habari za yote yaliyotendeka, akafadhaika kwa sababu watu wengine walisema ya kwamba Yohana amefufuka katika wafu,

8  na wengine ya kwamba Eliya ametokea, na wengine ya kwamba mmojawapo wa manabii wa kale amefufuka”.

Soma pia Luka 9:19..utaona jambo hilo hilo…

Mistari hii yote inathibitisha kuwa, wayahudi walikuwa wanatazamia kuwa mmojawapo wa manabii wa kale atanyanyuka kabla ya kuwasili masihi (Kristo) duniani, ambaye labda ni Yeremia, au Danieli, au Isaya… mtazamo ambao haukuwa sahihi.

Na ndio maana hata pale utaona sasa kwanini Yohana aliulizwa je “wewe u nabii yule” wakirejea mmojawapo wa manabii wa kale amekuja kuwahubiria maneno ya Mungu…Lakini yeye akajibu  La!.

Hivyo kwa hitimisho hakuna Nabii mwingine aliyetokea wala tunayemngojea sasa, atakayekuwa mkuu Zaidi ya Masihi YESU KRISTO. Huyo ndiye chapa na nafsi ya Mungu, na mkuu wa wa wafalme wa Dunia, na Bwana wa Mabwana.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE! MUNGU NI NANI?

Shetani ni nani?

Yeshuruni ni nani katika biblia?

Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?

NIFANYE NINI ILI NILITIMIZE KUSUDI LA MUNGU.

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?

Shalom, Karibu tujifunze Neno la Mungu. Lipo swali ambalo tunaweza tukajiuliza siku ya leo, ni kwanini miujiza yote ile mikubwa namna ile Mungu alimtumia musa kuifanya na si mtu mwingine?…Licha ya kuwa ulikuwa ni mpango wa Mungu kuwaokoa wana wa Israeli kwa mkono hodari lakini pamoja na hayo ipo siri nyingine ambayo tunaweza kujifunza kwa Musa ambayo tukiijua na sisi basi Mungu atafanya kazi na sisi katika viwango vingine vya juu zaidi…

Mwanzoni kabisa wa huduma ya Musa, tunaona Mungu hakujidhihirisha kwake kwa njia ya wazi, ikiwa na maana kuwa hakumwona malaika, wala nabii, wala hakusikia sauti yoyote ikimwambia Njoo! Musa nataka nikutume., alichoona tu ni muujiza, kama na sisi tunavyoona leo hii miujiza ya wazi.. na hiyo ndio inayotupa uthibitisho kuwa wito wa Musa hakuwa wa kipekee sana kama wengi wetu tunavyodhani..

Kama unadhani kuona kijiti kinaungua halafu hakiteketei ni muujiza mkubwa zaidi ya unayoona leo hii roho za wafu zinafufuliwa kwa jina la Yesu kutoka mautini, jifirie mara mbili tena…

Lakini biblia inatuonyesha tabia ambayo Musa alikuwa nayo, pindi alipouona muujiza ule tu, hakupita kando, badala yake, moyo wake uliguswa sana, akasema muujiza huu hautanipita mpaka nijue maana yake ni nini, na ni nani aliyeweza kufanya maajabu makubwa kama haya..Ndipo Musa akasogea karibu..Embu jaribu kutengeneza picha akiwa pale akikitazama ki-mti kile cha kijani, kwa butwaa, akikiangalia mara mbili mbili, pengine anajiuliza kichwani, huyu aliyeweza kufanya hivi bila shaka atakuwa ni mkuu sana kwa maajabu na uweza, laiti ningemjua ningemng’ang’ania nisingemwacha….

Sasa wakati akiwa anafikiria hivyo na anataka kukaribia karibu zaidi ili azidi kuchunguza anachokiona ni macho yake au la! saa hiyo hiyo Mungu akaanza kuzungumza naye na kumwambia Musa,usikaribie mahali hapa, maana unaposimama ni nchi takatifu…..Tusome..

Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.

2 Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea.

3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei.

4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.

5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.”.

Kama tunavyojua sote baada ya hapo, ni nini kilitokea katika huduma ya Musa..Mungu alimtumia kwa ishara na miujiza isiyokuwa ya kawaida kwa kipindi chote..

Lakini tujiulize, Ni kwanini Mungu hakuzungumza naye moja kwa moja tangu mwanzoni na kumpa huduma ile kubwa, mpaka akaruhusu kwanza ageuke?

Ni kwasababu Mungu alikuwa anapima kujali kwake kwanza..Na ndio maana akatanguliza kwanza ule muujiza mdogo wa kijiti kuteketea, ili aone kama Musa atauthamini kwa kutaka kujua maana yake au La! ..Na laiti kama Musa asingeuthamini, na kupita zake kuendelea na mambo yake ya uchungaji kamwe Mungu asingekuwa na habari na Musa..maisha yangeendelea kama kawaida tu, kama vile hakuna chochote kilichotokea.

Mungu huwa anawaza na kusema, ikiwa muujiza mdogo kama huu hauthamini, atauthamini vipi nikija kumpasulia habari huko mbeleni, atathamini vipi siku nikijifunua kwake kama nguzo ya moto huko mbeleni?, atathamini vipi wakati nawashushia mana kutoka mbinguni? Atathamini vipi siku nikiyowatolea maji mwambani?.

Lakini Musa alithamini madogo yale, na Ndio maana Mungu alimtumia Musa katika makubwa pia.

Hata sisi ni kwanini Mungu hasemi na sisi au hatembei na sisi katika viwango vingine? Ni kwasababu hatuithamini miujiza ile midogo anayoipitisha mbele yetu sasa.. Tunaona ni kawaida tu..Musa hakuona kawaida….Kama Musa leo hii angeona wafu wanafufuliwa, tujiulize angemshangaa Mungu kwa viwango gani?..Je! yale Mungu anayotutendea ambayo tunaona kabisa ni miujiza mikubwa, Je yanatutafakarisha usiku na mchana, na kutufanya tumshangae Mungu na kumshukuru daima mpaka kumpa Mungu aone sababu ya kutufanyia na makubwa zaidi ya hayo? Je! yale tunayoona wengine wanatendewa na Mungu, na tunaona kabisa ule ni muujiza, Yule kaponywa, Yule kafunguliwa, Yule kaokolewa, Je hayo yanatuingia mioyoni mwetu kiasi cha kwamba yanatugeuza na kutufanya tumshangae Mungu kwa kipindi kirefu au tunayapuuzia tu?

Nataka nikuambie tukiyathamini hayo tunayoona leo hii kama madogo, na kuyatafakari sana, na kumsifu Mungu kwa ajili ya hayo, tuwe na uhakika kuwa tutafungua milango ya kuoiona miujiza mikubwa isiyokuwa ya kawaida katika Maisha yetu, au katika huduma zetu. Kama Mungu alimtumia Musa anaweza kututumia na sisi pia kudhihirisha utukufu wake kwa wasio mjua.

Lakini leo tukiyapuuzia, tujue kuwa hatutafika popote,..Tuthamini haya madogo tunayoyaona kwanza, na ndipo hayo makubwa mengine Mungu atuzidishie..tujifunze kwa mababa hawa waliotutangulia tufanikiwe..

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312


Mada Nyinginezo:

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

FAHAMU ZA WATU HUWA ZINAONDOLEWA NA NINI?

Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, akamwacha Hawa ajaribiwe katika bustani ya Edeni?

“Ninyi ni chumvi ya dunia” Andiko hilo lina maana gani?

Rudi Nyumbani:

Print this post