Title Devis

KWANINI MAISHA MAGUMU?

Jibu jepesi la swali hili ni kwasababu hapo nyuma tulitoka nje ya kusudi la Mungu.

Tangu mwanzo Mungu hakumuumba mwanadamu ateseke wala asumbuke kwa namna ambayo tunaiona sasa hivi, Mungu alikuwa tayari ameshamwandalia mazingira marahisi sana ya kuishi kiasi kwamba siku zake zote tangu kuumbwa kwake hadi milele na milele asingewahi kujua kama kuna kitu kinachoitwa jasho, wala maumivu kwenye mwili wake…lakini kwasababu wazazi wetu wa kwanza waliasi, ndio ikawa chanzo cha kuvurugika mpango mzima au mfumo mzima wa maisha ambayo  Mungu alitupangia sisi tuuishi.

Mwanzo 3:17 “Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako;

18 michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni;

19 kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.”

Unaona hapo? Leo hii unahangaika huku na kule, chakula unakula cha shida, nguvu unayoitumia kutafuta pesa haiendani na unachokipata, kujenga tu nyumba 1 inakuchukua miaka 20 kumalizika kana kwamba unajenga mji wa New York, bado matibabu yanakuumiza kichwa, bado elimu, bado familia, bado ndugu, bado jamii inayokuzunguka, n.k. vyote hivyo vinakufanya uone kama haya maisha hayakupendi, mpaka unaliza swali kama hilo, unafika mpaka kwenye ukurasa huu..Fahamu kuwa ni Mungu ndiye kakuleta hapa anataka kusema na wewe.

Lakini pamoja na kuwa tulitoka nje ya mpango wake, hakutuacha yatima, aliahidi kutandalia makao mengine mapya ambayo raha yetu ile ya mwanzo tuliyokuwa nayo itarejea na hata pengine zaidi ya pale na hiyo inakuja mara  baada ya maisha haya kuisha, lakini pia aliahidi hata tukiwa hapa hapa duniani kwenye dhiki hizi nyingi, bado atakuwa na sisi kuhakikisha kuwa anatupa WEPESI wa maisha …Lakini neema hiyo ameahidi kuitoa tu kwa wale ambao watakuwa tayari kumpokea..

Bwana Yesu alisema maneno haya:

Mathayo 11:28 Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.

Unaona Ni YESU tu pekee ndiye anayekuahidia PUMZIKO LA MAISHA YAKO. Hakuna mwanadamu yoyote anaweza kukuahidi kitu kama hicho, ukiwa ndani ya Kristo atakupa AMANI ambayo hata kama mfukoni huna kitu, utajiona wewe ni zaidi ya tajiri yeyote duniani, utakupa tumaini ambalo, litakufanya usione haya maisha kuwa ni kitu cha kukisumbukia sana..atakutunza atakulinda atakuhifadhi..

Unachopaswa ni kumpa tu maisha yako, kuanzia leo aanze kuyaongoza nawe utaona wema wake

Anasema:

 Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini. (Zaburi 34:8).

Na hiyo inakuja kwa kutubu kabisa kwa kumaanisha kuacha dhambi zako zote…Na baada ya hapo atakuja ndani yako, lakini sharti ukabatizwe katika ubatizo wa kuzamishwa katika maji mengi, kwa Jina la YESU KRISTO upate ondoleo la dhambi zako, kama hukuwahi kufanya hivyo na yeye wenyewe atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu atakaye kulinda, na kukupa wepesi wa maisha haya. Mpaka siku ile ya kwenda mbinguni.

Mathayo 6:25 “Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?

26 Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao?

27 Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?

28 Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti

29 nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.

30 Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?

31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.”

Ubarikiwe.


 

Mada Nyinginezo:

JAWABU LA MAISHA YA MTU.

JE! KUBET NI DHAMBI?

JEHANAMU NI NINI?

MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya Neno Haleluya.

Hili ni Neno lenye asili ya kiebrania, lenye muunganiko wa maneno mawili “Halelu”, na “Yah”..Halelu ikiwa na maana “msifu” na “Yah” ikiwa na maana “Bwana” ..”Yah” ni ufupisho wa Neno Yehova,..Hivyo Haleluya Ni neno lililomaanisha kumsifu Bwana kwa nyimbo za furaha..

Kama wewe ni msomaji wa biblia utaona likijitokeza sehemu nyingi katika maagano yote mawili, Kwenye agano la kale utaliona kwenye kitabu cha Zaburi, na katika agano jipya utaliona  kwenye kitabu cha Ufunuo.

Zaburi 106:1 “Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.

2 Nani awezaye kuyanena matendo makuu ya Bwana, Kuzihubiri sifa zake zote?”

 

Zaburi 113:1 “Haleluya. Enyi watumishi wa Bwana, sifuni, Lisifuni jina la Bwana”.

 

Ufunuo 19:1 “Baada ya hayo nikasikia sauti kama sauti ya makutano mengi, sauti kubwa mbinguni, ikisema, Haleluya; wokovu na utukufu na nguvu zina BWANA MUNGU wetu”.

Hata sasa Neno hili tunalitumia wakristo pale tunapomsifu Mungu kwa furaha.. Au tunapoufurahia ukuu wake. Wewe nawe usione aibu kulitamka Neno hili kwa nguvu pale uufurahiapo utukufu wa Mungu.

Bwana akubariki.


 

Mada Nyinginezo:

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA JIKANE MWENYEWE?

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “WAACHE WAFU WAZIKE WAFU WAO.(MATHAYO 8:21)?

JE! KITABU CHA YASHARI NI KITABU GANI? (2SAMWELI 1:17-18),

JE! KUBET NI DHAMBI?

JE! KUFANYA MASTURBATION (PUNYETO) NI DHAMBI?

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

UNYAKUO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

SAA YA KIAMA.

Wingu la Mashahidi
Wingu la Mashahidi
SAA YA KIAMA.



Loading





/

Cha kushangaza ni kwamba wakristo tu peke yetu ndio hatujui saa tunayoishi na muda gani mchache tuliobakiwa nao, na hata kama tunajua basi wengi bado hatujachukulia kwa uzito jambo hili ukilinganisha na jinsi wanasayansi na shetani wanavyolichukulia kwa upande wao..Wanasayansi leo hii wameunda saa yao maalumu ijulikanyo kama “Doomsday clock” (saa ya kiama), ambayo hiyo inawakaumbusha ni wakati gani wanaoishi sasa, wameifananisha na saa  yetu hii ya kawaida, kwamba mshale ukifika tu saa 6 kamili usiku basi usiku wa manane umeanza, vilevile na siku mpya imeanza, Hivyo hiyo saa yao sasa ipo katika muundo huo huo kwamba zimebaki dakika chache sana kabla ya kuingia usiku wa manane wao(yaani kiama), wanakadiria kuwa  miaka yote ya nyuma saa hiyo ilikuwa haijafikia usiku wa manane lakini  kuanzia  mwaka 1947 ilifikia dakika 7 kabla ya kuingia usiku wa manane, na hiyo ni kwa jinsi walivyokuwa wanaona hali ya dunia inavyokwenda kwa matetesi ya vita vya mabomu ya Atomiki, kwamba muda wowote vita vinaweza kuanza na vikianza tu basi itachukua muda mfupi sana dunia kuwa sio sehemu tana ya kuishi mwanadamu.

Na kila siku mshale wao unapanda, mwaka 2015 walikadiria ni dakika 3 tu zimebaki , mwaka 2017 walikadiria dakika 2.5, mwaka jana walikadiria dakika 2 kabla ya kufikia saa 6 ya usiku wao…Yaani tafsiri yake ni kuwa hatari ya kukifikia kiama cha dunia ni kikubwa kuliko inavyodhaniwa katika miaka iliyopita…

Kama ulikuwa hujui sikuzote Mungu kabla hajaleta uharibifu wa hii dunia ni sharti kwanza wanadamu wajiharibu wenyewe, Ndivyo ilivyokuwa hata katika kipindi cha Nuhu, watu walijiharibu wenyewe kupindukia kukawa hakuna tena sababu ya maisha na ndipo Mungu akamaliza kila kitu (Mwanzo 6:12), ndugu  usione ukadhani kuwa duniani kuna amani, usidanganyike na siasa za dunia, ni jambo la kawaida kuficha ukweli ili watu wasiwe na wasiwasi lakini  nyuma yake ipo hofu kubwa ambayo wao wenyewe wanaitambua, pamoja na wanasayansi wao, kwa huu ugunduzi wa mabomu ya Atomiki ambayo hata leo kwenye vyombo vya habari unaona mataifa mengi yanagombana kila siku kuhusu hayo, kwasababu wanajua vita vikishaanza basi ndio mwisho wa kila kitu,..

muda mfupi chini nitakuonyesha video fupi, ya jaribio la kwanza la bomu la Atomiki lilidondoshwa huko Urusi tarehe 30 Octoba 1961, ukubwa wake ukiachilia mbali yale ya Nagasaki na Heroshima yaliyomaliza vita ya pili ya dunia kwa kuuwa  zaidi ya watu laki 2 kule Japan. Hili ni mara 1000 zaidi ya yale kwa uharibifu wake, tazama video fupi chini uone lilivyodondoshwa.

Lakini kabla hayo hayajatokea Unyakuo utakuwa umeshapita, katika ule mfufulizo wa maono 7 aliyoonyeshwa mtumishi wa Mungu maarufu William Branham  na kuambiwa hayo yatatokea kabla ya kuja kwa pili kwa Kristo, kama wengi tunafahamu na tunavyosoma katika historia, matano kati ya yale yalitimia kama yalivyo mawili bado, William Branham alionyeshwa kabla ya kutokea vita ya pili ya dunia jinsi hitler atakavyonyanyuka na kuiongoza dunia yote katika vita na jinsi  kifo chake kitakavyoishia na kuwa cha kiajabu ajabu, habari hiyo aliihubiri na ikajulikana na watu wote kabla hata ya kutokea kwa vita ya pili ya dunia, hilo lilikuwa ni ono la pili kati ya yale saba, sasa ono la saba ambalo lilikuwa ndio la  mwisho alionyeshwa kuangamizwa kwa taifa la Marekani, anasema alisikia mlipuko mkubwa usio wa kawaida nyuma yake na alipogeuka hakuona kitu chochote zaidi ya vipande vya mabaki na moshi tu,…Na hicho si kingine zaidi ya bomu la nyuklia.

Sasa hiyo alioneshwa kwa taifa lake, jambo hilo litakuja kuwa ulimwenguni kote, lakini mpaka hayo yote yatokee unyakuo utakuwa umeshapita, Mpaka sasa unaweza kuona ni saa gani hii tunaishi, Kama wanasayansi watu wa kidunia hawaishi kama vile wanayo wiki moja mbeleni, iweje mimi na wewe leo tuishi kama vile tuna maelfu ya miaka mbeleni,..Bwana anakuja, dalili zote zinaonesha, sijui tanataka tuoneshwe dalili zipi tena ndio tuamini na sisi kuwa tunaishi ukingoni mwa wakati..laiti kama na sisi tungekuwa na saa yetu basi saa yetu ingesoma tupo  visekunde vichache kabla ya kwenda katika unyakuo kwa Baba na kuanza kwa utawala mpya wa miaka 1000 wa Bwana wetu YESU KRISTO..

Tazama video fupi chini ya bomu lijulikanalo kama TSAR BOMBA, jinsi lilivyoachiwa ili ufahamu yatakayowakuta wale wote watakaokosa unyakuo.

Bwana Yesu akubariki sana Mtu wa Mungu, Tafadhali share na wengine


Mada Nyinginezo:

KATI YA UNYAKUO WA KANISA, DHIKI KUU, VITA VYA HAR-MAGEDONI, UTAWALA WA MIAKA 1000, VITA YA GOGU NA MAGOGU, HUKUMU YA KITI CHA ENZI CHEUPE. JE, NI KIPI KINAANZA NA KINGINE KUFUATA?

SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!

KITABU CHA UZIMA NI KIPI?

KUZIMU NI MAHALI PA NAMNA GANI ,JE! HUKO WANAISHI WATU WAKIFA NA KWENDA KUPATA MATESO AU NI VINGINEVYO?


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

Cheo cha Mpinga-Kristo, kimeshafunuliwa Zaidi ya Karne moja iliyopita huko nyuma, nacho si kingine Zaidi ya cheo cha ki-PAPA, Wakati wa Mwisho utakapofika atanyanyuka mmoja atakayekikalia hicho kiti, ambaye atafanya mambo maovu na ya ajabu, yale yote yaliyotabiriwa katika maandiko matakatifu. Huyo bado hajafunuliwa kwasasa jina lake ni nani?… Lakini hatatoka pengine mbali na kiti hicho cha Kipapa..Lakini kwasababu tunajua majira na nyakati, kwamba hizi ni siku za mwisho, labda huyu aliyeko sasahivi ndiye!..au kama siye miongoni mwa wachache sana wanaokuja huko mbeleni atakuwa mmojawapo!…Huyo ndiye atakayeihimiza chapa! Huyo ndiye atakayeidanganya dunia kuwa ataleta amani! Lakini badala yake ataipeleka kwenye matatizo na kiama.. Na ndiye atakayetafuta kwenda Yerusalemu kwenye Hekalu litakalotengenezwa kule hivi karibuni kule Israeli aabudiwe pale kama Mungu (2Wathesalonike 2).

Vipo viishara vingi vinavyotuthibitishia utendaji kazi wake, katika kizazi chetu…lakini pia kipo kiashiria kimoja kikubwa sana! Cha kutufanya tuzidi kuwa macho na kufunguka fahamu zetu, kujua ni majira gani tunaishi.

Kiashiria hicho si kingine Zaidi ya Roho yake huyo Mpinga-Kristo kuwavaa watu(wanaojiita watumishi),

Leo hatutazungumzia, jinsi hii roho ilivyoyavaa makanisa pamoja na serikali..Bali tutaangalia ni jinsi gani imewavaa wanaojiita watumishi.

Zamani, kusikia Mtu anayejiita mtumishi wa Mungu, kuwa na walinzi wa pembeni (ma-bodyguards) ilikuwa ni jambo la kushangaza sana…Hata hivyo halikuwepo kabisa, kwasababu Bwana Yesu mwenyewe ambaye sisi tunamwita Bwana! Hakuwa na mabody-guards, wapo watu wanasema wale mitume walikuwa ma-bodyguards wake, huo sio ukweli, bodyguard huwa anatembea na silaha na kazi yake ni kumlinda Yule ili asidhuriwe anakuwa tayari hata kuua ili kwamba tu Yule anayelindwa akae salama, lakini Bwana hakuwaita mitume kwa kazi hiyo, ya kumlinda yeye, kinyume chake Petro alipojaribu kufanya hivyo kwa kumkata Yule mtu sikio alimkemea …Zaidi ya yote yeye mwenyewe alijitoa kwa hiyari yake kufa kwa ajili ya wengi, ingawa alikuwa na uwezo wa kuagiza malaika waje wampiganie lakini hakutumia uwezo huo, ili kwamba awe sadaka kwa wengine (soma Mathayo 26:51-54 )…

Na Neno lake linatuambia kama yeye alivyojitoa kwa ajili yetu na sisi pia tunapaswa tujitoe kwa ajili ya wengine. (1Yohana 3:16)

Lakini leo ni kinyume chake utaona Mhubiri anakwenda kuhubiri injili na Mabody-guards ambao wameandaliwa mahususi kumtetea yeye, na ndani ya kifuko yao wamebeba silaha..yote hiyo hataki kufa! au Anaogopa kufa!..Ukimgusia habari za kwenda kuhubiri bila bodygurds anapambana na wewe!..Leo malengo ya wahubiri wengi ni kununua Helikopta na ndege, ili hatimaye waziandike majina yao, na wajulikane dunia nzima, na hatimaye waonekane mbele ya vyombo vya habari ili wapate heshima duniani kote…

Sasa hiyo yote imetoka wapi? Na kwanini haikuwepo kipindi cha nyuma?

Jibu ni rahisi! Hiyo yote ni ile nguvu ya mpinga-Kristo mkuu imewavaa hawa watumishi!….Roho ya Mpinga kristo ndiye inayowafanya watafute fahari na ufalme katika dunia hii, sasa roho hiyo haijaanzia kwao, bali imeanzia kwenye kile cheo cha Mpinga Kristo mwenyewe, (yaani kiti cha upapa)…Papa ambaye anajulikana kama mhubiri maarufu, ndiye Mhubiri pekee aliye kinyume na Kristo, ambaye analindwa na JESHI! Linaloitwa “Swiss guards” linalomzunguka na kumlinda kila anakokwenda..Mabodyguard hao kabla ya kumlinda Papa, wanaapa kuwa tayari hata kuutoa uhai wao ili tu kumlinda Papa asife!…jambo ambalo Kristo aliye Bwana hakufanya, wala hakutamani kulindwa kwa namna hiyo…hivyo si ajabu leo kuwaona hawa wahubiri wengine wadogo wakifanya hayo hayo…wakiajiri mabodygurd kuwalinda hadi madhabahuni..ni roho ile ile ya mpinga-kristo ipo kazini.

Papa ana ndege yake maalumu inayoitwa “Alitalia Flight AZ4000” inayokaribiana sana kufanana na Ndege ya Raisi wa Marekani Airforce one… roho hiyohiyo imewavaa manabii wa uongo wanaozuka sasahivi, nao pia wanafanya juu chini kumiliki ndege kama ya Papa, lengo lao sio kutumia hizo kumuhubiri Kristo, bali kujihubiri wao wenyewe na ufahari wao.

Papa anaabudiwa na ana pete iliyopo mkononi mwake ambao maelfu ya waumini wa kikatoliki, wamkaribiapo ni lazima waibusu, mkononi mwake…roho hiyo hiyo imewavaa manabii wa uongo leo, wanatafuta kwa bidii kuangukiwa na kusujudiwa..na hata watu kuwapa heshima fulani kubwa ya kipekee…Na mambo mengine mengi Papa anayafanya yameshaanza kuonekana kwa wanaojiita wahubiri.

Ndugu tuonapo Mambo hayo yaliyo kinyume na Kristo, ambapo hapo kwanza yalikuwa yanafanyika na mtu mmoja tu Papa, lakini sasa yanafanyika na maelfu ya watu wanaojiita watumishi wa Mungu, ni wakati wa kunyanyua vichwa vyetu juu, kwasababu ule mwisho umekaribia sana..Ile roho ya mpingakristo imeshateka ulimwengu mzima…kinachosubiriwa ni unyakuo tu! Dhiki kuu ianze..Ni kama ugonjwa! Ulioanzia kichwani kama upele lakini sasa umeenea mwili mzima…hiyo ni dalili mbaya!

Tabia hii, ikishamalizika kusambaa, itamsaidia baadaye mpingakristo kufanya kazi yake kirahisi. Atakapoanzisha chapa, afanye kazi kirahisi kwasababu watakuwepo watu wengi watakaosapoti mambo anayoyafanya…Kwasasa yataonekana si ajabu tena.

Je umeokolewa? Na kama umeokoka una uhakika na wokovu wako? Biblia inasema

2 Petro 1:10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe”

Ufunuo 3:20 “Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.

21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi”.

Bwana akubariki.

Tafadhali share na wengine


Mada Nyinginezo:

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

MPINGA-KRISTO NI NANI?

CHAPA YA MNYAMA NI NINI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UMEBEBA MTOTO.

Sehemu kubwa ya ndoto tunazoziota mara kwa mara huwa hazitokani na Mungu wala shetani bali zinatokana na sisi wenyewe..

Na hizi huathiriwa aidha na shughuli tunazozifanya kila siku, au mazingira yanayotuzunguka, Kwamfano, ikiwa wewe ni kondakta wa magari, na kazi ndio hiyo unayofanya kila siku, basi tarajia kuwa ndoto utakazokuwa unaota mara kwa mara zitahusiana na ukondakta utajiona unapiga debe, au upo kwenye magari,, au kama wewe ni mkulima ambaye mara zote  unashida mashambani, tazamia pia ndogo zako nyingi usiku zitahusiana sana na mambo ya mashambani,..

Na vivyo hivyo, ndoto nyingine nyingi kama hizo zinakuja kutokana na shughuli mtu anazozifanya mara kwa mara..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno.”

Vile vile ndoto nyingine huja kutokana na mabadiliko ya mwili yetu, kwamfano ikiwa jana usiku ulilala bila kula, tazamia kuwa usiku utaota ndoto zinazoendana na vyakula vyakula aidha unakula lakini hushibi, au unakunywa, au kama ulilala ukiwa umebanwa na mkojo, tarajia kuwa usiku utaona unakojoa mara kwa mara n.k.

Isaya 29:8 “Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani; hivyo ndivyo utakavyokuwa huo wingi wa mataifa waletao vita juu ya mlima Sayuni.”

Hivyo ndoto za namna hii zinawapata watu wengi wakidhani kuwa wameoteshwa na Mungu au shetani kumbe ni ubongo wao ndio umewaotesha, nataka nikuambie sio kila ndoto ni ya kuitilia maanani, ndoto za namna hii zikikujia zipuuzie tu.. kwasababu huwa hazibebi tafsiri yoyote yamaana ya rohoni.

Kama hujafahamu bado kuzitofautisha ndoto unazoziota zinadondekea katika kundi lipi..basi Pitia kwanza hili somo kisha ndio tuendelee..>>> NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?

Sasa Ikiwa ndoto uliyoota unaamini haitokani na mwili wako, inakupa utata mwingi na huwa inajirudia mara kwa mara, basi lipo jambo unapaswa ujue hapo.

Kumbuka Sikuzote kitu kinachobebwa  ni mzigo, lakini tatizo sio mzigo bali ni mzigo wa aina gani umebebwa, kwamfano kuna kuota umebeba maiti, au kuota umebeba mbao, au kuota umebeba jeneza unatembea  nalo,  hapo ndipo unapopaswa kuangalia sana hicho kilichobebwa ni nini…kwasababu vyote hivyo vinaeleza hali ya mtu ilivyo rohoni.

Sasa kama umeota ubeba mtoto,  na upo ndani ya Kristo fahamu kuwa mtoto ni jukumu, na jukumu lenyewe linahusiana na uleaji. hapo ni Mungu anakuonyesha kuwa kuna jukumu amekupa, au kama halipo sasahivi basi jiandae kukutana nalo hivi karibuni..Inaweza ikawa kwenye huduma yako ya utumishi, au familia yako, au kazini kwako, au popote pale ulipo..

Hivyo unachopaswa kufanya ni kutokulalamika, unapokutana na vizuizi, wala usikasirike mambo kama hayo yakujiapo, ongeza uhusiano wako kwa Mungu. Kwasababu jukumu ni ukomavu. Inawekana Mungu amekupa watu wa kukaa chini yako, hivyo usiwachukie na kuwaona ni mzigo, kaa nao, hujui pengine Mungu ameweka Baraka zako kwako kwa kupitia hao. Au wanakutegemea wewe uwape msaada ya kiroho usiwakatae wala usikwepe hilo jukumu, hujui mbeleni watakuja kuwa nani kwako na kwa wengine..Ndivyo ilivyokuwa kwa Mariamu, hakukataa kumbeba mtoto Yesu pepote alipoambiwa aende, lakini leo hii tunajua ni jinsi gani Bwana Yesu amempa Heshima kubwa.

Mathayo 2:12 “Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.

13 Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize.”

14 Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri;

15 akakaa huko hata alipokufa Herode; ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii, akisema, Kutoka Misri nalimwita mwanangu.”

Lakini kama unajijua upo nje ya Kristo fahamu pia, Mungu anakukumbusha, unabeba jukumu ambalo halitakuwa na faida kwako mbeleni.

Lakini Pia kama unaota umebeba kitoto kisichoeleweka, kibwengo si kibwengo, kama kinakuwekea mzigo mzito usioweza kuubeba, kinakukosesha raha, basi ujue hilo ni pepo, linasimama nyuma yako kukukawiisha katika safari yako ya wokovu hapa duniani, unachopaswa kufanya ni kudumu katika maombi, ombea kila eneo ulilopo, na kila jambo unalolifanya, ili kufunga milango yote shetani anayoweza kuitumia kukurudisha nyuma..

Vile vile kama unaota unabeba jeneza fahamu hiyo ni ishara kuwa unaenda kujiangamiza mwenyewe, hivyo angalia maisha yako, kama upo nje ya Kristo tubu haraka sana na anza kuishi au kufanya mambo yanayompendeza yeye katika eneo ulilopo.

Bwana akubariki.

Group la whatsappJiunge na Group letu ya whatsapp, la masomo ya kila siku kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

MTETEZI WAKO NI NANI?

VITA BADO VINAENDELEA.

HUYU AZAZELI NI NANI TUNAYEMSOMA KATIKA(WALAWI 16:8)

UNAMFAHAMU MUNGU WA KWELI?

MAFUNUO YA ROHO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Adamu alikuwa na watoto wangapi?

Biblia inasema katika kitabu cha Mwanzo.

Mwanzo 4:1 Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa Bwana.

2 Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi”

Mtoto mwingine aliyezaliwa na Adamu na Hawa alikuwa ni Sethi.

Mwanzo 5:1 “Hiki ndicho kitabu cha vizazi vya Adamu. Siku ile Mungu alipoumba mtu, kwa sura ya Mungu alimfanya;

2 mwanamume na mwanamke aliwaumba, akawabariki akawaita jina lao Adamu, siku ile walipoumbwa.

3 Adamu akaishi miaka mia na thelathini, akazaa mwana kwa sura yake, kwa mfano wake, akamwita jina lake Sethi”

Lakini pia Biblia haiishi hapo, inasema Adamu alizaa watoto wengine wakiume na wakike baada ya kumzaa Sethi.

Mwanzo 5:4 “Siku za Adamu baada ya kumzaa Sethi zilikuwa miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake”.

Na hao watoto wakike waliozaliwa ndio waliokuja kuwa wake wa hao watoto wengine wa kiume wa Adamu.

Hivyo Biblia  haitoi idadi kamili ya watoto wa Adamu, pengine walikuwa 5 au 10 au 20 au 30, hatujui lakini zaidi ya Sethi, walikuwapo pia watoto wengine wa Adamu ambao habari zao hazikuandikwa katika biblia.

ADAMU ALIISHI MIAKA MINGAPI?

Jibu tunalipata katika Mstari wa 5

Mwanzo 5:5 “Siku zote za Adamu alizoishi ni miaka mia kenda na thelathini, naye akafa.”

Kwahiyo siku zote za Adamu ilikuwa ni miaka 980, akafa


Mada Nyinginezo:

JE! ADAMU ALIWASALIANA NA MUNGU KWA LUGHA IPI PALE BUSTANINI?

UZAO WA NYOKA NI UPI?.

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA NI UPI?.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuna Malaika wangapi?

Biblia haijataja kuna idadi gani ya Malaika walioko mbinguni…Lakini tukisoma Biblia tunaweza kujua au kupata picha kuwa kuna idadi kubwa kiasi gani ya Malaika walioko mbinguni..

Kama maandiko yanasema katika…

Mathayo 18:10 “Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni”.

Mstari huo unatuonesha kwamba kila mtu aliyezaliwa mara ya Pili, anaye malaika wake akimlinda, akipeleka habari zake njema mbele za Mungu, na akimsaidia katika Kuishikilia Imani.

Sasa hebu fikiri endapo watu wote wangempa Kristo maisha yao, ina maana kila mtu angekuwa na angalau malaika mmoja.

Hivyo mbingu haiwezi kuwa na watenda kazi wachache wa kutuhudumia sisi kiasi kwamba kuna wanadamu wanaweza kukosa Malaika wa kuwahudumia. (Malaika wa Mungu watakaa mbali nasi endapo tu tutakuwa tunajitia unajisi na dhambi), lakini sio kwamba kuna idadi ndogo….Kwahiyo kama wanadamu duniani leo tupo Bilioni 7, basi Malaika ni wengi zaidi ya hiyo idadi…Hivyo unaweza kuona ni jeshi kubwa kiasi gani lililopo mbinguni.

Na Biblia pia inaonesha wazi kwamba inawezekana mtu kutembea na Malaika zaidi ya mmoja.. Soma (2Wafalme 6:16-17).


Mada Nyinginezo:

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.

KUNDI LA MALAIKA WALETAO MABAYA.

JE! MBINGUNI KUNA MALAIKA WA KIKE?. NA JE! TUKIFIKA MBINGUNI TUTAFANANA WOTE?


Rudi Nyumbani:

Print this post

JE MUSA ALIFIA WAPI?

Jibu la swali hili tunalipata katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 34, 

Kumbukumbu 34:1 “Musa akapanda kutoka uwanda wa Moabu mpaka mlima Nebo, hata kilele cha Pisga kukabili Yeriko. Bwana akamwonyesha nchi yote ya Gileadi hata Dani;

2 na Naftali yote, na nchi ya Efraimu na Manase, na nchi yote ya Yuda, mpaka bahari ya magharibi;

3 na Negebu, na uwanja wa bonde la Yeriko, mji wa mitende, hata mpaka Soari.

4 Bwana akamwambia, Hii ndiyo nchi niliyowaapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, nikisema, Nitawapa wazao wako. Basi nimekuonyesha kwa macho yako, lakini hutavuka huko.

5 Basi Musa, mtumishi wa Bwana, akafa huko, katika nchi ya Moabu, kwa neno la Bwana.

6 Akamzika bondeni, katika nchi ya Moabu, kukabili Beth-peori; lakini hapana mtu ajuaye kaburi lake hata leo”.

Moabu kwa sasa ni maeneo ya Magharibi mwa Nchi ya JORDANI, Na Mungu alificha kaburi la Musa, ili watu wasipagueze mahali pale mahali pa ibada,  na kufanya ibada za sanamu na kufanya machukizo mbele za Mungu.


Mada Nyinginezo:

FIMBO YA HARUNI NI NINI?

NABII MUSA NI NANI?.

JE! MWANADAMU WA KWANZA KUUMBWA NI YUPI MZUNGU MWAFRIKA AU MCHINA?

NI RAHISI KWA NGAMIA KUPENYA KATIKA TUNDU LA SINDANO, JE! NI SINDANO IPI HIYO INAYOZUNGUMZIWA?


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA MTU ALIYEKUFA.

Ndoto yoyote ni lazima idondoke kati ya mojawapo ya haya makundi matatu: Kundi la kwanza ni ndoto zinazotoka na Mungu, kundi la pili ni ndoto zinazotoka kwa shetani na kundi la tatu ni ndoto zinazotoka kwa mtu mwenyewe..

Hivyo ukiweza kuelewa jinsi ya kuzigawanya ndoto zako katika makundi haya basi itakuwa ni rahisi kwako kuitafsiri ndoto hiyo bila hata kutegemea msaada kutoka kwa watumishi yeyote wa Mungu.

Kwa mfano, ndoto nyingi tunazoota sisi wanadamu, zinaangukia katika kundi hilo la tatu, yaani ndoto zinazotoka ndani yetu wenyewe, hizi zinakuja kutokana na shughuli mtu anazozifanya mara kwa mara au mazingira yanayomzunguka, kwamfano kama mtu kazi yake ni kuranda mbao siku zote, moja kwa moja atajikuta ndoto anazoota mara kwa mara zinahusiana na urandaji mbao, au labda mazingira yanayomzunguka ni ya wafugaji, hivyo kujiona na yeye anachunga ng’ombe si jambo la kushangaza..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;…..”

Au utakuta mwingine kabla hajalala labda alikuwa anasikia njaa au  kiu, hivyo ni jambo la kawaida katika ndoto za usiku huo kujiona anakula hashibi, au anakunywa maji halafu kiu hakikati, au mwingine mkojo umembana sana usiku , sasa kuota unakoja kitandani hakuepukiki.

Isaya 29:8 “Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani;…….”

Hivyo ikiwa hujahamu bado jinsi ya kujua ndoto yako inaangukia kati ya kundi lipi, fungua kwanza somo hili ulipitie kisha tuendelee..>> NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?

Sasa ndoto hii kwa sehemu kubwa inaangukia katika lile kundi la tatu yaani ndoto zinazotokana na sisi wenyewe, kwamfano, ikiwa umefiwa na mtu wako wa karibu labda tuseme baba au mama au kaka, au mjomba au hata rafiki, hawa ni watu ambao muda mwingi umekuwa nao katika maisha yako, wengine wamekulelea kwa muda mrefu wengine hata miaka 10 au 20 au zaidi, hivyo wanapokufa ghafla, si jambo la kushangaza sana kuendelea kuwaona katika ndoto zako mara kwa mara, kuota unaongea na mtu aliyefariki,  na hiyo haitokani na Mungu au shetani..bali ni wewe mwenyewe..inaweza kuendelea hivyo hivyo pengine hata hadi wakati wa kufa kwako, hivyo ukiona ndoto za namna hiyo usiogope, ipuuzie tu,

Lakini pale inapotokea ndoto ya namna hiyo inaambata na vitisho, au unapewa maagizo Fulani, au unalishwa vitu Fulani usivyovijua, au unapelekwa mahali usipopafahamu basi fahamu kuwa hiyo ndoto  ni ya kutoka kwa adui, Hivyo hapo unapaswa unapoamka kemea hiyo roho kwa jina la YESU KRISTO, mara moja na mambo hayo yataisha.

Lakini pia wakati mwingine ndoto hizi zinatoka kwa Mungu mwenyewe.. Mungu anakuonyesha kuwa kuna maisha baada ya kifo, na kwamba kama mpendwa wako alikuwa ni mtakatifu basi hajafa bali yupo hai sehemu nyingine anaishi..Lakini sio kwamba Yule unayemwona unaongea naye kwenye ndoto ndiye mwenyewe hapana, ile ni lugha tu ya ndoto Mungu anaitumia kukufikishia ujumbe unaoweza kuuelewa juu ya ndugu zako waliolala katika Kristo.

1Wathesalonike 4:13 “Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.

14 Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.”

Vilevile kama upo nje ya Kristo, bado Mungu anakuonyesha kuwa kifo cha hapa duniani sio safari ya mwisho, kwamba ipo ng’ambo nawe siku moja utafika huko utakutana na wale waliokutangulia, Sasa kama utaendelea kuwa mwovu basi sehemu yako itakuwa na wale waovu Jehanum, lakini kama utataka kuwa mtakatifu basi pia sehemu yako nawe itakuwa na wale watakatifu walio paradiso wakingojea ufufuo siku ile ya Unyakuo waende na Bwana Yesu mawinguni..

Hivyo kama bado upo nje ya Kristo unasubiri nini?. Tubu leo mgeukie yeye..Ndoto za namna hiyo ni kuonyesha kuwa Mungu anataka umalize safari yako salama hapa duniani, ufikie mwisho mzuri…Siku ile ukutane na watakatifu wengine kwa pamoja mkaishi milele na Mungu.

Ubarikiwe sana..

Group la whatsappJiunge na Group letu ya whatsapp, la masomo ya kila siku kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

MTETEZI WAKO NI NANI?

NI JAMBO GANI LINALOMTAMANISHA SANA BWANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?

VITA DHIDI YA MAADUI.

KARAMU YA MWANA-KONDOO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI MOTO NA UPEPO VINAWAKILISHA TABIA ZA MUNGU?

Shalom, mtu Mungu nakukaribisha tujikumbushe tena Neno la Mungu kwa yale ambayo tulishawahi kujifunza huko nyuma lakini leo tutaangalia kwa upana zaidi, na naamini utaongeza kitu kipya katika ukristo wako(Wafilipi 3:1), Biblia inaufananisha utendaji kazi wa Mungu na vitu viwili cha kwanza ni Moto na cha pili ni Upepo. Bwana Yesu alipomuhubiria Nikodemo habari za kuzaliwa mara ya pili kwa Roho Mtakatifu, Nekodemu alistaajabia sana na kusema inawezekanikaje mtu kuzaliwa mara ya pili lakini Bwana Yesu akamwambia maneno haya:

Yohana 3:7 “Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili.

8 Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila mtu aliyezaliwa kwa Roho’’.

Sasa kama ukiichunguza tabia ya Upepo, wataalamu wanasema kuwa Upepo hauna sauti yoyote, Na Kama ni hivyo basi kile tunachokisikia ni nini?, wakati mwingine upepo ukivuma utasikia kama mluzi Fulani hivi unajipiga, au maporomoko Fulani au vitu Fulani vidogo vidogo vinadondoka,n.k. jibu ni kuwa ule upepo wakati unapovuma unakutana na vitu vingi katika safari yake, sasa pale unaposuguana na vitu hivyo inasababisha kutokee sauti fulani, au ule upepo ukisukuma vile vitu inasababisha vile vitu kugongana vyenyewe kwa vyenyewe na kusababisha sauti pia, kwamfano upepo ukikutana na mti, ukipita katikati yake unasababisha matawi kugongana gongana yenyewe kwa yenyewe na hapo hapo kelele ya matawi inasikika, vivyo hivyo unapokutana na vipande vidogo vidogo vya mawe na uchafu, vinapogongana gongana ndio sauti hapo hapo inatokea na hapo ndipo mtu anapogundua kuwa eneo hilo lina upepo mkali au mdogo..Lakini kama upepo ukiwa unapita tu hewani na haukutani na kizuizi au kipingamizi chochote basi kamwe hutakaa usikie au ujue kama kuna upepo wowote unapita hapo iwe ni mkali au mdogo..Eneo hilo litakuwa kimya na tulivu kuliko hata kitu chochote ulichowahi kukisikia.

Na ndiyo maana Bwana Yesu alimfananisha Roho Mtakatifu kama Upepo uvumao ndani ya mtu aliyezaliwa mara ya pili..Hawezi kumwona Roho jinsi anavyokuja juu yake wala huwezi kumchunguza jinsi anavyofanya kazi ndani yake, lakini kitu kitakachomtambulisha kama anavuma juu yake au la ni ile sauti anayoitoa yeye mwenyewe.. Na sauti hiyo ni tabia yako na mwenendo wako baada ya kuzaliwa mara ya pili.

Kwa jinsi utakavyoanza kuonyesha tabia nyingine ghafla, ulimwengu utajiuliza mtu huyu ni kitu gani kimemkumba kinachomfanya aishi hivi, au onyeshe tabia za namna hii, lakini kwamwe hawatapata jibu wala kukiona..Kwasababu Roho Mtakatifu ni kama upepo hautambuliki na ulimwengu, wala ulimwengu hauwezi kumtambua.

Yohana 14:16 “Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;

17 ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu”.

1Wakorintho 2:14 “Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.”

Hivyo ikiwa wewe umezaliwa mara ya pili kweli kweli kuna mambo utagundua Mungu ameyageuza ndani yako, utashangaa ile kiu ya kutamani mambo maovu imekufa ndani yako, utashangaa unapenda kila wakati kujifunza Neno la Mungu jambo ambalo hapo kwanza ulikuwa huwezi, utajikuta hupendi tena kukaa karibu na watu wabaya au waovu au zile kampani mbaya ulizokuwa nazo hapo nyuma, watu wataanza kukushangaa umekuwaje au umeingiliwa na nini. Sasa ukishaona hivyo ujue ni upepo wa Roho unavuma ndani yako, usihangaike kuwathibitishia kuwa huyo ni Mungu hawatakuelewa, ni rahisi wao kukutafsiri umedanganywa na walokole, au umepotoshwa…usiwasikilize hapo fahamu kuwa ni Roho Mtakatifu anatenda kazi ndani yako, wewe itii tu, usiichunguze sana, kwasababu hata wewe ukiichunguza ni ngumu kujua chanzo chake ni wapi na mwisho wake ni wapi, lakini wewe itii hiyo na uifuate maadamu inakupeleka kumpenda na kumtafuta Mungu zaidi..

Na ndio maana tunasema, mtu hawezi kudai amezaliwa mara ya pili na huku nyuma bado maisha yake kwa nje yapo vile vile hayajabadilika, ni wazi kuwa Roho Mtakatifu bado hajaanza kupita juu ya huyo mtu.

Tabia nyingine ya Roho Mtakafu ni Moto, Kama vile biblia inavyosema..

Mathayo 3:11 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto”.

Moto nao vile vile unatabia kama ya upepo huwa hautoi sauti, sauti yake huwa inakuja kutoka katika vile vitu unavyovichoma, kichaka kikiwashwa moto hapo nje, hata kama upo ndani utajua tu nje kuna moto unawaka kwa jinsi kile kichaka kitakavyokuwa kinatoa kelele zake. Na sauti inaweza kuwa kubwa kulingana na kitu kinachochomwa, kwamfano kama inachomwa nazi pale inapopasuka utasikia inapasuka inatoa mlimo mkubwa kama bomu tofauti na karatasi.. lakini pia tabia nyingine ya moto ni kwamba sio vitu vyote inaviteketeza, kwa mfano ukiweka karatasi na dhahabu pamoja, halafu vyote ukavichoma, mwisho wa siku utagundua lile karatasi limeteketea lote lakini ile dhahabu imezidi kuwa mpya ziadi.

Na ndivyo ilivyo Roho Mtakatifu anavyombatiza mtu kwa moto, ni ngumu kumwona, lakini kazi zake utaziona, vile vitu vyote dhaifu ambavyo ni uovu vilivyokuwa ndani yake ataviteketeza mara moja, lakini vile vitu imara na vizuri ndani ya mtu ni kama dhahabu hivyo vinazidi kuwa imara.

Vile vile Roho Makatifu hawabatizi tu watu wema, bali pia na watu waovu, biblia inasema hivyo katika Mathayo 5:45 “kwamba huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki”. lakini kwao inakuwa ni kinyume chake, badala ya kuimarishwa wanateketezwa, biblia inasema..

Waebrania 12:29 “maana Mungu wetu ni moto ulao.”

Na kibaya zaidi moto huu unapowateketeza hawajui kama unawateketeza kwasababu huwa hautoi sauti, utajua tu unawateketeza kwa kule kulalamika kwao na kutaabika kwao kiroho huo ndio uthibisho kuwa moto wa Mungu unapita juu yao kuwala. Na moto huo huo hauishii hapa duniani ndio ule unaoendelea mpaka kwenye ziwa la moto.

Usiulaumu moto na kuuona kuwa ni mbaya kwasababu ulikuchomea nyumba yako, ukasahau kuwa moto huo huo ndio unaokupikia chakula kila siku, ndio unaotumia kuchome taka, ndio unaokupa nishati kila siku, unaweza kukufanya kutazama tv,radio, unaoweza kukufanya kuchaji simu yako na kusoma ujumbe huu, unaweza kupigia pasi nguo zako ukawa mtanashaji, unaweza kusafiri kwa kutumia chombo chako cha moto n.k..

Vivyo hivyo usilaumu kwanini watu waovu watateketezwa kwa moto, kikubwa tu ni kujiepusha na ghadhabu na hasira ya Mungu kwasababu ni kawaida ukienda kinyume na sheria ya moto, utakuunguza hata wewe mwenyewe, moto unahitaji umakini wa hali ya juu kuendana nao. Kadhalika Moto wa Roho Mtakatifu unahitaji umakini wa hali ya juu kuendana nao vinginevyo ni rahisi kujikuta tunajipeleka wenyewe jehanamu ya moto.

Ukiyajua hayo na huku bado upo nje ya Kristo hakuna sababu ya wewe kuendelea kuwa hivyo,..Kwanini usimruhusu Roho Mtakatifu ayaumbe maisha yako upya?, kwanini usiruhusu moto wake na upepo wake uanzee kupita juu yako na kukuimarisha na kukupeleka kule atakapo? Jambo hilo la heri na neema ni bure kabisa.. Tubu hapo ulipo kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi zako zote, kumbuka kutubu ni kugeuka, na kuacha kile ulichokuwa unakifanya ambacho sio sahihi.. Na Bwana akishaona umedhamiria kabisa kwa moyo wako wote wote kugeuka basi yeye ataanza jukumu la moja kwa moja kukugeuza, na bila kuchelewa nenda katafute mahali ubatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi kwa jina la Yesu Kristo kukamilisha wokovu wako, naye atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu, kulingana na Matendo 2:38..Na kuanzia huo wakati na kuendelea utakuwa umehesabiwa kuwa mojawapo wa kondoo wa Bwana unayestahili uzima wa milele, na kuhesabiwa haki bure kwa Imani yako.

Bwana akubariki sana. Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine. Na Bwana atakubariki.


Mada Nyinginezo:

IMANI NI KAMA MOTO.

UPEPO WA ROHO.

NUHU WA SASA.

MATOWASHI NI WAKINA NANI?

NINI MAANA YA HAYA MANENO ALIYOSEMA BWANA ; TULIWAPIGA FILIMBI WALA HAMKUCHEZA; TULIOMBOLEZA WALA HAMKULIA?


Rudi Nyumbani:

Print this post