Title April 2024

Mwujiza wa kwanza wa Bwana YESU ni upi, na una ujumbe gani?

Swali: Muujiza wa kwanza wa Bwana YESU ulikuwa ni upi?


Jibu: Mwujiza wa kwanza wa Bwana YESU ni ule wa Kana ya Galilaya, ambapo aligeuza maji kuwa Divai.

Yohana 2:1 “Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.

2  Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.

3  Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.

4  Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia.

5  Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni.

6  Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu.

7  Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu.

8  Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka.

9  Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi,

10  akamwambia, Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa.

11  MWANZO HUO WA ISHARA YESU ALIUFANYA HUKO KANA YA GALILAYA, akaudhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini”.

Mstari huo wa 11 unatudhihirishia wazi kuwa hiyo ndio iliyokuwa ishara ya kwanza kufanywa na BWANA YESU mbele ya wanafunzi wake.

Sasa kujua kwa mapana ujumbe uliopo nyuma ya muujiza wa kwanza wa Bwana YESU wa Kana ya Galilaya fungua hapa >>Kwanini Bwana YESU ageuze maji kuwa Divai? Na ni ujumbe gani tunapata?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI NINI BWANA ANATAKA KUTOKA KATIKA MUUJIZA ALIOKUFANYIA?

JE UMEJIANDAA KUTIMIZA UNABII UPI?

Kumaka ni nini katika biblia? (Mathayo 8:27)

SIRI KUU NNE (4), UNAZOPASWA UZIFAHAMU NDANI YA KRISTO.

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

MIMI NIKO AMBAYE NIKO

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini Bwana YESU ageuze maji kuwa Divai? Na ni ujumbe gani tunapata?

Swali: Kuna nini katika Divai mpaka Bwana YESU ayageuze maji kuwa Divai?


Jibu: Hakukuwa na chochote maalumu au cha kipekee katika Divai.

Sababu ya Bwana YESU kuyageuza maji kuwa Divai na si kinywaji kingine ni kwasababu ndicho kinywaji kilichokuwa kimepunguka pale! (Kulingana na zile taarifa alizoletewa na mama yake).. Endapo kama ingekuwa ni chakula ndicho kilichopunguka basi Bwana YESU angefanya muujiza wa chakula kuongezeka cha kuutosha ule umati wote, huenda angefanya muujiza kama ile ya  Mikate na Samaki, alipolisha maelfu ya watu. (Marko 6:38-44 na Luka 9:13-17).

Sasa kabla ya kuangalia ni ujumbe gani tunapata kwa mwujiza ule, hebu kwanza tuangalie matokeo ya kukosa Divai katika ile Harusi.

Kufahamu kwa kina matumizi ya Divai katika biblia fungua hapa >>MATUMIZI YA DIVAI.

Kulingana na Desturi za kiyahudi ilikuwa ni aibu kubwa sana arusi ikose Divai, au chakula…Hivyo ni aibu kubwa sana kwa wanafamilia, sawasawa tu sasa sherehe ikipungukiwa na chakula inakuwa ni aibu kubwa kwa walioandaa na huzuni na karaha!..

Sasa kitendo cha Bwana YESU kubadili yale maji na kuwa Divai, tena yenye kuwatosha watu wote ni kitendo KILICHOWAONDOLEWA AIBU WANA ARUSI NA WAZAZI.. vile vile ni kitendo kilichowaondolewa huzuni, na masononeko na fadhaa.. na ni kitendo kilichowapa heshima. Ndio maana utaona yule mkuu wa Meza alimfuata Bwana arusi kumsifu badala ya Bwana YESU.

Sasa ni ujumbe gani mkuu tunaupata hapo?

Ujumbe mkuu si upekee wa Divai.. bali ni Faida ya BWANA YESU ndani yetu au katikati yetu. Kuwa yeye anapoingia ndani yetu anazichukua aibu zetu, na fadhaa zetu na masikitiko yetu, na kutuheshimisha na kutuondolea aibu zetu..

Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.

5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.

Unauona upendo wa YESU kwetu pale tunapomkaribisha na kumtwika fadhaa zetu?.. Wale wanaharusi waliona thamani ya YESU na kumwalika katika sherehe yao, na pale walipopungukiwa ndipo Kristo alipozuchukua fadhaa zao na aibu yao..

Wenye harusi , (wao hawakumwalika Bwana kwasababu walijua divai itaisha ili baadaye wamwite awageuzie maji kuwa Divai).. La! Ile ilitokea tu kama dharura na ndipo Bwana akafanya miujiza.. Wao lengo lao kubwa lilikuwa ni kumwitaji YESU ndani ya harusi yao, na si wamtumie.

Na sisi leo hatupaswi kumfuata BWANA YESU kwasababu tu tunataka uponyaji, au heshima au kuinuliwa kimaisha (watu wote waliomfuata Bwana YESU kwa haja kama hizo aliwakimbia Soma Yohana 6:25-26)..Lakini tumfuate Bwana YESU kwasababu tunataka uzima kwanza, na kuyafanya mapenzi yake na hayo mengine yawe ni dharura tu, kama wale waliomwalika.

Ukishahikiki kwamba uzima upo ndani yako, ndipo tumtwike hayo mengine..

1Petro 5:7 “huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Manabii walisema “Neno la Mungu likanijia” ..Maana ya hili neno ni nini?.

Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.

WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.

BUSTANI YA NEEMA.

MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Bwana Yesu alizaliwa katika nchi gani?

Bwana YESU KRISTO alizaliwa katika Nchi/Taifa la ISRAELI, lililopo mashariki ya kati. Na mji aliozaliwa ni Bethlehemu ambao ulikuwa katika urithi wa kabila la YUDA.

Mika 5:2 “Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele”.

Pamoja na kwamba Bwana YESU alizaliwa Bethlehemu kulingana na unabii huo wa Mika, lakini hakulelewa katika huo mji wa Bethlehemu badala yake wazazi wake waliishi mahali palipojulikana kama NAZARETI, Mji mdogo sana uliopo kaskazini mwa Taifa hilo la Israeli, na huko ndiko Kristo alikokulia, ndio maana mahali pengine anajulikana kama Mnazorayo (yaani mtu wa Nazareti).

Mathayo 2:23 “akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo”.

Lakini pia Mji huo wa Nazareti ulikuwa ndani ya Wilaya iitwayo Galilaya, wakati mji wa Bethlehemu aliozaliwa Bwana YESU ulikuwa katika Wilaya iliyoitwa Yudea au Uyahudi.

Wilaya ya Galilaya ndio uliyojumuisha miji mingine midogo midogo kama Kapernaumu na Korazini na Bethsaida, ambapo wanafunzi wengi wa Bwana YESU walitokea katika hiyo miji, na ndio miji ambayo iliona miujiza mingi ya Bwana YESU lakini haikutubu (Mathayo 11:21)…. Wakati Wilaya ya Uyahudi ndio iliyobeba miji ya Bethlehemu pamoja na Yerusalemu.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba BWANA YESU alizaliwa Bethlehemu ya Uyahudi na kulelewa Nazareti ya Galilaya, na alifia YERUSALEMU na kuzikiwa hapohapo, na kufufuka hapo hapo YERUSALEMU. Na sasa yupo hai na atarudi tena mara ya pili na siku hizo zimekaribia kulingana na unabii wa biblia.

Je umeokoka?

Bwana YESU ANARUDI.

Kama unatamani kuokoka basi fuatiliza sala hii >>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Bwana Yesu alizaliwa mwaka gani?

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA

Yerusalemu ni nini?

AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya “mwondokeeni mtu mwenye mvi? (Walawi 19:32)”

Jibu: Turejee,

Walawi 19:32 “Mwondokeeni mtu mwenye mvi; heshimuni uso wa mtu mzee; nawe mche Mungu wako, Mimi ndimi Bwana”.

Maana ya kumwondokea ni “kumsogelea au kumkaribia ili kumsikiliza”. Hivyo biblia iliposema mwondokeeni mtu mwenye mvi, maana yake “tumsogeleeni mtu mwenye mvi na kumsikiliza”..

Na kwanini tumsogelee mtu/watu wenye mvi?..Ni kwasababu “kuna hekima katika wazee, kwani wameishi muda mrefu na kukutana na mengi na kujifunza mengi”. (wazee walio ndani ya KRISTO).

Ayubu 12:12 “Wazee ndio walio na hekima, Na katika kuishi siku nyingi iko fahamu”.

Soma pia Ayubu 32:6-7 na Mithali 23:22.

Hivyo ukitaka mashauri sahihi kuhusu maisha basi watafute walio na mvi, (yaani wazee) walio ndani ya Kristo, watakuambia au ukutahadharisha na mengi…

> Vile vile ukitaka maarifa na ushauri sahihi kuhusu ndoa, kazi au elimu watafute wenye mvi walio ndani ya KRISTO watakushauri na kukutahadharisha mambo yaliyo sahihi na yale yasio sahihi.

> Vile vile ukitaka mashauri sahihi ya kiroho watafute wenye mvi za kiroho watakushauri mambo sahihi.

Na mambo mengine yote ni hivyo hivyo, wenye mvi wanafahamu Zaidi kuliko vijana.

Lakini hasemi tu! Kumwondokea mwenye mvi… bali pia anasema “heshimuni uso wa mzee”. Maana yake mzee/wazee wanapaswa kuheshimiwa sana…. ni kosa kumvunjia mzee heshima, hata kama kafanya jambo lisilo sahihi mbele ya macho yako. Si ruhusa kumkemea mzee kama wanavyokemewa vijana au watoto.

 1Timotheo 5:1 “Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu;

2  wanawake wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TUTAMKARIBIA MUNGU KWA IDADI YA MVI ZETU ROHONI.

HATA WAKATI WENU WA MVI NITAWACHUKUENI. (Isaya 46:3)

UTAKAPOKUWA MZEE, UTAINYOSHA MIKONO YAKO. NA MWINGINE ATAKUFUNGA

WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?

MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.

Rudi Nyumbani

Print this post

Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru.

Huwenda ukawa unajiuliza, Bwana Yesu alikuwa na maana gani kusema, Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru? . Je huko gizani ni wapi, na sirini ni wapi? Je yeye huwa anazungumza gizani.

Mathayo 10:26  “Basi, msiwaogope, kwa maana hakuna neno lililositirika, ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa, ambalo halitajulikana.

27  Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba”

JIBU: Ni vema tukaifahamu tabia ya Bwana wetu Yesu Kristo, katika kufundisha jinsi ilivyokuwa alipokuwa anazungumza na watu mbalimbali. Yapo maneno au mafundisho au mafunuo aliyoyaweka wazi kwa watu wote, lakini yapo ambayo hakuyaweka wazi kwa kila mtu.

Mahubiri yake mengi aliyazungumza hadharani, lakini mengine haikuwa hivyo, kwamfano upo wakati alijitenga akapanda milimani, na wale waliomfuata ndio aliowafundisha (Mathayo 5:1), wakati mwingine aliingia nyumbani, hakutana kujulikana kwasababu alikuwa akitaka kuwafundisha wanafunzi wake tu, peke yao (Marko 9:29-31), wakati mwingine aliwaponya watu akawataka wasimdhihirishe, (Marko 1:44), wakati mwingine alijifunua utukufu  wake, kwa wale tu waliokwenda naye kuomba mlimani, uso wake ukawa unameta meta, kama jua, alipomaliza  akawakataza wasimwambie mtu, mpaka atakapofufuka (Mathayo 16).

Hayo ni mazingira mbalimbali, ambayo Yesu alisema nao bila kujulikana na kila mtu, Sasa mazingira hayo ndio aliyaita  “Gizani, au sirini”

Hii ni kufunua kuwa hata sasa Yesu anazungumza hadharani, lakini pia anazungumza sirini. Na yale ya sirini huwa ni makubwa zaidi na ndio maana haitaji yajulikane na kila mtu.

Watu wengi wanamsikia Yesu hadharani, lakini hawamsikii sirini. Hadharani, ni pale unaposikia mafundisho kanisani, mahubiri, semina, mkutano  n.k. Ni kweli Yesu atakufundisha mengi kupitia matumishi wake mbalimbali, na yatakujenga na ni muhimu ufanye hivyo.

Lakini lazima pia sirini pa Yesu uwe napo.

Je hapo ni wapi?

Ni eneo lako la utulivu la kimaombi na kutafakari”.

Ni muhimu sana kila mkristo, awe na wakati wake maalumu kila siku alioutenga wa kuzama uweponi, katika maombi, kusoma Neno na kutafakari shuhuda za Mungu maishani mwake. Ni muhimu sana.

Zaburi 91:1 AKETIYE MAHALI PA SIRI PAKE Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.

Mathayo 6:6  Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.

Hapa Yesu anataka uingie gharama, kidogo ili umsikie, au akuhudumie, au akufundishe. Ndio mfano wa wale waliomfata milimani. Vivyo hivyo na wewe, ingia gharama ya kudumu uweponi mwa Mungu. Ukiona mchana pana usumbufu, usiku ni muda mzuri sana, kuamka, tena masaa yako kadhaa kila siku,. Kumpa Bwana nafasi ya kukufundisha.

Ukiwa wa namna hii, hutamkosa Bwana popote pale. Kaa mahali pake pa siri. Kwasababu yupo pia sirini, akupe mambo mambo utayasema hadharani wakati fulani.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kujazi ni nini? (Mathayo 6:4)

UMEFUNGWA KATIKA GIZA NA UVULI WA MAUTI?

AGIZO LA UTUME.

MKUU WA GIZA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya sulubu/ sulubisha?

Neno sulubu huzaa kusulibisha/kusulubisha,

Maana ya Sulubu, ni kuadhibisha kwa kuning’iniza kwenye mti wa msalaba, au nguzo iliyonyooka, kwa kufungwa au kugongelewa miguu na mikono, na kuacha hapo mpaka ufe.

Hii ni aina ya adhabu ya kifo, ambayo ilitumika zamani, kwenye falme zilizokuwa na nguvu na katili kama Rumi.

Watu walioshitakiwa kwa makosa makubwa ikiwemo uhaini, au uuaji, uvunjaji amani, hawakupewa adhabu ya kawaida ya kifo kama vile kukatwa kichwa na kufa mara moja,. Bali walipewa adhabu kali kama hii, lengo lake ni kumfanya Yule mshitakiwa kupitia mateso makali ya muda mrefu kabla ya kufa, kwasababu, baada ya kuning’inizwa kwake pale msalabani itamchukua siku tatu mpaka wakati mwingine wiki hadi kufa. Hivyo kipindi chote hicho unatakuwa unateseka tu pale mtini.

Hiyo ndio adhabu waliyoichagua kwa mwokozi wetu Yesu Kristo, ambaye hakuwa na hatia yoyote, wala kosa, jambo ambalo hata mtawala yule Pilato alilishuhudia kuwa hakukuwa na uovu wowote ndani yake. (Luka 23:4). Lakini kwasababu ilipasa maandiko yatimie ili sisi tupate ukombozi mkamilifu, ndio maana ilimpasa Yesu aadhibiwe vikali, ili mimi na wewe tupokee ONDOLEO LA DHAMBI. Kwa kifo chake.

Gharama aliyoilipa ni kubwa sana, kusulubiwa uchi wa mnyama, bila nguo, kudhalilishwa na kupigwa, na kuharibiwa mwili wote. Ni kwasababu mimi na wewe tupokee msamaha wa dhambi, tuepushwe na hukumu ya milele ya jehanamu ya moto.

Ndio maana maandiko yanasema..

Waebrania 2:3  sisi je! Tutapataje kupona, tusipojali wokovu mkuu namna hii? Ambao kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia.

Je! Umempokea Yesu maishani mwako?

Ikiwa ni la! Basi waweza kufanya hivyo sasa, kwa kubofya hapa ili upate mwongozo wa sala hiyo. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ALIFANYIKA SADAKA KWA AJILI YETU!

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Rudi Nyumbani

Print this post

SIFA SITA (6), ZINAZOIKAMILISHA ILE SIKU YA BWANA ITISHAYO.

Nyakati tunazoishi ni za hatari kubwa, zaidi hizo zinazokuja wakati si mwingi ndio za hatari mno. Watu wengi hawajui kuwa mwisho umekaribia sana, dunia imekwisha, na kwamba SIKU YA BWANA, ipo mlangoni.

Siku ya Bwana ni nini?

Siku ya Bwana ni kipindi fulani maalumu ambacho Mungu amekiandaa ili kuuharibu huu ulimwengu pamoja na watu wote waovu waliopo duniani, na mifumo yao mibovu. Na hiyo itakuja baada ya kanisa la Kristo kunyakuliwa 

Tukisoma katika kitabu cha Sefania tunaelezwa kwa urefu juu ya sifa kuu za siku hiyo itakavyokuja. 

Ametaja sifa zake sita (6), kwa kuziita “siku ya”..”siku ya”…”siku ya”

Tusome..

Sefania 1:14-16

[14]Hiyo siku ya BWANA iliyo kuu i karibu; I karibu, nayo inafanya haraka sana; Naam, sauti ya siku ya BWANA; Shujaa hulia kwa uchungu mwingi huko!

[15]Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu,

[16]Siku ya tarumbeta na ya kamsa, Juu ya miji yenye maboma, Juu ya buruji zilizo ndefu sana.

1) Anaanza kwa kusema ni Siku ya ghadhabu.

Ghadhabu ni zao la hasira, na hasira hufuatana na mapigo. ndio hapo tunaposoma kitabu cha ufunuo 16, tunaona kipindi hicho kikifika wale malaika saba watavimimina vile vibakuli vyao saba vya ghadhabu ya Mungu juu ya nchi. na kitakachofuata kwa tendo lile ni mapigo, ndio hapo utaona majipu mabovu, yanawatokea wanadamu, na tena jua linashushwa na kiwaunguza watu, mpaka wanafikia hatua ya kumtukana Mungu.

Ufunuo 16:8-9

[8]Na huyo wa nne akakimimina kitasa chake juu ya jua, nalo likapewa kuwaunguza wanadamu kwa moto. 

[9]Wanadamu wakaunguzwa maunguzo makubwa, nao wakalitukana jina la Mungu aliye na mamlaka juu ya mapigo hayo; wala hawakutubu wala kumpa utukufu. .

2) Siku ya fadhaa na dhiki.

Dhiki na fadhaa ni taabu ambazo mtu anazipata hususani kutoka katika mazingira ya nje. Ukiendelea kusoma sura ile ya 16, utaona mito, chemchemi na bahari zote zinageuzwa kuwa damu, wanadamu wanakosa maji. hofu na mashaka ya mabadiliko ya nchi. Duniani hatakuwa ni mahali penye utulivu, tengeneza picha unaishi katika dunia ya namna hii, utastahimili vipi. Bwana anasema wanadamu watafuta kifo, lakini kifo kitawakimbia.

Ufunuo 16:3  Na huyo wa pili akakimimina kitasa chake juu ya bahari, ikawa damu kama damu ya mfu, na vitu vyote vyenye roho ya uhai katika bahari vikafa.

4  Na huyo wa tatu akakimimina kitasa chake juu ya mito na chemchemi za maji; zikawa damu. 5  Nami nikamsikia malaika wa maji akisema, Wewe u mwenye haki, uliyeko na uliyekuwako, Mtakatifu, kwa kuwa umehukumu hivi;

6  kwa kuwa walimwaga damu ya watakatifu na ya manabii, nawe umewapa damu wainywe; nao wamestahili

3) Siku ya uharibifu na ukiwa

Sio tu mapigo na dhiki, lakini pia kuharibiwa kwa huu ulimwengu na mifumo yake kutafuata, kwasababu biblia inasema siku hiyo kutatokea tetemeko kubwa la ardhi ambalo halijawahi kutokea tangu dunia kuumbwa, mpaka visiwa kuhama, inasema moto utatokea kuharibu huu ulimwengu, mfano wa sodoma na gomora na mfano wa kipindi cha gharika.

2 Petro 3:10-12

[10]Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. 

[11]Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa, 

[12]mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka? 

4) Siku ya giza na utusitusi.

Giza na utusitusi unaozungumziwa hapa ni ule wa rohoni. ni kipindi ambacho watu watautafuta uso wa Mungu lakini hawatauona, ndio maana Yesu alisema imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyetupeleka maadamu ni mchana, usiku waja asioweza mtu kufanya kazi. watu watamwita Mungu, lakini hakutakuwa na majibu yoyote.

Mithali 1:27 Hofu yenu ifikapo kama tufani, Na msiba wenu ufikapo kama kisulisuli, Dhiki na taabu zitakapowafikia.  28 Ndipo watakaponiita, lakini sitaitika; Watanitafuta kwa bidii, wasinione.  29 Kwa kuwa walichukia maarifa, Wala hawakuchagua kumcha Bwana.  30 Hawakukubali mashauri yangu, Wakayadharau maonyo yangu yote

5) Siku ya mawingu na giza kuu. 

Vilevile kwa jinsi dunia hii itakavyoharibiwa jua na mwezi na nyota vitazuiliwa.. duniani kutakuwa na giza ambalo halijawahi kutokea, na hayo ndio yatakuwa yale mapigo ya mwisho mwisho kabisa yatakayokuwa yanaukaribisha ujio wa pili wa Yesu duniani.

Vilevile wingu zito litatandaa angani, mawe mazito yatashuka duniani kama talanta, jiwe lenye uzito wa kg 34, hatujui itakuwa ni mvua ya namna gani, hiyo.

Ufunuo 16:18-21

[18]Pakawa na umeme na sauti na radi; na palikuwa na tetemeko la nchi kubwa, ambalo tangu wanadamu kuwako juu ya nchi hapakuwa namna ile, jinsi lilivyokuwa kubwa tetemeko hilo. 

[19]Na mji ule mkuu ukagawanyikana mafungu matatu, na miji ya mataifa ikaanguka; na Babeli ule mkuu ukakumbukwa mbele za Mungu, kupewa kikombe cha mvinyo ya ghadhabu ya hasira yake. 

[20]Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena. 

[21]Na mvua ya mawe kubwa sana, ya mawe mazito kama talanta, ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu. Wanadamu wakamtukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe; kwa maana pigo lake ni kubwa mno.

6) Anasema pia ni siku ya tarumbeta na ya kamsa.

Kamsa ni kelele za vita. Maana yake katika kipindi hicho cha siku ya Bwana, vita vitakuwepo, ndio ile vita ya mwisho ijulikanayo kama Harmagedoni.Mataifa yote yatahusika. lakini Bwana awataua watu wengi sana. damu nyingi sana zitamwagika. ni nyakati ambayo hakutakuwa na shujaa, kila mtu ataomboleza mpaka mashujaa, wafalme na matajiri wote hao watalia sana, pesa zao hazitawasaidia wataomba milima iwaangukie wafe haraka, kuliko kushuhudia huo mfululizo wa mapigo ya Mungu mwenyezi.

Na ndio maana ukimalizia kusoma mistari inayofuata pale kwenye kitabu cha Sefania anasema

Sefania 1:17-18

[17]Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda BWANA dhambi; na damu yao itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi. 

[18]Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya BWANA; bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu wote wakaao katika nchi hii, naam, ukomo wa kutisha. 

Ndugu yangu, ikiwa unyakuo ukipita leo, fahamu haya utayashuhudia, wakati huu si wa kumbelelezewa wokovu, ni kuamka na kuikimbilia neema, nyakati mbaya zimekaribia, haya mambo ya duniani yatakufikisha wapi? uhai wako umefichwa wapi? Ukifa leo huko uendako utakuwa mgeni wa nani.Kwasababu huko nako kuna mateso makali vilevile kama hapa.

Embu dhamiria kutubu na kumgeukia Bwana Yesu leo, akupe msamaha wa dhambi bure. Hukumu ya Mungu inatisha. 

Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu maishani mwako. Na unatamani leo Yesu akutue hiyo mizigo ya dhambi. Basi waweza kusali sala hii kwa imani. Ukijua Kristo wakati wote yupo kutuokoa. Kumbuka kinachotangulia ni kuamini. Kisha ndipo kukiri.

Hivyo

Hapo ulipo piga magoti, kisha dhamiria moyoni mwako kuyasema maneno haya, na moja kwa moja leo, utapokea msamaha wa dhambi zako hapo hapo ulipo, 

Sema.

Ee Bwana Yesu asante kwa kuja kwako duniani, kutukomboa sisi wanadamu tuliokuwa tumepotea, kwa kifo chako pale msalabani na kufufuka kwako. Ninaamini kuwa wewe ndio Bwana na mwokozi, nami napokea neema uliyonipa bure ya ondoleo la dhambi, tangu leo ninakubali kufanyika mwana wako, na kugeuka kuacha njia mbaya za kale. Asante kwa kuwa unanipa nguvu hiyo na kuliandika leo jina langu katika kitabu cha uzima. Nami nafanyika kiumbe kipya. Asante kwa kunipokea, asante kwa kunisamehe, Asante kwa kunifanya mwana wako.  Ninaomba nikiamini katika jina la Yesu Kristo Amen.

Basi ikiwa umesema sala hiyo toka moyoni kwa imani. Tayari umeshaupokea wokovu. Na hivyo hatua zilizobakia kwako ili kuitimiza haki yote, ni wewe kubatizwa. Tafuta mahali wabatizwapo kwa maji tele, na kwa jina la Yesu Kristo.  Ikiwa utahitaji msaada pia waweza kuwasiliana nasi kwa namba zetu chini.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Rudi Nyumbani

Print this post

HAJIRI NI KAMA MLIMA SINAI ULIOKO ARABUNI.

(Mfululizo wa masomo yahusuyo Uhuru wa Roho na Utumwa wa sheria).

Jina la Bwana YESU, MKUU WA UZIMA libarikiwe. Karibu tujifunze biblia, Neno la MUNGU wetu lililo Taa na Mwanga wa njia yetu (Zab. 119:105).

Biblia inamfananisha HAJIRI, (yule aliyekuwa “kijakazi” wa Sara na Ibrahimu) na YERUSALEMU YA DUNIANI. Na tena inamfananisha “Ishmaeli” aliyekuwa mwana wa Hajiri na “wale wote walio chini ya utumwa wa sheria” waliopo pale katika mji wa YERUSALEMU uliopo Israeli.

Vile vile “Sara” aliye mwungwana (yaani huru) inamfananisha na YERUSALEMU YA MBINGUNI (mji wa kimbinguni) na mtoto wake “Isaka” inamfananisha na “watu wote wa kimbinguni” (yaani walio huru na utumwa wa sheria)..ndivyo maandiko yanavyosema..

Wagalatia 4:22 “Kwa maana imeandikwa ya kuwa, Ibrahimu alikuwa na wana wawili mmoja kwa mjakazi, na mmoja kwa mwungwana.

23  Lakini yule wa mjakazi alizaliwa KWA MWILI, yule wa mwungwana KWA AHADI.

24  Mambo haya husemwa kwa mfano; kwa maana hawa ndio kama maagano mawili, moja kutoka mlima Sinai, lizaalo kwa utumwa, ambalo ni Hajiri.

25  Maana HAJIRI NI KAMA MLIMA SINAI ULIOKO ARABUNI, umelingana na Yerusalemu wa sasa; kwa kuwa anatumika pamoja na watoto.

26  Bali Yerusalemu wa juu ni mwungwana, naye ndiye mama yetu sisi.”

Sasa maelezo marahisi ya maandiko haya ni kwamba Wana wa Israeli walipokea sheria kutoka kwa Musa alipopanda kule mlima Sinai/Horebu..na kuwaletea wana wa Israeli agano la sheria..ambalo watu wote waliokuwa chini ya hilo walikuwa ni “watumwa wa sheria”..na ndio wayahudi.

Sasa Agano hili la sheria wana wa Israeli walilolipokea kutoka Mlima SINAI,  lililowafunga na kuwafanya kuwa watumwa wa hiyo sheria na ndilo linalofananishwa na HAJIRI (aliyekuwa kijakazi wa Sara), kwasababu Hajiri alikuwa ni mtumwa na wala si Huru. Na mtoto wake Ishmaeli pamoja na wengine wote waliofuata (watoto wa Ishmaeli) bado walikuwa ni wana wa mjakazi tu vile vile.

Lakini Sara hakuwa mjakazi, bali alikuwa HURU pamoja na Mtoto wake Isaka, ikifunua agano la pili la UHURU ambalo ndilo la wale watu waliozaliwa kwa roho, ambao sheria imeandikwa ndani ya mioyo yao na si katika mawe, au makaratasi.

Na hawa ni watoto wa Sara kwa namna ya roho na ndio wana wa YERUSALEMU YA MBINGUNI, kwasababu wote wanaoishi kwa kuongozwa na roho ndio watakaoirithi YERUSALEMU MPYA na ndio wenyeji wao upo kule, lakini wanaoishi kwa sheria ambayo asili yake ni mlima Sinai, hao ni wa Yerusalemu ya duniani.

Na kama vile Hajiri alivyofukuzwa pamoja na mwanae, kwasababu si mwana wa ahadi…vile vile wote wanaoataka kuishi kwa sheria watatengwa na Kristo.

Wagalatia 5:4 “Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema”.

Biblia inatufundisha kuwa tunahesabiwa haki kwa Neema, kwa njia ya Imani na si kwa matendo ya sheria.

Warumi 3:9 “Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani.

10  Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye.

11  Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa Imani”.

Sasa kujua kwa undani tofauti ya Matendo ya sheria na Matendo ya Imani fungua hapa >>NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?

TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!

Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?

KATIKA MLIMA WA BWANA ITAPATIKANA.

NI WAPI UTAKUTANA NA MALAIKA WA BWANA?

Rudi Nyumbani

Print this post

MSALABA NI ZANA YA UJENZI WA MAISHA YAKO.

Mwimbaji mmoja wa tenzi za rohoni aliandika hivi “Kama alivyoonyeshwa Yakobo zamani, msalaba umekuwa ngazi ya mbinguni (Tenzi no. 81, ubeti wa 2)”.. akirejea wakati ule  Yakobo alipokuwa amelala pale Betheli na akaona maono, ngazi kubwa kutokea mbele yake, na malaika wakikwea na kushuka kutoka mbinguni.

Mwanzo 28:11 “Akafika mahali fulani akakaa huko usiku kucha, maana jua lilikuwa limekuchwa; akatwaa jiwe moja la mahali pale akaliweka chini ya kichwa chake, akalala usingizi pale pale.

12 Akaota ndoto; na tazama, NGAZI IMESIMAMISHWA JUU YA NCHI, na ncha yake yafika mbinguni. Tena, tazama, malaika wa Mungu wanapanda, na kushuka juu yake…..

16 Yakobo akaamka katika usingizi wake, akasema, Kweli Bwana yupo mahali hapa, wala mimi sikujua.  17 Naye akaogopa akasema, Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka, hapa ni nyumba ya Mungu, NAPO NDIPO LANGO LA MBINGUNI”.

Na ufunuo wa ngazi hiyo ni MSALABA.. Hakika! Kupitia msalaba wa YESU tunafika mbinguni, kupitia ufunuo wa msalaba wa BWANA YESU maishani mwetu, na si shingoni mwetu, tutamwona MUNGU!..

Lakini nataka pia tuutafakari msalaba kwa jicho lingine, kama “ZANA YA KUJENGEA MAISHA”. Hebu turejee kisa kimoja katika biblia kilichomhusu Nabii Elisha pamoja na wana wa manabii na kisha tutauelewa Zaidi msalaba wa BWANA.

2Wafalme 6:1 “Kisha, wana wa manabii wakamwambia Elisha, Angalia basi, mahali tukaapo mbele yako ni padogo kwetu.

2 Basi twende mpaka Yordani, twakuomba, tutwae huko kila mtu mti mmoja, ili tujifanyie huko mahali pa kukaa. Akajibu, Haya! Nendeni.

3 Mmoja wao akasema, Uwe radhi, basi nakusihi, uende pamoja na watumishi wako. Akajibu, Nitakwenda.

4 Basi, akaenda pamoja nao. Nao walipofika Yordani, wakakata miti.

5 Lakini mmojawapo alipokuwa katika kukata boriti, chuma cha shoka kikaanguka majini; akalia, akasema, Ole wangu! Bwana wangu, kwani kiliazimiwa kile.

6 Mtu wa Mungu akasema, Kilianguka wapi? Akamwonyesha mahali. AKAKATA KIJITI, AKAKITUPA PALE PALE, CHUMA KIKAELEA.

7 Akasema, Kiokote. Basi akanyosha mkono, akakitwaa”

Nataka tuutafakari huo mstari wa sita..“AKAKATA KIJITI, AKAKITUPA PALE PALE, CHUMA KIKAELEA”.

Hiki kijiti ni NINI?, na Chuma ni nini?

Chuma ni zana ya ujenzi, kumbuka huyu mtu alikuwa anakata mti kwaajili ya ujenzi ya makazi, na kwa bahati mbaya kichwa cha shoka kikaangukia majini, na shoka halikuwa la kwake bali aliazima tu!. Hivyo kazi ya ujenzi wa makazi yake ikasimama, na vile vile akabaki na deni ya kulipia kile kifaa.

Huenda shoka lako likawa ni elimu uliyo nayo, ambayo pengine kupitia hiyo ndio umefikiri kujenga maisha yako, au kazi uliyo nayo ambayo kupitia hiyo ndio unafikiria kujenga maisha yako, na makazi yako..Huenda shoka lako ni kipawa au uwezo Fulani ulionao ambao kupitia huo unaamini kazi yako itaisha salama.

Nataka nikuambie wakati unafikiri Elimu yako ni chuma kigumu cha kujenga maisha, au kazi yako ndio chuma kigumu cha kujenga maisha yako, au utashi wako ndio chuma kigumu cha kuchonga maisha yako..usisahau kuwa yapo maji pembeni yako!!!, na hiko chuma saa yoyote kitazama..na kile ulichotazamia kukikamilisha kitasimama, na hata kupata hasara kubwa ya madeni.

Sasa kitu pekee kinachoweza kutoa chuma ndani ya maji, hata kielee, si winchi, au sumaku, au kifaa kingine chochote chenye uwezo…bali ni KIJITI KIDOGO TU!.. Na kijiti hiko si kingine Zaidi ya MSALABA BWANA YESU!!.

(Kumbuka msalaba wa Bwana YESU si Rozari shingoni, au sanamu madhahabuni, au mti wa msalaba juu ya kaburi, bali ni ufunuo wa Mauti ya YESU moyoni)…Maana yake wokovu unaopatikana kupitia uelewa wa mauti ya BWANA YESU…ambao huo unazaa mtu kujitwika msalaba wake na kumfuata yeye.

Marko 8:34  “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.

35  Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha”.

Je! msalaba wa KRISTO upo moyoni mwako??, Umeubeba msalaba wako na kumfuata yeye??.. Au unajitumainisha na chuma ulicho nacho!..ukiamini kuwa elimu yako itakuokoa, au kazi yako, au cheo chako.. Hivyo vyote ukiwa navyo na KRISTO HAYUPO MOYONI MWAKO, UNAFANYA KAZI BURE!!!.

Na tena ni heri ukose hivyo vyote, Ukose elimu, ukose kazi, ukose cheo, ukose kila kitu…lakini msalaba wa KRISTO upo moyoni mwako, kuliko kuwa na vyote hivyo halafu huna YESU moyoni!!…NI HASARA KUBWA!!!

Ni heri ukayasalimisha maisha yako kwa BWANA YESU leo, kama bado hujafanya hivyo, na BWANA ATAKUSAIDIA, Ikiwa utahitaji msaada huo wa kumpokea YESU, basi waweza wasiliana nasi na utapata msaada huo…

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ONA FAHARI JUU YA BWANA.

Je Mungu ana njia ngapi za kuzungumza?

NJIA YA MSALABA

Kama ulimwengu ujao utakuwa na watakatifu tu, sasa hao watakaotawaliwa watatoka wapi?

UTHAMINI WITO WA PILI WA YESU ZAIDI YA ULE WA KWANZA.

Rudi Nyumbani

Print this post