Ifuatayo ni baadhi ya mistari ambayo itamsaidia mtu kupata kibali aidha KWA MUNGU au kwa WANADAMU, au KWA WAKUU Au vyote kwa pamoja (Mungu pamoja na wanadamu).
KIBALI CHA MUNGU:
Mwanzo 4:6 “Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?
7 Kama ukitenda vyema, HUTAPATA KIBALI? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde”
1Samweli 1:17 “Ndipo Eli akajibu, akasema, Enenda kwa amani; na Mungu wa Israeli akujalie haja yako uliyomwomba.
18 Naye akasema, Mjakazi wako na AONE KIBALI MACHONI PAKO. Basi huyo mwanamke akaenda zake, naye akala chakula, wala uso wake haukukunjamana tena”.
KWA WATU:
Kutoka 11:3 “Bwana akawapa watu hao KIBALI MACHONI PA WAMISRI. Zaidi ya hayo, huyo Musa alikuwa ni mkuu sana katika nchi ya Misri, machoni pa watumishi wa Farao, na machoni pa watu wake”
Esta 2:15 “Hata ilipowadia zamu yake Esta, binti Abihaili, mjomba wake Mordekai, ambaye alimtwaa kuwa binti yake, ili aingie kwa mfalme, yeye hakutaka kitu, ila vile vilivyoagizwa na Hegai, msimamizi wake mfalme, mwenye kuwalinda wanawake. Naye huyu Esta alikuwa amepata kibali machoni pa wote waliomwona”
KWA WAKUU NA WAFALME:
Mwanzo 39:21 “Lakini Bwana akawa pamoja na Yusufu, akamfadhili, AKAMPA KIBALI machoni pa mkuu wa gereza.
22 Mkuu wa gereza akawatia mkononi mwa Yusufu watu wote waliofungwa, waliomo gerezani; na yote yaliyofanyika humo ndiye aliyeyafanya”
1Samweli 16:22 “Kisha Sauli akapeleka watu kwa Yese, akasema, Tafadhali, mwache Daudi asimame mbele yangu; maana AMEONA KIBALI machoni pangu”.
1Samweli 27:5 “Daudi akamwambia Akishi, Sasa kama nimeona KIBALI MACHONI PAKO na nipewe mahali katika miji hii mmojawapo mashambani, nipate kukaa huko; mbona mtumwa wako akae katika mji wa kifalme pamoja na wewe?”
Nehemia 2:4 “Ndipo mfalme akaniambia, Una haja gani unayotaka kuniomba? Basi nikamwomba Mungu wa mbinguni.
5 Nikamwambia mfalme, Mfalme akiona vema, na ikiwa mimi, mtumishi wako, NIMEPATA KIBALI MACHONI PAKO, tafadhali unipeleke mpaka Yuda, niuendee mji wa makaburi ya baba zangu, nipate kuujenga”
Esta 5:2 “Ikawa, mfalme alipomwona malkia Esta amesimama uani, yeye AKAPATA KIBALI machoni pake; naye mfalme akamnyoshea Esta fimbo ya dhahabu aliyokuwa nayo mkononi. Basi Esta akakaribia, akaigusa ncha ya fimbo”
KWA MUME:
Ruthu 2:10 “Ndipo aliposujudia, akainama mpaka nchi, akamwambia, Jinsi gani NIMEPATA KIBALI machoni pako, hata ukanifahamu, mimi niliye mgeni?
11 Naye Boazi akajibu, akamwambia, Nimeelezwa sana yote uliyomfanyia mkweo, tangu alipokufa mumeo; na jinsi ulivyowaacha baba yako na mama yako, na nchi yako uliyozaliwa, ukawafikilia watu usiowajua tangu hapo”.
Esta 2:17 “Mfalme akampenda Esta kuliko wanawake wote, naye AKAPATA NEEMA NA KIBALI machoni pake kuliko mabikira wote; basi akamtia taji ya kifalme kichwani pake, akamfanya awe malkia badala ya Vashti”
KWA MUNGU PAMOJA NA WANADAMU:
1Samweli 2:26 “Na yule mtoto, Samweli, akazidi kukua akapata kibali kwa Bwana, na kwa watu pia”
Mithali 3:4 “Rehema na kweli zisifarakane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.
4 Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri, Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu.
5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe”
BWANA AKUBARIKI.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.
Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)
MAPAMBO YA WANAWAKE WALIOUKIRI UCHAJI WA MUNGU.
WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU
SWALI: Biblia inamaana gani inaposema “Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango”.
Yakobo 5:9 Ndugu, msinung’unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.
JIBU: Neno la Mungu halitoi nafasi ya sisi, kunung’unikiana kwasababu yoyote. Aidha ya kuonewa, au kudhulumiwa, kuaibishwa au kufanyiwa jambo ambalo halikupasa utendewe, Manung’uniko ni zao la kutokuwa na uvumilivu. Na kwamba tukifanya hivyo basi, tafsiri yake ni kuwa tunamfanya Mungu naye aghahiri uvumilivu wake kwetu.
Lakini anatoa, suluhisho, kwamba hayo tuyaache mikononi mwake. Kwasababu yeye ndio mwamuzi wetu. Na kwamba, sio tu mwamuzi lakini ni mwamuzi ambaye yupo mlangoni. Akiwa na maana kuwa Kristo yupo karibu sana na maonevu, au dhuluma hizo, na kwamba yeye mwenyewe atalipa, wala hatakawia, kwasababu yupo mlango.
Atalipa aidha kwa wakati huu huu duniani, au siku ile ya mwisho wa Hukumu. Kwake yeye ni lazima haki itendeke. Pia kwa upande mwingine anataka uogope kwasababu ukinung’unika yeye hayupo mbali kukusikia.
Wafilipi 4:5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa, popote tusimamapo kutoa malalamiko, laumu, kuhesabu makosa, n.k. basi tutambua kuwa Kristo yupo hapo hapo katikati yetu kutusikia. Hivyo tusiwe wepesi ya kunena, bali tujifunze kuwa wavumilivu katika mambo yote. Ili Mungu atuachilie neema yake.
Bwana akubariki.
Je! Umeokoka? Je, umebatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo? Kama ni hapana, basi wakati ndio huu, tubu dhambi zako, kwa kumwamini Yesu upokee ondoleo la dhambi zako, Na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu.
Ikiwa upo tayari kumkabidhi leo maisha yako. Basi fungua hapa kwa mwongozo huo. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
NI ALIYEFIFIA MAVAZI AU MWENYE MAVAZI MEUPE?
Yesu anajifunua kwa watu kulingana na jinsi mtu huyo anavyotembea naye. Wapo watu wanatembea na Bwana Yesu katika mng’ao wake wa ajabu. Lakini wapo wanaotembea naye katika hali ya kawaida sana. Utajiuliza kwa namna gani.
Wakati mwingi sana, Yesu alipokuwa na wanafunzi pamoja na makutano. Zaidi ya asilimia 98 ya maisha yake, alikuwa hana tofauti na watu wengine wowote. Kiasi kwamba akijichanganya kati ya watu 10, huwezi mtofautisha na yoyote, kimwonekano. Ndio maana wengi, walishindwa kumngundua, alipokuwa na watu soma (Yohana 18:7).
Lakini kuna wakati, alibadilika sura, mpaka mwonekano wake. Tutaona ni nini kilichomfanya awe vile jambo lililowafanya mitume wake kumchukulia kitofauti sana tangu ule wakati.
Marko 9:2 “Hata baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani, peke yao; akageuka sura yake mbele yao; 3 mavazi yake yakimeta-meta, meupe mno, jinsi asivyoweza dobi duniani kuyafanya meupe.
4 Wakatokewa na Eliya pamoja na Musa, nao walikuwa wakizungumza na Yesu. 5 Petro akajibu, akamwambia Yesu, Rabi, ni vizuri sisi kuwapo hapa; na tufanye vibanda vitatu, kimoja chako wewe, kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya. 6 Maana, hakujua la kunena, kwa kuwa waliingiwa na hofu nyingi.
7 Kisha likatokea wingu, likawatia uvuli; sauti ikatoka katika lile wingu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, msikieni yeye. 8 Mara hiyo walipotazama huku na huku, hawakuona mtu pamoja nao ila Yesu peke yake.
9 Na walipokuwa wakishuka mlimani aliwakataza wasimweleze mtu waliyoyaona, hata Mwana wa Adamu atakapokuwa amefufuka katika wafu”.
Sababu iliyowafanya Petro, Yohana, na Yakobo, kumwona Bwana katika mwonekano ule. Ni mahali walipokwenda naye. Walikwenda naye mlimani “KUOMBA”. Maombi ndio yaliyopelekea, Yesu abadilike ghafla mbele yao na kuwa na ule utukufu wake wa asili.
Vivyo hivyo na sisi ili tumwone Kristo katika utukufu wake mkamilifu katika maisha yetu, Tupende maombi. Ukiwa mvivu katika kuomba, Yesu atakuwa ni wa kufifia maishani mwako. Hutafurahia uweza wake mtimilifu katika maisha yako, hutafurahia wokovu wako. Mfanye awe kama JUA kwako, ang’ae kweli kweli, mpe nafasi kwasababu yeye ndio Nuru ya ulimwengu. Penda maombi, kila siku omba, kutana naye hapo, hudhuria mikesha sana, omba kwa bidii, ondoa uvivu.
Usipomruhusu Yesu akupangie maisha yako, kimaombi, shetani atakusaidia kuyapanga.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?
Je! Umejengwa kweli juu yake?
Ukimuuliza mtu, mwamba ni nini, ni rahisi kukujibu YESU. Jibu ambalo ni sahihi, maandiko yanatuthibitishia hilo Yesu kuwa Yesu ni mwamba (Mathayo 21:42, 1Wakorintho 10:4). Lakini lazima ufahamu pia MWAMBA mwenye anasemaje, kuhusu yeye mwenyewe alivyo.
Ni maneno ambayo tunayasoma lakini si rahisi kuyatafakari kwa ukaribu, embu tusome tena, halafu utaona mwamba alimaanisha nini. (Zingatia vifungu vilivyo katika herufi kubwa) Soma kwa utulivu.
Mathayo 7:24 Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na KUYAFANYA, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;
25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba. 26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu ASIYAFANYE, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;
27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.
28 Ikawa, Yesu alipoyamaliza maneno hayo, makutano walishangaa mno kwa mafundisho yake; 29 kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye amri, wala si kama waandishi wao.
Umeelewa? Vema hayo maneno?
Kumbe mtu yeyote anayesikia maneno ya Yesu. Hapo hapo huwa anaanza ujezi.
Lakini tofauti inakuja mahali anapokwenda kujengea,. Yule aliyejenga kwenye mchanga tafsiri yake Yesu anasema, anasikia, lakini hayatendei kazi (Hayafanyi), aliyoyasikia. Hivyo hapo Mchanga, ni KUTOTENDA.
Lakini Yule mwingine aliyekwenda kwenye mwamba tafsiri yake ni anasikia lakini pia anatenda. Hivyo MWAMBA, ni kutenda.
Mwamba sio kumjua Yesu ndugu, mwamba sio kusoma sana biblia na kujua mafumbo na siri zote zilizo katika biblia, mwamba sio kujua kujua tafsiri zote za kigiriki na kiebrania kwenye maandiko, mwamba sio kujua kufundisha vema biblia,.. Sio hivyo vyote.
Mwamba ni KULITENDEA KAZI NENO, Unalolisikia kwake. Hilo tu. Sio kumjua Yesu.
Hatari iliyopo leo, miongoni mwa wakristo wengi, ni kwamba tumejengwa juu ya mafundisho mengi. Lakini hatujajengwa juu ya kutendea kazi mafundisho tunayofundishwa. Ndugu fundisho halikusaidii kuyashinda majaribu, au tufani za mwovu, au dhoruba, au pepo, hapo unafanya kazi ya kuchosha tu,kudumu katika kusikia, kusoma, kusikiliza, bado si suluhisho, kusema nimebarikiwa, nimefunguliwa ufahamu, bado hakukufikishi popote, kama HUTALIISHI hilo Neno.
Ukiwa ni wa kufanya bidii kuliishi NENO moja, wewe ni imara sana kuliko Yule mwenye kujiona anaijua biblia yote
Penda Utakatifu, penda usafi wa moyo, penda kupiga hatua rohoni. Penda matendo mema.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Gumegume ni nini? (Isaya 50:7)
Swali: Kwanini katika biblia lisitumike neno “Mwizi” na badala yake linatumika neno “Mwivi”…Mwivi ni nini?
Jibu: Mwivi na Mwizi ni Neno moja, lenye maana moja.. isipokuwa ni lugha mbili za nyakati mbili tofauti.
Kiswahili kilichotumika katika kutafsiri biblia ni Kiswahili cha zamani, kilichoitwa “kimvita” ambacho ndicho kimebeba maneno ambayo hatuyaoni katika Kiswahili cha sasa, na mojawapo ya maneno ndio kama hayo “Mwivi na wevi” ikimaanisha “mwizi na wezi”. Ndio maana katika biblia yote huwezi kukuta neno Mwizi, badala yake utakuta mwivi (Soma Kutoka 22:2, Ayubu24:14, Zaburi 50:18, Mithali 6:30, Yoeli 2:9, Luka 12:39 n.k )
Maneno mengine ya kimvita (Kiswahili cha zamani) ambayo mengi ya hayo hayatumiki sasa ni pamoja na “jimbi” badala ya “Jogoo”… “Kiza” badala ya “Giza”….”Nyuni” badala ya “ndege”…. “Kongwa” badala ya “Nira” na mengine mengi.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba “Mwivi” na “Mwizi” ni Neno moja, lenye maana ile ile moja (ya mtu anayeiba).
Lakini mbali na hilo, maandiko yanatufundisha kuwa Bwana YESU atakuja kama “Mwivi”..
Ufunuo 16:15 “(Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake)”
Je umewahi kujiuliza ni kwanini aje kama Mwivi na si Askari?.. Kwa upana juu ya hilo basi fungua hapa >>ANAKUJA KAMA “MWIVI” NA SI KAMA “ASKARI” FANYIKA CHOMBO CHA THAMANI.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Nini maana ya Mithali 6:30 Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha
Wale waliowekewa tayari ufalme ni akina nani?. (Mathayo 20:23).
Swali: Je Neno “Kalvari” tunalisoma wapi katika biblia?, na tofauti yake na Golgotha ni ipi?
JIbu: Katika biblia ya Kiswahili hakuna neno “Kalvari”, bali kuna neno “Golgotha” ambalo tunalisoma katika kitabu cha Yohana 19:17
Yohana 19:17 “Akatoka, hali akijichukulia msalaba wake, mpaka mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, au kwa Kiebrania, GOLGOTHA.
18 Wakamsulibisha huko, na wengine wawili pamoja naye, mmoja huku na mmoja huku, na Yesu katikati”.
Maana ya Neno “Golgotha”, tayari biblia imeshatoa tafsiri yake hapo kwenye mstari wa 17 kuwa ni “Fuvu la Kichwa”
Sasa neno “Kalvari” maana yake ni nini?
Neno Kalvari linapatikana katika tafsiri chache za lugha ya kiingereza, ambalo asili yake ni lugha ya Kilatini “CALVARIAE” lenye maana ile ile ya “Fuvu la kichwa cha mtu”.
Hivyo “Kalvari” na “Golgotha” ni Neno moja lenye maana moja, isipokuwa lugha tofauti, ni sawa na neno “church” na “kanisa” ni kitu kimoja ila lugha tofauti.
Kufahamu kwa upana ufunuo uliopo nyuma ya Golgotha, (Fuvu la kichwa), basi fungua hapa >>>FUVU LA KICHWA.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)
Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?
AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.
ALIFANYIKA SADAKA KWA AJILI YETU!
Swali: Je wale waliowekewa tayari ni akina nani na kwanini Bwana Yesu aseme maneno yale?
Jibu: Tuanzie kusoma mstari wa 20..
Mathayo 20:20 “Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno.
21 Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako.
22 Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.
23 Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, SINA AMRI KUWAPA, BALI WATAPEWA WALIOWEKEWA TAYARI NA BABA YANGU”.
Ili tuelewe vizuri, hebu tafakari mfano huu.. “wanafunzi wawili wamemfuata mwalimu wao wa darasa na kumwomba washike nafasi ya kwanza kitaifa na mwingine ashike ya pili kitaifa katika mitihani yao ya mwisho wa kuhitimu”.. Unadhani jibu la mwalimu litakuwa ni lipi?..
Bila shaka mwalimu atawauliza.. je! Mtaweza kusoma kwa bidii??.. Na kama wale wanafunzi watajibu NDIO!.. Bado Mwalimu hataweza kuwapa hizo nafasi, bali atawaambia mimi sina mamlaka ya kuwapa bali “Wasahishaji watakaosahisha mitihani ya wote ndio watakaotoa majibu ya mitihani yenu na kuwapanga kama mmestahili hizo nafasi au la”..
Ndicho Bwana YESU alichowaambia hawa wana wa Zebedayo!.. ambao walienda kumwomba nafasi ya kuketi pamoja naye katika kiti chake.. na jibu la Bwana YESU likawa, ni “kukinywea kikombe”.. maana yake kukubali mateso kwaajili yake!.. Na wao wakajibu “wataweza”.. Lakini jibu la Bwana likawa “Nafasi hizo watapewa waliowekewa tayari”..maana yake waliostahili.
Na hao waliostahili ni akina nani?
Ni wale watakaofanya vizuri Zaidi ya wengine wote katika mambo yafuatayo.
1. KUKINYWEA KIKOMBE.
Kikombe alichokinywea Bwana Yesu ni kile cha Mateso ya msalabani (Soma Mathayo 26:39), kutemewa mate, kupigwa Makonde, kuvikwa taji ya miiba, na kugongomelewa misumari mikononi..
Na yeyote ambaye atakubali kuteswa kwaajili ya Kristo, na si kwaajili ya mtu au kitu kingine chochote, basi yupo katika daraja zuri la kumkaribia Kristo katika siku ile kuu.
2. KUBATIZWA UBATIZO WA BWANA YESU.
Marko 10:38 “Yesu akawaambia, Hamjui mnaloliomba. Mwaweza kunywea kikombe ninyweacho mimi, au KUBATIZWA UBATIZO NIBATIZWAO MIMI?”
Swali Ubatizo aliobatizwa Bwana YESU KRISTO ni upi?…. si mwingine Zaidi ya ule wa kufa, kuzikwa na siku ya tatu kufufuka, na kupaa juu (soma Luka 12:50), Na ubatizo huu mpaka sasa hakuna rekodi ya wazi ya yoyote aliyeupitia..
Ubatizo tubatizwao sasa ni ule wa maji mengi, ambao ni ishara ya kufa na kufufuka na Kristo (Wakolosai 2:12), kwamba tunapozamishwa katika maji mengi na kuibuka juu, ni ishara ya kufa pamoja na Kristo na kufufuka pamoja naye… Lakini Ule hasa wa kufa na kufufuka na kupaa, hakuna rekodi ya wazi ya aliyeupitia.
Isipokuwa unawezekana ndio maana tunasoma katika Ufunuo 11, kuwa wale washahidi wawili, ni miongoni mwa watakaoupitia..
Ufunuo 11:10 “….Nao wakaao juu ya nchi wafurahi juu yao na kushangilia. Nao watapelekeana zawadi wao kwa wao, kwa kuwa manabii hao wawili waliwatesa wao wakaao juu ya nchi.
11 NA BAADA YA SIKU HIZO TATU U NUSU, roho ya uhai itokayo kwa Mungu ikawaingia, wakasimama juu ya miguu yao; na hofu kuu ikawaangukia watu waliowatazama.
12 WAKASIKIA SAUTI KUU KUTOKA MBINGUNI IKIWAAMBIA, PANDENI HATA HUKU. WAKAPANDA MBINGUNI KATIKA WINGU, ADUI ZAO WAKIWATAZAMA”.
Je umempokea YESU?, Fahamu kuwa tunaishi katika siku za mwisho, na Kristo yupo mlangoni.
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA
Swali: Wenye kutia Kalafati ni watu gani?
Jibu: Neno “Kalafati” limeonekana mara mbili tu katika biblia, katika Ezekieli 27:9 na Ezekieli 27:27.
Na maana yake ni “Kamba nyembamba iliyotengenezwa kwa pamba” ambayo inawekwa katikati ya mianya ya mbao za merikebu, ili kuzuia maji yasipenye katika ile miunganiko. (Tazama picha juu)
Hivyo watu wanaofanya hiyo kazi ndio waliotajwa hapo katika Ezekieli 27:9,
Ezekieli 27:9 “Wazee wa Gebali na wenye akili wake walikuwa ndani yako, WENYE KUTIA KALAFATI; merikebu zote za bahari na mabaharia wao walikuwa ndani yako, ili kubadiliana biashara yako”.
Lakini habari hii inahusu nini?
Ukisoma kitabu hicho cha Ezekieli mlango wa 27 kuanzia mstari wa kwanza, utaona ni unabii unamhusu mfalme wa Tiro. (Kwa urefu kuhusu Taifa la Tiro fungua hapa >>>Miji ya Tiro na Sidoni ni miji gani kwasasa?
Lakini hapa ni unabii wa Mfalme wa Tiro, Kwamba kwa kiburi chake na biashara zake nyingi alizozifanya juu ya nchi na katika bahari kupitia merikebu zake, siku inakuja ambapo ataanguka na kushuka chini kwasababu ya dhambi zake nyingi.
Na biashara za baharini alizokuwa anazifanya kupitia merikebu zake kubwa ambazo ndani yake kulikuwa na wana-maji, na “watiao Kalafati” na manahodha, zitaanguka na shughuli zao hizo zitaisha!
Ezekieli 27:27 “Mali zako, na bidhaa yako, na utajiri wako, wana-maji wako, na rubani zako, na WENYE KUTIA KALAFATI WAKO, na wafanya biashara wako, na watu wako wa vita wote, walio ndani yako, pamoja na jeshi lako lote lililo ndani yako, wataanguka katika moyo wa bahari katika siku ya kuangamia kwako”.
Ufunuo kamili pia kwa anguko la ulimwengu pamoja na dini zake za uongo katika siku za mwisho..
Ufunuo Ufunuo 18:2 “Akalia kwa sauti kuu, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli ule mkuu; umekuwa maskani ya mashetani, na ngome ya kila roho mchafu, na ngome ya kila ndege mchafu mwenye kuchukiza;
3 kwa kuwa mataifa yote wamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa nchi wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali kwa nguvu za kiburi chake………………..
9 Na hao wafalme wa nchi, waliozini naye na kufanya anasa pamoja naye, watalia na kumwombolezea; wauonapo moshi wa kuungua kwake;
10 wakisimama mbali kwa hofu ya maumivu yake, wakisema, Ole, ole, mji ule ulio mkuu, Babeli, mji ule ulio na nguvu! Kwa kuwa katika saa moja hukumu yako imekuja.
11 Nao wafanya biashara wa nchi walia na kumwombolezea, kwa sababu hapana mtu anunuaye bidhaa yao tena;
12 bidhaa ya dhahabu, na fedha, na kito chenye thamani, na lulu, na kitani nzuri, na nguo ya rangi ya zambarau, na hariri, na nguo nyekundu; na kila mti wa uudi, na kila chombo cha pembe, na kila chombo cha mti wa thamani nyingi, na cha shaba, na cha chuma, na cha marimari;
13 na mdalasini, na iliki, na uvumba, na marhamu, na ubani, na mvinyo, na mafuta ya mzeituni, na unga mzuri, na ngano, na ng’ombe, na kondoo, na farasi, na magari, na miili na roho za wanadamu.
14 Na matunda yaliyotamaniwa na roho yako yamekuondokea; na vitu vyote vilivyo laini na vitu vya fahari vimekupotea; wala watu hawataviona tena kamwe.
15 Na wafanya biashara ya vitu hivyo, waliopata mali kwake, watasimama mbali, kwa hofu ya maumivu yake; wakilia na kuomboleza”
Je Umeokoka kwa kumwamini Bwana Yesu Kristo na kubatizwa, sawasawa na Marko 16:16?. Fahamu kuwa tunaishi katika siku za mwisho na Kristo amekaribia kurudi.
Kwa msaada Zaidi katika kumpokea Kristo fuatiliza sala hii ya Toba >>KUONGOZWA SALA YA TOBA au wasiliana nasi kwa namba zetu zilizoanishwa mwisho wa somo hili.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
KWANINI DANI ALIKAA KATIKA MERIKEBU.
EZEKIELI, ITABIRIE MIFUPA MIKAVU.
Tarshishi ni mji gani kwasasa?
Mashonde ni nini? (Ezekieli 4:15).
Je! Unaona Fahari juu ya nini? Ni kitu gani unachokionea Fahari?.. Je ni mali?, ni vyeo?, au uwezo ulio nao?..
Kama Bwana amekujali kukupa hivyo vyote, basi mshukuru lakini usijionee fahari juu ya hivyo, kwasababu vyote hivyo ni “UBATILI”….bali ona FAHARI juu ya BWANA YESU kama umeshamjua!.
Kwasababu kumjua YESU ni UTAJIRI mkubwa, na CHEO kikubwa na UWEZO mkubwa.. kuliko utajiri wowote wa kiduni, wala cheo chochote cha kidunia wala uwezo wowote wa kidunia.
Maana yake Kama ni kuringa, au kutamba…basi tamba kwa kuwa UMEMJUA YESU!. (Furahia kwa kuwa umekipata kitu kikubwa na cha thamani, furahi kwa kuwa umelenga shabaha)..ndivyo maandiko yanavyotufundisha..
1Wakorintho 1:30 “Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu HEKIMA itokayo kwa Mungu, na HAKI, na UTAKATIFU, na UKOMBOZI;
31 kusudi, kama ilivyoandikwa, YEYE AONAYE FAHARI NA AONE FAHARI JUU YA BWANA”.
Hapo anasema YESU KRISTO amefanyika kuwa HEKIMA itokayo kwa Mungu, maana yake kama yeye yupo ndani yetu, basi ni hekima ya Mungu imeingia ndani yetu. (sasa kwanini usione fahari juu yake kama yupo ndani yako)
Na tena amefanyika kuwa “HAKI”, Maana yake ni kwamba kama yeye yupo ndani yetu, basi tumepata haki ya kuishi milele, na kupata yote tunayoyahitaji ambayo ni mapenzi ya Mungu, (sasa kwanini usione fahari juu yake huyo kama yupo ndani yako?).
Na tena amefanyika “UTAKATIFU”.. Maana yake akiingia ndani yetu, tunahesabika na kuitwa watakatifu, (Kwanini usione fahari juu ya huyo).
Zaidi sana amefanyika “UKOMBOZI”. Maana yake anapoingia ndani yetu, tunapata ukombozi wa Laana, na zaidi sana tunapata Kuokoka na hukumu ya milele ijayo, ya ziwa la moto aliloandaliwa shetani na malaika zake (Ufunuo 12:9)… Kwanini usione fahari juu ya huyo aliyekupa ukombozi..
Aibu inatoka wapi!!!, ikiwa YESU KRISTO, aliye hekima ya Mungu yupo ndani yako?… Aibu ya kubeba kitabu chake (biblia) na kutembea nacho kikiwa wazi inatoka wapi? Ikiwa yeye ni mwokozi wako?
Aibu ya kuzungumza habari zake mbele za watu inatoka wapi? Ikiwa yeye ni Haki yako?… Aibu ya kushika amri zake inatoka wapi ikiwa yeye amekupa wokovu kutoka katika hukumu ya milele?.
ONA FAHARI JUU YAKE!.. wala usimwonee haya (aibu), maana alisema mtu akimwonea haya katika kizazi hiki yeye naye atamwonea haya mbele za malaika zake wa mbinguni.. Maana yake ni kwamba kama tukimwonea fahari, naye pia atatuonea fahari mbinguni (Marko 8:38)
ONA FAHARI JUU YAKE,…MTANGAZE KWA KUJITAMBA KABISA!.. MDHIHIRISHE KWA WATU, WAONE KUWA ULIYE NAYE NI KILA KITU KATIKA MAISHA YAKO!… Na itakuwa baraka kubwa kwako.
Wagalatia 6:14 “Lakini mimi, hasha, nisione fahari juu ya kitu cho chote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulibishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu”.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Maana ya Mithali 19:11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake.
Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.
KWANINI NABII ISAYA ALIAGIZWA KUHUBIRI UCHI?
VAZI KUU AMBALO MUNGU AMETUANDALIA KILA MMOJA WETU.
SWALI: Je! Mithali 6:30 inamaana gani?
Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha, iwapo aona njaa; 31 Lakini akipatikana, atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake.
JIBU: Chukulia mfano mtu hajala siku tatu, halafu akaona kuna duka lipo wazi pale jirani, na mwenyewe ametoka, akashawishika kuingia haraka na kubeba mkate, ili akale. Lakini mwenye duka aliporudi na kuona mkate umeibiwa, alianza kumfuatilia, mwishowe akamkuta amejificha mahali Fulani anakula akiwa katika hali mbaya.
Kibinadamu, atakapoona hali halisi ya mwizi, huwenda ataishia kukasirika tu, au kumgombeza, au kwenda kumwajibisha, kwa mambo madogo madogo. Kwasababu anaona alichokifanya ni kwa ajili ya kusalimu maisha yake tu, ale asife, lakini sio kwa lengo la kuchukua vya watu, akauze, au kuleta hasara kwa wengine.
Lakini sehemu ya pili ya mstari huo anaendelea kusema kama “akipatikana atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake”.
Maana yake ni kuwa kama “atapatikana na kosa”, basi atalipa mara saba. Atagharimikia vyote alivyoviiba mara saba. Sasa kauli hiyo haimaanishi kwamba mwizi huyo huyo aliyeiba kwa ajili ya kujishibisha tumbo lake ndio atalipa mara saba, hapana, vinginevyo mstari huo ungekuwa unajipinga unaposema “watu hawamdharau mwizi akiiba kwa kujishibisha”, bali anamaanisha kama akipatikana na hatia tofauti na hiyo..mfano aliiba vitu ili akauze, aliiba fedha ili akajiendeleze kwenye mambo yake, alete hasara kwa wengine. Huyo atalipa gharama zote mara saba.
Ndio maana utaona adhabu nyingi za wezi huwa ni kubwa sana zaidi ya vile walivyoviiba, wanapigwa faini kubwa, wengine mpaka wanauliwa, kwa wizi tu mdogo. Hapo ni sawa na wamelipa mara saba.
Kama njaa ya mwilini, inaweza kumfanya mwizi asihesabiwe kosa. Kwasababu watu wanaelewa umuhimu wa kunusuru uhai kwa chakula, vipi kuhusu rohoni. Hata kuna wakati Daudi alikula mikate ya makuhani ambayo hawakupaswa watu wengine kula, lakini kwasababu alikuwa na njaa yeye na wenzake haikuhesabiwa kwake kuwa ni kosa (1Samweli 21).
Vivyo hivyo rohoni, Mungu anatufundisha sio kwamba tuwe wezi, hapana, lakini anataka tuthamini sana roho zetu, pale zinapokuwa hazina kitu, zina njaa. Iweje mtu unakaa hadi unakufa kiroho halafu unaona ni sawa kuwa hivyo hivyo kila siku. Hufanyi jambo Fulani la kujinasua katika hiyo hali yako mbaya rohoni, unaendelea tu hivyo hivyo. Tafuta kwa bidii chakula cha kiroho usife ndugu. Jibidiishe.
Iba muda wako wa kufanya mambo mengine ili ukipate chakula cha kiroho. Ni kweli ulipaswa kuwepo mahali Fulani pa muhimu, embu ghahiri muda huo, nenda kasome biblia, nenda kaombe, nenda kasikilize mahubiri yatakayokujenga. Ulipaswa uwepo kazini, lakini kwasababu ibada ile ni muhimu embu usione shida kughahiri.
Huna biblia Iba hata pesa yako ya matumizi ya muhimu kanunue, acha uonekane mjinga nenda kanunue biblia au vitabu vya rohoni vikujenge. Tafuta ile MANA iliyofichwa.
Siku hizi ni za mwisho. Na Bwana alishatabiri duniani kutakuwa na njaa, sio ya kukosa chakula au maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Mungu ya kweli. Usipojiongeza katika eneo la ukuaji wako kiroho. Ni ngumu kuvuka hizi nyakati mbaya za manabii wengi wa uongo, na mafundisho ya mashetani. Usipoyajenga maisha yako ya kiroho, shetani akusaidie kuyajenga kwake.
Amosi 8:11 “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Bwana”
Penda biblia, penda kujifunza, penda maombi zaidi ya vingine.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
YEYE ALIYEUWASHA HUO MOTO LAZIMA ATALIPA.
(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.
(Opens in a new browser tab)KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.(Opens in a new browser tab)