Title Devis

MKUMBUKE TOMASO.

Nakusalimu katika jina la Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tuzitafakari habari njema.

Tomaso alikuwa ni mtume  wa Bwana. Lakini alikuwa na tabia ya kitofauti na wale mitume wengine 11. Yeye hakuwa msaliti kama Yuda, zaidi sana alikuwa hata radhi kufa na Bwana wake, kipindi Fulani aliposikia anatafutwa ili  auawe (Yohana 11:16), hiyo ni ishara ya upendo wake kwa Yesu.

Lakini alikuwa na tabia nyingine ambayo ilimgharimu kwa sehemu Fulani, Na tabia yenyewe ni mashaka juu ya uweza wa Mungu, ni hiyo ikapelekea hata kuathiri mahudhurio yake, ya kiibada na kiutendaji kazi pale alipolazimika kuwepo na wenzake kama mtume.

Hakutaka kuamini kwamba Yesu anaweza kufufuka, hivyo wakati huo alipoitwa waombe pamoja, hakuwa tayari kukusanyika na wenzake, alipoitwa awafariji watu yeye kama mtume wa Bwana aliyepewa mamlaka hiyo, hakutaka kufanya hivyo kinyume chake akaenda kuendelea na shughuli zake. Walipokuwa wanatafakari maneno ya Yesu, yeye mawazo yake yalikuwa mbali kabisa na wenzake. Ni kama alikuwa amechoka.

Matokeo yake ikawa Yesu alipowatokea mitume wake, walipokuwa wamejifungia kuomba, yeye hakuwepo. Hata walipokuja kumuhadithia bado hakuamini, kwasababu moyo wake ulikuwa umeshahama kabisa.

Yohana 20:24  Walakini mmoja wa wale Thenashara, Tomaso, aitwaye Pacha, hakuwako pamoja nao alipokuja Yesu. 25  Basi wanafunzi wengine wakamwambia, Tumemwona Bwana. Akawaambia, Mimi nisipoziona mikononi mwake kovu za misumari, na kutia kidole changu katika mahali pa misumari, na kutia mkono wangu katika ubavu wake, mimi sisadiki hata kidogo. 26  Basi, baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwamo ndani tena, na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu, na milango imefungwa, akasimama katikati, akasema, Amani iwe kwenu 27  Kisha akamwambia Tomaso, Lete hapa kidole chako; uitazame mikono yangu; ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu, wala usiwe asiyeamini, bali aaminiye.

Wewe kama mtumwa wa Yesu usiwe tomaso, wakutanikapo wenzako kamwe kataa kujitenga, hata kama hakuna tumaini, dumu na wenzako, epuka utoro, epuka udhuru, dumu hapo. Zipo nyakati ambazo Bwana hamtokei mtu kivyake-vyake, bali wawapo wote. Zipo Baraka, ipo neema, katika umoja na wenzako, kupo kumwona Mungu unaposhikamana na wenzako kiuaminifu, katika kujengana na kutiana moyo.

Kamwe usifikiri kivyako, kataa hiyo hali, Bwana anasema ajitengaye na wenzake anatafuta matakwa yake mwenyewe, Tomaso alikuwa hivyo. Lakini fikra zake hazikuwa sahihi, aliligundua hilo baadaye aliporudi kujumuika na wenzake, ndipo akamwona Bwana, alidhani angemwonea kule alipokimbilia. Dumu na wenzako maadamu Bwana wenu ni mmoja, Roho wenu ni mmoja, Ubatizo wenu mmoja. Hiyo inatosha. Dumu hapo.

Bwana atusaidie.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Kwanini Tomaso atake kwenda kufa pamoja na Lazaro? (Yohana 11:14-16).

Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

KWANINI MITUME WAMUULIZE BWANA FARAGHANI?

Rudi nyumbani

Print this post

KIMBIA MACHAFU YA DUNIA. (2Petro 2:20)

2 Petro 2:20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia MACHAFU YA DUNIA kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza”. 

Mstari huo unatupa uelewa kwamba kumbe tukimjua mwokozi wetu Yesu Kristo, ni lazima kuambatane na kuyakimbia machafu ya dunia. Haiwezekani mtu akamjua Yesu Kristo halafu asiyakimbie Machafu ya dunia Kwa mujibu wa huo Mstari.

Machafu ya dunia ni yapi?

Machafu ya dunia ni Yale mambo maovu uliyokuwa unayafanya ulipokuwa mwenye dhambi, mfano ulevi, uzinzi, wizi, ushirikina, anasa, utoaji mimba, ulawiti,  n.k.

Sasa ikiwa ukinaswa, na kushindwa kutoka huko, maandiko yanasema hali yako ya mwisho inakuwa mbaya kuliko Ile ya kwanza, maana yake kama ulikuwa ni mgonjwa kidogo, kutokana na madhara uliyoyapata katika Ile dhambi, basi ugonjwa unakuwa mara dufu zaidi, kama ulikuwa unaweza kujizuia usilewe mara Kwa mara, basi nguvu ya ulevi inakulemea mara mbili unakuwa mlevi yule wa kupindukia kabisa kabisa.. hiyo ni kutuonyesha ni jinsi gani tunapaswa tuwe makini kama vile maandiko yanavyosema  pindi tuokokapo tuutimize wokovu wetu Kwa kuogopa na kutetemeka.

Wafilipi 2:12  “Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.

Bwana Yesu alitumia mfano wa Yule mtu ambaye alikuwa na pepo, lakini alipomtoka hakujiweka sawa, matokeo yake ikawa ni Yule pepo kuchukua pepo wengine saba waovu kuliko yeye, na hali yake ya mwisho ikawa mbaya kuliko ile ya kwanza. (Mathayo 12:43)

Lakini ikitokea tayari umeshaanguka kwenye machafu ya dunia, ambayo uliyaacha huko nyuma. Je ufanyaje?

Ni kutubu haraka sana. Angali nafasi unayo. Kumbuka hapo anasema “akinaswa na kushindwa”

Maana yake ni kuwa kama umenaswa, ni kufanya hima ujinasue kabla mwindaji wako (ibilisi), hajakuweka mikononi mwako kabisa kabisa. Lakini ukishindwa.basi Ndio mwisho wako umefika.

Ikiwa ulirudia uzinzi, ulirudia ulevi, ulirudia anasa, ulirudia kujichua, kutazama picha chafu mitandaoni.. Acha haraka sana, toka huko kwa kasi zote, jitakase kwa Bwana, kisha maanisha kumfuata Yesu, huku ukiutimiza wokovu wako kwa kuogopa na kutetemeka, kwasababu huo tumekabidhiwa mara moja tu.

Na Bwana atakurehemu.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Ikiwa bado hujaokoka na utapenda leo kumpokea Kristo maishani mwako. Basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Wokovu wa milele/ Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?

MFALME ANAKUJA.

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.

TABIA ZITAKAZOMTAMBULISHA MPINGA-KRISTO AJAYE.

Rudi nyumbani

Print this post

Fahamu maana ya Warumi 14:7 hakuna mtu miongoni mwetu aishiye kwa nafsi yake.

SWALI: Warumi 14:7 Inamaana gani?

“Kwa sababu hakuna mtu miongoni mwetu aishiye kwa nafsi yake, wala hakuna afaye kwa nafsi yake”. 

JIBU: Ni andiko linalotuonyesha uweza wa Mungu ulivyo wa kutawala/ kuendesha vitu vyote. Kwamba mwenye maamuzi yote yahusuyo maisha ya mwanadamu ni Mungu, Wala sio nafsi ya mtu kama atakavyo yeye mwenyewe.

ikiwa na maana kuishi kwako unalitimiza kusudi fulani la Mungu,(haijalishi wewe ni mwema au mtenda maovu) vilevile kufa kwako ni matokeo ya kusudi Fulani la Mungu.

Vifungu vinavyofuata vinazidi kuelezea vizuri zaidi…Anasema;

Warumi 14;8 Kwa maana kama tukiishi, twaishi kwa Bwana, au kama tukifa, twafa kwa Bwana. Basi kama tukiishi au kama tukifa, tu MALI YA BWANA. 

Umeona?  Wanadamu wote ni Mali ya Bwana, Hakuna mtu aliyejiumba mwenyewe..akawa na maamuzi yake yanayojitegemea yasiyopitishwa kwanza na Mungu.. mtu hawezi kusema kesho nitajitoa uhai wangu na kuurudisha, au kesho nitafanya hiki au kile, bila Mungu kulijua au kuliruhusu, au kulipanga ,. Au aseme baadaye nitaliamuru jua lisichomoze kwa matakwa yangu, Hilo jambo haliwezekani.

Sisi wote hatuishi Kwa nafsi zetu(mapenzi yetu ) wenyewe, Bali Kila jambo kama sio limeagizwa na Mungu, basi Mungu ameliruhusu.. Hata vifo vyetu vivyo hivyo. Na vitu vyote tuvifanyavyo. Kwasababu sote tunamilikiwa na Mungu.

Ndio maana ya hilo neno “hakuna mtu miongoni mwetu aishiye kwa nafsi yake, wala hakuna afaye kwa nafsi yake. ”

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Bwana Yesu alikuwa kabila gani?

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Je! sheria ilikuwaje dhaifu kwasababu ya mwili? (Warumi 8:3)

Anaposema mwanamume mmoja katika elfu nimemwona anamaana gani?

NJIA YA WOKOVU NDANI YA KITABU CHA WARUMI.

Rudi nyumbani

Print this post

Makasia ni nini? (Yona 1:13).

Swali: Kuvuta Makasia maana yake nini?


Likiwa moja linatiwa ”Kasia”, yakiwa mengi ni “Makasia” … Hizi ni  “Zana” ya kukisaidia chombo kutembea juu ya maji. Zana hii kwa mwonekano ni kama “Mwiko mkubwa”, (tazama picha juu), ambapo mabaharia walipoyavuta basi chombo kilisogea mbele..

Yona 1:13 “Lakini wale watu WAKAVUTA MAKASIA kwa nguvu, ili wapate kurudi pwani, wasiweze; kwa maana bahari ilizidi kuwachafukia sana”.

Unaweza kusoma Zaidi kuhusu makasia katika mistari ifuatayo; Marko 6:48, Yohana 6:19,  Isaya 33:21, na Ezekieli 27:6.

Je ni nini tunajifunza katika habari ya Yona na mabaharia hawa kuvuta makasia kurudi pwani?.. Fungua hapa >>>YONA: Mlango 1

Shalom.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

YONA: Mlango wa 2

HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI.

MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA.

YONA: Mlango wa 3

YONA: Mlango wa 4

Rudi nyumbani

Print this post

Upepo wa Mbisho maana yake nini? (Mathayo 14:24)

Swali: Pepo za Mbisho ni nini?


Jibu: Turejee kuanzia mstari wa 23.

Mathayo 14:23 “Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake.

24  Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; MAANA UPEPO ULIKUWA WA MBISHO.

25  Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.

26  Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu”.

Maana ya neno “Mbisho” ni “Ukinzani”. Hivyo hapo aliposema “Upepo ulikuwa wa Mbisho”, maana yake upepo ulikuwa ni wa ukinzani, (yaani ulikuwa unavuma kinyume na uelekeo waliokuwa wanauendea).

Utasoma tena aina ya upepo huu ikitajwa katika Matendo 27:4,

Matendo 27:4 ”Kutoka huko tukatweka, tukasafiri chini ya Kipro ili kuukinga upepo, kwa maana PEPO ZILIKUWA ZA MBISHO”.

Safari yoyote ya majini, ikikutana na pepo za mbisho, safari hiyo inakuwa ni ngumu sana.. Kwasababu upepo utakuwa unavuma kinyume na ile merikebu na hivyo kuchelewesha safari au hata kuirudisha nyuma.

Lakini pepo za Mbisho zinafunua nini kiroho?

Pepo za mbisho kiroho ni kila aina ya matatizo, na shida na dhiki na vikwazo kutoka kwa yule adui vinavyokawisha au kurudisha nyuma safari yetu ya Imani hapa duniani.

Ndio maana utaona katika habari hiyo ya Mathayo 14:23-36, kabla wanafunzi wa Bwana YESU kufika nchi ya Wagerasi kwaaijli ya huduma ya kufundisha na kuponya wagonjwa na kuwafungua walioteswa na shetani, adui aliwatumia “Upepo huu wa mbisho”, lengo ni ili wasifanikiwe safari yao hiyo.

Lakini BWANA YESU alipoingia ndani ya chombo kile ule upepo ukakoma na misuko suko yake, kufunua kuwa zile zilikuwa ni hila za ibilisi.

Hivyo hata sisi tunapokutana na pepo za namna hii katika Imani, suluhisho ni kuzikemea kwa Imani na kwa jina la YESU, na zitatii.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

MAJARIBU MATANO (5) YA MKRISTO.

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

Rudi nyumbani

Print this post

Kufufuka kwa Bwana kulitabiriwa wapi katika agano la kale?

Swali: Bwana Yesu alitabiriwa wapi katika agano la kale kwamba atafufuka?


Jibu: Kabla ya kuona ni wapi alitabiriwa kufufuka, tutazame kwanza ni wapi alipotabiriwa kuteswa, na kuzikwa, na kukaa kaburini siku tatu.

  1.KUTESWA

Unabii wa mateso ya Bwana Yesu kwaajili ya dhambi zetu upo wazi katika unabii wa Isaya.

Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.

5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

   2. KUZIWA NA KUKAA KABURINI SIKU TATU (3)

Unabii wa Bwana Yesu kukaa kaburini siku tatu, umejificha nyuma ya maisha ya nabii YONA,..Bwana YESU mwenyewe alisema kama vile Yona alivyokaa tumboni mwa samaki siku tatu mchana na usiku ndivyo na yeye atakavyokaa katika moyo wa nchi siku tatu.

Mathayo 12:39 “Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.

40  Kwani kama vile Yona alivyokuwa siku tatu mchana na usiku katika tumbo la nyangumi, hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku tatu mchana na usiku katika moyo wa nchi”.

Kwahiyo maisha ya Yona yalibeba unabii wa Bwana YESU wa kukaa kaburini siku tatu. Na ndiyo ishara pekee iliyofanikiwa kuwafanya watu wa Ninawi waokoke na adhabu kutoka kwa Mungu. Vivyo hivyo kwa kuamini ishara ya Bwana Yesu ya kufa na kufufuka tunapata kuokoka na ziwa la moto, aliloandaliwa shetani na malaika zake.

     3. KUFUFUKA

Unabii wa kufufuka kwa Bwana Yesu kwa sehemu tunaupata katika habari hiyo hiyo ya Yona, kwani Yona baada ya kukaa katika tumbo la samaki mwishowe alitapikwa na yule samaki, vile vile kwa KRISTO, baada ya siku tatu alifufuka kutoka kaburini.

Lakini Zaidi sana pia Daudi, kwa kuwa ni nabii aliona ufufuo wa YESU (Masihi)..na kutabiri kuwa “hataona uharibifu wala roho yake haitasalia kuzimu” (Soma Zaburi 16:10). Lakini Mtume Petro anakuja kuuweka vizuri unabii huo wa Daudi katika kitabu cha Matendo ya Mitume mlango wa pili.

Matendo 2:29 “Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo.

30  BASI KWA KUWA NI NABII, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi;

31  yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, ALITAJA HABARI ZA KUFUFUKA KWAKE KRISTO, YA KWAMBA ROHO YAKE HAIKUACHWA KUZIMU, WALA MWILI WAKE HAUKUONA UHARIBIFU.

32  Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake”.

Na ndivyo ilivyotokea kama Daudi alivyotabiri “mwili wa Bwana haukuona uharibifu (yaani haukuoza)” na vile vile “roho yake haikubaki kuzimu” ndio maana alifufuka baada ya siku tatu.

Kwahiyo biblia ilishatabiri yote kuhusiana na maisha ya Bwana Yesu kuanzia kuzaliwa kwake mpaka kufa kwake na mpaka kupaa na kurudi kwake mara ya pili, na utawala wake wa miaka elfu hapa duniani, na nafasi yake katika umilele ujao.

Unabii wa Bwana Yesu kuzaliwa Bethlehemu kasome Mika 5:2, unabii wa Bwana Yesu kuingia Yerusalemu kwa shangwe akiwa juu ya mwana-punda huku akiimbiwa Hosana Hosana kasome Zekaria 9:9, unabii wa Bwana Yesu kusalitiwa na Yuda kasome Zaburi 41:9, unabii wa mavazi ya Bwana Yesu kugawanywa kwa kura kasome Zaburi 22:18.

Unabii wa Bwana Yesu kupewa kuzungumza maneno yale “Mungu wangu mbona umeniacha” kasome Zaburi 22:1,  Unabii wa Bwana Yesu kupewa Siki badala ya maji kasome Zaburi 69:21, unabii wa Bwana Yesu kusulibiwa pamoja na wahalifu upo katika Isaya 53:12 n.k N.K

Je umempokea huyu YESU?..kama bado basi fahamu kuwa nafasi yako ni leo na si kesho. Kwasababu upo unabii wa kurudi kwake ambao tupo mbioni kuushuhudia, saa yoyote KRISTO anatokea mawinguni na kuwanyakua walio wake, je wewe ambaye hujaokoka utakuwa wapi?

Mpokee Bwana Yesu leo na kubatizwa na kujazwa Roho Mtakatifu.

Ikiwa utahitaji msaada leo katika kuokoka basi wasaliana nasi kwa namba zetu zilizoanishwa mwisho wa somo hili au fungua hapa >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

TUNAMHITAJI SANA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUYAELEWA MAANDIKO.

MADHARA YA KUTAFUTA ISHARA.

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

YONA: Mlango 1

YONA: Mlango wa 2

Rudi nyumbani

Print this post

Edomu ni nchi gani kwasasa?

Swali: Edomu ni wapi kwa sasa?


Maana ya “Edomu” ni “mwekundu”.. Asili ya jina hili kabla halijawa jina la Taifa, ni mwana wa kwanza wa aliyeitwa “Esau”. Biblia inasema Esau alipozaliwa alikuwa mwekundu mwili mzima kama vazi la nywele, tofauti na ndugu yake Yakobo!.

Mwanzo 25:21 “Isaka akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye Bwana akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba.

22 Watoto wakashindana tumboni mwake. Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda kumwuliza Bwana.

23 Bwana akamwambia, Mataifa mawili yamo tumboni mwako,Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako.Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili,Na mkubwa atamtumikia mdogo.

24 Siku zake za kuzaa zilipotimia, tazama! Mapacha walikuwamo tumboni mwake.

25 Wa kwanza akatoka, NAYE ALIKUWA MWEKUNDU MWILI WOTE kama vazi la nywele. Wakamwita jina lake Esau”.

Baadaye Esau ambaye aliitwa jina lingine “Edomu”(Soma Mwanzo 36:8 na 25:30 na 36:19) alisafiri pande za kusini pamoja na familia yake na Bwana akawabariki na kuzaliana na kuwa Taifa kubwa, na ndipo Taifa hilo likaitwa Edomu, kufuatia jina la baba yao Esau, kama tu vile Taifa la Israeli linavyoitwa leo, kufuatia jina la baba yao Yakobo, aliyeitwa Israeli.

Mwanzo 36: 1 “Hivi ndivyo vizazi vya Esau, ndiye Edomu.

2 Esau alitwaa binti za Kanaani, kuwa wakeze; Ada, binti Eloni, Mhiti, na Oholibama, binti Ana, binti Sibeoni, Mhivi;………………………………

6 Esau akawatwaa wakeze, na wanawe, na binti zake, na watu wote wa nyumbani mwake, na ng’ombe zake, na wanyama wake wote, na mali yake yote, aliyoyapata katika nchi ya Kanaani; AKAENDA MPAKA NCHI ILIYO MBALI NA YAKOBO NDUGUYE.

7 Maana mali yao yalikuwa mengi wasiweze kukaa pamoja, wala haikuweza nchi ya kusafiri kwao kuwachukua, kwa sababu ya wanyama wao.

8 Esau AKAKAA KATIKA MLIMA SEIRI, ESAU NDIYE EDOMU.

9 Hivi ni vizazi vya Esau, baba ya Edomu katika mlima Seiri”

Eneo la Edomu kwa sasa ni sehemu katika nchi ya Yordani upande wa kusini magharibi na  katika nchi ya Israeli upande wa kusini, Taifa hili kwasasa halipo tena!!, lilishapotea… isipokuwa eneo Taifa hilo lilipokuwepo ndio sasa linamilikiwa na Israeli pamoja na Yordani katika upande wa kusini wa nchi hizo mbili.

Kufahamu unabii na ujumbe tunaoweza kuupata kupitia Taifa hili la Edomu soma kitabu cha Obadia, au fungua hapa >>>VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 14 (Yoeli, na Obadia).

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MWINUE YESU KRISTO KATIKA MAISHA YAKO.

NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?

MWINUE YESU KRISTO KATIKA MAISHA YAKO.

SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Uweza wa kifalme utakuwa begani mwake” (Isaya 9:6)?.

Jibu: Turejee Isaya 9:6,

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; NA UWEZA WA KIFALME UTAKUWA BEGANI MWAKE; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa Amani”.

Katika jeshi lolote lile, liwe la Ulinzi au la wananchi, kunakuwa na vyeo.  Si askari wote wanafanana kimadaraka, wapo wenye madaraka makubwa na wapo wenye madaraka madogo. Na utaona ili kumtofautisha askari mmoja na mwingine kimadaraka, wanakuwa na sare ambazo zina alama Mabegani mwao, alama hizo ni maarufu kama “Nyota”.

Sasa nyota zile mabegani si ‘urembo’ bali zinafunua mamlaka Fulani/cheo cha yule askari.. ndio utaona wale wenye nyota nyingi basi wanakukuwa na Vyeo vikubwa Zaidi na mamlaka makubwa Zaidi.

Kwamfano utaona “Jenerali wa Jeshi” ndiye mtu mwenye cheo kikubwa Zaidi katika jeshi, na mara nyingi anakuwa ameshapitia ngazi zote za chini kama Ukoplo, Brigedia Jenerali, meja-Jenerali, au luteni-Jenerali.

Na mpaka amefikia ngazi hiyo ya Ujenerali, maana yake ndiyo ngazi ya juu na hakuna nyingine. Na anatofuatishwa na Askari mwingine si kwa sura, jinsia au kimo, bali anatofautishwa na “ule uwezo uliopo begani mwake” (yaani zile nyota nne begani mwake). Askari wengine waonapo zile nyota mabegani basi watapiga saluti na kutii..

Sasa serikali nyingi za kidunia zimenakili baadhi ya mambo kutoka katika Serikali iliyo juu (yaani ya mbinguni).

Kama yupo Jenerali wa jeshi la wanadamu, vile vile yupo JENERALI MKUU WA JESHI LA MBINGUNI, na huyo si mwingine Zaidi ya BWANA YESU KRISTO!. Ambaye ana nyota zi kifalme begani mwake, nazo ndizo hizo zilizotajwa (MSHAURI WA AJABU, na MUNGU MWENYE NGUVU, na BABA WA MILELE na MFALME WA AMANI).

Hiyo ndio maana biblia inamtaja BWANA YESU KRISTO kama BWANA WA VITA, na MFALME WA WAFALME, Kwasababu yeye ni Jenerali Mkuu.

Ufunuo 17:14  “Hawa watafanya vita na Mwana-Kondoo, na Mwana Kondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana, na Mfalme wa Wafalme, na hao walio pamoja naye ndio walioitwa, na wateule, na waaminifu”.

YESU pekee ndiye njia ya  UZIMA, na Bwana wa vita, na Mfalme wa Wafalme, ambaye hana wa kulinganishwa naye, kwasababu ndiye mwenye mamlaka yote ya mbinguni na duniani (Mathayo 28:18).

Je umemwamini Huyu Mkuu (YESU)?.. Je bado hujaona tu kuwa hakuna wokovu kwa mwingine yoyote isipokuwa yeye?..bado hujaona tu kuwa hakuna mwenye nguvu nyingi Zaidi yake yeye?.

Yeye pekee yake ndiye mwenye uwezo wa kufungua na kufunga, leo hii kama utampokea Basi atakufungua katika vifungo vya dhambi na mizigo yote ya adui shetani (Mathayo 11:28), vile vile atakufungua na vifungo vyote vinavyokutesa, kwasababu Bega lake linahubiri UWEZA MKUU.

Isaya 22:22 “Na ufunguo wa nyumba ya DAUDI NITAUWEKA BEGANI MWAKE; yeye atafungua wala hapana atakayefunga; naye atafunga wala hapana atakayefungua.”

Bwana akubariki.

Maran atha!

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

Nini maana yake, mpumbavu kuwa na fedha mikononi mwake ya kununulia hekima, Ikiwa hana moyo wa ufahamu?

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Swali: Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.

Je ni kweli hakuna aliyepaa mbinguni zaidi ya Mwana wa Adamu? (Yohana 3:13)

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya kumsulibisha mwana wa Mungu mara ya pili?

SWALI: Nini maana ya kumsulibisha mwana wa Mungu mara ya pili, na kumfedhehi kwa dhahiri?

JIBU: Neno hilo tunalisoma katika kifungu hiki;

Waebrania 6:4  Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, 5  na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,

6  wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.

Anazungumzia kundi la watu ambao walishapitishwa katika hatua zote tano (5), za uzuri wa Mungu na matendo makuu ya Mungu ndani ya maisha ya mwaminio. yaani.

i)Kupewa nuru ya injili,

ii)kuonja kipawa cha mbinguni,

iii) kufanywa mshirika wa Roho Mtakatifu,

iv) kulionja Neno zuri la Mungu,

v) na kuonja nguvu za zamani zijazo.

Kwamba watu wa namna hii wakianguka, kamwe haiwezekani kuwafanya wakatubu upya.

Lakini halengi kundi la watu walio wachanga kiroho, au waliorudi nyuma kwa kukosa maarifa, au kudanganywa au kwasababu nyingine zozote, bali kundi la watu ambao wanamjua  vema Mungu wao, na wanaelewa kabisa wanachokwenda kukifanya ni nini, Ni watu ambao wameshaonja Baraka na neema zote za Bwana, hawa ndio haiwezekani kuwageuza upya wakatubu pale wanapoanguka. Biblia inasema wanachofanya ni  sawa na kumsulibisha Yesu mara ya pili.

> Sasa swali linakuja wanamsulibishaje mwana wa Mungu mara ya pili, na wanamfedhi kwa namna gani?

Tengeneza, picha mume amemfumania mke wake katika uzinzi. Sasa kutokana na yale maumivu ya kusalitiwa akataka kumfukuza, lakini Yule mwanamke akamlilia kwa kumwomba msamaha, akikiri kuwa hatarudia tena uovu ule, asamewapo. Basi Yule mwanamume akamsamehe, na kuachilia uchungu wote, maisha yakaendelea. Lakini baada ya kipindi kupita Yule muma akamfumania tena mke wake katika uzinzi, Unadhani kitendo kile kitanyanyua hisia gani kwa Yule mwanaume?

Bibla shaka ataona ni kama ametoneshwa majeraha ambayo yalishapona zamani kwa gharama kubwa alizoingia kumsamehe wakati ule. Ni sawa, anakumbushwa yale maumivu ya mwanzo. Ndivyo ilivyo kwa Bwana wetu Yesu Kristo, pale unapoacha wokovu ambao umeshaujua uzuri wake, kisha ukarudia yale yale maisha ya kale, ni sawa na kumrudishia Kristo maumivu aliyoyapata pale msalabani siku ile alipokusamehe dhambi zako. Unamsulibisha mara ya pili. Unampa mateso ambayo tayari alishayamaliza, unakuwa huna tofauti na wale waliompiga pale masalabani.

>Lakini hapo anaposema unamfedhehi kwa dhahiri. Anamaana ya unamzalilisha kwa wazi (yaani hadharani).

Chukua tena mfano; Mtu ameingia gharama ya kukupikia chakula kizuri cha heshima, akitarajia kuwa  utakapokula utakifurahia na kukipenda. Lakini ulipopewa kukila ulionyesha kukipenda pale mwanzoni, mara ghafla ukakichukia na kukitema mbele yake, na baadaye ukakimwaga, na baada ya hapo ukaenda kununua chakula chako kingine,ukala tena mbele yake. Jiulize Yule mpishi wako atajisikiaje?

Ataona umemfedhi, umemzalilisha, kama vile kazi aliyoifanya kwako ni bure, . Ndivyo Bwana, anavyoona, wale wanaorudi nyuma. Wanamdhalilisha, kuifanya kama vile kazi ya msalaba, inamapungufu fulani, ni ujinga tu uliofanyika pale, Roho Mtakatifu ni uongo, nguvu za Mungu ni dhaifu. Na ndio maana umeamua kugeukia mambo ya kidunia  uliyokuwa umeyaacha zamani.

Hivyo hatua kama hii, ni mbaya sana. Vifungu hivi ni kutufundisha zipo hatari nyingi kwa mkristo anayerudi nyuma kwa makusudi. Kamwe usiruhusu jambo hilo maisha mwako.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

FUVU LA KICHWA.

VITA VYA KIFIKRA BAADA YA KUZALIWA MARA YA PILI

MJUE SANA YESU KRISTO.

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

Rudi nyumbani

Print this post

Mata ni nini (Mwanzo 27:3).

Mata ni kitu gani na imebeba  ujumbe gani kiroho?


Jibu: Turejee,

Mwanzo 27:2 “Akasema, Tazama, sasa mimi nimekuwa mzee, wala sijui siku ya kufa kwangu.

3 Basi, nakuomba, chukua MATA yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo;  4 ukanifanyie chakula kitamu namna ile niipendayo, ukaniletee, ili nile; na roho yangu ikubariki, kabla sijafa”.

“Mata” Ni jina jingine la “Silaha”. Kwahiyo badala ya kutumia neno “silaha” ni sahihi pia kutumia neno “Mata”.

Kwahiyo mstari huo wa tatu (3) ni sahihi kuuweka hivi,… “chukua SILAHA yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo ”

Na silaha hiyo inaweza kuwa mkuki, mshale au upanga, lakini katika andiko hilo silaha (Mata), iliyomaanishwa pale ni “Mshale”. Na kwanini ni mshale na si upanga wala mkuki?.. ni kwasababu kuna Podo imetajwa pale na upinde..

Maana yake huwezi kubeba upanga na upinde bila mshale, hivyo ni wazi kuwa Mata iliyomaanishwa pale ni mshale, kwasababu kuna upinde na Podo.

Sasa kwa maarifa kuhusu “Podo” na ufunuo wake kiroho waweza fungua hapa >>> Podo ni nini na umuhimu wake ni upi rohoni?

Sasa hizi zote ni silaha za mwili, lakini biblia inatufundisha kuwa zipo silaha za roho ambazo kila mkristo ni lazima azivae, na silaha hizo tunazisoma katika kitabu cha Waefeso 6:10-18, ambazo ni Chapeo ya Wokovu, Dirii ya Haki, Ngao ya Imani, Kweli, Upanga wa Roho, na Utayari miguuni pamoja na sala na maombi.

Na kwa silaha hizo pekee ndio tutaweza kumshinda adui yetu shetani, kwa mapana kuhusiana na silaha hizi jinsi ya kuvizaa na namna zinavyotenda kazi fungua hapa >>>MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

UTHABITI WA AGANO LA MUNGU KWA MKRISTO.

JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.

KWANINI UPIGE MISHALE CHINI?

NDUGU,TUOMBEENI.

Nini maana ya  Mithali 21:1 Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana;

Rudi nyumbani

Print this post