SWALI: Naomba kufahamu ujumbe ulio katika Mithali 29:5
‘Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake, Hutandika wavu ili kuitega miguu yake’.
JIBU: Mithali hii inazungumzia madhara yanayoibuka katika tabia ya kujipendekeza.
Kujipendekeza ni kitendo cha mtu kumthaminisha mtu, hata kama alikuwa hastahili sifa hizo, ili tu upate kitu Fulani kutoka kwake. Kumthaminisha kunaweza kuwa kumsifia, au kumpongeza, au kumzungumzia mema yake kupita kiasi, au kueleza mabaya ya wengine kwa huyo mtu, n.k.
Na yote hayo hayawi kwa lengo la kuuthamini kweli uzuri wa Yule mtu, hapana bali ni aidha upate kupendwa wewe zaidi ya wengine, au usaidiwe, au upewe cheo, au kipaumbele Fulani. Hata kama utaona mabaya yake huwezi kumwambia kwasababu, huna lengo la kusaidia bali upate matakwa yako tu.
Sasa hilo ni kosa, matokeo ya hilo biblia inatuambia “unamtandikia wavu ili kuitega miguu yake”. Yaana unampeleka kwenye mtego au aungamivu wake kabisa. Hii ni kweli, tunaona hata viongozi wengi wa nchi wameponzwa na wasaidizi wao wa karibu,na matokeo yake wakaiharibu nchi, kwasababu tu ya kupokea sifa za uongo kutoka kwao, kwamba wanafanya vema, wanawajibiki vizuri n.k.. Kama ilivyokuwa kipindi kile cha Mfalme Sedekia na wale manabii wa uongo wajipendekezao, walimtabiria uongo, lakini Yeremia alimweleza mfalme ukweli hawakutaka kumsikiliza. Matokeo yake Mfalme Sedekia akaingia katika matatizo makubwa ya kutobolewa macho na kupelekwa utumwani, hiyo yote ni kwasababu alikaa na manabii wajipendekezao (Yeremia 34-41), kama tu ilivyokuwa Kwa Mfalme Ahabu naye na manabii wake mia nne wa uongo.
Hii ni kutufundisha nini?
Hasaa biblia hailengi, tuwe makini na watu wajipendekezao. Hapana, kwasababu wakati mwingine si rahisi kuwatambua, inahitaji neema ya Mungu. Lakini inalenga hasaa katika upande wetu , kwamba sisi tujiepushe na ‘tabia ya kujipendekeza”. Kwasababu tunaweza kudhani tunatafuta faidi yetu tu wenyewe, lakini kumbe tunamsababishia madhara Yule mtu ambaye tunajipendekeza kwake. Tunategea wavu mbaya sana, aanguke na kupotea kabisa, na huo si upendo.
Itakusaidia nini akutendee mema, halafu yeye aangamie?
Hivyo, pastahilipo kweli kusifia tusifie, lakini si kwa lengo la kujipendekeza, kwasababu tukienda huko, tunatenda dhambi kubwa zaidi. Hiyo ndio maana ya hivyo vifungu, tufikiriapo kujipendekeza, tuone kwamba ni watu wasio na hatia tunawategea wavu waangamie.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
TUZIJARIBU HIZI ROHO.
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
USIJISIFIE KARAMA KWA UONGO.
Rudi Nyumbani
Nehemia 8:10
[10]Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa BWANA wetu; wala msihuzunike; KWA KUWA FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU.
Ni habari ya kutafakarisha, lakini zaidi sana ya kuwafariji watu wote wampendao Mungu. Tukisoma katika biblia ile habari ya Ezra na Nehemia, katika juhudi zao wa kuwarejesha Israeli katika ibada na njia za Mungu Yerusalemu.
Tunaona wakati ule ukuta wa Yerusalemu ulipomalizwa kujengwa baada ya kurudi kwao utumwani Babeli, Ezra hakuwaacha tu hivi hivi, wafurahie kukamilika kwa majengo, bali alitaka wakamilishwe na mioyo yao hivyo, alikichukua kitabu cha Torati na kuanza kuwasomea wayahudi wote tangu asubuhi mpaka adhuhiri, ili wajue ni nini Bwana anataka kwao (Nehemia 8).
Na waliposikia waliona makosa yao mengi sana, na hukumu nyingi za Mungu, alizowatamkia kufuatana na makosa yao, yaliyowapelekea mpaka wakachukuliwa mateka. Ikumbukwe kuwa kitabu hicho cha torati hakikuwahi kusomwa tangu zamani walipochukuliwa utumwani, ndio ilikuwa mara yao ya kwanza kukisoma baada ya miaka mingi kupita.
Hivyo wayahudi kusikia vile wakaanza kulia sana na kujuta na kuomboleza. Lakini tunaona kuna jambo lilifanyika la kitofauti.
Nehemia, alitambua wazo la Mungu…Hivyo akawazuia watu kulia na kuomboleza kwa ajili ya makosa yao. Kinyume chake akawaambia leo ni siku takatifu kwa Bwana, hivyo mle ,.mnywe, mtoe sadaka, mfurahi mbele za Mungu wenu kwasababu “furaha ya BWANA ni nguvu zenu”
Hivyo watu wakasheherekea, badala ya kulia, Sio kwamba Nehemia alisheherekea makosa yao, hapana, bali alipewa kujua kwamba furaha ya mtu kwa Mungu wake, ndio chanzo cha nguvu ya kumtumikia yeye.
Ndio hapo baada ya wayahudi kujua makosa yaowakimfurahia Mungu, siku hiyo, na wakapokea nguvu nyingi za kuishika sheria ya Mungu.
Yaani kwa namna nyingine, Mungu kuwakemea makosa yao,lengo lake lilikuwa sio awahukumu, au wainamishe vichwa vyao wakidhani kuwa wao ni kichefu-chefu kwake. Hapana..Bali anawapenda na hivyo anatarajia wajue nia ya makemeo yake.
Nehemia 8:10 Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu.
11 Hivyo Walawi wakawatuliza watu wote, wakasema, Nyamazeni, kwa maana siku hii ni takatifu; wala msihuzunike.
12 Na watu wote wakaenda zao kula na kunywa, na kuwapelekea watu sehemu, na kufanya furaha nyingi, kwa sababu walikuwa wameyafahamu maneno yale waliyohubiriwa
Ni hata sasa, unaposoma biblia na kuona inakushitaki, inakuambia usiibe, usisengenye, amchukiaye ndugu yake ni sawa na muuaji, wazinzi wote sehemu yao ni katika lile ziwa la moto, inapokukemea maovu yako ya siri.. Usiinamishe kichwa na kusema “mimi sifahi mbele za Mungu, mimi ni mkosefu sistahili kuitwa mwana wake”..Ukaacha kukisoma kabisa, ukawa unalia tu, umenyong’onyea, na kujihisi wewe ni wajehanamu tu, Mungu hakupendi, ameshakuacha, ona sasa unamkosea kosea kila siku… Fahamu kuwa hilo sio kusudi la Mungu.
Kusudi la Mungu sio usome biblia, ujawe na hisia za Mungu kukuhukumu, au kukulaumu, au kukushitaki, bali kusudi la Mungu ni ujue upendo wake uliozidi sana kwako, kiasi cha yeye kuonyesha hisia zake kwako namna ambavyo unapaswa uwe kama yeye.
Hivyo ukitoka kuonywa na kukemewa, unapaswa utoke kwa kufurahi moyoni na kuruka-ruka, na hapo ndipo utapokea nguvu ya kuishinda hiyo dhambi. Lakini ukitoka kinyonge na mashaka utashindwa kwasababu furaha ya Bwana ndio chanzo cha nguvu zetu. Ukilipenda hilo katazo, utalitenda, usipolipenda kamwe huwezi litenda.
Mtunga Zaburi alisema,
Zaburi 119:52
[52]Nimezikumbuka hukumu zako za kale, Ee BWANA, nikajifariji.
Bwana anataka tuone upendo wake kwetu katika makemeo yake, tufarijike tupokee nguvu ya kushinda. Pengine umetoka kufanya dhambi fulani ya makusudi na Roho Mtakatifu akakumbusha kuwa watu wa namna hii, huangukia katika mtego mbaya wa shetani bila kunasuka, Sasa hapo usianze kupoteza ladha na Mungu wako, au biblia, ukauchukia wokovu, kabisa, maanisha kutubu, jifunze kutokana na makosa, kisha furahia mwambie Bwana asante kwa kunipenda,
hata wachezaji wa mpira, wafungwao kipindi cha kwanza, wanapotulia na kujihamasisha tena, hupokea nguvu ya kucheza vema kipindi cha pili, lakini wajilaumupo, hufanya vibaya zaidi
Na sisi pia tuiamshe furaha ya Bwana daima.Kila tusomapo Neno lake, tufurahi kwasababu ni barua ya upendo wa Mungu kwetu Ili tuweze kuwa na nguvu.
Kwasababu furaha ya Bwana ndio nguvu yetu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SHUKURU KWA KILA JAMBO.
Furaha ni nini?
Fahamu maana 1Wakorintho 14:20 “Ndugu zangu msiwe watoto katika akili zenu;
Usi!.. Usi!.. Usi! na sio Msi!… Msi!.. Msi!..
Amri za Mungu zinasema Usiue, Usizini, Usiibe … na sio Msiibe, Msiue, Msizini… Ikifunua kuwa Mungu anaongea na mtu mmoja mmoja… Anasema na Mimi kivyangu, lakini pia anasema na wewe kivyako… Na hatuambii wote kwa pamoja.
Kutoka 20:13 “Usiue.
14 Usizini.
15 Usiibe.
16 Usimshuhudie jirani yako uongo.
17 Usiitamani nyumba ya jirani yako…”
Siku ya Hukumu, hatutahukumiwa kwa pamoja, kila mtu atasimama peke yake, na kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe..
Wagalatia 6:5 “Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe”.
Na tena kila mtu atatoa habari zake mwenyewe na si pamoja na mwenzake..
Warumi 14:12 “Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu”
Sasa kama ni hivyo kwanini Boss wako akukoseshe?..kwanini Rafiki akukoseshe, kwanini wanadamu wakukoseshe??… Na ilihali utasimama peke yako siku ile.
Kumbuka unapofanya uzinzi, siku ile hutakuwa na yule aliyefanya naye uzinzi, badala yake utasimama wewe kama wewe (kwasababu ile amri inakuhusu wewe, na Mungu alikuwa anazungumza na wewe kivyako na si wewe pamoja na mwenzako)..
Kama unaiba, siku ile hutasimama na aliyekushawishi ukaibe, au uliyekuwa unashirikiana naye katika wizi.. wewe utakuwa peke yako, na yeye peke yake….kwasababu Amri ya Usiibe, uliambiwa wewe, nimeambiwa mimi na si wewe pamoja na mimi… Hivyo kila mtu atatoa habari zake mwenyewe.
Kama unaua, ni hivyo hivyo, kama uwaheshimu wazazi ni hivyo hivyo, na amri zote ni hivyo hivyo..
Hukumu ya Mungu inatisha!.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je! sisi kama watakatifu tunaowezo wa kuamuru hukumu?
WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA; NAO WATAMWOMBOLEZEA.
NI WAKATI GANI SHETANI ANAPENDA KUMSHAMBULIA MWAMINI?
Kuna wakati Elisha alifika Gilgali na mahali pale palikuwa na njaa kali, na watu wengi (manabii) pia walikuwa wamekusanyika kusikiliza mashauri ya mtu wa Mungu.
Hivyo akawaambia waweke sufuria motoni waandae chakula.
Lakini mmojawao akatoka akaenda mashambani kutafuta mboga. Na huko akafanikiwa kweli kukusanya zilizo bora, lakini kwasababu hakuwa na maarifa ya kutosha jinsi ya kutambua mboga sahihi ziwafaazo wanadamu akaona huko matango mwitu, na bila kujua, akidhani ni matango halisi, akayachuma na kuyaleta sufuriani. Matango yale yalikuwa ni sumu.
Lakini walipoonja kwa neema za Mungu walijua kuna kitu ambacho sio sahihi kimewekwa sufuriani, hivyo waacha wote kula. Ndipo Elisha akataarifiwa, juu ya jambo hilo, kama kimwagwe lakini kile chakula hakikumwagwa, bali aliwaagiza watie unga mule (kwa Neno la Bwana), na chakula kitaponyeka. Wakafanya hivyo, kikawa sawa, wakala wakashiba.
2 Wafalme 4:38-41
[38]Elisha akafika Gilgali tena; na kulikuwa na njaa katika nchi; na hao wana wa manabii walikuwa wakikaa mbele yake. Akamwambia mtumishi wake, Teleka sufuria kubwa, uwapikie wana wa manabii.
[39]Na mmoja wao akaenda nje kondeni ili kuchuma mboga, akaona mtango-mwitu, akayachuma matango-mwitu, hata nguo yake ikawa imejaa, akaja akayapasua-pasua sufuriani; kwa maana hawakuyajua.
[40]Basi wakawapakulia hao watu ili wale. Ikawa, walipokuwa katika kula chakula, wakapiga kelele, wakasema, Mauti imo sufuriani, Ee mtu wa Mungu. Wala hawakuweza kula.
[41]Lakini yeye akasema, Leteni unga. Naye akautupa ndani ya sufuria; akasema, Wapakulie watu, ili wale. Wala hakikuwamo kitu kibaya sufuriani.
Inatueleza hali ya kiroho ya watu iliyopo sasa.
Palipo na njaa ni rahisi mtu kula kila kitu, ilimradi tu asife. si rahisi akae chini na kufikiria ubora wa kile anachokula. Leo hii njaa ya Neno la kweli la Mungu ni kubwa, hivyo kila mtu anaenda kondeni kuokota kitu kimfaacho, huko huko tunakutana na vizuri lakini pia tunakutana na vibaya..
shida ipo hapo, je tunaweza kupambanua?
Kwasababu ukila sumu, ile sumu haitakuambia ngoja nisikuletee madhara kwasababu hukukusudia kunila, au hukujua kuwa mimi ni sumu, utakufa tu sawasawa na yule anayejua anachokifanya.Kumbe ujinga una gharama kubwa.
Bwana Yesu alisema..
Mathayo 7:15
[15]Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.
Mafundisho yasiyomhubiri Kristo na utakatifu, ni kuwa makini nayo, ni heri usiyasikilize kabisa kwa usalama wako wa kiroho. Yanayokuambia tunaokolewa kwa neema tu, hivyo matendo yako ni kazi bure mbele za Mungu, ukiokolewa umeokolewa milele, hata ukiwa unatenda dhambi vipi huwezi potea, yapime sana hayo mafundisho.
Mafundisho ya kuzimu-kuzimu tu na majini na wachawi epukana nayo, Mafundisho ya sanamu ibadani, ni mauti chunguni. Mafundisho yanayopinga habari za mwisho wa dunia, ambayo hayana habari na unyakuo au kumfanya mtu atazame kurudi kwa pili kwa Kristo, kinyume chake ni kukuweka kidunia, ufikirie mafanikio ya mwilini ni matango mwitu.
Manabii wa uongo ni wengi, wapo wanaotenda kazi kwa uwazi, lakini wapo wanaotenda kazi kwa siri.
Jifunze kusoma biblia, jinsi usomavyo Neno la Mungu utagundua kuwa mtu uliyeokoka kwa wakati uwapo hapa duniani Bwana anakutana Utembee katika utakatifu (Waebrania 12:14). Lakini pia uelekeze macho yako mbinguni kwa yale mambo yajayo, ya mbingu mpya na nchi mpya.
Luka 12:35-36
[35] Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka; [36]nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.
Jihadhari na matango mwitu.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>>> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini Mungu akuumbe hivyo ulivyo? Kwanini asingeweka pembe kichwani kwako, au kwanini asingekuwekea vilemba vya nyama kama vile vya kuku kichwani, au antena mbili kama zile za konokono au mdudu, bali amekuwekea nywele kichwani pako.
Sauti ya Mungu ipo katika maumbile yetu. Sisi kujikuta hivi tulivyo sio kwamba, ndio umbile bora zaidi ya yote Mungu aliloona linamfaa mtu, hapana, tungeweza kuumbwa vizuri zaidi hata ya mwonekano huo tulionao, lakini tumebuniwa hivi, kwa kusudi la kipekee ambalo tunapaswa tulijue, na sio kwa kusudi la urembo.
Kwamfano usipoweza kuelewa utendaji kazi wa mwili wako jinsi viungo vinavyoshirikiana huwezi kuelewa jinsi kanisa la Kristo linavyopaswa kufanya kazi likutanikapo, kwasababu sisi tunaitwa viungo mbalimbali ndani ya mwili wa Kristo.Umeona? Bwana akasema kiungo kimoja kikiumia, vyote vimeumia.
Hivyo tumeumbwa, kimalengo sio kimwonekano bora au kiuzuri,. Ni sawa na mtu aulizwe kati ya jiko, na maua kipi kina umuhimu zaidi kuwepo ndani mwako. Ni wazi kuwa atasema jiko,kwasababu litamsaidia kupika. Hakulichagua kwasababu lina mwonekano bora, lakini kwasababu lina matumizi muhimu zaidi ya vingine.
Vivyo hivyo na wewe ujitazamapo mwili wako, usijitazame kiuzuri kuliko viumbe vingine, au wanadamu wenzako, bali fikiria tu katika picha ya matumizi ya kila kiungo ulichopewa, kinakufundisha nini kuhusu muumba wako au kinatimiza kusudi gani kwa Mungu wako. Hilo ndio lengo hasaa la wewe kubuniwa hivyo ulivyo.
Leo tutaanza na NYWELE, kisha wakati mwingine tutatazama na viungo vingine;
Utazamapo nywele zako Bwana anataka ujue yafuatayo;
Mathayo 10:30 lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. 31 Msiogope basi; bora ninyi kuliko mashomoro wengi
Ni kawaida kudhani kuwa Mungu hathamini, au hajui kila kitu, au anasahau sahau. Lakini sivyo, ukimfuata Mungu, vitu vyako vyote vinavyotoka na kuingia vipo kimahesabu, hakuna kitu kinachotokea kwa ghafla tu, bila yeye kujua au kuruhusu, Hivyo mashaka yakija, kumbuka nywele zako zilivyo nyingi lakini zimehesabiwa, vivyo hivyo mambo yako yote yamehesabiwa.
Zaburi 69:4 Wanaonichukia bure ni wengi Kuliko nywele za kichwa changu. Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari, Adui zangu kwa sababu isiyo kweli. Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu Vitu nisivyovichukua
Jinsi nywele zako zilivyo nyingi, maadui nao vivyo hivyo. Na maadui zetu sio wanadamu bali ni mapepo ambayo mara nyingine huweza pia yavaa wanadamu, kutudhuru. Hivyo usiwe mtu wa kunung’unika au kulamimika, ujue kila mwanadamu yupo vitani. Kama Bwana wetu Yesu Kristo hakuwa na dhambi hata mmoja lakini alikuwa na jopo la maadui kwanini wewe usiwe nao. Hivyo kuwashinda ni kuwa mwombaji daima, na kutembea katika njia za Bwana sikuzote. Ukikumbuka kuwa maadui ni jambo la kawaida, kama tu nywele zako zilipo hapo kichwani.
Mathayo 5:36 Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi.
Wakati mwingine, tunajiaminisha na kujihakikishia mambo na kuweka na viapo juu yake kana kwamba mambo yote yapo ndani ya uwezo wetu. Kauli kama, “leo nife,kama sitakupa hiyo fedha” au “Mungu anipige hapa hapa kama ninalokuambia ni uongo” Kauli kama hizi, za kuongezea hakikisho lingine juu, hazitokani na Mungu, maneno yetu tumeambiwa yawe ndio ndio, au sio sio, zaidi ya hapo yanatokana na Yule mwovu. Kwahiyo popote unapojiona unakaribia kuzidi mipaka kumbuka hizo nywele zilizo juu yako hujawahi kuzifanya ziwe hivyo ulivyo, Bwana ndiye azibadilishaye, hivyo jiwekee mipaka.
Nywele zako hufunua nguvu zako za rohoni. Wanadhiri wote wa Mungu hawakuruhusiwa kukatwa nywele, Samsoni alipewa nguvu, kwa agano la kutokatwa nywele, kufunua kuwa watakatifu wote nywele zao za rohoni ndio nguvu zao. Lakini unapoacha mpango wa Mungu adui anazikata, kama ilivyokuwa kwa Samsoni. Lakini baadaye alipojua amefanya makosa ziliota tena lakini katika gharama za ‘kutoona’ tena.
Waamuzi 16:22 Lakini zile nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa kwake.
Tunza nguvu zako, usiruhusu kiwembe chochote cha mwovu kikupitie. Kwasababu hata zikirejea tena, hutakuwa kama hapo mwanzo.
Yeremia 7: 29 Zikate nywele zako, Ee Yerusalemu, uzitupe, Ukafanye maombolezo juu ya vilele vya milima; Kwa maana Bwana amekikataa na kukitupa Kizazi cha ghadhabu yake.
Zamani, kukatwa nywele zote kuisha kabisa ilikuwa ni ishara ya kuingia kwenye maombolezo, kwasababu utukufu wako umeuvua.
Maombolezo, kwa agano jipya sio kulia kama msiba, hapana bali kuingia kwenye maombi ya ndani kabisa, ya kuutafuta uso wa Mungu, ambayo huambatana na mifungo. Na leo, ni kila mara tunakwenda saluni kukata nywele zetu. Tujue Bwana anatutaka kama vile tukatavyo nywele zetu mara kwa mara ndivyo tukumbuke maombi ya kujimimina sana mbele zake.
Je! Somo hilo unajifunza mwilini mwako?
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
Mithali 13:20 Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.
Tulipokuwa watoto wazazi wetu walitufundisha kubagua baadhi ya marafiki tuliokuwa nao, na cha ajabu vigezo walivyotumia havikuwa hata rangi zao, au kimo chao, au afya zao, bali tabia zao na akili zao. Wale watoto waliokuwa na nidhani, na akili shuleni wazazi wetu walitushurutisha sana kukaa nao karibu, kwasababu waligundua kuwa na sisi tutaambukizwa tabia zao, lakini wale waliokuwa watukutu, hata tulipokutwa tunacheza nao tu, tuliadhibiwa, sisi tuliona kama ni uonevu usio kuwa na tija, lakini baadaye tulipokuwa watu wazima, na kuona hatma ya wale watoto, ndio tulijua ni nini wazazi wetu walikuwa wanakiona.
Vivyo hivyo katika maisha ya rohoni, tunaambiwa.
Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.
Ni watu waliookoka, wenye hofu ya Mungu ndani yao.
Mtu yeyote aliyemwamini Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake, huku akiendelea katika kumcha Mungu kwelikweli, huyo ni wa kukaa karibu naye sana. Kwasababu na wewe utajifunza njia za wokovu, utaambukizwa kuomba, utaambukizwa mifungo, utaambukizwa upendo wa ki-Mungu, lakini pia na maarifa ya Neno la Mungu, pamoja na uinjilisti.
Watu hawafahamu kuwa hata hekima ya mwokozi wetu Yesu haikuja tu kwa kutegemea hekima kutoka juu kwa baba yake, hapana, ilichangiwa pia na watu aliowachagua kukaa nao karibu, tangu alipokuwa mdogo, tunalithibitisha hilo pindi alipokuwa amekwenda Yerusalemu na wazazi wake kwa ajili ya kuila sikukuu, kama kijana angeweza kukaa na wenzake, kujifunza uchezaji wa kamari, au kutembea mitaani kutafuta wasichana, au kwenda kwenye dansi na sinema, na kujiunga na makundi ya wavuta bangi. Lakini, haikuwa hivyo kwake, yeye alichagua watu ambao wangekuwa ni wa muhimu kwake, ndio wale viongozi wa imani na waalimu waliotwa marabi, akawa akiwasikiliza hao na kuwauliza maswali, na ghafla akaambukizwa tabia zao, mpaka akawa yeye ndio RABI wao mkuu.
Luka 2:40 Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu, amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake. 41 Basi, wazee wake huenda Yerusalemu kila mwaka, wakati wa sikukuu ya Pasaka.
42 Na alipopata umri wake miaka kumi na miwili, walipanda kama ilivyokuwa desturi ya sikukuu;
43 na walipokwisha kuzitimiza siku, wakati wa kurudi kwao, yule mtoto Yesu alibaki nyuma huko Yerusalemu, na wazee wake walikuwa hawana habari.
44 Nao wakadhani ya kuwa yumo katika msafara; wakaenenda mwendo wa kutwa, wakawa wakimtafuta katika jamaa zao na wenzao;
45 na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta. 46 Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, AMEKETI KATIKATI YA WAALIMU, AKIWASIKILIZA NA KUWAULIZA MASWALI.
47 Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake. 48 Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.
49 Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu? 50 Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia
Mambo mengine hutaweza kuyaacha, au tabia nyingine hutaweza kuziondoa ndani yako. Kama hutaweka machaguzi ya watu sahihi wa kuongozana nao. Utakuta ni mkristo analalamika ni mzito wa kuomba, au kushuhudia, au kufunga. Ukiangalia kampani ya watu wake muda wote, ni wafanyakazi wenzake wa ofisini, ni marafiki zake wa chuo, ni majirani zake hapo mtaani. Lakini wapendwa, au watumishi wa Mungu waaminifu, ni jumapili tu kukutana nao kanisani, hata anapotafutwa, kukumbushwa wajibu wake kiroho, anawakwepa. Na wakati huo huo anatumainia awe moto kiroho. Hapo ni kujidanganya.
Tunahitaji kupashana moto, kamwe huwezi simama kipeke yako, haijalishi wewe ni nani, au unamjua Mungu kwa ukubwa kiasi gani. Tembea na waombaji ili uwe mwombaji, tembea na washuhudiaji ili uweze kushuhudia, kaa na waalimu ili uwe mwalimu. Nje ya hapo utageuzwa na ulimwengu,.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Usimwache rafiki yako mwenyewe, wala rafiki ya baba yako.
NGUVU YA HEKIMA NA AKILI
IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.
Rudi Nyumbani
SWALI: Nini maana ya hii Mithali 10:25
Kisulisuli kikiisha pita asiye haki hayuko tena; Bali mwenye haki ni msingi wa milele.
JIBU: Mstari huo unajifafanua vizuri kwenye ule mfano Bwana Yesu aliutoa kuhusiana na watu wanaoyasikia maneno yake, halafu hawayatendi. Tusome.
Mathayo 7:24 Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;
25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.
26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;
27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.
Hivyo tukirejea katika vifungu vile vya kwenye mithali. Unaweza kuelewa mtu asiye haki hasaa ni nani?
Ni Yule ambaye anaisikia injili, halafu hatii. Mtu Yule anayesema ameokoka, lakini zao la wokovu halionekana ndani yake. Rohoni anaonekana hana tofauti na yule ambaye hajamjua Mungu kabisa. Wote hao huitwa wasio haki. Bado wapo dhambini, hawajakombolewa na damu ya Yesu Kristo.
Hawa wataonekana kwa nje kama vile ni watakatifu. Lakini kinapokuja tu kisulisuli aidha cha majaribu, shida, dhiki, udhia,au mapigo kwa ajili ya Kristo, mara ghafla wanarudi nyuma, wanakuwa kama watu ambao hawajawahi kumjua Mungu kabisa, kwasababu hakujikita katika mwamba. Wengine sio majaribu ya shida, bali yale ya mafanikio makubwa, ndio hapo anasa zinawazidi wanamsahau Mungu, wanaiaga imani, kwani walimfuata Yesu kwasababu ya shida tu. Wengine ndoa, elimu, vyeo wakishavipata, huwaoni tena kwa Yesu.
Lakini mtu anayeyasikia maneno ya Kristo na kuyatii, ni kinyume chake, huitwa msingi wa milele. Huyo hatikiswi na wimbi, kisulisuli au dhoruba yoyote. Kwasababu yupo juu ya mwamba.
Okoka, upokee msamaha wa dhambi, kisha ishi kufuata na toba yako, ili uhakika wa kusimama uwe nao wakati wote.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
SWALI: Nini maana ya Mithali 28:28 Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha; Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.
JIBU: Mithali hii hulenga hasaa watawala, iwe ni serikalini, kwenye mataasisi, makanisa n.k. endapo waongozao ni waovu, basi hufanya hata watu (hususani wale wema) kujificha, Au kutoonekana kabisa.
Ndio kama ilivyokuwa katika kipindi cha mfalme Ahabu, alipoiharibu nchi yote ya Israeli kwa kuweka miungu migeni, akichochewa na mkewe Yezebeli. Wakati huo Manabii wengi wa Mungu waliuliwa, na wale waliosalia walijificha wasionekane kabisa, wakabakia tu makuhani wa baali na wenye dhambi. Kiasi kwamba Eliya akadhani ni yeye tu peke yake nabii aliyebakia Israeli. Kuonyesha ni jinsi gani wenye haki, walivyokuwa adimu wakati huo. Lakini Mungu alimwambia Eliya, nimejisazia watu elfu saba wasiopigia goti baali.
Warumi 11:3 Bwana, wamewaua manabii wako, wamezibomoa madhabahu zako, nami nimesalia peke yangu, nao wananitafuta roho yangu.
4 Lakini ile jawabu ya Mungu yamwambiaje? Nimejisazia watu elfu saba wasiopiga goti mbele ya Baali.
5 Basi ni vivi hivi wakati huu wa sasa, yako mabaki waliochaguliwa kwa neema.
Ni kama leo tu ulimwenguni, tunavyoona kiwango cha watenda maasi na maasi kinavyozidi kuongezeka, ndivyo inavyokuwa ngumu kukutana na watakatifu halisi, na hiyo inaweza pelekea pengine ukajidhani mpo wachache, au hakuna kabisa kama wewe.
Ukiwa katika mazingira kama haya usipumbazike, ukafanana na ulimwengu. Bali fahamu kuwa wapo, isipokuwa Mungu amewaficha tu. Siku watakapoondolewa waovu duniani ndipo utajua kuwa Mungu anao watakatifu wake, wengi.
Ndio maana ya hilo neno Bali “waangamiapo wasio haki, wenye haki huongezeka”.
Binti ambaye unatembea kwa kujisitiri barabarani, na huwenda huoni aliye kama wewe mtaa mzima, usife moyo, ni kwasababu wasio haki ni wengi. Kijana uliyeamua kuishi maisha ya mbali na uzinzi na anasa usijidhani upo peke yako, songa mbele tambua, ni Mungu amewaficha tu watu wake.
Kwasababu ni Neno la kweli kabisa wasio haki wastawipo, wenye haki hujificha, (sio kwamba wamekufa, bali wapo). Wakati utafika waovu wataondolewa, na sisi tutamiliki na kuangaza. Usiwe mfauta wimbi, nyakati hizi ni za hatari. Ni sawa na kichuguu tu, waweza kudhani hakina kumbikumbi ndani, kina huoni chochote kinachotoka humo, lakini wakati wa mvua, unastaajabia wingi wao umetoka wapi. Vivyo hivyo na wewe endelea kutembea kwa ujasiri katika wokovu wako. Unyakuo umekaribia. Tambua Bwana analo jeshi lake.
Mithali 28:28 Wasio haki wainukapo, wanadamu hujificha; Bali waangamiapo, wenye haki huongezeka.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
SWALI: Nini maana ya Mithali 27:15 Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi, Na mwanamke mgomvi ni sawasawa;
JIBU: Neno Kutona-tona kama lilivyotumika hapo, ni “maji yanayovuja darini”.
Hivyo anaposema Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi. Anamaanisha kitendo cha kuvuja sana kwa dari siku ya mvua nyingi, na kitendo cha kukaa na mwanamke mgomvi ndani ni sawasawa.
Kwa namna gani?
Tunajua ukikaa kwenye nyumba ambayo dari lake halikujengwa vizuri, mvua kubwa inaponyesha maji mengi huchuruzika na kuingia ndani. Wakati umelala utashangaa maji yanakudondekea kitandani mwako, yanachuruzikia kwenye makochi, yanakwenda mpaka kwenye makapeti, jambo ambalo litakufanya usitulie hata kidogo humo ndani utakuwa tu bize, kusogoza vitu ovyo ovyo visilowe, na mbaya ni pale mvua inapokuwa kubwa, na maji kuongezeka ndani, mwisho huwa ni kutoka kabisa nje na kuiacha nyumba.
Ikiwa umeshawahi kupitia changamoto kama hiyo ya kuvujiwa nyumba, unaelewa ni kero kiasi gani.
Ndivyo anavyofananisha kutendo hicho na kuishi na mwanamke mgomvi. Ikilenga hasaa wanandoa. Kumbuka aliyeandika mithali hizi ni Sulemani, alikuwa anatambua anachokisema, kwasababu aliishi na wanawake elfu moja(1000) kama wake zake, na alijua masumbufu yao. Alikutana na changamoto za baadhi yao.
Mwanamke mgomvi, kibiblia ni Yule asimheshimu mumewe, ni Yule anayemwendesha mumewe, anayemkaripia, asiyekuwa msikivu, kila jambo analolifanya mumewe ni kulikosoa tu, mwenye kiburi na mwenye maneno mengi, asiye na staha.
Wanawake wa namna hii, huwataabisha waume zao sana, na hatimaye wengine huwafanya wahame kabisa nyumba, kukaa mbali na familia zao. Ni dari linalovuja utawezaje kukaa kwenye nyumba hiyo?
Andiko hilo limerudiwa pia katika;
Mithali 19:13 Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye; Na ugomvi wa mke kama kutona-tona daima.
Uonapo familia zenye migogoro ya namna hii ni kuziombea sana Bwana aziponye.
Maandiko hayo yamewekwa sio kuonyesha mabaya kwa jinsia ya kike, hapana, bali imetoa tahadhari ili yasitokee kwa wanawake wa kikristo.
Biblia imetoa mwenendo wa mwanamke halisi wa kikristo, inasema awe ni wa kumtii mume wake. Awe ni mwenye kiasi, na MPOLE, na adabu. Akifanya hivyo atasimama vema kwenye nyumba yake, badala ya kuiharibu kinyume chake ataijenga.
1Timotheo 2:9 Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.
11 Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.
Soma pia.
1Petro 3:1 Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;
2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu. 3 Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;
4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, ROHO YA UPOLE NA UTULIVU, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.
5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.
6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote.
Hivyo wewe kama mwanamke ukitembea katika hayo, utakuwa katika upande salama wa Mungu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Wokovu wa milele/ Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?
Rudi Nyumbani
Sisi tuliookolewa pamoja na Bwana wetu Yesu Kristo, tunafananishwa na mti mmoja alioupanda Mungu mwenyewe ulimwengu. Na wote tunayo sehemu katika mti huo, na tumewekewa wajibu wa kufanya.
Bwana wetu Yesu Kristo anafananishwa na shina la mti, halafu sisi tunafananishwa na matawi.
Shina ni kuanzia kwenye mizizi, hadi mahali matawi yanapotokea. Hivyo Bwana wetu Yesu, ndiye anayechukua uhai wetu moja kwa kutoka kwa Mungu na kutuletea sisi. Lakini sisi ni kuanzia kwenye matawi mpaka kwenye matunda.
Yohana 15:1-2,5
[1]Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.
[2]Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa….
[5]Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.
Sasa wengi wetu tunachoona katika mashina ni matunda tu peke yake. lakini leo ni vema tuone jambo hili kwa ndani. Kwa kawaida tawi huundwa na vitu viwili, cha kwanza ni majani, na cha pili ni matunda.
na vyote viwili vinapaswa vionekane katika shina.
Hivyo mimi na wewe kama watakatifu, ni lazima tujiulize je majani yapo? na je matunda yake pia yapo?
Matunda ni nini?
Tafsiri ya awali ya matunda kama ilivyozungumziwa kwenye mfano ya mti, sio kuwavua watu kwa Kristo, kama inavyodhaniwa, hapana bali ni Kutoa tunda la wokovu wako. Yaani tunda la toba.
Yohana mbatizaji kwa uvuvio wa Roho alilifafanua vema..Tusome.
Mathayo 3:7-10
[7]Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?
[8]Basi zaeni matunda yapasayo toba;
[9]wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto.
[10]Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
Aliwaona mafarisayo ambao walikiri kwa ujasiri wao ni wajumbe wa Yehova, uzao wa Ibrahimu, lakini mioyoni mwao, maovu na machafu ya kila namna yamewajaa. Hivyo wakaonekana ni miti isiyo na matunda.
Matunda ndio yale yanayojulikana kama tunda la Roho, ambayo kila mwamini anapaswa afanye bidii kuyatoa moyoni mwake katika maisha yake yote ya wokovu, awapo hapa duniani. Ambayo ni;
Wagalatia 5:22
[22]Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu
[23]upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.
Mtu yeyote anayefanya bidii kuonyesha wokovu wake kimatendo, mtu huyo humzalia Mungu matunda, ambayo ndio chakula cha Roho wa Mungu. Na hivyo hufurahishwa sana na sisi..
Lakini kama tulivyosema shina huundwa na majani pamoja na matunda. Sasa majani, ni utumishi ambao kila mmoja wetu amepewa wa kuwavuta wengine kwa Kristo, kwa karama aliyopewa ndani yake.
Tuliagizwa na Bwana tuenende ulimwenguni kote, tukahubiri injili na kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi wake (Mathayo 28:19),
Unapowashuhudia wengine, ni kwamba majani yako yanawaponya mataifa, na hivyo unawaokoa. Kumbuka majani kimsingi hayana ladha, mara nyingi hutumika kama tiba. Ndicho Bwana anachokifanya kwa wenye dhambi kupitia sisi, tunapowashuhudia.
Ufunuo wa Yohana 22:1-2
[1]Kisha akanionyesha mto wa maji ya uzima, wenye kung’aa kama bilauri, ukitoka katika kiti cha enzi cha Mungu, na cha Mwana-Kondoo,
[2]katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na MAJANI YA MTI HUO NI YA KUWAPONYA MATAIFA.
Umeona? Kumbe majani yake, ni lengo la kuwaponya mataifa, watu wasiomjua Mungu. Tujiulize je na sisi tunayaponya mataifa kwa kuhubiri injili?
Wewe kama mkristo uliyemshirika wa mti wa uzima huna budi kuwa mhubiri wa injili usikae tu, hivi hivi ukasema tayari nimeokolewa inatosha, fanya jambo kwa Bwana. Waeleze wengine habari za Yesu, waponywe. Usijidharau ukasema siwezi, kumbuka aitendaye kazi hiyo ni Kristo ndani yako, wewe ni tawi tu. washuhudie wengine.
Lakini si kuhubiri tu, halafu maisha yako yapo kinyume na Kristo, hapana hilo nalo ni hatari, ukiwa na majani tu, halafu huna matunda ya wokovu moyoni mwako..Utalaaniwa.
Marko 11:13
[13]Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini.
[14]Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia.
Umeona hawa ni watu, wanaodhani kumtumikia Mungu tu yatosha hakuna haja ya kuishi maisha matakatifu. wanakutwa na majani tu peke yake.
Tuhakikishe tuna majani, lakini vilevile tuna matunda kwasababu sisi ni shina, ndani ya mti wa uzima. Na neema ya Mungu itatusaidia.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tafsiri ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;
KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?
UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?
Rudi Nyumbani