Category Archive Mafundisho

BARAKA ZA WAZAZI KWA WATOTO.

Masomo maalumu kwa wazazi/walezi.

Je unazijua kanuni za kuwabariki watoto wako?.. Wengi tunaijua kanuni moja tu ya kuwatamkia Baraka!..Hiyo ni sahihi kabisa na ipo kibiblia..(kwasababu maneno ya kinywa yana nguvu).

Lakini ni vizuri kufahamu jambo moja, kama Maneno yako hayataambatana na matendo yako, uwezekano wa hayo uliyoyasema kutokea bado utakuwa ni mdogo sana.

Kama unataka mtoto wako apate Baraka zote ulizozitamka juu yake, (na kwa njia ya maombi) ikiwemo Baraka katika kumjua Mungu, kuwa na afya na mafanikio, basi ongezea yafuatayo..

   1.MFUNDISHE SHERIA ZA MUNGU.

Wafundishe watoto wako sheria za Mungu, huku wewe mwenyewe ukiwa kielelezo cha kuzifanya, ili wasione kama ni sheria tu za MUNGU bali hata zako wewe mzazi!.. Mtoto wako anapaswa azione sheria za Mungu kama ni za kwako wewe. Lakini asipoona wewe mwenyewe ukizifanya hata yeye hataweza kukusikiliza wala kuzitenda, hata kama kwa mdomo atakuitikia.

Mithali 1:8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,

9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako”.

   2. USIMNYIME MAPIGO.

Yapo makosa yanayoweza kurekebishwa kwa maneno peke yake na mtoto akajengeka na kubadilika, lakini yapo yanayohitaji kurekebishwa kwa maneno pamoja na kiboko, hususani yale ya kujirudia rudia tena ya makusudi.

Biblia inasema ukimpiga hatakufa bali utakuwa umemwokoa roho yake na kuzimu.. (Hapo utakuwa umembariki pakubwa Zaidi ya kumtamkia tu baraka za maneno halafu hufanyi chochote).

Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.

   3. MFUNDISHE KUSHIKA ELIMU

Badala ya kumtakia tu Baraka kwa kinywa (au kumwombea tu katika chumba chako cha ndani), tenga muda wa kumfundisha Umuhimu wa Elimu (kwanza ya Mungu) na pili ya dunia… Hapo utakuwa umembariki kwa vitendo na si mdomo tu.

Mithali 4:13 “Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; Mshike, maana yeye ni uzima wako”

    4. MFUNDISHE KUSHIKA SHERIA ZA NCHI na KUWAHESHIMU WENYE MAMLAKA (Wafalme).

Badala ya kumtamkia tu mafanikio, na kumwombea.. tenga muda kumfundisha umuhimu wa kuwatii wenye mamlaka na kuzingatia sheria ya nchi, hiyo itakuwa Baraka kwake katika siku zijazo za maisha yake.

Mithali 24:21 “Mwanangu, mche Bwana, NA MFALME; Wala usishirikiane na wenye kigeugeu;

    5. MFUNDISHE KATIKA NJIA INAYOMPASA

Ni njia gani inampasa katika umri wake na jinsia yake?.. Je! Katika umri wake huo anapaswa amiliki simu??..je katika umri wake anapaswa asemeshwe maneno hayo unayomsemesha?..je katika umri wake anapaswa atazame hayo anayoyatazama katika TV?.. je katika umri wake huo anapaswa awepo hapo alipo?..anapaswa afanye hicho anachokifanya?.Je! Kwa jinsia yake anapaswa kuvaa hayo mavazi unayomvika??..

Ni muhimu sana kujua mambo yampasayo mwanao/wanao kwa rika walilopo na jinsia zao…

Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”

Ukiyafanya hayo na mengine kama hayo pamoja na MAOMBI umwombeayo kila siku, basi utakuwa umembariki mwanao/wanao  kweli kweli.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

JE! UMEYABATILISHA MAMBO YA KITOTO?

FIMBO YA HARUNI!

MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

MAOMBI YA KUOMBEA WATOTO.

Rudi nyumbani

Print this post

BWANA ANA NGUVU KAMA ZA NYATI! USIOGOPE UCHAWI!

Kama umeokoka kikweli kweli kwanini uchawi uwe na nguvu kwako??


Hesabu 23:22 “Mungu amewaleta kutoka Misri, Naye ana nguvu kama NGUVU ZA NYATI.

23 Hakika HAPANA UCHAWI juu ya Yakobo, WALA HAPANA UGANGA juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!”

Umewahi kujiuliza kwanini Nguvu za Mungu zifananishwe an za NYATI kipindi anawatoa wana wa Israeli Misri na kuwapeleka nchi ya ahadi??..Je unajua tabisa za nyati ni zipi mpaka zifananishwe na za Mungu?

NYATI ni Mnyama jamii ya Ng’ombe, na anafanana sana na Ng’ombe… lakini ana nguvu nyingi kuliko Ng’ombe.. Lakini tabia za huyu mnyama ni kwamba HAKUBALI KUFUNGWA NA MTU na ANAWAPIGA WOTE WANAOJARIBU KUMSOGELEA.. Laiti angekubali kufungwa na mwanadamu basi angekuwa nyenzo moja bora sana ya kazi.. kwani ana nguvu kuliko Ng’ombe.

Kwa nguvu alizonazo huenda matrekta ya kulimia yangekosa soko, kama angekubali kufungwa NIRA kama Ng’ombe!..Lakini hakubali kufugika ingawa ni Ng’ombe, mwenye sifa zote za kufugika lakini hafungiki….Nguvu zake anazimalizia kutishia na kudhuru maadui zake na wote wanaomsogelea, wakati Ng’ombe ni mnyenyekevu na mwenye kukubali NIRA. .

Ayubu 39:9 “Je! Nyati atakubali kukutumikia? Au atakaa katika zizi lako?

10 Je! Waweza kumfunga nyati kwa kamba matutani? Au, yeye atayalima mabonde nyuma yako?

11 Je! Utamtumaini kwa sababu ana nguvu nyingi? Au, utamwachia yeye kazi yako?

12 Je! Utamtumaini kwamba ataileta mbegu yako nyumbani. Na kukusanya nafaka ya kiwanja chako cha kupuria?”

Sasa tabia hiyo ya NYATI ya kukataa KUFUNGWA Nira, na BADALA YAKE KUWADHURU WANAOMSOGELEA KWA NGUVU ZAKE..ndiyo ilikuwa ndani ya WANA WA ISRAELI, walipokuwa wanasafiri jangwani.. Hakuna aliyewafunga tena Nira ya utumwa tena, na walikuwa wanawapiga maadui zao.

Pale ambapo Balaamu aliyekuwa mchawi (Yoshua 13:22) alipojaribu kuwalaani (yaani kuwafunga nira kichawi/kuwaloga), Ilishindaka kwasababu wanatembea na NGUVU ZA NYATI, ASIYEKUBALI NIRA!. Balaamu alipojaribu kuwafunga Mafundo kiroho ili wawe wanyonge mbele ya Balaki alishindwa, ule uchawi uligota.

Na Balaamu-mchawi alipoona kwamba mambo hayawezekaniki…Ndipo akasema, “HAKUNA UCHAWI WALA UGANGA JUU YA YAKOBO” Maana yake hakuna Nira ya kichawi wala ya kiganga kwa wana wa Israeli wanatembea kwa nguvu kama za NYATI…

Hesabu 23:22 “Mungu amewaleta kutoka Misri, Naye ana nguvu kama NGUVU ZA NYATI.

23 Hakika HAPANA UCHAWI juu ya Yakobo, WALA HAPANA UGANGA juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!”

Je umeokoka na hizi nguvu zinatembea nawe?

Kama bado hujaokoka kikamilifu basi ni haki yako kuuogopa uchawi tena uugope sana!!. Lakini ukitaka usiuogope wala usiwe na nguvu juu yako suluhisho si kutafuta maji, au mafuta ya upako.. bali suluhisho ni wewe kuwa Israeli wa kiroho..Ukiwa Isreali wa kiroho uchawi unadunda, kwasababu utakuwa unatembea na NGUVU ZA NYATI ndani yako.

Na unafanyikaje Israeli wa kiroho?..Si kwa njia nyingine Zaidi ya kutubu na kubatizwa katika ubatizo sahihi na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Ikiwa utahitaji msaada wa kuongozwa namna ya kumpokea Bwana Yesu na kubatizwa basi waweza wasiliana nasi kwa namba zetu.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU

JE! WEWE NI MFUNGWA WA BWANA?

YESU ANA KIU NA WEWE.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya kurarua mavazi? (Mwanzo 37:34).

Kurarua mavazi ni utamaduni wa wayahudi na watu wa zamani kuonyesha hisia zao kwa kuyararua (kuchana) sehemu ya mavazi yao kama isha ya Toba (kujishusha) au  maombolezo au majuto.

      1. Ishara ya kushuka (kunyenyekea) na kutubu.

Mfalme Yosia alipokiona kitabu cha Torati alitambua Israeli wamefanya dhambi kulingana na yaliyoandikwa kule, hivyo akajishusha mbele za Mungu Soma 2Wafalme 22:11-15..

Vile vile Mfalme Ahabu baada ya kutamkiwa hukumu yake na Mungu kwaajili ya shamba la Nabothi alilomdhulumu na tena kumwua..Ahabu alijishusha mbele za Mungu kwa kuyararua mavazi yake..

1Wafalme 21:27 “Ikawa, Ahabu alipoyasikia maneno hayo, akayararua mavazi yake, akavaa magunia mwilini mwake, akafunga, akajilaza juu ya magunia, akaenda kwa upole”.

      2. Maombolezo.

Kwamfano utaona baada ya Yakobo kupokea taarifa za kifo cha mwanae Yusufu (ambaye kimsingi hakufa) aliyararua mavazi yake kama ishara ya kuhuzunika na kumwombolezea..

Mwanzo 37:34 “Yakobo akararua mavazi yake, akajivika gunia viunoni, na kumlilia mwanawe siku nyingi”

Utasoma tena tukio kama hilo katika Mwanzo 37:29 pale Rubeni alipopata taarifa za kifo cha ndugu yake. Na pia 2Samweli 13:29-31, Esta 4:1, na Ayubu 1:20.

      3.Majuto

Utaona Mwamuzi Yeftha baada ya kukutana na mwanae, anaijutia nadhiri aliyoiweka kwa kurarua mavazi yake..

Waamuzi 11:35 “Ikawa alipomwona akayararua mavazi yake, akasema, Ole wangu! Mwanangu, umenitweza sana, nawe u mmoja miongoni mwa hao wanisumbuao; kwa kuwa mimi nimemfunulia Bwana kinywa changu, nami siwezi kurejea nyuma”.

Lakini je kiroho kurarua mavazi ni kufanya nini? Na je mpaka sasa tunapaswa tuyararue mavazi yetu kwa namna ya kimwili kama walivyofanya wayahudi zamani pindi tunapopitia maombolezo, au tunapotaka kutubu au kunyinyenyekeza kwa Mungu?

Jibu tunalipata katika kitabu cha Yoeli 2:13.

Yoeli 2:13 “Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea;

13 RARUENI MIOYO YENU, WALA SI MAVAZI YENU, MKAMRUDIE BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya.

14 N’nani ajuaye kwamba hatarudi na kugeuka, na kutuachia baraka nyuma yake, naam, sadaka ya unga, na sadaka ya kinywaji, kwa Bwana, Mungu wenu?”

Umeona?.. Kumbe kurarua mavazi ni kutubu!.. Na kwamba tunapotubu na kugeuka na kubadili njia zetu, mbele za Mungu ni sawa na tumeyararua mavazi yetu!.

Je leo umeurarua moyo wako?,  Umetubu kwa kumaanisha kabisa kuacha njia ile mbovu?…

Isaya 66: 2 “….lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu”.

Kujua maana ya “Kuvaa mavazi ya magunia” basi fungua hapa >>Nguo za magunia katika biblia ni zipi?

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

MAVAZI YAPASAYO.

USIYAACHE MAVAZI YAKO NA KWENDA UCHI!

FAHAMU JINSI MUNGU NA SHETANI WANAVYOZUNGUMZA NA WATU.

YEYE AJAYE ATAKUJA WALA HATAKAWIA.

Rudi nyumbani

Print this post

YEYE AJAYE ATAKUJA WALA HATAKAWIA.

Waebrania 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, YEYE AJAYE ATAKUJA, wala hatakawia”.

Angalia muda unavyokimbia, angalia majira yanavyobadilika, angalia maasi yanavyoongezeka kwa kasi.. Je! yote haya unajua ni ishara ya nini?..Si ya kitu kingine bali  ya YEYE AJAYE!!.. Ndio! Yupo mmoja anayekuja! na yupo karibu sana..

Gari likipita huwa linaacha vumbi!, lakini ikitokea vumbi linatangulia kabla ya gari kufika basi ni upepo unavuma kuelekea mbele, na una mbio kuliko gari lenyewe!.

Na YESU KRISTO anakuja, na ishara zake zinatangulia mbele yake!..zina mbio kabla ya kuwasili kwake, Uvumi wa ujio wake unatufikia kabla ya yeye kuwasili.

Zifuatazo ni sifa za “Yeye ajaye”

        1. Yeye ajaye anakuja kutoka Juu mbinguni.

Yohana 3:31 “YEYE AJAYE kutoka juu, huyo yu juu ya yote. Yeye aliye wa dunia, asili yake ni ya dunia, naye anena mambo ya duniani. Yeye ajaye kutoka mbinguni yu juu ya yote”.

       2. Yeye ajaye ana nguvu kuliko manabii wote.

Mathayo 3:11 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali YEYE AJAYE nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake…”.

      3. Yeye ajaye Ni Mbarikiwa na amejaa utukufu.

Mathayo 21:9 “Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, YEYE AJAYE kwa jina la Bwana; Hosana juu mbinguni”.

      4. Yeye ajaye Anakuja Upesi wala hakawii.

Waebrania 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, YEYE AJAYE ATAKUJA, wala hatakawia”.

>Jiulize!…Utajisikiaje siku umeamka asubuhi unajiandaa kwenda kazini, halafu ghafla unapokea taarifa za kuwa KRISTO kashawachukua watu wake, na wewe umebaki?

> Utajisikiaje umeamka vizuri na unaelekea shuleni, halafu unapata taarifa kuwa unyakuo wa kanisa umepita na wewe umeachwa?

> Utajisikiaje ule muda unapewa taarifa kuwa Kanisa limenyakuliwa na jana tu uliyasikia mahubiri na hukuzingatia??..

>Tafakari utakuwa katika hali gani utakapoanza kutafakari mambo yatakayoupata ulimwengu baada ya hapo?..Kwamaana maandiko yanasema baada ya hapo itakuwa ni dhiki kuu na  hukumu kwa wanadamu na mlango wa rehema utakuwa umefungwa!.

Isaya 26:21 “Kwa maana, tazama, Bwana anakuja kutoka mahali pake, ili kuwaadhibu wakaao duniani, kwa sababu ya uovu wao…”.

Zaburi 96:13 “Mbele za Bwana, kwa maana anakuja, Kwa maana anakuja aihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, Na mataifa kwa uaminifu wake”

Wakati huo watu watatamani kuingia katika mlango wa Neema lakini watakuwa wamechelewa…kwasababu mwenye nyumba (YESU) atakuwa ameshasimama na ameufunga mlango, hakuna anayeingia wala anayetoka..

Luka 13:23  “Mtu mmoja akamwuliza, Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache? Akawaambia,

24  Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba WENGI WATATAKA KUINGIA, WASIWEZE.

25  Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;

26  ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

27  Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.

28  Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje”.

Kwanini leo usijitahidi kuingia katika mlango ulio mwembaba???… hao marafiki watakusaidia nini siku ile au watakushauri nini utakapoukosa unyakuo?.. hizo mali zitakutetea vipi wakati huo?… hizo fasheni za kidunia na huo urembo utakupa kibali gani nyakati hizo?… Kumbuka YEYE AJAYE, ANAKUJA WALA HATAKAWIA!!

Ni heri ukayasalimisha maisha yako kwa YESU leo, maana hizi ni nyakati za hatari!.. na muda wowote parapanda inalia!.

Ufunuo 22:20 “Yeye mwenye kuyashuhudia haya asema, Naam; naja upesi. Amina; na uje, Bwana Yesu”

Ikiwa unahitaji kumpokea YESU basi fungua hapa kwa mwongozo >>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Maran atha!

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

ANAKUJA KAMA “MWIVI” NA SI KAMA “ASKARI” FANYIKA CHOMBO CHA THAMANI.

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

MWANAMKE, USIFUNGUE MLANGO WA MAPEPO KUKUINGIA!.

LIITE JINA LA BWANA KATIKA NYAKATI MBALIMBALI ZA MAISHA.

Rudi nyumbani

Print this post

Mistari ya biblia kuhusu kibali.

Ifuatayo ni baadhi ya mistari ambayo itamsaidia mtu kupata kibali aidha KWA MUNGU au kwa WANADAMU, au KWA WAKUU Au vyote kwa pamoja (Mungu pamoja na wanadamu).

KIBALI CHA MUNGU:

Mwanzo 4:6 “Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana?

7 Kama ukitenda vyema, HUTAPATA KIBALI? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde”

1Samweli 1:17 “Ndipo Eli akajibu, akasema, Enenda kwa amani; na Mungu wa Israeli akujalie haja yako uliyomwomba.

18 Naye akasema, Mjakazi wako na AONE KIBALI MACHONI PAKO. Basi huyo mwanamke akaenda zake, naye akala chakula, wala uso wake haukukunjamana tena”. 

KWA WATU:

Kutoka 11:3 “Bwana akawapa watu hao KIBALI MACHONI PA WAMISRI. Zaidi ya hayo, huyo Musa alikuwa ni mkuu sana katika nchi ya Misri, machoni pa watumishi wa Farao, na machoni pa watu wake”

Esta 2:15 “Hata ilipowadia zamu yake Esta, binti Abihaili, mjomba wake Mordekai, ambaye alimtwaa kuwa binti yake, ili aingie kwa mfalme, yeye hakutaka kitu, ila vile vilivyoagizwa na Hegai, msimamizi wake mfalme, mwenye kuwalinda wanawake. Naye huyu Esta alikuwa amepata kibali machoni pa wote waliomwona”

KWA WAKUU NA WAFALME:

Mwanzo 39:21 “Lakini Bwana akawa pamoja na Yusufu, akamfadhili, AKAMPA KIBALI machoni pa mkuu wa gereza.

22 Mkuu wa gereza akawatia mkononi mwa Yusufu watu wote waliofungwa, waliomo gerezani; na yote yaliyofanyika humo ndiye aliyeyafanya”

1Samweli 16:22 “Kisha Sauli akapeleka watu kwa Yese, akasema, Tafadhali, mwache Daudi asimame mbele yangu; maana AMEONA KIBALI machoni pangu”.

1Samweli 27:5 “Daudi akamwambia Akishi, Sasa kama nimeona KIBALI MACHONI PAKO na nipewe mahali katika miji hii mmojawapo mashambani, nipate kukaa huko; mbona mtumwa wako akae katika mji wa kifalme pamoja na wewe?”

Nehemia 2:4 “Ndipo mfalme akaniambia, Una haja gani unayotaka kuniomba? Basi nikamwomba Mungu wa mbinguni.

5 Nikamwambia mfalme, Mfalme akiona vema, na ikiwa mimi, mtumishi wako, NIMEPATA KIBALI MACHONI PAKO, tafadhali unipeleke mpaka Yuda, niuendee mji wa makaburi ya baba zangu, nipate kuujenga”

Esta 5:2 “Ikawa, mfalme alipomwona malkia Esta amesimama uani, yeye AKAPATA KIBALI machoni pake; naye mfalme akamnyoshea Esta fimbo ya dhahabu aliyokuwa nayo mkononi. Basi Esta akakaribia, akaigusa ncha ya fimbo”

KWA MUME:

Ruthu 2:10 “Ndipo aliposujudia, akainama mpaka nchi, akamwambia, Jinsi gani NIMEPATA KIBALI machoni pako, hata ukanifahamu, mimi niliye mgeni?

11 Naye Boazi akajibu, akamwambia, Nimeelezwa sana yote uliyomfanyia mkweo, tangu alipokufa mumeo; na jinsi ulivyowaacha baba yako na mama yako, na nchi yako uliyozaliwa, ukawafikilia watu usiowajua tangu hapo”.

Esta 2:17 “Mfalme akampenda Esta kuliko wanawake wote, naye AKAPATA NEEMA NA KIBALI machoni pake kuliko mabikira wote; basi akamtia taji ya kifalme kichwani pake, akamfanya awe malkia badala ya Vashti”

KWA MUNGU PAMOJA NA WANADAMU:

1Samweli 2:26 “Na yule mtoto, Samweli, akazidi kukua akapata kibali kwa Bwana, na kwa watu pia”

Mithali 3:4 “Rehema na kweli zisifarakane nawe; Zifunge shingoni mwako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.

4 Ndivyo utakavyopata kibali na akili nzuri, Mbele za Mungu na mbele ya mwanadamu.

5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe”

BWANA AKUBARIKI.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.

Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe;(Mithali 16:2)

MAPAMBO YA WANAWAKE WALIOUKIRI UCHAJI WA MUNGU.

WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

Rudi nyumbani

Print this post

Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.(Yakobo 5:9)

SWALI: Biblia inamaana gani inaposema “Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango”.

Yakobo 5:9  Ndugu, msinung’unikiane, msije mkahukumiwa. Angalieni, mwamuzi amesimama mbele ya milango.


JIBU: Neno la Mungu halitoi nafasi ya sisi, kunung’unikiana kwasababu yoyote. Aidha ya kuonewa, au kudhulumiwa, kuaibishwa au kufanyiwa jambo ambalo halikupasa utendewe, Manung’uniko ni zao la kutokuwa na uvumilivu. Na kwamba tukifanya hivyo basi, tafsiri yake ni kuwa tunamfanya Mungu naye aghahiri uvumilivu wake kwetu.

Lakini anatoa, suluhisho, kwamba hayo tuyaache mikononi mwake. Kwasababu yeye ndio mwamuzi wetu. Na kwamba, sio tu mwamuzi lakini  ni mwamuzi ambaye yupo mlangoni. Akiwa na maana kuwa Kristo yupo karibu sana na maonevu, au dhuluma hizo, na kwamba yeye mwenyewe atalipa, wala hatakawia, kwasababu yupo mlango.

Atalipa aidha kwa wakati huu huu duniani,  au siku ile ya mwisho wa Hukumu. Kwake yeye ni lazima haki itendeke. Pia kwa upande mwingine anataka uogope kwasababu ukinung’unika yeye hayupo mbali kukusikia.

Wafilipi 4:5  Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa, popote tusimamapo kutoa malalamiko, laumu, kuhesabu makosa, n.k. basi tutambua kuwa Kristo yupo hapo hapo katikati yetu kutusikia. Hivyo tusiwe wepesi ya kunena, bali tujifunze kuwa wavumilivu katika mambo yote. Ili Mungu atuachilie neema yake.

Bwana akubariki.

Je! Umeokoka? Je, umebatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo? Kama ni hapana, basi wakati ndio huu, tubu dhambi zako, kwa kumwamini Yesu upokee ondoleo la dhambi zako, Na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu.

Ikiwa upo tayari kumkabidhi leo maisha yako. Basi  fungua hapa kwa mwongozo huo. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MWAMUZI WA KWELI:

“Kinga kilichotolewa motoni “Kinafunua nini kibiblia?

Bwana Yesu alikuwa anamaanisha nini kusema Marko 2:19″walioalikwa harusini wawezaje kufunga maadamu bwana-arusi yupo pamoja nao?”

MBINGUNI YUPO NANI SASA?

Rudi nyumbani

Print this post

JE! MWAMBA HALISI NI NINI KULINGANA NA BIBLIA?

Je! Umejengwa kweli juu yake?

Ukimuuliza mtu, mwamba ni nini, ni rahisi kukujibu YESU. Jibu ambalo ni sahihi, maandiko yanatuthibitishia hilo Yesu kuwa Yesu ni mwamba (Mathayo 21:42, 1Wakorintho 10:4). Lakini lazima ufahamu pia  MWAMBA mwenye anasemaje, kuhusu yeye mwenyewe alivyo.

Ni maneno ambayo tunayasoma lakini si rahisi kuyatafakari kwa ukaribu, embu tusome tena, halafu utaona mwamba alimaanisha nini. (Zingatia vifungu vilivyo katika herufi kubwa) Soma kwa utulivu.

Mathayo 7:24  Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na KUYAFANYA, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;

25  mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba. 26  Na kila asikiaye hayo maneno yangu ASIYAFANYE, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

27  mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.

28  Ikawa, Yesu alipoyamaliza maneno hayo, makutano walishangaa mno kwa mafundisho yake; 29  kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye amri, wala si kama waandishi wao.

Umeelewa? Vema hayo maneno?

Kumbe mtu  yeyote anayesikia maneno ya Yesu. Hapo hapo huwa anaanza ujezi.

Lakini tofauti inakuja mahali anapokwenda kujengea,. Yule aliyejenga kwenye mchanga tafsiri yake Yesu anasema, anasikia, lakini hayatendei kazi (Hayafanyi), aliyoyasikia. Hivyo hapo Mchanga, ni KUTOTENDA.

Lakini Yule mwingine aliyekwenda kwenye mwamba tafsiri yake ni anasikia lakini pia anatenda. Hivyo MWAMBA, ni kutenda.

Mwamba sio kumjua Yesu ndugu, mwamba sio kusoma sana biblia na kujua mafumbo na siri zote zilizo katika biblia, mwamba sio kujua kujua tafsiri zote za kigiriki na kiebrania kwenye maandiko, mwamba sio kujua kufundisha vema biblia,.. Sio hivyo vyote.

Mwamba ni KULITENDEA KAZI NENO, Unalolisikia kwake. Hilo tu. Sio kumjua Yesu.

Hatari iliyopo leo, miongoni mwa wakristo wengi, ni kwamba tumejengwa juu ya mafundisho mengi. Lakini hatujajengwa juu ya kutendea kazi mafundisho tunayofundishwa. Ndugu fundisho halikusaidii kuyashinda majaribu, au tufani za mwovu, au dhoruba, au pepo, hapo unafanya kazi ya kuchosha tu,kudumu katika kusikia, kusoma, kusikiliza, bado si suluhisho, kusema nimebarikiwa, nimefunguliwa ufahamu, bado hakukufikishi popote, kama HUTALIISHI hilo Neno.

Ukiwa ni wa kufanya bidii kuliishi NENO moja, wewe ni imara sana kuliko Yule mwenye kujiona anaijua biblia yote

Penda Utakatifu, penda usafi wa moyo, penda kupiga hatua rohoni. Penda matendo mema.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!

NAYAJUA MATENDO YAKO.

Gumegume ni nini? (Isaya 50:7)

Ngome ni nini?  Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?

JE! UNA MASIKIO YANAYOSIKIA?

Rudi nyumbani

Print this post

ONA FAHARI JUU YA BWANA.

Je! Unaona Fahari juu ya nini? Ni kitu gani unachokionea Fahari?.. Je ni mali?, ni vyeo?, au uwezo ulio nao?..


Kama Bwana amekujali kukupa hivyo vyote, basi mshukuru lakini usijionee fahari juu ya hivyo, kwasababu vyote hivyo ni “UBATILI”….bali ona FAHARI juu ya BWANA YESU kama umeshamjua!.

Kwasababu kumjua YESU ni UTAJIRI mkubwa, na CHEO kikubwa na UWEZO mkubwa.. kuliko utajiri wowote wa kiduni, wala cheo chochote cha kidunia wala uwezo wowote wa kidunia.

Maana yake Kama ni kuringa, au kutamba…basi tamba kwa kuwa UMEMJUA YESU!. (Furahia kwa kuwa umekipata kitu kikubwa na cha thamani, furahi kwa kuwa umelenga shabaha)..ndivyo maandiko yanavyotufundisha..

1Wakorintho 1:30  “Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu HEKIMA itokayo kwa Mungu, na HAKI, na UTAKATIFU, na UKOMBOZI;

31  kusudi, kama ilivyoandikwa, YEYE AONAYE FAHARI NA AONE FAHARI JUU YA BWANA”.

Hapo anasema YESU KRISTO amefanyika kuwa HEKIMA itokayo kwa Mungu, maana yake kama yeye  yupo ndani yetu, basi ni hekima ya Mungu imeingia ndani yetu. (sasa kwanini usione fahari juu yake kama yupo ndani yako)

Na tena amefanyika kuwa “HAKI”, Maana yake ni kwamba kama yeye yupo ndani yetu, basi tumepata haki ya kuishi milele, na kupata yote tunayoyahitaji ambayo ni mapenzi ya Mungu, (sasa kwanini usione fahari juu yake huyo kama yupo ndani yako?).

Na tena amefanyika “UTAKATIFU”.. Maana yake akiingia ndani yetu, tunahesabika na kuitwa watakatifu, (Kwanini usione fahari juu ya huyo).

Zaidi sana amefanyika “UKOMBOZI”. Maana yake anapoingia  ndani yetu, tunapata ukombozi wa Laana, na zaidi sana tunapata Kuokoka na hukumu ya milele ijayo, ya ziwa la moto aliloandaliwa shetani na malaika zake (Ufunuo 12:9)Kwanini usione fahari juu ya huyo aliyekupa ukombozi..

Aibu inatoka wapi!!!, ikiwa YESU KRISTO, aliye hekima ya Mungu yupo ndani yako?… Aibu ya kubeba kitabu chake (biblia) na kutembea nacho kikiwa wazi inatoka wapi? Ikiwa yeye ni mwokozi wako?

Aibu ya kuzungumza habari zake mbele za watu inatoka wapi? Ikiwa yeye ni Haki yako?… Aibu ya kushika amri zake inatoka wapi ikiwa yeye amekupa wokovu kutoka katika hukumu ya milele?.

ONA FAHARI JUU YAKE!.. wala usimwonee haya (aibu), maana alisema mtu akimwonea haya katika kizazi hiki yeye naye atamwonea haya mbele za malaika zake wa mbinguni.. Maana yake ni kwamba kama tukimwonea fahari, naye pia atatuonea fahari mbinguni (Marko 8:38)

ONA FAHARI JUU YAKE,…MTANGAZE KWA KUJITAMBA KABISA!.. MDHIHIRISHE KWA WATU, WAONE KUWA ULIYE NAYE NI KILA KITU KATIKA MAISHA YAKO!… Na itakuwa baraka kubwa kwako.

Wagalatia 6:14 “Lakini mimi, hasha, nisione fahari juu ya kitu cho chote ila msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambao kwa huo ulimwengu umesulibishwa kwangu, na mimi kwa ulimwengu”.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Maana ya Mithali 19:11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake.

Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.

KWANINI NABII ISAYA ALIAGIZWA KUHUBIRI UCHI?

VAZI KUU AMBALO MUNGU AMETUANDALIA KILA MMOJA WETU.

Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya Mithali 6:30 Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha

SWALI: Je!  Mithali 6:30 inamaana gani?

Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha, iwapo aona njaa;  31 Lakini akipatikana, atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake.

JIBU: Chukulia mfano mtu hajala siku tatu, halafu akaona kuna duka lipo wazi pale jirani, na mwenyewe ametoka, akashawishika kuingia haraka  na kubeba mkate, ili akale. Lakini mwenye duka aliporudi na kuona mkate umeibiwa, alianza kumfuatilia, mwishowe akamkuta amejificha mahali Fulani anakula akiwa katika hali mbaya.

Kibinadamu, atakapoona hali halisi ya mwizi, huwenda ataishia kukasirika tu, au kumgombeza, au kwenda kumwajibisha, kwa mambo madogo madogo. Kwasababu anaona alichokifanya ni kwa ajili ya kusalimu maisha yake tu, ale asife, lakini sio kwa lengo la kuchukua vya watu, akauze, au kuleta hasara kwa wengine.

Lakini sehemu ya pili ya mstari huo anaendelea kusema kama “akipatikana atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake”.

Maana yake ni kuwa kama “atapatikana na kosa”, basi atalipa mara saba. Atagharimikia vyote alivyoviiba mara saba. Sasa kauli hiyo haimaanishi kwamba mwizi huyo huyo aliyeiba kwa ajili ya kujishibisha tumbo lake ndio atalipa mara saba, hapana, vinginevyo mstari huo ungekuwa unajipinga unaposema “watu hawamdharau mwizi akiiba kwa kujishibisha”, bali  anamaanisha kama akipatikana na hatia tofauti na hiyo..mfano aliiba vitu ili akauze, aliiba fedha ili akajiendeleze kwenye mambo yake, alete hasara kwa wengine. Huyo atalipa gharama zote mara saba.

Ndio maana utaona adhabu nyingi za wezi huwa ni kubwa sana zaidi ya vile walivyoviiba, wanapigwa faini kubwa, wengine mpaka wanauliwa, kwa wizi tu mdogo. Hapo ni sawa na wamelipa mara saba.

Je! Hili linafunua nini rohoni?

Kama njaa ya mwilini, inaweza kumfanya mwizi asihesabiwe kosa. Kwasababu watu wanaelewa umuhimu wa kunusuru uhai kwa chakula, vipi kuhusu rohoni. Hata kuna wakati Daudi alikula mikate ya makuhani ambayo  hawakupaswa watu wengine kula, lakini kwasababu alikuwa na njaa yeye na wenzake haikuhesabiwa kwake kuwa ni kosa (1Samweli 21).

Vivyo hivyo rohoni, Mungu anatufundisha sio kwamba tuwe wezi, hapana, lakini anataka tuthamini sana roho zetu, pale zinapokuwa hazina kitu, zina njaa. Iweje mtu unakaa hadi unakufa kiroho halafu unaona ni sawa kuwa hivyo hivyo kila siku. Hufanyi jambo Fulani la kujinasua katika hiyo hali yako mbaya rohoni, unaendelea tu hivyo hivyo. Tafuta kwa bidii chakula cha kiroho usife ndugu. Jibidiishe.

Iba muda wako wa kufanya mambo mengine ili ukipate chakula cha kiroho. Ni kweli ulipaswa kuwepo mahali Fulani pa muhimu, embu ghahiri muda huo, nenda kasome biblia, nenda kaombe, nenda kasikilize mahubiri yatakayokujenga. Ulipaswa uwepo kazini, lakini kwasababu ibada ile ni muhimu embu usione shida kughahiri.

Huna biblia Iba hata pesa yako ya matumizi ya muhimu kanunue, acha uonekane mjinga nenda kanunue biblia au vitabu vya rohoni vikujenge. Tafuta ile MANA iliyofichwa.

Siku hizi ni za mwisho. Na Bwana alishatabiri duniani kutakuwa na njaa, sio ya kukosa chakula au maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Mungu ya kweli. Usipojiongeza katika eneo la ukuaji wako kiroho.  Ni ngumu kuvuka hizi nyakati mbaya  za manabii wengi wa uongo, na mafundisho ya mashetani. Usipoyajenga maisha yako ya kiroho, shetani akusaidie kuyajenga kwake.

Amosi 8:11 “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Bwana”

Penda biblia, penda kujifunza, penda maombi zaidi ya vingine.

Bwana akubariki.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

YEYE ALIYEUWASHA HUO MOTO LAZIMA ATALIPA.

NJAA ILIYOPO SASA.

(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

(Opens in a new browser tab)KAMA MTUMISHI WA MUNGU, TAFUTA MAARIFA KWA BIDII.(Opens in a new browser tab)

Rudi nyumbani

Print this post

MKUMBUKE TOMASO.

Nakusalimu katika jina la Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tuzitafakari habari njema.

Tomaso alikuwa ni mtume  wa Bwana. Lakini alikuwa na tabia ya kitofauti na wale mitume wengine 11. Yeye hakuwa msaliti kama Yuda, zaidi sana alikuwa hata radhi kufa na Bwana wake, kipindi Fulani aliposikia anatafutwa ili  auawe (Yohana 11:16), hiyo ni ishara ya upendo wake kwa Yesu.

Lakini alikuwa na tabia nyingine ambayo ilimgharimu kwa sehemu Fulani, Na tabia yenyewe ni mashaka juu ya uweza wa Mungu, ni hiyo ikapelekea hata kuathiri mahudhurio yake, ya kiibada na kiutendaji kazi pale alipolazimika kuwepo na wenzake kama mtume.

Hakutaka kuamini kwamba Yesu anaweza kufufuka, hivyo wakati huo alipoitwa waombe pamoja, hakuwa tayari kukusanyika na wenzake, alipoitwa awafariji watu yeye kama mtume wa Bwana aliyepewa mamlaka hiyo, hakutaka kufanya hivyo kinyume chake akaenda kuendelea na shughuli zake. Walipokuwa wanatafakari maneno ya Yesu, yeye mawazo yake yalikuwa mbali kabisa na wenzake. Ni kama alikuwa amechoka.

Matokeo yake ikawa Yesu alipowatokea mitume wake, walipokuwa wamejifungia kuomba, yeye hakuwepo. Hata walipokuja kumuhadithia bado hakuamini, kwasababu moyo wake ulikuwa umeshahama kabisa.

Yohana 20:24  Walakini mmoja wa wale Thenashara, Tomaso, aitwaye Pacha, hakuwako pamoja nao alipokuja Yesu. 25  Basi wanafunzi wengine wakamwambia, Tumemwona Bwana. Akawaambia, Mimi nisipoziona mikononi mwake kovu za misumari, na kutia kidole changu katika mahali pa misumari, na kutia mkono wangu katika ubavu wake, mimi sisadiki hata kidogo. 26  Basi, baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwamo ndani tena, na Tomaso pamoja nao. Akaja Yesu, na milango imefungwa, akasimama katikati, akasema, Amani iwe kwenu 27  Kisha akamwambia Tomaso, Lete hapa kidole chako; uitazame mikono yangu; ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu, wala usiwe asiyeamini, bali aaminiye.

Wewe kama mtumwa wa Yesu usiwe tomaso, wakutanikapo wenzako kamwe kataa kujitenga, hata kama hakuna tumaini, dumu na wenzako, epuka utoro, epuka udhuru, dumu hapo. Zipo nyakati ambazo Bwana hamtokei mtu kivyake-vyake, bali wawapo wote. Zipo Baraka, ipo neema, katika umoja na wenzako, kupo kumwona Mungu unaposhikamana na wenzako kiuaminifu, katika kujengana na kutiana moyo.

Kamwe usifikiri kivyako, kataa hiyo hali, Bwana anasema ajitengaye na wenzake anatafuta matakwa yake mwenyewe, Tomaso alikuwa hivyo. Lakini fikra zake hazikuwa sahihi, aliligundua hilo baadaye aliporudi kujumuika na wenzake, ndipo akamwona Bwana, alidhani angemwonea kule alipokimbilia. Dumu na wenzako maadamu Bwana wenu ni mmoja, Roho wenu ni mmoja, Ubatizo wenu mmoja. Hiyo inatosha. Dumu hapo.

Bwana atusaidie.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Kwanini Tomaso atake kwenda kufa pamoja na Lazaro? (Yohana 11:14-16).

Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

KWANINI MITUME WAMUULIZE BWANA FARAGHANI?

Rudi nyumbani

Print this post