Mara kadhaa, Bwana Yesu kabla hajasema Neno lolote alianza kwanza na kauli hii “Nayajua matendo yako” Kwamfano Soma vifungu hivi uone alivyosema, (Ufunuo 2:2, 2:19, 3:1, 3:8).
Nikwanini aanze kwa kusema hivyo? Ni kwasababu anataka hilo tuliweke akilini, tufahamu kuwa yupo karibu sana na hatua zetu kuliko tunavyoweza kudhani, hususani zile ambazo tunafikiri kuwa yeye hazijui, au hazioni. Tutawaficha wanadamu lakini yeye kamwe hatuwezi kumficha chochote.
Wewe ni mchungaji, unazini na washirika, unazungumza lugha za mizaha na wake za watu, unadhani Kristo hajui nia yako, halafu unasimama madhabahuni unahubiri habari za wokovu..Bwana anakupa onyo, tena kali sana, anayajua matendo yako, na hasira yake ipo juu yako.
Wewe ni mkristo, unasema umeokoka, umebatizwa, unashiriki meza ya Bwana, lakini kwa siri unatazama picha za ngono, unafanya uasherati..Ukija kanisani unasema Bwana Asifiwe! Tena bila aibu unasimama na madhabahuni kuimba..utamficha mchungaji, utawaficha washirika wote, utamficha hata na shetani..Lakini Yesu anayajua matendo yako nje-ndani..Anajua mnapokutania, mnapotekelezea mipango yenu miovu, anajua ni nini unachofanya unapokuwa chumbani mwenyewe.
Wewe ni mwanandoa, unaigiza kwamba unampenda mwenzi wako, muwapo pamoja, lakini akisafiri kidogo tu, mkiwa mbali, unachepuka, mke umetoa mimba nyingi, na huko nje wewe mume umezaa watoto, hata mkeo haujui, unadhani unamficha nani rafiki? .
Leo hii lipo kundi kubwa la washirikina miongoni mwa watakatifu, tukiachilia mbali wachawi, lakini cha ajabu hujawahi kumsikia hata mmoja akijivunia kazi yake hiyo au akijitangaza? Wameficha hirizi chini ya biashara zao, wana mazindiko kwenye nyumba zao, wanajifanya wana maadili na hodari wa kusema AMEEN!!..Lakini hawajui kuwa Bwana anayajua matendo yao.
Ufunuo 3:1 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na hizo Roho saba za Mungu, na zile nyota saba. NAYAJUA MATENDO YAKO, ya kuwa una jina la kuwa hai, nawe umekufa.
2 Uwe mwenye kukesha, ukayaimarishe mambo yaliyosalia, yanayotaka kufa. Maana sikuona matendo yako kuwa yametimilika mbele za Mungu wangu.
3 Basi kumbuka jinsi ulivyopokea, na jinsi ulivyosikia; yashike hayo na kutubu. Walakini usipokesha, nitakuja kama mwivi, wala hutaijua saa nitakayokuja kwako”
Ndugu ni heri ukatubu, uwe na amani na Kristo katika nyakazi hizi za hatari, kwasababu ukiendelea na hali hiyo hiyo utakufa na kwenda kuzimu, na adhabu yako itakuwa ni kubwa sana.
Bwana anasema…
“Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema”. (Mithali 28:13)
Leo hii ziungame dhambi zako, usiyafiche moyoni hayo unayoyafanya, wala usione aibu, wakati ndio sasa, hata kama umeshindwa kuacha, au hujui cha kufanya kwa uliyoyatenda, embu mfuate kiongozi wako wa kiroho mshirikishe akupe ushauri,.aombe pamoja na wewe, Ili Bwana akusamehe makosa hayo uliyoyofanya.
Unachopaswa kufanya ni kutubu tu kwa kumaanisha..Ukiwa na nia kweli ya kuacha, ili Bwana atakusamehe na kukusaidia kuyashinda, lakini ukiwa upo vuguvugu, hueleweki, bado unayo hatia ya dhambi..kwasababu anayajua matendo yako.
Ufunuo 3:15 “NAYAJUA MATENDO YAKO, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.
16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa change”.
Jimimine kwelikweli kwa YESU akusaidie..Wakati wa Yesu kuyahukumu mambo yote ya sirini, umekaribia sana, Hukumu ipo karibu. Jiepushe nayo. (Warumi 2:16, 1Wakor 4:5). Ni wakati wa lala-salama.
Ikiwa utapenda kupata msaada huo wa kumkaribisha tena Kristo upya maishani mwako. Basi waweza wasiliana nasi kwa namba hizi kwa ajili ya mwongozo huo bure. +255693036618 / +255789001312.
Bwana akubariki.
Shalom. (Bwana Yesu anarudi).
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU
Kupiga ramli ni nini katika biblia?
Kumwambia mtu mwenye dhambi kuwa atakwenda kuzimu asipotubu Je! ni kuhukumu?
Je! Unamjua Diotrefe katika biblia?
Diotrefe alikuwa ni kiongozi katika kanisa moja ambalo mtu wa Mungu ,Gayo alikuwa akishiriki. Kiongozi huyu alianza vizuri na Bwana lakini mwisho wake ulikuwa mbaya.. mpaka Mtume Yohana anamwandikia Gayo waraka juu yake, ili asiziige tabia zake..
Hebu tumsome huyu Diotrefe jinsi alivyokuwa na tabia zake..
3Yohana 1:8 “Basi imetupasa sisi kuwakaribisha watu kama hao, ili tuwe watenda kazi pamoja na kweli.
9 Naliliandikia kanisa neno, lakini Diotrefe, apendaye kuwa wa kwanza kati yao, hatukubali.
10 Kwa hiyo, nikija, nitayakumbuka matendo yake atendayo, atoavyo upuzi juu yetu kwa maneno maovu; wala hatoshwi na hayo, ila yeye mwenyewe hawakaribishi hao ndugu, na wale watakao kuwakaribisha, huwazuia, na kuwatoa katika kanisa”.
Sasa hebu tuzitazame hizi tabia 4 Diotrefe alizokuwa nazo.
1: ANAPENDA KUWA WA KWANZA:
Hii ni tabia ya kwanza Diotrefe aliyokuwa nayo; Sasa Kupenda kuwa wa kwanza si jambo baya, lakini mtu anapotaka kuwa wa kwanza kwa lengo la kutukuzwa na watu, au kwa lengo la kuwatawala wa wengine, au kwa lengo la kutumikiwa.. hususani ndani ya kanisa, basi hiyo ni mbaya sana na ni kinyume na Neno la Mungu..
Kwasababu Bwana Yesu alisema..
Mathayo 20:25 “Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.
26 LAKINI HAITAKUWA HIVYO KWENU; BALI MTU YE YOTE ANAYETAKA KUWA MKUBWA KWENU, NA AWE MTUMISHI WENU;
27 NA MTU YE YOTE ANAYETAKA KUWA WA KWANZA KWENU NA AWE MTUMWA WENU;
28 kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi”.
Kwahiyo kama Mhubiri wa Injili: Katika nafasi yoyote uliyopo aidha ni Mchungaji, au Mwalimu, au Nabii, au Mtume au Mwimbaji kumbuka kuwa unapaswa uwe Mtumwa wa wote!, kama unataka kuwa wa Kwanza, lakini kamwe usijiinue wala usitafute utukufu wa wanadamu kama huyu Diotrefe. Ni hatari kubwa!
2. ANANENA MANENO YA UPUUZI JUU YA MITUME
Hii ni tabia ya pili Diotrefe aliyokuwa nayo.. Alikuwa anawachafua Mitume wa Bwana Yesu (Ikiwemo Yohana, Mtume wa Yesu ambaye alipendwa sana na Bwana Yesu). Ijapokuwa aliwajua kuwa wamechaguliwa na Bwana lakini yeye aliwachafua kwa maneno mabaya na kuwafanya waonekane si kitu mbele ya kanisa la Mungu…Na hiyo yote ni kutokana na wivu.
Roho hii pia ipo kwa baadhi ya watu, ambao kutokana na Wivu, basi wapo radhi hata kuwachafua watumishi wa kweli wa Mungu, na huku mioyoni wakishuhudiwa kuwa wanawachafua ni watumishi wa kweli wa Mungu, lakini kutokana na wivu wanaendelea tu kuwachafua!,.. Hili ni jambo la kuzingatia sana wewe kama Mwimbaji, au Mchungaji, au Mtume au Nabii au Mwinjilisti.
3. HAWAKARIBISHI NDUGU
Hii ni tabia ya tatu ambayo Diotrefe alikuwa anaionyesha katika kanisa… Yeye alikuwa ni kiongozi lakini kamwe hakutaka kupokea Watumishi wengine waliokuja kuhubiri katika mitaa yake, au mji wake, au waliokuwa wakipita njia yake kuelekea sehemu nyingine kuhubiri. Na sababu ya kufanya hivyo ni ile ile ya wivu na kutaka kuwa wa kwanza..
Aliona kama mtu mwingine akija kuhubiri katika mji wake basi yeye hadhi yake, au heshima yake itashuka, na Yule alitakayekuja atatukuzwa zaidi..Hivyo hiyo roho ikampelekea mpaka kukataa kupokea wahubiri walio wageni.
Vile vile na sisi hatuna budi kuikataa hiyo roho kwasababu ni roho kutoka kwa Yule adui, siku zote hatuna budi kuwakubali na kuwakaribisha Watumishi wengine wanaotaka kuja kuhubiri maeneo tuliyopo, maadamu tumewahakiki kuwa kweli ni watumishi wa Mungu kwa Neno la Mungu, na wamekuja kwa nia ya kuhubiri injili.
4. ALIWAZUIA WATU WENGINE WASIWAKARIBISHE NDUGU
Hii ni tabia ya mwisho aliyoionyesha huyu Diotrefe.. Hakuridhika tu kuwakataa Mitume waliokuja kuhubiri pande zake, bali pia aliwakataza washirika wa kanisa lile wasimpokee mtumishi mwingine yoyote atakayekuja kuomba hifadhi kwao, kwaajili ya kuhubiri injili.. Na hakuishia hapo, bali aliendelea na kuwafukuza katika kanisa wale wote waliodhubutu kuwakaribisha Mitume. (Uone jinsi hii roho ilivyoenda mbali).
Lakini huyu Diotrefe hakuanza hivi.. Alianza vizuri tu!, ndio maana hata akafikia hatua ya kuwa kiongozi wa Makanisa (Huenda alikuwa Askofu). Lakini roho nyingine ya kujiinua ilimwingia na ya kupenda kutukuzwa na watu na kuinuliwa, na akaipalilia mwishowe ikawa ni roho ya uadui mbaya sana na iliyoiharibu kanisa.
Na sisi hatuna budi kujifunza katika haya, ili tusijikute tunaangukia katika makosa hayo hayo ya Diotrefe (Ndio maana Mungu karuhusu kisa cha Diotrefe kiwepo katika biblia hata kama kwa ufupi sana). Ili tujifunze na tujihadhari na roho ya kujiinua, na kupenda utukufu wa wanadamu zaidi ya utukufu wa Mungu, na tama nyingine zote za kiulimwengu.
Bwana atusaidie tuwe kama Mzee Gayo aliyekubali kupokea mashauri hayo.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?
NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.
Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?.
SWALI: Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa? Kwani kunaendelea mabishano baina ya wakristo baadhi, wengine wanasema kwasasa huduma hizo hazitendi kazi tena kufuatana na andiko la Paulo katika
Waefeso 2:20 linalosema;
[20]Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.
…Lakini wengine wanasema huduma hizo hadi sasa zipo katika kanisa. Je ukweli ni upi?
JIBU: Kabla hatujafahamu kwanza kama huduma za mitume na manabii zinaendelea hadi sasa au la!…tutazame kwanza aina za manabii wa mwanzo, na mitume wa mwanzo walikuwaje..
1)Manabii wa kutia msingi wa wakati wote
2)Manabii wa kuthibitisha misingi.
1 ) Hawa manabii wa kutia misingi; Ndio wote waliotiwa mafuta na Mungu kaandika biblia takatifu…mfano wa hawa ndio kama Yeremia, Isaya, Nahumu, Malaki, Yoeli, Yona, Habakuki..n.k. Kwamba nabii zao zisimame kama msingi na mwongozo wa daima wa kuliongoza kanisa la Mungu wakati wote..
2 ) Manabii wa kuthibitisha: Hawa Mungu aliwanyanyua kutoa mwongozo wa wakati fulani tu mahususi.. Walikuwa wanasema Neno la Mungu lakini la wakati fulani tu ambapo ukishapita basi, unabii huo hauna umuhimu tena kwa vizazi vijavyo.
Mfano wa hawa utawasoma wengi sana..wakina Mikaya, Aguri, Odedi, Azuri, Ahiya, pia katika agano jipya walikuwepo wakina sila, agabo..n.k
Vivyo hivyo tukirudi na katika Mitume wa Kristo.
Wapo ambao waliotiwa mafuta kwa lengo la kuweka misingi ya daima. Hawa ndio wote tunaosoma nyaraka zao katika maandiko..mfano Paulo, Petro, Yakobo, Yohana, Yuda, Mathayo, Luka.
Na wapo waliowekwa kwa ajili ya kutihibitisha / kutia misingi midogo.midogo. Mfano wa hawa ni Epafrodito Wafilipi 2:25..
Sasa tukishafahamu…hilo…tunaporudi katika lile andiko linalosema..mmejengwa juu ya misingi ya mitume na manabii tunaweza kuelewa
Tusome;
Waefeso 2:20
[20]Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.
Maana yake ni kuwa sisi kama kanisa tumejengwa juu ya mafunuo ya manabii watangulizi na mitume watangulizi wale waliochaguliwa kuweka misingi ya daima..(Yaani kwa lugha rahisi tumejengwa juu ya BIBLIA TAKATIFU)…
Hakuna namna tutajengwa juu ya misingi mingine mipya zaidi ya hiyo yao.. Hivyo kwasasa hatuna manabii na mitume kama wale watangulizi, ambao walipokea mafunuo ya moja kwa moja ya namna ya kulijenga kanisa la Kristo..ni sawa na kusema hatuna mitume mfano wa Paulo au Petro au manabii mfano wa Yeremia au Isaya, kwasasa.
Lakini wapo mitume na manabii wa nyakati ndogo ndogo, ambao wanafanya kazi za kuthibitisha misingi ambayo tayari ipo lakini sio wa kuleta jambo jipya duniani..
Kwamfano kazi mojawapo ya mitume ilikuwa ni kwenda kupanda makanisani mapya maeneo mapya..hivyo, mtu yeyote mwenye huduma.hii ndani yake, ni mtume lakini kazi yake itakuwa ni kutembea katika mstari ule ule wa mitume wa kwanza..hapaswi kuja na jambo lake jipya..anapaswa ahubiri kilekile mitume walichokifundisha, hapo atakuwa amekidhi kuitwa mtume.
Ni sawa na mtu anayejenga nyumba ya gorofa..msingi mkuu ni mmoja..ule uliopo chini…lakini akitaka aweke nyumba juu yake ni sharti afuata ramani ya msingi wa chini….
Ndivyo ilivyo kwa huduma hizi za kitume na kinabii.. Ni lazima zirejee katika biblia takatifu chochote kitolewacho lazima kionekane katika biblia sio katika maono yao wenyewe wanayojitungia.
Paulo aliandika maneno haya;
1 Wakorintho 3:10-15
[10]Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake.
[11]Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo.
[12]Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri.
[13]Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani.
[14]Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu.
[15]Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto.
Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa tofauti ya wale na hawa ni kwamba wote kazi yao ni moja ya upandaji wa kanisa la Kristo,mahali na mahali, isipokuwa wasasa hawaleti fundisho jipya, au maono mapya isipokuwa yale ambayo tayari yameshaanzishwa na mitume.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Nitamjuaje nabii wa Uongo?
Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?
Hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.
JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.
Katika 1Wakorintho 1:17, Paulo anasema hakuitiwa kubatiza, Je na mimi kama sijaitiwa kubatiza, bali nimeitiwa kuhubiri watu waokoke tu!, nitakuwa na hatia, nisipohubiri suala la ubatizo wala kuligusia kabisa?
Jibu: Ni muhimu kufahamu kuwa kila mtumishi wa kweli wa Mungu, haijalishi awe nani, ameitiwa KULIHUBIRI NENO LA MUNGU KATIKA UKAMILIFU WOTE, pasipo kubagua kipengele chochote katika maandiko. Huo ndio wito tuliopewa..
Tutatofautiana tu namna ya kuhubiri, kwasababu tunazo karama mbali mbali lakini INJILI NI MOJA KWETU WOTE!, Na wote tutahubiri kitu kimoja.. Hakuna mahali tumepewa maagizo ya kuhubiri tofauti tofauti au kulipunguza Neno la Mungu.
Sasa tukirudi kwenye swali, ni kwanini Paulo aseme sikuitiwa kubatiza?
Hebu tusome, mstari huo kwa utarati kisha tuendelee..
1Wakorintho 1:17 “Maana Kristo HAKUNITUMA ILI NIBATIZE, bali niihubiri Habari Njema; wala si kwa hekima ya maneno, msalaba wa Kristo usije ukabatilika”.
Hapa hakusema “MAANA KRISTO, HAKUNITUMA NIHUBIRI UBATIZO,” lakini badala yake anasema “KRISTO HAKUNITUMA NIBATIZE”. Maana yake kuhubiri Ubatizo Paulo alikuwa anauhubiri kama kawaida,(Soma Matendo 19:1-5 utalithibitisha hilo), lakini kitendo cha kufanya Ubatizo hakuwa anakifanya sana, bali mara moja moja sana… Ndio maana tukirudi juu kidogo katika mistari hiyo tunaona yeye mwenyewe anajishuhudia kubatiza watu baadhi..
1Wakorintho 1:14 “Nashukuru, kwa sababu sikumbatiza mtu kwenu, ILA KRISPO NA GAYO;
15 mtu asije akasema kwamba mlibatizwa kwa jina langu.
16 TENA NALIWABATIZA WATU WA NYUMBANI MWA STEFANA; zaidi ya hao, sijui kama nalimbatiza mtu ye yote mwingine”.
Umeona hapo anasema aliwabatiza Krispo, na Gayo Pamoja na watu wa nyumbani mwa Stefana.. Kuashiria kuwa alikuwa anabatiza, lakini hakuwa anaifanya hiyo huduma mara kwa mara, kulinganisha na huduma ya kwenda kuzunguka huku na huko kuhubiri Neno kwa watu aliyokuwa anaifanya.. Na wote walioamini injili yake aliwaongoza katika makanisa wabatizwe au watu maalumu wakabatizwe!..ili yeye apate nafasi ya kuendelea kuhubiri injili sehemu nyingine…Na ilipotokea hakuna mtu wa kuwabatiza kwa mahali hapo, basi alichukua yeye hilo jukumu la kuwabatiza!. kama hapo kwenye Matendo 19:2-6.
Ni sawa na jinsi Mitume walivyogawanya jukumu la kuwahudumia wajane, kwa wale Mashemasi 7 ili wao wadumu katika kulihubiri Neno.
Matendo 6:2 “Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, HAIPENDEZI SISI KULIACHA NENO LA MUNGU NA KUHUDUMU MEZANI.
3 Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili;
4 na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno.
5 Neno hili likapendeza machoni pa mkutano wote; wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao mwongofu wa Antiokia;
6 ambao wakawaweka mbele ya mitume, na walipokwisha kuomba wakaweka mikono yao juu yao”.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba, Hakuna mtu yeyote ambaye ameitiwa kufundisha Neno moja la kwenye biblia na kuliacha lingine…Wote tunapaswa tuhubiri injili yote, iliyo kamili, yaani injili ya toba, ubatizo, Imani, Roho Mtakatifu, na mambo mengine yote ya kiimani, pasipo kupunguza chochote wala kuongeza. sawasawa na (Ufunuo 22:18-19).
Sababu kuu inayowafanya asilimia kubwa ya wahubiri wabague baadhi ya maneno kwenye biblia na kufundisha baadhi tu, ni kwasababu wanaogopa kuumiza hisia za watu au kupoteza waumini!, na wala si kitu kingine!!.. Jambo ambalo ni la hatari sana!.. kuacha kuhubiri Neno la Mungu kwasababu ya kohofia hisia za mtu, atajisikiaje, au atakuonaje.
Ni heri kuonekana hufai, lakini umelizungumza Neno la Mungu katika ukamilifu wote, Ni heri mtu ahuzunike moyoni kwasababu ya kweli ya Neno uliyomweleza, kwasababu itamuumiza moyo sasa, lakini baadaye itakuwa ni tiba kwake na atakuja kumshukuru Mungu sana kwaajili yako..
2Wakorintho 7:10 “Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti”.
Lakini unajua kabisa ubatizo aliobatizwa sio sahihi, mavazi anayovaa sio ya kiimani, kazi anayoifanya sio halali, na kwasababu unaogopa usiumie utakapomwambia ukweli, unaishia kumfariji kuwa wewe hujaitiwa kuhubiri ubatizo au Mavazi au kazi mtu anayoifanya, wewe umeitiwa kumhubiria amwamini Yesu tu!.. Fahamu kuwa ndio unazidi kumpoteza huyo mtu!.
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
Je! Ni kanisa lipi sahihi kumuabudia Mungu?
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
SWALI: Biblia inamaana gani kusema “ maana vitu vyote ni watumishi wako”?. Je wanaotumia vifaa vya upako kama vile chumvi, maji, udongo, kuombea watu, wanatimiza kusudi lile lile la Mungu kwasababu na vyenyewe vinafanya kazi ya Mungu kwa nafasi hiyo? Je kwa mujibu wa andiko hilo ni sawa?
Zaburi 119:90 “Uaminifu wako upo kizazi baada ya kizazi, Umeiweka nchi, nayo inakaa.
91 Kwa hukumu zako vimesimama imara hata leo, MAANA VITU VYOTE NI WATUMISHI WAKO”.
JIBU: Ni kweli kama andiko hilo linavyosema, vitu vyote tunavyoviona katika mbingu na katika nchi ni watumishi wa Mungu, yaani, jua, mwezi, nyota, mawingu, milima, moto, maji, upepo, mafuta, udongo, mende, mbu, nzi, konokono, kipepeo vyote vinamtumikia Mungu.
Lakini swali ambalo tunapaswa tujiulize je vinamtumkia Mungu katika utumishi gani?
Ulishawahi kwenda kumuomba mjusi akusaidie kuomba rehema mbele za Mungu? Ulishawahi kuliomba jua likupe ridhki, ulishawahi kuamka asubuhi na kuuambia mwezi ukuponye magonjwa yako, na ukuepushe na ajali?
Kwanini usifanye hivyo, ilihali vyote vinamtumikia Mungu?.. Lazima ufahamu utumishi wao ni upi mbele za Mungu, kwa mfano, biblia inasema..
Zaburi 19:1 “Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza kazi ya mikono yake”.
Ikiwa na maana kuwa tutazamapo mbingu na anga, basi tunahubiriwa utukufu wa Mungu kwa kupitia hivyo, hapo tayari vimeshamtumikia Mungu, lakini hatuwezi kwenda kutumia mawingu ili Bwana atujibu maombi yetu.
Mungu kaweka njia kwa kila jambo, Na njia pekee ambayo alituchagulia sisi ili tumfikie Mungu, na kupokea wokovu wetu, na baraka zetu ni kwa kupitia YESU KRISTO tu na JINA LAKE Hapo ndipo tunapoweza kusaidiwa mahitaji yetu, na dua zetu. Kwasababu hatuna jina lingine au kitu kingine chochote kiwezacho kutuokoa sisi isipokuwa Jina lake tu. . (Matendo 4:12)
Sasa wapo watu wanasema, mbona, Yesu alitumia udongo, mbona manabii walitumia chumvi,..Wanashindwa kuelewa yapo MAINGILIO YA MUNGU. Ambapo Mungu mwenyewe upo wakati anashuka mahali Fulani kwa muda , kulitimiza kusudi lake Fulani, ndipo anapotumia chochote apendacho, kisha baada ya hapo hakuna kitu kingine cha ziada katika hicho kitu.
Ndio maana utaona wakati ule alipomtumia punda kuzungumza na Balaamu, hatuona tena, punda wakitumika kuzungumza na watu, kana kwamba ndio kanuni, hali kadhalika, Elisha alipoambiwa alale juu ya yule kijana kisha atakuwa mzima, hatuona tena, tendo hilo likifanyika hadi leo hii, tukilala juu ya wagonjwa ili wapate afya.
Ipo hatari kubwa sana ya kutumia vitu vya Mungu na kuvigeuza kuwa ndio kanuni za uponyaji, kosa mojawapo lililowafanya wana wa Israeli Mungu achukizwe nao, hadi kupelekwa tena utumwani Babeli, lilikuwa ni kuitumia ile sanamu ya shaba, Musa aliyoagizwa na Mungu aitengeneze kule nyikani, watu waiangaliapo wapone.
Hivyo watu wasiomjua Mungu, na MAINGILIO YAKE YA MUDA, wakaigeuza kuwa ndio sehemu ya ibada, walipofika nchi ya ahadi wakaiundia madhabahu kisha wakaanza kumwomba Mungu kupitia ile, mwisho wa siku wakawa wanaabudu mapepo pasipo wao kujijua na matokeo yake wakapelekwa Babeli utumwani.
Hivyo nawe pia ukiona mahali popote uendapo, vitu kama hivyo vimefanywa kama kanuni, kila wiki ni maji ya upako, mafuta, chumvi, au kingine chochote, ujue kuwa huna tofauti na wale waabudu sanamu, na jua na mwezi, na unayemwabudu hapo sio Mungu bali ni shetani mwenyewe. Na Unamkasirisha Bwana sana.
Jina ambalo tumepewa sisi, tulitegemee kwa kila kitu, na kila saa ni jina la YESU KRISTO TU.. Hilo ndio uligeuze kuwa sanamu yako, na si kitu kingine chochote. Kama ulikuwa unafanya hivyo basi acha mara moja.
Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.
Hivyo, kwa hitimisho ni kuwa, mstari huo haumaanishi maji, au chumvi, au udongo, au kitu kingine chochote kinaweza kufanya shughuli ya upatanisho wa mwanadamu. Hapana ni uongo. Vinamtumikia Mungu, lakini sio katika mambo ya wokovu wetu.
Bwana atuepushe na sanamu.
Shalom
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
USIJARIBU KUMGEUZA MUNGU MGANGA WA KIENYEJI,UTAKUFA.
KWA KUWA WASEMA MIMI NI TAJIRI.
Bwana alimaanisha nini kusema“maana mtenda kazi astahili posho lake”
Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani,
Moja ya maagizo ambayo Bwana Yesu aliwapa wanafunzi wake alipowatuma kwenda kuhubiri injili mbali, lilikuwa ni kutokulipisha fedha katika huduma yoyote watakayoitoa, hali kadhalika kutokubeba chochote katika safari yao. Yaani wasiwe na maandalizi yoyote ya njiani, Lakini mwishoni kabisa mwa maagizo yake aliyasema maneno haya “maana mtenda kazi astahili posho lake”.. Sasa swali linakuja Je hili posho ni lipi alilostahili huyu mtandakazi ili hali ameitwa atoe bure?
Mathayo 10:8 “Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.
9 Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu;
10 wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, wala fimbo; maana mtenda kazi astahili posho lake”.
JIBU: Posho aliyostahili ni ile ambayo Bwana Yesu mwenyewe atampa katika kazi ya injili anayoipeleka, kwa kupitia watu wakarimu ambao Bwana Yesu mwenyewe atawagusa moyo huko waendako aidha kwa kuwapa maji, au chakula, au nguo, na wakati mwingine hata fedha.
Hiyo yote ni kuonyesha kuwa Bwana Yesu anaweza kumtunza mtumwa wake, katika mazingira yoyote atakayomtuma. Na ndiyo maana mwishoni kabisa akawaambia maneno haya;
Luka 22:35 “Akawauliza, Je! Hapo nilipowatuma hamna mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu? Wakasema, La!
Ni kufunua kuwa hatupaswi kuwa na wasiwasi wa maandilizi yoyote ya huduma ya Kristo, pale ambapo hatuna chochote, Bwana anataka tuwe wepesi (SIMPLE), tusijali sana tutakula nini, tutavaa nini huko tuendako, kesho tutatolea wapi nauli ya kurudi, hilo jambo Bwana hataki sisi kama watumwa wake tulifikirie, kwasababu ameahidi kabisa ikiwa tunatenda kazi yake kiuaminifu, basi tumestahili posho yake, hivyo anza kutumika.
Lakini haimaanishi kuwa, wakati wote, hata kama unacho, ndio ujifanye hauna, hapana, bali, upo wakati wewe kama mtumishi wa Mungu utabarikiwa na utakuwa navyo vya kuendea huko katika ziara, hivyo vitumie hivyo, Na ndio maana wakati mwingine Bwana aliwaambia wajibebe fimbo ya njiani, na kujifungia viatu, wakati sehemu nyingine kama tuliyosoma hapo juu aliwakataza.(Marko 6:8-9)
Kwahiyo, kwa vyovyote vile, Bwana atatutunza, ilimradi tunamtumkia yeye kwa uaminifu. Tusiwe na wasiwasi na huduma yake, Haleluya..
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
WITO WA MUNGU HAUVUKI NENO LAKE.
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.
BWANA AWEZA KUKUPA ZAIDI SANA KULIKO HIZO.
SWALI: Shalom… Pastor naomba kuuliza je ni sahihi mtumishi kuongoza kanisa hajafunga ndoa? na anaweza kubatiza washirika? Amina.
JIBU: Kigezo cha mtu kuwa Kiongozi wa kanisa, na kufanya kazi zote za madhabahuni, ikiwemo kubatiza, kuwawekea watu mikono ya utumishi, n.k. vimetolewa katika kitabu cha 1Timotheo 3:1-7
1 Timotheo 3 : 1-16
1 Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.
2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;
3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;
4 mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu;
5 (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)
6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.
7 Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.
Askofu maana yake ni mwangalizi wa kanisa, Hivyo yeyote anayelichunga kanisa, awe ni mchungaji, mwalimu, Mtume, maana yeye ndio mwangalizi basi vigezo hivyo vinamuhusu.
Lakini katika vigezo hivyo vyote, hakuna hata kimoja, kinachosema, ni lazima aoe.. Isipokuwa anasema Askofu ni lazima awe ni mume wa mke mmoja..Akiwa na maana kwamba ikiwa ni mwana-ndoa basi, anapaswa awe ni mume wa mke mmoja, na si Zaidi, kama anao wake wawili au watatu, tayari ameshakidhi vigezo vya kutostahili kuitwa mchungaji.
Lakini ikiwa ni mtu ambaye, hajaoa lakini ameshika vigezo vyote, hivyo, yaani, ni mtu asiyelaumika, si mlevi, mpole, si mpenda fedha, aliyeshuhudiwa na watu ni mwema, amekomaa kiroho. Basi huyo anavigezo vyote vya kuwa mchungaji, au kiongozi yoyote wa kanisa.
Mtume Paulo hakuwa ameoa, lakini alikuwa ni mwangalizi wa makanisa yote yaliyokuwa Asia, na mataifa mengine, Na Zaidi sana yeye ndiye aliyetoa mwongozi wa mafundisho ya ndoa.
Hivyo kuoa/ kutokuoa, si takwa, la kuwa askofu.
Kinyume chake mtume Paulo,alishauri watu wote wawe kama yeye (yaani wasioe), kwasababu watu wasiooa inawapa wigo mpana wa kumtumikia Mungu bila kuvutwa na mambo mengine, ikiwa wamemaanisha kweli kujikita kwa Bwana.
1Wakorintho 7:32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;
33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe”.
Lakini ikiwa huwezi kuishi Maisha hivyo, kwa jinsi ulivyoitwa, basi hakikisha unatumika kiuaminifu, hapo utakuwa umekidhi vigezo vya kulichunga kundi , kubatiza, n.k.
Bwana akubariki.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je! Shetani anao uwezo wa kuumba, kama Mungu?
Uvuvi bora hauchagui wa kuvua.
Askofu na mchungaji mkuu ni nani?
Nakusalimu katika jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo. Ni siku nyingine tena Bwana ametupa neema ya kuiona, hivyo nakukaribisha sasa tuzidi kuyatafakari maneno matukufu ya Mungu wetu, Maadamu katujalia kuiona leo.
Kwanini leo hii imekuwa ngumu sana kuipeleka injili kwa watu walio nje, ili wamwamini Yesu Kristo (Tukisema walio nje, tunamaanisha watu wa kidunia, au watu walio katika dini nyingine), Tunaweza kusema Mungu anawajua walio wake, ni kweli, lakini hicho sio kisingizio, ipo sababu nyingine ambayo tumeikosa sisi kama kanisa na sababu yenyewe ni kukosa UMOJA.
Tukiupata huo kama kanisa basi hatutamia nguvu nyingi sana kuulezea ulimwengu uzuri wa Yesu, bali huo umoja wenyewe tu utauaminisha ulimwengu yeye ni nani.
Bwana Yesu alilizungumza hilo katika..
Yohana 17:21 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ILI ULIMWENGU UPATE KUSADIKI YA KWAMBA WEWE NDIWE ULIYENITUMA.
22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.
23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ILI ULIMWENGU UJUE YA KUWA NDIWE ULIYENITUMA, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Umeona, kumbe ulimwengu unaweza kumwamini Yesu, kuwa ndiye mwokozi wa ulimwengu, ikiwa tu tutajitengeneza sisi kwanza katika umoja. Lakini tunapaswa tujue si kila umoja, ni umoja sahihi unaotokana na Mungu..Hapo Bwana hazungumzii umoja wa kichama au umoja wa kidini, au umoja wa kimadhehebu, kama unaoendelea sasa hivi ulimwenguni.. bali umoja anaouzungumzia hapo ni umoja wa Roho,. Kwasababu haiwezekani watu wawili wanaamini vitu viwili tofauti, halafu wawe na umoja, huo sio umoja utakuwa ni umoja wa kimaslahi tu, lakini sio wa Roho.
Waefeso 4:3 “na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.
5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.
6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote”.
Umeona vifungu hivyo? Agizo mojawapo ni kwamba tuutambue ubatizo mmoja na sahihi ni upi, kisha wote tuwe nao, ambao ni ule wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo sawasawa na Matendo 2:38, 8:16, 10:48, 19:5, kisha wote tumpokee Roho mmoja, ambaye ndiye Roho Mtakatifu, tuwe na Bwana mmoja ambaye ni YESU KRISTO jiwe kuu la pembeni, na sio mtume mwingine, au mtakatifu mwingine pembeni yake hapana,.. Na vilevile tuwe na Imani moja, ambayo mzizi wake na shina lake ni BIBLIA TAKATIFU na sio dini au dhehebu.
Tukizingatia hayo, kisha tukashirikiana na ulimwengu ukatuona, basi hatutatumia nguvu kubwa kuwaamishi Kristo kwao, kwani huo umoja wenyewe tu utawahubiria watu uzuri wa Kristo. Lakini tukizidi kuupoteza umoja huo, kila mtu na imani yake, dhehebu lake,. Ni ngumu sana kuugeuza ulimwengu. Hivyo ni wajibu wetu sisi, kama kanisa la Kristo tujipime, je! Umoja huu uliosahihi upo ndani yetu? Kama haupo, basi ipo kasoro. Tujitahidi sana tuunde kwa bidii zote, ili Bwana aaminiwe katikati ya mataifa, matunda mengi yaje kwake..
Hilo ni agizo la Bwana, na sio la mwanadamu.
“Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ILI ULIMWENGU UJUE YA KUWA NDIWE ULIYENITUMA, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi”.
Shalom.
Maran atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
SWALI: Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako, mafuta ya upako au chumvi katika kufanya maombezi?
JIBU: Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa kinachomponya mtu ni damu ya Yesu Pekee. Na ndani ya damu ya Yesu ndio kuna Jina la Yesu…Hivyo jina la Yesu linapotajwa ni tangazo maalumu la damu ya Yesu katika utendaji kazi wake, hivyo kila ugonjwa au tatizo kwa jina la Yesu linaondoka na kupotea kabisa!.
Kwahiyo haipaswi kwa vyovyote vile kufikiri au kuamini kwamba kitu kingine zaidi ya damu ya Yesu kinaweza kumponya mtu au kinaweza kuondoa matatizo ya mtu au kumbariki. Kuamini hivyo hakuna tofauti na kuabudu sanamu.
Sasa pamoja na hayo, Mungu ameruhusu uponyaji wa damu ya Yesu wakati mwingine ufuatane na maagizo Fulani…Kwamfano daktari anaweza kutoa dawa kwa mgonjwa wa ngozi na kutolea maagizo kwamba akameze vidonge hivi na maji ya kutosha..au akampa vidonge vingine na kumwambia akavitie kwenye maji kisha aogee, afanye hivyo mara tatu kwa siku tatu na huo ugonjwa huo wa ngozi utamwisha..Au anaweza asimpe kidonge chochote na badala yake akamchoma sindano tu na bado ukapona vile vile…Ni kwajinsi tu yeye atakavyopenda kuchagua njia iliyobora.
Na Roho Mtakatifu ni hivyo hivyo…katika suala la kumponya mtu, mara nyingine anaweza kuambatanisha na maagizo Fulani…aidha mtu atumie mafuta, au udongo kwa jinsi Roho Mtakatifu atakavyopenda…kama alivyofanya Bwana katika Yohana 9:6 (alimwongoza atumie tope la mate yake), au anaweza akampa mtu maelekezo atumie unga kama Elisha alivyofanya katika 2Wafalme 4:41, au chumvi kama alivyofanya Elisha katika 2Wafalme 2:21 au kutumia leso kama alivyofanya Paulo katika Matendo 19:11-12..au chochote kile…Lakini ni kulingana na uongozo wa Roho Mtakatifu…Na sio kama mtindo!..kama inavyofanyika leo na wengi wanaofahamika kama watumishi wa Mungu.
Leo hii kila tatizo linatatuliwa na chumvi wanazoziita chumvi za upako, au mafuta …hata mtu akiugua tu, suluhisho ni mafuta ya upako! Au maji ya upako!..kila kitu ni mafuta ya Upako na ni kitendo endelevu na kinachojirudia kila siku…Sasa hilo sio agizo la Roho Mtakatifu…kwasababu Roho Mtakatifu hana mtindo Fulani/staili Fulani ya kumponya mtu.
Kwasababu hata Bwana Yesu sio kila mahali watu walipomjia mwenye matatizo Fulani alikuwa anatema mate chini na kutengeneza tope na kuwapaka na kufunguliwa shida zao!…utaona alifanya hivyo mara moja tu! Na tena kuna jambo alikuwa anafundisha, Na hakuna sehemu nyingine yoyote alirudia kufanya hivyo, kuonyesha kuwa nyakati zote alikuwa anasubiria maagizo ya Roho Mtakatifu, na hakufanya agizo Fulani la Roho Mtakatifu kuwa kama mtindo.
Na sio yeye tu! Hata Elisha hakuwa na staili/mtindo wake maalumu, wala hata Mtume Paulo ambaye nguo zake na Leso yake kuna wakati ilitumika hata kuondoa mapepo(Matendo 19:12)…utaona kuwa haikuwa hivyo kila mara, na wala Paulo hakugeuza kuwa kama mtindo..kwamba kila aliyekutana naye alimtupia leso ili afunguliwe!..hutaona akizituma nguo zake korintho au Galatia watu wakafunguliwe wala hakuwahi kuhubiri hayo mambo… sehemu kubwa sana alikuwa anatumia jina la Yesu…na alikuwa anamuhubiri Kristo na si mavazi yake wala leso zake. Na mitume wengine wote wa Bwana Yesu ni hivyo hivyo…tunamsoma Mtume Petro kuna wakati hadi kivuli chake kilikuwa kikimpitia mtu mwenye ugonjwa, Yule mgonjwa anafunguliwa! (kasome Matendo 5:15). Lakini hutaona mahali popote Petro akiitumia hiyo kama ndio staili yake/mtindo wa kuwafanya watu wafunguliwe…bali utaona mara karibia zote alikuwa anatumia Jina la Yesu tu!..
Matendo 3:3 “Mtu huyu akiwaona Petro na Yohana wakiingia hekaluni aliomba apewe sadaka.
4 Na Petro, akimkazia macho, pamoja na Yohana, akasema, Tutazame sisi.
5 Akawaangalia, akitaraji kupata kitu kwao.
6 Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. KWA JINA LA YESU KRISTO WA NAZARETI, SIMAMA UENDE.
7 Akamshika mkono wa kuume, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu.
8 Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda; akaingia ndani ya hekalu pamoja nao, akienda, akiruka-ruka, na kumsifu Mungu”.
Hapo Petro hakutumia “kivuli” chake!…Bali jina kuu la YESU KRISTO!.
Sasa utauliza mbona kuna watu wanayatumia maji ya upako, au mafuta ya upako kama mtindo wao na wanafunguliwa?
Wengi wanaofunguliwa ni wale ambao ni wachanga kiimani, ambao ndio kwanza wamemjua Kristo, au wameingia kwenye imani ya kikristo, Hivyo Bwana anaruhusu wapokee miujiza yao kwa njia yoyote ile..ili wazidi kumsogelea Mungu katika hivyo vipindi vya awali, lakini baada ya kipindi Fulani kupita wakaujua ukweli, au kusikia injili kwa muda mrefu na kushupaza shingo, zinabadilika kwao kuwa ibada za sanamu, na havitawapii chochote zaidi ya kuzidi kuwaweka mbali na Mungu, na hata wakati mwingine kuingiliwa na mapepo, na kupoteza hata vile walivyo navyo kwasababu ni ibada za sanamu…wanatanga huko na huko kutafuta na kununua maji ya upako, chumvi ya upako…Na kwasababu wengi wao hawapendi kuzidi kumjua Mungu wanadanganyika!
Na manabii wengi wa uongo wamezuka sasa, katika siku hizi za mwisho kama ilivyotabiriwa…Mungu ameachilia nguvu ya upotevu kwa wale wote wanaoukataa ukweli…Na nguvu hiyo ya upotevu kaiweka ndani ya manabii wa uongo…Na lengo la nguvu hiyo ni ili watu wote wanaoukataa ukweli wazidi kudanganyika!…ili tofauti ya magugu na ngano ionekane kwaajili ya mavuno.(Mavuno hayawezi kuja bila magugu na ngano kujitenga kisawasawa!..)
2Wathesalonike 2:10 “na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.
11 Kwa hiyo Mungu AWALETEA NGUVU YA UPOTEVU, wauamini uongo;
12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu”.
Hivyo ni wakati wa kuwa makini sana na kuwa macho, na kujihadhari na roho zidanganyazo!…Kama hujapewa maagizo yoyote na Roho Mtakatifu basi usikurupuke kutumia maji,chumvi, udongo, au chochote kile ni hatari sana kwa roho yako!…Tumia Jina la Yesu tu pekee linatosha…
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 693036618/ 0789001312.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.
MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
BIRIKA LA SILOAMU.
Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?
Mtu astahiliye hofu ni yupi?
Kutokuihubiri injili, madhara yake ni yapi?
Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe..Karibu tujifunze Biblia mtu wa Mungu…Leo tutajifunza mambo machache muhimu yahusuyo majukumu yetu ya kuihubiri Injili.
Injili maana yake ni “Habari njema”..Habari yoyote au ujumbe wowote unaoupeleka kwa mtu au watu ulio mwema huo tayari ni injili…Zipo Injili za aina nyingi duniani lakini ipo injili moja tu ya wokovu..Au kwa lugha nyingine inaitwa “Injili ya Msalaba”…Injili ya Msalaba inamhusu Yesu Kristo mwana wa Mungu aliyetumwa kuichukua dhambi ya ulimwengu..Hiyo inahusu wokovu wa mwanadamu ambaye alipotea dhambi. Na Kumbuka wanadamu wote walipotea dhambini hivyo injili hii inamuhusu kila mmoja wetu.
Sasa Baada ya Bwana Yesu kuondoka ilikuwa ni sharti injili ihubiriwe ulimwenguni kote kwa kila kiumbe, na kwamba kila mwanadamu lazima aisikie injili hiyo ya wokovu…Na kwa hiari yake mwenyewe achague UZIMA au MAUTI. Kwasababu hiyo basi akawaagiza mitume wake akawaambia..
Marko 13.9 “Nanyi jihadharini nafsi zenu; maana watawapeleka ninyi mabarazani; na katika masinagogi mtapigwa; nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao.
10 NA SHARTI INJILI IHUBIRIWE KWANZA KATIKA MATAIFA YOTE”.
Hapo anasema ni SHARTI!..Maana yake ni lazima injili ifike kila mahali..Kwa uzima na kifo, hata ikigharimu uhai ni lazima injili iwafikie watu..Hivyo hilo ni jukumu tulilopewa watu wote tuliompokea Kristo..Ni lazima tuihubiri Injili…Na siku zote Mungu anatumia watu kuhubiri Injili, kawachagua watu kusimama madhabahuni kumwakilisha…kamwe hatumii wanyama, wala malaika, wala kiumbe kingine chochote kamchagua mwanadamu tu!!..
Sasa kuna hatari kubwa sana ya kutokuihubiri injili…Kuna hatari kubwa sana ya kutokuitumia karama Mungu aliyokupa katika kuwahubiria wengine..Bwana amekuokoa wewe, ili na wewe ukawe msaada kwa wengine…hajatuokoa ili tu tufurahi sisi wenyewe..Kama tunavyojua wengi wetu hatujampokea Yesu kwa kutokewa na yeye…wengi wetu tumesikia injili ikihubiriwa mahali fulani na mtu Fulani wa Mungu ndipo kwa kupitia hayo mahubiri tukaokoka… Kutokuihubiri injili ni kosa kwa mtu anayeitwa mkristo.
Kadhalika huo ndio utaratibu wa Mungu, Ni lazima tuisikie kutoka kwa mtu fulani wa Mungu…na hivyo na sisi pia lazima tuwahubirie wengine ambao nao watasikia kutoka kwetu, ni kama mnyororo huyu anamzaa huyu katika imani, huyo anamzaa Yule na kuendelea..
Sasa kama umeokolewa na hutaki kuzaa wengine…kuna hatari kubwa sana…Tukirudi kwenye biblia tunamsoma Nabii mmoja aliyeitwa EZEKIELI..Huyu alikuwa ni nabii wa Mungu wa kweli kabisa., ambaye alikuwa miongoni mwa watu wachache waliochukuliwa kwenda Babeli…wakati yupo huko Mungu mwenyewe alimtokea akamwonyesha maono akiwa ameketi katika kiti chake cha Enzi huku maserafi na makerubi wakiwa wamemzunguka pande zote..akasikia sauti ya Mungu mwenyewe..Na Mungu akamtuma aende kuwaambia wana wa Israeli maovu yao na maasi yao na mambo yatakayokuja kuwatokea huko mbeleni wasipotubu.
Lakini yeye alipotoka pale baada ya kuona maono hayo…akaenda kukaa kimya, hakuwaambia watu chochote… sio kwamba alikuwa na dharau hapana! Hakumdharau Mungu…lakini alikuwa anaogopa kuwaambia(Alikuwa na hofu)….alikuwa na uchungu kweli na hasira moyoni, kwa maovu yaliyokuwa yanafanyika katikati ya watu wake lakini alikuwa anajifikiria fikiria namna ya kuwaambia..…akakaa siku saba hawaambii hao watu maono aliyoonyeshwa na Mungu…Baada ya siku saba maono yakamjia tena na kumwonya kwa anachokifanya cha kutowaambia watu maneno ya Mungu..Mungu akamwonya vikali kwa tabia hiyo..
Ezekieli 3:15 “Ndipo nikawafikia watu waliohamishwa, huko Tel-abibu, waliokuwa wakikaa karibu na mto Kebari, nikafika huko walikokuwa wakikaa; nikaketi huko miongoni mwao muda wa siku saba, katika hali ya ushangao mwingi.
16 Hata ikawa, mwisho wa siku saba, neno la Bwana likanijia, kusema,
17 Mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi wa nyumba ya Israeli; basi, sikia neno hili litokalo katika kinywa changu, ukawape maonyo haya yatokayo kwangu.
18 Nimwambiapo mtu mbaya, Hakika utakufa; wewe usimpe maonyo, wala husemi na huyo mtu mbaya ili kumwonya, kusudi aache njia yake mbaya na kujiokoa roho yake; mtu yule mbaya atakufa katika uovu wake; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako.
19 Lakini ukimwonya mtu mbaya, wala yeye hauachi ubaya wake, wala njia yake mbaya, atakufa katika uovu wake; bali wewe umejiokoa roho yako”.
Umeona?..Ezekieli baada ya kusikia maneno hayo kutoka kwa Bwana kwamba “damu ya mtu itakuwa juu yake endapo hatamwambia maneno aliyoambiwa amwambie”..Ndipo akaelewa hakuna suala la mizaha tena kwenye kupeleka ujumbe wa Mungu kwa watu…Tangu wakati huo chochote alichoonyeshwa aliwafikishia wahusika kama kilivyo…Kwasababu alijua atadaiwa damu!. Hakuishi maisha ya kutokuihubiri injili tena.
Ndugu..Kama Bwana anakuonyesha maono ya kuwaonya watu juu ya dhambi zao na wewe huwaambii jifunze kwa Ezekieli hapo juu, kama unafahamu Neno na uwaambii wengine kuna hatari…Ni afadhali uwaambie wakatae kwa mapenzi yao wenyewe wewe utakuwa umenawa mikono..kuliko kutowaambia kabisa…mtu huyo akitoka na kwa bahati mbaya akagongwa na gari na kufa, unadhani wewe utakuwa katika hali gani?.
Kama umefahamu kuwa wazinzi na waasherati watakwenda kuzimu wasipotubu, na wewe mwenyewe sio mwasherati kwanini usiwaambie?…Mwambie ili aokoke, suala la kumbadilisha sio juu yako…wewe kazi yako ni kuhubiri tu injili…Lakini pia kama na wewe binafsi unafanya mambo hayo hayo wanayowafanya hao basi hapo usiwahubirie kwasababu wewe mwenyewe unahitaji wokovu..Na kipofu hawezi kumwongoza kipofu mwenzake..biblia inasema hivyo.
Hivyo kama ulikuwa uhubiri..anza leo!..Kama ulikuwa unaogopa kuwaambia watu juu ya habari ya siku za mwisho anza kuwaambia..Ezekieli aliogopa kuliko wewe lakini aliposikia suala la damu ya hao watu itatakwa juu yake, aligueka mara moja na wewe hivyo hivyo geuka leo..Na Bwana atakusaidia. Ipo hatari kubwa sana ya kutokuihubiri injili
Na kama hujaokoka kabisa..Tubu leo, mlango wa Neema bado upo wazi.. ila hautakuwa hivi siku zote..Umesoma hapo juu kitu gani kitamtokea mtu Yule atakayekufa katika dhambi zake huku ameonywa na amekataa…
Eze.3:19 “Lakini ukimwonya mtu mbaya, wala yeye , wala njia yake mbaya, atakufa katika uovu wake; bali wewe umejiokoa roho yako”.
Na wewe leo umesikia injili usipotaka kutubu utakufa katika dhambi zako na madhara ya kufa na dhambi ni ziwa la moto.
kwahiyo pale ulipo mwombe Bwana msamaha, tubia uasherati wako kama ni mwasherati, ulevi wako,uongo wako, rushwa zako, usengenyaji wako,wizi wako, matusi yako… kisha katafute Ubatizo sahihi kama hujabatizwa na Roho Mtakatifu atakutakasa na kukufanya kuwa mkamilifu kama yeye alivyo mkamilifu…
Marko 1:15 “akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni, na kuiamini Injili”.
Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Shalom.
Mada Nyinginezo:
KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?
JE VIBWENGO NI KWELI VIPO?
KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.
UPAKO NI NINI?
Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?