Category Archive maswali na majibu

Kwanini MUNGU alimzuia Daudi asimjengee HEKALU? (1Nyakati 17:12)

Jibu: Turejee…

1 Nyakati 17:11-12 “Hata itakuwa, siku zako zitakapotimia, uende na babazo, nitainua mzao wako nyuma yako, atakayekuwa wa wana wako; nami nitaufanya imara ufalme wake.

12 Yeye ndiye atakayenijengea nyumba, nami nitakifanya imara kiti cha enzi cha ufalme wake milele”.

Unabii huu unamuhusu BWANA YESU KRISTO, na si SULEMANI. yeye (YESU) ndiye atakayetokea na kuijenga nyumba ya MUNGU (Hekalu) lililo kamilifu na takatifu,  na nyumba hiyo ni MWILI wake (Yohana 2:19-22).

Lakini pamoja na hayo pia Hekalu la damu na Nyama, Mungu alimzuia Daudi asilijenge KWASABABU alimwaga damu nyingi za hatia na zisizo za hatia, na kwasababu hiyo Mungu hakumruhusu aijenge nyumba ile bali mwanae Sulemani.

1  Nyakati 28:3 “Lakini Mungu akaniambia, Wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu, kwa sababu umekuwa mtu wa vita, nawe umemwaga damu ………………

5 tena katika wana wangu wote (kwani BWANA amenipa wana wengi), amemchagua Sulemani mwanangu ili aketi juu ya kiti cha enzi cha ufalme wa BWANA, juu ya Israeli.

6 Akaniambia, Sulemani, mwanao, ndiye atakayeijenga nyumba yangu na nyua zangu; kwa kuwa nimemchagua awe mwanangu, nami nitakuwa babaye”

Na ni damu za akina na Daudi alizozimwaga?.

   1.DAMU ZA MAADUI.

Daudi alikuwa ni mtu wa vita tangu ujana wake, yeye pamoja na mashujaa wake walikuwa ni watu wa kuua maadui zao kwa upanga, hilo likawa kizuizi kwa Daudi kuijenga nyumba ya Bwana.

   2. DAMU YA URIA.

Damu ya Uria, jemedari aliyoimwaga Daudi, ilikuwa ni kikwazo kikubwa cha Daudi kupata ruhusu ya kuijenga nyumba takatifu ya Mungu atakayokaa..

Kwani laiti Daudi angeijenga nyumba ile pamoja na tendo lake hilo alilolitenda la kumuua Uria na kumchukua mke wake, basi maadui wa Bwana wangeiona hiyo nyumba aliyoijenga na kukumbuka Daudi aliyoyafanya, wangepata sababu ya kukufuru na kukashifu ile nyumba sawasawa na maneno ya Bwana.

2 Samweli 12:13 “Daudi akamwambia Nathani, Nimemfanyia BWANA dhambi. Nathani akamwambia Daudi, BWANA naye ameiondoa dhambi yako; hutakufa.

14 Lakini, kwa kuwa kwa tendo hili umewapa adui za BWANA nafasi kubwa ya kukufuru, mtoto atakayezaliwa kwako hakika yake atakufa”.

Ni lipi tunaloweza kujifunza hapo?

Bwana hakuwahi kupendezwa na mauaji tangu mwanzo, watu wa kale waliruhusiwa kuua kwasababu ya ugumu wa mioyo yao, lakini tangu mwanzo Bwana alikataza mauaji Soma Kutoka 20:13.

Hivyo hatuwezi kuishi sasa kwa kuyaangalia matendo ya Daudi, kama Daudi aliua basi na sisi ndio tuue, kama Daudi alioa wake wengi basi na sisi ndio tuoe wake wengi n.k.

Bali tunamtazama YESU KRISTO sasa aliye Ukamilifu na Utimilifu wa sheria, yeye anasema…

Mathayo 5:38 “Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino;

39 Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili.

40 Na mtu atakaye kukushitaki na kuitwaa kanzu yako, mwachie na joho pia.

41 Na mtu atakayekulazimisha mwendo wa maili moja, nenda naye mbili”.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Bwana alimaanisha nini kusema “Yeye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo”? (Mathayo 23:20)

Daudi alikuwa na wake wangapi, na je ni halali kuwa na wake wengi?

Je! Habari iliyo katika 1Nyakati 21:25, na 2Samweli 24:24, ya Daudi kununua kiwanja  inajichanganya?

MAANA ROHO HUCHUNGUZA YOTE, HATA MAFUMBO YA MUNGU.

Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita;

SWALI: Biblia humaanisha nini kwenye vifungu hivi?

Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita; Lakini mkosaji mmoja huharibu mema mengi.


JIBU: Ni vema kwanza kufahamu kwanini watu wanapigana vita?

Zipo sababu nyingi,baadhi ya hizo ni hizi,

Kujilinda, kutoelewana, kulipiza visasi, kutofautiana kiitikadi, au kutanua ngome.

Hivyo ili watu kufikia malengo hayo, njia pekee waionayo ni kutumia silaha, kuuana. Lakini biblia inashauri njia iliyo bora zaidi ambayo inaweza kutumiwa na hatimaye yote hayo yakatatulika. Na njia hiyo ni hekima.

Hekima ni nini?

Hekima ni uwezo wa kipekee utokao kwa Mungu, unaomsaidia mtu kuweza kupambanua, au kutatua, au kuamua jambo Fulani vema. Hivyo kupitia hekima mtu anaweza kuponya vitu vingi pasipo uharibifu wowote, na kuunda mfumo bora.

Sulemani ambaye ndiye aliyeyaandika maneno hayo alijaliwa amani katika ufalme wake, sio kwamba hakuwa na maadui wanaomzunguka hapana, bali alipewa hekima ya kuishi nao, na kuzungumza nao, na kukubaliana nao, hivyo Israeli hakukuwa na kumwagika damu kama ilivyokuwa kwa baba yake Daudi, ambaye yeye kutwa kuchwa alikuwa vitani. Kilichoweza kumsaidia ni hekima ya Mungu ndani yake.

Lakini sehemu ya pili ya mstari huo anasema;

Lakini mkosaji mmoja huharibu mema mengi’.  Akiwa na maana mkosaji mmoja (wa hekima), jinsi anavyoweza kuharibu mipango mingi mizuri ambayo huwenda ilikuwa tayari imeshaleta matokeo mema. Na kweli hili angalia mahali penye viongozi wabovu, huathiri jamii nzima, hata Israeli, Wafalme wa kule ndio waliisababishia Israeli kunajisika kwa muda mrefu hadi kupelekea kwenda utumwani Babeli mfano wa hao walikuwa ni Yeroboamu na Ahabu.

Kwa ufupi vifungu hivi vinatueleza uzuri wa hekima, lakini pia madhara yasababishwayo pale hekima inapokosekana, hata kwa udogo tu.

Je! Mtu anawezaje kupata hekima?

Hekima chanzo chake ni kumcha Mungu. (Mithali 9:10). Ambapo panaanzia kwenye wokovu, kisha kuendelea kuishi maisha ya utii kwa Kristo baada ya hapo.

Mtu wa namna hii, huvikwa, ujuzi huo wa ki-Mungu, na hivyo anakuwa na uwezo wa  kuutibu ulimwengu kwa namna zote. Mioyo, Ndoa,kanisa, jamii, taifa, vyote huponywa kwa hekima msingi huu wa hekima ya ki-Mungu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWA KUWA ROHO BORA ILIKUWA NDANI YAKE.

Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?

USIWE NA HAKI KUPITA KIASI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Matasa ni nini? (1Nyakati 28:17)

Jibu: Turejee..

1Nyakati 28:17 “na nyuma, na mabakuli, na vikombe vya dhahabu safi; na kwa MATASA ya dhahabu, kwa uzani kwa kila TASA; na kwa matasa ya fedha, kwa uzani kwa kila tasa”.

Ukisoma kuanzia juu utaona kuwa hivyo ni vyombo ambavyo vingepaswa viwepo ndani ya MUNGU aliyokusudia kuijenga Mfalme Daudi.

Lakini kwasababu haikuwa mapenzi ya MUNGU mfalme Daudi aijenge ile nyumba bali mwanae (Sulemani)…hivyo ilimbidi Mfalme Daudi ampe maelekezo ya namna ya kuijenga ile nyumba na viwango vyake.

Moja ya maagizo aliyompa kulingana na alivyooneshwa na Bwana ni uwepo wa MATASA ndani ya nyumba hiyo..(kwamba atakapoijenga basi aweke Matasa ya dhahahu ndani yake).

Sasa Matasa yalikuwa ni nini?

Matasa yalikuwa ni “Makarai/mabeseni” ya dhahabu yaliyowekwa ndani ya Hekalu kwa kusudi la kutawadha (kunawa).

Kwasababu ndani ya Hekalu kulikuwa na makuhani wengi waliokuwa wanafanya kazi mbalimbali na kwa zamu, na kulingana na desturi za wayahudi ilikuwa ni lazima kila Kuhani anawe

(atawadhe) kabla ya kuanza kazi ya kikuhani na hata baada ya kumaliza.

Hivyo vyombo hivyo (MATASA) vilitumika kuhifadhia maji kwaajili ya shughuli hiyo.

Na pia vilikuwepo VITASA hivi vilikuwa ni vibaluli vidogo vya kuweza kushikwa kwa mkono, tofauti na Matasa ambayo yalikuwa yanabeba ujazo mkubwa wa maji, na vitasa ndio vile vinavyotajwa katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana  mlango wa 15 na 16.

Ufunuo 15:5 “Na baada ya hayo nikaona, na hekalu la hema ya ushuhuda mbinguni lilifunguliwa;

6 na wale malaika saba, wenye mapigo saba, wakatoka katika hekalu, wamevikwa mavazi ya kitani safi, ya kung’aa, wamefungwa vifuani mwao mishipi ya dhahabu

7 Na mmoja wa wale wenye uhai wanne akawapa wale malaika saba VITASA SABA vya dhahabu, vimejaa ghadhabu ya Mungu, aliye hai hata milele na milele”.

Ni nini tunajifunza katika hayo?

Tunachoweza kujifunza ni kuwa matasa ya Hekalu la duniani yalijaa maji ya kuoshea makuhani lakini vile VITASA vya Hekalu la mbinguni vimejaa hasira na hukumu ya MUNGU kwa wanadamu wasiomcha yeye.

Bwana atusaidie tumtafute, tusipotee wala kuangukia katika hukumu yake.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?

YAKINI NA BOAZI.

Je wakati Bwana YESU anazaliwa shetani alikuwa amefungwa?

Vihekalu vya fedha vya Artemi vilikuwaje? (Matendo 19:24).

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Yohana 20:22 Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa;

SWALI: Biblia inaposema ‘Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa’. Je tuna mamlaka ya kufanya hivyo wakati wote?

Yohana 20:22 Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu. 23 Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa.


JIBU: Mstari huu ukitafsirika vibaya unaweza kuleta maana isiyosahihi ikidhaniwa kuwa kwa uweza wetu, tunaweza kuwaondolea watu dhambi, na kuwafungia pale tutakapo. Hapana.

Biblia inatuambia mwenye uweza wa kusamehe dhambi kwa namna hiyo ni Bwana Yesu tu.

Luka 5:21 Basi, wale waandishi na Mafarisayo wakaanza kuhojiana wakisema, Ni nani huyu asemaye maneno ya kukufuru? N’nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?

22 Na Yesu alijua hoja zao, akajibu akawaambia, Mnahojiana nini mioyoni mwenu? 23 Lililo jepesi ni lipi? Kusema, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, uende? 24 Lakini, mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (alimwambia yule mwenye kupooza). Nakuambia, Ondoka, ujitwike kitanda chako, ukaende zako nyumbani kwako.

Lakini kwanini Bwana Yesu atoe mamlaka yake Kwa mitume wake?

Ni kufuatana na ahadi aliyowaahidia ndani yao, ambayo ni Roho Mtakatifu tunayoisoma katika huo mstari wa 22. “Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu”.

Kazi ya Roho Mtakatifu ni kumshuhudia Kristo. Hivyo mitume walipewa ushuhuda wa Kristo ndani yao (ndio Injili). Na kwa kupitia hiyo, mamlaka ya kufunga na kufungua wanakuwa nayo, ndani ya hiyo hiyo injili.

Hivyo walipokwenda kuhubiri, na watu wakaamini. Walipotamka kusamehewa dhambi zao, basi wale watu walisamehewa. Vilevile walipokwenda kuhubiri, kisha injili yao ikapingwa, wakakatishwa tamaa na kuacha kuhubiri hapo, mpaka wakafikia hatua ya kuwakung’utia mavumbi yao, Basi hiyo nyumba au huo mji rohoni umefungiwa dhambi. Hauwezi kuokoka kwa namna nyingine yoyote, mpaka watakapokuwa tayari kugeukia injili ya wale waliopelekwa.

Mathayo 10:13 Na nyumba ile ikistahili, amani yenu na iifikilie; la, kwamba haistahili, amani yenu na iwarudie ninyi.

14 Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, kung’uteni mavumbi ya miguuni mwenu.

15 Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule.

Hiyo ndio namna ambayo watu wa Mungu, huondoa dhambi na kufungia dhambi wanadamu.

Mamlaka hii pia Yesu ameiweka katika kanisa.

Kwasababu kanisa pia ni mwili wake, Hivyo ikiwa yupo mwamini mmoja ambaye alitenda dhambi, akakutwa na mabaya, basi kanisa linaweza kumwombea, akasamehewa dhambi (Yakobo 5:14).

Lakini pia ikiwa yupo ambaye ni mwasi, ameiacha njia, anapoonywa mara kadhaa kisha harejei kwenye mstari, ndugu anapomwacha au kanisa linapomtenga moja kwa moja, basi Mungu naye anamhesabu kama mtu wa mataifa asiyeamini.(Mathayo 18: 15-18,)

Hivyo ni vema kufahamu, mamlaka hii ipo, kwenye injili ya Kristo, lakini pia ipo ndani ya kanisa. Kila mmoja anapaswa amtii Kristo kupitia watumishi wake. Kwasababu lolote walitendalo si wao bali ni Roho Mtakatifu ndani yao, aliyewavuvia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya andiko hili  “Sauti yake hamkuisikia wakati wo wote, wala sura yake hamkuiona.(Yohana 5:37)”

MAOMBI KWA WENYE MAMLAKA.

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

Rudi Nyumbani

Print this post

Maana ya Mithali 10:1 Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;

SWALI: Naomba kuelewa tafsiri halisi ya maneno tuyasomayo kwenye Mithali 10:1.

Mithali 10:1

[1]Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.


JIBU: Mpumbavu kibiblia ni mtu yeyote aliyemkosa Mungu ndani yake, ambaye kwa njia hiyo anaweza kuonyesha tabia yoyote mbaya, aidha wizi, au kiburi, au umalaya, au uchawi, au hasira, mwingine atakuwa mlevi, mtukanaji, mwongo, jambazi, mchoyo, mbinafsi, mkorofi n.k.

Chimbuko ni kumkosa Mungu ndani yako.

Sasa mwana wa namna hii kibiblia sio tu anaiathiri roho yake lakini pia hata waliomzaa.

Mithali 10:1

[1]Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.

Lakini kauli hiyo inapaswa eleweke vizuri, sio kwamba mwana akiwa na hekima ni furaha ‘tu’ kwa baba, mama hausiki, au akiwa mpumbavu ni mzigo tu kwa mama baba hausiki.

Hapana, mambo hayo yanawapata wote.. akiwa na hekima wote hufurahi, vilevile akiwa mpumbavu wote huhuzunika.. Ndio maana sehemu nyingine anasema..

Mithali 17:25

[25]Mwana mpumbavu ni huzuni kwa babaye, Na uchungu kwa mamaye aliyemzaa.

Wazazi wote hufurahishwa au huhuzunishwa kwa tabia husika za watoto wao.

Lakini alipoonyesha kama kuwatenganisha, ni kuelezea ‘hisia za juu zaidi’ zitokeazo kulingana na mzazi na mzazi.

Kimsingi mtoto akiwa na hekima, baba huwa anajivunia sana mtoto huyo, utaona baba anajigamba kwa ajili ya mwanae..Mfano tu wa Sulemani kwa Daudi, hekima yake ilikuwa ni fahari ya babaye Daudi.

Lakini akiwa ni mpumbavu, tengeneza picha mtoto ni teja, na kibaka, na mlevi, kiuhalisia utaona akina mama ndio wanateseka zaidi na kuumia juu ya watoto wao. Wanapatwa na mzigo mzito sana moyoni. Na hiyo huwa inawasukuma kuzunguka huku na huko kutafuta msaada. Tofauti na wababa, watamwonya, mara ya kwanza, mara ya pili, mara ya tatu wakiona haonyeshi geuko lolote, ni rahisi kuachana nao.

Ni nini tunaonyeshwa rohoni?

Si mwilini tu. Rohoni Kristo anafananishwa na Baba, na Kanisa lake ni Mama.

Wote sisi ni watoto ambao Kristo ametuzaa ndani ya kanisa lake, tuwapo na hekima (tunamcha), tunatembea katika misingi ya Neno lake, kwa kuzingatia viwango vya upendo na utakatifu, tujue kuwa Kristo hutukuzwa na hujivunia sana sisi. Lakini tuwapo wapumbavu, tunajiumiza zaidi sisi wenyewe. Kwamfano sababu mojawapo ipelekeayo makanisa kupoteza furaha na amani,  ni kukosekana umoja na upendo.

Bwana atusaidie.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.

MJUE SANA YESU KRISTO.

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

Rudi Nyumbani

Print this post

USIKOSE MAZIKO (Mhubiri 6:3)

SWALI: Naomba kufahamu nini maaana ya mhubiri 6:3?

Mhubiri 6:3

[3]Mtu akizaa watoto mia, akaishi miaka mingi, nazo siku za maisha yake ni nyingi, lakini nafsi yake haikushiba mema; tena ikiwa, zaidi ya hayo, amekosa maziko; mimi nasema, Heri mimba iliyoharibika kuliko huyo;


JIBU: Mhubiri katika jicho la kibinadamu anaelezea jinsi inavyoonekana kama ni hasara kubwa sana, kwa mtu ambaye amejitaabisha maisha yake yote, kutengeneza heshima, kwanza kwa kuwa na watoto wengi, lakini pia kwa kujinyima raha, kuwekeza vema vitu vyake ili siku za kufa iwe heshima kubwa kwake, hata baada ya hapo aache jina kwa uzao wake wote.

Lakini mambo yanatokea kinyume chake, anakufa kama mtu asiye na kitu, au kwa aibu,  hata baada ya hapo anasahaulika kabisa ijapokuwa aliwekeza muda wake mwingi kujijengea jina.. Sasa mhubiri anasema ni heri mimba iliyoharibika kuliko huyu kwasababu kimsingi mimba huwa inasahaulika kweli muda mfupi,na haiwi na maziko ya watu, lakini haijatabika kwa lolote, kuliko huyu ambaye ametabika sana maisha yake yote, kuacha kumbukumbuku , halafu amesahaulika mfano ule ule wa kama mimba iliyoharibika.

Mfano wa watu kama hawa alikuwa ni Ahabu, ambaye alikuwa na watoto sabini, na ufalme mkubwa lakini alikufa kwa aibu, damu yake ililambwa na mbwa. Pamoja na mkewe Yezebeli ambaye mzoga wake uliliwa kabisa na mbwa, hakuwa na maziko. Ikawa ni fedheha kubwa sana kwao (1Wafalme 22),

Lakini maana hasaa ya huo mstari rohoni ni ipi?

Maziko halisi ni yale ya Mungu. Kukosa maziko ya kibinadamu, hakuwezi kukufanya udharauliwe milele. Lakini ukikosa maziko ya Mungu ni aibu na kudharaliwa milele.

Ukipata fedha zote duniani, ukazaa watoto wengi ambao watalirithi jina lako, ukawa mtu maarufu, mpaka ukawa mfalme wa nchi, jina lako likakumbukwa hata vizazi elfu baadaye, kama hujafa ndani ya Kristo. Ni heri mimba iliyoharibika kuliko wewe. Huna kumbukumbu lolote mbinguni

Mwamini Kristo leo, akuoshe dhambi zako. Jiulize ukifa leo katika dhambi, huko uendako utakuwa mgeni wa nani? Wokovu ni sasa, saa iliyokubaliwa ni leo. Fungua moyo wako mpokee Yesu, hata kufa kwako kuwe kuna thamani.

Zaburi 116:15

[15]Ina thamani machoni pa BWANA Mauti ya wacha Mungu wake.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Maana ya Mhubiri 1:9 “wala jambo jipya hakuna chini ya jua”. 

Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)

Nini maana ya mhubiri 9:11? si wenye mbio washindao katika michezo?

Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?

Rudi Nyumbani

Print this post

Ni vitu vipi hivyo tumekirimiwa vitupasavyo uzima na utauwa? (2Petro 1:3)

SWALI: Ni vitu vipi hivyo tumekirimiwa vitupasavyo uzima na utauwa? (2Petro 1:3)

2 Petro 1:3

[3]Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia “vitu vyote” vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.


JIBU: Andiko hilo linatufundisha kuwa Mungu anao uweza wake, ambao una nguvu ya kumfanya mtu kuwa kama anavyotaka. Sasa hapo tunafunuliwa kuwa uweza huo ameuachilia katika maeneo mawili makuu la kwanza ni UZIMA la pili UTAUWA. Uzima ni maisha ya milele, na utauwa ni utakatifu.

Sasa swali linauliza ni vitu gani hivyo ambavyo Mungu ametukirimia vinavyozungumziwa hapo vitufanyavyo  kuufikia huo uzima na utauwa, anaousema?

Vitu vyenyewe ni kama vifuatavyo

1) Mwana wake (Yesu).

Bila Yesu Kristo kuja duniani, kuwa fidia ya dhambi zetu kwa kifo chake, tusingeweza kupokea uzima wa milele. Kwasababu ilihitajika kumwagika kwa damu isiyokuwa na dhambi ili kutuondolea sisi dhambi zetu tupokee uzima wa milele. Hivyo uweza huu wa uungu, umetukirima Yesu Kristo, kutuondolea dhambi ndani yetu.

Tuna kila sababu za kumshukuru Mungu sikuzote, kwa huruma zake hizi. Tunaye mkombozi ambaye kila amwaminiye tu. Uzima anao. (Yohana 3:16)

2) Roho Mtakatifu.

Roho wa Mungu ni msaidizi wetu, bila yeye, ni kweli tungesamehewa dhambi lakini tusingeweza kuwa watakatifu. Hivyo yeye anapokuja juu yetu na kujaa vizuri tunajikuta tunaweza enenda katika mwenendo wa utakatifu. Hivyo huu ni uweza wa Mungu mwenyewe.

Yohana 14:16

[16]Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;

Wagalatia 5:16

[16]Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

3) Biblia.

Hichi ni kitu kingine ambacho Mungu ametukirimia kwa uweza wake, kwa kuisoma tunatambua wazo lote la Mungu, na hivyo kuturahisishia kuisikia sauti ya Mungu. Tusomapo biblia tunabadilishwa tabia zetu, kwa maonyo, mafundisho, faraja, shuhuda n.k.

2 Timotheo 3:16

[16]Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

4) Kanisa.

Kanisa ni uweza wa Mungu kwetu, hekima ya Mungu ambayo aliibuni yeye mwenyewe siku ile ya pentekoste. Kuwakusanya watakatifu wake na kuwahudumia kwa karama mbalimbali. Kanisa humlinda mwamini, kanisa humwombea mwamini, humsaidia mwamini, humfariji mwamini na kumwongoza.

Sikuzote  Uthabiti wa mwamini hutegemea kanisa. Mtu asiye na kanisa (ushirika), ameukana uweza huu wa Mungu, ambao Mungu huutumia kutukamilisha sisi.(Waebrania 10:25)

1 Wakorintho 12:27-28

[27]Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.

[28]Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha.

5) Malaika

Bwana huwatuma malaika wake, kumlinda mwamini asijikwae. Huu ni uweza wa Mungu pia.

Waebrania 1:14

[14]Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?

Zaburi 91:11-12

[11] Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote. [12] Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

Kama si Mungu kutuagizia malaika zake, bila shaka adui angepata penyo nyingi sana za kutuletea majaribu na kutuangusha. Ukiwa ndani ya Kristo adui hana nguvu juu yako, kwasababu unalindwa na jeshi lake. Unapiganiwa kwa namna usiyojua wewe.

Na hivyo kuishi maisha ya utauwa kwako inakuwa ni vyepesi zaidi ya mtu mwingine yeyote aliye nje.

Swali ni je umepokea vitu hivi vyote?

Ukipungukiwa kimoja wapo, ni lazima tu eneo lako la utauwa  au uzima litakuwa na kasoro. Kumbuka Bwana ameshatukirimia ni sisi tu kukubali na kupokea.

Wokovu upo bure, biblia ipo wakaki wote, Roho yupo, kanisani lipo, malaika wapo. Amini tu na  kutubu dhambi zako, kwa Kumaanisha kabisa kugeuka na kumfuata Yesu, akupaye ondoleo la dhambi. Kisha ukabatizwe, upokee Roho. Na baada ya hapo, shiriki sasa vitu hivyo vya ki-ungu kwasababu vimewekwa tayari kwa ajili yako na mimi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Rudi Nyumbani

Print this post

Je! Paulo, alikuwa na injili yake tofauti na wengine?(Warumi 2:16)

SWALI: Je! Paulo, alikuwa na injili yake, tofauti na wengine?  sawasawa na (Warumi 2:16)

Warumi 2:16 katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu.


JIBU: Katika habari hiyo mtume Paulo hakumaanisha kwamba anayo injili nyingine ya kipekee tofauti na mitume wengine wa Kristo, na kwamba ya kwake tu  ndiyo Mungu atakayoitumia kuzihukumu siri za wanadamu.

Hapana mitume wote walikabidhiwa “injili moja”. Nayo ni kushuhudia wokovu ulioletwa duniani na mtu mmoja tu, ambaye ni YESU KRISTO, kwa lile tendo la kufa na kukufuka kwake kama fidia ya dhambi za ulimwengu, ambapo mtu akiamini basi amepokea ondoleo la dhambi na uzima wa milele. Na mtu yeyote ambaye hatamwamini huyu basi hukumu ya Mungu inakuwa juu yake.

Kwahiyo Paulo kama mmoja wa hao waliokabidhiwa injili hiyo, alikuwa na ujasiri kuwaeleza watu wale wa Rumi, kwamba kupitia injili yake hiyo sahihi, Mungu atawahukumu wanadamu, kwasababu anayehubiriwa ni Yesu Kristo. Ni sawa tu na Petro, au Yohana, au Yakobo, wangesema maneno kama hayo, wasingewezeka kupingana na Paulo kwasababu wanachokishuhudia wote ni kitu kimoja. Ndio maana tunaona maneno ya mitume wote, yameunganishwa katika kitabu kimoja kinachoitwa BIBLIA.

Lakini kwa nini Paulo aliongeze Neno hilo “sawasawa na injili yangu” Na asingeishia kwenye injili tu?.

Ni kwasababu wakati ule kulikuwa na watu waliomhubiri Yesu mwingine na injili nyingine, tofauti na ile waliyoihubiri mitume wa kweli.  Na hawa watu, wengi wao walikuwa ni  wayahudi wa tohara, Hivyo ilimbidi aliweke wazi hilo ili watu wabakie kwenye injili sahihi ya kweli.

Injili hizo Paulo aliziona kwenye makanisa kadha wa kadha kama tunavyosoma katika vifungu hivi;

2Wakorintho 11:4 Maana yeye ajaye akihubiri Yesu mwingine ambaye sisi hatukumhubiri, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye!

Na..

Wagalatia 1:6 Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na

kugeukia injili ya namna nyingine. 7 Wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo.

Umeona, hiyo ndio sababu ya Paulo na kule Rumi kuitamka kauli hiyo, “sawasawa na injili yangu”. Ili kuwapa ufahamu kuwa hizo nyingine wanazozisikia huko nje, hazina uhai wowote wa kumwokoa mtu, au kumtetea siku ile ya hukumu.

Hata sasa, mambo ni yale yale, kumekuwa na madhehebu mengi, imani nyingi, ambazo zote zinadai ni za kikristo, lakini ukiangalia uhalisia wake humwoni Kristo ndani yake, wala injili ya Kristo. Fundisho lililo mule ndani sio fundisho la mitume. Watu hawahubiriwi  tena toba ya kweli na kumwangalia Kristo kama kiini cha wokovu wao. Wanafundishwa mambo mengine kabisa wengine mafanikio, wengine  uchawi, wengine  miujiza n.k kama ndio utimilifu wa ukristo. Sasa mambo kama hayo, hayaweza kumtetea mtu siku ya hukumu.

Bali injili ya Yesu Kristo, kupitia mitume wake. Ambayo ni hii biblia tuliyonayo, ndio tunayopaswa tuiegemee, kwasababu katika hiyo ndio tutakayohukumiwa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

je! Paulo aliwalaani Wagalatia na Wakorintho?

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo? (Matendo 11:23)

SWALI:  Mitume walikuwa na maana gani kuwasihi wanafunzi kule Antiokia, waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo? Ni maana ya hiyo kauli?

Matendo 11:22 Habari hizo za watu hao zikafika masikioni mwa kanisa lililokuwako katika Yerusalemu; wakamtuma Barnaba, aende hata Antiokia.

23 Naye, alipokwisha kufika na kuiona neema ya Mungu akafurahi, akawasihi wote waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo.

24 Maana alikuwa mtu mwema amejaa Roho Mtakatifu na imani; watu wengi wakaongezeka upande wa Bwana.

JIBU: Kauli hiyo inamaanisha kwa “kusudi sahihi la moyo” sawasawa na imani waliyoipokea, Kwasababu Mitume walijua madhumuni ya wao kumfuata Yesu yakiwa sio sahihi, kusimama kwao kunaweza kusidumu. Kwasababu walijua wapo wanaomfuata Kristo kwa sababu ya fitna, wengine fedha, wengine watu, wengine vyeo, wengine kuajiriwa n.k.. Na hiyo haipaswi. Kwasababu Mungu huuchunguza kwanza moyo wako kilichokupelekea  kumfuata ni nini?. Ikiwa sio kwa lile kusudi lake sahihi, hauwezi kusimama.

Sifa hizo za Mungu kuchunguza makusudi ya moyo tunazisoma kwenye vifungu hivi;

Waebrania 4:12 Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukataokuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.

Hivyo hata sasa, Mungu anataka tuipokee imani kwa kusudi la kweli la moyo, ili tuweze kudumu, na kuona utendaji kazi wake bora, katika maisha yetu ya rohoni, na pia tuweze kusimama hadi mwisho .

Kusudi sahihi la moyo ni kumfuata Yesu ili akuokoe dhambini, kumtazama Kristo kama dhabihu kamilifu ya Mungu iliyotolewa kwa ajili ya kuondoa dhambi zetu, na sio atupe utajiri, au atuponye magonjwa, au atupe mke/mume.

Kwanini  iwe hivyo?

Kwasababu hayo yasipokuja kwa wakati  utamwacha Kristo, au yakipatikana basi Kristo hawezi kuwa tena na thamani moyoni mwako, kwasababu kusudi lako moyoni lilikuwa utatuliwe tu changamoto yako, si zaidi. Na ndio maana ni rahisi leo kuona watu wengi makanisani, lakini wasiwe wote wameokoka.

Mitume waliliona hili kama ni jambo muhimu sana kufundishwa mwanzoni kabisa mwa imani kwa waongofu wapya. Vivyo hivyo na sisi tuige fundisho hilo pindi tunapowajenga waongofu wapya.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUNA NGUVU YA ZIADA KATIKA KULING’ANG’ANIA KUSUDI LA MUNGU.

NAAM, HATA WABAYA KWA SIKU YA UBAYA. 

Nini tofauti ya Majira na Wakati?

Rudi Nyumbani

Print this post

Silwano  ni nani,kama tunavyomsoma kwenye biblia?(1Petro 5:12)

Silwano ni matamshi mengine ya jina la Sila. Kwa kiyunani ni Sila, lakini kwa kilatino ni silwano. Hivyo Silwano ndio Sila yule tunayemsoma kwenye maandiko.

Habari ya Silwano/Sila hasaa tunaipata katika kitabu cha matendo ya mitume, huyu ni mmoja wa manabii wawili walioteuliwa na wazee wa kanisa la Yerusalemu kuambatana na Paulo na Barnaba katika kupeleka waraka wa makubaliano kwa makanisa ya mataifa.(Matendo 15:22).

Tunaona Sila na Yuda walipofika Antiokia, na kumaliza huduma yao, Yuda alirejea Yerusalemu, lakini Sila aliamua kuungana na Paulo katika ziara zake za kupeleka injili kwa mataifa.

Tunafahamu nini kuhusu Silwano/sila?

> Sila alipigwa na kufungwa pamoja na Paulo kule Filipi (Matendo 16:19-25).

> Sila anatajwa kama mwandishi mwenza wa kitabu cha Wathesalonike pamoja na Paulo(1&2 Wathesalonike 1:1).

 “Paulo, na Silwano, na Timotheo, kwa kanisa la Wathesalonike, lililo katika Mungu Baba, na

katika Bwana Yesu Kristo. Neema na iwe kwenu na amani.”

> Sila alihudumu Beroya.

Matendo ya Mitume 17:10

[10]Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi.

> Alihudumu pia   Makedonia,  na Korintho pamoja na Paulo na wakati mwingine Timotheo (Matendo 15-18)

> Silwano anatajwa kama mjumbe wa mtume Petro, kama mwandishi wa ile barua yake ya kwanza,

> Lakini pia anatajwa kama mtu mwaminifu.

1 Petro 5:12

[12]Kwa mkono wa Silwano, ndugu mwaminifu kama nionavyo, nimewaandikia kwa maneno machache, kuonya na kushuhudia ya kuwa hii ndiyo neema ya kweli ya Mungu. Simameni imara katika hiyo.

Tunajifunza nini kwa Sila?

Uaminifu  aliokuwa nao ambao ulionekana na kutajwa mpaka kwa mitume, ni uaminifu wa kuwa tayari kujitoa maisha yake kwa ajili ya kuitetea injili bila kujali gharama yoyote.

Sila tunamfananisha na Ruthu, ambaye alipoambiwa arejee nyumbani kwake akakataa , akajilazimisha kwenda na Naomi katika hali ya ajane, katika nchi ya ugenini.

Ndivyo ilivyokuwa kwa Sila alikuwa na uwezo wa kurudi Yerusalemu pamoja na Yuda, kuhudumu kule lakini akakubali kwenda kwenda katika dhiki na Paulo mataifani. Lakini taabu yake haikuwa bure, bali kazi yake inatambulika mpaka leo.

Sila amekuwa kama kiungo wa kanisa la kwanza pamoja na mitume , tangu wazee wa kanisa Yerusalemu, mpaka Petro hadi Paulo anaonekana akihudumu nao tofauti na washirika wengine wa mitume, walikuwa wakiambatana na mtume Fulani maalumu, mfano tukimwona Timotheo hatuoni popote akihudumu pamoja na Petro, lakini Sila alikuwa kiungo kotekote.

Bwana atupe moyo kama wa Sila. Tupelekwapo, tunajitoa kikamilifu kabisa kwa kufanya zaidi ya tunavyoagizwa..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?

ORODHA YA MITUME.

Mwandishi wa kitabu cha Matendo ya mitume.

Rudi Nyumbani

Print this post