Swali: Neno la Mungu linasema Katika Yohana 3:18 na 36 ..amwaminiye mwana anao uzima wa milele, asiyemwamini hana uzima? .. Je kuna haja ya kutafuta jambo lingine tena baada ya kumwamini Bwana YESU?.
Jibu: Yapo maandiko katika biblia yanayokamilishwa na maandiko mengine, yako maandiko ambayo hayahitaji kukamilishwa na mengine kwani yanakuwa yamejitosheleza lakini yapo ambayo yanaelezwa kwa ufupi hivyo ni lazima yakamilishwe na maandiko mengine…
kwamfano andiko hilo la Yohana 3:18 na 36 ni kweli maandiko yanatuonyesha kuwa “tukimwamini Bwana YESU hatutahukumiwa bali tutapata uzima wa milele”.
Yohana 3:18 “AMWAMINIYE YEYE HAHUKUMIWI; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu…..
36 Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia.
Lakini tukirejea Marko 16:16 tunaona kuna jambo lingine linaongezeka..
Marko 16:16 “Aaminiye na KUBATIZWA ATAOKOKA; asiyeamini, atahukumiwa”.
Hapa kinachoongezeka ni “UBATIZO” Kwamba mtu akiamini pasipo kubatizwa bado hataurithi uzima wa milele, (ikiwa amesikia habari za ubatizo na hajataka kubatizwa).
Na ubatizo unaozungumziwa hapo sio ule wa MAJI TU, bali hata ule wa ROHO MTAKATIFU soma Luka 3:16.
Ili tuzidi kuelewe vizuri lugha hii, hebu tafakari kauli hizi mbili… “Ukipanda maharage utavuna maharage”… na kauli ya pili “Ukipanda maharage na kuyamwagilia maji utavuna maharage”.. Je kwa ni kauli ipi ipo sahihi kuliko nyingine?.. Ni wazi kuwa kauli zote zipo sahihi, isipokuwa ya pili imefafanua vizuri.. na inayofaa Zaidi ni hiyo ya pili, kwasababu ndio imekamilisha kauli ya kwanza.
Vivyo hivyo Neno linasema katika Yohana 3:18 kuwa amwaminiye YESU hatahukumiwa, lakini Marko 16:16, inakamilisha vizuri Zaidi kwamba Amwaminiye YESU na kubatizwa hatahukumiwa..Kwahiyo ya pili ni ya nzito Zaidi kwasababu imeikamilisha ile ya kwanza.
Sasa kwanini Imani pekee yake haitoshi ni lazima kubatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu??
Jibu: Kwasababu hata Mashetani yanaamini lakini bado hayana wokovu..
Yakobo 2:19 “Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda VEMA MASHETANI NAO WAAMINI NA KUTETEMEKA.
20 Lakini wataka kujua, wewe mwanadamu usiye kitu, kwamba imani pasipo matendo haizai”
Kwa hitimisho ni kwamba “IMANI YA KUMWAMINI BWANA YEESU ni LAZIMA IENDE NA MATENDO”.. Na tendo la kwanza ni hatua ya ubatizo wa Maji na nyingine ni ya Roho Mtakatifu.
Mtu anapomwamini Bwana YESU na kubatizwa kwa maji na kwa Roho anakuwa amekamilika, na kukidhi vigezo vya kuuona ufalme wa Mungu, kwani maana pia ya kuzaliwa mara ya pili ni kuzaliwa kwa maji na kwa ROHO.
Yohana 3:4 “Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?
5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, MTU ASIPOZALIWA KWA MAJI NA KWA ROHO, HAWEZI KUUINGIA UFALME WA MUNGU.
6 KILICHOZALIWA KWA MWILI NI MWILI; NA KILICHOZALIWA KWA ROHO NI ROHO.
7 Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?
TUMEPEWA, SI KUMWAMINI TU KRISTO, ILA NA KUTESWA KWA AJILI YAKE;
Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, alimaanisha hakuwa na wengine?
Msalaba ni kipande cha mti, kilichochongwa kwa kupishanishwa na kingine kwa juu. chenye lengo la kumuulia mwanadamu kwa kifo cha mateso.
Tofauti na sasa, ambapo adhabu nyingi za kifo kwa mataifa mbalimbali huwa ni kunyongwa, au kupigwa risasi, au kuwekwa kwenye kiti cha umeme, n.k.. Lakini katika falme za zamani watu waovu kupita kiasi, kwamfano wauaji, au wenye makosa ya uhaini, adhabu yao, ilikuwa ni kutundikwa au kugongelewa pale msalabani mpaka ufe. Ni mateso ambayo utataabika hapo kwa saa nyingi sana kabla ya kufa, hata siku mbili.
Hivyo kwa lugha rahisi tunaweza kusema msalaba ni chombo cha kuulia mtu.
Kwetu sisi tuliomwamini Kristo. Msalaba ni ishara kuu ya ukombozi tulioupata kwa kifo cha mwokozi wetu. Kufahamu kwa undani ni kwanini fungua link hizi; usome..
AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.
Nini maana ya sulubu/ sulubisha?
nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?
Je! msalaba kaburini una umuhimu wowote?
Isaya 34:11 “KAATI na NUNGU wataimiliki, bundi na kunguru watakaa huko, naye atanyosha juu yake kamba ya ukiwa na timazi ya utupu”.
Jibu: “Kaati” ni “bundi wa jangwani” (wanaoishi majangwani), na chakula chao ni jamii za panya na wadudu..Tazama picha chini.
“Nungu” ni aina nyingine ya bundi wanaopatikana katika misitu yenye miti iliyozeeka, yenye matundu. Aina hii ya bundi hutoa mlio mkali wakati wa usiku wanapowasiliana na jamii zao, na ndio wanaosikika katikati ya jamii za watu (Tazama picha na video chini).
Lakini swali ni je? Bundi hawa (Kaati na Nungu) ni roho za kichawi/majini?.
Jibu ni la!.. Bundi ni ndege tu kama ndege wengine walioumbwa na Bwana MUNGU, kama wakiwa katika mazingira yao ya asili, ni ndege tu kama ndege wengine, wanaohitaji pia kutunzwa.
Lakini pia ndege hawa wanaweza kutumika na wachawi katika shughuli za kichawi, kama tu vile kuku anavyoweza kutumiwa katika kafara za kichawi, na bundi ni hivyo hivyo, ila kwa mtu aliyeokoka hakuna silaha yoyote yenye uhai, au isiyo na uhai itampata.
Lakini kwa mtu aliye nje ya KRISTO, basi ni haki yake kuogopa bundi, na viumbe wengine kwani ni kweli yupo hatarini kudhuriwa na ibilisi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nimekuwa kama mwari nyuni wa jangwani,
IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.
Je! Ni dhambi kumpiga au kumuua mnyama bila sababu yoyote?
Mjombakaka ni nani kwenye maandiko? (Walawi 11:29)
Jibu: Tuirejee.
Isaya 62:4 “ Hutaitwa tena ALIYEACHWA, wala nchi yako haitaitwa tena, UKIWA; bali utaitwa HEFSIBA; na nchi yako BEULA; kwa kuwa Bwana anakufurahia, na nchi yako itaolewa.
5 Maana kama vile kijana amwoavyo mwanamwali, ndivyo wana wako watakavyokuoa wewe; na kama vile bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi, ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.
6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha Bwana, msiwe na kimya;
7 wala msimwache akae kimya, mpaka atakapoufanya imara Yerusalemu, na kuufanya kuwa sifa duniani”
Hii ni habari ya tumaini la kuinuliwa tena kwa Yerusalemu na Israeli kwa ujumla, Kwamba siku ile watakapomrudia Bwana kwa mioyo yao yote basi nchi yao hiyo Bwana aliyoikataa na kuiacha na kuifanya UKIWA, basi ataibarikia tena na kuifanya kuwa FURAHA yake na ILIYOOLEWA.
Sasa tafsiri ya Hefsiba na Beula tayari imeshatolewa pale.. Hefsiba/Hefziba maana yake ni “Furaha yangu iko kwake” na Beula maana yake ni “Aliyeolewa”.. Haya ni maneno ya kiebrania yenye tafsiri hiyo. Hali kadhalika tafsiri ya “Aliyeachwa” kiebrania ni “Abuba” na “Ukiwa” ni “Shemama”..
Kwahiyo kinyume cha aliyeachwa (Abuba) ni Hefsiba (furaha yangu iko kwake)…. Na kinyume cha shemama(ukiwa) ni aliyeolewa(Beula). Ni majina ya kiebrania yaliyotumika kwa jinsia ya kike (soma 2Wafalme 21:1)
Sasa swali kwanini Mungu atumie lugha hizo za “ndoa” kuzungumza na watu wake?.
Ni kwasababu watu wa Mungu wote kiroho wanafananishwa na “mwanamke aliyeolewa/bibi arusi”
Isaya 54:4 “Usiogope; maana hutatahayarika; wala usifadhaike; maana hutaaibishwa; kwa kuwa utaisahau aibu ya ujana wako, pia mashutumu ya ujane wako hutayakumbuka tena.
5 KWA SABABU MUUMBA WAKO NI MUME WAKO; Bwana wa majeshi ndilo jina lake; na Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako; Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote.
6 Maana Bwana amekuita KAMA MKE ALIYEACHWA na kuhuzunishwa rohoni, kama mke wakati wa ujana, atupwapo, asema Mungu wako.
7 Kwa kitambo kidogo nimekuacha; lakini kwa rehema nyingi nitakukusanya”.
Soma pia Yeremia 31:31-32, 2Wakorintho 11:2 na Ufunuo 21:9 utazidi kuliona jambo hilo..
Kwahiyo ujumbe huo haukuwa kwa Israeli peke yao, bali pia unatuhusu sisi, kwamba tumrudiapo Mungu wetu kwa mioyo yetu yote, basi tunazo ahadi za Baraka na mafanikio, na majina yetu kiroho yatabadilika na kuwa Hefsiba na Beula…Na furaha ya Bwana itakuwa juu yetu nasi tutakuwa na muunganiko wa kiroho na Bwana YESU.
Isaya 62:1 “Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, na kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia, hata haki yake itakapotokea kama mwangaza, na wokovu wake kama taa iwakayo.
2 Na mataifa wataiona haki yako, na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha Bwana.
3 Nawe utakuwa taji ya uzuri katika mkono wa Bwana, na kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako.
4 Hutaitwa tena ALIYEACHWA, wala nchi yako haitaitwa tena, UKIWA; bali utaitwa HEFSIBA; na nchi yako BEULA; kwa kuwa Bwana anakufurahia, na nchi yako itaolewa.
5 Maana kama vile kijana amwoavyo mwanamwali, ndivyo wana wako watakavyokuoa wewe; na kama vile bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi, ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.
6 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha Bwana, msiwe na kimya;
7 wala msimwache akae kimya, mpaka atakapoufanya imara Yerusalemu, na kuufanya kuwa sifa duniani”
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Uasherati wa Kiroho maana yake nini?
HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.
Ni kweli Paulo alipuuzia maonyo aliyopewa ya kwenda Yerusalemu?
Swali: Je kwanini Bwana YESU aseme Yuda ni shetani, na kwanini amchague shetani kama mwanafunzi wake?
Jibu: Turejee..
Yohana 6:70 “Yesu akawajibu, Je! Mimi sikuwachagua ninyi Thenashara, NA MMOJA WENU NI SHETANI?
71 Alimnena Yuda, mwana wa Simoni Iskariote; maana huyo ndiye atakayemsaliti; naye ni mmojawapo wa wale Thenashara”.
Swali hili linafanana na lile la kwanini Bwana YESU amwite Herode “MBWEHA”.
Luka 13:31 “Saa ile ile Mafarisayo kadha wa kadha walimwendea, wakamwambia, Toka hapa, uende mahali pengine, kwa sababu Herode anataka kukuua.
32 Akawaambia, Nendeni, mkamwambie yule mbweha, Tazama, leo na kesho natoa pepo na kuponya wagonjwa, siku ya tatu nakamilika”.
Sasa kiuhalisia Herode sio “Mbweha”, wala Yuda siye “shetani”…Isipokuwa watu hao ndani yao wamebeba tabia za “Mbweha” na “shetani”.. Ni sawa na Bwana YESU anavyojulikana kama Mwanakondoo…haimaanishi Bwana YESU ni kondoo (mnyama), La!, isipokuwa ndani yake (katika roho) ipo tabia ifananayo na ya kondoo yaani ya “unyenyekevu”.
Hali kadhalika Yuda si “shetani” bali ndani yake kulikuwa na roho ya shetani ya usaliti na mauaji.
Luka 22:3 “SHETANI AKAMWINGIA YUDA, AITWAYE ISKARIOTE, naye ni mmoja wa wale Thenashara.
4 Akaondoka, akaenda akasema na wakuu wa makuhani na majemadari, jinsi atakavyoweza kumtia mikononi mwao”.
Hivyo Bwana YESU alikuwa anamaanisha roho iliyokuwemo ndani ya Yuda na si utambulisho wa YUDA, utaona pia kuna wakati alimwambia Petro kuwa ni shetani..
Mathayo 16:22 “Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata. 23 Akageuka, akamwambia Petro, NENDA NYUMA YANGU, SHETANI; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu”.
Hapa Bwana hakuwa anaongea na Petro, wala hakuwa anamkemea Petro, bali ile roho iliyokuwa ndani ya Petro (yaani ya ibilisi) ndio aliyokuwa anaikemea.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Bwana YESU hakumchagua shetani, wala Yuda hakuwa shetani bali alikuwa na roho ya shetani ndani yake.
Na hata leo kuna watu ambao ni “mashetani” katika muktadha huo, kwamba ndani yao kuna roho ya shetani.. Hivyo hatuna budi kila siku kujipambanua na kujipima na kujitakasa, ili tusiwe tusionekane kama mashetani.. na utakaso mkuu ni ule Bwana aliowaambia baadae wanafunzi wake, baada ya kumkemea Petro.
Mathayo 16:23 “Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.
24 Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.
25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona”.
Hapo baada ya maneno hayo kwa Petro, Bwana anaanza kusema “…Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake..”
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je Yuda alienda wapi, ni mbinguni au jehanamu?
Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?
ZIFAHAMU KAZI KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.
Kibiblia Neno laana linatafsiri kwa namna mbili.
Namna ya kwanza, ni Kupoteza sifa ya kukubaliwa na Mungu kwa jambo lolote lile. Na hii chanzo chake ni lile anguko la mwanadamu tangu mwanzo.
Namna ya pili, ni apizo alitoalo mtu kwa mwenzake au alitoalo Mungu mwenyewe, kwa mwanadamu ili wafikiwe na ubaya fulani, au wakasifikiwe na Mema waliyokusudiwa.
LAANA YA KWANZA:
Sasa laana hii ya kwanza, inazalika kwasababu ya asili yetu, ambayo ilionekana tangu Adamu, kuhasi maagizo ya Mungu, ambayo hata sisi sote tuliopo leo, asili hiyo ipo ndani yetu. Ni sawa na unavyomwona mdudu kama mende, ukimtazama tu tangu akiwa mtoto, utamchukia hata kabla hajaonyesha hali yake ya kupenda uchafu, kwasababu unajua asili hiyo ipo ndani yake. Atakuja kuwa mchafu tu.
Ndivyo ilivyo kwetu sisi, tayari Mungu alishaona tangu tunazaliwa tutamwasi tu yeye, mfano wa baba yetu Adamu.
Na ndio maana akaandaa mpango wa kuzaliwa upya mara ya pili, kupitia Yesu Kristo. Hivyo mtu yeyote anayezaliwa mara ya pili, anaondolewa katika laana hiyo ya kukataliwa na Mungu, na anakuwa mwana wa Baraka. Laana hii haiwezi kuondoka bila damu ya Yesu.
Hiyo ndio sababu kwanini maandiko yanasema Yesu alifanyika laana kwa ajili yetu. Maana yake, tunapokombolewa na yeye tunafanywa kuwa watu wengine kabisa wenye asili nyingine wasio na laana, wenye kukubaliwa na kupendwa na Mungu.
Wagalatia 3:13 Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;
14 ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.
Hivyo wewe uliyeokoka, na kupokea Roho Mtakatifu unaitwa, mbarikiwa, unaitwa mungu duniani, mtoto wa Mungu kwelikweli.
LAANA YA PILI
Lakini laana ya pili, kama tulivyoona ipo katika maapizo ambayo huyatoa Mungu au mwanadamu mwenyewe.
a) Tukianzana na zile zinazonenwa na Mungu
Mungu anaweza kukutamkia laana, hata kama utakuwa umekombolewa na yeye. Unaweza kushiriki mabaya. Laana hizi zinaweza kukufanya usipoteze wokovu wako, lakini zikakukosesha mambo mengi sana duniani.
Mfano wa hizi ndio zile alizowaambia wana wa Israeli, kwamba watakapoacha sheria zake, basi watatawanywa katika mataifa yote, watakuwa mikia na sio vichwa, nchi itazuliwa Baraka zake, wataondokeshewa adui zao N.k. (Kumbukumbu 28)
Mfano pia wa hizi, ndio kama ile aliyoilaani nchi, na nyoka pale Edeni. Akasema itatoa miiba, na nyoka atakwenda kwa tumbo (Mwanzo 3:17). Vilevile ndio ile aliyomwambia Kaini kuwa atakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani (Mwanzo 4:12).
Hata sasa wapo wengi wanaokutana na maapizo hayo ya Mungu kwa kufanya dhambi au makosa ya makusudi. Namna ya kueupuka laana hizi ni kutii agizo la Mungu.
Kwasababu unapozizoelea zitakufanya uangukie kabisa kwenye kundi lile la kwanza la kukataliwa kabisa..la watu ambao hawajaokoka.
Waebrania 6:4 Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,5 na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,
6 wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.
7 Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu; 8 bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.
Kinyume cha laana ni Baraka, unapotii amri za Mungu, umejiwekea mazingira mazuri ya kupokea Baraka.
b) Lakini pia zipo laana zinazonenwa na mwanadamu.
Hizi nazo zimegawanyika katika makundi mawili.
i) Kundi la kwanza ni la watu wa Mungu/wenye haki.
Kwamfano Utakumbuka Hamu alipoona uchi wa baba yake. Nuhu aliulaani uzao wake, Hivyo watu wa Mungu wamepewa mamlaka hiyo, hata sasa, ndio maana Bwana Yesu alisema mtakalolifunga duniani, limefungwa mbinguni, na akatusihi pia tuwe watu wa kubariki kuliko kulaani. (1Petro 3:9)
Unapokosewa na mwenye dhambi epuka kutoa neno la madhara kwake, kwasababu hakika jambo hilo litampata na kumwangamiza kabisa. Ndicho alichokifanya Elisha kwa wale vijana arobaini na wawili waliomdhihaki.
ii) Kundi la pili ni laana zitokazo kwa watu waovu.
Husasani wachawi, nao pia huweza kusema jambo likatokea, Utakumbuka kisa cha Balaamu mchawi, alipoajiriwa na Balaki kwenda kuwalaani Israeli wa Mungu, lakini alishindwa akajikuta anawabariki badala ya kuwalaani.
Akasema hakuna uchawi (Hesabu 23:23).
Ikiwa wewe umeokoka, huna haja ya kuogopa laana za hawa, kwasababu haziwezi kukupata, kwasababu unalindwa na nguvu za Mungu, hizi huwa zinawapata watu ambao wapo nje ya Kristo YESU.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NUHU WA SASA.
MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.
KUVUNJA MAAGANO YA UKOO.
Rudi Nyumbani
Swali: Neno “Kututa” lina maana gani kama tusomavyo katika Mhubiri 2:26?
Jibu: Turejee..
Mhubiri 2:26 “Kwa sababu Mungu humpa yeye aliyemridhia hekima na maarifa na furaha; bali mkosaji humpa taabu, ili kukusanya na KUTUTA, apate kumpa huyo ambaye Mungu amridhia. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.
“Kututa” maana yake ni “KULIMBIKIZA”..
Kwahiyo maneno hayo tunaweza kuyaweka katika Kiswahili hiki.. “Kwa sababu Mungu humpa yeye aliyemridhia hekima na maarifa na furaha; bali mkosaji humpa taabu, ili kukusanya na KULIMBIKIZA, apate kumpa huyo ambaye Mungu amridhia. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.
Andiko hili linatufundisha hatari ya kukusanya mali na kulimbikiza, ikiwa tupo nje ya KRISTO. Kwa maana hapo maandiko yanasema, mali za mtu huyo (mkosaji), alizojikusanyia na kujilimbikizia, atanyang’anywa na kupewa yule Mungu aliyemridhia.
Lakini pia mstari huo unatuonyesha thawabu kuu ambazo Mungu humpa yule aliyemridhia. Na hizo si nyingine Zaidi ya HEKIMA, MAARIFA na FURAHA.
Kabla ya kumpa mtu Mali humpa Hekima, Maarifa na Furaha na hivi vitatu ndivyo vitu vya kuvitafuta kwa MUNGU kabla ya kuomba vitu vingine kama Mali. Kama Sulemani aliomba Hekima kwanza na Mungu akampa Hekima na Mali ikawa ni nyongeza.
Hali kadhalika na sisi hatuna budi kutafuta hekima, Maarifa, Ufahamu na Furaha kwa bidii kwani tukiyapata hayo basi hayo mengine tutazidishiwa, na hata tusipoyapokea, bado hekima na maarifa vitabaki kuwa utajiri mkuu.
Mithali 3:13 “Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu.
14 Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha, Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi.
15 Yeye ana thamani kuliko marijani, Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye.
16 Ana wingi wa siku katika mkono wake wa kuume, Utajiri na heshima katika mkono wake wa kushoto.
17 Njia zake ni njia za kupendeza sana, Na mapito yake yote ni amani.
18 Yeye ni mti wa uzima kwao wamshikao sana; Ana heri kila mtu ashikamanaye naye”
Tafuta Hekima, tafuta Maarifa, tafuta Ufahamu, Busara na Furaha..
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tofauti kati ya Hekima, ufahamu na maarifa, ni ipi?
NI NANI ANAYEUFUNGA MLANGO WA MAARIFA?.
IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.
JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?
Swali: Katika Kutoka 3:2 tunasoma kuwa Mungu alisema na Nabii Musa kupitia kile kijiti ambacho kilikuwa kinawaka moto lakini hakikuteketea, je kulikuwa kuna sababu gani au ufunuo gani katika ishara ile?
Jibu: Tuanze kusoma mstari ule wa kwanza mpaka ule wa tatu, ili tupate kuielewa vizuri habari..
Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.
2 Malaika wa Bwana akamtokea, KATIKA MWALI WA MOTO ULIOTOKA KATIKATI YA KIJITI; AKATAZAMA, NA KUMBE! KILE KIJITI KILIWAKA MOTO, NACHO KIJITI HAKIKUTEKETEA.
3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei”
Lengo la Mungu kumwonyesha Musa Ono hilo kubwa, halikuwa kumburudisha au kumsisimua, bali ulikuwa ni ujumbe wa MUNGU kwa Musa na kwa Israeli wote ambao watasumiliwa baadae.
Na ujumbe huo si mwingine Zaidi ya ule tuusomao katika Isaya 43:1-4..
Isaya 43:1 “Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu.
2 Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; UENDAPO KATIKA MOTO, HUTATEKETEA; WALA MWALI WA MOTO HAUTAKUUNGUZA.
3 Maana mimi ni Bwana, Mungu wako; Mtakatifu wa Israeli, mwokozi wako, nimetoa Misri kuwa ukombozi wako; nimetoa Kushi na Seba kwa ajili yako.
4 Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako”
Hapo katika mstari wa Pili (2) anasema… “UENDAPO KATIKA MOTO, HUTATEKETEA; WALA MWALI WA MOTO HAUTAKUUNGUZA”.
Na hiyo ndio sababu ya Mungu kumwonesha Musa ono lile, kwamba watakapopita (wana wa Israeli) katika Moto (yaani majaribu mbalimbali) hawataungua..mfano wa kile kijiti kilichowaka moto lakini hakikuteketea.
Hivyo kwa ufunuo huo Israeli walielewa kuwa Mungu anasema nao, kwamba atakuwa pamoja nao katika mapito yote, hivyo wasiogope majaribu wala moto watakaokutana nao, kwani hautawateketeza, kinyume chake utawateketeza maadui zao…mfano wa akina Shadraka, Meshaki na Abednego, ambao walitupwa katika tanuru la moto, na badala ya moto ule kuwala wao, uligeuka na kuwala maadui zao wale walioshika na kuwatupa motoni.
Danieli 3:20 “Kisha akawaamuru baadhi ya watu mashujaa wa jeshi lake kuwafunga Shadraka, na Meshaki, na Abednego, na kuwatupa katika ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.
21 Basi watu hao wakafungwa, hali wamevaa suruali zao, na kanzu zao, na joho zao, na mavazi yao mengine, wakatupwa katikati ya ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.
22 Basi kwa sababu amri ya mfalme ilikuwa ni kali, na ile tanuru ilikuwa ina moto sana, mwako wa ule moto ukawaua wale watu waliowashika Shadraka, na Meshaki, na Abednego.
23 Na watu hao watatu, Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakaanguka, hali wamefungwa, katikati ya ile tanuru iliyokuwa inawaka moto.
24 Ndipo Nebukadreza akastaajabu, akainuka kwa haraka; akanena, akawaambia mawaziri wake, Je! Hatukutupa watu watatu, hali wamefungwa, katikati ya moto? Wakajibu, wakamwambia mfalme, Kweli, Ee mfalme.
25 Akajibu, akasema, Tazama, mimi naona watu wanne, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu”
Ni hivyo hivyo hata sasa, Mungu anawalinda wale wote wamwaminio na kumtumainia yeye, wanakuwa kama kijiti kilichopo motoni lakini hakiteketei.. Wengine wakipitia majaribu wanapotea kabisa, lakini watu wa Mungu wanapita katikati ya moto na wanatoka salama.
Je umempokea Bwana YESU?. Je yeye ni tumaini lako na ngao yako?..Kama upo nje ya Kristo fahamu kuwa Moto utakuunguza, na ibilisi atakumaliza. Lakini ukiwa ndani ya YESU utakuwa salama.
Mpokee YESU kama bado hujampokea, hizi ni siku za mwisho naye amekaribia kurudi sana.
Waebrani 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia.
38 Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye”.
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.
UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.
SWALI: Huyu “Yeye ashindaye” anayezungumziwa katika kila mwisho wa jumbe za makanisa saba. Ni mtu mmoja maalumu au wengi?
JIBU: Tunasoma Bwana Yesu alipotoa agizo au onyo kwa yale kanisa saba mwishoni alimalizia na kutoa thawabu. Lakini thawabu hiyo aliielekeza kwa yule ashindaye tu.
Kwa mfano ukisoma juu ya lile kanisa la Thiathira alisema..
Ufunuo wa Yohana 2:26
[26]Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,
Sasa swali huulizwa je? kuna mtu mmoja maalumu ambaye anaonekana atashinda? na kupokea tuzo hiyo ya kuwa na mamlaka juu ya mataifa au ni mjumuiko wa watu.
Ni raisi kudhani tuzo hiyo imeelekezwa kwa mtu fulani mmoja lakini ukweli ni kwamba inamuhusu kila mtu…ni sawa na mwalimu awaambie wanafunzi wake atakayefaulu mtihani wangu..nitamlipia ada ya muhula mmoja.
Sasa yeye kutumia lugha ya umoja “atakaye” na sio “watakao”…hamaanishi kuwa amemlenga mtu fulani mmoja.
maana yake ni kuwa yeyote yule atakayefaulu, basi atalipiwa ada, iwe ni mmoja, au wawili au wote. watalipiwa. Kwasababu wamefaulu. Kigezo ni kufaulu sio atakayefaulu kuliko wote.
Vivyo hivyo na Bwana alichokimaanisha hapo kwenye hayo makanisa saba. Lengo lake ni wote washinde lakini inaonekana ni kama si wote watakaoshinda…bali wale watakaoshinda watazipokea hizo thawabu.
Hivyo ni kujitahidi…kwasababu kuna uwezekano wa wengi kukosa thawabu hizo.
Mtume Paulo alitumia mfano wa wachezaji ambao hushiriki katika mchezo, kwamba wachezao ni wengi lakini apokeaye tuzo ni mmoja..(1Wakor 9:24)
Lakini hakumaanishi kwetu sisi atakuwa mmoja, ni mfano tu alitumia kueleza uhalisia kwamba kuna kunga’ng’ana ,sio jambo rahisi rahisi…fahamu kuwa sisi wakristo hatuna mashindano ya ukubwa na nafasi mbinguni…tunashindana ili tuyatende yale tuliyoagizwa na Bwana kikamilifu na sio kuzidiana…
Ndio maana mahali pengine akasema watatoka wengi, kutoka mashariki, na magharibi kuja kuketi na Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote, (Luka 13:28-29) Umeona kumbe wazee wetu hao, ni kama vile wamewekwa sehemu moja na wengine watakuja kuungana nao. Na wote watakua kitu kimoja na wao, lakini pia angalizo ni kwamba watakaofikia hapo si wengi sana.
Mathayo 8:11
[11]Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;
Kwahiyo ni kujitahidi hapo tusikose..Kwa kumaanisha kweli kweli kujitwika misalaba yetu na kumfuata Yesu. Na kujitenga na dhambi, na hakika thawabu hizo tutazifikia wote.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)
TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 4)
Rudi Nyumbani
Danieli 2:2
[2]Ndipo mfalme akatoa amri kuwaita waganga, na wachawi, na wasihiri, na Wakaldayo, wapate kumweleza mfalme ndoto zake. Basi wakaingia, wakasimama mbele ya mfalme.
Wasihiri ni kundi la wachawi, lililojikita kwenye mazingaumbwe. Linatumia uchawi kubadili vitu kwa hila, mbele ya macho ya watu kuwafanya waone kama ni muujiza umetendeka, na wakati mwingine kutumia njia hiyo kuleta madhara kwa watu.
kwamfano wale yane na yambre kipindi cha Musa walikuwa ni wasihiri, walijaribu kubadili fimbo kuwa nyoka, na kuleta vyura.(Kutoka 8:7)
Mfano mwingine ni yule Simoni mchawi, tunayemsoma katika;
Matendo 8:9-11
[9]Na mtu mmoja, jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa.
[10]Wote wakamsikiliza tangu mdogo hata mkubwa, wakisema, Mtu huyu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu.
[11]Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake.
Tofauti na waganga ambao, wenyewe wanajifanya kama matabibu, na wachawi na wale wakaldayo ambao ni wanajibu(wasoma nyota)…hawa wasihiri kazi yao hasaa ni ile ya kiini macho.
Lakini Mungu anathibitisha kwamba makundi yote haya, hakuna hata moja lenye uwezo wa kufikia hekima ya Mungu ipitayo vyote Hayana nguvu ya kupambanua mambo. au kufanya miujiza. Hakuna mganga wala wachawi, mwenye uwezo wa kufanya muujiza.
Sasa utauliza ni nini kile wanachokifanya kama sio miujiza?
Awezaye kutenda miujiza ni Mungu tu. wasihiri na waganga wanafanya kazi ya kulaghai fikra za watu kwa elimu ambayo ni ya siri (ya mashetani), ndio maana wanaofanya hizo kazi huenda kujifunza kufanya hivyo, namna ya kuchezea fikra za watu, na si kingine.
Sasa wewe kwasababu hujaijua hiyo elimu unaweza ukasema umeona muujuza kumbe ni uongo tu..wamekudanganya.
ni sawa na leo unapoona mtu akiwasiliana na mtu mwingine akiwa mbali na kuiona sura yake kwenye kioo, kama huijui elimu ya darasani, utasema ni muujiza lakini kumbe ni maarifa tu ya kibinadamu.
vivyo hivyo na hawa wachawi na wasihiri, hawana jipya kusema wanafanya muujiza fulani, ni elimu zao tu za kipepo
Hawawezi kuumba chochote. wale vyura waliofanya kutokea kipindi cha Farao, hawakuumba vyura wao wapya kimiujiza..Vinginevyo mpaka leo shetani angekuwa na uwezo wa kuumba na angeumba vyura wake wengi tu na viumbe vyake vimwabudu. Alichokifanya pale ni kuchukua vyura walioumbwa na Mungu, na kuwapumbaza watu macho, waone ni mawe yamegeuzwa vyura kumbe hakuna kitu. Ndio maana ujinga wao ulikuwa wazi baadaye…walipodhani kila eneo ni kiini macho, walipojaribu kwa chawa wakashindwa, kibao kikawageukia, wakakiri ni Mungu tu awezaye.
Kwahiyo wewe uliye na Yesu, shetani anakuona kama mungu duniani, mwenye nguvu nyingi sana, hekima mamlaka zaidi ya yeye. Wewe unaweza kutenda muujiza kabisa kwa jina la Yesu. yeye hawezi
mwamini Yesu mtegemee yeye tu, kwanini kutafuta msaada kwa vitu dhaifu, ukamtia Mungu wivu?. Kwenda kwa waganga ni kupungukiwa akili, ni kujitenga na fadhili zako, mwenyewe, ni kumdharau muumba wa mbingu na nchi, Yehova, atupaye vyote.
Okoka sasa, mpokee Yesu, upate uzima wa milele. Wachawi waliokutana na Yesu walisalimu amri na kuchoma mikoba yao. sasa wewe unaenda kufanya nini huko?
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Falaki ni elimu gani? (Isaya 47:13).
JIHADHARI NA ROHO YA YEZEBELI.
Rudi Nyumbani